Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kijana adaiwa kumbaka bibi kizee hadi kufariki

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Dodoma, linamshikilia mkazi wa Chikoa, William Saimon (28), kwa tuhuma za kumkaba na kumbaka bibi kizee Jema Macheho (77), ambaye alifariki dunia baadaye wakati akipatiwa matibabu.
 
Hayo yalielezwa jana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa.
 
Muroto alisema mtuhumiwa huyo alimkaba na kumbaka bibi kizee huyo ambaye ni mkazi wa Bihawana ambaye alifariki dunia katika Hospitali ya Rufani ya Dodoma akiwa anapatiwa huduma ya kwanza.

Alisema tukio hilo lilitokea Jumatatu saa 5:55 usiku katika kijiji cha Bihawana wakati marehemu akiwa njiani kurudi nyumbani kwake.

"Akiwa njiani ghafla alikutana na mtuhumiwa na kumvutia vichakani kwa kumkaba shingo na kumfanyia kitendo cha ubakaji,” alisema.
 
Kamanda Muroto alisema mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani kwa kosa la mauaji.

Katika tukio jingine, Muroto alisema jeshi hilo linamshikilia Leusi Lazaro (23), mkazi wa mkoani Dar es Salaam, kwa kudaiwa kuwaibia wanafunzi mali mbalimbali kwenye mabweni ya vyuo vikuu jijini hapa.

Alisema katika Chuo cha Biashara (CBE), mtuhumiwa aliiba kompyuta mpakato (laptop) aina ya Dell Spiral Min ,Chuo cha St. John aliiba simu aina ya Iphone 6+ na Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), aliiba simu mbili aina ya Tekno W2 na Tekno K7.

Alisema mbinu anazotumia ni kuwavizia wanafunzi wa vyuo hivyo wanapoingia madarasani na yeye anaingia kwenye mabweni na kuiba mali zao.

Alitoa wito kwa wananchi walioibiwa Tv aina ya Flat Screen, Lap top, ving’amuzi na simu kufika Kituo Kikuu cha Kati cha Polisi kuzitambua mali zao wakiwa na risiti walizonunulia.

Alisema mali hizo zilikamatwa na jeshi hilo katika msako uliofanyika maeneo mbalimbali ya mkoa huu kuanzia Januari hadi Februari, mwaka huu.


Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,

Waziri wa Madini, Doto Biteko Aitaka bodi ya STAMICO kuhakikisha Inachangia Pato la Taifa kabla ya Mwezi Juni, 2019

$
0
0
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameitaka Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Madini la Taifa (Stamico) kuhakikisha kuwa sekta ya Madini kupitia shirika hilo inaongeza mchango wake kwa pato la taifa kwa kulipa mrabaha na kodi mbalimbali za serikali na kuongeza wigo wa ajira za watanzania kwa kuzingatia maslahi mapana ya nchi katika kuendesha shirika hilo.

Ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika hilo uliofanyika katika ukumbi wa ofisi za Stamico zilizopo maeneo ya Upanga jijini Dar es Salaam mnamo tarehe 12 February, 2019.

Biteko alisema anautambua wazi umuhimu wa Bodi hiyo katika kufanya maamuzi, kupitia Sheria na sera zinazohusiana na uendeshaji wa shirika hilo na ndio maana uundwaji wa bodi hiyo ulipewa kipaumbele mara tu baada ya yeye kuteuliwa kushika wadhifa huo wa Waziri wa Madini.

Ameendelea kwa kusema, uteuzi wao haukuwa rahisi na ulizingatia uwezo na uzoefu wa wajumbe katika kutekeleza majukumu ya Bodi pamoja na uzalendo walionao kwa taifa na kuwasihi kuhakikisha wanakuwa wasimamizi wazuri wa shirika hilo kwa manufaa ya Taifa.

Alisema, kigezo kikubwa kilichotumika katika uteuzi huo ni kuangalia ubunifu wa mtu mmoja mmoja, mahali anakofanyia kazi au alipofanyia kazi, “ninyi katika ofisi mlizopita mliacha mambo makubwa Imani yetu wizara ni kuwa mtatumia ubunifu huo katika kusimamia na kubadilisha taswira ya shirika letu”. Alisisitiza.

Alikiri kuwa Serikali imewaamini na kuwapa mamlaka ya kusimamia Shirika hilo tunaamini mnaweza ndio maana katika wengi mliteuliwa  ninyi.

Akibainisha majukumu ya Bodi hiyo, Biteko alisema ni pamoja na Kuisimamia Menejimenti ya Shirika katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku kwa mujibu wa Sheria.

Kusimamia sera ya Shirika na kuanzisha mifumo ya udhibiti katika utekelezaji wa Sera hizo, Kupitia na kuidhinisha miundo ya Maendeleo ya Watumishi wa Shirika, kupitia na kuidhinisha mishahara na marupurupu ya watumishi wa shirika pamoja na kuanzisha mfumo mzuri wa kutoa gawio kwa wana hisa wa Shirika.

Aidha, Biteko alilipongeza shirika kwa hatua nzuri waliyoifikia katika kutekeleza baadhi ya miradi ikiwa ni pamoja na uchimbwaji na uuzwaji wa makaa ya mawe wa Kabulo, kuanza uchenjuaji wa mabaki ya mchanga wa dhahabu katika eneo la mradi wa dhahabu wa Buhemba, kuzalisha na kuuza kokoto Ubena Zomozi, kuimarisha usimamizi wa miradi ya ubia ya TanzaniteOne na Buckreef na kampuni tanzu ya STAMIGOLD, na kuratibu shughuli za kuwaendeleza wachimbaji wadogo.

Biteko alikiri kuwa Serikali imechoshwa na kupata hasara kupitia katika shirika hilo, na kusema badala ya miradi inayoanzishwa katika shirika hilo kuzalisha faida inazalisha madeni na kuliingizia Taifa hasara ya mabilioni ya pesa.

Akitoa mfano wa watu wawili waliokwenda vitani, mmoja akiwa na moyo wa vita bila silaha na mwingine akiwa na silaha bila moyo wa kupigana Biteko alisema ni dhahiri yule mwenye moyo wa vita atashinda na kuitaka bodi hiyo kuiga mfano huo katika kutekeleza majukumu yake.

Aliendelea kusisitiza kuwa Serikali anaamini wajumbe wa bodi hiyo wanao moyo wa kupigana vita bila kubeba silaha na kuwasihi kuanzia hapohapokutekeleza majukumu yake, “anzeni hivyo mlivyo, ipeni Serikali sababu ya kuishawishi serikali kuleta pesa”. Alisisitiza.

Serikali ya awamu ya tano inafanya vitu vilivyoshindikana, Vilee vitu ambavyo watu wanasema haviwezekani ndivyo vinavyofanyika nasi tunaamini mmeteuliwa ili kurekebisha madhaifu ya Stamico yaliyoshindikana kwa muda mrefu, wakurekebisha na kulifanya shirika la Stamico kuwa bora ni ninyi bodi pamoja na  menejimenti ya shirika.

Aidha, ameitaka bodi hiyo kumtafuta popote pale mtu yeyote wanayedhani anaweza kulisaidia Shirika kuzalisha faida na vile vile amewataka kumpeleka mtu yeyote mwenye cheo chochote anayelirudisha shirika hilo nyuma ili atafutiwe kazi nyingine ya kufanya.

“Haiwezekani shirika kutoka kuundwa kwake mwaka 1972 halijawahi kutoa gawio, haiwezekani lipo kwa ajili ya nini? Lakini watu wakizunguka wanalipwa posho lakini mwenye mali hapati kitu”. Biteko aling’aka.

Aidha, Biteko aliwataka wanabodi hao kubadilisha wimbo wa lawama unaosbabaishwa na shirika hilo na kuimba wimbo wa sifa, amekiri kutaka matokeo na sio stori. Alisema kwa namna anavyowafahamu wajumbe hao wa bodi wakishindwa kulibadilisha shirika hilo kwa awamu hii yeye binafsi atakuwa wa kwanza kuomba shirika hilo lifutwe.

Aliwataka wajumbe hao wa bodi kuifanya Stamico kuwa eneo la mataifa mengine kujifunzia namna bora ya kuendesha mashirika ya umma ikiwa ni pamoja na kuwaacha kufanya maamuzi yao kama shirika.

Alimuhakikishia Mwenyekiti wa bodi hiyo kuifanyia kazi changamoto ya uhaba wa wafanyakazi unaolikabili shirika mara tu baada ya kuurekebisha muundo wa uongozi wa shirika hilo aliokiri kuwa na vyeo vingi kulioko uwezo na uzalishaji wa shirika.

Aliitaka bodi hiyo kuhakikisha inabadilisha fikra na taswira ya shirika kwa kubadilisha namna ya kufikiri kwa watendaji wake ili wafikiri kibiashara zaidi na si kimishahara.

Alisisitiza kuwa anataka aibu ya Stamico ya miaka mingi iondolewe sasa na kama sio sasa basi sasa hivi, na kuwataka kutoa taarifa wakati wowote wanapoona wanakwama katika kutekeleza majukumu yao.

Aidha, Biteko aliitaka bodi hiyo kwenda kufuatilia suala la hisa za kampuni ya Tanzania Gemstone Industries Ltd (TGI) iliyosajiliwa mnamo mwaka 1969 ikiwa ni kampuni Tanzu ya Stamico na kutoliingizia faida yeyote shirika licha ya uzalishaji kufanyika na kuwa na umiliki wa hisa za kampuni ya Mundarara Mining Ltd kwa asilimia 50.

Alihitimisha kwa kusisitiza kuwa wizara haitaingilia masuala ya shirika lakini jicho lake litakuwa Stamico kutokana na kwamba kushindwa kwa shirika ni kushindwa kwa wizara na kushindwa kwa wizara ni kushindwa kwa Waziri kitu ambacho hatakikubali.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Mej. Gen (Mstaafu) Michael Isamuyo alitoa shukrani zake kwa uteuzi uliofanywa wa kumpatia fursa ya kuwa Mwenyekiti wa bodi hiyo ambapo alieleza kuwa aliyeteuliwa mwezi Disemba Tarehe 6 na baadaye kuteuliwa kwa wajumbe wengine wa bodi ambao amekiri watafanya kazi kubwa kwa shirika na taifa.

Alikiri kuwa wajumbe wa bodi wametoka katika maeneo mbalimbali wakiwa na ujuzi na uzoefu tofauti tofauti ambao wakikaa pamoja katika kutekeleza majukumu watafanya kitu kikubwa na kusababisha mabadiliko makubwa kwenye Shirika kubwa la Taifa la madini.

Amekiri kuwa masuala yote waliyoagizwa watatekeleza kama walivyoelekezwa “Majukumu yetu tunayafahamu lakini haya majukumu ni muongozo tu, naamini tutatumia uwezo wetu, tutatumia akili zetu, uzoefu tulionao katika maeneo mbalimbali kuhakikisha kuwa tunatekeleza majukumu yetu kwa ufanisi kuhakikisha kwamba zile changamoto ambazo zipo na zitakazoendelea kujitokeza tunazigeuza kuwa fursa na tunazitatua”. Alisisitiza.

Amesema katika ameneo yote changamoto hazikosekani, lakini kufanya kazi kwa mazoea ndiko kunakorudisha nyuma mafanikio “huu mfumo wa kufanya kazi kwa mazoea bila ubunifu wowote utaturudisha nyuma alisema na haya ndiyo masuala uliyotushauri” amekiri kuwa bodi yake ina utashi huo na watahakikisha kuwa wanakuwa na ubunifu wa hali ya juu na kuifanya Stamico kujikwamua kutoka mahali walipo.

Akijibu hoja ya kuwa na moyo wa vita kabla ya kupata silaha, Isamuyo alisema yapo matatizo mengi kwa shirika ikiwa ni pamoja na suala la uhaba wa mitaji pamoja na wafanyakazi, na kuiri kuwa kutokana na moyo wa vita walionano changamoto hizo zitageuzwa na kuwa fursa.

Akitolea mfano ujenzi wa nyumba zenye vioo zilivyowafanya wezi kuichukulia ujenzi huwa kama fursa kwa kuwarahisishia kuingia  ndani ndani ya nyumba bila shida lakini pia hiyo kuwa ni fursa kwa wajenzi na wafanyabiashara kuzalisha kuzalisha nondo na kujengea ili kuwapa wezi kazi ya kufanya pindi wanapotaka kuvamia majengo ya watu kwa lengo la kuwaibia. Isamuyo ameahidi kugeuza changamoto za Stamico kuwa fursa na kulipeleka shirika mbele.

Amemuhakikishia Waziri wa Madini kuwa bodi hiyo haitashindwa kazi, “Hatutashindwa kwa sababu hamkushindwa kututeua, mlikuwa na majina mengi yenye sifa zinazofanana na zetu lakini hamkushindwa kututeua na kwa sababu ninyi hamkushindwa kututeua na sisi hatutashindwa kuhakikisha kwamba tunasonga mbele katika kutekeleza majukumu ya shirika” alisisitiza .

Amekiri kwamba kabla ya kuomba silaha ya mizinga sehemu yeyote tutahakikisha kwamba silaha ndogo zitafanya kazi na kuhakikisha adui anapigwa, amesema watumishi waliopo lazima wahakikishe kuwa wanafanya kazi na kuliletea shirika faida bila kutegemea mtu kutoka eneo lingine. Alisema waajiliwa wengine wakipatikana waje kuongeza nguvu lakini si kwa sababu waliopo wameshindwa kazi.

Kuhusu Mikataba isiyokuwa na tija, Isamuyo amewataka wanasheria kuhakikisha mikataba inayoingiwa sasa hivi inazalisha faida tofauti na ilivyokuwa awali.

Kuhusu agizo la kuhakikisha shirika linatoa gawio kwa serikali, Isamuyo amesema agizo hilo limetolewa kwa mwanajeshi, hilo ni agizo na litatekelezwa vizuri sana na kuahidi kufuatilia suala la kushughulikia hisa za kampuni ya Tanzania Gemstone Industries Ltd(TGI) ambayo ni kampni tanzu ya Stamico itashughulikiwa ipasavyo.

Ameiomba serikali kushughulikia changamoto za msingi na masuala mengine yanayopaswa kutatuliwa na wizara kufanyiwa maamuzi mapema ikiwa ni pamoja na suala la ajira mpya na kukiri kuwa shirika ni la kibiashara hivyo kila dakika inayopotea inazalisha hasara kwa shirika.

Uzinduzi wa Bodi hiyo ulishirikisha viongozi wote waandamizi wa wizara ikiwa ni pamoja na Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo aliyewataka Bodi hiyo kwenda kufanya kazi na kuithibitisha Imani ya serikali kwao, Katibu Mkuu wa Wizara, Prof. Simon Msanjila pamoja na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Issa Nchasi.

Mwigulu Nchemba asimulia punda walivyosababisha Apate Ajali

$
0
0
Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba, amesema chanzo cha ajali aliyopata ni dereva kukwepa punda watatu.

Ajali hiyo ilitokea leo Jumatano Februari 13, katika eneo la Migori Mkoani Iringa akiwa safarini kuelekea Singida kuhudhuria kikao cha kamati ya siasa ya mkoa.

“Punda walikuwa wanavuka barabara sasa dereva wangu akajaribu kuwakwepa lakini ikashindikana, baada ya hapo nilisikia kishindo kikubwa na moshi umetanda ndani ya gari, ilikuwa imepinduka.

“Wasamaria wema wakaja kutuchukua na kutuleta hapa hospitalini, lakini namshukuru Mungu kutoka mzima kwani mkanda ulikuwa umenibana sana,” amesema. 

Mwigulu amelazwa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma akiendelea na matibabu.

Nkoma: Tiba Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
NKOMA
_________________________
NKOMA Ni dawa bora ya nguvu za kiume  yenye mchanganyiko wa mitishamba (7) yenye maajabu yafuatayo/

🔖 (1) inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimalisha misuli ya uume uliolengea wakati wa tendo la ndoa/
🔖 (2) Kurefusha maumbile ya kiume yaliyorudi ndani kuazia nchi 5 - 9/
🔖 (3) kunenepesha uume cm 5 ya upana itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15 - 20 kwa tendo la kwanza na utakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya 2-4 bila hamu kuisha/

📌 Na inatibu kabisa, unashauriwa uitumie dawa hii kama kinga ya magonjwa sugu./
 📌 Haijalishi umri hata kama una miaka 85 itumie huanza kufanya kazi dk 50 tu na haina madhara yoyote kwa mtumiaji/

📍📍📍📍📍📍📍📍📍
            MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA.
_________________________
🔖 (1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖 (2)Choo kama cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(4)Kaswende/
🔖(5)Gono/

📌Haya yote husababisha kuishiwa nguvu za kiume na kuwa na uume mdogo/
📌 Itumie leo, bado hujachelewa ni tofauti na nyingine.
_________________________
DR MAKOBA ANAPATIKANA DAR ES SALAAM, PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
___________________________
WASILIANA NA
Dr MAKOBA SIMU.
📞0754832349
📞0683490600
____________________________
*****************************

Upelelezi Kesi Ya Wema Sepetu Wakamilika

$
0
0
Upelelezi wa kesi ya kuchapisha video ya ngono kupitia ukurasa wa Instagram inayomkabili Msanii wa Filamu, Wema Sepetu, umekamilika na itaanza kusikilizwa Februari 21, mwaka huu baada ya kusomewa maelezo ya awali.
 
Hayo yameelezwa na Wakili wa Serikali, Glory Mwendi mbele ya Hakimu Mkazi Maira Kasonde.

Wakili Glory ameeleza kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na anaomba tarehe kwa ajili ya kumsomea mshtakiwa maelezo ya awali.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Kasonde ameahirisha kesi hiyo hadi February 21, 2019

Katika kesi hiyo namba 322 ya mwaka 2018, Wema anadaiwa Oktoba 15 katika maeneo tofauti ya jiji la Dar alichapisha video za ngono kupitia ukurasa wake wa Instagram wakati akijua ni kinyume na sheria.

Super Mkongo: Kiboko ya Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
********************************
SUPER MKONGO MPYA,
_______________________________
********************************
Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile,

- kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa
- maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo
- kukosa hamu ya tendo la ndoa
- kushindwa kurudia tendo la ndoa
- uume kusimama kwa kulegea
- uume kulegea katikati ya tendo
- kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu
- kuishiwa nguvu kutokana na punyeto.

Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MCONGO MPYA, kiboko ya matatizo haya.
_______________________________
Pia kuna MCONGO POWER Kiboko ya uume mdogo inaboresha maumbile ya uume kwa kurefusha na kunenepesha kwa saizi uipendayo haijalishi umri hata kwa walioathirika na upigaji punyeto.
_______________________________
Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume na uume mdogo.
_______________________________
(1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea.
(2) ngiri
(3) kuugua chango la uzazi kwa muda mrefu.
(4) kupungukiwa hormone za testosterone.
(5) ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na visivyo na virutubisho  vya kutosha.
(6) kutokufanya mazoezi na mwenendo wa maisha.
(7) kisukari.
(8) tumbo kuunguruma na kujaa gesi.
(9) maumivu ya kiuno nk.
_______________________________
Kwanini uhangaike? Kwanini uhuzunike?
Hii ni spesho kwa waliotumia madawa mengi bila kufanikiwa hakika hautajuta kuitumia. _______________________________
WASILIANA NA:
DR. MCONGOMANI
SIMU NO:
📞0658816558
📞0682323682
Popote ulipo huduma hii inakufikia
_______________________________
********************************

Godzilla alioneshwa kifo chake siku 3 zilizopita, aacha ujumbe mzito twitter

$
0
0
Msanii Godzilla ambaye amefariki dunia alfajiri ya leo, alizungumza juu ya kifo chake siku chache zilizopita, kwenye mtandao wa twitter ambao alikuwa akipenda sana kuutumia.

Kwenye ukurasa wake mnamo februari 9, Godzila aliandika ujumbe kuwa hata kama akifa, jina lake litaendelea kubaki kwa watu, jambo ambalo limetafsiriwa kama alikuwa anakaribia kufikwa na umauti.
Godzilla aliendelea kutumia ukurasa huo mpaka jana saa 9 alasiri, ambapo alitweet ujumbe wake wa mwisho, ambao ulisomeka hivi.

Mawaka ATCL Kuendelea Kusota Rumande

$
0
0
Mawakala 10 wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) wanaokabiliwa na mashtaka matatu ikiwemo kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu Sh10,874,280 kwa lengo la kuwakatia watu tiketi za ndege za shirika hilo wanaendelea kusota rumande kutokana na upelelezi kutokakamilika.

Washtakiwa katika kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba 97 /2018 ni Fabian  Ishengoma (34), Adamu Kamara(27), Mlon  Masubo(29),  Alexander Malongo(24).

Wengine ni Tunu Kiluvya (32), Jobu Mkumbwa(30), Mohamed Issa (38), Godfrey Mgomela, Absalom Nyusi na Janeth Lubega(24).

Wakili wa Serikali, Janeth Magoa amedai leo Jumatano Februari 13, 2019  mbele ya hakimu mkazi mkuu, Salum Ally kuwa shauri hilo limekuja kwa ajili ya kutajwa na upelelezi haujakamilika.

Wakili Magoa ameiomba mahakama hiyo ipange tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa na hakimu Ally ameahirisha hadi Februari 26, 2019.

Washtakiwa wote wamerudishwa rumande kutokana na shtaka la utakatishaji kutokuwa na dhamana.

Mkurabita Inatekeleza Kwa Vitendo Dira Ya Maendeleo Ya Taifa 2025

$
0
0
Na Ismail Ngayonga-MAELEZO
KATIKA kipindi cha miaka minne (2005 – 2008) uchumi wa Tanzania umeendelea kuimarika na Pato la Taifa lilikua kwa wastani wa asilimia 7.2 kwa mwaka kuongezeka kutokana na shughuli za kiuchumi katika sekta za viwanda, ujenzi na fedha.

Pamoja na mwaka 2009 kuwa ni mwaka ambao kasi ya ukuaji wa Pato la Taifa inatarajiwa kupungua kutokana na athari za msukosuko wa uchumi wa dunia, takwimu za Pato la Taifa kwa robo mwaka zinaonesha kuwa, katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka (Januari – Machi 2009) uchumi wa Taifa ulikua kwa asilimia 5.6 ikilinganishwa na asilimia 6.2 katika kipindi kama hicho mwaka 2008.

Ingawa uchumi wa Tanzania umekuwa ukikua katika siku za hivi karibuni matokeo ya ukuaji huo wakati mwingine hayawafikii watu masikini katika jamii ikiwa na ina maana kuwa kasi ya upunguzaji umasikini bado hairidhishi.

Serikali imeanzisha sera na programu kadhaa zenye lengo la kukuza uchumi na kupunguza umasikini kwa kupanua ushiriki wa Watanzania wote katika shughuli za kiuchumi.

Sera ya Uwezeshaji Kiuchumi ndiyo msingi wa juhudi hizo za Serikali, ikiwa na malengo ya kuwawezesha Watanzania kumiliki, kuendesha na kunufaika na uchumi wao wenyewe ikiwa ni pamoja na kuondoa baadhi ya vikwazo vinavyowakabili Watanzania katika shughuli za kiuchumi.

Moja ya mawazo ambayo Serikali iliyazingatia kama mbinu rahisi ya kupanua ushiriki wa Watanzania katika uchumi ni pamoja na kuwaingiza watu wengi zaidi katika uchumi rasmi na wenye kutumia kumbukumbu.

Miongoni mwa programu hizo ni pamoja na Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara Tanzania (MKURABITA) ulioanzishwa na Serikali kwa lengo la kuhakikisha kuwa biashara na rasilimali za wanyonge zilizo kwenye sekta isiyo rasmi zinarasimishwa kuziwezesha kutambulika kisheria.

Akiwasilisha Hotuba ya Makadirio ya Bajeti ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2018/19, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika anasema Serikali imeendelea kutekeleza jukumu la kuandaa na kusimamia mfumo wa Kitaifa wa umiliki wa rasilimali na uendeshaji wa biashara nchini unaotambulika na kukubalika kisheria.

Anaongeza kuwa katika kipindi cha mwaka 2017/18, MKURABITA imefanikiwa kuwajengea uwezo Wakulima 589 na viongozi 89 jinsi ya kutumia hati za haki Miliki za Kimila kupata Mitaji katika Benki na Taasisi zingine za Fedha katika Halmashauri za Wilaya za Misungwi, Mpwapwa na Serengeti.

Waziri Mkuchika anasema MKURABITA kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Urambo imefanikisha kuanzishwa kwa Kituo Kimoja cha Urasimishaji wa Biashara, ambapo huduma muhimu  ikiwemo utoaji wa namba ya utambulisho wa mlipa kodi (TIN), usajili wa jina la biashara (BRELA) na utoaji leseni za biashara zinapatikana sehemu moja.

“Hadi kufikia Machi, 2018 Kituo kimesajili biashara 380 ambapo Shilingi milioni 4.5 zimekusanywa kutokana na ada za leseni na wafanyabiashara 79 wamepata leseni na 200 wamefungua akaunti katika benki kwa ajili ya kuweka akiba na kukopa fedha” anasema Waziri Mkuchika.

Kwa mujibu wa Waziri Mkuchika anasema MKURABITA pia imefanikisha kutoa mafunzo ya urasimishaji na uendeshaji wa biashara kwa Wafanyabiashara 100 katika Wilaya za Kusini Unguja (50) na Micheweni, Pemba (50) ambapo wafanyabiashara 10 wamesajili Majina ya Biashara na kupata Leseni za kuendesha Biashara.

Akifafanua zaidi Mkuchika anasema MKURABITA pia iliwezesha Wafanyabiashara 13 waliorasimisha biashara zao Unguja na Pemba kushiriki kwenye Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki yaliyofanyika Nchini Burundi mwezi Desemba, 2017.

Mkuchika anasema MKURABITA Kwa kushirikiana na Ofisi za Taifa za Takwimu Tanzania Bara na Zanzibar, imeanza kufanya utafiti kuhusu Sekta isiyo Rasmi nchini kwa lengo la kubaini ukubwa na thamani ya Sekta isiyo, ambapo utafiti wa Majaribio umefanyika katika Mikoa sita (6) ya Tanzania Bara na miwili (2) Zanzibar.

Anaitaja Mikoa hiyo kuwa ni Dar es Salaam, Dodoma, Mbeya, Mtwara, Mwanza, Tanga, Mjini Magharibi na Kusini Pemba na utafiti huo ulilenga kuona kama methodolojia, sampuli na madodoso yaliyoandaliwa yanaweza kuleta matokeo tarajiwa juu ya ukubwa wa Sekta isiyo Rasmi kwa sasa.

Naibu Waziri wa Fedha : Fedha Za Maboresho Ya Shule Kongwe Zitumike Kwa Lengo Lililokusudiwa Na Kwa Ubora

$
0
0
Na Peter Haule, WFM, Korogwe
Serikali imewataka watendaji katika maeneo yote ambayo fedha zimetolewa zikiwemo sh. bilioni 18 za kuboresha shule kongwe nchini, kusimamia matumizi yake ipasavyo ili kufikia lengo lililokusudiwa na kwa ubora unaotakiwa.

Agizo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji, alipotembelea na kukagua maboresho ya Shule Kongwe ya Sekondari ya Wasichana Korogwe, Mkoani Tanga, ambayo hivi sasa imekuwa ya kisasa na mwonekano mzuri.

Dkt. Kijaji alisema kuwa Serikali imeamua kutekeleza kazi zake nyingi kwa mfumo ujulikanao kama Force Account, ambao unatoa fursa kwa Wakandarasi wazawa kushiriki kikamilifu kwa lengo la kufanikisha maendeleo kwa gharama nafuu na kwa ubora unaotakiwa.

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Korogwe, Bi. Annisia Mauka, katika taarifa ya utekelezaji wa maboresho ya shule hiyo, alisema,   Serikali, kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) iliwapatia kiasi cha  Sh. bilioni1.3 kwa ajili ya kujenga miundombinu 27 ya Shule, ikiwemo umeme, majisafi na taka na pia Mfumo wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).

“Tumefanikiwa kukarabati majengo 26 ambayo ni pamoja na  vyumba vya madarasa 23,  maabara, maktaba, jengo la utawala, mabweni, bwalo la chakula, vyoo vyenye matundu 116, jengo la Zahanati, Mfumo wa Maji taka na safi na pia mfumo wa kupikia kwa njia ya nishati ya gesi” alifafanua Bi. Mauka.

Alisema kuwa hadi sasa fedha zilizotumika kununulia vifaa ni takribani Sh. bilioni 1.05 huku gharama za ufundi zikiwa Sh. milioni 315.9 hivyo kusalia na zaidi ya Sh. milioni 2.09.

Bi. Mauka, ameiomba Serikali kufanikisha ujenzi wa Bweni jipya linalogharimu zaidi ya Sh. milioni 109.6 kwa kuwa Bweni hilo lilishindikana kufanyiwa maboresho kwa kuwa uharibifu wake ulikua mkubwa baada ya kufanyiwa tathmini ya kina, pia aliiomba Serikali kufanikisha ujenzi wa ukuta wa Shule hiyo kwa kuwa kukosekana kwa ukuta huo kunahatarisha usalama wa wanafunzi na watumishi wengine.

Naibu Waziri Dkt. Kijaji, ameahidi kufanyia kazi maombi hayo kwa kushirikiana na Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mhe. Mary Chatanda, na kutoa agizo kwa Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, kufanya tathmini ya gharama ya ukuta huo ili kujua gharama halisi  kwa lengo la kupata fedha za ujenzi ili kulinda usalama wa Wanafunzi.

Dkt. Kijaji, aliupongeza Uongozi wa Shule na Wadau wengine kwa kuwezesha ukarabati Mkubwa wa Shule hiyo hivyo kurudisha hadhi yake na kuwa sehemu bora ya wanafunzi kupata taaluma kwa viwango vya juu.

Akizungumza na wanafunzi wa Shule hiyo Dkt. Kijaji aliwataka kusoma kwa bidii ili kuweza kufaulu masomo yao na kuwa chachu ya maendeleo ya Taifa na pia kuwa viongozi imara wa baadae.

Jumla ya Sh. bilioni 18 zimetolewa na Serikali kwa ajili ya ukarabati wa Shule Kongwe za Sekondari 17 kuanzia mwaka wa Fedha 2016-217.

Mwisho.

Je Kwanini Baadhi Ya Wanaume Wengi Wana Ukosefu Ama Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
JE KWANINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA UKOSEFU AMA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO ???

Pata sululisho la matatizo haya na  magonjwa mengine utapona kwa mda mfupi sana hatakama ulihangaika mpaka ukakata tamaaa 

GALIMBO 3 MIX  ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa aina mbili ili kukidhi mahitaji ya mtumiaji, imetengenezwa kwa muundo wa vidonge pamoja na unga kwaajili ya kuponesha tatizo moja kwa moja , huimalisha misuli ya uume iliyolegea wakato wa tendo la mdoa ,na kukufanya ucherewe kufika kileleni kwa mda wa dk ( 20 - 45 ) itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu nira hamu kuisha wara kuhisi kuchoka vilivile huzalisha viini vya uzazi ( manii ) 

YOLAN  hurefusha na kunenepesha  maumbile madogo ya uume na kuwa na uume kuanzia nchi (6-8) tiba kwa mda mfupi sana

Zipo sananu nyingi sana zinazosababisha matatizo hayo  km vile -:punyeto, kisukali,ngili,chango,vidonda vya tumbo,  tumbo kuunguluma na kujaa gesi maumivu ya mgongo ama kiume ,kolodani moja kuvimba ama kuingia ndani  presha nk 

Matatizo haya yote sio mageni, kigeni ni tiba sahihi ya kuponesha matatizo hayo

SUPER MBUKE -:  nidawa ya kuponesha tatizo la kisukali kwa mda mfupi sana , usihangaike wara kuteseka tumia dawa ya mitishamba kwaajili ya tatizo hili na upone kabisa

NTINJIWA  nidawa ya mvuto wa biashara,kazi, kupandishwa cheo,kumfanya mfanyakazi apendwe na bos wake

Pia ninadawa za kumvuta mme , mke,mchumba,hawara, au mtu yoyote unaemuhitaji katika maisha yako hata km yupo mbali na atatulia na kukutimizia cjovjote utakacho na kumfunga asiwe na mtu mwingime ,

Pata tiba za magonjwa mbalimbali ikiwemo miguu kuwaka moto, mgongo,bawasili ,kaswende ,gono na mengine mengi

KWAUSHAULI NA TIBA WASILIANA NA DR CHIKAGO    0759 208 637

Km huna nafasi ya kufika ofisini hudumahii utaletewa hapo ulipo , kwa wale wa mikoani natuma kwanjia ya basi

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro Asema Njombe iko Shwari Kabisa kwa Sasa

$
0
0
MKUU  wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro amewataka wananchi mkoani Njombe kuendelea na shughuli zao za kila siku kwa kuwa mji huo uko shwari.

IGP Sirro ametoa wito huo leo Jumatano 13, 2019 katika mahojiano ya Kipindi cha Jambo Tanzania kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC). Amesema kuwa ulinzi umeimarishwa mkoani humo hivyo wananchi waendelee na shughuli zao za kila siku bila wasiwasi.

 “Njombe ni shwari na itaendelea kuwa shwari, Watanzania wenzangu fanyeni kazi zenu maana tumetawanya polisi wa kutosha. Mzazi huna sababu ya kuhangaika kumpeleka mtoto shuleni, niwahakikishie kuwa mambo yako vizuri,” amesema Sirro

Amesema kuwa waliofanya mauaji hayo wameshakamatwa na watapelekwa mahakamani

 “Waliofanya matukio ya mauaji Njombe wote wamekamatwa, wengine utaona ilikuwa ni ugomvi wa familia, mtoto akaona baba mdogo ananichukia ngoja niue watoto wake, akaua watoto watatu” amesema Kamanda Sirro.

“Huyo mwingine anasema amepewa uchawi na babu yake, kwa hivyo anapata maluweluwe, huyu amekamatwa, akipata maluweluwe anajisikia anataka damu na anaua watoto. Ukiangalia matukio haya yanaanzia kwenye familia,” amesema.

Amesema hata mauaji ya watoto yaliyoripotiwa kutokea mkoani Simiyu yanahusiana na imani ya kishirikina.

 “Lakini pia hata hii ya Simiyu (mauaji) tumeshatuma watu wetu kule na yenyewe yameshaonekana ni ya kishirikina, tumewaomba watu wa Simiyu watupe taarifa ili tuwashughulikie,” amesema.

Dada afunguka alichoambiwa na Godzilla Dakika chache kabla ya kufariki Dunia

$
0
0
Dada wa msanii Godzilla, Joyce Mbunda, amefunguka juu ya kile alichoambiwa na marehemu Godzila, wakati umauti ukimkuta

Joyce amesema wakati umauti ukimkuta mdogo wake, yeye na mama yake walikuwa wamemshika baada ya kumuona anatapatapa, na ndipo alipomwambia dada yake asimuachie kwani kuna watu wanamfuata.

“Alinifuata chumbani kwangu akaniambia, sister naomba nilale hapa kidogo, maana kule kuna watu, watu wengi sana wananifuata, na mimi sitaki, nikamuacha alale

"Dakika kumi hazijafika akatoka ananiambia naenda nje, nikamwambia twende wote, mama akamshika na mimi nikamshika, tunamzuia atulie maana anahangaika, tulivyomshika analegea huku anakaa chini, alikuwa ananiambia cha tu sister, nimemshikilia hivi, namwambia niambie kitu, anashindwa hata kuzungumza, mpaka analegea yuko mikononi mwangu”, amesema Joyce.

Joyce ameendelea kwa kusema kwamba Godzilla alikuwa mtu mwenye upendo, na mtu ambaye alikuwa karibu sana na familia yake.

Godzila amefariki alfajiri ya leo baada ya kuzidiwa, kutokana na maradhi ya sukari na presha iliyokuwa ikimsumbua.

Upelelezi kesi walioghushi saini ya Makamba haujakamilika

$
0
0
Upelelezi wa kesi ya  kughushi saini ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Muungano na Mazingira), January Makamba inayowakabili wafanyakazi sita wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) bado haujakamilika.

Mbali na kughushi washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka mengine ikiwemo kula njama, kughushi, kuwasilisha nyaraka za uongo, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kusababisha hasara ya Sh160milioni.

Mwanasheria wa Serikali, Jenipher Masue leo Jumatano Februari 13, 2019 mbele ya hakimu mkazi mwandamizi, Augustina Mmbando  ameeleza upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilia.

Washtakiwa katika kesi hiyo ni ofisa mazingira NEMC, Deusdith Katwale;  mtaalamu wa Tehama, Luciana Lawi; ofisa mazingira Magori Wambura; katibu muhtasi, Edna Lutanjuka; msaidizi wa  wa ofisa Mwaruka Mwaruka na ofisa mazingira baraza hilo, Lilian Laizer.

Wafanyakazi hao walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu  Oktoba  31, 2018 na kusomewa mashtaka sita ya uhujumu uchumi likiwamo la kughushi saini ya  Makamba katika vyeti vya tathmini ya uharibifu wa mazingira.

Katika kesi hiyo mshtakiwa namba moja ambaye ni Wambura anaendelea kusota rumande baada ya kukosa dhamana na washtakiwa wengine watano wako nje kwa dhamana.

Hakimu Mmbando ameahirisha kesi hiyo hadi Februari 27, 2019 itakapotajwa.

Muswada bima ya afya kuwasilishwa bungeni Aprili, 2019

$
0
0
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amesema muswada wa sheria ya bima ya afya kwa wote unatarajiwa kuwasilishwa bungeni Aprili, 2019.

Ummy ameyasema hayo leo Jumatano Februari 13, 2019 katika kikao cha pamoja kati ya wizara hiyo, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa afya kutoka ndani na nje ya nchi.

Amesema lengo la Serikali ni kuwafikia Watanzania wote na kuwaingiza katika mfumo huo ili kufikia lengo la dunia namba tatu.

“Hatua ya majadiliano ndani ya Serikali imekamilika, tunatarajia kupeleka muswada bungeni mwezi Aprili,  kuwa ni lazima kwa kila Mtanzania kuwa na bima ya afya. Tukiwa na wananchi wengi waliojiunga na mifuko ya Bima ya Afya tutaweza kutoa huduma za afya kwa ufanisi zaidi,” amesema Ummy.

Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Anna Makinda amesema hatua hiyo itasaidia kuondoa maswali mengi yanaulizwa mara kwa mara na wachangiaji wa mfuko huo.

John Kadatu, akizungumza kwa kwa niaba ya mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii,  Peter Serukamba, amesema ushiriki wao katika mjadala huo wa pamoja utawasaidia kupata uelewa ili waweze kupitisha vifungu vya sheria ya masuala ya bima itakapofika bungeni.

“Tumetembelea nchi nyingi zilizofanikiwa katika mpango huu ikiwemo Ethiopia, Ghana na kwingineko tumejifunza mengi, tupo tayari kuisaidia Serikali na tuliyoyapata yatatusaidia wakati wa kupitisha vifungu kwa vifungu,” amesema Kadutu.

Serikali Yaanzisha Huduma Za Kibingwa Matibabu Ya Moyo Dodoma

$
0
0
Na WAMJW – Dodoma.
Katika azma ya kuboresha huduma za kibingwa za matibabu, Serikali kupitia Hospitali ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma imeanzisha huduma za matibabu ya moyo kwenye maabara ya uchunguzi na tiba ya magonjwa ya moyo kwa kutumia mashine maalum (Cathlab).

Maabara hiyo ya tatu nchini na ya pili kwenye taasisi ya serikali inatarajiwa kutoa huduma za uchunguzi na tiba ya magonjwa ya moyo ndani ya muda mfupi hivyo kuhudumia wagonjwa wengi ndani ya muda mfupi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa maabara hiyo, mgeni rasmi Waziri Ummy Mwalimu amesema kuwa kufunguliwa kwa maabara hiyo ni mafanikio makubwa kwa serikali katika kusogeza huduma za kibingwa karibu na wananchi hivyo kupunguza idadi ya wagonjwa waliokuwa wakisafiri kwenda mbali kufuata huduma za matibabu.

“Huduma za kibingwa zimepunguza idadi ya wagonjwa waliokuwa wanasafiri au kupelekwa nje ya nchi kwa ajili ya matibabu kwa asilimia 95 kutokana na uboreshaji wa huduma za afya ndani ya nchi” amesema Waziri Ummy Mwalimu.

Waziri Ummy Mwalimu amesema kuwa Serikali imekuwa ikiwajengea uwezo wataalam wa afya nchini ili waweze kutoa huduma bora kwa wananchi jambo ambalo limezaa matunda kwa kuwa wagonjwa wengi hivi sasa wanapata matibabu ndani ya nchi.

Hata hivyo Waziri Ummy ametoa ufafanuzi wa upatikanaji wa rufaa ya matibabu nje ya nchi na kusema kuwa Serikali haijazuia rufaa za matibabu nje ya nchi bali ni lazima kujiridhisha kwanza huduma za matibabu hazipatikani hapa nchini kabla ya kutoa rufaa.

“Hakuna daktari tuliyemkataza kutoa rufaa nje ya nchi, sasa hivi tuna uwezo wa kutoa huduma za matibabu ya kibingwa ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni lazima daktari awe amejiridhisha na kuthibitisha kwamba matibabu hayo hayapatikani hapa nchini kabla ya kutoa rufaa” alisema Waziri Ummy Mwalimu.

Waziri Ummy ameupongeza uongozi wa Hospitali ya Benjamin Mkapa na Taasisi ya Jakaya Kikwete kwa kuwa wabunifu na kushirikiana kutoa huduma bora za matibabu ya moyo kwa wananchi na kuzitaka hospitali na taasisi nyingine za afya kuiga mfano wao katika kuboresha huduma za afya nchini.

Katika hatua nyingine Waziri Ummy amewataka wananchi kujiunga na Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya ili waweze kupata bima ya afya ambayo itawasaidia kupata huduma za matibabu kwa uhakika. Waziri Ummy amesema kuwa ni muhimu kwa watanzania kuwa na bima ya afya ambayo itawapunguzia gharama za matibabu huku akiwataka wananchi kujiwekea malengo na kukata bima ya afya ambayo gharama zake ni nafuu.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula amesema kuwa ipo haja ya kuwathamini madaktari wazalendo ambao wamekuwa wakijitoa kuokoa maisha ya wagonjwa. Dkt Chaula amesema kuwa Serikali itaendelea kuwekeza katika wataalam wa afya nchini ili kuweza kuwa na madaktari bingwa wengi wanaotoa huduma za kibingwa hapa hapa nchini pamoja na kuwekeza kwenye miundombinu na vifaa.

Awali akitoa salamu zake, Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Bakari Kambi, ametoa rai kwa wananchi kuzingatia mtindo bora wa maisha, kufanya mazoezi na kula chakula bora ili kuepukana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza yakiwemo kisukari, presha na shinikizo la damu.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa Dkt. Alphonce Chandika amesema kuwa maabara hiyo imegharimu kiasi cha Tsh Bilioni 5 na inatarajiwa kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo hivyo kupunguza adha ya wagonjwa kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za matibabu ambapo awali zilikuwa zikipatikana Dar Es Salaam kwenye Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete pamoja na Hospitali nyingine moja isiyo ya kiserikali.

Dkt. Chandika amesema kuwa wataendelea kushirikiana na wataalam kutoka Taasisi ya Moyo ya jakaya Kikwete ili kuweza kutoa huduma bora kwa wananchi huku akiiomba serikali kuongeza wataalam ili kuboresha zaidi upatikanaji wa huduma za afya.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi amesema kuwa hadi kufikia jioni jumla ya wagonjwa 13 kutoka Dodoma na mikoa ya jirani tayari walishakuwa wamefanyiwa uchunguzi katika maabara hiyo ambapo kati yao  wagonjwa wanne wakitakiwa kwenda JKCI kwa uchunguzi na tiba zaidi.

Aidha Prof. Janabi alitumia nafasi hiyo kuishukuru Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa kuwapa nafasi na heshima kubwa ya kuja kushirikiana katika kutoa huduma za matibabu kwa wananchi.

Kangi Lugola aagiza mkurugenzi kampuni ya Ortello Business Cooperation(OBC) ya Falme za Kiarabu kukamatwa

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola ameagiza mkurugenzi wa kampuni ya wawekezaji kutoka falme ya Kiarabu ya Ortello Business Cooperation(OBC), Isack Mollel kukamatwa kwa tuhuma za kuwaingiza nchini  wafanyakazi wa kigeni bila kufuata taratibu.

Lugola ametoa agizo hilo leo Jumatano Februari 13, 2019  katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Arusha.

Amemuagiza kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Longinus Ribishumbwamu kumsaka mkurugenzi huyo kabla hajamaliza ziara yake jijini Arusha.

Amesema mkurugenzi huyo alitakiwa kujisalimisha polisi tangu wiki iliyopita sambamba na wafanyakazi 10 wa kampuni hiyo, waliokuwa wameingia nchini kinyume cha sheria ambao tayari wamefikishwa mahakamani na kesi yao itatajwa tena Februari 22, 2019.

"Kazi ambazo walikuja kufanya wafanyakazi hao zinaweza kufanywa na Watanzania hivyo kisheria hawakupaswa kuja nchini kufanya bila kufuata utaratibu,” amesema.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images