Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Naibu Waziri Mavunde Azitaka Halmashauri Kuwawezesha Vijana Kiuchumi Kupitia Zabuni Za Halmashauri

$
0
0
Na; Mwandishi Wetu
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde amezitaka Halmashauri za Wilaya, Manispaa na Majiji nchini kuwawezesha Vijana kiuchumi kwa kutumia Vikundi na Kampuni za Vijana katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kimaendeleo kwa kuzipa zabuni kampuni na vikundi hivyo kupitia utaratibu wa “force account” hasa katika utengenezaji wa madawati na ujenzi wa madarasa, matundu ya vyoo, zahanati na vituo vya Afya.

Naibu Waziri Mavunde kayasema hayo Wilayani Musoma wakati alipotembelea Chuo cha Ufundi cha Mt. Anthony ambapo jumla ya Vijana 240 wanasoma hapo fani mbalimbali kwa ufadhili wa Serikali kupitia Programu ya Ukuzaji Ujuzi Nchini iliyopo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu ambapo mwaka huu wa fedha 2019/2020 inatrajiwa kuwajengea uwezo Vijana 46,000 katika fani mbalimbali.

"Serikali inayo nia ya dhati ya kuhakikisha kwamba tunaijengea Ujuzi stahiki nguvukazi ya Taifa hili ili vijana wengi zaidi waweze kushiriki kikamilifu katika uchumi wa viwanda na kuwawezesha kujikwamua kiuchumi kupitia shughuli za uzalishaji mali.Mamlaka za Serikali za Mitaa ziwe kichocheo katika kuwawezesha Vijana kiuchumi kwa kutoa zabuni kwa vikundi na makampuni ya Vijana nchini kote hasa zile zinapitia katika mfumo wa manunuzi wa force account," alisema Mavunde

Akitoa salamu za Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Dkt. Vicent Naano amewahakikishia Vijana hao kupata mikopo ya asilimia 4 na asilimia 2 kwa wenye ulemavu itokanayo na mapato ya ndani ya Halmashauri na kuwataka kuunda vikundi kutokana na fani zao za Ufundi.

Akizungumza kwa niaba ya Vijana wenzake wanafuika ya Programu ya kukuza Ujuzi, Bw. Baraka Emmanuel ameishukuru Serikali kwa kuwajali Vijana na kuwawezesha kupata Ujuzi kupitia mafunzo wanayoyapata hapo Chuoni ambayo pia yatawafanya waweze kujiajiri na kuajiri Vijana wengine.

Wizara Ya Fedha Na Mipango Kuboresha Mkataba Wa Huduma Kwa Wateja

$
0
0
Na. Peter Haule, WFM, Arusha
Wizara ya Fedha na Mipango inaboresha Mkataba wa utoaji Huduma kwa wananchi kwa kupata maoni katika maeneo mbalimbali ya utoaji huduma lengo likiwa kuongeza ufanisi na kufikia maendeleo stahiki kwa wakati.

Hayo yamebainishwa na Mchumi Mwandamizi wa Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Fortunata Soka, wakati wa mafunzo ya ukusanyaji wa maoni ya maboresho ya Mkataba wa Huduma kwa Wateja   kwa wadau wa Wizara hiyo yaliyofanyika Jijini Arusha na kuwakutanisha wadau kutoka Wizara hiyo pamoja na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Bi. Soka alisema kuwa Wizara ya Fedha na Mipango imekuwa na Mkakati wa Utoaji huduma kwa wananchi ambao sasa unahitaji maboresho ili kuongeza ufanisi wa huduma na kuharakisha maendeleo ya wananchi.

‘’Muundo wa Wizara umebadilika na pia wadau wanaongezeka hivyo kuna kila sababu ya kuboresha mkataba wa huduma kwa wateja ili kukidhi uhitaji, tunalazimika kufanya mafunzo ya namna ya kufanya tafiti kwa wadau ili kuja na mkataba bora uliosheheni weledi na kuleta matokeo chanya kwa walengwa.’’, alieleza Bi. Soka

Alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imejipambanua kwa kufikisha huduma kwa haraka kwa wananchi hivyo  Wizara inalengo la kupata mrejesho wa utoaji wa huduma zake ili kuweza kuandaa mipango yenye manufaa kwa wananchi na Taifa kwa ujumla

Bi Soka alisema kuwa maboresho ya Mkataba wa huduma kwa wateja ni sehemu ya kujali wananchi hasa wa hali ya chini ambao wanataka kupata huduma bora kwa ufanisi kwa maendeleo yao kwa kupunguza urasimu usio wa lazima.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi wa Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambaye pia ni mtoa mada, Bw. Raphael Waida, alisema kuwa ili kuweza kutoa huduma bora kwa wananchi lazima mikataba ya huduma kwa wateja ikafanyiwa maboresho kila inapobidi kwa kuwa teknolojia na mazingira ya kihuduma yanabadilika.

Aidha, ameipongeza Wizara ya Fedha na Mipango kwa jitihada zake za kuhakikisha inatoa huduma kwa wadau kwa wakati hasa katika kipindi hiki ambacho Serikali imejidhatiti kufikia uchumi wa Kati uliojikita katika viwanda kwa manufaa ya wananchi.

Naye Mchumi wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Henrico Ndagula ambaye ni mmoja wa Washiriki wa Mafunzo amesema kuwa, mafunzo hayo yanasaidia kufanya tathmini ya utoaji huduma na kuangalia maeneo ambayo Wizara imefanikiwa na yanayohitaji maboresho, hivyo kuwa na umuhimu hasa katika wakati huu ambao mabadiliko makubwa yakiuchumi yanafanyika nchini.

Mwisho.

Fahamu Zaidi Kuhusu Ugonjwa Wa Mshipa Wa Ngiri (Hernia/Hydrocele)

$
0
0
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji. 

Ugonjwa huu wa ngiri unawapata wanaume na wanawake wa rika zote. Mshipa wa ngili ni jina linalokusanya magonjwa kama Ngiri kavu (Hernia), Ngiri maji (Hydrocele) na Ngiri nyinginezo kama vile kuvimba kokwa au mfereji unaopitisha manii unaojulikana kitaalamu kama Epididmorchitis.

Dalili za Jumla za  Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya maumbile ya kiume kulegea,korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

1.Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.

2.Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.

3.Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.

4.Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

==>Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika
 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬  

==> MATIBABU. 
Matibabu ya ngiri  ni kupasuliwa (operation) japo kuna wengine hujitibu kwa njia za kawaida.  Wahi hospitali ya mkoa kwa uchunguzi na tiba.

Makala hii ni kwa Hisani ya ya Mtaalamu wa Ngiri; 0713785111.

Ugonjwa wa Zinaa wa Kisonono (gonorrhea) : Dalili Zake, Madhara Yake Na Jinsi Ya Kujikinga

$
0
0
Kati ya magonjwa yanayoathiri watu wengi sana duniani ni magonjwa ya zinaa. Haya ni magonjwa yanayoambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kupitia vitendo vya ngono. 

Vitendo hivi vya ngono vinaweza kuwa kujamiana, kupiga denda (kissing), vitendo vya ngono kwa kutumia mdomo (oral genital sex), kujamiana kupitia njia ya haja kubwa (anal sex) iwe kwa mwanamume na mwanamke au kati ya wanaume wenyewe na hata wale wanaotumia vifaa vya kufanyia ngono (vibrators). 

Magonjwa ya zinaa huathiri sana watu walio katika umri wa miaka 15 – 24 lakini hata kwa watu wengine ambao wana umri chini au zaidi ya huu niliotaja pia yanaonekana kwa wingi.

Kuna magonjwa ya zinaa zaidi ya ishirini yanayotambulika duniani, baadhi ya magonjwa ya zinaa ni
  1.  Kisonono (Gonorrhoea – “Gono” kama wengi wanavyopenda kuita kwa kifupi).
  2.     Chlamydia
  3.     Kaswende (Syphillis)
  4.     Human papilloma virus (HPV)
  5.     HIV/AIDS (Ukimwi/Upungufu wa kinga mwilini)
  6.     Hepatitis B, C, A
  7.     Herpes virus
  8.     Trichomoniasis
  9.     Bacteria Vaginosis
  10.     Pubic lice (chawa kwenye nywele za kinena)
  11.     Chancroid
Magonjwa mengi ya zinaa yanatibika lakini kuna baadhi ambayo hayana tiba ya uhakika kama HPV, Hepatitis B na C, na HIV. Mengine yameanza kuwa sugu kutokana na matumizi ya dawa za antibiotics bila mpangilio, magonjwa hayo ni kama gono (gonorrhoea) na nk.
 
Visababishi vya magonjwa ya zinaa
  1. Vitendo vya ngono kama nilivyoeleza hapo awali
  2. Kuanza vitendo vya ngono mapema au wakati wa umri mdogo
  3. Kuwa na wapenzi wengi
  4. Kufanya mapenzi ambao sio salama
  5. Maambukizi kupitia michibuko au sehemu zilizokatika kwenye ngozi kwa kugusana na majimaji ya aina yoyote yanayotoka kwa mtu mwenye ugonjwa wa zinaa kama damu, shahawa nk. Hii inaweza kutokea bila mtu kujua kwani mara nyingi dalili za magonjwa ya zinaa zinakuwa hazionekani kwa wanawake na hata baadhi ya wanaume.
Watu wengi huhisi kitendo cha kula denda (kissing) ni salama lakini si kama wanavyofikiria kwani baadhi ya magonjwa kama kaswende, herpes nk, yanaweza kuambukizwa kupitia njia hii. 

Soma pia:Tatizo la Kutokwa na usaha Wakati wa Kukojoa 

Kondomu husaidia kupunguza maambukizi ya magonjwa ya zinaa kama gono, Chlamydia lakini sio kinga muafaka dhidhi ya magonjwa ya zinaa kama kaswende, genital herpes, genital warts, na magonjwa ya upungufu wa kinga mwilini (AIDS).

Kisonono (gonorrhea) ni nini?
Kisonono ni ugonjwa kati ya magonjwa ya zinaa unaosababishwa na bakteria aina ya Neisseria gonorrhoeae, bakteria ambao hukuwa na kuzaliana kwa haraka katika sehemu zenye unyevunyevu na joto mwilini kama kwenye shingo ya kizazi kwa wanawake (cervix), mirija ya kupitisha mkojo au shahawa (urethra), mdomoni na kwenye puru. Maambukizi mengi kwa wanawake hutokea kwenye shingo ya kizazi (cervix). 

Asilimia 75 ya ugonjwa wa gono hutokea kwa watu wenye umri wa miaka 15 – 29, wanawake walio katika umri wa miaka 15 -19 na wanaume walio katika umri wa miaka 20 – 24 wako kwenye hatari zaidi ya kupata ugonjwa huu.
 
Ugonjwa huu huambukizwa vipi?
Ugonjwa huu huambukizwa kupitia vitendo vya ngono kupitia uke, njia ya haja kubwa (anus), kupitia mdomoni (oral sex). Ugonjwa unaweza kujitokeza kwenye sehemu za kujamiana, kwenye mdomo na kwenye puru (rectum). 

Soma Pia: Ugonjwa wa Zinaa wa Kaswende (Syphilis) : Dalili Zake, Madhara Yake Na Jinsi Ya Kujikinga 

Ugonjwa wa gono huonekana sana kwa vijana, watu wenye maisha duni kiuchumi, watu wanaoishi mijini, watu weusi na watumiaji madawa ya kulevya.
 
Dalili za ugonjwa wa kisonono
Dalili za ugonjwa wa kisonono huanza kujitokeza kuanzia siku ya 2 hadi ya 7 baada ya mtu kupata maambukizi na huweza kuchelewa kwa wanawake. Dalili ni kama zifuatazo

Kwa wanaume
  1. Kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa (burning sensation)
  2. Kutokwa na majimaji ya njano au meupe au ya kijani kutoka kwenye uume yanayoambatana na maumivu makali sana
  3. Wakati mwengine maumivu au kuvimba kwa korodani (swollen testicles)
  4. Maambukizi yakiwa kwenye puru (rectum) huambatana na maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa, kuwashwa sehemu za haja kubwa, na hata haja kubwa inaweza kutoka ikiambatana na damu, hii inatokea kwa wanaume na wanawake.
Kwa wanawake
Dalili kwa wanawake huwa si nyingi lakini wanawake wengi hawaonyeshi dalili zozote
  1. Maumivu au kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa
  2. Kuongezeka kwa kutoka majimaji kutoka kwenye tupu ya mwanamke ambayo ni ya njano au yamechanganyika na damu
  3. Kutokwa na damu kupitia tupu ya mwanamke kabla ya hedhi kufika.
  4. Kutokwa na damu baada ya kujamiana au baada ya tendo la ndoa
  5. Kichefuchefu
  6. Homa (fever)
  7. Kutapika
Vipimo vya ugonjwa wa kisonono
  1. Swab for culture – Kipimo hiki hufanyika maabara kwa kupandikiza bakteria baada ya kufuta sehemu za siri kwa kutumia swab ili kuona kama kuna bakteria wanaosababisha gono.
  2. Polymerase Chain Reaction (PCR)– Kipimo cha kuangalia vina saba (DNA) ya bakteria, ni ghali sana.
Tiba ya ugonjwa wa kisonono ni nini?
Tiba ya gono inahusisha na tiba ya ugonjwa wa Chlamydia kwani mara nyingi magonjwa haya huambatana kwa pamoja.Tiba hutegemea na umri wa mgonjwa na kama mtu ni mjamzito au la. 

Tiba ya gono ambayo sio sugu iliyo kwenye shingo ya kizazi (cervix), urethra na puru, dawa zinazotumika ni aina za cephalosporin dozi moja pamoja na dawa za aina ya macrolide antibiotics (mfano azithromycin) na za jamii ya penicillin (mfano doxycyclin) ili kutibu ugonjwa wa chlamydia. Mara nyingi kwa wale chini ya miaka 18 na wanawake wajawazito, hutibiwa kwa kuchomwa sindano.

Soma Pia: Saratani ya tezi dume : Madhara Yake, Dalili Zake, Chanzo na Tiba Yake

Fuata ushauri wa daktari kabla ya kutumia dawa hizi kwani dawa nyingi zina madhara kwa wajawazito (mfano doxycyclin). Ushauri nasaha hutolewa kwa wapenzi wote wawili na ni vizuri wapenzi wote wawili kutibiwa hata kama mmoja hana dalili za ugonjwa huu.
 
Madhara ya ugonjwa wa kisonono
  1. Kutoweza kuzaa kwa mwanamke (tasa) au kutoweza kutungisha mimba kwa mwanamume (infertility)
  2. Huweza kuathiri moyo (heart valves), ubongo,ngozi nk ambayo ni hatari sana kwa mtu yoyote.
  3. Madhara kwenye sehemu za maungio au jointi (joint inflammation)
  4. Kwa wanawake wale ambao hawajatibiwa wanaweza kupata ugonjwa wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) ambao huongeza asilimia ya mwanamke kuwa tasa.
  5. Wale wanawake ambao ni wajawazito na wameambukizwa gono wako kwenye hatari ya mimba kutoka au kuzaa mapema kabla mimba haijatimiza umri wake (preterm labor).
  6. Kwa wale wanaoambukizwa gono kipindi cha kukaribia kujifungua, wanaweza kuwaambukiza watoto wao na hivyo watoto kupata ugonjwa wa uti wa mgongo (meningitis), kuwa kipofu (blindness), homa ya mapafu (pneumonia) na ugonjwa wa mifupa (septic arthritis).
Kinga ya kisonono
  1. Kutumia kondomu wakati wa kujamiana
  2. Kuwa na mpenzi mmoja mwaminifu
  3. Kuacha vitendo vya ngono kama matumizi ya vifaa vya ngono hasa kwa wanawake mfano vibrators nk.
  4. Kwa wanawake wajawazito – Hakikisha unahudhuria kliniki mapema ili upate kuchunguzwa na kupatiwa tiba muafaka kama utagundulika na ugonjwa wa gono au ugonjwa mwengine wowote.
  5. Wanawake wajawazito wanashauriwa kujifungulia hospitali ili kama mtoto ameathirika na gono apate matibabu ya haraka baada ya kuzaliwa kuepusha kuwa kipofu.
  6. Epuka kufanya ngono na mtu aliyeambukizwa gono.

Waziri Kamwelwe aagiza kukamatwa kwa anayeendesha mtandao wa ATCL Aviation TV kwa kutangaza UONGO kuwa ndege nyingine mpya Inakuja

$
0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano nchini Tanzania, Isack Kamwelwe ameagiza anayeendesha mtandao wa ATCL Aviation TV kukamatwa kwa kutangaza kuwa ndege nyingine mpya aina ya Dreamliner inakuja nchini wakati si kweli.

Kamwelwe ameeleza hayo leo Oktoba 24, 2019  jijini Dar es Salaam katika kongamano la Tehama lililowakutanisha wadau mbalimbali wa sekta hiyo kujadili mchango wake kwa maendeleo ya uchumi wa viwanda.

Amesema kila jambo lina mamlaka zake za kutangaza na kama ni suala la ndege, wizara yake ndio ina dhamana ya kutangaza.

Amesema ameliuliza Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) wakamueleza kuwa hawakifahamu chombo hicho, nao pia wanashangaa.

"Nimeagiza atafutwe nimemwambia na Waziri wa Mambo ya Ndani (Kangi Lugola) kuangalia sheria ya kumshtaki. Kama hakuna sheria tutamsumbua tu mpaka wenzake wamuonee huruma," amesema Kamwelwe.

Amesema imefikia hatua vyombo vya habari vinatangaza kifo cha mtu, kusisitiza kuwa Taifa  lina maadili yake na hali hiyo haitaachwa iendelee.

"Kuna utaratibu wa kutangaza jambo, kama ni kifo familia ndiyo watatangaza. Kama mimi naumwa, wewe inakuhusu nini kama sijakwambia?" amehoji waziri Kamwelwe.

Amesema siku chache zilizopita, ndege ya ATCL ilizuiwa nchini Afrika Kusini kwa sababu baadhi ya Watanzania kutoa taarifa za uongo mitandaoni.

Credit: Mwananchi

CCM Yatoa Tamko Kulaani Vikavyo Vya Uchumi ilivyowekewa Zimbabwe

$
0
0
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM – Taifa), Philip Mangula ametoa tamko la azimio la chama hicho juu ya vikwazo vya kiuchumi ilivyowekewa Zimbabwe tangu mwaka 2000.

Mangula ametoa tamko hilo leo Jumatano Oktoba 24, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salam ambapo amesema kuwa vikwazo hivyo ni mwendelezo wa fikra na matendo ya unyojaji kwa Afrika na hivyo wameazimia kuwa uonevu huo ufike mwisho.

“Kwa kutambua jukumu letu katika kuimarisha umoja, ushikamano wa Waafrika na kuendeleza mapambano dhidi ya ukoloni mamboleo pamoja na kuimarisha uhusiano mwema wa vyama vya siasa vya nchi nyingine vyenye itikadi kama ya CCM, chama kinaamini kuwa vikwazo dhidi ya watu wa Zimbabwe ni muenedelezo wa fikra na matendo ya unyojaji kwa Afrika na sasa tuaazimia kuwa uonevu huo ufike mwisho,”.

“Ni miaka 19 ya kuwekewa vikwazo hata wale ambao walikuwa hawajazaliwa wanaadhibiwa na vikwazo hivi nadhani huu sio ubinadamu, sambamba na kutekeleza maamuzi hayo CCM kwa nafasi yake ya kuwa chama kiongozi wakati wote wa kulikomboa Bara la Afrika kisiasa inatumia nafasi hii kupaza sauti na kushinikiza mataifa yote yaliyoiwekea vikwazo Zimbabwe kuviondoa bila masharti yoyote ili nchi hiyo iweze kupiga hatua za haraka za maendeleo kiuchumi na kijamii kwa watu wake,” amesema Mangula.

Aidha Mangula amevitaka Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika na watu wote wenye mapenzi mema kuendelea kupaza sauti hadi pale Zimbabwe itakapoondolewa vikwazo hivyo vya kiuchumi ambavyo havizingatii ubinadamu.

Miaka Minne Ya Rais Magufuli; Ahadi Zake Zimewagusa Wananchi.

$
0
0
Na: Jovina Bujulu, MAELEZO, Dar es salaam
Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli imefanikiwa kutimiza ahadi zilizoahidiwa kwa wananchi wakati wa kampeni za Urais, mwaka 2015, na wakati wa ufunguzi wa Bunge la 11 la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Novemba 2015.
 
Rais alihutubia Bunge kwa mujibu wa matakwa ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 91, ibara ndogo ya kwanza inayomtaka Rais aliyechaguliwa kufungua rasmi Bunge hilo.
 
Akihutubia bunge hilo, Rais Magufuli aliwaambia wabunge kuwa wananchi waliwachagua wakiwa na matarajio makubwa na watawapima kwa namna watakavyokidhi kiu na matarajio yao.
 
“Wananchi wamewapa imani na ridhaa ya kuwawakilisha katika kipindi cha Awamu ya Tano ambapo matarajio yao ni makubwa sana, sote tuliahidi kuwatumikia na kutokana na utumishi wetu kwao tuweze kutatua matatizo yao mbalimbali  na kuongoza mabadiliko makubwa ya kiutendaji” alisema Rais Magufuli.
 
“Mimi na Mhe. Samia, Makamu wa Rais tuliwaahidi wananchi kuwa tutawatumikia na kuhakikisha kuwa katika utumishi wetu tutawajali wananchi wote, lakini zaidi wananchi wa kawaida” alisema Rais Magufuli.
 
Ni dhahiri uchapakazi wake umeonyesha mabadiliko makubwa ya kiutendaji, tumeshuhudia Rais akifanya mikutano mbali mbali na viongozi kuanzia ngazi ya mawaziri hadi watendaji wa kata Tanzania bara na kuzungumza nao masuala mbalimbali ya kiuongozi ikiwemo wajibu wao kwa wananchi.
 
Mkutano kati ya Rais na watendaji wa kata ni mwendelezo wa mikutano yake na watendaji wa serikali wakiwemo Wakuu wa mikoa, makatibu tawala wa mikoa, Wakuu wa wilaya, Wakurugenzi wa wilaya, Makatibu tawala ya wilaya na Makatibu watendaji wa tarafa.
 
Akizungumza na Makatibu watendaji wa tarada Rais alisema “Ninyi ni wawakilishi wangu ngazi ya kata, tunapozungumza mafanikio ya Serikali, ninyi ndio wasimamizi wa mwanzo wa mafanikio hayo.”
 
Hatua ya Rais kuwaita Watendaji hao wa tarafa kutoka Tanzania Bara na kuzungumza nao, ni kitendo kinachoonyesha jinsi anavyowajali viongozi wote kuanzia ngazi ya chini hadi juu. Pia ni kitendo kinachoonyesha kuwa uongozi wa chini ukifanya kazi vizuri utawezesha hata uongozi wa juu kutenda kazi kwa ufanisi na yenje tija kwa taifa na wananchi kwa ujumla.
 
Katika bunge hilo Rais pia aliahidi kusimamia matumizi ya mali za umma na rasilimali za Taifa ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa  rasilimali zetu zinatumika kwa matumizi kwa manufaa ya umma na si kwa manufaa ya mtu binafsi. Aidha, kuhakikisha kuwa ugawaji wa rasilimali hizo unafanyika kwa haki.
 
Katika siku za mwanzo za utawala wake Rais Magufuli alianza kwa kufanya ufuatiliaji wa rasilimali zetu ambapo aliunda kamati maalum ya kuchunguza mchanga na madini yalikuwa yanasafirishwa nje ya nchi. Kamati hiyo ilionyesha upotevu mkubwa wa mapato na rasilimali za nchi ambapo nchi ilikuwa inapoteza kiasi cha bilioni 829.4 hadi trilioni 1.439 kwa kusafirisha mchanga nje ya nchi.
 
Ili kuhakikisha anazuia upotevu huo, kamati ilitoa mapendekezo kadhaa ambayo Rais aliyakubali. Miongoni mwa mapendekezo hayo ni usitishwaji wa  usafirishaji wa mchanga huo hadi mrabaha stahiki utakapolipwa, na kujengwa kwa vinu vya kuchakata madini yote ili yaweze kufahamika na kutozwa kodi.
 
Aidha, Rais aliwaagiza Wakuu wa mikoa inayozalisha madini kuanzisha masoko ya madini ili kudhibiti utoroshaji na uuzaji holela wa madini. Hadi sasa baadhi ya  masoko yamekwisha anzishwa katika mikoa ya Mwanza, Geita, Dar es salaam, Mtwara, Manyara, Morogoro, Kagera na Arusha. Kwa upande wa wilaya masoko hayo yamefunguliwa Simanjiro na Chunya.
 
Ufunguzi wa masoko hayo umeleta neema si kwa Serikali tu bali hata kwa wauzaji wa madini hayo ambao walikuwa wakiyauza kwa kudhulumiwa na wanunuzi wakubwa. Kwa Serikali na nchi kwa ujumla masoko haya yameongeza pato la taifa kwa kiasi kikubwa na ongezeko la upatikanaji wa madini.
 
Eneo lingine ambalo Rais aliahidi kulishughulikia ni kusimamia ukusanyaji wa mapato na matumizi mabaya ya fedha za umma. Katika kutimiza ahadi yake kwa upande wa kusimamia mapato tumeshuhudia Rais akifanya mabadiliko ya mara kwa mara ya uongozi katika mamlaka ya kukusanya kodi (TRA) na kuzindua kituo kikuu cha Taifa cha kuhifadhi mifumo ya ukusanyaji wa mapato kwa njia ya elektroniki ambapo makusanyo ya mwezi Septemba 2019 yalikuwa trilioni 1.7 sawa na asilimia 97.20 kiasi ambacho ni hakijawahi kukusanywa na mamlaka hiyo tangu kuanzishwa kwake Julai mosi, 1996. 
 
Ni dhamira ya TRA kukusanya mapato kwa utaratibu rahisi na wa wazi na walipakodi watapata urahisi wa kupata huduma zinazotolewa kwa wakati.  Matokeo ya kuongezeka kwa ukubalifu yatadhihirika kwa kuongezeka kwa mapato kwa ajili ya Serikali kutoa huduma za jamii zinasostahiki na kwa ubora. Hii itaifanya jamii ya walipakodi kufurahia manufaa ya kijamii na kiuchumi kutokana na kodi wanazolipa katika kuboresha hali ya maisha.
 
Kituo hiki ni mashirikiano ya pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB), ambacho kimeundwa ili kusaidia kuondoa mianya ya uvujaji wa mapato ya serikali zote mbili.
 
Akizindua kituo hicho Rais alizitaka taasisi mbalimbali zikiwemo za Serikali, kampuni na benki kujisajili katika kituo hicho ili kuweza kukusanya kodi kwa ufanisi. ‘Kituo hicho ni muhimu sana kwa ustawi wa maendeleo ya nchi ili kulinda usalama wa taifa, taasisi za serikali na makampuni binafsi yanayoendesha shughuli zake nchini na kukuza sekta ya teknolojia ya habari na mawasiliano ambayo ni kichocheo kikubwa cha maendeleo’ alisema Rais.  
 
Katika kuhakikisha kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inakuwa kinara wa utawala bora, Rais aliahidi kupambana na rushwa na ufisadi. Awali akihutubia bunge la kwanza, Rais aliwaambia wabunge kuwa mojawapo ya maeneo yaliyolalamikiwa na wananchi wakati wa kipindi cha kampeni ni rushwa ambapo sehemu nyingi wananchi walisema kuwa rushwa ni mojawapo ya kero kubwa wanazokumbana nazo.
 
Baadhi ya mafanikio ya mapambano ya vita dhidi ya rushwa ni pamoja na kuanzishwa kwa ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Hadi ngazi za wilaya. 

Pia Serikali hii inajipambanua kwa uwazi na uwajibikaji katika utoaji wa huduma kwa umma, ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa utoaji wa elimu kwa umma kuhusu rushwa na madhara yake.
 
Katika mkutano wa 32 wa wakuu wa nchi za Afrika (AU) uliofanyika Addis Ababa, Ethiopia mwaka 2017, Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa alisema kuwa Tanzania ilitajwa kuwa miongoni mwa nchi zinazofanya vizuri katika ufuatiliaji na utekelezaji wa mapambano dhidi ya rushwa.
 
Taasisi ya Transparency International imesifu juhudi za Rais Dkt. John Pombe Magufuli na kuitaja Tanzania kuwa ni  nchi ya pili kwa kupunguza rushwa  na kufanikiwa kuifanyia kazi mianya mingi ya rushwa. 
 
Akizungumza hivi karibuni jijini Dar es Salaam aliyekuwa Mkurugenzi wa TAKUKURU, CP. Diwani Athuman alisema kuwa utafiti uliofanywa na taasisi za kimataifa za Transparency International na Afro Barometer inayoitwa Global Corruption Barometer Africa 2019, alisema kuwa Tanzania ni ya kwanza kati ya nchi 35 za Afrika katika kipengele cha juhudi za serikali katika kupambana na rushwa kwa mwaka 2019. 
 
Aliongeza kusema kuwa Tanzania imefanya vizuri katika maeneo mawili ambayo ni utendaji mzuri wa Serikali na kukuza imani kwa wananchi dhidi ya Serikali yao na jitihada za kupambana na rushwa.
 
Kuhusu kero ya migogoro ya ardhi, Serikali ya Awamu ya Tano imefuta mapori tengefu 12 yenye ukubwa wa ekeri 707,659.94 ambayo yamepoteza sifa na kuyagawa kwa wananchi kwa ajili ya shughuli za makazi, kilimo na ufugaji, na misitu 7 yenye ukubwa wa  ekari 46,715 kurudi kwa wananchi.
 
Hatua hii ilifuatiwa na kubaini uwepo wa vijiji 975 vyenye migogoro, ambapo iliamuliwa kuwa vijiji 920 vibaki ndani ya hifadhi na mipaka irejerewe upya na kupatiwa vibali vya ardhi vya kijiji. Pia serikali iliridhia kumega misitu 14 kwa ajili ya kilimo na mifugo na kufuta mashamba 16 yasiyoendelezwa ili yapangiwe matumizi ya kilimo na mifugo.
 
Ahadi nyingine ambazo Rais amezitimiza ni katika sekta ya afya na elimu ambapo katika elimu aliahidi elimu bure kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha nne. Kutokana na utekelezaji wa ahadi hiyo, kumekuwa na mwamko mkubwa wa wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao shule ambapo kumekuwa na ongezeko kubwa la wanafunzi wanaoandikishwa darasa la kwanza shule ya msingi ambao idadi yao imefikia 1,670,919 mwaka 2019 kutoka 896,584 mwaka 2016. Kwa upande wa shule za sekondari idadi ya wanafunzi walioandikishwa kwa mwaka 2019 ni 710,436 kutoka wanafunzi 238,365 walioandikishwa mwaka 2016 wakati sera ya elimu bure ilipoanza kutekelezwa nchini. 
 
Katika sekta ya elimu pia tumeshuhudia maboresho mbalimbali ambapo vifaa vya kufundishia na kujifunzia vimeongezwa, michango isiyo ya lazima imeondolewa, kuongezewa madawati na kujengwa kwa nyumba za walimu.
 
Aidha, katika eneo la afya, dhamira ya Rais kujenga uchumi wa kisasa na suala la kupambana na umaskini amelipa msukumo wenye tija ili kuwa na wananchi wenye afya bora. Tumeshuhudia uboreshaji wa sekta hii ikiwa ni pamoja na kuimarisha huduma za afya, kuzipatia vifaa bora na vya kisasa hospitali, vituo vya afya na zahanati. Lengo likiwa ni kuwaondolea usumbufu wananchi na kutolazimika kupeleka watu kutibiwa nje ya nchi. 
 
Katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Awamu ya Tano, Kwa tumeshuhudia mafanikio mengi katika sekta mbalimbali kama vile sekta za afya, elimu, miundombinu, nishati na madini, ikiwa ni kutimiza ahadi ambazo ziliahidiwa na Rais wakati anaingia madarakani. Maendeleo yote haya yamewagusa wananchi kwa kiasi kikubwa kwa sababu yameweza kutatua kero nyingi ambazo wananchi walikuwa nazo.
 
Mwisho.

Fahamu Zaidi Kuhusu Ugonjwa Wa Mshipa Wa Ngiri (Hernia/Hydrocele)

$
0
0
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya maumbile ya kiume  kulegea, kutokuwa na hamu ya kurundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Kwa Ushauri na Msaada  Wasaliana na 
0713785111

Jeshi La Polisi Dodoma Lawanasa Raia Wanne Wa Somalia Na Ethiopia Kwa Uhamiaji Haramu.....Walitaka Kutoa Rushwa Ya Milioni Moja , Jeshi Likagoma

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma  linawashikilia Raia wanne kutoka nchini za Somalia na Ethiopia Kwa kuingia nchini bila kibali huku pia likiwashikilia watu wawili  Raia wa Tanzania waliokuwa wakiwasafirisha  wahamiaji haramu hao .
 
Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Okt.24,2019  jijini Dodoma,Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma Girres Muroto amesema mnamo tarehe 23,10,2019  majira ya saa 10:00 huko katika kijiji na kata ya MTERA  Tarafa ya RUDI Wilaya ya MPWAPWA   Mkoani Dodoma ,walikamatwa wahamiaji haramu wanne walioingia nchini bila vibali.
 
Kati yao ,Wawili ni Raia wa Ethiopia  na Wawili ni Raia wa SOMALIA huku pia wakikamatwa watanzania wawili waliokuwa wakisafirisha wahamiaji haramu hao kutoka ARUSHA Kwenda IRINGA kwa Kutumia Usafiri wa pikipiki mbili .

Waliokamatwa ni Sellamu Yohanes[24] Raia wa Ethiopia,Ashetu Tesfaye[20]Raia wa Ethiopia,Mahamoud Mapaa[19]Raia wa Somalia,Cuse  Ciise [18]Raia wa Somalia 

Kamanda Muroto amewataja Raia wa Kitanzania waliokuwa wakiwasafirisha wahamiaji haramu hao kwa kutumia pikipiki ni Jamali Babuu Martin [26] dereva wa bodaboda ,mkazi wa ORASITE ARUSHA akiendesha pikipiki  namba MC 942 AXK KINGLION Chassis Na.LTBPK8BG5F2KO9729 rangi nyeusi.

Mwingine ni Wiston Alex  MAKIA  ALLY [25] Dereva wa Bodaboda mkazi wa Mbauda ARUSHA akiendesha pikipiki Na.MC 767 CEB DAYUN  Chassis Na.L7GPCJLYH1099156 rangi nyeusi.
 
Kamanda Muroto ametaja mbinu waliyotumia kuingia nchini ni  kwa kutumia usafiri wa pikipiki kuvuka mipaka na vizuizi vya barabarani.
 
Aidha ,amebainisha kuwa watuhumiwa walijaribu kuwarubuni askari kwa kutoa rushwa ya Tsh. Milioni moja [1,000,000/=] ili waweze kuachiliwa  na wakati wanakamatwa walikuwa na pesa Tsh.laki tano[500,000/=] lakini askari walikataa hongo ya rushwa hiyo  na waliwakamata pamoja na pesa yao  na kuwafikisha kituoni na watafikishwa mahakamani.
 
Katika hatua nyingine kamanda Muroto amesema Jeshi hilo limekamata nyara za Serikali  ambapo mnamo Tarehe 21,10,2019 majira ya saa 1:30 jioni  huko kijiji na kata ya MKOKA Tarafa ya ZOISA Wilaya ya KONGWA  Mkoani Dodoma  alikamatwa STEPHANO MTAGWA  KOGANI[39] Mkazi wa kijiji cha SONGAMBELE na HAMIS MATHAYO  MABUKU [45] na mkazi wa kijiji cha MATONGOLO  Wakiwa na pembe moja ya tembo   ndani ya mfuko wa Salfeti kiroba  kinyume cha sheria na watafikishwa mahakamani upelelezi ukikamilika.
 
Tukio jingine Kamanda Muroto amesema ni la kuvunja nyumba mchana na kuiba ambapo amekamatwa ELIAS SHABAN JOSEPH [21]Mkazi wa Mailimbili Mnadani   baada ya kuvunja nyumba mchana na kuiba maboksi 8 ya mafuta ya kupaka  na maboksi 4 ya pipi  mali yenye thamani ya TSH.720,000 Maeneo ya IPAGALA WEST  Dodoma  mali ya Willy Fidelis  Mgeni huku pia wakikamatwa wengine walioshiriki uhalifu huo .
 
Hata hivyo,Kamanda Muroto ameipongeza vyombo vya habari kwa kuendelea kutoa ushirikiano katika kuuhabarisha umma.

Tanzania Kuendelea Kushirikiana Na Umoja wa Mataifa Ili Kuleta Maendeleo Kwa Wananchi Wake

$
0
0
Na.Faustine GimuGalafoni,Dodoma.
Serikali ya Tanzania imesema itaendelea kuliunga mkono Shirika la umoja wa Mataifa UN, katika jitihada zake za kuleta maendeleo hapa nchini, kupitia mashirika yake mbalimbali.

Hayo yamezungumzwa Jijini Dodoma na Waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi, wakati wa sherehe za Shirika la umoja wa Mataifa UN, katika kutimiza miaka 74 tangu kuasisiwa kwake.

Prof. Palamagamba Kabudi amesema  serikali wataendelea kuliunga mkono Shirika hilo kwa juhudi zake, na kwamba wameweka misingi katika Mataifa mbalimbali kupitia mashirika yake, ikiwamo kukuza amani miongoni mwa nchi ikiwamo Tanzania.

"Serikali ya Tanzania tutaendelea kuwaunga mkono kwa juhudi zenu, nimeweka misingi katika Mataifa mengi kupitia mashirika yenu, ambayo yamekuwa Chachu katika kukuza amani, na Amani hiyo imekuwa nguzo katika kujiletea maendeleo" amesema Prof. Kabudi.

Sherehe hizo zilizobebwa na kauli mbiu isemayo wanawake na wasichana wapewe kipaumbele katika kufikia malengo, ambayo imelenga kuwainua wanawake katika kufikia malengo Kama nchi na kwamba wasiachwe nyuma.

Prof. Kabudi amesema serikali ya Tanzania imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali kuhakikisha wanawake hawaachwi nyuma, na hasa katika elimu bure ambayo imeweza kuwawezesha watoto wa kike kupata elimu.

"Serikali tunatambua umuhimu wa kumuwezesha mtoto wa kike, na ndio maana tulipogundua wanakosa elimu kwa visingizio vya kukosa ada, tumeamua kutoa elimu bure toka msingi hadi kidato cha nne" amesema.

Aidha kuhusu afya amesema wamejenga vituo vya Afya takribani 352, na hospitali za Wilaya 67, zote hizo ni jitihada za kuhakikisha mwanamke anakuwa salama hasa katika eneo la uzazi salama.

Pia wameanzisha mpango wa kukomesha vitendo vya ukatili wa kijinsia, mpango ambao unatekelezwa nchi nzima kuhakikisha mwanamke na wasichana wanakuwa salama na kutoathirika na vitendo hivyo.

Amesema Kama nchi wamejipanga kufikia malengo endelevu, na kufanikisha hilo wanatekeleza miradi mikubwa hapa nchini, Kama mradi wa reli ya kisasa, mradi mkubwa wa kufua umeme, wa Mwalimu Nyerere, yote hayo ni kuhakikisha wanafikia malengo endelevu.

Kwa upande wake Mwakilishi Mkazi wa Shirika la idadi ya watu la Umoja wa Mataifa, Jackrine Mahon, amesema leo Shirika la Umoja wa Mataifa UN linatimiza miaka 74, tangu kuasisiwa kwake, na lilianza na nchi 51, na mpaka Sasa umefikia nchi 193 kote ulimwenguni.

Aidha wameipongeza nchi ya Tanzania kwa kuendelea kupokea wakimbizi na kuwahifadhi, amesema wanatambua changamoto wanazokutana nazo katika kuwahifadhi wakimbizi na UN wataendelea kushirikiana katika hilo.

Amesema ni muhimu kuona mtoto wa kike anafikia malengo yake na kuwa viongozi hapo baadaye, na kutoa wito kwa wasichana kushikilia ndoto zao bila kulubuniwa na kitu chochote hadi kufikia malengo.

Naye mwenyekiti wa YUNA Tanzania Hortencia Nuhu, amewataka wasichana kuweza kuweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha wanafikia malengo waliyojiwekea katika maisha yao,ili baadaye waweze kujumuishwa katika nyanja mbalimbali.

Nchi Za Afrika Zatakiwa Kuwajengea Uwezo Wataalam Wa Jiolojia

$
0
0
Na Asteria Muhozya, DSM
Waziri wa Madini Doto Biteko ametoa wito kwa kuzitaka nchi za Afrika kujenga uwezo kwa Wataalam wa ndani wa Jiolojia ili kuwawezesha kujenga uwezo wa tafiti za rasilimali madini ili pindi nchi au taasisi wafadhili wanapoacha kufadhili, mamlaka husika ziwe kwenye nafasi ya kuendeleza shughuli hizo.
 
Waziri Biteko ameyasema hayo Oktoba 24, 2019 wakati akifungua Mkutano wa 36 wa Wataalam wa Jiolojia kutoka nchi mbalimbali za Afrika ambao wanakutana jijini Dar es Salaam. 
 
Mkutano huo unalenga katika kuwapatia wataalam hao mafunzo yanayogusa masuala mabalimbali kuhusu sekta ya Madini ikiwemo kubadilishana uzoefu katika utafutaji rasilimali madini na kuangalia namna bora ya kuendeleza rasilimali hizo ili kuhakikisha kwamba zinayanufaisha mataifa husika. 
 
Aidha, amewataka washiriki wa mkutano huo kujifunza na kutumia vyema uzoefu mzuri utakaotolewa na mataifa mengine ili kuwezesha kuongeza thamani  katika kutekeleza majukumu  ya taasisi zao  katika uendelezaji wa rasilimali madini.
 
‘’ Afrika lazima tujifunze wenyewe kuendeleza na kujenga miradi yetu wenyewe. Katika mkutano yapasa kujiuliza siku Wafadhili wetu Umoja wa Ulaya na  taasisi nyingine zinazofadhili mafunzo haya zikiacha tutaweza kujisimamia wenyewe?,’’ amehoji Waziri Biteko.
 
Amesema kwa upande wa Tanzania kama taifa linaamini katika kuwajengea uwezo wataalam wa ndani ambapo tayari serikali imechukua hatua kadhaa za kuhakikisha zinawendeleza wataalam wake ili kuwezesha taifa kuzalisha wataalam waliobobea katika taaluma ya jiolojia na ambao watakuwa na mchango katika utafutaji wa rasilimali madini.
 
Amesema mradi huo wa kutoa Mafunzo kwa Taasisi za Jiolojia Afrika unafadiliwa na Umoja wa Ulaya pamoja na taasisi nyingine 12 ambapo tangu kuanzishwa kwa mradi huo mnamo mwaka 2017, tayari umewezesha kuwapatia mafunzo wataalam wapatao 1,100 kutoka Mataifa mbalimbali ya Afrika huku wataalam 30 wa Tanzania wakiwa wamepatiwa mafunzo hayo.
 
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkuu wa Idara ya Ushirikiano  Kutoka Umoja wa Ulaya, Jose Dorreia Nunes, amewataka washiriki wa mkutano huo kutafakari namna rasimali hizo zitakavyozinufaisha nchi zao ikizingatiwa kwamba madini ni chanzo kikubwa cha mapato kwa nchi za Afrika hivyo ni muda sahihi kupitia mafunzo yanayotolewa na Umoja huo yawezeshe kujenga uwezo wa wataalam wa ndani katika kutafiti, kusimamia na kuendeleza rasilimali katika nchi zao.
 
Naye, Kaimu Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), Yorkberth Myumbilwa akizungumza na waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo amesema mafunzo yanayotolewa na Taasisi wafadhili yana umuhimu mkubwa kwa kuwa yanagusa moja kwa moja shughuli zinazofanywa na taasisi hizo zikiwemo tafiti, wingi wa mashapo, urithi wa Jiolojia, namna ya kuhifadhi data na masuala mengine.
 
Ameongeza kwamba, suala la kukutanishwa na taasisi nyingine lina umuhimu kwa GST kwa kuwa linawezesha kujenga mahusiano mapya na Taasisi nyingine za Jiolojia kutoka nchi nyingine. 
 
Nchi zinazoshiriki mkutano unafanyika kwa siku mbili kuanzia tarehe 24 – 25 Oktoba, 2019 ni pamoja na Tanzania, Namibia, Sengel Morroco, Kenya, Afrika Kusini , Rwanda, Zambia na Ghana.

Wafanyabiashara Washauriwa Kutunza Kumbukumbu Ili Kulipa Kodi Stahiki

$
0
0
Na Veronica Kazimoto
Wafanyabiashara nchini wameshauriwa kutunza kumbukumbu za biashara zao ili kulipa kodi stahiki na hatimaye kupunguza kero ya madai yao kwamba Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inawakadiria kodi kubwa isiyoendana na uhalisia wa biashara wanazofanya.

Akizungumza wakati wa semina ya wafanyabiashara hao iliyofanyika Wilaya ya Busega mkoani Simiyu, Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi kutoka mamlaka hiyo Diana Masalla, amesema kuwa, wafanyabiashara walio wengi hawana tabia ya kutunza kumbukumbu za biashara zao suala linalosababisha malalamiko mengi baada ya kukadiriwa kodi na TRA.

“Ndugu zangu wafanyabiashara sote tunajua kwamba, mali bila daftari hupotea bila habari hivyo basi, niwaombe mjenge tabia ya kutunza kumbukumbu za biashara zenu siyo tu kwa ajili ya TRA lakini pia kwa ajili yenu wenyewe kwani mtaweza kujua kama biashara zenu zinakua au zinashuka lakini pia mtaweza kupanga bajeti za mauzo na manunuzi yenu vizuri na mwisho wake mtalipa kodi stahiki na kuchangia maendeleo ya nchi yetu,” amesema Masalla.

Masalla ameongeza kuwa, kuna tofauti kubwa kati ya mfanyabiashara anayetunza kumbukumbu na yule asiyetunza kumbukumbu kwani asiyetunza kumbukumbu kwa mauzo ya shilingi milioni 14 atalipa kodi shilingi 450,000 kwa mwaka wakati anayetunza kumbukumbu kwa mauzo hayo atalipa shilingi 320,000 kwa mwaka.

“Tukichukulia mfano wa wafanyabiashara wawili wenye mauzo ya shilingi milioni 14, lakini mmoja anatunza kumbukumbu na mwingine hatunzi kumbukumbu tunaona kwamba, kuna tofauti ya shilingi 130,000 kwa kuwa asiyetunza atalipa shilingi 450,000 na anayetunza kumbukumbu atalipa shilingi 320,000. Hivyo kuna umuhimu mkubwa sana wa kutunza kumbukumbu,” amesisitiza Masalla.

Meneja huyo wa Elimu kwa Mlipakodi amewaambia wafanyabiashara hao kuwa, nyenzo muhimu inayosaidia utunzaji wa kumbukumbu ni pamoja na Mashine ya Kielektroniki ya Kutolea Risiti (EFD) na kama mfanyabiashara hajafikia mauzo ya kutumia mashine ya EFD ambayo ni chini ya shilingi milioni 14 anashauriwa kutumia kitabu cha risiti za kuandika kwa mkono ambapo mfanyabiashara atakwenda na kumbukumbu hizo TRA kwa ajili ya kukadiriwa kodi.

Kwa upande wake mfanyabiashara wa mbao wilayani humo, Zakaria Manyilizu amesema kuwa, elimu aliyoipata ya utunzaji kumbukumbu za biashara ni nzuri hata hivyo ameiomba TRA kutoa elimu juu ya namna ya kutumia mashine za EFD kwani walio wengi hawana utalaamu wa kutumia mashine hizo.

“Kwa kweli tunaishukuru TRA kwa kutuletea elimu hii ya utunzaji wa kumbukumbu hapa wilayani Busega lakini sisi tulio wengi hatujui kutumia vizuri mashine za EFD hivyo ninaiomba TRA itufundishe namna ya kutumia mashine hizi ili na sisi tunufaike na faida za utunzaji kumbukumbu alizozieleza meneja wa TRA,” alisema Manyilizu.

Timu ya Maofisa wa kodi wakiongozwa na Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi Diana Masalla kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania wako Mkoani Simiyu katika Wilaya ya Busega na Bariadi ambapo wanakutana na wafanyabiashara mbalimbali kwa ajili ya kutoa elimu ya kodi ikiwa ni pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili wafanyabiashara hao.

Mwisho.

Waziri Lukuvi Aagiza Wananchi Wote Waliodhurumiwa Kulipwa Fidia.

$
0
0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi ameziagiza Halmashauri za Miji pamoja na watu wenye mashamba makubwa wahakikishe wanawalipa fidia Wananchi wote ambao hawajalipwa kwa muda mrefu tangu kufanyika kwa tathmini kwani wananchi wengi wamekuwa wakiishi ndani ya mashamba yao kwa muda mrefu na wakiamishwa hawalipwi fidia zao kwa miaka mingi na wengine kuondolewa bila kulipwa kabisa.

Waziri Lukuvi meyasema hayo alipofanya ziara Wilayani Handeni Mkoani Tanga wakati wa kusikiliza kero za wananchi katika uwanja wa Soko la zamani Chanika maarufu Nyerere Squre Katika mkutano huo Waziri wa Ardhi aliongozana na Mkuu wa Wilaya hiyo Godwin Gondwe akiwa pamoja na Mbunge wa Jimbo la Handeni Mhe. Omari Abdallah Kigoda na watendaji mbalimbali wa Halmashauri ya wilaya hiyo.

Kupitia kampeni yake ya "FUNGUKA KWA WAZIRI"   Mhe. Lukuvi amesikiliza kero za ardhi za wananchi zaidi ya 200 wa wilaya ya Handeni zilizowasilishwa kwake. Kampeni hiyo iliyoanza saa 4 asubuhi hadi saa 12 jioni ambapo wakazi wengi wa mji huo wamelalamikia suala la kulipwa fidia ndogo au kutokulipwa fidia zao kabisa.

Mh. Lukuvi amesema Halmashauri nyingi zimekuwa na pupa za kupanga viwanja bila kuwalipa wananchi fidia na hata ikitokea wakalipa fidia basi fidia itakuwa ndogo sana kwani kwa kufanya hivyo kutazidisha migogoro mingi ya ardhi isiyo ya lazima, hivyo amezitaka halmashauri kupitia upya madai ya wananchi na kuwalipa stahiki zao.

”Kwa kuwa hapa sasa mashamba mengi ya mji huu yamegeuka kuwa ni miji, lazima hawa watu muwafidie viwanja zaidi kuliko pesa kama wanataka pesa basi wauze wenyewe hivyo viwanja, hamuwezi kuwapa shilingi milioni tatu wakati nyinyi mnauza viwanja milioni kumi. Kumekuwepo na unyang’anyi na kuwalazimisha watu kupima viwanja kwa fidia kidogo. Na kwa mujibu wa sheria ya fidia kama hujamlipa mwananchi kwa miaka zaidi ya miwili basi inatakiwa ufanye tathmini upya”.   

Hata hivyo Mh.Lukuvi ameshangazwa na wingi wa migogoro ya Ardhi ambayo ilikwisha patiwa ufumbuzi wake na mingine ilikwisha tolewa hukumu na Mahakama lakini cha kushangaza bado wananchi wanacheleweshewa haki zao hivyo kuwaamuru Maafisa ardhi kuhakikisha wanashughulikia swala hilo haraka iwezekanavyo kwani asingependa kuona swala hilo likijirudia tena.

Mhe. Lukuvi amesema kuwa amebaini 90% ya Wananchi wa Handeni hawana uwelewa juu ya hatimiliki ya ardhi zao wanazomiliki kwani ameshangazwa sana kuona wengi wao hawafahamu mipaka ya maeneo yao hali inayopelekea kuzuka kwa migogoro ya mipaka hivyo amewaasa wananchi kuyafatilia maeneo yao na kuyapatia hati miliki ili kuyalinda na wavamizi kwani Hati ndio kielelezo namba moja kinachotambulika kisheria.

"Mimi kama Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ipo migogoro ambayo nina uwezo wa kuitafutia ufumbuzi kutokana na mamlaka niliyonayo na ndio maana nimeamua kuwa na kampeni ya Funguka kwa Waziri ili kusikiliza kero mbalimbali za Ardhi lakini hii migogoro ya mtu na mtu inatakiwa kutafutiwa ufumbuzi ndani ya ofisi zenu za ardhi au wilaya" Amesema Waziri Lukuvi.

Hata hivyo baada ya kusikiliza kero za wananchi Waziri Lukuvi ameahidi kuanzisha Baraza jipya la Ardhi na Nyumba la Wilayani Handeni kwani wananchi wamekuwa wakisafiri hadi Wilayani Korogwe kusikiliza mashauri yao jambo ambalo limekuwa na ucheleweshaji wa kusikiliza na kutatua kero za ardhi kwa wakati kwani ndio chanzo cha migogoro mingi Wilayani hapo.

Aidha, akifunguka mbele ya Waziri Bi. Telessa Petro Gumbo ambae ni mkazi wa Handeni amelalamikia uvamizi wa uliofanywa katika shamba lake ambapo amemuomba Waziri Lukuvi kuingilia kati swala lake la kutolulipwa fidia baada ya Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kulimega eneo lake na kupitisha barabara hali inayomlazimu kulipwa fidia ya eneo hilo.

Naye, Bi. Amina Ali Kiale ambae pia ni mkazi wa Handeni amemlalamikia Waziri lukuvi kwa baadhi ya watendaji wa Ardhi ambao sio waaminifu kushiriki katika vitendo vya kudhurumu ardhi kwa kuwacheleweshea hati zao kwa muda mrefu wanapokuwa wanazifatilia.

Katika kutoa shukurani kwa Mhe. Waziri, Mkuu wa Wilaya ya Handeni Godwin Gondwe amemshukuru Mh. Lukuvi kwa kitendo cha kuifanya programu hiyo ya FUNGUKA KWA WAZIRI katika Wilaya yake ya Handeni kwani imeweza kutatua migogoro ya ardhi iliyodumu muda mrefu na kuahidi kushughurikia migogoro iliyobaki katika ofisi yake ya Wilaya.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa October 25

Wapinzani Wapinga Mpango wa Nyuklia Rwanda

$
0
0
Nchi ya Urusi imeahidi kusaidia baadhi ya mataifa ya Afrika kujenga uwezo wake wa kutumia teknolojia ya nyukilia.

Hayo yamejitokeza katika mkutano baina ya Urusi na wakuu wa mataifa 40 ya Afrika uliomalizika huko Sochi nchini Urusi.

Rwanda ni miongoni mwa mataifa yanayotarajiwa kunufaika kwa ushirikiano huu. Hata hivyo,mpango huo umeanza kupata upinzani kutoka chama cha upinzani.

Kiongozi wa chama cha upinzani cha Green nchini Rwanda, Frank Habineza  amepinga mpango wa nchi yake kujenga kiwanda cha nyuklia kwa ushirikiano na Urusi akisema utakuwa na athari mbaya kwa wananchi.

Akizungumza na BBC, Habineza amesema wao hawakuunga mkono ushirikiano huo baina ya serikali ya Rwanda na Urusi kutokana na athari zake.

"Kulikuwa na mapatano ya Vienna kuhusu maswala ya nyuklia, na wakati huo huo Rwanda ilisaini mapatano mengine na Urusi kuanzisha kiwanda cha nyuklia hapa Rwanda. Mapatano ya Vienna yalikuwa kama kupalilia njia ya hayo ya Urusi kuanza kutekelezwa."

"Bungeni sisi hatukupigia kura mswada huo kwa sababu tuliona kwamba bado ni mapema kwa nchi ya Rwanda kujiingiza katika kuidhinisha matumizi ya nishati ya nyuklia kwa sababu sehemu zote kulikojengwa nyuklia kumekuwa na athari mbaya kwa wananchi na kwa mataifa yenyewe" amefafanua.

Muswada huo wa ujenzi wa nguvu za nyuklia ulipitishwa bungeni Rwanda ukipingwa na wabunge wawili pekee.

Lakini Serikali ya Rwanda inasema teknolojia ya nyuklia itaifaa kwa matumizi ya kutengeneza nishati, dawa na matumizi mengine ya amani.


-BBC

Waziri Mkuu: Biashara Kati Ya Tanzania Na Urusi Iratibiwe

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameutaka ubalozi wa Tanzania nchini Urusi uratibu mipango ya wafanyabiashara wa Urusi wanaokusudia kuja nchini kuwekeza kwa kuwaunganisha na Taasisi na Wizara husika ili waweze kuwekeza mitaji yao kwa kuzingatia maslahi ya Taifa.

Ametoa agizo hilo jana (Alhamisi, Oktoba 24, 2019) baada ya kugundua uwepo wa wafanyabiashara wengi wa Urusi wanakusudia kuja Tanzania kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji pamoja na kutafuta wafanyabiashara wa Kitanzania watakaoungana nao katika uwekezaji wanaokusudia kuufanya.

“Tayari miadi imekwishawekwa ya kuwakaribiasha wawekezaji wa Urusi kuja Tanzania kwa ushawishi wa kwangu mwenyewe pamoja na ushawishi wa wafanyabiashara wa Tanzania, hivyo nisingependa wafanyabiashara hao wasumbuliwe au kukatishwa tamaa katika kutimiza nia yao hiyo.” Waziri Mkuu alisisitiza.

Alisema Mkutano baina ya Wakuu wa nchi na Serikali kutoka Mataifa ya Afrika na Urusi uliomalizika jana Oktoba 24, 2019 ulilenga kujenga uhusiano mzuri zaidi katika nyanja mbalimbali hususani za kiuchumi.

Akizungumza baada kumalizika mkutano huo kwenye ukumbi wa Olympic Park wa Sochi nchini Urusi, Waziri Mkuu alisema Urusi imeutumia mkutano huo kueleza bayana maeneo ambayo wako tayari kushirikiana na Afrika katika kuwekeza kwa faida ya pande zote mbili.

Waziri Mkuu aliyataja maeneo hayo kuwa ni pamoja na uuzaji wa zana za kilimo kama vile matrekta, sekta ya mafuta na gesi pamoja na madini, Ujenzi wa miundombinu hasa reli, masuala ya elimu hasa utoaji wa nafasi za mafunzo nchini humo.

Alisema kwa upande wake Tanzania imejinadi vizuri ikIngozwa na yeye mwenyewe kwani alifanya mazungumzo na viongozi wa makampuni zaidi ya manane ya Urusi ili kuyashawishi yawekeze nchini na yote yalikubali kufika Tanzania mapema iwezekanavyo.

“Viongozi wa makapuni yote niliyopata nafasi ya kuzungumza nao wamesema wako tayari kuja nchini ili waweze kufanya mazungumzo na Serikali pamoja na wafanyabiashara wazalendo ambao wako tayari kuungana na wafanyabiashara hao katika kuwekeza nchini Tanzania.”

Waziri Mkuu alisema viongozi hao walimueleza maeneo ambayo wao wanaamini kuwa wanafanya vizuri na wangependa kupata kibali cha kuwekeza Tanzania baada ya mazungumzo yao na Serikali. Pia walieleza ni kwa namna gani Taifa litanufaika na uwekezaji wao.

Alisema, tayari wafanyabiashara binafsi 18 wa Tanzania walijitokeza kushiriki katika Mkutano huo na walifanya kazi kubwa na nzuri ya kuwahabarisha wenzao wa Urusi kuhusu mazingira mazuri ya kuwekeza yaliyopo nchini hasa baada ya Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais, Dkt. John Pombe Magufuli kuondoa kero, kanuni na taratibu ziliokuwa zikiyafanya mazingira ya uwekezaji kuwa magumu.

Awali, akizungumza kwenye Mkutano baina ya Wakuu wa nchi na Serikali kutoka mataifa ya Afrika na Urusi, Waziri Mkuu alisema kwa sasa Tanzania ni nchi sahihi kwa uwekezaji kwa wanaotaka kuwekeza barani Afrika kwani imedhamiria kukuza uchumi wake na kufikia wa kati ifikapo 2025 kwa kupitia sekta ya viwanda. Pia ni nchi yenye amani na utulivu.

 “Nchi yetu imejaliwa kuwa na maliasili nyingi ambazo vilele ni malighafi kwa viwanda kama vile mazao ya kilimo, misitu, bahari, maziwa, madini na mbuga za wanyama ambazo ni kivutio cha watalii,” alifafanua Waziri Mkuu.

Leo Oktoba 25, 2019 Mheshimiwa Majaliwa ataondoka nchini Urusi kwenda nchi ya Azerbaijan ambako pia atamwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika Mkutano wa Nchi zisizofungamana na upande wowote. Mkutano huo ni wa siku mbili.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Serikali Yaelekeza Kukamilika Kwa Ujenzi Wa Kiwanda Ili Kukuza Soko La Mifugo Nchini

$
0
0
Na. Edward Kondela
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel ameuelekeza uongozi unaosimamia ujenzi wa kiwanda cha kusindika nyama cha Eliya kinachojengwa katika Wilaya ya Longido Mkoani Arusha kuhakikisha unakamilisha ujenzi wa kiwanda hicho mapema mwanzoni mwa mwaka 2020 ili kiweze kuleta tija kwa taifa na wafugaji wanaoishi katika Mkoa wa Arusha, mikoa ya jirani na nchi ya jirani ya Kenya.

Prof. Gabriel amesema hayo jana (24.10.2019) mara baada ya kutembelea ujenzi wa kiwanda hicho akiwa pamoja na uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido na kukuta tayari ujenzi wa kiwanda umefikia asilimia 90 ambapo mitambo mbalimbali imeanza kufungwa katika kiwanda ambacho kitakuwa na uwezo wa kuchinja ng’ombe 500 kwa siku na mbuzi takriban Elfu Mbili kwa siku.

Katibu mkuu huyo ametoa wito kwa wadau wa mifugo kujipanga vizuri namna ya kutumia fursa ya uwepo wa kiwanda hicho ili wafugaji na wafanyabiashara waweze kuuza mifugo katika kiwanda hicho ambacho kitaongeza ajira na kukuza sekta ya mifugo nchini.

Awali akizungumza na wakuu wa idara na vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Wilaya ya Longido kabla ya kutembelea ujenzi wa kiwanda hicho, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel amepokea maoni ya namna ya kudhibiti vitendo vya kutorosha mifugo mipakani hali inayochangia kuikosesha serikali mapato ambapo elimu imesisitizwa kwa watu wanaoishi mipakani.

Prof. Gabriel amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi inazidi kuchukua maoni ya namna ya kuhakikisha vitendo vya utoroshaji wa mifugo hususan katika mpaka wa Namanga ambao ni kati ya mipaka ya nchi za Tanzania na Kenya vinadhibitiwa ili kuhakikisha mapato ya serikali hayapotei pamoja na kusimamia  viwanda vya kusindika nyama kikiwemo cha Eliya kinachotarajia kukamilika mapema mwaka 2020 kinapata mifugo ya kutosha kutoka Mkoa wa Arusha na mikoa ya jirani ili kusindika nyama katika kiwanda hicho.

Mwisho.

Mahakama Kuu Yakubali ACT- Wazalendo Kujiunga Kwenye Kesi Kuhusu Ukomo Wa Urais

$
0
0
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imekubali ombi la Chama cha ACT-Wazalendo kujiunga kama washtakiwa kwenye kesi ya kikatiba iliyofunguliwa na Dezydelius Mgoya, maarufu kama Mkulima, kuhusu ukomo wa urais.

Uamuzi huo ulitolewa jana na Jaji Dk. Benhaj Masoud baada ya kusikiliza maombi ya ACT-Wazalendo kujiunga na kesi hiyo kwa sababu wana maslahi nayo.

Wakili wa ACT-Wazalendo, Jebra Kambole, alidai kuwa mteja wake ameomba kujiunga kwa sababu ni chama kilichosajiliwa na kimeshiriki katika uchaguzi.

Pia alidai kuwa chama hicho kina wanachama Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar kwa mujibu wa matakwa ya kisheria na kikatiba.

Mgoya alifungua kesi hiyo chini ya kifungu cha 4 cha sheria ya utekelezaji haki na wajibu, sura ya 3 ya mwaka 1994 chini ya Ibara ya 30(3) ya Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.

Kwa mujibu wa hati ya madai ya kesi hiyo, Mgoya anahoji Ibara ya 40(20) ya Katiba ambayo imeweka ukomo wa mihula miwili tu ya miaka mitano mitano ya uongozi katika nafasi hiyo ya urais.

Hivyo anaiomba mahakama hiyo itoe tamko na tafsiri ya maana sahihi na athari za masharti ya ibara hiyo.Pia anaiomba mahakama itoe tafsiri ya maana dhahiri ya masharti ya Ibara ya 42(2) ya Katiba kwa kuhusianisha na masharti ya Ibara za 13, 21 na 22 za Katiba hiyo.

Kadhalika, Mgoya anaiomba mahakama itoe tafsiri ya maana ya Ibara hiyo ya 40(2) kwa kuhusianisha na Ibara ya 39 ya Katiba.

Credit:Nipasahe

Nafasi 100 za Kazi Zilizotangazwa Wiki Hii......Tazama Hapa

$
0
0
Hapa nimekuwekea mkusanyiko wa Nafasi mbalimbali za Kazi Zilizotangazwa Wiki Iliyopita na Wiki Hii. Usisahau kushare na rafiki yako anayetafuta kazi
  1.  Job Opportunity​ at CRDB Bank | Senior Specialist; Financial Literacy
  2. Job Vacancy at CRDB Bank | Manager; Strategic Partnership
  3. New Government Job | Senior Corporate Communications Officer II at UCSAF
  4. Job Vacancy at Precision Air | Reservation & Ticketing Sales Agent
  5. Job Vacancy at Precision Air | Sales Manager Northern & Lake Zone
  6.  Job Vacancy at Standard Chartered Bank | Credit Analyst, Global Subsidiaries
  7. New Job Opportunity | Sales Capability Manager – Serengeti Breweries Limited
  8. New Job Opportunity | Marketing Manager, Spirits – Serengeti Breweries Limited 
  9. Nafasi 61 za Kazi Shirika la Hifadhi ya Taifa TANAPA | Elimu ni Kuanzia Cheti/Diploma/Degree | Mwisho Tarehe 30 Mwezi Huu 
  10. Jobs at UNICEF | Individual Consultant -Evaluation of the Zanzibar Social Protection Policy  
  11. Project Finance Assistant Job at Sightsavers Singida, Tanzania
  12. Project Assistant Job at Sightsavers Singida, Tanzania 
  13. Compliance Manager at IntraHealth International Mwanza, TZ 
  14. Research and Innovation Hub Coordinator Job at International Rescue CommitteeDar es Salaam, TZ 
  15. Electrical Manager Job at Radar Recruitment Tanzania 
  16. Job Opportunity at VodacomTanzania, Network Director 
  17. Monitoring, Evaluation, and Learning (MEL) Team Lead – Tanzania PS3+ 
  18. Job Opportunity at Abt Associates, Communications Team Lead 
  19. Jobs in Tanzania 2019 : New Job Opportunities at Mom Easy Company Limited | Sales Officers (15 Post) 
  20. Job Opportunity at Bariadi District Council | Mtendaji wa Kijiji Daraja la III 
  21. Jobs in Tanzania 2019: New Job Vacancies at Oxfam Tanzania| Donor Contracts Coordinator (INT5881) 
  22. Jobs in Tanzania 2019: New Job Vacancies at Oxfam Tanzania| Warehouse Officer (INT5995) 
  23. Technical Manager Job at Mbeya Water Supply and sanitation Authority 
  24. Job Opportunity at PCI Tanzania ,Documentation Specialist 
  25. Job Opportunity at Pact Tanzania,Gender and Youth Officer 
  26. Job Opportunity at Pact Tanzania, Technical Services Coordinator-Case Management 
  27. Job Opportunity at Pact Tanzania, Technical Services Coordinator-Bi-Directional Referrals and Linkages 
  28. Job Opportunity at Pact Tanzania, Logistic Assistant/Driver 
  29. Field Assistant Grade Ii Job at Tropical Pesticides Research Institute TPRI 
  30. Job Opportunity at UONGOZI Institute, Research And Policy Department (Intern) 
  31. Job Opportunity at UONGOZI Institute, Finance And Administration Department (Intern)

==Kwa nafasi zingine za Kazi zaidi ya 5000, <<INGIA HAPA>.

Serikali yaagiza waliokimbia na Bilioni 1.2/= za Wakulima Mtwara wakamatwe

$
0
0
Na Mwandishi Wetu
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ameliagiza Jeshi la Polisi Mkoani Mtwara kuwakamata  Viongozi wa Vyama vya Msingi vya Ushirika wanaotuhumiwa kukimbia na  Kiasi cha Shilingi Bilioni 1.2/= za wakulima ambazo ni madeni ya Korosho.

Ametoa kauli hiyo leo wakati akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Newala  katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika Viwanja vya Stendi Kuu baada ya kupokea Ripoti ya Jumla ya Madeni wanayodai wakulima katika Wilaya za Mtwara, Masasi, Nanyumbu, Newala na Tandahimba.

“Nilivyofika hapa Mtwara jambo la kwanza lilikuwa kumuuliza Kamanda wa Polisi wa hapa juu ya utekelezaji wa agizo la Mheshimiwa Rais alilolitoa siku za hivi karibuni alipokuwa ziara na kuagiza kukamatwa kwa viongozi wawili wa vyama vya msingi vya  ushirika  wanaodaiwa fedha za korosho na wakulima, ameniambia walitekeleza agizo na hao viongozi  wawili tayari wameanza kulipa hizo fedha,” amesema Masauni

Akizungumza baada ya kupokea ripoti ya madeni kwa Wilaya zote za Mkoa wa Mtwara Naibu Waziri Masauni amelitaka Jeshi la Polisi kuwakamata viongozi wengine katika wilaya zilizobakia za Mtwara, Newala, Masasi, Nanyumbu na Tandahimba ambazo katika taarifa ya jumla ya mkoa inaonyesha takribani Shilingi Bilioni 1.2 bado zinadaiwa na wakulima hao kutoka kwa viongozi wa vyama hivyo.

“Mheshimiwa Rais kwenye ziara yake aliishia wilaya ya Masasi lakini katika ripoti hapa inaonyesha katika wilaya zingine wakulima pia wanadai fedha zao ambacho ni kiasi kikubwa,nakuagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara kuwakamata viongozi wengine katika wilaya zilizobakia na hakikisha kiasi hicho cha fedha cha wakulima hao kinalipwa,” amesema Masauni

Katika taarifa hiyo iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara,Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Blasius Chitanda inaonyesha jumla ya Vyama vya Ushirika 61 bado vinadaiwa na wakulima katika wilaya za Mtwara, Masasi, Tandahimba na Newala kuanzia Msimu wa Korosho wa Mwaka 2015/2016 hadi 2017/2018.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mkutano huo baadhi ya wakulima wanaodai fedha zao waliiomba serikali kuhakikisha wanalipwa haki yao kwani madeni hayo yamechukua muda mrefu hali inayopelekea kuzorotesha shughuli zao za kuchumi huku familia zao zikipata taabu kutokana na fedha zao kutopatikana kwa wakati.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images