Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya May 10


Naibu spika Guaido akamatwa

$
0
0
Maafisa wa upelelezi wa Venezuela wamemkamata kiongozi wa ngazi ya juu wa bunge linalotawaliwa na upinzani, Edgar Zambrano, ikiwa ni hatua ya hivi karibuni dhidi ya wabunge walioamua kujiunga na vuguvugu lililoshindikana na kumuondoa madarakani Rais Nicolas Maduro mwezi uliopita. 

Zambrano ni naibu wa spika wa Juan Guaido, mtu anayetambuliwa kama kiongozi wa mpito wa Venezuela na mataifa zaidi ya 50, na ambaye aliongoza vuguvugu la kumuondoa madarakani Maduro mnamo Aprili 30. 

Rais wa Marekani Donald Trump amelaani hatua hiyo ya kukamatwa kwa Edgar Zambrano. "Kinachotokea nchini Venezuela ni aibu .. Watu wanakufa, hawana chakula, hakuna maji. Hii ni moja ya nchi zilizo tajiri sana ulimwenguni. Na sasa wanaishi vibaya sana. 

"Na tunafanya kazi kwa bidii juu ya tatizo hilo na tunajitahidi kuwa wagumu," amesema Rais Donald Trump. 

Kwa upande mwingine, Mahakama Kuu ya Venezuela iliwashtaki wabunge watatu kuunga mkono uasi wa Guaido uliosababisha siku mbili za mapigano kati ya vikosi vya usalama na waandamanaji.

Kanyasu Aahidi Miradi Ya Maendeleo Itakayotekelezwa Mjini Geita Itafuata Taratibu Zote

$
0
0
NA LUSUNGU HELELA
Mbunge wa Geita Mjini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu,ametoa ahadi ya kuhakikisha kuwa miradi ya maendeleo itakayotekelezwa mwakani katika Halmashauri ya Mji wa Geita  itazingatia taratibu zote zinazotakiwa ili isiweze kukataliwa.

Kauli hiyo imekuja mara baada ya mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka huu kubaini baadhi ya kasoro katika miradi iliyotekelezwa katika Halmashauri hiyo hali iliyolazimu  mradi wa maji  kushindwa kuzinduliwa.

Hayo ameyasema wakati alipokuwa akizungumza na Wananchi wa Kasamwa katika eneo ambalo mkesha wa Mwenge ulipofanyikia  katika Halmashauri ya Mji wa Geita mkoani Geita.

Kufuatia hali hiyo ya  mradi wa maji kushindwa kuzinduliwa unaodaiwa  kugharimu shilingi bilioni sita,  hali hiyo  imempelekea Kiongozi wa mbio za Mwenge wa mwaka huu, Mzee Mkongea Ally kuiagiza  Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa  kuchunguza mradi huo .

Mhe.Kanyasu amesema mwaka huu ukimbizaji Mwenge umekuwa na maana kubwa  kufuatia kufanya ukaguzi usiotia shaka kwenye miradi iliyotekelezwa na pale wanapobaini ukiukwaji miradi hiyo imekuwa haizinduliwi.

" Ukaguzi mnaoufanya katika miradi hii ni ishara tosha kabisa kuwa mmekuja kufanya kazi kwa ajili ya wananchi'' alisisiiza Kanyasu

Amesema miaka ya nyuma zoezi la ukimbizaji Mwenge lilikuwa la kawaida hali iliyopelekea kila miradi iliyotekelezwa kuzinduliwa bila kujalisha thamani ya pesa inayoendana na miradi halisi.

" Mimi binafsi niliweza kupata bahati ya kukimbiza Mwenge wa Uhuru hapo nyuma kidogo, Tulikuwa hatufanyi ukaguzi makini kama unaofanyika mwaka huu.

Akizungumzia kuhusu kasoro zilizojitokeza katika miradi ya mwaka huu, Mhe.Kanyasu amesema kasoro zote zilizojitokeza mwaka huu hazitajirudia katika Halmashauri hiyo, hivyo ameahidi kuzifanyia kazi.

Katika hatua nyingine, Mhe, Kanyasu amesema  mkoa wa Gieta ni nyumbani kwa Mhe, Rais, Joseph Pombe Magufuli hivyo mwaka ujao atahakikisha hakuna miradi wowote utakaotaliwa kwa vile ni aibu kwao.

TFDA Kanda Ya Kati Yasema Itaendelea Kukagua Na Kudhibiti Vipodozi Feki Na Vilivyoisha Muda

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni ,Dodoma.
Mamlaka ya chakula na dawa TFDA   imesema itaendelea   kukagua na kudhibiti bidhaa za vipodozi na bidhaa nyingine na kuhakikisha bidhaa ambazo zinamfikia mwananchi zinakuwa  zenye ubora ,salama na fanisi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kaimu meneja wa TFDA kanda ya kati inayo simamia mikoa ya Dodoma,singida pamoja na morogoro na Halmashauri zake zote Benedict Blush amesema  TFDA  imepewa jukukumu la kuthibiti,ubora,usalama pamoja na ufanisi wa bidhaa za chakula  dawa,vipodozi,vifaa tiba pamoja na vitendanishi.

Aidha amesema mamlaka hiyo inafanya kazi kwa mujibu wa sheria ya chakula na dawa No 1 sura ya 219 huku akizungumzia mifumo ya udhibiti ambayo mamlaka ya chakula na dawa  imekuwa ikitumia katika bidhaa za vipodozi na bidhaa nyingine.

Mbali na hilo pia amezungumzia  vipodozi vyenye viambato  vya sumu kama zebaki hii imekuwa na tabia ya kupenya kwenye ngozi na kadri  inavyo endelea kurundikana katika  mwili  kunaweza kuleta shida ya ini.
 
Katika hatua nyingine amesema kwa wale ambao wamekuwa wakitumia viambato hivyo inaweza kusababisha kansa ya damu na hatimae kupelekea  kupoteza maisha huku akigusia kwa upande wa wakina mama wajawazito ambao wamekuwa na tabia ya kutumia vipodozi kipindi cha ujazito.
 
Hata hivyo, amesema kama serikali inaendelea kuweka mkazo katika uthibiti wa vipodozi ili kuondoa madhara kama ambayo yanaweza kuajitokeza.

Serikali Kuwa Na Mchakato Wa Kuajiri Wataalam Wa Lishe Wawili Wawili Kwa Kila Kijiji

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Katika kukabiliana na tatizo la utapiamlo  jambo ambalo hupelekea  udumavu   kwa watoto ,kwa kusababishwa na lishe duni,Serikali ina mchakato wa kuajiri wataalam wa lishe wawili  kwa kila kijiji hapa nchini hali  itakayosaidia kutoa elimu ya lishe  kwa kila kaya.
 
Hayo yamesemwa  Mei 7,2019 bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Afya ,Maendeleo ya jamii ,jinsia Wazee na Watoto Mhe.Faustine Ndugulile wakati akijibu swali la mbunge wa     Viti Maalum  Zainab Mwamindi aliyehoji mpango mkakati wa serikali wa kuajili wataalam wa lishe katika vijiji.
 
Akijibu swali hilo,Mhe.Ndugulile alisema wizara ya Afya ,Mandeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto pamoja na Wizara ya Ofisi ya Rais ,Tawala za mikoa na serikali za mitaa,TAMISEMI zina mchakato wa kuajiri wataalam wa lishe wawili wawili kwa kila kijiji kwa ajili ya kutoa elimu umuhimu wa lishe bora.
 
Hata hivyo,Mhe.Ndugulile amesema serikali inaendelea kupambana na utapiamlo pamoja  na lishe iliyopitiliza ambapo asilimia 10 ya     Watanzania wanavitambi.
 
Vipaumbele vya serikali vinavyolenga kupunguza utapiamlo  ifikapo mwaka 2021  ni pamoja na kupunguza viwango vya udumavu  chini ya umri wa miaka mitano  kutoka asilimia 34% mwaka 2015  hadi 28% ,kudhibiti viwango vya ukondefu  kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano  ibaki chini ya 5% kama ilivyo sasa,Kupunguza viwango vya watoto  wanaozaliwa na uzito pungufu  kutoka 7%  kwa mwaka 2015 hadi 5%.
 
Vipaumbele vingine ni kupunguza idadi ya wanawake walio katika umri wa uzazi  miaka 15 hadi 49  wenye upungufu wa damu  kutoka 44.7% kwa mwaka 2015 hadi kufikia 33%,kupunguza tatizo la upungufu wa vitamin A Kwa watoto wenye umri wa miezi 6 hadi miezi 59 kutoka 33% hadi kufikia 26% na kupunguza uzito uliozidi kwa watoto walio na umri chini ya miaka mitano na kubaki asilimia 5%.

LIVE: Fuatilia kipindi cha maswali na majibu kutoka Bungeni Dodoma

$
0
0
LIVE: Fuatilia kipindi cha maswali na majibu kutoka Bungeni Dodoma

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521

Serikali Yaagiza Makampuni Ya OCP Na ETG Kufikia Julai 2019 Kuwa Na Maghala Ya Kuhifadhia Mbolea

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imeyaagiza makampuni ya Premium Agrochem, OCP na Export Trading Group (ETG) kuhakikisha kwamba ifikapo Julai, 2019 kampuni hizo ziwe na ghala za kuhifadhia mbolea na mawakala wa kusambaza katika mikoa inayotumia mbolea kwa wingi ukiwemo mkoa wa Katavi ili kuondoa changamoto ya upungufu wa mbolea kwa wakulima katika maeneo hayo.

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba (Mb) ameyasema hayo leo tarehe 10 Mei 2019 wakati akijibu swali la Mbunge wa viti maalumu Mhe Taska Restituta Mbogo aliyetaka kufahamu kuwa serikali ina mpango gani wa kusambaza mbolea kwa wakati katika mkoa wa Katavi.

Alisema kuwa Serikali inatumia Mfumo wa Ununuzi wa mbolea kwa pamoja Bulk Procurement System - BPS kuagiza mbolea ya kupandia (DAP) na mbolea ya kukuzia (UREA), Mfumo huo unawezesha upatikanaji wa mbolea kwa wakati na kwa bei nafuu na kudhibiti upandishaji wa bei za mbolea kiholela.

Mhe Mgumba aliongerza kuwa Serikali inakamilisha zabuni ya kuingiza mbolea tani 280,000 ambapo tani 170,000 ni mbolea ya kupandia na tani 110,000 ni mbolea ya kukuzia kwa ajili ya msimu wa 2019/2020 kupitia mfumo wa BPS.

Alisema, Mbolea hiyo inatarajiwa kufikishwa hapa nchini mwezi Agosti, 2019 na kusambazwa kwa wakulima wa mkoa wa katavi na maeneo mengine nchini kabla ya mwezi Septemba 2019. Vile vile, ziada ya mbolea iliyopo nchini inaendelea kusambazwa katika maeneo mbalimbali kulingana na msimu ambapo hadi tarehe 30 Machi, 2019 kulikuwa na tani 147,913 za mbolea.

Aidha, Serikali inatumia Mfumo wa Ununuzi wa mbolea kwa pamoja Bulk Procurement System - BPS kuagiza mbolea ya kupandia (DAP) na mbolea ya kukuzia (UREA). Mfumo huo unawezesha upatikanaji wa mbolea kwa wakati na kwa bei nafuu na kudhibiti upandishaji wa bei za mbolea kiholela.

Serikali inakamilisha zabuni ya kuingiza mbolea tani 280,000 ambapo tani 170,000 ni mbolea ya kupandia na tani 110,000 ni mbolea ya kukuzia kwa ajili ya msimu wa 2019/2020 kupitia mfumo wa BPS. Mbolea hiyo inatarajiwa kufikishwa hapa nchini mwezi Agosti, 2019 na kusambazwa kwa wakulima wa mkoa wa katavi na maeneo mengine nchini kabla ya mwezi Septemba 2019.

Kadhalika, Mhe Mgumba alisema kuwa ziada ya mbolea iliyopo nchini inaendelea kusambazwa katika maeneo mbalimbali kulingana na msimu ambapo hadi tarehe 30 Machi, 2019 kulikuwa na tani 147,913 za mbolea.

“Serikali imelielekeza Shirika la Reli Tanzania kutoa kipaumbele cha kusafirisha mbolea ili kusafirisha mbolea nyingi kwa wakati mmoja na gharama nafuu ili kumfikia mkulima kwa wakati na bei nafuu” Alikaririwa Mhe Mgumba na kuongeza kuwa

Serikali inakusanya mahitaji ya mbegu bora na viuatilifu kutoka katika mikoa ili kuhamashisha kampuni na wafanya biashara kupeleka pembejeo hizo kwa wakulima kabla ya msimu wa kilimo kuanza na wakati wa mauzo ya mazao.
 
MWISHO

Tanasha akiri kuchanganywa na penzi la Diamond Platnumz

$
0
0
Mpenzi  wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Tanasha Donna Oketch amesema kuwa, ilibaki kidogo apate uchizi baada ya kutoka na msanii huyo.

Akizungumza na Citizen TV katika Kipindi cha 10 Over 10, Tanasha ambaye pia ni msanii wa muziki na Mtangazaji wa Radio NRG ya nchini humo alisema kuwa alipoanza kuwa na uhusiano na Diamond  yalizuka maneno mabaya kwake ambayo yalitaka kumpa uchizi.

“Mwanzoni maneno hayo nilichukulia kawaida tu. Yakaanza kunifanya kupata msongo wa mawazo, lakini nilikabiliana nayo,” alisema Tanasha.

Kutana na shariff Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam shariff Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

$
0
0
Kutana  na shariff Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam shariff  Mwenye UWEZO wakufanya dua mbali mbali  Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?

Wasilina na Adam shariff Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO   Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? . Adam shariff Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN  . Anatafsiri Ndoto. , KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na Biashara.


Mawasiliano: (+255 )715971688 au (+255  )756914036

Walimu Watakiwa Kutodai Nyongeza Ya Mishahara Kama Haijatolewa

$
0
0
Serikali imesema walimu hawapaswi kudai nyongeza ya mwaka ya mshahara kwa miaka ambayo nyongeza hiyo haikutolewa.

Hayo yamesemwa bungeni leo, Ijumaa Mei 10, na Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mwita Waitara wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Zainab Mussa Bakar (Chadema).

Katika swali lake Zainabu aliuliza; “Walimu nchini wameingia mkataba na mwajiri wao ambao pamoja na mambo mengine unaonyesha uwepo wa nyongeza ya mshahara kila ifikapo Julai, lakini tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani hawajapewa stahiki hizo, je ni lini walimu watalipwa malimbikizo hayo?”

Katika majibu yake, Waitara alisema Serikali imekuwa ikitekeleza miongozo mbalimbali kuhusu maslahi ya walimu zikiwamo nyongeza za mwaka za mishahara kulingana na utendaji wa mhusika na tathmini ya kila mwaka.

“Kwa mujibu wa kanuni E.9 (1) ya kanuni ya kudumu katika utumishi wa umma za mwaka 2009 toleo la tatu, nyongeza ya mwaka ya mshahara haipaswi kuombwa au kudaiwa na walimu, bali serikali ndiyo yenye uamuzi wa kutoa au kutotoa nyongeza hiyo kutokana na sera za kibajeti kwa mwaka husika." Amesema.

Amesema nyongeza hiyo haikutolewa kwa watumishi katika miaka 2003/2004 hadi 2016/17, lakini imetolewa kwa watumishi wote wakiwamo walimu mwaka wa fedha 2017/18.

Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani Asema Polisi Hawaruhusiwi Kumpiga au Kumtesa Mtuhumiwa

$
0
0
Wizara ya Mambo ya Ndani  imesema hakuna sheria inayomruhusu askari wa Jeshi la Polisi kumpiga au kumtesa mtuhumiwa wa makosa mbalimbali akiwa mikononi mwa polisi au kituoni.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Yusuf Masauni amesema kanuni za kudumu za utendaji wa Jeshi la Polisi (PGO) zinakataza na kuelekeza utendaji mzuri wa askari  ambapo polisi yeyote anapobainika kufanya vitendo vya kumpiga au kumtesa mtuhumiwa hufikishwa mahakamani.

Masauni alikuwa akijibu swali la msingi la Mbunge Chonga (CUF), Mohamed Juma Khatibu bungeni, leo Mei 10, 2019, aliyetaka kujua ni kwa mazingira gani askari polisi anapaswa au hulazimika kumtesa mtuhumiwa wa makosa mbalimbali wakati akiwa mikononi mwake au kituo cha polisi.

Naibu waziri huyo amesema, "kwa kutumia PGO, askari wanaokiuka na kufanya vitendo hivyo tunachukua hatua za kinidhamu ikiwemo kufukuzwa kazi au kufikishwa mahakamani."

Masauni ameliambia Bunge kwamba Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai sura ya 20, kifungu cha 11 kinaeleza namna ya ukamataji.

Chama cha ANC chaongoza uchaguzi wa Afrika Kusini

$
0
0
Chama tawala cha Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa ANC kitahifadhi wingi wake wa viti bungeni baada ya uchaguzi, ijapokuwa umaarufu wake utapungua na hivyo kuathiri jitihada za kukifufua chama hicho na pamoja na uchumi unaoyumba wa nchi hiyo. 

African National Congress, ambacho kimekuwa madarakani tangu 1994, kinaendelea kuongoza kikiwa na karibu asilimia 57 ya kura baada ya zaidi ya nusu ya maeneo ya kupigia kura kuhesabiwa rasmi kufuatia uchaguzi wa Jumatano. 

Ramaphosa mwenye umri wa miaka 66, alichukua usukani mwaka jana baada ya chama hicho kumlazimu aliyekuwa rais wakati huo Jacob Zuma kujiuzulu baada ya miaka tisa iliyozongwa na madai ya rushwa na matatizo ya kiuchumi. 

Matokeo yaliyotolewa na tume ya uchaguzi yanaonyesha kuwa mpinzani wa karibu kabisa wa ANC, chama kikuu cha upinzani cha Democratic Alliance - DA kinafuata na asilimia 23. Chama cha Economic Freedom Fighters kikiongozwa na Julius Malema ni cha tatu na asilimia 10.

 Matokeo rasmi yanatarajiwa kutolewa Jumamosi.

Marekani yaongeza tena ushuru kwa bidhaa za China

$
0
0
Marekani leo imeongeza kiwango cha ushuru kwa bidhaa za China hatua ambayo China imejibu mara moja ikisema italipiza kisasi. Mzozo huo umeshika kasi kabla ya siku ya pili ya mazungumzo ya kibiashara

Rais Donald Trump alipata ufafanuzi kutoka kwa wajumbe wake wa kibiashara baada ya siku ya kwanza ya mazungumzo na upande wa China jana, lakini hakuchukua hatua yoyote kuhusu kutotangaza ushuru mpya – na hivyo kuua matumaini kuwa huenda kukawa na ahueni katika dakika za mwisho wakati mazungumzo hayo yakiendelea.

Dakika chache baada ya Marekani kuongeza kodi zake kali kwa bidhaa za China za thamani ya dola bilioni 200, kutoka asilimia 10 hadi 25, wizara ya biashara ya China ikasema "imesikitishwa sana” na uamuzi huo na kurudia ahadi yake ya kuchukua "hatua mwafaka za kulipiza kisasi”, bila kufafanua.

Kufuatia mgogoro wa zaidi ya mwaka mmoja, maafisa kutoka nchi hizo mbili kubwa kiuchumi duniani walirejea kwenye meza mazungumzo jana usiku, wakiongozwa na Naibu Waziri Mkuu wa China Liu He, Mwakilishi wa Biashara wa Marekani Robert Lighthizer na Waziri wa Fedha wa Marekani Steven Mnuchin. 

Liu He alisema kuwa anataraji kuwa mazungumzo hayo yatakuwa ya wazi na ya tija kwa kila mmoja 

"Bila shaka China inaamini kuwa kurudisha ushuru katika hali ya sasa sio suluhisho la tatizo hilo, bali kutaiumiza China, Marekani na ulimwengu mzima. Kwa hiyo kulitatua tatizo hilo ni kupitia njia imara ili mwishowe tupate suluhisho pekee la ushirikiano"
 
Licha ya matumaini kutoka kwa maafisa katika wiki za karibuni kuwa mazungumzo hayo yako kwenye mkondo wa kupata ufumbuzi, mivutano imezuka tena wiki hii baada ya Trump kwa hasira kuituhumu China kwa kujaribu kulegeza ahadi zake.

Shirika la Fedha la Kimataifa limetoa wito wa kupatikana ufumbuzi wa haraka, likionya kuwa mapambano hayo ya kibiashara ni "kitisho” kwa ukuaji wa uchumi duniani. Ushuru ulioongezwa utaathiri vifaa vya kielektroniki vya China, mashine, vipuri vya magari na samani.

Lakini kutokana na mchakato wa utekelezwaji wa viwango hivyo vya ushuru, bidhaa ambazo tayari zinapelekwa katika bandari za Marekani kabla ya usiku wa manane zitalipa tu kiwango cha awali cha asilimia 10 ya ushuru. Hayo ni kwa mujibu wa Ofisi ya Marekani ya Forodha na Ulinzi wa Mpakani.

Marekani inaishinikiza China kubadilisha sera zake kuhusu ulinzi wa hakimiliki za mali na kiwango kikubwa cha ruzuku kwa makampuni yanayomilikiwa na serikali, katika jaribio la kupunguza upungufu wa biashara.

Tangu mwaka jana, pande hizo mbili zimepandisha kodi za bidhaa za mwenzake za thamani ya zaidi ya dola bilioni 360 katika biashara ya pande mbili, na kuathiri bidhaa za kilimo za Marekani zinazouzwa China na kusababisha hasara kwa sekta za kutengeneza bidhaa za nchi zote mbili.

Taarifa ya wizara ya biashara ya China imesema wanatumai kuwa pande za Marekani na China zinaweza kukutana katikati na kufanya kazi pamoja kuyatatua matatizo yaliyopo kupitia ushirikiano na mazungumzo.

-DW

Marekani yaikamata meli ya Korea Kaskazini

$
0
0
Marekani imeikamata meli ya Korea Kaskazini ikiilaumu nchi hiyo kukiuka vikwazo vya kimataifa.

Idara ya haki ya Marekani imesema meli hiyo ilitumika kusafirisha makaa ya mawe ambayo ndiyo biashara kubwa ya taifa hilo licha ya kupigwa marufuku na Umoja wa Mataifa kuendelea kuyauza nje.

Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), meli hiyo ‘The Wise Honest’, ilikamatwa nchini Indonesia April mwaka jana, lakini Marekani ilitoa kibali cha kuikamata Julai mwaka huo.

Indonesia imeikabidhi Marekani meli hiyo na sasa inaelekea Marekani.

Hii ni mara ya kwanza Marekani kuikamata meli ya Korea Kaskazini kwa kukiuka vikwazo na hatua hiyo imekuja wakati ambapo uhusiano kati ya mataifa hayo mawili umedorora.

Mkutano kati ya kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un na Rais wa Marekani, Donald Trump uliisha bila makubaliano Februari mwaka huu, huku Marekani ikiisisitizia Korea Kaskazini kusitisha mpango wake wa nyuklia na nchi hiyo kwa upande wake ikitaka kuondolewa vikwazo vya kiuchumi kwanza.

Korea Kaskazini imetekeleza majaribio mawili ya makombora ya angani katika kipindi cha wiki moja katika kile kinachoonekana kuwa jaribio la kuishinikiza Marekani kufanya makubaliano.

Hata hivyo, maofisa wa Marekani wanasema uamuzi huo hautokani na majaribio ya makombora yaliyofanywa na Korea Kaskazini.

“Ofisi yetu iligundua mbinu ya Korea Kaskazini kuuza nje tani za makaa ya mawe ya kiwango cha juu kwa wanunuzi wa kigeni kwa kuficha asili ya meli The Wise Honest,” amesema mwendesha mashtaka wa Marekani, Goeffrey Berman.

"Mbinu hiyo iliifanya Korea Kaskazini kukwepa vikwazo mbali na kwamba meli hiyo ilitumika kuingiza mashine nzito nchini Korea Kaskazini ikisaidia uwezo wa taifa hilo na kuendeleza msururu wa ukiukaji wa vikwazo.”

Malipo ya utunzaji wa Wise Honest yanadaiwa kufanywa Marekani kupitia benki zisizojulikana, hivyo kuzipatia mamlaka za Marekani fursa ya kuchukua hatua hiyo.

Korea Kaskazini imekumbwa na msururu wa vikwazo vya Marekani na vile vya kimataifa kutokana na hatua yake ya kutengeneza silaha za nyuklia pamoja na kufanya majaribio ya silaha.

Kutana na Sheikh Omary Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali za Matatizo Yako Na Kutafsiri Ndoto kwa kutumia Vitabu vya QUR-AN

$
0
0
Sheikh Omary Ni bigwa wa kutatua matatizo kwa haraka, ni mtu aliye jaliwa kubuli Shufaa pia anatoa Duah  za Ruhia. Ukija na Maradhi yanaondoka hapo hapo bila kungoja kesho,  UKIPEWA MKONO  na Sheikh Omary .
 
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
 
Sheikh Omary ni Mtaalamu wa Nyota za Binadamu  Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
 
Je una NUKSI  zisizo kwisha.!? JE umekimbiwa na Mume/Mke na Anaishi na Mtu Mwingine..!? Muone Akutatulie,
 
Una kosa bahati ya wanaume au mume wa kukuoa..Unataka nyota ing'ae Au huna hamu na Mkeo/ Mumeo.
 
Jini mahaba. Kama Unakasirika ovyo ukiwa na bwana au mwanamke wako na  kumchukia Mpaka  kushindwa kufanya nae tendo la ndoa.
 
Njoo umuone Sheikh Omary  na ujuwe  yanayo kusibu.Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN

Mawasiliano: Sheikh Omary 0673531992 WhatsApp/Call
Tembelea Page ya @Mtabibu_Omar  @Mtabibu_Omar
Usome Makala Tofauti Tofauti Kama.

Serikali Yaipongeza Total Kwa Kuwekeza Sh. 460 Bilioni

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameipongeza kampuni ya TOTAL Tanzania kwa kuwekeza hapa nchini mtaji wa dola za Marekani milioni 200 (sawa na sh. bilioni 460) ndani ya miaka mitatu.

Alitoa pongezi hizo jana usiku (Alhamisi, Mei 9, 2019) kwenye sherehe za kutimiza miaka 50 kwa kampuni ya TOTAL hapa nchini, zilizofanyika jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Waziri wa Nishati, Dk. Medard Kalemani, mabalozi, Rais wa TOTAL Africa, wakandarasi na wafanyabiashara mbalimbali.

“Tangu mwaka 2015, kampuni ya TOTAL imewekeza hapa nchini mtaji mkubwa wa zaidi ya dola za Marekani milioni 200 ili kutoa huduma za uagizaji, uuzaji na usambazaji wa bidhaa za mafuta ikiwemo mafuta ya dizeli, petrol, vilainishi mbalimbali pamoja na bidhaa za nishasti mbadala (solar products),” alisema.

Sambamba na uwekezaji huo, Waziri Mkuu alisema, Watanzania zaidi ya 800 wamenufaika na ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja kutoka TOTAL ambapo kampuni hiyo imekuwa ikichangia sh. milioni 25 kila mwaka kwa ajili ya masuala ya usalama barabarani.

Shughuli nyingine za kijamii ambazo zimenufaika na uwepo wa kamuni hiyo nchini ni ujenzi wa madarasa (sh. milioni 45), ujenzi wa vituo vya afya (sh. milioni 80) na uchangiaji wa madawati 3,000 kwa baadhi ya shule za mkoa wa Dar es Salaam.

“Serikali ya awamu ya tano inaipongeza kampuni ya TOTAL kwa kuendelea kuwekeza nchini katika kipindi hicho cha miaka 50. Hongereni sana kwa ubunifu wenu na uwekezaji wa zaidi ya shilingi milioni 200 ili kusaidia wajasiriamali kupitia mpango ujulikanao kama The African Start Upper Challenge.”

“Nimearifiwa kuwa tayari Watanzania sita wamenufaika na mpango huo kwa kupatiwa zaidi ya shilingi milioni 25 za kuanzisha shughuli mbalimbali za ujasiriamali,” alisema Waziri Mkuu akielezea mpango huo ulioanzishwa mwaka 2016.

Kuhusu uwekezaji, Waziri Mkuu alisema Rais Dkt. John Pombe Magufuli kupitia Baraza la Biashara nchini amekuwa akikutana na jumuiya ya wafanyabiashara ili kujadili na kuzipatia ufumbuzi changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Alisema Rais Magufuli alianzisha Wizara ya Uwekezaji na kuiweka chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu ili iwe rahisi kwake kukutana na wawekezaji na kuzungumza nao moja kwa moja kuhusu vikwazo vya kibiashara wanavyokutana navyo.

“Tumeanza utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Kuboresha Mazingira ya Uwekezaji na Biashara nchini (blueprint) na tunafanya mapitio ya vivutio mbalimbali vya uwekezaji ikiwemo vivutio vya kikodi, kupitia timu maalumu,” alisema.

Aliwataka wawekezaji waliohudhuria sherehe hizo, waangalie Jiji la Dodoma kama fursa nyingine ya uwekezaji na njia ya kuunga mkono mkakati wa Serikali kuhamia Dodoma. “Sasa hivi Serikali tumetengeneza fursa nyingine ya uwekezaji, nayo ni Dodoma. Milango ya uwekezaji iko wazi na fursa za uwekezaji zipo. Ukitaka kujenga viwanda, majumba, mahoteli, njoo Dodoma. Ardhi tunayo, tutakupa,” alisisitiza.

Mapema, akielezea utendaji wa kampuni hiyo, Rais kampuni ya TOTAL Africa anayeshughulikia masoko na huduma, Bw. Stanislas Mittelman alisema kampuni hiyo ilianzishwa mwaka 1969 na siku zote wamekuwa wakiamini kuwa uimara wa mahusiano yao na Serikali, utatokana na uvumilivu na uaminifu wao kwa jamii ya Watanzania.

Alisema uwekezaji wanaoufanya ni sehemu ya ukuaji wao lakini pia ni njia yao ya kushiriki kuchangia azma ya Serikali ya ukuzaji wa viwanda ili kuelekea “Tanzania ya Viwanda”. “Tumeitikia wito wa Rais Magufuli wa kuongeza uwekezaji hapa nchini, tuliamua kuwa wabia Wakuu (leading partner) kwenye mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta litakalosafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda kuja Tanga, Tanzania,” alisema.

“Pia tumewekeza mtaji wa dola za marekani milioni 200 hasa kwenye ununuzi wa kampuni ya GAPCO, jambo ambalo limetusaidia tuongeze mtandao wetu mara tatu zaidi na kufikisha vituo zaidi ya 100 vya kuuzia mafuta hapa nchini. Pia tumezindua mtambo wa kisasa wa kusafishia mafuta ambao umetuwezesha kuingiza bidhaa mpya kwenye soko la Tanzania,” alisema.

“Kampuni ya TOTAL itaendelea kuwashirikisha Watanzania ubunifu tunaoupata kwnye Nyanja za kimataifa na hii inadhihirishwa na mabadiliko tuliyoyafanya kwenye kituo chetu cha kuhifadhia mafuta (fuel storage terminal) na utoaji wa mafuta bora ya kusafishia injini ya TOTAL Excellium,” alisema.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Rais wa Marekani Donald Trump Kasema Yuko Tayari Kufanya Mazungumzo na Iran

$
0
0
Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa yuko tayari kufanya mzungumzo na viongozi wa Iran, kama watamtafuta. 

Akizungumza na waandishi wa habari katika Ikulu ya Marekani, Trump alisema anatarajia viongozi wa Iran wampigie simu. 

Aidha rais huyo amesema kuwa aliamuru kupelekwa kundi la manowari zinazobeba ndege za kivita katika Ghuba ya Mashariki ya Kati kwa sababu ya vitisho vya Iran.

 Mwaka jana, Trump alijiondoa kutoka mkataba wa nyuklia na Iran na kisha akaongeza vikwazo dhidi ya nchi hiyo. Umoja wa Ulaya umetoa wito wa kuwepo suluhisho la kidiplomasia kwa mzozo huo. 

Hapo jana, viongozi wa jumuiya hiyo wakiongozwa na Kansela wa Ujerumani Angela Merkel walisisitiza kuhusu dhamira yao ya kuuheshimu muafaka huo wa mwaka wa 2015, lakini wakasisitiza kuwa hawatakubali masharti yoyote.

Iran Yaijibu Marekani Kuhusu Kufanya Mazungumzo......"Trump si mtu wa kuaminika"

$
0
0
Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amejibu madai ya rais wa Marekani kuhusu mazungumzo na Iran na kusema: "Donald Trump si mtu wa kuaminika".

Majid Takht-Ravanchi Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa ameyasema hayo wakati  akijibu swali la mtangazaji wa Televisheni ya NBC ya Marekani kuhusu iwapo Iran iko tayari kufanya mazungumzo na Marekani. Takht-Ravanchi aliongeza kuwa: "Awali Rais Donald Trump wa Marekani anapaswa kufafanua ni kwa nini alijiondoa katika meza ya mazugumzo."

Aidha Takht-Ravanchi amesema Trump aliondoka katika meza ya mazungumzo wakati ambao ulimwengu mzima ulikuwa katika meza ya mazungumzo na hata Baraza la Usalama liliidhinisha mazungumzo hayo.

Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa ameongeza kuwa, yamkini mazungumzo yakianza, rais wa Marekani kwa mara nyingine atajiondoa katika mazungumzo kwani anapinga na kubatilisha sheria za kimataifa.

Takht-Ravanchi aidha ameashiria madai ya rais wa Marekani kuwa anataka kufanya mazungumzo na Iran kwa lengo la kuizuia kupata silaha za nyuklia

Rais Trump wa Marekani jana aliandika katika ukurasa wake wa Twitter kuwa: "Nataka viongozi wa Iran wanipigie simu ili tuzungumze kuhusu mapatano mazuri mapatano ambayo yatawasaidia kuondoka katika mgogoro wa kiuchumi." 

Trump amedai kuwa, hataki mengi kutoka Iran isipokuwa tu kuhakikisha Iran haimiliki silaha za nyuklia.

Ikumbukwe kuwa mnamo Mei 8 mwaka 2018, Rais Trump wa Marekani aliamua kuondoa nchi yake katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA, ambayo ni mapatano ya kimataifa, na baada ya hapo akarejesha vikwazo dhidi ya Iran.

Polisi na Askari Magereza wapigana makonde hadharani, mabomu na risasi zarindima stendi ya mabasi

$
0
0
Polisi na Askari wa Jeshi la Magereza wilayani Masasi Mkoani Mtwara, wamepigana makonde hadharani katika eneo la stendi kuu ya mabasi barabara kuu iendayo Tunduru.

Akizungumzia tukio hilo,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Blasius Chatanda, alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 6 mchana baada ya askari polisi kumkamata askari Magereza ambaye inadaiwa alikuwa anaendesha pikipiki bila ya kuvaa kofia ngumu.

Hata hivyo, Kamanda Chatanda hakutaja majina ya askari huyo na polisi.

Chatanda alisema baada ya kutokea kwa ugomvi huo, Polisi walifyatua risasi hewani na kurusha mabomu ya machozi hali ambayo ilisababisha taharuki kubwa kwa wananchi wilayani humo.

Alisema muda kidogo walitokea askari Magereza watano ambao walifika eneo la tukio kwa ajili ya kumuokoa mwenzao, ndipo polisi na askari wa Magereza walipoanza kupigana.

Kamanda Chatanda alisema polisi huyo alikuwa doria katika operesheni ya kawaida ya ukamataji wa vyombo vya moto hasa pikipiki maarufu kama bodaboda, ambao wamekuwa wakiendesha bila ya kufuata sheria za usalama barabarani.

Alisema baada ya Polisi huyo kumshika askari magereza ambaye alikuwa kiendesha pikipiki bila ya kuvaa kofia ngumu na kumtaka kwenda kituo cha polisi au kuiacha pikipiki yake, alipinga ndipo mzozo ulipoanza.

“Baada ya muda kidogo kundi la askari magereza walifika kumuokoa mwenzao mara baada ya kumuona ameshikwa na Polisi, pia kundi la askari polisi walifika nao kumuokoa mwenzao, ndipo makundi hayo mawili ya jeshi walipoanza kuchapana makonde na kufyatua risasi hewani,” alisema Kamanda Chatanda.

Kamanda Chatanda alisema kufuatia tukio hilo, Jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi wa kujua chanzo zaidi ya vurugu hizo ikiwamo kufanya vikao vya dharura kati ya Jeshi la Polisi na Magereza, na kwamba uchunguzi utakapokamilika sheria itachukua mkondo wake.

 
Chanzo: Nipashe.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images