Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli amteua Rais Mstaafu Alhaji Ali Hassan Mwinyi, kuendelea kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS).


Gunia 515 Za Kahawa Ya Magendo Zakamatwa Mkoani Kagera Zikisafirishwa Kwenda Nchi Jilani Ya Uganda.

$
0
0
Na Avitus Benedicto Kyaruzi, Kagera.
Jeshi la Polisi Mkoani Kagera limekamata magendo ya kahawa katika kata ya Kemondo halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Mkoani Kagera

Hayo yamebainishwa na mkuu wa kituo cha polisi Bukoba mkoani Kagera  SSP Babusanare wakati akiongea na waandishi wa habari  na kusema kwamba mnamo tarehe 24 Septemba  mwaka huu askari waliokuwa doria walipata taharifa kuwa gari lenye usajili NO.T.205 DHX Mitsubishi Fuso lilikamatwa kwa kosa la kusafirisha kahawa bila kibali.

Ameongeza kuwa magendo hayo yalikamatwa  katika maeneo ya Bulila, Kata Kemondo, Halmashauri ya wilaya ya Bukoba mkoani Kagera ambapo yalikuwa yanapitia Mwalo wa Bilolo kemondo kuelekea nchini Uganda.

Bwana Babusanare amesema kuwa gari hilo lilikuwa na kahawa gunia 515 na kila gunia lina kilo 70  na kuongeza kuwa dereva wa gari iyo alitokomea kusiko julikana baada ya kuona anakamatwa na polisi na kuongeza kwamba jitihada za kumtafuta dereva huyo bado zinaendelea  na kusema kwamba watuhumiwa wote wamekamatwa na kufikishwa katika kituo cha polisi wilaya ya Bukoba kwa mahojianio zaidi.

Amewataja watuhumiwa waliokamatwa kuwa ni pamoja na Sadick Charles, Jonizius Gerad na Lazaro Mdesa.

Kwa upande wake Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Bukoba DC Deodatus Kinawilo amepongeza juhudi za jeshi la polisi kukamata gari hilo na kuhakikisha kila aliyehusika katika kusafirishwa kwa magendo hayo ya kahawa sheria inafuata mkondo wake na kuwawajibisha ipasavyo.

“Dolia hii iwe endelevu hasa katika maeneo mnayoyadhania yanaweza kuwa na makosa ili kutetea juhudi za Rais wetu Mh.Dk.John Pombe Magufuli kutokana na makosa yanayojitokeza katika kahawa maana watu kama hawa wanarudisha maendeleo nyuma hawatakiwi kuachwa kabisa” Alisema Kinawilo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi September 26

TCU Yafungua Dirisha la Awamu ya Nne ya Udahili

VIDEO: Rosa Ree X Spice Diana - Jangu Ondabe Remix

$
0
0
VIDEO: Rosa Ree X Spice Diana - Jangu Ondabe Remix

Waziri wa Maji Asitisha Vibali vya Ujenzi wa Miradi kwa Wakandarasi kwa Kukosa Uadilifu

$
0
0
Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa amesema kuanzia sasa amesitisha kutoa vibali vya ujenzi wa miradi ya maji kwa wakandarasi kutokana na wengi wao kuwa wadanganyifu katika makadirio ya gharama za utekelezaji wa miradi hiyo na kuisababishia Serikali mzigo mkubwa na kukwama kwa miradi mingi katika maeneo mbalimbali nchini.

Kauli imekuja akiwa ziarani mkoani Lindi akitembelea na kukagua ujenzi wa miradi ya maji katika Manispaa ya Mji wa Lindi na Halmashauri ya Wilaya ya Lindi katika kuhakikisha utekelezaji wa miradi hiyo inaenda kwa kasi na kukamilika kwa wakati.

Profesa Mbarawa amesema baada ya kutembelea miradi mingi ya maji amegundua tabia ya wakandarasi wengi wasio waadilifu kuweka gharama kubwa ili kupata faida kubwa, na kumfanya kuchukua uamuzi wa kusitisha vibali vya ujenzi kwa wakandarasi na kutoa kazi hizo kwa Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) pamoja na Mamlaka za Maji.

Akifafanua kuwa maamuzi hayo yamelenga kukomesha tabia hiyo ya wizi wa fedha za Serikali na kuokoa fedha nyingi zinazoweza kutumika katika utekelezaji wa miradi katika maeneo mengine mengi na pia kuipa nafasi Serikali kukamilisha ujenzi wa miradi yake kwa wakati.

Katika hatua nyingine, Profesa Mbarawa amemtaka Mkurugenzi wa Manispaa ya Lindi na Mkandarasi wa Kampuni ya M/S Halem Construction Co. Ltd wakae chini na kufikia makubaliano ya kuiacha Wizara ya Maji ifanye utaratibu wa manunuzi ya bomba za kusambaza maji kwa ajili ya Mradi wa Maji wa Nandambi kwa dhumuni la kuhakikisha unakamilika kwa wakati kutokana na mkandarasi huyo kusuasua.

Profesa Mbarawa amesema fedha za ununuzi wa mabomba hayo zipo na ndani ya wiki mbili mabomba yatakuwa yamefika site kwa ajili ya kukamilisha mradi huo unaotakiwa kukamilika mwishoni wa mwezi Septemba, 2019 kwa gharama ya Shilingi milioni 825.

Aidha, wakazi wa Kijiji cha Nandambi wamweleza Waziri wa Maji, Prof. Mbarawa kuwa hatua hiyo itakuwa na msaada mkubwa kwao ikizingatiwa kuwa mradi huo ulioanza utekelezaji wake Agosti, 2018 na unatakiwa kukamilika mwezi Septemba, 2019 bado mkandarasi hatoi matumaini ya kukamilisha mradi huo kwa asilimia 100 pamoja na ujenzi wa tenki kuwa umekamilika.

Wakati huo huo, Kaimu Mkuu wa Mkoa ya Lindi, Shaibu Ndemanga amesema Serikali ya Mkoa wa Lindi itahakikisha mazungumzo hayo yanafanyika pasipo kupoteza muda ili hatua iliyobaki ikamilike na wananchi wa Nandambi wanufaike na maji.

Katibu Mkuu wizara ya afya Dkt.Chaula Ahitimisha Kongamano La Tatu La Kutathimini Masuala Ya Afya Nchini.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Katibu Mkuu  wizara ya afya , Maendeleo ya jamii,jinsia,Wazee na watoto Dkt Zainabu Chaula amefunga kongamano la tatu la mwaka la kufuatilia na kutathmini masuala ya afya Nchini.

Akizungumza katika Kongamano hilo Septemba 25,2019   jijini Dodoma  ,Dkt Chaula amesisitiza juu ya matumizi ya takwimu kwa wadau wa afya ili iwasaidie katika upataji wa taarifa sahihi.

Awali Akitoa taarifa fupi mbele ya Mgeni Rasmi yenye tathmini ya mafunzo ikiwa na mjumuisho wa kongamano la pili lililofanyika mwaka jana na la tatu mwaka huu, kaimu mkuu wa shule ya utawala na Management ya chuo kikuu cha Mzumbe Dkt Eliza Mwakasangula amesema tafiti zifanyike na kuleta majibu juu ya namna bora ya kuimarisha na kujenga mifumo ya kuchakata taarifa za  huduma za afya nchini.

Katika hatua nyingine Dkt Eliza amesema vituo vya afya kumiliki miradi na taarifa kwa matumizi yao wenyewe ni chachu kuu ya kuboresha taarifa zinazokusanywa na kuzitumia katika kufanya maamuzi.

Mbali na hilo Dkt eliza amesema kuwe na ushirikiano baina ya wizara na vyuo vya ndani na nje ya nchi kuendelea kuchapisha na kuwasilisha matokeo ya tafiti zinazofanyika kwa wahusika  ili waweze kutumia matokeo ya tafiti hizo kwa kuboresha huduma ya afya Tanzania.

Akizungumza kwa niaba ya washiriki walioshiriki katika kongamano hilo Joseph Bura amesema maelekezo yote yaliyotolewa katika kongamano hilo watakwenda kuyafanyia kazi kama inavyotakiwa.
 
Kongamano hilo  la kutathimini na kufuatilia masuala ya Afya nchini limeandaliwa na chuo kikuu cha Mzumbe kwa kushirikiana na chuo cha St Fransisco Nchini Marekani na kushirikisha wadau mbalimbali  kwa lengo la kufuatilia na kutathimini masuala ya afya.

RC Makonda Atangaza Vita Na Watendaji Wanao Mhujumu

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema katika kipindi cha uongozi wake hajawahi kutoa onyo kwa njia ya barua kwa kiongozi yeyote chini yake ndani ya mkoa huo, lakini sasa ataanza kuwashughulikia kutokana na hujuma anazofanyiwa

Jumapili iliyopita, wakati wa kuwaapisha viongozi aliowateua, akiwamo Mkuu wa Morogoro, Rais Magufuli alionyeshwa kusikitishwa na kusuasua kwa miradi ya maendeleo ilhali mkuu huyo wa mkoa yupo.

Kutokana na madai hayo ya kuhujumiwa, Makonda ametangaza kuwa atawachongea watendaji hao kwenye ngazi za juu za utawala.

Pia amelalamika kuwa amekuwa akitoa maagizo kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo lakini badala ya kutekeleza, baadhi ya watendaji hao wamekuwa wakitafuta uhakika kutoka kwa wakuu wa idara.

Makonda aliyasema hayo jana, wakati akizungumza na wakuu wa wilaya zote tano za mkoa wa Dar es Salaam, wakurugenzi wa manispaa, viongozi wa jiji na watendaji wote katika kikao cha kujadili sababu za kukwama kwa miradi mbalimbali ya maendeleo.

"Haina maana kama mimi natoa maagizo na nyie viongozi badala ya kuyafuata mnaanza kupitisha vimemo kuuliza kama mtafanyaje ili kutafuta uhakika, ina maana mkuu wa mkoa hana washauri wazuri ndio sababu ya kutofuata maelekezo yake," alisema Makonda.

Alimtaja Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ally Happi, ambaye aliwahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni kuwa alikuwa akifuata maelekezo yake bila vikwazo tofauti na viongozi wengine walio chini yake, akiwamo anayeshika nafasi hiyo kwa sasa. Kwa sasa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ni Daniel Chongolo.

"Nilikuwa nikifanya vikao ofisini kwangu na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi na wa Ilala Sophia Mjema. Walikuwa wakifuata ninachowaeleza lakini hawa wengine kila nikiwaambia lazima waanze kupita pita na kuuliza hapa sijamwelewa. Mnapiga majungu yenu, sasa inatosha na mimi nitaanza kuwashughulikia," Makonda alisema.

Alisema viongozi na watendaji wa mkoa huo, wanapaswa kufuata maagizo yake kwa sababu ndiye aliyepewa jukumu la kusimamia mkoa huo.

"Haijalishi kama umenipita umri au nilikukuta serikalini lakini uko chini yangu tu," alisema Makonda na kuongeza kuwa ili kumaliza utata na fitina hizo, naye atakuwa akitoa taarifa za viongozi wasiotimiza wajibu wao kwa viongozi wa juu yake.

Alisema pia kila maagizo atakayokuwa akiwapatia, atakuwa akituma nakala kwa uongozi wa juu ili kuondokana na changamoto ya kuonekana mzembe ilhali anatimiza wajibu wake.

"Tangu nimekuwa mkuu wa mkoa huu, sijawahi kuandika barua kwa viongozi wa juu kumsema kiongozi yeyote, awe mkuu wa wilaya au wakuu wa idara. Lakini sasa nitaanza kuwasema. Nimeshamwambia Katibu Tawala wa Mkoa kila ninapotoa maagizo atoe na nakala kwenda kwa viongozi wa juu," alisema Makonda.

Aidha, aliwataja viongozi wa wilaya ya Kinondoni ambao mradi wa fukwe za Coco umekwama na anapowapa maagizo hawayafuati na kusababisha mkoa kupata sifa mbaya za kukwama kwa miradi.

"Natoa ushauri nyie mnafuata wa kwenu. Nikiuliza mnaitisha vyombo vya habari kusema mnafuata sheria. Mnapindua maagizo yangu na kufuata yenu. Tusishindane, tunapozidiana madaraka kila mtu atimize wajibu wake," alisema.

DC Ole Sabaya aagiza TANESCO kukata umeme ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Hai kwa kushindwa kulipa bili ya umeme Soko Kuu

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya, ameagiza kukatwa umeme  ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya  Hai, mahali ambapo ofisi yake pia ipo hapo, kwa kile alichokieleza Halmashauri hiyo haijalipa bili ya Soko Kuu la Hai kwa muda wa miezi 2, na kuitaka TANESCO wakawashe umeme kwenye soko hilo.

Alitoa agizo hilo jana baada ya kutembelea soko hilo akimtaka Meneja wa Shirika la Umeme (Tanesco) kurejesha huduma ya umeme sokoni hapo iliyoondolewa na shirika hilo kutokana na halmashauri kutolipa bili.

"DED (Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya) na watu wako mnakuja kukusanya fedha kwa miezi mitatu mfululizo, mnasahauje kulipa bili kupitia fedha hizo?

"Hili nalo Rais asimamishwe aambiwe? Mimi na wewe tuwaombe radhi hawa wananchi, ila wakati huo nakuagiza Meneja wa Tanesco ukate umeme Ofisi ya Mkurugenzi na uwashe hapa sokoni na alipe deni hilo, na alipe bili za miezi sita ijayo.

"Umeme uwake hapa leo (jana) na 'go ahead' (maelekezo) ya kuwasha umeme kwa DED nitakupa baada ya kuona risiti. Na kwa kuwa ofisi yangu iko kwenye jengo hilo (la DED) tukapambane wote na hilo joto la kuwapuuza hawa wananchi tunaoambiwa kila siku kuwasikiliza na kuwahudumia."

Hata hivyo, Ole Sabaya alimweleza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Yohane Sintoo, kuwa hayuko tayari kufanya kazi kwenye ofisi ambayo haina huduma ya umeme na hayuko tayari kuona wananchi wanatozwa kodi ambayo hairudi kulipa deni la umeme.

Kutokana na agizo hilo, Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo (Sintoo) alikiri kuwapo kwa changamoto hiyo na kuwaomba radhi wananchi kutokana na kukatwa kwa umeme kwenye soko hilo.

Hatimaye Benjamin Netanyahu achaguliwa kuunda serikali mpya Israel

$
0
0
Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu hapo jana usiku amepewa jukumu na Rais wa Israeli Reuven Rivlin la kuunda serikali mpya, kufuatia uchaguzi uliosababisha mkwamo wa kisiasa. 

Rais Rivlin amechukua uamuzi huo baada ya juhudi za kuunda serikali ya umoja wa kitaifa kati ya chama cha Netanyahu cha Likud na chama cha Bluu na Nyeupe cha mpinzani wake Benny Gantz kushindikana. 

Rais ana jukumu la kikatiba la kumteua waziri mkuu baada ya uchaguzi wa kitaifa. Netanyahu anazo siku 28 za kuunda serikali mpya, na anaweza kuomba kuongezwa wiki mbili. 

Netanyahu akishindwa kupata uungwaji mkono wa kutosha ili awe na wingi wa viti bungeni, Gantz badala yake atapewa nafasi ya kuunda serikali ya mseto.

Iran yakataa kufanya mazungumzo na Marekani hadi Iondolewe Vikwazo

$
0
0
Rais wa Iran hapo jana ameondoa uwezekano wa kufanya mazungumzo na Rais Donald Trump, licha ya juhudi za dakika za mwisho za viongozi wa mataifa ya Ulaya wanaotaka kupunguza mvutano huku Marekani ikiongeza tena vikwazo vya adhabu dhidi ya Iran. 

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kwa siku mbili bila ya mafanikio amekuwa akijaribu kuwakutanisha viongozi hao wawili wakiwa katika Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. 

Macron anajaribu kufanikisha mkutano huo wa kihistoria ambao anatumai utaepusha kutokea vita katika Mashariki Kati. 

Lakini Rais wa Iran Hassan Rouhani, akihutubia katika Hadhara Kuu ya Umoja wa Mataifa amesema hatokubali kufanya mazungumzo wakati Marekani inaendelea kuiwekea vikwazo nchi yake.

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO . Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,KUSAFISHA NYOTA, Mvuto wa Mwili na BIASHARA, ...MIGUU Kufa GANZI na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na 
0747100745

Waziri Mkuu: Imarisheni Mahusiano Na Wadau

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema mahusiano kati ya Serikali na wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa kidini, kimila ni muhimu yakaimarishwa.

Ameyasema hayo jana (Jumanne, Septemba 24, 2019) wakati akipokea taarifa ya mkoa wa Iringa alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Iringa kwa ajili ya ziara ya kikazi.

Waziri Mkuu alisema ni lazima mahusiano hayo yakadumishwa katika ngazi zote kwa sababu Serikali ipo kwa ajili ya wananchi wote na inawahudumia bila ya ubaguzi.

Aliwataka viongozi waliopewa dhamana ya kusimamia maeneo mbalimbali nchini wahakikishe wanatekeleza majukumu yao ipasavyo na uwajibikaji wao uwe na tija.

 Waziri Mkuu amesisitiza kuwa watendaji wahakikishe suala la ukusanyaji wa mapato linapewa kipaumbele katika maeneo yao.

“Ukusanyaji wa mapato ni muhimu kwa ajili ya maendeleo ya Taifa kwa sababu miradi ya maendeleo kama ujenzi wa shule haiwezi kutekelezeka bila ya kukusanya mapato.”

Awali, Akisoma taarifa ya mkoa, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ally Hapi alisema mkoa huo umepewa zaidi ya sh. bilioni saba kwa ajili ya ujenzi wa hospitali za wilaya.

Alisema fedha hizo zimetumika kwa ajili ya ujenzi wa hospitali kwenye Manispaa ya Iringa (98%), Halmashauri ya wilaya ya Iringa (90%), Kilolo(99%), Mufindi (89%).

Mkuu huyo wa mkoa alisema mbali na fedha hizo za ujenzi wa hospitali pia Serikali imetoa zaidi ya sh. bilioni tatu kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa vituo vya afya.

Akizungumzia kuhusu uchaguzi wa Serikali za mitaa, kiongozi huyo alisema wanaendelea na maandalizi.Mkoa una vijiji 360, mitaa 222 na vitongoji 2,216

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Walimu Mkoani Kagera Watakiwa Kuwa Mabalozi Wazuri Wa a Kulipa Kodi Ili Kukuza Uchumi Wa Nchi.

$
0
0
Na Avitus Benedicto Kyaruzi, Kagera.
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti  amewataka walimu mkoani humo kuwa mabalozi wazuri kwa kulipa kodi ili kuweza kuchangia ukuaji wa pato la nchi.
 
Mkuu wa Mkoa Gaguti amesema hayo Septemba 23, 2019 wakati akifungua kongamano la Walimu na Benki ya NMB Bukoba katika siku ya walimu kwenye ukumbi wa Hoteli ya ELCT Bukoba .
 
Ameongeza kwamba walimu  ni  jeshi kubwa kila watakapo kuwa wenasimama waendelee kutoa elimu kwa wananchi kuhusu ulipaji kodi na kuwahamasisha wananchi kudai risiti kila wakinunua bidhaa na kuwahamasisha wanaouza kutoa risiti.
 
Mkuu wa Mkoa Gaguti ametoa rai kwa benki ya NMB kuona namna ya kuwapunguzia riba walimu sababu ni wadau wakubwa wa benki hiyo tangu mwanzo.
 
 Pia amewataka walimu kutanua wigo wa kuunda vikundi vya pamoja mfano kwenye Kata na kuomba mikopo ya miradi mikubwa na ya pamoja ili kuinua vipato vyao hasa pale wanapostaafu. 
 
 Kwa upande wake Mkuu wa shule ya Sekondari Gabulanga iliyopo wilayani Missenyi bwana Mutalemwa Makwabe kwa niaba ya Walimu wenzake amesema kuwa wanaishukuru benki hiyo kwa namna inavyoendelea kuwajali walimu pamoja na kutoa misaada mbalimbali katika shule uku akitaja kuwa shule yake iliwahi kupatiwa misaada mbali mbali na benki hiyo ikiweno madawati pamoja na mbao za kuezekea.

Kwa upande wake Meneja wa NMB kanda ya ziwa bwana Ibrahimu Agustino amesema kuwa benki hiyo inatenga 1% kila mwaka katika kuhudumia jamii  na kuongeza kuwa kwa mwaka huu wametenga shilingi bilioni moja na mpaka sasa wametoa zaidi ya milioni mia sita katika  kusaidia jamii.





Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na 
0747100745

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0673878343

watsap +255 0620510598

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Masoko Ya Mazao Kuinua Sekta Ya Kilimo

$
0
0
Na Ismail Ngayonga,MAELEZO
RIPOTI ya Shirika la Kilimo Duniani (FAO) inasema mahitaji ya bidhaa za kilimo yanatarajiwa kukua kwa asilimia 15 katika kipindi cha muongo mmoja ujao huku, ukuaji wa uzalishaji wa bidhaa za kilimo ukitarajiwa kuongezeka kwa kasi zaidi na kusababisha mfumuko wa bei.

Aidha ripoti hiyo iliyotolewa  mwezi Julai mwaka huu inatoa utafiti unaolenga mwelekeo wa miaka kumi ijayo katika soko la bidhaa za kilimo na samaki katika viwango vya kitaifa, kikanda na kimataifa.

Katika ripoti hiyo inaelezwa kuwa miongoni mwa changamoto kubwa inayowakabili wakulima katika Mataifa yanayoendelea ikiwemo Tanzania ni pamoja na ukosefu wa masoko ya mazao yao ndani na nje ya nchi.

Changamoto hiyo imekuwa ikiwakwaza sana wakulima katika miaka ya nyuma wakulima kiasi cha baadhi ya wakulima wa baadhi ya mazao kadhaa kuamua kuachana kabisa na uzalishaji wa mazao husika ikiwemo zao la kahawa na korosho.

Changamoto za wakulima kukosa masoko haziwaathiri wakulima pekee, bali hata serikali hivyo ni suala linalogusa pande zote, kwa sababu serikali nayo inategemea kupata mapato kutokana na usafirishaji wa mazao nje.

Hata hivyo, matumaini yameanza kuonekana kutokana na hatua kadhaa ambazo zinachukuliwa na Serikali ya Awamu ya Tano katika kuboresha sekta ya kilimo ikiwemo kuhimiza uongezaji wa thamani ya mazao na kuweka bei elekezi ya mazao, ambayo inampa motisha mkulima.

Akiwasilisha Hotuba ya Makadirio ya Bajeti ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2019/2020, Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga anasema Wizara kwa kushirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara imeendelea kutekeleza mipango na mikakati ya kupata masoko na kuongeza thamani ya mazao ya kilimo.

Waziri Hasunga anasema Ili kuongeza juhudi zaidi za utafutaji wa masoko ya mazao ya kilimo, Wizara katika mwaka 2018/2019, imeanzisha kitengo cha masoko ya mazao ya kilimo ambacho kitahusika na kutafuta masoko ndani na nje ya nchi na kufanya utafiti na uchambuzi wa kina wa mahitaji ya mazao na bidhaa za kilimo.

“Wizara pia iliboresha mifumo ya masoko ya mazao ya kimkakati kwa kufanya utafiti wa mahitaji ya masoko na kuimarisha vyama vya ushirika, kusimamia mikataba baina ya wanunuzi na wakulima” anasema Waziri Hasunga.

Anaongeza kuwa matokeo ya awali ya utekelezaji ya mifumo hiyo, yameonesha kuwepo kwa tija kwa mkulima, bei nzuri, takwimu na ubora wa mazao, ambapo bei kwa mazao ya kahawa, korosho na kakao kwa soko la ndani ziliimarika ikilinganishwa na masoko ya nje.

Akitolea mfano Hasunga anasema bei ya kahawa ya Arabika katika soko la dunia ilikuwa ni Dola za Marekani 107.04 ikilinganishwa na Dola 112 katika soko la ndani kwa gunia la kilo 50, bei ya kahawa ya Robusta katika soko la dunia ilikuwa Dola 73.90 ikilinganishwa na Dola 87.13 katika soko la ndani kwa gunia la kilo 50.

Akifafanua zaidi anasema Serikali pia imeendelea kutafuta masoko ya zao la muhogo ikiwemo kuingia Makubalino ya Itifaki ya Usafi baina ya Tanzania na Serikali ya China kuwezesha kuuza zao hilo nchini China.

“Hadi mwezi Machi 2019, kampuni tano za Dar Canton Investment, Jielong Holdings (T) Company, EPOCH Agriculture Development, Gelimesha Company na Tanzania Export Processing Zone (TAEPZ) zimesajiliwa kwa ajili ya kuuza muhogo nchini China” anasema Waziri Hasunga.

Hasunga anasema katika mwaka 2018/ 2019, Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko ilipanga kununua tani 14,000 za mahindi na tani 6,000 za mbegu za alizeti, ambapo hadi kufikia Machi 2019, Bodi imenunua mahindi tani 7,230 na alizeti tani 621 na kusaga tani 1,003.0 za mahindi ambazo zimetoa tani 802.4 za unga wa mahindi na tani 208.9 za pumba.

Kwa mujibu wa Hasunga anasema Tani 1,003.0 za unga wa mahindi zenye thamani ya Shilingi 561,680,000 na tani 208.9 za pumba zenye thamani ya Shilingi 45,570,000 ziliuzwa katika mikoa ya Iringa, Mwanza, Dodoma na Dar es Salaam.

Waziri Hasunga anasema ili kujiimarisha zaidi, Bodi imefunga mashine za kukamua mafuta ya alizeti na kusaga mahindi katika eneo la Kizota Jijini Dodoma hadi Machi, 2019 ufungaji wa mashine za kusaga mahindi umefikia asilimia 90 na alizeti asilimia 65.

Mkakati wa Serikali wa kuimarisha masoko ya mazao ni muhimu na wenye tija kwa sababu unalenga kuwatafutia wakulima ufumbuzi wa kero yao ya muda mrefu ya masoko, ambayo pia imekuwa ikisababisha serikali isinufaike zaidi na pato

Aidha masoko ya mazao pia yatasaidia kuchochea kasi ya ukuaji wa viwanda ambavyo Tanzania imepania kuvijenga katika wakati huu wa kuelekea uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Waziri Mkuchika Azitaka Taasisi Zilizo Chini Ya Ofisi Ya Rais Kuwa Mfano Wa Kuigwa Kiutendaji Na Kimaadili

$
0
0
Na James K. Mwanamyoto
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika amewataka watumishi wa taasisi za umma zilizo chini ya Ofisi ya Rais kuwa mfano wa kuigwa na watumishi wa taasisi nyingine za umma kiutendaji na kimaadili kwa kuwa jamii inaitazama Ofisi ya Rais kama kioo cha utendaji kazi mzuri katika utumishi wa umma.

Waziri Mkuchika ametoa wito huo wakati wa kikao kazi chake na Watumishi Waandamizi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa chuo hicho.

Mhe. Mkuchika amewaasa watumishi wa taasisi hizo kujiona kuwa ni sehemu ya kuitunza heshima ya Ofisi ya Rais kwa kufanya kazi kwa uadilifu.

Amewasisitiza watumishi wa chuo hicho kufanya kazi kwa bidii, umoja na mshikamano ili kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli za kuharakisha maendeleo ya nchi.

“Mimi nipo kwa ajili ya kumsaidia Mhe. Rais ambaye ndiye Waziri wa Ofisi hii kusimamia utendaji kazi wa taasisi zote zilizopo chini ya ofisi yake, hivyo hatuna budi kufanya kazi kwa bidii, maarifa na weledi kama ambavyo yeye mwenyewe amekuwa mstari wa mbele kutekeleza majukumu yake kwa vitendo”, amesisitiza Mhe. Mkuchika.

Aidha, Mhe. Mkuchika ametoa rai kwa Watumishi wa Umma wote nchini kufanya kazi kwa kuzingatia Kanuni, Sheria, Taratibu na Miongozo ya kiutumishi iliyopo ili kuepukana na vitendo vya ubaguzi wa kijinsia, dini, ukabila na  itikadi za kisiasa kwa wananchi na watumishi wenzao wanaowahudumia.

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Emmanuel S. Shindika kwa niaba ya chuo, amemthibitishia Mhe. Mkuchika kuwa, atahakikisha maelekezo yote aliyoyatoa yanatekelezwa ili kuendana na kasi ya kiutendaji ya Mheshimiwa Rais yenye lengo la kuleta maendeleo ya Taifa.

Iran Yaiachia Huru Meli Ya Mafuta ya Uingereza

$
0
0
Meli ya mafuta iliyokuwa na bendera ya Uingereza na ambayo ilikuwa ikishikiliwa katika bandari ya Abbas nchini Iran kwa zaidi ya miezi miwili, imeanza safari kuelekea Uingereza. Tovuti maalum inayofuatilia safari za baharini imeripoti hayo.

Hapo jana, msemaji wa serikali Ali Rabiei alitangaza kuwa mchakato wa kisheria umekamilika na meli hiyo inayomilikiwa na Sweden iko huru kuondoka. 

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, tovuti ya Tanker Trackers imeandika kuwa picha za satelaiti zinaonyesha kuwa meli hiyo imeondoka. 

Mnamo Julai 19, kikosi maalum cha askari wa mapinduzi nchini Iran kiliizingira meli hiyo kwa jina Stena Impero katika mlango bahari wa Hormuz. 

Meli hiyo ilikamatwa kufuatia tuhuma  za kushindwa kuitikia wito wa dharura uliotolewa baharini. 

Hata hivyo kukamatwa kwa meli hiyo kulitizamwa kama ni kulipiza kisasi baada ya maafisa wa Uingereza kuikamata meli ya Iran mapema mwezi Julai kwa tuhuma za kusafirisha mafuta kupeleka Syria.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images