Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Upelelezi Kesi ya Wanaodaiwa kughushi saini ya waziri Makamba wakaribia Kukamilika

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imeambiwa kwamba upelelezi wa kesi ya uhujumu uchumi inayowakabili wafanyakazi watano wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) unakaribia kufikia mwisho.

Kesi hiyo ilipangwa jana kwa ajili ya kutajwa mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Janeth Mtega.

Wakili wa Serikali, Jenipher Massue, alidai kuwa kesi hiyo ilipangwa kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi unakaribia kufikia mwisho na maendeleo ya kesi hiyo ni mazuri.

"Mheshimiwa Hakimu kesi hii upelelezi wake unakaribia kufika mwisho na maendeleo ni mazuri. Tunaomba tarehe nyingine ya kutajwa ili kuja kuangalia kama tutakuwa tumekamilisha kipengele kilichobakia," alidai Wakili Massue.

Wakili wa Utetezi, Bernard Mbakileki, aliwaomba mawakili wa serikali siku ya tarehe nyingine ya kesi hiyo waje na taarifa nzuri zaidi ili kila upande ujue hatima yake katika kesi hiyo.

Hakimu Mtega alisema kesi hiyo itatajwa Machi 27, mwaka huu, na washtakiwa wataendelea kukaa mahabusu.

Wafanyakazi hao wanakabiliwa na mashtaka sita ya uhujumu uchumi likiwamo la kughushi saini ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba, katika vyeti vya tathmini ya uharibifu wa mazingira na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu, hivyo na kusababisha hasara ya Sh. milioni 160.

Washtakiwa hao ni Ofisa wa Mazingira NEMC, Deusdedit Katwale (38) na Mtaalamu wa IT, Luciana Lawi (33) wote wakazi wa Ubungo Msewe, Katibu Muhtasi wa NEMC, Edna Lutanjuka (51) Mkazi wa Mbezi Beach St Gasper, Msaidizi wa Ofisi Mwaruka Mwaruka (42) na Ofisa Mazingira wa NEMC, Lilian Laizer (27), wote wakazi wa Ukonga Mombasa na Ofisa Mazingira wa NEMC, Magori Wambura (38) mkazi wa Bombambili.

Kwa pamoja washtakiwa hao wanadaiwa kati ya Septemba 27, 2016 na Aprili Mosi, mwaka jana, jijini Dar es Salaam, walikula njama ya kutenda kosa la kughushi.

Waziri wa Mambo ya Nje Prof. Kabudi apokea Salamu za Pongezi kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa China

$
0
0
 Mheshimiwa Prof. Palamagamba J. Kabudi (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, leo tarehe 13 Machi, 2019 amekutana na kufanya mazungumzo na Mheshimiwa WANG Ke, Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China.

Mheshimiwa WANG Ke pamoja na masuala mengine amewasilisha kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki barua ya pongezi kutoka kwa Mheshimiwa Wang Yi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa China kufuatia Prof. Kabudi kuteuliwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Aidha Prof. Kabudi kupitia kwa Mheshimwa Balozi ameshukuru kwa salamu hizo za pongezi alizopokea.

Katika mazungumzo yao, Prof. Kabudi na Balozi WANG Ke, wameahidi kufanya kazi kwa pamoja ili kuimarisha ushirikiano wa kihistoria baina ya nchi hizo mbili. Na kwa pamoja wamesisitiza umuhimu wa kuendelea na jitihada za kuimarisha mahusiano ya kisiasa, kijamii, kiuchumi hususan kwenye maeneo la uwekezaji, biashara, utalii na miundombinu.
                                                                     
Prof. Kabudi ametumia fursa hiyo kuishukuru Jamhuri ya Watu wa China kwa misaada ya kimaendeleo wanayoendelea kuitoa na kwamba Serikali inafurahishwa na Jinsi China inavyounga mkono jitihada zake za kuwaletea wananchi maendeleo na kujenga uchumi.

Tanzania na China zimekuwa na mahusiano ya kidiplomasia tangu mwaka 1964 na mwaka huu zinatarajia kuadhimisha miaka 55 ya ushirikiano huo.

Mheshimiwa Wang amekuwa Balozi wa kwanza kuonana na Mhe. Kabudi tangu kuteuliwa kwake na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuiongoza Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
13 Machi 2019

Kamati ya Bunge yaipongeza Wizara ya Madini

$
0
0
Na Issa Mtuwa Dodoma
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeipongeza Wizara ya Madini kwa utekelezaji wa Ujenzi wa Jengo la Taaluma la chuo cha Madini Dodoma (MRI) na Ujenzi wa Jengo la Ofisi za Wizara ya Madini lilipo eneo la Mji wa Serikali Ihumwa, Jijini Dodoma.
 
Hayo yamesemwa Machi 13, 2019 na Wajumbe wa Kamati hiyo wakati wa kikao cha majumuhisho kilichofanyika kwenye jengo la wizara ya Madini Ihumwa, mara baada ya kukagua majengo yote mawili na kupewa taarifa ya ujenzi wake.
 
Wakiwa kwenye jengo la taaluma la chuo cha madini, wajumbe wamepongeza na kuridhishwa na hatua ya ujenzi iliyofikiwa na kupongeza SUMA JKT kujenge jengo hilo.
 
Jengo la Taaluma ni la ghorofa tatu lenye ofisi, vyumba vya kufundishia na ukumbi wa mikutano. Ujenzi huo utagharimu jumla ya shilingi 2, 863, 161, 369.00 hadi kukamilika kwake na unatekelezwa chini ya chini ya Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Raslimali Madini (SMMRP) kwa mkopo kutoka Benki ya Dunia.
 
Akizungumzia ujenzi wa jengo la Wizara, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila amewaeleza wajumbe wa kamati kuwa, ujenzi huo ulianza tarehe 4/12/2018 na ulitakiwa kukamilika tarehe 31/01/2019, hata hivyo mkandarasi hakuweza kukamilisha ndani ya muda huo kutokana na sababu mbalimbali. Prof. Msanjila ameongeza kuwa, kwa kuzingatia ushauri wa msimamizi wa ujenzi huo, walifikia makubaliano ya kumuongezea muda mkandarasi hadi kufikia tarehe 28/02/2019.
 
Prof. Msanjila ameongeza kuwa, mpaka sasa ujenzi huo umefikia asilimia 80 na mwezi ujao wizara itakuwa tayari kuhamia. Amesema ujenzi huo umegharimu Jumla ya shilingi Milioni 975,360,028.10 zitatumika katika ujenzi huo.
 
Naye, Waziri wa Madini Doto Biteko ameiambia kamati kuwa, mkandarasi wa ujenzi huo, alipewa muda wa mwezi mmoja kukamilisha ujenzi wake ili wafanyakazi wa Wizara hiyo waanze kulitumia. Waziri emeleza kuwa wizara inaridhishwa na kasi ya mkandarasi katika ujenzi huo.

Biteko ameongeza kuwa, wizara imedhamiria kuhakikisha ujenzi huo unakamilika kwa wakati na kuthibitisha hilo wizara imemteuwa Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala na Raslimaliwatu, Nsajigwa Kabigi ambae yupo muda wote wote eneo la ujenzi.
 
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Dunstan Kitandula amesema pamoja na wabunge kuipongeza wizara kwa kazi nzuri, ameishauri wizara na mkandarasi wa ujenzi huo, Mzinga Holdings Company kujielekeza kwenye manunuzi ya vifaa vinavyopatikana hapa nchini.
 
Wakichangia wajumbe wa kamati hiyo, Joseph Musukuma na Ally Keissy wakichangia wakati wa majumuhisho waliipongeza wizara na mkandarasi, hata hivyo, walishangaa muda waliopewa na hatua iliyofikia, msukuma alisema ni kazi ya kupongeza na wameeleza pamoja na mkandarasi kutokamilisha kazi yake kwa wakati bado utendaji wake wa kazi unaridhisha na kasi yake inaonekana.
 
Naye, Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo aliwaambia wajumbe wa kamati kuwa, ujenzi wa jengo hilo la wizara unafanana ramani na wizara nyingine ikiwemo kiasi cha fedha zilizotolewa na serikali zote zikiwa na kiwango cha shilingi Bilioni moja.
 
Amesema muda uliotolewa ulilenga kutimiza azma ya wizara kuhamia eneo hilo kwa wakati. Aliwashukuru wajumbe kwa ushauri wao na kueleza kwamba kama wizara watauzingatia.

Taarifa Ya Jeshi La Polisi Kutoka Mkoa Wa Mbeya

$
0
0
AJALI YA MOTO KUUNGUZA NYUMBA NA KUSABABISHA MAJERUHI NA UHARIBIFU WA MALI.
Mnamo tarehe 12.03.2019 majira ya saa 20:00 usiku huko katika Kitongoji cha Mapogoro, Kijiji cha Kapunga, Kata ya Itamboleo, Tarafa ya Ilongo, Wilaya ya Mbarali, Mkoa wa Mbeya, CATHERINE MFIKWA [32] Mkazi wa Kapunga pamoja na mtoto wake aitwaye PRISCAN PIUS @ MWAFWALO [14] Mkazi wa Kapunga walijeruhiwa kwa kubabuliwa na moto sehemu za miguu yao kutokana na moto uliozuka ghafla kwenye duka lao.
 
Katika tukio hilo moto huo ulisababisha uharibifu wa bidhaa zilizokuwa zinauzwa kwenye maduka ya (1) PIUS AIDAN @ MWAFWALO [41] Mkazi wa Kapunga, aliyekuwa anauza vinywaji baridi (2) JOMBAA @ RAS aliyekuwa anauza vitu vya jumla (3) JUMA MWAMJINGA aliyekuwa anauza bidhaa za dukani na mahindi.
 
Majeruhi wamelazwa na wanapata matibabu katika Hospitali ya Misheni Chimala na wanaendelea vizuri. Bidhaa zote zilizokuwa zipo stoo zimeokolewa na zimekabidhiwa kwa wamiliki. Chanzo cha ajali hiyo ya moto ni kulipuka kwa jiko la gesi lililokuwa linatumiwa na CATHERINE MFIKWA (mke wa PIUS AIDAN @ MFIKWA) na kushika kwenye bidhaa za dukani na kusambaa kote. Moto huo umezimwa na kikosi cha zimamoto na uokoaji Wilaya ya Mbarali, Polisi na wananchi. Thamani ya mali iliyoungua bado kufahamika.

AJALI YA GARI KUGONGA UZIO NA NYUMBA NA KUSABABISHA MAJERUHI.
Mnamo tarehe 12.03.2019 majira ya saa 14:00 mchana huko maeneo ya Inyala, Wilaya ya Kipolisi Mbalizi, Mkoa wa Mbeya katika barabara ya Mbeya/Iringa, gari no. T. 608 DNP/T. 214 DNW aina ya FAW iliyokuwa ikitokea mkoa wa Songwe kuelekea Dar-es- Salaam ikiwa inaendeshwa na dereva asiyefahamika iliacha njia na kugonga uzio na nyumba inayotumika kwa huduma ya vipimo vya magonjwa mbalimbali ya binadamu [kliniki] na kusababisha majeruhi kwa 1. ZAKARIA CHINA [24] Mkazi wa Uyole ambaye ni mhudumu katika kliniki hiyo, 2. ELIUD FUNGO [38] Mkazi wa Inyala

ambaye ni Daktari wa kliniki hiyo 3. MAGRETHI HASSAN [32] Mkazi wa Inyala aliyekuwa anapata huduma 4. PILI MWANGAMBA [28] Mkazi wa Tunduma na alikuwa abiria kwenye gari hilo. Majeruhi wote wamepata majeraha ya kawaida mwilini na wamelazwa Kituo cha Afya Inyala. Chanzo cha ajali ni ubovu wa gari. Gari hiyo ilikuwa imebeba mzigo aina ya shaba. Msako mkali wa kumtafuta Dereva na mmiliki wa gari unaendelea.

KUFANYA SHUGHULI ZA UGANGA BILA KIBALI (LAMBALAMBA)
Mnamo tarehe 12.03.2019 majira ya saa 07:00 asubuhi huko katika Kijiji na Kata ya Sangambi, Tarafa ya Kiwanja, Wilaya ya Chunya, Mkoa wa Mbeya, Askari wakiwa katika msako waliwakamata 1. PETER DAUDI [37] Mkazi wa Mlimanjiwa 2. SIMON PAMBO [44] Mkazi wa Sangambi 3. AZOLE MWANAHELA [31] Mkazi wa Sangambi na 4. MASUMBUKO CHARLES @ MWANAHELA [36] Mkazi wa Sangambi wakiwa wanafanya shughuli za uganga wa lambalamba isivyo halali. Watuhumiwa walikamatwa wakiwa na madawa mbalimbali ya kienyeji, manyanga na ngoma mbili. Watuhumiwa wengine walitoroka kabla ya kutiwa nguvuni na juhudi za kuwasaka zinaendelea.

TAARIFA YA KIFO – RUNGWE.
Mnamo tarehe 07/03/2019 saa 12:30 mchana huko katika Mto Kiwira uliopo Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa Mbeya Mwanafunzi wa Chuo cha Ualimu Tukuyu Mwaka wa Tatu aitwaye SAMWEL JAMES CHACHA [25] alikufa maji akiwa anaogelea kwenye Mto huo na mwili wake kutoonekana baada ya kusombwa na maji.
 
Kutokana na tukio hilo zilifanyika jitihada za kuutafuta mwili wa mwanafunzi huyo ambapo tarehe 11/03/2019 majira ya saa 16.00 jioni huko katika Kijiji cha Mboyo, Kata ya Lupepo, Tarafa ya Ukukwe, Wilaya ya Rungwe na Mkoa wa Mbeya kwenye mto kiwira mwili wa mwanafunzi huyo ulipatikana.
 
Chanzo cha tukio ni uzembe wa marehemu kutaka kuogelea kwenye mto huo bila kuchukua tahadhari. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Rungwe – Makandana kusubiri uchunguzi wa kitabibu. Upelelezi unaendelea.
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa tahadhari kufuatia matukio ya kufa maji yanayosababishwa na uzembe wa kutovaa maboya wakati wanapoingia majini, mtoni au ziwani. Aidha kufuatia mvua zinazonyesha nawasihi wazazi kuwapeleka watoto wadogo shuleni na kuwapokea ili kuwalinda dhidi ya madhara ya kutumbukia katika maji.

KUZINI NA MAHARIMU.
Mnamo tarehe 09.03.2019 saa 21:00 usiku huko Mtaa wa Ghana, Tarafa ya Sisimba, Jiji na Mkoa wa Mbeya TUMAINI MWASOMI, Mkazi wa Mama John aligundua kubakwa kwa binti yake aitwaye CAREEN BONIPAHCE [14] Mkazi wa Ghana, Mwanafunzi wa Kidato cha Kwanza katika Shule ya Sekondari LEJIKO na baba yake mzazi aitwaye BONIPHACE JULIUS [42] Mkazi wa Ghana.

Aidha CAREEN BONIPHACE anaishi Ghana na baba mzazi baada ya kutengana na mama yake na ndipo baba yake akaanza kumbaka mara kwa mara tangu Septemba, 2018 bila kumwambia mtu yeyote na ndipo juzi tarehe 09.03.2019 majira ya saa 21:00 usiku baba yake alitaka kumbaka tena na ndipo binti huyo alikataa na baba yake alianza kumpiga na kumsababishia maumivu makali mwilini na hivyo kupelekea kumsimulia shangazi yake aitwaye LUCY MWASUMBULE juu ya vitendo vya kubakwa anavyofanyiwa na baba yake.
 
Chanzo cha tukio ni tamaa za kimapenzi. Mtuhumiwa amekamatwa na yupo mahabusu. Mhanga anaendelea na matibabu Hospitalini.

KUPATIKANA NA MICHE YA BHANGI.
Mnamo tarehe 10.03.2019 saa 07:00 asubuhi huko eneo la Mapanga, Kijiji cha Stamiko, Kata ya Mkola, Tarafa ya Kiwanja, Wilaya ya Chunya, Mkoa wa Mbeya. Askari Polisi walikamata miche 30 ya bhangi ikiwa imelimwa kwenye shamba la mahindi lenye ukubwa wa robo heka mali ya NDUSHI SHIJA. Mtuhumiwa alikimbia na juhudi za kumtafuta zinaendelea lakini GUMBA ZALA [32] mkazi wa mapanga-stamiko ambaye ni mke wa mtuhumiwa na LUHENDE SHIJA [18] ambaye ni mtoto wa mtuhumiwa wamekamatwa kwa mahojiano. Mtuhumiwa ni mkulima na muuzaji wa bhangi. Upelelezi unaendelea.

MALI YA KUOKOTA.
Mnamo tarehe 10.03.2019 saa 21:30 usiku huko Kitongoji cha Lubele, Kata ya Ikimba, Tarafa ya Unyakyusa, Wilaya ya Kyela, Mkoa wa Mbeya. Askari Polisi wakiwa doria pamoja na kikundi cha ulinzi shirikishi waliona gari aina ya Toyota Ractics rangi nyeupe ikiwa imeegeshwa maeneo ya uchochoroni kwenye pagala na watu wasiofahamika ambapo msako mkali wa kuwatafuta watuhumiwa unaendelea. Watuhumiwa waliacha gari hilo.
 
Baada ya kulikagua iligundulika kubomolewa kioo kidogo cha mbele upande wa dereva na pia kuharibika mfumo wa kuwashia gari, hivyo kuunganisha nyaya kwa urahisi wa kuliwasha. Gari hilo lilikuwa limebandikwa namba za kitanzania T 512 DCL na ndani ya gari hilo kumekutwa nyaraka zinazoonyesha kuwa ni IT iliyokuwa ikielekea Blantyre nchini Malawi. Ufuatiliaji unaendelea

KUPATIKANA NA MALI ZIDHANIWAZO ZA WIZI.
Mnamo tarehe 10.03.2019 saa 10:00 asubuhi huko maeneo ya ZZK Mbalizi na maeneo mbalimbali ya Mbalizi Wilaya ya Kipolisi Mbalizi. Askari Polisi wakiwa katika msako wa wahalifu na uhalifu na matukio ya uvunjaji walimkamata GOODLUCK JOSHUA [21] mkazi wa Nsalala akiwa na speaker mbili kubwa aina ya Dynamic Ailiong na Equalizers 1 aina media com na baada ya mahojiano alikiri kuhusika katika matukio mbalimbali ya uvunjaji na kutaja washiriki wenzake ambao ni JOHN MBEMBEJA, RAMADHANI, BONKE JIRANI na EMMANUEL MAPUNDA wote wakazi wa Mbalizi.

Makazi yao yamefanyiwa upekuzi na kupatikana mali mbali mbali ambazo ni:-
Mashine ya kuchezea bahati nasibu ya kichina 1,
Monitor aina ya dell 1,
CPU aina ya hp 1,
Radio za aina ya sub woofer zenye majina mbalimbali 5 na speaker zake 8,
King’amuzi cha kampuni ya startimes 1,
Mashine za kunyolea nywele aina home cut 2,
Cable ya umeme aina tronic 1,
Deck ya cd aina singsung 1,
Keyboard na mtungi mdogo wa gas kampuni ya Orexy,
Burner, pamaoja na stand yake mali zote zikidhaniwa kuwa za wizi.
 
Baadhi ya mali zimetambuliwa katika matukio ya uvunjaji. Mbinu ni kuvunja makufuri ya maduka na sehemu za biashara nyakati za usiku na kuiba.

Imesainiwa na:
[ULRICH O. MATEI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA

Acacia yazungumza na Serikali kunusuru Mgodi usifungwe

$
0
0
Na Issa Mtuwa, Dodoma
Uongozi wa Kampuni ya Acacia kupitia Mgodi wa North Mara umezungumza na Serikali kuelezea hatua zilizochukuliwa hadi sasa kudhibiti maji yenye sumu ikiwa ni wiki moja tu ipite tangu Waziri wa Madini Doto Biteko, atangaze kufunga shuguli za mgodi huo endapo utashindwa kudhibiti maji ya sumu yanayotiririka kwenye makazi ya watu, ifike Machi 30 mwaka huu.

Tamko hilo la serikali limeifanya kampuni ya Acacia kuchukua hatua za haraka za kudhibiti maji hayo ili kukwepa rungu la serikali la kuufunga mgodi huo.  Machi 12, uongozi wa Acacia North Mara ulikutana na Waziri Biteko ofisini kwake jijini Dodoma kwa lengo la kueleza hatua iliyofikiwa ya kutekeleza agizo la serikali.

Uongozi wa kampuni hiyo ukizungumza katika kikao hicho, ulieleza kuwa, tayari mgodi huo umechukua hatua za haraka tangu kutolewa kwa agizo na kwamba hadi sasa suala la kudhibiti maji yenye sumu limeshetekelezwa na hakuna maji yanayotiririka kuelekea kwenye makazi ya watu.

Aidha, ulimweleza kuwa, pamoja na kudhibiti maji hayo kupitia bwawa la kuhifadhia maji yenye sumu yajulikanayo kitaalam kama “topesumu” (Tailings Storage Facility- TSF) mgodi umeanza kuchukuwa hatua za kujenga TSF mpya.

“Mhe. Waziri tumekuja kutoa mrejesho wa utekelezaji wa agizo lako, tunafurahi kukuambia kuwa tumetekeleza agizo hilo na kwa sasa hakuna maji yanayotiririka. Pamoja na hatua hiyo mgodi umeanza mchakato wa ujenzi wa bwawa jipya (TSF) la kuhifadhia topesumu,” walieleza.

Aidha, ulimweleza Waziri Biteko kuhusu hujuma za uharibifu wa miundombinu ya bomba la maji yenye sumu unaofanywa kwa maksudi na wakazi wanaozunguka mgodi ili kufifisha juhudi zao za kudhibiti maji hayo wakiwa na lengo la kuufanya mgodi uonekane haujachukuwa hatua kudhibiti jambo hilo, ambapo walionesha picha mbalimbali ya namna bomba lilivyo pasuliwa ili maji yatiririke kuelekeka kwa wananchi.

Akizungumza katika kikao hicho, Waziri Biteko alieleza kuwa, amepokea taarifa ya kampuni husika na kuwapongeza kwa hatua zilizochukuliwa na kusema kuwa, ukweli wa jambo hilo atauthibitisha mara baada ya kupata ripoti ya wataalam watakaokwenda kuhakikisha kuhusu utekelezaji wa agizo hilo na kuongeza,“katika hili sitanii juu ya kuufunga mgodi ikiwa utashindwa kudhibiti tope sumu,”.

 “Naomba nirudie tena katika hili sitanii, sitabadilisha msimamo wangu kama serikali na utaendelea kubaki pale pale dawa pekee ni kutekelezwa kwa agizo hilo. Lakini niseme ukweli, nasikitishwa sana na kitendo hiki cha wananchi kupasua bomba, kwa hili sikubaliani nao na siwaungi mkono.

 Pia, aliongeza kuwa, atawasiliana na Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya kuona namna ya kudhibiti hali hiyo ili wale watakao bainika wachukuliwe hatua.

Waziri Biteko alilitoa agizo hilo   Machi 6, alipoutembelea mgodi huo hapo kwa ziara ya kikazi  pamoja na kuzungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji cha Nyamongo wilaya ya Tarime.

Tundu Lissu Afutiwa Mshahara Na Posho Zake Bungeni

$
0
0
Mbunge  wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu amethibitisha kuwa Uongozi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia kwa Spika wake, Job Ndugai na katibu wa Bunge, Steven Kagaigai umemfutia rasmi mshahara wake na posho za kibunge kwa kile alichoeleza kuwa ofisi ya spika imesema haina taarifa zake kuhusu aliko na anachokifanya.

Lissu amesema amesitishiwa mshahara na posho za kibunge tangu Januari 2019 bila kuelezwa sababu zozote za hatua hiyo na kusema anakusudia kuchukua hatua za kisheria kufikisha suala hilo, Mahakama Kuu ya Tanzania kudai haki zake.

Mnadhimu huyo Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ametoa malalamiko hayo jana Jumatano Machi 13, 2019 kupitia waraka uliosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ukizungumzia jinsi anavyonyimwa stahiki zake za msingi akiwa mbunge.

Lissu amesema tangu Septemba 7, 2017 ameshindwa kuhudhuria shughuli za kibunge kutokana na kuwa nje ya nchi baada ya kushambuliwa na risasi zaidi ya 30 na watu wasiojulikana kisha kupelekwa nje ya nchi kwa matibabu zaidi.

Katika waraka huo, Lissu amezungumzia sheria na taratibu ambazo mbunge anaweza kukosa sifa ya kuwa mbunge ambazo yeye bado anazo ni pamoja na mtu kuhama chama, kuteuliwa kuwa makamu wa rais au kuchaguliwa kuwa rais.

“Ninautaka uongozi wa Bunge yaani Spika Ndugai na Katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai kurudisha mshahara wangu na posho za kibunge bila masharti yoyote,” amesema Lissu.

Amesema Bunge likiwa mhimili mkubwa wa kutunga sheria na kuisimamia Serikali, linapaswa kuheshimu sheria, kusimamia haki na taratibu zake na kuzingatia misingi ya haki katika utendaji wa kazi zake.

“Ili kuhakikisha sheria za nchi yetu zinaheshimiwa na haki inatendeka, ninawaelekeza mawakili wangu nchini Tanzania kuanza mchakato wa kufungua mashauri katika Mahakama Kuu ya Tanzania ili kudai Bunge la Spika Ndugai na Katibu wa Bunge Kagaigai lirejeshe stahili zangu zote zilizozuiwa na kulizuia lisiziingilie na kuziathiri kwa namna nyingine yoyote,” amesema Lissu.

Profesa Lipumba Ashinda Nafasi ya Uenyekiti CUF

$
0
0
Mkutano mkuu wa CUF umemchagua Profesa Ibrahim Lipumba kuwa mwenyeki wa chama hicho, huku nafasi ya Maalim Seif Sharif Hamad ikiwekwa kiporo.

Akitangaza majina ya washindi katika uchaguzi huo, mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi, Thenei Ally Juma alisema jana  Machi 13, 2019 kuwa  Lipumba amepata kura 516 sawa na asilimia 88.9.

Alimtaja aliyeshinda nafasi ya Makamu Mwenyekiti Bara kuwa ni Maftaha Nachuma aliyepata kura 231 sawa na asilimia 40.9.

Juma alimtangaza pia Abbas Juma Muhunzi kuwa mshindi wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti Zanzibar baada ya kupata kura 349 sawa na asilimia 60.9.

Maalim Seif, katibu mkuu wa chama hicho amewekwa kiporo kutokana na mabadiliko ya katiba yaliyofanyika juzi ambayo yamempa nguvu mwenyekiti kuteua majina matatu ya wanachama kwa kushauriana na makamu wenyeviti wa Bara na Zanzibar.

Baada ya hatua hiyo, majina hayo yatapelekwa katika kikao cha Baraza la Uongozi ambalo litakuwa na jukumu la kumpigia kura mmoja.

Mabadiliko hayo yaliyofanywa na mkutano huo yamefuta utaratibu wa awali ambao katibu mkuu alikuwa akichaguliwa na mkutano mkuu na sasa Profesa Lipumba atakuwa ameshikilia hatima ya Maalim Seif.

Uchaguzi huo umefanyika kipindi ambacho CUF iko katika mgogoro mkubwa wa kiuongozi ulioigawa katika pande mbili - mmoja ukiwa wa Profesa Lipumba na ule wa Maalim Seif.

Mgogoro huo umekifikisha chama hicho mahakamani ambako kuna kesi kadhaa ikiwamo ya kumpinga Profesa Lipumba kuwa mwenyekiti na Machi 17, hukumu ya ama ni mwenyekiti au la itatolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.

Mbowe Awashukuru Waliomsaidia Akiwa Gerezani

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Freeman Mbowe amewashukuru viongozi wa chama chake wakiwemo wabunge na wananchi ambao walijitokeza kumpigania ili kuhakikisha kiongozi huyo anatoka nje kwa dhamana.

Mbowe ametoa shukrani hizo baada ya kukaa rumande kwa zaidi ya miezi mitatu baada ya kudaiwa kukiuka  masharti ya dhamana yeye pamoja na Mbuge wa Tarime Mjini Esther.
 
Katika ujumbe huo, Mbowe ameanza kwa kusema, “Naomba niwashukuru sana wale wote walioshiriki nasi kupigana, kulia  na hata kuimarishana kwa njia mbalimbali  katika kipindi chote cha miezi mitatu na nusu tuliyoishi gerezani.”

“Natambua na kuheshimu mno ushiriki wenu kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na sala, ushauri, huduma ya chakula, michango ya fedha, solidarity support mahakamani na  zaidi walioweza kutenga muda wao na kuja kututembelea na kutufariji gerezani Segerea kulikoambatana na zawadi mbalimbali vikiwemo vitabu na magazeti, matunda, maji, juisi na hata machozi!!!.

“Nitambue kipekee kazi kubwa na ya kutukuka iliyofanywa na Mawakili Wasomi waliounda defence team yetu!! You were great all the way through!!

"Nitoe shukrani vilevile kwa wale wote waliotoa support kwa familia  zetu na hata kututunzia na kujenga kwa njia mbalimbali majimbo yetu ya uchaguzi ikiwemo kazi  ya Chadema ni Msingi.”

“Kwa wale walioshindwa vyote hivyo, watambue kwa dhati nawapenda na kuwaombea yote yaliyo mema... au kama wapo wengine waliokwazika kwa njia moja au nyingine.... pia nichukue fursa hii kuwaomba msamaha na kuitaka amani miongoni mwetu!!.

"Niwape pole nyingi wenzetu wote waliokumbwa na masahibu mbalimbali katika kipindi chote hiki!! Tuimarishwe zaidi katika mapito haya ili itimie kauli ya “kesho yetu kuwa bora kuliko jana.Mbarikiwe sana!!" Amesema Mbowe

Kesi ya Mbowe na viongozi wengine Chadema yapangiwa hakimu mwingine

$
0
0
Kesi ya uchochezi inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na viongozi wenzake wanane wa chama hicho, imetua kwa Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Kesi hiyo iliyokuwa ikitajwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Kelvin Mhina leo imepangwa rasmi kusikilizwa mbele ya Hakimu Simba baada ya hakimu aliyekuwa akiisikiliza kuanzia mwanzo, Wibard Mashauri kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Mbali na Mbowe, washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ya uchochezi ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Vincent Mashinji, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu na Naibu Katibu Mkuu Bara na Mbunge wa Kibamba, John Mnyika.

Wengine ni Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, Mbunge wa Bunda, Esther Bulaya, Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko na Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa.

Washtakiwa hao kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 13, ikiwamo kula njama, kufanya mkusanyiko wenye ghasia, kuhamasisha hisia za chuki, kushawishi hali ya kutoridhika, uchochezi na kushawishi utendaji wa kosa la jinai kati ya Februari Mosi na 16, mwaka jana jijini Dar es Salaam.

Viwanja Vikubwa Vinauzwa: Bunju na Mapinga (Baobab Sec)

$
0
0
Viwanja Vikubwa Vinauzwa: Bunju na Mapinga (Baobab Sec)
Viwanja vipo mtaa wa Kimele, Kata Mapinga, km 2 tu kutoka Shule ya secondary Baobab (main road ya Dar to Bagamoyo).
Viwanja vimepangwa vizuri, vina miundombinu ya maji na umeme. 


Viwanja viko vya size na bei tofauti kuanzia mita 20/25 kwa bei ya tsh 6 milion, mita 20/30 kwa bei ya tsh 8 milion, mita 20/40 kwa bei ya tsh 10 milion, mita 30/50 kwa bei ya tsh 18 milion, mita 40/50 kwa bei ya tsh 24 milion, mita 40/60 kwa bei ya tsh 30 milion,

Pia ipo nyumba pagala (haijapauliwa) na ina vyumba 3, kimoja master, sebure, dining, public toilet, kitchen etc na bei yake ni tsh 23,000 (kiwanja chake ni sqm 400 au 20/20 mita)

Na pia, kwa Bunju sokoni, kipo kiwanja cha sqm 1800 kinauzwa tsh 54 milion.

Luksa kulipa kwa awamu (anza na 75%, maliza na 25%)
Ukipata ujumbe huu mjulishe ndugu/jamaa/rafiki yako.
Biashara hii haina dalali, mpigie mhusika: 0758603077, whatsap 0757489709

Boeing 737 Max: Kampuni ya Marekani inayotengeneza ndege iliyoanguka Ethiopia yasitisha matumizi ya ndege zote aina hiyo

$
0
0
Kampuni ya Boeing Marekani inayotengeneza ndege iliyoanguka Ethiopia imesitisha matumizi ya ndege zote aina hiyo baada ya wachunguzi kubaini ushahidi mpya katika eneo ambako ndege ya Ethiopia Airlines ilianguka.

Kampuni hiyo ya Marekani imesema itasitisha usafiri wa ndege zote 371 zinazohudumu.

Shirika linalosimamia usafiri wa anga Marekani FAA, limesema ushahidi mpya pamoja na data mpya za satelaiti zimechangia uamuzi huo wa kupiga marufuku kwa muda usafiri wa ndege hizo.

FAA awali lilisisitiza ndege ya Boeing 737 Max 8 ni salama wakati mataifa mengine yakipiga marufuku usafiri wa ndege hizo.

Ajali hiyo siku ya Jumapili mjini Addis Ababa ulisababisha vifo vya watu 157.

Ni ajali ya pili kuwahi kushuhudiwa ya ndege hiyo chapa Max 8 katika miezi mitano baada ya ajali nyingine nchini Indonesia mwaka jana Oktoba iliosababisha vifo vya watu 189.

FAA lina kundi la maafisa wanaochunguza mkasa huo katika eneo ambapo ajali ya shirika la ndege la Ethiopia ilipotokea likishirikiana na bodi ya kitaifa ya usalama wa safari.

Dan Elwell, kaimu msimamizi katika shirika hilo FAA, amesema Jumatano: " Imebainika wazi kwa pande zote kwamba safari ya ndege ya Ethiopia ilikaribiana na namna ilivyoshuhudiwa kwa ndege iliyoanguka awali ya Lion Air ."

Ameongeza kwamba "ushahidi tuliopata katika eneo, umefanya kuwa na uwezekano mkubwa kwamba hata njia ya ndege ilikaribiana na ile ya Lion Air".

Rais Donald Trump awali alitangaza kwamba shirika la FAA litatoa tangazo la dharura kufuatia "taarifa mpya na ushahidi tuliopokea kutoka eneo la mkasa na kutoka maeneo mengine kupitia malalamiko mengine tofauti".

Marekani ni nchi ya hivi karibuni kusitisha usafiri wa ndege hiyo ya Boeing 737 Max yakiwemo mataifa mengine kama Uingereza, Umoja wa Ulaya, China India na Australia ambayo yote yameamua kusitisha usafiri wa ndege hizo.


-BBC

Migogoro Ya Ardhi Yamrudisha Waziri Lugola Mkoani Morogoro

$
0
0
Na Felix Mwagara, MOHA.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola anatarajia kuwasili kwa mara nyingine Mkoani Morogoro leo, kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imeibua mifarakano baina ya wananchi Mkoani humo.

Waziri Lugola, wiki iliyopita alimaliza ziara yake Mkoani humo iliyokuwa na lengo la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi kuhusiana na utendaji kazi wa Taasisi za Wizara yake.

Lugola katika ziara yake Mkoani humo, alifanya mikutano ya hadhara ambapo alikutana na migogoro mbalimbali lakini kero kubwa kati ya hizo ni kuhusiana na ardhi ambayo inapelekea wananchi kuwekeana chuki, kujeruhiana, kufikishana Polisi pamoja na kuuana.

Kati ya Wilaya tatu alizozitembelea alipokuwa Mkoani humo, ni Morogoro, Mvomero na Kilosa, licha ya wananchi kutoa kero zao mbalimbali, mgogoro wa ardhi uliibuka kwa sehemu kubwa hasa katika Wilaya ya KIlosa.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii, Waziri Lugola alisema alipokuwa Wilaya ya Kilosa, alikutana na mgogoro wa ardhi ambapo umeleta mgawanyiko miongoni mwananchi hivyo akawaahidi kurejea tena Wilayani humo kwa ajili ya kutatua kero zao baada ya kukutana na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Lugola alisema mipango yote ipo sawa, hivyo anatarajia kufanya mkutano wa hadhara na wananchi wa Kilosa Kesho Machi 15 Wilayani humo ili kuwapa majibu ya kero zao pamoja na kumaliza mgogoro wa ardhi unaowakabili.

“Migogoro mingi inaletwa vituo vya polisi hasa Wilaya ya Kilosa, na wananchi katika mikutano yangu ya hadhara wanalalamika kuhusiana na ardhi, baadhi wanawalaumu polisi wangu kutokuwatendea haki na wengine pia wanawapongeza kwa kazi nzuri, na wengi wao wanalalamikia kuwa matajiri ndio wananyang’anya ardhi zao wakitumia fedha kwa wakiwahonga Polisi,” alisema Lugola.

Aliongeza kuwa, alipokuwa katika mkutano wake wa mwisho katika Tarafa ya Kimamba, Wilaya ya Kilosa Mkoani humo, kuliibuka na hoja nyingi za migogoro ya ardhi, kutokana na usugu wa tatizo hilo, aliwaahidi wananchi wa Wilaya hiyo atarejea tena kwa ajili ya kutatua mgogoro huo.

“Ziara yangu niliikatisha katika Mkoa huo, kwa ajili ya kwenda Dar es Salaam kuhudhuria kikao cha Baraza la Mawaziri, hata hivyo, niliwaahidi wananchi nitakutana na Waziri wa Ardhi, ili tushirikiane kutatua mgogoro huu ambao unaweza ukaleta vurugu kubwa pale Kilosa na Mkoa wa Morogoro kwa ujumla,” alisema Lugola.

Lugola anatarajia kufanya mkutano mwingine wa hadhara kuleta majibu ya ahadi alizowaahidi wananchi hao pamoja na kusuluhisha mgogoro huo ili wananchi waendelee kufanya shughuli zao za maendeleo.

Waziri huyo alisema, hawezi kukaa ofisini huku wananchi wakiwa wanapata matatizo mitaani, hivyo atazunguka nchi nzima kuzungumza na wananchi na kupokea kero mbalimbali zinazowakabili. 

“Wananchi wanapojitokeza kwa wingi inasaidia kusikiliza matatizo yao yanayowakabili, ndio mana nimepanga kufanya ziara kama hizi nchi nzima, hii inasaidia sana kujua matatizo mbalimbali ya wananchi pamoja na kuangalia utendaji kazi wa Taasisi zangu zilizopo ndani ya Wizara hii, na hakika Serikali ya Dokta Magufuli inawajali wananchi wake ndio mana inawafuata mahali walipo, ili wazungumze na Serikali yao uso kwa uso,” Alisema Lugola.

Lugola alisema Taasisi zilizopo ndani ya Wizara yake ambazo ni Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza, Idara ya Uhamiaji, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) pamoja na Idara ya Probesheni na Huduma kwa Jamii, zifanye kazi za kiweledi bila kuwaonea wananchi.

Waziri wa Kilimo Atoa Maagizo Mazito Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA)

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) umetakiwa kuhakikisha kuwa katika msimu huu wa mwaka 2019/2020 unanunua mahindi kwa zaidi ya Tani 500,000 kwa wakulima ili kutimiza azma ya serikali ya kuimarisha masoko ya wakulima.

NFRA pia imetakiwa Kubadili mfumo wa ununuzi wa mahindi ili kupunguza gharama kubwa zinazojitokeza wakati wa msimu wa ununuzi.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) leo tarehe 14 Machi 2019 katika hafla ya kukabidhi mtambo wa kusafisha nafaka kwa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) kutoka kwa Mpango wa Chakula Duniani (WFP), makao makuu ya NFRA, Jijini Dodoma.

Hasunga alisema kuwa NFRA imekuwa ikinunua nafaka kidogo kwa wakulima kwa ajili ya kuhifadhi pekee badala yake wametakiwa kufanya biashara ya kununua na kuuza nafaka kwa wingi.

Alisema WFP imekuwa mdau mkubwa wa maendeleo nchini kwa muda mrefu na kwa upande wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula, ushirikiano huo umedumu tangu mwaka 2012. WFP na NFRA wamekuwa wakishirikiana kikamilifu katika kutekeleza majukumu yao kwa manufaa ya pande zote mbili.

Mpango Mkakati wa WFP wa miaka mitano (Country Strategy Plan 2017-2021) unaendana na mipango ya Serikali inayolenga kufikia Maendeleo Endelevu ya Dunia (SDGs), hususani lengo la kutokomeza njaa (Zero Hunger) ifikapo mwaka 2030.

Aliongeza kuwa, mkakati wa WFP wa kuwasaidia wakulima wadogo kupitia mpango wa Farm To Market Alliance (FTMA) unashabihiana na Mpango wa Kuendeleza Sekta ya Kilimo nchini (ASDP II), kwa kuwa mikakati yote imelenga katika kuwasaidia wakulima kuongeza uzalishaji, kupunguza upotevu wa mazao baada ya mavuno, kuongeza thamani ya mazao na kufikia masoko.

Mhe Hasunga alisema kuwa kutokana na mkakati huo, Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, inathamini na kuipongeza WFP katika kuimarisha usalama wa chakula na lishe hapa nchini.

Aidha, alisema serikali inaishukuru WFP kwa kuichagua Tanzania kuwa moja wapo ya Kituo cha Usimamizi wa Bidhaa za Kimataifa (Global Commodity Managed Facility) ambacho kinasaidia kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa masoko ya mazao ya chakula kwa wakulima nchini.

Vivevile, Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) alimuhakikishia Mwakilishi Mkazi wa WFP Michael Dunford kuwa WFP haikukosea kuichagua Tanzania kuwa Kituo cha Usimamizi wa Bidhaa za Kimataifa (GCMF) kuwa, ukiacha faida za kijiografia, Tanzania inajivunia kuwa na kiwango kizuri cha utoshelevu wa chakula. 

Mfano, katika mwaka huu, nchi ina kiwango cha utoshelevu wa chakula kwa 124%, hivyo, nchi ina ziada ya chakula, hii inadhibitisha na kuwahakikishia kuwa Tanzania ina uwezo wa kuuza kwa WFP tani zaidi ya 200,000 wanazohitaji za chakula ambapo ni hitaji lao la kila mwaka.

Breaking News: Spika wa Bunge Job Ndugai Atangaza kumvua Ubunge Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari

$
0
0
Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari, amevuliwa ubunge baada ya kukosa sifa za kuendelea kuwa mbunge kwa kutohudhuria mikutano mitatu ya Bunge mfululizo. 

Spika wa Bunge, Job Ndugai, amemwandikia barua Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi, kumtaarifu kuwa jimbo hilo liko wazi.

Agizo la Rais Magufuli Lasaidia Kuwatoa Kifungoni Wananchi Waliobambikwa Kesi Ya Mauaji Na Polisi

$
0
0
Na.Alex Sonna,Dodoma
BARUA ya wazi aliyoandikiwa Rais Dk. John Magufuli kupitia gazetini na mwananchi aliyebambikiziwa kesi ya mauaji imewezesha kuachiwa huru kwa mwananchi huyo huku Rais akiagiza hatua zaidi zichukuliwe kwa waliohusika kwenye tukio hilo linaloichafua serikali.

Mwananchi huyo Mussa Sadiki, aliandika barua ya wazi kwa rais Machi sita mwaka huu, akilalamikia kubambikiziwa kesi ya mauaji namba 8/2018 katika Mahakama ya Tabora baada ya kukamatwa na polisi ambapo baada ya rais kuisoma aliiagiza Ofisi ya Mwendesha Mashataka Mkuu wa Serikali, kuchunguza kubaini ukweli.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dodoma, Mwendesha Mashataka Mkuu wa Serikali (DPP), Biswalo Mganga, amesema kuwa  baada ya mwananchi huyo kukamatwa, polisi walimnyang’anya sh. 778,000, simu ya mkononi na mali alizokuwa amenunua kwa ajili ya wakulima wakati akienda kwenye manunuzi.

“Kwa mujibu ya malalamiko yake aliyoyaandika gazetini, baada ya kukamatwa aliwekwa kwenye Kituo cha Polisi Tabora Mjini na kubambikizwa kesi ya kuvunja na kuiba ambapo alikaa kituoni kwa muda wa juma moja na alipopelekwa mahakamani alisomewa shtaka la mauaji,” alieleza.

DPP amefafanua  kuwa, baada ya Rais Dk. Magufuli kusoma barua hiyo, aliagiza Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ifuatilie malalamiko ya mwananchi huyo haraka ili kujua ukweli.

Aidha amesema kuwa Ofisi ya DPP ilifuatilia suala hilo kwa kufanya mahojiano na mlalamikaji pamoja na kupitia nyaraka zilizopo katika kituo cha Polisi Tabora Mjini zinazohusiana na sakata hilo.

“Katika kufuatilia malalamiko hayo, ofisi ya DPP imebaini malalamiko hayo ni ya kweli. Hii ni kwa sababu kitabu cha kuzuia wahalifu (detention register) kilichopo katika kituo hicho cha polisi, kinaonyesha kuwa mwananchi huyo alikamatwa Juni 21 mwaka jana kwa kosa la kuvunja nyumba usiku na kuiba na aliingizwa mahabusu ya polisi saa tisa alasiri.

Hata hivyo amaesema kuwa  kitabu hicho kinaonyesha kuwa Juni 29 mwaka jana, mlalamikaji alitolewa mahabusu saa mbili asubuhi na kupelekwa mahakamani.

Mwendesha Mashtaka Mkuu  ameeleza alieleza kuwa, tarehe hiyo hiyo mwananchi huyo alifunguliwa kesi ya mauaji namba 8/2018 ikionyesha Mei sita mwaka jana katika barabara ya Kazima Tabora Mjini, alimuua Jackson Thomas.

Ameeleza  kuwa wakati wa kufuatilia malalamiko hayo, ofisi ya DPP ilibaini Julai mosi mwaka jana, alikamatwa Edward Matiku kwa makosa ya kuvunja nyumba usiku na kuiba lakini Julai 16 mwaka jana, naye aliunganishwa katika shauri la mauaji namba 8/2018 kuhusika na mauaji ya Jackson Thomas.

“Baada ya kuyabaini hayo, Machi nane mwaka huu, niliwafutia washtakiwa wote wawili mashtaka hayo na mahakama ikawaachia huru.

DPP  ameeleza kuwa baada ya Rais Dk. Magufuli kupokea ukweli wa malalamiko hayo na hatua zilizochukuliwa, anampongeza Mussa Sadiki kwa ujasiri aliouonyesha kwa kuweka wazi malalamiko yake.

Aidha amesema kuwa Rais anavishauri vyombo vingine vya habari kuchunguza na kuchapisha habari zenye ukweli kwa kuzingatia maslahi ya taifa.

“Mheshimiwa Rais ameagiza hatua zaidi zichukuliwe kwa wote waliohusika na tukio hilo kwa lengo la kukomesha tabia kama hizo zinazoichafua serikali kwa wananchi wake na dunia nzima,” amesisitiza

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya March 15

Spika Ndugai azungumzia Tundu Lissu kutolipwa mshahara

$
0
0
Spika wa Bunge Job Ndugai amesema hajapata taarifa yeyote juu ya kuzuiliwa kwa mshahara wa Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu, huku akimtaka Mbunge huyo kuandika barua kwa ofisi ya Spika juu ya madai yake.
 
Spika Ndugai ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na EATV  juu ya kauli yake dhidi ya madai ya Mbunge Tundu Lissu ambaye amelalamikia kusitishwa kwa mshahara wake.

Ndugai amesema "kiukweli sijasikia lolote lakini hayo madai ya mshahara alimwandikia Spika barua kwamba hakupata mshahara wake na akajibiwa ni kwanini hakupewa mshahara wake?".

"Bunge linataratibu kwani hata wewe ukiwa hujapata mshahara huwa unadai kwenye mitandao, hebu muulize kwanza yeye amezifuata hizo taratibu?" ameongeza Ndugai.

"Unajua nyinyi mnawafanya wabunge kama Mungu watu ila wabunge ni kama watumishi wengine wa umma kama wewe unavyokuwa hujapata mshaharana Mbunge anatakiwa afanye hivyohivyo."

Mtambo Wa Kuchakata Asali Wafungwa Wilayani Manyoni

$
0
0
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS) umefunga mtambo wa kuchakata asali wilayani Manyoni mkoani Singida.

Akizungumza jana Machi 14,2019 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano TFS Tulizo Kilaga amesema mtambo  huo wa kisasa una uwezo wa kuchakata lita 500 kwa siku.

Amesema kuwa mtambo huo umegharimu Sh.milioni 80 na unatarajiwa kuondoa changamoto ya uwepo wa asali yenye kiwango duni cha ubora katika ukanda huo na maeneo maeneo ya jirani.

“Mtambo huu umefungwa katika kiwanda cha TFS na utatumiwa na wafugaji wa nyuki wa ndani pamoja na nje wote wataruhusiwa kuchakata mazao yao,”amesema Kilaga.

Ameongeza kuwa kiwanda hiko kwa kiasi kikubwa kitategemea mali ghafi toka kwenye msitu wa Aghondi uliopo eneo la Itigi na uwepo

wa mtambo huo pia utasaidia kutunza mazingira kwani watakuwa na uhakika wa soko la asali yao.

Pia amesema katika uvunaji wa awali wamefanikiwa kuvuna mizinga 459 kati ya 729 na kupata asali kilo  6,175 sawa na tani 6.175 wastani kilo 13.45 kwa mzinga.

Akizungumzia mtambo huo, Meneja wa TFS wilayani Manyoni Juma Mambo amesema utasaidia kupatikana kwa asali bora na hivyo kuwa na uhakika wa soko la ndani na nje ambalo litawafanya wadau kujiongezea kipato.

Lugola Afanya Ziara Ya Kushtukiza Kituo Cha Trafiki Buigiri Mkoani Dodoma, Baada Ya Kupata Malalamiko Ya Madereva

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, MOHA
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amefanya ziara ya kushtukiza kituo cha Askari wa Usalama Bararani (Trafiki) Buigiri Mkoani Dodoma, baada ya kupokea malalamiko mara kwa mara kutoka kwa madereva wanaoitumia barabara hiyo.

Lugola alifika katika kituo hicho kilichopo barabara kuu ya Dodoma-Morogoro, nje kidogo ya Jiji la Dodoma, jana saa kumi alasiri akiwa ameambatana na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoani humo, SSP Nuru Selemani, na kuanza kutaka kujua utendaji kazi wa askari hao katika kituo hicho.

Akizungumza na askari hao, Lugola aliwataka wafanye kazi kiweledi bila kuwaonea madereva kwa kuwaomba rushwa au kuwapiga faini kwa uonevu.

“Licha ya kuwapongeza kwa kazi nzuri kwa kuyaongoza magari lakini mnapaswa kufuata sheria na si kufanya kazi kwa uonevu, nimekua napokea malalamiko mara kwa mara kutoka kwa madereva kuhusu kituo hiki, fanyeni kazi kwa mujibu wa sheria za usalama barabarani zinavyoelekeza,” alisema Lugola.

Kwa upande wake SSP Selemeni, alimweleza Waziri huyo kuwa, wanakabiliwa na changamoto mbalimbali katika utendaji wa kazi zao, lakini maelekezo ya utendaji kazi wa weledi waliopewa wameyapokea na kuahidi kuyafanyia kazi.

Lugola alisema yeye ni Waziri ambaye anafuatilia maagizo yake kila anapoyatoa, hivyo askari ambao wanachafua Jeshi la Polisi hatawavumilia, na ataendelea kufanya ziara za kushtukiza kama hizo mara kwa mara sehemu mbalimbali nchini.

Waziri huyo yupo njiani kuelekea Mjini Morogoro kwa ajili ziara ya kikazi atakayoifanya Kesho Machi 15, Tarafa ya Kimamba, Wilayani Kilosa, Mkoani humo.

Mkuu Wa Idara Ya Ardhi Kyerwa Apewa Wiki Moja Vinginevyo Kutumbuliwa

$
0
0
Na Munir Shemweta, KYERWA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amempa wiki moja Mkuu wa Idara ya Ardhi katika Halmashauri ya wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera kuhakikisha anaingiza viwanja 516 katika Mfumo wa Malipo ya Serikali kwa njia ya Kielektroniki vinginevyo ataondolewa katika wadhifa huo.

Agizo hilo limafuatia Dkt Mabula kuelezwa na Mkuu huyo wa Idara kuwa katika halmashauri hiyo jumla ya viwanja 348 pekee ndvyo vilivyoingizwa katika Mfumo wa Kielektroniki huku viwanja 516 vikiwa havijaingizwa kwenye mfumo huo.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alitoa agizo hilo jana tarehe 15 Machi 2019 wakati akiwa katika mfululizo wa ziara yake ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia sekta ya ardhi katika wilaya za mkoa wa Kagera.

Dkt Mabula alisema kuna uzembe mkubwa kwa Mkuu huyo wa Idara ya Ardhi ambaye pia ni Afisa Ardhi Mteule wa halmashauri ya wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera kusimamia uingizaji viwanja kwenye mfumo ambao ndiyo unaosaidia kuongeza mapato ya serikali.

Naibu Waziri alishangazwa na Mkuu huyo wa Idara kushindwa kuingiza idadi hiyo ya viwanja kwenyea mfumo wa kielektroniki katika kipindi cha mwaka mzima wakati alieleza kuwa kwa siku moja anao uwezo wa kuingiza viwanja ishirini.

‘’Kuna uzembe katika kusimamia idara hii ya ardhi na kama mzigo ni mkubwa kwako kusimamia idara hii basi chagua kuachia nafasi moja katia ya Ukuu wa idara ya ardhi au Afisa Ardhi Mteule  ili uweze kuifanyia nafasi moja kwa ufanisi’’ alisema Mabula.

Akigeukia suala la utoaji hati katika halmashauri hiyo ya Kyerwa, Dkt Mabula aliiagiza halmashauri ya Kyerwa kuhakikisha maeneo yote yaliyochukuliwa kwa ajili ya matumizi ya umma yanapatiwa hati ili kuepuka migogoro ya ardhi.

Alisema, migogoro mingi kwenye taasisi za umma inasababishwa na taasisi hizo kutokuwa na hati kwenye maeneo yake na kutolea mfano moja ya maeneo yanayovamiwa sana ni yale ya wazi na kuzitaka  idara husika kusimamia suala hilo kwa makini.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa Rashid Mwaimu alisema viwanja vingi katika wilaya yake havina hati jambo alilolieleza kuwa wakati mwingine linawapa ugumu wa kuchukua hatua kwa wamiliki wake ambao aliwaeleza kuwa wengi wameacha maeneo yao kuwa mapori.

Kwa mujibu wa Mwaimu wilaya hiyo imetoa miezi sita kwa wamiliki wote wa viwanja ambao hawajaviendeleza na kuviacha mapori kuviendeleza vinginevyo watafutiwa umiliki wake.

Katika hatua nyingine Dkt Mabula ametaka halamashauri ya wilaya ya Karagwe mkoa wa Kagera kulitumia Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kujenga nyumba kwa ajili ya watumishi wake ili kuondoa uhaba wa makazi kwa watumishi wa halmashauri hiyo.

Alibainisha kuwa, hata kama halmashauri hiyo haihitaji nyumba kwa ajili ya watumishi wake basi inaweza kujengewa nyumba na shirika hilo kwa ajili ya kuutengeneza mji wa Karagwe na wakati huo kuzitumia nyumba hizo kama rasilimali ambapo nyumba hizo zinaweza kupangishwa na  kuiwezesha halmashauri kujipatia kipato.

‘’Halmashauri badala ya kutegemea kuingiza mapato katika baadhi ya vyanzo kama vile kituo cha mabasi wanaweza kulitumia shirika la nyumba kuongeza hadhi ya mji na mapato kwa halmashauri’’ alisema mabula.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images