Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mfanyakazi TAKUKURU Makao Makuu adakwa akiomba na kupokea Rushwa

$
0
0
Mchunguzi Mkuu kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na rushwa (Takukuru), Cosmas Batanyita (44), amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, Tanzania  akikabiliwa na mashtaka saba likiwemo la kuomba rushwa ya Sh200 milioni na kutakatisha fedha.

Batanyita ambaye ni mkazi wa Chamazi, Dar es Salaam amefikishwa mahakamani hapo, leo Ijumaa Agosti 9, 2019 na kusomewa mashtaka yake mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Kelvin Mhina.

Wakili wa Serikali Mkuu, Paul Kadushi akisaidiana kusomewa mashtaka yake na Wankyo Simon amedai mshtakiwa huyo anakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 76/2019.

Miongoni mwa mashtaka yanayomkabili mshtakiwa huyo ni kushawishi, kuomba rushwa na kutakatisha fedha, ambapo anadaiwa kuyatenda kati ya Februari  9, 12 na 24, 2019.

Katika shtaka la kuomba rushwa, Batanyita anadaiwa Februari 9, 2019 eneo la Upanga, Dar es Salaam akiwa mwajiriwa wa Takukuru alishawishi na kuomba rushwa ya Sh200 milioni kutoka kwa Hussein Gulamal Hasham ili aweze kuharibu ushahidi katika kesi ya ukwepaji wa kodi iliyokuwa inamkabili Hasham.

Mshtakiwa baada ya kusomewa mashtaka yanayomkabili, hakutakiwa kujibu chochote mahakamani hapo kutokana na mashtaka yanayomkabili kutokuwa na dhamana.

Hakimu Mhina ameahirisha kesi hiyo hadi Agosti 23, 2019 itakapotajwa na mshtakiwa amerudishwa  rumande.

Jeshi la Polisi Lamtia Mbaroni Afisa Usalama wa Taifa FEKI

$
0
0
Jeshi la polisi nchini kupitia kikosi chake cha viwanja vya ndege jijini Dar es Salaam limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa wawili katika uwanja wa Mwl. JK Nyerere kwa makosa tofauti.

Tiba Halisi ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
*NKOLOMIJE*/
√Ni dawa bora ya mitishamba yenye kuimarisha, kurefusha na kukufanya uwe imara hata kama umelala pia huimarisha na kukuza  maumbile yaliyosinyaa na kuwa regevu

*📌SUPER GAFINA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri ya uume ulio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/


Bado hujachelewa

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM  AU UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO SIMU NO:/
*📞0752723508*

Mbunge Wa CHADEMA Akubali Utendaji Kazi Wa Rais John Pombe Magufuli.

$
0
0
NA Avitus Benedicto Kyaruzi, Kagera.
Mbunge wa jimbo la Bukoba mjini kupitia chama cha Demokrasia na maendelelo (CHADEMA) Mh Wilfredy Muganyizi Rwakatale amempongeza Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania   Dk John Pombe Magufuri kwakuendelea kukarabati meli ya abiria na mizigo itakayokuwa inafanya safari zake Bukoba-Mwanza.
 
Mh Rwakatale amesema hayo katika mkutano wa hadhara na wananchi wa jimbo la Bukoba  Mjini uliofanyika  August 7 2019 katika kata ya Hamugembe manispaa ya Bukoba mkoani Kagera wenye lengo la kuzungumzia miradi mbalimbali ya kimaendeleo iliyofanyika kwa kipindi cha miaka minne kwenye uongozi wake wa  jimbo na kuongeza kuwa jitihada za ukarabati wa meli hiyo unaendelea kwa kasi chini ya uongozi wa awamu ya tano unaoongozwa na Dk John Magufuri.
 
Aidha mh Rwakatale amewataka wananchi wa mkoa wa Kagera ususani jimbo lake la manispaa ya Bukoba kuwa na subira katika kipindi hiki ambapo meli inaendelea kutengenezwa na itakapo kuwa imekamilika itawaondolea usumbufu wa kuendelea kusafiri kwa kutumia mabasi kwenda mkoani Mwanza.
 
Katika miaka minne ya uongozi wake mh Rwakatale ameweza kutekeleza miradi mbalimnbali ya kimaendeleo katika jimbo lake ikiwemo kuchangia shilingi milioni 16 kuwezesha ukarabati wa uwanja wa michezo wa shule ya msingi Kashai, mabati 56 kwa ajili ya kuezeka shule ya msingi Nyamkazi, ametoa shilingi milioni 2 kila kata kwenye kata 14 ili kuwezesha utengenezwaji wa madawati na mengine mengi.
 
Kwa upande wake mbunge wa viti maalumu kupitia Chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) Mh Conchesta Rwamulaza amewaomba wananchi wa mkoa wa Kagera kujitokeza katika kujiandikisha kwenye daftari la mpiga kura ili waweze kushiriki katika ushaguzi wa serikari za mitaa utaotarajia kufanyika mnamo mwaka huu.
 
Mh Rwamulaza ameongeza kuwa ili wananchi  wapate  kiongozi bora inabidi washiriki katika zoezi la kujiandikisha kwenye daftari la mpiga kura ambapo zoezi ilo kwa upande wa mkoa wa kagera limetajwa kuanza kufanyika mnamo mwezi wa tisa  mwaka huu.

Wizara Ya Ardhi Kwa Kushirikiana Na TAKUKURU Yaunda Tume Ya Uchunguzi Dhidi Ya Watumishi 183

$
0
0
Na.Faustine     Gimu Galafoni,Dodoma.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, WILIAM LUKUVI, amesema Wizara hiyo imeunda timu  ya uchunguzi ambayo itakuwa chini ya TAKUKURU, ikijumuisha vyombo vya ulinzi na usalama, kuwachunguza watumishi 183 waliosimamishwa kwa kuingilia mfumo wa kukadilia na kukusanya kodi ya pango la ardhi.
 
Waziri Lukuvi ameyasema hayo leo Jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari, kutolea ufafanuzi juu ya kusimamishwa kwa watumishi 183 wa wizara hiyo amesema serikali ilitilia shaka mfumo huo  na kufanya uhakiki.
 
Uhakiki huo wa miezi sita umebaini kuna watu walitakiwa kulipa kiwango  cha kodi ya pango lakini  kiwango kilichoingia hazina ni kidogo ukilinganisha na kiwango kilichofutwa katika mfumo wa malipo ikionesha kiwango hicho kimelipwa.
 
Amesema kutokana na matokeo ya uhakiki huo Wizara kupitia kwa katibu Mkuu wa Wizara hiyo wanaunda timu ambayo itakuwa chini ya TAKUKURU na vyombo vingine vya usalama kuchunguza jambo hilo na makosa mengine yatakayoonekana katika uchunguzi huo.
 
Waziri Lukuvi ametumia fursa hiyo kuwapongeza wananchi hususan Wa wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga na Mkoani Mtwara  kwa kuonesha  ushirikiano wa kutoa taarifa dhidi ya watumishi wa ardhi waiokuwa waaminifu.

Aidha waziri Lukuvi amewatoa hofu wana nchi kutokana na idadi kubwa ya maafisa ardhi waliosimamishwa amesema Shughuri za kiserikali katika Ofisi hizo zitaendelea kama kawaida.
 
Pia amewataka wananchi kutumia mfumo wa kielecronic kulipia kodi ya pango ili kuepusha vitendo vya rushwa, na amesema kwa wale wote ambao fedha za malipo ya pango zilifutwa bila malipo kuonekana katika mfumo na wale ambao yameingia malipo pungufu wote watalipa kiasi kilichobaki kukamilisha malipo hata kama wamelipa.
 
Hata hivyo,Waziri Lukuvi ametolea Mfano suala la Mmiliki wa  Mbeya Hotel ambapo alipunguziwa ukubwa wa eneo  lililokuwa na Ukubwa wa Mita za Mita za mraba 20,234 lakini kwenye mfumo wa malipo akawa analipia gharama ya   Mita za Mraba  502 badala ya 20,234 tangu mwaka 2002 baada ya kufanyiwa ujanja na mtumishi wa ardhi .
 
Hivyo alitakiwa kulipa zaidi ya  Tsh.Milioni 6  kwa Mwaka, kutokana na ujanja amepatana na mtu wa mfumo  badala yake wanamtoza zaidi ya 63 elfu pekee tangu mwaka 2002 pekee kwa mwaka na kwa malipo halisi serikali inamdai zaidi ya Tsh.Milioni 68.

Timu hiyo ya Uchunguzi itaanza kufanya kazi kuanzia Wiki ijayo Siku ya Jumanne ambapo itafanya uchunguzi kwa muda wa siku 30.

Wananchi Mkoani Kagera Wahimizwa Kuongeza Uzalishaji Wa Mazao Ya Kilimo Ili Kufikia Uchumi Wa Viwanda.

$
0
0
Na Avitus Benedicto Kyaruzi, Kagera.
Wananchi mkoani Kagera wamehimizwa kufanya kazi kwa bidii ili kuweza kuongeza uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.
 
Hayo yamebainishwa na mkuu wa Wilaya ya Biharamulo Bi Saada Malunde kwenye kilele cha kufunga maadhimisho ya siku ya wakulima na wafugaji nane nane yaliyofanyika katika viwanja vya Kyakailabwa kata nyanga mkoani Kagera.
 
Bi Saada amesema kuwa ili kufikia uchumi wa viwanda ni lazima wananchi wafanye kazi kwa bidii ikiwemo kulima mazao ya kilimo, mifugo pamoja na kuendelea kushiriki katika maadhimisho ya siku ya wakulima kila mwaka.
 
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Ngara mkoani Kagera  Luteni Kanaly  Michael Mtenjele amewashukuru wananchi wote walio jitokeza katika maadhimisho hayo na kuwaomba kuongeza uzalishaji katika mazao.
 
Sanjali na hayo mh Mtenjele ameongeza kuwa elimu aliyoipata katika maadhimisho ya mwaka huu ataichukua katika wilaya yake ili kuongeza uchumi wa jamii na taifa kwa ujumla.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Kijana mbaroni kwa kubaka na kumpa mimba wanafunzi mwenye umri wa miaka 17 kahama

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Mkazi wa mtaa wa Manzese wilayani Kahama mkoani Shinyanga, Lazaro Mateyo (18) amefikishwa katika Mahakama ya wilaya kwa tuhuma ya kumbaka na kumpa mimba mwanafunzi umri wa miaka (17).

Mbele ya Hakimu mkazi wa Mahakama hiyo Ushindi Swalo mwendesha mashitaka wa jeshi la Polisi Peter Masau amedai kuwa Lazaro alitenda kosa hilo mwezi April mwaka huu katika mtaa huo.

Amesema Mshitakiwa baada ya kutenda makosa hayo alitoroka kusiko julikana hadi alipokamatwa na polisi Agosti hii na kufikishwa Mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili kwa mujibu wa sheria.

Katika shauri hilo la jinai namba 281 la mwaka huu Lazaro anatuhumiwa kumbaka mwanafunzi huyo kinyume na kifungu namba 130 (1) na (2) 132  vya kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2002.

Kosa la pili anatuhumiwa kumpa mimba mwanafunzi huyo kinyume na kifungu cha 60 (1) sura 133 cha sheria ya elimu ya mwaka 2016.

Kwa upande wake Lazaro amekanamashitaka hayo na shauri hilo limeahirishwa hadi Agosti 23 mwaka huu na dhamana ya mshitakiwa ipo wazi kwa kuwa na wadhamini wawili ambao watatakiwa kulipa bondi ya shilingi milioni mbili kila mmoja.

Mshitakiwa ameshindwa kutimiza mashariti ya dhamana na amepelekwa gerezani na upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.

Gramu 30.5 za bangi zampandisha kizimbani baada ya kukamatwa na Polisi Kahama

$
0
0
Mkazi wa Mwime wilayani Kahama mkoani Shinyanga, Azard Ibrahimu amefikishwa katika Mahakama ya wilaya kwa tuhuma ya kupatikana na dawa za kulevya aina ya bangi gramu 30.5 kinyume cha sheria.

Mbele ya hakimu mkazi wa Mahakama hiyo Ushindi Swalo mwendesha Mashitaka wa Jeshi la Polisi Peter Masau amesema Azard alitenda kosa hilo Agosti 6 mwaka huu katika eneo la mwime.

Amesema katika shauri hilo la jina namba 283 la mwaka huu mtuhumiwa amekiuka kifungu namba 17 (1) b (2) sura 5 ya sheria ya kuzuia na kupambana na dawa za kulevya ya mwaka 2015.

Kwa upande wake  Azardi amekana kutenda kosa hilo na shauri hilo limeahirishwa hadi agosti 23 mwaka huu litakapotajwa mahakamani hapo na upelelezi wake bado haujakamilika.

Dhamana ya Mtuhumiwa iko wazi kwa kuwa na wadhamini wawili ambao watasaini bondi ya shilingi milioni mbili kila mmoja na amepelekwa gerezani kwa kushindwa kutimiza mashariti hayo.

Download App Yetu Kwenye Simu Yako Ili Uweze Kupata Habari Zetu Kwa Haraka Zaidi

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Mkongo: Kibongo ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
********************************
SUPER MKONGO MPYA,
_______________________________
********************************
Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile,

- kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa
- maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo
- kukosa hamu ya tendo la ndoa
- kushindwa kurudia tendo la ndoa
- maumbile kusimama kwa kulegea
-  kulegea katikati ya tendo
- kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu
- kuishiwa nguvu kutokana na punyeto.

Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MCONGO MPYA, kiboko ya matatizo haya.
_______________________________
Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume
_______________________________
(1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea.
(2) ngiri
(3) kuugua chango la uzazi kwa muda mrefu.
(4) kupungukiwa hormone za testosterone.
(5) ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na visivyo na virutubisho  vya kutosha.
(6) kutokufanya mazoezi na mwenendo wa maisha.
(7) kisukari.
(8) tumbo kuunguruma na kujaa gesi.
(9) maumivu ya kiuno nk.
_______________________________

WASILIANA NA:
DR. MCONGOMANI
SIMU NO:
📞0658816558
📞0682323682
Popote ulipo huduma hii inakufikia

Tiba Halisi ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
*NKOLOMIJE*/
√Ni dawa bora ya mitishamba yenye kuimarisha, kurefusha na kukufanya uwe imara hata kama umelala pia huimarisha na kukuza  maumbile yaliyosinyaa na kuwa regevu

*📌SUPER GAFINA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri ya uume ulio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/


Bado hujachelewa

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM  AU UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO SIMU NO:/
*📞0752723508*

Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga aongeza siku tatu maonyesho ya Nanenane Simiyu

$
0
0
Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga, ameongeza siku tatu kuendelea kuwepo kwa maonyesho ya sikuu ya wakulima kitaifa (Nanenane), kuanzia kesho Ijumaa Agosti 9, hadi jumapili ya wiki hii.

Waziri Hasunga ametangaza uamuzi huo wakati akiongea kwenye kilele cha maonyesho hayo mbele ya Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo iliyofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.

Hasunga amesema kuwa uamuzi huo unatokana na wakuu wa mikoa ya Mara, Shinyanga na Simiyu ambao ndiyo waandaji wa maonyesho hayo kanda ya Magharibi kutaka kuongezewa muda.

“Nilipokea ombi la wakuu wa mikoa ya Mara, Simiyu na Shinyanga ambao ndiyo waaandaaji wa maonyesho haya, wakitaka kuongezewa siku, nami kwa mamlaka niliyopewa nimekubali ombi lao na kuongeza siku tatu hadi jumapili ya wiki hii ndiyo yamalizike,” amesema Hasunga.

Waziri Mkuu Atoa Maagizo Mazito Kwa Wizara Tano

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameziagiza Wizara za Kilimo, Viwanda na Biashara, Uvuvi na Mifugo kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji kutengeneza mkakati wa kuanzisha viwanda vya kuchakata mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi nchini.

Amevitaja viwanda kuwa ni pamoja na vya nyuzi, nguo, ngozi, maziwa, minofu, nyama, kubangua korosho, kutengeneza unga, mafuta ya kula, sabuni, usindikaji wa matunda na mbogamboga, “Kwani ndiyo msingi wa kauli mbiu yetu ya kufikia uchumi wa viwanda 2025”.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Alhamisi, Agosti 8, 2019) katika kilele cha maadhimisho ya sikukuu ya wakulima nane nane Kitaifa kwenye viwanja vya maonesho Nyakabindi mkoani Simiyu kwa niaba ya Rais Dkt. John Magufuli.

Waziri Mkuu amsema sambamba na mkakati huo, pia ameagiza kuimarishwa kwa vyama vya ushirika ili kumwezesha mkulima kuendelea kumiliki zao lake mpaka hatua ya kuuza sokoni. “Vyama vya ushirika vikiweza kuchakata mazao na kuyaongeza thamani vitamuwezesha mkulima kuwa na umiliki na kufaidika na bei ya soko”.

Amesema mfano uliooneshwa katika zao la Kahawa kupitia Chama Kikuu cha Ushirika Kagera (KCU) ni mzuri ambapo wanamiliki asilimia 100 ya Kiwanda cha Kukoboa Kahawa (BUCOP), pamoja na asilimia 54 ya Kiwanda cha Kuzalisha Kahawa – Tanganyika Instant Coffee (TANICA).

“Kwa upande wa Pamba, Nyanza Cooperative Union (NCU) walianza vizuri kwa kumiliki viwanda vinane vya kuchambulia pamba. Tunataka jitihada za namna hii zianzishwe katika shughuli za wakulima wetu na zilizopo ziimarishwe”.

Hivyo, ameitaka Tume ya Maendeleo ya Ushirika kwa kushirikiana na wadau, ifanye tathmini kwenye vyama vya ushirika vinavyomiliki viwanda ili kubaini hali ilivyo kwa sasa na kuweka mikakati ya kuvifufua na kuviongezea uwezo.

Amesema safari ya kujenga uchumi wa viwanda itaiwezesha Tanzania kuwa nchi yenye kipato cha kati imeanza na inaendelea vizuri na  matarajio yake ni kuona wananchi wote bila kujali tofauti za kiitikadi, wataendelea kuunga mkono juhudi hizo kwa kuwa maendeleo wanayoyapigania ni kwa manufaa ya wote waliopo leo na vizazi vijavyo.

Waziri Mkuu amesema kwa mantiki hiyo, kila Mtanzania hanabudi kuongeza bidii katika kufanya kazi, kupiga vita rushwa, kulipa kodi ya Serikali na kulinda rasilimali za Taifa ili ziweze kutumika sasa na kwa faida ya vizazi vyetu vijavyo.

“Niwaombe muendelee kuiunga mkono Serikali ya Awamu ya Tano kwa namna ambavyo imeamua kwa makusudi kuanzisha miradi mikubwa ya ujenzi wa miundombinu ya kiuchumi inayoendelea kujengwa nchini ikiwemo reli ya kisasa ya mwendokasi, mradi mkubwa wa umeme wa Mto Rufiji, upanuzi wa viwanja vya ndege, bandari na ununuzi wa ndege kubwa”.

Amesema kuboreshwa kwa miundombinu hiyo, pamoja na mambo mengine kutachochea uwekezaji mkubwa katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi, kurahisisha usafirishaji wa mazao, mifugo, samaki, na kupunguza gharama za uzalishaji na hivyo kuwezesha viwanda vya ndani kushindana kibiashara na bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya nje ya nchi.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kutoawito kwa viongozi wa Mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga kuendelea kushirikiana na Wizara za Sekta ya Kilimo kuhakikisha viwanja hivyo vya Nyakabindi, vinakuwa kituo cha mafunzo ya wakulima, wafugaji na wavuvi. 

“Kumbukeni kuwa kila mmoja wetu akitimiza wajibu wake ipasavyo, maendeleo ya viwanda yanawezekana, ajira zitapatikana, uhakika wa chakula na lishe bora itakuwepo na sote kwa pamoja tutasonga mbele kufikia nchi yenye uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025”.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya Nane Nane ya mwaka huu inasema: - “Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa Ukuaji wa Uchumi wa Nchi”.Kaulimbiu hiyo inakwenda sambamba na azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kukuza uchumi wa viwanda na biashara, ikilenga kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja, Pato la Taifa na wakati huo huo kupunguza umaskini.

Awali, Waziri Mkuu alitembelea na kukagua mabanda mbalimbali katika maoneosho hayo. Miongoni mwa mabanda aliyoyatembelea ni pamoja na banda la EPZA, NMB, CRDB, NBC, BOT kitengo cha mifumo ya malipo ya Kielektroniki ya Serikali, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi na JKT.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally, Waziri wa Ulinzi Dkt. Hussein Mwinyi, Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina, Naibu Waziri Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, Naibu Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI, Josephat Kandege, Naibu Waziri wa Madini, Stansalaus Nyongo pamoja na maafisa wengine wa Serikali.
 

Waziri Mkuu: Watakaohujumu Ushirika Kuchukuliwa Hatua

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameagiza watendaji wote watakaobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa na ubadhirifu katika vyama vya ushirika wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria.

Kadhalika, Waziri Mkuu amewataka viongozi wote wa ushirika nchini wahakikishe wanaongoza vyama vya ushirika kwa kufuata Sheria ya Ushirika Namba 6 ya mwaka 2013, kanuni na taratibu zilizopo.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Alhamisi, Agosti 8, 2019) katika kilele cha maadhimisho ya sikukuu ya wakulima nane nane Kitaifa kwenye viwanja vya maonesho Nyakabindi mkoani Simiyu kwa niaba ya Rais Dkt. John Magufuli.

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kutoa rai kwa Wanaushirika wote nchini kuhakikisha wanachagua viongozi wenye weledi, wachapakazi, waadilifu na wanao upenda ushirika ili ushirika uimarike na kuwa endelevu.

Amesema historia inaonesha kwamba miaka ya nyuma ushirika ulifanya kazi nzuri katika kusimamia uzalishaji, tija, uchakataji na masoko ya mazao. “Hata hivyo, ushirika ulianza kulegalega katika miaka ya 1980”.

Waziri Mkuu amesema kutokana na hali hiyo, Serikali iliamua kuanzisha Tume ya Maendeleo ya Ushirika kama chombo cha kusimamia shughuli za maendeleo ya ushirika nchini.

Amesema katika kuimarisha vyama vya ushirika nchini, tume hiyo imeendelea kuweka mazingira rafiki kwa Vyama vya Ushirika ili kuzalisha kwa tija na kuongeza uzalishaji kutokana na matumizi ya zana bora za kilimo. Amesema vyama vya ushirika 33 vimekopeshwa trekta moja kwa kila chama kupitia makubaliano yaliyofikiwa kati ya Tume na Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) na Bodi ya Pamba (TCB).

Pia, Waziri Mkuu amesema katika kuendeleza azma ya Serikali ya kuwa na uchumi wa viwanda, Vyama vya Ushirika vimeendelea kuwekeza katika miradi mingine ya kimaendeleo ambayo inaisaidia katika kuleta maendeleo.

 “Hadi kufikia Juni 30, 2019 jumla ya Vyama vya Ushirika 104 vinamiliki viwanda vidogo kwa ajili ya kuongeza thamani ya mazao wanayoyazalisha hali ambayo imeleta tija kwa jamii inayozunguka maeneo hayo”.

Amesema hadi Desemba 2018, mikopo yenye thamani ya sh. trilioni 1.3 imetolewa kwa wanachama ikilinganishwa na sh. bilioni 902 iliyotolewa kufikia Desemba 2017. Akiba na amana za wanachama katika SACCOS zimefikia sh. bilioni 575 na hisa sh. bilioni 79.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu kwa mara nyingine, ametumia fursa hiyo kuwaelekeza Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya wafanye tena mapitio ya idadi ya Maafisa Kilimo waliopo Wilayani na kuwahamishia katika kata na vijiji ili kuimarisha usimamizi wa mazao.

Hivyo, Waziri Mkuu amesema ngazi ya Makao Makuu ya Wilaya wabaki wataalamu wawili akiwemo Mkuu wa Idara na msaidizi wake kwa ajili ya uratibu. Maafisa Kilimo wa Wilaya wawe na ratiba za kwenda vijijini kuwatembelea maafisa ugani ili kutatua changamoto zinazowakabili katika uendelezaji wa kilimo na hawapaswi kukaa maofisini.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya Nane Nane ya mwaka huu inasema: - “Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa Ukuaji wa Uchumi wa Nchi”. Kaulimbiu hiyo inakwenda sambamba na azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kukuza uchumi wa viwanda na biashara, ikilenga kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja, Pato la Taifa na wakati huo huo kupunguza umaskini.

Awali, Waziri Mkuu alitembelea na kukagua mabanda mbalimbali katika maoneosho hayo. Miongoni mwa mabanda aliyoyatembelea ni pamoja na banda la EPZA, NMB, CRDB, NBC, BOT kitengo cha mifumo ya malipo ya Kielektroniki ya Serikali, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi na JKT.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally, Waziri wa Ulinzi Dkt. Hussein Mwinyi, Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina, Naibu Waziri Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, Naibu Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI, Josephat Kandege, Naibu Waziri wa Madini, Stansalaus Nyongo pamoja na maafisa wengine wa Serikali.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

MAKALA: Mbinu Za Kupanga Jinsia Ya Mtoto Wakuzaa ( Mvulana Au Msichana ) Kabla Mkeo Hajashika Mimba

$
0
0
Mpendwa  msomaji  wetu, Maada  yetu  nyingine  ya  leo  ni  mbinu za kupanga  jinsia  ya  mtoto  wa  kuzaa  kabla  mkeo  hajashika  mimba....

Siku  hizi  ulimwengu  umeendelea  sana, matatizo  mengi  yanatibika  kwa  msaada  wa  wataalamu...Hakuna   tena  haja  ya  kupigana  na  kupeana  talaka  kisa  jinsia  ya  mtoto...

Somo letu   la  leo  litajikita  zaidi  katika  mbinu  za  kuzaa  mtoto  wa  kike. 


Ni vipi jinsia ya mtoto huainishwa?
Kinyume na wengi wanavyofikiria kwamba mwanamke au mwili wa mwanamke ndio wenye jukumu la kuainisha jinsia ya mtoto kwa kuwa yeye ndiye anayebeba mimba, uhakika wa mambo ni kuwa mwanamume ndie mwenye uwezo wa kuainisha jinsia.
 
Kila yai la mwanamke lina chromozomu mbili za X. Iwapo manii ya mwanamume au spemu(ambayo ina chromozomu X na Y) itakuwa na X na kurutubisha yai la mwanamke lenye X tupu, basi mtoto atakayezaliwa atakuwa mwanamke.
 
Vilevile iwapo spemu ya mwanaume itakuwa na Y na kurutubisha yai la mwanamke lenye X, basi mtoto atakayezaliwaatakuwa mwanamume.
 
Hivyo kwa kufahamu suala hilo, ni matumaini yetu kuwa vile visa vya kinamama kuachwa eti kwa kuwa hawakuzaa watoto wa kiume au wa kike vitapungua katika jamii zetu. Mke wako asipozaa mtoto wa jinsia uitakayo, usifikiri kuwa yeye ndiomwenye makosa.
 
Wakati mwanamume anapomwaga mbegu, spemu kati ya milioni 200 hadi 400 humwagwa katika uke wa mwanamke. Baadhi ya spemu hizo huwa zina chromozomu X na baadhi zina chromozomu Y.
 
Hata hivyo, ni spemu moja tu ambayo hutakiwa kwa ajili ya kurutubisha yai la mwanamke nakuunda mimba.
 
Nadharia mbalimbali zinazotolewa kwa ajili ya kusaidia kuchagua ni jinsia gani unaitaka awe nayo mwanao, zinategemea suala la kuandaa mazingira katika uke na mwili wa mwanamume na mwanamke,yatakayosaidia spemu ya baba yenye chromozomu inayotakiwa irutubishe yai la mama, na hivyo kutungwa mimba ya jinsia inayotakiwa.
 
Njia ya Dr. Shettles ya kuzaa mtoto wa kike
Njia hii imekuwa ikitumiwa na watu wengi kwa miaka mingi sana na imewasaidia kuweza kuzaa mtoto wa kike.
 
Wengi wanasema kuwa uwezekano wa kufanikiwa njia hii ni asilimia 90. Njia ya Dr. Shettles inategemea msingi kwamba, chromozomu Y (yenye kuwezesha kutungwa mimba ya mtoto wa kiume) ni ndogo na yenye kwenda kwa kasi zaidi ikilinganishwa na chromozomu X(yenye kuwezesha kutungwa mimba ya mtoto wa kike) ambayo ni kubwa na huenda polepole.
 
Pia kwa kutegemea kuwa chromozomu X inaishi muda mrefu zaidi kuliko ile ya Y.Hivyo Dr. Shettles anashauri kuwa iwapo unataka kuzaa mtoto wakike uhakikishe kuwa:
 
1.Unajamiiana siku 2 au 3 kabla ya Ovulation. Kinadharia spemu za kiume zitakuwa zimeshakufa hadi kufikia siku hasa ya Ovulation na kuziacha spemu za kike zikiwa hai tayari kurutubisha yai na kuunda mtotowa kike.
 
2.Anashauri pia wanawake wajizuie kufikia kileleni (orgasm) kwani hali hiyo itaufanya uke uwe na hali ya asidi ambayo ni kwa faida ya spemu ya kike yenye chromozomu X.
 
3.Pia anawashauri wazazi wanapojamiina wawe katika haliya mwanamke kulala chini na mwanamume juu au missionary position. Kwani anasema kuwa mtindo huo huziwezesha spemu zenye chromozamu X zimwagike karibu na mlango wa uke na kuwa na uwezekano mkubwa wa kuingia ukeni na kutungwa mimba.
 
Kuna wengine wanaamini kwamba baadhi ya lishe na vyakula vya aina mbalimbali husaidia kutunga mimba ya mtoto wa kike.
 
Kwa mfano kuna wanaoamini kuwa kula baadhi ya vyakula huufanya uke uwe na hali ya asidi ambayo husaidia Chromozomu Y ife katika uke.
 
Nadharia nyingineyo inayotumiwa katika kuchagua jinsia ya mtoto inasema kwamba,mwanamke anayetaka kubeba mimba ya mtoto wa kike ale vidonge vya virutubisho (supplements) vya Calcium na Magnessium mwezi mmoja kablaya kubebea mimba.
 
Iwapo unataka kutumia vidonge vya virutubisho ili uweze beba mimba ya mtoto wa kike, ni bora ushauriane na daktari wako kwanza.
 
Hii ni kwa sababu dawa hizo huweza kuingiliana na dawa nyinginezo za magonjwa mbalimbali.
 
Baadhi ya vyakula vinavyotajwa kuwa vinasaidia katika kutunga mimba ya mtoto wa kike ni.
 
-->>>Mahindi, nyama, maharagwe, samaki, tunda damu, mayai na maini.
 
Vyakula hivyo ni vya asidi hivyo huifanya PH ya mwili wako hupungua na kuwa ya acidi. Hali hiyo husaidia kuua spemu za Y na hivyo kusaidia kuzifanya spemu za X ziwe na uwezekano mkubwa wa kurutubisha yai.
 
Hivyo mwanamke anayependelea kubebea mimba ya mtoto wa kike anashauriwa kutokula vyakula vyenye alikali ambavyo ni kama, ndizi, chokleti, juisi ya machungwa, viazi, tikiti maji na vinginevyo.

Mkongo: Kibongo ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
********************************
SUPER MKONGO MPYA,
_______________________________
********************************
Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile,

- kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa
- maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo
- kukosa hamu ya tendo la ndoa
- kushindwa kurudia tendo la ndoa
- maumbile kusimama kwa kulegea
-  kulegea katikati ya tendo
- kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu
- kuishiwa nguvu kutokana na punyeto.

Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MCONGO MPYA, kiboko ya matatizo haya.
_______________________________
Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume
_______________________________
(1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea.
(2) ngiri
(3) kuugua chango la uzazi kwa muda mrefu.
(4) kupungukiwa hormone za testosterone.
(5) ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na visivyo na virutubisho  vya kutosha.
(6) kutokufanya mazoezi na mwenendo wa maisha.
(7) kisukari.
(8) tumbo kuunguruma na kujaa gesi.
(9) maumivu ya kiuno nk.
_______________________________

WASILIANA NA:
DR. MCONGOMANI
SIMU NO:
📞0658816558
📞0682323682
Popote ulipo huduma hii inakufikia

Tiba Halisi ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
*NKOLOMIJE*/
√Ni dawa bora ya mitishamba yenye kuimarisha, kurefusha na kukufanya uwe imara hata kama umelala pia huimarisha na kukuza  maumbile yaliyosinyaa na kuwa regevu

*📌SUPER GAFINA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri ya uume ulio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/


Bado hujachelewa

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM  AU UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO SIMU NO:/
*📞0752723508*

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Serikali yawatoa hofu wakulima wa zao la Pamba nchini

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Serikali imewahakikishia soko wakulima wa pamba katika mikoa yote inayolima zao hilo kwa kufungua masoko katika maeneo yao ili waweze kuuza kwa bei elekezi ya shilingi elfu mmoja na mia mbili.

Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Kassim Majaliwa baada ya kutembelea kiwanda cha Kuchambua pamba cha Fresho mkoani Shinyanga na kujionea hali halisi ya ununuzi wa pamba kutoka kwa wakulima unaofanywa na Kampuni ya Fresho Investment Company Limited.

Amesema pamba yote iliyozalishwa na wakulima wa katika msimu huu wa kilimo  itanunuliwa kwa bei elekezi ya shilingi elfu 1,200   hivyo wakulima wasiwe na hofu makampuni mbalimbali nchini yanaendelea na ununuzi wa zao hilo.

Amefafanua kuwa anaendelea ziara kwenye mikoa inayolima pamba lengo la kufuatilia mwenendo wa masoko ya pamba na katika mkoa wa  Shinyanga ameshuhudia namna zoezi la ununuzi linavyoendelea unaofanywa na kampuni ya fresho.

Katika hatua nyingine Waziri Majaliwa amempongeza  Mkurugenzi Kampuni ya Fresho Fredy Shoo kwa  kununua pamba kama serikali tunakushukuru  na tutakulinda,hatutakuangusha. Hapa kuna mkuu wa mkoa,ukipata tatizo usisite kumuona.

Mbali na hilo  Majaliwa amewapongeza wakulima kwa kuzingatia usafi kwenye pamba kwa kuachana na tabia ya kuweka maji,mchanga,mafuta na takataka mbalimbali zinazosababisha pamba ichafuke na kuchangia sasa pamba ya Tanzania inapendwa duniani kote.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images