Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Mkuu: Watakaohujumu Ushirika Kuchukuliwa Hatua

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameagiza watendaji wote watakaobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa na ubadhirifu katika vyama vya ushirika wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria.

Kadhalika, Waziri Mkuu amewataka viongozi wote wa ushirika nchini wahakikishe wanaongoza vyama vya ushirika kwa kufuata Sheria ya Ushirika Namba 6 ya mwaka 2013, kanuni na taratibu zilizopo.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Alhamisi, Agosti 8, 2019) katika kilele cha maadhimisho ya sikukuu ya wakulima nane nane Kitaifa kwenye viwanja vya maonesho Nyakabindi mkoani Simiyu kwa niaba ya Rais Dkt. John Magufuli.

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kutoa rai kwa Wanaushirika wote nchini kuhakikisha wanachagua viongozi wenye weledi, wachapakazi, waadilifu na wanao upenda ushirika ili ushirika uimarike na kuwa endelevu.

Amesema historia inaonesha kwamba miaka ya nyuma ushirika ulifanya kazi nzuri katika kusimamia uzalishaji, tija, uchakataji na masoko ya mazao. “Hata hivyo, ushirika ulianza kulegalega katika miaka ya 1980”.

Waziri Mkuu amesema kutokana na hali hiyo, Serikali iliamua kuanzisha Tume ya Maendeleo ya Ushirika kama chombo cha kusimamia shughuli za maendeleo ya ushirika nchini.

Amesema katika kuimarisha vyama vya ushirika nchini, tume hiyo imeendelea kuweka mazingira rafiki kwa Vyama vya Ushirika ili kuzalisha kwa tija na kuongeza uzalishaji kutokana na matumizi ya zana bora za kilimo. Amesema vyama vya ushirika 33 vimekopeshwa trekta moja kwa kila chama kupitia makubaliano yaliyofikiwa kati ya Tume na Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) na Bodi ya Pamba (TCB).

Pia, Waziri Mkuu amesema katika kuendeleza azma ya Serikali ya kuwa na uchumi wa viwanda, Vyama vya Ushirika vimeendelea kuwekeza katika miradi mingine ya kimaendeleo ambayo inaisaidia katika kuleta maendeleo.

 “Hadi kufikia Juni 30, 2019 jumla ya Vyama vya Ushirika 104 vinamiliki viwanda vidogo kwa ajili ya kuongeza thamani ya mazao wanayoyazalisha hali ambayo imeleta tija kwa jamii inayozunguka maeneo hayo”.

Amesema hadi Desemba 2018, mikopo yenye thamani ya sh. trilioni 1.3 imetolewa kwa wanachama ikilinganishwa na sh. bilioni 902 iliyotolewa kufikia Desemba 2017. Akiba na amana za wanachama katika SACCOS zimefikia sh. bilioni 575 na hisa sh. bilioni 79.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu kwa mara nyingine, ametumia fursa hiyo kuwaelekeza Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya wafanye tena mapitio ya idadi ya Maafisa Kilimo waliopo Wilayani na kuwahamishia katika kata na vijiji ili kuimarisha usimamizi wa mazao.

Hivyo, Waziri Mkuu amesema ngazi ya Makao Makuu ya Wilaya wabaki wataalamu wawili akiwemo Mkuu wa Idara na msaidizi wake kwa ajili ya uratibu. Maafisa Kilimo wa Wilaya wawe na ratiba za kwenda vijijini kuwatembelea maafisa ugani ili kutatua changamoto zinazowakabili katika uendelezaji wa kilimo na hawapaswi kukaa maofisini.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya Nane Nane ya mwaka huu inasema: - “Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa Ukuaji wa Uchumi wa Nchi”. Kaulimbiu hiyo inakwenda sambamba na azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kukuza uchumi wa viwanda na biashara, ikilenga kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja, Pato la Taifa na wakati huo huo kupunguza umaskini.

Awali, Waziri Mkuu alitembelea na kukagua mabanda mbalimbali katika maoneosho hayo. Miongoni mwa mabanda aliyoyatembelea ni pamoja na banda la EPZA, NMB, CRDB, NBC, BOT kitengo cha mifumo ya malipo ya Kielektroniki ya Serikali, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi na JKT.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally, Waziri wa Ulinzi Dkt. Hussein Mwinyi, Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina, Naibu Waziri Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, Naibu Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI, Josephat Kandege, Naibu Waziri wa Madini, Stansalaus Nyongo pamoja na maafisa wengine wa Serikali.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Dkt Shein: Nchi Za SADC Tutoe Kipaumbele Kwa Bidhaa

$
0
0
Na Mwandishi Wetu,  MAELEZO
RAIS wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein amezitaka Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuweka mkazo wa matumizi ya bidhaa zake  na wataalamu wake wa ndani katika kutengeneza fursa za ajira na masoko ndani ya ukanda huo ili kukuza sekta za viwanda na biashara ndani ya jumuiya hiyo. 

Akizungumza katika hafla ya kufunga Maadhimisho na Maonesho ya Nne ya Wiki ya Viwanda katika Nchi za SADC leo Alhamisi (Agosti 8, 2019) Jijini Dar es Salaam, Rais Shein alisema umefika wakati kwa mataifa hayo kuzalisha bidhaa bora zenye kuweza kuleta ushindani katika masoko ya ndani na nje ya Jumuiya hiyo. 

Dkt. Shein alisema Mataifa ya SADC hayana budi kutumia fursa ya maonesho hayo katika kutangaza fursa za ujuzi na ubunifu  kwa kuzalisha na kutengeneza mtandao wa imara wa mawasiliano baina ya Nchi hizo na kuweza kuwa na soko la pamoja litakalowawezesha kutengeneza fursa za ajira kwa wananchi wa Mataifa hayo. 

Kwa mujibu wa Dkt. Shein aliongeza kuwa ili kufikia malengo ya uzalishaji wa bidhaa bora za viwandani ni wajibu wa Serikali zote kutengeneza mtandao imara wa miundombonu ikiwemo matumizi ya tekonolojia ya habari na mawasiliano kwa kuunda mikakati ya pamoja ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Jumuiya hiyo uliolenga katika kuimarisha sekta ya viwanda ndani ya jumuiya hiyo. 

“Hatujakataa mchango wa wataalamu na bidhaa za nje, lakini chako ni chako na mwenzako si chako, hivyo hakikunyima usikasirike, ni wakati wetu sasa kuweka mkazo katika kutegemea wataalamu wetu na teknolojia zetu katika uzalishaji wa bidhaa zetu” alisema Dkt. Shein.  

Aliongeza kuwa Nchi za Jumuiya hiyo hazina budi kutumia fursa za Maonesho na midahalo mbalimbali ya wataalamu inayojadiliwa katika Mikutano ya Jumuiya hiyo ili kuweza kubaini changamoto na hatua mbalimbali zinazopaswa kuchukuliwa ili kuiwezesha jumuiya hiyo kupiga hatua kubwa za Maendeleo ikiwemo kutengeneza fursa za ajira kwa wananchi wake. 

Akifafanua zaidi Dkt. Shein aliongeza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Zanzibar zimekuwa zikichukua hatua mbalimbali katika uboreshaji wa miundombinu ya miradi ya Maendeleo ambayo imekuwa kichocheo kikubwa cha fursa za ajira kwa vijana sambamba na kutengeneza mazingira wezeshi kwa sekta binafsi kushiriki katika uchumi wa viwanda. 

Akitolea mfano, Dkt. Shein alitaja baadhi ya miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa mradi wa reli ya kisasa (SGR), ujenzi wa viwanda  vikubwa, vya kati na vidogo ambavyo kwa pamoja vinaifanya Tanzania kuwa kielelezo cha mfano katika Nchi za SADC katika utekelezaji wa Ajenda ya Maendeleo ya Viwanda ndani ya Jumuiya hiyo. 

Kwa upande wake, Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa alisema maonesho hayo yamekuwa chachu na kipimo kwa Nchi za SADC kutekeleza ajenda yake ya Viwanda, kwa kuwa makundi mbalimbali ya wazalishaji, wafanyabiashara na watoa huduma wameonesha udhubutu wa kufikia malengo hayo katika Nchi wanachama wa jumuiya hiyo. 

Aliongeza kuwa jumla ya washiriki 5352 walishiriki katika midahalo mbalimbali ikiwemo Nchi SADC 14, taasisi za umma 64, viwanda 64, taasisi za kifedha 35, ambazo zote kwa pamoja zilitoa uzoefu na kuweza kuongeza fursa ya masoko na kuweza kuimarisha mitandao ya mawasiliano baina yao.  

Naye Waziri wa Habari, Utalii na Malikale wa Zanzibar,     Mahmoud Thabit Kombo alisema ili kufikia malengo ya Mpango Mkakati wa Jumuiya hiyo, nchi za SADC hazina budi kutoa na kuweka mkazo wa ushiriki wa sekta binafsi katika ujenzi wa uchumi shirikishi, kwa kuwa ushirikiano baina ya sekta hiyo na serikali utawezesha kutengeneza fursa mbalimbali za kiuchumi katika mataifa hayo. 

Naye Katibu Mtendaji wa Jumuiya hiyo, Dkt. Stagomena Tax, aliisifu Serikali ya Tanzania kwa kuwa mfano ndani ya Jumuiya hiyo katika eneo la ujenzi wa uchumi wa viwanda, na hivyo kuzitaka nchi nyingine kuiga mfano huo ili kuweza kuleta mtangamano ndani ya Nchi wanachama. 

Aliongeza kuwa ili kuweza kujenga uchumi jumuishi kwa wananchi ndani ya jumuiya hiyo, Sekretarieti ya jumuiya hiyo itaelekeza nguvu yake katika kuimarisha miundombinu ya usafiri wa bidhaa zilizopo ndani ya jumuiya hiyo, kwani bila miundombinu ya uhakika hakutoweza kuwa na mazingira wezeshi ya kuwasaidia wananchi ikiwemo kuondoa vikwazo vya kibiashara ndani ya jumuiya hiyo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa 09 August

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi August 10

Breaking: Lori la Mafuta Laripuka Na Kuua Idadi Kubwa ya Watu Morogoro

$
0
0
Idadi kubwa ya Watu wanasadikiwa kufariki Duania  baada ya kuungua na moto kufuatia Lori la mafuta kulipuka eneo la Msamvu mjini Morogoro. 

Watu hao wanadaiwa kuwa walikuwa wakiiba mafuta kwenye Lori hilo ambalo lilipata ajali majira ya saa 1:00 Asubuhi leo Aug 10.

Endelea kuwa nasi kwa habari kamili

RPC Morogoro Kasema Zaidi ya Watu 56 Wamefariki Dunia Katika Ajali ya Lori Lililowaka Moto

$
0
0
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Wilbroad Mutafungwa amesema karibu watu 56 wamepoteza maisha baada ya lori la mafuta ya petroli kupinduka eneo la Msamvu mkoani Morogoro na kuwaka moto

Ajali hiyo imetokea leo Jumamosi August 10, 2019  umbali wa mita 200 kutoka kituo kikuu cha mabasi Msamvu ukitokea Dar es Salaam.

Imeelezwa kuwa , baada ya lori hilo kupinduka, watu walianza  kujazana  wakigombania kuchota mafuta ambapo mmoja wa waliokuwa wakichota mafuta hayo alianza kuvuta betri ya gari na ikawa ndo chanzo cha moto kulipuka

Utupaji Holela wa Taka Kudhibitwa

$
0
0
Na Lulu Mussa,Mwanza
Serikali imezitaka halmashauri zote nchini, kutenga maeneo maalumu mbali na makazi ya watu yatakayotumika kujenga madampo ya kisasa ili kuzingatia hifadhi ya mazingira.
 
Rai hiyo imetolewa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima mara baada ya kutembelea na kukagua ujenzi wa dampo la kisasa linalojengwa eneo la Buhongwa Jijini Mwanza.
 
Alisema ujenzi wa huo wa dampo la kisasa utasaidia juhudi za Serikali za kutotumia fedha nyingi kwenye ununuzi wa vifaa tiba kwa kuwa taka zitakazolishwa katika Jiji la Mwanza zitapelekwa dampo kwa wakati na kunusuru magonjwa ya mlipuko.

“Huwezi kutenganisha afya na mazingira, mradi huu ni mkubwa sana na kwa namna utakavyotekelezwa hatutaraji kuona taka mjini zinazagaa.Tunatarajia kuona taka zote zinakuja hapa,” alisema Sima.

“Natoa rai kwa halmashuri zingine ambazo zinatekeleza miradi ya kimkakati kutoa kipaumbele kwa ujenzi wa madampo ya kisasa”.

Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Kiomoni Kibamba alisema dampo hilo lina ukubwa wa hekta 34 na linatarajia kukamilika desemba mwaka huu na kwa sasa ujenzi upo asilimia 78 ukigharimu Sh bilioni 16.6, ukienda sambamba na ujenzi wa barabara.

“Dampo hilo litakuwa na chemba sita za kuhifadhi taka na mabwawa ya kuhifadhi maji taka, barabara za kisasa zenye urefu wa kilomita 1.9, taa za nishati ya jua na maabara maalumu ya kupima maji taka” Kibamba alisema

Kukamilika kwa dampo hilo la kisasa litakuwa na uwezo wa kuteketeza taka mara baada ya kufikishwa kwenye eneo hilo na,litaongeza  mapato katika jiji hilo

Kwa mujibu wa Kibamba, tani 33 hadi 36 zinatarajia kupelekwa katika dampo hilo mara baada ya ujenzi kukamilika na linatarajia kudumu kwa zaidi ya miaka 15

Rais Magufuli atoa salamu za rambirambi kufuatia vifo vya ajali ya lori la mafuta Morogoro

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa ya vifo vya watu zaidi ya 60 na majeruhi takribani 70 walioungua kwa moto baada ya lori lililokuwa na shehena ya mafuta kupata ajali na kisha kulipuka moto Mjini Morogoro.

Ajali hiyo imetokea leo tarehe 10 Agosti, 2019 majira ya saa 2 asubuhi ambapo lori hilo lililokuwa linatoka Dar es Salaam limepinduka jirani na Kituo Kikuu cha Mabasi cha Msamvu baada ya dereva wa lori kumkwepa mwendesha pikipiki na kisha mafuta yaliyokuwa yakimwagika kushika moto na kuunguza watu waliokuwa wanayachota.

Mhe. Rais Magufuli ametoa pole kwa familia, ndugu, marafiki na wote waliopoteza jamaa zao katika ajali hii na pia amewaombea majeruhi wapone haraka.

“Nimeumia sana kusikia idadi kubwa ya Watanzania wenzetu waliopoteza maisha katika ajali hii, natoa pole kwa wote walioguswa na vifo hivi hasa familia za Marehemu wote, nawaombea Marehemu wapumzike mahali pema peponi na majeruhi wote wapone haraka” amesema Mhe. Rais Magufuli na kumuagiza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Steven Kebwe kufikisha salamu zake za pole kwa familia na wote walioguswa na vifo hivyo.

Mhe. Rais Magufuli ameagiza Wizara zote zinazohusika kushughulikia ajali hii na ametaka Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa kushirikiana na Hospitali ya Taifa Muhimbili kuhakikisha majeruhi wote wanapatiwa matibabu ili kuokoa Maisha yao.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli ameelezea kusikitishwa kwake na vitendo vya watu kuvamia magari yanayopata ajali kwa lengo la kujipatia bidhaa mbalimbali zilizobebwa na magari hayo na ametaka vitendo hivyo vikome.

“Baadhi ya magari haya yanabeba mafuta ambayo ni hatari kama ilivyotokea Morogoro, yapo magari yanabeba kemikali za sumu, yapo magari yanabeba milipuko nakadhalika, nawaomba sana tuache tabia hii” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
10 Agosti, 2019

Ujumbe Wa SADC Watembelea Viwanda Kikiwemo Kiwanda Kikubwa Cha Kuzalisha Malumalu Afrika Mashariki Na Kati

$
0
0
NA.Mwandishi Wetu-MAELEZO.
Wawakilishi wa Ujumbe wa SADC wametembelea viwanda Vitatu katika Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo na Chalinze kikiwemo kiwanda kikubwa za kuzalisha malumalu(Tiles) kwa Afrika Mashariki na Kati cha KEDA. 
 
Akizungmza katika ziara hiyo Mwakilishi wa Ujumbe wa SADC,Genoveva Kilabuka, alisema kuwa ujumbe kutoka SADC umefurahishwa kuona Tanzania inasonga mbele kwenye utekelezaji wa ujenzi wa viwanda kwani ndiyo azma kubwa kwa nchi pamoja na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika SADC.
 
Lengo kubwa la ziara hiyo ni kujifunza namna ya uzalishaji wa bidhaa kwa kutumia malighafi mbalimbali za ndani ili kuongeza thamani ya malighalifi hizo kwa kuchakata na kuzalisha bidhaa zilizobora kwa masoko ya ukanda wa Kusini mwa afrika hususani katika nchi wanachama wa Jumuiya hiyo.
 
“Kwa kweli tumefarijika kuona Tanzania ya Viwanda inasonga mbele sawasawa na mikakati yetu ya kuendeleza viwanda vinavyotumia malighafi za ndani, huu ni mkakati mkubwa wa nchi na SADC ambao unasisitiza ujenzi wa viwanda  ili kutengeneza ajira kwa vijana wengi, kwa hiyo tumeendana kabisa na kauli mbiu ya mwaka huu ya Wiki ya viwanda SADC, “ kwa hiyo viwanda hivi ni moja ya alama kubwa Nchini kwetu”, Alisema Genoveva.
 
Alisema kuwa katika kutekeleza mikakati ya kufanya  viwanda kuwa endelevu Jumuiya ya SADC ni muhimu kwa soko la bidhaa zinazozalishwa nchini, SADC inajikita zaidi kusisitiza ujenzi wa Viwanda na ikiwa Wilaya ya Bagamoyo ina takribani viwanda 65 vikiwemo viwanda vikubwa vilivyotembelewa na wajumbe kutoka SADC, viwanda hivyo ni Elven Agri, SAYONA na kiwanda kikubwa Afrika Mashariki na Kati cha kuzalisha Malumalu cha KEDA, na mkakati huo unalenga zaidi kuzalisha ajira kwa vijana wa nchi wanachama SADC.
 
Genoveva alitoa rai kwa wazalishaji wa viwanda nchini kuchangamkia Fursa zilizoko SADC ili kuweza kupanua masoko kwa bidhaa zao kwenye nchi mbalimbali zilizoko Ukanda huo wa Afrika, kwani shughuli za Jumuiya hiyo sasa zitahamia Tanzania ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.John Pombe Magufuli atakuwa Mwenyekiti wa SADC kwa muda wa mwaka mmoja.
 
“Ni rai kwa wenye viwanda kama hiki cha KEDA kinachotoa ajira za moja kwa moja kwa watanzania 1,000, na ajira ambazo siyo za moja kwa moja 3,000, tumieni fursa hii ambayo Tanzania tutakuwa wenyeji wa Jumuiya ya SADC kwa muda wa Mwaka mmoja  ili kujitangaza na kupata soko, kwani shughuli nyingi za Jumuiya hii zitafanyika Tanzania”, Alisisitiza Genoveva.
 
Kwa Upande wake Katibu Tawala Wilaya ya Bagamoyo, Kasrida Mgeni kuwa ni fursa kubwa kutembelewa na Ujumbe wa SADC kwani ujio wao utafungua mtandao mkubwa wa kujua masoko ya kupeleka bidhaa zao kwenye nchi wanachama wa Jumuiya hiyo ya kusini mwa Afrika.
 
Mgeni alisema kuwa kati ya mikoa ambayo ina viwanda vingi, Mkoa wa Pwani moja wapo huko halmashauri ya Bagamoyo ikiwa na viwanda takribani 65 huku viwanda 6 vikiwa ni vikubwa na ugeni huo ulipata kutembelea viwanda vitatu vikiwemo Elven Agri, SAYONA na kiwanda cha kuzalisha  Malumalu cha KEDA.
 
“Ujumbe huu ni muhimu sana kwetu, na kama mnavyofahamu Mkoa wetu wa pwani una viwanda vingi na Wilaya yetu ya Bagamoyo tuna takribani viwanda 65,na  viwanda 6 kati ya hivyo ni vikubwa kwa hiyo ugeni huu utaweza kufungua Fursa ya kupata masoko kwa Nchi wanachama wa SADC”, Alisema Mgeni.
 
Mgeni alisema kuwa wawakilishi hao kutoka SADC, wataiwezesha Serikali, Wananchi pamoja na wawekezaji kupat fursa kubwa ya masoko na kutengeneza faida kubwa itakayowezesha ujenzi wa viwanda vingine na kutengeneza ajira kwa vijana nchini.
 
Naye Afisa Masoko kutoka kiwanda cha Alven Agri, Salumu Kabuluta alisema kuwa ugeni wa SADC katika kiwanda hicho siyo tu fursa kwa nchi bali utawezesha uzalishaji kuimarika na kuweza kutimiza kikamilifu ujenzi wa Tanzania ya Viwanda kama Sera ya Serikali ya Awamu ya Tano inayosisitiza kuwa na uchumi wa viwanda.
 
“Tukiendana na sera ya Serikali ambayo inataka Tanzania iwe na viwanda vingi na tukihusianisha na hii wiki ya viwanda ya Jumuiya ya Maendeleo kusini mwa Afrika SADC, sisi kama kampuni ya kitanzania tuahakikisha zaidi suala la viwanda linafanikiwa na sasa nchi yetu inaenda kuwa wenyeji wa SADC kwa hiyo masoko ambayo yapo kwenye nchi hizi 15 tutaweza kuyafikia kwa kirahisi.
 
Alisema kuwa mpaka sasa bidhaa zao zimefika nchi hizo zikiwemo Zambia, Congo DRC, Malawi na Botswana na Mkutano wa SADC itakuwa ni kichocheo zaidi ya Bidhaa zao kuweza kuenda kwenye nchi hizo 15 ili kukuza masoko ambayo hapo awali hayakuwepo.
Mwisho.

DC Ndejembi : Waliofanya Ubadhilifu Wa Fedha Ujenzi Wa Kongwa Sekondari Watazitapika.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Mkuu wa wilaya  Kongwa jijini Dodoma Deo Ndejembi amesema wahusika wote waliofanya ubadhilifu wa fedha za ujenzi katika Shule ya Sekondari Kongwa mkoani Dodoma Watazitapika.
 
Ndejembi amesema hayo Agosti 9,2019  alipofanya ziara shuleni  hapo kwa lengo la  kuangalia mwenendo wa  ujenzi wa Shule ya Sekondari Kongwa Dodoma   unaogharimu  zaidi ya  Tsh.Milioni 290 fedha zilizotolewa na Serikali.
 
Mkuu huyo wa wilaya ametaja miundombinu inayojengwa katika shule hiyo ni pamoja na mabweni mawili ambapo  kila moja lilitengewa  Tsh.Milioni 75 lakini hayatakamilika kutokana na fedha kuisha,Bwalo lilitengewa milioni 100 lakini nalo pia halitakamilika kutoka na kubaki mifuko ya saruji 40 pekee .
 
Hata hivyo, amebainisha kuwa kwa upande wa Madarasa yatakamilika kwa milioni 36 huku  fedha zilizobaki kwenye akaunti ni milioni 74  pekee ambazo hazitaweza kutosheleza katika ukamilishaji wa miundombinu yote na zilizobaki nje ya akaunti laki moja na nusu pekee.
 
Mhe.Ndejembi amesema sababu zilizosababisha majengo hayo kutokamilika licha kutengewa fedha nyingi ni kutokana na kutofuata maelekezo ya Serikali ya kutumia Force akaunti ambapo walitangaza tenda hali iliyosababisha ununuzi wa vifaa vya ujenzi kununuliwa kwa bei kubwa tofauti na ilivyo kawaida na ameshangazwa kwa maeneo mengine hapa nchini yamekamilika.
 
Hivyo Mkuu huyo wa wilaya ameagiza TAKUKURU kufuatilia bei ya Manunuzi ya Bidhaa hizo za Ujenzi ,milioni 74 zilizobaki kwenye akaunti zisitume mpaka uchunguzi ukamilike  na wale  wote waliohusika katika ubadhilifu huo wanachukuliwa hatua kwa kumdanganya  na kumdharau Rais,Waziri wa TAMISEMI pamoja na yeye.

Waziri Mkuu Awalilia Waliofariki kwa Ajali ya Lori Morogoro

$
0
0
Waziri Mkuu  Kassim Majaliwa ametumia dakika moja kuwaombea dua majeruhi na watu waliopoteza maisha yao kwenye ajali ya moto iliyotokea leo asubuhi katika eneo la Msamvu- Mkoani Morogoro.

Akitoa salamu za pole kabla ya kuanza hotuba ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Wanafunzi wa Elimu ya Juu nchini (Tahliso) unaofanyika katika ukumbi wa Nkuruma, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) leo Jumamosi, Majaliwa amesema ajali hiyo inasikitisha.

"Mpaka sasa kuna majeruhi zaidi ya 63 hali zao sio nzuri sana, tunawaombea kwa Mungu ili wapone haraka. Ajali hii imetokana na lori na ndugu zetu hawa walienda kujipatia mafuta," amesema Majaliwa.

Akizungumzia mkutano huo, Majaliwa amesema amani na utulivu vilivyopo kwenye vyuo vya elimu ya juu nchini vinaonyesha kuna watu wanatekeleza wajibu wake ipasavyo.

Amempongeza Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako na taasisi zilizo chini ya wizara hiyo kwa kuendelea kutatua changamoto zinazowakabili wanafunzi wa elimu ya juu.

Waziri Mkuu: Bodi Ya Mikopo Tafakarini Vigezo Vya Kutoa Mikopo Kwa Wanafunzi

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameutaka uongozi wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kutafakari namna ya kurekebisha baadhi ya dosari zilizopo likiwemo suala la kuwanyima mikopo wanafunzi kwa kutumia kigezo cha kusoma katika shule binafsi.

Amesema kuna baadhi ya wanafunzi ambao wamefaulu vizuri kidato cha nne na wamekosa nafasi katika shule za Serikali na wanatoka katika familia zisizokuwa na uwezo, hivyo wanatafuta wafadhili ambao wanawasomesha kwenye shule binafsi.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumamosi, Agosti 10, 2019) wakati akifungua mkutano Mkuu wa Mwaka wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO) kwenye ukumbi wa Nkrumah, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Amesema kitendo cha bodi hiyo kuwanyima mikopo baadhi ya wanafunzi kwa kigezo cha kusoma katika shule binafsi bila ya kujiridhisha kama wanatoka kwenye familia zenye uwezo au zisizokuwa na uwezo kinawanyima wanafunzi hao fursa za kuendelea na masomo.

 Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwaonya wakuu wa vyuo vikuu ambao wanatumia vibaya fedha za mikopo ya wanafunzi kwa kuzipeleka katika miradi mbalimbali baada ya kuzipokea kutoka HESLB na kuwacheleweshea wanafunzi stahiki yao.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amewaagiza viongozi wa vyuo vikuu kuimarisha mafunzo kwa njia ya vitendo kwani tafiti nyingi zinazohusu mambo ya ajira zimebainisha umuhimu wa mafunzo ya vitendo katika kumuwezesha mhitimu kuwa na uelewa na ujuzi mpana wa kile alichokisoma kwa njia ya nadharia.

“Vyuo viongeze umakini na ufuatiliaji wa karibu wa vijana wetu wanapokuwa kwenye elimu kwa vitendo ili kuhakikisha kwamba wanapata maarifa na ujuzi uliokusudiwa katika mitaala yao. Pia natoa wito kwa waajiri wa sekta ya umma na binafsi watoe ushirikiano wa dhati kwa wanafunzi wanaotafuta nafasi za kufanya mafunzo kwa njia ya vitendo kwenye taasisi zao.”

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TAHLISO, Bw. Peter Niboye amesema miongoni mwa changamoto zinazowakabili wanafunzi wa elimu ya juu ni ucheleweshwaji wa mikopo kwa baadhi ya vyuo licha ya HESLB kuwasilisha fedha hizo mapema, hivyo ameiomba Serikali kuwasaidia katika kutatua tatizo hilo.

Kadhalika, Mwenyekiti huyo wa TAHLISO, ameishukuru Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli kwa ushirikiano mkubwa inaoipatia jumuiya hiyo hivyo kurahisisha utendaji wake.

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Bw. Patrobas Katambi alimkabidhi Waziri Mkuu hati ya kiwanja kilichoko katika eneo la Mtumba jijini Dodoma kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za TAHLISO, ambapo baada ya kupokea hati hiyo, Waziri Mkuu aliikabidhi kwa Mkwenyekiti wa jumuiya hiyo Bw. Niboye.

Mkutano huo umehudhuriwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Paul Makonda, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Bw. Godfrey Chongolo, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Bw. Kisare Makori pamoja na viongozi kutoka vyuo mbalimbali nchini vinavyounda TAHLISO.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,        
JUMAMOSI, AGOSTI 10, 2019.

Korea kaskazini Yarusha Makombora Zaidi

$
0
0
Korea kaskazini imerusha makombora 2 ya masafa mafupi katika bahari  ya mashariki.

Taarifa zilizotolewa na jeshi la Korea kusini inasema majaribio ya makombora mawili yalifanyika mashariki mwa Korea kaskazini. 

Makombora hayo yaliyofikia kimo cha kilomita 48 baada ya kusafiri umbali wa kilomita 400 yalianguka bahari ya mashariki.

Kutana na Sheikh Omary Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali za Matatizo Yako Na Kutafsiri Ndoto kwa kutumia Vitabu vya QUR-AN

$
0
0
Sheikh Omary Ni bigwa wa kutatua matatizo kwa haraka, ni mtu aliye jaliwa kubuli Shufaa pia anatoa Duah  za Ruhia. Ukija na Maradhi yanaondoka hapo hapo bila kungoja kesho,  UKIPEWA MKONO  na Sheikh Omary .
 
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
 
Sheikh Omary ni Mtaalamu wa Nyota za Binadamu  Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
 
Je una NUKSI  zisizo kwisha.!? JE umekimbiwa na Mume/Mke na Anaishi na Mtu Mwingine..!? Muone Akutatulie,
 
Una kosa bahati ya wanaume au mume wa kukuoa..Unataka nyota ing'ae Au huna hamu na Mkeo/ Mumeo.
 
Jini mahaba. Kama Unakasirika ovyo ukiwa na bwana au mwanamke wako na  kumchukia Mpaka  kushindwa kufanya nae tendo la ndoa.
 
Njoo umuone Sheikh Omary  na ujuwe  yanayo kusibu.Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN

Mawasiliano: Sheikh Omary 0673531992. WhatsApp/Call
Tembelea Page ya @Mtabibu_Omar  @Mtabibu_Omar
Usome Makala Tofauti Tofauti Kama.

Huawei Waamua Kuachana na Android....Watengeza Program Yao

$
0
0
Kampuni ya Huawei imeweka wazi jina la programu endeshaji mpya kwa ajili ya simu na vifaa vya kisasa vya kielektroniki ambayo itaanza kutumika badala ya Android.

Mfumo huo wa Huawei-HarmonyOS unalenga kupunguza utegemezi wake kwa kampuni za Marekani.

HarmonyOS utakuwa tayari kuwekwa katika skrini za samart kwenye bidhaa kama vile Televisheni, saa za smart , na magari baadae mwaka huu, amesema Richard Yu, Mkurugenzi mkuu wa wa kitengo cha walaji cha Huawei katika mkutano wa ubunifu.
 
Katika kipindi cha miaka mitatu ijayo Huawei,kampuni ambayo ni ya pili kwa ukubwa duniani ya mauzo ya smartphone ,  imesema itaangalia jinsi ya kuuweka mfumo wa HarmonyOS kwenye vifaa zaidi zikiwemo simu zake za mkononi aina ya smartphones.
 
Kampuni ya Huawei inasema kuwa imeazimia kuendelea kutumia Android ,lakini HarmonyOS utatumika kama mpango mbadala kama mambo yataenda kombo

Tangazo hilo la Huawei limekuja miezi kadhaa baada ya serikali ya Marekani kuweka masharti ya kibiashara nchini Marekani yanayoilenga kampuni hiyo pamoja na kampuni nyingine washirika .

Serikali ya Marekani imeishutumu Huawei kwa kuiba siri za kibiashara , na ikasema inaleta hatari kwa usalama wa taifa.

Baada ya shutuma hizo , Google, Intel,na makumpuni mengine yanayochangia  kwa kiasi kikubwa katika teknolojia na utatuzi wa matatizo ya smartphone walisitisha biashara na Huawei

Ajali ya Moto Morogoro: Lugola Akatisha Ziara Yake Mkoani Rukwa

$
0
0
Waziri  wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola  ameamua kuahirisha  ziara yake Mkoani  Rukwa  kutokana na ajali ya moto iliyotokea eneo la Msamvu Mjini Morogoro.

Ajali hiyo imetokea leo tarehe 10 Agosti, 2019 majira ya saa 2 asubuhi ambapo lori hilo lililokuwa linatoka Dar es Salaam limepinduka jirani na Kituo Kikuu cha Mabasi cha Msamvu baada ya dereva wa lori kumkwepa mwendesha pikipiki na kisha mafuta yaliyokuwa yakimwagika kushika moto na kuunguza watu waliokuwa wanayachota.

Waziri huyo ameanza safari kuelekea eneo la tukio.

Jeshi la Polisi Lataja idadi kamili ya marehemu na majeruhi wa ajali ya moto mkoani Morogoro.

$
0
0
Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo Lebaratus Sabas,  ameitaja idadi ya watu waliofariki katika ajali ya gari iliyoanguka nakupelekea kulipuka kwa moto leo Agosti 10,  imefikia 62.
 
Ameeleza kuwa kati yao wanaume ni  58 na wanne ni wanawake ambapo mmoja katika wanawake hao ni mtoto.

Kwa upande wa idadi ya majeruhi imefikia  72, wanawake wakiwa 8 na wanaume 64 ambapo wote wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hosptali ya rufaa ya Morogoro.

Ajali hiyo imetokea majira ya asubuhi katika eneo la Msamvu Mkoani Morogoro na hadi sasa Jeshi la polisi,  limekwishakamata lita takribani 206 za mafuta ya petroli , zilizokuwa zimefichwa katika mabanda pembezoni mwa eneo la ajali ilipotokea.

''Pia katika eneo la  tukio zimepatikana pikipiki zilizoungua kwa moto zipatazo 26 na baiskeli 6, pia yamaeonekana mabaki ya madumu na ndoo za plastiki zilizoungua'' amesema Kamishna Sabas.

Aidha Kamishina Sabas amewataka wananchi wanaoishi kandokando  ya barabara kutokuwa na tamaa na kujiepusha na ajali ambazo zinaepukika, pamoja na kuwataka wale wote waliopata majeraha madogomadogo na  kutokomea wasisite kwenda hospitali kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Ufugaji wa nguruwe : Gharama na Faida Zake

$
0
0
 Utangulizi
Nguruwe ni mnyama amabaye hutumika kama chakula / mboga na pia ni zao la biashara kwa mfugaji, mjasirimali na mfanyabiashara.
 
NGURUWE HUTEGEMEA SANA MAMBO YAFATAYO
1 . Banda imara na rafiki kwake
2. Usafi ni muhimu sana katika banda la Nguruwe
3 Mchaganyo bora wa chakula
4. Tiba bora na kinga
5. Maji na Lishe ( access ya vyakula Muhimu kwake )
 
CHANGAMOTO
KATIKA UFUGAJI WA NGURUWE KUNACHAGAMOTO ZAKE LAKINI ZAWEZA KUTATULIWA KWA KUFATA MAMBO KADHAA.
Katika ufugaji wa nguruwe kunachagamoto ya vifo vya nguruwe wachanga ambao hupunguza faida ya biashara ya nguruwe kwa kupunguza idadi ya nguruwe wazima wa kuuzwa lakini utunzaji mzuri wa nguruwe wachanga huepusha vifo vinavyotokana na shida kama:
 
Matatizo ya kupumua
Ni kifo kinachosababishwa na mama anapomlalia nguruwe mchanga.chagamoto hii inaweza kutatuliwa kwa kuwatenga au kuwa na mabanda makubwa ya kulelea watoto.
 
Baridi
Nguruwe wachanga huathiriwa na baridi haswa katika majuma mawili au matatu ya mwanzo. Hii ni kwa kuwa wana kiwango kidogo cha utando wa mafuta wa kuwakinga.
 
Unashuriwa kuwaweka katika hali ya joto, wape matandiko na utumie vipasha joto kama vile kuwasha globu za joto kama utakuwa umewaweka kwenye mabanda ya kuta au nyumba yenye sakafu baridi.
 
Namna bora utunzaji wa nguruwe wachanga
Nguruwe moja wa kike ana uwezo wa kuzaa watoto 12. Namna ifuatayo itasaidia kupunguza idadi ya vifo vya nguruwe wachanga:
1.Pale nguruwe awapo na kidonda nyunyizia dawa ya ayodini 5% kwenye kovu ili kuzuia kuambukizwa kwa magonjwa.
2.Wawekee matandiko (nyasi kavu au maganda ya miti) mahali pa mapumziko ili wapate joto au utumie globu za joto.
3Wadunge sindano ya madini ya chuma (iron) siku ya tatu baada ya kuzaliwa ili kuzuia upungufu wa damu.
3. Yalainishe meno ya vichaga kabla ya masaa 24 ili kuzuia uharibifu wa matiti wakati wanaponyonya.
4. Watie vibandiko au utoboe masikio ili uwatambue na uhifadhi rekodi zao kama kuna umuhimu kama vile wafanyavyo wafugaji wa ng’ombe.
5. Wapime uzani wanapozaliwa na uhifadhi rekodi hiyo itakusaidia kujua ukuaji wao na maendeleo yao
6. Wahasi wale wa kiume juma la tatu, wale ambao hawafai katika kuendeleza kizazi kwa kutumia mtindo wazi (open method) kama unaona inafaa.
7. Wapatie dawa ya kuzuia minyoo pia zipo dawa za asili kama unga wa mkaa na majivu pia zipo za kitaalamu, wasiliana na wataalamu wa mifugo
8.Waachishe kunyonya katika juma la nane au wafikapo kilo 14 hadi 20 hii itasaidia kujitegemea na kukua kwa haraka.
 
Nguruwe Walioachishwa Kunyonya
1.Walioachishwa kunyonya wawekwe makundi ya 10 hadi 12 kulingana na uzito au ukubwa wao kwenye eneo ambalo watajitosheleza.
2.Watenganishe wakubwa kwa wadogo ili kuzuia kupigana.
3.Wakati wa kuwaachisha kunyonya mwondoe mama yao kutoka kwa watoto ili kupunguza usumbufu.
4Watoto wa nguruwe wa mama tofauti wasiwekwe pamoja maana hii husababisha mapigano kati yao na
5.Unapowachanganya watoto wa mama tofauti wapake mafuta ya gari yaliyotumika kwenye ngozi yao au mafuta ya kula ili kuiondoa harufu ya kutambulika ili wasipigane
 
FAIDA YA UFUGAJI WA NGURUWE
Faida kuu ya nguruwe ni zao la chakula lakini pia ni zao la kukuongezea kipato ukiwa kama mjasirimali / mfanyabiashara.
Lengo langu nikueleza namna unavyoweza kufuga na kutupa faida, Steps zifatazo ni muhimu kuzigatia.
 
JIPE MTAJI WA MILLION 4 / 3.5 KWA NGURUWE 50
UANDAAJI WA BADA WEKA MAKADILIO YA LAKI TANO (800,000/=) .
Hapo nazugumzia banda lenye heru U yenye mstatili ikiwa na kitako kirefu
Eneo lenye ukubwa wa mita 50 kwa 50 litafaa zaidi ili kuhakikisha usalama wa nguruwe wako na ukuaji bora.
1. Tafuta mabati used kwa bei ya 5000 mfano mabati 20 ya futi 10 /10 = 100,000/=
2. Tafuta mabazi ya futi 10 kwa 2000 kila moja utapata mabazi pic 100 = 200,000/=
3. Tafuta miti ya nguzo na kechi ya 1000 na 2000 miti ya 1000*70 na 2000*3 = 120,000/=
4. Tafuta chagalawe / moramu trip 10*3000 =30000/=
5. Cement mifuko kwa ajiri ya sakafu na mashimo ya kulishia 5 *18000 = 90,000/=
6. Misumari ya aina 4, nch 6 kg5,nch 3 kg5 nch 5 kg10 na nch4 kg10, Bawaba na komeo =100,000/=
7. Malipo ya fundi 75000 fundi uashi na 75000 fundi seremala =150,000
JUMLA HAPO INAKUWA 790,000/= MAKADILIO INAKUWA 800,000/=
 
UNUNUZI WA NGURUWE WA KUANZIA .
Nguruwe wadogo wadogo ni vinzuri zaidi kuanza nao kwa sababu watakuzalia watoto wengi na kwa muda mrefu . Chukua mfano MILLION 2.5 . Nguruwe wadogo wa dogo wanauzwa 50000 au 40000 inategemeana na mahala na maelewano . Milioni 2.5 inakupa vitoto 50 au 55 . Hivyo unawexa kuwa na vitoto jike 50 na vidume 5. baadaye ukaongeza madume matano ya kuazima au kukondi kwa ajiri ya kupandishia
 
MAANDALIZI YA CHAKULA
Mchaganyiko wa chakula cha nguruwe na gharama zake tunaweza ukadilia kujitosheleza kwa laki tatu kwa mwenzi mmoja kwa nguruwe hao 50, kwa 300,000/= , ambapo itajumuisha tiba / kinga, lishe, vyakula vya nguruwe vinaweza kuwa pumba ya mpunga ile laini,pumba ya mahindi, mashundu, mabaki ya magada ya vianzi amba mabaki ya chakula yaliyosalama
 
MALIPO YA MSIMAMIZI NA ENEO LA KUWEKEZA
Katika kipengele hiki makadilio ya juu ama ya chini kwa msimamizi wa kazi yako waweza mlipa 100,000/= ama chini yake pia kwa mwenye eneo huwa nimaelewano tu aunaweza pata kwa fair au kukakodi kwa laki tatu, 300,000/= kwa mika miwili.
 
HIVYO JUMLA YOTE YA GHARAMA ZA UAZISHAJI UWEKEZAJI WA NGURUWE 50 ZITAKUGHARIMU MILLION 4 AMA MILLION 3.5 KWA MAANA KUWA HAPO JUU NIMETUMIA MAKADILIO YA JUU NA UKIINGIA KWENYE UHALISIA KAMA MJASIRIMALI LAZIMA IPUNGUE NA KUFIKIA 3.5

KIPATO AU FAIDA YA UFUGAJI NGURUWE
Nguruwe wanafaida ya haraka na nimradi wa uhakika kabisa, ukipitiia mchanganuo hapo juu wa nguruwe 50 utatupa faida kama ifatavyo
 
Nguruwe huzaa Mara mbili kwa mwaka na huzaa watoto zaidi ya watanoyaani huzaa watoto 12 ama nane .
Basi chukua nguruwe 50 * vitoto 5 yaani ufanye kuwa nguruwe wako 50 wakupatie vitoto vitano vya uhakika
Nguruwe 50*5 = 250 ukijumlisha na wale 50 wa mtaji umakuwa nao 300 . Chukua zao la nguruwe la 250 na uza kwa 200000 kwa kila nguruwe yaan bei ya kawaida kabisa. Utapata Million 50.

Hivyo zao la kwanza ndani ya robo tatu ya mwaka inakutegenezea million 50 pia na mienzi sita ijayo inakupa tena 50 na zaidi ili kukamilisha uzao wa pili hii inkupa uhakika wa kutegeneza million 100 za uakakika ndani ya mwaka mmoja na nusu ama miaka miwili ukijipa timeframe work lakini kumbuka hapo tumefanya kwa hesabu ya uzao wa chini kabisa ambapo tumeangalia na hasara ya vifo kama vifo visipotokea na uzao ukawa mkubwa utakuwa na uhakika wa kutegeneza million 150 kwa miaka miwili.

Kwenye hesabu ya kuwale unaweza kuwaza sana kuwa itaongezeka na kukughalimu sana jibu ni hapana mpka kufikia kuuza hawatokugharimu zaidi ya million 7 je million 7 kwenye million 150 ni kitu kisicho nafaida ?
 
NB . jambo lolote linahitaji umakini naa dhamira ya dhati pia kushirikisha wataalamu na wenye uzoefu ili kufikia leng Ewe ndugu kila kitu kinawezekana UTAYARI WAKO / UTHUBUTU WAKO, UAMINIFU .NA MAAMZI YAKO.
 

Jinsi ya Kumtambua Mpenzi Tapeli na Muongo

$
0
0
Inawezekana upo katika uhusiano na tapeli wa mapenzi bila kujua, hiyo ni sumu na unachotakiwa kufanya sasa ni kuanza kumchunguza mpenzi wako mapema isije kuwa upo kwenye foleni!

Hakuna kitu kibaya kama kuwa katika foleni ya wapenzi kwa mpenzi mmoja, tena mbaya zaidi awe ni yule ambaye moyo wako umempenda kwa dhati.

Kumbuka, kuwa katika uhusiano na mtu ambaye haeleweki ni sawa na kukaribisha matatizo katika maisha yako, huna sababu ya kuishi kwa wasiwasi ukiwa hujui mpenzi wako anakuchukulia vipi.

Anza kumuwekea mitego mapema. Lakini katika mitego yako achana na simu yake kabisa, huna sababu ya kuchunguza simu yake lakini kama ni msaliti utajua tu, unafikiri atajificha mpaka lini?

Atafanya mambo yake gizani mpaka lini? Kuna siku utagundua na kumuacha aendelee na umalaya wake kama ameona ndiyo maisha. Usikubali kabisa kuwa katika penzi la kitumwa, penzi la kisaliti, kuwa na mtu ambaye anakuchanganya wa kazi gani zaidi ya kukupotezea muda na kukukaribishia machozi?

UTAMJUAJE MPENZI LAGHAI?
Hapa ndipo kwenye kazi, kwa bahati mbaya sana kama ikitokea ukampenda mtu sana hata kama akifanya mabaya kiasi gani unaweza usiyaone, kama wewe ni wa aina hii unapaswa kubadilika kifikra. Mwone wa kawaida, fanya uchunguzi wako polepole na kama ukiona moja kati ya mambo yafuatayo, ujue kuna kitu.

(a) Hataki ujulikane na rafiki zake
Hii ni kati ya alama walizonazo matapeli wa mapenzi, ni mtu wa kufanya mambo kwa upekee sana. Kila dakika hakaukiwi na neno nakupenda sana, lakini moyoni mwake hakuna alama hata moja ya mapenzi kwako.

Ni vigumu kumtambua mtu wa aina hii lakini chunguza kuhusu hili, hapendi kabisa kukukutanisha na rafiki zake na hata mkikutana nao kwa bahati mbaya basi hatakutambulisha na kama akikutambulisha hatakutambulisha kama mpenzi wake rasmi. Ataishia kusema ninyi ni marafiki mlioshibana!

Tangu lini mpenzi akatambulishwa kama rafiki? Mtu anapomtambulisha mpenzi wake humtambulisha kwa kujisikia furaha moyoni kwamba anamtambulisha mpenzi wake lakini inakuwaje kwako akutambulishe kama rafiki?

Baadaye utakapomuuliza hawezi kuwa na jibu la maana, atabaki kukuambia hata kama akikutambulisha kama rafiki jamaa ataelewa kuwa ni mpenzi wake, hii inaingia akilini kweli?

Hakuna ukweli kama huo ndugu zangu! Huo ni ulaghai na anaogopa kukutambulisha kama mpenzi maana tayari ameshaonwa akiwa na wapenzi wengine. Sasa kama ndivyo, atatambulisha wangapi? Aseme wewe ni nani? Amka ndugu yangu!

(b) Msiri kupitiliza
Hii ni alama nyingine waliyonayo wanaume wa aina ninayoielezea katika mada hii. Siku zote mambo yake ni kwa siri kubwa, kama mna ahadi ya kukutana, hataki muongozane, atakuambia mkutane moja kwa moja sehemu husika. Hata muda wa kuondoka atafanya kila njia ili kila mmoja aondoke mwenyewe na kama mkiondoka pamoja basi ujue ni usiku na hakuna atakayewaona.

Ikitokea akakubali kuongozana na wewe, hatapenda muongozane pamoja. Atalazimisha utangulie mbele yeye afuate nyuma, kwa nini? Kwa sababu anaogopa kujulikana kuwa yeye ni mpenzi wako na kama anaogopa anakupenda kweli? Mapenzi gani hayo yanafanywa kwa siri? Anakupotezea muda huyo.

(c) Hapendi ndugu wafahamiane
Mpenzi wa aina hii ni mjanja sana, kwanza kabisa atajifanya mtu mwenye ‘ubize’ sana, yote hii ni kukwepa kuwajua ndugu zako au wewe kuwajua ndugu zake! Wakati mwingine anakuwa hapendi ndugu zako na wake wakutane wakijua wazi kuwa nyie mna uhusiano, hili ni tatizo.

Hakuna uhusiano wenye heri na malengo ya kuishi pamoja siku zijazo ukawa wa kificho cha kiasi hicho. Kama ana nia na wewe basi atahakikisha anawafahamu baadhi ya ndugu zako na wewe unawafahamu baadhi ya ndugu zake, hayo ndiyo mapenzi ya kweli.

Mapenzi hayaishii kwa nyie wawili pekee bali hata kwa ndugu zenu. Mnapojuana inakuwa rahisi kusaidiana hata katika mambo mengine ya kawaida.

MWILI wako  una thamani kubwa sana, usiidharau jinsi yako, usijishushe kiasi hicho, huyo anayekupotezea muda na kukuchezea sasa hivi hana thamani kama huyo aliyeandaliwa kwa ajili yako. 

#Pakua App Yetu tukuhabarishe


Tiba Halisi ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
*NKOLOMIJE*/
√Ni dawa bora ya mitishamba yenye kuimarisha, kurefusha na kukufanya uwe imara hata kama umelala pia huimarisha na kukuza  maumbile yaliyosinyaa na kuwa regevu

*📌SUPER GAFINA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri ya uume ulio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/


Bado hujachelewa

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM  AU UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO SIMU NO:/
*📞0752723508*
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images