Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi April 27


Halmashauri Zakusanya Bil 449 Mapato Ya Ndani

$
0
0
Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI
IKIWA imepita robo tatu ya mwaka wa fedha 2018/2019, halmashauri zote zimekusanya Sh bilioni 449.8 ambayo ni asilimia 61 kati ya Sh bilioni 735.6 kutoka kwenye vyanzo vya ndani huku Halmashauri ya Jiji la Dodoma na Mkoa wa Dar es Salaam zikiongoza kwa mapato ghafi.

Hayo yabamebainishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa alipokuwa akitoa taarifa za makusanya kwa halmashauri kuanzia Juni mwaka jana hadi Machi mwaka huu na kusisitiza kuwa vyanzo vya mapato vinavyokuswanywa na serikali kuu havijumuishi katika makusanyo hayo.

Akifafanua zaidi Jafo alisema halmashauri tano zilizoongoza kwa kigezo cha asilimia ya mapato ya ndani kuwa ni Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi(asilimia 113), Geita (asilimia 109), Wanging’ombe(asilimia 105), Kilolo (asilimia 103) na Sumbawanga (asilimia 92) huku zile zilizofanya vibaya kuwa ni Newala na Tandahimba (asilimia 15), Momba na Masasi (asilimia 13) na Nanyamba (asilimia 12)

Kwa kigezo cha pato ghafi, Jafo alisema halmashauri zinazongoza kwa wingi wa mapato kuwa ni Halmashauri ya Jiji la Dodoma 9 (Sh bilioni 49.9), Ilala (Sh bilioni 44.8), Kinondoni(Sh bilioni 23.5) Temeke Sh bilioni 20.6) na Jiji la Arusha (Sh bilioni 12.5) wakati halmashauri tano zilizofanya vibaya katika kundi hili ni Madaba(Sh milioni 293.7), Newala (Sh milioni 268.3) Kakonko (Sh milioni 238.6) Buhigwe (Sh milioni 177.3) na Momba(Sh milioni 170.4).

Aidha, katika kundi la mikoa kwa kigezo cha asilimia, Jafo alisema mikoa inayoongoza kwa kigezo cha asilimia ya mapato ya ndani ni Mkoa wa Iringa (asilimia 77), Geita (asilimia 73), Dar es salaam (asilimia 72), Dodoma na Songwe (asilimia 68) wakati mikoa iliyofanya vibaya katika kundi hili ni Shinyanga (asilimia 46), Katavi (asilimia 43), Kigoma na Lindi (asilimia 42) na Mtwara (asilimia 26).

Kwa upande wa mikoa kwa kigezo cha pato ghafi, Jafo alitaja mikoa inayoongoza kuwa ni Dar es Salaam (Sh bilioni118.4) Dodoma (Sh bilioni 57.30), Mwanza (Sh bilioni 22.9) Arusha (Sh bilioni 22.8) na Mbeya (Sh bilioni 19.8) wakati mikoa iliyofanya vibaya katika kundi hili ni Manyara (Sh bilioni 6.5) Lindi (Sh bilioni 6.1), Rukwa (Sh bilioni 5.8) Kigoma (Sh bilioni 4.5) na Katavi Sh bilioni 3.8).

Aidha, Jafo alisema Jiji la Dar es Salaam linaongoza katika kundi la halmashauri za majiji kwa asilimia kwa kukusanya asilimia 87 ya makisio huku jiji la Tanga likiwa la mwisho katikakundi hilo baada ya kukusanya asilimia 57 ya makisio.

Alisema Halmashauri ya Dodoma inaongeza kwa kigezo cha patoghafi ambapo imekusanya Sh bilioni 50 na halmashauri ya jiji la Tanga imekuwa ya mwisho baada ya kukusanya Sh bilioni 8.7.

Aidha, Jafo alisema halmashauri ya manispaa ya Sumbawanga imeongoza kundi la halmashauri za Manispaa kwa kukusanya asilimia 92 ya makisio huku Lindi ikishika nafasi ya mwisho kwa kukusanya asilimi 23 ya makisio.

Jafo alisema kwa upande wa halmashauri ya Manispaa ya Ilala imeoongoza katika kundi la halmashauri za Manispaa kwa kigezo cha mapato ghafi baada ya kukusanyw Sh bilioni 50 huku Tanga ikiwa ya mwisho kwa kukusanya Sh bilioni 8.7.

Aidha, JAfo alisema halmashauri ya Mji wa Kondoa imeongoeza kundi la halmashauri za miji kwa kigezo cha asilimia ambapo wamekusanya kwa asilimia 92 ya makisio huku halmashauri ya Mji wa Nanyamba imekuwa ya mwisho baada ya kukusanya asilimi 12 ya makisio.

“ Katika kigezo ya pato ghafi kwa halmashauri za mji, Geita inaongeza baada ya kukusanya Sh bilioni 5.9 na halmashauri ya mji wa Nanyamba imekuwa ya mwisho ikiwa imekusanya Shilingi milioni 293.9.

Kwa upande wa halmashauri za wilaya, Jafo alisema Mbozi inaongoza kwa kukusanya kwa asilimia 113 ya kamkisio nay a mwisho ni Masasi iliyokusanya asilimia 13 ya makisio wakati kwa upadne wa pato ghafi, Chalinze inaoongoza kwa kukusanya Sh bilioni 4.6 na ya mwisho katika kundi hili ni Momba iliyokusanya Sh milioni 170.4.

Aidha, Jafo aliwataka wakurugenzi ambao makusanyao yao hayajafika asilimia 50 kuaza kujitathimini huku asikisisitiza kuwapo taarifa za baadhi ya watumishi kuhujumu ukusanyaji wa mapato.

“ Mkurugenzi usikubali kurudishwa nyuma na watendaji wasio waamini, maana kuna baadhi ya maeneo watu wamekuwa wahatumii mifumo ukusanyaji wa mapato kwa njia ya kieletroniki na wengine hawatumii kabisa,”

Aidha, Jafo ameendelea kusisitiza wakurugenzi kuhakikisha fedha za mapato ya ndani asilimia 40 au 60 kuelekezwe kwenye miradi ya maendeleo eneo husika sambamba na utoaji wa asilimia 10 za fedha za ndani kwa walemavu, vijana na wanawake na kusisitiza kuwa mwisho wa mwaka mambo hayao yatakuwa ni tathimini ya utendaji wa wakurugenzi hao.

Rais Magufuli Abadili matumizi ya eneo la uwanja wa ndege wa zamani wa Mbeya na kulifanya kuwa la wamachinga

$
0
0
 Rais John Magufuli amebadili matumizi ya eneo la uwanja wa ndege wa zamani wa Mbeya na kulifanya kuwa la wamachinga kufanyia shughuli zao.

Amesema amechukua uamuzi huo ili kuwawezesha wafanyabiashara hao ndogo kufanya biashara zao katikati ya mji, huku akiagiza mikoa yote kutenga maeneo kwa ajili yao.

Rais Magufuli alitoa agizo hilo jana mjini Mbeya wakati akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Ruanda Nzovwe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku tano inayoendelea mkoani humo.

Alisema kuanzia sasa eneo hilo litengenezewe miundombinu ya kuwawezesha wafanyabiashara hao kuendesha shughuli zao katika mazingira mazuri ikiwemo vyoo, kituo cha mabasi na litakalobaki lijengwe kituo cha uuzaji madini.

Rais alitoa agizo hilo baada ya kupokea maombi ya viongozi wa mkoa huo wakitaka kutengwa eneo maalumu kwa wamachinga ambao wanafikia 350,000 ili wafanye biashara zao kwa utaratibu mzuri tofauti na sasa wanavyojipanga kila mahali.

“Hili eneo nimelitoa bure, nendeni mkafanye biashara, lakini haina maana yale maeneo mengine mliyokuwa mnakaa msiende, endeleeni na shughuli zenu kote, wamachinga ndio walionipa kura na niliahidi kuwatetea, nitawatetea wafanye biashara zao,” alisema.

Waziri Mhagama Awapa Hamasa Tucta Kuanzisha Viwanda

$
0
0
Na. MWANDISHI WETU
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amewataka viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi kuanzisha viwanda ili kuinua uchumi na kuchangia adhma ya Serikali ya kuwa na uchumi wa viwanda.

Ametoa kauli hiyo jana Aprili 26, 2019 Jijini Dodoma wakati wa mkutano wake na viongozi hao uliohudhuriwa na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo pamoja na Naibu Waziri anayeshughulikia Kazi, Ajira na Vijana Mhe. Anthony Mavunde ili kujadili masuala yanayohusu wafanyakazi nchini.

Waziri mhagama aliwataka viongozi hao kuwa wabunifu kwa kuanziasha viwanda vitakavyowezesha kujikwamua kiuchumi pamoja na kuwajengea uwezo wa kujitegemea na kukuza mapato ya vyama vyao.

“Niwaombe sana muwe na mitazamo chanya katika kuchangia adhma ya Serikali kuwa na uchumi wa viwanda kwa kuanzisha viwanda vitakavyowawezesha kukuza uchumi mfano viwanda vya chaki, mbao na vingine vingi”, alieleza waziri Mhagama

Aidha aliwaeleza umuhimu wa kuanzisha viwanda hivyo ikiwa ni pamoja na kuchangia ukuaji wa uchumi nchini, kusaidia kuboresha maslahi ya wafanyakazi na kuongeza motisha na kutoa fursa za ajira kwa wananchi kwa ujumla.

“Hii leo nimeona niwape changamoto ya kuona umuhimu wa kuwa na viwanda vyenu kwa kuangalia mchango wenu katika jamii na kuendelea kuwa na tija kwa kuzingatia umuhimu wa kuwa na viwanda nchini,” alisisitiza Mhagama

Kwa upande wake rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini Bw. Tumaini Nyamhokya alishukuru mchango wa serikali na maoni yao kwa kuwapa chachu ya kuona umuhimu wa kuwa na viwanda na kuahidi kulifanyika kazi suala hilo.

“Kipekee nimefurahishwa na maoni na mawazo ya serikali hivyo hatuna budi kuanza kulifanyia kazi suala hilo ili kuendelea kuwa na mchango katika ukuaji wa uchumi wa nchi yetu”, alisema Nyamhokya

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Wanawake Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bi. Rehema Ludanga alieleza alivyopokea ushauri huo wa serikali na kuona ni namna bora ya kujishirikihsha katika uchumi wa viwanda na kuonesha utayari wa kufanyia kazi suala hilo.

“Binafsi nikiwa kama mwenyekiti Kamati ya Wanawake nimelichukua kwa dhati kabisa na nitajitahidi kulifanyia kazi mapema iwezekanavyo ili wanawake nao waweze kunufaika na fursa hii hasa upande wa sekta ya kilimo,” alieleza Bi. Rehema.

MWISHO

Kimbunga Kenneth Chabadili Uelekeo

$
0
0
Mamlaka  ya Hali ya Hewa (TMA), imewataka wananchi wa mikoa ya Mtwara na Lindi kuendelea na shughuli zao kama kawaida kwa sababu kimbunga ambacho kilitarajiwa kusababisha athari kwenye ukanda huo kimebadili mwelekeo.

Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk. Agnes Kijazi, alitoa kauli hiyo jana na kueleza kuwa kimbunga hicho kimekwenda kusini zaidi mwa Pwani ya Msumbiji, lakini akatahadharisha kuwa bado kipo kwa kuwa kitarudi tena baharini.

"Kwa sasa, kimbunga bado kipo ardhi ya Msumbiji na mwishoni mwa wiki kinatarajia kurudi baharini kama tulivyoeleza awali kwa kitaalamu, tunaomba wananchi kwa sasa waendelee na shughuli zao huku wakiendelea kufuatilia utabiri wa TMA,” alisema.

Dk. Kijazi alisema kimbunga hicho kitakaporejea baharini kama walivyoeleza awali, kitaleta athari ukanda huo wa kusini lakini wananchi wataarifiwa ili wachukue tahadhari.

Alisema kwa wakati huo aliokuwa anazungumza, hali ya hewa ya mikoa ya Lindi na Mtwara ilikuwa ya mawingu ambayo hayakuwa na athari.

“Maeneo ya Magharibi mwa Ziwa Viktoria kuna wingu zito limetanda. Tunawapongeza sana wananchi kwa kusali na kutii kwa kwenda maeneo maalum yaliyotengwa huku wasipate athari. Tunazishukuru mamlaka mbalimbali, zimeonyesha ushirikiano mkubwa kwenye suala hili," alisema.

Wimbo Mpya wa Alikiba - Mbio

$
0
0
Msanii wa muziki kutoka Bongo, Alikiba anakuletea video ya wimbo wake mpya unakwenda kwa jina la Mbio. Itazame hapa.

Video Mpya ya Rose Muhando Ft. Stephen Kasolo – MsinifateFate

$
0
0
Video Mpya ya  Rose Muhando Ft. Stephen Kasolo – MsinifateFate

LIVE: Ziara Ya Rais Magufuli, Chunya – Mbeya

$
0
0
LIVE: Ziara Ya Rais Magufuli, Chunya – Mbeya

Waziri Mkuu kufungua maonyesho ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote Nchini (UCSFA)

$
0
0
Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote Nchini (UCSFA) yanayotarajiwa kufanyika leo hadi Aprili 30, mwaka huu.

Akizungumza jijini hapa jana, Mtendaji Mkuu wa UCSFA, Peter Ulanga, alisema Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo yatakayokwenda sambamba na shughuli mbalimbali.

Alisema maadhimisho hayo yatakuwa pamoja na maonesho ya watoa huduma mbalimbali za mawasiliano nchini.

Ulanga alisema wamekusudia kutekeleza mradi wake wa kuunganisha shule na  mtandao wa intaneti na kutoa vifaa vya tehama zikiwamo kompyuta, printa pamoja na projekta za kufundishia.

“Mradi huu utaenda sambamba na kutoa elimu ya mafunzo ya Tehama kwa walimu ili waweze kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wakati wa utumiaji wa vifaa mbalimbali vya Tehama ili vifaa husika viweze kuleta tija katika shule husika,” alisema.

Pia alisema watatoa ruzuku ya ujenzi katika maeneo mbalimbali ya nchi hususan makao makuu ya wilaya ili kufikisha matangazo ya kidijitali ya runinga.

“Mfuko unachukua fursa hii kuualika umma wa wananchi wa Jiji la Dodoma kuhudhuria maonesho hayo. Sambamba na maonesho hayo mfuko utazindua Klabu za Tehama katika shule za sekondari Dodoma na Msalato,” alisema Ulanga.

Katika hatua nyingine, alisema tangu kuanzishwa kwake umetumia zaidi ya Sh bilioni 118 katika miradi mbalimbali katika kata 703 zenye vijiji 2,500 vyenye wananchi zaidi ya milioni tano.

“Tangu kuanzishwa kwa mfuko mwaka 2009 hadi sasa hivi 2019 umetumia shilingi bilioni 118 kufikisha mawasiliano katika kata 703 katika vijiji 2,500 vyenye watu zaidi ya milioni tano,” alisema.

Trump kuiondoa Marekani katika Mkataba wa Silaha wa UN

$
0
0
Katika mwendelezo wa sera zake kuu za kujitoa kwenye mikataba na makubaliano ya kimataifa, Rais Donald Trump wa Marekani ametangaza azma ya kuiondoa nchi hiyo katika Mkataba wa Uuzaji Silaha wa Umoja wa Mataifa (ATT).

Trump alitoa tangazo hilo jana Ijumaa, wakati akiwahutuhubiwa wanachama wa Chama wa Wamiliki wa Bunduki nchini humo NRA, ambacho kilifadhili asilimia kubwa ya kampeni zake katika uchaguzi wa mwaka 2016.

Trump amesema, "Tutachukua sahihi yetu. Hatuwezi kusalimisha uhuru wa kujitawala Marekani kwa mtu yeyote."

Mkataba huo wa ATT wa kudhibiti biashara ya silaha duniani ulisainiwa na mtangulizi wa Trump, Barack Obama mwaka 2013, lakini ukapingwa vikali na Chama wa Wamiliki wa Silaha NRA na makundi mengine ya kihafidhina nchini humo.

Tarehe 20 Oktoba 2018, Rais Donald Trump wa Marekani alitangaza kuwa nchi yake itajiondoa pia kwenye mkataba wa silaha za nyuklia za masafa ya kati (INF).
 
Chunguzi za kila mwaka za  taasisi ya Stockholm International Peace Research Institute (SIPRI) zimekuwa zikibaini kuwa, Marekani ndiye muuzaji mkubwa zaidi wa silaha duniani, huku Saudi Arabia ikishika nafasi ya kwanza kwa kununua silaha katika eneo la Mashariki ya Kati.

Trump ameiondoa Marekani kwenye mikataba mingi ya kimataifa tangu ashike hatamu za uongozi, kama vile makubaliano ya nyuklia ya Iran (JCPOA), Makubaliano ya Tabianchi ya Paris, pamoja na mikataba mingine mingi.

Katibu Mkuu wa CCM: Nape, Bashe walipita UVCCM wakati mfumo wa kuandaa viongozi umekufa

$
0
0
Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally amesema Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye anahitaji kupikwa, kusikilizwa, kuaminiwa na kusimamiwa.

Dk Bashiri pia amemtaja Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe akisema ni miongoni mwa vijana waliopitia katika Umoja wa Vijana wa CCM wakati mfumo wa kuandaa viongozi ukiwa umekufa.

Dk Bashiru alikuwa akizungumza katika mahojiano kupitia kituo cha televisheni cha ZBC2 kuhusu Muungano uliotimiza miaka 55.

Mhadhiri huyo wa zamani wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) alizungumzia pia umuhimu wa vijana kuandaliwa kupitia mifumo ya chama.

Julai 28, 2018, akizungumza na wanachama wa CCM mjini Nzega, Dk Bashiru alisema kuwa Nape na Bashe ni watukutu wanampa wakati mgumu kutokana na udadisi wao wa mambo mbalimbali wawapo bungeni, jambo linalowafanya Mawaziri wafikiri kwa kina kabla ya kutoa majibu na maamuzi.

“Nawafahamu wabunge hawa kuwa ni watukutu kwelikweli, wadadisi kwelikweli, lakini wanapishana, kwa kuwa Nape ni mdadisi na mtukutu ambaye joto lake ni kali, hivyo kazi yake ni kupoza,” alisema.

Serikali Yaajiri Walimu Wapya 4,549

$
0
0
Serikali kupitia Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OR-TAMISEMI) imepata kibali Cha kuajiri jumla ya walimu 4549 Kati ya 91108 walio tuma maombi yao.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo 27 Mei 2019 Magogoni, Dar es Salaam, Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI, Seleman Jafo amesema kuwa Rais Dk.John Pombe Magufuli katika kuhakikisha Serikali inawahudumia vizuri wananchi ameamua kufungua dirisha la ajira kwa walimu.

Jafo alisema jumla ya waombaji 91108 waliojitokeza na kutuma maombi yao katika nafasi mbalimbali na kati ya hayo 43770 sawa na asilimia 48.04 yalikuwa na viambatanisho vyote vilivyohitajika.

Hata hivyo alieleza kuwa maombi 47338 sawa na asilimia 51.96 hayakuwa na vigezo ikiwa ni pamoja na kukosa viambatanisho muhimu vilivyohitajika.

" Kutokana na mahitaji makubwa kwa walimu katika shule za msingi na sekondari kwa masomo ya sayansi, Tamisemi imefanya uchambuzi na kutoa vipaumbele katika ajira za walimu daraja la tatu (A) cheti kwa ajili ya kufundisha shule za msingi.

"Walimu daraja tatu (B) stashahada wa masomo ya sayansi kwa ajili ya kufundisha shule za sekondari( kidato cha kwanza hadi nne); na walimu daraja la tatu (C)shahada, wa masomo ya sayansi kwa ajili ya kufundisha kwa kidato cha tano na sita," alisema Jafo.

Pia walimu daraja la tatu (C) shahada, wa masomo ya elimu maalum , biashara, uchumi, kilimo na maarifa ya nyumbani kwa ajili ya kufundisha shule ya sekondari.

" Mchakato wa kupitia maombi ulijumuisha uhakiki wa uhalali wa vyeti vya elimu ya taaluma vya waombaji na ukamilishaji wa nyaraka zilizohitajika," alisema Jafo.

Aidha Jafo alieleza kuwa waombaji wa masomo ya sayansi na sanaa waliotimiza vigezo na hawakufanikiwa kupata nafasi kwa kipindi hiki, maombi yao yamechambuliwa na yamehifadhiwa kwenye kanzidata ya Tamisemi.

Alisema kwa walimu hao pindi fursa za ajira zitakapojitokeza utaratibu wa ajira utatolewa dhidi yao.

"Jumla ya walimu 4549 wamepangiwa moja kwa moja kufundisha shule zilizo na uhitaji wa walimu ambapo 3059 shule ya msingi na 1490 kwa sekondari," alisema.

Jafo alisema kuwa walimu wote waliopata ajira wanatakiwa kuripoti kwa wakurugenzi wa Halmashauri zenye shule walizopangiwa kwa ajili ya kuhakikisha vyeti vyao na kujaza mikataba ya ajira Kisha kuripoti kwenye vituo vyao kuanzia Mei 7, mwaka huu.

Jafo alisema walimu wapya ambao hawataripoti katika vituo vyao ifikapo Mei 21, 2019 nafasi zao zitajazwa moja kwa moja na walimu walio na sifa ambao hawakupangiwa bila kuwataarifu.

" Wakurigenzi wa Halmashauri wasikubali kubadilisha vituo vya kazi vya walimu bila kibali Cha katibu mkuu wa OR-TAMISEMI. Walimu Hawa tumewapangia kulingana na mahitaji ya sehemu husika.

Hata hivyo alisema kwa mwajiriwa atakayeripoti nakuchukua posho ya kujikimu Kisha akaondoka katika kituo chake cha kazi alichopangiwa atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521

Rais Magufuli Akemea Vitendo Vya Ubakaji na Ulawiti Jijini Mbeya

$
0
0
Rais Dk John Magufuli amekemea vikali vitendo vya ubakaji vinavyoendelea jijini Mbeya, amewataka viongozi na wananchi kushirikiana kwa pamoja kutokomeza tatizo hilo kwa kuwachukulia hatua wanaohusika na vitendo hivyo.

Ametoa kauli hiyo Jumamosi Aprili 27, wakati akizungumza na Wananchi wa wilaya ya Chunya mkoani humo katika ziara yake ya kikazi ya siku nane ambapo ameshazindua barabara ya Mbeya – Chunya yenye urefu wa kilomita 72 na kuweka Jiwe la msingi la ujenzi wa Barabara ya Chunya – Makongorosi.

Dk Magufuli amewataka viongozi hao kuiga mfano wa marehemu Abbas Kandoro kwa namna alivyosaidia kwenye hukumu ya mwanaume aliyehukumiwa kifungo cha maisha kutokana na kupatikana na  hatia ya kulawiti mtoto ambaye hadi sasa yupo katika hali mbaya.

“Tatizo la ubakaji linaonekana linataka kuwa ugonjwa katika maeneo haya, jana kuna mama alijitokeza katika mkutano wetu akaeleza shida yake kwamba ana mtoto wake ambaye alilawitiwa akiwa na miaka sita kukawa na ujanja ujanja na baadaye alienda kumuona aliyekuwa Mkuu wa Mkoa, Abbas Kandoro akaishughulikia kesi hiyo vizuri na hakimu akatumia sheria zote na mtuhumiwa akahukumiwa kifungo cha maisha.

“Nitoe wito kwa viongozi kuiga mfano wa Mzee kandoro maana alisimamia haki popote palipokuwa hakuna haki, hivyo yeyote atakayefanya vitendo vya ajabu apelekwe kwenye vyombo vya dola na nina imani tukilisimamia hili kwa pamoja tutazaa matunda mazuri,” amesema.

Aidha ametoa agizo kwa viongozi mkoani huo kuhakikisha wanafungua soko la madini katika Wilaya ya Chunya ndani ya siku saba na kwamba hilo ndilo litakuwa jaribio lao kubwa licha ya kuwa na utendaji mzuri mkoani humo.

Waziri Mkuu Awaaga Watalii 1,000 Kutoka Israel

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watalii kutoka Israel wakawe mabalozi wazuri wa kuitangaza Tanzania pindi wakirudi  huko kwao.

Ametoa wito huo leo mchana (Jumamosi, Aprili 27, 2019) kwenye uwanja wa ndege wa Kilimanjaro (KIA) wakati akiwaaga watalii 274 walioondoka nchini leo mchana kurejea kwao.

Watalii hao ni miongoni mwa watalii 1,000 waliowasili nchini tangu Aprili 20, mwaka huu na kutembelea maeneo kadhaa ya vivutio kwenye ukanda wa Kaskazini.

Kundi la kwanza liliondoka jana usiku, la pili leo mchana, la tatu litaondoka leo saa 10 jioni na la mwisho litaondoka leo saa 2 usiku.

Waziri Mkuu amewaomba watalii hao wapange muda wao na watafute fursa nyingine ya kuja Tanzania kutembelea mbuga nyingine za ukanda wa Kusini pamoja fukwe nzuri za Zanzibar.

"Tumefarijika sana na ujio wenu na tunaamini mtaenda kutangaza mazuri mliyoyaona kwa wengine. Tunazo mbuga nyingine za Rubondo, Katavi, Ngorongoro, Ruaha, Selous, fukwe nzuri za Zanzibar na mlima Kilimanjaro," amesema.

Pia amewashukuru mawakala wa utalii nchini pamoja na Mkurugenzi wa kampuni wakala wa utalii ya Another World kutoka Israel Bw. Carmel Shlomo kwa kuamua kuitangaza Tanzania kama kivutio namba moja cha utalii barani Afrika.

Kwa upande wake, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla aliwashukuru watalii hao kwa kuamua kuitembelea Tanzania licha ya kuwa wangeweza kwenda maeneo mengine yaliyo jirani na Israel.

"Natambua uchovu mlionao sababu ya urefu wa safari kutoka Israel hadi hapa, lakini nawashukuru kwa uamuzi wenu wa kuja Tanzania katika kipindi hiki ambacho tunafanya maboresho kwenye sekta ya utalii ili tuweze kutoa huduma bora zaidi," alisema.

Alisema Tanzania ina vivutio vingi vya utalii na hii inawezekana kwa sababu iliamua kutenga zaidi ya robo ya ardhi yake kwa ajili ya mbuga na hifadhi za taifa za wanyama.

Pia alizishukuru kampuni za utalii za Tanzania na Israeli kwa kushirikiana kuleta watalii wengi kiasi hicho. Alizitaja kampuni hizo kuwa ni Excellent Guides, Mauly Tours and Safaris, Matembezi, Leopard Tours and Safaris, African Queen Adventures na TAWISA zote za kutoka Tanzania. Kamuni za kutoka Israeli ni Another World, My Trip, Camel na Safari Company.

Kwa upande wao, baadhi ya watalii kutoka Israel wamesema wamevutiwa na waliyaona hapa nchini na wameahidi kurudi tena ili watembelee vivutio vingine zaidi.

Bibi Naomi Peer Moscovich na mabinti zake Dana na Lihi wamesema wamevutiwa na wingi wa wanyama waliowaona lakini pia wameguswa na ukarimu wa watu waliokutana nao.

"Tunaondoka na neno moja kubwa nalo ni kwamba hatutaisahau Tanzania (we say Unforgettable Tanzania) na tutarudi tena hivi karibuni," alisema Dana Peer Moscovich ambaye ni dada yake Lihi.

Hafla ya kuwaaga watalii hao ilihudhuriwa pia na Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii nchini, Jaji Thomas Mihayo, Katibu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Adolf Mkenda na Wakuu wa Mikoa ya Kilimanjaro na Arusha. Mama Anna Mghwira na Bw. Mrisho Gambo.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Pigo kwa Kenya baada ya China ‘kukataa’ kuipa mkopo wa kujenga reli (SGR)

$
0
0
China imekataa kwa mara ya pili kutoa mkopo kwa ajili ya kufadhili awamu ya tatu ya ujenzi wa reli ya kisasa nchini Kenya (SGR) kutoka Naivasha hadi Malaba.

Uamuzi huo wa China wa kukataa kuipa Kenya mkopo huo ambao imekuwa ikiomba kwa muda sasa, unaziweka katika sintofahamu awamu mbili za ujenzi wa reli hiyo (Mombasa hadi Nairobi, na Nairobi hadi Naivasha).

Badala ya kupata mkopo wa kujenga SGR, Kenya imeweza kupata mkopo wa TZS bilioni 906.8 kwa ajili ya kukarabati reli ya zamani (meter gauge) ambayo sasa italazimika kuunganishwa na SGR ili kuwezesha usafirishaji wa mizigo kutoka Mombasa kwenda Uganda.

Kenya ilikuwa inahitaji mkopo wa TZS trilioni 8 kwa ajili ya kukamilisha awamu hiyo ya mwisho ya ujenzi wa reli hiyo, na kuiunganisha na Uganda.

Kufuatia uamuzi wa China, baadhi ya wataalamu wa uchumi wamesema kuwa sasa Kenya imebakiwa na reli ambayo haiendi popote (a railway to nowhere), huku mkopo uliotumika kutengeneza awamu mbili za kwanza ukitakwa kuanza kurejeshwa.

Waziri wa Usafiri wa Kenya, James Macharia  alisema kuwa wameafikiana na China waikarabati kwanza reli ya zamani, ili SGR kutoka Nairobi hadi Naivasha itakapokamilika mwezi wa 8, mizigo inayotoka Mombasa iweze kufika Malaba kwa wakati.

Hata hivyo imeelezwa kuwa masharti magumu ndiyo yaliyosababisha Kenya kushindwa kupata mkopo huo, ambapo China ilikata kutoa sehemu za fedha hizo kama ruzuku, lakini pia iimetaka kuwepo na maelezo ya namna reli hiyo itakavyozalisha faida kabla ya kufadhi ujenzi huo wa Naivasha.

Reli hiyo ya Kenya tayari imekamilika katika sehemu ya Mombasa hadi Nairobi huku kipande cha Nairobi hadi Naivasha kikitarajiwa kukamilika Agosti mwaka huu.

Tangu kuzinduliwa kwa reli ya Mombasa hadi Nairobi Juni 2017, tayari abiria milioni 2.6 wameshatumia usafiri huo huku mizigo yenye tani 3.6 ikiwa imesafirishwa.

Katika mwaka wake wa kwanza wa kutoa huduma, reli hiyo ilipata hasara ya TZS bilioni 227, ambapo waziri mwenye dhamana alisema hasara hiyo ilitarajiwa kutokana na uelewa mdogo wa wananchi kuhusu usafiri huo.

Katibu Mkuu Mambo Ya Ndani Aitaka Suma Jkt Kumkabidhi Jengo Jipya La Uhamiaji Jijini Dodoma Baada Ya Miezi 18,

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, MOHA
KATIBU Mkuu wa Wizara Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu amelitaka Shirika la Uzalishaji Mali Jeshi la Kujenga Taifa (Suma JKT), kujenga jengo la Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji kwa ufanisi mkubwa na akabidhiwe jengo hilo baada ya miezi 18.

Akizungumza kabla ya kusaini mkataba wa makubaliano wa ujenzi wa jengo hilo, kati ya Wizara yake na Suma JKT ambayo iliongozwa katika kikao hicho na Mkuu wa JKT, Meja Jenerali Martin Busungu, katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, iliyopo Mji wa Serikali, Kata ya Mtumba, jijini Dodoma, leo, alisema hana shaka na uwezo wa Mkandarasi huyo, ila anaamini ujenzi huo utakua bora na utakamilika kwa wakati.

“Baada ya maandalizi ya ujenzi huu kuchukua muda mrefu lakini hatimaye tumekamilisha, hivyo nawaomba ndugu zangu tufanye kazi vizuri kabisa, na leo ndio siku ya kusaini mkataba kwa ajili ya ujenzi huu,” alisema Meja Jenerali KIngu.

Meja Jenerali Kingu alisema Wizara yake itafuatilia kwa karibu ujenzi huo, ambapo Mkandarasi ni Suma JKT na Mshauri Elekezi ni Chuo Kikuu cha Ardhi, hivyo jengo hilo anatarajia kuwa bora zaidi kutokana na uwepo wa wadau hao.

Kwa upande wake, Mkuu wa JKT, Meja Jenerali Busungu, alisema aliishukuru Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa kuwa na imani na Suma JKT na kuipa kazi ya ujenzi wa jengo la makao makuu ya uhamiaji jijini Dodoma.

“Tunaishukuru Wizara yako kwa kutupa kazi hii ya ujenzi wa jengo hili ambalo ni la ghorofa nane, tunaahidi kulikamilisha baada ya miezi 18, na tutapiga kadiri inawezekana, tupo tayari kwa kazi yenye uweledi wa kuzingatia muda na ubora ambao utawauza zaidi Suma JKT,” alisema Meja Jenerali Busungu. 

Mkataba huo ulisainiwa na viongozi hao huku ukishuhudiwa na wanasheria wa taasisi hizo ambao ni Mkurugenzi wa Sheria, Marlin Komba wa Wizara hiyo na Kapteni Joyce Mwaikofu kutoka JKT.

Rais Magufuli Atoa Siku 7 Kwa Wakuu Wa Mikoa Inayozalisha Dhahabu Kufungua Masoko Ya Madini

$
0
0
Na Mwandishi Wetu,MAELEZO
RAIS Dkt. John Pombe Magufuli ametoa siku saba kwa Wakuu wa Mikoa inayozalisha dhahabu nchini kushirikiana na Wizara ya Madini katika kufungua masoko ya madini ikiwemo dhahabu ili kuifanya sekta ya madini kuweza kuleta tija ya kiuchumi kwa Watanzania wote hususani wachimbaji wadogo.

Akizungumza Mkoani Mbeya leo Jumamosi (April 27, 2019) wakati wa katika hafla ya uzinduzi na uwekaji wa jiwe la msingi la barabara ya Mbeya-Lwanjilo-Chunya-Makongosi yenye urefu wa Kilometa 111, Rais Magufuli alisema Serikali anayoiongoza kamwe haitokubali kuona wachimbaji wadogo wakiendelea kuteseka nchini.

Aliongeza kuwa tangu mwaka 2017, Serikali imepitisha Sheria Bungeni inayotoa maelekezo kuhusu usimamizi wa sekta ya madini nchini na hivyo anashangwa na baadhi ya Viongozi wake hususani Wakuu wa Mikoa inazozalisha dhahabu kusuasua katika kusimamia maelekezo ya maelekezo yake aliyoyatoa katika siku za nyuma.

Alisema kuwa Serikali pia imefuta kodi mbalimbali za madini na kuendelea kuwahamasisha wachimbaji wadogo kupeleka dhahabu zao katika masoko hayo, lakini hadi sasa baadhi ya Wakuu wa Mikoa wameshindwa kujenga masoko hayo, pamoja na faida mbalimbali zinazopatikana katika masoko hayo ikiwemo kuepusha dhuluma kwa wachimbaji, kupata dhahabu yenye ushindani pamoja na kuzuia upotevu wa kodi ya Serikali.

Aliongeza kuwa katika mkutano wake alioufanya hivi karibuni na Viongozi wa Wizara ya Madini na Wakuu wa Mikoa ya Tanzania Bara inayozalisha Dhababu, alitoa maelekezo ya kufungua masoko ya madini katika maeneo yao, ingawa ni Mkoa wa Geita pekee uliyotekeleza maelekezo hayo wakati ujenzi huo hauhitaji nyumba au eneo kubwa.

“Kama Mkoa wa Geita, umeweza kuwa na Kituo cha soko la kuuzia madini, nashangazwa kwanini Wakuu wengine wa Mikoa wanashindwa kutekeleza maelekezo hayo, hivyo hili ni agizo kwa Wakuu wa Mikoa ya Katavi, Singida na Arusha kuhakikisha kuwa watatekeleza maagizo haya” alisema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli alisema Serikali anayoiongoza haiwezi kuwa na Viongozi na Watendaji wasiotaka kutekeleza maagizo, hivyo ametoa kipindi cha muda huo kuhakikisha kuwa vituo hivyo vinafunguliwa na hivyo kuwahakikishia masoko ya uhakika wachimbaji wadogo ambao wamekuwa wakidhulumiwa dhahabu zao na baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu.

Aidha Rais Magufuli aliutaka Uongozi wa Mkoa wa Mbeya hususani Wilaya ya Chunya kuhakikisha kuwa soko hilo la dhahabu linafunguliwa haraka iwezekanavyo kwa kuzingatia kuwa rasilimali zote muhimu za kufanikisha  maagizo hayo zipo ikiwemo vyombo vya ulinzi na usalama ambavyo vitatumika kwa ajili ya ulinzi wa madini ya dhahabu wakati wa mauzo hayo yakifanyika.

Kwa mujibu wa Rais Magufuli, alisema kuwa suala la kujiletea maendeleo kwa Watanzania linacheleweshwa na baadhi ya Viongozi Watendaji Serikali kwani wananchi hususani wachimbaji wadogo wa madini wamekuwa na juhudi kubwa za kujiletea maendeleo yao lakini wamekuwa wakikatishwa tamaa pamoja na juhudi kubwa wanazozionyesha katika kuchimba dhahabu.

Kwa upande wake, Waziri wa Madini, Dotto Biteko alisema tangu kutungwa kwa Sheria ya Madini mwaka 2017, Serikali imeweza kuokoa kiasi kikubwa cha madini kutoroshwa nje ya nchi, ambapo katika Wilaya ya Chunya ambayo ni Wilaya ya pili kwa uzalishaji wa dhahabu Serikali imeweza kutoa jumla ya kilo 30 zilizokuwa zikitoroshwa nje ya nchi kutokana na kukosekana kwa mtambo wa kuchenjulia madini.

Mara baada ya kujiridhisha na taratibu zote za kisheria, tumeweza kufungua mitambo 38 ya kuchenjulia dhahabu hapa Chunya, ambayo tulisimamisha shughuli hizi huko nyuma kutokana na utoroshaji mkubwa uliokuwa ukifanyika” alisema Biteko.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya April 28

Waziri Mkuu Aagiza Mabango Ya Utalii Yawekwe Uwanja Wa Ndege Wa KIA

$
0
0
*Ni yenye kuonyesha wanyama, milima, fukwe, mambo ya utamaduni

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameuagiza uongozi wa bodi ya KADCO uhakikishe unaweka mabango ya kielektroniki yenye kuonesha vivutio vya utalii kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

“KADCO na Wizara ya Maliasili na Utalii, shirikianeni kuweka utaratibu wa kutangaza vivutio vyetu vya utalii hasa wanyama kwenye viwanja vyote vya ndege. Tunazo mbuga, milima, fukwe za bahari na ngoma za makabila mbalimbali, wekeni mabango yanayobadilisha picha.”

“Screens zenye wanyama wanaobadilikabadilika zinaleta mvuto lakini pia ni fursa ya kutangaza vivutio vyetu. Nimezunguka humu ndani, kuta zote ni nyeupe tu, tumieni fursa hiyo kutangaza tamaduni zetu na vivutio tulivyonavyo," Waziri Mkuu alimweleza Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kilimanjaro Airports Development Company (KADCO), Mhandisi Christopher Mukoma.

Alitoa agizo hilo jana mchana (Jumamosi, Aprili 27, 2019) wakati akikagua miundombinu ya uwanja wa ndege wa Kilimanjaro (KIA) mara baada ya kuwaaga watalii 274 kutoka Israeli wanaowawakilisha wenzao 1,000 walioondoka nchini jana kurejea kwao.

Akiwa uwanjani hapo, Waziri Mkuu alikagua eneo la mapokezi, sehemu ya abiria wanaoondoka na wanaowasili, sehemu ya uhamiaji, mashine za kukagua mizigo ya wanaoondoka na wanaowasili, sehemu za kutolea huduma na maduka.

Pia alimwagiza Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji kwenye kiwanja hicho cha ndege, Bw. Filbert Ndege awasiliane na makao makuu yake ili waangalie uwezekano wa kuongeza madirisha ya kutolea huduma za uhamiaji (counters) ili huduma hiyo itolewe kwa kasi zaidi.

“Angalieni cha kufanya, ikibidi eneo hili lipanuliwe na counters nyingine ziongezwe ili kufast-track utoaji wa huduma hasa msimu ambao watalii wengi huingia nchini.”

Pia aliwataka KADCO waboreshe eneo la maegesho ya magari kwa kufanya upanuzi na kujenga maturubai ya vivuli (shades) ili kuyakinga na jua kali magari ya wateja.

(mwisho).

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAPILI, APRILI 28, 2019.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images