Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Serikali Kuokoa Fedha Za Umma Kwa Kujinasua Kwa Mawakala Wa Ununuzi Wa Magari Yake

$
0
0
Na. Peter Haule, WFM, Dar es Salaam
Serikali  inaangalia njia mbadala ya ununuzi wa magari yake kwa kwenda moja kwa moja kiwandani bila kupitia kwa mawakala kutokana na gharama kuwa juu na hazitabiliki.

Hayo yalibainishwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu, alipofanya ziara ya kikazi katika Ofisi za Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA), jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kubaini changamoto na mafanikio ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2018/19 kwa taasisi hiyo.

Dkt. Kazungu alisema kuwa, ununuzi wa magari ya Serikali unatumia gharama kubwa kutokana na kuwatumia Mawakala wa Ununuzi ambao bei zao ni za juu na zinabadilika mara kwa mara, hivyo kuna haja ya kwenda moja kwa moja kiwandani ili kuokoa fedha za walipakodi zinazopotea.

Aidha Serikali inaangalia namna itakavyo boresha miundombinu ya GPSA hasa kwa kuwekeza katika Visima vya mafuta ili kuwa na mafuta ya kutosha hivyo kusaidia kuongeza ufanisi katika kuhudumia magari ya Serikali.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa GPSA, Dkt. Geraldine Rasheli, alimshukuru Dkt. Kazungu, kwa kutembelea taasisi yake na kuahidi kuyafanyia kazi maagizo yaliyotolewa ili kupunguza malalamiko katika utoaji huduma na kuongeza tija kwa Taifa.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Kazungu, anaendelea na ziara ya kikazi katika taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo, kuangalia changamoto za utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2018/19 na njia za kuzitatua kwa bajeti ya mwaka 2019/20.

Mwisho.

Viongozi Wa SADC Tanzania Ni Nyumbani Kwao- Dkt Abbassi

$
0
0

Na Pascal Dotto-Maelezo
Msemaji Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Hassan Abbasi amesema kuwa Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa  Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini Mwa Afrika- SADC kwa viongozi Tanzania ni nyumbani. 
 
Akizungumza katika Kipindi cha 360 cha Clouds TV, Dkt. Abbasi amesema kuwa Tanzania ina historia kubwa kwa nchi za kusini mwa Afrika tokea enzi za ukombozi wa nchi hizo, ambapo Tanzania ilitumika kama kitovu cha wapigania uhuru. 

“Viongozi hawa wengi wanarudi nyumbani, ikumbukwe kuwa Tanzania ndiyo ilikuwa moja kati ya mataifa matatu yaliyoasisi kamati ya Ukombozi ya Nchi za Kusini mwa Afrika, Tanzania ndiyo ilikuwa Makao Makuu ya ukombozi na  Ofisi Kuu ya ukombozi ipo Jijini Dar es Salaam, kwa hiyo hii ni hitoria kubwa kwa nchi yetu”, Dkt.Abbasi. 
 
Dkt.Abbasi amesema kuwa Mkutano huu ambao ni fursa kwa watanzania maandalizi yake yamekamilika na sasa Tanzania ipo tayari kuwakaribisha wageni kutoka nchi wanachama wa SADC, huku baadhi ya mambo yakikamilishwa na kamati ya maandalizi kutoka SADC, Serikali ya Tanzania, wabia wa SADC pamoja na Sekta binafsi. 
 
Aidha, Dkt. Abbasi amesema kuwa nchi za SADC zimekuwa na ajenda kubwa ya kutekeleza ujenzi na kuimarisha viwanda Jambo ambalo alisisitiza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe magufuli wakati wa ufunguzi wa maonesho ya nne ya wiki ya viwanda ya Nchi wanachama wa SADC. 
 
“Mhe.Rais Magufuli anaamini kwenye Sera ya Viwanda kama Tanzania tunavyotekeleza Sera hii, siyo kwa Tanzania tu bali hata kwenye nchi wananchama wa SADC. Rais  ata sukuma maendeleo ya viwanda kwani atakuwa Mwenyekiti wa SADC, na kama mnavyojua nchi wanachama wanatengeneza ajenda kuhusu ukuaji na uimarishaji wa viwanda”, Dkt.Abbasi. 
 
Amesema kuwa viwanda ndiyo nguzo ya Maendeleo kwa nchi wanachama na kama Rais Magufuli, alivyosisitiza kuwa Afrika lazima ifanye biashara yenyewe kwa yenyewe badala ya kutegemea kufanya biashara na Nchi za Ulaya. Hivyo, SADC ni fursa kwa nchi wanachama kununua na kuuza bidhaa kwenye jumuia, kama nchi inahitaji mahindi basi Tanzania iuze mahindi yake ndani ya Jumuiya ili kukuza soko. 
 
Dkt.Abbasi alisema kuwa Rais Magufuli amekuwa ni kiongozi ambaye anasimamia yale anayoyaamini ili kuwaletea Maendeleo wananchi wake kwa hiyo sasa atakwenda kusukuma utekelezaji wa ujenzi wa viwanda kwa nchi wanachama. 
 
“Kuna mwanahistoria mmoja anaitwa Walter Rodney ambaye aliandika kitabu kushusu namna gani mataifa ya Ulaya yanayadidimiza mataifa ya Afrika, lakini pia unaona siku ile Rais anaongea na kukubaliana na msomi mwingine aliyeandika kuwa namna gani Afrika inajididimiza kwa hiyo msimamo wake utaifanya Tanzania na SADC kutekeleza ujenzi wa viwanda akiwa kama mwenyeketi wa Jumuiya hiyo kwa mwaka mmoja”, Dkt.Abbasi. 
 
Dkt.Abbasi alisema kuwa nchi za SADC zinatakiwa kuwa na viwanda vya kuchaka malighafi na kuzalisha bidhaa ili kuongeza thamani, akitolea mfano wa mahindi ukiuza bila kuchakatwa hindi moja shilingi 200. Lakini kumbe likiwa limechatwa na kuzalisha unga unaweza ukauza kilo moja kwa shilingi  2,000, kwa hiyo ajenda ya kujenga viwanda vya kuchakata mazao itasimamiwa vema itakuza thamani ya bidhaa ndani na Nje ya Jumuiya. 
 
Dkt. Abbasi alisema kuwa watanzania wengi sasa wameamka na Serikali ambacho inafanya ni kuwawezesha waamke na kuchangamkia fursa za biashara ndani ya SADC. Alitolea mfano kwenye maonesho ya SADC ambayo yanaendelea Jijini Dar es Salaam kuwa wapo watanzania ambao wanaonesha bidhaa zao wanazopeleka SADC. 
 
“Takwimu zinaonesha watanzania tumeaka sana kwenye soko la SADC, tumepeleka bidhaa zinazofikia dola za kimarekani milioni 900 na tumengiza bidhaa zinazokadiriwa kufikia Dola milioni 600, kwa hiyo sisi bado kitakwimu tumechangamka zaidi kwenye soko la SADC. 
 
Dkt.Abbasi alisema kuwa Serikali imeweka mikakati kwa Taasisi zinazohusisha masula ya biashara ikiwemo Tantrade na Bodi ya Masoko ya Mazao Mchanganyiko, kuitafuta masoko na kufanya utafiti ili kuwasaidia wafanyabiashara.

Msemaji Mkuu Wa Serikali Apata Kitabu Kinachoonesha Madini Yapatikanayo Nchini.

$
0
0
Leo tarehe Augusti 7, 2019 , Dr Hassan Abbas ambaye ni msemaji Mkuu wa serikali ya Jamhuri wa Muungano Tanzania ametembelea Banda la *GST* katika wiki ya Maonesho ya Mkutano Mkuu wa 39 wa  *SADC* kwa lengo la kupata taarifa mbalimbali za kitaalam juu ya Madini na Miamba iliyopo nchini.

Kitabu hicho ambacho ni toleo jipya  kinaonesha Madini kuanzia ngazi ya Wilaya , kata na Kijiji kimeainisha Zaidi ya madini 220.

Akiambatana na jopo la waandishi wa Habari , Dr.Hassan alipata maelezo mbalimbali kutoka kwa Mtaalam Mhandisi Priscuss Kaspana hususani katika sekta ya Madini ya viwanda yaani Industrial Minerals.

Sambamba na taarifa hizo Dr.Hassan kwa niaba ya serikali alipata zawadi ya kitabu Cha Madini Yapatikanayo Tanzania toleo jipya.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Download App Yetu Kwenye Simu Yako Ili Uweze Kupata Habari Zetu Kwa Haraka Zaidi

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Waziri Mkuu Aongoza Mazishi Ya Mke Wa Mwanasheria Mkuu Wa Serikali

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo, Agosti 7, 2019 ameongoza mazishi ya mke wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Profesa Adelardus Kilangi, Bibi Natalia Bahati Kilangi.

Akizungumza kwa niaba ya Serikali katika mazishi hayo yaliyofanyika nyumbani kwa Profesa Kilangi eneo la Luchelele jijini Mwanza, Waziri Mkuu amemuomba Profesa Kilangi na familia yake kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu ambapo wamempoteza mama ambaye ni nguzo muhimu ya familia.

Kadhalika, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwasilisha salamu za pole kutoka kwa Rais Dkt. John Magufuli kwa Profesa Kilangi na familia yake kutokana na msiba mzito walioupata.

Katika salamu zake Rais Dkt. Magufuli amesema Serikali inathamini sana mchango mkubwa na mahili unaotolewa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na anamini kwamba kwa vyovyote vile wakati wa uhai wake, marehemu Natalia alishiriki kwa kiwango kikubwa kuhakikisha kwamba mumewe anaifanya kazi yake vizuri.

Awali, Spika wa Bunge, Job Ndugai aliwasihi waombolezaji wote wamkumbuke katika sala zao, Mwanasheria Mkuu wa Seriakali Profesa Kilangi ambaye ana kazi nzito ya kuishauri Serikali na alimtaja kuwa ni kiungo muhimu cha mihimili yote mitatu.

Naye, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza, Renatus Nkwande alimuomba Profesa Kilangi na familia yake wajipe moyo kwa sababu binadamu anapokuwa hai au anapokufa bado anabaki kuwa mali ya Mwenyezi Mungu.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Umoja wa Wamiliki wa Mabenki nchini, Abdulmajid Msekela ambaye pia ni Mkurugenzi wa Benki ya CRDB alisema wanachama wote wa umoja huo wanatoa pole kwa familia na wanamwombea Mwanasheria Mkuu wa Serikali na familia nzima, Mungu awape uvumilivu katika kipindi hiki cha majonzi.

Baadhi ya viongozi waliohudhuria katika mazishi hayo ni pamoja na Waziri wa Katiba na Sheria, Balozi Augustine Mahiga, Waziri wa Madini, Doto Biteko, Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga.

Wengine ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama na Katibu Mkuu wa CCM, Bashiru Ally, Manaibu Mawazi, Wakuu wa Mikoa na wilaya na viomgozi mbalimbali wa Serikali.

Mazishi hayo pia yalihudhuriwa na Askofu wa Jimbo la Geita na Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania(TEC), Flavian Kassala, Mapadri na Masheikh kutoka maeneo mbalimbali nchini.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,        

Waziri Lugola Apokea Taarifa Ya Bodi Ya Shirika La Magereza, Awataka Wajumbe Wahakikishe Magereza Inajitosheleza Kwa Chakula Kupitia Miradi Yao

$
0
0
Na Felix Mwagara, Dodoma (MOHA)
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amepokea taarifa ya Bodi ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Magereza, na kuwataka Wajumbe wa Bodi hiyo kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha Magereza inajitosheleza kwa chakula kupitia miradi mbalimbali inayomilikiwa na Jeshi hilo.

Waziri Lugola aliizindua Bodi hiyo Mei 30, 2019, na kutoa miezi miwili Wajumbe wa Bodi hiyo, kutembelea miradi mbalimbali ya Jeshi hilo na kumletea taarifa ya awali kuhusu miradi hiyo pamoja na maoni yao.

Akizungumza na Wajumbe wa Bodi hiyo baada ya kupokea taarifa yao, katika ukumbi wa mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dodoma, leo, Waziri Lugola alisema taarifa walioiwasilisha ameifurahia licha ya kuwa na mapungufu kadhaa ambayo yanahitaji uboreshaji zaidi.

Alisema Bodi hiyo inawataalamu mbaimbali ambao wanaweza wakaleta mabadiliko makubwa ya uzalishaji mali na kuweza kufanikisha Jeshi hilo linajitosheleza kwa chakula kupitia wafungwa mbalimbali waliopo magerezani.

“Nawapongeza sana kwa kazi nzuri, ila nawataka mfanye kazi zaidi ambayo itatuwezesha kuona mipango mizuri zaidi katika kulisimamia Shirika hili ambalo bodi yake tuliizindua,”alisema Lugola.

Pia Lugola aliwataka Magereza kutumia wataalamu wa Jeshi kupima viwanja vyao ili kufanikisha maendeleo zaidi na siyo kushirikiana na makampuni binafsi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Meja Jenerali Mstaafu, Raphael Muhuga, alisema Bodi yake kwa muda wa miezi miwili ilitembelea mradi wa ng’ombe wa nyama Mbigiri, mradi wa maziwa Kingolwira, mradi wa Uhunzi, mradi wa Kilimo Idete, mradi wa kilimo Kiberege na Mradi wa kilimo Isupilo ambapo Bodi hiyo ilifanya tathmini ya mali zilizopo, mipaka pamoja na historia ya miradi hiyo.

“Pia miradi mingine tuliyoitembelea ni mradi wa kilimo Ludewa, mradi wa kilimo na mifugo Kitai, mradi wa kilimo Mkwaya, na pia Bodi itaendelea kutembelea miradi mbalimbali ya Jeshi na kuendelea kutoa taarifa,” alisema Muhuga.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu aliitaka Bodi hiyo, ifanye ukaguzi wa kina wa mali za Shirika hilo kiundani zaidi ili taarifa hizo zije kiuhalisia zaidi na kuleta mikakati imara ya mafanikio.

Baadhi ya maelekezo aliyoyatoa Waziri Lugola kwa Bodi hiyo mara baada ya kuizindua, aliitaka kutekeleza maelekezo ya Rais John Magufuli kuhusu suala la Magereza kujitosheleza kwa chakula na pia bodi ihakikishe maeneo ya magereza yanapimwa na kupata hati miliki kwa kutumia wataalamu wa kupima ardhi wa Jeshi hilo.

Pia aliielekeza Bodi hiyo itembelee Magereza yote yenye miradi ya Shirika, na ifanye mkakati wa kutafuta wawekezaji kama vile wawekezaji kwenye mabwawa ya ufugaji wa samaki, na pia bodi itoe mawazo mapya ili kuondoa kufanya biashara kwa mazoea.

Waziri Mkuu: Maonesho ya Wiki ya Viwanda SADC Yatafungua Milango Mingi ya Masoko

$
0
0
Na Paschal Dotto-MAELEZO
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa amewataka watanzania kuchangamkia fursa zitokanazo na maonesho ya Viwanda ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) ili kuwezesha ukuaji wa uchumi wa viwanda ambao Serikali inaujenga. 

Akizungumza wakati wa kutembelea maonesho hayo yanayoendelea katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere, Viwanja vya Karimjee na Gymkana, Waziri Mkuu amesema kuwa maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 39 wa Wakuu wa Nchi za SADC yamekamilika yakihusisha kuwepo kwa maonesho ambayo nchi wanachama wataonesha teknoloji, Ubunifu na bidhaa zao kutoka katika Viwanda vya nchi za SADC.  

Waziri Mkuu alisema kuwa Serikali imetoa fursa kwa wafanyabiashara Wakubwa, wa kati, wadogowadogo na  wenye bidhaa zinazozalishwa kwa  mikono kuja kuonesha na kuchukua teknolojia kutoka nchi wageni ambao wapo nchini kwa maonesho hayo ya wiki moja. 

“Sisi kama Serikali tumetoa Fursa kwa wale ambao wanafanya kazi na kuzalisha bidhaa zao kwa kutumia mikono kuja kuonesha bidhaa zao ili ziweze kupata masoko kwa nchi wanachama wa SADC kwani nchi zote zinakuja hapa kuleta bidhaa mbalimbali kwa hiyo watanzania wanatakiwa kutumia fursa hii kuwauzia wageni bidhaa zetu”, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa. 

Alisema kuwa Fursa ambayo watanzania wameipata kutokana na mkutano huo wa SADC itawawezesha kukuza mitaji kwa kuungana na wageni ili kujenga viwanda vikubwa na kuimarisha uzalishaji wa bidhaa zitakazokidhi soko la nchii wanachama wa SADC.  

Majaliwa alisema kuwa Maonesho hayo ni muhimu kwani yamezikutanisha nchi za SADC kuja Tanzania kuonesha bidhaa, teknolojia ya uzalishaji viwandani, pamoja na ubunifu katika kuzalisha bidhaa hizo, kwa  watanzania ambao hawajawahi kufika Namibia, Msumbiji, Malawi pamoja na Nchi zingine za kusini mwa afrika ni fursa kubwa kwao kuleta bidhaa zao ili ziweze kupata soko kutoka SADC. 

“Maonesho haya ya wiki ya Viwanda kutoka Nchi wanachama wa SADC yanafursa nyingi kwa watanzania kwani yatafungua milango mingi ya masoko kwa bidhaa zinazozalishwa nchini, pia yatakuwa ya wazi kwa hiyo watanzania wanatakiwa kutumia fursa hii kubwa kuona bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya hapa nchini na nchi wanachama kutoka Jumuiya hii”, Kassimu Majaliwa, Waziri Mkuu Tanzania. 

Waziri Mkuu, alisema kuwa yako mataifa ambayo yameleta bidhaa mbalimbali ikiwemo nguo na madawa mbalimbali, kwa hiyo fursa ni pana kwa watanzania na ambayo ikitumiwa ipasavyo kuelekea uchumi wa kati wenye viwanda itawezesha kuinua uchumi kwa wananchi, na sasa inawakakaribisha wageni kuja kuwekeza katika sekta za madini na kilimo ili kuweza kujenga viwanda vikubwa kutokana na mitaji ya wazawa na wageni kutoka SADC. 

Aidha Waziri Mkuu, alisema kuwa Mkutano huo ni fursa kwa watanzania kutangaza vivutio vya utalii vilivyoko nchini ili kuweza kukuza sekta hiyo na kuwawezesha wageni kutoka nchi wanachama wa SADC kuja kuwekeza  

“Watanzania tutumie pia fursa ya Mkutano huu wa SADC kutangaza vivutio vilivyoko nchini, ili tuweze kuleta watalii kuja kutalii hapa kwetu, banda la Wizara ya Maliasili na Utalii lipo, lakini kila mtanzania popote alipo, kwa wakati wake, atumie muda wake kuwaeleza wageni ikiwezekana kuwapeleka kwenye maeneo ya utalii kwenda kutalii, aeleze kuhusu mbuga zetu kama vile Serengeti, Ngorongoro, Ruaha na Gombe, lakini pia Mlima kimanjaro, bonde la Olduvai Gorge  na fukwe zetu nzuri ili wageni waweze kutembelea maeneo haya”, Kassim Majaliwa,Waziri Mkuu wa Tanzania. 

Mwisho.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano 07 August

Upatikanaji Wa Vifaranga Vya Samaki Na Chakula Bora Wawekewa Mikakati.

$
0
0
Na. Edward Kondela
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeweka mikakati ya upatikanaji wa vifaranga vingi vya samaki pamoja na chakula bora cha samaki sambamba na kuendelea kutoa elimu ya ufugaji ili wananchi waweze kufuga samaki kwa tija.

Akizungumza kwenye maonesho ya wakulima, wafugaji na wavuvi (Nanenane) kitaifa, katika viwanja vya Nyakabindi vilivyopo Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah amesema serikali imelazimika kuweka mikakati hiyo kutokana na wananchi wengi kuwa na mwamko wa kufuga samaki kibiashara licha ya kuwepo kwa changamoto ya upatikanaji wa vifaranga bora na chakula kwa bei nafuu.

“Kwa mfano mwaka jana uhitaji wa mbegu za samaki ulikuwa unafikia takriban samaki Milioni 40 lakini sisi tumeweza kuzalisha kama Milioni 18 kwa hiyo kuna mikakati ipo kuhakikisha vituo vya serikali pamoja na kuhamasisha vile vya watu binafsi kuzalisha vifaranga bora, changamoto nyingine ni chakula ambapo wapo wanaotengeneza hapa nchini lakini vinakuwa havijafikia ubora unaotakiwa na wengine wanaagiza kutoka nje ya nchi ambapo ni bei ghali, hivyo tunaweka mikakati ya uwepo wa chakula bora na bei nafuu pamoja kutoa elimu ya utengenezaji wa chakula hicho.” Amesema Dkt. Tamatamah

Amefafanua kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia Maonesho ya Nanenane mwaka huu, sekta ya uvuvi imejikita zaidi katika kutoa elimu ya ufugaji bora wa samaki ili kuwavutia wananchi kuwekeza katika ufugaji samaki kibiashara.

Kuhusu ulaji wa samaki nchini Dkt. Tamatamah amesema kulingana na tafiti kutoka Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) kwa sasa kila mtanzania anakula walau Kilogramu 8.2 za samaki kwa mwaka ilhali FAO inapendekeza mtu mmoja kula samaki kilogramu 20.3 kwa mwaka, hivyo serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekuwa ikiweka pia mikakati ya uwepo wa ongezeko la uzalishaji wa samaki hapa nchini lakini pia kuhakikisha samaki wachache wanaozalishwa wanamfikia mlaji wakiwa katika hali nzuri.

Katibu mkuu huyo anayeshughulika na sekta ya uvuvi amebainisha pia kupitia Maonesho ya 27 ya Nanenane kwa Mwaka 2019 Wizara ya Mifugo na Uvuvi imejikita zaidi katika utoaji wa elimu kwa wadau katika sekta za mifugo na uvuvi ili kutatua changamoto mbali zinazowakabili na kuweza kufuga kwa tija.

Mwisho.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi 08 August

Lukuvi awasimamisha kazi watumishi 183 Wizara ya Ardhi

$
0
0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi , William Lukuvi  amewasimamisha kazi watumishi 183 wa wizara hiyo kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazowakabili.

Watumishi hao ambao waziri huyo amekabidhi majina yao Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa ajili ya uchunguzi, wanadaiwa  kuingilia mfumo wa kukadiria na kukusanya kodi ya pango ya ardhi kinyume na taratibu na kusababisha upotevu wa mapato ya Serikali.


MWAUWASA Yatangaza Bei Mpya za Maji

Naibu Waziri Wa Maliasili Na Iutalii Mhe, Constantyine Kanyasu Aziagiza Taasisi Za Uhifadhi Nchini Kuunda Vikosi Maalum Vya Kudhibiti Wanyamapori Wakali

$
0
0
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu ameagiza kila Taasisi ya Uhifadhi nchini ihakikishe inaunda kikosi maalum cha askari wanyamapori watakaokuwa wakitumika kudhibiti wanyama wakali na waharibifu pindi wanapovamia makazi ya wananchi badala ya kutegemea kikosi kimoja p cha  Askari  kutoka Kikosi Dhidi ya Ujangili (KDU)

Agizo hilo amelitoa jana wakati alipokuwa akizungumza na watumishi wa Shamba la miti la Rondo  ikiwa ni ziara yake ya kikazi katika mkoa wa  Lindi.

Akizungumza na watumishi hao, Mhe.Kanyasu amesema kutokana na Serikali kudhibiti ujangili kwa kiasi kikubwa wanyamapori kama vile tembo, chui na simba  wamekuwa wakitembea kila mahali kwa sababu hawana hofu ya kuuliwa kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma.

Amesema hali hiyo imepelekea mazao pamoja na maisha ya wananchi kuwa hatarini hasa kwa wananchi wanaoishi karibu na Hifadhi.

Amesema licha ya wanyamapori hao kuongezeka ikiwa moja ya sababu ni Serikali  kuzuia kusafirisha wanyamapori hai nje ya nchi wanyama hao wamekuwa wakipita njia zao za asili  ambazo tayari zimevamiwa na hivyo kusababisha matatizo makubwa kwa wananchi.

Kufuatia hali hiyo, Mhe.Kanyasu ameitaka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania ( TFS) Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) Hifadhi za Taifa( TANAPA) na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania ( TAWA) ziwe na vikosi maalum vya askari watakaotumika  kukabiliana na wanyamapori hao wakati wanapovamia vijiji.

" Kwa sasa kukutana na kundi la tembo zaidi ya 500 katika miji ya Butiama, Dodoma pamoja Morogoro ni jambo la kawaida, Hatuwezi kutegemea  KDU pekee lazima nguvu iongezwe" alisema Mhe.Kanyasu.

Amesema TFS ihakikishe inakuwa kikosi hicho cha Askari katika Hifadhi za Mazingira Asilia ambako kuna wanyamapori wakali ma waharibifu wakiwemo tembo na viboko, simba na chui.

Amesema kwa sasa Wizara ya Maliasili na Utalii imekuwa ikipokea maombi mengi kwa siku kutoka kwa wananchi walioathiriwa na wanyamapori wakali na waharibifu.

Katika hatua nyingine, Mhe.Kanyasu ametoa pole kwa wananchi wa Kijiji cha Rondo kufuatia kifo cha kumpoteza Mwalimu  wa shule ya msingi pekee katika kijiji hicho  aliyekufa baada ya  kuuliwa na tembo baada ya kumpiga picha tembo aliyekuwa akihangaika kumnasua mtoto wake aliyekuwa amenaswa kwenye kichaka.

Aidha, Mhe.Kanyasu amezitaka Halmashauri nchini zinazopakana na Hifadhi zihakikishe zinaajiri askari Wanyamapori watakaokuwa wakisaidia kutoa msaada wa haraka pindi wanyamapori hao wanapovamia vijiji

Pia, Amezitaka Halmashauri ziangalie uwezekano wa kuwatumia askari wanyamapori wa vijiji (VGS) kwa kuandaa utaratibu maalum wa kuwakabidhi silaha pindi wanyamapori wanapovamia mashamba na makazi ya wananchi.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Lindi, Shaibu Mgenda amesema kutokana na juhudi za uhifadhi unaofanywa na Mkoa huo umechangia wanyamapori kuongezeka na kuwa huru kutembea kila mahali

Kufuatia na hali hiyo, Mhe. amemuomba Naibu Waziri huyo ahakikishe  Taasisi zake za  Uhifadhi nchini zunatoa elimu kwa wananchi ili waweze kujihami wakati wanyamapori hao wanavamia mali na makazi yao.

Waziri Mpina Ashangazwa Na Uwepo Wa Chama Cha Wavuvi Ngazi Ya Taifa Bila Wizara Yake Kuwa Na Taarifa

$
0
0
Na. Edward Kondela
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina ameitaka Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini kukaa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi ili kupitia kwa pamoja taratibu za usajili wa Chama Kikuu cha Ushirika wa Wavuvi nchini (CHAKUWATA) ambao hautambuliki katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi ilhali kinafanya kazi na wavuvi.

Waziri Mpina amesema hayo  jana  (07.08.2019) katika Maonesho ya wakulima, wafugaji na wavuvi nchini (Nanenane) kwenye viwanja vya Nyakabindi katika Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu mara baada ya kutembelea banda la Wizara ya Kilimo na kukuta uwepo wa chama hicho CHAKUWATA na kushangazwa kwa kuwa kinajishughulisha na wavuvi bila Wizara ya Mifugo na Uvuvi yenye dhamana na wavuvi kufahamu uwepo wake ambapo hakuridhishwa na sababu zilizotolewa na Naibu Mrajis Uhamasishaji kutoka Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini Bw. Charles Malunde juu ya uhalali wa CHAKUWATA.

“Mpaka chama kinasajiliwa wizara haijui, lazima wizara ihusishwe katika hatua zote sasa kama katibu anayehusika na uvuvi hajui, mimi waziri sijui yaani hapa ndiyo tunashangaa kuna Chama Kikuu cha Ushirika wa Wavuvi Tanzania (CHAKUWATA). Sasa kwa sababu mmeshalifikisha hapa nia ya kuanzisha ushirika ni nzuri ibaki palepale lakini nyinyi (Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini) mkae muone namna bora kama kuna vitu havikufuatwa vikamilishwe kwa ukamilifu kwa sababu kuanzishwa huko bado hautuzuii kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza huko nyuma.” Amesema Waziri Mpina

Akitembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye maonesho hayo Waziri Mpina amesema ameridhishwa na umati wa watu unaofika katika banda hilo ili kupata elimu na kusema nia ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi ni kuwafikia wadau ili kutatua changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika sekta za mifugo na uvuvi.

“Tunataka tuwahakikishie zile changamoto ambazo wametuwasilishia hapa tunaenda kuzifanyia kazi ili kuhakikisha tunapokutana mwaka mwingine wa Maonesho ya Nanenane zitakuwa zimesharekebishwa ili mwaka unaofuata wawe mashahidi kwa kushuhudia mageuzi makubwa ambayo yatakuwa  yamefanyika.” Amefafanunua Waziri Mpina

Amefafanua kuwa baadhi ya changamoto kubwa ambazo amekutana nazo ni upungufu mkubwa wa chakula cha samaki na mifugo ambapo amesema anawahakikishia wadau katika sekta za mifugo na uvuvi katika kipindi kinachofuata Wizara ya Mifugo na Uvuvi itapanga mikakati madhubuti kuhakikisha changamoto hizo zinatatuliwa.

Kuhusu masoko ya bidhaa mbalimbali zinazotokana na mifugo ambazo amezishuhudia kwenye Maonesho ya Nanenane Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina amesema wizara itahakikisha wadau wake wanatafutiwa soko la uhakika ili waweze kuuza mazao yao pamoja na bidhaa zinazotokana na mazao ya mifugo.

Akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na watendaji wa taasisi zilizo chini ya wizara ambao wanashiriki katika Maonesho ya Nanenane kwenye viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu, Waziri Mpina amesema ameridhishwa na namna wananchi wanavyohudumiwa kwa kupatiwa elimu na ufahamu juu ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa kesho (08.08.2019) anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha maadhimisho ya Maonesho ya Nanenane kitaifa yanayofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi vilivyopo katika Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu.

Mwisho

Waziri Wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga Akagua Utekelezaji Wa Maagizo Ya Waziri Mkuu Kuhusu Ununuzi Wa Pamba Katika Wilaya Ya Bariadi, Itilima Na Maswa

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Simiyu
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) Leo tarehe 6 Agosti 2019 amefanya ziara ya kikazi mkoani Simiyu kukagua utekelezaji wa maagizo ya Waziri Mkuu aliyoyatoa hivi karibuni kwa wafanyabiashara kununua Pamba ya wakulima.

Mhe Hasunga ametembelea na kukagua Kituo cha ununuzi wa Pamba cha Itemelo kilichopo kata ya Dutwa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Kituo cha ununuzi cha Lugulu katika kata ya Lugulu Wilaya ya Itilima na Kituo cha Kumalija kilichopo katika kata ya Shanwa wilayani Maswa.

Katika ziara hiyo Mhe Waziri amejionea hali ya ununuzi wa Pamba ya wakulima ukiwa unaendelea kutokana na serikali hivi karibuni kupata muarobaini wa mustakabali wa zao hilo.

Waziri huyo wa Kilimo amepiga marufuku Pamba ya wakulima kupimwa katika mizani zisizofahamika badala yake lazima ipimwe katika mizani iliyothibitishwa na wakala wa vipimo.

Katika hatua nyingine pia Mhe Hasunga ametoa kalipio Kali kwa wanunuzi wa Pamba kadhalika vyama vya ushirika vinavyowakata kilo moja wakulima kwa madai ya mifuko ya kupimia badala yake ameagiza mkulima akatwe kutokana na uzito wa mfuko sio kukadiria kilo moja.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli imekusudia kuwanufaisha wakulima kupitia mazao wanayozalisha kwa kuwaongezea elimu ya Kilimo bora na chenye tija.

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga yupo mkoani Simiyu kwa ajili ya sherehe za wakulima (Nanenane) ambazo kilele chake ni tarehe 8 Agosti 2019 na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatarajiwa kuwa mgeni rasmi wakati wa kufunga maadhimisho hayo akimuwakilisha Rais wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli.

Wachimbaji wadogo wa dhahabu Watakiwa Kuzingatia Sheria za Mazingira

$
0
0
Na Lulu Mussa, GEITA
Wachimbaji wadogo wa dhahabu katika Kata ya Mugusu Mkoani Geita wametakiwa kufuata taratibu za hifadhi ya mazingira ili kunusuru afya zao na kuchukua tahadhari ya kukabiliana na uwezekano wa milipuko ya magonjwa.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima mara baada ya kufanya ziara ya kikazi kutembelea eneo la Mgusu, kuona uzingatiaji na utekelezaji wa Sheria ya Mazingira ya Mwaka 2004.

Akiwa katika eneo la Mugusu Naibu Waziri Sima amesema bado kuna tatizo la usafi wa mazingira katika maeneo wanayoyatumia kuchenjua dhahabu kwa kutumia zebaki, na kuna haja wachimbaji hao kukaa na halmashauri ya Geita Vijijini ili kuhakikisha wanakuwa na vyoo bora.

Akitoa kauli ya Serikali kuhusu mpango kazi wa Taifa wa kupunguza matumizi ya zebaki kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu katika shughuli za uchenjuaji, Sima amewataka wakazi wa Mgusu kuendelea na shughuli za uzalishaji wa dhahabu bila kuathiri sekta ya mazingira kwa kupunguza matumizi ya zebaki inayoharibu mazingira na afya za binadamu.

“Nimeona namna vijana wanavyojishughulisha kwa ajili ya kujipatia kipato, hili ni jambo jema kwenye Taifa letu, lakini nimetembea hadi chini kwenye ule mto wa Nyamasenge hakuna vyoo, watu wanatumia pori na mto kwa ajili ya haja ndogo na kubwa.

“Kwa mazingira yetu ni hatari sana, tunaweza kufanya kazi nzuri lakini ugonjwa utasitisha shughuli zetu. Nawasisitiza kuwa Usafi ni jambo la kwanza katika kufanya kazi, huwezi kuwa na nguvu isiyojali usafi,” alisema Sima.

Awali, Naibu Waziri Sima alitembelea chanzo cha maji cha maji cha Mto Mabubi na kujionea hali mbaya inayotishia kutoweka kwa chanzo hicho kutokana na shughuli za kibinadamu zinazoendelea kandokando ya eneo hilo.

“Chanzo cha maji cha mto Mabubi, hakitadumu na maji hayatakuwa salama kwa matumizi ya binadamu endapo kitaendelea kuingia kemikali ya zebaki nanyi wachimbaji kujisaidia katika eneo hilo” Sima alisisitiza.

Diwani wa Kata ya Mgusu Bw. Pastory Ruhusa amesema kuwa ataitisha mkutano wa wananchi mapema iwezekanavyo ili kuweka mikakati ya haraka kutokomeza hali hiyo ikiwa ni pamoja na usafi wa mazingira na kupunguza matumizi ya zebaki.

Naibu Waziri Sima yuko katika ziara ya kikazi Kanda ya Ziwa kukagua uzingatiaji na usimamizi wa Sheria ya Mazingira pamoja na uwaelimisha wananchi mpango wa Serikali wa kupunguza matumizi ya zebaki nchini.

Jeshi la Polisi Latoa ONYO Kwa Madereva Nchini

$
0
0
Jeshi la Polisi nchini limetoa ufafanuzi na kuweka msisitizo kwenye katazo alilotoa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es salaam tarehe 05/08/2019 kuhusu kupiga marufuku magari kufunga taa za vimulimuli au za rangi rangi, taa zenye mwanga mkali (spot light) na kufunga ving’ora kwenye magari ya kiraia au watu binafsi na pikipiki za kiraia.

Akitoa tamkoa hilo Msemaji wa Jeshi hilo SACP, David Misime amesema kuwa, katazo hilo ni kwa nchi nzima, kutokana na kujitokeza kwa baadhi ya watu walioamua kufunga vimulimuli na ving’ora na kuvitumia wawapo barabarani na kusababisha usumbufu kwa watumiaji wengine wa barabara.

Wamefunga vifaa hivyo kutaka kupewa kipaumbele wawapo barabarani kwa kujua au kwa kutofahamu kuwa ni kinyume na sheria, kanuni na taratibu zilizopo.

Na kwa mujibu wa sheria ya usalama barabarani sura ya 168 ya mwaka 1973 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002 kifungu cha 39 B (I) na (2) kinafafanua juu ya matumizi ya ishara ikiwepo ving’ora na vimulimuli.

Wakurugenzi Wakutana Kuboresha Mwongozo Wa Ukopaji Na Upokeaji Misaada

$
0
0
Na. Scola Malinga, WFM, Dar es Salaam
Serikali imejipanga upya kuongeza ufanisi wa kiutendaji kwa kupitia na kuboresha mwongozo wa ukopaji, utoaji wa dhamana na upokeaji misaada nchini.

 Hayo yamebainishwa jijini Dar es Saalam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na mipango, Bw. Doto James,wakati wa ufunguzi wa warsha ya wakurugenzi wa Sera na Mipango wa wizara mbalimbali iliyoangazia kujadili na kuweka mkakati wa mwongozo huo.

Bw. James alisema kuwa, chimbuko la Mwongozo huo ni changamoto ambazo Serikali imekuwa ikikabiliana nazo wakati wa kutekeleza miradi ya maendeleo hususan miradi inayotekelezwa kwa fedha za mikopo na misaada kutoka kwa wadau wa maendeleo.

“Kama Wizara ya Fedha na Mipango, tumeshuhudia uwepo wa maandalizi duni ya miradi,na pia miradi kuchukua muda mrefu kuanza kutekelezwa na hivyo kuigharimu Serikali muda na fedha", alieleza Bw. James.

Aidha, Katibu Mkuu huyo wa Wizara ya Fedha, alieleza kuwa eneo lingine ambalo limekuwa na changamoto katika utekelezaji wa miradi ni misamaha ya kodi. Katika kulifanyia kazi jambo hilo, Wizara ya Fedha na Mipango imeandaa taarifa na mapendekezo kuhusu namna ya kukabiliana na changamoto za masuala ya kodi ili miradi yote yenye changamoto za kodi itekelezwe ipasavyo kwa mujibu wa sheria na kanuni za nchi.

Bw. James, aliwasisitiza wakurugenzi hao kufanya majadiliano ya  rasimu ya Mwongozo na kutoa mapendekezo ambayo yatatumika katika kukamilisha Mwongozo huo ili uje kusaidia katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini.

Aidha, Mwenyekiti wa Warsha hiyo ambaye ni Katibu Mkuu Msaafu, Bw. Peniel Lyimo, aliwasisitiza wajumbe wa kamati hiyo kuendelea kusaidia usimamizi wa miradi ya serikali kwenye maeneo yao.

Bw. Lyimo aliwapongeza wajumbe wa mkutano kwa michango yao itakayowezesha kufanikisha kukamilika kwa mwongozo huo, ambapo utakapokamilia utasaidia katika kutekeleza na kusimamia miradi mbalimbali ya maendeleo na hivyo kuleta tija kwa wananchi.

Aidha Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi Amina Shaaban, alieleza kuwa, nchi ya Tanzania imeshuhudia kuongezeka kwa ukusanyaji wa mapato ya ndani katika miaka ya karibuni, hususan kuanzia mwaka 2016. Pamoja na kuongezeka kwa mapato, bado nakisi ya bajeti imekuwa ikiongezeka kutokana na Serikali kujikita katika kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo, ukiwemo mradi wa Umeme wa Maporomoko ya mto Rufiji, Reli ya Kisasa kwa kiwango cha Kimataifa (SGR), ujenzi na ukarabati wa madaraja na miundombinu mbalimbali.

Alisema ili kuziba pengo la nakisi, Serikali imekuwa ikiingia katika michakato mbalimbali ya madeni, dhamana na misaada kwa kutumia sheria ya Mikopo, Dhamana na Misaada, Suraya 134.

Bi. Amina Shaaban alibainisha kuwa, changamoto iliyojitokeza miaka ya hivi karibuni, ni kupungua kwa mikopo yenye masharti nafuu (concessional loans), hivyo Serikali imelazimika kuingia katika mikopo ya kibiashara (commercial loans).

Aidha, mikopo hiyo huambatana na masharti magumu na hivyo huhitaji umakini mkubwa (responsible borrowing) ili kuepuka kuingiza Taifa katika mikopo isiyolipika.

Alisema kuwa pamoja na michango wajumbe wa warsha hiyo katika kupitia na kuboresha rasimu ya mwongozo huo, Serikali imejipanga kuutekeleza mara utakapokamilika.

Mwalimu Atiwa Mbaroni Kwa Rushwa ya Laki Moja

$
0
0
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa Temeke, imemkamata Mwalimu Mkuu wa Shule ya Awali na Msingi Real Hope iliyopo Mbagala Majimatitu, Dar es Salaam, Ayubu Mtondo kwa kosa la  kuomba na kupokea rushwa.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Naibu Mkuu wa Takukuru, Ramadhani Ndwatah, alisema mwalimu huyo alipokea Sh 100,000 ili kumsaidia kumrudisha kazini mtumishi mmoja ambaye jina lake limehifadhiwa.

Ndwatah alisema Februari 28, mwaka huu, saa 11 jioni,  mwalimu huyo akiwa ofisini kwake, alipokea fedha za mtego ili aweze kumsaidia mtumishi wake aliyesimamishwa kazi kurudi kazini.

Alisema uchunguzi dhidi ya tuhuma hizo umekamilika na mtuhumiwa anatarajiwa kufikishwa mahakamani na kufunguliwa mashtaka kwa kosa la kushawishi kuomba na kupokea rushwa.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images