Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Serikali yasimamisha leseni ya gazeti la The Citizen kwa Wiki Moja

$
0
0
Serikali imesimamisha leseni ya uchapishaji na usambazaji wa gazeti la The Citizen kwa siku 7 kuanzia leo, Februari 27, 2019, kwa madai ya kuandika habari ya uongo na upotoshaji kuhusu kuporomoka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania.

Barua ya Februari 27, 2019 ya kusimamishwa kwa The Citizen iliyosainiwa na msajili wa magazeti, Patrick Kipangula kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) inaeleza kuwa adhabu hiyo inahusu pia mtandao wa gazeti hilo.

“Katika habari hiyo kwa makusudi uliandika habari za uongo na upotoshaji kwa kuaminisha umma wa Watanzania na kwamba thamani ya Shilingi ya Tanzania imeporomoka ikilinganishwa na miaka mitatu iliyopita pasipo kufuata utaratibu wa kisheria na kanuni za fedha ambapo viwango vya fedha ya Tanzania hutolewa na Benki Kuu ya Tanzania,” inasema aya mmojawapo ya barua hiyo.

 “Uamuzi wa kusimamisha kwa muda leseni hiyo unatokana na mwenendo na mtindo wa habari na makala ambao kwa kiasi kikubwa unakiuka misingi ya maadili ya taalamu ya habari kwa upotoshaji wa mara kwa mara wa taarifa zinazohusu Serikali na uchochezi bayana unaokiuka masharti ya leseni,” inasema aya nyingine katika hiyo iliyotumwa kwenda kwa Mhariri Mtendaji Mkuu wa Mwananchi Communications Limited (MCL).

Katika barua hiyo, Serikali imeeleza kuwa licha ya gazeti la The Citizen kuomba radhi mara kwa mara bado limeendelea na uandishi ule ule wenye utata na ikalitaka lijirekebishe na kuzingatia misingi ya taalamu ya habari na sheria za nchi.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari amesema licha ya habari hiyo, The Citizen limewahi kuchapisha habari nyingine inayokiuka misingi na maadili ya uandishi wa habari Julai 22, 2018. 

Habari hiyo iliyokuwa na kichwa cha habari ‘US Senator Raises Alarm on Tanzania” ilimnukuu seneta wa Jimbo la New Jersey nchini Marekani, Bob Menendez alieleza kuhusu mwelekeo wa ukuaji wa demokrasia nchini Tanzania.

Mradi Wa Soko La Kisasa Manispaa Ya Morogoro Wamkuna Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji

$
0
0
Na Peter Haule, WFM, Morogoro
Halmashauri zote nchini zimetakiwa kujifunza kutekeleza miradi ya Kimakakati inayopatiwa ruzuku na Serikali, katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa kuwa thamani halisi ya mradi wa Soko la kisasa utakaogharimu Sh. bilioni 17 hadi kukamilika kwake inaonekana.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji, alipofanya ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua mradi wa kimkakati wa ujenzi wa Soko la Kisasa katika Manispaa ya Morogoro Mkoani Morogoro wenye lengo la kuzifanya Mamlaka za Serikali za Mitaa ziweze kujitegemea kimapato.

Dkt. Kijaji alisema kuwa Kama ipo halmashauri iliyopewa fedha za kutekeleza miradi ya kimkakati kwa kuwekeana mkataba na Serikali na bado inashindwa kufuata makubaliano ya mkataba ijifunze kutoka Manispaa ya Morogoro.

“Ukilinganisha na miradi mingine ya kimkakati niliyoikagua katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani, huu ni wa mfano, zipo halmashauri ambazo zimepewa fedha halafu zinarudi tena kuangalia upya mikataba ambayo waliwekeana saini na Serikali jambo ambalo linatia mashaka, tuje tujifunze kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro kwa nini ameweza kwenda na wakati ulio katika mkataba”alisema Dkt. Kijaji.

Alipongeza hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa mradi huo ambao umefikia asilimia 30 japo walitakiwa kufikia asilimia 40 katika kipindi hiki kutokana na changamoto ya kujaa maji na kuutaka uongozi wa Manispaa hiyo kukamilisha ujenzi ndani ya kipindi cha miezi mitano ili wafanyabiashara waanze kulitumia soko hilo.

“Mapato ya Soko hili yataongezeka kutoka Shilingi bilioni moja, kwa mwaka hadi Sh. bilioni 4 kwa kuwa idadi ya wafanyabiashara itaongezeka kutoka 400 kwa sasa hadi 900 na huduma zingine zitatolewa kama Benki” alieleza Dkt. Kijaji.

Dkt. Kijaji alisema kuwa dhamira ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, ya kuanzisha miradi ya kimkakati kwa manufaa ya watanzania itatimia kupitia mradi wa Soko la Kisasa la Manispaa ya Morogoro.

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Bi. Regina Chonjo, ameishukuru Serikali kwa kupeleka mradi huo Wilayani kwake, kwa kuwa soko lililokuwepo lilijengwa mwaka 1953 hivyo kuwa na miundombinu mibovu iliyosababisha wananchi kuwa na magonjwa ya mlipuko kikiwemo kipindupindu, hivyo mradi huo si tu utaongeza mapato na kuweka mandhari nzuri, lakini pia utaimarisha afya za wananchi.

Naye Meya ya Manispaa ya Morogoro  Bw. Pascal Kihanga, alisema kuwa waliwaahidi wananachi kusimamia ujenzi wa Soko hilo jambo ambalo linatekelezwa kwa juhudi kubwa, hivyo kufikia mwezi Septemba mwaka huu mradi utakabidhiwa kwa Serikali na wafanyabiashara wote walioondolewa kupisha mradi na  wengine watarudi.

Mhandisi wa Mradi huo Antonio Mkinga, amesema kuwa mradi huo utakamilika katika muda uliopangwa, kwa kuwa mpaka sasa hakuna vikwazo ambavyo vinaweza kuzuia utekelezaji wake.

Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro ni miongoni mwa Halmashauri 17 zilizokidhi vigezo vya kutekeleza jumla ya miradi 22 ya kimkakati nchini kwa mwaka wa fedha 2018/2019 kwa gharama ya shilingi bilioni 147 ambapo Manispaa hiyo ilipata mradi huo wa soko la kisasa litakalogharimu shilingi bilioni 17.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya February 28

"Asante Baba" -Wimbo Maalumu toka THT Group kwa Ajili ya Ruge Mutahaba.

$
0
0
"Asante Baba" -Wimbo Maalumu  toka THT Group kwa Ajili ya Ruge Mutahaba.

BREAKING: Kiwanda cha viatu cha Bora Taraza Dar es Salaam Kinateketea kwa Moto

$
0
0
Sehemu ya kiwanda cha viatu cha Bora kinawaka moto katika eneo la Tazara jijini Dar es Salaam. 

Chanzo bado hakijajulikana, lakini Kikosi cha zimamoto tayari  kiko eneo la tukio na juhudi za kudhibiti moto huo zinaendelea.

Kim, Trump waanza siku ya pili ya mazungumzo

$
0
0
Rais wa Marekani Donald Trump na Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un wameanza siku ya pili ya mazungumzo, baada ya kukutana jana katika hafla ya chakula cha jioni
 
Trump alisifu kile alisema ni "uhusiano maalum” alipokutana na Kim katika mji mkuu wa Vietnam Hanoi hapo jana na akasema kuwa ameridhiswha na kasi ya mazungumzo, licha ya kuwepo kwa ukosoaji kuwa hayasongi haraka iwezekanavyo.

Ikulu ya Marekani imesema viongozi hao wawili wanapanga kusaini "makubaliano ya pamoja” baada ya kufanya mazungumzo zaidi leo. Hata hivyo haikutoa maelezo yoyote kuhusu sherehe hiyo ya utiaji saini, ijapokuwa mazungumzo ya pande zote yamejumuisha uwezekano wa taarifa ya kisiasa ya kutangaza kumalizika kwa Vita Vya Korea vya mwaka wa 1950 – 53, ambayo baadhi ya wakosoaji wanasema bado mapema.

Maafisa Marekani na Korea Kaskazini wamesema Trump na Kim pia walijadili kwa sehemu hatua za kuondoa silaha za nyuklia, kama vile kuwaruhusu wakaguzi kushuhudia kuharibiwa kwa kinu cha nyuklia cha Korea Kaskazini cha Yongbyon.
 
Makubaliano ya Marekani huenda yakajumuisha kufunguliwa kwa ofisi za mawasiliano au kuruhusu miradi kati ya Korea mbili, lakini wakosoaji wanasema Trump anakabiliwa na hatari ya kupoteza kabisa uwezo wa kujiinua kama atalegeza sana Kamba na kwa haraka.

Mkutano wa kilele wa Hanoi ni wa pili kwa Trump na Kim tangu mkutano wa kwanza nchini Singapore mwezi Juni ambao ulikuwa wa maneno tu na sio hatua zozote thabiti na tangu hapo hakujawa na maendeleo yoyote muhimu yaliyopatikana.

Rais huyo wa Marekani hata hivyo alionekana kuwa mchangamfu na Kim hata wakati wakili wake wa zamani Michael Cohen akitoa ushahidi katika kikao cha bunge mjini Washington, akimuita Trump "mlaghai” ambaye alifahamu kabla kuhusu kutolewa kwa barua pepe zilizoibiwa ambazo zililenga kumdhuru mpinzani wake wa Democratic katika kampeni za uchaguzi wa mwaka wa 2016.

Huku akikabiliwa na shinikizo nyumbani kuhusu uchunguzi wa Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani, Trump anatafuta kupata ushindi kwa kujaribu kuishawishi Korea Kaskazini kuachana na silaha zake za nyuklia kwa kubadilishana na ahadi za Amani na maendeleo, lengo la seria ya kigeni ambalo liliwatatiza watangulizi wake kadhaa.

Trump na Kim walifanya mazungumzo ya ana kwa ana kabla ya hafla ya chakula cha jioni ambayo ilihudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nchi za Kigeni wa Marekani Mike Pompeo, kaimu mkuu wa shughuli za serikali Mick Mulvaney, mjumbe mkuu wa Kim Yong Chol na Waziri wa Mambo ya kigeni wa Korea Kaskazini Ri Yong Ho.

Hii leo, viongozi hao wawili wana msururu wa mikutano kwenye hoteli ya Metropole, wakianza na mazungumzo mengine ya ana kwa ana ambayo yatadumu kwa dakika 45.

Credit:DW

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

India, Pakstani Zaingia Vitani Rasmi

$
0
0
India na Pakistan zimesema kila mmoja imetungua ndege za kivita za mwenzie , siku moja baada ya ndege za kivita za India kushambulia ndani ya Pakistan kwa mara ya kwanza tangu vita vya mwaka 1971, na kusababisha mataifa makubwa duniani kuzitaka nchi hizo kuonesha uvumilivu. 

Nchi zote zimeamuru mashambulizi ya anga katika nchi hizo, ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ambapo nchi hizo zenye silaha za kinyuklia kufanya hivyo, wakati majeshi ya ardhini yameshambuliana katika maeneo zaidi ya kumi na mbili. 

Hali ya wasi wasi imeongezeka tangu pale shambulio la kujitoa muhanga katika gari lililofanywa na wanamgambo kutoka Pakistan na eneo la Kashmir linalomilikiwa na India kuwauwa kiasi ya wanajeshi 40 wa India hapo Februari 14, lakini kitisho cha mzozo kiliongezeka haraka jana wakati India ilipoanzisha mashambulizi ya anga katika kile ilichosema ni kituo cha mafunzo ya wanamgambo.

Tapeli Awaliza Watumishi wa Umma.....Serikali Yatoa Tahadhari

Waziri Kigwangala Ateua Wajumbe Wa Bodi Ya Wakurugenzi Ya Mamlaka Ya Usimamizi Wa Wanyamapori Tanzania – (Tawa)

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamisi A. Kigwangalla (Mb.), amekamilisha uteuzi wa safu ya wajumbe wa bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania – (TAWA), kulingana na mamlaka aliyonayo kwa mujibu wa kifungu cha 3.1.1 cha amri ya uanzishwaji wa Mamlaka ya TAWA ( GN na. 135 ya mwaka 2014)  kwa kuwateua wajumbe wengine wawili.
 
Wajumbe walioteuliwa kukamilisha safu inayotakiwa ni;
(i)    Bi. Jane Claude Mihanji  na
(ii)    Bi Magdalena Joseph Kimaty
 
Uteuzi huu ni wa miaka mitatu kuanzia tarehe 26 Oktoba, 2018.
 
Wakati huo huo, Waziri wa Maliasili na Utalii, amebatilisha uteuzi wa Dkt. Freddy S. Manongi kuwa mjumbe wa bodi ya TAWA.

Imetolewa na

Dorina G. Makaya
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
27 Februari, 2019

Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Wamiliki Wa Leseni Za Uchimbaji Madini Zisizotumika Wakalia Kuti Kavu

$
0
0
Na Peter Haule, WFM, Morogoro
Serikali imeahidi kulifanyiakazi suala la Leseni mfu za uchimbaji madini mkoani Morogoro, ili kutoa fursa ya wachimbaji wadogo  kuchimba madini hayo na kulipa kodi stahiki kwa manufaa mapana ya Taifa.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji alipofanya Mkutano na Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na Watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Mkoani Morogoro na wadau wengine.

Maelekezo hayo yanafuatia maelezo ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Steven Kebwe, ambaye pamoja na kuishukuru Serikali kwa  kutoa fedha zenye lengo la kuzisaidia Mamlaka za Serikali za Mitaa kujitegemea kimapato na akaiomba Serikali kuhakikisha inafuta Leseni mfu za wachimba madini takribani 174 ambao wanazuia wachimbaji wadogo kufanya shughuli za kujipatia kipato kutokana na  madini na kulipa kodi.

Dkt. Kabwe alimweleza Dkt. Kijaji kwamba mkoa wa Morogoro umesheheni madini ya kila aina na jambo linalosababisha ukosefu wa mapato unachangiwa pia na  utoroshaji wa madini ambapo ameeleza kuwa mikakati ya Mkoa huo ni kuanzisha Soko la Madini mkoani humo ili kuepusha utoroshaji huo.

Dkt. Kijaji alisema kuwa kama wapo watu wenye Leseni za uchimbaji madini 178 na wanaolipa kodi ni wanne pekee hakukuwa na sababu ya kuendelea kuwa nao, hivyo atalifikisha suala hilo kwa Waziri mwenye dhamana ya madini ili kuangalia ni namna gani wachimbaji wadogo wataweza kupewa fursa hiyo ili waweze kujipatia kipato na kulipa kodi.

Akizungumza kuhusu uwezo wa nchi kujitegemea kimapato, Dkt. Kijaji alisema kuwa Tanzania imepunguza  utegemezi na kufikia asilimia 12, na kwamba  fursa nyingi za kimapato hazijatumika kikamilifu na kutoa wito kwa kila kiongozi na watumishi kuwajibika kikamilifu katika maeneo yao ya kazi ili Taifa liweze kujitegemea zaidi.

 “Wanafalsafa mbalimbali wanasema Taifa lisilojitegemea kimapato ni watumwa, Taifa lisilojisimamia kwa mapato yake halijapata uhuru kamili kwa sababu mapato ndio moyo wa Taifa lolote na  mapato ya Taifa lolote ndio usalama wa Taifa hilo”, alieleza Dkt. Kijaji.

Alisema Taifa likiwa imara kimapato hakuna yeyote atakae lichezea hasa likiwa limejiimarisha kwa mapato ya ndani,  kwa kuwa  mapato yanasababisha kuwa na uhuru wa kufikiri na kupanga mipango ya maendeleo bila kusubiri kupangiwa na watu wengine.

Naibu Waziri huyo alibainisha kuwa ni lazima kuhakikisha  mianya yote ya ukwepaji kodi inafungwa na  kuzuia matumizi yote yasiyo ya lazima ili kuzielekeza fedha hizo kwenye maeneo yenye maslahi mapana ya Taifa.

Alisema kodi zinazokusanywa, matokeo yake yanaonekana ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa ujenzi wa Reli ya Kisasa kipande cha Dar es Salaam hadi Morogoro ambapo umefikia asilimia 42 katika utekelezaji wake.

Aidha vijiji zaidi ya 3,500 vimewashwa umeme ndani ya miaka miwili ya uongozi wa awamu ya Tano, Hospitali 67 kwenye halmashauri nchini zimeanza kujengwa na  Tanzania inaangaza Dunia baada ya kununua ndege zake kwa  mapato ya ndani kutokana na  kuiishi falsafa ya Mhe. Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Amewataka viongozi wa Mkoa huo na watumishi wengine kuhakikisha wanatenda kile walichoamriwa katika nafasi zao kwa bidii na kuepukana na rushwa kwa kuwa Taifa litajengwa na wazalendo  na sio wenye meno.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Gairo Bi. Siriel Mchembe alieleza kuwa  ni vema kuwa na uhusiano mzuri kati ya Uongozi wa Mkoa, Wilaya na Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa kushirikiana na uongozi wa vijiji na mitaa ili kuwa na kanzi data hasa ya majengo ili kuhakikisha makusanyo yanaongezeka na lengo la Mkoa kukusanya Sh.  Bilioni 91 kwa mwaka linafikiwa.

Dkt. Kijaji anaendelea na ziara ya kukagua miradi iliyopewa fedha na Serikali ikiwemo ya Kimkakati Mkoani Morogoro iliyo na lengo za kuzisaidia Halmashauri kujitegemea kimapato

Mwisho.

Dudu Baya Ajisalimisha Polisi

$
0
0
Kamanda wa Polisi Kinondoni, Mussa Taibu amesema msanii, Godfrey Tumaini ‘Dudu Baya’ anashikiliwa na Jeshi la Polisi katika Kituo cha Polisi Oyster Bay jijini Dar es Salaam kwa mahojiano kutokana na tuhuma za kukashifu na kutoa lugha za kejeli kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media, marehemu Ruge Mutahaba.

Dudu Baya amejisalimisha leo Februari 28, 2019 baada ya kuamriwa na Baraza la Sanaa la Taifa kufanya hivyo.

Jana, Waziri wa Habari na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe aliagiza Jeshi la Polisi na Basata wamchukulia hatua mwanamuziki huyo kwa makosa ya kumkashifu, aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji, Ruge Mutahaba.

Baada ya amri hiyo, Basata ilimtaka mwanamuziki huyo kujisalimisha katika kituo cha polisi Oysterbay asubuhi ya leo.

Dereva Basi la Mwendokasi kizimbani kwa kumkata abiria kidole kwa kioo cha gari

$
0
0
Dereva wa basi la Mwendokasi, Khalid Shaha (43), amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni, Dar es Salaam, akikabiliwa na shtaka la kumkata kidole Godfrey Liwa kwa kioo cha gari.

Akisoma shtaka hilo mbele ya Hakimu Hanifa Mwingira, Mwendesha Mashtaka wa Jamhuri, Matarasa Hamisi, alidai Oktoba 12 mwaka jana eneo la Magomeni, Wilaya ya Kinondoni, dereva huyo alimkata Liwa kwa kioo cha gari.

Mshtakiwa alikana kutenda kosa hilo na aliachiwa kwa  dhamana hadi Machi 12, mwaka huu kesi itakapotajwa tena.


Super Mbushi Power:ni Maalum Kwa Wenye Matatizo Ya Upungu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Wanaume wengi wamekuwa na upungufu wa Nguvu za kiume na kuwa na maumbile madogo ya kiume .

Magonjwa kama Kisukari,Presha,Ngiri ya kupanda na kushuka,Tumbo kuunguruma chini ya kitovu,Kutokupata choo vizuri,Tumbo kujaa gesi,Unywaji wa pombe kupita kiasi Pamoja na msongo wa mawazo huchangia kwa kiasi kikubwa upotevu wa nguvu za kiume

Tumia dawa za mitishamba ambayo haina madhara kwa mtumiaji hata awe na miaka 70-85 inatibu na kumaliza matatizo hayo kwa mda mfupi tu.

SUPER MBUSHI POWER:Hii ni dawa yenye uwezo mkubwa wa kuongeza nguvu za kiume mara dufu; huanza kufanya kazi ndani ya dk kumi na tano(15)toka uitumie.
(1)Itakufanya uwe na NGUVU za ajabu ukiwa unafanya tendo la ndoa
(2)Inaongeza hamu ya kurudia tendo la ndoa bila kuchoka.(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 27 kwa tendo la pili nakuendelea bila kuchoka.

NKINDA:INAREFUSHA NA KUNENEPESHA MAUMBILE YA KIUME SAIZI INAYOKUBARIKA KIAFYA KUANZIA nch 3-71/2 NA UNENE CM 2-4.
(4)Itaimalisha mishipa ya uume uliolegea
(5)Inasaidia kusafisha mishipa ya kwenye uume na hivyo kuongeza kasi ya msukumo wa damu ndani yauume,na inasidia kuzarisha HORMONES ZA CETROGEN,Vile vile inazalisha kwa wingi mbegu za kiume yaani(manii)

NGUMO: Ni dawa inayotibu Kisukari kwa mda wa wiki mbili(14)tu nakuwa  nomo.

NGITO:Ni kwale waliochwa na mpenz,mke,hata kwa wewe unayetafuta mchumba majibu ni ndani ya masaa kumi na mbili(12)tu.

WASILIANA NA DR.SEMEKA 

TEL 0753-459433 -ANAPATIKANA MAGOMENI MAPIPA.

Kutana na Dr Majebele Kutoka Mwagala Ukoo wa Watemi .....Anatibu Busha, Nguvu za Kiume, Vidonda vya Tumbo, Presha

$
0
0
DR MAJEBELE KUTOKA MWAGALA UKOO WA WATEMI NI MTANZANIA HALISI.
**********************************
Anatoa tiba ya mitishamba iliyo na ubora asilia ya kienyeji.
🔖(1)Anatatua tatizo la nguvu za kiume linalowatesa wanaume wengi duniani_chanzo Cha tatizo hilo ni maelezo mafupi yafuatayo:
♦Kama uliwahi kuugua kichocho wakati yu mdogo mbeleni nguvu za kiume lazima zipungue.
♦Kama uliwahi kuwa na chango lolote nguvu za kiume lazima zipungue.
♦Vyakula vya kisasa, mafuta mengi, msongo wa mawazo, kukaa kipindi kirefu zaidi ya masaa 8,.
________________________________
📌MWAGALA 4 POWER,
NI dawa iliyochanganywa mizizi 66 .NI Bora na yenye kutoa tatizo la kutokua na  nguvu za kiume kwa kina baba pia inafanya kazi kwa haraka sana,okoa ndoa yako Sasa usitembee na aibu,kimoja kwa dakika 2 na huwez kurudia tena tiba Sasa yapatikanikal,usinywe dawa ya kuongeza nguvu kunywa dawa ya kuponyesha tatizo la nguvu miaka mingi,ni dawa ya mfumo wa   unga tu
🔸NI dozi ya siku 7🔸
Utakua umepona milele,pia unaruhusiwa kutumia kama Kinga inafanya kazi ndani ya masaa 2
MWAGALA 4 POWER Sasa ni suluhisho la nguvu za kiume.
________________________________
📌LUGOBHI na NGOLOLO ni   dawa ya kubadili maumbile yaliyosinyaa na kurefusha usilalamike uume mfupi tumia LUGOBHI utarefuka size uitakayo,tumia NGOLOLO kwa kuufanya uume uwe mnene size uitakayo dozi siku 7 
🔸mabadiliko ndani ya siku 2 ipo ktk mfumo wa unga tu.🔸
________________________________
📌UGOMOLA,
Ni mchanganyiko wa miti 8 wenye kutibu kisukari ulichosumbuka nacho kwa mda mrefu iwe ya kupanda au kushuka, dawa hii inaponesha kabisa dozi siku 18 na itakupa mabadiliko mazuri sana kabla ya siku 18,anaruhusiwa kutumia mwny umri wa miaka15_ na kuendelea.
🔸Ni mfumo wa unga tu.🔸

📌IDUNI,
Ni mchanganyiko wa miti 4 yenye kutibu presha kwa haraka sana.
🔸dozi siku 3 ina mfumo wa unga.🔸
________________________________
📌KOONYA,
Ni dawa ya mchanganyiko wa miti 10 inayotibu tezi dume kwa mda wa siku 14 haihitaji kulazwa unatumia na kuendelea kufanya mambo yako,
🔸NI mfumo wa unga tu🔸
________________________________
📌MALEMALE,
Hutibu busha bila operation na kusambaa kabisa kwa siku 20.
🔸Dawa hii IPO katika mfumo wa unga tu.🔸
________________________________
📌MWENDO WA YEGE,
Ni dawa yenye kufanikisha:
🔖Kumvuta umpendae aliyekuacha wakati bado unampenda pia
🔖Inafanya kazi kwa haraka sana.
🔸Matokeo ndani ya masaa 4,ina mfumo wa unga tu🔸
________________________________
📌KONDWAHULI,
NI dawa yenye uwezo mkubwa kuzuia CHUMAULETE, iwe:
🔖Nyumbani au katika
🔖Biashara pia
🔸Haina kikomo ni hadi milele🔸
________________________________
📌SALE,NI dawa ya kutibu miguu,kiuno magoti kuwaka Moto,
🔸Dozi siku 10, Mfumo wa unga.🔸
________________________________
📌MALELA,
NI dawa ya kutibu:
🔖Vidonda vya tumbo
🔖Tumbo kujaa gesi
🔖Minyoo tumboni
🔖Kilungulila au muungurumo tumboni.
🔸mfumo wa unga  dozi siku 5🔶
________________________________
📌SALIUNGU,NI dawa ya kuvutia wateja ktk biashara yako unayofanya..
________________________________

📌TOBO,NI dawa ya uzazi kwa akina mama waliohangaika  bila kupata watoto kwa mda mrefu,kutoa uvimbe tumboni,pia kupanga mayai yaliyo mbali na kumaliza chango lolote.dozi NI siku 12 na kupona kabisa,NI mfumo wa unga tu.
________________________________
📌NUNDANUNDA,ni dawa inayotibu kupooza/strock,msongo wa mawazo na uti wa mgongo.
________________________________
📍Kama una tatizo ambalo halijaorodheshwa hapo utanifahamisha,huduma kuanzia saa 1 asubuhi_1jioni.kama huwezi kufika nilipo nakuletea dawa mwenyewe unayohitaji..Nipo ktk mikoa miwili tu SHINYANGA &DAR ES SALAAM (kinondoni na temeke)..Piga namba
📞+255 753 928 576 (WhatsApp)
📞+255 716 608 959
----------------------------------------
For non tanzanian residents, please contact us through Whatsapp number
📞 +255 753 928 576
For the delivery of our services
______________________________
________________________________

Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Kabudi Afanya Mazungumzo Na Kamishna Wa Haki Za Binadamu Wa Umoja Wa Mataifa

$
0
0
Waziri wa Katiba na Sheria,Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi amekutana na kufanya mazungumzo na Kamishna wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Bi. Michelle Bachelet Jeria Mjini Geneva, Uswisi.

Prof. Kabudi amekutana na Kamishna wakati akihudhuria Kikao cha 40 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kinachoendelea Mjini Geneva-Uswisi.

Katika mazungumzo yao Kamishna Bachelet alitaka kujua kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu haki za binadamu nchini hususan haki za kina mama na watoto, makundi maalum na kwa jinsi gani Baraza hilo la Mataifa linaweza kuisaidia Tanzania kuendelea kukuza, kudumisha na kulinda haki za binadamu nchini.

Akizungumza katika mazungumzo hayo Prof. Kabudi alisema licha ya Serikali kuendelea na mikakati mbalimbali ya kulinda na kukuza haki za wanawake, imeendelea kutoa fursa kwa wanawake kupata nafasi za uongozi wa juu Serikalini na kwenye taasisi mbalimbali za umma ambazo zinawawezesha kushiriki katika utoaji wa maamuzi yenye manufaa kwa nchi.

Prof. Kabudi alisema Tanzania inaheshimu uhuru wa vyombo vya habari na uwepo wa vyama vya siasa na demokrasia nchini na kuongeza kuwa mwaka huu inatarajia kufanya uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambao utafuatiwa na uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka 2020.

Prof. Kabudi alimhakikishia Kamishna Bachelet kuwa Tanzania itaendelea na jitihada za kukuza, kuheshimu na kulinda haki za binadamu nchini pamoja na kutekeleza wajibu wake na ahadi zake mbele ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa.

Aidha Prof. Kabudi alielezea jitihada zinazofanwa na Serikali kwenye maeneo ya elimu, afya, mapambano dhidi ya rushwa na dawa za kulevya pamoja na malengo ya kuleta maendeleo nchini.

Prof. Kabudi alisema Serikali imeboresha mfumo wa ukusanyaji kodi na hivyo kuiwezesha Serikali kutoa huduma za kijamii kwa wananchi wake bila ubaguzi.

Mhe. Kabudi alimshukuru Kamishna Bachelet kwa ushirikiano uliopo kati ya Ofisi yake na Wizara ya Katiba na Sheria na Ubalozi wa Kudumu wa Tanzania Mjini Geneva-Uswisi na kwamba Serikali kwa ujumla itaendelea na mazungumzo kuhusu maeneo ambayo wataweza kushirikiana.

Ofisi ya Kamishna ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu iliundwa mwaka 1993 ili kusimamia ukuzaji na ulinzi wa haki za binadamu duniani. Ofisi ya Kamishna wa Haki za Binadamu pamoja na mambo mengine inazisaidia Serikali za nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kwa kutoa mafunzo na utaalamu kwenye maeneo ya upatikanaji wa haki, mabadiliko ya sheria na masuala ya uchaguzi. Vile vile inazisadia Serikali za Nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kutekeleza wajibu walionao kimataifa wa kulinda, kuheshimu na kukuza haki za binadamu.

PICHA: Lowassa Afika Nyumbani kwa Ruge Mutahaba Kutoa Pole na kuwafariji wafiwa.

$
0
0
Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa na mkewe Mama Regina Lowassa leo asubuhi wamefika nyumbani kwa Prof. Mutahaba ambaye ni baba mzazi wa Ruge Mutahaba aliyekuwa mkurugenzi wa uzalishaji vipindi wa Clouds Media Group kutoa pole na kuwafariji wafiwa.

Ruge Mutahaba Alifariki dunia Juzi nchini Afrika Kusini alikokuwa akipatiwa matibabu ya figo zilizoanza kumsumbua mwaka jana. 

Mwili  unatarajiwa kuwasili jijini Dar es salaam kutokea Afrika Kusini siku ya kesho Ijumaa, Machi 1, 2019.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Magonjwa yanayoababisha Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Ni Kama Vile, Kisukari ,presha, Ngiri Ya Kupanda Na Kushuka, Kiuno, Maumivu Ya Mgongo, Tumbo Kuuma Chini Ya Kitovu, Tumbo Kujaa Gesi. Yote Matatizo Yote Haya husababisha Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Kushindwa Kufanya Kazi Kwa Mwenza Wako  .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa Dar anapatikana mbagala Zakhem.  Songea ,bombambili, Shinyanga, Kahama ,mjini, Kwa ,maelezo, Zaidi , Piga Simu 0763172670/ 0715172670,/ ,Sema ,haloo, Dr Sitta... Wote  mnakalibishwa. 

Hatma Ya Dhamana Ya Freeman Mbowe Na Matiko Kujulikana Kesho

$
0
0
Hatima ya dhamana ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko inatarajiwa kujulikana kesho March 1, 2019 katika Mahakama ya Rufani ambapo mahakama hiyo  inatarajia kutoa uamuzi wa rufaa iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) dhidi ya Mbowe na Matiko.

Katika uamuzi huo, mahakama inatarajiwa ama kukubali Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kuendelea kusikiliza rufaa iliyokatwa na Mbowe na Matiko, kutokana na kufutiwa dhamana katika kesi ya uchochezi iliyopo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu au kuitupilia mbali rufaa hiyo.

Mapema Leo Februari 28.2019  katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kesi  ya uchochezi  inayowakabili vigogo hao na  wenzao saba wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), iliitwa kwa ajili ya kutajwa na Wakili wa Serikali, Wankyo Simon akadai kuwa bado wanasubiri hatua za rufaa zilizopo Mahakama ya Rufaa na Mahakama Kuu.

Hata hivyo, Wakili wa Utetezi, Profesa Abdallah Safari alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi kuwa ni muhimu mahakama ikapewa taarifa ya maendeleo ya rufaa zote na kwamba wao wamepata taarifa kuwa kesho  Mahakama ya Rufaa itatoa uamuzi dhidi ya rufaa hiyo

Wakili Wankyo alipoulizwa  alidai kuwa yeye bado hajapata taarifa kuhusu uamuzi huo na kwamba hata kama isingekuwa hivyo bado wanaomba tarehe ya kutajwa.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Machi 14, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.

Novemba 23, 2018 Jaji Wilbard Mashauri akiwa Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, alifuta dhamana ya Mbowe na Matiko kutokana na kukiuka masharti ya dhamana.

Wawili hao walikata rufaa katika Mahakama Kuu ya Tanzania kupinga uamuzi wa Kisutu kufuta dhamana yao ambapo rufani yao ilipangwa kwa Jaji Sam Rumanyika.

Hata hivyo, baada ya Mahakama Kuu chini ya Jaji Sam Rumanyika kusikiliza mapingamizi ya pande zote iliamua kuanza usikilizaji wa rufaa hiyo.

Upande wa serikali ukiongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Paul Kadushi ulidai kuwa wamekata rufaa katika Mahakama ya Rufani kupinga maamuzi yaliyotolewa na Mahakama Kuu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images