Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Urusi na Uturuki Kuunda mifumo ya makombora ya S-500

$
0
0
Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki amesema kuwa nchi yake na Russia kwa pamoja zitaunda mifumo ya makombora ya S-500 baada ya mpango wake wa awali wa kunununua mfumo wa makombora wa S-400 kutoka Moscow kuzusha mivutano.

Jitihada za Uturuki za kutilia mkazo kununua mfumo wa makombora wa S-400 umezorotesha zaidi uhusiano wa nchi hiyo na Marekani; nchi ambayo imeionya mara kadhaa Ankara kuhusu hatari zinazoikabili vikiwemo vikwazo iwapo itaendelea na mpango wake wa kununua mfumo huo wa makombora kutoka Moscow.

Hata hivyo akizungumza mjini Istanbul, Rais wa Uturuki amesema kuwa na hapa ninamnukuu, "kutakuwepo uundaji wa pamoja wa mfumo wa makombora wa S-500 badala ya ule wa S-400", mwisho wa kunukuu. Ameongeza kuwa makubaliano yamefikiwa, na hapa hakuna swali kwamba Uturuki imeachana na ununuzi wa mfumo wa makombora wa S-400.

Itakumbukwa kuwa, uhusiano kati ya Uturuki na Marekani; nchi mbili ambazo zote ni waitifaki wa Muungano wa Nato umeingia dosari kutokana na masuala kadhaa ikiwemo hatua ya Marekani ya kuwaunga mkono wapiganaji wa Kikurdi wa Syria; wapiganaji ambao Ankara inawataja kuwa magaidi; na pia hatua ya Marekani ya kukataa kumrejesha nchini Uturuki mwanazuoni wa Kiislamu anayetuhumiwa kupanga njama ya mapinduzi dhidi ya Rais Erdogan mwaka 2016.

Wakati huo huo Washington imedai kuwa makubaliano baina ya Ankara na Moscow ya kuunda kwa pamoja mfumo wa makombora wa S-500  ni tishio kwa ulinzi wa Magharibi. 

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya May 20

Membe Amjibu Rostam Aziz Sakata La Kugombea Urais Mwakani

$
0
0
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa serikali ya awamu ya nne, Bernard Membe amemjibu mfanyabishara Rostam Aziz kuhusu suala la kugombea urais 2020 akimtaka hivi sasa ajikite kwenye masuala ya kitaifa yanayohusu uchumi.

Membe ametoa kauli hiyo akiwa nje ya jengo la Mahakama kuu ya Tanzania, wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutoka kusikilizwa kwa kesi anayodai fidia dhidi ya mmiliki wa gazeti la Tanzanite Cyprian Musiba, ambapo aliulizwa swali kuhusiana na kauli inayodaiwa kutolewa na mfanyabiashara Rostam Aziz kuhusiana na uchaguzi wa mwakani.

Jana Mei 16, 2019, picha moja ya video ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonyesha Rostam akizungumzia suala la urais 2020 na kumshauri Membe asijitokeze kuwania nafasi hiyo badala yake aachiwe Rais John Magufuli kwa awamu nyingine.

Membe amesema kuwa ; "Kuhusu kugombea mwakani napata kigugumizi kumjibu Rostam, lakini yeye ni mchumi na nitakutana naye nimshauri anafanya vizuri kwa Watanzania anapozungumzia masuala ya uchumi, inabidi azungumzie 'main issue' za nchi sio 'personal', hizi tunaachia watu wa chini."

"Kwa 'level' yetu ni kuzungumzia masuala ya kitaifa masuala ya kiuchumi, kwanini uchumi wetu upo hapa ulipo? kwanini wafanyabiashara wanafunga biashara zao, Rostam ni 'economist' namshauri ajiadress kwenye masuala ya kiuchumi, Rostam wewe ni mwenzetu sisi tumekatwa mkia." amesema Membe.

"Ukikatwa mkia hata ujitahidi vipi mkia wako ni mfupi tu, tunayoyazungumza ni vizuri tuwe 'consistency' mdomoni na dhamira yetu, Rostam ni mchumi mzuri sana, tuzungumzie masuala ya uchumi wa nchi yetu, kuliko kujaribu kuwa mtoto mzawa badala ya kukubali 'status' ..Rostam na mimi ni watoto wa kambo." alimalizia Membe.

Mbunge wa Shinyanga mjini na Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika (PAP) Stephen Masele Ameshafika Bungeni Tayari Kwa Kuhojiwa

$
0
0
Spika wa Bunge,Job Ndugai ameitaka Kamati ya Kudumu ya Haki,Maadili na Madaraka Bunge kwenda kumuhoji Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Afrika,Stephen Masele.

Agizo hilo amelitoa Leo Mei 20 wakati Wabunge wakichangia mjadala wa Wizara ya Kilimo.

“Nawaomba Kamati ya Maadili mwende sasa maana Mheshimiwa Masele ameishafika,” amesema Spika Ndugai.

Lugola Atangaza Kiama Kwa Trafiki wanao wabambikizia makosa Madereva

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amewatangazia kiama askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini wanaowabambikia madereva makosa ya picha za mwendokasi (Speed rader) zisizo na uhalisia kwa nia ya kujipatia mapato wakibainika watawajibika kuzilipa wao wenyewe faini hizo na kuondolewa katika kitengo hicho.

Alitoa agizo hilo mjini Morogoro wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu maafikiano kati ya vyama vya watoa huduma za usafirishaji nchini kuhusu kusitisha kusudio la madereva wa mabasi ya abiria kufanya mgomo wakishinikiza kutimiziwa madai yao mbalimbali ikiwamo ya mikataba ya kazi.

Alisema maamuzi hayo yametokana na makubaliano ya pamoja baina viongozi wa vyama hivyo vya usafirishaji pamoja na wizara mtambuka za serikali kwa nia ya kutatua changamoto walizowasilisha katika kikao hicho kuhusu kubambikiwa makosa na askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani.

Waziri Lugola, alisema moja ya makosa yanayolalamikiwa na madereva hao ni pamoja tochi zinazopiga picha mabasi na kurushwa kwenye simu za maaskari zinakosa uhalisia wa tukio ikiwamo kutoonekana kwa namba za usajili pamoja na vibao vya kuzuia makatazo mbalimbali na kusababisha utata na mivutano yenye nia ya kujenga mazingira ya rushwa.

Alisema kuanzia sasa askari hao wanapaswa kupiga picha katazo mbalimbali za barabara mbele ya gari ikionyesha mwonekano usio na mashaka, namba ya usajili pamoja na eneo la alama iliyokiukwa na dereva ili kuwapo na ushahidi halali vinginevyo dereva huyo asichukuliwe hatua yoyote.

“Dereva anapokuwa na mashaka na picha iliyopigwa dhidi ya gari lake kama haionyeshi usajili wa namba za gari na eneo la kibao cha zuio asikubali kuadhibiwa na badala yake amweleze huyo askari azitume picha hizo kwa msimamizi wa kikosi cha usalama barabarani na aende huko,” alifafanua Waziri Lugola.

Pia alisema tabia ya baadhi ya askari kukamata mabasi yenye abiria na kuyafikisha kituo cha polisi kwa nia ya kumuadhibu dereva aliyetenda makosa, jambo hilo liachwe mara moja na badala yake dereva aliyetenda kosa anapaswa kukamatwa katika kituo cha mwisho cha safari yake.

“Sheria ya Mamlaka ya Usafirishaji wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), inaeleza wazi kila basi linalofanya safari za masafa marefu lazima liwe na madereva wawili, hivyo ukimkamata dereva na kumweka ndani tayari unaenda kinyume na sheria za Sumatra na kulifanya basi kushindwa kuendelea na safari yake,” alisema.

Aidha, aliliagiza Jeshi la Polisi kupitia Kikosi cha Usalama Barabarani kuendelea kuwanyang’anya leseni madereva wanaofanya makosa ya kujirudia pamoja na kukamata magari yanayofanya shughuli za usafirishaji bila kuwa na leseni kwa kushirikiana na Sumatra.

Wafuatao Sio Watumishi wa Jeshi la Zima Moto na Uokoaji

Marekani Yatishia Kuiangamiza Iran

$
0
0
Rais wa Marekani Donald Trump ameapa kuizuia Iran kuwa na silaha za nyuklia saa chache baada ya kutishia kuiangamiza kufuatia matamshi ya kikosi cha walinzi wa Mapinduzi cha nchini Iran kwamba hawahofii vita.

Aidha Saudi Arabia imeionya Iran kuwa itajibu hatua za uchokozi kwa nguvu zote na kuiambia ni jukumu lake kuhakikisha inazuia vita.

Rais Trump alipozungumza na kituo cha televisheni cha Marekani cha Fox News amesema  hapendelei mvutano, lakini hatukubali kuiruhusu Iran kuwa na silaha za nyuklia na kusisitiza hilo halitaweza kutokea.

Rais Trump aliandika kwenye ukurasa wake wa twitter jana Jumapili kwamba, kama Iran inataka vita, huo utakuwa mwisho rasmi wa taifa hilo. Aliongeza kuionya Iran kutoitishia tena Marekani. Hatua hiyo imezidi kuongeza hofu kuhusu kuibuka kwa mzozo kati ya mataifa hayo, wakati hali ya wasiwasi ikizidi kuongezeka.
 
Salami hapo awali alinukuliwa akisema ni rahisi kuwashinda wanajeshi wa Marekani kwa sababu wanahofia kifo, tofauti na wanajeshi wa kikosi cha walinzi wa Mapinduzi wanaoamini katika kufia imani kulingana na dini ya Kiislamu.

Hata hivyo mvutano kati ya Marekani na Iran umezidi kuongezeka tangu Tehran ilipotangaza kwa kiasi itajiondoa kwenye mkataba wa silaha za nyuklia, ambao ilikubaliana na mataifa yenye nguvu duniani mwaka 2015, ambao hata hivyo Marekani ilijiengua mwaka jana.

Wiki iliyopita kiongozi wa juu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei alisisitiza kwamba Iran haitaki vita na Marekani, ingawa anakataa mazungumzo na Trump na kusema Iran imechagua  kuwa mpinzani.

Kwa upande mwingine waziri wa mambo ya nje wa Saudi Arabia, Adel al-Jubeir imeionya Iran kwamba imejiandaa vyema kujibu kwa nguvu zote uchokozi dhidi yake, na ni jukumu la Iran kuvizuia vita. 

Vita hivi vya maneno vimeongezeka kufuatia mashambulizi ya wiki iliyopita kwenye mabomba ya mafuta na mashambulizi ya jana ya roketi kwenye eneo lenye ulinzi mkali, ambako kunapatikana majengo ya ofisi za serikali na balozi za mataifa ya kigeni.

Saudi Arabia ambayo hata hivyo nayo inasisitiza haiko tayari kwa vita, imeituhumu Iran kwa kuagiza mashambulizi hayo kwenye mabomba ya mafuta yaliyofanywa na waasi wa Houthi wa Yemen. Hata hivyo, Iran imekana madai hayo.

Lakini ili kutuliza hali ya mambo, Saudi Arabia imeitisha mazungumzo ya dharura ya kikanda kujadiliana kuhusu kuongezeka kwa wasiwasi katika eneo hilo la Ghuba.

Kulingana na shirika rasmi la habari nchini humo la SPA, Mfalme Salman amewaalika viongozi wa mataifa ya Ghuba na Muungano wa mataifa ya Kiarabu kwenye mkutano huo wa dharura wa kilele wa siku mbili utakaofanyika mjini Mecca Mei 30 kujadilia uchokozi wa hivi karibuni na matokeo yake.

SPA limesema mkutano huo utakuwa ni fursa muhimu kwa mataifa ya ukanda huo kukubaliana kuhusu matarajio yao katika kuimarisha amani na utulivu wa kikanda.

-DW

Google yaizuia Huawei kutumia programu za android

$
0
0
Uhasama wa Rais Donald Trump wa Marekani dhidi ya makampuni makubwa ya mawasiliano kutoka China umeanza kuiweka kampuni ya simu za mkononi ya Huawei katika matatizo makubwa. 

Kampuni ya Kimarekani ya Google imetangaza kuizuia Huawei kutumia toleo jipya la programu ya kuendesha simu za mkononi ya Android, hiyo ikiwa na maana kuwa kampuni hiyo ya Kichina haitapata tena ruhusa ya kutumia programu hiyo muhimu katika simu zake mpya. 

Marekani inashuku kuwa Huawei huweka katika vifaa inavyovitengeneza, programu za siri za kijasusi zinazoweza kuhatarisha usalama wake wa taifa. 

Huawei inazikanusha shutuma hizo. Katika tangazo lake la hivi punde, Huawei imesema itaendelea kutoa huduma za kiusalama kwa watumiaji wa simu zake ambazo tayari zimekwishanunuliwa, na zile ambazo bado ziko madukani.

Naibu Waziri: Askari Polisi anamamlaka ya Kusimamisha, kukagua na kukamata chombo barabarani

$
0
0
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,imesema Sheria ya Usalama Barabarani sura ya 168 iliyorejewa 2002 inampa Mamlaka askari polisi kusimamisha chombo chochote barabarani na kukikagua na hatimaye kukizuia na kukikamata.

Hayo yameelezwa Leo Mei 20 Bungeni na Naibu Waziri wa Wizara hiyo,Hamadi Masauni wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum,Rehema Juma Migilla (CUF).

Katika swali lake,Migilla alitaka kujua ni kwanini askari polisi wanapowakamata huchukua baadhi ya vifaa.

Picha: Mbunge Masele mbele ya Kamati ya Bunge

$
0
0
Mbunge wa Shinyanga mjini na Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika (PAP), Stephen Masele akiwa mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge jijini Dodoma kujibu tuhuma za utovu wa nidhamu zinazomkabili

Taarifa Muhimu Toka Kurugenzi Ya Mawasiliano Ya Rais IKULU

$
0
0
Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) umetenga shilingi Bilioni 127.3 kwa ajili ya kufadhili miradi ya kilimo nchini Tanzania kwa kipindi cha miaka 3 kuanzia mwaka 2020.

Rais wa IFAD, Gilbert Fossoun Houngbo amesema hayo leo Ikulu Jijini DSM alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

Pamoja na kutenga fedha hizo, Houngbo ambaye ni Waziri Mkuu Mstaafu wa Togo amempongeza Rais Magufuli na Serikali anayoiongoza kwa juhudi kubwa anazozifanya katika kukuza uchumi ikiwemo utekelezaji mzuri wa miradi inayofadhiliwa na IFAD, kutilia mkazo umuhimu wa uwekezaji usiokuwa tegemezi, unaolinda utu, unaozalisha kipato kwa wananchi na unaojenga misingi endelevu ya kujitegemea.

Amebainisha kuwa baada ya kutenga fedha hizo, IFAD inasubiri upande wa Tanzania kuainisha maeneo mahususi ya miradi ya kilimo ambako fedha zitaelekezwa na ameeleza kuwa ana matumaini miradi hiyo itafanikiwa kwa kuzingatia kuwa Tanzania ni nchi yenye amani na namna Serikali ilivyo na dhamira ya maendeleo.

Rais Magufuli ameishukuru IFAD kwa ushirikiano wake mzuri na Tanzania na amemhakikishia Mhe. Houngbo kuwa ushirikiano na uhusiano huo ulioanza mwaka 1978 utadumishwa kwa maslahi ya Watanzania.

Rais Magufuli amesema fedha zilizotengwa katika mpango huo wa miaka 3 zitaelekezwa katika maeneo yenye maslahi mapana ya sekta ya kilimo ikiwemo kuwezesha matumizi ya zana bora za kilimo katika uzalishaji, kuzalisha mbegu bora za mazao, kutatua changamoto ya masoko ya mazao, kuboresha ufugaji na ameipongeza IFAD kwa kutoa fedha pasipo kuweka masharti ya maeneo zinakopaswa kuelekezwa.

Rais Magufuli ameiagiza Wizara ya Kilimo kuharakisha mchakato wa kuainisha maeneo yatakayopokea fedha hizo ili utekelezaji wa mpango huo uanze.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa wa Sweden, Peter Eriksson.

Baada ya mazungumzo hayo, Peter Eriksson amempongeza Rais Magufuli na Serikali yake kwa mafanikio makubwa katika mapambano dhidi ya rushwa na ameeleza dhamira ya Sweden kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano wake na Tanzania.

Mazungumzo hayo yamehudhuriwa na Balozi wa Sweden hapa nchini Mhe. Anders Sjöberg na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Prof. Palamagamba Kabudi.

Meet with a doctor who is kubri from Allah Mohamedi Buluhani ....the doctor of human stars

$
0
0
Meet with a doctor who is kubri from Allah Mohamedi Buluhani the doctor of human stars and the natural medicine of Africa who is able to identify you are left and you love him.

Be a husband,wif and you still love him?And you have tried many places without success? Wasiliana and Mohamedi Buluhani see an instant miracle,,He is able to return your relationships and enhance your marriage within just 12 hours.

Do you agree with your husband.wif or lover and he is living with someone else? See  akutafutie is able to do the top of their relationships if they don't know what they want to direct

He will make him fulfill all the promises for a short time .Muhamedi Buluhani is using the name of a character or picture to finish your problem,,

He is treating using the books of the Qur-an, .Interprets the dream winning the lottery, cleaning the stars The gravity of the body and the business, the  immunity of the body

He gives you a genie of wealth ot the way of polytheism.He gives you a genie of wealth ot the one who needs wealth without conditions.

Contacts:  (+255) 715971688 or (+255)756914036 NB :Cure for all religions and all beliefs,,,,,,,,,,,,,

Wimbo Mpya: Dudu Baya - Dude

Nape Ageuka Mbogo Kwa Waliohujumu Zao la Korosho

$
0
0
Mbunge wa Mtama,Nape Nnauye (CCM) ametaka wote waliohusika na kuhujumu Korosho wachukuliwe hatua na wasipochukuliwa ataleta kusudio jinsi walivyofanya mmoja mmoja.

Kauli hiyo ameitoa leo,Mei 20 bungeni,wakati akichangia mjadala wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, kwa mwaka wa fedha 2018-2019.

Nape amesema waliofanya mambo ya hovyo katika kuhujumu Korosho,Serikali inatakiwa iwachukulie hatua kali na isipofanya hivyo atakuja na kusudio jinsi walivyofanya mmoja mmoja

“Watu waliofanya hovyo wanajulikana na kama wasipochukua hatua wenyewe, wasipofanya tutaleta kusudio jinsi walivyofanya mmoja mmoja na jinsi ambavyo wanatakiwa kuchukua hatua kwa sababu waliyoyafanya ni kuhujumu,Korosho,wananchi lakini pia ni kuhujumu uchumi wa Nchi.

Nape amesema Rais alikuwa na nia njema lakini walioenda kuitekeleza wameenda kuiua sekta ya Korosho.

“Hivi tunavyoongea Mheshimiwa Spika bahati mbaya zoezi lilikuwa na dhulma,lilikuwa na rushwa lilikumbwa na ubabaishaji mwingi na uongo mwingi sana.

“Hivi tunavyoongea Jimbo la Mtama peke yake kwenye vyama vya msingi 11 wakulima ambao wana korosho chini ya tani 1500 ambao wamehakikiwa mashamba yao zaidi ya 1281 kwa miezi nane tangu Korosho yao ichukuliwe hawajapa hata senti tano.

“Lakini Korosho yao imechukuliwa hawana fedha za kutengeneza mashamba yao.

Nape alisema mapendekezo yake ni iletwe sheria ya Korosho yote ili ipitiwe upya.

“Kile kipengele tulichokinyofoa kimetuletea shida sana sasa leteni sheria yote tuipitie.

“Napendekeza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali aende kukagua atuletee ripoti hapa ndani namna zoezi lilovyoenda ili tuchukue hatua ya kuziba mapengo.

“Kama nilivyosema Rais wengi wamemdanganya sasa ni vizuri wawajibike na Mheshimiwa Spika ni vizuri tukawa ‘Specific’ si sahihi kuiingiza Serikali katika mambo yaliyofanyika hovyo.

“Leo tukiulizana Korosho yetu ipo wapi haiwezi kukaa zaidi ya miezi sita hapa nchini ikabaki salama mngetuambia kuna korosho sahihi, huu ni uongo na tukiendelea kuusema huu uongo na bado tunaendelea kubaki hatutabaki salama,amesema Nape.

Wizara Ya Kilimo Yaunda Tume Maalumu Kushughulikia Udhaifu Uliopo Katika Miradi Ya Umwagiliaji

$
0
0
Wizara  ya Kilimo imesema imeona udhaifu mkubwa katika miradi ya umwagiliaji hivyo imeunda timu maalum kulishughulikia hilo.

Hayo yameelezwa leo Mei 20 Bungeni na Naibu Waziri wa Kilimo,Omari Mgumba wakati ahitimisha mjadala wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, kwa mwaka wa fedha 2018-2019.

Mgumba amesema ripoti ya CAG imeonesha kuna udhaifu mkubwa katika miradi ya umwagiliaji nchini hivyo Wizara ya Kilimo imeunda timu maalum kwenda kuthibitisha hayo.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521

Mbunge wa Kahama Ataka Kilimo Cha Bangi Kiruhusiwe Tanzania

$
0
0
Mbunge wa Kahama Mjini (CCM),   Jumanne Kishimba ameishauri Serikali ya Tanzania kuruhusu kilimo cha  bangi nchini kwa ajili ya utengenezaji wa dawa za binadamu.

Amesema hayo leo Jumatatu Mei 20,  2019 bungeni jijini Dodoma katika mjadala wa bajeti ya Wizara ya Kilimo mwaka 2019/2020.

Amesema nchi nne barani Afrika zimeruhusu kilimo cha bangi kwa ajili ya matumizi ya dawa za binadamu.

“Amebainisha dawa nyingi za maumivu ya saratani asilimia 80 zinatokana na bangi, “Nashangaa wataalam wetu wa Mamlaka ya Chakula la Dawa (TFDA) wangekuwa wameshachukua sampuli na wangewajulisha kuwa dawa zilizo na bangi ndani yake.”

“Wangemuuliza  msambazaji hiyo bangi anaitoa wapi? Spika sisi wenyewe tunayo bangi hiyo tunaona kila siku inakatwa ukweli nyingi sio kwa ajili ya kuvuta. Bangi hiyo imekuwa ikienda katika dawa za binadamu.”

Amesema ana ushahidi Lesotho na Zimbabwe kuruhusu ulimaji wa bangi na kuna viwanda vya kutengeneza dawa za binadamu kwa kutumia bangi.

Amesema gunia  moja la bangi nchini ni kati ya Sh4milioni hadi Sh4.5milioni na kwamba Lesotho na Zimbabwe gunia moja ni Sh20milioni.

“Bangi yote ya Tanzania inakwenda katika dawa za binadamu ambazo tunaletewa kutumia. Kuna ubaya gani ikaanza kutoa vibali kwenye maeneo mbalimbali na kuhalalisha watu waanze kulima bangi hiyo na kupata faida.” amesema.

Amesema haungi mkono kauli ya mbunge wa Geita (CCM),  Joseph Msukuma ambaye amekuwa akitaka bangi kuhalalishwa kwa ajili ya kuvuta.

Akichombeza Spika Ndugai aliwataka Wabunge kuchangia kama ambavyo amechangia Mbunge huyo kwa kujikita katika eneo moja

“Niwape siri muongee kama Kishimba unakuja na kitu chako fulani.unajikita sehemu moja.Hii hoja ni nzuri sana Naamini Jenista (Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu,Sera,Bunge,Ajira,Kazi,na watu wenye ulemavu) ameipigia mstari,”amesema Spika Ndugai.

CCM Watuma Salamu za Rambirambi Kifo cha Brigedia Jenerali Hassan Ngwilizi

Wizara Ya Ardhi Yaandaa Mpango Wa Kuendeleza Maeneo Ya Ukanda Wa reli ya kisasa ya Standard Gauge (SGR)

$
0
0
Na Grace Semfuko,MAELEZO
Wizara ya ardhi nyumba na Maendeleo ya Makazi  inaandaa mpango maalum wa uendekezaji wa Ukanda wa reli ya kisasa ya Standard Gauge (SGR) inayotoka Dar Es Salaam hadi Kigoma unaolenga kuwawezesha wakazi waishio kando ya Reli hiyo kunufaika kiuchumi kupitia ardhi zao kwa kufanya biashara zitakazopangwa kwenye maeneo hayo na ambazo wananchi wataamua kuzifanya.

Lengo la mpango huo  ni kutoa mwongozo wa namna matumizi ya ardhi yatakavyofanyika katika ukanda mzima wa SGR ambao utasaidia kuondoa matumizi yasiyokusudiwa na pia  utasaidia kuondoa migogoro ya adhi na kuibua fursa ambazo bado hazijajulikana na Wakazi wa maeneo hayo.

Hayo yalibainishwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi wakati akizungumza na wakazi wa Vijiji vya Kwala na Soga vilivyopo Wilayani Kibaha Mkoani Pwani kuhusu mpango bora wa matumizi ya ardhi kwenye ukanda wa Reli ya Kisasa ya SGR.

“Kila mahali kutakuwa na fursa za kiuchumi zinazopatikana mahali husika, haimaanishi tunaipanga ile ardhi ili ichukuliwe na serikali, hapana!  wananchi wenyewe watayatumia maeneo yao kwa mpango maalum,  tunataka wananchi wanufaike na ardhi yao” alisema Waziri Lukuvi.

Waziri Lukuvi aliwatoa hofu wakazi wa Maeneo yote ya SGR kuwa Serikali haina mpango na kuchukua ardhi zao na kuwataka pia kutouza ardhi hizo kwani tayari Serikali imeshazipandisha hadhi na thamani.

“Serikali inapanga matumizi bora ya ardhi yote katika Wilaya zote ambapo SGR inapita, tunataka kuwa na ukanda wa maendeleo ya kiuchumi , yaani mtu akifika hapa anajua kitu gani anakipata wapi, ukanda huu unaopitiwa na SGR sasa utapangwa rasmi, hatuwezi kuwa na reli ya kisasa yenye gharama kubwa kama hii lakini uendelezaji wa ardhi ni mbovu,mtu hataruhusiwa kufanya shughuli isiyoruhusiwa, hapa lazima ardhi ipangwe vizuri na tuwe na mpango mzuri  wa kiuchumi” alisema Lukuvi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi wa Mipango Miji wa Wizara ya Ardhi Immaculata Senje alisema pamoja na kuinua pato la wakazi waishio kando ya reli hiyo mpango huo pia unalenga kulinda mazingira na kupendezesha maeneo hayo na wameshaanza maandalizi ya awali ya kukusanya taarifa za mpango huo.

 “Utakuwa ni mpango shirikishi kuanzia ngazi za vijiji hadi Taifa, mpaka sasa timu ya wataalamu imeundwa na imeshaanza maandalizi ya awali kwa kukusanya taarifa muhimu ambazo zitasaidia kuutekeleza mpango huu, tutafanya kazi na wote, lengo la mpango huu ni kutoa mwongozio wa namna matumizi ya ardhi yatakavyofanyika katika ukanda mzima” alisema Senje

Ufafanuzi Kuhusu Kuwepo Kwa Dawa Za Vidonge Zinazodhaniwa Kutibu Homa Ya Dengue

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images