Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya February 13


Serikali Yaahidi Kuendelea Kushirikiana Na Halotel.... Yaipongeza kutimiza ahadi ilizozitoa kwa serikali.

$
0
0
Kwa kutambua umuhimu na ukuaji wa sekta ya mawasiliano nchini Tanzania, serikali imeiahidi kampuni ya mawasiliano ya Halotel kuendelea kushirikiana nayo katika kutatua changamoto wanazozikabili kwa pamoja.

Hayo yalisemwa wakati wa ziara maalum ya Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Atashasta Nditiye wakati alipoitembelea kampuni hiyo ili kujua shughuli wanazozifanya katika kuwahudumia wateja pamoja na changamoto wanazokumbana nazo kila siku.

“Lengo la ziara hii ni kuja kuwasikiliza, kujua shughuli mnazozifanya pamoja na changamoto mnazokumbana nazo. Serikali inatambua ukuaji na umuhimu wa sekta ya mawasiliano katika kuchangia uchumi. Na wadau wakubwa katika sekta hii ni makampuni ya simu kama Halotel. Hivyo hatuna budi kuyatembelea, kuongea nayo, kuyasikiliza na kushirikiana nao wapi tufanye kipi kama serikali katika sekta nzima ya mawasiliano. Ningependa kuwatoa hofu kwamba kama serikali tuko pamoja nao,” alisema Mhandisi Nditiye.

“Serikali inatambua sana mchango wa makampuni ya simu na ndiyo maana tumeamua kuwatembelea ili kujua shughuli wanazozifanya. Kwa mfano, mbali na kuzungumza na kusikiliza changamoto zao lakini nimepata fursa ya kutembelea kitengo chao wanacho hudumia wateja, mitambo na kitengo chao wanakitumia kufanyia huduma za kifedha. Nimezisikiliza changamoto zao na ninaahidi kwenda kuzifanyia kazi,” alihitimisha Mhandisi Nditiye.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halotel Nguyen Van Son, aliezea mafanikio ambayo kampuni yake imeyafikia mojawapo ikiwa ni ahadi ilizozitoa kwa serikali katika utoaji wa huduma nchini.

“Katika utoaji wa huduma za mawasiliano Tanzania tulitoa ahadi kadhaa kwa serikali na ningependa kuchukua fursa hii kuifahamisha serikali kuwa tumetekeleza kwa kiasi kikubwa. Tuliahidi kutoa huduma za mtandao wa intaneti katika shule 450 na tumevuka lengo kwa 455. Tuliahidi kutandaza kebo za huduma ya intaneti katika ofisi za mabaraza ya wilaya 150 na tumefanikiwa kwa kufikia ofisi 147. 

"Pia kusambaza miundombinu ya mawasiliano ya fibre katika hospitali za wilaya 150 na tumefanikiwa zote 150. Tuliahidi kusambaza miundombuni ya mawasiliano ya fibre kwa vituo vya polisi vya wilaya 150 na tumefanikiwa 121. Lakini pia, tuliahidi kusambaza miundombinu ya mawasiliano ya fibre katika vituo vya ofisi za posta za wilaya 65 na tumevuka kwa kufunga 66,” alisema na kuongezea Son.

Licha ya mafanikio hayo ambayo Halotel imeyafanikisha kwa kutimiza ahadi ambazo iliipatia serikali, kampuni hiyo ilielezea changamoto kadhaa inazokumbana nazo.

“Ili kutimiza dhima yetu ya kuhakikisha kila Mtanzania anafikiwa na huduma za mawasiliano kwa bei nafuu lakini pia tunakumbwa na changamoto kadhaa. Mojawapo ni pamoja na kuharibiwa kwa mifumo yetu ya miundombinu ya mawasiliano na baadhi ya wananchi ambao sio waaminifu katika baadhi ya mikoa. 

"Vitendo hivi si tu vinakwamisha juhudi zetu za kufikisha mawasiliano katika kila pembe ya nchi lakini pia inawazuia wananchi kufikiwa na huduma zetu hivyo kukwamisha shughuli za mawasiliano na uchumi. Tungeomba katika hili serikali kushirikiana nasi ili kuzuia vitendo hivi vya kihalifu na kujenga hamasa juu ya umuhimu wa mitambo hii,” aliongezea Son.

“Pia tunaiomba serikali kushirikiana na Halotel katika kupambana na changamoto ya wizi wa mitandaoni. Kama mnavyojua huduma za mawasiliano hususani huduma za fedha kwa njia ya simu za mkononi yanatumika kwa kiasi kikubwa katika kurahisisha shughuli mbalimbali. 

"Wahalifu wa mitandaoni nao wanaoitumia fursa hii kuwalaghai wateja hivyo kuvunja uaminifu baina yetu. Halotel inapendekeza kuwepo na ushirikiano na serikali katika kulikabili hili na kulitatua kwa pamoja. Tunapendekeza kuwepo kwa vikao, semina au warsha za mara kwa mara ili kupanga mikakati na kumaliza kabisa changamoto hii,” alihitimisha Son.

Super Mkuyati: Tiba Sahihi ya Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
ASILIMIA 45-88 YA WANAUME WAPO TOFAUTI NA WENGINE KUTOWATIMIZIA NYEMA WAKE ZAKE ZAO AU WAPENZI WAO SUPER MKUYATI NI TIBA YA MARADHI YAKO
------------------
SUPER MKUYATI; nidawa  iliyo katika mfumo wa vidonge  na  unga , inapambana  na magonjwa sugu  yakina baba.  dawahii inaNguvu  (3) inafanya kazi kwa pamoja (1) inaongeza nguvu zakiume ( 2) itakufanya kuchelewa kufika kileleni  kwa muda wa dk 10-15(3)inazalisha homoni  kwa wingi na kuku fanya uwe na mbegu nyingi zenye vimeleo vingi nya uzazi vilivokomaa
------------------
MDINGO POWER nidawa inayo lefusha na kunene pesha maumbile madogo yaliyosinyaa kunzia nchi
6-8 upana 3-4     dawa hizi hazina madhara hata kwa wazee    TUMIA LEO UONE MAJABU YAKE TIBA HIZI NIZAKUDUMU
------------------
DR GATUNDU anazo dawa zakutibu mangonjwa sugu kama vile kisukali presha henia ngili ya kushuka bila upasuji vidonda vya tumbo kuondoa sumu mwilini  kushikwa na ganzi mwilini
------------------
DR GATUNDU ANA PATIKANA DAR-ES SAALM  WALE WAMIKOANI WATA TUMIWA KWA NJIA YA MABASI PASIPO NA MASHAKA TIBA NI WITO NYOTE MNA KALIBISWA
 DR GATUNDU📞 0716 948950

Video: Jux Ft. Nyashinski - Incase You Don't Know

$
0
0
Video:  Jux Ft. Nyashinski - Incase You Don't Know

Kero Ya Mpaka Kati Ya Kenya Na Tanzania Kupatiwa Ufumbuzi

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.  Dkt. Damas Ndumbaro akiwa Kenya na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) akiwa Tanzania wakiwa wameshikana mikono kudhihirisha changamoto ya Mpaka huo uliopo Jasini Mkinga Mkoani Tanga.
 *****
Na. Peter Haule WFM, Tanga
Serikali imeahidi kutatua mgogoro wa Mpaka kati ya Tanzania na Kenya katika Kijiji cha Mahandakini, Wilayani Mkinga mkoani Tanga, baada ya kupata malalamiko kutoka kwa wanakijiji wanaoishi katika mwambao huo wa Bahari ya Hindi baada ya kuzuiwa kufanya shughuli zao za uvuvi na kuwasababishia hali ngumu ya maisha.

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji, na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro walipotembelea na kukagua eneo hilo la mpaka na nchi Jirani ya Kenya.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mahandakini,  Bw. Nasoro Mbarook, alisema kuwa wavuvi wa Kijiji hicho wanashindwa kuendelea na shughuli za uvuvi baada ya vifaa vyao vya uvuvi  kukamatwa na wavuvi takribani 112 kukamatwa na vikosi vya ulinzi vya Serikali ya Kenya nakufunguliwa mashtaka kisha kutozwa faini ya Sh. 5000 ya Kenya, jambo ambalo wavuvi hao wanaamini halikua sahihi kwa kuwa walikua wanavua katika maji ya Tanzania katika Bahari ya Hindi hivyo hawakutenda kosa kama ilivyodaiwa.

Manaibu Waziri hao, walisema dhumuni la ziara yao katika mpaka huo ni kujionea hali halisi na pia kuweka mikakati ya namna ya  kutatua changamoto zilizopo ikiwemo ya wananchi kushindwa kulipa kodi kutokana na kukosa kipato kilichotokana na uvuvi ambapo kwa sasa wanazuiwa kufanya shughuli za uvuvi.

Walisema kuwa wamejionea hali halisi ya mpaka huo hivyo Serikali itafanya tathmini kisha kufanya majadiliano na wenzao wa Kenya ili kulitafutia ufumbuzi suala hilo.

Aidha walibaini kuwa eneo la mpaka halijazingatia taratibu  kwa kuwa zipo nyumba ambazo zimejengwa chini ya umbali wa mita 30  mahali ambapo palipaswa kutokuwepo makazi hayo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mkinga Bw. Yona Mark, ameiomba Serikali kutoa fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Shule ya Msingi katika Kijiji cha Mandakini Wilayani humo ili wanafunzi waanze kusoma kwa kuwa kwa sasa watoto wanasoma katika shule iliyopo eneo la Kenya.

Pia ameomba  kujengwa kwa barabara katika eneo hilo la Kijiji ambalo linawakazi zaidi ya 3666 na Kituo cha kukusanya mapato kwa kuwa eneo hilo kuna bidhaa nyingi zinazoingia na kutoka nchini.

Zaidi Ya Washiriki 300 Kuhudhuria Kongamano La Tano La Wadau Wa Sekta Ya Kilimo, Mifugo Na Uvuvi Dodoma.

$
0
0
NA.MWANDISHI WETU
Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Kushirikiana na Wadau wa masuala ya Mifugo, Kilimo na Uvuvi wameandaa Kongamano la Tano la Wadau wa Sekta hizo ili kujadili matokeo ya tafiti zinazohusu sera za kilimo na maboresho ya sera hizo ili kujenga mazingira wezeshi kwa wakulima na sekta binafsi.

Kongamano hilo linatarajiwa kuhudhuriwa na washiriki zaidi ya 300 Februari 13, 2019 Jijini Dodoma.

Hayo yameelezwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Shughuli za Serikali Ofisi ya Waziri Mkuu, Joseph Kiraiya alipokutana na waandishi wa habari hii jana, Februari 12, 2019 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi hiyo.

Kongamano hilo linalenga kuchambua namna sekta ya kilimo inavyoweza kuwa msingi na chachu ya mageuzi ya viwanda pamoja na kuainisha mapendekezo ya maeneo ya kisera ambayo yanahitajika kuboreshwa.

Kaulimbiu ya Kongamano hilo kwa mwaka huu 2019 ni “Mchango wa Sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi katika Kuhamasisha Mageuzi ya Uchumi na Viwanda Kupitia ASDP-II”

Aidha, Mgeni rasmi wa kongamano hilo anatarajiwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji Mhe.Angellah Kairuki kwa niaba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa.

Akielezea kuwa, kongamano hilo linatarajiwa kuhudhuriwa na washiriki kutoka Sekta binafsi, wakulima, wataaluma, wabia wa maendeleo, watafiti na wadau kutoka sekta ya Umma na kuwataka waandishi wa habari kuendelea kulitangaza kongamano hilo kwani linaleta chachu kwa kuzingatia mchango wa wadau katika kuboresha sera za kilimo ili kufikia mageuzi ya viwanda.

“Wito wa Serikali kwa vyombo vya habari ni kuhakikisha mnaendelea kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa kuboresha sera mbalimbali zinazohusu masuala la kilimo, mifugo na uvuvi kwa kuzingatia kaulimbiu ya mwaka huu ambayo inahimiza juu ya mchango wa sekta hizo katika kuchochea mageuzi ya viwanda  nchini”,alisema Kiraiya.

Naye Mratibu wa Jukwaa la Uchambuzi wa Sera za Kilimo Profesa, David Nyange alieleza umuhimu wa kongamano hilo ambalo litatoa fursa kwa wadau kujadili mada nane ikiwemo; Mazao ya Chakula na Lishe, Mazao ya Biashara, Mazao mapya, bidhaa mbadala na zile zinazoagizwa nje, Mazao ya Mifugo na Samaki pamoja na Pembejeo na huduma za kilimo

“Kongamano hili limekuja wakati sahihi kwani kati ya vipaumbele vya ukuaji wa uchumi, kilimo ndiyo msingi wa ukuaji wa viwanda kwani malighafi zilizotumika viwandani nyingi zinatokana na kilimo, hiyo kongamano hili ni muhimu kwani linatupa kujadili na kuchambua sera za kilimo na nini kifanyike kuwa na kilimo kinachokuwa kwa kasi na kuleta mageuzi ya viwanda,”alisisitiza Prof.Nyange

=MWISHO=

Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya Lakamata vipodozi vya aina mbalimbali vilivyopigwa marufuku nchini

$
0
0
Mnamo tarehe 11.02.2019 majira ya saa 23:45 usiku huko eneo la Soweto, Kata ya Ruanda, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya. Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya lilikamata gari lenye namba za usajili T.937 CKD aina Toyota Saloon likiwa na vipodozi vya aina mbalimbali vilivyopigwa marufuku nchini. Vipodozi vilivyokamatwa ni:-
  1.     Extra Clair katoni nane [08].
  2.     Perfect White katoni mbili [02].
  3.     Epiderm Cream dazani arobaini na saba [47]
  4.     Diproson dazani ishirini na moja [21]
  5.     Coco Pulp katoni mbili [02]
  6.     Carolight katoni sita [06]
  7.     Citro Light katoni tatu [03]
  8.     Teint Clair katoni mbili [02]
  9.     Top Lemon katoni nne [04]
  10.     Clair Men katoni mbili [02]
  11.     Princes Clair katoni nne [04]
  12.     Movet boksi mbili [02]
  13.     Miki Clair katoni mbili [02]
  14.     Top Clair Plus katoni moja [01]
  15.     Collagen formula boksi mbili [02]
  16.     Mont Clair boksi mbili [02]
  17.     Movet tube pcs mbili [02]
  18.     Movet boksi mbili [02]
  19.     Cocoderm boksi moja [01]
KUPATIKANA NA VIPODOZI VILIVYOPIGWA MARUFUKU NCHINI.
Mnamo tarehe 12.02.2019 majira ya saa 07:15 asubuhi huko eneo la Check Point Igurusi, Kata ya Igurusi, Tarafa ya Ilongo, Wilaya ya Mbarali na Mkoa wa Mbeya, Polisi wakiwa doria walimkamata SAID IDDY @ MOHAMED [32] Dereva na Mkazi wa Mbadula Arusha akiendesha gari lenye namba za usajili T.298 DCH aina ya Scania Basi la abiria – HAJI’s akitokea Mbeya kuelekea Arusha akiwa na vipodozi vilivyopigwa marufuku nchini aina mbalimbali.

Vipodozi vilivyokamatwa ni:-
  1.     Diana Boksi mbili [02].
  2.     White Max Boksi tatu [03].
  3.     Secret White Location Boksi moja [01]
Upelelezi unaendelea na mara baada ya kukamilika, mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani.

KUPATIKANA NA SILAHA [GOBORE] BILA KIBALI.
Mnamo tarehe 11.02.2019 majira ya saa 14:35 mchana huko eneo la Makasini – Uyole, Kata ya Uyole, Tarafa ya Iyunga, Jiji na Mkoa wa Mbeya. Askari Polisi walimkamata PAUL ABRICK [66] Mkazi wa Mtaa wa Nyahoro – Uyole akiwa na silaha Gobore aina ya Tower yenye namba 1878 bila kibali. Upelelezi unaendelea.

Maafisa Manunuzi na Wakaguzi wa ndani kutoka halmashauri 118 wapigwa msasa

$
0
0
Na Mathew Kwembe, Morogoro
Jumla ya watumishi 280 ambao ni Maafisa Manunuzi na Wakaguzi wa Ndani kutoka Halmashauri 118 za Mikoa 16 nchini wanashiriki mafunzo ya siku nne ya marekebisho ya sheria ya ununuzi wa umma na mfumo wa utoaji taarifa za manunuzi (PMIS) yanayofanyika mkoani Morogoro kwa lengo la kuwajengea uwezo maafisa hao ili waweze kuutumia vizuri Mfumo wa utoaji wa taarifa za ununuzi pamoja na marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2016 pamoja na marekebisho ya kanuni zake.
 
Mafunzo hayo yanaendeshwa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kupitia Programu ya Maboresho ya Fedha za Umma Awamu ya V (PFRMP V)kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA).
 
Akifungua mafunzo hayo jana mjini Morogoro, Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro bwana Clifford Tandari alisema kuwa baada ya serikali kuifanyia marekebisho kadhaa sheria ya manunuzi ya umma kulikuwa na umuhimu mkubwa kwa watendaji hao kujengewa uwezo ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
 
Aliongeza kuwa Serikali iliona kulikuwa na haja ya kuifanyia marekebisho sheria hiyo ili iweze kuleta matokeo yaliyokusudiwa hasa kufanikisha lengo la upatikanaji wa thamani halisi ya fedha katika manunuzi kama ilivyokuwa imekusudiwa.
 
Kwa mujibu wa Katibu Tawala huyo, baadhi ya changamoto zilizokuwa zikiikabili sekta ya Ununuzina kupelekea Sheria na Kanuni hizo kurekebishwa ni pamoja na bei ya manunuzi kuwa kubwa kulinganisha na bei ya soko, gharama za mchakato wa manunuzi kuwa juu kutokana na mpangilio mbaya wa ununuzi na pia kutozingatia sheria, kanuni na miongozo inayotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA.
 
Bwana Tandari alizitaja changamoto nyingine kuwa ni pamoja na mchakato wa ununuzi kuchukua muda mrefu jambo ambalo limekuwa likileta athari mbalimbali ikiwemo kupanda kwa bei ya huduma, vifaa au kandarasi kutokana na hali ya soko kubadilika.
 
Changamoto nyingine ni kutotumiwa kwa viwango hasa kwenye huduma na bidhaa kama vile utengenezaji wa magari, ununuzi wa bidhaa mtambuka hasa bidhaa zinazopatikana GPSA na MSD kwani lazima bidhaa hizo zitoke huko.
 
Bwana Tandari alieleza pia tofauti kati ya taratibu za ununuzi zinazotumiwa na Halmashauri na Taasisi nyingine za Umma hasa kutokana na kukosekana kwa taratibu za kisheria zinazowahakikishia wauzaji kuwa ununuzi unazingatia ushindani thabiti, haki, uwazi na uwajibikani, uadilifu na maslahi ya taifa.
 
Katibu Tawala wa Mkoa aliongeza kuwa kutokana na marekebisho ya sheria ya ununuzi serikali inatarajia kuongezeka kwa ushindani na uwazi katika ununuzi wa uma, kuongezeka kwa uwajibikaji na kupungua kwa gharama za ununuzi wa magari kwa kupitia Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini na kuboresha ukidhi na uzingatiaji wa sheria ya ununuzi ambapo sheria imetoa fursa kwa PPRA kuzikagua taasisi nunuzi na kupima kama zimezingatia ukidhi wa sheria katika ununuzi.
 
Bwana Tandari alisema kuwa sheria imetoa mwanya pia wa kutumia mfumo wa TEHAMA  ambapo taasisi nunuzi huwasilisha taarifa zake PPRA kwa kutumia mifumo iliyowekwa.
 
Kwa upande wake Mratibu wa Mafunzo hayo bwana Lucas Mrema alisema kuwa mikoa 16 inayoshiriki mafunzo haya ni  mbali na ile mikoa 10 iliyokuwa ilishiriki kwenye utekelezaji wa programu ya usimamizi wa fedha za Umma awamu ya nne.
 
” Katika utekelezaji wa programu ya Usimamizi wa Matumizi ya fedha za Umma awamu ya tano tunatarajia kuwa mikoa yote 26 na halmashauri zake 185 zitashirikishwa,” alisema.
 
Kwa upande wake Mhandisi Mary Swai Kaimu Mkurugenzi Msaidizi kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) aliwataka Maafisa Manunuzi kuhakikisha kuwa wanafuata taratibu zote za manunuzi pindi wanapotekeleza najukumu yao.
 
Aliongeza kuwa Maafisa Manunuzi wanapaswa kuhakikisha kuwa makini katika utekelezaji wa mikataba mbalimbali ambapo alidai kuwa pindi mkataba unaposainiwa wahakikishe kuwa mkataba huo unatekelezwa vizuri.

TANZIA: Msanii Godzilla Afariki Dunia

$
0
0
Msanii maarufu wa muziki wa Hip Hop Golden Mbunda maarufu Godzilla amefariki dunia ghafla usiku wa kuamkia leo Jumatano, February 13, 2019 akiwa nyumbani kwao, maeneo ya Salasala, Dar.

Mwili wa marehemu umepelekwa kuhifadhiwa katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, iliyopo Mwenge jijini Dar es Salaam na msiba upo nyumbani kwao Salasala.

Ntunzu Herbarist Clinic : Ni Kituo Cha Tiba Asilia Kitoacho Huduma Bora Na Sahihi

$
0
0
Acha kuongopewa at kukaa ukilalamika kuwa umetumiwa madawa mengi sana bila mafanikio... acha kukata tamaa kumbuka atafutaye hupata 

SASA DR   BRUNO  kakuletea tiba bora ya nguvu za kiume ni hii hapa;

 GASAMILO POWER ;ni dawa bora kwa sasa ambayo hutibu matatizo manne kwa pamoja kama vile 1 kuwai kufika kileleni  kabla ya mwenzi wako  2. kukupa hamu ya kurudia tendo zaidi ya Mara Mbili 3. kuimalisha misuli ya uume uliyolegea na kusinyaa asa kwa Wale waliojichua 4 .Huondoa uchofu pale umalizapo kufanya tendo 

Dawa hii hutumiwa ata na wazee pia tunatibu kile kinachochangia kuishiwa nguvu Kama vile,vidonda vya tumbo, kisukari, presha, tumbo kuunguruma na kuuma chini ya Kitovu ,ngiri,korodani korodani kuvimba, magonjwa ya moyo 

NI NINI KINASABABISHA  KUWA NA maumbile  MaFUPI NA MEMBAMBA? 1.kufanyia tohara ukubwani 2 unene kupita kiasi 3. kuridhi kutoka kwa wazazi, 4 .uvaaji wa nguo za kubana sehemu ya uume 5. chango na ugonjwa wa zinaa 

Ili uweze kuwa mwanaume mashine ebu tumia dawa hii 

MKULULU MIX; dawa hii huongeza uume saizi upendayo inch urefu wa inch 5 adi 8 na unene wa sentimita 2 adi 5 dawa hizi hazna madhara yoyote ata kwa miaka ya baadaye 

FUNGA RUZIZI ;ni dawa ya uzazi inatoa matokeo ndani ya siku kumi na mbili tu 

KWA USHAURI NA TIBA FIKA  OFISINI KWANGU MBAGALA ZAKHEMU njoo mpaka pale kwenye ukumbi wa DAR LIVE... ni dakika tano tu kufika ofisini kwangu MOROGORO,MWANZA,NA KAHAMA WAPO MAWAKALA au piga simu 0744 040 721 AU 0683 645 920. Kama hauna nafasi utaletewa

Usikate Tamaa....Okoa Ndoa yako kwa Tiba Hii ya Asili

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

GALIMBO 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0620510598  / 0743543944

Waziri wa Kilimo: Hakuna Vibali vya Kuagiza Sukali kwa Wazalishaji wa ndani

$
0
0
Serikali imesema kuanzia sasa haitatoa vibali vya uagizaji sukari nje ya nchi kwa wazalishaji wa sukari badala yake serikali itatafuta utaratibu mwingine wa kuagiza.

Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga ameyasema hayo jana tarehe 12 februari 2019 wakati akifungua mkutano na Wadau wa Sekta Binafsi ambapo; lengo lilikuwa ni kubadilishana uzoefu, kupata maoni yao namna bora ya kuongeza mahusiano pamoja na utekelezaji wa Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP II) ambayo inatekelezwa kwa pamoja kati ya Serikali na Sekta Binafsi.

Waziri Hasunga imewataka wazalishaji hao wa sukari nchini kuja na mkakati wa namna gani wataongeza uzalishaji ili Tanzania iondoke na hitaji la kuagiza bidhaa hiyo nje ya nchi.

Waziri Hasunga amesema kwa kuwapa vibali vya kuagiza nje wazalishaji wa ndani hawataongeza uzalishaji ili waendelee kuagiza nje kwa kuwa sukari ya kutoka nje ni bei nafuu.

"Wazalishaji wa ndani ndio hao hao wanapewa vibali vya kuagiza, umewahi sikia wapi? Wataongeza ukweli kasi ya uzalishaji? Na Mimi niwaambie kabisa hilo hapa kwangu halipo kabisa kama ni kuagiza nitaagiza mimi," alisema Waziri Hasunga.

Amesema mahitaji la sukari kwa mwaka ni Tani 670,000 wakati inayozalishwa na viwanda vya ndani Tani 320,000 na kuwaagiza Wazalishaji hao badala ya kutafuta vibali vya kuagiza sukari nje ya nchi waje na mkakati wa kuboresha zaidi uhitaji uliopo kwani Tanzania ina ardhi nzuri pamoja na mashamba ya kutosha.

"Kama kuna Wafanyabiashara ambao walikuwa wanasubiri baada ya kikao hiki waje kuomba vibali wasahau kabisa, kwangu halipo badala yake nina mkakati wa kuboresha uzalishaji ili tusiagize tena nje," alisema Waziri Hasunga.

Amesema kuwa anataka kuhakikisha ndani ya miaka mitatu Tanzania haitaagiza sukari nje tena kwa kujitosheleza kwa kilimo cha miwa na kukaribisha wawekezaji kujenga viwanda vya kutengeneza sukari, "kama tutakunywa kwa chumvi sawa, hapo ndio tutafanya bidii."

Waziri Hasunga amesema hayuko tayari kuondoshwa kazini kwa utoaji wa vibali vya sukari kwa Wafanyabiashara wanaoagiza nje ya nchi kwani anaamini kuwa uwezo wa kuzalishwa hapa nchini upo. Waziri huyo alisema serikali inatoa fedha nyingi kuagiza bidhaa za chakula kutoka nje.

Alisema kwa mwaka zaidi ya Shilingi Bilioni 400 zinatumika kuagiza mafuta nje ya nchi wakati kuna uwezo wa kulima mazao mbalimbali yanayozalisha mafuta ikiwa ni pamoja na michikichi.

"Mimi naamini katika nchi zilizobarikiwa na kupendelewa ni pamoja na Tanzania, ardhi yenye rutuba, mito mingi na mbuga za wanyama lakini watu hawalimi kilimo cha umwagiliaji," alisema.

Ameitaka Sekta Binafsi kuhakikisha kunakuwa na mashamba makubwa ambayo yatazalisha mazao yanayohitajika kwa viwanda na pia mazao ya chakula.

Waziri Hasunga amewataka Wadau wa Sekta Binafsi kutumia kikao hicho kutoa maoni, mapendekezo yenye muelekeo wa kutatua changamoto katika Sekta ya Kilimo ambapo anategemea maboresho hayo yataleta mabadiliko makubwa katika mfumo mzima wa pembejeo za kilimo, masoko, uzalishaji wenye tija na utungwaji wa sheria ya kilimo.

Mwisho

BREAKING: Mwigulu Nchemba Apata Ajali.....Akimbizwa Hospitali Dodoma

$
0
0
Mbunge wa Iramba Magharibi Mwigulu Nchemba1 amepata ajali ya gari akiwa njiani barabara ya Iringa kuelekea Dodoma na amekimbizwa hospitali ya Dodoma. 

Taarifa zaidi zitakujia hivi punde.

Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Nchini (NGOs) Yanayokiuka Uwazi Na Uwajibikaji Kubanwa

$
0
0
Na Mwandishi wetu Kilimanjaro
Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Nchini kutoka Wizara ya Afya, Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii Bi. Neema Mwanga ametoa onya kuwa atachukua hatua kali dhidi ya Shirika lolote Lisilo la Kiserikali litalokiuka kufanya kazi kwa mujibu wa matakwa ya Sheria ya NGOs ya Mwaka 2002 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2005.

Akiwa katika ziara ya kutembelea mashirika Yasiyo ya Kiserikali yaliyoko katika Mkoa wa Kilimanjaro Msajili Bi. Mwanga amesema kuwa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yanawajibu wa kuzingatia kanuni mpya za Sheria ya NGOs zinazoelekeza Mashirika hayo kufanya kazi kwa kuzingatia Misingi ya uwazi na uwajibikaji maana miradi hiyo imeanzishwa kwa lengo la kuwanufaisha wananchi ambao ndio walengwa wakuu.

Msajili Mwanga aliwaambia viongozi wa Mashirika manne aliyoyatembelea jana ikiwemo TAWREF, White Orange, Elimu Mwangaza na Tusonge Community Organisation kwamba Misingi ya uwazi na uwajibikaji kama inavyobainishwa katika Sheria hiyo inasisitizwa kwa lengo la kukuza ushiriki wa wanufaika katika kutambua vyanzo vya mapato ya NGOs, kiasi cha fedha zinazopolkelewa na mashirika na kutoa taarifa za miradi yao inayotekelezwa kwenye ngazi ya jamii ili kufuata matakwa ya kisheria na kuacha kufanya kazi kwa mazoea.

Kufuatia azma ya Serikali ya kuacha kufanya shughuli za NGO kwa mazoea, Msajili Mwanga ameonya kuwa NGO yoyote itakayobainika kufanya kazi bila kusajiliwa au kupata hati ya ukubalifu itakosa sifa na kupelekea kupata zuio la usajili kwa mujibu wa kanuni ya sheria ya NGO ya mwaka 2002 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2005.

‘’Naelekeza NGO zote kubainisha kazi zinazotekelezwa, kwa sasa tuko kwenye hatua ya kuwajengea wadau wote wa NGOs uelewa ili kuwezesha kila mmoja kuzingatia sheria na mashirika amabyo yatashindwa kuzingatia sheia, taratibu na kanuni za utekelezaji wa miradi yao zitashurutishwa kusitisha miradi yao maana hazitakuwa na sifa stahiki”. Alisema Msajili Bi. N. Mwanga.

Katika ziara hiyo ya kikazi Msajili wa NGOs amepongeza kazi inayofanywa na Mashirika ya TAWREF, White Orange, Elimu Mwangaza na Tusonge Community Organisation na kuwataka Wakurugenzi wa taasisi hizo kwa kuzingatia vipaumbele vya Mikoa, Halmashauri, na changamoto zinazowakabili wananachi katika Mkoa wa Kilimanjaro na nje ya Mkoa huo. 

Ameongeza kuwa utendaji wa Taasisi hizo umeonesha kuzingatia yale yaliyobainishwa katika kanuni za sheria ya NGOs na kuwataka kuwasiliana na Ofisi ya Msajili ngazi ya Taifa, Mkoa na Halmashauri katika kuendelea kuboresha mazingira ya kazi zao kama kutakuwa na suala lenye kuwatatiza katika utendaji wa akzi zao. 

Aidha Msajili Mwanga amewataarifu wadau wa NGOs kuwa katika kuhakikisha Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yanatatuliwa chanagmoto zinazowakabili, Serikali Inaendelea kukamilisha mfumo wa usajili na utoaji wa taarifa kwa njia ya mtandao (online). 

Mfumo huu utatumiwa na wadau, wasajili wasaidizi ngazi ya mikoa na Halmashauri pamoja na Ofisi ya Msajili ya taifa. Juhudi hizi zitasaidia Taifa kukuza mchango wa Mashirika katika uchumu wa Taifa na kukuza uwajibikaji.

Wakati huo huo Mkurugenzi wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Nchini Bi. Neema Mwanga amebainisha kuwa Serikali kupitia Wizara ya Afya Idara kuu ya Maendeleo ya Jmaii Jinsia wazee na watoto inakamilisha kanzidata ya Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali hapa Nchini ili kuwa na nyenzo ya kufuatilia mchango wa mashirika hayo katika pato la Taifa. 

Wakti huo huo Ofisi ya Msajili wa NGOs inaandaa mfumo wa Ufuatiliaji na tathmini ili kufanikiha kazi ya uratibu kwa kuonesha wadau kutambua maungufu yao na kuyafanyia maboresho katika muda stahiki. Juhudi hizi zitasaidia mfumo wa uratibu katika ngazi mablimbali kuwa na uelewa wa pamoja na kuchukua hatua dhidi ya Taasisi ambayo itaonekana kutozingatia sheria.

Wakiongea kwa muda tofauti wakati wa ziara hiyo Bw. Michael Reuben ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la ‘Elimu Mwangaza’ amepongeza juhudi za Wizara katika kutatua chanagmto zinazokwamisha ufanisi katika utendaji wa NGOs Nchini. Moja ya hatua iliyofurahiwa na wadau wengi ni uandaaji wa mfumo wa usajili kwa njia ya matandao ili kupunguza gharama za safari wakati wa kufuata huduma hiyo.

Vilevile mmoja wa viongozi wa NGOs moja kutoka Manispaa ya Moshi(jina limehifadhiwa) ameeleza ziara ya Msajili amabye amefika katika Ofisi ya Shirika hilo imekuwa na manufaa makubwa maana imemjengea ari na uelewa wa kukamilisha taratibu za uasajili ili atambuliwe na hivyo kuendesha kazi zake kwa mujibu wa matakwa ya kisheria.  

Mwisho Bi. Neema amepongeza Maafisa Wasaidizi wa Mkao wa Kilimanjaro kwa namana wanavyotekelezakazi yao ya kusimamia na kuratibu kazi za NGos kwa weledi katika uzingatiaji wa kanuni za sheria ya NGOs ya Mwaka 2002 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2005. 

Watendaji hao wa ngazi ya Mkoa na Halmashauri wamekumbushwa wajibu wao wa kuyasimamia Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kwa  kufuata katiba, Sera za kitaifa, kanuni za maadili, vipaumbele vya kijamii, vibali vya kazi kwa watendaji wasio raia wa Tanzania pamoja na umuhimu wa uwasilishaji wa mikataba ya miradi ya kazi zilizopata ufadhili kwa ajili ya utekelezaji.

Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yanadhamana ya kutoa mchango katika jamii masikini na isiyo na uwezo ili kuwezeshwa katika kuboresha ustawi na maendeleo ya maisha ya wananchi wenye uhitaji. 

TAKUKURU Yaomba Kumhoji Mshitakiwa Kesi ya kutakatisha fedha inayomkabili Mkurugenzi Mkuu wa zamani NIDA

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,imekubali mshtakiwa wa tano, Xavery Kayombo, katika kesi ya kutakatisha fedha inayomkabili Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dickson Maimu na wenzake watano, kwenda kuhojiwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Amri hiyo ilitolewa jana Februari 12,2019 na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Salum Ally, baada ya upande wa Jamhuri kuwasilisha maombi kwamba mshtakiwa huyo anakwenda kuchukuliwa maelezo yake.

Wakili wa Serikali, Leonard Swai, alidai kesi hiyo imepangwa kwa ajili ya kutajwa na upande wa Jamhuri unaomba kibali cha kumchukua mshtakiwa kwenda kumhoji Takukuru.

Hakimu alisema mahakama yake imekubali mshtakiwa huyo kwenda kuhojiwa kwa siku moja kisha apelekwe mahabusu.

Alisema kesi hiyo itatajwa Februari 19, mwaka huu na washtakiwa wataendelea kukaa mahabusu.

Baada kesi hiyo kupigwa kalenda, ndugu na wanafamilia wa washtakiwa walilalamikia hatua ya mahakama kuendesha kesi hiyo katika chumba kidogo badala ya ukumbi wa mahakama ya wazi.

Baadhi yao waliangua vilio kutokana na kukosa kuonana na ndugu zao walioko mahabusu, huku wakidai kuwa wamesafiri kutoka mikoani kwa ajili ya kusikiliza kesi hiyo.

“Tumetoka Mbeya kuja kusikiliza kinachoendelea katika kesi za ndugu zetu, lakini tumeshindwa kusikia kwa sababu ya watu kufurika katika chumba kidogo walipoingia washtakiwa,” alisema mmoja wa wanaodaiwa kuwa wanafamilia wa washtakiwa hao huku akiangua kilio.

Mbali na Maimu na Kayombo washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Meneja Biashara wa (NIDA), Aveln Momburi, Mkurugenzi wa Kampuni ya Aste Insurance Brokers, Astery Ndege, Ofisa Usafirishaji, George Ntalima, Mkurugenzi wa Sheria, Sabina Raymond.

Awali washtakiwa hao walikuwa wakikabiliwa na mashtaka 26 likiwamo la uhujumu uchumi, ila Januari 28,2019 waliachiwa huru na mahakama hiyo baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kusema hana nia ya kuendeleza mashtaka dhidi yao.

Hata hivyo, baada ya washtakiwa kuondolewa mashtaka hayo na kuachiwa huru walikamatwa tena na walifikishwa katika mahakama hiyo kisha kusomewa mashtaka mapya 100 yakiwamo 25 ya utakatishaji fedha.


Video: Cadelana - CHEKECHA

Serikali Kupitia Upya Mkataba Wa Ujenzi Kituo Cha Forodha Horohoro- Tanga

$
0
0
Na Peter Haule, WFM, Tanga
Serikali imetoa agizo kwa watendaji wa Kituo cha pamoja cha Forodha Mpakani- Horohoro, kuwasilisha nyaraka za ujenzi wa Kituo hicho ukiwemo mkataba kwa kuwa miundombinu iliyopo haijakidhi viwango jambo lililosababisha kutofunguliwa rasmi kwa kituo hicho tangu mwaka 2015.

Agizo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.  Dkt. Damas Ndumbaro walipofanya ziara ya kutembelea na kukagua Kituo hicho ambapo hawakuridhishwa na miundombinu yake.

Dkt. Kijaji, alisema kuwa Kituo hicho hakina mawasiliano kati ya upande wa Tanzania na Kenya hivyo kutokidhi vigezo vya kuwa Kituo cha pamoja cha Forodha kati ya nchi hizo mbili.

Alisema kuwa ukosefu wa mawasiliano unasababisha urasimu katika kuwahudumia wananchi jambo linalosababisha wateja katika mpaka huo kutafuta njia nyingine ambazo sio rasmi katika usafirishaji bidhaa jambo ambalo linaathari kubwa katika ukusanyaji wa mapato.

Miongoni mwa kasoro zilizobainika wazi ni kamera maalum za usalama zinazotakiwa kufanyakazi ni zaidi ya 14 lakini zinazofanyakazi mpaka sasa ni 4 pekee jambo linalotiashaka kuhusu usalama wa Kituo hicho

Dkt. Kijaji, alisema pia, utaratibu wa wakazi wa Horohoro kwenda kupata huduma za TRA katika Wilayani Muheza usitishwe na badala yake watumishi wa Mamlaka hiyo waende kuwahudumia wananchi katika Wilaya ya Mkinga ili kuondoa usumbufu kwa wafanyabiashara wanapotaka kulipa kodi au kutafuta huduma za masuala ya forodha.

Aidha, Manaibu Waziri hao wameiagiza Mamlaka ya Mapato (TRA) Mkoani Tanga kuhakikisha Jenereta la Kituo hicho cha Pamoja cha Forodha linafanyakazi ndani ya saa 24 ili kukabiliana na upotevu wa mapato katika eneo hilo kinyume na hapo hatua zingine zitachukuliwa.

Manaibu Waziri hao wametoa maagizo hayo baada ya kuelezwa kuwa jenereta halifanyikazi baada ya kuharibika kwa takribani siku 14 na kusababisha Seikali ikose mapato na kuleta usumbufu kwa watumiaji wa Kituo hicho kwani hulazimika kukaa muda mrefu kusubiri umeme urejee baada ya kukatika.

“Kutofanya kazi kwa Jenereta katika Kituo cha Forodha- Horohoro kumechangia kukosekana kwa kumbukumbu sahihi ya magari yanayopitisha bidhaa katika mpaka huo hivyo kuwa na athari katika takwimu za mapato ya eneo hilo lakini pia usalama wa Taifa”. Alisema Dkt. Kijaji

Viongozi hao wameiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA kutengeneza skana ya kuchunguza usalama wa mizigo na wateja wanaoingia kwenye Kituo hicho ambayo imeharibika muda mrefu hali inayohatarisha usalama wan chi, raia na mali zao

Kwa upande wake Mhe. Dkt. Ndumbaro, ameagiza kuchimbwa kwa kisima cha maji eneo hilo kwa kuwa kiasi cha Sh. milioni sita kinachotumika kuagiza maji kila mwezi kinaweza kutumika kujenga kisima cha kudumu na kuokoa fedha nyingi zisipotee.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.  Damas Ndumbaro wapo katika ziara mkoani Tanga na maeneo mengine katika kutatua changamoto za ukusanyaji wa mapato na suala la usalama katika mpaka wa Tanzania na Kenya.

Waziri wa fedha wa zamani kutoa ushahidi kesi ya Kitilya

$
0
0
Waziri wa zamani wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, ameitwa kutoa ushahidi dhidi ya Kamishna Mkuu wa zamani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya, na wenzake wanne.

Kitilya na wenzake hao wanakabiliwa na tuhuma za uhujumu uchumi pamoja na mashtaka 58 ya kula njama, kutakatisha fedha na kuisababishia serikali hasara ya Dola za Marekani milioni sita.

Mbali na Kitilya, washtakiwa wengine ni Miss Tanzania wa 1996, Shose Sinare, Sioi Solomon, aliyekuwa Kamishna wa Sera na Madeni kutoka Wizara ya Fedha, Bedason Shallanda (kwa sasa Ofisi ya Waziri Mkuu) na Alfred Misana, aliyekuwa Kamishna Msaidizi wa Sera na Madeni kutoka wizara hiyo (kwa sasa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto).

Wote kwa pamoja wanakabiliwa na tuhuma ya uhujumu uchumi iliyopewa usajili namba 2/2019.

Licha ya waziri huyo wa zamani mbali na Mkulo, shahidi mwingine aliyetajwa mahakamani kwa upande wa Jamhuri ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali wa zamani, Jaji (mstaafu) Frederick Werema.

Katika kesi hiyo, upande wa Jamhuri unatarajiwa kuwasilisha vielelezo 218 zikiwamo nyaraka za benki kesi itakapopangwa kuanza kusikilizwa ushahidi katika Mahakama Kuu Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, maarufu kama Mahakama ya Mafisadi.

Madai hayo yalitolewa jana na jopo la mawakili wa Jamhuri mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shaidi.

Washtakiwa hao wanadaiwa kuongoza mtandao wa uhalifu, uliosababisha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupata hasara ya dola za Kimarekani milioni 600.

Jopo la Jamhuri liliongozwa na Mawakili wa Serikali Wakuu, Fredrick Manyanda, Tumaini Kweka na Mawakili wa Serikali, George Barasa, Ester Martin na Leonard Swai.

Akiongoza jopo la mawakili wa serikali, Kweka alidai kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), amewasilisha taarifa na kutoa kibali kwa Mahakama ya Uhujumu Uchumi kusikilizwa kesi hiyo.

Jopo la utetezi liliongozwa na Mawali Cathbert Tenga, Majura Magafu na Alex Mgongolwa.

Katika Kesi ya msingi washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka 49 ya utakatishaji fedha, mashtaka matatu ya kughushi, moja la kuongoza mtandao wa uhalifu, mawili ya kutoa nyaraka za uongo, shtaka moja la kujipatia fedha kwa njia ya udanyanyifu, kula njama ya kutenda kosa kutumia nyaraka kwa nia ya kumdanganya Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Uchumi (wakati huo ikijulikana hivyo, sasa Wizara ya Fedha na Mipango).

Upande wa Jamhuri ulidai katika shtaka la kwanza, ambalo ni la kuongoza mtandao wa uhalifu, washtakiwa kwa pamoja walitenda kosa hilo kati ya Februari 20, 2012 na Juni, 2015, katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar Es Salaam. Ilidaiwa kuwa kwa makusudi, washtakiwa waliongoza mtandao wa uhalifu, uliosababisha serikali kupata hasara ya dola za Kimarekani milioni 600.

Katika shtaka la kujipati fedha kwa njia ya udanganyifu, washtakiwa kwa pamoja wanadaiwa kati ya Machi 15, 2013 na Januari 10, 2014, jijini Dar es Salaam, kwa nia ya kudanganya, walijipatia Dola za Kimarekani milioni sita wakionyesha kuwa fedha hizo zilikuwa malipo ya ada ya uwezeshaji wa upatikanaji wa mkopo na zililipwa kupitia Kampuni ya Egma (T) Ltd.

Katika shtaka la utakatishaji fedha, ilidaiwa kuwa washtakiwa wote Machi 18, 2013 na Januari 10, 2014, jijini Dar es Salaam, walitakatisha Dola za Marekani milioni sita kwa kuzitoa fedha zilizoko katika akaunti ya Egma (T) Ltd iliyoko katika benki ya Stanbic Tanzania.

Aidha, katika shtaka la kuisababisha hasara serikali, ilidaiwa kuwa kati ya Mei Mosi, 2012 na Juni Mosi, 2015 jijini Dar Es Salaam, washtakiwa waliongeza gharama ya mkopo wa Dola milioni 600 kutoka asilimia 1.4 hadi asilimia 2.4, hivyo kuisababishia serikali hasara ya dola milioni sita.

Pia Sinare anadaiwa kuwa Agosti 2, 2012, akiwa na nia ya kudanganya, aliandaa nyaraka ya pendekezo la kifedha, akijaribu kuonyesha kuwa Benki ya Standard ya Uingireza ikishirikiana na Stanbic ya Tanzania watatoa mkopo wa Dola milioni 550 kwa serikali ya Tanzania kama ada ya uwezeshaji wa asilimia 2.4 ya kiasi cha mkopo huo wakati akijua kuwa si kweli.

Kwa upande wao, Shallanda na Misana, wanadaiwa kutumia nyaraka kumdanganya mwajiri wao na tukio hilo wanadaiwa kutenda kati ya Septemba 11, 2012 na Oktoba 3, 2012 katika Wizara ya Fedha.

Katika kufanya hivyo, wanadaiwa kuwasilisha nyaraka za uongo kwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Uchumi wakionyesha nyaraka za pendekeo la kifedha la mkopo huo limetolewa Agosti 2, 2012 wakati wakijua ni uongo.

Mapema Aprili 2016, Kitilya, Sinare na Solomon, walifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza na kusomewa mashtaka ya kula njama, kughushi na kutakatisha fedha.

Jana washtakiwa walipokumbushwa mashtaka yao hawakutakiwa kujibu chochote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo.

Super Moringa : Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORINGA DAWA BORA YA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME NA KUNENEPESHA UUME
_________________________
🔖🌸SUPER MORINGA Ni dawa bora ya nguvu za kiume  yenye mchanganyiko wa mitishamba (7) yenye maajabu yafuatayo/

🔖 (1) inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimalisha misuli ya uume uliolengea wakati wa tendo la ndoa/
🔖 (2) Kurefusha uume uliorudi ndani kuazia nchi 5 - 9/
🔖 (3) kunenepesha uume cm 5 ya upana itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15 - 20 kwa tendo la kwanza na utakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya 2-4 bila hamu kuisha/

📌 Na inatibu kabisa
 📌 Haijalishi umri hata kama una miaka 85 itumie huanza kufanya kazi dk 50 tu na haina madhara yoyote kwa mtumiaji/

🌳🌳🌳🌳🌳🌳🌳🌳            
MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA.
_________________________
🔖 (1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖 (2)Choo kama cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(4)Kaswende/
🔖(5)Gono/

📌Haya yote husababisha kuishiwa nguvu za kiume na kuwa na uume mdogo/
📌 Itumie leo, bado hujachelewa ni tofauti na nyingine.
_________________________
DAR ES SALAAM OFISI IPO BUGURUNI SHELI AU UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
___________________________
WASILIANA NA
Dr ATHUMAN SIMU.
📞0714 884 677
📞0767 104 343
____________________________
*****************************

Makanga 3 Power, Dawa Bora Za Nguvu Za Kiume

$
0
0

Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.

Tupo dar es salam Buguruni

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images