Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Wimbo Mpya wa Enock Bella - I Swear

$
0
0
Wimbo Mpya wa   Enock Bella - I Swear

Video Mpya:ngel GoodLuck - NISHIKE

$
0
0
Video Mpya:ngel GoodLuck - NISHIKE

Wanafunzi 30 Wanusurika Kifo Dereva Akichat na Simu

$
0
0
Jumla ya wanafunzi 30 wa shule ya msingi binafsi ya Little Treasure, iliyoko Manispaa ya Shinyanga, wamenusurika kifo baada ya kupata ajali wakirejea nyumbani kuto shule.

Chanzo cha ajali ni dereva wa basi hilo, Emmanuel Faustine (32), ambaye alikuwa akichati na simu ya mkononi huku akiendesha, Januari 10 majira ya ya saa 9 alasiri katika eneo la Kalogo mjini humo.

Akizungumzia ajali hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoani Shinyanga, Kamishina Msaidizi (ACP) Simon Haule, amesema wanafunzi 30 walikuwa wamesalia kwenye basi hilo na hakuna aliyepoteza maisha zaidi ya kupata majeraha sehemu mbalimbali za miili yao.

Amesema chanzo cha ajali hiyo ni dereva ambaye alikuwa akichati na simu wakati akiendesha hatua ambayo ilisababisha kutumbukia mtaroni na kusababisha ajali na mwenyewe kukimbilia kusikojulikana.

“Jeshi la Polisi linamsaka dereva wa basi hili ambaye alikimbia mara baada ya kusababisha ajali, ili achukuliwe hatua kali za kisheria na liwe fundisho kwa madereva wengine ambao wamekuwa wakisababisha ajali za lazima na kugharimu maisha ya watu pamoja na kuwapatia ulemavu”, amesema Haule.

Naye Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufani ya Mkoa, Dk. Albert Masigati amesema alipokea wanafunzi 30 na baada ya kuwapatia matibabu, 26 waliruhusiwa na kubakia wanne wakiendelea kupatiwa matibabu na hali zao zinaendelea vizuri.

Aliyedaiwa kuiba Sh mil saba kila dakika Asomewa Mashitaka Mapya 600

$
0
0
Mfanyabiashara Mohamed Yusufal aliyetajwa na Rais John Magufuli kuiba Mil.7 kwa dakika na mfanyakazi wake, Arital Paliwala wamesomewa mashtaka 600 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ikiwemo kuisababishia serikali hasara ya Bilioni 14.98.

Washtakiwa hao wamesomewa mashtaka yao na jopo la Mawakili wa serikalo wakiongozwa na Hashimu Ngole mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Wilbard Mashauri.

Katika mashtaka hayo yaliyosomwa kwa takribani saa mbili, washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama, kughushi, kuwasilisha taarifa za mwezi za mahesabu ya uongo kwa TRA, kukwepa kodi na kuisababishia serikali hasara ya sh. 14,987,707,044.58

Miongoni mwa mashtaka hayo ni kuisababishia serikali hasara, ambapo wanadaiwa kukwepa kodi ya serikali kwa kipindi cha mwaka 2008 hadi 2015 kupitia kampuni ya Pamplant ltd iliyokuwa inamilikiwa na mshtakiwa Yusufali ambapo mshtakiwa Paliwala alikuwa mfanyakazi wake.

Pia inadaiwa washtakiwa walitenda kosa hilo wakiwa wanatumia stakabadhi za kughushi pamoja na kutumia makampuni ya kughushi wakidai kuwa wamenunua vitu kutoka katika makampuni mbali mbali wakati wakijua baadhi ya kampuni hizo ni za kughushi huku zikiwa hazijasajiliwa Brela.

Hata hivyo washtakiwa hawakuruhusiwa kujibu kitu chochote mahakamani hapo kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi isipokuwa kwa kibali kutoka kwa DPP.

Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi katika kesi hiyo umeshakamilika ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi January 24, 2019.

Lugola awashukia wanaoponda ujio wa ndege mpya

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amesema kuwa ujio wa ndege mpya za kisasa utaongeza hali ya amani na usalama katika viwanja vya ndege kwa kuimarisha mifumo mbalimbali ya usalama.

Ameyasema hayo jijini Dar es salaam jana mara baada ya kuwasili kwa ndege mpya, ambapo amesema kuwa ujio wa ndege hizo utaimarisha huduma za usafiri wa anga ndani na nje ya nchi, kitu ambacho kilikosekana kwa muda mrefu.

”Ujio wa ndege hizi kwanza kabisa utakuwa kivutio kwa watalii, ambapo naimani kabisa idadi yao itaongezeka baada ya kuwa na usafiri wenye uhakika, hivyo kulingana na ongezeko hilo, tutaweza kuongeza uimarishaji maradufu wa usalama katika viwanja vya ndege,”amesema Lugola

Hata hivyo, Lugola amewataka wananchi kuwapuuza baadhi ya watu ambao wamekuwa wakibeza jitihada za rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli za kuiletea nchi maendeleo na kusema kuwa waachwe kama walivyo.

Katika kusherehekea sikukuu ya Mapinduzi ya Zanzibar, kanisa la Shekinah Presbyterian Madale Lajitolea kufanya usafi katika jiji la Dar es Salaam

$
0
0
Waumini wa kanisa la Shekinah Presbyterian Tanzania wamezindua rasmi zoezi la kufanya usafi kwa kujitolea katika mtaa wa Madale mahali kanisa lilipo. 

Katika kusherehekea sikukuu ya Mapinduzi, walizindua zoezi hili katika serikali ya mtaa wa Madale. Wakiongozwa na mchungaji kiongozi wa kanisa hilo, Mch. Daniel John Seni asubuhi na mapema walianza usafi katika kituo cha daladala cha Madale mwisho, baadaye Kisauke shule, na kisha Madale sokoni.

 Baada ya kusafisha katika maeneo hayo waliondoka moja kwa moja mpaka kwenye serikali ya mtaa wa Madale ambapo katibu/Msaidizi wa kanisa ndugu George Shiganga alitoa maelezo kwa mwenyekiti wa serikali ya Mtaa huo.

Wakiongozwa na Kauli mbiu ya  “USAFI WA MAZINGIRA NI SEHEMU YA UTAKATIFU,” mchungaji Daniel alifafanua kwamba “hakuna kitu ambacho kilianzia kwenye imani kikashindikana.” 

Mchungaji huyu alielezea kuwa “Siyo kwamba Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, ndugu Makonda ameshindwa kwenye zoezi la usafi, tatizo ni wapi alianzia.” Alikaza kwamba “sisi katika kumuunga mkono mkuu wetu wa mkoa; tumekuja na mbinu mpya ambayo tunapenda watu wa dini zote katika Mkoa wa Dar es salaam waige, na mbinu hiyo ni kuwafundisha waumini wetu kwa vitendo na kuwabadilisha katika mawazo.” 

Aliendelea kusema kuwa “Katika kuhakikisha tunaunga mkono juhudi za maendeleo zinazofanya na serikali ya awamu wa tano, tunapaswa kupunguza maneno na tuongeze kwenye vitendo zaidi, ifike mahali wachungaji tuwaambie wazi waumini wetu kwamba uchafu ni dhambi! Na kama uchafu ni dhambi, maana yake wakristo wote wanapaswa kuwa wasafi kuanzia rohoni hadi nje (mazingira). 

Alisisitiza kwamba kanisa lazima liwe na athari chanya katika jamii. Kazi ya mchungaji siyo kukemea pepo tu, bali ni kuwafundisha waumini pia waweze kujitolea kwenye jamii inayowazunguka. 

Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Madale bwana Mberwa aliwashukuru sana waumini hawa, na kuomba watu wa dini zote kuhubiri habari za usafi katika makanisa na misikiti yao, ili kujenga fikra mpya kwao. Katika kuhakikisha kwamba zoezi hili linakuwa ni endelevu, waumini hawa wamekubaliana kwamba watakuwa wanafanya usafi mara moja kwa mwezi kwa kujitolea.

Mchungaji Daniel aliwakaribisha watu wa Madale ambao wangependa kuunga mkono zoezi hili la usafi kuwasiliana naye kwa 0769080629 ili kupata ratiba kamili ya zoezi zima.

Imetolewa na ofisi ya kanisa la Shekinah Presbyterian Church
Madale Dar es salaam.

Rais Magufuli Akwama Kuhudhuria Sherehe za Mapinduzi Zanzibar....Dr Shein Ataja Sababu

$
0
0
Rais wa Tanzania, John Magufuli ameshindwa kuhudhuria sherehe za maadhimisho ya miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar yanayofanyika leo Jumamosi Januari 12, 2019 katika Uwanja wa Gombani, Pemba visiwani humo.

Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein akihutubia mamia ya wananchi na viongozi mbalimbali waliojitokeza uwanja hapo amesema Rais Magufuli amesema hajaudhuria sherehe hizo kwa sababu amepata dharura.

Viongozi wengine waliohudhuria ni; Makamu wa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, marais wastaafu wa Tanzania,  Ali Hassan Mwinyi na Jakaya Kikwete.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya January 14


Serikali Haitabomoa Nyumba Za Watu Waliojenga Katika Makazi Holela

$
0
0
Na Hassan Mabuye, Wizara ya Ardhi
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi amesema kwamba Serikali ya awamu ya tano kuanzia sasa haitabomoa tena nyumba za wananchi waliojenga maeneo ya makazi yasiyo rasmi badala yake itarasimisha makazi holela.

Waziri Lukuvi amesema Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli ametoa fursa kwa wananchi wote masikini waishio mijini waliojenga bila ya kufuata mipango miji na hawana hatimiliki za ardhi kufanyiwa urasimishaji wa makazi yao na wasibomolewe nyumba zao tena kwakuwa haikuwa ni makosa yao kujenga maeneo hayo.

Lukuvi ameyasema hayo alipokuwa wilayani Simanjiro mkoa wa Manyara alipofanya ziara yake ya kusikiliza na kutatua migogoro ya ardhi kwa wakazi wa mji huo, ambapo amesema wananchi wote wachangamkie fursa hii iliyotolewa na Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ya kuwapa fursa ya kumiliki hati katika maeneo ambayo siyo rasmi kwa kurasimishiwa.

“Serikali ya awamu ya tano inajali sana wananchi wake kwakuwa zamani wananchi ambao hawakujenga kwa kufuata mipango miji wangebomolewa nyumba zao, lakini kwa sasa Serikali ya awamu ya tano imeanzisha mpango kurasimisha makazi holela na kuwapatia hati wananchi wote waishio mijini ili waishi katika makazi rasmi” Amesema Lukuvi.

Aidha, Lukuvi amewataka wananchi wote waishio mijini kuwa wazalendo kwa kurasimisha maeneo yao waweze kujipatia hati na ili walipe kodi ya pango la ardhi jambo ambalo litaiongezea Serikali mapato.

Lukuvi alipokuwa ziarani Simanjiro mwishoni mwa wiki aligundua kuwa wakazi wa mji wa Simanjiro walio na hatimiliki za ardhi hawazidi 1,000 wakati nyumba zilizopo ni nyingi zaidi ya idadi hiyo. Hivyo Waziri Lukuvi akawataka wachangamkie fursa hii ya kujipatia hati ili kuzipa hadhi nyumba zao.

“Nyumba isiyokuwa na hati haina thamani kwakuwa hata ukienda Benki kukopa pesa hawatakuuliza umejenga nyumba ya uzuri gani, lakini watakachotaka ni hati yako ya kumiliki ardhi ambacho ndio kitu kilicho na thamani zaidi kwako kuwa nacho” aliongeza Lukuvi.

Naye Mbunge wa Simanjiro Mheshimiwa James Ole Millya ambaye amehamia CCM akitokea Chadema amemshukuru Mhe. Lukuvi pamoja na Serikali ya Awamu ya Tano katika kuwajali wananchi wake kwa kuwaletea maendeleo makubwa na kusimamia suala la wananchi wa kawaida kupata fursa ya kumiliki ardhi kutoka kwa wawekezaji wakubwa ambao walikuwa hawayaendelezi mashamba yao kwa muda mrefu.

Simanjiro ndio wilaya inayoongoza kwa wamiliki wa mashamba makubwa walio na hati na hata wengine wasio na hati rasmi. Kwa sasa wamiliki wa mashamba walio na hati rasmi wanafika 158 yaliyo na hekari zaidi ya 120,000 ambapo wasio na hati ni zaidi ya hao, hivyo Waziri amenza utaratibu wa kufuta mashamba makubwa 55 yanayomilikiwa kwa kuwa wamiliki wake wamekiuka masharti ya umiliki.

Kangi Lugola awasimamisha kazi maofisa watano Kisa Sare za Jeshi Za Burundi Zilizoingizwa Nchini

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola  amewasimamisha kazi vigogo watano wa idara ya wakimbizi kwa madai ya kushindwa kutoa taarifa mapema za uwepo wa marobota  1,947 ya nguo zinazodaiwa kuwa ni za jeshi katika kambi za wakimbizi za Nduta na Mtendeli zilizopo mkoani Kigoma.

Waliosimamishwa ni mkurugenzi wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi,  Harrison Mseke; mkurugenzi msaidizi wa huduma kwa wakimbizi,  Deudsdedit Masusu; mkurugenzi msaidizi huduma kwa wakimbizi usalama na operesheni, Seleman Mziray.

Mkuu wa kambi ya Nduta,  Peter Bulugu na John Mwita ambaye ni mkuu wa kambi ya Mtendeli.

Lugola ametangaza uamuzi wake huo jana Jumapili Januari 13, 2019 katika mkutano wake na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam.

Alisema nguo hizo za msaada zilitolewa na shirika la Uniqlo la Japan kwa ajili ya wakimbizi wa kambi hizo lakini viongozi wa idara hiyo hawakutoa taarifa mapema kwa viongozi wa wizara.

“Mizigo yote ya wakimbizi inayotolewa lazima ikaguliwe lakini hawa walikaa kimya. Uwepo wa nguo hizo hauleti picha nzuri hasa katika kipindi hiki ambacho Serikali ipo katika mchakato wa kuwarudisha wakimbizi Burundi," alisema Lugola.

“Kwa vyovyote nchi ya Burundi itakuwa na mtazamo hasi dhidi ya Tanzania baada ya wananchi wake kupewa nguo za kijeshi. Lazima tuwe makini maana tusipofanya hivi tunaweza tukakuta hadi silaha katika misaada.”

Lugola alisema baada ya kuwasimamisha kazi amemwagiza katibu mkuu wa Wizara hiyo kuunda kamati kwa ajili ya kuchunguza tukio hilo, kuipa siku 10 za kuchunguza.

Lugola ameagiza mamlaka zinazohusika kumchukulia  hatua mratibu  wa wakimbizi kanda ya Kigoma,  Tony Laizer kuhusiana na mchakato huo.

Vyama vya siasa vyaalikwa kutoa maoni muswada wa sheria ya vyama vya Siasa

$
0
0
Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria inatarajia kukutana na wawakilishi wa vyama vya siasa Januari 19 na 20, 2019  kuwasikiliza na kupokea maoni yao kuhusu muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa wa mwaka 2018.

Kamati hiyo itapokea maoni yao baada ya kumaliza vikao vyake na wadau wengine vitakavyofanyika Januari 17 na 18, 2019  mjini Dodoma kuhusu muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa mwaka 2018 na kufuatiwa na mkutano wake na wawakilishi wa kila chama cha siasa chenye usajili wa kudumu hapa nchini ambao wanapinga muswada huo.

Bunge litapokea maoni hayo wakati leo kesi iliyofunguliwa kupinga Bunge kujadili muswada huo ikiwa inatolewa uamuzi mahakamani.

Kesi hiyo ilifunguliwa Mahakama Kuu na wanasiasa watatu ambao ni kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, Joram Bashange na Salim Bimani kutoka Chama cha Wananchi (CUF) kwa niaba ya wanachama wa vyama 10 vya siasa dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).

Waziri Lugola, Mwakilishi UNHCR Wajadiliana Masuala Ya Wakimbizi Waliopo Nchini

$
0
0
Na Felix Mwagara, MOHA
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amekutana na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Chansa Kapaya, ofisi ndogo ya Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo, na kujadiliana masuala mbalimbali ya wakimbizi nchini.

Waziri Lugola pamoja na Mwakilishi huyo, pia walijadiliana masuala ya ushirikiano kati ya Serikali na Shirika hilo la Kimataifa kwa mujibu wa sheria zinazowaongoza.

Akizungumza katika kikao hicho kilichofanyika jana Jumapili, Lugola alisema Wizara yake haiwezi ikafanikiwa kikamilifu katika masuala ya kuwahudumia wakimbizi nchini kama haitashirikiana ipasavyo na UNHCR.

“Licha ya kuwa baadhi ya wakimbizi wanaendelea kurudishwa kwa hiari nchini kwao Burundi, lakini katika kufanikisha zoezi hili, lazima tushirikiane ipasavyo kati ya Serikali pamoja na nyie UNHCR, naamini Wizara yangu itafanya vikao nanyi mara kwa mara ili kufanikisha zoezi hilo pamoja na mengineo yanafanikiwa,” alisema Lugola.

Kwa upande wake Mwakilishi wa UNHCR, Kapaya, alisema Serikali ya Tanzania inashirikiana na Shirika lake vizuri, na jambo lolote la majadiliano linapotokea ujadiliana ili kuweka sawa ushirikiano huo.

“Mheshimiwa Waziri mimi nakushukuru sana kwa kuniruhusu kuja kufanya mazungumza nawe, nimefarijika na haya madiliano na pia tutaendelea kushirikiana zaidi,” alisema Kapaya.

Katika kikao hicho Mwakilishi wa UNHCR aliambatana na Msaidizi wake Zephania Amuiri, na Waziri Lugola aliambatana na Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi wa Wizara yake, Harrison Mseke.

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) Wafungua kesi kushinikiza polisi kuwafikisha kortini watuhumiwa

$
0
0
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefungua kesi Mahakama Kuu ya Arusha, kutaka iwalazimishe polisi kuwapeleka mahakamani watuhumiwa watano wa Loliondo, waliowekwa mahabusu kwa siku saba

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mratibu wa THRDC, Onesmo Olengurumwa, alidai watetezi wa haki za binadamu Clinton Kairungi, Supuk Maoi, Manyara Kaita na wananchi wengine wawili walikamatwa na polisi Janauri 7, mwaka huu.

“Ikumbukwe kwamba kwa mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya Mwaka 1985, mtuhumiwa anapokamatwa, anakuwa na haki mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuambiwa kosa analotuhumiwa nalo, kupewa dhamana, kuonana na ndugu, kupelekwa mahakamani kwa wakati pamoja na kuelezwa haki yake ya kupata msaada wa kisheria," alisema na kuongeza:

“Hata hivyo, watetezi hawa baada ya kukamatwa na Jeshi la Polisi, hawakupatiwa haki yoyote ile kati ya haki zilizotajwa kwa mujibu wa sheria. THRDC ilimpeleka Wakili Samson Rumembe, pamoja na Msaidizi wa Kisheria ndugu Charles Nangoya, kwenda kuwapa msaada wa kisheria, lakini walizuiwa na Jeshi la Polisi hata kuwaona watuhumiwa hao.”

Olengurumwa alisema Wakili Rumembe alipouliza kosa wanalotuhumiwa nalo watuhumiwa, polisi pia hawakutaka kuonyesha ushirikiano na hivyo jitihada za kuwasaidia kupata dhamana zikagonga mwamba.

Alisema: “Mpaka sasa tunavyoongea, watetezi hawa bado wako rumande, jambo ambalo ni kinyume cha Kifungu cha 64(1)(c) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya Mwaka 1985, ambayo inaelekeza polisi kukaa na mtuhumiwa kwa saa zisizozidi 24 kabla ya kuwapa dhamana ya polisi au kuwapeleka mahakamani kwa mujibu wa sheria.”

Akizungumzia hali ya ukiukwaji wa haki za binadamu Loliondo, alisema imeendelea kuwa mbaya siku hadi siku kwa kuwa kuna uharibifu wa mali, ukiukwaji wa haki za binadamu, watu kukamatwa na kuweka mahabusu bila kufikishwa mahakamani.

“Watetezi wa haki za binadamu ambao wapo mstari wa mbele kutetea haki za raia Ngorongoro, wamekuwa wakikamatwa na kufunguliwa mashtaka ya kughushi, ambapo mpaka sasa wapo baadhi ya watetezi Loliondo bado wa wana kesi mahakamani,” alidai.

Kwa mujibu wa Olengurumwa, mwaka 2016, Supuk Maoi na mwenzake Clinton Mshao, walifunguliwa mashataka ya kughushi kwa kutuhumiwa kwa kosa la ujasusi (espionage), lakini walishinda kesi baada ya kupata msaada wa kisheria na kwamba chanzo cha mitafuruku yote ni msimamo wa wanachi na watetezi juu ya mikakati ya siku nyingi ya kutaka kuchukua eneo la wananchi (OSERO) na kuikabidhi moja kwa moja Kampuni ya Uwindaji ya Kiarabu (OBC).

“Katika kipindi chote ambacho mgogoro wa ardhi Loliondo umedumu, tumeshuhudia Jeshi la Polisi likitumia nguvu kubwa kuwashuhulikia watetezi wa haki za binadamu pamoja na raia, huku wakibambikiziwa kesi mbalimbali,” alisema.

Olengurumwa alilitaka Jeshi la Polisi kuwaachia mara moja watuhumiwa hao pamoja na wengine waliokamatwa bila masharti yoyote au wawafikishe mahakamani ili wakakabiliane na mashtaka dhidi yao.

“Pia tunamwomba IGP kuwachukulia hatua OCD wa Ngorongoro pamoja na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha kwa kukiuka utaratibu wa Jeshi la Polisi pamoja na sheria za nchi, ili iwe fundisho wa wengine wanaokiuka,” alisema.

Tundu Lissu Aaanza Ziara Barani Ulaya

$
0
0
Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu ameanza ziara barani Ulaya na leo atakuwa London, Uingereza ambako amesema ataeleza kwa kina kile alichoandika katika waraka aliotoa kwa ajili ya mwaka huu.

Ziara ya Lissu inaanza baada ya Desemba 31, mwaka jana kuhitimisha safari ya matibabu aliyoanza Septemba 7, 2017 baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana kwa zaidi ya risasi 30 mjini Dodoma muda mfupi baada ya kutoka kuhudhuria kikao cha mchana cha Bunge.

Akizungumza na  gazeti la Mwananchi jana, Lissu ambaye hivi karibuni ameeleza nia yake ya kugombea urais kupitia Chadema, alisema leo ataitikia mwaliko wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC).

Lissu alikwenda Ubelgiji Januari 6 mwaka jana kuendelea na matibabu akitokea Hospitali ya Nairobi, Kenya na katika kipindi chote cha matibabu, amefanyiwa upasuaji mara 22.

Alisema baada ya kutoka Uingereza, amepata mwaliko mwingine wa kwenda katika ofisi za Umoja wa Ulaya (EU) zilizopo Brussels, Ubelgiji na baadaye ataelekea Marekani na katika ziara hizo amesema ataelezea kile kilichomtokea Septemba 7, 2017, hali ya kisiasa nchini na mambo mengine.

Katika waraka wake huo alioutoa Januari 5, Lissu alitaja matukio ya uvunjifu wa haki za binadamu huku pia akihoji sababu ya Bunge kutogharamia matibabu yake, mambo ambayo pia amesema kwamba atayaeleza katika ziara yake hiyo.

Waraka huo wenye kichwa cha habari ‘Mwaka mpya 2019, Mwaka wa kurudisha demokrasia, haki za binadamu na utu wetu Tanzania’ umegusia pia masuala ya haki za binadamu yakiwamo matukio ya utekaji, mauaji na mashambulio ya kudhuru mwili.

Credit: Mwananchi

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Hizi Hapa Dawa Za Kutibu Kisukari,nguvu Za Kiume, Na Presha

$
0
0
Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power Kwaajili Ya Nguvu Za Kiuume Na Promix Kwaajili Ya Kuongeza Maumbile;

Kwa mwanaume aliyekamilika na mwenye Afya njema ili kumridhisha mke au mpenzi anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara mbili hapo utamridhisha mpenzi wako ila ukiwa unapiga moja au mbili hapo ujue umejilidhisha wewe 

Tiba Ya Tatizo Lako Ni Dawa Hiitwayo Simpo Power No, 1; dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge vya miti shamba na unga ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja :-1 itakufanya urudie tendo zaidi ya mara tatu 
2 itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika 15-20 kwa tendo la Kwanza 
3 huimarisha uume uliolegea na kusinyaa 

Je Una Mke Au Mpenzi Aliyebalikiwa Kuwa Na Kario Kubwa Au Mwili Mnene Na Wewe Mume Wake Una   Maumbile Mafupu?; tumia sasa dawa ya PROMIX dawa itakufanya umfikishe shemu nyeti maana inaboresha maumbile saizi upendayo.

Dawa zangu haziina madhara yoyote kwa mtumiaji 

MARKSU; ni dawa ya kisukari dozi siku 21 
MWARU; ni dawa ya uzazi,hufungua milija ya uzazi ata kwa Wale waliofungiwa uzazi  
MTUNDUU; ni dawa ya busha bila kupasua 
MAZANZA; ni dawa ya kisukar zipo dawa za miguu Kuuma,tumbo,kupunguza Matiti,kutoa minyama uzembe ngiri,vidondo vya tumbo  

FIKA OFISINI KWANGU BUGURUNI MALAPA ,MOROGORO YUPO WAKALA MAENEO YA STENDI KUU MWANZA YUPO MTAA WA BIZA C NA KAHAMA MJINI na kama hauna nafasi ya kufika ofisini utaletewa ulipo uduma hii piga simu 0783185060  0752348593 DR AGU

Mawaziri Watano Watembelea Mradi Wa Kufua Umeme Stiegler's Gorge

$
0
0
Na.Lusungu Helela-Morogoro
Serikali imesema maandalizi ya miundombinu wezeshi kabla ya kumkabidhi Mkandarasi aliyepewa kazi katika Mradi wa kufua umeme wa Mto Rufiji tayari imekamilika kwa asilimia themanini.

Miundombinu hiyo ni pamoja na maji, umeme, barabara pamoja na  nyumba za kukaa wafanyakazi.

Kauli  hiyo imetolewa jana na Mawaziri wa Wizara tano  kutoka Nishati, Maliasili na Utalii, Nyumba, Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,  Fedha na Mipango baada ya kutembelea na kujionea miundombinu hiyo ambayo kwa kiasi kikubwa imeshakamilika.

Ziara hiyo katika Pori la Akiba la Selous kanda ya Matambwe mkoani Morogoro iliongozwa na Waziri wa Nishati, Dkt.Medard Kalemani ikilenga kukagua hatua zilizofikiwa katika ujenzi wa miundombinu wezeshi ili kumuwezesha Mkandarasi kuanza kusafirisha mizigo kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo.

Alisema kukamilika kwa miundombinu hiyo kutamuwezesha Mkandarasi huyo kuanza maandalizi ya awali ikiwemo kuanza kusafirisha mizigo kuileta katika maeneo ya ujenzi wa bwawa.

Aliongeza kuwa kutokana na Mkataba uliopo Mkandarasi huyo ataanza kazi rasmi Juni 15 mwaka huu na ataukamilisha mradi huo ifikapo mwezi  April 2022.

Katika upande wake  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu alitoa tahadhari kwa wafanyakazi wanaokuja kufanya kazi katika mradi huo wasiende kupumzika vichakani kuna wanyama wakali kama vile Simba, Nyati pamoja na  tembo.

" Wale wenye tabia ya kujipumzisha vichakani baada ya kufanya kazi chonde chonde jiepusheni na haya mazoea la sivyo mtaliwa na Simba.

Aidha, Mhe.Kanyasu alitumia fursa hiyo kuiomba Wizara ya Utumishi kutoa kibali cha kuajiri Askari Wanyamapori zaidi ya 200 ambao watatoa ulinzi kwa Wafanyakazi wa mradi huo,

Ombi hilo linakuja kufuatia Askari wanyamapori 115 kutoka mapori mengine kuhamishiwa kwa muda  katika Pori hilo  katika kanda ya Matambwe kwa lengo la  kuongeza nguvu baada ya askari 115 waliokuwepo kuonekana hawatoshi.

Hata hivyo , Mhe.Kanyasu alisema  hatua za haraka zimeanza kuchukuliwa ikiwa ni pamoja  kutengeneza  vyoo, malazi pamoja na maji kwa vile miundombinu iliyokuwepo katika Kanda hiyo ilikuwa na uwezo wa kuhudumia Askari Wanyamapori 85 tu lakini hadi hivi sasa kuna jumla ya askari 230.

Kukamilika kwa mradi huo wa kufua umeme, Bwawa hilo la Rufijin litakuwa la nne kwa ukubwa kwa Afrika na la kwanza kwa Afrika Mashariki, Duniani ni la 60 katika ya mabwawa sabini makubwa.

Mbunge kuwasilisha hoja binafsi Bungeni Kuhusu lugha ya kufundishia

$
0
0
Tiganya Vincent, Tabora
Mbunge wa Tabora Kaskazini,  Almas Maige (CCM), amesema wakati umefika kwa Watanzania kuanza kutumia   Kiswahili kwa ajili ya kufundishia katika shule za sekondari na elimu ya juu kwa masomo yote.

Amesema hatua hiyo itasaidia kuwawezesha vijana wengine kuelewa wanachofundishwa na kuwa na ufanisi katika utendaji kazi.

Maige alisema hayo jana mjini Tabora alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu hoja yake aliyoiwasilisha bungeni  kutaka Kiswahili kitumike kama lugha ya kifundishia na kujifunza katika shule za sekondari na vyuo  nchini.

Alisema utafiti uliofanywa na wataalamu na wanazuoni mbalimbali umeonyesha  asilimia 50 ya wanafunzi hawaelewi wanachofundishwa kutokana na matumizi ya Kiingereza.

Maige alisema hata wanavyuo vya ufundi wanaofundishwa kwa   Kiingereza wanapomaliza masomo yao wanapokuwa kazini hawatumii lugha hiyo katika kutekeleza  majukumu yao ya kila siku bali wanatumia Kiswahili.

Mbunge huyo wa Tabora Kaskazini alisema   tayari maandalizi ya vitabu vya kufundishia kidato cha kwanza kwa masomo yote vimekamilika pamoja na kamusi kubwa ya tafsiri wa maeneo yote ya Kiswahili iko tayari.

Alisema  wataalamu walioandika vitabu hivyo wanasema ikiwa Kiswahili kitaanza kutumia wako tayari kuandaa na vitabu vya kidato cha pili na kuendelea kwa muda mfupi na wanafunzi waanze kuvitumia.

Maige alisisitiza kuwa kwa juhudi hizo za wataalamu hakuna sababu ya kuendelea kutumia lugha ambayo baadhi ya wanafunzi  hawaelewi wanachofundishwa.

Alisema  hata wananchi wamekuwa wakizielewa zaidi hotuba za Rais Dk. John Magufuli na mijadala ya vikao vya Bunge kwa sababu ya matumizi ya Kiswahili.

Maige alisisitiza kuwa wakati umefika wa kumuunga mkono Rais Magufuli kwa moyo wake aliouonyesha wa kukiimarisha Kiswahili ndani na nje ya Tanzania  anapohutubia mikutano mbalimbali.

Makanga 3 Power, Dawa Bora Za Nguvu Za Kiume

$
0
0

Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.

Tupo dar es salam Buguruni

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images