Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Iran yaapa kujilinda kwa nguvu zote dhidi ya uchokozi

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Iran, Mohammad Javad Zarif, amesema nchi yake itajilinda kwa nguvu zote dhidi ya uchokozi wa kijeshi na kiuchumi, huku akizitolea wito nchi za Ulaya kuchukua hatua zaidi kuyanusuru makubaliano ya nyuklia waliyotia saini. 

Akizungumza kwenye mkutano na waandishi habari mjini Baghdad, Iraq, hivi leo, Zarif amesema nchi yake inataka kujenga mahusiano ya usawa na jirani zake wa eneo la Ghuba na imekwishapendekeza kutiwa saini mkataba wa kuepuka uchokozi.

 Wakati huo huo, Rais Hassan Rouhani wa Iran ameashiria kuwa Iran inaweza kuitisha kura ya maoni kuhusu mpango wa nyuklia wa nchi hiyo kufuatia kuongezeka mvutano kati yake na Marekani. 

Rouhani amesema amewahi kupendekeza suala hilo kwa Kiongozi  Mkuu Ayotallah Ali Khamenei mwaka 2004 alipokua mjumbe mwandamizi kwenye mazungumzo ya nyuklia. 

Kura hiyo ya maoni itaipa serikali ya Iran uhalali wa kisiasa iwapo itaamua kuongeza urutubishaji wa madini ya urani unaozuiwa chini ya makubaliano ya 2015 na mataifa yenye nguvu.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521

Mahakama yaamuru kura kuhesabiwa upya Malawi

$
0
0
Mahakama nchini Malawi imeiamuru tume ya uchaguzi kutotangaza matokeo ya uchaguzi wa rais wa Mei 21 kufuatia malalamiko ya wizi wa kura yaliyotolewa na upinzani. 

Katika amri hiyo, Mahakama Kuu ilitaka kusitishwa utangazaji wa matokeo ya kura ya rais na kuelekeza kuhesabiwa upya kwa kura za theluthi ya maeneo yaliyoshiriki uchaguzi. 

Tume ya uchaguzi nchini humo ilisimamisha kutangaza matokeo hayo baada ya kupokea malalamiko 147 kutoka kwa baadhi ya vyama vilivyoshiriki katika uchaguzi huo wa Jumanne iliyopita. 

Chama kikuu cha upinzani cha Malawi Congress (MCP) kinachoongozwa na Lazarus Chakwera, kiliwasilisha malalamiko mahakamani juu ya kile ilichodai kuwa makosa yaliyojitokeza katika wilaya 10 kati ya 28 nchini humo. 

Ujumbe wa Waangalizi wa Umoja wa Ulaya uliueleza uchaguzi huo kuwa ulisimamiwa vizuri, ulikuwa na uwazi pamoja na ushindani mkali.

Rais Magufuli Afanya Mazungumzo Na Rais Wa Afrika Kusini Ikulu Ya Pretoria

$
0
0
Rais wa Tanzania, John Magufuli leo Jumapili Mei 26, 2019, amekutana na kufanya mazungujza na Rais  Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, Ikulu Jijini Pretoria.

Katika mazungumzo hayo, Rais Magufuli amempongeza Rais huyo kwa kuapishwa kuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Afrika Kusini na amemhakikishia kuwa Tanzania itadumisha uhusiano na ushirikiano wa kidugu na kihistoria na nchi hiyo.

 Rais Magufuli amaesema uhusiano wa Tanzania na nchi hiyo uliasisiwa na Baba wa Taifa wa Tanzania, hayati Mwalimu Julius Nyerere na hayati Nelson Mandela kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha ANC (African National Congress).

Amemwambia kuwa ni matarajio yake kuona uhusiano huo unaimarishwa zaidi katika nyanja za uchumi na kukuza lugha ya  Kiswahili.

Rais huyo wa Tanzania, amemshukuru Ramaphosa kwa kumkaribisha na kufanya naye mazungumzo ya siku moja baada ya kuapishwa kwake.

Kwa upande wake, Rais Ramaphosa naye amemshukuru Magufuli kwa kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwake na amemhakikishia kuwa Afrika Kusini inatambua mchango mkubwa wa Tanzania katika ukombozi wa Taifa hilo.

Hivyo, amemuahidi katika kipindi chake cha uongozi atauendeleza na kukuza zaidi uhusiano huo.

Rais Ramaphosa amesema kufuatia uamuzi wa Afrika Kusini kuanza kufundisha lugha ya Kiswahili, nchi yake itachukua walimu wa Kiswahili kutoka Tanzania ili watumike kufundisha somo hilo katika shule za msingi na sekondari.

Aidha, ameahidi kufanya ziara rasmi ya Tanzania kabla ya Mkutano wa 39 wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), uliopangwa kufanyika Agosti 2019 nchini Tanzania. Pia, atahudhuria mkutano huo.

Kabla ya mazungumzo hayo,  Rais Magufuli ambaye ameongozana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi, alimkabidhi Ramaphosa zawadi ya vitabu vya kusoma na kufundishia lugha ya Kiswahili kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Marais hao wawili wamefanya  mazungumzo hayo ikiwa ni kabla ya  Rais Ramaphosa hajatangaza Baraza lake la Mawaziri.

Kesho, Rais Magufuli ataondoka Afrika Kusini kuelekea nchini Namibia ambako atafanya ziara rasmi ya Kitaifa kwa mwaliko wa Rais wa Namibia, Hage Geingob.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya May 27

Waziri Kivuli wa Nishati, John Mnyika Ataka Mikataba ya Stiegler's Gorge pamoja na mikataba yote ya bomba la gesi Mtwara Ipelekwe Bungeni

$
0
0
Waziri Kivuli wa Nishati, John Mnyika, ameitaka serikali iwasilishe bungeni mkataba wa utekelezaji wa mradi mkubwa wa uzalishaji umeme wa Stiegler's Gorge pamoja na mikataba yote ya bomba la gesi Mtwara na ripoti zote zilizotokana na kamati zilizoundwa kuhusu mafuta na gesi ili Bunge iipitie.

Pia ametaka serikali iwasilishe ripoti ya tathmini ya kimazingira iliyofanyika ya utekelezaji wa mradi wa Stiegler’s ili Bunge lione athari zake.

Mnyika aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari na kueleza kuwa mikataba hiyo pamoja na ripoti hizo ziwasilishwe bungeni kesho wakati waziri akiwasilisha hotuba ya wizara yake.

Akizungumzia kuhusu mkataba wa Stiegler’s, Mnyika ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kibamba (Chadema), alidai umekuwa na mkanganyiko wa gharama zitakazotumika, hivyo ametaka upelekwe bungeni ili waone ni miujiza gani iliyofanyika kutoka utekelezaji wake wa miaka 12 awali hadi miaka mitatu sasa.

“Binafsi nimeshaandaa rasimu ya hotuba yenye kurasa 80 na aya 145 inayozungumzia mambo mbalimbali ya sekta ya umeme, gesi na mafuta,” alisema.

“Serikali ilileta bungeni muswada wa sheria unaohusu sekta inayogusa rasilimali za nchi, muswada mmojawapo ukiwa na kifungu chenye kutoa wajibu na haki kwa Bunge na wajibu kwa serikali kwenye mikataba mikubwa ya nchi inayogusa rasilimali za nchi.

“Mikataba hii ilikuwa na kifungu kwamba inabidi ipelekwe bungeni kwa sababu kumeshatokea utata wa mradi wa Stiegler's Gorge, wito wangu ni kwamba tarehe 28 (Jumanne) wakati waziri anasoma hotuba yake bungeni pamoja na hotuba ya serikali, awasilishe mkataba wa ujenzi wa mradi wa Stiegler's ili mbivu na mbichi zijulikane.”

Mnyika alisema serikali ilisema mkataba ambao umesainiwa na mkandarasi ni wa Sh. trilioni 6, lakini awali iliwahi kusema mradi mzima utagharimu Sh. trilioni 10.

“Uchambuzi mbalimbali ukianzia na wa serikali yenyewe ikiwamo Wizara ya Nishati na Madini wakati huo (mwaka 2016) ilifanya uchambuzi kuhusu gharama za mradi huu ambao ungetumia miaka 12 kujengwa, hii ni kwa tathmini ya wizara na tathmini ya wataalamu kuanzia mwaka 2012,” alisema.

Credit: Nipashe

Wamiliki Tanzanite Wapewa Miezi Sita Kuboresha Miundombinu

$
0
0
Ofisa madini Mkazi wa Mkoa wa kimadini wa Simanjiro, Daudi Ntalima amewapa miezi sita wamiliki na wachimbaji wa madini ya Tanzanite Mji mdogo wa Mirerani, kuboresha miundombinu ya migodi yao la sivyo itafutiwa leseni.

Ntalima aliyasema hayo wakati akizungumza kwenye kikao kazi na mameneja, wachimbaji na wamiliki wa migodi ya Tanzanite Mji mdogo wa Mirerani.

Alisema ametoa miezi sita hadi mwezi Septemba kwani ikifika mwezi Octoba wataanza kuchukua hatua na wanaanza kuhesabu miezi sita hiyo kuanzia mwezi Aprili hadi Septemba.

Alisema hawezi kutoa muda wa mwaka mmoja kwani ni muda mrefu hivyo wamiliki wa migodi hiyo zaidi ya 800 wajitahidi kuboresha miundombinu yao kabla ya miezi sita kumalizika.

“Migodi yote inapaswa kuwekewa uzio wa ukuta wa matofali au mabati ili kuimarisha ulinzi na usalama mgodini na siyo senyenge mmiliki akishindwa hilo mgodi utafutiwa leseni,” alisema Ntalima.

Mwenyekiti wa chama cha wachimbaji madini mkoani Manyara (Marema) Tawi la Mirerani, Shwaibu Mushi alisema wachimbaji hao wanaiomba Serikali kuwapa muda mwaka mmoja ili waboreshe miundombinu ya migodi yao ikiwemo kuweka uzio.

Mushi alisema wengi wao uchumi wao ni mdogo hivyo wanaomba muda huo ili kutekeleza hilo kwani agizo hilo limekuja kipindi ambacho wengi wao wana hali ngumu.

“Wachimbaji wadogo bado wanahitaji kuwa wachimbaji wakubwa baada ya kupata madini, tuliomba tuongezewe muda wa mwaka mmoja ili tutekeleze hilo japo tunashukuru kwa kutuongezea miezi sita,” alisema.

Mwenyekiti wa kamati ya Tanzanite, Money Yousuph alisema wachimbaji wamegawanyika kwenye matabaka tofauti kiuchumi hivyo wanaomba mwaka mmoja wa kutekeleza hilo.

“Ofisa madini mkazi Ntalima wewe ni mlezi wetu na mchimbaji asiyekuwa rasmi mnamtambua na hamchukulii hatua kali na pia ukuta siyo kero ni tija tunaomba busara na hekima zako kwani sisi ni wasikivu,” alisema Yousuph.

Vikosi Maalum Vikiongozwa Na Kamishna Operesheni Na Mafunzo Ya Jeshi La Polisi CP Liberatus Sabas, Wafanya Operesheni Mapango Ya Amboni Mkoani Tanga.

$
0
0
Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi La Polisi CP Liberatus Sabas, ameongoza Vikosi Maalum ya Kupambana na Uhalifu katika Operesheni iliyofanyika maeneo yote ya Mapango ya Amboni Jijini Tanga juzi baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema kuwa kumeonekana baadhi ya watu wasiofahamika na baadhi yao ni wahalifu waliokuwepo kipindi cha nyuma ambao wengi wao walishakaatwa na Jeshi la Polisi na mwisho amewataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano na taarifa katika Vyombo vya Ulinzi na Usalama. (Picha na Jeshi la Polisi).


LIVE: Fuatilia kipindi cha maswali na majibu kutoka Bungeni Dodoma

$
0
0
LIVE: Fuatilia kipindi cha maswali na majibu kutoka Bungeni Dodoma

Auawa kwenye sherehe akigombea mwanamke

$
0
0
Mkazi  wa Mtaa wa Tagota Halmashauri ya mji Tarime mkoani Mara, Muniko Kinyunyi (30) amekufa kwa kuchomwa na kisu shingoni baada ya kutokea ugomvi na mwenzake ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja.

Wawili hao wanadaiwa kuwa walikuwa wakigombea mwanamke katika sherehe iliyofanyika nyumbani kwa aliyekuwa mgombea ubunge mwaka 2015 Jimbo la Tarime Mjini, Michael Kembaki.

Kwa mujibu wa diwani wa Kenyamanyori, Ganga Mgendi tukio hilo la kusikitisha lilitokea usiku wa kuamkia jana nyumbani kwa Kembaki Tarime mjini.

Kembaki katika uchaguzi huo wa mwaka 2015 aliwania nafasi hiyo ya ubunge Tarime Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuangushwa na mbunge wa sasa, Esther Matiko (Chadema).

Mgendi alisema tukio hilo lilitokea wakati wa sherehe iliyofanyika nyumbani kwa mwanasiasa huyo aliyetembelewa na dada yake aliyekwenda na kikundi cha watu kuwasalimia mama na ndugu zake.

Alisema katika shamrashamra hizo ndipo kulipoibuka ugomvi kati ya Mniko na mtu ambaye hakufahamika mara moja jina lake wakigombea mwanamke hali iliyosababisha mtu huyo kumchoma Mniko kisu shingoni karibu na kifuani na kisha kutoroka wakati watu wakihangaika kumkimbiza katika Hospitali ya Wilaya Tarime ambapo alifariki kabla ya kupatiwa matibabu kutokana na kutokwa damu nyingi.

Kamanda wa Polisi Tarime Rorya, Henry Mwaibambe alithibitisha kutokea kwa tukio hilo la mauaji na kueleza kuwa Jeshi la Polisi linamsaka mtuhumiwa na kuwaomba raia wema kutoa ushirikiano ili kuweza kumkamta mtuhumiwa huyo aliyetoroka.

Credit: Habarileo

RC Olesendeka aridhishwa na ukamilishwaji wa kituo kipya cha mabasi Njombe

$
0
0
Na Amiri kilagalila-Njombe
Mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Olesendeka amefanya ukaguzi katika kituo kituo kipya cha mabasi kitakachogharimu zaidi ya bil 9.6 Hadi Kukamilika Kwake pamoja na ujenzi wa mradi wa soko kuu mjini Njombe lenye hadhi ya kimataifa litalogharimu bil 9.3 na kuonyesha kuridhishwa na mwenendo wa ukamilishaji wa miradi hiyo inayofadhiliwa na benk ya dunia.

Pamoja na kuridhishwa na ujenzi unaoendelea akiwa katika kituo cha mabasi ambacho kilianza kufanya kazi Mei  11 kwa agizo la rais ,mkuu wa mkoa amepokea malalamiko kutoka kwa abiria,machinga,mama na baba lishe ambao wanasema wanashindwa kufanya biashara kama ilivyokuwa awali katika stendi ya zamani kwani halmashauri imezuia kufanya biashara ndani ya stendi hata kwa wenye vitambulisho vya mjasiriamali.

"Unapotoka toka pale ile lisiti waliyonipa wanachana natoka tena kuchukua abiria ninavyoingia nalipa tena mia mbili sasa kuanzia saa kumi na mbili ile asubuhi mpaka saa moja jioni ninakuwa nimelipa shilingi ngapi,lakini humu ndani hakuna mboga wala cha nini kuna mwingine anahitaji mboga mfano samaki aende nazo kijijini hamna haya chungwa hamna" walisema baadhi ya wajasiriamali ndani yastendi

Mara baada ya kusikiliza kero hizo Christopher Olesendeka anawataka Wajasiliamali Hao Kuvuta Subira Wakati Yakiwekwa Sawa Mazingira Ya Wao Kufanya Biashara Ndani ya Stendi Hiyo Baada ya Ujenzi Wake Kukamilika.

"Nataka niwahakikishieni mheshimiwa Rais ametoa fedha kwa ajili ya stendi hii na akaelekeza kituo hiki cha mabasi kikamilike haraka ili ninyi kina baba lishe na mama lishe muweze kufanya biashara katika maeneo mazuri zaidi,tunaendelea kukagua kuonamaeneo yaliyobaki ili stendi ikamilike vizuri halafu tuendelee kuungana na halmashauri yenu tuweke utaratibu rafiki ili kuona wanyonge wa Njombe ndio watakaonufaika na vibanda vilivyoko stendi na uendeshaji wabiashara katika eneo hili''

Katika hatua nyingine Olesendeka amekagua ujenzi wa soko kuu ambao Ameonyesha kuridhishwa na kasi na ubora katika ujenzi Huo  huku Mhandisi wa mradi huo Mboka Justin akidai mradi umefika asilimia 60 na kuahidi kukamilika ndani ya muda uliopangwa.

DC Nyimbi Afagiria Umahiri Wa Serikali Ya Magufuli Katika Kutekeleza Miradi Ya Maendeleo

$
0
0
Na  Amiri kilagalila
Kaimu mkuu wa mkoa Mwanza Dkt. Philis Nyimbi ambaye pia ni mkuu wa Wilaya Nyamagana amefagiria serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Dkt. John Pombe Magufuli kwa namna ilivyoonesha umahiri mkubwa wa kuibua miradi inayotatua changamoto za watu wote katika nyanja ya elimu, afya, miundombinu ya barabara, anga, reli, bandari,  kilimo na mifugo.

Dkt. Nyimbi amebainisha hayo akifunga kongamano la  kuelezea mafanikio ya serikali ya awamu tano katika miaka minne mkoani  Mwanza. 

Ambapo amepongeza umahiri wa uwasilishaji wa mada mbali mbali zilizotolewa katika kongamano, umakini  wa ichangiaji Mada kwa  washiriki wote. Dkt. Nyimbi akihitimisha kwa kuomba waandaji wa kongamano hilo taasis ya Sautu ya Jamii Tanzania mwaka ujao kuuongeza mada itakayo pima mafanikio kwa kuakisi usawa wa kijinsia.

Akitoa salamu za Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo la Nyamagana, Bi Florah Magabe amepongeza umahiri wa uongozi wa Magufuli kwa kutekeleza ahadi zote alizozitoa katika Ilani yake ya Uchaguzi kwa zaidi ya 75%. 

Kadharika amesifia uongozi huu umewezesha wilaya ya Nyamagana kupata ongezeko ya 100% ya madawa na vifaa tiba, ujenzi wa Zahanati tano mpya pamoja na kituo cha afya chenye hadhi ya hospitali ya wilaya.

Bi. Magabe ameomba mwaka ujao kongamano hilo lifanyike wazi kuongeza idadi ya washiriki maana uongozi wa   Magufuli kwa kushirikiana na Mhe. Mabula wilayani Nyamgana serikali imewezesha  ujenzi wa madaraja mawili ambayo yalijengw enzi za ukoloni zitakazo unganisha wilaya ya Magu, Kwimba na Misungwi. 

Kadharika amefafanua namna ambavyo Nyamagana imejidhatiti kutatua uhaba wa maji kwa miaka 20 ijayo kwa serikali kwa kutoa fedha kwa miradi mikubwa ya miwili ya maji,  ujenzi wa barabara zote za mjini kwa kiwango cha rami pamoja na kujenga barabara za moramu na mawe.

Kongamano hilo la pili kufanyika kitaifa limeandaliwa ba taasis ya Sauti ya Jamii Tanzania na kuwakutanisha wadau wa maendeleo ambapo mada mbali zilitolewa ba TAKUKURU, TRA, NIDA, Taasis za fedha, Wanazuoni pamoja na mfuko wa Pembejeo.

Askari Magereza anaswa kwa utapeli Mwanza

$
0
0
Polisi  jijini Mwanza imemkamata askari magereza Kibemba Warioba (27) mwenye namba za usajili B.9205 WDR, akiwa na simu tano za aina tofauti na mitandao tofauti akijihusisha na makosa ya kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jumanne Muliro amesema kuwa tukio hilo limetokea juzi saa nne na nusu asubuhi, ambapo polisi wa mkoa wa Mwanza kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi la Mkoa wa Kagera walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo ambaye alikuwa anafanya kazi wilayani Biharamulo mkoani Kagera na tayari amesimamishwa kazi kwa hatua zaidi za kisheria.

Kamanda Muliro alisema polisi walimbaini mtuhumiwa huyo akitumia njia ya mitandao hiyo ya simu ambapo alianzisha Saccos ‘Bandia,’ iliyojulikana kwa jina la Info Tell CCM, akilenga kuwatapeli wanachama wa CCM na wengine katika mikoa ya Mara na Kagera.

Alitoa onyo kwa wananchi wenye tabia ya kufanya vitendo hivyo vya uhalifu waache mara moja kwa kuwa ni kinyume cha sheria.

Waziri Mkuu Awaonya Wamiliki Wa Vituo Vya Kulelea Watoto Yatima

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaonya baadhi ya wamiliki na waendeshaji wa makao ya watoto wasiofuata taratibu za usajili wa watoto, wanaowatumia watoto kama mitaji au kwa maslahi binafsi na wanaoendesha makao hayo kwa minajili ya kidini na kikabila.

Amewataka pia wamiliki hao waache mara moja kuwalea watoto hao katika maadili yasiyofaa na yasiyo ya Kitanzania na kwamba maofisa ustawi wa jamii wahusike moja kwa moja katika usajili wa mtoto ili kuhakikisha kuwa ni watoto wanaostahili tu kuwekwa kwenye makao ndiyo wanasajiliwa.

Alikuwa akizungumza jana usiku (Jumapili, Mei 26, 2019) kwenye Viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam alikokuwa mgeni wa heshima wakati wa futari ya pamoja na watoto yatima kutoka kwenye vituo sita vya kulea watoto yatima vya jijini humo.

“Nitoe rai kwamba watu mmoja mmoja, taasisi na makao wazingatie baadhi ya taratibu za msingi za uendeshaji wa makao kama vile mtoto kukuzwa katika mazingira ya familia, kuzingatia misingi ya kitaifa badala ya misingi ya tamaduni za kigeni.

“Mtoto kukuzwa kwa kuzingatia maslahi bora ya mtoto; kuzingatia umuhimu wa kuwa na mwendelezo katika dini ya mtoto na utamuduni wake; kutotenganisha watoto na ndugu na kuhakikisha watoto wote wanapata huduma stahiki, kulindwa dhidi ya vitendo vya ukatili na unyanyasaji; na kutunzwa na  kuendelezwa hadi kufikia kimo cha utimilifu wao,” alisema.

Waziri Mkuu alitumia hadhara hiyo pia kutoa maelekezo mahsusi kwa waendeshaji wa makao pamoja na wasimamizi wa sheria na taratibu za uendeshaji wa makao ya watoto yatima.

“Afisa Ustawi wa Jamii katika eneo yanakoanzishwa makao, ahusike moja kwa moja katika usajili wa mtoto ili kuhakikisha kuwa ni watoto wanaostahili tu kuwekwa kwenye makao ndio wanasajiliwa.

“Taasisi na makao zihakikishe kuwa kila mtoto anawekewa mpango maalumu wa kuondoka kwenye makao na namna ya kumuunganisha mtoto huyo na familia yake.

“Wamiliki wa taasisi na makao, waruhusuni maafisa ustawi wa jamii na maafisa wengine wa Serikali wafanye ukaguzi kwa mujibu wa sheria na wekeni utaratibu wa kuandaa taarifa za kila mwezi za watoto na taarifa ya mwaka wa fedha,” alisema Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu pia alionya dhidi ya wale “wanaowabadili watoto dini kinyume cha sheria; wanaofanya vitendo vya unyanyasaji na ukatili dhidi ya watoto; wasiowaruhusu watendaji wa Serikali kufanya ufuatiliaji na usimamizi; wasioandaa mpango wa kuwaunganisha watoto na familia zao na hivyo, kusababisha watoto kukaa kwa muda mrefu kwenye makao na wale wote wanaondesha makao bila kuwa na leseni ya uendeshaji.”

Alisema Serikali haitowafumbia macho watu wa namna hiyo, na mara tu watakapogundulika kuanzisha au kuendesha makao bila kufuata taratibu, hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Alisema tangu mwaka 2016 hadi sasa, kuna jumla ya watoto 24,067 wanaolelewa katika makao yaliyosajiliwa nchini yakiwemo makao 140 yanayoendeshwa na kumilikiwa na watu au taasisi binafsi. Kati yao wavulana ni 11,925 na wasichana ni 12,142.

Alisema Serikali kupitia Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inaratibu upatikanaji wa huduma za msingi kwenye makao kwa kushirikiana na wadau mbalimbali. Baadhi ya huduma hizo ni pamoja na kuwezesha upatikanaji wa Bima ya Afya kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi. “Hadi sasa, watoto 900 kutoka Dar es Salaam, Mbeya, Kilimanjaro na Arusha wamepatiwa kadi hizo na zoezi hilo linaendelea,” alisema.

Waziri Mkuu alisema Serikali itaendelea kusimamia na kufuatilia kwa karibu uendeshaji wa makao ya watoto sambamba na kutoa elimu kuhusu malezi, makuzi, haki, ulinzi na usalama wa mtoto kwa mujibu wa sheria zinazosimamia haki na ustawi wa mtoto.

Mapema, akielezea azma ya kuandaa futari hiyo, Mkurugenzi wa Chocolate Princess na mwandaaji wa kipindi cha televisheni maarufu cha The Mboni Talk Show, Bi. Mboni Masimba alisema jumla ya watoto yatima 325 walikuwa wamealikwa kushiriki futari hiyo.

Watoto hao wanatoka vituo vya Ijango Zaida Orphanage Centre kilichopo Sinza, Alzama Orphanage Centre (Mbagala), Ashura Foundation (Vingunguti), Madina Orphanage Centre (Tandale), Hiyari Orphanage Centre (Mbagala) na Hisani Orphanage Centre (Mwasonga).

Futari hiyo iliandaliwa na Mboni Masimba kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Asure Yetim Vafki, United Bank of Africa (UBA), Junaco, Mo Dewji Foundation, Lake Oil, ASAS, AZAM, Uncle K Catering, Zurii, Simply Special Decor na State Oil na kuhudhuriwa na watu mbalimbali wakiwamo Balozi wa Uturuki nchini, Bw. Ali Davutoğlu, Mjumbe wa Baraza la Ulamaa Taifa, Sheikh Issa Othman, masheikh, maimamu wa misikiti na viongozi wa taasisi zinazojihusisha na malezi ya watoto yatima.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Kesi ya Shamim Mwasha na mumewe Yapigwa Kalenda

$
0
0
Upelelezi wa Kesi ya kusafirisha dawa za kulevya aina ya Heroin Hydrochloride   inayomkabili  mmiliki wa Blog 8020 Fashion, Shamim Mwasha (41) na mumewe, Abdul Nsembo(45) bado haujakamilika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Wakili wa Serikali, Wankyo Simon amemueleza Hakimu Mkazi, Kelvin Mhina kuwa shauri hilo limeitishwa kwa ajili ya kutajwa lakini upelelezi haujakamilika, hivyo anaomba ahirisho.

Baada ya kueleza hayo Wakili utetezi, Charles Kisoka amedai kuwa shauri hilo halina dhamana hivyo wanauonba upande wa mashtaka kuharakisha upelelezi.

Wakili Wankyo ameeleza kuwa amesikia kilichozunguzwa na upande wa utetezi, hivyo watawahimiza wenzao wa upelelezi wafanye haraka na tarehe ijayo wataeleza upelelezi ulipofikia.

Hakimu Kelvin Mhina ameahirisha kesi hiyo hadi June 10, 2019, washitakiwa wamerudishwa rumande kwa sababu kesi yao haina dhamana.

Washtakiwa hao wanatuhumiwa kusafirisha dawa hizo za kulevya, Mei 1,2019 wakiwa eneo la Mbezi Beach, Wilaya ya Kinondoni, jijini  Dar es Salaam kinyume na sheria ya uhujumu uchumi.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521

Rais Magufuli Apokelewa Na Mwenyeji Wake, Rais Hage Geingob Wa Namibia

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akipokewa na Mwenyeji wake Rais Hage Geingob wa Namibia alipowasili katika Ikulu ya nchi hiyo, Jijini Windhoek leo Mei 27, 2019. Rais Dkt. Magufuli amewasili nchini Namibia kwa Ziara Rasmi ya Kikazi ya Siku
mbili.

Waziri wa Nishati, Dk Medard Kalemani Asema Hakuna Upungufu wa Nyaya wa Nguzo za Umeme

$
0
0
Waziri wa Nishati, Dk Medard Kalemani amesema Tanzania haina upungufu wa nguzo za umeme, nyaya wala transfoma hivyo akaomba wakandarasi wa umeme kuacha visingizio.

Dk Kalemani ametoa kauli hiyo bungeni leo Jumatatu Mei 27, 2019 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Nyang’ hwale (CCM), Hussein Amar.

Mbunge huyo ametaka kujua ni kwa nini mkandarasi wa umeme katika jimbo lake ametandaza nguzo lakini hafungi umeme kwa kisingizio cha upungufu wa nyaya.

Waziri amesema kauli kuwa hakuna nyaya za umeme haina ukweli kwani katika kipindi hiki hakuna upungufu wowote kuhusu vifaa hivyo na akaonya kwa wakandarasi wanaotoa sababu hizo waache mara moja na badala yake wakafunge umeme kwa wakati waliopangiwa.

Mradi Wa Reli Ya Kisasa (SGR), Mwamba Wa Changamoto Za Usafirishaji Nchini

$
0
0
 Na Paschal Dotto-MAELEZO
Ni Takribani Miaka 120 ambapo historia iliandikwa, mwaka 1912, Serikali ya Kikoloni nchini iliamua kuimarisha sekta ya usafirishaji Kwa kujenga Reli, ambapo njia zake ziliunganisha Miji hasa maeneo ya kilimo, uzalishaji na kibiashara, reli kuu kutoka Dar es Salaam mpaka Mwanza, hatimaye Kigoma na Tanga.

Ni dhahiri sasa tunaona Rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akifanya mageuzi makubwa Kwa kujenga reli ya kisasa, maarufu SGR (Standard Gauge Railway) ambapo kwa vyovyote tutasogeza nyuma zaidi kuhusu historia ya reli nchini, kwani Rais anatakeleza Ujenzi wa Reli ya Kisasa, Standard Gauge Railway (SGR) kwa maslahi makubwa kiuchumi.

Katika hafla ya uwekaji wa Jiwe la msingi la ujenzi wa Reli ya SGR awamu ya pili, Morogoro-Makutupola, iliyofanyika 14, Machi, 2018, Rais Magufuli aliwakumbusha Watanzania kuwa Tanzania imekuwa nchi ya pekee Barani Afrika katika kutekeleza mradi huo mkubwa kwa pesa za walipa kodi wake.

“Kwa bahati nzuri, hivi karibuni tulitembelewa na Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, na alishuhudia kwamba Tanzania tumetayarisha fedha zetu wenyewe, kwa nguvu zetu wenyewe, na walipa kodi ni watanzania wenyewe, Tsh Trilioni 2.8 na kutangaza tenda zilizokuwa wazi, makampuni zaidi ya 40 yalijitokeza kuwania tenda, na bahati nzuri kampuni kutoka Uturuki ikashinda tenda hii,” alisema Rais Magufuli na kuongeza kuwa Uturuki itatupa mkopo wa masharti nafuu kwa awamu zingine za ujenzi, Rais akaongeza, “ kwa hiyo Tanzania tunaweza”,

Rais Magufuli aliwataka watanzania kutambua fursa za upitapo mradi wa SGR na kuwataka wafanyabiashara wakubwa, wadogowadogo, mama ntilie, kunufaika wakati wa ujenzi na mara baada ya ujenzi, na kwamba itakuwa nguzo kubwa kwa usafarishaji kwenye maeneo hayo na nchi nzima.
 
“Katika uchumi wa nchi yoyote duniani, Sekta ya Usafirishaji ni muhimu sana, kwa hiyo Serikali kuchukua hatua madhubuti ya kuimarisha sekta ya usafirishaji kwa kujenga reli ya kisasa, SGR, ni moja ya Mwarobaini wa kutatua changamoto ya usafirishaji mizigo na kulinda usalama wa barabara”. Alisikika mmoja wa wahandisi akiwaeleza waliowatembelea.

Mageuzi ya Rais Magufuli yanalenga kuwaimarisha wananchi, si tu wafanyabiashara bali hata wasafiri kwa utekelezaji wa ujenzi wa Reli ya kisasa, SGR yenye kasi ya 160km/saa utakuwa na faida kuwabwa kwani masaa 2.5 Dar es Salaam-Morogoro na masaa tisa kutoka Dar es Salaam kwenda Mwanza, ni dhahiri kutakuwa na Furaha kubwa kwa watu kuwahi kufika Mwanza mapema badala ya saa saba usiku au kulala Shinyanga.

“Ujenzi wa Reli hii (SGR), kwa Tanzania siyo chaguo bali ni lazima, kwani hatua hii ilitakiwa ifikiwe zamani, lakini sasa Rais Magufuli ameamua kutufikisha kwenye teknolojia mpya katika sekta ya usafirishaji, kwani matatizo mengi ya barabara yanatokea kwababu ya mizigo mizito, hakuna reli imara ya kubeba mizigo hiyo, kwa hiyo ujenzi wa Reli hii ni maamuzi sahihi kwa Serikali yetu.”, Anaeleza Mkurugenzi TRC, Masanja Kadogosa.

Kadogosa anasema, Reli hiyo ambayo inatumia nishati ya umeme imekuja wakati mwafaka ikiwa Serikali inatekeleza mradi mkubwa wa kuzalisha umeme wa Mto Rufiji (Rufiji Hydroelectric Power), wenye kutoa Megawati 2,115, kwa hiyo treni hiyo itapata umeme wa kutosha.
 
“SGR, Ni mradi mkubwa ambao unatekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Magufulu kwa kutumia fedha za walipa kodi wake kwahiyo ni vyema watu wakafahamu kuwa kodi yao inaenda wapi Trilioni 7 siyo mchezo”, alisema Kadogosa.

Ili kutekeleza adhima ya kuutangaza mradi huo kwa wananchi, Mei 17, 2019, Jopo la Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri pamoja na Makatibu Tawala takribani 400 wakiongozwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Seleman Jafo walitembelea kuona mradi huo ili kupeleka ujumbe kwa wananchi.

Kabla ya Safari hiyo Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa aliwapitisha kidogo wageni wake katika shule ndogo kuhusu mradi ili kutambua umuhimu wa Mradi huo kwenye sekta ya usafirishaji na kwa wananchi.

Masanja alieleza kuwa Reli hiyo inayojengwa inaenda kufuta zana mbalimbaliikiwemo ile historia ya kikoloni, kuwa reli iliyopo ilijengwa na wakoloni, lakini pia ujenzi wa Reli hiyo sasa unaenda kuimarisha sekta ya usafirishaji. Serikali inatekeleza ujenzi huo Kwa Kipande cha Dar es Salaam-Morogoro, Morogoro-Makutupola na badae kutekeleza ujenzi huo hadi Mwanza, kilometa 1,219.

Kadogosa alisema kuwa Reli hiyo, SGR inauwezo wa kubeba tani milioni, 10,000, kwa mkupuo sawa na malori 500 yenye tani 20, Treni tano zenye tani 10,000 na kuwa na kasi kubwa ya 160km/saa, tofauti na ya sasa ambayo inakasi ya 30km/saa, kwa Afrika itakuwa ni Reli pekee yenye uwezo mkubwa kama huo, tani Miliomi 10-17 zitasafirishwa kwa mwaka, kwa hiyo SGR ni mwamba sekta ya usafirishaji nchini.

Aidha, Kadogosa alieleza kuwa ujenzi wa Reli (SGR), Dar es Salaam-Morogoro unatekelezwa na Kampuni kutoka Uturuki, Yapi Merkezi takribani Trilioni 2.7, lakini kwa sehemu nyingine ni Yapi Merkezi na Portuguese Construction Group Motel-Engil.

kukamilika kwa mradi huo kutakuwa na ufanisi mkubwa kwenye sekta ya usafirishaji nchini kwa kubeba mizigo tani nyingi lakini pia kasi yake katika kusafirisha abiria, kutoka Dar es Salaam- Dodoma treni itakuwa inafanya safari mara nane kwa siku, kwa hiyo ni hatua kubwa kwa sekta ya usafirishaji.

Kadogosa alizitaja baadhi ya Faida za Mradi huo Kwa sasa kwa wananchi na uchumi wa nchi kwa ujumla kwani kwa sasa watanzania walioko sehemu za ujenzi wanafaidika na kupeleka malighafi za ujenzi, mama ntilie kupika chakula na biashara zingine.

“Takribani mifuko ya simenti milioni, 9,200,000 ambayo ni sawa na tani 600, nondo kilo milioni 115 sawa na tani 1500 na mataluma 1,400,000, kutoka kwa wasambazaji wa malighafi hizo takribani 500, wafanyakazi 10, 000, huku asilimia 94 ya wafanyakzi hao ni watanzania, pia asilimia 48 ya wataalam ni watanzania, kwa hiyo pamoja na mradi huu  kuwa nguzo imara ya usafirishaji nchini, SGR imekuja kutoa Fursa za ajira kwa watanzania”, Alisema Kadogosa.
Kadogosa alisema kuwa mradi huo ni mkubwa na uwezo wake ni wa juu, na sasa matatizo ya usafarishaji nchini yatapata suluhu kubwa, kuimarisha na kulinda barabara nchini.

Katika sekta ya usafirishaji wa mizigo hasa ile mikubwa inayotoka bandarini kwenda sehemu zingine za nchi na mengine nje ya nchi, kwani kuwepo kwa Reli imara itasababisha utendaji kazi wa bandari kuwa na ufanisi mkubwa, “Bandari inategemea kuwepo kwa miundombinu imara kwa upande wa nchi kavu, hakuna ufanisi wa Bandari bila kuwa na Reli imara, Serikali imeliona hilo ndiyo maana ikaamua kutekeleza haraka ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) na Reli yetu hii inabeba mizigo mingi Takribani Tani Milioni 17 kwa mwaka, hakuna Reli kama hii Barani Afrika” Kadogosa.

Mifuko Ya Fidia Kwa Wafanyakazi Ya Zambia Na Tanzania Yasaini Mkataba Wa Ushirikiano

$
0
0
NA Mwandishi wetu, Dodoma
TANZANIA na Zambia kupitia Mifuko ya Fidia kwa Wafanyakazi, wamesaini mkataba wa ushirikiano utakaosaidia kubadilishana uzoefu kati ya mifuko hiyo.

Akizungumza mara baada ya kutiliana saini mkataba huo, kwenye ofisi za WCF jijini Dodoma Jumatatu Mei 27, 2019, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bw. Masha Mshomba alisema, Zambia inauzoefu wa zaidi ya miaka 40 katika sekta ya hifadhi ya jamii katika kulipa mafao ya Fidia kwa Wfanyakazi kwa hivyo makubaliano hayo yana manufaa makubwa.

Alisema makubaliano hayo ni ya kawaida kati ya mifuko na kwamba WCF na WCFCB watabadilishana uzoefu katika masuala ya namna ya ulipaji mafao, namna ya kuzuia ajali na magonjwa kazini kwa sababu mambo hayo ni muhimu sana katika mifuko ya fidia.

“Nguvu kazi ya taifa inapolindwa tija huongezeka makazini na jambo hili hudhihirika pale pato la taifa linaongezeka hususan kwetu sisi ambao tunajenga uchumi wa viwanda jambo hilo ni muhimu sana.”Alisema Bw. Mshomba.

Alisema kwa uzoefu ambao Zambia watakuwa wameupata kutoka kwao wataweza kuboresha huduma zao, na tayari Dkt. Nkumbula amethibitisha kuwa serikali ya Zambia inautegemea Mfuko huo katika kusaidia nguvu kazi ya taifa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi Zambia (WCFCB), Dkt. Elizabeth Lungu Nkumbula alisema, imekuwa ni siku njema kwao kwa kujenga ushirikiano wa pamoja katika eneo la hifadhi ya jamii.

“Zambai na Tanzania chini ya uongozi wa Dkt. Keneth Kaunda na Mwalimu Nyerere, waliweza kujenga reli ya TAZARA na bomba la mafuta TAZAMA kwa hivyo ushirikiano huu wa leo ni kumbukumbu ya ushirikiano uliojengwa kwa muda mrefu na viongozi hao wa mataifa hayo mawili.” Alifafanua.

AlIsema ushirikiano huu utasaidia pande mbili kubadilishana uzoefu katika kutoa huduma za ulipaji fidia na mbinu za kuzuia majanga yatokanayo na kazi na hivyo kusaidia mataifa hayo kukuza uchumi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images