Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Watumishi Wa Umma Nchini Marufuku Kutumika Kisiasa

$
0
0
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) amewataka watumishi wa umma nchini kutotumika kisiasa kwani uwepo wao una lengo mahususi la kuboresha utoaji huduma wenye viwango stahiki ikiwa ni pamoja na kuijenga Serikali ili iweze kuleta maendeleo kwa wananchi.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri huyo wakati wa kikao kazi na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi hao, kabla ya kutembelea wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini wilayani Kisarawe ili  kujiridhisha na utekelezaji wa mpango huo.

Mhe. Dkt. Mwanjelwa amesema, serikali inahitaji utaalam wa watumishi wa umma katika kujenga utumishi wa umma imara uliotukuka, utumishi ambao utaziwezesha taasisi za umma zote nchini kutoa huduma stahiki kwa wananchi.

Mhe. Dkt. Mwanjelwa amesisitiza kuwa, hategemei kumuona mtumishi wa umma yeyote akijihusisha na siasa zinazosababisha kukwamisha azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuwahudumia wananchi wake kikamilifu.

Aidha, Mhe. Dkt. Mwanjelwa amewataka Makatibu Tawala wa Mikoa kuwasimamia kikamilifu Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri ili kujenga ushirikiano wa kiutendaji kati ya Makatibu Tawala wa Wilaya  na Wakuu wa Wilaya kwa lengo la kuboresha utoaji huduma bora kwa umma.

Mhe. Dkt. Mwanjelwa amehimiza ushirikiano wa watendaji hao ili kurahisisha utendaji kazi wa shughuli za serikali kwa ujumla, na kuongeza kuwa, serikali iliyopo madarakani ni moja tu inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, hivyo anashangaa inakuwaje Makatibu Tawala wa Wilaya wasiarifiwe masuala yanayoendelea katika halmashauri.

“Kuanzia sasa barua yoyote ya kiutendaji itakayotoka mkoani kuelekezwa kwa Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri, ni lazima nakala ya barua hiyo ielekezwe pia kwa Makatibu Tawala wa Wilaya ili wafahamu kinachoendelea na kumuarifu Mkuu wa Wilaya kufanya ufuatiliaji wa utendaji kazi’, amesisitiza Dkt. Mwanjelwa.

Mhe. Dkt. Mwanjelwa ameyasisitiza yote hayo wilayani Kisarawe ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kikazi yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma Mkoani Pwani ambapo mpaka hivi sasa ameshakutana na watumishi katika Halmashauri ya Mji Kibaha, Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze na Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe.

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) yafanya upasuaji wa fuvu kwa darubini

$
0
0
Madaktari  Bingwa wa Upasuaji ubongo wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI), wamefanikiwa kufanya upasuaji mgumu wa kuondoa uvimbe uliokuwa chini ya fuvu la kichwa kwa kutumia darubini ya kisasa.

Akizungumza na waandishi wa habari hospitalini hapo jana Daktari Bingwa wa Upasuaji Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu MOI, Nicephorus Rutabasibwa alisema upasuaji huo ni mgumu na huchukua muda mrefu kukamilika.

“Tumefanikiwa kufanya upasuaji huo kwa kushirikiana na mabingwa wenzao kutoka  Hospitali ya Kimataifa ya Chuo Kikuu cha Peking cha nchini China.

“Tumepokea jopo la mabingwa watatu, ushirikiano wetu ni wenye manufaa makubwa kwani huduma za MOI zitaendelea kuwa bora na watanzania wataendelea kupata huduma hizo hapa nchini billa ya kwenda nje ya nchi.

“Huu ni muendelezo wa ushirikiano tulioingia na wenzetu hawa wa Peking mwaka jana, tunaamini tutabadilishana uzoefu na wenzetu hawa ambao wamepiga hatua kubwa kwenye teknolojia ya matibabu, kupitaia ushirikiano huu mbinu tunazopata zitatusaidia kuendelea kutoa tiba bora na kwa wakati kwa wagonjwa wetu” alisema.

Alisema ujio huu wa wataalamu kutoka peking umelenga kuweka mazingira bora ya ushirikiano na MOI ili watakapo kuja tena wajue ni maeneo gani yanahitaji kuwa kipaumbele kwenye ushirikiano.

Kiongozi wa jopo la madaktari bingwa kutoka Peking, Profesa Yuani Zhao, alisema ushirikiano kati ya MOI na Peking utakuwa wenye mafanikio makubwa na utawanufaisha wagonjwa pamoja na madaktari vijana ambao watapata fursa ya kusoma kwenye chuo chao.

Rais Magufuli Akutana Na Kufanya Mazungumzo Na Daktari Bingwa Wa Upasuaji Wa Ubongo Na Mishipa Ya Fahamu Profesa Zhao Yuanil Kutoka China

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu Profesa Zhao Yuanil kutoka Hospitali ya Kimataifa ya Chuo Kikuu cha Peking cha Beijing nchini China mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika Mazungumzo na Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu Profesa Zhao Yuanil kutoka Hospitali ya Kimataifa ya Chuo Kikuu cha Peking cha Beijing nchini China aliyeambatana na ujumbe wake pamoja na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Profesa Lawrence Maseru na Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Respicious Boniface Ikulu jijini Dar es Salaam.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu Profesa Zhao Yuanil kutoka Hospitali ya Kimataifa ya Chuo Kikuu cha Peking cha Beijing nchini China wanne kutoka kulia, Balozi wa China hapa nchini Wang Ke watatu kutoka kulia pamoja Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Respicious Boniface. Wengine katika picha ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, Balozi Zuhura Bundala pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Profesa Lawrence Maseru.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu Profesa Zhao Yuanil kutoka Hospitali ya Kimataifa ya Chuo Kikuu cha Peking cha Beijing China wanne kutoka kulia mara baada ya kumaliza kupiga picha ya kumbukumbu Ikulu jijini Dar es Salaam.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Magonjwa yanayoababisha Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Ni Kama Vile, Kisukari ,presha, Ngiri Ya Kupanda Na Kushuka, Kiuno, Maumivu Ya Mgongo, Tumbo Kuuma Chini Ya Kitovu, Tumbo Kujaa Gesi. Yote Matatizo Yote Haya husababisha Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Kushindwa Kufanya Kazi Kwa Mwenza Wako  .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa Dar anapatikana mbagala Zakhem.  Songea ,bombambili, Shinyanga, Kahama ,mjini, Kwa ,maelezo, Zaidi , Piga Simu 0763172670/ 0715172670,/ ,Sema ,haloo, Dr Sitta... Wote  mnakalibishwa. 

Je Kwanini Baadhi Ya Wanaume Wengi Wana Ukosefu Ama Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
JE KWANINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA UKOSEFU AMA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO ???

Pata sululisho la matatizo haya na  magonjwa mengine utapona kwa mda mfupi sana hatakama ulihangaika mpaka ukakata tamaaa 

GALIMBO 3 MIX  ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa aina mbili ili kukidhi mahitaji ya mtumiaji, imetengenezwa kwa muundo wa vidonge pamoja na unga kwaajili ya kuponesha tatizo moja kwa moja , huimalisha misuli ya uume iliyolegea wakato wa tendo la mdoa ,na kukufanya ucherewe kufika kileleni kwa mda wa dk ( 20 - 45 ) itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu nira hamu kuisha wara kuhisi kuchoka vilivile huzalisha viini vya uzazi ( manii ) 

YOLAN  hurefusha na kunenepesha  maumbile madogo ya uume na kuwa na uume kuanzia nchi (6-8) tiba kwa mda mfupi sana

Zipo sananu nyingi sana zinazosababisha matatizo hayo  km vile -:punyeto, kisukali,ngili,chango,vidonda vya tumbo,  tumbo kuunguluma na kujaa gesi maumivu ya mgongo ama kiume ,kolodani moja kuvimba ama kuingia ndani  presha nk 

Matatizo haya yote sio mageni, kigeni ni tiba sahihi ya kuponesha matatizo hayo

SUPER MBUKE -:  nidawa ya kuponesha tatizo la kisukali kwa mda mfupi sana , usihangaike wara kuteseka tumia dawa ya mitishamba kwaajili ya tatizo hili na upone kabisa

NTINJIWA  nidawa ya mvuto wa biashara,kazi, kupandishwa cheo,kumfanya mfanyakazi apendwe na bos wake

Pia ninadawa za kumvuta mme , mke,mchumba,hawara, au mtu yoyote unaemuhitaji katika maisha yako hata km yupo mbali na atatulia na kukutimizia cjovjote utakacho na kumfunga asiwe na mtu mwingime ,

Pata tiba za magonjwa mbalimbali ikiwemo miguu kuwaka moto, mgongo,bawasili ,kaswende ,gono na mengine mengi

KWAUSHAULI NA TIBA WASILIANA NA DR CHIKAGO    0759 208 637

Km huna nafasi ya kufika ofisini hudumahii utaletewa hapo ulipo , kwa wale wa mikoani natuma kwanjia ya basi

Sekta za Afya Nchini Zashauriwa Kuitekeleza Afya Moja

$
0
0
Na. OWM DODOMA.
Afya Moja ni dhana inayojumuisha sekta ya afya ya binadamu , wanyamapori, mifugo na  mazingira katika kujiandaa, kufuatilia  na kukabili magonjwa yanayoathiri binadamu ,wanyamapori na mifugo.

Kwa kutambua  umuhimu wa  Afya moja nchini, sekta za Afya zenye kujumuisha wataalam wa sekta ya Afya ya binadamu, Afya ya wanyamapori na mifugo pamoja na mazingira wametakiwa kuanza kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia dhana hiyo ili uimarishaji wa Afya ya binadamu uwe wa Ufanisi na matokeo bora.

Akiongea wakati wa warsha ya  maafisa viungo wa Afya moja kutoka Wizara, Idara, Taasisi,  Mashirika ya serikali na ya Kimataifa, mjini Morogoro leo tarehe 26, Februari, 2019, Mkurugenzi Idara ya Uratibu Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Matamwe Jimmy, amefafanua kuwa tayari wataalamu hao wanao Mkakati wa kuzileta pamoja  Sekta za Afya kwa ajili ya kuzuia, kukinga na kuthibiti madhara na magonjwa yanayoikumba nchi yetu, yaani magonjwa ambukizi kati ya wanyama na binadamu pamoja na usugu wa vimelea vya magonjwa hivyo ni wakati wa kutekeleza mkakati huo kwa  kuitumia dhana ya Afya moja.

“Ninaamini kwamba, wote mnafahamu kuhusu tishio kubwa la magonjwa kama vile homa ya bonde la ufa, kwenye nchi za Afrika Mashariki , virusi vya Ebola Afrika Magharibi, kusambaa kwa kiasi kikubwa cha ugonjwa wa mafua ndege, (HPAI), matatizo ya kupumua yanayosababishwa na virusi vya Corona, mlipuko wa homa ya Lassa huko Africa Magharibi na homa ya Zika huko Amerika ya Kusini, kwa hiyo mifano michache magonjwa hayo yamekuwa tishio kubwa kwa afya ya binadamu na wanyama duniani kote.” Amesisitiza Kanali Matamwe.

Wakiongea wakati wa warsha hiyo wataalamu wa sekta za Afya hizo wamebainisha kuwa tayari wamekubaliana mfumo wa kutoa taarifa na kuhuisha utekelezaji wa mpango mkakati wa afya moja nchini.

Tarehe 13 Februari 2018, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa alizindua Dawati la Uratibu la Afya moja chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, likiwa na lengo la kusimamia na kuratibu shughui za Afya moja nchini. Kwa kutambua umuhimu huo  Idara ya Uratibu Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, kupitia Dawati la Uratibu wa Afya moja  kwa kushirikiana na USAID na   Chemonics International wameandaa mkutano wataalam hao.

MWISHO.

CUF Upande wa Maalim Seif Waiangukia Mahakama

$
0
0
Chama cha Wananchi (CUF) kimeiomba Mahakama kutoa hukumu ya shauri lao namba 23/2016 linalohusu uhalali wa uenyekiti wa Profesa Ibrahim Lipumba kwa chama hicho.

Chama hicho upande wa Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad kimesema ucheleweshwaji wa hukumu ya  shauri hilo unawasababishia madhara ikiwamo kuibiwa fedha za ruzuku zaidi ya Sh1.5 bilioni, kuondolewa kwenye nafasi za uongozi na kuwapo kwa mashauri mengi mahakamani yanayowagharimu fedha na muda.

Hayo yamesemwa leo Jumanne Februari 26, 2019 na wabunge wake, Ally Saleh (Malindi) na Hamidu Bobali wa Mchinga wakati wakizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za wabunge wa chama hicho, Magomeni jijini Dar es Salaam.

Saleh ambaye ni mnadhimu wa kambi ya CUF bungeni amesema si lengo lao kutoa shinikizo la aina yoyote, kuingilia taratibu za mahakama ila wanaomba shauri hilo litolewe hukumu.

"Tupo tayari kwa hukumu yoyote itakayotolewa, ila tumepata mashaka namna shauri hilo linavyoahirishwa mara kwa mara licha ya kuwa limeshasikilizwa," amesema Saleh.

"Kwa heshima na taadhima tunamuomba Jaji Mkuu na Jaji Kiongozi waliangalie suala hili kwa umuhimu na uzito maalumu kwa sababu kuchelewa kwake kunakiathiri chama chetu kwa kiasi kikubwa," amesema.

Amefafanua baadhi ya athari wanazopata tangu kupandikizwa kwa mgogoro huo ni kupoteza wabunge, madiwani na wenyeviti wa mitaa hata kwenye maeneo ambayo kichama wapo vizuri.

Ameitaja athari nyingine ni kuwapo kwa mashauri kadhaa Mahakama Kuu yanayowagharimu rasilimali fedha na muda na kuibiwa ruzuku zaidi ya Sh1.5 bilioni na uharibifu wa mali za chama zikiwamo magari na majengo.

"Chama kinashindwa kuendesha shughuli kwa utulivu na kujiandaa na chaguzi za ndani na za kiserikali kwa mwaka huu 2019 na uchaguzi mkuu 2020" amesema Saleh.

Naye Bobali amesema athari anazopata ni kubwa ikiwamo kutofanya siasa kwa kipindi chote tangu mgogoro huo ulipoanza.

Bobali ambaye pia ni mwenyekiti wa vijana wa chama hicho amesema mgogoro huo unawatoa kwenye ushindani wa kisiasa kwa sababu unawaweka mbali na wanachama wao na majimbo yao kwa ujumla.

"Tunashindwa kufanya siasa, kwa sababu baadhi ya maeneo wenyeviti wa chama kwa eneo husika wanakuwa upande wa Lipumba na sisi tupo upande halali wa Maalim Seif, huu mkanganyiko unatusukuma kuiomba mahakama kutoa hukumu ya kesi hiyo ili tuendelee na majukumu yetu angalau kwa kipindi hiki kifupi kabla ya uchaguzi mkuu 2020," amelalama Bobali.

Februari 22, 2019 Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ilisogeza mbele utoaji  hukumu ya mgogoro wa uongozi ndani ya CUF na sasa hukumu hiyo itatolewa Machi 17, 2019.

Finland yaipongeza Tanzania vita dhidi ya Rushwa.

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje wa Finland, Mhe. Timo Soini.amepongeza jitihada zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli za kupambana na rushwa na kusimamia uwajibikaji.

Pongezi hizo alizitoa wakati alipofanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga ambaye yupo nchini Finland kwa ziara ya kikazi ya siku mbili tarehe 25 na 26 Februari 2019.

Kwenye mazungumzo yao, Mawaziri hao wamesisitiza umuhimu wa Tanzania na Finland kuboresha ushirikiano kwenye sekta mbalimbali zikiwemo za biashara, uwekezaji, mafunzo ya ufundi, ajira kupitia sekta ya misitu, ushirikiano katika majukwaa ya kimataifa kwa kuzingatia usawa, pamoja na kuwajengea uwezo wanawake na watoto.

Aidha, Mhe. Soini  alitoa shukrani zake za dhati kwa Serikali ya Tanzania kwa kuendelea kuhifadhi wakimbizi na mchango mkubwa katika usuluhishi wa migogoro inayozikabili baadhi ya nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu. Hivyo, walikubaliana kuendelea kushirikiana katika kukabiliana na changamoto mbalimbali za kiusalama ikiwa ni pamoja na biashara ya madawa ya kulevya, biashara haramu ya kusafirisha binadamu, na matishio ya ugaidi.

Kabla ya mazungumzo hayo, Mhe. Balozi Mahiga alikutana na kufanya mazungumzo na Bw. Sampo Suihko, Mkurugenzi Mkuu wa Chuo cha OMNIA Espoo ambaye alieleza utayari wa Taasisi yake wa kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kubadilishana uzoefu wa kutoa mafunzo ya elimu ya ufundi yanayoendana na soko la ajira.

Mhe. Mahiga pia alifanya mazungumzo na Mhe. Matti Ahtisaari, Rais Mstaafu wa Finland na Mwanzilishi wa Taasisi ya Utatuzi wa Migogoro. Mhe. Ahtisaari aliipongeza Tanzania kwa kazi nzuri inayofanya katika utatuzi wa migogoro kwenye nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu na kusihi kuendeleza jitihada hizo kwa ustawi wa Dunia nzima.

Vilevile, Dkt. Mahiga alifanya mazungumzo na Bw. Jukka Kallio, Makamu wa Rais wa Helsinki. Katika mazungumzo hayo, uongozi wa Bandari ya Vuosaari umeahidi kushirikiana na uongozi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania katika kuboresha mifumo ya kidigitali (Digitalization) itakayoongeza ufanisi wa Bandari ya Dar es Salaam.

Katika kuhamasisha uwekezaji wa viwanda nchini, Mhe. Waziri Mahiga alifanya mazungumzo na Jumuiya ya Wafanyabiashara (Business Finland) na Makampuni makubwa ya kibiashara nchini humo. Wafanyabiasha hao walipongeza jitihada zinazoendelea kufanyika nchini Tanzania katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji na  waliahidi kuwekeza na kushawishi makampuni mengine kuona umuhimu wa kuwekeza nchini Tanzania.

Mhe. Waziri anahitimisha ziara hiyo kwa kufanya mazungumzo na Bi. Anne-Mari Virolainen, Waziri wa Biashara na Maendeleo wa Finland; Bw. Mauri Pekkarinen, Naibu Spika wa Bunge la Finland, Bw. Juhan Damski, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi  ya Utabiri wa Hali ya Hewa ya nchini Finland na baadaye kuzungumza na Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge la Finland.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
26 Februari 2019

Makamu wa Rais Atua Shinyanga

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewasili mkoani Shinyanga tayari kwa ziara ya kikazi ya siku 5.

Makamu wa Rais ambaye amesafiri kwa njia ya barabara akitokea mkoani Tabora ambapo napo alikuwa na ziara yenye lengo la kuhamasisha na kukagua shughuli za kimaendeleo.

Mara baada ya kuwasili mkoani Shinyanga Makamu wa Rais alitembelea kituo cha Afya cha Samuye na kupata nafasi ya kuzungumza na wananchi wa eneo hilo.

“Serikali ina kila nia ya kusogeza huduma za afya bora kwa wananchi”alisema Makamu wa Rais.

Aidha aliwaambia wananchi hao kuwa Serikali inakuja na sheria ya mpango wa bima za afya kwa wote ambayo itamuhitaji kila mtanzania kuwa na bima ya afya.

Makamu wa Rais amewataka wakazi wa kata ya Samuye kushirikiana katika kuzuia mimba za utotoni kwani kwa kiasi kikubwa zinahatarisha maisha ya watoto wa kike.

Kwa upande wake Naibu Waziri TAMISEMI Mhe. Mwita Waitara amesisitiza Halmashuri kutenga asilimia 40 kwa ajili ya miradi ya maendeleo na kuzitaka halmashauri zote kumalizia maboma ya zahanati wakati serikali kuu inaleta pesa za kumalizia maboma ya shule na madawati.

Alichokisema Rais Magufuli Baada ya Kukutana Na Daktari Bingwa Wa Upasuaji Wa Ubongo Na Mishipa Ya Fahamu

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 26 Februari, 2019 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Idara ya Upasuaji wa Ubongo na Mishipa kutoka Hospitali ya Kimataifa ya Chuo Kikuu cha Peking (PUIH) iliyopo Beijing nchini China Prof. Zhao Yuanil ambaye ameongoza timu ya wataalamu wanaoshirikiana na Taasisi ya Tiba ya Mifupa, Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu ya Muhimbili (MOI).

Mazungumzo hayo yamefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Balozi wa China hapa nchini Mhe. Wang Ke, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Lawrence Mseru.

Katika mazungumzo hayo Mhe. Rais Magufuli ameishukuru Hospitali ya Kimataifa ya Chuo Kikuu cha Peking kwa kukubali ombi lake la kuanzisha ushirikiano na MOI na amemhakikishia Prof. Yuanil kuwa Serikali ipo tayari kutoa ushirikiano zaidi utakaowezesha MOI kuongeza uwezo wake wa kutoa huduma za upasuaji wa ubongo na mishipa ya fahamu kwa Watanzania ambao wamekuwa wakikosa huduma hiyo ama kulazimika kutumia gharama kubwa kwenda nje ya nchi.

Mhe. Rais Magufuli ameelezea kufurahishwa kwake na taarifa za kufanyika kwa mafanikio kwa upasuaji wa kwanza uliofanywa na Daktari Bingwa Prof. Yuanil hapo jana na kwamba anaamini wataalamu zaidi wataendelea kuja hapa nchini kutoka PUIH kwa ajili ya kutoa huduma na kuwafundisha madaktari wa Tanzania, na pia Watanzania wengi watakwenda nchini China kujifunza upasuaji wa ubongo na mishipa ya fahamu.

Kwa upande wake Prof. Yuanil amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa juhudi zake kubwa za kuhakikisha MOI inaimarishwa ikiwemo kufanya uwekezaji mkubwa katika miundombinu na amemhakikishia kuwa PUIH itahakikisha makubaliano yaliyotiwa saini mwaka jana kati ya hospitali hiyo na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto yanatekelezwa kikamilifu.

“Tanzania kuna watu zaidi ya Milioni 50 na kuna idadi kubwa ya watu wenye magonjwa ya ubongo, wanaopata majeraha kichwani, uvimbe wa ubongo, matatizo ya mishipa ya damu ya ubongo na magonjwa ya uti wa mgongo ambao wanahitaji kupata matibabu mazuri hapahapa, lakini naambiwa kuna wataalamu 10 tu ambao hawatoshelezi mahitaji, ndio maana tupo hapa kuangalia mnafanya nini na tuone namna ya kusaidia kuwaongezea uwezo” amesema Prof. Yuanil.

Nae Mhe. Ummy Mwalimu amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa jitihada zake za kuwatafuta Madaktari Bingwa kutoka PUIH na kutoa maelekezo ya kuanzishwa kwa ushirikiano na MOI, pamoja na kuhakikisha Serikali inatoa zaidi ya Shilingi Bilioni 12.5 za kuimarisha miundombinu ya MOI ili itoe matibabu ya kibingwa ya upasuaji wa ubongo na mishipa ya fahamu kwa Watanzania wengi.

“Kwa kweli Watanzania wawe na matumaini makubwa kuwa huduma zile za kibobezi zitapatikana ndani ya nchi na hakuna kwenda nje, mambo yote ndani ya nchi, kwa hiyo tunashukuru sana kwa maono haya ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli, yeye ndio alipata taarifa kuwa kuna Daktari Bingwa huyu wa upasuaji wa ubongo na kisha akatupa maelekezo kuwa daktari huyo ameweza kutoa matibabu kwa wagonjwa walioshindikana katika nchi nyingi, kwa hiyo tukafanya mawasiliano kupitia Ubalozi wetu wa China na baadaye tukasaini mkataba Septemba 2018 nilipokwenda China na sasa tumeanza kutekeleza” amesema Mhe. Ummy Mwalimu.

Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt. Respicious Boniface amesema kupitia ushirikiano huu Tanzania inatarajia kupata wataalamu wengi wa upasuaji wa ubongo na mishipa ya fahamu na amebainisha kuwa pamoja na kufanya upasuaji wa mafanikio kwa mgonjwa mmoja hapo jana, wagonjwa wengine wawili watafanyiwa upasuaji leo na kwamba ushirikiano huu utaiwezesha MOI kuwa kituo bora cha upasuaji wa ubongo na mishipa ya fahamu Barani Afrika.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
26 Februari, 2019

BREAKING: Ruge Mutahaba Afariki Dunia.....Rais Magufuli Amlilia

$
0
0
Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba amefariki dunia leo nchini Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matibabu ya figo.

 Ruge atakumbukwa zaidi kwa mchango wake mkubwa katika sekta ya muziki nchini. 

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais Magufuli ametoa salamu za pole kwa ndugu na jamaa kwa kuandika maneno yafuatayo: Nimepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha kijana wangu Ruge Mutahaba. Daima nitamkumbuka kwa mchango wake mkubwa ktk tasnia ya habari, burudani, na juhudi za kujenga fikra za maendeleo kwa vijana. Poleni wanafamilia,ndugu,jamaa na marafiki. Mungu amweke mahali pema, Amina.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa: Dunia isilale katika udhibiti wa silaha

$
0
0
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres hii leo akihutubia mkutano maalumu unaofanyika mjini Geneva Uswisi kuhusu udhibiti wa silaha amesema maono mapya ya kimataifa ya udhibiti wa silaha yanahitajika na nchi hazipaswi "kulala" katika mbio mpya ya silaha za nyuklia.

Guterres ameeleza kuhusu vitisho kadhaa dhidi ya usalama wa dunia kutokana na kuenea kwa silaha akitolea mfano silaha za kemikali, silaha zinazojiendesha zenyewe na kuweza kushambulia kwa kadri zilivyoelekezwa kwa mfumo wa komputa na pia silaha za masafa marefu.

Maoni ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa yamekuja siku chache kabla ya mkutano wa pili kati ya Rais wa Marekani Donald Trump na Kim Jong-un wa Korea kaskazini.

Guterres amesema, “maelfu ya maisha ya raia yanaendelea kupotea kwasababu ya matumizi haramu ya silaha ndogondogo na matumizi ya silaha za uwanja wa vita katika miji.

Amesema miaka 70 iliyopita imeshuhudia maendeleo makubwa katika juhudi za udhibiti wa silaha, Guterres amesisitiza, akisema kuwa zile zilizofanikiwa zaidi ni zile zilizoongozwa na “nguvu kubwa” lakini mafanikio hayo yako hatari kutokana na aina mpya ya silaha.

Akielezea hatari ya kuruhusu kukoma kwa mkataba wa udhibiti wa silaha uliofikiwa kati ya Marekani na Urusi, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Guterres ameonya kuwa nchi za Ulaya zitakuwa miongoni mwa nchi za kwanza ambako ukosefu wa usalam utahisiwa zaidi.

Guterres amesisitiza, “juhudi zinatakiwa kufanyika ili kuongeza mwanzo mpya wa mkataba kati ya Marekani na Urusi kabla haujafika mwisho wake mwaka 2021.

Wabunge Nape Nnauye, Sugu, January Makamba, Mwigulu Nchemba Wamlilia Ruge Mutahaba

$
0
0
Kifo cha Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba kimewashtua wengi, miongoni ni wanasiasa ambao wametumia mitandao yao ya kijamii kuelezea hisia zao na kutoa salamu za pole.

Miongoni mwa wanasiasa waliomzungumzia Ruge ni Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba ameandika kwenye Twitter akisema, “Ruge. Ruge. Ruge. Nakosa maneno ya kutosheleza kuelezea maumivu na huzuni niliyonayo.”

“Kwa sasa, dua na fikra zangu ni kwa mama, Dk Mutahaba, ndugu na marafiki ambao walihangaika sana kuhakikisha anapona. Nikipata nguvu nitasema zaidi. Tangulia jamaa yangu, tunakuja. #RIPRuge.”

Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ameandika kwenye Instagram, “Sikutaka kuamini habari hii mpaka nimezungumza na Joseph Kusaga na kaniambia ni kweli umetutoka!”

“Pole sana kwa familia, Clouds Media Group, uongozi na wafanyakazi wote pamoja na wadau wote wa tasnia ya muziki na burudani tulioguswa na msiba huu mzito... R.I.P RUGE.”

Waziri wa zamani wa mambo ya ndani, Mwigulu Nchemba ameandika, “Umeondoka Ruge Mutahaba, umeondoka shujaa, umeondoka mpambanaji.”

“Pole kwa familia, ndugu na jamaa, pole zaidi kwa Watanzania wote kwa msiba huu mzito.”

“Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika" Ayubu 42:2,” ameandika Mwingulu kwenye akaunti yake ya Instagram akiambatanisha na picha ya Ruge.
Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye ameandika kwenye Twitter akisema, “Pumzika kwa amani kaka! Huna mfano wako duniani, maisha yako yameacha alama kubwa, utaishi milele kwa wema wako! Ndugu, Rafiki na mzalendo wa kweli!”

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya February 27


Mradi Wa Soko La Kisasa Manispaa Ya Morogoro Wamkuna Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji

$
0
0
Na Peter Haule, WFM, Morogoro
Halmashauri zote nchini zimetakiwa kujifunza kutekeleza miradi ya Kimakakati inayopatiwa ruzuku na Serikali, katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa kuwa thamani halisi ya mradi wa Soko la kisasa utakaogharimu Sh. bilioni 17 hadi kukamilika kwake inaonekana.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji, alipofanya ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua mradi wa kimkakati wa ujenzi wa Soko la Kisasa katika Manispaa ya Morogoro Mkoani Morogoro wenye lengo la kuzifanya Mamlaka za Serikali za Mitaa ziweze kujitegemea kimapato.

Dkt. Kijaji alisema kuwa Kama ipo halmashauri iliyopewa fedha za kutekeleza miradi ya kimkakati kwa kuwekeana mkataba na Serikali na bado inashindwa kufuata makubaliano ya mkataba ijifunze kutoka Manispaa ya Morogoro.

“Ukilinganisha na miradi mingine ya kimkakati niliyoikagua katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani, huu ni wa mfano, zipo halmashauri ambazo zimepewa fedha halafu zinarudi tena kuangalia upya mikataba ambayo waliwekeana saini na Serikali jambo ambalo linatia mashaka, tuje tujifunze kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro kwa nini ameweza kwenda na wakati ulio katika mkataba”alisema Dkt. Kijaji.

Alipongeza hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa mradi huo ambao umefikia asilimia 30 japo walitakiwa kufikia asilimia 40 katika kipindi hiki kutokana na changamoto ya kujaa maji na kuutaka uongozi wa Manispaa hiyo kukamilisha ujenzi ndani ya kipindi cha miezi mitano ili wafanyabiashara waanze kulitumia soko hilo.

“Mapato ya Soko hili yataongezeka kutoka Shilingi bilioni moja, kwa mwaka hadi Sh. bilioni 4 kwa kuwa idadi ya wafanyabiashara itaongezeka kutoka 400 kwa sasa hadi 900 na huduma zingine zitatolewa kama Benki” alieleza Dkt. Kijaji.

Dkt. Kijaji alisema kuwa dhamira ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, ya kuanzisha miradi ya kimkakati kwa manufaa ya watanzania itatimia kupitia mradi wa Soko la Kisasa la Manispaa ya Morogoro.

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Bi. Regina Chonjo, ameishukuru Serikali kwa kupeleka mradi huo Wilayani kwake, kwa kuwa soko lililokuwepo lilijengwa mwaka 1953 hivyo kuwa na miundombinu mibovu iliyosababisha wananchi kuwa na magonjwa ya mlipuko kikiwemo kipindupindu, hivyo mradi huo si tu utaongeza mapato na kuweka mandhari nzuri, lakini pia utaimarisha afya za wananchi.

Naye Meya ya Manispaa ya Morogoro  Bw. Pascal Kihanga, alisema kuwa waliwaahidi wananachi kusimamia ujenzi wa Soko hilo jambo ambalo linatekelezwa kwa juhudi kubwa, hivyo kufikia mwezi Septemba mwaka huu mradi utakabidhiwa kwa Serikali na wafanyabiashara wote walioondolewa kupisha mradi na  wengine watarudi.

Mhandisi wa Mradi huo Antonio Mkinga, amesema kuwa mradi huo utakamilika katika muda uliopangwa, kwa kuwa mpaka sasa hakuna vikwazo ambavyo vinaweza kuzuia utekelezaji wake.

Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro ni miongoni mwa Halmashauri 17 zilizokidhi vigezo vya kutekeleza jumla ya miradi 22 ya kimkakati nchini kwa mwaka wa fedha 2018/2019 kwa gharama ya shilingi bilioni 147 ambapo Manispaa hiyo ilipata mradi huo wa soko la kisasa litakalogharimu shilingi bilioni 17.

Chama cha Waigizaji Kinondoni ( KAMAMIKI ) Chamlilia Ruge

$
0
0
Chama cha Waigizaji Kinondoni, kimetoa pole zake kwa kifo cha  Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media Group, Ruge Mutahaba aliyefariki jana Jumanne Februari 26,2019.

Katika taarifa yao iliyosainiwa na  Mkuu wa Idara ya Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma, Masoud Kaftany imesema enzi ya uhai wake, Ruge alitoa mchango mkubwa kwa  wasanii wa muziki na fani zingine na kutoa elimu ya ujasiriamali

Pia alitoa mchango kwa Taifa la Tanzania katika nyanja ya muziki ambazo zilikuwa  chachu kubwa ya kujenga na kuandaa jamii ya Kitanzania kukabiliana na changamoto mbalimbali za kimaendeleo, kiuchumi, kisiasa na kijamii katika ujenzi wa taifa.

==>>Hii ni taarifa yao 
*Kamati ya Matukio Maadili na mikataba ya Chama cha Waigizaji ( M) Kinondoni ( KAMAMIKI ) Inatoa pole kwa *CLOUDS MEDIA GROUP na Familia Ya Marehemu *RUGE MUTAHABA* Kwa kuondokewa na Mpendwa Wetu Ruge Mutahaba ambaye Enzi za Uhai wake alikuwa Mwasisi na Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media

Enzi ya uhai wake *Ruge* alitoa mchango Mkubwa Kwa Wasanii wa Muziki na Fani zingine na kutoa Elimu ya Ujasirimali kwa Taifa La Tanzania Katika Nyanja Ya Muziki , ambazo Zilikuwa Chachu Kubwa ya Kujenga na Kuandaa Jamii ya Kitanzania Kukabiliana na Changamoto Mbali Mbali za Kimaendeleo , Kiuchumi , Kisiasa na Kijamii Katika Ujenzi wa Taifa.

Tunamuombea Kwa Mungu apumzike kwa Amani kwenye Nyumba Yake ya Milele. 


Bwana Ametoa , Bwana Ametwaa , Jina la Bwana Lihimidiwe . Inna Lillah wa Inna Illayhi Raj'uun. Asante. 

Imetolewa Na; Mkuu wa Idara ya Habari , Uenezi na Mahusiano na Umma - TDFAA ( KINONDONI ). *Masoud kaftany*

Tiba ya Tatizo la Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana duniani kote.

Upungufu wa nguvu husababisha tendo la ndoa kutokufanyika kwa kujiamini na kwa usahihi na hivyo kusababisha ndoa na mahusiano kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-

☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.

Kwa kutumia mimea na matunda  Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-

1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza  size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=

2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6 hadi 7  @130,000/=

3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @130,000/=

4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @250,000/=

5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni @130,000/=

BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA NA NI SALAMA KIAFYA

    Wasiliana nasi Popote

  ulipo duniani kwa (+255)

      Whatsap     0653 074067 )

             0752 92 34 61

Muhammad Buhari Atangazwa Kuwa Mshindi wa Kiti cha Urais Nigeria

$
0
0
Muhammad Buhari ametangazwa na Tume ya Uchaguzi Nigeria kuwa mshindi wa kiti cha Urais kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika Februari 23

Buhari ameshinda kwa kura millioni 15 akiwa zaidi kwa kura millioni 4 zaid ya mpinzani wake Atiku aboubakar . Hata hivyo, Upinzani wamekataa matokeo hayo.

Chama cha Buhari kimeshinda majimbo 19 kati ya 36 , wakati chama cha upinzani cha PDP wakishinda majimbo 17.

Tume ya uchaguzi imesema kuwa itaangalia malalamiko yote kabla ya kutangaza Rasmi matokeo ya uchaguzi.

Urusi yaituhumu Marekani kutaka kuiingilia kijeshi Venezuela

$
0
0
Urusi imeelezea wasiwasi wake kwamba Marekani inajiandaa kuiingilia Venezuela kijeshi, kufuatia hatua kadhaa za kijeshi zinazofanywa na taifa hilo katika ukanda huo, ambazo Urusi inadai kwamba ni maandalizi ya kumuondoa rais Nicolas Maduro madarakani. 

Marekani inamuunga mkono, kiongozi wa upinzani Juan Guaido, aliyejitangaza kuwa rais wa mpito nchini humo.

Katibu wa baraza la usalama la Urusi Nikolai Patrushev, amenukuliwa na vyombo vya habari nchini humo akisema kuhamishwa kwa vikosi vya operesheni maalumu vya Marekani nchini Puerto Rico, kuwasili kwa vikosi Colombia na mambo mengine yanaashiria kwamba wizara ya ulinzi ya Marekani inapeleka vikosi vyake kwenye ukanda huo ili kuvitumia kwenye operesheni ya kumuondoa Maduro.

Amesema, Urusi ilikubaliana na mapendekezo kutoka Marekani kuhusu mashauriano ya mzozo wa Venezuela, nchi ambayo ni mshirika wa karibu wa Moscow, lakini Marekani mara kadhaa imeliahirisha pendekezo hilo.

Mapema, makamu wa rais wa Marekani Mike Pence pamoja na kiongozi wa upinzani, Juan Guaido walikubaliana kuhusu mkakati wa kuimarisha vikwazo dhidi ya watu wanaomzunguka rais Nicolas Maduro, kufuatia mkutano wake na washirika wa kikanda nchini Colombia mnamo siku ya Jumatatu.
 
Makamu wa rais wa Marekani, Mike Pence ametangaza vikwazo zaidi dhidi ya Venezuela na dola milioni 56 za msaada kwa taifa hilo jirani, linalokimbiwa na idadi kubwa ya raia wake  kutokana na hali mbaya ya kiuchumi. 

Amesema wanataraji kuwepo kwa mabadilishano ya mamlaka kwa amani, lakini rais Donald Trump wa Marekani ameliweka hilo wazi, akisema mapendekezo yote yako mezani.

Maduro, alijibu hatua hiyo kwenye mahojiano yaliyofanyika siku hiyohiyo, akisema mkutano wa kikanda ulilenga kuandaa serikali yenye usawa na kuituhumu Marekani kwa kutaka kufanya lolote, hata kuingia vitani  ili kuweza kupata mafuta yake.

-DW
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images