Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Mkuu Aongoza Mazishi Ya Askofu Mmole Mtwara

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa wito kwa Watanzania wote wamuenzi marehemu Askofu Mstaafu Gaberiel Mmole (80) wa Jimbo Katoliki Mtwara kwa wema, upole  na utumishi mwema aliouonesha wakati wote wa maisha yake.

Ametoa wito huo leo (Jumanne, Mei 21, 2019) wakati wa mazishi ya Askofu Mmole yaliyofanyika katika Kanisa Katoliki Mtwara na kuhudhuriwa na viongozi, waumini wa Kanisa Katoliki pamoja na wakazi wa mkoa wa Mtwara

Askofu Mmole alizaliwa Januari Mosi, 1939 katika Parokia ya Nangoo, ambapo alibatizwa na kupata kipaimara Oktoba 5, 1952. Mwaka 1971 alipata daraja ya upadre na kuwa Askofu kuanzia mwaka 1988, alifariki Mei 15, 2019 Mkoani Mtwara baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Maeneo aliyoyatumikia tangu apate daraja la padri ni Paroko msaidizi wa Mnero (1972), Pastoral Institute GABA-Uganda (1973), Gombera Namupa seminari (1974 hadi Mei 1988), alitangazwa kuwa askofu wa Jimbo la Mtwara Machi 12, 1988 na alisimikwa kuwa askofu wa Jimbo la Mtwara Mei 25, 1988.

Mwaka 1951 hadi 1954 alipata elimu ya singi katika shule ya msingi Ndanda, 1955 alisoma Nyangao Middle School, 1956 akahamia Lukuledi ambako alihitimu 1958. Alienda chuo cha ualimu Peramiho 1959 hadi 1960, ambapo 1962 alijiunga na seminari ndogo ya Namupa na alihitimu 1964.

1965 hadi 1966 alichukua masomo ya falsafa kwenye seminari kuu ya Peramiho na mwaka 1967 hadi 1971 alichukua masomo ya theolojia katika seminari hiyo hiyo ya Peramiho. 1971 alifanya mitihani ya Baccalaureate inayotoka chuo kikuu cha Kipapa Urbaniana Roma na kupata shahada ya theolojia.

Ibada ya mazishi imeongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo la Songea, Mhashamu Askofu Damian Dallu ambaye alitumia muda huo kuwaasa Watanzania kuishi katika maadili mema na kuheshimiana.

Waziri Mkuu amesema enzi za uhai wake Askofu Mmole alitoa kipaumbele katika masuala muhimu ya maendeleo ya jamii ikiwemo elimu ambapo alisaidia sana watawa waliomaliza darasa la saba na kuwasaidia wajiunge na shule za sekondari.

“Hata uanzishwaji wa chuo kikuu cha STEMMUCO ambacho ni tawi la SAUT hapa Mtwara ni moja ya jitihada zake alizozifanya katika kuhakikisha anawapa elimu bora vijana na jamii.

Kifo chake ni pigo kubwa kwa Taifa kwa sababu tumepoteza kiongozi wa kiroho aliyesimamia kwa uadilifu ustawi wa jamii ya Kitanzania.”

Kwa upande wake, Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania, Mhashamu Askofu Gervas Nyaisonga wa Jimbo Kuu la Mbeya amesema wamepata simanzi kubwa kufuatia kifo cha Askofu Mmole kwani walitegemea hekima zake katika Baraza la Maaskofu.

Ameongeza kuwa Askofu Mmole alikuwa kielelezo cha dhamira njema na alilitumikia kanisa katika hali yoyote, hivyo yatupasa kumuombea apumzike kwa amani.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwaaliwashukuru viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini mkoani Mtwara kutokana kwa ushirikiano mzuri anaopata unaomwezesha kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

Mazishi hayo yamehudhuriwa na maelfu ya wananchi, maaskofu wa majimbo mbalimbali nchini, Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mheshimiwa Benjamin Mkapa na mkewe Mama Anna Mkapa, Waziri wa Nchi OR-Utumishi na Utawala Bora Mheshimiwa Huruma George Mkuchika.
 

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya May 22

Marekani yalegeza vikwazo dhidi ya kampuni ya Huawei

$
0
0
Serikali ya Marekani imeondoa kwa muda vikwazo vya kibiashara ilivyoweka wiki iliyopita dhidi ya kampuni ya simu ya China Huawei, hatua inayolenga kupunguza hali ya kuvurugwa wateja wake. 

Hatua hiyo hata hivyo imepuuziliwa mbali na muasisi wa kampuni hiyo anayesema kuwa Huawei ilikuwa imejiandaa kwa hatua ya Marekani. 

Wizara ya Biashara ya Marekani itairuhusu kampuni ya Huawei kununua bidhaa zinazotengenezwa Marekani kwa siku nyingine 90 ili kudumisha mitandao iliyopo na kutoa programu tumishi mpya kwa simu za sasa za Huawei. 

Kampuni hiyo kubwa kabisa duniani ya kutengeneza vifaa vya mawasiliano ya simu bado imezuiwa kununua vifaa kutoka nchini Marekani vya kutengenezea bidhaa mpya bila idhini za leseni ambazo kuna uwezekano kuwa zitakataliwa. 

Serikali ya Marekani ilisema iliweka vikwazo hivyo kwa sababu ya Huawei kujihusisha na shughuli zinazoenda kinyume na usalama wa taifa au maslahi ya sera za kigeni.

Irani Yakataa Mazungumzo na Marekani

$
0
0
Rais Hassan Rouhani wa Iran amekataa mazungumzo na Marekani, baada ya Rais Donald Trump kusema kuwa Iran itampigia simu na kuomba kufanya mazungumzo "iwapo na wakati watakapokuwa tayari". 

Iran na Marekani zimeendeleza vita vya maneno katika wiki za karibuni wakati Marekani ikiimarisha vikwazo na kile inachosema ni lengo la kuishinikiza Iran kufanya makubaliano mengine mbali na masharti ya mkataba wake wa nyuklia wa 2015.

Shirika la habari la serikali ya Iran limemnukuu Rouhani akisema kuwa hali ya sasa sio nzuri kwa mazungumzo na chaguo lao kwa sasa ni kuyakataa. 

Trump alisema jana kuwa Iran itakabiliwa vikali kama itajaribu kufanya chochote dhidi ya maslahi ya Marekani katika Mashariki ya Kati. 

Alisema ripoti kuwa Marekani inajaribu kuanzisha mazungumzo na Iran ni za uwongo, lakini akaongeza kuwa Iran itawasiliana nao iwapo, ama lini watakapokuwa tayari. Rouhani amesema Wairan hawatawahi kumpigia magoti mnyanyasaji.

Tundu Lissu Kurejea Nchini Septemba 7

$
0
0
Mbunge Tundu Lissu amesema atarejea nchini Septemba 7, 2019, siku ambayo itatimia miaka miwili tangu aliposhambuliwa kwa risasi jijini Dodoma Septemba 7, 2017, Lissu ambaye yuko nchini Ubelgiji kwa matibabu alishambuliwa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana.

Mara baada ya kushambulia, mwanasiasa huyo  alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma na usiku wa siku hiyo alihamishiwa Hospitali ya Nairobi nchini Kenya alikopata matibabu hadi Januari 6, 2018 na kuhamishiwa  Ubelgiji kuendelea na matibabu zaidi.

Lissu ambaye kwa sasa anatembea kwa msaada wa gongo moja akizungumza na wapiga kura wake mwishoni mwa wiki kupitia simu ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema anarudi nchini Septemba 7, 2019.

Amesema katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Oktoba, 2019 atakuwepo Tanzania.

Rais Magufuli Atoa Heshima Za Mwisho Kwa Mwili Wa Marehemu Brigedia Jenerali Mstaafu Athumani Hassan Ngwilizi Lugalo Jijini Dar Es Salaam

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiandika katika kitabu cha maombolezo mara baada ya kuwasili katika Hospitali kuu ya Jeshi ya Lugalo Jijini Dar es Salaam Mei 22,2019 kwaajili ya kuaga mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Mstaafu Athuman Hassan Ngwilizi aliyefariki dunia hospitalini hapo Mei 20,2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Mstaafu Athuman Hassan Ngwilizi katika Hospitali kuu ya Jeshi ya Lugalo Jijini Dar es Salaam Mei 22,2019 ,Marehemu alifariki dunia hospitalini hapo Mei 20,2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Shekhe Mkuu wa Dsm Alhaji Mussa Salum baada ya kuwasili katika Hospitali kuu ya Jeshi ya Lugalo Jijini Dar es Salaam Mei 22,2019 kwaajili ya kuaga mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Mstaafu Athuman Hassan Ngwilizi aliyefariki dunia hospitalini hapo Mei 20, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo mara baada ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Mstaafu Athuman Hassan Ngwilizi katika Hospitali kuu ya Jeshi ya Lugalo Jijini Dar es Salaam Mei 22,2019 ,Marehemu alifariki dunia hospitalini hapo Mei 20, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameungana na Viongozi wengine na ndugu kusindikiza kwenye gari mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Athuman Hassan Ngwilizi kutoka katika Hospitali kuu ya Jeshi ya Lugalo Jijini Dar es Salaam Mei 22,2019 kuelekea Mlalo Lushoto Mkoani Tanga kwaajili ya mazishi ,Marehemu alifariki dunia hospitalini hapo Mei 20,2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa pole kwa Mjane wa Marehemu mara baada ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Athuman Hassan Ngwilizi katika Hospitali kuu ya Jeshi ya Lugalo Jijini Dar es Salaam Mei 22,2019 ,Marehemu alifariki dunia hospitalini hapo Mei 20, 2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa pole kwa Familia ya  Marehemu mara baada ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Brigedia Jener ali Athuman Hassan Ngwilizi katika Hospitali kuu ya Jeshi ya Lugalo Jijini Dar es Salaam Mei 22,2019 ,Marehemu alifariki dunia hospitalini hapo Mei 20, 2019.

PICHA NA IKULU

Umoja Wa Wazalishaji Mifuko Mbadala Wawatoa Hofu Watanzania

$
0
0
Na Mwandishi Wetu,MAELEZO
UMOJA wa Wazalishaji wa Mifuko Mbadala Nchini imewaondoa hofu Watanzania na kusema kuwa vipo viwanda vya kutosha vya kuzalisha mifuko hiyo hapa nchini na hivyo kuweza kutosheleza mahitaji ya soko ya bidhaa hiyo ifikapo Juni Mosi, mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa vyombo vya habari leo Jumatano (Mei 22, 2019) Jijini Dar es Salaam kuhusu Mipango na  Mikakati ya Umoja huo katika uzalishaji wa mifuko mbadala nchini, Mwakilishi wa Umoja huo Allan Ngumbuke  alisema Watanzania hawana budi kubadili mtazamo kuhusu matumizi ya mifuko ya plastiki inayoisha matumizi yake Mei 31, mwaka huu.

Aliongeza kuwa mara baada ya Serikali kutoa Tamko kuhusu Katazo la Mifuko ya plastiki ifikapo Mei 31, mwaka huu na kuanza kutumika kwa mifuko mbadala kuanzia Juni Mosi, mwaka huu Umoja huo walijipanga kikamilifu kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kwa ajili ya kutoa elimu na mafunzo mbalimbali, ili kuwafanya Watanzania kuona kuwa mifuko mbadala ni sehemu ya kujiongezea kipato.

“Baada ya katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki, wazalishaji wa mifuko mbadala wameongeza kasi ya uzalishaji na wengi wameshaagiza mashine zipo njiani kuja na nyingine zinatengeneza mifuko mbadala, mfano hai ni Tanpak Tissue Paper Ltd, Hanpal, Green Earth Paper Products Ltd, Harsho Group” alisema Ngumbuke.

Kwa mujibu wa Ngumbike alisema uzalishaji wa mifuko mbadala utaibua viwanda vingi vya nyumbani, kwani teknolojia yake ni rahisi na pia mifuko hiyo inayozingatia utunzaji wa  mazingira ipo ya aina nyingi na itakuwepo ya kutosha kuendana na mahitaji ya soko na ukuaji wa uchumi na hivyo kuendelea kuhudumia soko la ndani na nje ya nchi.

Aidha Ngumbuke aliwataka wadau na wananchi wanaotaka kuwekeza kwenye mifuko mbadala kuwa zipo malighafi za kutosha zinayopatikana katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo kwa malighafi ya karatasi inayopatikana katika viwanda vya Mufindi Paper Mills Ltd na Tanpak Tissue Ltd wakati kwa upande wa malighafi ya vitambaa laini zitapatikana katika cha kiwanda cha Harsho Group kilichopo Moshi, Mkoani Kilimanjaro.

“Tunaiomba Shirika la Viwanda Vidogovidogo Nchini (SIDO) waweke kipaumbele na viatamizi vya uzalishaji wa mifuko mbadala kwa kuwa SIDO ipo nchi nzima na ni mahiri kwa kutoa mafunzo ili washiriki wake wataleta matokeo chanya na makubwa kwa haraka zaidi” alisema Ngumbuke.

Kwa upande wake Afisa Tawala wa Kiwanda cha Tanpak Tissue Ltd, Michael Mjungu alisema kiwanda chake kimejipanga kikamilifu kuzalisha malighafi za kutosha kwa ajili ya uzalishaji wa mifuko hiyo na kuwataka wafanyabiashara kuondoa hofu kuhusu uwezo wa viwanda vya ndani ya Tanzania kuweza kuzalisha mifuko mbadala.

Mlinga ahoji Kondom kutolewa bure badala ya taulo za kike

$
0
0
Mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga (CCM) ameomba mwongozo bungeni akihoji sababu ya Serikali kutoa mipira ya kiume (Kondomu) bure badala ya kugawa taulo za kike bure kwa wanafunzi.

Mlinga ameomba mwongozo huo leo Mei 22 bungeni mara baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu.

“Mheshimiwa Spika lazima tuwe wakweli ukiangalia ufaulu idadi kubwa inayofeli ni watoto wa kike hasa kutoka maeneo ya vijiji na kitendo cha kufeli ni kutokana na kutoudhuria vizuri masomo pindi wanapokuwa katika siku zao za hedhi.

“Mheshimiwa Spika, bunge limekuwa likipiga kelele ni namna gani ya kuwasaidia watoto wa kike wapate pedi za kike bure.

“Lakini tumeshuhudia serikali ikitoa vifaa tiba bure katika makundi mbalimbali ili kuwasaidia kuepuka magonjwa mbalimbali kwa mfano tumeshuhudia ikitoa ARV, dawa za Tb bure.

“Mheshimiwa Spika Serikali inagawa mipira ya kiume bure kweli Serikali yetu inawapa kipaumbele wazinifu na kuwaacha wanafunzi, Mheshimiwa Spika naomba mwongozo wako ni kwanini isitoe pedi za kike bure,” amehoji Mlinga.

Akijibu muongozo huo Spika Ndugai amesema ni wakati muafaka wa Serikali kuzungumza na bunge kuhusina na mambo hayo.

Bil. 93.8 Zatumika Kuboresha Miundombinu ya Shule 588

$
0
0
Na: Lilian Lundo - MAELEZO, Dodoma
Katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2018/19, zaidi ya shilingi Bilioni 93.8 zimetumika katika uboreshaji wa miundombinu ya shule 588 ambapo shule  303 ni za msingi na sekondari 285.

Hayo yameelezwa leo, Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Bumbwini, Muhammed Amour Muhammed juu ya juhudi zipi za makusudi ambazo Serikali inakusudia kuchukua ili kupandisha hali ya ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha Nne.

"Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali ili kuongeza ufaulu katika ngazi mbalimbali za Elimu. Hatua hizo ni pamoja na kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia kwa kujenga na kufanya ukarabati mkubwa wa miundombinu katika shule mbalimbali za Serikali nchini," amesema Ole Nasha.

Ole Nasha amesema kuwa uboreshaji wa miundombinu uliofanyika katika shule hizo 588 umehusisha madarasa 1,190, mabweni 222, vyoo 2,141, mabwalo 76 na nyumba 99.

Ameongeza kuwa, Serikali imeendelea kusambaza vifaa vya kufundishia na kujifunzia vikiwemo, vifaa vya maabara katika shule, na vifaa vya kielimu kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Aidha Naibu Waziri Ole Nasha ameongeza kuwa katika kipindi cha mwaka 2017 hadi Aprili 2019 Serikali imeajiri jumla ya walimu 17,884 ili kukabiliana na uhaba wa walimu nchini.

Vile vile Serikali imeendelea kuimarisha Idara ya Uthibiti Ubora wa Shule kwa kununua na kusambaza magari 45 ya Uthibiti Ubora wa Shule na Pikipiki 2,897 kwa ajili ya Maafisa Elimu kata na kuongeza kuwa katika Mwaka wa Fedha 2019/2020 Serikali inatarajia kujenga ofisi 100 za wathibiti ubora wa shule na kuongeza idadi ya watumishi.

Aidha amesema ufaulu wa wanafunzi katika mtihani wa kidato cha IV umekuwa ukiongezeka mwaka hadi mwaka ambapo katika mwaka 2018 watahiniwa waliofaulu ni asilimia 78.36 ikilinganishwa na asilimia 77.09 ya mwaka 2017, asilimia 70.35 ya mwaka 2016 na asilimia 67.91 ya mwaka 2015.

Serikali Kuendelea Kuchukua Hatua Dhidi Ya Wamiliki Wa Kumbi Za Starehe Wanaopiga Muziki Mnene Na Kuwa Kero Katika Makazi Ya Watu.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Serikali imesema itaendelea kuwachukulia hatua kali za kisheria  wamiliki wa  Bar kote nchini  wanaopiga muziki mkubwa katika bar zilizokaribu na  Makazi ya watu na kusababisha kero kwa Wakazi husika na kukosa usingizi.
 
Rai hiyo imetolewa leo Mei 22,2019 na Waziri wa Ofisi ya Rais[TAMISIMI]Mhe Seleman Jafo wakati akijibu swali la mbunge wa  Viti Maalum Maryam Salum Msabaha aliyehoji ,kuna baadhi ya Bar na Club ambazo zimejengwa kwenye makazi ya watu  ambazo zimekuwa na kero kwa jamii kwa kupiga muziki mkubwa na usiozingatia  Maadili ya Kitanzania, je,nini kauli ya Serikali kuhusu Bar  na Club  ambazo zinakiuka  maadili ya jamii na sheria.
 
Katika majibu yake ,Waziri wa Ofisi ya Rais ,TAMISEMI Mhe.Seleman Jafo amesema serikali inawaelekeza wamiliki wote wa Bar na Club kuzingatia maelekezo ya  sheria ya Vileo  Na.28 ya Mwaka 1968  kifungu cha 14[1] katika uendeshaji wa shughuli zao  ambapo amesema serikali haitasita kuchukua hatua  kwa vitendo vyovyote  vitakavyobainika kukiuka sheria na kusababisha kero kwa wananchi wengine.
 
Kutokana na Bar na Club  kuwa  kero katika makazi ya Watu kwa kupiga muziki mkubwa ,Waziri Jafo amewaagiza viongozi wa Serikali za mitaa wakiwemo wakuu wa wilaya na Mikoa  kote nchini kufuatilia jambo hilo .

Naye Mbunge wa Rombo,Joseph Selasini amehoji,Mara nyingi Bar zimekuwa zikijengwa kwa kutozingatia mipango miji  na watu wenye Madaraka wakiwemo wabunge wenyewe  kwanini Serikali isitoe tamko juu ya Bar zinazojengwa Ovyo ovyo iwe Marufuku na mtu atakayetoa kibali cha ujenzi akamatwe.

Akijibu swali hilo,Waziri Seleman Jafo amesema sheria zipo na kinachotakiwa ni kusimamia sheria husika kwa viongozi wa serikali za mitaa na kufanya ufuatiliaji dhidi ya wamiliki wa Kumbi za starehe wanaokiuka sheria hizo.
MWISHO.

Tanzania Kuwa Mwenyeji Wa Zoezi La Kupima Utayari Wa Kukabiliana Na Magonjwa Ya Mlipuko Mipakani Kwa Dhana Ya Afya Moja

$
0
0
Kufuatia nchi za Kanda ya Afrika Mashariki kuwa katika hatari ya kuathirika na magonjwa ya mlipuko kama Homa ya Bonde la Ufa, Mafua Makali ya Ndege na Ebola, na kwa kuwa magonjwa hayo husambaa kutoka nchi moja kwenda nchi nyingine, Tanzania inatarajia kuandaa zoezi la Kupima Utayari wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Kukabiliana na magonjwa ya mlipuko mipakani, litakalofanyika mpakani mwa Tanzania na Kenya kwenye eneo la Namanga,  kuanzia tarehe 11 hadi 14 Juni mwaka huu.

Zoezi hilo, litazingatia Dhana ya Afya moja ambayo hujumuisha sekta ya afya ya binadamu, wanyamapori, mifugo na  mazingira katika kujiandaa, kufuatilia  na kukabili magonjwa yanayoathiri binadamu. Jumla ya washiriki 150 ambao watatoka Sekretarieti ya Afrika Mashariki, Kenya na Tanzania washiriki 130 kutoka ngazi ya taifa, mkoa na wilaya katika mpaka wa Namanga; pamoja na nchi nyingine wanachama ambapo watakuwa watazamaji ikiwa ni Uganda, Burundi, Rwanda na Sudani Kusini wanatarajiwa kushiriki zoezi hilo.

Akiongea, mjini Dodoma leo, katika kikao cha maandalizi ya zoezi hilo kwa ngazi ya Taifa, Mkurugenzi wa Kitengo cha Dharura na Majanga, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee, na Watoto, Dkt. Eliasi Kwesi,  amefafanua kuwa zoezi  hilo linalenga kufanyia majaribio ya utekelezaji wa Mipango ya Dharura ya Taifa na Kanda, Miongozo ya Utendaji na kuwapa washiriki fursa ya kujifunza namna sekta zingine zinavyotekeleza majukumu katika kuzuia na kupunguza madhara pamoja na kujiandaa kukabiliana na maafa ya magonjwa ya mlipuko.

“Zoezi hili tunalenga kutathmini utaratibu wa kutuma kikosi cha taifa cha dharura cha kukabili lakini pia  kuhakiki matumizi ya maabara zinazohamishika, kutathmini uwezo wa uchunguzi na usimamizi wa magonjwa ya mlipuko kwa vituo vilivyopo mpakani kwa magonjwa ya mifugo na binadamu; kupima hatua za kujiandaa kukabiliana katika viwanja vya kimataifa vya Jomo Kenyatta na Kilimanjaro.” Alisisitiza Dkt. Kwesi.

Kwesi alibainisha kuwa zoezi litaandaliwa kwa kuhusisha mlipuko wa virusi vinavyoshabihiana na Homa ya Bonde la Ufa katika eneo la mpakani, ambapo washiriki watahitajika kuonesha utayari wa kukabiliana na ugonjwa huo kwa kuzingatia mfumo wa Afya Moja.

Zoezi hilo linafanyika nchini Tanzania kufuatia Kikao cha 11 cha Kawaida cha Mawaziri wa Sekta ya Afya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kilichofanyika mwezi Machi, 2015, ambapo kilielekeza Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuandaa Zoezi la Nadharia la kukabiliana na magonjwa ya mlipuko katika mpaka wa Tanzania na Kenya kwenye eneo la Namanga. Zoezi hilo ambalo litafanyika hapa nchini  linaratibiwa na Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kushirikiana na nchi wanachama kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Ujerumani la GIZ na Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa.

Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Unaotokana Na Kisukari (Diabetic Nephropathy)

$
0
0
Ugonjwa wa kisukari (Diabetes Mellitus) huambatana na ongezeko la sukari(glucose) katika damu kwa kiwango kinachozidi kawaida. 

Homoni aina ya insulin ambayo hutolewa na kongosho ama hushindwa kufanya kazi yake vema kwa sababu ya kasoro za seli au hutolewa kwa kiasi kisicho kidhi uhitaji wa kuratibu sukari katika damu. 

Kwa hivyo sukari hubaki katika damu kwa wingi na kuleta madhara kadhaa.Wagonjwa wa kisukari pia huweza kuwa na kiwango kikubwa cha lehemu (cholesterol) katika damu. Na zaidi huweza kuwa na tatizo la mgandamizo wa damu (hypertension) au presha. Asilimia 55 ya wanaume wenye kisukari hupatwa na tatizo la nguvu za kiume.

Mambo haya matatu, Sukari, lehemu (Cholesterol) na Mgandamizo wa damu, Huweza kusababisha upungufu wa nguvu za kiume.(Erection dysfunction).

1. Sukari.
Sukari nyingi katika damu huweza kupelekea kuharibiwa kwa kuta za mishipa ya damu. Kisha kuta hizi hushindwa kuzalisha homoni aina ya Nitrogen Oxide ambayo husaidia kutanua mirija ya damu kwa ajili ya kupitisha damu kwa ufasaha. Ikitokea katika mirija ya damu inayotiririsha katika uume kushindwa kutanuka vema, ni wazi kuwa uume utapungua uimara wake.

2. Lehemu (Cholesterol).
Lehemu huganda kwenye kuta za mirija ya damu mithiri ya mafuta yanavyoganda katika chupa. Hali hii hupelekea kupungua kipenyo (diameter) cha mirija ya damu na kushindwa kupitisha damu vizuri.

3. Mgandamizo wa damu au Presha (Hypertension).
Katika hali hii moyo hushindwa kusukuma damu vizuri na hivyo kupungua kwa kasi na ujazo wa damu katika maeneo yaliopo mbali na moyo, ikiwa ni pamoja na viungo vya uzazi.

Pia, Mishipa ya fahamu (nerves) au Neva za fahamu huweza kuharibiwa na kupunguza ufanisi wake.Katika hali hii, maeneo yanayohudumiwa na neva hizo hupungua hisia na wakati mwengine kupata ganzi ya kudumu. Uume pia huweza kuathiriwa kwa namna hiyo.

 Kumbuka
Ili  mgonjwa  wa  kisukari  aweze  kupata  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, ni  lazima   apate  pia  tiba   itakayo  saidia  ku- control  sukari  kwenye  damu   yake.

Hivyo  basi ,  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  inatakiwa  kwenda   sanjari  na  tiba  ya  ku - control  sukari  kwenye  damu  ya  mgonjwa.

Hii  ina  maana  kuwa,   ili  tiba  ya  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  iweze  kufanya  kazi  barabara, ni  lazima  mgonjwa  huyo, pamoja  na   kutumia  tiba  ya  nguvu  za  kiume , apate  pia  tiba  ya  sukari.


Kama unatatizo la Kisukari, lililosababisha upungukiwe nguvu za kiume basi wasiliana nami kwa ushauri zaidi. Simu:   0757996194 au 0717339771

Mwenyekiti Wa Bunge Aishauri Serikali Kuwa Na Mtaala Mmoja Wa Elimu Kwa Pande Zote Mbili Za Muungano

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma
Mwenyekiti wa Bunge La Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Mhe.Nagma Giga ameishauri serikali ya  Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Tanzania bara kukaa pamoja kuona namna ya kuwa na Mtaala mmoja wa Elimu ili kuinua na kuboresha kiwango cha ufaulu kwa pande zote mbili.
 
Mhe.Giga amesema hayo leo Mei 22,2019 Bungeni jijini Dodoma wakati akielekeza swali la nyongeza kwa wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambapo amesema pamekuwepo na mkanganyiko mkubwa katika suala la Elimu kwa Zanzibar na Tanzania Bara kutokana na Mitaala ya Elimu kutofautiana hali ambayo husababisha Zanzibar kuwa nyuma.
 
Akijibu Swali hilo Naibu Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia ,Mhe.Wiliam Ole Nasha amesema serikali itaangalia namna ya kufanya ili kuweza kutoa mitaala ya elimu inayofanana ili kuondoa mkanganyiko kwa pande zote mbili za Muungano kati ya Tanzania bara na Zanzibar.
 
Aidha.Mhe.Wiliam Ole Nasha amesema serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali  ili kuongeza ufaulu katika ngazi mbalimbali za elimu ikiwa ni pamoja na uboreshaji wa miundo mbinu  ambapo kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2018/209 zaidi ya Tsh.  Bilioni 93.8  zimetumika kuboreha miundombinu  ya shule 588.
 
Pia amesema  serikali imeendelea kuimarisha  Idara ya Uthibiti  Ubora wa shule  ambapo imenunua na kusambaza magari 45  ya uthibiti Ubora  wa shule na pikipiki 2,897 kwa ajili ya Maafisa Elimu Kata kwa mwaka 2019/2020  huku ikitarajia kujenga ofisi 100  za wathibiti Ubora   wa Shule  na kuongeza idadi ya watumishi.
 
Ikumbukwe kuwa ufaulu wa wanafunzi katika kidato cha nne  umekuwa ukiongezeka mwaka hadi mwaka  ambapo mwaka 2018   asilimia 78.36% ya watahiniwa walifaulu  ikilinganishwa  na 77.09 %  ya mwaka 2017 ,70.35 %ya mwaka 2016 na 67.91 % ya mwaka 2015.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521

Waasi wa Yemen waushambulia tena uwanja wa ndege wa Saudia

$
0
0
Waasi wa Kihouthi nchini Yemen wanaoungwa mkono na Iran wamesema leo kuwa wameushambulia uwanja wa ndege katika mji wa mpaka wa Saudi Arabia kwa mara ya pili mfululizo wakati mivutano ya kikanda ikiendelea.

 Saudia, mshirika wa kikanda wa Iran, inaongoza kampeni ya kijeshi nchini Yemen dhidi ya Wahouthi. 

Televisheni inayoegemea upande wa Wahouthi ya al-Masirah imeripoti kuwa shambulizi hilo la ndege isiyoruka na rubani ilizilenga barabara za uwanja wa ndege wa mji wa kusini magharibi mwa Saudia wa Najran. 

Televisheni hiyo, ikinukuu duru ya jeshi la Houthi, imesema shambulizi hilo lilifanikiwa, bila ya kutoa maelezo zaidi. 

Hapo jana, wahouthi walisema waliushambulia uwanja wa ndege wa Najran na kulenga ghala la silaha. 

Mashambulizi hayo yaliyothibitishwa na Saudia, yanakuja wakati mivutano ikiendelea kati ya Marekani, mshirika wa Saudia, na Iran.

Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Tangaza Biashara Yako Au Bidhaa Yako Kwenye Mtandao huu Kwa BEI NZURI Kabisa

$
0
0

Tunakaribisha  matangazo  ya  aina  zote( Bishara, Viwanja, Bidhaa, matangazo ya Vyuo na mengine mengi)  .Bei  zetu  ni  nzuri  sana  na  kamwe  hutajuta  kutangaza  biashara  yako  kupitia  mtandao  huu....

Kwa Siku tunafunga na Pageviews zaidi  ya  laki tano kama graph  inavyoonyesha  hapo  chini
Kama  una  tangazo, basi  wasiliana  nasi   sasa.

Email  yetu:  mpekuziblog@gmail.com
Simu:     +255682493833 

IFAD Kuendelea Kuisaidia Tanzania Kuendeleza Sekta Ya Kilimo

$
0
0
Na Peter Haule, WFM, Dodoma
WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), Bw. Gilbert Houngbo, na kuiomba Taasisi hiyo kusaidia kuendeleza zaidi Sekta ya Kilimo kupitia mpango wake mpya wa awamu ya  11 wa kuendeleza kilimo nchini.

Dkt. Mpango ameyataja baadhi ya maeneo ya kipaumbele kuwa ni uzalishaji wa mbegu bora, kusaidia kilimo cha umwagiliaji, kutafuta masoko ya uhakika ya mazao ya wakulima, kusaidia upatikanaji wa mitaji kwa wakulima na kuanzisha taasisi za utafiti wa kilimo za kikanda.

Aidha, Dkt. Mpango alimwomba kiongozi huyo kusaidia pia mbinu za kupunguza upotevu wa mazao wakati na baada ya mavuno ili kuchochea na kuongeza tija katika sekta ya kilimo ambayo amesema inaajiri zaidi ya asilimia 66 ya Watanzania.

”Takiribani asilimia 66 ya watanzania wanategemea kilimo na kilimo ndio mwajiri mkuu hivyo kwa kuwa IFAD ina program mpya, tumeamua kushauriana ili wajue vipaumbele vya Serikali na fedha tutakazo zipata tuzielekeze katika maeneo hayo”, alieleza Dkt. Mpango.

Dkt. Mpango alisema kuwa Serikali inaunda kikosi kazi kitakacho husisha Wizara ya Kilimo, Wizara ya Fedha na Mipango na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ili kuweka nguvu ya pamoja kwa kuangalia maeneo ya vipaumbele ambavyo Mfuko wa IFAD utasaidia.

Kwa upande wake Rais wa IFAD Bw. Gilbert Houngbo, alisema kuwa Taasisi yake itashirikiana na Tanzania katika jitihada zake za kupunguza umasikini wa wananchi kupitia kilimo kwa kuyapatia ufumbuzi masuala kadhaa ikiwemo changamoto ya upatikanaji wa mbolea na mbegu bora za kilimo na mifugo, masoko ya bidhaa, upatikanaji wa mitaji, kuongeza ujuzi wa wakulima, kuendeleza kilimo cha umwagiliaji na kuwashawishi vijana wengi kujihusisha na kilimo.

Alielezea kufurahishwa kwake na mwamko pamoja na mwitikio wa baadhi ya wakulima na wafugaji walionufaika na awamu zilizotangulia za uendelezaji sekta ya kilimo na mifugo kupitia taasisi yake aliowatembelea, ambao amesema  wanamtazamo mzuri wa kilimo cha kibiashara kinachozingatia uongezaji wa mnyororo wa thamani, suala ambalo ni moja ya lengo la Mfuko huo katika kuendeleza Sekta hiyo.

Mfuko wa IFAD ulianza kuisaidia Tanzania kutekeleza miradi ya maendeleo ya kilimo kuanzia mwaka 1978, ambapo hadi sasa imesaidia miradi 15 yenye thamani ya dola za Marekani milioni 385.80 na katika awamu mpya ya miaka mitatu kuanzia mwaka 2019/2021, IFAD imetenga zaidi ya dola za Marekani milioni 58.8 kwa ajili ya kuendeleza Sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi nchini.

Miongoni mwa miradi  hiyo ni pamoja na kuwasaidia wakulima kutumia teknolojia ya kisasa ya kilimo na mifumo ya masoko, kuhamasisha Sekta binafsi katika uwekezaji na kuwasaidia wakulima wadogo na wavuvi kuongeza kipato na kupunguza umasikini kwa kuzingatiakuongeza  mnyororo wa thamani ya mazao husika.

Sekta ya Kilimo nchini inachangia asilimia 30.1 ya jumla ya pato la ndani (GDP), asilimia 26 ya mapato ya kigeni, ajira takribani asilimia 65.5, inachangia malighafi za viwandani kwa takribani asilimia 65 na  inachangia kwenye mahitaji ya chakula kwa asilimia 100.

Nafasi za kazi 645 Toka TANESCO

$
0
0

Waziri Mpina Atoa Onyo kwa Watumishi Wanaokamata Mifugo na zkuishikilia Hadi Kufa ikiwa Mikononi mwao

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Luhaga Mpina  amesema serikali itaendelea kuwachukulia hatua za kisheria  watu wanaofanya ukatili kwa wanyama ambapo amesema ifikapo tarehe 1.Julai ,2019  watendaji wanaoshikilia mifugo hadi kufa ikiwa mikononi mwao  watashughulikiwa. 

Mhe.Mpina amesema hayo leo Mei 22,2019 Bungeni jijini Dodoma  ambapo amesema  mifugo ni rasilimali za nchi kama rasilimali nyingine na wizara yake haitavumilia kuona mtendaji wa Serikali akishikilia mifugo mpaka ina kufa kwa kigezo cha kufuata sheria kwani hata mifugo nayo ina sheria zake. 

Awali ,Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Abdallah Ulega wakati akijibu swali la mbunge wa Wa Morogoro Kusini  Prosper Mbena aliyehoji  juu ya ukatili wa wanyama kushamiri nchini ,chama cha kuzuia ukatili wa wanyama Tanzania ,TSPCA  kina shirikiana kwa kiasi gani na Serikali ili kuzuia ukatili ,Mhe.Ulega amezitaja sheria za wanyama pindi wanapokamatwa ikiwa ni pamoja na kupatiwa malisho,maji na chanjo. 

Kuhusu uanzishwaji wa viwanda vya kuchakata na kusindika nyama katika maeneo yaliyo karibu na wafugaji ili kupunguza ukatili wa wanyama pindi wanaporundikwa kwenye magari wakati wanaposafirishwa Kwenda Dar Es Salaam  kwa ajili ya kuchinjwa,Mbunge wa Msalala  Ezekiel Maige  amehoji lini serikali itaanzisha viwanda  katika maeneo mbalimbali ya wafugaji nchini ikiwa ni pamoja na Shinyanga. 

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amesema mchakato wa kufufua viwanda vya kuchakata na kusindika  nyama nchini upo palepale  na kinachotakiwa ni kupata mwekezaji aliyejipanga vizuri.

Hata hivyo,Serikali inashirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali  kama TSPCA  katika kudhibiti vitendo vya kikatili kwa wanyama  kwa kuzingatia sera ya mifugo  ya mwaka 2006  na sheria ya Ustawi wa wanyama ya mwaka 2008 kwa kuelimisha jamii. 

Mwaka 2018 jumla  ya Makosa  3,542 kwa kosa la ukatili wa wanyama yaliripotiwa  ambapo ni  ng’ombe  847 ,mbuzi na kondoo 1,578,nguruwe 88,kuku 539 na punda 490. .
 
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images