Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais wa Venezuela asitisha mazungumzo na upinzani kutokana na vikwazo vya Marekani

$
0
0
Rais wa Venezuela Nicolas Maduro ameilaumu Marekani kwa vikwazo ilivyoiwekea nchi hiyo na kuamuru wawakilishi wa serikali yake kutosafiri kuelekea Barbados kwa mazungumzo yaliyopangiwa kufanyika na wanasiasa wa upinzani. 

Taarifa ya serikali ya Venezuela imesema Maduro ameamua kutowatuma maafisa wake kwa mazungumzo hayo yaliyopangiwa kufanyika leo Alhamis na kesho pamoja na kiongozi wa upinzani Juan Guaido kutokana na uchokozi mkubwa unaoendelezwa na utawala wa rais Trump. 

Rais Trump ameagiza kufungiwa kwa mali zote za serikali ya Venezuela zilizoko Marekani na pia amezuia kufanyika kwa biashara ya aina yoyote na uongozi wa nchi hiyo.

Kutana na Sheikh Omary Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali za Matatizo Yako Na Kutafsiri Ndoto kwa kutumia Vitabu vya QUR-AN

$
0
0
Sheikh Omary Ni bigwa wa kutatua matatizo kwa haraka, ni mtu aliye jaliwa kubuli Shufaa pia anatoa Duah  za Ruhia. Ukija na Maradhi yanaondoka hapo hapo bila kungoja kesho,  UKIPEWA MKONO  na Sheikh Omary .
 
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
 
Sheikh Omary ni Mtaalamu wa Nyota za Binadamu  Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
 
Je una NUKSI  zisizo kwisha.!? JE umekimbiwa na Mume/Mke na Anaishi na Mtu Mwingine..!? Muone Akutatulie,
 
Una kosa bahati ya wanaume au mume wa kukuoa..Unataka nyota ing'ae Au huna hamu na Mkeo/ Mumeo.
 
Jini mahaba. Kama Unakasirika ovyo ukiwa na bwana au mwanamke wako na  kumchukia Mpaka  kushindwa kufanya nae tendo la ndoa.
 
Njoo umuone Sheikh Omary  na ujuwe  yanayo kusibu.Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN

Mawasiliano: Sheikh Omary 0673531992. WhatsApp/Call
Tembelea Page ya @Mtabibu_Omar  @Mtabibu_Omar
Usome Makala Tofauti Tofauti Kama.

Dampo la taka laendelea kuzigombanisha halmashauri mbili Njombe

$
0
0
Na Amiri kilagalila-Njombe
Baadhi ya madiwani akiwemo diwani wa kata ya Saja wilayani Wanging’ombe mkoani Njombe Adrew Mangula wamelitaka baraza la madiwani la halmashauri hiyo kuridhia hoja ya kutaka Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania atoe tamko rasmi juu ya matumizi ya dampo lilipo katani kwake linalotumiwa na halmashauri ya mji wa Makambako licha ya malalamiko yao kufikishwa kwa naibu waziri wa mazingira na baraza la taifa la mazingira(NEMC).

Akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani katika halmashauri hiyo,diwani huyo amesema kuwa anashindwa kuelewa kinacho endelea juu ya matumizi ya dampo hilo kwa kuwa naibu waziri wa mazingira na baraza la taifa la mazingira lilitoa zuio kwa halmashauri ya mji wa makambako kutotumia dampo hilo lakini bado linaendelea kutumika.

“Hivi ni waziri wa namna gani ambaye anaweza kuja kusema ,mimi naona sasa hivi anayeweza kusema neno ni Rais mwenyewe wa jamhuri ya muungano wa Tanzania,labda mwenyekiti uridhie  kwa baraza lako hili tukufu kwamba Rais aseme neno ili kuwaokoa wananchi wale wa Itengeru na Saja maana yake hata sielewi nani anaweza kusema ni mkuu wa wilaya,mkuu wa mkoa, ni waziri ama ni nani mimi naona amebaki Rais”alisema diwani Mangula

Aidha madiwani wa halmashauri hiyo wamesema hatua za haraka zinatakiwa kuchukuliwa ikiwemo kufika mahakamani na kwenda kufunga dampo hilo ili kuwanusuru wananchi wao na athali ambazo zinaweza kujitokeza hapo baadae hususani magonjwa ya mlipuko.

“Sisi tunaona kuna mtu anafumba macho kwa maslahi yake,eneo lile lipo ndani ya halmashauri yetu tunajitambua sisi ndio wenyewe tununue makufuri tukafunge tuandike bango litakaloonesha ni marufuku kutumia hili”walisema madiwani

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Wanging'ombe Antony mawata amesema anashangazwa na kitendo cha halmashauri ya mji wa Makambako kuendelea kutumia dampo hilo licha ya zuio la naibu waziri na athali ambazo zinaweza kuwapata wananchi wa Saja.

“Ivi mamlaka yanayoendelea kutumia na kubeza nini na mkurugenzi wa Makambako nimewahi kumsikia akisema sasa tumeshapanga na tumeingiza kwenye bajeti na tunahela ya kwenda kutengeneza mifereji ili tuendelee kutumia hii sio sawa hawa wamepanga kutudhulumu na kuendelea kutuulia watu wetu”alisema Mawata

Hata hivyo hii leo hoja za madiwani wa halmashauri hiyo zimeibuka katika baraza la madiwani halmashauri ya mji w Makambako huku mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa makambako Hanana Mfikwa akisema kuwa wao wanaendelea kutumia dampo hilo kutokana na kibali halali ambacho wamekipata kutoka kwa mkuu wa mkoa wa Njombe,na hakuna barua yoyote ambayo wameipata ya kuzuia wasiendelee kutumia dampo hilo.

“Kimsingi lile dampo ni la halmashauri yetu na lilijengwa na hao hao wanaolalamika wakiwa Wanging’ombe lakini wote tukiwa Njombe tulipanga kwa pamoja tukajenga hilo dampo,kwa hiyo sisi kama Makambako tulipewa barua rasmi na mkuu wa mkoa kwamba tutupe taka pale kwa hiyo tunategemea kupata barua kwa vyombo vyenye mamlaka,Nemc wamekuja ni sahihi lakini kama hawajatoa waraka wowote  kusimama kutupa taka pale sisi hatuwezi kusimama,lakini kimsingi lile dampo liko salama na wala halina madhara kwa kuwa hata wenyewe wanaweza kutumia”alisema  Hanana Mfikwa

Joseph Makinga ni katibu tawala msaidizi osifi ya Rais na serikali za mitaa tamisema mkoa wa Njombe,akizungumza katika baraza la madiwani halmashauri ya mji wa Makambako amesema kwa sasa swala hilo lipo mezani kwa mkuu wa mkoa wa Njombe lakini waendelee kuwa na subira kwani bado halijashughulikwa.

Zaidi ya miaka mitano sasa kumekuwa na mgogoro kati ya h almashauri hizo kuhusu matumizi ya dampo hilo

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) Yaupongeza Mfuko Wa Mawasiliano Kwa Wote Nchini

$
0
0
Na Mwandishi Wetu.
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeupongeza Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) nchini kwa kuipa kipaumbele miradi mbalimbali inayotekelezwa na Mfuko huo kwa upande wa Zanzibar.
 
Pongezi hizo zimetolewa na Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mheshimiwa Dk. Sira Ubwa Mamboya alipotembelea Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) jijini Dodoma akiongozana na mwenyeji wake Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Atashasta Nditiye (Mb) pamoja na ujumbe wake kutoka katika Wizara anayoiongoza. 
 
Akizungumza na Uongozi wa Mfuko huo, alisema UCSAF imetoa kipaumbele kwa miradi mikubwa mitatu ambayo itaongeza maendeleo ya matumizi ya TEHAMA Visiwani Zanzibar.
 
“Nawashukuru sana kwa kujenga vituo vya mawasiliano Zanzibar na minara ya mawasiliano ambapo inawawezesha wananchi kutuia huduma za mawasiliano kwa shughuli za kijamii na kiuchumi visiwani humo. Aidha, ameongeza kuwa amefurahishwa  na mkakati wa kuwahamasisha wasichana kujitokeza na kupata mafunzo katika programu ya Wasichana na TEHAMA, “Hii itawafanya wasichana wa Zanzibar kuwa mstari wa mbele kutumia TEHAMA na kuingia katika mfumo wa Elimu ya TEHAMA,” amesema. 

Pia, ameishukuru na kuipongeza Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana  na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji katika kupanga na kutekeleza mipango mbali mbali inayohusu Sekta ya Mawasiliano kwa kuwa mawasiliano ni suala la Muungano. 
 
Naye Mhe. Nditiye (Mb) alisema kuwa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano imefarijika sana kuupokea ujumbe wa Mheshimiwa Dk. Mamboya ambao umekuja Tanzania Bara kujifunza na kubadilishana uzoefu kuendana na utendaji kazi wa kila siku wa taasisi za Mawasiliano kwani mawasiliano ni suala la Muungano. 

Nditiye alimhakikishia Mhe. Dk. Mamboya kuwa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itahakikisha inaendelea kutoa ushirikiano kwa SMZ kupitia Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji ili kuendelea kutekeleza majukumu na kuhudumia wananchi katika nyanja ya mawasiliano.
 
Wakati akitoa taarifa ya Wizara kwa ugeni huo, Nditiye alisema kuwa tayari Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano imejenga na kufikisha Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kwenye Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambapo Unguja inaunganishwa na Mkongo huo kupitia mkongo wa baharini uliopo kwenye waya wa umeme kutoka Dar es Salaam na Pemba imeunganishwa kutoka Tanga. 

Pia, aliongeza kuwa vituo kumi vya TEHAMA vimejengwa na UCSAF kwa gharama ya shilingi milioni 754.8 ambapo vituo sita vimejengwa Unguja na vituo vine vimejengwa Pemba na tayari kila kituo kimepewa kompyuta saba na printa moja kutoka UCSAF
 
Akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya UCSAF aliishukuru Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji ya SMZ kwa kutoa ushirikiano mkubwa kwa Mfuko wakati wa kutekeleza miradi ya TEHAMA kwa upande wa Zanzibar. Alisema Wizara hiyo imekuwa karibu na Mfuko jambo ambalo limepelekea mafanikio ya miradi ya TEHAMA visiwani humo.
 
Akielezea utekelezaji wa miradi ya TEHAMA Visiwani Zanzibar, Kaimu Mtendaji Mkuu wa UCSAF, Bibi Justina Mashiba amesema, jumla ya wasichana 40 kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wamepewa mafunzo ya utengenezaji wa mifumo ya TEHAMA kutoka mikoa ya Kaskazini Pemba na Mjini Magharibi. Aidha alisema Mfuko umetoa vifaa vya TEHAMA kwa shule 16 Zanzibar, uboreshaji wa mawasiliano kwenye Kata 10 zenye vijiji 18 Zanzibar.
 
Ujumbe wa Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ukiongozwa na Mhe. Dkt. Sira Ubwa Mamboya pamoja na kutembelea Ofisi za Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, pia, ulitembelea mradi wa TEHAMA katika Shule ya ekondari ya Wasichana Msalato, Dodoma uliofadhiliwa na UCSAF na kutembelea mnara wa mawasiliano uliofadhiliwa na UCSAF uliopo Dodoma, Wilayani Bahi kijiji cha Makanda. Pia, ujumbe huo utaendelea na ziara yake kwa kutembelea taasisi mbalimbali za Mawasiliano za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa upande wa Tanzania Bara.

Imetolewa na Prisca Ulomi,
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Serikali Yawataka Wanunuzi Wa Pamba Waongeze Kasi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wanunuzi wa zao la pamba katika maeneo mbalimbali nchini wahakikishe wanaongeza kasi ya ununuzi wa zao hilo ili wakulima waweze kupata fedha zao kwa wakati.

Pia, Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga pamoja na Manaibu Waziri wake kubaki katika mikoa yote inayolima zao la pamba hadi wakulima wote watakapolipwa fedha zao na kuhakikisha pamba yote iliyomo mikononi mwa wakulima inauzwa.

Ameyasema hayo leo (Alhamisi, Agosti 8, 2019) wakati alipotembelea Chama cha Msingi cha Itemelo kilichoko eneo la Dutwa wilayani Bariadi, Simiyu kwa ajili ya kujionea mauzo ya zao la pamba.

Waziri Mkuu amesema ataendelea kusimamia mwenendo wa zao hilo kwa ukaribu lengo likiwa kuona wakulima wananufaika kwa kupata tija. “Ilani ya CCM ya 2015/2020 inasisitiza kilimo na inataka wakulima wapate masoko ya uhakika na tunalitekeleza jambo hilo na pamba yote itanunuliwa.”

Amesema Serikali inataka kuona pamba yote iliyoko kwa wakulima inatoka ili wakulima waweze kulipwa fedha ambazo zitawawezesha kujikimu kimaisha pamoja na kununua pembejeo kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao.

Kadhalika, Waziri Mkuu amewataka viongozi wa AMCOS wahakikishe wanawatambua wakulima kwa majina, maeneo wanayoishi pamoja na ukubwa wa mashamba yao ili waweze kuagiza pembejeo kulingana na mahitaji halisi.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amewasihi wakulima kufungua akaunti katika taasisi mbalimbali za kifedha lengo likiwa ni kuhifadhi vizuri fedha wanazozipata kutokana na mauzo ya pamba ili ziweze kuwasaidia baadaye.

Pia, Waziri Mkuu amewasisitiza wakulima hao waendelee kutunza vizuri pamba yao na kuipeleka ghalani ikiwa katika hali nzuri ya usafi na ubora wa hali ya juu, kwani kwa sasa pamba ya Tanzania inasifika kwa ubora katika soko la dunia.

Kwa upande wa masoko hususan ya pamba, Waziri Mkuu aliwasisitizia wananchi wa Dutwa na Watanzania kwa ujumla kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. Magufuli inaendelea kuhakikisha uwepo wa masoko ya uhakika wa mazao yote hususan yale ya kimkakati.

Pia, Waziri Mkuu ameongeza kuwa moja ya agenda muhimu ya ziara yake ya Kiserikali aliyoifanya nchini Misri mwezi Julai 2019 ilikuwa ni kutafuta masoko ya uhakika ya mazao ya Tanzania likiwemo na zao la pamba.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally alipokaribishwa kuwasalimu wananchi alimshukuru Waziri Mkuu kwa kutoa msukumo katika ununuzi zao la pamba. Aidha alimuomba Waziri Mkuu aongeze msukumo zaidi ili wakulima walipwe fedha zao kwa wakati.

Naye,Waziri wa Kilimo Hasunga amesema kuwa hali ya malipo kwa wakulima wa zao la pamba kwa sasa ni ya kuridhisha kwa kuwa wakulima katika maeneo mbalimbali wameanza kulipwa.

Pia Waziri huyo amemuahidi Waziri Mkuu kwamba wataendelea kubakia katika mikoa inayolima pamba kwa ajili ya kufuatilia mwenendo wa mauzo ya pamba ili kuhakikisha wakulima wote wanalipwa fedha zao kwa wakati.

Kuhusu suala la makato ya fedha za pembejeo ambazo wakulima wanalalamikia kukatwa kiasi kikubwa kuliko kiwango halisi wanachostahili, Waziri huyo wa Kilimo amesema atalishughulikia.

Aidha,Mbunge wa jimbo la Bariadi, Andrew Chenge amesema amefanya ziara katika kata 20 kati ya 30 kwenye jimbo hilo na changamoto kubwa ya wananchi ni mauzo ya pamba. “Ujio wa Waziri Mkuu umeleta manufaa kwani wanunuzi wameanza kuja kwa kasi”.

Mbunge huyo amemuomba Waziri Kuu awafikishie salamu zao kwa Rais Dkt. John Magufuli kwamba wanamshukuru kwa namna anavyowajali wakulima mbalimbali nchini wakiwemo na wa zao la pamba.

Kwa upande wake, Mbunge wa jimbo la Itilima, Njalu Silanga ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Nsangali ambayo inanunua pamba amemuahidi Waziri Mkuu kwamba ifikapo kesho (Ijumaa, Agosti 9, 2019) saa nane mchana atakuwa amelipa sh. milioni 135 zinazohitajika na amcos ya Itemelo ili kulipia deni la pamba iliyoko ghalani.

Awali, Katibu wa Amcos ya Itemelo, Lucas Ephraim alimuomba Waziri Mkuu awasaidie kuyahimiza makampuni mbalimbali yanayonunua yapeleke fedha kwa wakati ili kukidhi makisio tarajiwa.

Katibu huyo alisema chama chao kinahudumia vijiji vitano vikiwa na jumla ya wakulima 2,665 wa pamba wenye jumla ya ekari 9,675. Pia chama chao kinahitaji sh. milioni 135.139 ili kulipia deni la pamba ambayo iko ghalani.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Tiba Halisi ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
*NKOLOMIJE*/
√Ni dawa bora ya mitishamba yenye kuimarisha, kurefusha na kukufanya uwe imara hata kama umelala pia huimarisha na kukuza  maumbile yaliyosinyaa na kuwa regevu

*📌SUPER GAFINA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri ya uume ulio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/


Bado hujachelewa

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM  AU UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO SIMU NO:/
*📞0752723508*

Ucheleweshwaji Malipo Ya Wakulima Kuwa Historia

$
0
0
*Ni baada ya Serikali kuzindua mfumo wa uuzaji wa mazao kupitia TMX

CHANGAMOTO ya ucheleweshwaji wa malipo kwa wakulima baada ya kuuza mazao yao inatarajiwa kuwa historia baada ya Serikali kuzindua mfumo wa uuzaji wa Mazao kupitia Soko la Bidhaa (TMX) ambao kuanzia mwaka ujao utaanza kutumika kununua na kuuza baadhi ya mazao ndani na nje ya nchi.

Ununuzi wa mazao ya wakulima kupitia Soko la Bidhaa unalenga kuongeza ufanisi katika mifumo ya masoko ambayo imekuwa na changamoto kwa muda mrefu kwa kuwaunganisha wauzaji na wanunuzi wa bidhaa, kuleta ushindani kwenye bei, kupunguza gharama na kuweka uwazi.

Uzinduzi wa mfumo huo umefanywa leo (Alhamisi, Agosti 8, 2019) na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika kilele cha maadhimisho ya sikukuu ya wakulima nane nane Kitaifa kwenye viwanja vya maonesho Nyakabindi mkoani Simiyu kwa niaba ya Rais Dkt. John Magufuli.

Waziri Mkuu amesema mfumo huo utawahakikishia wakulima upatikanaji wa malipo kwa muda mfupi na wanunuzi kuwa na uhakika wa kupata mazao na bidhaa zenye ubora na zinazotosheleza mahitaji yao.

“Baadhi ya mazao tunayotarajia kuanza nayo ni pamoja na dengu, choroko, mbaazi, ufuta, korosho, kahawa na kokoa. Mfumo huu utasaidia upatikanaji wa masoko ya uhakika na kwa uwazi na hivyo kuifanya nchi ijulikane kimataifa juu ya uzalishaji wa mazao hayo na mengine”.

Pia, Waziri Mkuu amesema katika kuhakikisha mafanikio yanapatikana kwenye sekta za kilimo, viwanda na biashara ni lazima soko la bidhaa lipewe ushirikiano kwenye ngazi zote kuanzia Wizara, Mikoa na Halmashauri za Wilaya ili mazao ya kimkakati pamoja na yale yenye changamoto ya masoko yauzwe kupitia soko hilo muhimu.

“Taratibu zote za unedeshaji wa biashara hiyo zikamilike kwa ushirikiano wa vyama vya ushirika, TAMISEMI, Wakala wa Stakabadhi Ghalani na Wizara ya Kilimo, Wizara ya Viwanda na Biashara na Wizara ya Fedha na Mipango. “Pia elimu kwa wadau wote itolewe kwa muda wote ili kuwaandaa washiriki wa mnyororo mzima wa thamani za mazao”.

Waziri Mkuu amesema Soko la Bidhaa Tanzania ni taasisi iliyoanzishwa na kusimamiwa kwa mujibu wa Sheria ya Masoko ya Bidhaa ya mwaka 2015 na Kanuni za Masoko ya Bidhaa za mwaka 2016.

“Aidha, napenda kusisitiza kuwa kuanza kufanya kazi kwa mfumo huu ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ibara namba 22(g)(ii) ya 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2016/17– 2020/21) na Awamu ya Pili ya Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo (ASDP II)”.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amezindua mfumo mwinginewa Kielektroniki wa Kusimamia Biashara za Kilimo (Agricultural Trade Management Information System – ATMIS).“Mifumo hii inalenga kuongeza ufanisi wa shughuli mbalimbali za kuendeleza sekta za kilimo nchini na kuimarisha biashara ya mazao na bidhaa za kilimo.

Vilevile, Waziri Mkuu aliongeza kuwa Serikali inasimamia utekelezaji wa BluePrint inayolenga kuboresha mazingira ya uwekezaji na biashara nchini. “Kupitia BluePrint hiyo, changamoto mbalimabali zimeainishwa na kuwekewa utaratibu wa kutatuliwa”.

Amesema miongoni mwa changamoto hizo ni kuwepo kwa mlolongo mrefu wa kupata vibali na leseni za uwekezaji na biashara na wateja kulazimika kufuata vibali hivyo kwenye Ofisi za Taasisi zilizopewa mamlaka ya kutoa leseni na vibali hivyo.

“Niwapongeze Wizara ya Kilimo na Taasisi ya TradeMark East Africa kwa kusanifu na kuanza kutumia mfumo wa kielektroniki wa kutoa vibali, leseni na huduma za malipo kwa wafanyabiashara”.

Pia, Waziri Mkuu ametoa wito kwa Wizara ya Kilimo kusimamia utekelezaji wa mfumo huo ili lengo linalotarajiwa na Serikali hususani kurahisisha biashara liweze kufikiwa. Pia, Taasisi na Idara zote zinazotumia mfumo huo zihakikishe zinatoa elimu kwa watumiaji na wadau wote wa mfumo kwa lengo la kuondoa urasimu katika kuwahudumia wateja.

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema katika kutekeleza mkakati wa kuimarisha mfumo wa biashara za mazao nchini Serikali imetengeneza Mfumo wa Kielektroniki wa utoaji wa leseni, vibali na malipo ya huduma (ATMIS) ili kurahisisha biashara za mazao ya kilimo.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amewaagiza viongozi wa Wizara ya Kilimo wahakikishe wanashirikiana na viongozi wa Wizara ya Viwanda na Biashara kusimamia mifumo hiyo sanjari na kupambana na wanunuzi nje ya mifumo iliyokusudiwa.

Kwa upande wake, Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga amesema kuwa maendeleo ya Sekta ya Kilimo na Tasnia ya Ushirika nchini itaimarika baada ya kuzinduliwa mfumo rasmi wa mauzo ya mazao ya kilimo kupitia Soko la Bidhaa Tanzania (TMX).

Amesema kuwa TMX imeanzishwa kwa lengo la kuongeza ufanisi katika juhudi za Serikali za kurasimisha mifumo ya masoko ambayo imekuwa na changamoto kwa muda mrefu; kwa kuwaunganisha Wauzaji na Wanunuzi wa bidhaa, kuleta ushindani kwenye bei, kupunguza gharama za uendeshaji biashara na kuweka uwazi.

Mbali na soko la bidhaa pia amesema kuwa kuzinduliwa kwa Mfumo wa Kielektoniki wa Kusimamia Biashara (Agricultural Trade Management Information System – ATMIS) utaimarisha makusanyo ya maduhuli na tozo kwa kuhakikisha huduma zote za utoaji vibali, leseni na vyeti unafanyika kielektroniki na pia kudhibiti udanganyifu katika hati na nyaraka za huduma hizo.

Amesema faida zingine ni kuhakikisha kuwa kazi ya kumhudumia mteja inafanyika kwa wakati mara tu baada ya hatua zote za maombi ya utoaji vibali, na vyeti kumalizika.  Pia kuimarisha upatikaji wa taarifa na takwimu muhimu za uingizaji na usafirishaji mazao ya kilimo nje ya nchi na Kuondoa tatizo la nyaraka bandia ambalo huchangiwa na matumizi ya mfumo.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya Nane Nane ya mwaka huu inasema: - “Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa Ukuaji wa Uchumi wa Nchi”.Kaulimbiu hiyo inakwenda sambamba na azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kukuza uchumi wa viwanda na biashara, ikilenga kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja, Pato la Taifa na wakati huo huo kupunguza umaskini.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally, Waziri wa Ulinzi Dkt. Hussein Mwinyi, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina, Naibu Waziri Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, Naibu Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI, Josephat Kandege, Naibu Waziri wa Madini, Stansalaus Nyongo pamoja na maafisa wengine wa Serikali.
 (mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Waziri Mkuu Atoa Maagizo Mazito Kwa Wizara Tano

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameziagiza Wizara za Kilimo, Viwanda na Biashara, Uvuvi na Mifugo kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji kutengeneza mkakati wa kuanzisha viwanda vya kuchakata mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi nchini.

Amevitaja viwanda kuwa ni pamoja na vya nyuzi, nguo, ngozi, maziwa, minofu, nyama, kubangua korosho, kutengeneza unga, mafuta ya kula, sabuni, usindikaji wa matunda na mbogamboga, “Kwani ndiyo msingi wa kauli mbiu yetu ya kufikia uchumi wa viwanda 2025”.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Alhamisi, Agosti 8, 2019) katika kilele cha maadhimisho ya sikukuu ya wakulima nane nane Kitaifa kwenye viwanja vya maonesho Nyakabindi mkoani Simiyu kwa niaba ya Rais Dkt. John Magufuli.

Waziri Mkuu amsema sambamba na mkakati huo, pia ameagiza kuimarishwa kwa vyama vya ushirika ili kumwezesha mkulima kuendelea kumiliki zao lake mpaka hatua ya kuuza sokoni. “Vyama vya ushirika vikiweza kuchakata mazao na kuyaongeza thamani vitamuwezesha mkulima kuwa na umiliki na kufaidika na bei ya soko”.

Amesema mfano uliooneshwa katika zao la Kahawa kupitia Chama Kikuu cha Ushirika Kagera (KCU) ni mzuri ambapo wanamiliki asilimia 100 ya Kiwanda cha Kukoboa Kahawa (BUCOP), pamoja na asilimia 54 ya Kiwanda cha Kuzalisha Kahawa – Tanganyika Instant Coffee (TANICA).

“Kwa upande wa Pamba, Nyanza Cooperative Union (NCU) walianza vizuri kwa kumiliki viwanda vinane vya kuchambulia pamba. Tunataka jitihada za namna hii zianzishwe katika shughuli za wakulima wetu na zilizopo ziimarishwe”.

Hivyo, ameitaka Tume ya Maendeleo ya Ushirika kwa kushirikiana na wadau, ifanye tathmini kwenye vyama vya ushirika vinavyomiliki viwanda ili kubaini hali ilivyo kwa sasa na kuweka mikakati ya kuvifufua na kuviongezea uwezo.

Amesema safari ya kujenga uchumi wa viwanda itaiwezesha Tanzania kuwa nchi yenye kipato cha kati imeanza na inaendelea vizuri na  matarajio yake ni kuona wananchi wote bila kujali tofauti za kiitikadi, wataendelea kuunga mkono juhudi hizo kwa kuwa maendeleo wanayoyapigania ni kwa manufaa ya wote waliopo leo na vizazi vijavyo.

Waziri Mkuu amesema kwa mantiki hiyo, kila Mtanzania hanabudi kuongeza bidii katika kufanya kazi, kupiga vita rushwa, kulipa kodi ya Serikali na kulinda rasilimali za Taifa ili ziweze kutumika sasa na kwa faida ya vizazi vyetu vijavyo.

“Niwaombe muendelee kuiunga mkono Serikali ya Awamu ya Tano kwa namna ambavyo imeamua kwa makusudi kuanzisha miradi mikubwa ya ujenzi wa miundombinu ya kiuchumi inayoendelea kujengwa nchini ikiwemo reli ya kisasa ya mwendokasi, mradi mkubwa wa umeme wa Mto Rufiji, upanuzi wa viwanja vya ndege, bandari na ununuzi wa ndege kubwa”.

Amesema kuboreshwa kwa miundombinu hiyo, pamoja na mambo mengine kutachochea uwekezaji mkubwa katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi, kurahisisha usafirishaji wa mazao, mifugo, samaki, na kupunguza gharama za uzalishaji na hivyo kuwezesha viwanda vya ndani kushindana kibiashara na bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya nje ya nchi.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kutoawito kwa viongozi wa Mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga kuendelea kushirikiana na Wizara za Sekta ya Kilimo kuhakikisha viwanja hivyo vya Nyakabindi, vinakuwa kituo cha mafunzo ya wakulima, wafugaji na wavuvi. 

“Kumbukeni kuwa kila mmoja wetu akitimiza wajibu wake ipasavyo, maendeleo ya viwanda yanawezekana, ajira zitapatikana, uhakika wa chakula na lishe bora itakuwepo na sote kwa pamoja tutasonga mbele kufikia nchi yenye uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025”.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya Nane Nane ya mwaka huu inasema: - “Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa Ukuaji wa Uchumi wa Nchi”.Kaulimbiu hiyo inakwenda sambamba na azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kukuza uchumi wa viwanda na biashara, ikilenga kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja, Pato la Taifa na wakati huo huo kupunguza umaskini.

Awali, Waziri Mkuu alitembelea na kukagua mabanda mbalimbali katika maoneosho hayo. Miongoni mwa mabanda aliyoyatembelea ni pamoja na banda la EPZA, NMB, CRDB, NBC, BOT kitengo cha mifumo ya malipo ya Kielektroniki ya Serikali, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi na JKT.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally, Waziri wa Ulinzi Dkt. Hussein Mwinyi, Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina, Naibu Waziri Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, Naibu Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI, Josephat Kandege, Naibu Waziri wa Madini, Stansalaus Nyongo pamoja na maafisa wengine wa Serikali.
 

Kuzinduliwa Kwa Mfumo Rasmi Wa Mauzo Ya Mazao Ya Kilimo Kutaimarisha Maendeleo Ya Kilimo Na Ushirika Nchini– Mhe Hasunga

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo, Simiyu
Serikali imesema kuwa kuwa maendeleo ya Sekta ya Kilimo na Tasnia ya Ushirika nchini itaimarika baada ya kuzinduliwa mfumo rasmi wa mauzo ya mazao ya kilimo kupitia Soko la Bidhaa Tanzania (TMX).

TMX ina lengo la kuongeza ufanisi katika juhudi za Serikali za kurasimisha mifumo ya masoko ambayo imekuwa na changamoto kwa muda mrefu; kwa kuwaunganisha Wauzaji na Wanunuzi wa bidhaa, kuleta ushindani kwenye bei, kupunguza gharama za uendeshaji biashara na kuweka uwazi.

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) amesema hayo tarehe 8 Agosti 2019 wakati wa kilele cha maadhimisho ya sherehe za wakulima (Nanenane) zinazofanyika kitaifa katika viwanja vya Nyakabindi Katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.

Amesema kuwa mbali na soko la bidhaa pia kuzinduliwa kwa Mfumo wa Kielektoniki wa usajili wa wakulima na mfumo wa kielekroniki wa Kusimamia Biashara (Agricultural Trade Management Information System – ATMIS) utaimarisha makusanyo ya maduhuli na tozo kwa kuhakikisha huduma zote za utoaji vibali, leseni na vyeti unafanyika kielektroniki na pia kudhibiti udanganyifu katika hati na nyaraka za huduma hizo.

Alizitaja faida zingine kuwa ni pamoja na Kuhakikisha kuwa kazi ya kumhudumia mteja inafanyika kwa wakati mara tu baada ya hatua zote za maombi ya utoaji vibali, na vyeti kumalizika na kuimarisha upatikaji wa taarifa na takwimu muhimu za uingizaji na usafirishaji mazao ya kilimo nje ya nchi na Kuondoa tatizo la nyaraka bandia ambalo huchangiwa na matumizi ya mfumo

Mhe Hasunga ameyataja maeneo maalumu ya kimkakati katika sekta ya kilimo ambacho kinafanyiwa maboresho ili kuimarisha usimamizi wa kilimo na kuwapatia Wakulima huduma kwa urahisi zaidi ambayo ni Bima ya Mazao, Ambapo wizara ya Kilimo imeanzisha mwongozo wa Bima ya Mazao kwa Wakulima ambao ukielekeza jinsi ya kujiunga, kutekeleza na kuwasilisha madai ili kumwezesha kulipwa fidia pale anapopata hasara.

Mapitio ya Sera na Sheria, Mhe Hasunga amesema kuwa Wizara imeanza na itaendelea kuipitia Sera ya Taifa ya Kilimo ya mwaka 2013 na sheria mbalimbali kwa lengo la kubaini maeneo ambayo yatapaswa kuhuishwa ili kwenda na hali halisi ya sasa na mwelekeo wa Serikali wa kubadili kilimo kuwa kilimo cha kibiashara.

“Mtazamo wa Wizara ni kuwa na Sheria moja itakayosimamia rasilimali watu, matumizi bora ya pembejeo, ardhi ya kilimo na maeneo mengine muhimu” Alikaririwa Mhe Hasunga

Zingine ni Mfumo wa upatikanaji wa Pembejeo za Kilimo, Wizara inaendelea na zoezi la kupitia kwa kina mifumo iliyopo ya uzalishaji, uagizaji na usambazaji wa mbegu, mbolea na viuatilifu. Aidha wizara inaendelea kutoa elimu kwa Wakulima ili wazalishe kulingana na mahitaji ya soko na kufanya kazi kwa karibu na Taasisi nyingine zinazohusika na masoko nchini ikiwemo TANTRADE na Soko la Bidhaa (TMX).

Sambamba na hayo amesema kuwa wizara ya Kilimo imejipanga kuhakikisha kuwa kupitia Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II) Sekta ya Uvuvi inaongeza ufugaji wa samaki wenye tija na endelevu katika mabwawa ili kuwe na uwezekano wa kuzalisha samaki wengi zaidi na kuondoa kabisa uvuvi haramu.

“Ni imani yangu kuwa kama ASDP II itatekelezwa vizuri, Tanzania itakuwa nchi ya kipato cha kati kabla ya mwaka 2025” Alisisitiza

Mkongo: Kibongo ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
********************************
SUPER MKONGO MPYA,
_______________________________
********************************
Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile,

- kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa
- maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo
- kukosa hamu ya tendo la ndoa
- kushindwa kurudia tendo la ndoa
- maumbile kusimama kwa kulegea
-  kulegea katikati ya tendo
- kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu
- kuishiwa nguvu kutokana na punyeto.

Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MCONGO MPYA, kiboko ya matatizo haya.
_______________________________
Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume
_______________________________
(1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea.
(2) ngiri
(3) kuugua chango la uzazi kwa muda mrefu.
(4) kupungukiwa hormone za testosterone.
(5) ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na visivyo na virutubisho  vya kutosha.
(6) kutokufanya mazoezi na mwenendo wa maisha.
(7) kisukari.
(8) tumbo kuunguruma na kujaa gesi.
(9) maumivu ya kiuno nk.
_______________________________

WASILIANA NA:
DR. MCONGOMANI
SIMU NO:
📞0658816558
📞0682323682
Popote ulipo huduma hii inakufikia

Mawakili Watano Kutetea Ubunge wa Tundu Lissu Mahakamani

$
0
0
Mawakili wanne wakiongozwa na Wakili Peter Kibatala watamtetea Tundu Lissu katika kesi ya kupinga kuvuliwa ubunge. Lissu anaiomba mahakama ibatilishe yeye kuvuliwa ubunge, izuie Mbunge Mteule, Miraji Mtaturu kuapishwa, na kuamuru Bunge kumlipa stahiki zake zote wakati akitibiwa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Alute Mughwai ambaye ni kaka yake Lissu amesema kesi hiyo itaanza kuunguruma Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam.

Mbali na Kibatala, mawakili wengine ni Jeremia Mbesya, John Malya na Fredi Kalonga.

Amebainisha kuwa maombi ya kufunguliwa kesi hiyo  chini ya hati ya dharura, kupitia kwake (Mughwai) aliyempa mamlaka ya kisheria kufanya hivyo, yatasikilizwa Agosti 21, 2019.

Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga aongeza siku tatu maonyesho ya Nanenane Simiyu

$
0
0
Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga, ameongeza siku tatu kuendelea kuwepo kwa maonyesho ya sikuu ya wakulima kitaifa (Nanenane), kuanzia kesho Ijumaa Agosti 9, hadi jumapili ya wiki hii.

Waziri Hasunga ametangaza uamuzi huo wakati akiongea kwenye kilele cha maonyesho hayo mbele ya Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo iliyofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.

Hasunga amesema kuwa uamuzi huo unatokana na wakuu wa mikoa ya Mara, Shinyanga na Simiyu ambao ndiyo waandaji wa maonyesho hayo kanda ya Magharibi kutaka kuongezewa muda.

“Nilipokea ombi la wakuu wa mikoa ya Mara, Simiyu na Shinyanga ambao ndiyo waaandaaji wa maonyesho haya, wakitaka kuongezewa siku, nami kwa mamlaka niliyopewa nimekubali ombi lao na kuongeza siku tatu hadi jumapili ya wiki hii ndiyo yamalizike,” amesema Hasunga.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Msemaji Mkuu Wa Serikali Apata Kitabu Kinachoonesha Madini Yapatikanayo Nchini.

$
0
0
Leo tarehe Augusti 7, 2019 , Dr Hassan Abbas ambaye ni msemaji Mkuu wa serikali ya Jamhuri wa Muungano Tanzania ametembelea Banda la *GST* katika wiki ya Maonesho ya Mkutano Mkuu wa 39 wa  *SADC* kwa lengo la kupata taarifa mbalimbali za kitaalam juu ya Madini na Miamba iliyopo nchini.

Kitabu hicho ambacho ni toleo jipya  kinaonesha Madini kuanzia ngazi ya Wilaya , kata na Kijiji kimeainisha Zaidi ya madini 220.

Akiambatana na jopo la waandishi wa Habari , Dr.Hassan alipata maelezo mbalimbali kutoka kwa Mtaalam Mhandisi Priscuss Kaspana hususani katika sekta ya Madini ya viwanda yaani Industrial Minerals.

Sambamba na taarifa hizo Dr.Hassan kwa niaba ya serikali alipata zawadi ya kitabu Cha Madini Yapatikanayo Tanzania toleo jipya.

Waziri Mkuu Aongoza Mazishi Ya Mke Wa Mwanasheria Mkuu Wa Serikali

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo, Agosti 7, 2019 ameongoza mazishi ya mke wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Profesa Adelardus Kilangi, Bibi Natalia Bahati Kilangi.

Akizungumza kwa niaba ya Serikali katika mazishi hayo yaliyofanyika nyumbani kwa Profesa Kilangi eneo la Luchelele jijini Mwanza, Waziri Mkuu amemuomba Profesa Kilangi na familia yake kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu ambapo wamempoteza mama ambaye ni nguzo muhimu ya familia.

Kadhalika, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwasilisha salamu za pole kutoka kwa Rais Dkt. John Magufuli kwa Profesa Kilangi na familia yake kutokana na msiba mzito walioupata.

Katika salamu zake Rais Dkt. Magufuli amesema Serikali inathamini sana mchango mkubwa na mahili unaotolewa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na anamini kwamba kwa vyovyote vile wakati wa uhai wake, marehemu Natalia alishiriki kwa kiwango kikubwa kuhakikisha kwamba mumewe anaifanya kazi yake vizuri.

Awali, Spika wa Bunge, Job Ndugai aliwasihi waombolezaji wote wamkumbuke katika sala zao, Mwanasheria Mkuu wa Seriakali Profesa Kilangi ambaye ana kazi nzito ya kuishauri Serikali na alimtaja kuwa ni kiungo muhimu cha mihimili yote mitatu.

Naye, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza, Renatus Nkwande alimuomba Profesa Kilangi na familia yake wajipe moyo kwa sababu binadamu anapokuwa hai au anapokufa bado anabaki kuwa mali ya Mwenyezi Mungu.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Umoja wa Wamiliki wa Mabenki nchini, Abdulmajid Msekela ambaye pia ni Mkurugenzi wa Benki ya CRDB alisema wanachama wote wa umoja huo wanatoa pole kwa familia na wanamwombea Mwanasheria Mkuu wa Serikali na familia nzima, Mungu awape uvumilivu katika kipindi hiki cha majonzi.

Baadhi ya viongozi waliohudhuria katika mazishi hayo ni pamoja na Waziri wa Katiba na Sheria, Balozi Augustine Mahiga, Waziri wa Madini, Doto Biteko, Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga.

Wengine ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama na Katibu Mkuu wa CCM, Bashiru Ally, Manaibu Mawazi, Wakuu wa Mikoa na wilaya na viomgozi mbalimbali wa Serikali.

Mazishi hayo pia yalihudhuriwa na Askofu wa Jimbo la Geita na Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania(TEC), Flavian Kassala, Mapadri na Masheikh kutoka maeneo mbalimbali nchini.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,        

Viongozi Wa SADC Tanzania Ni Nyumbani Kwao- Dkt Abbassi

$
0
0

Na Pascal Dotto-Maelezo
Msemaji Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Hassan Abbasi amesema kuwa Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa  Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini Mwa Afrika- SADC kwa viongozi Tanzania ni nyumbani. 
 
Akizungumza katika Kipindi cha 360 cha Clouds TV, Dkt. Abbasi amesema kuwa Tanzania ina historia kubwa kwa nchi za kusini mwa Afrika tokea enzi za ukombozi wa nchi hizo, ambapo Tanzania ilitumika kama kitovu cha wapigania uhuru. 

“Viongozi hawa wengi wanarudi nyumbani, ikumbukwe kuwa Tanzania ndiyo ilikuwa moja kati ya mataifa matatu yaliyoasisi kamati ya Ukombozi ya Nchi za Kusini mwa Afrika, Tanzania ndiyo ilikuwa Makao Makuu ya ukombozi na  Ofisi Kuu ya ukombozi ipo Jijini Dar es Salaam, kwa hiyo hii ni hitoria kubwa kwa nchi yetu”, Dkt.Abbasi. 
 
Dkt.Abbasi amesema kuwa Mkutano huu ambao ni fursa kwa watanzania maandalizi yake yamekamilika na sasa Tanzania ipo tayari kuwakaribisha wageni kutoka nchi wanachama wa SADC, huku baadhi ya mambo yakikamilishwa na kamati ya maandalizi kutoka SADC, Serikali ya Tanzania, wabia wa SADC pamoja na Sekta binafsi. 
 
Aidha, Dkt. Abbasi amesema kuwa nchi za SADC zimekuwa na ajenda kubwa ya kutekeleza ujenzi na kuimarisha viwanda Jambo ambalo alisisitiza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe magufuli wakati wa ufunguzi wa maonesho ya nne ya wiki ya viwanda ya Nchi wanachama wa SADC. 
 
“Mhe.Rais Magufuli anaamini kwenye Sera ya Viwanda kama Tanzania tunavyotekeleza Sera hii, siyo kwa Tanzania tu bali hata kwenye nchi wananchama wa SADC. Rais  ata sukuma maendeleo ya viwanda kwani atakuwa Mwenyekiti wa SADC, na kama mnavyojua nchi wanachama wanatengeneza ajenda kuhusu ukuaji na uimarishaji wa viwanda”, Dkt.Abbasi. 
 
Amesema kuwa viwanda ndiyo nguzo ya Maendeleo kwa nchi wanachama na kama Rais Magufuli, alivyosisitiza kuwa Afrika lazima ifanye biashara yenyewe kwa yenyewe badala ya kutegemea kufanya biashara na Nchi za Ulaya. Hivyo, SADC ni fursa kwa nchi wanachama kununua na kuuza bidhaa kwenye jumuia, kama nchi inahitaji mahindi basi Tanzania iuze mahindi yake ndani ya Jumuiya ili kukuza soko. 
 
Dkt.Abbasi alisema kuwa Rais Magufuli amekuwa ni kiongozi ambaye anasimamia yale anayoyaamini ili kuwaletea Maendeleo wananchi wake kwa hiyo sasa atakwenda kusukuma utekelezaji wa ujenzi wa viwanda kwa nchi wanachama. 
 
“Kuna mwanahistoria mmoja anaitwa Walter Rodney ambaye aliandika kitabu kushusu namna gani mataifa ya Ulaya yanayadidimiza mataifa ya Afrika, lakini pia unaona siku ile Rais anaongea na kukubaliana na msomi mwingine aliyeandika kuwa namna gani Afrika inajididimiza kwa hiyo msimamo wake utaifanya Tanzania na SADC kutekeleza ujenzi wa viwanda akiwa kama mwenyeketi wa Jumuiya hiyo kwa mwaka mmoja”, Dkt.Abbasi. 
 
Dkt.Abbasi alisema kuwa nchi za SADC zinatakiwa kuwa na viwanda vya kuchaka malighafi na kuzalisha bidhaa ili kuongeza thamani, akitolea mfano wa mahindi ukiuza bila kuchakatwa hindi moja shilingi 200. Lakini kumbe likiwa limechatwa na kuzalisha unga unaweza ukauza kilo moja kwa shilingi  2,000, kwa hiyo ajenda ya kujenga viwanda vya kuchakata mazao itasimamiwa vema itakuza thamani ya bidhaa ndani na Nje ya Jumuiya. 
 
Dkt. Abbasi alisema kuwa watanzania wengi sasa wameamka na Serikali ambacho inafanya ni kuwawezesha waamke na kuchangamkia fursa za biashara ndani ya SADC. Alitolea mfano kwenye maonesho ya SADC ambayo yanaendelea Jijini Dar es Salaam kuwa wapo watanzania ambao wanaonesha bidhaa zao wanazopeleka SADC. 
 
“Takwimu zinaonesha watanzania tumeaka sana kwenye soko la SADC, tumepeleka bidhaa zinazofikia dola za kimarekani milioni 900 na tumengiza bidhaa zinazokadiriwa kufikia Dola milioni 600, kwa hiyo sisi bado kitakwimu tumechangamka zaidi kwenye soko la SADC. 
 
Dkt.Abbasi alisema kuwa Serikali imeweka mikakati kwa Taasisi zinazohusisha masula ya biashara ikiwemo Tantrade na Bodi ya Masoko ya Mazao Mchanganyiko, kuitafuta masoko na kufanya utafiti ili kuwasaidia wafanyabiashara.

Tiba Halisi ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
*NKOLOMIJE*/
√Ni dawa bora ya mitishamba yenye kuimarisha, kurefusha na kukufanya uwe imara hata kama umelala pia huimarisha na kukuza  maumbile yaliyosinyaa na kuwa regevu

*📌SUPER GAFINA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri ya uume ulio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/


Bado hujachelewa

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM  AU UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO SIMU NO:/
*📞0752723508*

Waziri Mkuu: Watakaohujumu Ushirika Kuchukuliwa Hatua

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameagiza watendaji wote watakaobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa na ubadhirifu katika vyama vya ushirika wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria.

Kadhalika, Waziri Mkuu amewataka viongozi wote wa ushirika nchini wahakikishe wanaongoza vyama vya ushirika kwa kufuata Sheria ya Ushirika Namba 6 ya mwaka 2013, kanuni na taratibu zilizopo.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Alhamisi, Agosti 8, 2019) katika kilele cha maadhimisho ya sikukuu ya wakulima nane nane Kitaifa kwenye viwanja vya maonesho Nyakabindi mkoani Simiyu kwa niaba ya Rais Dkt. John Magufuli.

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kutoa rai kwa Wanaushirika wote nchini kuhakikisha wanachagua viongozi wenye weledi, wachapakazi, waadilifu na wanao upenda ushirika ili ushirika uimarike na kuwa endelevu.

Amesema historia inaonesha kwamba miaka ya nyuma ushirika ulifanya kazi nzuri katika kusimamia uzalishaji, tija, uchakataji na masoko ya mazao. “Hata hivyo, ushirika ulianza kulegalega katika miaka ya 1980”.

Waziri Mkuu amesema kutokana na hali hiyo, Serikali iliamua kuanzisha Tume ya Maendeleo ya Ushirika kama chombo cha kusimamia shughuli za maendeleo ya ushirika nchini.

Amesema katika kuimarisha vyama vya ushirika nchini, tume hiyo imeendelea kuweka mazingira rafiki kwa Vyama vya Ushirika ili kuzalisha kwa tija na kuongeza uzalishaji kutokana na matumizi ya zana bora za kilimo. Amesema vyama vya ushirika 33 vimekopeshwa trekta moja kwa kila chama kupitia makubaliano yaliyofikiwa kati ya Tume na Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) na Bodi ya Pamba (TCB).

Pia, Waziri Mkuu amesema katika kuendeleza azma ya Serikali ya kuwa na uchumi wa viwanda, Vyama vya Ushirika vimeendelea kuwekeza katika miradi mingine ya kimaendeleo ambayo inaisaidia katika kuleta maendeleo.

 “Hadi kufikia Juni 30, 2019 jumla ya Vyama vya Ushirika 104 vinamiliki viwanda vidogo kwa ajili ya kuongeza thamani ya mazao wanayoyazalisha hali ambayo imeleta tija kwa jamii inayozunguka maeneo hayo”.

Amesema hadi Desemba 2018, mikopo yenye thamani ya sh. trilioni 1.3 imetolewa kwa wanachama ikilinganishwa na sh. bilioni 902 iliyotolewa kufikia Desemba 2017. Akiba na amana za wanachama katika SACCOS zimefikia sh. bilioni 575 na hisa sh. bilioni 79.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu kwa mara nyingine, ametumia fursa hiyo kuwaelekeza Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya wafanye tena mapitio ya idadi ya Maafisa Kilimo waliopo Wilayani na kuwahamishia katika kata na vijiji ili kuimarisha usimamizi wa mazao.

Hivyo, Waziri Mkuu amesema ngazi ya Makao Makuu ya Wilaya wabaki wataalamu wawili akiwemo Mkuu wa Idara na msaidizi wake kwa ajili ya uratibu. Maafisa Kilimo wa Wilaya wawe na ratiba za kwenda vijijini kuwatembelea maafisa ugani ili kutatua changamoto zinazowakabili katika uendelezaji wa kilimo na hawapaswi kukaa maofisini.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya Nane Nane ya mwaka huu inasema: - “Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa Ukuaji wa Uchumi wa Nchi”. Kaulimbiu hiyo inakwenda sambamba na azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kukuza uchumi wa viwanda na biashara, ikilenga kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja, Pato la Taifa na wakati huo huo kupunguza umaskini.

Awali, Waziri Mkuu alitembelea na kukagua mabanda mbalimbali katika maoneosho hayo. Miongoni mwa mabanda aliyoyatembelea ni pamoja na banda la EPZA, NMB, CRDB, NBC, BOT kitengo cha mifumo ya malipo ya Kielektroniki ya Serikali, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi na JKT.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally, Waziri wa Ulinzi Dkt. Hussein Mwinyi, Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina, Naibu Waziri Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, Naibu Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI, Josephat Kandege, Naibu Waziri wa Madini, Stansalaus Nyongo pamoja na maafisa wengine wa Serikali.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Kutana na Sheikh Omary Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali za Matatizo Yako Na Kutafsiri Ndoto kwa kutumia Vitabu vya QUR-AN

$
0
0
Sheikh Omary Ni bigwa wa kutatua matatizo kwa haraka, ni mtu aliye jaliwa kubuli Shufaa pia anatoa Duah  za Ruhia. Ukija na Maradhi yanaondoka hapo hapo bila kungoja kesho,  UKIPEWA MKONO  na Sheikh Omary .
 
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
 
Sheikh Omary ni Mtaalamu wa Nyota za Binadamu  Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
 
Je una NUKSI  zisizo kwisha.!? JE umekimbiwa na Mume/Mke na Anaishi na Mtu Mwingine..!? Muone Akutatulie,
 
Una kosa bahati ya wanaume au mume wa kukuoa..Unataka nyota ing'ae Au huna hamu na Mkeo/ Mumeo.
 
Jini mahaba. Kama Unakasirika ovyo ukiwa na bwana au mwanamke wako na  kumchukia Mpaka  kushindwa kufanya nae tendo la ndoa.
 
Njoo umuone Sheikh Omary  na ujuwe  yanayo kusibu.Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN

Mawasiliano: Sheikh Omary 0673531992. WhatsApp/Call
Tembelea Page ya @Mtabibu_Omar  @Mtabibu_Omar
Usome Makala Tofauti Tofauti Kama.

Mkongo: Kibongo ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
********************************
SUPER MKONGO MPYA,
_______________________________
********************************
Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile,

- kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa
- maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo
- kukosa hamu ya tendo la ndoa
- kushindwa kurudia tendo la ndoa
- maumbile kusimama kwa kulegea
-  kulegea katikati ya tendo
- kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu
- kuishiwa nguvu kutokana na punyeto.

Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MCONGO MPYA, kiboko ya matatizo haya.
_______________________________
Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume
_______________________________
(1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea.
(2) ngiri
(3) kuugua chango la uzazi kwa muda mrefu.
(4) kupungukiwa hormone za testosterone.
(5) ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na visivyo na virutubisho  vya kutosha.
(6) kutokufanya mazoezi na mwenendo wa maisha.
(7) kisukari.
(8) tumbo kuunguruma na kujaa gesi.
(9) maumivu ya kiuno nk.
_______________________________

WASILIANA NA:
DR. MCONGOMANI
SIMU NO:
📞0658816558
📞0682323682
Popote ulipo huduma hii inakufikia
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images