Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Naibu Waziri Mavunde Akutana Na Kufanya Mazungumzo Na Mwakilishi Wa UNICEF Nchini

$
0
0
Na; Mwandishi Wetu
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde amekutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi Mkazi wa UNICEF nchini Bi. Maniza Zaman ambaye amemaliza muda wake alipomtembelea Ofisi kwake iliyopo Jijini Dodoma.

Katika mazungumzo yao, Mhe. Mavunde amelipongeza Shirika la Umoja wa Mataifa la UNICEF kwa kushirikiana na Serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo na kwa kutoa misaada katika sekta mbalimbali nchini.

“UNICEF imekuwa ikishirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu katika masuala mbalimbali yaliyolenga kuboresha na kuimarisha utekelezaji wa Sera ya Hifadhi ya Jamii (Social Security Policy of 2003), kuwapatia mafunzo watumishi katika masuala ya virutubishi na hifadhi ya jamii, pia kuwapatia vitendea kazi kama vile komputa na magari ambayo yanatumika kwenye miradi mbalimbali,” alieleza Mavunde. 

Aliongeza kuwa, Serikali imeguswa na jitihada za UNICEF na itaendeleza ushirikiano na shirika hilo katika kutekeleza jukumu la kuhudumia Watoto.

Aidha, Naibu Waziri Mavunde alimpongeza Bi. Maniza Zaman kwa kazi nzuri aliyofanya kipindi cha muda wake na kumsihi kuendelea kuwa balozi mzuri wa masuala ya Watoto.

“Tutakukumbuka kwa juhudi na ushauri uliokuwa ukitupatia katika masuala ya elimu na haki za Watoto,” alisema Mavunde. 

Kwa upande wake, Bi. Maniza Zaman amesema anaishukuru Serikali kwa ushirikiano iliompatia kwa kipindi chote alichokuwa hapa nchini.
 

Waziri wa Fedha Dkt. Mpango Aagana Na Mwakilishi Wa UNICEF Tanzania.

$
0
0
Na Josephine Majura, WFM, Dodoma
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.  Dkt.  Philip Isdor Mpango amelishauri  Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Watoto (UNICEF), kuweka namna bora ya kuingiza ajenda ya uwekezaji kwa watoto katika mikutano mbalimbali  inayofanyika Barani Afrika.

Hayo ameyasema alipokuwa akiagana na Mwakilishi Mkazi wa  Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Watoto (UNICEF) Bi.  Maniza Zaman, anayehamia nchini Kenya.

Dkt. Mpango alisema Shirika hilo linatakiwa kuweka mkazo huo ili kuhakikisha nchi za Afrika zinaweka mipango ya kuwekeza kwa ajili ya watoto kwa kuwa kundi hilo  ndiyo Taifa la kesho.

Alisema Serikali ya Tanzania kwa kutambua umuhimu wa Sekta ya Elimu Nchini, imekuwa ikitoa kipaumbele katika elimu kwa kutoa elimu ya awali, msingi na sekondari bure kwa lengo la kutoa nafasi kubwa kwa watoto ili wapate haki yao ya msingi.

Aidha Dkt. Mpango alisema kuwa katika kuboresha Sekta ya Elimu Duniani ni vema pia masuala ya lishe bora kwa mtoto yakatiliwa mkazo kwani lishe bora inachangia afanye vizuri dararasani lakini pia itamsaidia mtoto kuwa na afya bora itakayomfanya aweze kufikiri vizuri.

“Nitahakikisha agenda za kulinda haki ya mtoto nchini inapewa kipaumbele kwenye mikutano yetu mikubwa tunapokuwa tukijadili masuala ya maendeleo kwa ujumla”, alisisitiza Dkt. Mpango.

Aliongeza kuwa jukumu la kumlinda mtoto ni la kila mmoja kwakuwa wote walishawahi kuwa watoto hivyo ni vema kila mmoja atomize jukumu hilo.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Watoto (UNICEF) Tanzania Bi.  Maniza Zaman, anaye hamia nchini Kenya, ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa kufanya nae kazi vizuri kwa kipindi chote alichokaa nchini.

“Tanzania ni nchi nzuri, watu wake wana upendo, wana utu na wakarimu  karibu kwa mikoa yote 19 hadi 20 niliyowahi kutembelea wakati wa kutekeleza majukumu yangu”, alisema Bi. Maniza.

Alitoa wito kwa Serikali, kuendelea kutoa kipaumbele kwa ajili ya Sekta ya Elimu na Afya kwa kuongeza angalau asilimia moja ya bajeti kila mwaka kwakua zimekuwa na changamoto nyingi kutokana na ongezeko kubwa la  idadi ya watu kila siku.

Pia aliiomba Serikali ibuni mbinu na kuweka mipango endelevu kwa ajili  ya watoto itakayowasaidia katika siku zijazo kwa kuwa takwimu zinaonesha kuwa takriban watoto milioni 2 huzaliwa kila mwaka.

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Isdor Mpango alimuahidi aliyekuwa Mwakilishi mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Watoto (UNICEF) Bi.  Maniza Zaman, kuwa Wizara yake itaendelea kuhakikisha Sekta hizo zinapata bajeti ya kutosha katika mgawanyo.

Dkt. Mpango amemshukuru kwa kufanya kazi nchini na kumkaribisha tena na tena hasa kipindi cha mapumziko ambapo amesema milango ipo wazi muda wowote atakapojisikia kutembelea Tanzania.

Mbunge Ataja Sababu za Wananchi Wa Lindi Kuwa Wafupi

$
0
0
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Lindi, Riziki Lulida (CUF), amesema wananchi wa mkoa huo wanakuwa wafupi kwasababu ya kubeba mizigo kichwani kwa kukosa usafiri kupitia barabara.

Lulida ameyasema hayo bungeni bungeni leo Mei 10, ambapo amesema kuwa Mkoa huo umekuwa ukitengwa kila mwaka kwa kunyimwa miradi mikubwa ya kiuchumi ikiwamo ya barabara.

Lulida ametolea mfano wa barabara za jimbo la Liwale kwamba hazikuwahi kujengwa kwa kiwango cha lami tangu serikali ya awamu ya kwanza.

“Mheshimiwa Naibu Spika kuna ubaguzi unafanywa na mawaziri katika kugawa miradi hapa nchini, huko Lindi  Liwale tumekuwa kama Guantanamo,  ninashauri Bunge tutengue kauli ya kuapa kwa kutumia biblia au quran, tutumie katiba badala ya hiyo misahafu kwa sababu hivyo vitabu havitaki uongo.

“Niwaambie huko Lindi mnazuia kangomba ya korosho wakati hamjengi barabara,  wale wafanyabiashara wanaamua kupeleka magari yao hata kwa shida lakini mnawazuia kununua korosho, je mnataka watu wafanyeje, leo hii watu wa Lindi wamekuwa wafu

Serikali Yatoa Wito Kwa Wadau Kuunga Jitihada Za Ujenzi Kituo Cha Kumbukumbu Za Baba Wa Taifa

$
0
0
Na Anitha Jonas – WHUSM
Serikali yatoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza kuunga mkono jitihada za ukarabati na ujenzi  kituo cha kitalii Wilayani Kongwa Jijini Dodoma ambacho kitahifadhi kumbukumbu za Baba wa Taifa Hayati Mwl.Julius Nyerere .

Wito  huo umetolewa leo bungeni  jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Habari  Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza  alipokuwa akijibu Swali la Msingi la Mbunge wa Mtera Livingstone Lusinde (CCM) lililokuwa likiuliza ni lini serikali itajenga maktaba yenye kumbukumbu za kazi za Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambapo kituo hicho kitakuwa sehemu ya utalii na kitajengwa Makao Makuu ya nchini  ya Jijini Dodoma.

“Katika utekelezaji wa Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika,Serikali imeteua Wilaya ya Kongwa kuwa Kituo Kikuu cha Kumbukumbu za ukombozi nchini na katika kituo hicho kitakuwa na miundombinu kadhaa ya uhifadhi wa historia za viongozi ambazo zitajengwa ikiwemo kazi adhimu za Baba wa Taifa,”alisema Mhe.Shonza.

Akiendelea kuzungumza wakati akijibu swali hilo la msingi Naibu Waziri huyo alisema Serikali kwa kushirikiana na UNESCO imekarabati Studio za Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) zilizopo Barabara ya Nyerere na kuwa kituo adhimu cha hifadhi rejea ya kazi za Baba wa Taifa.

Pamoja na hayo Mheshimiwa Shonza  akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalum Dodoma (CCM) Felister Bura lililohoji lini ujenzi wa kituo hicho cha kumbukumbu cha Kongwa utaanza,Mheshimiwa Shonza alisema ujenzi wa kituo hicho umekwishaanza tangu mwaka 2015 ambapo ukarabati wa kituo hicho ulikwisha anza na unaendelea na pia kuna mipango mikubwa katika kituo hicho ikiwemo kujenga miundombinu ya kisasa mfano hoteli za nyota tano na kiwanja cha ndege.

Halikadhilika katika swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalum Tabora (CCM)Mwanne Mchemba lini serikali itaingiza katika orodha kituo cha Tabora kutambulika rasmi kama kituo cha kumbukumbu za Baba wa Taifa kutokana na historia yake na mambo aliyoyafanya Mkoani hapo,ambapo Mheshimiwa Shonza alimuhakikishia Mbunge huyo kuwa Mkoa wa Tabora ni miongoni mwa Mikoa Kumi na Tano iliyoteuliwa kupitia Programu ya Urithi wa Ukombozi  wa Bara la Afrika kuwa vituo vya uhifadhi wa historia hiyo.

Pamoja na hayo serikali inaunga mkono juhudi za taasisi mbalimbali zinazofanya uhifadhi wa amali za Urithi wa kumbukumbu za Baba wa Taifa na baadhi ya taasisi hizo ni Maktaba ya Taifa Dar es Salaam,Makumbusho ya Taifa  Dar es Salaam,Makumbusho ya Mwl.Nyerere Butiama,Taasisi ya Mwalimu Nyerere na Vituo vya Televisheni vya TBC na ITV.

Taarifa Ya Mwenendo Wa Hali Ya Hewa Hususan Mvua Za Mfululizo Zinazoendelea Kunyesha Katika Baadhi Ya Maeneo Hapa Nchini.

$
0
0
Taarifa hii inatoa mwenendo wa hali ya hewa hususan mvua za mfululizo zinazoendelea kunyesha katika baadhi ya maeneo hapa nchini.

Mvua zinazoendelea kunyesha hapa nchini hususan katika maeneo ya pwani ya kaskazini, nyanda za juu kaskazini mashariki na kanda ya ziwa Victoria ni sehemu ya mvua za Masika. 

Mvua hizi zinatokana na kuimarika kwa ukanda wa mvua (ITCZ). Mvua za mfululizo katika baadhi ya maeneo ya pwani ya kaskazini (mikoa ya Tanga, Dar es salaam na Pwani pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba) zinatarajiwa kuendelea kwa kipindi cha siku mbili zijazo (mpaka siku ya jumapili tarehe 12 Mei 2019). 

Aidha vipindi vya mvua za mfululizo vinatarajiwa kujirudia kuanzia katikati ya mwezi Mei, 2019. Mamlaka itatoa taarifa za mara kwa mara za mwenendo wa mvua hizo katika taarifa zake za utabiri.

ANGALIZO: Pamoja na kwamba mvua za masika zinatarajiwa kupungua katika maeneo mengi mwishoni mwa mwezi Mei, 2019; athari za mvua kubwa zilizonyesha katika kipindi cha wiki moja mfululizo katika ukanda wa pwani ya kaskazini pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba zimesababisha kutuama kwa maji na mafuriko. 

Hivyo kutokana na ardhi kuwa na unyevunyevu mwingi, ongezeko kidogo la mvua linaweza kuendelea kusababisha athari kama zilizokwisha jitokeza.

USHAURI: Wananchi wanashauriwa kuendelea kufuatilia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania na kuzingatia tahadhari zilizotolewa na mirejeo yake pamoja na kupata na kuzingatia ushauri na miongozo ya wataalam katika sekta husika ili kupunguza athari zinazoweza kujitokeza.

Mahakama Kuu ya Tanzania Yabatilisha vifungu vya sheria vinavyowapa mamlaka Wakurugenzi wa Halmashauri kusimamia Uchaguzi

$
0
0
Mahakama Kuu ya Tanzania  imebatilisha sheria inayowapa mamlaka Wakurugenzi wa Halmashauri kusimamia Uchaguzi Mkuu.

Uamuzi huo umetolewa na Jaji Atuganile Ngwala kwenye kesi ya msingi namba 6 ya mwaka 2018 iliyofunguliwa na mtoto wa marehemu Chacha Wangwe ambaye ni Bob Chacha Wangwe.

Katika kesi hiyo ya Kikatiba, Jaji Ngwala amebatilisha vifungu viwili vya Katiba cha 7 (1) ambapo kinaeleza kuwa ‘Kila Mkurugenzi wa Jiji na Halmashauri wanakuwa wasimamizi wa Uchaguzi Mkuu’

Pia imebatilisha Kifungu cha 7 (3) kinachoeleza kuwa Tume inaweza kumchagua mtu yoyote kuwa msimamizi wa Uchaguzi wakati katiba inasema huwezi kuwa Mwanasiasa na ukawa msimamizi wa uchaguzi bali inatakiwa achaguliwe mtu huru.

Baada ya kueleza hayo, Jaji Ngwala amesema anazifuta sheria hizo na kama kuna upande haujaridhika ukate rufaa.

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Taarifa Inayosambaa Mitandaoni Kuhusu mifuko ya Plastiki

Naibu spika Guaido akamatwa

$
0
0
Maafisa wa upelelezi wa Venezuela wamemkamata kiongozi wa ngazi ya juu wa bunge linalotawaliwa na upinzani, Edgar Zambrano, ikiwa ni hatua ya hivi karibuni dhidi ya wabunge walioamua kujiunga na vuguvugu lililoshindikana na kumuondoa madarakani Rais Nicolas Maduro mwezi uliopita. 

Zambrano ni naibu wa spika wa Juan Guaido, mtu anayetambuliwa kama kiongozi wa mpito wa Venezuela na mataifa zaidi ya 50, na ambaye aliongoza vuguvugu la kumuondoa madarakani Maduro mnamo Aprili 30. 

Rais wa Marekani Donald Trump amelaani hatua hiyo ya kukamatwa kwa Edgar Zambrano. "Kinachotokea nchini Venezuela ni aibu .. Watu wanakufa, hawana chakula, hakuna maji. Hii ni moja ya nchi zilizo tajiri sana ulimwenguni. Na sasa wanaishi vibaya sana. 

"Na tunafanya kazi kwa bidii juu ya tatizo hilo na tunajitahidi kuwa wagumu," amesema Rais Donald Trump. 

Kwa upande mwingine, Mahakama Kuu ya Venezuela iliwashtaki wabunge watatu kuunga mkono uasi wa Guaido uliosababisha siku mbili za mapigano kati ya vikosi vya usalama na waandamanaji.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya May 11

Tanasha Akataa Kubadili Dini Aolewe Na Diamond Platnumz

$
0
0
Mpenzi wa msanii Diamond Platnumz, Tanasha amesema kuwa si rahisi kwa yeye kubadilisha dini kisa mahusiano  ila mapenzi yake na muimbaji huyo  yako pale pale.

Tanasha amefunguka hayo alipokuwa akihojiwa na Block 89 ya Wasafi FM kwa kueleza kuwa kila mmoja anaheshimu dini ya pande zote mbili.

"Mara ya kwanza nilikuwa na wasiwasi wakati tunaanza uhusiano, Diamond Platnumz ni star na nini. Naheshimu dini yake na yangu pia, sitabadilisha dini lakini mapenzi yatabaki" amesema Tanasha. 

==>>Msikilize hapo chini

Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari Kuhusu Fursa Za Masomo

$
0
0
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imepokea nafasi za masomo ya muda mrefu katika fani ya Sayansi kutoka Serikali ya Misri.

Masomo hayo ambayo ni  kwa ngazi ya Shahada ya Uzamili na Uzamivu yatatolewa kwenye Chuo Kikuu cha Alexandria kilichopo nchini Misri chini ya udhamini wa Mpango wa Bonde la Mto Nile (Nile Basin Initiative).

Mwisho wa kuomba nafasi hizo ni tarehe 30 Mei 2019. Kwa maelezo zaidi kuhusu kozi hizo na namna ya kuomba, tafadhali tembelea tovuti ifuatayo: www.nbs.alexu.edu.eg
 
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
10 Mei 2019

Marekani yatuma mfumo wa kukinga makombora na meli ya kijeshi mashariki ya kati huku wasiwasi kati yake na Iran ukiendelea

$
0
0
Marekani inatuma mfumo wa kujilinda dhidi ya makombora na meli ya kivita katika eneo la mashariki kutokana na hali ya waiswasi iliopo katiya taifa hilo na Iran.

Meli hiyo ya kivita ya USS Arlington, inayosafirisha magari na ndege , itajiunga na kundi la kijeshi la USS Abraham Lincoln katika ghuba , maafisa wanasema.

Makombora ya US B-52 bombers pia yamewasili katika kambi moja nchini Qatar , idara hiyo imesema.

Imesema kuwa hatua hiyo inafuatia vitisho vya operesheni za vikosi vya kijeshi vya Marekani katika eneo hilo.

Marekani imetoa habari chache kuhusu uwezo wa tishio hilo , ambao Iran umepinga kama ujinga, ikitaja hatua hiyo ya Marekani kama vita vya kiakili vyenye lengo la kuitishia nchi hiyo.

Wakati huohuo chombo cha habari cha Isna News Agency kilimnukuu kiongozi mmoja mkuu wa dini , Yousef Tabatabai-Nejad akisema kuwa ''msafara huo wa Marekani unaweza kuharibiwa na kombora moja pekee''.
 
Siku ya Ijumaa idara ya Pentagon ilisema kuwa Marekani haitaki vita na Iran lakini Washington iko tayari kulinda vikosi vya Marekani na mali yake katika eneo hilo.

''Idara ya ulinzi inaendelea kufuatilia kwa karibu vitendo vya utawala wa Iran'', ilisema katika taarifa.

Iliongezea kuwa mfumo huo wa makombora ambao unaweza kutungua makombora ya masafa marefu na yale ya chini chini na ndege za kijeshi pia utapelekwa katika eneo hilo iwapo kuna uwezekano wa shambulio lolote.
 
Maafisa wameambia vyombo vya habari vya nchini Marekani kwamba meli hiyo ya USS Arlington ilitarajiwa kuwasili katika eneo hilo lakini imepelekwa katika eneo hilo mapema ili kutoa uwezo wa amri zitakazotolewa na udhibiti.

Siku ya Jumapili , mshauri wa maswala ya usalama nchini ,Marekani John Bolton amesema kuwa kupelekwa kwa vifaa hivyo vya kijeshi kutatoa ujumbe wa wazi kwa utawala wa Iran kwamba shambulio lolote dhidi ya mali ya Marekani katika eneo hilo litajibiwa na uwezo mkubwa wa kijeshi.

Meli hiyo ya USS Abraham Lincoln ilipita kupitia rasi ya Suez siku ya Alhamisi , kulingana na idara ya ulinzi nchini Marekani

Taarifa kuhusu matibabu ya Homa ya Dengue kwa wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

Ufahamu ugonjwa wa Homa Ya Dengue

$
0
0
Dengue ni ugonjwa unaosababishwa na virusi viitavyo Dengue vinavyosambazwa na mbu aina ya Aedes . 

Mbu huyu anayeambukiza homa ya dengue hupendelea kuishi karibu na makazi ya watu na huweza kuuma binadamu mchana na usiku. 

Ugonjwa huu huathiri sana nchi za tropiko kama Amerika ya kusini na Africa. Ni moja kati ya homa kali inayodhoofisha na  kuambatana na maumivu makali. 

Kwa sasa, hakuna kinga ya homa ya dengue, njia pekee ya kuepuka ugonjwa huu ni kuzuia kuumwa na mbu anayesambaza homa ya dengue.
 
Dalili za homa ya dengue

•Homa kali ya ghafla

•Maumivu makali ya kichwa

•Macho kuuma

•Maumivu ya viungo

•Kichefuchefu

•Kutapika

•Vipele ambavyo hutokea siku nne baada ya homa kuanza

•Kutoka damu puani, kwenye fizi na kuchubuka kirahisi

Mara nyingi dalili huwa sio kali na wengi hudhania ni homa ya mafua au maambikizi mengine ya virusi. Dalili hizi huanza kutokea baada ya wiki mbili, lakini kwa wengi huchukua wiki moja ya kwanza na tayari utaanza kuona dalili za dengue.

Matatizo ambayo yanaweza kutokea baada ya maambukizi ya homa hii ni

•Homa kali zaidi

•Kuharibiwa kwa tezi na mishipa ya damu

•Kutokwa na damu zaidi puani na kwenye fizi

•Ini kuwa kubwa

•Na huweza kupelekea kifo

Vipimo

•Damu huchukuliwa na kuangalia virusi vya dengue au

• Kingamwili dhidi ya virusi hizi

Matibabu

Mpaka sasa hamna dawa kwa ajili ya ugonjwa huu ila  dawa za kupunguza homa na maumivu huweza kutumika kwa mfano:

•Paracetamol

•Pumzika vya kutosha

•Kunywa maji

•Nenda hospitali ukapate ushauri wa daktari

NEC yakana tangazo la ajira la kitapeli

$
0
0
Tume ya Taifa ya chaguzi inapenda kuutaarifu Umma kuwa, haihusiki na matangazo ya nafasi za ajira yaliyobandikwa katika maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Moshi Mkoani Kilimanjaro.
 
Matangazo hayo yanaeleza kuwa, Tume imetoa ajira za muda, na wananchi walioomba ajira hizo wamekuwa wakiambiwa watoe kiasi cha fedha kwa madai kuwa ni kwa ajili ya mafunzo.
 
Hatua kali za Kisheria zitachukuliwa dhidi ya mtu au kundi la watu wanaotumia au wanaopanga kutumia jina la Tume ya Taifa ya Uchaguzi kufanya vitendo vya kihalifu.
 
Tunapenda kuwashukuru wananchi na kuwasihi kuendelea kutoa taarifa mara tu wanapohisi uwepo wa watu au kundi la watu wenye nia mbaya ya kulichafua jina la Tume yaTaifa yaUchaguzi.
 
Dkt. Athumani Kihamia
MKURUGENZI WA UCHAGUZI

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521

Aunty Ezekiel awavaa wanaohoji kuhusu mpenzi wake

$
0
0
Staa wa Bongo movie, Aunt Ezekiel amewataka wanaofuatilia mahusiano yake kumwachia mwenyewe, huku akidai suala la yeye kuwa na wanaume aliowazidi umri kwake si tatizo.

Aunt Ezekiel amesema amekuwa akikutana na maneno mengi, huku wengi wakidai amekuwa na tabia ya kutembea na wanaume wadogo kuliko umri wake, kitu ambacho kwake haoni tatizo, kwa kuwa wengi hawajui hayo ni maisha binafsi ya mtu.

“Suala la mimi kutembea na wanaume wadogo sidhani kama linatakiwa liingiliwe, haya ni maisha binafsi ya mtu, najua kila mmoja ana aina ya maisha anayotaka aishi, nadhani sipaswi kuingiliwa katika hili zaidi ya watu kushabikia kile ninachofuata,”alisema Aunt.

Kwa sasa inadaiwa staa huyo ameachana na baba wa mtoto wake, Mose Iyobo, ambaye ni mnenguaji wa lebo ya WCB, ambao walijaliwa kupata mtoto aitwaye Cookie.

Mauaji Ya Mwanafunzi Wa Scolastica: Wazee washauri wa mahakama Watoa Ya Moyoni

$
0
0
Wazee washauri wa mahakama katika kesi ya mauaji ya mwanafunzi wa shule ya Scolastica, Humphrey Makundi (16), wametofautiana huku mmoja akisema washtakiwa wote wana hatia ya mauaji ya kukusudia.

Hata hivyo, mmoja wa wazee hao ameona mshtakiwa wa pili, Edward Shayo ambaye ni mmiliki wa shule hiyo apewe adhabu ndogo kwa maelezo kuwa kosa lake ni kuzembea kutoa taarifa ya mauaji.

Kifungu cha 196 cha kanuni ya adhabu sura ya 16, kinaeleza mtu yeyote anayesababisha kifo cha mtu mwingine bila uhalali wa kisheria anatenda kosa la mauaji na adhabu yake ni kunyongwa hadi kufa.

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni mshtakiwa namba moja, Hamis Chacha ambaye ni mlinzi wa shule na Laban Nabiswa, mshitakiwa wa tatu ambaye ni mwalimu wa nidhamu shuleni hapo.

Kauli za wazee hao zilijitokeza juzi kati ya saa 11:00 alasiri na saa 1:30 usiku wakati Mahakama Kuu chini ya Jaji Firmin Matogolo anayesikiliza kesi hiyo, ilipoketi kupokea maoni ya wazee hao.

Kabla ya kuanza kupokea maoni hayo, Jaji Matogolo aliwasomea wazee hao muhtasari wa ushahidi wa upande wa mashtaka na ule wa utetezi wa washtakiwa pamoja na mashahidi wao waliowaita.

“Nyie (wazee washauri) ni waamuzi wa ushahidi siyo waamuzi wa sheria. Ili kuthibitisha shtaka la mauaji ya kukusudia ni lazima kuwe na kitendo cha kuua na dhamira ya kuua,” alisema Jaji Matogolo.

“Dhamira ya kuua inaweza kuthibitishwa na aina ya silaha iliyotumika kama ipo na nguvu iliyotumika. Mambo mengine ni matendo ya mshtakiwa kabla, siku ya mauaji na baada.”

Jaji alisema, “mmesikia mazingira yote ya kupotea kwa mwanafunzi (Humphrey) na baadaye mwili wake kupatikana mtoni na kutambuliwa kwake. Pia mmesikia sababu za kifo kuwa ni kuumia sana kichwani.

“Naamini pia mlisikia ushahidi wa shahidi wa 14 (Irene Mushi) wa upande wa mashtaka ambaye ni mlinzi wa amani kitu ambacho ndicho kitovu na ubishani mkubwa wa tukio hili.” Shahidi huyo ndiye aliyeandika maelezo ya ungamo ya mshtakiwa Chacha, akidaiwa kueleza hatua kwa hatua namna alivyomua mwanafunzi huyo na baadaye kuwashirikisha Nabiswa na Shayo.

Jaji Matogolo alisema katika mashauri ya mauaji mshtakiwa anaweza kuwa na utetezi na unaweza kuegemea katika ulevi, ukichaa au bahati mbaya na sababu nyingine.

“Lakini Utetezi huo haumuondolei kabisa mshtakiwa kosa la mauaji ya kukusudia, bali linampunguzia tu kutoka kuwa kosa la mauaji ya kukusudia na kuwa kosa la kuua bila kukusudia,”alifafanua jaji huyo.

“Vilevile mliweza kuwapima washtakiwa nani anasema ukweli na nani hasemi ukweli. Katika kesi hii imeegemea ushahidi wa mazingira kwa vile hakuna shahidi aliyeshuhudia mauaji hayo.”

Hata hivyo, Jaji Matogolo alisema ushahidi wa mazingira unakubalika pia kutokana na muunganiko wa ushahidi, hivyo ni wajibu wa wazee hao kupima mambo hayo wakati wanatoa maoni yao.

Baada ya maelezo hayo, mzee wa kwanza, Focus Mrema alisema amesikiliza kesi hiyo na mashahidi kwa umakini mkubwa, na kwamba hakuna ubishi kuwa kifo cha mwanafuzni huyo kilitokana na kuuawa.

Mzee huyo alieleza kwa maoni yake, upande wa Jamhuri umeweza kuthibitisha shtaka dhidi ya washtakiwa wote na akaiomba mahakama iwatie hatiani na iwape adhabu kwa mujibu wa sheria.

Kwa upande wake, mzee wa pili, Fatuma Ndutu, alisema baada ya kusikiliza ushahidi uliotolewa ana maoni kuwa mshtakiwa namba moja (Chacha) ana hatia kwa sababu alikiri kwenye ungamo lake.

Hata hivyo, alisema ana maoni kuwa ushiriki wa mshtakiwa namba mbili (Shayo) na namba tatu (Nabiswa) ni kwa kupitia mshtakiwa wa kwanza, hivyo wao wanaweza kupunguziwa adhabu.

“Jamhuri wamethibitisha shtaka kwa mshtakiwa wa kwanza bila kuacha mashaka, hivyo ana hatia kutokana na kukiri kwake. Mahakama itoe adhabu kwa mujibu wa sheria kwa kila mshtakiwa,” alisema.

Naye Khalfan Abrahaman alisema anaona kuwa upande wa mashtaka umeweza kuthibitisha shtaka la mauaji ya kukusudia dhidi ya mshtakiwa Chacha na Nabiswa.

“Kwa kitendo walichokifanya washtakiwa cha kushiriki kutupa mwili wa mtoto Mto Ghona ni kitendo cha kinyama na huwezi kutupa au kuhamisha mtu aliyekufa bila kuhusika na kifo chake,” alisema.

“Hivyo naiomba mahakama iwaone mshtakiwa wa kwanza na wa tatu wana hatia ya mauaji ya kukusudia. Hao wawili ni wahusika wakuu waliosababisha kifo cha mwanafunzi.”

Alisema, “vilevile pamoja na mshtakiwa wa pili (Shayo) yeye apewe adhabu kutokana na kuzembea ku-report (kutoa taarifa ya mauaji) aliyoipata kutoka kwa mshtakiwa wa kwanza.

Baada ya kumaliza kutoa maoni yao, Jaji Matogolo aliwaeleza wazee hao kuwa kwa kawaida hafungwi na maoni yao, bali anaweza kuyatumia au asiyatumie wakati anafanya uamuzi wa kesi hiyo.

“Kama nilivyosema nyinyi ni waamuzi wa ushahidi na mimi sasa nakwenda mbele zaidi kuangalia sheria inasemaje. Tarehe ya hukumu mtajulishwa na msajili. Hukumu haitachukua muda,” alisema.

Mwanafunzi huyo anadaiwa kuuawa Novemba 6, 2017 na mwili wake kutupwa Mto Ghona uliopo mita 300 kutoka ilipo shule ilipo na baadaye ukazikwa na Manispaa ya Moshi kwa kuwa haukutambuliwa.

Baadaye polisi kupitia Divisheni ya Mashtaka ya Taifa (NPS) waliomba kibali cha kufukuliwa kwa mwili huo na baba mzazi, Jackson Makundi aliutambia na baadaye kuthibitishwa na vinasada (DNA).

Katika kesi hiyo, upande wa mashtaka uliwajumuisha mawakili wanne huku washtakiwa wakitetewa na jopo la idadi kama hiyo ya mawakili.

Credit: Mwananchi

Dalili za Mimba Kuharibika

$
0
0
Kuna sababu nyingi zinazoweza kusababisha mama mjamzito mimba yake kuharibika. Sababu kuu huwa ni magonjwa kama vile ugonjwa hatari wa malaria, ugonjwa unaotokana na zinaa kama vile kaswende na kisonono na U.T.I, dawa fulani fulani mfano Albendazole, Misoprostol, Metronidazole na kadhalika.

Lakini pia mjamzito akifanya kazi za kutumia nguvu nyingi anaweza kusababisha mimba yake kuharibika. Lakini kuna sababu nyingi ambazo zinasababisha mimba kutoka huweza kuzuilika kwa kwenda kliniki mapema yaani pale tu unapohisi una mimba hata kama ni wiki mbili na kufuata ushauri wa wataalamu.

Ukweli ni kwamba kuna wanawake wengi mimba zao huharibika na wao hushindwa kugundua mapema na matokeo yake anakaa na mtoto mfu hata miezi kadhaa bila kujua.

DALILI ZA MIMBA KUHARIBIKA
Zipo dalili ambazo husababisha mimba kuharibika kama tutakavyoona leo hapa. Dalili hizo ni hizi zifuatazo:

KUTOKA DAMU NYINGI SEHEMU ZA SIRI
Mjamzito akitokwa na damu nyingi sehemu za siri ni dalili kwamba mimba imeanza kuachia na mlango wa uzazi umeanza kufunguka, na hiyo inaashiria kwamba kuna mambo mawili yameshatokea kwanza inawezekana mtoto ameshafia tumboni au bado hajafa, lakini kama damu imetoka kwa wingi inaashiria kuwa mtoto huyo aliye tumboni atakufa tu.

MTOTO KUACHA KUCHEZA TUMBONI
Ikiwa mtoto ataacha kucheza tumboni ni tatizo kubwa kwani kwa kawaida mtoto huanza kucheza akiwa na wiki ya 18 mpaka 20 kwa wanawake ambao hawajawahi kubeba mimba na wiki ya 16 mpaka 20 kwa wanawake ambao wameshawahi kuzaa. Ikitokea mtoto aliye tumboni ameshawahi kucheza lakini ghafla akawa hachezi au muda huo umepitiliza na bado kimya kuna uwezekano mkubwa ikawa mtoto huyo amefia tumboni, hivyo haraka sana wahi hospitali kumuona daktari.

KUPOTEA KWA DALILI ZA UJAUZITO
Kupotea kwa dalili za ujauzito ni tatizo lingine baya kwa mama mjamzito. Mara kwa mara mwanamke akiwa na ujauzito anakuwa na dalili nyingi kama vile kuwa na kichefuchefu, kukosa hamu ya kula baadhi ya vyakula, kutapika, kulamba vitu vichachu kama vile limao, ndimu, wengine hula udogo na wengi hubadilika sana tabia, hivyo basi dalili zote hizo za mimba zikisimama ghafla basi ujue mimba imeharibika. 

MIMBA KUTOKUA 
Ikiwa mimba itaacha kuongezeka au kukua ni dalili nyingine ya mimba kuharibika. Kila mtu aliye mjamzito anategemea mimba iwe inakua kila siku  na iwe kubwa kulingana na umri unavyozidi kwenda mbele, ikiwa mimba iko vilevile kwa miezi kadhaa, yaani haikui au ukubwa wa tumbo haubadiliki ujue kwamba mimba hiyo imeharibika, ili kupata uhakika wahi hospitali kupimwa.

TUMBO KUWA NA MAUMIVU MAKALI
Ikiwa mjamzito atakuwa ana maumivu makali ya tumbo wakati ni mjamzito hiyo pia ni dalili mbaya. Kwa kawaida maumivu makali ya tumbo hasa kwa mimba kubwa ya miezi zaidi ya mitano au mimba ndogo kama mwezi mmoja, basi kuna uwezekano mkubwa kondo imeanza kujiondoa kwenye kizazi kwa mimba kubwa au mimba ndogo imeshindwa kuendelea kukua na moja kwa moja hiyo inaweza kuwa dalili ya kuwa mimba imeharibika.

KUTOKA VIPANDE VYA NYAMA SEHEMU ZA SIRI
Ikiwa mama mjamzito atakuwa akitokwa na vipande vya nyama sehemu za siri ni dalili mbaya sana. Kutokwa na vipande vya nyama sirini ni kuashiria kwamba kuna mtoto ameharibika tumboni. Hali hiyo ya hatari ikitokea mjamzito anatakiwa asafishwe kuondoa masalio yaliyobaki.

Maambukizi ya Fangasi katika Sehemu za Siri

$
0
0
Kati ya maambukizi yanayowasumbua wanawake wengi duniani ni maambukizi ya fangasi. Inakisiwa asilimia 75 ya wanawake wote duniani hupata maambukizi haya katika kipindi cha uhai wao.

Maambukizi ya fangasi katika sehemu za siri za mwanamke husababishwa na uwepo wa fangasi wanaojulikana kitaalamu kama Candida albicans. 

Maambukizi haya pia hujulikana kama yeast infection au thrush. Fangasi hupatikana kama vimelea vya kawaida katika mdomo, mpira wa kupitisha chakula sehemu inayojulikana kama pharynx, katika kibofu cha mkojo, uume na hata kwenye uke.

Mfumo mzuri wa kinga wa mwili pamoja aina fulani za bakteria wanaoishi pamoja na fangasi hawa husaidia sana katika kuthibiti maambukizi yanayoyosababishwa na aina hi ya fangasi. 
 
Nini hutokea?
Kwa kawaida, Candida albicans huishi kwenye uke na sehemu nyingine (kama zilivyoelezewa hapo juu) bila kusababisha madhara yoyote yale isipokuwa pale mazingira ya eneo husika yanapobadilika kama vile mabadiliko katika hali ya pH ya  eneo husika (ifahamike ya kwamba pH ya kawaida ndani ya  uke ni 4.0 - 4.5) au uwiano wake na vimelea  (microorganisms) wengine unapoharibiwa kutokana na sababu mbalimbali kama vile matumizi ya madawa aina ya antibiotics, kupungua kwa kinga mwilini kutokana na magonjwa mbalimbali n.k.

Maambukizi haya ya fangasi yanaweza kugawanywa katika sehemu kuu mbili
  1. Maambukizi yasiyo makali yaani uncomplicated thrush: Katika kundi hili, mgonjwa hupatwa na maambukizi  mara moja hadi nne kwa mwaka na dalili zake huwa si mbaya sana na maambukizi haya husababishwa na fangasi wa jamii hii ya Candida albicans.
  2. Maambukizi makali yaani complicated thrush: Katika kundi hili, mgonjwa hupatwa na maambukizi zaidi ya mara nne kwa mwaka, dalili zake kuwa mbaya zaidi au kama maambukizi  yatakuwa yametokea kipindi cha ujauzito, ugonjwa wa kisukari, upungufu wa kinga mwilini. Aina hii kusababishwa na vimelea vya aina nyingine tofauti na Candida albicans.
Vihatarishi
Watu walio katika hatari ya kupata maambukizi ya fangasi hawa ni  wale wenye

• Kutumia sana dawa aina ya detergents kwenye sehemu za siri au douches (vifaa vinavyotumiwa kusafishia uke kwa kutumia maji yaliyochanganywa na siki au antiseptic yoyote ile) kwa sababu hali husababisha kuharibika kwa uwiano wa fangasi na aina nyingine ya vinyemelezi kama bakteria aina ya lactobacilli

• Kutumia sana madawa aina ya antibiotics, steroids ambayo yana tabia ya kushusha kinga ya mwili

• Mabadiliko ya mfumo wa homoni mwilini ambayo husababisha mabadiliko katika s ehemu za siri na hivyo kufanya kuwepo kwa ukuaji wa kasi wa fangasi hawa

• Ujauzito (kutokana na kubadilika kwa mfumo wa homoni mwilini na kupungua kwa kinga ya mwili). Hata hivyo ieleweke hapa kuwa si kila mjamzito hupatwa na maambukizi haya.

• Matumizi ya dawa za kupanga uzazi (vidonge vya majira)

• Upungufu wa kinga mwilini kutokana na magonjwa sugu kama kisukari, saratani aina yoyote ile, ugonjwa aina ya mononucleosis na nk.

• Ugonjwa wa ukimwi (HIV/AIDS)

• Matibabu ya homoni (hormonal replacement therapy) kutokana na sababu mbalimbali

• Matibabu ya kusaidia kushika mimba kwa wale wenye matatizo ya uzazi (infertility treatment)

• Msongo wa mawazo (stress)

• Utapia mlo (malnutrition)

• Kuvaa nguo au mavazi yanayoleta joto sana sehemu za siri kwa muda mrefu kama nguo za kuogelea (swimwear), nguo za ndani (chupi)  zilizotengenezwa kwa kitambaa aina ya nylon, nguo za ndani zinazobana sana nk.

• Kujamiana kwa njia ya kawaida mara tu baada ya kujamiana  kupitia njia ya haja kubwa (anal sex) au matumizi ya vilainishi venye glycerin wakati wa kujamiana pia yamehusishwa na maambukizi haya.

• Kuvimba kwa tezi la koo (goiter)

• Saratani ya tezi la koo (thyroid cancer)

• Wanawake wenye umri wa miaka kati ya ishirini na thelathini wapo kwenye hatari kubwa ya kupata maambukizi haya wakati wale ambao wameshaacha kupata hedhi au wale ambao hawajaanza kupata hedhi kabisa hawako kwenye hatari kubwa.

Kwa wanaume vihatarishi  vya maambukizi haya ni

• Kujamiana na mwanamke mwenye tatizo hili au maambukizi haya

• Upungufu wa kinga mwilini

• Matumizi ya madawa aina ya antibiotics kwa muda mrefu bila ushauri wa daktari

• Magonjwa sugu kama kisukari, saratani ya aina yoyote ile na nk.

Dalili na viashiria kwa wanawake
• Kuwashwa  sehemu za siri  (kwenye tupu ya mwanamke)

• Kuhisi kuwaka moto sehemu za siri (burning sensation)

• Kufanya kama vidonda katika sehemu za siri (soreness)

• Maumivu wakati wa kujamiana (superficial dyspareunia)

• Maumivu  au usumbufu wakati wa kujisaidia haja ndogo (wakati mtu anakojoa)

• Kuvimba na kuwa rangi nyekundu kwa  mdomo wa nje wa tupu ya mwanamke (labia minora)

• Kutokwa na uchafu wa rangi nyeupe au nyeupe kijivu, unaoweza kuwa mwepesi, majimaji au mzito na ambao umefanana na jibini (cottage cheese like discharge) wenye muonekano unaojulikana pia kama curd-like appearance. Kwa kawaida, uchafu huu haumbatani na harufu yoyote isipokuwa panapokuwa na tatizo la ziada kama ugonjwa wa zinaa aina ya Bacteria vaginosis. Uchafu huu unaotoka hapa unaweza kuenea kwenye maeneo mengine yaliyokaribu na tupu ya mwanamke kama kwenye mitoki (groin area) au perineum na kusababisha kuharibika kwa ngozi katika sehemu hizo.

Dalili na viashiria hivi huwa mbaya zaidi wakati  mwanamke anapokaribia  kupata hedhi.

Dalili na viashiria kwa wanaume ni
• Kuwashwa sehemu za siri 
• Kuvimba na kuwa rangi nyekundu kwenye ncha ya uume
• Kuwepo kwa uchafu wa rangi nyeupe (kama nilivyoeleza hapo juu) kwenye sehemu ya juu ya uume.
• Kuwa na vidonda vidogo kwenye uume (sore on the glans)

Hata hivyo, mara nyingi wanaume hawaoneshi dalili zozote zile, ni vizuri kwa mwanamke kumueleza mwenza wake pale anapopata maambukizi haya ili naye pia apate kutibiwa. 
 

Matibabu
Matibabu ya fangasi huusisha dawa za kutibu fangasi (antifungal drugs) kama vile dawa za kupaka za topical Clotrimazole, topical Nystatin, Fluconazole au topical Ketoconazole. 

Wagonjwa wenye maambukizi yasiyo makali yaani uncomplicated vaginal candidiasis wanaweza kutumia dawa za kupaka (cream) kutoka dawa za fangasi za jamii ya -azole kama vile Butoconozale, Miconazole, Clotricomazole nk. 

Dawa hizi hutumika kwa muda wa siku 3-7 kulingana na aina ya dawa. Mgonjwa anashauriwa kupaka dawa ndani ya uke pamoja na maeneo yote yanayozunguka sehemu hiyo. Jinsi ya kupaka dawa hizi ni kuanzia mbele kuelekea nyuma.

Aidha mgonjwa anaweza kupewa dawa za kutumbukiza ukeni ambayo atatumia kwa muda wa siku 3-14 kulingana na aina ya dawa. Dawa hizo ni pamoja na Miconazole, Tiaconazole, Terconazole, Nystatin nk.

Kidonge cha kumeza aina ya fluconzole pia huweza kutolewa. Dawa hizi nilizotaja hapa juu zina kawaida ya kuharibu ubora wa mipira ya kondomu zilizotengenezwa na mpira aina ya latex (latex condoms) pamoja na vifaa vya upangaji uzazi aina ya diaphragms.

Ni vizuri kwa daktari kabla ya kumpa mgonjwa dawa hizi kumfahamisha kwa ufasaha jinsi ya kuzitumia na tahadhari anayotakiwa mgonjwa kuchukua. Inashauriwa kama baada ya matumizi haya bado mgonjwa ana dalili za maambukizi au mgonjwa akapata tena maambukizi haya ndani ya miezi miwili baada ya matibabu ya awali, basi anashauriwa kwenda kumuona daktari ili apate matibabu zaidi.
 
Kinga ya maambukizi ya fangasi
• Kuosha sehemu ya siri kwa kutumia kitambaa kisafi kila siku na kuosha kuanzia mbele kuelekea nyuma, epuka kurudia ukishafika nyuma.

• Epuka matumizi ya sabuni zenye manukato, bubble baths, vaginal deodorant products, feminine hygiene, na bath powder.

• Vaa chupi ambazo hazibani sana na zilizotengenezwa kwa kutumia pamba au hariri (silk), epuka synthetic underwear.

• Epuka mavazi yoyote ya kubana kama jeans za kubana nk.

• Badilisha nguo za ndani (chupi) kila zinapopata unyevunyevu.

• Fua chupi zako kwa maji yenye nyuzi joto 90 na kuendelea.

• Tumia pad wakati tu unapozihitaji (kama umeingia kwenye mzunguko wako wa hedhi)

• Kula mlo wenye virutubisho vyote kamili (balanced diet)

• Epuka kufanya mapenzi  na mpenzi wako ambaye amepata maambukizi ya fangasi.

• Epuka kuoga  maji moto sana (hot baths) tumia maji ya uvuguvugu, hii kwa wale ambao wanaishi kwenye ukanda wa joto (tropical climate).

• Matumizi ya vifaa vya ngono (sex toys), vifaa vya upangaji uzazi (diaphragms, cervical caps) yanaweza kuleta kujirudia kwa maambukizi ya fangasi kama havitaoshwa  na kukaushwa vizuri baada ya kutumiwa.

• Baadhi ya tafiti zilizofanyika, zimethibitisha ya kwamba unywaji wa maziwa ya mtindi yenye live culture, husaidia kupunguza maambukizi ya fangasi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images