Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mnyika Ataka Baraza la Mawaziri Livunjwe

$
0
0
Mbunge wa Kibamba John Mnyika (Chadema) ,amemwomba Rais Dk.John Magufuli alivunje Baraza la Mawaziri kwa kumshauri vibaya katika suala la Korosho.

Kauli hiyo ameitoa leo bungeni Mei 20 wakati akichangia mjadala wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, kwa mwaka wa fedha 2018-2019.

Mnyika amesema Baraza la Mawaziri linatakiwa kuwajibishwa kwa kumshauri vibaya Rais Dk.John Magufuli katika suala la Korosho kwani kwa sasa Korosho inaoza kutokana na kukosekana kwa wanunuzi.

Selasini Amshauri Spika Job Ndugai kuunda kamati ya wabunge ikague maghala ya kuhifadhi korosho ili kubaini nzima na zilizooza.

$
0
0
Mbunge wa Rombo (Chadema), Joseph Selasini amemshauri Spika Job Ndugai  kuunda kamati ya wabunge wachache ikague maghala ya kuhifadhi korosho ili kubaini nzima na zilizooza.

Kaimu Mnadhimu huyo wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Mei 20, 2019 katika mjadala wa bajeti ya Wizara ya Kilimo mwaka 2019/2020.

Huku akimsifu Ndugai kwa kuunda kamati zilizochunguza masuala mbalimbali ikiwemo ya madini ya Tanzanite, Selasini amesema, “Nimeitazama picha ya Rais akiwa ameshika paji la uso anaonyesha kutafakari sana.

“Inaonekana Rais ana mawazo mengi. Kazi ya Bunge hili ni kuishauri Serikali. Kazi ya Bunge hili ni kuisimamia Serikali tunafanya makosa makubwa sana kufanya siasa ndani ya Bunge hili.”

Huku akieleza kuwa yeye ni msafirishaji wa korosho, amesema zao hilo huoza kama  vitunguu

“Nimetangulia kukusifu Spika kama kuna ubishi wa korosho zimeoza ama hazijaoza tengeneza kamati ya watu wachache waende wakague kwenye maghala. Nataka nikwambie kuwa korosho imeoza kwa asilimia 30. Weka watu wakakague maana tukiendelea kuzubaa hata zilizopo zitaoza tutapata hasara zaidi.”

Mdude CHADEMA ataja sababu ya Yeye Kutekwa na Wasiojulikana

$
0
0
Mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mdude Nyagali amesema licha ya kupotea hivi karibuni kwa kile alichokidai kuwa ni kutokana na misimamo yake, alifikia hatua ya kukata tamaa ya kuishi.

Mdude ametoa kauli hiyo jijini Dar es salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari, ambapo ameeleza namna tukio hilo lilivyotokea.
 
"Mimi nilikata tamaa ya kuendelea kuishi na nilishaomba sala ili Mungu aipokee roho yangu, mwacheni Mungu aitwe Mungu, Mungu ni fundi", amesema Mdude.

Aidha Mdude amesema kuwa, "moja ya vitu ambavyo vinashangaza, sikuguswa maeneo mengine zaidi ya kupigwa kichwani lakini cha kushangaza zaidi, baada ya kupata fahamu nikakutwa nina majeraha mikononi na kwa mujibu wa wataalamu ni majeraha yalitokana na kufungwa pingu".

"Vitu vinavyothibitisha kuwa tukio langu la kutekwa ni la kisiasa, ni tweets zangu za mara ya mwisho kuhusu yule wakili aliyepotea", ameongeza Mdude.

Katika mkutano huo na wanahabari Mdude alimwaga machozi wakati akizungumzia namna alivyojikuta yupo porini baada ya waliomteka kumtupa.

“Nilijiuliza kosa langu ni lipi katika nchi hii na kama nina kosa mahakama si zipo kwa nini nifanyiwe hivi,” amesema Mdude huku akilia.

Mapema wiki mbili zilizopita zilienea taarifa juu ya kupotea kwa mwanachama huyo wa CHADEMA, lakini baadaye alipatikana wilayani Mbozi mkoani Mbeya akiwa hajitambui.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya May 21

Basi la Arusha Express lateketea kwa moto

$
0
0
Basi la kampuni ya Arusha Express linalofanya safari zake kati ya Bukoba na Arusha limeungua moto asubuhi ya leo katika maeneo ya Kibeta, Manispaa ya Bukoba. 

Hakuna madhara kwa binadamu yaliyoripotiwa wala chanzo cha moto huo hakijajulikana.

Iran yasema Marekani haiwezi kuiangamiza

$
0
0
Waziri wa mambo ya nje wa Iran Mohammed Javad Zarif amesema kile alichokiita ''kejeli za maangamizi'' za rais wa Marekani Donald Trump haziwezi kuimaliza Iran. 

Kupitia mtandao wa Twitter, Zarif amesema Iran imesimama imara kwa maelfu ya miaka, wakati maadui wake wote wakiwa wametoweka. 

Haya Zarif anayasema wakati mvutano ukizidi kushamiri baina ya nchi yake na Marekani, na onyo la Trump kwamba ikiwa Iran haitaacha kuitishia Marekani, basi mwisho rasmi wa Iran utakuwa umewadia. 

Mahusiano baina ya nchi hizo mbili yalizidi kuzorota mwaka jana baada ya Rais Trump kuiondoa Marekani katika makubaliano kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran, yaliyosainiwa mwaka 2015 kati ya taifa hilo la Kiislamu na nchi zenye nguvu duniani. 

Mvutano huo ulichukuwa sura mpya mwezi huu pale Marekani ilipopeleka katika eneo la Ghuba manowari na ndege za kivita chapa B-52 kujibu ilichokitaja kuwa kitisho kutoka Iran ambacho haikukifafanua.

Video Mpya: Lava Lava ft. Salha - Hatuachani

$
0
0
Msanii wa muziki nchini, Lava Lava anakukaribisha kutazama video ya wimbo wake unaokwenda kwa jina la Hatuachani. Itazame hapa.

Video ya Dayna Nyange – Dua


Kauli ya Masele baada ya Kuhojiwa...."Sijawahi kukurupuka, nasimamia haki na najitambua"

$
0
0
Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge imemhoji mbunge wa Shinyanga Mjini (CCM), Stephen Masele kuhusu tuhuma zinazomkabili za utovu wa nidhamu.

Masele alihojiwa na kamati hiyo inayoongozwa na  Emmanuel Mwakasaka  jana Jumatatu Mei 20, 2019.

Mara baada ya kutoka katika mahojiano Masele alizungumza na wanahabari, “Mimi ninaheshimu  sana viongozi wangu, nimelelewa vizuri na wazazi, nimelelewa vizuri na chama changu, nimetokea umoja wa vijana kuanzia ngazi ya chini kabisa mpaka ngazi ya kitaifa na kuwa mjumbe wa baraza kuu Taifa, nimekuwa mbunge hii awamu ya pili.

“Nimekuwa naibu waziri  natambua miiko ya uongozi, sijawahi kukurupuka, fuatilia rekodi zangu chochote ninachokisema ninasimamia haki, ukweli na ninaheshimu viongozi wenzangu.

“Ni matarajio yangu haki itatendeka na mimi sijafanya jambo lolote kinyume na taratibu, kwenye kazi zangu ndani ya Bunge na pia Bunge la Afrika kama makamu wa rais.”

Kuhusu utovu wa nidhamu amesema, “Nawahakikishia Watanzania, nilichokuwa nasimamia ni misingi ya haki za binadamu na kufanya hivyo nisitafsiriwe kwamba ni utovu wa nidhamu.”

RC Makonda atoa Sadaka zaidi ya misikiti 1,000

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Mhe. Paul Makonda leo amewakabidhi shehena ya viungo vya kutengeneza futari kwa maimamu, mashehe na viongozi wa Dini ya Kislamu kutoka Misikiti zaidi ya 1,000 kama sehemu ya sadaka na shukrani ya Amani na Utulivu ndani ya mkoa huo.

Miongoni mwa vitu alivyokabidhi RC Makonda ni Mchele, Sukari, Unga, Maharage, Mafuta na vitu mbalimbali kwaajili ya kuwawezesha viongozi hao kufurahia futari majumbani mwao.

RC Makonda amewashukuru viongozi wa dini kwa kuwa wasimamizi wazuri wa Amani na mshikamano ndani ya mkoa huo jambo linalofanya mkoa huo kuendelea kuwa kisima cha Amani.

Hata hivyo RC Makonda amewaeleza Viongozi wa Dini kuwa namna bora ya kumuunga mkono Rais Dkt. John Magufuli na kumuombea ni kuhakikisha waumini wao wanajiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ili wachague viongozi wa serikali za mitaa wanaochukia Rushwa.

Aidha RC Makonda amemshukuru Balozi wa Falme za Kiarabu kwa kumkabidhi misaada hiyo huku akiwasihi waislamu kutumia mfungo huu Kuliombea taifa na viongozi pamoja na kuwahimiza wazazi kuwalea watoto katika malezi bora.

Kwa upande wake Balozi mdogo wa Falme za Kiarabu amesema wameamua kumuunga mkono RC Makonda kwakuwa wanamuamini akipokea kitu kinawafikia walengwa na amekuwa mtu wa kuwasaidia watu wasiojiweza bila kujali dini wala kabila.

Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Unaotokana Na Kisukari (Diabetic Nephropathy)

$
0
0
Ugonjwa wa kisukari (Diabetes Mellitus) huambatana na ongezeko la sukari(glucose) katika damu kwa kiwango kinachozidi kawaida. 

Homoni aina ya insulin ambayo hutolewa na kongosho ama hushindwa kufanya kazi yake vema kwa sababu ya kasoro za seli au hutolewa kwa kiasi kisicho kidhi uhitaji wa kuratibu sukari katika damu. 

Kwa hivyo sukari hubaki katika damu kwa wingi na kuleta madhara kadhaa.Wagonjwa wa kisukari pia huweza kuwa na kiwango kikubwa cha lehemu (cholesterol) katika damu. Na zaidi huweza kuwa na tatizo la mgandamizo wa damu (hypertension) au presha. Asilimia 55 ya wanaume wenye kisukari hupatwa na tatizo la nguvu za kiume.

Mambo haya matatu, Sukari, lehemu (Cholesterol) na Mgandamizo wa damu, Huweza kusababisha upungufu wa nguvu za kiume.(Erection dysfunction).

1. Sukari.
Sukari nyingi katika damu huweza kupelekea kuharibiwa kwa kuta za mishipa ya damu. Kisha kuta hizi hushindwa kuzalisha homoni aina ya Nitrogen Oxide ambayo husaidia kutanua mirija ya damu kwa ajili ya kupitisha damu kwa ufasaha. Ikitokea katika mirija ya damu inayotiririsha katika uume kushindwa kutanuka vema, ni wazi kuwa uume utapungua uimara wake.

2. Lehemu (Cholesterol).
Lehemu huganda kwenye kuta za mirija ya damu mithiri ya mafuta yanavyoganda katika chupa. Hali hii hupelekea kupungua kipenyo (diameter) cha mirija ya damu na kushindwa kupitisha damu vizuri.

3. Mgandamizo wa damu au Presha (Hypertension).
Katika hali hii moyo hushindwa kusukuma damu vizuri na hivyo kupungua kwa kasi na ujazo wa damu katika maeneo yaliopo mbali na moyo, ikiwa ni pamoja na viungo vya uzazi.

Pia, Mishipa ya fahamu (nerves) au Neva za fahamu huweza kuharibiwa na kupunguza ufanisi wake.Katika hali hii, maeneo yanayohudumiwa na neva hizo hupungua hisia na wakati mwengine kupata ganzi ya kudumu. Uume pia huweza kuathiriwa kwa namna hiyo.

 Kumbuka
Ili  mgonjwa  wa  kisukari  aweze  kupata  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, ni  lazima   apate  pia  tiba   itakayo  saidia  ku- control  sukari  kwenye  damu   yake.

Hivyo  basi ,  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  inatakiwa  kwenda   sanjari  na  tiba  ya  ku - control  sukari  kwenye  damu  ya  mgonjwa.

Hii  ina  maana  kuwa,   ili  tiba  ya  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  iweze  kufanya  kazi  barabara, ni  lazima  mgonjwa  huyo, pamoja  na   kutumia  tiba  ya  nguvu  za  kiume , apate  pia  tiba  ya  sukari.


Kama unatatizo la Kisukari, lililosababisha upungukiwe nguvu za kiume basi wasiliana nami kwa ushauri zaidi. Simu:   0757996194 au 0717339771

Polepole Ateuliwa Kuwa Mjumbe Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa

Zitto Aiomba Serikali Kuingilia Kati Dhidi Ya Vijana Wanaojipaka Oil Chafu Na Kubaka Wanawake.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Zuberi Kabwe ameiomba Serikali kuingilia kati dhidi ya baadhi ya vijana  wanaokuwa wakijipaka Oil Chafu na kuvamia wanawake  na kuwabaka   jambo ambalo ni Udhalilishaji wa kijinsia . 

Zitto ametoa ombi hilo leo Mei 21,2019  mbungeni jijini Dodoma wakati  akiwasilisha hoja ya dharura ambapo amesema suala la baadhi ya vijana kujipaka oil chafu na kuvamia wanawake  na kuwabaka limekuwa likijitokeza mara kwa mara jimboni kwake ambapo amebainisha kuwa lengo la kujipaka Oil chafu kwa vijana hao ni kurahisisha kuteleza na  kutojulikana sura zao pindi wanapokamatwa. 

Mhe.Zitto amesema mpaka sasa kuna jumla ya Matukio 43 ya unyanyasaji wa wanawake jimboni kwake tangu Mwaka 2016  na wamekuwa wakipokea vipigo mbalimbali kutoka kwa vijana hao wahuni ,hivyo kuna haja ya serikali kuingilia kati ili kulinda usalama wa wanawake. 

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya     ndani ya Nchi,Kangi Lugola amesema serikali ya Tanzania haiwezi kuvumilia vitendo vya kinyama na udhalilishaji kuendelea katika nchi ya Tanzania hivyo atahakikisha  vitendo hivyo vinadhibitiwa  

Hata hivyo,Waziri Lugola amesema kuna baadhi ya Taasisi zimekuwa zikifanya uchunguzi na kukuza mambo na kujenga hofu kwa wananchi hata kama ni madogo  hali na serikali imeshaanza kuziorodhesha taasisi hizo hali iliyoleta mvutano bungeni kati ya Waziri wa Mambo ya ndani na Zitto Kabwe. 

Mwenyekiti wa Bunge Mhe.Nagma Giga amesema suala la ubakaji sio la kuvumiliwa liwe dogo au kubwa hivyo amemwagiza Waziri wa Mambo ya ndani Kangi Lugola kushughulikia jambo hilo.


 

Serikali Yaendelea Kuwa Na Dhamira Ya Kuondoa Kero Kwa Wachimbaji Wadogo Wa Madini.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Serikali imedhamiria kuondoa kero  kwa wachimbaji wadogo  wa Madini hapa nchini  ikiwa ni pamoja na kero za kuondolewa na wachimbaji wakubwa   kwani  asilimia kubwa wachimbaji wadogo  ndio wagunduzi wa kwanza kwenye maeneo ya  Madini   . 

Hayo yamesemwa leo Mei 21,2019 bungeni jijini  Dodoma na Naibu waziri wa Madini Stanslaus Nyongo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum  Rhoda Kunchela aliyehoji serikali iko tayari kutatua kero za wachimbaji wadogo  na vibarua ambao wananyanyasika nchini. 

Katika Majibu yake  Naibu Waziri Stanslaus Nyongo amesema viongozi wanaonyanyasa wenzao serikali ipo tayari kuwafutia leseni zao huku akisema kuwa  serikali imekuwa ikiendelea kutatua migogoro ya Wachimbaji wakubwa na wadogo wanaovamia kwenye maeneo yasiyo ya kwao. 

Aidha ,Mhe.Nyongo amefafanua kuwa hata mchimba kokoto ana wajibu wa kulipia kitambulisho cha Wajasiliamali wadogo ambacho kilitolewa na Rais John Pombe Magufuli kwa ajili ya Maendeleo ya nchi. 

Waziri mwenye dhamana ya Madini, Mhe.Dotto Biteko  ametoa wito kwa watozaji wa kodi za madini zilizoondolewa Bungeni waache Mara moja  kwani imebainika kuna baadhi ya maeneo hapa nchini wanaendelea kutoza. 

Migodi yote nchini inaendeshwa kwa mujibu wa sheria ya madini ya mwaka 2010  na marekebisho yake ya mwaka 2017 na kuzingatia kanuni za uchimbaji,usalama,mazingira na Afya kwa wakazi.

 

Serikali Kupokea Mashine 60 Za Kusafishia Figo Toka Saudi Arabia

$
0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema Serikali inatarajia kupokea mashine 60 za kusafishia figo kutoka Nchini Saudi Arabia ambazo zitafungwa katika maeneo ambayo hayafikiki kirahisi.

Ameyasema hayo Leo Jumanne Mei 21 bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Kilolo, Venance Mwamoto (CCM).

Katika swali lake, Mwamoto  amedai kwamba mashine za kusafishia figo zipo sehemu chache  hapa nchini na wagonjwa wanapata shida.

Aidha Mbunge huyo amedai kwamba Serikali haioni kwamba umefika muda wa kila Hospitali ya Rufaa  kuwa na Mashine  ya kusafishia figo.

Akijibu swali hilo Ummy amekiri  kuona ongezeko ya magonjwa yasiyo ya kuambukiza ambapo amedai kwamba Serikali inatarajiwa kupata mashine 60 kutoka Serikali ya Saudi Arabia na kwamba changamoto ambayo itajitokeza ni ukosefu wa wataalamu lakini wameongea na Serikali ya Saudi Arabia kwa ajili ya kupeleka wataalamu kwaajili ya kujifunza.

TTCL yatoa gawio la Sh Bilioni 2.1 kwa Serikali

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Waziri Kindamba amesema mwaka huu wanatoa gawio la Sh2.1 bilioni kwa Serikali kutokana na kukua kwa mapato ukilinganisha na mwaka uliopita.

Ameyasema hayo leo Jumanne ya Mei 21, 2019 katika hafla ya utoaji wa gawio kwa Serikali iliyoenda sambamba na uzinduzi wa awamu ya pili ya huduma ya video conference.

Kindamba amesema katika mwaka uliopita mapato yalikuwa Sh119 bilioni na mwaka huu imefikia Sh167 bilioni.

Akizungumza na wafanyakazi wa TTCL, Magufuli amesema: “Tangu Shirikia la TTCL lianze kuendeshwa na wabia wetu, halikuwahi kutoa gawio hata la shilingi tano kwa miaka 15 na lilikuwa likipata hasara ya Tsh bil.15 kwa mwaka, lakini tangu tulirudishe kwenye mikono ya serikali, shirika hili sasa limeanza kutengeneza faida kubwa.

“Niseme kwa uwazi, TTCL mmekuwa mkipigwa vita sana, vita zingine sio za uwazi ni vita vya chinichini, hata leo kuja hapa kulikuwa na mbinu za kijanja-kijanja kunizuia nisije kupokea gawio, na zimechezwa kwelikweli, hii inathibitisha kuwa nyinyi mnastahili,  lazima tuwasaidie.

“Waziri amesema Mfuko wa Mawasiliano upo chini ya wizara yake, pesa zinachangwa na Watanzania na TTCL ni ya Watanzania, kwa nini inakodi minara ya mashirika mengine na kulipia Sh mil. 700 hadi mil. 800?   Kwa nini usitumie pesa hizo kujenga minara ukawapa TTCL moja kwa moja?

“Mashirika mengine yanalipia kodi, lakini TTCL wanalipa kodi na wanalipa gawio, kwa hiyo faida itayakopatikana itakuwa ni ya serikali, hakuna haja ya kuwaacha TTCL wakateseka, huwezi kumuacha mwanao anateseka na chakula unawapa watu wengine,  lazima tuisaidie TTCL.

“Naomba niletewe orodha ya viongozi ambao wanatumia laini za TTCL na sio ziwepo tu bila kutumika, huwezi kulipwa mshahara wa Serikali na hutumii mtandao huo, asije akawa anaandika meseji tu halafu anaicha, nataka ziwe zinatumika, sijamaanisha msitumie mitandao mingine. Msajili wa Hazina hakikisha ifikapo mwezi Julai, mashirika yote 253 nchini ambayo yamekuwa hayatoi gawio kwa serikali, yawe yametoa gawio la sivyo yafungwe.

“Taasisi zilizojiunga kutumia TTCL, ofisi yangu ya rais haikutajwa, chama changu CCM hakikutajwa, inaonekana hawa hata kwenye ofisi yangu wamo. Kama wananisikia ninataka ndani ya mwezi mmoja tuanze kutumia simu za TTCL na wizara nyingine,” amesema.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521

Rais Magufuli Aiagiza UCSAF Kuiwezesha Miundombinu Ya Mawasiliano TTCL

$
0
0
Na Paschal Dotto
RAIS Dkt. John Magufuli ameitaka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kutoa kipaumbele katika uwekezaji wa miundombinu ya mawasiliano kwa Kampuni ya Mawasiliano Nchini (TTCL) ili liweze kumiliki idadi kubwa ya minara ya mawasiliano ya simu  na kumudu ushindani wa soko la mawasiliano nchini. 

Akizungumza katika hafla ya upokeaji wa Gawio la Serikali la Tsh Bilioni 2.1 kutoka TTCL, leo Jumanne (Mei 21, 2019), Rais Magufuli alisema  njia pekee ya kuiendeleza TTCL ni kwa Viongozi na Watendaji wa Serikali kuwa na moyo wa uzalendo wa kusimamia rasilamali za umma ikiwamo za shirika hilo. 

Kwa mujibu wa Rais Magufuli alisema TTCL imekuwa ikitumia kiasi cha Tsh Milioni 700-800 kila mwezi kwa ajili ya kukodisha minara ya mawasiliano, wakati Serikali ina mfuko wa mawasiliano kwa Wote (UCSAF) unaotoa ruzuku kwa makampuni mbalimbali ya mawasiliano kwa ajili ya kujiwekeza katika miundombinu ikiwemo minara ya mawasiliano maeneo mbalimbali nchini. 

“Hili la TTCL kukopa minara katika makampuni mengine halikubaliki,  Serikali ina mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) ambao wanatoa ruzuku kwa makampuni mengine ya simu lazima tulitazame upya, nataka sasa TTCL tuwape mitaji ya kutosha ili kuhakikisha kuwa linaendelea kupanua huduma zake kwa Watanzania wengi zaidi” alisema Rais Magufuli. 

Aidha Rais Magufuli aliitaka Wizara ya Fedha na Mipango kuhakikisha inaipatia TTCL kiasi cha Tsh Bilioni 30 kilichobaki kati ya Tsh Bilioni 66 ilizotoa katika mwaka wa fedha 2018/19 kwa ajili ya kupanua mtandao wa huduma zake nchini, kwa kuwa Shirika hilo limeonesha mafanikio makubwa zaidi katika kipindi kifupi tangu serikali ichukue uamuzi wa kununua hisa zake kutoka kampuni ya Airtel mwaka 2016. 

Akifafanua zaidi Rais Magufuli alisema Serikali itandelea kuiwezesha TTCL ili iweze kupanua mtandao wa mawasiliano yake nchini, na kuhakikisha kuwa linatekeleza vyema majukumu yake ikiwemo kusimamia mawasiliano ya Kimkakati nchini kupitia Mkongo wa Mawasiliano wa Taifa kufuatia kupitishwa kwa Sera ya Taifa ya TEHAMA mwaka 2016. 

Kwa upande wake Mkurugenzi  Mkuu wa TTCL, Waziri Kindamba alisema TTCL imeendelea kupiga hatua kubwa zaidi katika utoaji wa huduma ya mawasiliano nchini ambapo katika mwaka 2018/19, shirika hilo limeweza kupata faida ya Tsh Bilioni 8.3 ambapo kiasi cha Tsh Bilioni 2.1 imetoa gawio kwa Serikali. 

“Katika mwaka 2017/18, tulitoa Tsh Bilioni 1.5, lakini kwa mwaka huu tumetoa Tsh Bilioni 2.1 ikiwa ni ongezeko la Tsh Milioni 600, hii imetokana na kuongezeka kwa makusanyo ya mapato yetu kutoka Bilioni 119 mwaka 2017/18 hadi kufikia Bilioni 167 mwaka 2018/19” alisema Kindamba. 

Kwa  mujibu wa Kindamba alisema TTCL pia imeendelea kusimamia majukumu yake ya msingi ya ikiwemo kuimarisha mfumo wa viwango vya huduma kwa mteja, kujenga uwezo wa teknolojia na miundombinu pamoja na kusimamia mkakati wa mawasiliano kupitia Mkongo wa Mawasiliano wa Taifa. 

Kindammba anasema katika kuwajengea uwezo vijana katika kujiajiri, TTCL kwa kushirikiana na Ofisi ysa Waziri Mkuu imeweza kuajiri vijana 50 waliomaliza vyuo vikuu mbalimbali nchini ambao baadae wataweza kuajiriwa na makampuni mbalimbali ya mawasiliano nchini kwa ajili ya kuongeza mtandao wa utoaji wa huduma ya mawasiliano nchini. 

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Mhandisi Omary Nundu aliishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kutokana na uwekezaji mkubwa unaoendelea kufanywa kwani katika kipindi cha miaka mitatu, shirika hilo limeweza kupata mafanikio makubwa kutokana na maono na dhamira ya Rais Dkt. John Magufuli   kwa shirika hilo.

Rais Magufuli Atoa Maagizo Mazito kwa Mashirika Yasiyotoa Gawio kwa Serikali

$
0
0
Rais Magufuli ameyataka mashirika na Taasisi zinazotakiwa kutoa gawio kulingana na sheria kuhakikisha hadi kufikia mwei Julai mwaka huu wawe wameshakamilisha zoezi hilo.

Ameyasema hayo leo Jumanne Mei 21 Jijini Dar es salaam wakati akizungumza katika hafla ya kukabidhi gawio kwa serikali kutoka shirika la masiliano Tanzania TTCL ambapo ameagiza mashirika hayo kuchukuliwa sheria iwapo watashindwa kutekeleza agizo hilo.

“Mashirika ambayo hayatoi gawio kila siku ni hasara tu itabidi kutumia sheria na ikishindikana yaondoke maana haiwezekani wao wanaangalia wenzao wakati walipewa mashirika hayo sawa na bure hivyo kabla ya mwezi Julai mashirika yote 253 yanatakiwa yawe yameshafanya hivyo ” amesema.

“Fedha hizi ni ndizo zinazosaidia katika shughuli mbalimbali za kijamii kama vile ujenzi wa barabara, hospitali shule hivyo kwa wale wote wanaotakiwa kutoa gawio kulingana na sheria wanapaswa kufanya hivyo,” amesema.

Aidha ametoa wito kwa watanzania kuendela kuliunga mkono shirika la TTCL kwa kusema kuwa ni la nyumbani lakini pia mapato na faida zitakazopatikana zitatumika kuwasaidia watanzania na kwamba ndio nembo pekee ya kumkumbuka baba wa taifa Mwalimu Julius Nyerere.

Uharibifu wa mazingira waishusha Tanzania hadi nafasi ya 8 vivutio vya dunia

$
0
0
Waziri wa Malisili na Utalii Dk. Hamisi Kigwangala amesema Tanzania imeshuka kutoka nafasi ya pili mpaka ya nane katika vivutio vya dunia sababu akizitaja ni uharibifu wa mazingira.

Ameeleza hayo leo Jumanne Mei 21 bungeni wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Vunjo James Mbatia (NCCR Mageuzi).

Katika swali lake Mbatia amedai kwamba mwaka 1984 Tanzania ilikuwa inashika nafasi ya pili katika vivutio vinavyochea utalii pamoja na miundombinu.

Mbunge huyo amehoji Je kwa sasa Tanzania inashika nafasi ya ngapi na miundombinu inayochochea inashika nafasi ya ngapi?

Akijibu swali hilo Kingwangala amesema utafiti unaonesha kwamba Tanzania imeshuka katika vivutio  kutoka  nafasi ya pili mpaka ya nane sababu kubwa ni uharibifu wa mazingira.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images