Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Serikali Yasema Ipo katika maandalizi ya muswada wa marekebisho ya Sheria ya VVU na UKIMWI ili kuruhusu watu kujipima wenyewe

$
0
0
Serikali iko mbioni kukamilisha muswada wa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote na kuuwasilisha bungeni Septemba.

Pia wizara hiyo ipo katika maandalizi ya muswada wa marekebisho ya Sheria ya VVU na Ukimwi sura Na 431 ili kuruhusu watu kujipima wenyewe na kushusha umri wa mtu kupima bila ridhaa ya mzazi au mlezi kutoka miaka 18 hadi 15.

Waziri wa  Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, akisoma bajeti ya wizara yake kwa mwaka 2019/20 bungeni jana, alisema maandalizi ya mpango huo yamekamilika ikiwamo mkutano wa kuelimisha wabunge kuhusu mkakati wa uboreshaji mfumo wa ugharamiaji wa bima  za afya.

Katika maandalizi hayo, alisema wabunge 19 walifanya ziara nchini Rwanda na Ghana Disemba mwaka jana kwa lengo la kupata uzoefu wa namna nchi hizo zilivyoweza kutekeleza mfumo huo wa bima kwa wote.

Katika hotuba hiyo, waziri Ummy alitaja vipaumbele vya wizara hiyo kwa mwaka 2019/20 kuwa ni pamoja na kuendelea kununua na kusambaza chanjo kulingana na mahitaji, kuwakinga watoto wa umri chini ya mwaka mmoja na magonjwa yanayozuilika kwa chanjo ambapo Sh bilioni 30 zimetengwa.

Kuhusu ukimwi, Ummy alisema huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na maambukizi na VVU zimeendelea kutolewa na idadi ya watu wanaotumia dawa ya kupunguza makali ya virusi vya Ukimwi imeongezeka kufikia wati 1,103,016 mwa Machi.

Alisema pia wizara yale kwa kushirikiana ile ya Viwanda na Biashara na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na Bohari ya Dawa imeandaa mwongozo unaoainisha fursa mbalimbali za uwekezaji katika viwanda vya dawa na vifaa tiba.

Mwongozo huo utarahisisha upatikanaji wa taarifa katika uwekezaji wa viwanda vya dawa nchini ambapo hadi kufikia Machi mwaka huu viwanda nane vya dawa vinaendelea kujengwa nchini.

Serikali Kuendelea Kutoa Elimu Ya Matumizi Ya Mbolea Ya Asili -Naibu Waziri wa Kilimo

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Serikali kwa kushirikiana na taasisi za sekta binafsi imeendelea kutoa elimu ya kilimo bora inayojumuisha matumizi sahihi ya mbolea za asili, viuatilifu vya asili, mbegu bora na hifadhi ya mazingira ili kuzalisha mazao kwa tija na kuwa na kilimo endelevu.

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba (Mb) ameyasema hayo bungeni Jijini Dodoma leo tarehe 8 Mei 2019 wakati akijibu swali la Mbunge wa Chambani Mhe Yussuf Salim Hussein aliyetaka kufahamu Serikali imeweka mikakati gani ya kutoa elimu ya mbolea ya asili kwa wakulima na hatua Serikali inayoichukua ili kuona kuwa Tanzania ni nchi inayoongoza kwa kuzalisha mazao yasiyotumia mbolea za viwandani.

Alisema kuwa katika kutekeleza mpango wa muda mrefu wa matumizi sahihi ya virutubisho vya udongo, Serikali kupitia Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) inafanya utafiti wa afya ya udongo katika Kanda zote saba za kiikolojia za kilimo nchini.

Utafiti huo unalenga kubaini aina za virutubisho na tabia za udongo katika maeneo mbalimbali nchini ili kuweza kutoa elimu kwa wakulima kuhusu kiasi, aina na matumizi sahihi ya mbolea za viwandani na asili. Utafiti huo umeanza kwa kuchukua sampuli za udongo katika Kanda za Nyanda za Juu Kusini, Kanda ya Kati, Kanda ya Kaskazini na sehemu ya Kanda ya Mashariki (Mkoa wa Morogoro) na utaendelea katika maeneo mengine nchini na kukamilika Juni 2020.

Alisema, kwa kutambua ongezeko la mahitaji ya mazao na bidhaa za kilimo zinazozalishwa kwa kutumia mbolea za asili na viuatilifu vya asili, Serikali imeboresha mtaala wa mafunzo katika vyuo vya kilimo ambapo mada za kilimo hai na hifadhi ya mazingira zimejumuishwa ili kuwawezesha maafisa ugani na wakulima kupata elimu hiyo.

Mhe Mgumba aliongeza kuwa Serikali kwa kushirikiana na Tanzania Organic Agriculture Movemet (TOAM), Sustainable Agriculture Tanzania (SAT), Ecology Agriculture chini ya SWISSAID, Zanzibar Organic Producers (ZANOP), Tanzania Alliance for Biodiversity (TABIO) na TANCERT inatoa elimu ya kilimo hai kwa wakulima na kutoa vyeti vya ubora wa mazao kwa ajili ya masoko maalum. Baadhi ya mazao ambayo yanazalishwa katika mfumo wa kilimo hai hapa nchini ni pamoja na kakao, kahawa, pamba na viungo.

Kadhalika, akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe Easter Michael Mmasi aliyetaka kufahamu kuhusu ushiriki wa wanawake kwenye sekta ya kilimo, Mhe Mgumba alisema kuwa Sekta ya Kilimo inajumuisha sekta ndogo za kilimo mazao, mifugo, uvuvi na misitu.

Bajeti za Wizara za Sekta ya Kilimo zinajumuisha bajeti za Wizara za sekta husika, Bodi za mazao na Taasisi mbalimbali zilizo chini ya Wizara za Kisekta. Utekelezaji wa bajeti hizo huwawezesha  wanaume na wanawake katika shughuli za kilimo. Wanawake wanachangia asilimia 90.4 ya nguvukazi ya wanawake inayotumika katika shughuli za kilimo na kuchangia wastani wa asilimia 70 ya mahitaji ya chakula nchini. 

Mhe Mgumba alisema kuwa katika kutatua changamoto hizo Serikali inaendelea kusimamia utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ya mwaka 2004 kupitia mifuko ya uwezeshaji ikiwemo Mfuko wa Maendeleo wa Wanawake (Women Development Fund - WDF) ambao huchangiwa asilimia 4 ya mapato ya Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kila mwaka. Katika mwaka 2017/2018, jumla ya Shilingi 15,633,312,764.91 zimetolewa kwa vikundi 2,919 vya wanawake na vijana vyenye jumla ya wanawake wajasiriamali 29,190 katika Halmashauri mbalimbali nchini.

Aidha, alisema kutokana na umuhimu wa wanawake katika kilimo Serikali imeielekeza Benki ya Maendeleo ya Kilimo (Tanzania Agricultural Development Bank – TADB) katika mikopo inayotoa asilimia 20 ya mikopo itolewe kwa vikundi vya wanawake. Hadi Januari 2019, asilimia 33 ya mikopo imetolewa katika vikundi vya wanawake kupitia Benki ya TADB. Vilevile, benki za NMB na Azania zimeanzisha dirisha maalumu la kutoa mikopo kwa vikundi vinavyo jishughulisha na kilimo na miradi mbalimbali. Pia Serikali imehamasisha wanawake kujiunga kwenye vikundi vya ushirika wa akiba na mikopo kama SACCOS, VICOBA ili kupata huduma za kifedha na mikopo kwa urahisi ili kuongeza mitaji yao katika kilimo.

Mhe Mgumba aliongeza kuwa, Serikali imeuelekeza Mfuko wa Pembejeo za Kilimo (Agricultural Input Trust Fund - AGITF) kutoa kipaumbele kwa vikundi vya wanawake vinavyoomba mikopo ya kuendeleza kilimo. Vile vile, Serikali imeendelea kutoa hati miliki za ardhi za kimila na hati miliki za ardhi kwa ajili ya kuwawezesha wanawake kumiliki ardhi na kuzitumia kama dhamana kukopa katika taasisi mbalimbali za kifedha ili waweze kupata mitaji ya kununua pembejeo na zana bora za kilimo ili kuongeza uzalishaji, tija na kuanzisha viwanda vidogo vidogo vya usindikaji wa mazao ya kilimo.

Serikari Kuwasilisha Taarifa Ya Utekelezaji Wa Malengo Ya Maendeleo Endelevu Umoja Wa Mataifa

$
0
0
Na Josephine Majura na Farida Ramadhani, WFM, Dodoma

Katika kutekeleza ajenda za Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG’s), Serikali imejipanga kuwasilisha Taarifa ya Mapitio ya Hiari (VNR) katika Jukwaa la Siasa la Umoja wa Mataifa (HLPF) mwezi Julai mwaka huu mjini Newyork nchini Marekani.

Hayo yameelezwa na  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango (Sera), Bw. Adolf  Ndunguru wakati akifungua kikao cha kujadili Taarifa ya utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG’s).

Bw. Ndunguru alisema kuwa uwasilishwaji wa taarifa hiyo utakuwa ni wa kwanza miongoni mwa mfululizo wa taarifa za mapitio mengine ambayo yanatokana na mapitio hayo yanayoonesha namna nchi inavyotekeleza Malengo hayo.

Alisema kikao hicho ambacho kinahusisha wadau wa ndani na nje ya nchi, ni muhimu kwa maendeleo ya nchi na wananchi kwa ujumla kwa kuwa kitajadili taarifa mbalimbali za utekelezaji wa Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu (SDG’s) kwa kuangalia maeneo muhimu kama elimu, afya na uchumi.

Bw. Ndunguru alisema kikao hicho kinatoa fursa kwa wadau hao kujadili rasimu ya awali ya taarifa ya utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG’s) na kutoa nafasi kwa wadau hao kuchangia  maoni yao kuhusu namna ya kuboresha taarifa hiyo kabla ya kuiwasilisha Umoja wa Mataifa.

“Tukiwa kama wananchama wa Umoja wa Mataifa, tumekubali kuingia mkataba wa kuutekeleza  Maendeleo Endelevu katika ajenda ya 2030 , kwa lengo la kuboresha maisha ya watanzania, kwa kuhakikisha tunapeleka elimu bora, afya bora  na kuboresha miundombinu”, alisema Bw. Ndunguru.

Bw. Ndunguru alibanisha kuwa mpaka sasa Tanzania inatekeleza kwa kasi ajenda hiyo ya 2030 ya Maendeleo Endelevu  kwa kuchukua hatua kadhaa ikiwemo kutoa kipaumbele katika masuala ya elimu, afya na kukuza uchumi wa nchi.

Naye mdau wa mkutano huo ambaye ni  mwakilishi wa Umoja wa Asasi za Kiraia nchini, Prisca Kowa alilisema kwa sasa nchi inaonekana imejipanga kisawasawa kutekeleza Maendeleo Endelevu kwa kuwa imeweza kuyahusisha maendeleo hayo katika mipango mikubwa ya maendeleo ya nchi.

 Ametoa wito kwa Serikali, Wizara, Taasisi na wadau wa maendeleo  kufanya kazi kwa kushirikiana ili kuhakikisha taarifa sahihi za utekelezaji wa Maendeleo Endelevu zinapatikana kwa usahihi na kwa wakati.

Waziri Mbarawa Atengua Uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Uchimbaji Visima na Uchimbaji Mabwawa- DDCA

PICHA: Mwili wa Reginarld Mengi Ulivyopokelewa Kijini Kwake Nkweseko Machame

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya May 9

Mdude Chadema Apatikana Akiwa Katika Hali Mbaya

$
0
0
Mdude Nyagali ‘Mdude Chadema’ , ambaye ni kada maarufu wa  Chadema amepatikana eneo la Inyala Mbeya Vijijini baada ya kudaiwa kutekwa na watu wasiojulikana Jumamosi jioni wiki iliyopita mjini Vwawa-Mbozi mkoani Songwe.

Taarifa za kupatikana kwa Mdude, zilitolewa na Diwani wa Kata ya Nsalala, Mbalizi, Kisman Mwangomale akisema amepigiwa simu na watu wa eneo la Makwenje Kijiji cha Inyala Mbeya vijijini, wakiomba msaada wa haraka kwenda kumbeba.
 
Mdude alidaiwa kutekwa Jumamosi wiki iliyopita na watu wasiojulikana ambao walifika ofisini kwake wakiwa na magari mawili yenye rangi nyeupe kisha kumchukua kwa nguvu na kumuingiza kwenye moja ya magari yao na kuondoka naye na kwenda kusikojulikana.

PolePole: Mzee Mengi alikuwa daraja kati ya CCM, sekta binafsi na serikali

$
0
0
Katibu Mwenezi wa CCM, Polepole amesema chama chake kinajivunia Mengi kuwa mwanachama wake kwa maelezo kuwa, alikuwa mshauri mkubwa wa masuala ya uchumi na biashara.

Polepole amesema mfanyabiashara huyo alikuwa bilionea mjamaa, alihangaika kuhakikisha kila binadamu anakuwa sawa na mwingine bila kujali hali wala nafasi yake na vilevile ndani ya CCM alikuwa kiungo kati ya chama na Serikali na wadau wa sekta binafsi.

“Alikuwa daraja kati ya sekta binafsi, CCM na Serikali yake, kila panapokuwa na mkwamo kabla mambo hayajaharibika Mzee Mengi alisimama kama kiungo kati ya chama, Serikali na wadau wa sekta binafsi ambao chama chetu kinaamini sana kwamba uchumi wetu unategemea ukuaji na uimara wa sekta hiyo,” amesema.

==>>Msikilize Hapo Chini

Mamia ya Waombolezaji Wajitokeza Kushiriki Ibada ya Mazishi ya Reginald Mengi

$
0
0
Mamia ya waombolezaji leo Alhamisi Mei 9, 2019 wamejitokeza katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Moshi Mjini kushiriki ibada ya mazishi ya aliyekuwa mwenyekiti wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi.

Baadhi ya waliofika kanisani hapo ni mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, mbunge wa kuteuliwa, Anne Kilango  na mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  ndo ataongoza ujumbe wa Serikali katika mazishi ya Mengi aliyefariki dunia usiku wa kuamkia Mei 2, 2019 Dubai, Falme za Kiarabu.

Mbowe Awataka Watanzania Kutogombanishwa.....Awataka waige Mfano wa Reginald Mengi

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amewataka Watanzania kutogombanishwa na kauli za viongozi hasa za kikabila na kidini huku akiwataka viongozi kutafakari maneno kabla ya kuyaongea kwani yanaweza kugawa watu na kuleta machafuko.

Aidha, Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai,  amemuelezea aliyekuwa Mwenyekiti wa Kampuni Tanzu za IPP, Dk. Reginald Mengi alikuwa ni mtu asiyekata tamaa.

Mbowe ameyasema hayo Mei 9, alipokuwa akitoa salamu za rambirambi katika ibada ya kumuaga aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni tanzu za IPP, Dk. Reginald Mengi iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Moshi Mjini mkoani Kilimanjaro.

“Kuna kauli zinasemwa sana watu na kwa ukweli zinakera kwa vile mimi si mnafiki lazima niseme na nitasema hapa hapa mbele za watu.

“Tuna nchi moja ambayo tunastahili kupendana na kusaidiana, na kila mtu ana haki ya kumsaidia mwenzie, tusikubali kauli za viongozi zitugawe na hasa za kidini na kikabila, kauli ya kusema kuna makabila hayawezi kuwasaidia walemavu si nzuri na haikutupendeza kwa kweli, tujitafakari tunapotaka kuongea maneno,” amesema Mbowe.

Aidha Mbowe ametoa wito kwa kila aliyeguswa na msiba wa Dk. Mengi kuyaenzi yale yate aliyokuwa akiyatenda enzi za uhai wake kwani hiyo ndiyo njia pekee ya kumuenzi.

“Mzee Mengi ameshatangulia mbele za haki haitajalisha tuzungumze mema kiasi gani kumuhusu hatutamrejesha, ila tujitafakari na kuyaenzi yale aliyokuwa akiyafanya, alikuwa mnyeyekevu na kauli zake zilijenga, kupatanisha na kuleta matumaini lakini pia hakuwahi kukata tamaa,” amesema Mbowe.

Rais Magufuli Akutana Na Ujumbe Kutoka Wizara Ya Ulinzi Ya Ujerumani, Ikulu Jijini Dar Es Salaam

Korea Kaskazini yarusha kombora huku mjumbe wa Marekani akiwasili Korea Kusini

$
0
0
Korea Kusini imesema jirani yake Korea Kaskazini imerusha kombora lingine leo ikiwa ni mara ya pili wiki hii. 

Kombora hilo limerushwa ikiwa ni masaa machache kabla baada ya kuwasili mjini Seoul, Mjumbe Maalum wa Marekani kwa Korea Kaskazini, Stephen Biegun, kwa mazungumzo na maafisa wa Korea Kusini kuijadili Korea Kaskazini na mpango wake wa makombora na silaha za nyuklia. 

Jumamosi iliyopita, Korea Kaskazini pia ilifanya zoezi la kijeshi na kurusha makombora kadhaa, mojawapo likiaminiwa kuwa ni la masafa mafupi. 

Ni ziara ya kwanza ya Biegun mjini Seoul, tangu mkutano wa kilele wa Hanoi kati ya Marekani na Korea Kaskazini kumalizika bila ya mafanikio. 

Katika mkutano huo, Kim Jong-un alisema atasitisha mpango wake wa nyuklia pale Marekani itakapoiondolea nchi yake vikwazo.

Iran yatishia kurejea katika matumizi ya nyuklia

$
0
0
Baraza la Usalama la Taifa la Iran limeamua kusitisha mara moja baadhi ya ahadi zake ilizozitoa chini ya mkataba wake wa nyuklia na nyengine katika siku 60 zijazo, iwapo hakutakuwa na hatua zozote kushughulikia mkwamo wa kiuchumi unaolikabili taifa hilo. 

Katika barua yake kwa mataifa yaliyoendelea kusalia kwenye makubaliano hayo ambayo Marekani ilijitoa, Iran imelalamikia kusitasita kwa makampuni ya mataifa hayo kufanya biashara nayo. 

Viongozi wa China, Ufaransa, Ujerumani, Uingereza na Urusi wamepokea barua hiyo, lakini walengwa zaidi ni viongozi wa mataifa ya Ulaya walioshindwa kutimiza ahadi zao ambazo zingesaidia kufufua uchumi wa Iran. 

Wataalamu wameliambia shirika la habari la AFP kwamba mkataba huo wa nyuklia unazitaka nchi zilizoweka saini kuimarisha uchumi wa Iran, lakini makampuni ya nchi za Ulaya bado yanaogopa kufanya biashara na Iran kwa hofu ya kuwekewa vikwazo na Marekani.

Taarifa Kwa Umma Kutoka Jeshi La Polisi Mkoani Mbeya Kuhusu Mdude Nyagali

$
0
0
Mnamo Mei 04, 2019 majira kati ya saa 19:00 na 20:00 usiku huko Vwawa, Wilaya ya Mbozi na Mkoa wa Songwe, Mtu mmoja aitwaye MDUDE MPALUKE NYAGALI [31] ilibainika kuwa amechukuliwa na watu ambao hakuweza kuwatambua na kupelekwa mahali pasipojulikana.

Taarifa zilifikishwa Polisi Mkoa wa Songwe na ufuatiliaji ulianza mara moja na mnamo tarehe 08 Mei, 2019 majira ya saa 21:00 usiku huko Inyala katika Kijiji cha Mtakuja kilichopo Mkoa wa Mbeya alionekana mtu anaomba msaada, ndipo Dereva wa Pikipiki @ Bodaboda aitwaye EMMANUEL KANAMGONDE na mwenzake AYUB WILSON walimbeba na Pikipiki hadi kwa uongozi wa serikali wa Kijiji cha Mtakuja.

Mhanga wa tukio hili baada ya kufikishwa kwa viongozi wa Kijiji hicho alijitambulisha kuwa yeye anaitwa MDUDE MPALUKE NYAGALI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo na akaomba wajulishwe viongozi wake. Kisha Mhanga alipelekwa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya kwa uchunguzi zaidi wa kitabibu.

Upelelezi wa shauri hili unaendelea ikiwa ni pamoja na msako mkali wa kuwatafuta waliohusika katika tukio hili.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521

Katibu Mkuu CCM Dk. Bashiru amuombea radhi Makonda, Askofu Shoo ampatanisha na Mbowe

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Bashiru Ally amemuombea msamaha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, kutokana na kauli yake aliyoitoa wakati wa kuaga mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Kampuni tanzu za IPP, Dk. Reginald Mengi katika viwanja vya Karimjee.

Katika kauli yake iliyozua sintofahamu, Makonda alisema hajawahi kuona mtu yeyote wa kabila la wachaga akitoa msaada au fedha kwa walemavu.

Kauli ambayo haikuwapendeza watu wengi akiwamo Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, ambaye wakati akitoa salamu za rambirambi katika ibada ya kuaga mwili wa Dk. Mengi iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Moshi Mjini, mkoani Kilimanjaro leo Alhamisi Mei 9, alikumbushia suala hilo na kuwataka Watanzania kutogawanywa kwa kauli na vitendo vya kibaguzi zinazotolewa na viongozi.

Akizungumza wakati akitoa salamu za rambirambi, Dk. Bashiru amesema kauli za Makonda zimesababishwa na wao kama walezi kushindwa kutoa malezi ya kutengeneza viongozi bora.

Dk. Bashiru amesema hayo baada ya kauli ya Askofu Mkuu wa KKKT Usharika wa Kaskazini, Fredrick Shoo kuzungumzia umuhimu wa kuwaandaa viongozi bora, watiifu na wanyeyekevu.

“Naomba nitumie fursa hii kumuombea msamaha kijana wangu Makonda, mimi namfahamu na hii ni mara yangu ya pili nimemsema hadharani, mara ya kwanza nilimsema Simiyu akaja analia ofisini nikamwambia ubadilike na kwa kweli ameanza kubadilika.

“Bado ni kijana mzuri shupavu na bado tunahitaji, lakini tunahitaji kuwasaidia vijana wetu,” amesema Dk. Bashiru.

Hata hivyo baada ya Dk. Bashiru kumaliza kuzungumza, Askofu Shoo alimuita Makonda na kumuombea msamaha kisha akawapatanisha na Mbowe.

“Makonda uko wapi? njoo tunakutangazia msamaha hapa hapa na nimekusamehe na hapa ni madhabahuni nimewaita kw ajili ya upatanisho,” alisema Askofu Shoo.

Aidha baada ya kuombewa msamaha Makonda aliwashukuru Dk. Bashiru na Askofu Shoo kwa kumuombea msamaha.

“Kwanza nashukuru kwa maelekezo na maonyo ya baba Askofu, na nashukuru kwa Katibu wangu Mkuu kwa kusimama na kuomba msamaha kwa niaba yangu lakini pia namshukuru kaka yangu Mbowe mimi na yeye tunafahamiana kwa muda mrefu na mbele ya baba yetu Mengi kwa kutamka yale yaliyomkwaza naye pengine angeweza kukaa kimya.

“Nahisi tafsiri inaweza kuwa tatizo naomba radhi kwa kumsifia mchaga katikati ya wachaga na si mchaga kati ya wengine na nitaendelea kumshukuru kwa yote aliyoyafanya katika mkoa wetu hususani kusaidia walemavu,” amesema Makonda.

Askofu Mkuu Dk. Shoo Awaonya Viongozi, Matajiri......Asema wasitumie nafasi zao kunyanyasa wengine, akemea ubaguzi

$
0
0
MKUU wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Mkuu Dk. Ferdinand Shoo amewaonya viongozi wa Tanzania na kuwataka watumie nafasi zao kuwasaidia wengine hasa wale wenye uhitaji.

Ametoa kauli hiyo leo (Alhamisi, Mei 9, 2019) wakati akitoa mahubiri kwenye ibada ya mazishi ya aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni za IPP, Dkt. Reginald Mengi iliyofanyika kwenye kanisa la KKKT, Usharika wa Moshi mjini.

Amesema kuna watu wakipata vyeo ama utajiri kidogo tu, wanatumia nafasi zao kunyanyasa wengine na akaonya Watanzania wasie wepesi wa kuhukumu, kunyanyasa wengine au kubagua wengine.

Katika mahubiri yake, Dk. Shoo amesema kama kuna dhambi ambayo binadamu anapaswa kuifanyia toba ni ile ya kubaguana na kama Watanzania wanahitaji Taifa lipokee baraka kutoka kwa Mungu, ni vema wakaacha kufanya hivyo. Amesema dhambi nyingine inayopaswa kufanyiwa toba ni ile ya watu wenye nafasi kuwakanyaga wengine.

“Ndugu zangu tukiwa na cheo, tukiwa matajiri, tukiwa na uwezo tuvitumie kuwasaidia wengine, tuache ubinafsi, tuache kiburi, tuache kujitutumua hasa kwa viongozi wa umri mdogomdogo. Kuna mahali mmefika mnajitutumua kama chatu, acheni kabisa. Naomba tuwe unyenyekevu ndugu zangu.”

“Wale wanaopata utajiri, acheni kukumbatia mali zenu, toeni na kuwasaidia wenye uhitaji kwani mnapata satisfaction kwa kufanya hivyo. Huu ni ujumbe kwetu sote na Mungu atusaidie tulishike hili. Muendelee kuiombea familia na yale mazuri mengi tuliyojifunza kwake tukayatende tukayatende, tuyaenzi,” amesema.

Akimuelezea Dkt. Mengi, Askofu Mkuu huyo amesema: “Aliwahi kusema kuwa, mali na utajiri ambao Mungu amempatia siyo kwa sababu yeye ni bora kuliko wengine, bali alimpa ili awe kama bomba la kufikisha baraka kwa wengine.”


“Leo mtu anapata vimilioni kadhaa tu anataka atembee juu ya migongo ya watu, anapata ka-cheo sijui ni diwani, Mkuu wa Mkoa au wa Wilaya, halafu unaona wenzako si kitu. Tuache na tutubu, acha kiburi namuomba Mungu atujalie roho hiyo ya unyenyekevu,” amesema.

Akizungumza kwa niaba ya Serikali, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Dkt. Mengi atakumbukwa kwa kitendo chake cha kuuchukia umaskini na zaidi kwa kazi mbalimbali ambazo alishiriki.

“Bila shaka kila mmoja wetu ameguswa kwa namna ya kipekee na mchango wa Dkt. Mengi. Kiukweli, marehemu Dkt. Mengi, atakumbukwa kama mwanahabari, mwanaviwanda na mfanyabiashara maarufu ambaye alitumia elimu, maarifa na utajiri wake kwa ajili ya manufaa ya wote hususan watu wenye mahitaji maalum,” amesema Waziri Mkuu.

Amewaomba wanafamilia wasimamie makampuni ambayo Dkt. Mengi aliyaanzisha na kama watakwama wasisite kuomba msaada serikalini kwani iko pamoja nao.

Akielezea wasifu wa baba yake, mtoto wa marehemu, Bw. Abdiel mengi alisema siyo rahisi kuyazungumzia yote kwa wakati mmoja mambo ambayo yamefanywa na Dkt. Mengi bali aliwashukuru waombolezaji wote, viongozi wa Serikali na wafanyakazi wa makampuni ya IPP kwa upendo wao.

“Mambo yote aliyoyafanya naweza kumwelezea katika sifa tatu kubwa ambazo ni alikuwa mzalendo, mwenye uthubutu na mwenye kupenda breakthrough. Alikuwa nafikiria tofauti na wengine. Kwanza anajiuliza kwa nini nifanye jambo hili, na nifanyeje ilikuwa ni suala la pili,” alisema.

Dkt. Mengi ambaye alifariki dunia alfajiri ya Mei 2, mwaka huu akiwa kwenye matibabu huko Dubai, Falme za Kiarabu, amezikwa katika makaburi ya familia huko Nkuu Sinde - Kisereni, Machame, wilayani Hai, mkoani Kilimanjaro. Ameacha mke na watoto wanne.

(mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
ALHAMISI, MEI 9, 2019.

Kutana na Sheikh Omary Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali za Matatizo Yako Na Kutafsiri Ndoto kwa kutumia Vitabu vya QUR-AN

$
0
0
Sheikh Omary Ni bigwa wa kutatua matatizo kwa haraka, ni mtu aliye jaliwa kubuli Shufaa pia anatoa Duah  za Ruhia. Ukija na Maradhi yanaondoka hapo hapo bila kungoja kesho,  UKIPEWA MKONO  na Sheikh Omary .
 
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
 
Sheikh Omary ni Mtaalamu wa Nyota za Binadamu  Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
 
Je una NUKSI  zisizo kwisha.!? JE umekimbiwa na Mume/Mke na Anaishi na Mtu Mwingine..!? Muone Akutatulie,
 
Una kosa bahati ya wanaume au mume wa kukuoa..Unataka nyota ing'ae Au huna hamu na Mkeo/ Mumeo.
 
Jini mahaba. Kama Unakasirika ovyo ukiwa na bwana au mwanamke wako na  kumchukia Mpaka  kushindwa kufanya nae tendo la ndoa.
 
Njoo umuone Sheikh Omary  na ujuwe  yanayo kusibu.Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN

Mawasiliano: Sheikh Omary 0673531992 WhatsApp/Call
Tembelea Page ya @Mtabibu_Omar  @Mtabibu_Omar
Usome Makala Tofauti Tofauti Kama.

Waziri Hasunga Aagiza Kufikia Julai 2019 Rasimu Ya Sheria Ya Kilimo Kuwa Imekamilika

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) leo tarehe 9 Mei, 2019 ameiagiza Timu ya wataalamu wa wizara ya Kilimo ambao wametuama kuandaa rasimu ya sheria ya kilimo na kufikia mwezi Julai 2019 iwe imekamilika.

Alisema kuwa ipo haja ya kuanzishwa kwa Sheria ya Kilimo itakayotoa suluhisho la changamoto zinazomkabili Mkulima na Sekta hiyo kwa ujumla hivyo ili kufikia malengo hayo ni lazima kuwa na ukomo wa ukamilishaji wa mpango kazi huo.

Waziri Hasunga ameyasema hayo leo tarehe 9 Mei 2019 wakati wa kikao na Menejimenti ya Wizara ya Kilimo, kikao kilichohudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Innocent Bashungwa, na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe.

“Kuna kila sababu ya kuanzishwa haraka sheria ya kilimo, kwa sababu hatuna Sheria ya Kilimo na inayotumika sasa ni Sera ya Kilimo, iliyotungwa mwaka 2013 ambayo pia inahitaji kuboreshwa ili iweze kuendana na mabadiliko mbalimbali ya kisera na wakati, ambapo lazima tuwe na rasimu yake kufikia mwishoni mwa mwezi huu wa Mei” amesema

Mhe. Hasunga ameongeza kuwa Sheria zinazotumika kwa sasa ni za Bodi za Mazao mbalimbali, ambazo pia zinachangamoto zake na kuna mazao ambayo hayana Bodi kiasi kwamba kuwatetea Wakulima wa mazao hayo inakuwa vigumu.

Mazao yaliyo katika utaratibu wa Bodi ni pamoja na zao la Pamba, Kahawa, Chai, Korosho, Pareto, Mkonge, Sukari na Tumbaku kwa upande wa mazao ya biashara, mazao ambayo hayana bodi ni yale ya chakula ambayo nayo yana mchango mkubwa katika uchumi wa Taifa.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Innocent Bashungwa (Mb) alisema kikao hicho ni cha kipekee kwakuwa kitapelekea kuimarisha mkakati wa pamoja wa Wizara ya kilimo kuwa na uelekeo katika utatuzi wa kero za wakulima kisheria.

Aidha, alipendekeza kuwa ni vyema sekta ya ushirika ikatajwa kwa umuhimu wake kwenye sera ya kilimo sambamba na Zana ndogo za Kilimo.

Tahadhari Kwa Umma Kuhusu Homa Ya Dengue Yazidi Kutolewa

$
0
0
NA WAJMW-DODOMA
Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imezidi kutoa tahadhari ya  kuwepo kwa ugonjwa wa homa ya Dengue nchini hususani katika Jiji la Dar Es Salaam na Tanga.
 
Tahadhari hiyo imetolewa leo na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhammad Kambi wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za wizara hiyo zilizoko jijini Dodoma.
 
Prof. kambi amesema hadi kufikia tarehe 6 Mei 2019, kati ya watu waliopimwa, wagonjwa 1237 wamethibitishwa kuwa na virusi au walikwishapata ugonjwa wa Dengue na kati yao 1150 ni kutoka Dar Es Salaam, 86 ni kutoka Tanga na mtu mmoja kutoka Singida.
 
Aidha, Prof Kambi amesema takwimu za ugonjwa wa Dengue kwa kipindi cha Januari hadi Aprili 2019 zinaonesha mwenendo wa ugonjwa huu kuwa na idadi ya wagonjwa 1237, vifo vya watu wawili na kuongeza kuwa waliofariki walikua na maradhi mengine.
 
Pamoja na hayo Mganga Mkuu huyo wa Serikali amelipongeza jiji la Dar Es Salaam kwa kuanza kunyunyizia dawa viuadudu (Biolarvicides) kwa ajili ya kuangamiza mazalia ya mbu ili kupambana na ugonjwa huu.
 
Vile vile amesema Wizara inaelekeza Mikoa na Halmashauri zote nchini kuendelea kuchukua hatua katika kudhibiti ugonjwa huu ikiwa ni pamoja na kufukia madimbwi ya maji, kunyunyizia dawa ya kuua viluwiluwi, kuondoa vitu vinavyosababisha mazalia ya mbu, kufyeka vichaka, kufunika mashimo ya maji taka kwa mifuniko pamoja kusafisha gata za paa la nyumba na kutoruhusu maji kusimama.
 
Prof. Kambi amesema Wizara kwa kushirikiana na Mikoa na Halmashauri zote nchini itaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kudhibiti ugonjwa huu ikiwa ni pamoja na kuendelea kuangamiza mazalia ya mbu na viluwiluwi, kuweka mpango wa dharura wa miezi sita kuanzia Mei mpaka Oktoba ili kukabiliana na ugonjwa huu. 

Pia amesema Serikali imenunua Vitendanishi vyenye uwezo wa kupima wagonjwa 1870 na vimesambazwa kwenye vituo maalum vya ufuatiliaji wa ugonjwa huu nchini kote.
 
Mwisho Prof. Kambi amewataka wananchi kuendelea kuchukua hatua za kujikinga kuumwa na mbu kwa kuvaa nguo ndefu, kutumia vyandarua vyenye viuatilifu, kutumia dawa za kufukuza mbu na kuweka nyavu kwenye madirisha na milango ya nyumba za kuishi ili kukabiliana na ugonjwa huu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images