Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mpelelezi nguli wa jeshi la Marekani Asaliti na Kuisaidia Iran.....FBI Wamsaka

$
0
0
Waendesha mashtaka wa Marekani wanamtuhumu Monica Witt aliyekuwa afisa wa kikosi cha anga cha jeshi la nchi hiyo kwa kuasi na kuwa mpelelezi wa jeshi la Iran akiwalenga aliokuwa akifanya nao kazi awali.

Kwa mujibu wa waendesha mashtaka hao, Monica alivigeuka vikosi vya Marekani mwaka 2013 akitumia maarifa ya kipelelezi ya kijeshi kuhujumu jeshi la nchi hiyo.

Shirika la Ujasusi la FBI limeeleza kuwa mwanamke huyo alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa na hati ya usalama wa hali ya juu alipokuwa akifanya kazi na jeshi la Marekani kati ya mwaka 1999 na 2013.

Aidha, watu wannne ambao ni raia wa Iran wanasakwa kwa tuhuma za kujaribu kuweka program ya kipelelezi kwenye kompyuta zinazomilikiwa na Monica.

Idara ya Hazina ya Marekani pia imeyafungia makampuni mawili ya Iran ambayo ni New Horizon Organization na Net Peygard Samavat kwa tuhuma za kuhusika kuwezesha kifedha mpango huo wa Iran.

“Hii ni siku mbaya kwa Marekani, ambapo raia mwenzetu ameisaliti nchi,” alisema Mwanasheria Mkuu Msaidizi, John Demers.

Monica anadaiwa kuvujisha siri za ndani za jeshi la Marekani kwa Iran yakiwemo majina ya wapelelezi na taarifa za ndani za oparesheni kadhaa.

Kupitia nyaraka za mashtaka, wapelelezi wameeleza kuwa mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 39 alipelekwa Mashariki ya Kati kwa ajili ya kufanya kazi maalum zilizobeba oparesheni za siri.

Kiwanda Cha Global Packaging Chapunguza Changamoto Ya Uagizaji Vifungashio

$
0
0
Na Lilian Lundo – MAELEZO
Kiwanda cha Global Packaging (T) Limited kilichopo Halmashauri ya Mji wa Kibaha, Mkoa wa Pwani kimepunguza kwa kiasi kikubwa uagizaji wa vifungashio nje ya nchi.

Hayo yameelezwa mapema wiki hii na Meneja Mradi wa kiwanda hicho, Hatibu Njuwila wakati wa mahojiano maalum na mwandishi wa habari hii.

“Kiwanda kilianza uzalishaji Januari, 2017 na  kuzinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli , kinazalisha tani 150 za mifuko au vifungashio kwa mwezi,” amesema Njuwila.

Ameendelea kusema, wateja wakubwa wa kiwanda hicho ni wakulima wanaozalisha bidhaa za nafaka kama vile mahindi, mtama na mchele, bidhaa zinazotokana na madini na mazao mengine yanayohitaji vifungashio.

Amesema, lengo la uanzishwaji wa kiwanda hicho ni kupunguza uagizaji wa vifungashio nje ya nchi kutokana na kuwepo na uigizaji mkubwa wa vifungashio kutoka nje ya nchi kwa gharama kubwa.

Aidha amesema, mafanikio waliyoyapata katika kipindi cha miaka miwili tangu kuanza kwa uzalishaji wa kiwanda hicho ni pamoja na kuajili wafanyakazi 98 ambao wote ni Watanzania,  ambapo kwa asilimia kubwa ni kutoka Halmashauri ya Kibaha.

Mafanikio mengine ni kupunguza kwa kiasi kikubwa uagizaji wa vifungashio kutoka nje ya nchi, kulipa kodi mbalimbali za Serikali Kuu pamoja na Halmashauri ambapo imeongezea Serikali mapato.

Matarajio ya kiwanda hicho ni kuzalisha vifungashio vyenye ubora na ambavyo vinakidhi mahitaji ya wateja ambayo itaongeza thamani ya mazao na uhifadhi na kupata masoko ya uhakika ndani na nje ya nchi.

Global Packaging (T) Limited imejipanga vyema kutekeleza sera ya Serikali ya viwanda kwanza kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025, inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Makamu Wa Rais Azungumza Na Wasanii Kuhusu Athari Za Matumizi Na Biashara Ya Dawa Za Kulevya

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewataka wasanii nchini kuiga mambo yenye kuleta manufaa kwa jamii.
 
Makamu wa Rais ameyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akihutubia Wasanii wa Sanaa mbalimbali waliohudhuria Kongamano la Wasanii nchini dhidi ya tatizo la dawa za kulevya.

“Naamini kuwa wasanii hawa ni vioo vya jamii lakini baadhi yao wamekuwa wakitumika kama ‘mapunda’ kusafirisha dawa na wengine kudumbukia kwenye uraibu wa dawa za kulevya” alisema Makamu wa Rais.

Makamu wa Rais aliwaasa wasanii hao kujiepusha na matumizi na biashara ya dawa za kulevya ambapo aliwaambia dawa za kulevya zina madhara mengi kiuchumi, kisiasa, mazingira, kiafya na kijamii, pia hudhoofisha afya za watumiaji na kuathiri uwezo wa kufanya kazi.

Kongamano hilo lililobeba kauli mbiu inayosema Usanii bila kutumia au kubeba Dawa za Kulevya inawezekana, Chukua Hatua.

Makamu wa Rais amepongeza kwa kuanzisha vituo 6 vya huduma ya methadone ambapo jumla ya waathirika 6,300 wametibiwa kwenye vituo hivi.

Makamu wa Rais ameagiza Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kuharakisha  miongozo hiyo na itakuwa vyema ikiwa kwenye udhibiti wa Dawa za hospitali zenye asili ya kulevya ili zitolewe na Bohari ya Kuu ya Madawa (MSD) badala ya watu binafsi.

Pamoja na mambo mengine Makamu wa Rais ametoa rai kwa vyombo vya ulinzi na usalama hususani polisi na maafisa uhamiaji kuhakikisha kuwa bidhaa zinazovuka mipaka yetu zisiwe bidhaa zinazokuja kuharibu Taifa.

Kwa upande mwingine Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana , Ajira na Walemavu) Mhe. Jenista Mhagama  alisema Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Uongozi wa Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amedhamiria kutokomeza dawa za kulevya hapa nchini.

Wakati huohuo, Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Harisson George Mwakyembe alisema amefurahishwa na nia njema iliyoonyeshwa na wasanii ya vita dhidi ya matumizi na biashara ya dawa za kulevya.

Lugola ahoji dereva wa Tundu Lissu kutopigwa risasi

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amesema kuna haja ya dereva ya Mbunge wa Singida Mashariki, Adam Bakari kueleza kwanini alipohisi kuwa wanafuatiliwa na watu wa siojulikana siku ya kushambuliwa kwa Lissu hawakuchukua hatua ya kulipeleka gari kituo cha polisi.

Kangi Lugoa ametoa kauli hiyo jana Jijini Arusha wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo amesema maelezo ya dereva huyo yanatia shaka, wanataka awaeleze mambo kadhaa yatakayosaidia uchunguzi wa tukio hilo.

"Kwa hali ya kawaida ni jambo la kushangaza risasi zote hizo wanasema 38, hata moja haikumpata dereva huyu,” alisema Lugola.

Waziri huyo pia amehoji risasi hizo kutoharibu kisanduku kilichopo katikati ya gari hilo sehemu ya mbele, kinachotenganisha dereva na abiria.

Kuhusu eneo hilo kuondolewa kamera za CCTV, Lugola amesema nyumba za Serikali jijini Dodoma hazina kamera hizo.

“Huu ni upotoshwaji mkubwa ambao unalenga kuwadanganya wananchi na kuwataka waichukie Serikali yao na Rais John Magufuli na mimi kama waziri wa mambo ya ndani sitokubali,” alisema.

Alibainisha kuwa eneo alilokuwa akiishi mbunge huyo linalindwa na askari wa kampuni binafsi za ulinzi, si polisi na kubainisha kuwa kutokana na utata huo ndio maana wanamtaka mbunge huyo na dereva wake kutoa maelezo kukamilisha upelelezi.

“Wao ndio walikuwepo watuambie hawa waliompiga risasi ni wanawake au wanaume, ni wanene au wembamba, warefu au wafupi,” alisema.

Viwanja Vikubwa Vinauzwa: Bunju na Mapinga (Baobab sec)

$
0
0
Viwanja Vikubwa Vinauzwa: Bunju na Mapinga (Baobab sec)

Viwanja viko Baobab sec, ni mpakani mwa Bunju na Mapinga. Viko umbali wa km 2 kutoka Main Road (DSM to Bagamoyo Road). Viwanja viko sehemu nzuri inayofaa kwa Makazi, Biashara na Ufugaji.

Viko Viwanja vya size tofauti:
20/20 (sqm 400) bei milion 5
20/30 (sqm 600) bei milion 8
20/40 (sqm 800) bei milion 10
sqm 2000 bei milion 25
sqm 2400 bei milion 31
Eka nzima (64/64) bei milion 48

Ruksa kulipa kwa awamu 2, kianzio ni 75% na luksa kujenga mara tu baada ya kulipa awamu ya kwanza.

Biashara hii haina dalali/udalali. Mpigie Mhusika: call 0758603077, whatsap 0757489709

Ukipata ujumbe huu, mjulishe ndugu/jamaa/rafiki.

Apandishwa kizimbani kwa kuandika taarifa za uongo Facebook

$
0
0
Mkazi wa Mwanza, Emmanuel Mahumbi (38) jana amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam akikabiliwa na mashitaka ya kuchapisha taarifa za uongo kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook.

Inadaiwa Septemba 2018 katika Jiji la Dodoma Mahumbi alichapisha taarifa za uongo katika mtandao wa facebook zikisema;"Kichaa m1 anatoa kafara kiboya kweli kaenda kumuona dada yake Bugando kumbe ndio anaenda kumkabidhi Freemason cku moja 2 baada ya kukuona akafa na kufa 2/ kaenda kuwatembelea Ukerewe cku 2 tu baada ya kuwaona wakafa na kufa kumbe alienda kuwakabidhi kwa freemason boya kweli mwambieni abadilike atamaliza watu".

Mahumbi alifikishwa mahakamani hapo na kusomewa mashitaka mbele ya Hakimu Mkazi, Augustine Mmbando.

Akisoma hati ya mashitaka, Wakili wa Serikali, Ester Martin alidai kuwa, mshitakiwa alitenda kosa hilo katika tarehe isiyofahamika Septemba mwaka jana jijini Dar es Salaam.

Mshitakiwa alikana mashitaka, na upande wa mashitaka umedai kwamba, upelelezi wa shauri hilo haujakamilika hivyo wameomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

Wakili wa utetezi, Hekima Mwasipu ameiomba Mahakama hiyo impatie dhamana mshitakiwa kwa sababu makosa yake yana dhamana na kwamba impe masharti nafuu kulingana na mashitaka yake.

Wakili Martin alisema, hawana pingamizi na dhamana, lakini watoe masharti ambayo yatamlazimu mshitakiwa kuwepo mahakamani wakati anapohitajika.

Hakimu Mmbando alimtaka kuwa na wadhamini wawili wanaotoka ofisi zinazotambulika ambao watasaini bondi ya Sh milioni 10 na kuwasilisha hati ya kusafiria.

Mshitakiwa alirudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana. Kesi imeahirishwa Februari 28, mwaka huu

Jeshi la Marekani lashambulia kambi za al Qaida Kusini mwa Libya

$
0
0
Jeshi la Marekani  kwa ushirikiano na  utawala wa Libya unaoungwa  mkono kimataifa  limeendesha operesheni  Kusini mwa Libya . Opereheni hiyo imetajwa kuwa walengwa ni magaidi wa kundi la al Qaida ambao wanajaribu kujikusanya katika eneo hilo.

Kulingana na  mshauri wa uongozi wa Libya unaotambulika kimataifa Muhammed es Sallak, shambulizi hilo la anga limelenga kambi za magaidi wa al Qaida Ubari Kusini mwa Libya.

Mshambulizi kama hayo yamewahi kuendeshwa na  jeshi la Marekani dhidi ya ngome za wangambo wa Daesh nchini Libya.

Ifahamike kuwa miaka  minane inakaribia tangu kupinduliwa na kuuawa kwa kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi na kuvamiwa na jeshi la Magharibi.

Je Unaupungufu Wa Nguvu Za Kiume au Maumbile Mafupi na Membamba...Suluhu iko hapa

$
0
0
Acha kusubilia mpaka mke au mpenzi wako akwambie Mme wangu wewe ni dhaifu tuwepo kitandani,unatakiwa ujitambue mapema ,kwa mwanaume aliyekamilika  na mwenye nguvu za kutosha  ili kumridhisha mke au mpenzi wake anatakiwa awe na uwezo wa kurudia zaidi ya Mara mbili lakini kama unakomea moja au mbili hapo ujue umejilidhisha wewe tu sio na yeye, ili uwe mwanaume mwenye uwezo kamili tumia dawa yako hii hapa

 SUPER MAJINJAS MIX; dawa hii ni tofauti na ambazo uliwai kutumia inamichanganyo ya miti na matunda zaidi ya saba ndio maana inakupa uwezo wa ,KURUDIA TENDO ZAIDI YA MARA TATU,NA ITAKUFANYA UCHELEWE KUFIKA KILELENI DAKIKA 10-15 KWA TENDO LA KWANZA,NA PIA HUIMALISHA MISULI ILIYOLEGEA NA KUSINYAA KWA WALE AMBAO WALIPIGA SANA PUNYETO,dawa hii ni ya vidonge na unga na haina madhara yoyote

MAKAKANUA NO 5 MPYA; dawa hii uboresha uume saizi upendayo UREFU WA INCHI 5,6,7,NA 8 NA UPANA WA CM 2,3,4 NA 5 dawa hii ipo ya kunywa na kupaka  na pia usahidia zaidi kwa mwanaume aliyefanyia tohara ukubwani,

ISENYE NO 3; hii ni dawa kwa wenye kisukari dozi siku 21 tatizo la kisukari na ndio chazo kikubwa cha kuishia nguvu za kiume,

NGWALUSA ; hii ni dawa ya uzazi ambayo ufungua milija ya uzazi ata kwa wale walifungwa uzazi,zipo dawa za busha,vidonda vya tumbo,miguu au viungo kufa gazi kupungza kitambi,minyama uzembe,na matiti makubwa 

FIKA NTUNZU HEBRISTI CLINIC ILIYOPO MBAGALA ZAKHEMU Njoo mpaka ulipo ukumbi wa DAR LIV ni dakika tano tu kufika ofisi ilipo. MOROGORO,MWANZA,NA KAHAMA WAPO MAWAKALA

 Kwa mawasiliano zaidi piga simu 0744040721, 0683645920 DR BRUNO pia unaweza ukaletewa popote ulipo

Usikate Tamaa....Okoa Ndoa yako kwa Tiba Hii ya Asili

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote .

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0620510598  / 0743543944

Benki Kuu yazindua mfumo wa malipo ya papo kwa papo

$
0
0
BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imezindua mfumo mpya wa malipo ya fedha kwa njia ya kielektroniki utakaowezesha utumaji wa huduma za kifedha kutoka katika taasisi moja kwenda nyingine.

Pamoja na kurahisisha utumaji wa fedha, pia utaondoa urasimu na udanganyifu kwa taasisi za fedha.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuzindua mfumo huo, Mkurugenzi wa Mifumo ya Malipo ya Taifa wa BoT, Benard Dadi, alisema mfumo huo pamoja na kurahisisha utumaji wa fedha, pia utasaidia benki hiyo kupata taarifa za kifedha katika kila benki badala ya kusubiri kupelekewa taarifa hizo na taasisi za benki.

Kwa mujibu wa Dadi, pia utasaidia kuonyesha kiwango cha mapato ambacho serikali inapaswa kupata kupitia taasisi za fedha.

Kadhalika, alisema pia utapunguza matumizi ya fedha taslimu na kuondoa usumbufu ambao umekuwa ukitokea wa kukosea taarifa za kifedha ikiwamo majina na taarifa nyingine muhimu.

“Mfumo huo utasaidia kuonyesha kila muamala unaofanyika katika kila kampuni nyingine, kwa hiyo kutusaidia kujua miamala ni mingapi kwa siku, kwa mwezi, kwa mwaka, kuleta udhibiti ndani ya BoT, badala ya kwenda kwenye kampuni kwenda kuomba taarifa, hizo taarifa tutakuwa nazo, tutajua serikali inapata ushuru kwa kiasi gani kwa usahihi zaidi bila kutegemea mpaka ifike mwisho wa mwezi ndio tupewe taarifa kujua serikali imepata ushuru kiasi gani,” alisema Dadi na kuongeza:

“Vyote hivyo vitarahisishwa sana kupitia mfumo huu na kufanyika miamala utakuwa unachukua muda mfupi ndani ya sekunde mbili au tatu kumfikia mteja na pia itasaidia kupunguza gharama. Mfumo huu unajengwa ndani ya miezi 18 na utatumia wataalamu kutoka BoT,” alisema Dadi.

Sosteness Kewe, Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Kuendeleza Sekta ya Fedha Tanzania (FSDT), alisema mfumo huo mpya utakuwa na manufaa makubwa kwenye uchumi wa nchi, wananchi wa kawaida, wafanyabiashara na wakulima kwa sababu utakapoanza kufanya kazi utasaidia kupunguza gharama za utumaji wa fedha pamoja na kutoa taarifa za watu wote wanaotumia huduma za kifedha.

Alisema taarifa hizo pia zitasaidia taasisi za fedha kuongeza ufanisi namna ya kuboresha huduma kwa wateja.

“Tunajua wengi tunatumia mfumo wa fedha taslimu ambao ni gharama kubwa, lakini mfumo huu wa kutuma pesa kwa haraka utaepusha mengi, kwa mfumo wa sasa unatakiwa uende benki ukachukue pesa au umtume mtu au umtume boda boda, lakini kwa mfumo huu ambao BoT umezindua utarahisisha miamala mbalimbali kulipa au kupokea pesa kiurahisi hasa wafanyabiashara, wakulima kufanya miamala kwa urahisi zaidi, hawatakuwa na haja ya kulipa fedha taslimu,”alisema Kewe.

Taasisi Binafsi Njombe zakwepa kutumia mashine za EFD

$
0
0
Na Amiri kilagalila
Mamlaka ya mapato TRA mkoa wa Njombe imefanya oparesheni ya dharura ya ukaguzi wa mashine za kielektronic za kukatia risiti katika taasisi za shule , Zahanati pamoja na vituo vya afya na kubaini kuwa idadi kubwa ya taasisi hizo hazitumii mashine hizo na kutoa muda wa wiki mbili kwa taasisi hizo kununua mashine hizo vinginevyo zitapigwa faini ya kuanzia mil 3 hadi 4 kwa kuisababishia hasara serikali.

Akizungumza mara baada ya kukamilisha zoezi la ukaguzi wa mashine hizo meneja wa TRA mkoa wa Njombe Musib Shaban amesema katika uchunguzi mdogo uliofanyika wamebaini kuwa kumekuwa na ukwepaji mkubwa wa ulipaji wa mapato katika taasisi binafsi za shule na afya hali ambayo inakwamisha jitihada za serikali katika ukusanyaji wa mapato na utekelezaji wa miradi ya maendeleo .

Musibu amesema wamiliki wengi wamekuwa wakikwepa matumizi ya mashine za kielektronic kwa madai ya kukosa elimu juu matumizi ya EFD katika taasisi hizo jambo ambalo halina ukweli na kuagiza ifikapo marchi mosi kila mmiliki wa taaisisi hizo awe amenunua mashine hizo.

Wakitoa utetezi wao mara baada ya kubainika kutotumia mashine za EFD baadhi ya wamiliki na wakuu wa shule akiwemo Anna Mwalongo ambaye ni mkurugenzi wa Hagafilo Holdings pamoja na Andrew Chikwanda mkurugenzi wa GILGAL wanasema sababu kubwa ya kutotumia mashine hizo ni uelewa mdogo .

Licha ya kubainika kwamba taasisi nyingi za biashara hazitumii EFD, lakini baadhi ya watumiaji wanasema mashine hizo zimekuwa na dosari kubwa na kutoa mapendekezo kwa serikali kuhakikisha zinarekebishwa kwa wakati

Kwa mujibu wa TRA kila mfanyabaishara mwenye mauzo ya kuanzia mil 14 anapaswa kutumia EFD mashine.

Raia 13 Wa Ethiopia Wanaswa Wakiwa Wamejificha Shambani Jijini Mwanza

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Mwanza linawashikilia raia 13 wa Ethiopia wakiwa wamejificha kwenye shamba la mkazi mmoja wa mtaa wa Nyaburogoya Kata ya Nyegezi jijini hapa.

Miongoni mwao, watano wamekutwa na hati za kusafiria zilizotolewa na Ethiopia zilizogongwa muhuri na Idara ya Uhamiaji ya Kenya, lakini bila kugongwa mhuri na idara hiyo nchini.

Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, Jumanne Muliro, alisema watu hao walikamtwa Februari 13, mwaka huu asubuhi, kufuatia taarifa za kiintelijensia kutoka kwa raia wema, na kwamba walipofuatilia walikuta ni kweli kisha kuwakamata13, ambao walitambulika kuwa ni raia wa nchi hiyo.

“Tunachoendelea nacho kwa sasa ni kutaka kujua hawa watu wamefikaje hapa nchini, wamesafirije hadi kupita mpakani na ni nani mwenyeji,” alisema Kamanda Muliro na kuongeza:

“Watakapobainika wanaowapatia mbinu za kuingia nchini bila vibali watachukuliwa hatua sitahiki za kisheria, ikiwamo kufikishwa kwenye vyombo husika.”

Aidha, alisema kutokana na watu hao kutokuelewa lugha ya Kiswahili wala Kiingereza, utaratibu unafanyika wa kumtumia mkalimani ili kubaini sehemu wanayotoka na wanapokwenda.

“Tunawashikilia katika kituo kikuu cha Nyamagana, taratibu zinafanyika za kuwafikisha katika idara ya Uhamiaji kwa ajili ya hatua nyingine za kisheria,” alisema.

Hiki Ndicho Wanacho Kiwaza Wanaume Wengi Kuhusu Kuingia Katika Mahusiano /ndoa Na Single Mothers

$
0
0
Wewe  ni  Single  Mother ?  Upo  katika  mahusiano  ya  kimapenzi  na  mwanaume ? Au  unataka  kuingia  katika  mahusiano ya  kimapenzi/uchumba/ndoa  na  mwanaume  ambae  si  baba  wa  mtoto  wako?

Basi  kabla  ya  kufanya  hivyo,unatakiwa  kujua  kitu  gani  wanacho  kiwaza  wanaume  wanao  ingia  katika  mahusiano  na  single  mothers.

Pia  unatakiwa  kuyafahamu  mambo  wanayo  yawaza wanaume  wengi  kabla  ya  kuingia katika  ndoa  na  single  mothers.

Mahusiano  mengi ya  single  mothers  yanashindwa kufika  mbali  kwa  sababu  single  mothers  wengi  huwa  wanaingia  katika  mahusiano  na  wanaume  bila  kuyafanyia   analysis  mambo  haya  muhimu  kabisa  kwa  kila  single  mother kuyafahamu.

AFRICANDADAZ ime kusanya maoni  kutoka  kwa  wanaume  mbalimbali kuhusu  uzoefu  wao  na  mtazamo  wao  kuhusu  kuingia  katika  mahusiano  ya kimapenzi  au ndoa  na  single  mothers.  

Maoni  haya  yamechukuliwa  kutoka  kwa  wanaume  mbalimbali  wa  hapa    Tanzania  na  waliopo  nje  ya  Tanzania.  Baadhi  ya  mambo  yanayo semwa  na  wanaume  hawa  kuhusu  kuingia  katika  mahusiano  ya  kimapenzi  au  ndoa na  single  mothers  yanatisha  na  kuogopesha   sana. 

 Ni  vyema  kila  single  mother ambae  anafikiria  kuingia  katika  mahusiano  ya  kimapenzi  au  kuingia  katika  ndoa  na  mwanaume  ambae  si  baba  wa  mtoto  wake  ayafahamu  mambo  haya.

Kusoma  zaidi  makala  haya tembelea Kwa kubofya hapo chini :

Serikali Yakabidhi Eneo La Mradi Wa Umeme Wa Maji Mto Rufiji Kwa Mkandarasi Tayari Kwa Kazi Kuanza

$
0
0
SERIKALI imekabidhi rasmi eneo la mradi wa umeme wa maporomoko ya maji ya Mto Rufiji (RHPP),  kwa mkandarasi Kampuni ya Arab Contractors kwa pamoja na ile ya Elsewedy  Electric zote kutoka nchini Misri.

Hatua hiyo sasa inaashiria kuanza kwa kazi ya ujenzi wa mradi huo wa umeme ambao utazalisha Megawati 2,115 ambazo zitaingizwa kwenye dridi ya Taifa na kuifanya Tanzania kuwa na umeme mwingi na wa uhakika.

Waziri wa Nishati, Dk Medard Kalemani alikabidhi mradi huo jana katika eneo la Hifadhi Matambwe lililopo mpakani mwa mikoa ya Pwani na Morogoro, akisema faida nyingine ya mradi huo utakapokamilika bei ya umeme itashuka kwa kiwango kikubwa na utasaidia nchini kutekeleza rasilimali muhimu za Taifa.

Alisema mradi huo utajenga bwawa kubwa, lenye mita za ujazo bilioni 34 na kituo cha kufua umeme, kitakachokuwa na mashine tisa za kuzalisha umeme zenye uwezo wa megawati 2,115.

Aidha, alisema pindi mradi huo ukikamilika, utasaidia kushusha gharama za umeme kutokana na uzalishaji wa umeme huo wa kutumia maji kuwa nafuu, tofauti na nishati nyingine kama mafuta, gesi, upepo na jua.

Aliwataka wakandarasi hao, kukamilisha mradi huo kwa muda waliokubaliana, huku akiwapongeza wataalamu kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa kuchangia utekelezaji wa mradi huo kwa hatua za awali. 

Aliwataka wakandarasi watakaotekeleza ujenzi huo, kujenga kwa ufanisi mkubwa na kwa viwango vinavyotakiwa na muda uliopangwa na utakaondoa shaka kwa wale wasioutakia mema mradi huo.

Dk Kalemani alimpongeza Rais John Magufuli kwa jinsi ambavyo amechukua ujasiri wa kuamua kutekeleza ndoto za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere ambaye mwaka 1958 alikuwa na mpango wa kujenga bwawa hilo, lakini ikashindikana kutokana na changamoto kadhaa ikiwemo za kifedha. 

Hivyo aliwataka wakandarasi wa kampuni hizo na timu ya wataalamu wa Tanesco, kutoondoka eneo la mradi baada ya kukabidhiwa eneo, kwa kuwa hadi sasa kila kitu kipo kuanzia nyumba za kuishi, umeme na maji. Aliwataka wajenge wakati wote wa mvua na jua.

“Hatutaki kugeuka nyuma kuanzia sasa, Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco ushiriki kikamilifu ili mradi huu uweze kukamilika kwa wakati uliopangwa,” alisema Dk Kalemani. 

Aliongeza, “Mimi na Naibu Waziri na hata Rais tutakuwa bega kwa bega usiku na mchana kuona mradi unakamilika kwa muda uliopangwa na kwa viwango na ubora wa kimataifa wa mabwawa ya kufua umeme.”

Alisema kukamilika kwa mradi huo, kutaleta tija katika kujenga uchumi wa nchi kupitia sekta ya viwanda. Alisema mahitaji ya umeme nchini kwa sasa ni makubwa kwani nchi inatekeleza Sera ya Uchumi wa Viwanda, hivyo huduma za umeme wa uhakika inahitajika zaidi. 

Dk Kalemani alisema ujenzi wa mradi huo, unajumuisha ujenzi wa bwawa kuu lenye uwezo wa kutunza maji takribani mita za ujazo bilioni 34, kituo cha kufua umeme kitakachokuwa na mashine tisa za kuzalisha umeme zenye uwezo wa megawati 235 kila moja, hivyo kufanya uwezo kuzalisha umeme wa mradi megawati 2,115.

Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Dk Tito Mwinuka alisema mradi huo wa kihistoria, uliosainiwa kati ya Tanesco na Kampuni ya Ubia Arab Contractors (Osman A. Osman Co na Elsewedy Electric), utakuwa na mkataba wa miezi 42. 

Msimamizi Mkuu wa kampuni mbili zilizopewa kandarasi hiyo, Makamu wa Rais wa kampuni hizo kutoka Serikali ya Misri, Wael Handy alisema mradi huo si wa Watanzania pekee, bali ni faida kwa wananchi wa Afrika yote.

Alisema mradi huo umeshirikisha timu mbalimbali za wataalamu wa sekta mbalimbali na katika kutekeleza mradi huo, Serikali ya Misri haitawaangusha na itahakikisha unatekelezwa kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa.

Airbus kusitisha uzalishaji wa ndege zake aina ya A380

$
0
0
Shirika la Airbus limetangaza kwamba ifikapo mwaka 2021 litasitisha uzalishaji wa ndege zake aina ya A380 superjumbo kutokana na kukosekana kwa soko.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na shirika hilo ifikapo mwaka 2021 oda zilizokuwepo za ndege aina ya A380 zitakabidhiwa kwa wanunuzi na uzalishaji wa ndege hizo utasimamishwa.

Katika taarifa hiyo mkurugenzi mkuu wa Airbus Tom Enders alisema, wanatoa tangazo hilo huku wao na wanahisa wengine wa A380 wakiwa na uchungu.

Mteja mkuu wa ndege hizo aina A380 shirika la ndege la Emirates limepunguza kiasi cha manunuzi ya ndege hizo kutoka ndege 162 hadi 123 imefahamishwa katika taarifa hiyo.

Emirates imeingia mkataba mpya wa kununua ndege 70 aina ya A330-900s na a350-900s mbadala wa A380. Mkataba huo mpya una thamani ya dola bilioni 21.4.

Ndege hizo za Airbus A380 zenye uwezo wa kubeba zaidi ya abiria 800 ziliazalishwa kutoa ushindani kwa ndege aina ya Boeing 747 za shirika la uzalishaji ndege la Marekani.

Super Moringa : Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORINGA DAWA BORA YA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME NA KUNENEPESHA UUME
_________________________
🔖🌸SUPER MORINGA Ni dawa bora ya nguvu za kiume  yenye mchanganyiko wa mitishamba (7) yenye maajabu yafuatayo/

🔖 (1) inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimalisha misuli ya uume uliolengea wakati wa tendo la ndoa/
🔖 (2) Kurefusha uume uliorudi ndani kuazia nchi 5 - 9/
🔖 (3) kunenepesha uume cm 5 ya upana itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15 - 20 kwa tendo la kwanza na utakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya 2-4 bila hamu kuisha/

📌 Na inatibu kabisa
 📌 Haijalishi umri hata kama una miaka 85 itumie huanza kufanya kazi dk 50 tu na haina madhara yoyote kwa mtumiaji/

🌳🌳🌳🌳🌳🌳🌳🌳            
MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA.
_________________________
🔖 (1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖 (2)Choo kama cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(4)Kaswende/
🔖(5)Gono/

📌Haya yote husababisha kuishiwa nguvu za kiume na kuwa na uume mdogo/
📌 Itumie leo, bado hujachelewa ni tofauti na nyingine.
_________________________
DAR ES SALAAM OFISI IPO BUGURUNI SHELI AU UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
___________________________
WASILIANA NA
Dr ATHUMAN SIMU.
📞0714 884 677
📞0767 104 343
____________________________
*****************************

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Baraza la Wawakilishi Marekani lasitisha msaada kwa Saudi Arabia

$
0
0
Baraza la Wawakilishi la Marekani lenye Wademokrat waliowengi limemkosoa Rais Donald Trump Jumatano na kupiga kura kusitisha msaada wa kijeshi unaotolewa na Marekani kwa majeshi ya ushirika yanayoongozwa na Saudi Arabia yanayo fanya mashambulizi nchini Yemen.

Kura zilikuwa 248 kwa 177 na ni mara ya kwanza kwa baraza hilo kutumia sheria ya War Powers Act.

Uamuzi huo sasa utapelekwa Baraza la Seneti ambalo lilipitisha hatua kama hiyo mwishoni mwa mwaka 2018, na kuwepo uwezekano wa kuzuka mvutano na White House.

Marekani imekuwa ikitoa msaada wa kipelelezi na vifaa kwa ushirika unaoongozwa na Saudi Arabia unaopigana na waasi wa kihouthi wanaoungwa mkono na Iran nchini Yemen.

Vita hiyo imeuwa maelfu ya raia tangu mwaka 2014 na tayari imesababisha janga kubwa la kibinadamu katika moja ya mataifa maskini sana duniani na kufanya hali kuwa mbaya zaidi nchini humo.

Mashambulizi ya anga yanayoongozwa na Saudi Arabia yanayowalenga waasi yameharibu maeneo ya shule na mahospitali.

Wakimbizi 500 watoroka machafuko DRC na kuingia Uganda

$
0
0
Mapigano ya ukabila yaliyotokea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) wiki iliyopita yamesababisha zaidi ya watu 500 kukimbilia Uganda.

Wakimbizi hao wamewafahamisha maofisa wa Uganda   na Shirika la Umoja Mataifa linalowahudumia Wakimbizi (UNHCR) kuwa mapigano hayo kati ya jamii za Lendu na Bagerere yamelitumbukiza eneo la mashariki mwa Congo katika hali ya sintofahamu.

Makundi hayo ya wakimbizi kutoka jimbo la Ituri mashariki mwa nchi, yanafanya safari za hatari kuvuka Ziwa Albert lililoko mpakani mwa nchi hizo mbili wakitumia mitumbwi isiyo na ubora.

Wengi wao  ambao ni wanawake na watoto, wameshuhudiwa wakiwa na mizigo yao hususan magodoro.

Kinachowatia hofu na wasiwasi viongozi wa wilaya za Hoima na Kikuube ni uwezekano wa kuzorota  hali ya usalama.

Inahofiwa huenda kuna uwezekano wa wakimbizi kuingia Uganda wakiwa wamejihami kwa silaha.

Shaka nyingine ambayo wimbi hilo jipya la wakimbizi kutoka DRC ni namna watu hao wanavyowasili bila kupitia njia rasmi za mipakani ambako wangepimwa kabla ya kutangamana na jamii za Uganda.

Wakazi wana wasiwasi kuwa kuna uwezekano wa milipuko ya magonjwa ya Ebola na kipindupindu.

Rugemarila , Seth waendelea kusota Rumande

$
0
0
Upelelezi wa kesi ya uhujumu uchumi na utakatishaji wa fedha inayowakabili wafanyabiashara Herbinder Seth na mwenzake James Rugemarila, bado unaendelea na washtakiwa wanaendelea kusota rumande.

Washtakiwa hao kwa pamoja walisomewa mashtaka 12 ya uhujumu uchumi na utakatishaji fedha na Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai  katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi.

Wakili Swai alidai mahakamani hapo jana kuwa kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kutajwa, lakini upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kuiomba mahakama hiyo kupanga tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Shaidi aliahirisha kesi hiyo hadi Februari 28, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.

Washtakiwa hao kwa pamoja wanakabiliwa na mashitaka hayo 12 ya uhujumu uchumi  kwa kula njama, kujihusisha na mtandao wa uhalifu, kughushi nyaraka, kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu,  kutakatisha fedha  na kuisababishia Serikali hasara ya Dola za Marekani  22, 198,544.60 na Sh 309,461,300,158.27.

Washitakiwa hao bado wanasota rumande kwa kuwa mashtaka hayo hayana dhamana kwa mujibu wa sheria.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images