Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Wimbo wa Rose Muhando - Wanyamazishe Bwana

$
0
0
Wimbo wa Rose Muhando - Wanyamazishe Bwana

Waziri Mkuu: Tunahitaji Watumishi Waaminifu

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli inahitaji watumishi waadilifu wenye uwezo wa kufanyakazi kwa uaminifu na waliotayari kuwahudumia wananchi wote bila ya ubaguzi.

Amesema Serikali inataka kuona watumishi wa umma wakitumia taaluma zao katika kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabili wananchi kwenye maeneo yao hususani wa vijijini, hivyo amewataka watenge muda wa siku nne kwa ajili ya kukutana nao.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Alhamisi, Septemba 26, 2019) wakati akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Mufindi na Halmashauri ya Mji wa Mafinga pamoja na Madiwani kwenye mkutano uliofanyika Halmashauri ya Mufindi.

Amesema watumishi hao wanapaswa kutekeleza matakwa ya ilani ya CCM, ambayo imeainisha kila kitu kinachotakiwa kufanyika katika halmashauri, hivyo wakuu wa idara hawanabudi kuisoma kwa makini ili waweze kupata mafanikio kwenye utendaji wao.

Waziri Mkuu amesema ni lazima watumishi hao wafanye kazi za Serikali na waache itikadi zao watekeleze ilani ya CCM. “Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri hakikisheni wakuu wa idara na wasaidizi wao wanawahudumia wananchi.”

“Tuelewane vizuri hapa, msimamo wa Serikali hii ni kuchapakazi mtu atakaye vurugavuruga hana nafasi katika Serikali hii na hatuta muundia tume tutamalizana naye hapo hapo. Rais wetu anataka kuona wananchi wakihudumiwa katika maeneo yao.”

Hata hivyo, Waziri Mkuu amezitaka halmashauri nchini zinapotoa huduma zihakikishe zinapotoa huduma kwa wananchi wasisahau kutenga asilimia 10 ya mapato yao kwa ajili ya makundi maalumu kama wanawake, vijana na wenye ulemavu.

Pia, Waziri Mkuu amewataka watendaji hao kutofanyakazi kwa mazoea, ambapo amemtaka Mhandisi wa Maji wa Wilaya ya Mufindi kuhakikisha anasimamia vyanzo vyote vya maji na kuwachukulia hatua watu wote wanaolima au kufanya shughuli katika vyanzo vya maji. Amesema kata ya Igowole iwe imepata maji ifikapo 2020.

Katika hatua nyingine,Waziri Mkuu amesema suala la ukusanyaji wa mapato limepewa kipaumbele na Serikali kwa sababu linasaidia katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo. “Madiwani msimamie ukusanyaji mapato na hakuna kumlinda mtu anayetafuna fedha hizo.”

Amesema watendaji nao wahakikishe wanawasimamia vizuri mawakala waliopewa zabuni za ukusanyaji wa mapato na watakaobainika kushindwa kutekeleza vizuri jukumu hilo wasipewe tena zabuni na badala yake watafutwe wazabuni watakaokusanya vizuri.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Joseph Kandege amesema utendaji wa kazi katika hospitali ya wilaya ya Mufindi si wa kuridhisha hasa siku za Jumamosi, amewataka watumishi wabadilike kwani huduma zinatakiwa wakati wote.

Awali,Mbunge wa Mafinga Mjini, Cosato Chumi amesema hali ya upatikanaji wa huduma za afya katika halmashauri ya Mji wa Mafinga si ya kuridhisha kutokana na uhaba wa watumishi kwani waliopo ni 204 huku mahitaji yakiwa 310. Waziri Mkuu amesema suala hilo linafanyiwa kazi, Serikali inaendelea kuajiri.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Happi amesema halmashauri za wilaya ya Mufindi na Halmashauri ya Mji wa Mafinga zinafanya vizuri katika sula zima la ukusanyaji wa mapato pamoja na kutenga asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya wanawake, vijana na wenyeulemavu.

Akizungumzia kuhusu hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Mafinga amesema inachangamoto ya utoaji wa huduma kwa sababu ya kuhudumia halmashauri mbili ya Mufindi na Mafinga lakini mgawo wa dawa wanaopewa ni kwa ajili ya wakazi wa Mafinga pekee.

Pia, Mkuu wa mkoa ametumia fursa hiyo kuishukuru Serikali kwa kupeleka zaidi ya sh. bilioni saba katika wilaya hiyo kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye Halmashauri ya wilaya ya Mufindi na Halmashauri ya Mji wa Mafinga.

Baada ya kuzungumza na watumishi, Waziri Mkuu amekagua na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa hospiyali ya wilaya ya Mufindi inayojengwa katika Kijiji cha Nzivi kata ya Igowole. Ujenzi wa hospitali hiyo utagharimu sh. bilioni 1.5 na upo katika hatua za umaliziaji.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Naibu wa Waziri wa Afya Dkt.Ndungulile: JAMAFEST Iwe Kichocheo Ulaji Vyakula vya Asili, Kulinda Afya

$
0
0
Na. Paschal Dotto – Maelezo, Dar es Salaam.
Naibu wa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Faustine Ndungulie ametembelea Maonesho ya Tamasha kubwa la Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki (JAMAFEST) na kusisitiza wananchi kutumia zaidi vyakula vya asili ili kupunguza uwezekano wa kupata magionjwa yasisyo ya kuambukiza. 


Dkt. Ndungulie amesisitiza utumiaji wa vyakula vya asili baada ya kutembelea Tamasha hilo jana Septemba 25, 2019 ambapo pamoja na mambo mengine alijionea vitu mbalimbali vikiwemo vyakula vya asili na kuwataka Watanzania kujifunza jinsi ya kutumia kuandaa na kutumia vyakula hivyo ambavyo havina madhara katika mwili. 


“Katika Tamasha hili Watanzania wanapaswa kujifunza njia za asili katika kuandaa chakula ambacho kinaweza kuwasaidia kulinda afya zao”, alieleza Naibu Waziri na kutoa mfano wa kuwepo kwa usindikaji wa chakula na mafuta ya asili yanayotokana na matunda. 


Amesema kuwa masuala ya michezo, sanaa na utamaduni yana uhusiano mkubwa na afya na kuwashauri wasanii kutumia Sanaa kuongelea masuala ya kuimarisha afya kkwa kuwasisitiza wananchi kula chakula bora na kufanya mazoezi ili kufikisha ujumbe kwa Jamii kuhusiana na ulaji bora wa chakula. 


Kwa mujibu wa Dkt. Ndungulile, asilimia 30 ya watoto chini ya miaka mitano wana utapiamlo na wamedumaa huku asilimia 10 ya watu wazima wakiwa na lishe iliyopitiliza (vitambi) na asilimia 30 wanapatwa na magonjwa yasiyo ambukizwa ambayo mengi yanatokana na vyakula visivyo bora. 

Kwa upande mwingine Naibu Waziri Ndungulile ameipongeza Wizara ya Habari, UtamaDUNI, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kuandaa Tamasha hilo kwa mafanikio ambapo washiriki kutoka nchi tano za Jumuiya ya Afrika Mashariki zimeshiriki. Nchi hizo ni wenyeji Tanzania, Burundi, Kenya, Rwanda na Uganda. 

JAMAFEST ni Tamasha la Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki ambalo lilipitishwa katika kikao cha 20 na 23 cha Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kilichofanyika mwezi Machi na Septemba 2012.  

Tamasha hili hufanyika mara moja kila baada ya miaka miwili na huzunguka katika nchi wanachama wa EAC. Mpaka sasa Tamasha limekwishafanyika katika nchi za Rwanda (2013) na kuhudhuriwa na washiriki 17,500, Kenya (2015) washiriki 21,000 na Uganda (2017) washiriki 42,600 na sasa linafanyika nchini kuanzia Septemba 21 - 28, 2019.

MWISHO 

Uteuzi Mpya Uliofanywa Na Rais Magufuli Leo

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Leonard Chamriho kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Uwekezaji wa Mapato ya Mafuta na Gesi (Portfolio Investment Advisory Board).

Dkt. Chamriho ni Katibu Mkuu wa Uchukuzi katika Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Pamoja na uteuzi wa Mwenyekiti, Rais Magufuli amewateua wajumbe wanne wa bodi hiyo ambao ni;
  1. Casmir Sumba Kyuki (Katibu Mtendaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria).
  2.  Dkt. Suleiman Magesa Missango (Mkurugenzi wa Utafiti wa Uchumi na Sera wa Benki Kuu ya Tanzania – BOT).
  3.  Safiel Fahamuel Msomvu (Kaimu Meneja Uwekezaji wa Shirika la Maendeleo ya Petrol Tanzania – TPDC).
  4.  Dkt. Mussa Daniel Budeba (Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam – UDSM).
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Dkt. Chamriho na Wajumbe hao umeanza tarehe 25 Septemba, 2019.

Kiboko Ya Maumbile Madogo Na Nguvu Za Kiume

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0673878343

watsap +255 0620510598

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Askari wawili JWTZ Wafariki kwa Ajali....20 Wajeruhiwa

$
0
0
Askari 2 wa JWTZ kikosi cha 24 KJ Kigoma,wamefariki na 20 kujeruhiwa katika  ajali iliyotokea Mkoani Katavi baada ya gari la jeshi lililokuwa limebeba askari kupinduka eneo la Hifadhi ya Taifa ya Katavi.

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Kigoma Maweni, Lameck Mdengo amethibitisha vifo hivyo na kupokea majeruhi hao na kuwataja waliofariki ni Bakari Mohammed (38) na Rashid Mwimbe (28).

Majeruhi wengine wanaendelea kupatiwa matibabu hospitalini hapo.

Uteuzi Mwingine Uliofanywa na Rais Magufuli Jioni Hii


NIDA Yapanua Wigo wa Kupata Namba ya Utambulisho wa Taifa..Tazama Hapa

$
0
0
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imewarahisishia  wananchi kwa kuweka utaratibu mpya wa kuipata namba ya utambulisho wa Taifa (NIN)  kwa njia ya mtandao.

Taarifa iliyotolewa na Nida jana Jumatano Septemba 25, 2019 kupitia kitengo cha mawasiliano na hifadhi hati ilisema namba hiyo sasa imeanza kutolewa kupitia tovuti ya mamlaka hiyo kwa muombaji kutembelea https://services.nida.go.tz/nidpotal/get_nin.aspx

Taarifa ya Nida ilibainisha kwamba huduma hiyo itawarahisishia waombaji wa vitambulisho vya Taifa kupata NIN bila kwenda ofisi za mamlaka hiyo.

Hatua za kufuta kupata namba ya NIN

1.Bonyeza kitambulisho cha Taifa

2.Fahamu namba ya utambulisho wa Taifa

Andika jina lako la kwanza, jina la ukoo, tarehe ya kuzaliwa, jina la kwanza la mama na jina la mwisho la mama

3.Bonyeza Tafuta

Wagonjwa Waliopelekwa Na Polisi Muhimbili Watafuta Nduguzao

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO . Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,KUSAFISHA NYOTA, Mvuto wa Mwili na BIASHARA, ...MIGUU Kufa GANZI na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Wagonjwa Waliopelekwa Na Polisi Muhimbili Watafuta Nduguzao

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa September 27

Waziri Mkuu: Fedha Za Ndani Zijenge Miradi Ya Kimkakati

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Mufindi na Halmashauri ya Mji wa Mafinga wahakikishe wanajenga mradi wa kimkakati kwa kutumia fedha za mapato ya ndani na si kusubiri miradi kutoka Serikali Kuu wakati wanakusanya zaidi ya sh. bilioni saba kwa mwaka.

Amesema halmashauri hizo licha ya kukusanya fedha nyingi kwa mwaka lakini matumizi yake si mazuri kwa sababu hawana mradi wowote wa kimkakati wanaoutekeleza, mfano ujenzi wa maeneo ya kuegeshea magari makubwa au hata ujenzi wa kituo cha mabasi, miradi ambayo ingewaongezea mapato.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana jioni (Alhamisi, Septemba 26, 2019) wakati akihutubia na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Wambi wilayani Mufindi akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Iringa.”Nataka kuona mradi wa kimkakati ukitekelezwa kwa fedha mnazokusanya kutoka kwa wananchi.”

Alisema viongozi hao wanaweza kutenga kiasi cha sh. bilioni moja kwa mwaka na kujenga hospitali au wakatenga fedha na kujenga barabara za lami kwa awamu katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga kwa kuwa ujenzi wa barabara za lami mijini ni sh. milioni 300 kwa kilomita moja, hivyo wangeweza kutekeleza ujenzi huyo kutokana na fedha wanazokusanya.

“Msitegemee fedha kutoka Serikali Kuu tu jengeni wenyewe barabara zenu kuzunguka Mji wa Mafinga kwa kiwango cha lami kwa sababu mna fedha za kutosha tena mnaweza kutumia fedha za mapato ya ndani mnazokusanya kutoka kwa wananchi badala ya kuzitumia kwa kulipana posho tu.”

Awali,Waziri Mkuu alitembelea shule ya Sekondari ya kata ya Mdabulo na kupokea taarifa fupi ya ujenzi wa bwalo, bweni kwa ajili ya wanafunzi wa kike pamoja na ujenzi wa madarasa na kisha alizungumza na wananchi na kuwaeleza miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali kwenye maeneo yao.

Waziri Mkuu alisema katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya karibu na maeneo yao ya makazi, Serikali inatekeleza mradi wa ujenzi wa vituo vya afya katika kila kata pamoja na ujenzi wa hospitali za wilaya ikiwemo na wilaya yao ya Mufindi ambayo ipo katika hatua mwisho kukamilika.

Kwa upande wao, wabunge wa mkoa wa Iringa wakiwemo wa majimbo na wa viti Maalumu kwa nyakati tofauti waliishukuru Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli kwa kutoa fedha za ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye mkoa wao.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Makundi Na Kutegeana Kumechelewesha Miradi Kukamilika Momba

$
0
0
Uwepo wa makundi yasiyo na tija, kutegeana katika kazi na kutoshirikiana baina ya watumishi kumesababisha miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika halmashauri ya Wilaya ya Momba kuchelewa kukamilika.

Hayo yamebainishwa jana na baadhi ya watumishi wa Halmashauri hiyo walipokuwa wakizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela alipokutana nao kutaka kufahamu sababu za kutokamilika kwa wakati ujenzi wa miradi mbalimbali katika halmashauri hiyo.

Mmoja wa watumishi amesema, “unapokuwa na mradi wa sekta fulani mfano afya, kilimo au elimu watumishi wenzako wanakaa pembeni hawakusaidii, ni kama wanakutegea waone utakavyoshindwa kitu ambacho sio sahihi, miradi yote ni ya halmashauri na inalenga kuwanufaisha wananchi wote.”

Watumishi hao wamesema baada ya kuzungumza na Mkuu wa Mkoa wameona kuwa makundi na kutoshirikiana havitaijenga halmashauri na hivyo wameapa kubadilika na kufanya kazi kwa pamoja kama timu moja.

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela amesema anaamini tatizo la kutoshirikiana baina ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Momba limeisha na watafanya kazi kwa pamoja.

Brig. Jen. Mwangela ameongeza kuwa mara baada ya kikao hicho ameona ushirikiano wa watumishi katika ujenzi wa Soko la Mazao la Kakozi ambapo wote kwa pamoja wameonyesha nia kufanikisha ujenzi huo kwakuwa umesha chelewa kwa zaidi ya miezi sita.

Naye Msimamizi wa Ujenzi wa soko la mazao la Kakozi Aloyce Sakaya amesema kwa sasa mradi huo utatekelezwa kwa kasi zaidi kwakuwa changamoto zilizo sababisha ukachelewa ikiwa ni pamoja na kutoshirikiana baina yao zimeondolewa.

Balozi Sokoine Amuwakilisha Waziri Simbachawene Kuzindua Mfumo Wa Ukusanyaji Takwimu Za Gesijoto

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Balozi Joseph Sokoine amezindua Mfumo wa Kitaifa wa Ukusanyaji Takwimu za Gesijoto, Ufuatiliaji, Uandaaji Taarifa na Uhakiki katika Ukumbi wa Kituo cha Kuratibu Hewa Ukaa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) mkoani Morogoro.

Akizindua mfumo huo kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa ais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene, Balozi Sokoine alisema kuwa utawezesha nchi kukusanya takwimu za gesijoto kutoka sekta mbalimbali kwa ajili ya kuchukua hatua stahiki na maamuzi.

Pamoja na mambo mengine alisema pia utasaidia kuandaa taarifa mbalimbali ambazo nchi inatakiwa kuandaa kama Mwanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi ambazo zinabainisha kiasi cha uzalishaji wa gesijoto kutoka sekta mbalimbali husika na uondoshaji wake kupitia misitu.

Balozi Sokoine aklibainisha kuwa hadi sasa Tanzania imeandaa taarifa mara mbili na kuwasilisha Sekretareti ya Mkataba mwaka 2003 na ya pili mwaka 2015 na kwa muda wote Tanzania kama ilivyokuwa kwa nchi nyingine.

Aliongeza kuwa Tanzania imetumia wataalamu elekezi kufanya kazi hii chini ya Mradi uliokuwa unatekelezwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) kuratibiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais Idara ya Mazingira hivyo kuleta ugumu katika kuthibiti ubora na kulinganisha takwimu za nchi mbalimbali kwani hakukuwa na mfumo au njia iliyokubalika kimataifa kufanya kazi na haikujenga uwezo wa sekta husika.
"Mfumo wa Kitaifa wa ukusanyaji na usimamizi wa Takwimu za gesijoto, unaozinduliwa leo utawezesha nchi kutoa  takwimu sahihi na za kutosheleza kuhusu uzalishaji wa gesijoto kutoka sekta mbalimbali husika na uondoshaji kwa njia ya misitu, kwa hatua sahihi za uamuzi na kutoa taarifa," alisema.

Aidha Balozi Sokoine alisema kuwa uzinduzi wa Mfumo huu umekuja wakati muafaka ambapo tunajipanga kuanza utekelezaji wa Makubaliano ya Paris ambayo yalipitishwa na Mkutano wa 21 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabinchi na Tanzania kuridhia Mei 2018.

Aliongeza kuwa kwa sasa Tanzania inakamilisha maandalizi ya Mchango wake katika juhudi za kupambana na Mabadiliko ya Tabianchi hivyo Mfumo huo utasadia katika upatikanaji wa takwimu na taarifa kuhusu utekelezaji wa NDCs na uandaaji wa Taarifa ya Tatu ya Mawasiliano.

" Utekelezaji wa Mfumo huu utahitaji kila mdau kubaini majukumu yake na kuyatekeleza na hivyo kila mdau anatakiwa kubaini majukumu yake kama yalivyobainishwa katika Mfumo ili  kuhakikisha kuwa Mfumo huu unatekelezwa na hivyo kutuwezesha kufikia malengo tarajiwa," alisisitiza Balozi Sokoine.

Naibu Katibu Mkuu aliagiza Kituo Cha Kitaifa cha Kuratibu Hewa Ukaa (NCMC) kuratibu na kusimamia mfumo wa Kitaifa wa Ukusanyaji Takwimu za Gesijoto, Ufuatiliaji, Uandaaji Taarifa na Uhakiki.

Aliagiza Wizara za Kisekta ziteue Wataalamu watakaohusika na usimamizi na uandaaji wa takwimu za uzalishaji wa gesijoto katika sekta zao na kuwasilisha kwenye Kituo cha Kitaifa cha Kuratibu Hewa Ukaa.

Pia aliagiza Wizara za Kisekta kwa kushirikiana na Kituo cha Kitaifa cha Kuratibu Hewa Ukaa ziweke Utaratibu wa kuwasilisha taarifa katika Kituo cha Kitaifa cha Kuratibu Hewa Ukaa kila mwaka.na kubainisha watoaji takwimu chini ya sekta zao za uzalishaji wa gesijoto na kuweka utaratibu wa kupata takwimu hizo.

Waziri Lugola Asema Serikali Itaendelea Kufuata Misingi Ya Kidemokrasia Kwa Kuzingatia Na Kulinda Haki Za Binadamu.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Kangi Lugola amesema kuwa serikali ya Tanzania  imekuwa  ikijidhatiti katika kufuata Misingi ya Kidemokrasia kwa kuzingatia na kulinda na kutetea haki za Binadamu.

Waziri lugola ameyasema hayo Septemba 26,2019  Jijini Dodoma wakati akizindua Ofisi ya kituo cha sheria na haki za Binadamu LHRC,ambapo amesema katika kuyatekeleza hayo  kwa vitendo serikali ya  Tanzania ni miongoni mwa nchi chache zenye katiba ambazo ndani mwake zimeonesha bayana masuala ya haki za binadamu na Utawala Bora.

Hata hivyo,waziri lugola amesema serikali imetoa fursa kwa Asasi za  kiraia kuanzishwa na kufanya kazi ya kuwajengea wananchi uwezo juu ya masuala mbalimbali ya kiraia ikiwemo sheria , haki za binadamu na uwajibikaji .

 Katika hatua nyingine Waziri Lugola amesema ujio wa Kituo cha sheria na haki za binadamu (LHRC) Jijini Dodoma ni fursa kwa wanachi wa Dodoma na mikoa ya kanda ya kati kwa ujumla .

Akisoma Hotuba mbele ya Mgeni Rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Bi Anna Henga amesema kituo hicho kimekuwa kikifanya tafiti mbalimbali hususan masuala ya Haki za Binadamu.

Sanjari na hayo Bi Henga amesema kuanzishwa kwa ofisi jijini Dodoma imetokana na msukumo usio zuilika wala kukwepeka wa kudumisha mashirikiano hayo na serikali pamoja na Bunge.

Uzinduzi wa ofisi hiyo unalenga  kudumisha mahusiano ya kikazi baina ya taasisi za kiserikali  kama vile Bunge na mahakama hasa ukizingatia  kuwa taasisi zote za kiserikali zimeshahamia Jijini hapa kufuatia dhamira ya dhati ya serikali  ya awamu ya tano ya kuifanya Dodoma kuwa makuu ya Nchi .

Kituo cha kisheria na haki za Binadamu ni Asasi ya kiraia  isilofungamana na itikadi zozote za kisiasa hivyo imekuwa ikitetea watu wote bila kujali itikadi zozote.

Serikali Kubadilisha Kilimo Cha Kujikimu Kwenye Kahawa Kuwa Kilimo Cha Biashara

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Songwe
Serikali imepanga kubadilisha kilimo kutoka kuwa cha kujikimu na kuwa kilimo cha kibiashara kama ilivyoainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 kwa kuzingatia mazao ya kipaumbele.

Miongoni mwa mazao hayo ya kipaumbele ni kahawa ambapo katika mwaka wa fedha wa 2019/2020, Wizara ya Kilimo kupitia Bodi ya Kahawa imepanga kuongeza uzalishaji kutoka tani 65,000 hadi tani 80,000. Aidha bodi imepanga kuzalisha na kusambaza miche milioni 10 ya kahawa katika wilaya 42.

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameyasema hayo  tarehe 26 Septemba 2019 wakati akizungumza na watendaji wa Taasisi ya utafiti wa kahawa Tanzania (TaCRI) alipotembelea taasisi hiyo Mkoani Songwe.

Alisema kuwa zao hilo lina mchango mkubwa kwa uchumi wa Taifa na kwa maendeleo ya jamii lakini katika miaka ya karibuni lilionekana kuzorota kutokana na kuwapo kwa changamoto mbalimbali.

Kutokana na hali hiyo Serikali imeendelea kubuni mikakati mipya ya taratibu za usimamizi wa sekta hiyo ili kuleta ufanisi katika uzalishaji wa zao hilo.

Mhe Hasunga amesema kuwa ili kuongeza uzalishaji wenye tija katika zao la kahawa serikali imejipanga kuimarisha upatikanaji wa miche bora kwa ajili ya kuzisambaza kwa wakulima nchini.

Pia ameipongeza Taasisi hiyo kwa kutoa elimu kwa wakulima kuhusu matumizi sahihi ya mbegu bora za kahawa huku akisisitiza taasisi hiyo kuongeza weledi katika utoaji elimu kwa wakulima.

Naye, Mwenyekiti wa Taasisi ya utafiti wa kahawa Tanzania (TaCRI) Ndg Aloyce Mdalavuma ameiomba wizara ya Kilimo kwa ushrikiano na wataalamu mbalimbali wa TaCRI kuongeza juhudi ili kuongeza tija na uzalishaji wa kahawa.

Pia amesema kuwa uwezo wa Taasisi hiyo katika kuzalisha mbegu bora bado ni mdogo hivyo ameiomba serikali kuongeza uwezekano ili kuzalisha mbegu nyingi ambazo zitawafikia wakulima wengi.

Kwa upande wake Meneja wa kituo cha utafiti wa Kahawa Mkoani Songwe Ndg Isack Mushi ameeleza kuwa jukumu kuu la TaCRI ni kurudisha matumaini ya tasnia ya kahawa kwa kutoa na kusambaza teknolojia za kuendeleza zao la kahawa kwa ajili ya kuongeza tija katika uzalishaji na ubora.

Nyingine ni kupunguza gharama za uzalishaji, kuboresha kipato na riziki kwa wakulima wote wa kahawa na kuongeza mchango wa sekta ya kahawa kwenye pato la Taifa.

Marekani kupeleka wanajeshi 200 na mifumo ya ulinzi eneo la Ghuba

$
0
0
Mvutano kati ya Marekani na Iran huenda ukaongezeka baada ya Washington kutangaza kuwa inatuma vikosi zaidi vya kijeshi katika eneo la ghuba huku Tehran ikiitaka Saudi Arabia ithibitishe madai kuwa Iran iliishambulia miundombinu ya mafuta ya nchi hiyo.

Wizara ya Ulinzi ya Marekani imesema jana kuwa inapeleka wanajeshi 200 pamoja na mifumo ya kujilinda dhidi ya makombora ili kuimarisha ulinzi wa Saudi Arabia.

Uamuzi huo wa Marekani ambao unajumisha pia kupelekwa kwa rada nne za kijeshi unafuatia mashambulizi ya Septemba 14 kwenye miundombinu ya kuzalisha mafuta nchini Saudi Arabia.

Marekani, Ufaransa, Ujerumani, Uingereza na Saudi Arabia kila moja  zimeilaumu Iran kuhusika na mashumbulizi hayo. 

Iran kwa upande wake imekanusha madai ya nchi hizo na jana Alhamisi rais wa nchi hiyo Hassan Rouhani ametaka utolewe ushahidi kuthibitisha kuwa Tehran ilikuwa nyuma ya hujuma hizo.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na 
0747100745
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images