Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Orodha Ya Majina Ya Walimu Walioajiriwa Shule Za Msingi Na Sekondari April, 2019

$
0
0
Serikali kupitia Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OR-TAMISEMI) imepata kibali Cha kuajiri jumla ya walimu 4549 Kati ya 91108 walio tuma maombi yao.

 Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI, Seleman Jafo amesema kuwa Rais Dk.John Pombe Magufuli katika kuhakikisha Serikali inawahudumia vizuri wananchi ameamua kufungua dirisha la ajira kwa walimu.

Jafo alisema jumla ya waombaji 91108 waliojitokeza na kutuma maombi yao katika nafasi mbalimbali na kati ya hayo 43770 sawa na asilimia 48.04 yalikuwa na viambatanisho vyote vilivyohitajika.

Hata hivyo alieleza kuwa maombi 47338 sawa na asilimia 51.96 hayakuwa na vigezo ikiwa ni pamoja na kukosa viambatanisho muhimu vilivyohitajika.

==>>Tazama Hapo chini



Naibu Waziri Ikupa Alipongeza Shirika La Compassion International Kwa Kusaidia Watoto Na Vijana Nchini

$
0
0
Na. Mwandishi Wetu
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Watu wenye Ulemavu Mhe. Stella Ikupa amelipongeza Shirika lisilo la kiserikali la Compassion International Tanzania (CIT) kwa kuwahudumia na kuwapatia watoto na vijana stadi za maisha zinazowawezesha kujitegemea.

Naibu Waziri Ikupa ametoa pongezi hizo wakati wa Maadhimisho ya Miaka 20 ya Shirika hilo yaliyofanyika  jana  Aprili 27, 2019 katika ukumbi wa Kanisa la TAG lililopo Mipango, Jijini Dodoma. Maadhimisho hayo yalikuwa na Kauli Mbiu isemayo; “Wekeza kwa Watoto na Vijana kwa Uchumi Endelevu.”

Alieleza kuwa Shirika la Compassion International Tanzania limekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha watoto na vijana nchini wanahudumiwa na kuondokana na hali ya umasikini kwa kuwa chachu ya maendeleo kwa jamii na Taifa.

“Shirika hili ni la mfano na limeendelea kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuwalinda watoto na kuwapa fursa ya kufikia ndoto zao na kuwapatia vijana ujuzi wa stadi za maisha zinazoleta mabadiliko chanya kwao na kuwaletea maendeleo yao binafsi na Taifa kwa ujumla,” alisema Ikupa

Aliongeza kuwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amekuwa akionesha watanzania namna gani nchi yetu imeweza kujitegemea katika kutekeleza shughuli mbalimbali, hivyo Mhe. Rais ni mfano tosha wa kuigwa na vijana nchini kwa kuona wanauwezo wa kujitegemea.

Aidha, Naibu Waziri Ikupa alitoa rai kwa vijana kuacha kukaa kwenye vijiwe bila sababu za msingi na kubadili mitazamo, bali watumie muda wao kutafakari shughuli za kufanya kwa bidii ambazo zitawaletea maendeleo na kuwawezesha kujikwamua kiuchumi.

“Serikali imekuwa ikitoa mikopo kwa vijana ili waweze kuanzisha shughuli mbalimbali zitakazo wawezesha kukua kiuchumi, tumieni fursa ya ujuzi mliopata kupitia shirika hili na ubunifu mlionao kuchangamkia fursa hiyo muhimu itakayowawezesha kuanzisha miradi mbalimbali ikiwemo viwanda,” alisema Ikupa

Pia alitoa wito kwa jamii kuripoti haraka vitendo vya unyanyasaji wa watoto katika madawati ya jinsia na watoto yaliyopo kwenye vituo vya polisi nchini na kwa maafisa ustawi wa jamii ili kutokomeza vitendo hivyo kwa kumjengea mazingira salama motto na kumuonesha jamii yake imejaa upendo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taifa wa Shirika la Compassion International Tanzania, Bi. Agness Stanley Hotay alisema kuwa wataendelea kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha wanawatetea na kuwasimamia watoto na kuwapatia nafasi vijana ya kujitambua kwa kuchangamkia fursa ambazo zipo katika jamii na kuleta ufumbuzi wa kimaendeleo.  

“Maono ya shirika ni kuona wanufaika wanatoka katika uhitaji na kujijengea dhana ya kujitegemea, vilevile kuwa wahisani wa watu wengine,” alisema Hotay

Shirika la Compassion International Tanzania (CIT) ni sehemu ya Compassion International ambalo ni shirika la kimataifa la Kikristo linalojihusisha kuhudumia watoto na vijana wanaotoka katika kaya maskini kwa njia ya ufadhili. Shirika hili limekuwa likifanya huduma hii hapa nchini toka mwaka 1999.

Kwa sasa Shirika hilo lipo katika Mikoa 19 ya Tanzania Bara ambayo ni Arusha, Dar es Salaam, Kigoma, Manyara, Pwani, Morogoro, Iringa, Dodoma, Kilimanjaro, Singida, Shinyanga, Mwanza, Mara, Tabora, Lindi, Geita, Mtwara, Simiyu na Kagera.

Wanajeshi na wapinzani wa Sudan wafikia makubaliano ya kubuni Baraza la Pamoja

$
0
0
Wanajeshi wanaotawala kwa sasa Sudan na makundi ya upinzani ya nchi hiyo wamefikia makubaliano ya kubuni Baraza la Pamoja kwa ajili ya kuendesha masuala ya nchi hiyo.

Akitangaza habari hiyo, Ahmad ar-Rabii' mmoja wa wakilishi wa makundi ya upinzani amesema kwamba katika kikao chao kilichofayika jana Jumamosi mjini Khartoum, wapinzani na Baraza la Kijeshi wamekubaliani umuhimu wa kubuniwa Baraza la Pamoja la wanajeshi na wapinzani kwa ajili ya kuendesha kwa muda masuala ya Sudan. 

Ar-Rabii' ambaye alihudhuria kikao hicho amesema kwamba mazungumzo yangali yanaendelea kuhusu kuainishwa kwa idadi ya wanajeshi na wapinzani watakaojumuishwa katika baraza hilo la pamoja.

Kikao hicho cha pamoja kati ya wanajeshi na wapinzani kimefanyika siku moja baada ya muungano wa upinzani kwa jina la 'Makundi Yanayopigania Uhuru na Mabadiliko' kutangaza habari ya kubuniwa ujumbe wa wapinzani kwa ajili ya kufanya mazungumzo na wanajeshi. 

Baraza la Kijeshi la Sudan lilibuniwa baada ya Rais Omar al-Bashir wa nchi hiyo kung'olewa madarakani na wanajeshi tarehe 11 Aprili. 

Baraza hilo lilikuwa limetangaza awali kwamba lingetawala kwa muda wa miaka miwili kabla ya kukabidhi madaraka kwa raia. 

Wananchi na makundi ya upinzani wamekuwa wakifanya maandamano na mgomo mbele ya makao makuu ya wanajeshi mjini Khartoum kwa ajili ya kushinikiza raia wakabidhiwe madaraka nchini.

Rais Magufuli Ataja Sababu za Kutengua Uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Chunya

$
0
0
Rais John Magufuli amesema alimtoa aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Chunya, Rehema Madusa kwa sababu alikuwa akichoma mazao ya wananchi kwa madai kuwa wamelima ndani ya hifadhi za wanyamapori.

Rais Magufuli ameyasema hayo jana Aprili 27, 2019  katika mkutano wa hadhara katika Viwanja vya Sabasaba wilaya ya Chunya mkoani Mbeya ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake mkoani humo.

Alisema licha ya asilimia 32.5 ya eneo lote la Tanzania kuwa na wanyama lakini baadhi ya maeneo hayo yamechukuliwa na kiasi cha pesa kinachopatikana hakijulikani.

“Sasa kama fedha nyingine hatujui zinakokwenda inakuwaje mtu aliyeamua kulima katika eneo la hifadhi wewe umchomee, nilikuwa nimekaa naangalia katika televisheni mtu na rehema zake unamchomea chakula ili akale wapi,” alihoji Magufuli.

“Ukimchomea mahindi yake kesho tena utampelekea mahindi ya kula, kwa hiyo hata msitafute sababu nyingine ni hiyo,” amesema Magufuli

“Yalikuwa mambo ya ajabu sana, nikamuambia mkuu wa mkoa (aliyekuwa- Amos Makala) lakini nikaona na yeye anafanya mambo kidogo kidogo nikaona ngoja nimtoe Mbeya nimpeleke Katavi kwa uangalizi zaidi,”

“Ndiyo maana tukatengeneza timu ya mawaziri waangalie maeneo ambayo zamani yalikuwa hifadhi za wanyama na hayatumiki tutayakata yatakuwa maeneo ya watu.”

Chama cha wenye ulemavu wa Ngozi Tanzania (TAS) chalaani vitendo vya ufukuaji makaburi.

$
0
0
Chama Cha Watu Wenye Ualbino Tanzania kwa masikitiko kinauarifu umma kuhusu tukio la kaburi la marehemu Aman Anywelwisye Kalyembe mwenye Ualbino, aliyezikwa mwaka 2015 kufukuliwa usiku wa kuamkia tarehe 23/4/2019 katika kijiji cha Ibililo kata ya Nkunga wilayani Rungwe ambapo wahusika waliondoka na masalia ya viungo vya marehemu. 

Tukio hili la tatu kwa mkoa wa Mbeya limeibua simanzi na hofu kwa  Watu Wenye Ualbino na familia zao, kwa uzoefu kuwa linahusishwa na imani za kishirikina hasa kipindi hiki tunapoelekea mwaka wa uchaguzi 2020. Ni ishara wazi ya ukatili kwa Watu Wenye Ualbino si tuu wakiwa hai bali hata wakiwa wafu.

Chama cha watu wenye ualbino Tanzania kinaungana na wadau na wote wenye mapenzi mema kukemea vikali tukio hili ovu. 

Ni tukio ambalo limejitokeza wakati baadhi ya wenzetu wako katika vituo maalum, huku kiu yao na jitihada za serikali na wadau wengine ikiwa ni kuona wanarejea kuishi na familia zao, ndugu zao, marafiki na jamii zao katika maeneo yao. 

Tukio hili  linarejesha hofu kwa Watu Wenye Ualbino na familia zao kwani ni tukio la 23 la vitendo ovu vya ukiukwaji wa heshima ya makaburi ya watu wenye ualbino likihusishwa na imani za kishirikina.

Watu Wenye Ualbino na familia zao watafurahi kuona serikali inachukua hatua stahiki kwa wakati ili matokeo mazuri tuliyokuwa tumeyafikia, yakiwemo: watoto wenye ualbino kuanza kuandikishwa shule za kawaida ndani ya maeneo yao na vituo vingi vikiwepo Buhangija (Shinyanga) na Kabanga (Kigoma) kuanza kupunguza idadi ya watoto na watu wazima wenye ualbino, yawe endelevu.

Tunamwomba Mhe. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuingilia kati suala hili, ikiwa ni kutumia nafasi yake kukemea uovu huu na kuwezesha kifedha mikakati iliyopo na itakayokuwepo yenye nia ya kukomesha uovu huu dhidi ya Watu Wenye Ualbino na zaidi  jamii ipate hamasa na kuziacha fikra potofu na matendo ya kishirikina.

 Miongoni mwa mipango tunayoomba iwezeshwe na serikali ni pamoja na:
1.    Mpango kazi wa kutokomeza mauaji na ukatili wa watu wenye ualbino Tanzania uliondaliwa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kwa kushirikiana na wadau wengine.
2.    ‘Cross-Border Cooperation Plan on Preventing and Combating Trafficking and the Protection of Persons with Albinism in Malawi, Tanzania and Mozambique’ Ulioandaliwa na International Organisation for Migration (IOM), serikali kwa uwakilishi kupitia wizara ya Mambo ya Ndani  na wadau wengine.
3.    ‘Joint Programme for the Protection and Wellbeing of People with Albinism in Tanzania’ Ulioandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa uratibu wa UNESCO kwa ushirikiano na wadau wengine.
4.    ‘ACTION STRATEGY: Minorities and Other Vulnerable Groups’ ulioandaliwa na Tanzania Human Rights Defenders Coalition (THRDC) kwa ushirikiano na wadau wengine.   
5.    ‘Regional Plan of Action on Albinism adopted on May 22, 2017 by the African Commission on Human and Peoples' Rights’ ulioandaliwa na mtaalamu wa kujitegemea wa UN akisimamia haki za watu wenye ualbino.

Tunaitaka serikali katika ngazi zote wakati huu wa kuelekea chaguzi za serikali za vijiji na mitaa na kwenye uchaguzi mkuu mwakani 2020 kuweka ajenda ya hamasa kwa jamii kuhusu ualbino na athari za vitendo vya kishirikina kwenye kampeni zao. 

Jeshi la Polisi limefanya kazi nzuri na ya kupongezwa kwa kipindi cha miaka kadhaa iliyopita. Juhudi zao zimechangia kupungua kwa matukio. Mafanikio haya yamechangiwa pia na jamii kutoa ushirikiano hivyo tunaomba mtu yeyote mwenye taaifa yoyote kuhusiana na matukio haya afikishe jeshi la polisi au awasiliane nasi kwa wakati ili kufanikisha kuwakamata watu hawa waovu. Tunamsihi sana IGP Simon Sirro kuongeza kasi hasa katika upelelezi na kushiriki katika mchakato wa kuelimisha na kuhamasisha jamii kulinda na kuheshimu utu na uhuru wa Watu Wenye Ualbino na familia zao.

Mahakama zina mchango mkubwa kukomesha mauji kupitia adhabu kali ili iwe kama elimu na fundisho kwa jamii. Watu Wenye Ualbino wana imani na Mheshimiwa Jaji Mkuu na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ujumla wakitarajia kwamba kesi zilizochukua muda mrefu zitashughulikiwa ziishe kwa wakati sanjari na adhabu stahiki kutolewa kwa watakaobainika kuwa na hatia.

Kutokana na matukio haya, Watu Wenye Ualbino na familia zao ni vyema kuendelea kuchukua tahadhari stahiki kwa ajili ya ulinzi wao wakati wote. Toa taarifa polisi na au mamlaka za karibu mapema iwezekanavyo uonapo kiashiria chochote cha uhalifu ili jitihada za kuzuia zifanikiwe.

Vyombo vya habari, viongozi wa dini, serikali kupitia viongozi wa kisiasa, Wizara na taaisi nyingine za kiserikali na za kiraia tuongeze juhudi hasa katika elimu kwa jamii kwa njia mbalimbali ambazo ni endelevu, hii itasaidia sana kuibadili jamii kifikra  ili hatimaye utu wa mtu mwenye ualbino uthaminike.

Mungu ibariki Tanzania

Nemes Colman Temba
Mwenyekiti – Taifa
Chama cha watu wenye Ualbino Tanzania
Aprili 27, 2019

Kwa mawasiliano
Simu (ofisi): 022 2110527
Mob. (Mwenyekiti): 0784 874 592
Email:   info@tas.or.tz


Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521

LIVE: Rais Magufuli Akiwa Kwenye Ibada Ya Kusimikwa Askofu Mteule Mbeya

$
0
0
LIVE: Rais Magufuli Akiwa Kwenye Ibada Ya Kusimikwa Askofu Mteule Mbeya

Rais Magufuli: Nilitamani Kuwa Askofu, Sijui Nini Kilitokea

$
0
0
Rais  Magufuli amesema alipokuwa mdogo alitamani kuwa Askofu lakini hajui ni nini kilitokea akashindwa kuingia katika njia hiyo.

Akizungumza katika ibada ya kuzindua Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki Mbeya na kumsimika Askofu Mkuu, Gervas Nyaisonga, Rais Magufuli amesema anashanga hadi sasa pamoja na matamanio yake hayo ameshindwa kuwa hata Katekista au Mwenyekiti wa jumuiya.

“Nilitamani sana kuwa Askofu lakini sijui ni nini kilitokea nikashindwa kuwa hata Katekista lakini au hata mwenyekiti wa Jumuiya.

“Leo nimefurahi na ninawaonea wivu Maaskofu, nilitamani niwe huko lakini niko huku, mlioko huko msitoke ni pazuri, sasa hivi niko huku na bado natamani kuja huko,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli pia aliwakumbusha Maaskofu kuhusu wito wa kazi ya uaskofu kupitia Kitabu cha Biblia cha 1Timotheo 3:1 unaosema “Ni neno la kuaminiwa mtu akitaka kazi ya Askofu atamani kazi njema.”

Kwa upande wake Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Polycarp Kadinali Pengo, amelitaka Kanisa kutimiza wajibu wake wa kuwasimamia waumini kiroho bila kusahau kutoa ushirikiano kwa serikali katika kuweka mazinga mazuri ya kiutawala.

“Tunahitaji uwepo wa roho mtakatifu katika kuboresha mazingira ya waumini ambao wanatambua vyema wajibu wao katika kuwaongoza vyema waumini, serikali ndiyo inayoweza kulifanya hili katika upeo mpana wa kiutawala, ili roho mtakatifu aweze kutenda kazi tunahitaji kuwa na kanisa linaloshirikiana vyema na serikali,” amesema Kadinali Pengo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya April 29

LIVE: Fuatilia kipindi cha maswali na majibu kutoka Bundeni Dodoma

$
0
0
LIVE: Fuatilia kipindi cha maswali na majibu kutoka Bundeni Dodoma

Iran: Marekani lazima iombe idhini kwa jeshi la Iran la SEPAH kuweza kupita Hormuz

$
0
0
Mkuu wa Majeshi ya Iran amesema kuwa meli za Marekani haziwezi kupita katika Lango Bahari la Hormuz bila ya kuomba idhini kwanza kutoka kwa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH.

Meja Jenerali Mohammad Baqeri amewaambia waandishi wa habari kwamba hakuna mabadiliko yoyote yaliyotokea hadi hivi sasa kuhusu meli za kivita, za kibiashara na za mafuta na vyombo vyote vya majini vya Marekani vinavyopita kwenye Lango Bahari la Hormuz. 

Wakati wowote vinapoamua kufanya hivyo lazima viombe idhini kwanza kutoka kwa jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH ndipo vinaweza kupita baada ya kuruhusiwa na jeshi hilo.
 
Amesema Iran inataka lango hilo libakie wazi na salama na kuonya kuwa Tehran haitoruhusu mtu yeyote kuhatarisha usalama wa eneo hilo. 

Itakumbukuwa kuwa karibu thuluthi nzima ya mafuta yanayotumika maeneo mbalimbali duniani yanapitia katika Lango Bahari la Hormuz la nchini Iran. 

Jukumu la kulinda usalama wa eneo hilo muhimu mno kiistratijia ni la Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH ambalo hivi karibuni rais wa Marekani Donald Trump alidai kuwa  jeshi hilo ni taasisi ya kigaidi.

Mkuu huyo wa vikosi vya ulinzi vya Iran ameongeza kuwa, madhali meli za nchi nyingine zinatumia lango hilo kusafirisha mafuta, Iran nayo ni haki yake kabisa kutumia eneo lake hilo kusafirishia mafuta. 

Hata hivyo amesema hii haina maana kwamba Iran inakusudia kulifunga lango hilo. 

Amesema: "Hatuna nia ya kulifunga Lango Bahari la Horumuz isipokuwa kama adui atatulazimisha kufanya hivyo. Na tukiamua kulifunga, basi tunao uwezo wa kufanya hivyo muda wowote ule."

Credit: Parstoday

Profesa Lipumba Afanya Uteuzi wa Viongozi Mbalimbali CUF

$
0
0
Chama Cha Wananchi (CUF) kimewateuwa wanachama 13 kushika nafasi mbalimbali za uongozi ili kusaidia kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba, aliwaeleza waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kuwa, wameteua wanachama ambao miongoni mwao ni wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa na Wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa.

Wanachama walioteuliwa ni pamoja na Mkurugenzi wa Fedha na Uchumi, Zainab Mndolwa na naibu wake, Omar Mohammed Omar, Mkurugenzi wa Mambo ya Nje, Bunge na Sera, Mohammed Habibu Mnyaa na naibu wake, Mohammed Ngulangwa.

Wengine ni Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi, Mneke Jafar na naibu wake, Mohammed Vuai Makame, Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma, Abdul Kambaya na naibu wake, Mbarouk Seif Salim.

Wengine ni Haroub Mohammed Shamis aliyeteuliwa Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Sheria, naibu wake Salvatory Magafu wakati Thinney Juma Mohammed akiteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Mafunzo na Uhamasishaji na naibu wake, Masoud Omary Mhina.
 

Profesa Lipumba alisema Kamati ya Uongozi imemteua Yusuph Mohammed Mbugiro kuwa Ofisa Tawala wa ofisi kuu ya chama hicho, jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti huyo wa CUF pia amefanya uteuzi wa viongozi wa jumuiya za chama huku akisema viongozi hao watakaimu nafasi zao mpaka pale watakapochaguliwa kuongoza kwa kipindi cha miaka mitano kwa mujibu wa katiba ya chama hicho.

Mbunge wa Mchinga, Hamidu Bobali ameteuliwa kuwa kaimu mwenyekiti Jumuiya ya Vijana wa CUF (Juvicuf), makamu wake Faki Suleiman Khatib na kaimu Katibu Mtendaji, Yusuph Kaiza Makame na naibu wake, Mbaraka Chilumba.

Kaimu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake (Jukecuf) ni Dhifaa Mohammed Bakar na makamu wake ni Kiza Mayeye, kaimu Katibu Mtendaji ni Anna Ryoba na naibu wake ni Leila Jabir Haji.

Kwa upande wa Jumuiya ya Wazee wa Cuf (Juzecuf), kaimu mwenyekiti ni Mzee Chunga na makamu wake ni Hamida Abdallah, kaimu katibu mtendaji ni Hamis Makapa na naibu wake ni Said Ali Salim.

Video Mpya ya Masanja Mkandamizaji – NII

$
0
0
Video Mpya ya Masanja Mkandamizaji – NII

Mkuu wa Wilaya Amtia Ndani Mwenyekiti wa Kijiji Kwa Kutafuta Mamilioni ya Mradi wa REA

$
0
0
Na Ahmed Mahmoud,Longido
Mwenyekiti wa Kijiji cha Ewor ndeke katika kata ya Kimokokua wilaya ya Longido, Moses Lesikar Leng’ese  Ole Nasuaku, anashikiliwa na jeshi la Polisi wilayani humo kwa amri ya Mkuu wa wilaya hiyo akituhumiwa kujipatia kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 135 zilizolipwa na wakala wa umeme vijijini Rea kama fidia ya kupisha usambazaji wa umeme.

Akiongea na vyombo vya habari Mkuu wa wilaya hiyo ,Frank Mwaisumbe amesema hatua hiyo imekuja kufuatia malalamiko ya wananchi wa kijiji hicho wakimtuhumu mwenyekiti wao kujipatia mamilioni ya fedha kupitia mradi wa Rea baada ya kudanganya  kuwa maeneo yanayopitiwa na mradi huo ni mali yake wakati si kweli.

Mwaisumbe alifafanua kuwa mwenyekiti huyo alilipwa mara mbili akitumia majina tofauti ,ambapo alilipwa kiasi cha sh,milioni 66 kwa hekari saba na sh,milioni 69 kwa hekari 10 huku akitumia majina ya Lesikar Leng’ese na Moses Leng’ese na kujipatia kiasi hicho cha fedha.

Alisema kuwa kabla ya kutiwa mbaroni kwa mwenyekiti huyo Wanakijiji saba waliohojiwa ,watano walidhibitisha  maeneo hayo ni ya kijiji huku wawili ndio walisema ni Mali ya mwenyekiti huyo anayemiliki tangu mwaka 2013 ,ingawa hatua ya upimaji maeneo ya mradi  ilishapita tangu mwaka ,2008 .

“Ni kweli tumemkamata kwa kosa la kujipatia fedha kinyume cha SHERIA na kosa hilo ninaangukia kwenye uhujumu uchumi ,nimempa siku saba arejeshe fedha hizo na baada ya hapo tutampeleka mahakamani” Alisema Mwaisumbe

Aliwataja wengine waliotumia mpango huo  kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kupitia maeneo hayo ya Kijiji ambao wanatafutwa ni pamoja na Elia Shapashina Kool   na Luka Sambeke Ole Mboloso

Wengine ni mwenyekiti wa kitongoji cha Maatiani aliyetambulika kwa jina moja la Kerimboti ,Sindiyo Leakui na Nengolo Sadaka wote wakazi wa Kijiji cha Ewor ndeke.

Mkuu huyo wa wilaya amesema kuwa fedha hizo zimelipwa wiki tatu zilizopita kama fidia kwa maeneo yaliyopitiwa na mradi huo wa Rea baada ya kupimwa na kuthaminishwa   mwaka 2008 ambapo fedha hizo ziliopaswa kuwekwa kwenye akaunti ya Kijiji lakini mwenyekiti huyo na wenzake walitumia akaunti binafsi kujinufaisha.

Wakati mkuu huyo wa wilaya akichukua hatua hiyo wananchi wa Kijiji hicho wakiwemo wanawake wametishia kufunga ofisi ya kijiji hicho kama njia pekee ya kushinikiza kiongozi huyo kuachia ngazi .

Mmoja ya wananchi wa Kijiji hicho, Mbayo Olotito alisema kuwa mwenyekiti wao amekosa uaminifu  kwa muda mrefu na wanajipanga kupeleka kilio chao kwa mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo ili kushinikiza kuweza kuchukuliwa hatua zaidi kwa mwenyekiti huyo na wenzake walioshiriki kuhujumu maeneo ya Kijiji na kujinufaisha wenyewe.

“Huyu mwenyekiti kwa muda mrefu amekuwa akichochea migogoro ya Ardhi kwa wananchi na kujinufaisha ” Amesema Olo Tito.

Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.


Jinsi ya Kumtambua Mpenzi Tapeli na Muongo

$
0
0
Inawezekana upo katika uhusiano na tapeli wa mapenzi bila kujua, hiyo ni sumu na unachotakiwa kufanya sasa ni kuanza kumchunguza mpenzi wako mapema isije kuwa upo kwenye foleni!

Hakuna kitu kibaya kama kuwa katika foleni ya wapenzi kwa mpenzi mmoja, tena mbaya zaidi awe ni yule ambaye moyo wako umempenda kwa dhati.

Kumbuka, kuwa katika uhusiano na mtu ambaye haeleweki ni sawa na kukaribisha matatizo katika maisha yako, huna sababu ya kuishi kwa wasiwasi ukiwa hujui mpenzi wako anakuchukulia vipi.

Anza kumuwekea mitego mapema. Lakini katika mitego yako achana na simu yake kabisa, huna sababu ya kuchunguza simu yake lakini kama ni msaliti utajua tu, unafikiri atajificha mpaka lini?

Atafanya mambo yake gizani mpaka lini? Kuna siku utagundua na kumuacha aendelee na umalaya wake kama ameona ndiyo maisha. Usikubali kabisa kuwa katika penzi la kitumwa, penzi la kisaliti, kuwa na mtu ambaye anakuchanganya wa kazi gani zaidi ya kukupotezea muda na kukukaribishia machozi?

UTAMJUAJE MPENZI LAGHAI?
Hapa ndipo kwenye kazi, kwa bahati mbaya sana kama ikitokea ukampenda mtu sana hata kama akifanya mabaya kiasi gani unaweza usiyaone, kama wewe ni wa aina hii unapaswa kubadilika kifikra. Mwone wa kawaida, fanya uchunguzi wako polepole na kama ukiona moja kati ya mambo yafuatayo, ujue kuna kitu.

(a) Hataki ujulikane na rafiki zake
Hii ni kati ya alama walizonazo matapeli wa mapenzi, ni mtu wa kufanya mambo kwa upekee sana. Kila dakika hakaukiwi na neno nakupenda sana, lakini moyoni mwake hakuna alama hata moja ya mapenzi kwako.

Ni vigumu kumtambua mtu wa aina hii lakini chunguza kuhusu hili, hapendi kabisa kukukutanisha na rafiki zake na hata mkikutana nao kwa bahati mbaya basi hatakutambulisha na kama akikutambulisha hatakutambulisha kama mpenzi wake rasmi. Ataishia kusema ninyi ni marafiki mlioshibana!

Tangu lini mpenzi akatambulishwa kama rafiki? Mtu anapomtambulisha mpenzi wake humtambulisha kwa kujisikia furaha moyoni kwamba anamtambulisha mpenzi wake lakini inakuwaje kwako akutambulishe kama rafiki?

Baadaye utakapomuuliza hawezi kuwa na jibu la maana, atabaki kukuambia hata kama akikutambulisha kama rafiki jamaa ataelewa kuwa ni mpenzi wake, hii inaingia akilini kweli?

Hakuna ukweli kama huo ndugu zangu! Huo ni ulaghai na anaogopa kukutambulisha kama mpenzi maana tayari ameshaonwa akiwa na wapenzi wengine. Sasa kama ndivyo, atatambulisha wangapi? Aseme wewe ni nani? Amka ndugu yangu!

(b) Msiri kupitiliza
Hii ni alama nyingine waliyonayo wanaume wa aina ninayoielezea katika mada hii. Siku zote mambo yake ni kwa siri kubwa, kama mna ahadi ya kukutana, hataki muongozane, atakuambia mkutane moja kwa moja sehemu husika. Hata muda wa kuondoka atafanya kila njia ili kila mmoja aondoke mwenyewe na kama mkiondoka pamoja basi ujue ni usiku na hakuna atakayewaona.

Ikitokea akakubali kuongozana na wewe, hatapenda muongozane pamoja. Atalazimisha utangulie mbele yeye afuate nyuma, kwa nini? Kwa sababu anaogopa kujulikana kuwa yeye ni mpenzi wako na kama anaogopa anakupenda kweli? Mapenzi gani hayo yanafanywa kwa siri? Anakupotezea muda huyo.

(c) Hapendi ndugu wafahamiane
Mpenzi wa aina hii ni mjanja sana, kwanza kabisa atajifanya mtu mwenye ‘ubize’ sana, yote hii ni kukwepa kuwajua ndugu zako au wewe kuwajua ndugu zake! Wakati mwingine anakuwa hapendi ndugu zako na wake wakutane wakijua wazi kuwa nyie mna uhusiano, hili ni tatizo.

Hakuna uhusiano wenye heri na malengo ya kuishi pamoja siku zijazo ukawa wa kificho cha kiasi hicho. Kama ana nia na wewe basi atahakikisha anawafahamu baadhi ya ndugu zako na wewe unawafahamu baadhi ya ndugu zake, hayo ndiyo mapenzi ya kweli.

Mapenzi hayaishii kwa nyie wawili pekee bali hata kwa ndugu zenu. Mnapojuana inakuwa rahisi kusaidiana hata katika mambo mengine ya kawaida.

MWILI wako  una thamani kubwa sana, usiidharau jinsi yako, usijishushe kiasi hicho, huyo anayekupotezea muda na kukuchezea sasa hivi hana thamani kama huyo aliyeandaliwa kwa ajili yako. 

#Pakua App Yetu tukuhabarishe, Sasa Tumerudi Upya


Serikali Kuendelea Kulinda Uhuru wa Kuabudu

$
0
0
Rais wa Tanzania, John Magufuli amesema Serikali itaendelea kulinda uhuru wa kuabudu kwa mujibu wa Katiba huku akiwapongeza Watanzania namna wanavyotumia uhuru huo bila kuuvunja.

Pia ameahidi kuwa Serikali itandelea kushirikiana na dini pamoja na madhehebu yote kwa sababu ni taasisi nyeti na muhimu katika jamii kwa sababu zinasaidia kuwafanya wananchi kuwa raia wema.

Ameyasema hayo  jana Aprili 28, 2019 katika misa ya kumsimika Askofu Mkuu Gervas Nyaisonga wa kanisa katoliki Jimbo Kuu la Mbeya iliyofanyika katika viwanja vya Sokoine na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali.

Alisema amefurahi kuona katika misa ya kumsimika askofu Nyaisonga kuhudhuriwa na viongozi kutoka madhehebu mbalimbali huku akiamini pia wahudhuriaji ni kutoka sehemu tofauti.

Kujichua Kwa Muda Mrefu Husababisha Maumbile ya Kiume Kusinyaa na Kupungukiwa Nguvu za Kiume

$
0
0
Wanaume  wengi  waliofanya  mchezo wa  kujichua  kwa  muda  mrefu hupatwa  na  madhara  ya kuwa  na  kusinyaa  na  kudumaa  kwa  maumbile  yao  ya  kiume  ambayo  huenda  pamoja  na  tatizo  a  Ukosefu au upungufu wa nguvu za kiume.

Tendo  la  kujichua  kwa  mwanaume  linapofanyika  kwa  kipindi  kirefu huathiri na  kuharibu mishipa  na  misuli  ya uume  na  hivyo  kusababisha  kujengeka  kwa mafuta na tishu zisizo vutika  kwenye  mishipa  ya  ateri.  Jambo  hili  husababisha  makuu mawili; 1. Huzuia  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  kuongezeka jambo  linalotajwa  na  wanasayansi  kama jambo  muhimu  sana  katika  kukua  kwa  uume. 2. Huzuika  kutirika  kwa  damu  kuingia  kwenye  misuli  ya  uume.

Mambo  hayo  mawili  huathiri  sana  ukuaji  wa  maumbile ya kiume  kwa  sababu  yanapo tokea huathiri uzalishaji  wa  homoni  muhimu  zinazo  husika  na  ukuaji  wa  misuli  ya  uume na matokeo  yake husababisha  uume  wa  mhusika  kudumaa, kusinyaa,kunywea  na  kurudi ndani  kiasi  cha  kuufanya  uonekane  kama uume  wa  mtoto.
 
Hii ndio  sababu  kwanini watu  wengi  walio athirika  na  punyeto  hulalamika  kwamba  maumbile  yao  ya  kiume  hayajaongezeka  tangu  walipo anza  kujihusisha  na  punyeto  wakiwa  na  umri mdogo. 

Maumbile  yao  huonekana  kama  ya  watoto  kwa  sababu hayakupata  nafasi  ya  kupokea  vichochea  vya  kuyafanya  yakue  na  kuongezeka  tangu  walipo  anza  kujihusisha  na  punyeto.

Suluhisho  La  Tatizo La Maumbile  Ya  Kiume  Yaliyo  Sinyaa  Kwa  Sababu  Ya  Punyeto.
Kama  bado  unaendelea  kujihusisha  na punyeto  basi  jitahidi  uache  tabia  hiyo  mara  moja  kwani  inakuharibu. Inaweza  isiwe  rahisi  sana  kuacha  mara  moja  lakini  ukiweka  nia  thabiti  basi  unaweza  kuacha  kabisa  kama  walivyofanikiwa  kuacha  wengine  ambao  walikuwa  wametopea  kwenye  tabia  hiyo  lakini  wakajitahidi  kujilazimisha  na  hatimaye  wakafanikiwa  kuachana  kabisa  na  tabia  hiyo.

==>> Acha kuangalia video chafu za ngono.
Video hizi ndio chanzo kikuu cha punyeto kwa watu wengi hua zinajenga picha nyingi kwenye ubongo na kila picha unayoiona utataka ukaipigie  punyeto hivyo kuacha kuziangalia tu ndio nafuu yako.. 


Weka mipango ya kuzuia kupiga punyeto wakati wa kuoga: bafuni ndio sehemu ambayo inatumika sana na watu wengi kupiga punyeto hivyo ni vizuri kua na mikakati ya kujizuia ukiwa huko kwa kuoga haraka na kuondoka, kuoga maji ya baridi ambayo mara nyingi hayatoi muhemko wa kupiga punyeto.

==>>Epuka kukaa nyumbani peke yako;
Mara nyingi kukaa peke yako kunakufanya ushawishike kufanya tendo hilo, hebu ondoka na ujichanganye na watu wengine au tafuta majirani wa kukaa na kuongelea mambo mengine. 


Fikiria kuhusu madhara yake: kila aliyewahi kupiga punyeto kuna madhara mabayo ameshayapata kama vile misuli ya uume kulegea, kushindwa kurudia tendo uwapo na mwenzi wako, kuishiwa nguvu za kiume, maumbile kusinyaa, kurudi ndani na kuwa kama ya mtoto mdogo.

Acha kusema eti hii punyeto ni ya mwisho: siku zote wapiga punyeto wana akili moja ya kufikiria eti sasa leo napiga afu sirudii tena. Hicho kitu hakipo, kwani kesho yake utasema hivyohivo, kama unaacha acha mara moja ili utunze heshima yako mbele ya mwenzi au mke wako.

Kama utaona  kuna  ugumu  wa  kuacha  tabia  hiyo  na tayari ushaapata madhara ya maumbile kusinyaa na kupungiwa nguvu za kiume, basi  wasiliana nasi kwa ushauri zaidi; Simu  0716-263605

Serikali Yazungumzia Dawa za Kuongeza Nguvu za Kiume

$
0
0
Suala la matumizi ya madawa ya kuongeza nguvu za kiume na makalio limeibuka bungeni huku Waziri wa Ulinzi, Dkt.Hussein Mwinyi akiwataka watanzania wanaotaka kutumia huduma hiyo kufuata taarifa rasmi kabla ya matumizi.

Awali swali hilo liliulizwa na Mbunge wa Viti Maalum, Rukia Kassim ambaye alihoji juu ya Serikali kuzifungia saluni ambazo zinatoa huduma ya kutumia dawa na kuongeza makalio na kubandika kucha bandia.

"Wanawake wengi wameathirika sana kwa dawa za kuongeza makalio, kope na kucha bandia, je Serikali iko tayari kuzifunga saluni zinazofanya hivi?", aliuliza  Mbunge huyo.

Akijibu swali hilo kwa niaba ya Wizara ya Afya, Waziri wa Ulinzi Dkt. Hussein Mwinyi amesema, "TFDA haijawahi kupokea taarifa ya madhara kuhusiana na kucha za kubandika, kukosekana kwa takwimu hizo Serikali haina sababu ya kufunga saluni, wala kuwachukulia hatua watoa huduma".

Kwa upande wa Mbunge wa Ulanga Goodluck Mlinga, aliyehoji juu ya kuongezeka kwa matumizi ya dawa za kuongeza nguvu za kiume hususani kwa vijana.

"Tunatambua kuna dawa maalum zilizopitishwa kwa ajili ya kuongeza nguvu za kiume, ushauri wetu ni kwamba  wanaotaka kutumia dawa hizi, wakatumie dawa ambazo zimethibitishwa na wataalam ambazo hazina madhara", amesema Waziri Mwinyi alipokuwa akijibu swali la Mbunge Mlinga.

CCM yavuna wanachama wapya 500 Dar es Salaam

$
0
0
Na MWANDISHI WETU
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Rodrick Mpogolo, amewapokea wanachama wapya wa chama hicho kupitia kampeni ya Dar ya kijani inayoratibiwa na Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Mkoa wa Dar es Salaam.

Kampeni hiyo ya Dar ya Kijani ina lengo la kurudisha mitaa, kata na majimbo yote katika himaya ya chama, inawataka vijana na wanachama wote kuimarisha ushirikiano na kupata ushindi wa pamoja wenye heshima kwa chama hicho tawala.

Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo kwa Wilaya ya Kinondoni, Mpogolo, amewataka vijana kuwa makini na waadilifu kwani wao ndio wataokaojenga hehima ya chama na Taifa kwa ujumla.

“Vijana ndio tunao wategemea katika uchaguzi ujao tunahitaji vijana makini na waadilifu ambao watakitumikia chama chetu cha Mapinduzi na Serikali yetu. jiepushieni mbali na tabia ambazo zitawaondelea maadili yenu. Ili mkawe viongozi makini kwani taifa letu linaitaji viongozi makini na wachapakazi .

Amesema yeye hatoita Dar ya Kijani ila anaitambua Tanzania ya Kijani kutokana na kaz kubwa inayofanywa na serikali ya Chama Cha Mapinduzi ya kuwaletea Watanzania maendeleo ya kweli.

“Mimi sitaita Dar es Salaam ya Kijani bali nitaita Tanzania ya Kijani kwa sababu Rais wetu mpendwa Dk. John Magufuli anafanya kazi kubwa ya kuleta maendeleo nchini, tunaona ujenzi wa barabara za juu pale Ubungo na tunashuhudia maendeleo makubwa yanayofanywa katika sekta ya elimu vituo vya afya, kuwasaidia wamachinga kwa kuwapa vitambulisho vya ujasiriamali, bodaboda.

“Pia ameleta usawa kwa Watanzania wote kuwa sawa. Kwahiyo kwa namna hii lazima chama chetu kiendelee kushika hatamu kwa sababu tunawatumikia wananchi ipasavyo kwa namna hii nina uhakika Tanzania inaenda kuwa ya kijani,” amesema Mpogolo

Kwa upande wake Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, Mussa Kilakala, amesema kuwa lengo la kampeni hiyo ya Dar es Salaam ya Kijani ni kuwaandaa vijana na chaguzi zijazo ikiwamo wa Serikali za Mitaa mwaka huu pamoja na Uchaguzi Mkuu mwaka 2020 ili chama hicho kipate ushindi wa kishindo.

“Lengo la Dar es salaam ya Kijani ni kuwaanda vijana wa Mkoa wa Dar es salaam katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa lakini kuwataka vijana kuhakikisha wanajitokeza katika kugombea nafasi lakini pia kuhakikksha CCM kinapata ushindi wa kishindo kwa mkoa wote,” amesema Kilakala

Amesema tangu kampeni hiyo ilipozinduliwa Machi 17, mwaka huu jijini Dar es Salaam imefanikiwa kuvuna zaidi ya wanachama 500  ambao wamejiunga na chama hicho
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images