Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Dkt Shein: Nchi Za SADC Tutoe Kipaumbele Kwa Bidhaa

$
0
0
Na Mwandishi Wetu,  MAELEZO
RAIS wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein amezitaka Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuweka mkazo wa matumizi ya bidhaa zake  na wataalamu wake wa ndani katika kutengeneza fursa za ajira na masoko ndani ya ukanda huo ili kukuza sekta za viwanda na biashara ndani ya jumuiya hiyo. 

Akizungumza katika hafla ya kufunga Maadhimisho na Maonesho ya Nne ya Wiki ya Viwanda katika Nchi za SADC leo Alhamisi (Agosti 8, 2019) Jijini Dar es Salaam, Rais Shein alisema umefika wakati kwa mataifa hayo kuzalisha bidhaa bora zenye kuweza kuleta ushindani katika masoko ya ndani na nje ya Jumuiya hiyo. 

Dkt. Shein alisema Mataifa ya SADC hayana budi kutumia fursa ya maonesho hayo katika kutangaza fursa za ujuzi na ubunifu  kwa kuzalisha na kutengeneza mtandao wa imara wa mawasiliano baina ya Nchi hizo na kuweza kuwa na soko la pamoja litakalowawezesha kutengeneza fursa za ajira kwa wananchi wa Mataifa hayo. 

Kwa mujibu wa Dkt. Shein aliongeza kuwa ili kufikia malengo ya uzalishaji wa bidhaa bora za viwandani ni wajibu wa Serikali zote kutengeneza mtandao imara wa miundombonu ikiwemo matumizi ya tekonolojia ya habari na mawasiliano kwa kuunda mikakati ya pamoja ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Jumuiya hiyo uliolenga katika kuimarisha sekta ya viwanda ndani ya jumuiya hiyo. 

“Hatujakataa mchango wa wataalamu na bidhaa za nje, lakini chako ni chako na mwenzako si chako, hivyo hakikunyima usikasirike, ni wakati wetu sasa kuweka mkazo katika kutegemea wataalamu wetu na teknolojia zetu katika uzalishaji wa bidhaa zetu” alisema Dkt. Shein.  

Aliongeza kuwa Nchi za Jumuiya hiyo hazina budi kutumia fursa za Maonesho na midahalo mbalimbali ya wataalamu inayojadiliwa katika Mikutano ya Jumuiya hiyo ili kuweza kubaini changamoto na hatua mbalimbali zinazopaswa kuchukuliwa ili kuiwezesha jumuiya hiyo kupiga hatua kubwa za Maendeleo ikiwemo kutengeneza fursa za ajira kwa wananchi wake. 

Akifafanua zaidi Dkt. Shein aliongeza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Zanzibar zimekuwa zikichukua hatua mbalimbali katika uboreshaji wa miundombinu ya miradi ya Maendeleo ambayo imekuwa kichocheo kikubwa cha fursa za ajira kwa vijana sambamba na kutengeneza mazingira wezeshi kwa sekta binafsi kushiriki katika uchumi wa viwanda. 

Akitolea mfano, Dkt. Shein alitaja baadhi ya miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa mradi wa reli ya kisasa (SGR), ujenzi wa viwanda  vikubwa, vya kati na vidogo ambavyo kwa pamoja vinaifanya Tanzania kuwa kielelezo cha mfano katika Nchi za SADC katika utekelezaji wa Ajenda ya Maendeleo ya Viwanda ndani ya Jumuiya hiyo. 

Kwa upande wake, Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa alisema maonesho hayo yamekuwa chachu na kipimo kwa Nchi za SADC kutekeleza ajenda yake ya Viwanda, kwa kuwa makundi mbalimbali ya wazalishaji, wafanyabiashara na watoa huduma wameonesha udhubutu wa kufikia malengo hayo katika Nchi wanachama wa jumuiya hiyo. 

Aliongeza kuwa jumla ya washiriki 5352 walishiriki katika midahalo mbalimbali ikiwemo Nchi SADC 14, taasisi za umma 64, viwanda 64, taasisi za kifedha 35, ambazo zote kwa pamoja zilitoa uzoefu na kuweza kuongeza fursa ya masoko na kuweza kuimarisha mitandao ya mawasiliano baina yao.  

Naye Waziri wa Habari, Utalii na Malikale wa Zanzibar,     Mahmoud Thabit Kombo alisema ili kufikia malengo ya Mpango Mkakati wa Jumuiya hiyo, nchi za SADC hazina budi kutoa na kuweka mkazo wa ushiriki wa sekta binafsi katika ujenzi wa uchumi shirikishi, kwa kuwa ushirikiano baina ya sekta hiyo na serikali utawezesha kutengeneza fursa mbalimbali za kiuchumi katika mataifa hayo. 

Naye Katibu Mtendaji wa Jumuiya hiyo, Dkt. Stagomena Tax, aliisifu Serikali ya Tanzania kwa kuwa mfano ndani ya Jumuiya hiyo katika eneo la ujenzi wa uchumi wa viwanda, na hivyo kuzitaka nchi nyingine kuiga mfano huo ili kuweza kuleta mtangamano ndani ya Nchi wanachama. 

Aliongeza kuwa ili kuweza kujenga uchumi jumuishi kwa wananchi ndani ya jumuiya hiyo, Sekretarieti ya jumuiya hiyo itaelekeza nguvu yake katika kuimarisha miundombinu ya usafiri wa bidhaa zilizopo ndani ya jumuiya hiyo, kwani bila miundombinu ya uhakika hakutoweza kuwa na mazingira wezeshi ya kuwasaidia wananchi ikiwemo kuondoa vikwazo vya kibiashara ndani ya jumuiya hiyo.

Msemaji Mkuu Wa Serikali Apata Kitabu Kinachoonesha Madini Yapatikanayo Nchini.

$
0
0
Leo tarehe Augusti 7, 2019 , Dr Hassan Abbas ambaye ni msemaji Mkuu wa serikali ya Jamhuri wa Muungano Tanzania ametembelea Banda la *GST* katika wiki ya Maonesho ya Mkutano Mkuu wa 39 wa  *SADC* kwa lengo la kupata taarifa mbalimbali za kitaalam juu ya Madini na Miamba iliyopo nchini.

Kitabu hicho ambacho ni toleo jipya  kinaonesha Madini kuanzia ngazi ya Wilaya , kata na Kijiji kimeainisha Zaidi ya madini 220.

Akiambatana na jopo la waandishi wa Habari , Dr.Hassan alipata maelezo mbalimbali kutoka kwa Mtaalam Mhandisi Priscuss Kaspana hususani katika sekta ya Madini ya viwanda yaani Industrial Minerals.

Sambamba na taarifa hizo Dr.Hassan kwa niaba ya serikali alipata zawadi ya kitabu Cha Madini Yapatikanayo Tanzania toleo jipya.

Waziri Mkuu Aongoza Mazishi Ya Mke Wa Mwanasheria Mkuu Wa Serikali

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo, Agosti 7, 2019 ameongoza mazishi ya mke wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Profesa Adelardus Kilangi, Bibi Natalia Bahati Kilangi.

Akizungumza kwa niaba ya Serikali katika mazishi hayo yaliyofanyika nyumbani kwa Profesa Kilangi eneo la Luchelele jijini Mwanza, Waziri Mkuu amemuomba Profesa Kilangi na familia yake kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu ambapo wamempoteza mama ambaye ni nguzo muhimu ya familia.

Kadhalika, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwasilisha salamu za pole kutoka kwa Rais Dkt. John Magufuli kwa Profesa Kilangi na familia yake kutokana na msiba mzito walioupata.

Katika salamu zake Rais Dkt. Magufuli amesema Serikali inathamini sana mchango mkubwa na mahili unaotolewa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na anamini kwamba kwa vyovyote vile wakati wa uhai wake, marehemu Natalia alishiriki kwa kiwango kikubwa kuhakikisha kwamba mumewe anaifanya kazi yake vizuri.

Awali, Spika wa Bunge, Job Ndugai aliwasihi waombolezaji wote wamkumbuke katika sala zao, Mwanasheria Mkuu wa Seriakali Profesa Kilangi ambaye ana kazi nzito ya kuishauri Serikali na alimtaja kuwa ni kiungo muhimu cha mihimili yote mitatu.

Naye, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza, Renatus Nkwande alimuomba Profesa Kilangi na familia yake wajipe moyo kwa sababu binadamu anapokuwa hai au anapokufa bado anabaki kuwa mali ya Mwenyezi Mungu.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Umoja wa Wamiliki wa Mabenki nchini, Abdulmajid Msekela ambaye pia ni Mkurugenzi wa Benki ya CRDB alisema wanachama wote wa umoja huo wanatoa pole kwa familia na wanamwombea Mwanasheria Mkuu wa Serikali na familia nzima, Mungu awape uvumilivu katika kipindi hiki cha majonzi.

Baadhi ya viongozi waliohudhuria katika mazishi hayo ni pamoja na Waziri wa Katiba na Sheria, Balozi Augustine Mahiga, Waziri wa Madini, Doto Biteko, Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga.

Wengine ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama na Katibu Mkuu wa CCM, Bashiru Ally, Manaibu Mawazi, Wakuu wa Mikoa na wilaya na viomgozi mbalimbali wa Serikali.

Mazishi hayo pia yalihudhuriwa na Askofu wa Jimbo la Geita na Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania(TEC), Flavian Kassala, Mapadri na Masheikh kutoka maeneo mbalimbali nchini.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,        

Waziri Lugola Apokea Taarifa Ya Bodi Ya Shirika La Magereza, Awataka Wajumbe Wahakikishe Magereza Inajitosheleza Kwa Chakula Kupitia Miradi Yao

$
0
0
Na Felix Mwagara, Dodoma (MOHA)
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amepokea taarifa ya Bodi ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Magereza, na kuwataka Wajumbe wa Bodi hiyo kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha Magereza inajitosheleza kwa chakula kupitia miradi mbalimbali inayomilikiwa na Jeshi hilo.

Waziri Lugola aliizindua Bodi hiyo Mei 30, 2019, na kutoa miezi miwili Wajumbe wa Bodi hiyo, kutembelea miradi mbalimbali ya Jeshi hilo na kumletea taarifa ya awali kuhusu miradi hiyo pamoja na maoni yao.

Akizungumza na Wajumbe wa Bodi hiyo baada ya kupokea taarifa yao, katika ukumbi wa mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dodoma, leo, Waziri Lugola alisema taarifa walioiwasilisha ameifurahia licha ya kuwa na mapungufu kadhaa ambayo yanahitaji uboreshaji zaidi.

Alisema Bodi hiyo inawataalamu mbaimbali ambao wanaweza wakaleta mabadiliko makubwa ya uzalishaji mali na kuweza kufanikisha Jeshi hilo linajitosheleza kwa chakula kupitia wafungwa mbalimbali waliopo magerezani.

“Nawapongeza sana kwa kazi nzuri, ila nawataka mfanye kazi zaidi ambayo itatuwezesha kuona mipango mizuri zaidi katika kulisimamia Shirika hili ambalo bodi yake tuliizindua,”alisema Lugola.

Pia Lugola aliwataka Magereza kutumia wataalamu wa Jeshi kupima viwanja vyao ili kufanikisha maendeleo zaidi na siyo kushirikiana na makampuni binafsi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Meja Jenerali Mstaafu, Raphael Muhuga, alisema Bodi yake kwa muda wa miezi miwili ilitembelea mradi wa ng’ombe wa nyama Mbigiri, mradi wa maziwa Kingolwira, mradi wa Uhunzi, mradi wa Kilimo Idete, mradi wa kilimo Kiberege na Mradi wa kilimo Isupilo ambapo Bodi hiyo ilifanya tathmini ya mali zilizopo, mipaka pamoja na historia ya miradi hiyo.

“Pia miradi mingine tuliyoitembelea ni mradi wa kilimo Ludewa, mradi wa kilimo na mifugo Kitai, mradi wa kilimo Mkwaya, na pia Bodi itaendelea kutembelea miradi mbalimbali ya Jeshi na kuendelea kutoa taarifa,” alisema Muhuga.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu aliitaka Bodi hiyo, ifanye ukaguzi wa kina wa mali za Shirika hilo kiundani zaidi ili taarifa hizo zije kiuhalisia zaidi na kuleta mikakati imara ya mafanikio.

Baadhi ya maelekezo aliyoyatoa Waziri Lugola kwa Bodi hiyo mara baada ya kuizindua, aliitaka kutekeleza maelekezo ya Rais John Magufuli kuhusu suala la Magereza kujitosheleza kwa chakula na pia bodi ihakikishe maeneo ya magereza yanapimwa na kupata hati miliki kwa kutumia wataalamu wa kupima ardhi wa Jeshi hilo.

Pia aliielekeza Bodi hiyo itembelee Magereza yote yenye miradi ya Shirika, na ifanye mkakati wa kutafuta wawekezaji kama vile wawekezaji kwenye mabwawa ya ufugaji wa samaki, na pia bodi itoe mawazo mapya ili kuondoa kufanya biashara kwa mazoea.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi 08 August

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa 09 August

Waziri Mkuu Akerwa Na Upandaji Wa Bili Ya Maji Maswa

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amekerwa na kitendo cha Mamlaka ya Maji wilayani Maswa kupandisha bili ya maji kutoka sh 5,000 hadi sh. 28,000 jambo ambalo amesema halikubaliki na amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka akutane na wahusika leo.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana jioni (Alhamisi, Agosti 8, 2019) wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kumalija, wilayani Maswa mara baada ya kutembelea ghala la pamba la Chama cha Msingi cha Kumalija.

“Haiwezekani bili ikapanda kwa kiasi hicho. Hapo utakuwa unamsaidia mwananchi myonge au utakuwa unamnyonga. Bili haiwezi kupandishwa kwa asilimia kubwa kiasi hicho yaani imetoka shilingi elfu tano hadi shilingi elfu ishirini na nane.”

Waziri Mkuu alisema Serikali inatekeleza Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo kichwani, inayolenga kuwaondolea wananchi tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama, hivyo upandishaji huo wa bili hauna tija kwa wananchi wanyonge.

Wakati huo huo,Waziri Mkuu alisema Serikali imetoa sh. milioni 440 kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo la upasuaji, ukarabati wa wodi na duka la dawa, upanuzi wa wodi ya watoto na ujenzi wa wodi ya wazazi katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa, ambapo ujenzi wake unaendelea.

Alisema mbali na fedha hizo, pia Serikali imepeleka sh. milioni 881 wilayani Maswa ambapo kati yake sh. milioni 481 ni kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa kituo vya afya cha Malampaka, kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu ya kituo cha afya cha Mwabayanda.

Akizungumza kuhusu elimu msingi bila malipo, Waziri Mkuu alisema kuanzia mwaka 2016 hadi 2019 Serikali imepeleka wilayani Maswa jumla ya sh. bilioni 2.1, kwa ajili ya ukarabati, utawala, michezo, mitihani na posho kwa Maofisa Elimu wa kata na Walimu Wakuu katika shule 28 za msingi.

Pia Waziri Mkuu alisema Serikali kuanzia mwaka 2016 hadi 2019  imepeleka wilayani Maswa jumla ya sh. bilioni 2.7 kwa ajili ya fidia ya ada, chakula kwa shule za bweni na posho ya madaraka kwa Wakuu wa Shule katika shule 16 za Sekondari.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,  

Wakulima Watakiwa Kujikita Kilimo Cha Umwagiliaji Na Kuchana Dhana Ya Kutegemea Mvua.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Wakulima hapa nchini wametakiwa kuachana na kilimo cha kutegemea mvua na badala yake wametakiwa kujikita zaidi katika kilimo cha Umwagiliaji  ili kuwa na  Uhakika wa Mavuno na kuleta tija katika sekta hiyo.
 
Hayo yamesemwa na   Mkuu wa  Mkoa wa Singida Dokta REHEMA NCHIMBI wakati akifunga kilele cha Maonesho ya  26  ya wakulima na Wafugaji Kanda ya kati  [NANENANE]  yaliyokuwa yakifanyika Viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma.
 
Dokta Nchimbi ambaye alikuwa mgeni Rasmi katika Maonesho hayo amesema moja ya changamoto kubwa inayowakabili wakulima na wafugaji hapa nchini ni kilimo cha kutegemea mvua pekee hivyo wanatakiwa kuondokana na dhana hiyo na badala yake wabadilike na wajikite katika kilimo cha umwagiliaji huku pia akisisitiza suala la uvunaji wa maji ya mvua.
 
Aidha Dokta NCHIMBI amesema ni aibu kwa mikoa hiyo kulalalmika uwepo wa njaa ilhali ina ardhi ya kutosha inayofaa kwa kilimo na mifugo.
 
Dokta nchimbi amekumbusha suala la utunzaji wa mazingira na kuwashauri wakala wa misitu Tanzania kuacha kuendesha operesheni ya kuacha matumizi ya mkaa bali pia wawe na operesheni ya kusambaza mizinga ya nyuki ili kuwepo na shughuli mbadala.

Pia Amependekeza kuongezwa kwa tuzo mbili katika maonyesho ya mwaka ujao ambazo ni tuzo ya wavunaji bora wa maji ya mvua na wakulima bora wa malisho ya mifugo.
 
Kwa upande wake,Mkuu wa Mkoa wa Dodoma dokta BINILITH MAHENGE amewataka wakulima waliopata utaalamu kupitia maonyesho hayo kuyatumia kwa vitendo.
 
Nae kaimu mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya bunge kilimo,mifugo na maji ambaye ni mbunge wa Singida Kaskazini Justine Monko amesema lengo la serikali ni kupunguza tozo mbalimbali zinazowakabili wakulima na wafugaji nchini na kama bunge linaunga mkono dhamira hiyo.
 
Maonesho hayo yamelenga kuwa shamba darasa kwa wakulima na wafugaji kujifunza yakiwa yameshirikisha kampuni zaidi ya 20,wajasiriamali zaidi ya mia Tatu,taasisi za serikali na binafsi zaidi ya 35 na  Kauli mbiu mwaka 2019 ni  Kilimo,Mifugo na Uvuvi kwa ukuaji wa uchumi wa nchi huku kitaifa yakifanyika mkoani Simiyu

Waziri Mkuu: Msimu Ujao Malipo Ya Wakulima Wa Pamba Yapitie Benki

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameagiza kwamba kuanzia mwakani malipo yote ya wakulima wa pamba yawe yanapitia benki ambapo wakulima wataingiziwa fedha kupitia akaunti zao.

Hivyo, ametumia fursa hiyo kuwasihi wakulima wafungue akaunti katika benki mbalimbali zilizopo kwenye maeneo yao ili waweze  kufanikisha mkakati huo na pia kuhifadhi fedha zao kwa ajili ya matumizi ya baadae.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana jioni (Alhamisi, Agosti 8, 2019) wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Luguru, wilayani Itilima mara baada ya kukagua ghala la pamba la Chama cha  Ushirika cha Msingi cha  Maendeleo.

Alitembelea kijiji hicho kwa lengo la kujionea mwenendo wa uuzaji wa zao la pamba katika Chama cha Msingi Maendeleo na alihakikishiwa kwamba kwa sasa uuzaji wa pamba unaendelea vizuri

Waziri Mkuu alisema ni vizuri malipo ya wakulima yapitie benki ili kuwawezesha kupanga matumizi mazuri ya fedha zao na pia watapa fursa ya elimu ya matumizi mazuri ya fedha.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alieleza miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali katika wilaya hiyo ukiwemo mradi wa ujenzi wa hospitali ya wilaya ambao umefikia asilimia 95.

“Jumla shilingi bilioni 1.5 zimetolewa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya inayojengwa eneo la Nguno, ambapo majengo yote saba ya kiupaumbele yamekamilika.”

Alisema mwaka 2017/2018 Serikali ilitoa sh. bilioni 2.34 kwa ajili ya miradi ya maji ya vijiji vya Lagangabilili, Mwamapalala, Kabale, Ikungulipu na Isengwa, yote imekamilika na inatoa maji.

Alisema mwaka 2019/2020 Halmashauri hiyo kupitia RUWASA imetengewa sh. bilioni 4.84 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya maji. Mradi huo utavinufaisha vijiji 78.

Awali,Katibu Mkuu wa Chama cha Msingi cha Maendeleo Luguru na Itubilo, Buzo Hussein alimshukuru Waziri Mkuu kwani wakati wote amekuwa mstari wa mbele katika kufuatilia kero mbalimbali zinazowakabili wakulima nchini na kuzitafutia ufumbuzi.

“Hii yote inatokana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli inayowataka viongozi kufuatilia changamoto za wananchi kwa vitendo na kuzitatua.”

Alisema katika ghala la chama chao kuna jumla ya kilo 175,235 za pamba ambazo zimekusanywa kutoka kwa wakulima ikiwa inasubiri wanunuzi.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Waziri Ummy azikaribisha nchi za SADC kutibiwa Muhimbili, MOI

$
0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu  amezikaribisha nchi wanachama wa SADC kutumia huduma za ubingwa wa juu zinazopatika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI), Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).

Ummy ameyasema hayo jana alipotembelea  mabanda ya MNH, MOI na JKCI yanayoshiriki maonesho ya viwanda yanayofanyika katika viwanja vya ukumbi  wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) kuelekea mkutano mkuu wa 39 wa Jumuiya ya Maendeleo ya nchi zilizopo Kusini mwa Afrika (SADC) ambao utaanza mapema wiki hii.

Waziri Ummy amesema Wizara yake imeweka wataalam wa afya ili kutoa huduma kwa wajumbe wa mkutano wa SADC watakaohitaji huduma za matibabu pamoja na wananchi wengine watakaokuwapo katika viwanja hivyo.

Aidha ameziomba nchi za SADC kupata huduma za ubingwa wa juu zinazopatikana MNH kama upandikizaji figo (kidney transplant), upandikizaji watoto vifaa vya kusaidia kusikia (cochlear implant), tiba kwa njia ya radiolojia (interventional radiology).

Kwa upande wa MOI, Waziri Ummy amezitaka nchi za SADC kuja kupata huduma za upasuaji wa mivunjiko ya kikombe cha mfupa wa nyonga, upasuaji wa kuweka nyonga na magoti bandia na upasuaji wa magoti, ubongo na mgongo kupitia matundu madogo.

Kwa upande wa JKCI amezitaka nchi za SADC kupata huduma za tiba ya umeme wa moyo, kuzibua mishipa ya damu na upasuaji wa kufungua kifua kwa ajili ya kurekebisha valvu au matundu kwenye moyo.

 “Kama Wizara tumeweka wataalam wa afya hapa eneo la mkutano  ili kutoa huduma kwa wajumbe wa nchi za SADC. Wataalam wetu wa Muhimbili, MOI, JKCI na pamoja  Hospitali ya Lugalo wako tayari kuhudumia wageni wetu ambao watapata changamoto yoyote ya kiafya,” amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy ametembelea kliniki maalumu zilizoandaliwa kwa ajili ya kuhudumia wageni na wananchi mbalimbali wanaotembelea maonesho ya viwanda na maandalizi ya mkutano wa 39 wa SADC.

Tanzania Yasema Iko Tayari Kuwapokea Wakuu Wa Nchi Na Serikali Kwa Ajili Ya Mkutano Wa 39 Wa SADC....Tazama Hapa Waziri Kabudi Akikagua Magari Yatakayowabeba

$
0
0
Serikali imesema maandalizi ya shughuli za SADC yamekamilika kwa kiwango kikubwa na sasa Tanzania iko tayari kuanza kupokea wageni na viongozi waandamizi wa Nchi 16 wanaotarajiwa kuhudhuria mkutano wa SADC unaofanyika Dar es Salaam Tanzania.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa magari yatakayotumiwa na viongozi mbalimbali watakaohudhuria mkutano huo wa SADC Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi amesema,maandalizi yamekamilika baada ya shughuli ya ukaguzi na kujiridhisha kuhusu utayari wa kuwapokea wageni.

Ameongeza kuwa Serikali imejiridhisha kuwa ina uwezo na iko tayari kuwapokea wageni na viongozi wakiwemo marais wa Nchi 16 za ukanda wa kusini mwa Afrika baada ya kukagua mahali watakapofikia,sehemu ya kufanyika kwa mikutano mbalimbali na mambo mengine muhimu kwa wageni hao.

Aidha, Prof. Palamagamba John Kabudi ameeleza kwa uchache utaratibu wa viongozi wakuu wa Nchi na Serikali watakavyoanza kuwasili kwa kufafanua kuwa marais na wafalme wanatarajiwa kuanza kuwasili Agust 16,2019, licha ya ukweli kuwa shughuli za SADC zimekwishaanza toka August 05,2019 ambayo ilikuwa na wiki ya maonesho ya viwanda na jana ilikuwa ni siku ya kilele ambapo Mgeni rasmi wa kufunga maonesho hayo ya viwanda alikuwa ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Mohamed Shein


Bw. Zuberi Kachingwe Afisa Usafirisahaji, IKULU,(katikati) akitoa maelezo kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akikagua magari yatakayotumiwa na viongozi na Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kujiridhisha juu ya matayarisho ya mapokezi kwa ajili ya mkutano huo utakaofanyika Dar es Salaam,Tanzania. Kulia ni Afisa Usafirishaji Msaidizi Bw. Athumani Natepe. August 8, 2019.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Zuberi Kachingwe Afisa Usafirisahaji, IKULU pamoja na Bw. Athumani Natepe Afisa Usafirishaji Msaidizi mara baada ya kumaliza kukagua magari yatakayotumiwa na viongozi na Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) mkutano utakaofanyika Dar es Salaam,Tanzania. August 8, 2019.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa amesimama mbele ya magari yanayotarajiwa kutumiwa na viongozi na Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kujiridhisha juu ya matayarisho ya mapokezi kwa ajili ya mkutano huo utakaofanyika Dar es Salaam,Tanzania. August 8, 2019.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa ndani ya mojawapo ya magari yanayotarajiwa kutumiwa na viongozi na Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kujiridhisha juu ya matayarisho ya mapokezi kwa ajili ya mkutano huo utakaofanyika Dar es Salaam,Tanzania. August 8, 2019.


Baadhi ya magari yanayotarajiwa kutumiwa na viongozi,wakuu wa Nchi na Serikali wakati wa mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) mkutano utafanyika Dar es Salaam,Tanzania. August 8, 2019.


Baadhi ya magari yanayotarajiwa kutumiwa na viongozi,wakuu wa Nchi na Serikali wakati wa Mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) mkutano utafanyika Dar es Salaam,Tanzania. August 8, 2019.

China Yatoa Msaada Wa Vifaa Vya Ofisini Kwa Ajili Ya SADC

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Wang Ke wamesaini hati za makabidhiano ya vifaa mbalimbali vya maofisini vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mia mbili na kumi na saba kwa ajili ya shughuli mbalimbali za ofisini ikiwemo computer,photocopy na printer kutoka kwa Ubalozi wa Jamhuri ya watu wa China kwa ajili ya mkutano wa SADC.

Katika mkutano huu wa 39 wa Jumuia ya Maendeleo kwa Nchi za Kusini mwa Afrika SADC,Tanzania inatarajiwa kukabidhiwa kijiti cha uongozi kwa kipindi cha mwaka mmoja ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli atakuwa Mwenyekiti wa SADC.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akikabidiana nyaraka za Msaada wa vifaa vya ofisini vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mia mbili kumi na saba vitakavyotumika wakati wa Mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Wanaoshuhudia ni maafisa kutoka Ubalozi wa China na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. August 08,2019. na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China hapa Nchini Mhe. Wang Ke

Basi la Abood lapata ajali eneo la Mkolani Jijini Mwanza

$
0
0
Basi la kampuni ya Abood linalofanya safari zake Mwanza-Dar limepata ajali asubuhi eneo la Mkolani Jijini Mwanza njiani likielekea Dar.

Inadaiwa kwamba chanzo cha ajali hiyo ni mwendesha pikipiki aliyekatiza barabara ghafla na kusababisha dereva wa basi kukosa mwelekeo.

Mwalimu Mkuu ahukumiwa kifungo cha maisha kwa kumlawiti Mwanafunzi wake

$
0
0
Mahakama ya Wilaya ya Babati Manyara, imemuhukumu Mwalimu Mkuu wa Shule ya Rift Valley Charles Msele,kifungo cha Maisha jela,kuchapwa viboko 4 na fidia ya Tsh. Million 3 kwa kosa la kuingia bweni la kiume na kumlawiti mtoto wa kiume wa miaka 11 anayesoma darasa la 5 shuleni hapo.

Akisoma hukumu hiyo hakimu wa mahakama ya Hakimu Simon Kobero, amesema adhabu hiyo imetolewa baada ya mtuhumiwa kutiwa hatiani.

Imeelezwa mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo September 28 mwaka jana.

Mtuhumiwa alimuita  mtoto huyo bwenini na baada ya  hapo na yeye alienda akiwa na vilainishi  ambapo baada ya kufika bwenini mtuhumiwa alimpaka mafuta  kwenye  sehemu za haja kubwa kisha na yeye kujipaka  na kumlawiti. 


Upande wa mashtaka alisema kwa kuwa mshtakiwa ametiwa hatiani, mwendesha mashtaka Wakili wa serikali Petro Ngassa, aliomba mtuhumiwa apewe adhabu kali pamoja na kutoa fidia kwa muhanga kutokana na kitendo alichokifanya.

Lugola Ataka Jeshi la Polisi Litende Haki Kwa Wananchi

$
0
0
Na Felix Mwagara, MOHA, IRINGA.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewasili mjini Iringa leo, na kulitaka Jeshi la Polisi Mkoani humo kutenda haki katika utendaji wao.

Lugola alifanya ziara ya saa mbili mkoani humo, akiwa safarini kuelekea Mkoa wa Rukwa kwa ziara ya siku tano mkoani humo.

Akizungumza katika kikao cha viongozi wa Polisi wa Mkoa huo, Lugola alisema amefika kuonana na viongozi hao akiwa safarini, kwa lengo la kufuatilia utendaji kazi ikiwa ni utaratibu wake ambao alijiwekea tangu aiongoze Wizara hiyo.

Lugola alisema lengo la ziara yake mkoani Rukwa ni kufuatilia maagizo yake aliyoyatoa kwa vyombo vya ulinzi na usalama vilivyopo ndani ya Wizara yake, na pia atafanya ziara kama hizo mikoa yote nchini.

Alisema anatarajia kutembelea Wilaya zote za Mkoa huo kusikiliza kero za wananchi kupitia mikutano mbalimbali ya hadhara itakayofanyika katika wilaya hizo.

“Natarajia kuanza ziara hiyo rasmi kesho Agosti 10, 2019  Mjini Sumbawanga kwa kukutana na Mkuu wa Mkoa pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, kupokea taarifa ya Kamati hiyo, kabla ya kuanza kuzungumza na Wakuu wa vyombo vyake na baadaye kukutana na Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa, na kumaliza kwa kuzungumza na Baraza la Askari na Watumishi wote wa Wizara hiyo waliopo mjini humo,” alisema Lugola.

 “Nitafanya mkutano mkubwa wa hadhara katika Mji wa Sumbawanga, utaanza saa 10:00 hadi 12:00 jioni, hivyo nawaomba wananchi wa mji huo wajitokeze kwa wingi kunisikiliza kile ambacho nimepanga kuwaambia, na pia nitawapa nafasi wananchi waulize maswali bila woga, waniambie kero zao nami nitazitatua katika mkutano huo,” alisema Lugola. 

Lugola alisema katika ziara yake aliyoifanya mwaka jana Mkoani Kigoma na mwezi Januari Mwaka huu Mkoa wa Kagera, Arusha Mwezi Februari na Morogoro wiki iliyopita, amegundua wananchi wanakabiliwa na changamoto mbalimbali hivyo hawezi kulala akiwa ofisini, lazima afanye ziara nchi nzima kuwasaidia wananchi kutatua kero zao ambapo wengi wao wakiwalalamikia Polisi wakiwaonea.

“kupitia kikao hiki hapa Iringa, napenda kuwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi, wanapojitokeza kwa wingi inasaidia kusikiliza matatizo yao yanayowakabili, ndio mana nimepanga kufanya ziara kama hizi nchi nzima, hii inasaidia sana kujua matatizo mbalimbali ya wananchi pamoja na kuangalia utendaji kazi wa Taasisi zangu zilizopo ndani ya Wizara hii, na hakika Serikali ya Rais Dokta John Magufuli inawajali wananchi wake ndio mana inawafuata mahali walipo, ili wazungumze na Serikali yao uso kwa uso,” Alisema Lugola.

Waziri Lugola baada ya kumaliza ziara yake Mjini Sumabwanga, ataenda Wilaya ya Sumbawanga Vijiji ambapo atatembelea Gereza Mollo kutatua mgogoro wa ardhi na baadaye atazungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara.

Waziri Lugola, Agosti 12, 2019, atafanya ziara Wilayani Kalambo, na baada atamaliza ziara yake Wilaya ya Nkasi kwa kutembelewa majimbo ya Nkasi Kaskazini na Kusini. 

Katika Wilaya zote atakazozitembelea pia atazungumza na wananchi pamoja na watumishi waliopo ndani ya Wizara yake ambao ni Jeshi la Polisi, Idara ya Uhamiaji, Jeshi la Magereza, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, pamoja na Idara ya Probesheni ambayo jukumu lake kuu ni kupunguza msongamano gerezani na kusimamia wafungwa waliopewa adhabu mbadala na Mahakama au wafungwa waliopata msamaha kupitia sheria ya huduma kwa jamii na kutumikia kifungo chao nje ya Gereza.

Maagizo aliyoyatoa Waziri Lugola mara baada ya kuteuliwa kuiongoza Wizara hiyo, ni dhamana zitolewe saa 24 katika vituo vyote vya polisi nchini, na pia alipiga marufuku tabia ya baadhi ya Polisi kubambikizia kesi wananchi, na pamoja na agizo la pikipiki zote zilizopo vituoni ziondolewe.

Pia aliagiza wakuu wa vyombo kuthibiti rushwa katika taasisi wanazoziongoza, na kutowanyanyasa watumishi katika taasisi zao.

Lugola anatarajia kumaliza ziara yake Agosti 17 mkoani humo na kurejea Dodoma kushiriki vikao vya Kamati ya Kudumu ya Bunge, Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.

Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Kuboreshwa Kuendana Na Mpango Wa Miaka Mitano

$
0
0
Na Peter Haule, WFM, Dar es Salaam
Serikali imeahidi kutoa fedha za kutosha kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) ili kuongeza udahili wa wanafunzi ikiwa ni pamoja na  kupatikana kwa wahasibu wa kutosha kama mpango wa Taifa wa miaka mitano ulivyoelekeza.

Hayo yamebainishwa jijini Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipang,o Dkt. Khatibu Kazungu, wakati wa ziara yake ya kikazi katika taasisi hiyo iliyochini ya Wizara ya  Fedha na Mipango  kubaini changamoto za utekelezaji wa Bajeti ya taasisi hiyo kwa mwaka 2018/19.

Dkt. Kazungu alisema kuwa Taasisi ya TIA inakabiliwa na changamoto kubwa ya ufinyu wa bajeti jambo lililosababisha baadhi ya miundombinu yake kutokamilika kwa wakati na hivyo kupunguza kiwango cha udahili wa wanafunzi.

“Lengo la Mpango wa Taifa wa maendeleo wa miaka mitano ni pamoja na taifa kuzalisha wahasibu wa kutosha ili kuleta chachu katika maendeleo ya uchumi na nyanja zingine za maendeleo, malengo yanayotegemewa kwa kuimarishwa kwa miundombinu ya taasisi hii”, alieleza Dkt. Kazungu

Alisema kuwa miundombinu inayoangaziwa kwa mwaka huu wa fedha ni pamoja na Mabweni ya wanafunzi, vyumba vya madarasa na ofisi za watumishi, aidha kuangalia uwezekano wa kuongeza wahadhiri kulingana na kozi zinazotolewa jambo litakalokwenda sambamba na ongezeko la wanafunzi.

Kwa upande wake Kaimu Afisa Mtendaji wa Taasisi ya TIA Bi. Luciana Hembe, alieleza  kuwa, hatua ya viongozi wa juu kutembelea taasisi wanazoziongoza na kuona uhalisia wa mambo, unaongeza morali ya kiutendaji ya watumishi kwa kuwa hutatua changamoto nyingi hususani za kibajeti.

Alisema kuwa Taasisi ya TIA imejipanga kikamilifu kuhakikisha wahitimu wake wanakuwa na weledi wa kutosha katika kuhimili ushindani wa soko la ajira ndani na nje ya nchi.

Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Kuendelea Kushirikiana Na Tanzania

$
0
0
Na. Saidina Msangi na Josephine Majura WFM Dodoma.
Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), imeridhishwa na utekelezaji wa miradi mbalimbali inayotekelezwa nchini chini ya ufadhili wa benki hiyo ambayo imekuwa na ushirikiano na Serikali ya Tanzania kwa muda mrefu.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Kanda ya Mashariki Bw. Gabriel Negatu alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb)  katika ofisi  Wizara ya Fedha  na Mipango Jijini Dodoma.

Bw. Gabriel ameeleza kuwa Tanzania ni nchi ya mfano ambayo imeonesha matokeo chanya katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuwa benki hiyo itaendelea kushirikiana nayo katika utekelezaji wa miradi ya mbalimbali ya  maendeleo.

Akizungumza katika hicho Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango ameipongeza Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), kwa kazi nzuri wanayofanya na kwa namna inavyowezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini.

Dkt. Mpango aliitaja baadhi ya miradi ambayo Benki hiyo imekuwa ikifadhili ni pamoja na  Sekta ya Miundombinu, Usafirishaji na Nishati ambayo kwa pamoja inachangia katika utekelezaji wa kujenga uchumi wa viwanda.

Aidha Waziri Mpango aliongeza  kuwa Sekta ya Nishati ni muhimu kwa nchi za Afrika kwani inahitajika kwa kiasi kikubwa katika kujenga uchumi wa viwanda kwani hakuna viwanda bila kuwa na umeme wa uhakika katika ukuaji wa Sekta ya Viwanda.

Dkt.  Mpango alifafanua  namna ya  upatikanaji wa umeme vijijini kupitia REA umesaidia katika kuwezesha wananchi kupata habari mbalimbali na pia kujifunza teknolojia na kuona maendeleo katika maeneo mengine.

Benki hiyo inatarajia kufadhili utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa kuunganisha Tanzania na Rwanda ambayo itachochea maendeleo  baina ya nchi hizo na Afrika Mashariki kwa ujumla.

Taarifa ya Mfumuko Wa Bei Kwa Mwezi Julai 2019

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, MAELEZO
Ofisi ya Taifa ya Takwimu imetoa taarifa ya mfumuko wa bei nchini ambapo pamoja na mambo mengine mfumuko wa bei ya mwezi Julai 2019, umebakia kuwa asilimia 3.7 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2019.

Akizungumza na waandishi wa vyombo vya habari leo Ijumaa (Agosti 9, 2019) Kaimu Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii, Ruth Minja alisema kiwango hichi kubakia kuwa sawa kwa kiwango hicho kumechangiwa na kuongezeka na kupungua kwa bei za baadhi za vyakula na bidhaa zisizo za chakula kwa kipindi kilichoisha Julai 2019.

Aidha Minja alisema mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi Julai 2019 umeongezeka kidogo hadi kufikia asilimia 2.9 kutoka asilimia 2.3 ilivyokuwa kwa mwezi Juni 2019.

“Baadhi ya bidhaa zilizoongezeka bei kwa mwezi Julai zikilinganishwa na Julai 2018 ni pamoja na unga wa mahindi (6.0%), unga wa mhogo (4.0%), mafuta ya kupikia (8.9%), na mbogamboga (4.6%) ambapo kwa uoande wa bidhaa zisizokuwa za vyakula ni pamoja na vifaa vya kieletroniki, majiko ya gesi pamoja na vifaa pamoja na bidhaa za huduma”.

Akizungumzia hali ya mfumuko wa bei kwa baadhi ya Nchi za Afrika Mashariki, taarifa inaonyesha kuwa Nchi ya Kenya ilikuwa na Kiwango cha juu cha mfumuko wa bei kwa mwezi Julai 2019, ambapo kiwango chake kilifikia asilimia 6.27 ikilinganishwa na asilimia 5.70 kwa mwaka ulioishia Juni 2019.

Akifafanaua zaidi Minja alisema taarifa ya mfumuko wa bei katika Nchi ya Uganda katika mwaka ulioishia Julai 2019, taarifa zinaonyesha kuwa Nchi hiyo ilikuwa na kiwango kidogo cha mfumuko wa mdogo bei kilichofikia asilimia 2.6 kutoka asilimia 3.4 kwa mwaka ulioishia Juni, 2019.

MWISHO.

Mkongo: Kibongo ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
********************************
SUPER MKONGO MPYA,
_______________________________
********************************
Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile,

- kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa
- maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo
- kukosa hamu ya tendo la ndoa
- kushindwa kurudia tendo la ndoa
- maumbile kusimama kwa kulegea
-  kulegea katikati ya tendo
- kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu
- kuishiwa nguvu kutokana na punyeto.

Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MCONGO MPYA, kiboko ya matatizo haya.
_______________________________
Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume
_______________________________
(1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea.
(2) ngiri
(3) kuugua chango la uzazi kwa muda mrefu.
(4) kupungukiwa hormone za testosterone.
(5) ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na visivyo na virutubisho  vya kutosha.
(6) kutokufanya mazoezi na mwenendo wa maisha.
(7) kisukari.
(8) tumbo kuunguruma na kujaa gesi.
(9) maumivu ya kiuno nk.
_______________________________

WASILIANA NA:
DR. MCONGOMANI
SIMU NO:
📞0658816558
📞0682323682
Popote ulipo huduma hii inakufikia
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images