Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Mkuu: Tutumie Mwezi Wa Ramadhani Kwa Kudumisha Amani

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Watanzania watumie Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwa kudumisha amani na mshikamano na kuwaombea viongozi wa kitaifa.

“Mwezi huu tuna majukumu makubwa ya kufanya ibada, kutubu dhambi zetu na kuomba rehma kwa Mwenyezi Mungu pamoja na kudumisha mshikamano na kuwa wavumilivu.”

Waziri Mkuu alitoa wito huo jana jioni (Ijumaa, Mei 24, 2019) aliposhiriki hafla ya futari iliyoandaliwa na benki ya NMB iliyofanyika katika Hoteli ya Dodoma.

Alisema kila wananchi aendelee kuliombea Taifa lizidi kudumisha amani na mshikamano. “Tuhakikishe tunatenda matendo mema yenye kumpendeza Mwenyezi Mungu.”

Kadhalika, Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuipongeza benki ya NMB kwa huduma bora wanazozitoa kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kuwa na matawi mengi hadi vijijini.

Awali, Mkurugenzi wa benki ya NMB, Albert Jonkergouwalisema lengo la kuandaa hafla hiyo ya futari ni kuimarisha ushirikiano uliopo baina yao na wateja wao.

Mkurugenzi huyo alisema katika kipindi hiki Waislamu wanapaswa kumrudia Muumba wao na kumshukuru kwa mema yote anayowajalia waja wake.

“Mwezi wa Ramadhan ni kipindi muafaka cha kufuturu pamoja hivyo, nawashukuru wateja wetu kwa kujumuika nasi nawaomba muendelee kutumia huduma zetu.”

Alisema mkusanyiko huo unadhihirisha kuwa wao ni sehemu ya jamii ya Watanzania wote, hivyo aliwasisitiza wateja wa benki hiyo waendelee kutumia zaidi huduma za kidijitali.

Hafla hiyo ilihudhuliwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai, Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson, Mashekhe wa Mikoa ya Kanda ya Kati (Dodoma, Singida na Manyara).

Wengine ni Wazee wa Dodoma, Waheshimiwa Wabunge , Viongozi wa dini, wananchi, Wawakilishi wa Taasisi mbalimbali na Wafanyakazi wa NMB.

Tanzania Yashiriki Kongamano La Matumizi Endelevu Ya Rasilimali Za Bahari Nchini Msumbiji.

$
0
0
Na Edward Kondela
Nchi zinazopakana na Bahari ya Hindi zikiwemo Tanzania, Kenya, Msumbiji na Afrika ya Kusini na Visiwa vya Ushelisheli zimepewa rai ya kuhakikisha zinafanya kila njia kulinda rasilimali za pamoja hususan zinazopakana na bahari ili ziweze kusaidia kukuza uchumi wa nchi hizo.

Rai hiyo imetolewa (24.05.2019) na Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Jacinto Nyusi wakati wa ufunguzi wa kongamano la kujadili matumizi endelevu ya rasilimali za bahari linaloendelea katika mji wa Maputo nchini humo.

Rais Nyusi amesema kongamano hilo la siku mbili lina umuhimu mkubwa kwa kuwa linafanyika wakati huu ambapo uvunaji holela na usiofuata utaratibu wa rasilimali za bahari umeshamiri katika nchi nyingi za bara la Afrika na Asia.

Akihutubia washiriki wa Kongamano hilo, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega ameelezea hatua mbalimbali ambazo nchi ya Tanzania imepiga katika kuhakikisha malengo ya milenia kuhusu uhifadhi na matumizi endelevu ya rasilimali za asili yanafikiwa.

Mhe. Ulega amezitaja hatua hizo kuwa ni pamoja na kupambana na uvuvi haramu na biashara haramu ya utoroshwaji wa mazao ya uvuvi, kudhibiti uvuvi wa mabomu katika pwani ya Bahari ya Hindi, kutekeleza miradi ya kuhifadhi mazingira ya bahari kwa lengo la kuinua maisha ya jamii za wavuvi, kulinda maeneo tengefu ya bahari, kufanya utafiti na kuzuia uharibifu wa bahari unaotokana na matumizi ya bidhaa za plastiki.

Aidha, Mhe. Ulega amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na nchi za ukanda wa Bahari ya Hindi kuhakikisha rasilimali zilizopo zinalindwa na zinazinufaisha nchi wanachama.

Pamoja na mambo mengine mkutano huo umeangazia mchango wa sekta zingine ambazo kwa pamoja zinachochea ukuaji wa uchumi wa bluu ambao unahimiza matumizi ya bahari katika kukuza uchumi wa nchi.

Sekta hizo ni pamoja na usafirishaji, utalii wa bahari, uhifadhi wa mazingira, utafutaji na uchimbaji wa gesi, pamoja na usalama wa chakula na ajira.

Kwa pamoja washiriki wa kongamano hilo wamekubaliana katika kuimarisha ushirikiano, kuendelea kubadilishana uzoefu na kwamba juhudi za pamoja zinahitajika ili kulinda rasilimali za bahari kwa kuwa baadhi ya rasilimali hizo hazina mipaka kama ilivyo kwa samaki aina ya jodari ambao huhama kutoka nchi moja kwenda nchi nyingine.

Kongamano hilo limeandaliwa na nchi ya Msumbiji kwa kushirikiana na Norway pamoja na mashirika mbalimbali ikiwemo Benki ya Dunia, ambapo zaidi ya washiriki 300 kutoka sehemu mbalimbali duniani wakiwemo wataalam wa sayansi za bahari, mazingira, usafirishaji majini, viongozi wa
kisiasa, wakuu wa mashirika ya fedha na mashirika binafsi yanayojihusisha na uhifadhi wa rasilimali za bahari wanahudhuria kongamano hilo.

Tanzania, imewakilishwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega na wengine ni Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Mmanga Mjengo Mjawiri, Mkurugenzi wa Uvuvi Zanzibar Mussa Aboud Jumbe na maofisa kutoka Mamlaka ya Bahari Kuu nchini.

Maelfu ya Wananchi waAfrika Kusini Walipuka Kwa Shangwe Baada ya Rais Magufuli Kuingia Uwanjani

$
0
0
Umati mkubwa wa wananchi umelipuka kwa shangwe na chereko wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipowasili  katika uwanja wa michezo wa Loftus Versfeld jijini Pretoria kuhudhuria sherehe za kuaishwa kwa Rais wa Afrika ya Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa leo Jumamosi Mei 25, 2019

Makampuni Matatu Yatakayosafirisha Mashabiki Wa Soka Kulekea Misri Na Taifa Stars Yatangazwa

$
0
0
SERIKALI kwa kushirikiana na Shirikisho la Soka Nchini (TFF) imeyataja Makampuni matatu yatakayotumika kusafirisha Mashabiki wa Soka na Watanzania kwa ajili ya kuishangilia Timu ya Soka ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ wakati wa Michuano ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) zitakazofanyika Mwezi Juni, mwaka huu nchini Misri.

Akizungumza na Waandishi wa Vyombo ya Habari leo Jumamosi (Mei 25, 2019), Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo, Yusuph Singo aliyataja Makampuni hayo kuwa ni pamoja na Clouds Entertainment Group Ltd, Travel Link na World Link, ambayo yalishinda mchakato wa ushindani na makampuni mengine kutokana na kukidhi vigezo mbalimbali vilivyoanishwa.

Kwa mujibu wa Singo alisema Serikali na kwa kushirikiana na Shirikisho la Soka Nchini (TFF) waliamua kusimamia mchakato wa kupata makampuni hayo ili kuzuia aina yoyote ya utapeli kwa Watanzania hususani Mashabiki wa Soka wa hapa nchini watakaojitokeza kwenda Nchini Misri kuipa nguvu ya ushingiliaji Taifa Stars.

“Katika miaka ya nyuma kulikuwa na utapeli katika haya makampuni ya usafirishaji, hivyo Serikali kwa kushirikiana na TFF tumeyapata Makampuni matatu, bei zao zitakuwa rahisi na wamepanga kuwa na nembo ya pamoja ambayo wataitangaza ili iweze kujulikana na Watanzania” alisema Singo.

Aidha Singo alisema kuhusu utaratibu wa visa za kusafiri makampuni hayo kwa kushirikana na TFF yatatoa taarifa ya jinsi Mashabiki wa Soka watavyoweza kupata huduma hiyo kabla ya kuanza kwa michuano hiyo inayotarajia kuanza kutimua vumbi tarehe 21 Juni mwaka huu.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Kampuni ya Clouds Entertainment Group Ltd, Shaffih Dauda alisema Kampuni yao imejipanga vyema kuhakikisha kuwa inatoa huduma zote muhimu kwa Watanzania watakaosafiri kwenda Nchini Misiri kuishangalia Taifa Stars ikiwemo visa, usafiri wa ndani, malazi katika kipindi cha siku 10 za mechi tatu za makundi itayocheza Taifa Stars.

“Clouds Entertainment Ltd kila mwaka tuna msimu wa kulevya wa soka, mwaka jana tulikuwa na  Msimu wa kulevya wa Kombe la Dunia kule nchini Urusi, na sasa tunarudi Afrika na tutawahudumia vyema mashabiki watakaojitokeza kwa kiasi cha Dola za Kimarekani 1650 na pia tutaoa ofa ya Mashabiki hao kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo nchini Misri” alisema Dauda.

Aliongeza kuwa katika kutoa urahisi wa huduma kwa Watanzania hususani suala la malazi, Kampuni yao tayari kwa kushirikiana na wakala wao aliyopo nchini Misri, wamepata mmoja wa Mitaa maarufu nchini Misri ujulikanao Kilimanjaro ambapo utawezesha Mashabiki wa Watanzania kupata huduma zote muhimu kuwafanya Mashabiki hao huko kujiona kuwa wapo nyumbani.

Kwa upande wake, Meneja Maendeleo ya Masoko wa Kampuni ya World Link, Zaki Admani alisema kampuni hiyo itatoza kiasi cha Dola za Kimarekani 1550 kwa Mashabiki wa Soka, ambayo watasafiri kuelekea Nchini Misri pamoja na kutoa ofa ya kuchagua mechi moja yoyote ambayo mshabiki wa Soka atapenda kuingalia katika timu zitakazochuana na Taifa Stars.

Aliongeza kuwa kuanzia Jumatatu ya wiki ijayo Kampuni hiyo itatoa kifurushi kitakachomwezesha Shabiki wa Soka hapa nchini kuweza kuchagua idadi ya mechi ambazo atapenda kuziangalia wakati akiwa na Timu ya Taifa Stars nchini Misri.

“Wapo wengine watapenda kuangalia mechi moja, na hili tumeliangalia na mapema wiki ijayo kuanzia jumatatu tutatoa utaratibu wake wa namna ya kuwasaidia mashabiki wa aina hii” alisema Admani.

Naye Meneja Utawala wa Kampuni ya Travel Link, Ephrem Mtuya alisema kuwa kwa miaka 15 sasa Kampuni hiyo imekuwa ikifanya kazi pamoja na TFF kwa ajili ya kuwasifirisha wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania katika nchini mbalimbali na hivyo amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi kusafiri na Kampuni hiyo ili kwenda kuipa nguvu Timu ya Taifa ya Tanzania ikiwa nchini Misri.

Alisema Kampuni imeweka kiwango cha Dola za Kimarekani 1300 pekee kwa Mtanzania yotote atayapenda kusafiri na Timu hiyo hususani Mashabiki wa Soka ikihusisha Gharama za Tiketi ya Ndege, usafiri, pamoja na huduma za malazi.

Marekani yatishia kuiwekea vikwazo Uturuki kuhusiana na makombora ya Urusi

$
0
0
Marekani imetishia kuiwekea vikwazo Uturuki endapo haitoacha kununua mfumo wa ulinzi wa makombora wa S-400 kutoka Urusi.

 Uturuki inakusudia kulilinda anga lake kwa kutumia mfumo huo wa ulinzi uliotengenezwa Urusi, lakini maafisa mjini Washington wanaitaka Uturuki ambayo ni mshirika wake katika ya Jumuiya ya kujihami NATO kununua mfumo kama huo wa ulinzi uliotengenezwa Marekani. 

Kwa mujibu wa kituo cha utangazaji cha CNBC, serikali ya Marekani imeipatia Uturuki muda wa wiki mbili kuachana na mfumo kutoka Urusi la sivyo itakabiliwa na vikwazo ikiwa ni pamoja na kuacha kuiuzia ndege za kivita za F-35. 

Hata hivyo mapema wiki hii waziri wa ulinzi wa Uturuki Hulusi Akar alisema vikosi vyake tayari vinapokea mafunzo ya kutumia mfumo wa S-400 nchini Urusi na kuwa mfumo huo ulitarajiwa kuwasili nchini Uturuki mwezi Juni au Julai.

Dc Wa Ruangwa Awapiga Stop Mangariba Na Waganga Wa Jadi Wasio Na Vitambulisho Vya Wajasiriamali.

$
0
0
Na Bakari Chijumba, Lindi.
Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi, Hashim Mgandilwa amepiga marufuku wamiliki wa viwanja vya kucheza unyago kutumia Mangariba wasio na vitambulisho vya wajasiriamali wadogo.

Amesema hayo 23 Mei 2019, wakati wa kikao cha mangariba(Wanaotahiri watoto), waganga wajadi na wamiliki wa viwanja vya kuchezea unyago kilichofanyika ukumbi wa CCM Ruangwa mjini.

Mgandilwa amemtaka kila waganga wa jadi kuwa na kitambulisho cha mjasiriamali mdogo kama anataka kuendelea kutoa tiba katika Wilaya ya Ruangwa.

Mkuu huyo wa wilaya amesema wamiliki wa viwanja vya unyago wanapaswa kuzingatia ratiba ya kufunga na kufungua shule ili mtoto anafanyiwa unyago asikose haki ya kupata elimu.

"Msitafute shida,Halmashauri ikianza kutoa vibali vya sherehe hizo nitafuatilia kama umepokea watoto siku husika ya tarehe 8 mwezi wa 6 na kumaliza tarehe 6 mwezi wa  7 ikifika tarehe ya mwisho  watoto wote wawe wametoka Jando" amesema Mgandilwa.

Aidha Mgandilwa amewataka wazazi na wahusika wa shughuli za unyago, kuhakikisha watoto wanapokuwa jandoni wanalazwa kwenye vyandarua ili kuepusha maradhi na pia amesisitiza umuhimu kuzingatia usafi wa  maeneo ya viwanja vya unyago.

"Mnapofanya shughuli hizi zingatieni msingi ya afya kila mwenye kiwanja awe na uhakika na daktari ni vyema tukaangalia usalama wa watoto wetu" amesema  Mgandilwa

Mgandilwa amewataka pia wanaohusika  na shughulia za jando, kuzingatia  mafunzo  wanayotoa kwenye jando na unyago  yaendane na maadili ya kitanzania na umri wa watoto wanaopewa hayo mafunzo.

Bei ya Viwanja Imeshuka: Bunju na Mapinga (Baobab sec)

$
0
0
Bei ya Viwanja Imeshuka: Bunju na Mapinga (Baobab sec)

Tumeshusha sana bei za viwanja vilivyobaki ili kufunga mradi huu wa Viwanja kwa Bunju na Mapinga kama ifuatavyo:

Kwa Mapinga bei ya kiwanja cha sqm 2000 ilikuwa tsh 26 milion sasa imeshuka mpaka tsh 23 milion; bei ya kiwanja cha sqm 2400 ilikuwa tsh 31 milion sasa imeshuka mpaka tsh 27 milion.

Umbali kutoka main road (Dar to Bagamoyo Road) ni km 2 tu, huduma za maji na umeme zipo. Viwanja viko flat na access roads zake zinapitika vizuri hata kama mvua imenyesha mwezi mzima mfululizo.

Kwa Bunju Kipo kiwanja cha sqm 1750, bei yake ni tsh 50 milion tu. kipo main road ya Dar to Bagamoyo.

Wahi uone viwanja hivi na ulipie tufunge mradi huu.
Namba za mmiliki ni 0758 603077 au whatsap 0757489709

Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Unaotokana Na Kisukari (Diabetic Nephropathy)

$
0
0
Ugonjwa wa kisukari (Diabetes Mellitus) huambatana na ongezeko la sukari(glucose) katika damu kwa kiwango kinachozidi kawaida. 

Homoni aina ya insulin ambayo hutolewa na kongosho ama hushindwa kufanya kazi yake vema kwa sababu ya kasoro za seli au hutolewa kwa kiasi kisicho kidhi uhitaji wa kuratibu sukari katika damu. 

Kwa hivyo sukari hubaki katika damu kwa wingi na kuleta madhara kadhaa.Wagonjwa wa kisukari pia huweza kuwa na kiwango kikubwa cha lehemu (cholesterol) katika damu. Na zaidi huweza kuwa na tatizo la mgandamizo wa damu (hypertension) au presha. Asilimia 55 ya wanaume wenye kisukari hupatwa na tatizo la nguvu za kiume.

Mambo haya matatu, Sukari, lehemu (Cholesterol) na Mgandamizo wa damu, Huweza kusababisha upungufu wa nguvu za kiume.(Erection dysfunction).

1. Sukari.
Sukari nyingi katika damu huweza kupelekea kuharibiwa kwa kuta za mishipa ya damu. Kisha kuta hizi hushindwa kuzalisha homoni aina ya Nitrogen Oxide ambayo husaidia kutanua mirija ya damu kwa ajili ya kupitisha damu kwa ufasaha. Ikitokea katika mirija ya damu inayotiririsha katika uume kushindwa kutanuka vema, ni wazi kuwa uume utapungua uimara wake.

2. Lehemu (Cholesterol).
Lehemu huganda kwenye kuta za mirija ya damu mithiri ya mafuta yanavyoganda katika chupa. Hali hii hupelekea kupungua kipenyo (diameter) cha mirija ya damu na kushindwa kupitisha damu vizuri.

3. Mgandamizo wa damu au Presha (Hypertension).
Katika hali hii moyo hushindwa kusukuma damu vizuri na hivyo kupungua kwa kasi na ujazo wa damu katika maeneo yaliopo mbali na moyo, ikiwa ni pamoja na viungo vya uzazi.

Pia, Mishipa ya fahamu (nerves) au Neva za fahamu huweza kuharibiwa na kupunguza ufanisi wake.Katika hali hii, maeneo yanayohudumiwa na neva hizo hupungua hisia na wakati mwengine kupata ganzi ya kudumu. Uume pia huweza kuathiriwa kwa namna hiyo.

 Kumbuka
Ili  mgonjwa  wa  kisukari  aweze  kupata  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, ni  lazima   apate  pia  tiba   itakayo  saidia  ku- control  sukari  kwenye  damu   yake.

Hivyo  basi ,  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  inatakiwa  kwenda   sanjari  na  tiba  ya  ku - control  sukari  kwenye  damu  ya  mgonjwa.

Hii  ina  maana  kuwa,   ili  tiba  ya  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  iweze  kufanya  kazi  barabara, ni  lazima  mgonjwa  huyo, pamoja  na   kutumia  tiba  ya  nguvu  za  kiume , apate  pia  tiba  ya  sukari.


Kama unatatizo la Kisukari, lililosababisha upungukiwe nguvu za kiume basi wasiliana nami kwa ushauri zaidi. Simu:   0757996194 au 0717339771

PICHA: Zijue Alama za barabarani pamoja na matumizi yake

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521

Tuhuma 13 Za Mkurugenzi Ileje Kuchunguzwa

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. (Mst) Nicodemus Mwangela ameunda timu ya kuchunguza tuhuma 13 zilizo elekezwa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ileje na kuelekeza kuwa timu hiyo ifanye uchunguzi huo kwa haraka.

Brig. Jen. (Mst) Mwangela amefikia uamuzi huo mara baada ya majadiliano ya kikao cha pamoja na madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje waliomuandikia barua wakiwasilisha tuhuma za kutoridhishwa na utendaji wa Mkurugenzi huyo.

“Nimefanya ziara Wilaya ya Ileje baada ya kupata barua kutoka kwa Madiwani wakimtuhumu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ileje, kabla ya kufanya maamuzi tumejadiliana na nimefikia uamuzi wa kuunda tume ambayo itachunguza tuhuma zote 13 walizowasilisha”, ameeleza Brig. Jen. (Mst) Mwangela.

Amesema kazi kubwa ya tume hiyo ni kuhakikisha wanapata ukweli na uhalisia juu ya tuhuma hizo huku akielezea kuwa moja ya tuhuma ni udhaifu katika kukusanya mapato.

“Kuna tuhuma ambazo tunaona zina ukweli mfano Ileje haijafanya vema katika suala la ukusanyaji wa mapato, sasa tumebakiza mwezi mmoja mwaka wa fedha uishe lakini wamefikia asilimia 58 tu ya makusanyo ambapo ni asilimia ndogo ikiwa lengo ni angalau zaidi ya asilimia 80 kwahiyo hapo kuna dalili za uvujishaji wa mapato”, amefafanua Brig. Jen. (Mst) Mwangela

Brig. Jen. (Mst) Mwangela ameongeza kuwa licha ya kwamba uchunguzi unaendelea ametoa maelekezo na mikakati ambayo itasaidia kuhakikisha kazi ya ukusanyaji wa mapato inaendelea vizuri.

“Lengo ni kukusanya vizuri kwahiyo katika kikao tumeweka mikakati itakayosaidia kukusanya mapato na tuna amini waendaji wote wa halmashauri ya Wilaya ya Ileje watafanya kazi kwa umakini mkubwa huku kamati ya fedha na mipango ya madiwani itasimamia hilo vema”, amesema Brig. Jen. (Mst) Mwangela.

 Baadhi ya tuhuma ambazo Madiwani wamezielekeza kwa Mkurugenzi wa halmashauri ni pamoja na matumizi mabaya ya ofisi na tuhuma katika masuala ya nidhamu

 

Nyongo ashuhudia Jiwe la Almasi la Uzito wa “Ct” 512.15 likiuzwa kwa Bilion 3, 262, 149, 332

$
0
0
Na: Issa Mtuwa (Wizara ya Madini) – Shinyanga
Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo, ameshuhudia mchimbaji mdogo wa madini ya almasi bwana Joseph akijizolea fedha, dola za kimarekani (USD) milioni 1, 418,510.82 ambazo sawa na Tsh. bilioni 3, 262,149,332.75 kutokana na mauzo ya jiwe moja lenye  uzito wa Kareti  (ct)512.15.

 Shuguli ya mauzo ya Almas hiyo  imefanyika leo tarehe 25/05/2019 katika soko la Madini la mkoa wa Shinyanga na kushuhudiwa pia na Kamishna wa Tume ya Madini Prof. Mruma na vyombo mbalimbali vya usalama na wawakilishi wa benki ya CRDB Shinyangai.   

Akiongea wakati wa kushuhudia mauzo hayo , Naibu waziri Nyongo amesema, kutokana na mauzo hayo serikali  itapata USD 103,551.29 sawa na Tsh. milioni 238,136,901.61. Ameongeza na kusisitiza kuwa, adhima ya serikali ya awamu ya tano ni kuwezesha shuguli za wachimbaji wadogo na wadau wote  wa sekta ya madini kufanyika kwa utaratibu unao eleweka kwa faida yao na ya serikali. 

“Nimpongeze bwana Joseph ambae anauza almasi yake hapa leo kwenye soko hili la madini, kila kitu kinakuwa wazi mbele ya serikali, polisi, watu wa usalama na wawakilishi wa Bank ya CRDB, bila usumbufu wowote, na hiki ndicho tunachokitaka sisi kama serikali, wachimbaji wote kufuata utaratibu tuliouweka. 

Niwaombe wachimbaji kwa mara nyingine, acheni kuuza madini mchochoroni haita wasaidia zaidi ni kuhatarisha usalama wenu, na pengine hata kupunjwa kutokana na kuto kujua thamani halisi na bei ya madini yenu igeni mfano wa bwana Joseph, na niwaambie ukweli ukikamatwa unauza madini nje ya soko madini hayo yanataifishwa, hivyo utakuwa umekula hasara na utachukuliwa hatua za kisheria.” amesema Nyongo 

Kwa upande wake Afisa msaminishaji madini kutoka tume ya Madini Bi. Dorcas Moshi, Mchambuzi na Mthamini wa Madini ya Vito na Almasi kutoka tume ya Madini aliekuwa anafanya shuguli nzima ya uthaminishaji wa Almasi hiyo, amefafanua kuwa fedha iliyopata serikali, Milioni 238,136,901.61 inajumuisha Mrabaha wa  USD 85,110.65 sawa na  Tsh.

 Milioni 195,728,959.97, Ada ya ukaguzi ni USD 14,185.11 sawa na Tshs. 32, 621, 493, .33 na Mrabaha wa Halmashauri ya wilaya ya Kishapu ilikotokea Almasi hiyo (Service Levy) ni USD 4,255.53 sawa na Tsh. 9, 786,448. 

Kwa upande wake Kamishina wa Madini prof. Mruma amewasisitiza wachimbaji wadogo kuzingatia sheria na taratibu hususani kuchimba kihalali kwa kuhakikisha wanakuwa na leseni za uchimbaji na kulipa tozo zote za serikali kwani serikali ipo kwa ajili yao hivyo hawana sababu ya kuikwepa. 

Kwa upande wake bwana Joseph mmiliki wa almasi hiyo, ameishukuru Wizara ya madini na Tume ya madini kwa utaratibu waliouweka katika kutoa muongozo na usimamizi wa namna ya mauzo ya madini unavyotakiwa kufanyika, ulinzi wa madini yao pindi wanapoyapata na ametoa wito kwa wachimbaji wadogo wenzake kuwa hakuna sababu ya kuyakimbia masoko yaliyoanzishwa na serikali kwani yanafaida nyingi ikiwemo usalama, ulinzi, uwazi na utambuzi wa thamani halisi ya madini kitu ambacho nadra sana kwenye masoko yasiyo rasmi.  
 

Namba Za Simu Kuhusu Katazo La Mifuko Ya Plastiki

$
0
0
Kufuatia Katazo la Matumizi ya Mifuko ya Plastiki kuanzia tarehe 1Juni 2019, Ofisi ya Makamu wa Rais imeandaa namba maalumu za simu kwa ajili ya wananchi kuuliza maswali na kutoa maoni, ushauri ama taarifa yoyote.

Mwananchi hataingia gharama kupiga simu katika namba hizi ambazo zinapatikana masaa 24, ukiwa na swali, maoni, ushauri ama taarifa yoyote usisite kuwasiliana nasi au kutuma ujumbe mfupi (SMS) au Ujumbe wa Whatsapp kwa namba zifuatazo:

KUPIGA BILA MALIPO                    SMS/WHATSAPP
(0800 110 115)                          +255 737 796 253
(0800 110 116)                         +255 737 796 252
(0800 110 117)                         +255 737 796 249
(0800 110 118)                         +255 737 796 250
(0800 110 119)                         +255 737 796 251

•    Namba hizi zitaanza kutumika rasmi siku ya Jumatatu 27/05/2019

IMETOLEWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
25 MEI 2019

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili May 26

Masoko Mapya ya Madini Yaingiza Bilioni 34.3 Kwa Mwezi Mmoja

$
0
0
Na Frank Mvungi- MAELEZO
Dhahabu ya Bilioni 34.3 imeuzwa katika Kipindi cha mwezi mmoja kupitia katika masoko 21 yaliyoanzishwa kwa ajili ya kuuza madini katika mikoa mbalimbali hapa nchini.
 
Akizungumza katika mahojiano maalum na idara ya habari MAELEZO, Bungeni Jijini Dodoma Waziri wa Madini Mhe. Dotto Biteko amesema kuwa kuanzishwa kwa masoko hayo kumekuwa chachu ya kuongeza mchango wa sekta ya madini katika kukuza uchumi na pato la Taifa kwa ujumla.
 
“ Katika kipindi cha mwezi mmoja tu yaani Machi 17 mpaka Aprili 17 mwaka huu,jumla ya kilo 409.3 za dhahabu pekee zenye thamani ya shiilingi bilioni 34.3 imeuzwa kupitia katika maduka yaliyoanzishwa katika mikoa mbalimbali” Alisisitiza Biteko.
 
“Katika kilo hizo,Mkoa wa Geita umeongoza kwa kufanya biashara ya jumla ya kilo 289,Kahama kilo 44,Mara kilo 13,lakini cha kufurahisha zaidi ni kwa Wilaya ya Chunya ambako jumla ya kilo 52 zimeuzwa katika soko hilo zikiwa nia siku chache toka kufunguliwa kwake ,”,aliongeza, mheshimiwa Biteko.
 
Aidha mheshimiwa Biteko, katika mahojiano hayo maalum,ameeleza kuridhishwa na biashara inayofanyika katika maduka hayo ya madini kote nchini na kueleza kuwa licha ya mafanikio hayo yaliyofikiwa katika kipindi kifupi,serikali inashughulikia changamoto ndogondogo ikiwemo wafanyakazi,mashine za XRF na idadi ya watoa vibali.
 
Akifafanua amesema kuwa dhamira ya Serikali ni kuona sekta hiyo inatoa mchango stahiki katika kujenga uchumi na kuchangia maendeleo hapa nchini ndio sababu mkazo umewekwa katika kusimamia sekta hii.
 
Pia aliwataka wachimbaji wadogo na madalali wa madini kuhakikisha kuwa wanatumia masoko hayo kikamilifu na kujiepusha na vitendo vyovyote vinavyoweza kusababisha kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kufutiwa leseni jambo alilosema serikali haipendi,
 
Akizungumzia mikakati ya kusimamia sekta hiyo Mhe. Biteko amesema kuwa ni pamoja na kushirikisha wachimbaji wadogo katika kuhakikisha kuwa vitendo vya utoroshaji wa madini unakomeshwa ili kulinda mapato ya Serikali.
 
Aliongeza kuwa hatua nyingine ni usimamizi wa karibu katika maeneo yote ya uzalishaji wa madini ya aina mbalimbali na kuchukua hatua za kutatua changamoto mbalimbali katika sekta hiyo.

Katika mwaka wa fedha 2019/2020 Waziri Biteko amebainisha kuwa masoko mengine 7 yanatarajiwa kufunguliwa.
 
Baadhi ya Mikoa ambayo imeshafungua masoko ya kuuza madini ni pamoja na Geita, Dodoma, Mwanza, Tabora, Shinyanga, Morogoro, Mbeya, ambapo tayari mikoa 21 imeshafungua maduka hayo hadi sasa ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli alilolitoa kwa wakuu wa mikoa wote hapa nchini.

Dkt. Bashiru: Uwezo Wa Kuhifadhi Vitabu Vitakatifu Uwe Chachu Ya Ubunifu Katika Nyanja Ya Sayansi Na Teknolojia

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi- CCM Dkt. Bashiru Ally, amewataka watanzania kutumia  uwezo wa kuhifadhi Vitabu vitakatifu kuongeza ubunifu katika nyanja ya Sayansi na Teknolojia na nyingine ili kuendeleza jamii kwa kuipatia maendeleo stahiki.
 
Dkt. Bashiru ametoa wito huo katika Kata ya Pahi wilayani Kondoa mkoani Dodoma, wakati wa mashindano ya kuhifadhi Qur'an yaliyowashirikisha wadau kutoka maeneo mbalimbali nchini. 
 
Alisema kuwa kuna umuhimu mkubwa katika kuwekeza kwenye elimu kwa watoto, kwa kuwa watoto wakisoma si tu wanajengewa maarifa lakini pia wanaunganishwa na hivyo kuwa chachu ya kuweza kuisaidia jamii inayowazunguka. 
 
Mratibu na Mwandaaji wa mashindano hayo, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa, Dkt. Ashatu Kijaji, amesema kuwa lengo la mashindano hayo ya kuibua vipaji vya watoto vya kusoma Kitabu Kitukufu cha Qur'an na kuwajengea vijana uwezo wa kuwa na ujasili katika kueleza wanayo yaamini yakiwemo mambo mazuri ambayo yanafanywa na Serikali. 
 
Pause: Dkt. Ashatu Kijaji-Naibu Waziri wa Fedha na Mipango
Kwa upande wake Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson, alisema kuwa kazi zinazofanywa na Dkt. Ashatu Kijaji, ni zakupigiwa mfano hasa kwa wanawake na akawataka wazazi katika Wilaya ya Kondoa kumuunga mkono kwa kushiriki kikamilifu katika mikakati ya kuinua elimu katika eneo hilo, kwa kuhakikisha wanawapeleka watoto katika makambi yaliyo na lengo la kuongeza ufaulu wa wanafunzi.
 
Mgeni Rasmi katika Mashindano hayo, Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,  Mustapher Shabaan, amewapongeza vijana walioshiriki mashindano hayo na kuonesha umahili mkubwa wa kuhifadhi Qur'an na kuwataka waumini wa kiislamu kusoma na kukielewa kitabu hicho kitukufu kwa kuwa kimejaa elimu na maarifa mengi yatakayo wasaidia kuenenda vyema katika jamii na kupata thawabu kutoka kwa Mungu.
 
Mwisho

Vijana Wawili Wa Tanzania Bara Na Zanzibar Waibuka Kidedea Tuzo Ya Kimataifa Ya Kuhifadhi Quran

$
0
0
VIJANA wawili wa Kitanzania, Zakaria Sheha Ally na Shamsi Mwalimu Said wamechukua nafasi ya kwanza na ya tatu kwenye fainali za 27 za tuzo ya kimataifa ya kuhifadhi Quran tukufu.

Zakaria Sheha Ally (16) kutoka Tanzania Bara na Shamsi Mwalimu Said (19) kutoka Zanzibar wameibuka na kitita cha dola za Marekani 5,000 na dola 3,000 kila mmoja baada ya kuwashinda wenzao nane waliofanikiwa kuingia fainali hizo ambao walitoka Afrika Kusini, Sudan, Malaysia, Uturuki, Yemen, Kenya, Burundi na Uingereza.

Nafasi ya pili imechukuliwa na kijana Gaffari Mohammed (14) kutoka Uingereza ambaye ameibuka na kitita cha dola za Marekani 4,000. Mashindano hayo yaliyoandaliwa na Jumuiya ya Kuhifadhisha Quran Tanzania, mwaka huu yalishirikisha vijana 10 kutoka nchi 10 duniani.

Tuzo hizo zimetolewa leo (Jumapili, Mei 26, 2019) wakati wa kilele cha mashindano ya 27 ya Kimataifa ya Kuhifadhi na Kusoma Qur’an tukufu na utoaji tuzo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na mamia ya waumini wa Kiislamu waliofurika kushuhudia kilele cha Tuzo ya Kimataifa ya Quran iliyoandaliwa na Jumuiya ya Kuhifadhisha Quran nchini, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuhifadhisha Quran kunapaswa kuwa msingi imara katika kujenga jamii bora.

“Tuendelee kuhimiza suala la malezi bora ya vijana wetu kwa lengo la kuwafanya wawe raia wema, wakweli, wazalendo na wenye manufaa kwa nchi yao. Quran inatusisitizia sana kuhusu suala la uadilifu. Kwa mfano, katika Quran 9:119, Mwenyezi Mungu Mtukufu anatukumbusha waumini kumuogopa Mungu na kuambatana na wale walio wakweli wa maneno na vitendo,” amesema Waziri Mkuu.

Amewataka wazazi wa Kiislamu wahakikishe wanawasimamia vema watoto wao na kuwahifadhisha Quran badala ya kutoa msukumo pekee kwenye elimu ya kimazingira. “Sote ni mashahidi kwamba vijana wetu wanao uwezo wa kuhifadhi Quran na wakati huohuo wakasoma na kuhitimu fani mbalimbali katika elimu ya mazingira.”

“Tukumbuke kwamba mafanikio ya duniani na akhera hayapatikani kwingine isipokuwa ni kupitia Quran. Hivyo basi, tuwafunze Quran vijana wetu ili waweze kukabiliana na changamoto nyingi zinazoibuka kwenye ulimwengu wa sasa hususan suala zima la mmomonyoko mkubwa wa maadili,” amesisitiza.

Amesema njia mojawapo ya kuwasaidia vijana kukabiliana na hali ya sasa ya dunia ya utandawazi ni kuwasomesha na kuwahifadhisha Quran. “Vijana waliosoma na kuihifadhi Quran ni vigumu kuenenda kinyume na maadili kwani Quran ndiyo njia pekee ya kuwachunga na kuwafanya waonyeke dhidi ya vitendo vinavyokwenda kinyume na uadilifu.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameipongeza Jumuiya ya Kuhifadhisha Quran nchini kwa kuendelea kuwapatia vijana wa Kitanzania mwongozo na msingi wa maisha yao kupitia Quran kwani kwa kufanya hivyo wanakuwa wanawaongezea vijana hao uelewa sahihi wa dini yao na elimu ya kutosha ya mazingira (yaani circular education).

“Kwa kufanya hivyo, Jumuiya inalipatia Taifa la Tanzania nguvu kazi yenye uadilifu mkubwa katika utekelezaji wa majukumu yake sambamba na uwezo na kujiamini katika kuisoma na kuihifadhi Quran tukufu,” amesema.

Amewakumbusha viongozi wa taasisi hiyo watenge muda maalum wa mashindano hayo kuanzia ngazi ya wilaya, mkoa, kanda, kitaifa ndipo wawagawe kwenye makundi mawili makubwa. “Mkitoka hapo washindanishwe kwa bara la Afrika na kisha mashindano ya dunia. Siyo mnamaliza mashindano ya kimataifa halafu unasikia kuna mashindano ya wilaya au mkoa,” amesema.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na hadhira hiyo, Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir bin Ali alisema tuzo za leo zimethibitisha kuwa kusoma elimu ya mazingira hakuharibu elimu ya dini. “Iwe changamoto kwa Waislamu kwamba msingi wa elimu ya dini hauchafui elimu ya dini, kwani kuna watu hawataki kusoma elimu ya mazingira kwa kisingizio kuwa mtume hakusoma, sasa mtume atasoma kila kitu?” alihoji.

“Mambo ya uchumi, kijamii, sheria na ufundi yalielezwa na Mtume Muhammad (S.A.W) na Quran imeyazungumzia sana. Kusoma elimu ya mazingira ni muhimu kwa sababu zipo pia aya zaidi ya 70 katika Quran tukufu ambazo zinaelezea mambo hayo,” alisema.

Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kuhifadhisha Quran Tanzania, Sheikh Othman Ali Kaporo alisema walilazimika kuanzisha taasisi ili kuwafundisha vijana maadili mema kwani miaka ya 80 - 90 ilikuwa shida kumpata kijana mwenye uwezo wa kuhifadhi hata juzuu tatu tu.

“Hivi sasa taasisi yetu ina vijana zaidi ya 1,000 katika sekta tofauti lakini hakuna hata mmoja aliyekutwa katika mambo ya dawa za kulevya, ufisadi au mambo ya hovyo. Quran ni kinga. Quran ndiyo mafanikio, na kwa malengo hayo, ndiyo maana tunafanya mashindano haya,” alisema.

(mwisho)

Kocha Wa Simba Apewa Mkataba Wa Mwaka Moja

$
0
0
Kocha wa Simba Patrick Aussems amesaini mkataba mpya wa mwaka mmoja kuendelea kuinoa timu hiyo.

Hatua hiyo ni baada ya kufikia malengo aliyowekewa katika mkataba unaomalizika hivi karibuni ya kuhakikisha timu inatetea ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara na inafika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Jeshi la Yemen latekeleza mashambulizi mapya ya kulipiza kisasi Saudia

$
0
0
Jeshi la Yemen limetekelza mashambulizi mapya ya kulipiza kisasi katika eneo la Jizan, kusini magharibi mwa Saudi Arabia.

Televisheni ya Al Masirah imeripoti leo Jumapili kuwa, Jeshi la Anga la Yemen na kamati za wananchi zimetumia ndege isiyo na rubani au drone kushambulia maeneo ya kuegeshea ndege za kivita za Saudia katika uwanja wa ndege wa Jizan.

Taarifa zinasema kuwa oparesheni hiyo imetekelezwa na drone ya kivita ya Yemen aina ya Qasef-K2 baada ya oparesheni ya upelelezi.

Hali kadhalika Jeshi la Yemen limetangaza kuitungua ndege ya kijasusi ya adui katika eneo la mashariki mwa Jabal al-Dudud katika eneo la Jizan.

Wakurugenzi wa Halmashauri 10 Watakiwa Kuhakikisha Mradi wa Timiza Ndoto Yako Unatekelezwa Kikamilifu

$
0
0
Na Mwandishi Wetu
Wakurugenzi 10 wa Halmashauri za Wilaya wametakiwa Kuhakikisha kuwa mradi wa timiza ndoto zako kwa wasichana Balehe waliopo mashuleni na walio nje ya mfumo wa elimu unatekelezwa kama ilivyopangwa na Serikali ili kuleta matokeo chanya.
 
Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama Mei 25, 2019 Wilayani Bahi mkoani Dodoma wakati wa uzinduzi wa mradi huo, Katibu Mkuu Ofisi hiyo anayeshughulikia Sera Uratibu na Uwekezaji Bi. Dorothy Mwaluko amesema kuwa dhamira ya Serikali ni kuona mradi huo unaleta ukombozi wa kweli kwa mtoto wa kike.
 
“ Waliopo shuleni na nje ya mfumo wa elimu ni vyema mkatambua kuwa mradi huu ni fursa yakuwawezesha kujikwamua kiuchumi na kuepeuka vishawishi na maambukizi ya Virusi vya ukimwi kwani Serikali inatambua kuwa kumuwezesha mtoto wa kike ni kuiwezesha jamii nzima”Alisema Bi. Doorthy.
 
Mradi huu unatekelezwa katika mikoa ya Dodoma, Morogoro na Singida ambapo jumla ya Halmashuri 10 katika mikoa hiyo zinanufaika.Utekelezaji wake unatokana na usaidizi wa fedha kutoka kutoka Mfuko wa Dunia kwa ajili ya kuendeleza
mapambano dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI na athari zake.
 
Akifafanua amesema kuwa watekelezaji wa mradi huo wanalo jukumu la kuwajengea uwezo wanaufaika ili hata baada ya kipindi cha mradi waweze kujitegemea na kuondokana na utegemezi kutoka kwa serikali ambapo kwa sasa wanafunzi kutoka Kaya masikini wanawezeshwa kupata taulo za kujisitiri pamoja na mahitaji mengine ikiwemo sare za shule.
 
Aliongeza kuwa wanafunzi wote wanapaswa kutambua kuwa
Serikali inawekeza fedha nyingi katika mradi huo kwa kutambua umuhimu wa kundi hilo ili kujikwamua kielimu na kutumia vyema vipaji walivyo navyo.
 
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mhe. Mwanamisi
Mukunda akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Binilith Mahenge amasema kuwa mradi huo umesaidia kuongeza kiwango cha ufaulu katika Wilaya hiyo, mahudhurio ya wanafunzi shuleni yameongezeka kwa kiwango kikubwa.
 
“Tunaishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kwa kutuletea mradi huu katika Wilaya yetu kwani umeonesha mafanikio makubwa kwa kipindi cha majaribio ambacho umetekelezwa kwani umewanufaisha Wanawake Vijana wenye umri wa kati ya miaka 10- 24”, alisisitiza Mhe. Mwanahamisi.
 
Akifafanua amesema kuwa mradi huo umefikia Kaya 265 na
wasichana 129 unawanufaisha wasichana balehe waliopo shuleni na wale wa nje ya shule 45.
 
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) Dkt. Leonard Maboko amesema kuwa mradi huo ni wa miaka 3 na unatekelezwa katika mikoa 3 ambapo wanufaika wa mradi walio nje ya shule watajengwewa uwezo kwa kupewa stadi za maisha.
 
Alitaja sababu za kuwalenga wasichana wanaobalehe Dkt. Maboko amesema kuwa ni pamoja na kundi hilo hilo kuwa waathirika wakubwa ambapo asilimia 80 ya maambukizi ya VVU yamewaathiri vijana wa kundi hilo.

Mmoja wa wazazi wa wanafunzi walionufaika na mradi huo Bi Mayasa Mussa amesema kuwa wanafunzi wanafurahia mradi huo na ari ya kwenda shule imeongezeka kwani kila mwezi wanapokea elfu 25,000/- kwa mwezi kuwawezesha kukidhi mahitaji muhimu ya wanafunzi hao ikiwemo kupata taulo za kike, sare za shule na mahitaji mengine.
 
Mradi wa Timiza ndoto zako unatekelezwa katika mikoa 3 na
Halmashuri na Halmashuri 10 ukilenga kuwawezesha wasichana waliobalehe wakiwa mashuleni na wale walio nje ya mfumo wa elimu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>