Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Amlilia Ruge...."Nimeelemewa, Nakosa Maneno ya Kuelezea Huzuni Niliyonayo"

0
0
Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete ameeleza maumivu aliyonayo kufuatia  kifo cha Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba.

Kupitia akaunti yake ya Instagram, Kikwete ameandika ujumbe  maneno yafuatayo:

“Nimelemewa! Nakosa maneno ya kuelezea huzuni na majonzi niliyonayo kwa kifo cha Ruge Mutahaba. 

"Taifa limepoteza kijana wake mahiri, mbunifu na mzalendo wa kweli. Nimepoteza rafiki, mshirika mwaminifu na mtu ambaye amenisaidia kwa mengi ktk uongozi wangu na hata baada ya kustaafu.

"Moyo wangu uko pamoja na wazazi wake, ndugu zake na familia yake katika kipindi hiki kigumu. Namuombea kwa Mola ampe Mapumziko Mema Peponi. Ameen. "

Chama cha Mapinduzi (CCM) Chatoa Salamu za Pole Kufuatia Kifo cha Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba

FIFA Yamfungia Maisha Mwamuzi Wa Tanzania Kwa Rushwa Na Upangaji Matokeo

0
0
Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) chini ya Mwenyekiti wake Vassilios Skouris imemfungia maisha Mwamuzi wa zamani wa Kimataifa na Katibu wa Chama Cha Waamuzi Tanzania (FRAT) Oden Charles Mbaga kwa kujihusisha na masuala ya rushwa ya upangaji matokeo.
 
Baada ya uchunguzi uliofanyika kuanzia July 11,2018 Mbaga amekutwa na hatia ya kuhusika kwenye upangaji wa matokeo ikiwa ni kinyume na kanuni za Maadili za FIFA.
 
Mbaga amevunja Ibara ya 11 ya Kanuni ya rushwa ya FIFA ya mwaka 2009.
 
Anafungiwa maisha kutojihusisha na shughuli zozote za Mpira wa Miguu katika ngazi ya Kitaifa na Kimataifa kwa mujibu wa Ibara ya 7j ya Kanuni za Maadili za FIFA za mwaka 2018 pamoja na Ibara ya 22 ya Kanuni ya Nidhamu ya FIFA.
 
Aidha Mbaga anatakiwa kulipa faini ya kiasi cha fedha ya Uswis Faranga 200,000 ndani ya siku 30 tokea amepata taarifa hizo na anaweza kulipa kwa fedha ya Swiss au kwa dola za Kimarekani.
 
Vilevile Mbaga anatakiwa kulipa gharama za shauri hilo kiasi cha Faranga za KiSwiss 1,000 ndani ya siku 30 tokea amepata taarifa.
 
Anaweza kukata rufaa kwenye mahakama ya kimichezo ya FIFA CAS,rufaa ambayo inawasilishwa moja kwa moja CAS ndani ya siku 21 tokea maamuzi yalipofanyika na ndani ya siku 10 baada ya kumalizika siku 21.
 
Mbaga ambaye ni Katibu wa Chama cha Waamuzi Tanzania (FRAT) anapoteza sifa ya nafasi hiyo kutokana na adhabu ya kufungiwa maisha kutojihusisha na masuala ya Mpira wa Miguu.

Mwili Uliokaa Mochwari Miezi 8 Wazikwa Mbeya

0
0
Mwili wa Kijana Frank Kapange (22) aliyefariki zaidi ya miezi nane  na siku 26 na kuhifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya, umechukuliwa na ndugu  kwenda kuzikwa katika kijiji cha Syukula katika Wilaya ya Rungwe  mkoani Mbeya  baada Mahakama kuamuru mwili huo kuzikwa.
 
Akizungumza  hospitalini hapo, Msemaji wa Familia, Julius Kapange amesema kupitia mahakama mbalimbali mkoani Mbeya  waliomba mwili ufanyiwe uchunguzi ili kujua sababu za kifo cha kijana wao  ambaye anadaiwa kufariki  kwenye mazingira ya kutatanisha lakini  waliamuriwa kuuzika mwili huo ndani ya wiki moja vinginevyo Halmashauri ya Jiji ingezika.

Shangazi wa marehemu Sophia Kapange amesema hawakususia mwili bali walitaka kujua sababu za kifo cha mtoto wao ndiyo maana walikuwa wakifuatilia mahakamani ili haki itendeke lakini imekua tofauti na matarajio yao huku  Mama mzazi wa marehemu akidai  kifo cha mwanae kimekuwa pigo kwake kwani  alikuwa akiendesha familia kwa kufanya biashara ndogo ndogo katika Soko la Sido.

Hata hivyo Mkurugenzi wa Hospitali hiyo Godlove Mbwanji amesema wameamua kusamehe gharama zote za  kutunzia mwili wa marehemu  ili fedha ambazo waliziandaa zikatumike kwenye msiba.

Frank alifariki Juni 4, 2018 huku kifo chake kikigubikwa na utata kutokana na mazingira yake baada ya ndugu kudai kijana wao ambaye alikuwa ni mfanyabiashara wa nguo za mitumba soko la Sido jijini Mbeya alifariki kwa kipigo akiwa mikononi mwa polisi hivyo ndugu waligoma kumchukua na kwenda kumzika.

Leseni Za Migodi Mikubwa Kuanza Kutolewa Nchini Hivi Karibuni

0
0

Na Asteria Muhozya, Dodoma
Serikali kupitia Wizara ya Madini inakamilisha taratibu za utoaji wa Leseni kwa Migodi Mikubwa ambazo hazijawahi kutolewa nchini, huku migodi hiyo ikitarajiwa kuanzishwa hivi karibuni.
 
Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila alipokutana na viongozi wa Jumuiya ya Watendaji Wakuu wa Taasisi Binafsi ofisini kwake, jijini Dodoma.
 
Viongozi hao walikutana na Prof. Msanjila Februari 26, kwa lengo la kujitambulisha, kuelewa shughuli za serikali upande wa sekta ya madini, kupata uelewa kuhusu mabadiliko ya Sheria ya Madini na namna pande hizo mbili zinavyoweza kushirikiana katika kuendeleza sekta husika.
 
Prof. Msanjila aliwakaribisha viongozi hao kwenye sekta ya madini huku akiwataka kuzishawishi kampuni mbalimbali kuwekeza nchini hususani katika shughuli za uongezaji thamani madini na kueleza kuwa, suala hilo ni miongoni mwa maeneo ambayo serikali inayapa kipaumbele ikiwemo ujenzi wa vinu vya kusafisha na kuyeyusha madini.
 
Akizungumzia Sheria Mpya ya Madini ya Mwaka 2017, Prof. Msanjila amesema hakuna tatizo lolote katika utekelezaji wa sheria na kueleza kuwa, serikali kupitia wizara ya madini inapokea wawekezaji wengi wenye utayari na nia ya kuwekeza nchini huku utekelezaji wa sheria hiyo ukiwa si kikwazo na kuongeza kwamba, “hakuna mahali ambapo serikali inatengeneza sheria kwa ajili ya kumkandamiza mfanya biashara”. 
 
“Hakuna tatizo lolote kwenye sheria ya madini. Hata wageni huwa tunakaa nao tunawaelimisha na wanatuelewa vizuri.  Kama kuna dosari ni vitu ambavyo tunaweza kuvirekebisha na tayari tumekwishakufanya hivyo kwa baadhi ya maeneo,” alisema Prof. Msanjila.
 
Aidha, katika kikao hicho Prof. Msanjila alitoa ushauri kwa viongozi hao kujitangaza zaidi kuhusu kazi zao huku akiwataka kutafuta wasaa kwa ajili ya pande hizo mbili kukutana ili wizara iweze kutoa elimu zaidi kwa Jumuiya hiyo kuhusu sekta ya madini ikiwemo fursa za uwekezaji zilizopo.
 
Pia, Prof. Msanjila alisema kuwa suala la kuaminiana linaweza kujengwa huku akiwataka watanzania kuwa wazalendo na namna wanavyotumia fedha za umma. Prof. Msanjila alizungumzia jambo hilo baada ya mmoja wa viongozi hao kueleza kuwa, bado kuna hali ya kutokuaminiana baina ya serikali na taasisi binafsi.
 
Kwa upande wake, mmoja wa viongozi wa jumuiya hiyo, Francis Nanai ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited amemweleza Prof. Msanjila kuwa, kama viongozi wa umoja huo, wamezipokea changamoto zilizotolewa kwao na Prof. Msanjila ikiwemo ushauri wa kukutana na wizara kwa lengo la kupata ufafanuzi na elimu  zaidi  kuhusu sekta ya madini.

Kifo cha Ruge Mutahaba: Familia Yaelezea kilichojiri dakika zake za mwisho

0
0
Familia ya Marehemu Ruge Mutahaba ambaye amefariki dunia hapo Jana nchini Afrika Kusini, imeweka wazi kilichotokea mpaka Ruge akakutwa na mauti, akiwa hospitali akiendelea na matibabu ya figo ambayo ilikuwa ikimsumbua,

Mombeki Barego ambaye ni ndugu wa Ruge Mutahaba amesema kwamba jana asubuhi Ruge aliamka huku presha yake ikiwa haiko sawa, lakini licha ya madaktari kufanya jitihada zao ili kumuweka sawa, ilishindikana na kusababisha kupoteza maisha.

“Asubuhi leo (jana) ndugu yetu Ruge Mutahaba, aliamka katika hali ambayo presha yake ilikuwa haijatulia, madaktari na wasaidizi wengine wa hospitali walijaribu kumsaidia, lakini mnamo saa 10:30 Jioni kwa saa za South Afrika au saa 11:30 kwa muda wa hapa nyumbani, ndugu yetu Ruge Mutahaba, alifariki akiwa na mdogo wake na watu wa dini ambao walikuwepo naye”,amesema Mombeki.

Mombeki ameendelea kwa kusema kwamba utaratibu wa kurudisha mwili wa marehemu unaanza kufanyika, huku akiwashukuru watu waliojitokeza kuifariji familia yao.

“Na kwa sasa familia inashukuru watu amabo wamefika hapa kutufariji kwa muda mfupi, na utaratibu wa kuangalia namna ya kumrudisha ndugu yetu nyumbani kwa ajili ya mazishi ndio zinaanza, kesho (leo) tutakuwa tunafahamu zaidi kuhusu huo utaratibu na kuweza kutoa taarifa rasmi ya utaratibu na mazishi”, amesema Mombeki.

Ruge Mutahaba alikuwa mmoja wa waasisi wa Clouds Media Group na mmoja ya watu aliochangia kukuza sanaa ya bongo kwa kuibua wasanii mbali mbali, na atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa kwenye maisha ya vijana wengi.

Ruge alianza kusumbuliwa na tatizo la figo mwishoni mwaka 2018 ambapo alilazwa katika hospitali ya Kairuki, na baadaye kuhamishiwa nchini Afrika Kusini ili kupata matibabu zaidi, mpaka kifo kilipomkuta Februari 26, 2019.

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Bima ya Taifa (NHIF) Watakiwa kutochelewesha Kadi za Wanachama

0
0
Na WAMJW – MTWARA
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ameuagiza uongozi wa  wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kutatua changamoto ya uchelewaji wa vitambulisho vya bima ya afya kwa wananchi.

Ameyasema hayo mapema leo wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utendaji kazi wa mfuko huo Mkoa wa Mtwara, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya Mkoani hapo.

DKt. Ndugulile amesema kuwa NHIF ni lazima ihakikishe inawahudumia vizuri wananchi wanaokuja kujiunga katika mfuko huo, ikiwemo kuhakikisha ndani ya wiki mbili baada ya kujaza fomu, wateja wapate kadi zao.

“Tuendelee kuwahudumia vizuri, na kuhakikisha kwamba, ndani ya wiki mbili baada ya kujaza fomu na kukamilisha taratibu, waweze kupata kadi zao” alisema DKt. Ndugulile

Pia, Dkt. Ndugulile amesema Serikali imeridhishwa kwa kiasi kikubwa na mwitikio mzuri wa wananchi kujiunga na Bima ya Ushirika jambo litalowasaidia kupata huduma za afya katika vituo takribani 6,000 nchi nzima.

Aidha, Dkt. Ndugulile ameagiza NHIF kuweka utaratibu wa kuwafuata na kuwapatia kadi za bima wateja waliojiandikisha ili kuweka hamasa kwa wananchi wengine kujiunga na bima ya afya na kuwapunguzia usumbufu.

Mbali ya hayo DKt. Ndugulile ametoa onyo kwa watoa huduma za afya wanaofanya udanganyifu, na kuwataka watoe huduma kwa kufata sheria, na kwa mujibu wa miongozo ya Wizara ya Afya,

DKt. Ndugulile aliendelea kusema kuwa Serikali ipo katika hatua za mwisho za maboresho ya sheria ambazo zitatoa adhabu kali kwa yeyote atakayehusika na udanganyifu wowote utaopelekea hasara kwa Serikali.

Kwa upande mwingine DKt. Ndugulile amewaagiza watoa huduma za afya kuhakikisha wanawasilisha madai yao kwa NHIF kwa wakati, huku akisisitiza kuwa NHIF nayo inapaswa kulipa madeni kwa wakati.

“Haipendezi wananchi wanahudumiwa katika vituo vyetu vya kutolea huduma za Afya, na madai yanakaa zaidi ya miezi miwili au mitatu, kwahiyo niombe watoa huduma waharakishe madai yao, ili waweze kulipwa kwa wakati” alisema DKt. Ndugulile.

Nae Mkulima wa Korosho kutoka Halmashauri ya Nanyamba kijiji cha Nyundo, amewataka wakulima kupitia vyama vya Ushirika wajiunge na Bima ya Afya ili kuepuka gharama kubwa za matibabu na ugonjwa hauchagui muda wa kuja.

“Nimehamasika kujiunga na bima ya afya baada ya kuelewa kwamba ukulima una muda wa kupata pesa na una muda wa kukosa, alafu homa haichagui muda,” alisema Bw. Said Akili.

Aidha Bw. Said Akili ameiomba Serikali kuendelea kuboresha utoaji wa huduma za afya hasa kwa Wateja wanaotumia kadi za Bima ya Afya, jambo litalo wahamasisha wakulima wengi zaidi kujiunga na mfuko huo.

Waziri wa Kilimo: Asilimia 60 ya wanafunzi wanaohitimu vyuo vikuu nchini sio wazalishaji

0
0
Asilimia 60 ya wanafunzi wanaohitimu vyuo vikuu wanakuwa sio wazalishaji  kutokana na kusubiri ajira mbalimbali katika Serikali, Mashirika na taasisi mbalimbali  huku wakiacha kilimo ambacho ndiyo chenye ajira kubwa na ya moja kwa moja huku wakiacha  Kilimo Biashara ambacho ndiyo suluhisho la ajira kwa vijana nchini.

Hayo ameyasema Waziri wa Kilimo Mh.  Japhet Hasunga wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusiana na Kongamano la vijana  Kimataifa kuhusu Kilimo Biashara (Youth Agro Summit International) litakalofanyika Machi 20 hadi 22 katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.


Serikali imesema kuwa katika kuelekea uchumi wa viwanda tunahitajika kuwekeza nguvu kwa vijana kuingia katika Sekta ya Kilimo na kuacha kuzunguka na bahasha ya kaki ya kuomba ajira sehemu mbalimbali katika mashirika na taasisi nchini.


“Vijana wakiingia katika Kilimo suala la kutembea na bahasha kwa ajili ya kutafuta ajira  litakuwa historia kwani kijana kuendesha Kilimo  hakuhitaji watu wa kufanya usaili”amesema Hasunga.

Hasunga amesema kuwa serikali imedhamiria kuweka mazingira ya Kilimo kwenda kisasa kwa kuhakikisha masoko ndani yanakuwa nafasi na ziada kuuza nje ya nchi.

Aidha amesema Kilimo kimekuewa kikilimwa kwa mazoea na kufanya kilimo kuonekana kigumu lakini serikali ya awamu ya tano tunakwenda na Kilimo cha kisasa kwa kuhusianisha masoko pamoja na viwanda kwa kwa ajili ya kuongeza thamani ya mazao.

Hasunga amesema nchi yeyote duniani inategemea vijana katika kupata Maendeleo  hivyo serikali haitawaacha nyuma vijana katika sekta ya Kilimo na biashara.

Amewataka  vijana  kuwa na mwamko wa elimu huku wengine wakiwa wataalam katika fani mbalimbali jambo ambalo  litawatafanya kuwa chachu ya Kilimo na biashara  na kufanya vijana  waliokata tamaa kuingia katika sekta hiyo.

Amesema takwimu zinaonyesha asilimia 53 ndio wanatumia jembe la mkono katika kilimo huku asilimia 27 wakitumia wanyama katika kuendesha katika kuendesha kilimo chao wakati  takwimu zinaonyesha  asilimia 20 wanatumia trekta .

Nae Mwenyekiti wa Kongamano la Vijana Kimataifa Kuhusu Kilimo Biashara Majabi Emmanuel amesema kuwa  wanatarajia kuwa na washiriki 1000  kutoka sehemu mbambali wa ndani na nje ya nchi.

Amesema kuwa wameandaa Kongamano hilo kutokana na vijana kujitenga katika kilimo wakati ndio chenye fursa ya kujiajiri moja kwa moja.

Afisa Utumishi Mkuranga Aonywa Kutumia Cheo Chake Vibaya Kuomba Rushwa Ya Ngono Kwa Watendaji Wa Vijiji

0
0
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) amemuonya Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, Bw. Valintine Mbai ambaye ni Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu wa Halmashauri hiyo kuacha tabia mbaya  ya kutumia cheo chake kuomba rushwa ya ngono kwa Watendaji wa Vijiji katika Halmashauri hiyo na kumtaka afisa huyo kubadili mwenendo wake haraka iwezekanavyo.

Onyo hilo amelitoa wilayani Mkuranga, wakati wa kikao kazi na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji, kabla ya kuanza kutembelea wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika halmashauri hiyo ili kujiridhisha na utekelezaji wake.

Akizungumza na watumishi hao, Mhe. Dkt. Mwanjelwa amesema, ni aibu kwa afisa huyo mwenye dhamana ya kusimamia maadili ya kiutumishi kutumia madaraka yake vibaya kwa kuomba rushwa ya ngono toka kwa Watendaji wa Vijiji jambo ambalo ni kinyume cha maadili ya kiutendaji katika utumishi wa umma.

Amemtaka afisa huyo kuacha tabia hiyo na kujirekebisha maramoja ili awe mfano bora kwa watumishi anaowasimamia kimaadili.

Pi amemtaka, afisa huyo kuwa na heshima kwa wakuu wake wa kazi akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo ili kutengeneza mazingira mazuri ya kiutendaji.

Aidha, Mhe. Dkt. Mwanjelwa ametoa angalizo kwa Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Mhe. Juma Abeid kutowatetea watumishi wasio waadilifu na badala yake awachukulie hatua za kinidhamu hata kama ni marafiki zake.

Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) ameendelea kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma nchini akiwa wilayani Mkuranga na kutoa wito kwa watumishi wote wa umma kuhakikisha wazingatia Kanuni za Maadili ya Utendaji Kazi katika Utumishi wa Umma.

Serikali Yasema Itaendelea Kulinda na Kukuza Haki za Binadamu

0
0
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi amesema Serikali ya Awamu ya Tano itaendelea kutekeleza wajibu wake wa kukuza na kulinda haki za binadamu na ustawi wa jamii kama kipaumbele chake na  itaendelea kushirikiana na Baraza hilo kuhakikisha haki za binadamu nchini na duniani kote zinadumishwa.

Prof. Kabudi amesema hayo alipolihutubia Kikao cha 40 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kinachofanyika jijini Geneva nchini Uswisi.

Prof. Kabudi amesema Serikali ya Tanzania imelenga pamoja na mambo mengine kuimarisha haki za binadamu, utawala bora na utii wa sheria nchini na kuondoa ukatili dhidi ya wanawake, watoto na watu wenye ulemavu.

“Serikali imelenga kuimarisha haki za binadamu, utawala bora, utii wa sheria na kuondoa ukatili dhidi ya wanawake, watoto na watu wenye ulemavu, kwa sasa tunatekeleza mpango mkakati wa kitaifa wa kuondoa ukatili dhidi ya wanawake na watoto wa mwaka 2017/18 – 2021/22, lengo likiwa ni kulinda na kudumisha haki za wanawake, watoto na watu wenye ulemavu,” alisema Prof. Kabudi.

Amesema Serikali pia inazingatia suala la kuwapatia haki kwa haraka wananchi wasio na uwezo kwa kutolea maamuzi kwa haraka mashauri yanayowahusu watu wasio na uwezo na kuwapatia msaada wa kisheria kupitia utekelezaji wa Sheria ya Msaada wa Kisheria ya mwaka 2017 ili wananchi hao waweze kupata haki zao kwa wakati.

Aidha, Prof. Kabudi amelihakikishia Baraza hilo kuwa Serikali inatambua kazi kubwa inayofanywa na vyombo vya habari nchini na imeendelea kuhakikisha uhuru wa vyombo hivyo unalindwa huku jumla ya vituo vya redio 152, televisheni 34, magazeti 172  nchini kote yamesajiliwa na kuongeza kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira stahiki yatakayowezesha vyombo vya habari kufanya kazi zao kwa uhuru.

Ameongeza kuwa Serikali imedhamiria kuleta ustawi wa jamii kwa kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo ikiongozwa na Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025 na kunadi kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuhakikisha kuwa haki ya kupata elimu, afya na maji zinawafikia wananchi wote.

“Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuhakikisha kuwa haki ya kupata elimu, afya na maji zinawafikia wananchi wote na kuongeza kuwa Serikali inatumia zaidi ya Shilingi Bilioni 23 kwa mwezi kutoa elimu pasipo malipo na hivyo kuongeza udahili wa watoto wanaojiunga darasa la kwanza kwa asilimia 35.2 na asilimia 20.1 kwa wanaojiunga na kidato cha kwanza,” alisema.

Prof. Kabudi pia amesema Serikali imedhamiria kufikisha huduma za afya karibu na watanzania wote ambapo imeongeza bajeti ya afya kutoka Shilingi bilioni 31 mwaka 2015/2016 hadi Shilingi bilioni 269 mwaka 2017/2018 na kuongeza kuwa Serikali inatekeleza mikakati ya kujenga vituo vya afya ambapo hadi sasa imejenga vituo 304, na nyumba za watumishi wa afya 578 zimejengwa nchini kote.

Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa ni chombo cha Umoja wa Mataifa chenye jukumu la kukuza na kulinda haki za binadamu duniani kote na kushughulikia uvunjwaji wa haki za binadamu unaotokea katika nchi wanachama wa umoja huo na kushauri hatua za kuchukuliwa ili kuboresha haki za binadamu duniani.

Baraza hilo pamoja na mambo mengine linatarajia kupokea taarifa mbalimbali kuhusu haki za binadamu duniani na kutoa nafasi kwa viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kutoa maelezo yao kuhusu utekeelezaji wa wajibu wao wa kulinda na kukuza haki za biandamu katika nchi zao.

Serikali Yashikilia Msimamo wake Kuhusu Mgodi wa North Mara

0
0
Na Issa Mtuwa, Dodoma
Serikali kupitia Wizara ya Madini imesema bado imeshikilia msimamo wake kuhusu muda uliotolewa kwa Mgodi wa North Mara kutekeleza maagizo ya serikali yaliyotolewa kwenye kikao cha Januari 9, 2019 kuhusu Bwawa la kuhifadhi topesumu (Tailings Storage Facility -TSF).  

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila Februari 26, 2019 wakati akizungumza katika mahojiano maalum ofisini kwake Jijini Dodoma, mara baada ya kufungua kikao cha pamoja baina ya wajumbe kutoka serikalini na wajumbe kutoka Mgodi wa North Mara waliokutana kujadili kuhusu hatua zilizofikwa na Mgodi katika kutekeleza maagizo hayo. 

Amesema serikali haitoongeza muda zaidi ya ule uliotolewa katika kikao cha awali, na kusema kuwa msimamo wa serikali utabaki kuwa hivyo. 

 “Ndugu zangu katika kikao hiki kilenge kutoa majibu ya utekelezaji wa maagizo ya serikali kama yalivyowasilishwa kwenye kikao cha Januari 9, 2019, ni kwa kiasi gani mmetekeleza maagizo hayo,” alisema Prof. Msanjila. 

Serikali kupitia kikao chake cha Januari 9, 2019 chini ya Makatibu Wakuu wa wizara saba (Madini, Makamu wa Rais Mazingira (NEMC), Ardhi, TAMISEMI, Afya, Fedha na Maji) kilitoa maagizo mbalimbali yakiwemo: Kujenga TFS mpya na Kukarabati TFS iliyopo kwa aajili ya kudhibiti mtiririko wa topesumu, maagizo ambayo mgodi ulipewa kuyatekeleza kwa muda wa miezi Nane (8) kuanzia Januari 9, 2019. 

Akiongoza wakati wa mjadala wa uwasilishaji wa mada mbalimbali wa kikao hicho, chini ya Mwenyekiti wa kikao hicho Prof. Hudson Nkotaga aliwataka North Mara kueleza namna gani wametekeleza maagizo ya serikali kwa lengo la kupata mrejesho wa utekelezaji. 

Kuhusu utekelezaji wa maagizo hayo, Meneja Usalama, Afya na Mazingira Reuben Ngusaru, kutoka mgodi wa North Mara amesema mgodi umeanza kutekeleza maagizo hayo na bado wanaendelea kutekeleza maagizo hayo na hata kikao cha tarehe 26 Februari ikiwa ni moja mkakati wa kutekeleza maagizo hayo kwa ufanisi.  

Akizungumzia kuhusu hatua zilizochukuliwa na mgodi kudhibiti uvujaji unaoendelea kwenye (TSF) mpaka kufikia siku ya kikao cha Februari 26, mambo yaliyotekelezwa ni pamoja na: Kuondoa mawe na kusafisha mtaro uliopo upande wa Kaskazini mwa TSF. Kuvukiza (evaporation) maji yaliyotokana na uchenjuaji wa mawe yanayotengeneza tindikali asili (PAF Rock) (leachate water) badala ya kuyapeleka yote kwenye TSF na Programu zote zilizokuwepo za kupunguza maji katika TSF bado zinaendelea.

Aidha, kuhusu utekelezaji uliofikiwa katika kutekeleza agizo la Serikali la kujenga TSF mpya (Construction of a new TSF) Reuben amesema mpaka kufika tarehe 26 Februari, mgodi umefanya utambuzi wa eneo linalofaa kwa ajili ya ujenzi wa TSF mpya (Site Identification) nau sanifu wa awali (Conceptual design) ambapo usanifu wa awali umefanyika na ujenzi wa TSF mpya unatarajiwa kuwa na uwezo wa kuhifadhi tani milioni 45 za tope sumu (tailings) kavu kwa kadirio la ongezeko la tani 8200 kwa siku. 

Maagizo ya serikali kwa mgodi wa North Mara yalitokana na ukaguzi uliofanywa na serikali kwenye mgodi huo uliohusisha timu kutoka ofisi mbalimbali za serikali zikiwemo, NEMC, Mkemia Mkuu wa Serikali, Wizara ya Madini, na Wizara ya Afya, uliopelekea kutolewa kwa maagizo yaliyolenga kudhibiti uharibifu wa mazingira uliokuwa unafanywa na mgodi.

Maziri Mwakyembee Aagiza Msanii Dudubaya Akamatwe kwa Kosa la Kumdhihaki Marehemu Ruge Mutahaba

0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe amelitaka Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) kumchukulia hatua msanii Tumaini Godfrey  maarufu ‘Dudu Baya’ ambaye amekuwa akimdhihaki Ruge Mutahaba kabla na baada ya kifo chake.

Katika taarifa ya Wizara hiyo iliyotolewa leo Februari 26,2019 imesema: ’Waziri Mwakyembe ameelekeza Basata kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi  nchini kumchukulia hatua msanii Dudu Baya kwa kumdhihaki marehemu,”.

Kwa nyakati tofauti, Dudu Baya kupitia mtandao wa Instagram amekuwa akimdhihaki Ruge akidai amekuwa akiwadhulumu wasanii na kumuombea afe na hata baada ya msiba wake ameendelea kufanya hivyo huku akiahidi kulipua bomu lingine linalomuhusu leo mchana.



Serikali Kuendelea Kusimamia Maadili ya Askari Polisi

0
0
Serikali imesema haitakua tayari kuona Jeshi la Polisi linachafuliwa na baadhi ya Askari Polisi wasiofuta maadili huku ikisisitiza haitosita kumchukulia hatua askari atakaebanika kukiuka maadili

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni wakati akifunga mafunzo kwa Vikundi vya Ulinzi Shirikishi Visiwani Zanzibar ambapo jumla wa walinzi 681 walihitimu mafunzo hayo

Akizungumza na wahitimu pamoja na askari katika hafla hiyo Naibu Waziri Masauni alisema Serikali inatambua kazi nzuri inayofanywa na askari polisi waadilifu huku akiweka wazi kuwepo kwa askari wasio waadilifu

“Jeshi letu la Polisi lina miiko yake katika utendaji wa kazi zake,lakini wapo askari wachache wanaovujisha taarifa kwa wahalifu, wanasaidia wahalifu kutenda makosa sambamba na kupokea rushwa,hali hiyo haikubaliki na atakebainika hatutosita kumchukukia hatua kwa mujibu wa taratibu za jeshi,” alisema Masauni

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo Kaimu Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Saleh Mohamed Saleh, aliwataka wananchi kufichua wahalifu wanaowafahamu katika makazi yao ili matendo ya uhalifu yaweze kupungua

“Polisi Jamii ni dhana pana,tunawategemea wananchi mtusaidie kufichua wahalifu katika maeneo mnayoishi maana uhalifu ukifanyika nyie ndio mnaathirika hivyo basi ni bora mkawa mabalozi wazuri katika maeneo yenu kwa kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi,” alisema Kamishna Saleh

Katika mafunzo hayo jumla ya Walinzi Shirikishi 681 walihitimu ambapo walipitishwa katika maeneo mbalimbali ikiwemo ukamataji salama,namna ya kuendesha doria,jinsi ya kumfikisha mtuhumiwa kituo cha polisi na elimu jinsi ya kujikinga na vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia kwa watoto.

Mwili wa Ruge Kuwasili Nchini Ijumaa ya March 1, 2019

0
0
Mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa vipindi na uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba unatarajiwa kuwasili nchini  Ijumaa ya  Machi 1,2019 na utazikwa Bukoba, mkoani Kagera wiki ijayo.

Annik Kashasha ambaye ni msemaji wa Familia ya Mutahaba amesema Leo Jumatano February 27 kuwa  kama mambo yakienda kama yalivyopangwa,  wakazi wa Dar es Salaam watatoa heshima za mwisho na kumuaga Ruge siku ya Jumamosi,March 2.

Baada ya hapo Familia imeamua kwamba Ruge atakwenda kuzikwa nyumbani kwao huko Bukoba siku ya Jumatatu ya March 4, 2019.

Waziri Mkuu: Ruge Alikuwa Tayari Kusaidia Vijana

0
0
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema Taifa limepoteza kijana aliyekuwa msatari wa mbele kuwahamasisha vijana wajitambue wawe wazalendo kwa nchi yao na watambue fursa za maendeleo zilizopo na wasiwe walalamikaji.

Ameyasema hayo leo (Jumatano, Februari 27, alipokwenda kuhani msiba wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba kwa niaba ya Serikali, nyumbani kwa wazazi wa marehemu Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu amesema vijana nchini walikuwa na kiongozi aliyekuwa akiwaongoza kwa kuwafungua kimawazo na kuwaonesha fursa mbalimbali zitakazowawezesha kuwakwamua kifikra na kiuchumi ili waweze kujitegemea.

Waziri Mkuu amesema msiba huo ni wa wote kwani marehemu amefanya kazi kubwa ya kushirikiana na Serikali kuhamasisha vijana kujitambua na kutambua fursa zilizpo na kuzifanyia kazi. “Ruge ametoa mchango mkubwa kwa Taifa

Amesema marehemu Ruge katika kipindi cha uhai wake amefanya kazi kubwa kwa upande wa Serikali, kuanzia awamu ya nne hadi ya tano hususani katika suala la kuhamasisha vijana kujikwamua na kutokuwa wategemezi.

Pia, Waziri Mkuu amesema historia yake inaeleza namna alivyozunguka nchi nzima na kukutana na makundi ya vijana mbalimbali na kuwaelimisha namna ya kutambua fursa zilizopo nchini huku akiwahamasisha wawe wazalendo.

"Marehemu alikuwa akitoa hadi fedha zake binafsi kwa ajili ya kuwawezesha vijana hasa wale ambao hawakuwa na uwezo wa kiuchumi ili nao washiriki katika shughuli mbalimbali za ujasiriamali na hatimaye waondokane na utegemezi.”

Kadhalika, Waziri Mkuu ametoa wito kwa wazazi, watoto wa marehemu pamoja na wananchi kwa ujumla waendelee kuwa na subira na watulivu katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wao.

 (mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATANO, FEBRUARI 27, 2019.

Waziri Makamba Aandika Waraka Mzito....."Ruge, naomba nisikilize kidogo. "

0
0
Na January Makamba
Ndugu yangu Ruge, najua ndio umewasili huko upande wa pili na si ajabu una mambo mengi na bado unasalimiana na jamaa zetu wengi waliotangulia.

Lakini naomba uchukue muda wako kidogo kunisikiliza. Nimeumia sana na nimelia peke yangu kwamba umetuacha namna hii. Sawa, umeitwa kwa wakati wako na sisi hatuna kauli kwenye suala la wakati wa kuitwa lakini nilitegemea, na sikuwa na shaka kabisa, kwamba tutakamilisha yale mawazo yako mengi mazuri uliyoniambia. Sikuwa na shaka kwasababu nilishuhudia pale Hospitali ya Kairuki kabla hujaenda India, ulivyorudi kutoka India, na siku nimekuona Afrika Kusini, ulivyokuwa unapigana kupona — hadi madaktari wa Afrika Kusini wakakupa jina “Ruge, The Fighter”. Jina sahihi kabisa lililotafsiri harakati za maisha yako.

Unajua nini? Nilikuwa nangoja urudi Dar nikwambie nilichogundua mara ya mwisho nilivyokuona hospitali. Lakini ngoja tu nikwambie kabla sijaja huko uliko. Ile kiu kubwa ya kupona niliyoiona kwenye macho yako haikuwa kwa ajili yako wewe, bali kwa ajili ya kutoiangusha familia yako nzima iliyosimamisha kila kitu kukuuguza na Watanzania wote waliokuwa wanakuombea. Ulipigana kupona, sio kwa ajili yako, bali kwa ajili yetu. Hukuamka kitandani lakini hukushindwa mapambano kwasababu umeamkia ndani ya mioyo ya Watanzania. Huku tuliko karibu watu wote tunakumbuka ulivyotugusa. Jamaa yangu, tunakuomboleza wakati huu, halafu tutabaki tunafurahia nuru yako katika maisha ya wengi kwa urefu wa uhai wetu. Umekimbia mbio njema, umemaliza safari yako vyema.

Majonzi yangu ni kwamba umeondoka kabla sijalipa kwa ukamilifu deni langu kwako. Deni la upendo na urafiki wa kweli. Ulinipa heshima kubwa ya kuwa msiri wako — kwa kuniamini na kunielezea wasiwasi wako, ndoto zako, matumaini yako, harakati zako, mipango yako. Ulinipa heshima ya kunipa fursa ya kubishana nawe kuhusu mawazo na fikra zako.

Majonzi yangu ni kwamba kuna vitu fulani vikubwa na vizuri tulivipanga — mimi na marafiki na wadogo zako, kwa ajili yako, kwa staili yako — mapema mwezi Machi, ambavyo naamini vingekupa tabasamu. Kama unaweza, hapo ulipolala, tupe ishara tufanyeje.

Nafarijika kidogo kwamba nilipata nafasi ya kukukumbatia kwa mara ya mwisho. Sikujua kwamba tunaagana. Ulinishika mkono kwa nguvu, hukutaka kuuachia, na ulitabasamu niliposema nakungoja Dar tukae pale THT, kama kawaida yetu, kujadili mawazo na mipango yako mingi.

Ingawa umeshawasili huko upande wa pili, familia yako na watu wengi watauaga mwili wako kwa heshima kubwa. Utajengewa kaburi. Nadhani litawekwa marumaru. Lakini tukitaka kukusalimia tena hatutakutafuta kaburini kwako. Tutakutafuta kwenye nyoyo za watu uliowagusa na kuwasaidia. Na ni wengi kweli. Kumbukumbu yako itabaki kwenye nyoyo zao na kwenye mafanikio yao. Watoto wako hawapo peke yao. Watalia sana, lakini ni kwa muda tu; kwasababu watafunikwa kwa upendo wetu sote na watafarijika, na watakuwa na fahari, kwa jinsi unavyosemwa na unavyokumbukwa.

Ndugu yangu, nisikuchoshe. Mengine tutaongea tutakapokutana tena kwasababu kwa hakika sisi sote, mmoja mmoja na kwa wakati wetu, kwa kadri ya mipango ya yeye aliyetuumba, tutakufuata huko. Miaka yote nimekujua, sijawahi kukuona umepumzika. Pumzika kwa amani kwa sasa — na milele.

Ndimi, rafiki yako,
January Makamba
27 Februari 2019

Watu 7 Wafikishwa Mahakamani Mauaji ya Watoto Njombe

0
0
Na Amiri kilagalila Njombe
Watu saba wamefikishwa mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Njombe  kwa tuhuma za mauaji ya watoto mkoani Njombe yanayohusishwa na imani za kishirikina.

Mmoja wa watuhumiwa hao ni David Kasila ambaye alifikishwa kwa mara ya kwanza mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Njombe februari 18 mwaka huu akituhumiwa kuwaua watoto watatu ambao ni Oliver Ng’ahala(5),Goodluck Mfugale(5)Meshack Myonga(4) wote ni wakazi wa wilaya ya Njombe.

Watuhumiwa wengine ni Mariano Malekela,Edwini Malekela,kalistus Costa wakazi kijiji cha Matembwe tarafa ya Lupembe walifikishwa mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Njombe mnamo februari 19 mwaka huu kwa tuhuma za kumuua mtoto wao Rachel Malekela(7) februari moja mwaka huu ambapo mwili wake ulikutwa mita 50 kutoka nyumbani kwao akiwa amechinjwa.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana kamanda wa polisi Mkoa wa Njombe Renata Mzinga,alisema kati ya watuhumiwa 49 waliokuwa wakishikiliwa na jeshi la polisi baada upelelezi watuhumiwa saba pekee ndio walikutwa na hatia na kufikishwa mahakamani kwa tuhuma hizo.

‘’Hata hivyo oparesheni zetu ziliendelea hadi tulipofika mikoa jirani ya Mbeya,Iringa na hata Songea ambako tuliweza kuwapata watu mbalimbali pamoja na msako wetu tuliendelea kuwakamata waganga wa jadi na hasa wale wapiga ramli chonganishi ambao waliweza kuchochea chuki katika mkoa wetu’’alisema Renata.

Alisema jeshi la Polisi  limewafikisha mahakamani watu saba,watatu kwa tukio la mauaji ya watoto watatu kijiji cha Ikando,mtuhumiwa mmoja kwa mauaji ya watoto watatu mjini Njombe,na watuhumiwa watatu kwa mauaji ya mtoto mmoja kijiji cha Matembwe.

Alisema kutokakana na oparesheni iliyofanyika wanaendelea kuwaomba wananchi kuendelea kutoa taarifa za mtu yoyote atakaebainika na kuwa na dalili zozote za kujihusisha kwenye mauaji hayo.

‘’Tunaomba wananchi waendelee kutuletea taarifa ambazo ni za kweli. taarifa ambazo zitaweza kutusaidia sio taarifa za fitina au za kukomoa watu wakidai kuwa wanajihusisha na matukio haya kwa mfano wananchi wanaotuletea taarifa za maandishi wakieleza kuwa kuna matumizi ya gari namba zimehifadhiwa,kuna watu walioshuhudia majina yamehifadhiwa kuna gereji zinazotumika kuficha waalifu jina la gereji limehifadhiwa hapo itatuletea ugumu  sisi polisi kukamilisha upelelezi wetu’’alisema.

‘’Tunaomba taarifa za kueleweka ili kuweza kukomesha mauaji haya moja kwa moja sio taarifa ambazo zinaeleza majina yamehifadhiwa,sisi tunazichukulia kama taarifa za majungu ambazo hazina utafiti wowote na haziwezi kutuletea mafanikio.pia wananchi waendelee kutuletea taarifa za waganga wa jadi hasa wale wapiga ramli chonganishi ili tuwakamate na kuwafikisha mahakamani’’alisema Renata.

Pia Kamanda huyo amewataka wazazi na walimu kuendelea kushirikiana kuwalea watoto sambamba na kuwaasa wananchi waache kuamini imani za kishirikina na badala yake wafanye shughuli halali ili waweze kuhakikisha jamii inakuwa salama.

Kamanda Mzinga alisema wananchi wazingatie taratibu za kisheria kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi na wafuate taratibu za mirathi ili kuepuka kufanya mgawanyo wa mali kwa kutumia ubabe na visasi.

Aidha jeshi la polisi  mkoa wa Njombe linaendelea na upelelezi juu ya mtoto Gaudes Kihombo(7) mkazi wa kijiji cha Ikando kata ya Kichiwa aliyepotea tangu Januari sita ambaye hadi sasa hajapatikana.

Mpaka sasa watuhumiwa saba wamefikishwa mahakama ya hakimu mkoa wa Njombe kwa matukio ya mauaji ya watoto nane wakiwemo wa familia moja.

Waziri Mwakyembe Amlilia Ruge Mutahaba

Waziri Mkuu Atembelea Hispitali ya Rufaa Temeke na Mwananyamala....Wananchi Waimwagia Sifa Serikali

0
0
WANANCHI wameishukuru Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli kwa kuwabana watumishi wa umma, kwa sababu uamuzi huo umezaa matunda na sasa hali ya utoaji wa huduma katika maeneo mbalimbali nchini yakiwemo ya hospitali yameimarika.

Kauli hiyo imetolewa leo (Jumatano, Februari 27, 2019) na wagonjwa waliolazwa katika wodi ya wazazi kwenye hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke jijini Dar es Salaam, wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa hospitali hapo.

“Huduma zimeimarishwa dawa tunapata, hakuna lugha chafu wala kuombwa rushwa. Tunahudumiwa vizuri na kuna wakati hadi tunabembelezwa kunywa dawa mambo ambayo hapo nyuma hayakuwepo, hivyo tunaishikuru Serikali.”

Mmoja wa wagonjwa hao ambaye amelazwa katika wodi ya wazazi hospitalini hapo baada ya kujifungua, Mwajuma Mohammed amesema baada ya Serikali ya Awamu ya Tano kuingia madarakani na kuwabana watumishi wa umma sasa kuna mabadiliko makubwa sana ya kiutendaji.

Amesema zamani baadhi ya wauguzi hususani wanaofanyakazi kwenye wodi ya wazazi hawakuwa na lugha nzuri walikuwa wakiwatukana na kuwakashifu jambo ambalo kwa sasa halipo, kwani wakifika wapokelewa vizuri.

Mama mwingine aliyelazwa kwenye wodi hiyo, Crista Moyo amemuomba Waziri Mkuu kuisadia hospitali hiyo kwa kuiongezea watumishi kwa kuwa walipo ni wachache ukilinganisha na idadi ya wagonjwa wanaofika hospitalini hapo kila siku.

Crista ameishauri Serikali ikiwezekana iajiri hata watu wasiokuwa na taaluma ya udaktari au uuguzi ili wakafanyekazi ambazo hazihitaji ujuzi kama za  kuwasaidia wagojwa kutoka eneo moja kwenda lingine.

Kwa upande wake, Waziri Mkuu amezishauri Halmashauri jijini Dar es Salaam zihakikishe zinaendelea kuimarisha vituo vya afya na kuongeza vingine ili utoaji kupunguza msongamano wa wagonjwa kwenye hospitali za rufaa.

Pia ameshauri ianzishwe miradi ya ujenzi wa nyumba za watumishi katika hospitali hizo kwa lengo ya kuwezesha utoaji wa huduma mbalimbali zikiwemo za dharura kwa wakati.

“Rais Dkt. Magufuli anataka wananchi wapate huduma za afya karibu na  makazi yao ili kuwaondolea adha ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma hizo. Ndio maana tunajenga vituo vya afya vilivyokamilika vinavyotoa huduma zote muhimu kama maabara, upasuaji na mama na mtoto.”

Waziri Mkuu amesema lengo la ziara hiyo ni kukagua utoaji wa huduma za afya zinazotolewa katika hospitali hizo na kubaini kama kuna changamoto ili Serikali iweze kuzitambua na kuzitafutia ufumbuzi.

“Tumesikia changamoto zinazowakabili madaktari, tumezichukua na tutazifanyia kazi ikiwepo ya upungufu wa watumishi mbalimbali kama madaktari na wauguzi ili kuboresha zaidi utoaji wa huduma kwa wananchi.”

Waziri Mkuu amesema dhamira ya dhati ya Serikali kwao ni ya kuwatumikia wananchi wote bila ya ubaguzi wa aina yoyote, hivyo waendelee kuwa wazalendo na washirikiane na Serikali yao. Wafanye kazi kwa bidii.

Naye,Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo Dkt. Amaani Malima amesema hospitali hiyo inahudumia wagonjwa wa nje 1,800 hadi 2,000 kwa siku na wagonjwa wa ndani 250 hadi 300. Wagonjwa hao watoka wilaya mbalimbali.

Dkt. Malima amesema hospitali hiyo ina jumla ya watumishi 439 kati yao madaktari bingwa ni 16, madaktari 76 na wauguzi 209 na watumishi wengine 138. “Idadi hii ni ndogo kulingana na mahitaji ya hospitali kwani tuna upungufu wa watumishi 278 sawa na asilimia 39.”

Akizungumzia hali ya upatikanaji wa  dawa muhimu kwenye hospitali hiyo, Dkt. Malima amesema kwa kipindi cha Januari upatikanaji ulikuwa wa kuridhisha kwa asilimia 85 ya kiasi cha dawa na vifaa tiba vilivyohitajika.

Awali, Waziri Mkuu alitembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala ambapo alikagua mradi wa ujenzi wa jengo la kuhudumia wagonjwa mashuhuri ambalo lilianza tangu mwaka 2014 na bado halijakamilika.

Hivyo, ameishauri Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kuangalia namna ya kuweza kusaidia ujenzi wa jengo hilo ili mradi huo uweze kukamilika na hatimaye huduma zilizokusudiwa kutolewa katika jengo ziweze kufanyika.

Pia, Waziri Mkuu amewataka Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo Dkt. Daniel Nkungu na Kiongozi wa Wauguzi, Wambura wahakikishe wanaimarisha ushirikiano wao na hata wanapotoa maagizo kwa wasaidizi wao wawe wanataarifiana.

Kwa upande wa watumishi wanaofanya kazi katika idara za maabara amewataka wawe wanawahi kutoa huduma kwa sababu kuna malalamiko ya ucheleweshwaji wa huduma katika eneo hilo.

Kadhalika, Waziri Mkuu amewataka watumishi wanaofanya kazi katika kitengo cha radiolojia kwenye hospitali za Rufaa za Mkoa za Mwananyamala na Temeke jijini Dar es Salaam waache urasimu na wafanye kazi kwa kuzingatia maadili ya taaluma zao.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images