Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

TPSC Yatakiwa Kutoa Mafunzo Yatakayowawezesha Watumishi Wa Umma Kuboresha Huduma Kwa Wananchi

0
0
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk. Mary Mwanjelwa, amewataka watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) kutoa mafunzo bora yenye kuzingatia weledi.

Alisema mafunzo hayo yawajengee uwezo wa  utendaji watumishi wa umma wanaopata fursa ya kujiendeleza katika chuo hicho.

Wito huo aliutoa   Dar es Salaam jana alipozungumza na watumishi wa TPSC makao makuu na Kampasi ya Dar es Salaam wakati wa ziara yake  yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji, kufahamu majukumu ya TPSC na kujiridhisha na utendaji kazi wa chuo hicho.

Dk. Mwanjelwa aliwahimiza watumishi wa TPSC kuwa wabunifu kwa kuboresha mitaala itakayowaandaa vema watumishi wa umma, sekta binafsi na wananchi wanaohitimu katika chuo hicho  waweze kuwa na mchango katika maendeleo ya taifa.

Alisema katika dunia ya sasa, jamii inabadilika, uchumi unabadilika na siasa inabadilika pia, hivyo amewataka watumishi wa TPSC wabadilike kwa utendaji wao uwe wenye kujali matokeo na wenye tija.

  Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Dk. Henry Mambo, alisema TPSC ilianzishwa  kusaidia hatua ya kujenga uwezo wa watumishi wa umma uwe wenye kujali matokeo katika kutoa huduma bora kwa umma.

Alisema kwa sasa chuo kina matawi sita yaliyopo Dar es Salaam, Mtwara, Singida Tabora,Tanga na Mbeya.

Alisema madhumuni ya kuanzisha chuo ilikuwa ni kuziba pengo lililokuwapo la kukosekana   chuo rasmi kinachoshughulikia mafunzo ya watumishi wa umma  waendane na mabadiliko yaliyoletwa na maboresho katika utumishi wa umma.

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 52

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA  
     
“Mbezi ya chini”
“Ndio ipi?”
Niliwauliza walilinzi.
“Hapo anazungumzia Mbezi ya Kimara”
“Si unapakumbuka nyumbani?”
“Ehee napakumbuka”
“Wewe na wewe ingieni kwenye gari tuelekee huko”
“Sawa mkurugenzi”
Tukaingia kwenye gari na walinzi wa kampuni yangu na taratibu tukaianza safari ya kuelekea Mbezi ya kimara huku Clara akituelekeza njia ya kuweza kufika kwao.
   
ENDELEA
“Mkurugenzi”   
Mlinzi niliye kaa naye siti  ya mbele aliniita kwa sauti ya upole, nikamuitikia huku nikimtazama usoni mwake.
“Bila ya kukuvunjia heshima, nina wazo”
“Zungumza tu”
 
“Kwa mtazamao wangu ninaona kuelekea nyumbani kwa huyu binti sio jambo sahihi, unaonaje tukaanza na taratibu za kisheria kwa mfuno kuelekea polisi, kule kuna kitengo kabisa kinashuhulika na watoto wa aina hiyo na tukitoka huko basi tutakuwa na hata nguvu ya kuelekea kwao”
Nikajifikiria kwa muda kwani wazo  hili alilo litoa huyu mlinzi  wa kampuni yangu ni zuri sana.
“Alfau kweli, sasa tunaelekea katika kituo gani cha polisi?”
“Kituo kikuu cha kati nina imani kwamba ndio kituo kizuri, wanaweza kusikiliza shida yetu”
“Sawa nielekezeni”
 
Mlinzi huyu akaanza kunielekeza njia za kupita kwa maana jiji hili la Dar es Salaam, mimi bado ni mgeni kwa baadhi ya maeneo. Tukafika katika kituo hicho, tukakaguliwa kabla  ya kuingia ndani. Baadhi ya askari walianza kuulizana mara baada ya kuniona nikiwa nimesimama kwenye moja ya foleni huku nikiwa nimemshika mkono Clara.
“Samahani kaka sogea hapa”
Askari mmoja wa kike ambaye yupo eneo la mapokezi  aliniita, taratibu tukasogea eneo alipo.
“Tuwasaidie nini?”
“Ahaa kuna swala la huyu binti hapa, kama tunaweza kuzungumza ofisini basi ningeomba msaada huo”
“Afande Mwanaidi hembu mchukue huyu kaka na mukafanye mazungumzo naye ofisini”
Afande huyu wa kike alitoa maelekezo kwa mwenzake, tukaongozana na Afande Mwanaidi hadi kwenye moja ya ofisi, akatukaribisha na tukaketi kwenye viti vilivyomo katika eneo hili. Nikanza kuelezea jinsi nilivyo kutana na mtoto huyu, kisha Mery naye akahojiwa historia ya maisha yake. Kila ambacho ytulikizungumza afande Mwanaidi alikiandika kwenye faili.
“Nisubirini”
Afande Mwanaidi alizungumza huku akinyanyuka kwenye kiti chake na tukatoka ndani ofisi hii. Baada ya muda kidogo akarejea na baba mtu  mzima mwenye kitambi kikubwa kiasi huku begani mwake akiwa na nyota kadhaa ambazo sifahamu ana cheo gani katika jeshi hili la polisi.
“Kijana kwa maelezo niliyo pewa ni kwamba umemuokota huyu binti”
“Ndio hujakosea mzee”
“Sawa. Binti unapakumbuka kwenu?”
“Ndio”
“Mwanaidi andaa askari wanne ninakuja”
“Sawa mkuu”
Afande Mwanaidi akatoka humu na kutuacha na huyu mzee.
“Naitwa Kimaro ni mkuu wa polisi kanda maalumu”
“Nashukuru  kukufahamu mzee mimi ninaitwa Ethan”
“Sura yako sio ngeni machoni mwangu. Wewe ndio yule mchezaji  wa mpira?”
“Ndio mimi”
 
“Ohoo karibu sana Tanzania”
“Nashukuru, kuna jambo jengine ambalo hatukukueleza afande aliye toka. Kuna haya makovu mgongoni mwa huyu binti hakika yameniumia sana moyo wangu”
Nilizungumza huku nikiinyanyua tisheti hii ya Clara mgongoni mwake, mkuu  wa polisi akashikwa na butwaa, kwani ni makovu makubwa sana.
“Yaani kwa uzee wangu wote huu na mambo mengi niliyo pitia katika jeshi la polisi ila sijawahi kuwa na makovu kama haya. Aisee kuna watu wanyama sana hapa duniani. Binti aliye fanya hivi ni nani?”
“Baba mdogo na mke wake”
Mlango ukafunguliwa akaingia afande Mwanaidi.
“Mkuu tayari”
“Sawa ninakuja”
 
Afande Kimaro alizungumza huku akiendelea kutazama majeraha ya Clara mgongoni ambayo kwa namna moja ama nyingine pia yalimshangaza afande Mwanaidi. Tukatoka ofisini humu, askari wakaingai kwenye gari lapo pamoja na mkuu wao nasi tukaingia kwenye gari tulilo jia na walinzi wa kampuni yangu kisha tukaanza safari ya kueleka nyumbani kwa baba mdogo wa Clara huku gari  letu likiwa limetangulia mbele. Kutokana na foleni za hapa na pale ikatuchukua lisaa zima kufika katika nyumba moja kubwa ya kifahari ambayo ina gorofa moja kwa juu. Tukashuka kwenye magari, mkuu wa polisi kanda maalumu, akatembea hadi getini, akagonda kwa muda kidogo na mlango ukafunguliwa na mlinzi wa nyumba hiyo.
 
“Bosi wako tumemkuta?”
“Nd…ioo…o”
Mlinzi alijibu kwa kigugumizi, mkuu wa polisi akaanza kuingia na askari wengien wakimfwatia kwa nyuma akiwemo askari anaye mlinda. Nami nikaingia ndani ya nyumba hii huku tukiwa nimeshika mkono Clara. Akatoka msichana mmoja mweupe kiasi huku akiwa amevalia kijisketi kifupi.
“Kuna nini kinacho endelea?”
Clara akajificha nyuma yangu mara ya msichana huyo kutazamana nasi.
“Huyo ndio ma mdogo”
“Mpigeni pingu huyo kwanza, na mume wako yupo wapi?”
“Jamani kuna nini, munanikamataje nikiwa sina kosa jamani”
Maneno ya msichana huyu hayakuwazuia askari hawa kumpiga pingu mikononi mwake. Akatoka kijana kwa kukadiria ana umri wa miaka kama thelathini hivi.
 
“Baby nini kinacho endelea?”
Alizungumza kwa sauti ya mapozi,  Clara huku machozi yakimwagika usoni mwake, akanyoosha  mkono kwa mwanaume huyu.
“Ndio baba mdogo?”
Nilimuuliza Clara huku nikimtazama usoni mwake, Clara akanijibu kwa kutingisha kichwa kwamba ndio huyo baba yake mdogo. Askari wakamkamata kijana huyu naye akapigwa pingu, askari wakawaingiza nani ya nyumba hii nasi tukaingia, hatukuamini macho yetu kukuta pakti kadhaa za madawa ya kulevya zikiwa mezani eneo  la hapa sebleni, huku misokoto ya bangi na pombe kali nazo zikiwa juu ya meza hii.
 
“Washenzi kabisa, kagueni nyumba nzima”
Mkuu wa kituo kanda maalumu  alizungumza na askari walianza kutawanyika huku wengine wakipandisha gorofani wakiwa na bunduki zao. Clara akakimbilia moja picha iliyopo pembezoni mwa meza ya tv kubwa. Akaikumbatia picha hiyo huku akiendelea kulia kwa uchungu sana, nikamsogelea na kuitazama picha hiyo na kukuta, akiwa yeye pamoja na wazazi wake baba na mama.
“Mkuu tumekuta begi hili, lina pesa za kigeni”
Askari mmoja alizungumza huku akiwa anashuka kwenye ngazi na kuelekea gorofani. Begi kubwa kiasi la mgoni likawekwa mbele ya mkuu wa polisi. Pesa za kigeni, dola za kimarekani zimejaa katika begi hili.
 
“Pumbavu hawa ni wauzaji wa madawa ya kulevya. Clara unafahamu juu ya hilo swala?”
Mkuu wa polisi alimuuliza Clara. Clara akatingisha kichwa akimaanisha kwamba ana fahamu.
“Ohoo Mungu wangu. Pigeni picha vidhibitisho vyote kisha hakikisheni kwamba hawa waalimu  wanafika kituoni”
“Sawa mkuu”
“Wewe mtoto wewe mtoto hujakomaa eheee?”
Baba mdogo wa Clara alizungumza huku akimtazama Clara kwa hasira sana. Askari mmoja akamzaba kofi zito la usoni.
“Kaa kimya, washenzi nyinyi”
 
“Nikitoka Clara nakata shingo yako hiyo, nakuapia haki ya Mungu nakata shingo yako”
“Twende bwana”
Baba mdogo wa Clara alisindikizwa na mateke ya askari walio wakamata. Wakapakizwa kwenye gari la polisi huku sisi tukibaki na mkuu wao pamoja na mlinzi wake.
“Hawa watu ni washenzi sana, kumbe chanzo cha kummpa mateso huyu binti ni kutokana na hii biashara yao”
“Hata mimi nahisi hivyo mkuu”
“Tunashukuru sana Ethan na hawa tunakwenda kuwabana na kuhakikisha kwamba wanatueleza juu ya wasambazaji wezao wa madawa ya kulevya”
 
“Sawa sawa mkuu nitashukuru sana kama mukilichukulia hatua jambo hili na kama inawezakana wakapolelee kabisa jela, kwa maana kama mulivyo msikia baba mdogo, anakiri kwamba lazima atamuua huyu binti, sasa hiyo ni hali ya kumtishia”
“Kweli, ila nitahakikisha kwamba sheria inafwata mkondo wake”
“Nashukuru, huyu binti mimi ngoja nimpeleke sehemu hivi akafanyie matibabu na usafi wa mwili wake, nitajitahidi kumuwekea wana sheria wenye uwezo mkubwa, kuhakikisha kwamba wanasimamia kesi yake na mali za wazazi wake zinarudi mikononi mwake.”
“Sawa sawa Ethan, laiti kama Tanzania tungekuwa na vijana kumi kama wewe, wenye mioyo kama yako nina imani kwamba nchi hii isinge kuwa na omba omba wengi hivi”
“Nashukuru sana mkuu”
Polisi wengine wakafika katika eneo hili, tukaaga na nikaondoka na Clara, tukiwa njiani ndani ya gari nikampigia simu Biyanka na kumueleza kila jambo lililo tokea, Biyanka akashangazwa sana na akaniomba nimpeleke Clara nyumbani kwake akapatie huduma na msichana wake wa kazi.
“Ngoja kwanza nimpeleke hospitalii, akifanyiwa huduma zote za kiafya ndio aelekee nyumbani”
“Sawa mume wangu, naona nitachelewa kurudi, si unajua mambo ya siasa haya”
“Usijali mpenzi wangu”
“Sawa baadae”
Nikakata simu na kuelekea hospitali. Nikalipa matibabu ya Ckara yoye na madaktari wakanishauri waweze kumpumzishwa kwa siku ya leo kwa maana wanahitaji kumuongezea maji mwilini pamoja na damu  kwani afya yake ime dhohofika sana. Nikakubaliana na madaktari hawa huku nikiahidi kwamba nitarudi siku inayo fwata ili nimjulie hali kisha nikaanza safari ya kuelekea hotelini kujipumzisha.
                                                                                                               ***
Asubuhi na mapema nikaelekea hospitalini na kukuta hali ya Clara ikiendelea vizuri sana.
“Naamini akikaa hapa kwa siku ya leo, kesho basi tunaweza kumruhusu”
Daktari niliye muaachia jukumu la kumtazama alizungumza huku tukiwa tumesimama pembezoni mwa kitanda cha Clara.
“Je vipimo vingine vipo vizuri”
“Ndio, ila ana Malaria pamoja na UTI ila magonjwa yote hayo tumesha anza kumpatia dozi kwa kumchoma sindao na kesho atamalizia sindano hizo”
“Clara unajisikiaje?”
“Safi tu Ethan, nashukuru kwa msaada wako”
Clara alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake.
 
“Ohoo usilie mtoto mzuri, ni jukumu langu kuhakikisha kwamba unakuwa salama, sawa”
“Sawa”
Simu yangu ikaanza kuita, nikaitoa mfukoni na kukuta ni Biyanka ndio anaye nipigia. Nikatoka nje ya chumba hichi ili niweze kuzungumza naye.
“Umeamkaje mume wangu”
“Salama, vipi wewe”
“Safi upo hoteli au?”
“Hapana nipo hospitalini hivi sasa, nimekuja kumtazama mtoto”
“Ohoo anaendeleaje?”
“Yupo vizuri”
“Sawa, ila samahani mume wangu, leo hatuto weza onana kwa sababu, tutatakiwa kwenda Mwanza na mama kuna wanawake wengine anakwenda kuonana nao hivyo tunaweza kurudi usiku na ndege au tukarudi kesho asubuhi.”
“Ohoo sawa, ila kuwa makini”
 
“Usijali mume wangu, nipo makini sana katika kila hatua ya maisha ninayo ipiga”
“Sawa mimi nitashinda hapa na huyu binti kisha nitakwenda kazini mara moja. Tutawasiliana”
“Sawa mume wangu, nakupenda sana”
“Ninakupenda pia mke wangu”
Biyanka akakata simu na nikairudisha mfukoni mwangu, nikarudi chumbani humu na kujikuta nikiwa nimejawa na mshaongo kwa maana dokta nimemkuta akiwa amelala chini huku damu nyingi zikiwa zinamwagika shingoni mwake na Clara akiwa hayumo ndani ya chumba hichi huku dirisha  moja la chumba hichi likiwa lipo wazi jambo lililo nipa ishara kwamba kuna jambo  la hatari lililo tokea katika eneo hili.

==>>ITAENDELEA KESHO

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 188 na 189 )

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   
Akaingia msichana mrefu, mweupe amevalia gauni jeusi lenye mpasuo mkubwa hadi karibi kabisa na kiuno chake, paja lote la mguu wa kulia lipo wazi. Nywele zake ni ndefu zinaning’inia mgongoni mwake na baadhi zimeficha jicho lake la kushoto kidogo. Umbo lake ni namba nane yenyewe, kwani ana hispi ambazo kusema kweli zinanitamanisha.
“Dany huyu anaiwa Magreti, ndio utakuwa naye kwenye kazi unayo kwenda kuifanya ya kumkamata Osama Bin Laden”
‘Mmmmm kweli lazi itafanyika hapa?’
Nilizungumza kimoyo moyo huku nikiendelea kumtazama binti huyu aliye jaribu kunipa mkono wake wa kulia ila nikabaki nikimazama kwani ni mzuri kupindukia hata Livna mwenyewe hamfikii msicha huyu hata nusu yake.
   
ENDELEA
“Dany si unapewa mkono?”
Livna alizungumza huku akinigonga kidogo kwenye bega kangu an kujukuta nitoka kwenye dibwi la mawazo la kumfikiria msichana huyu.
 
“Ndio habari yako”   
Nilizungumza huku nikimabidhi mkono msichana huyu, akatabasamu na kunifanya nizidi kujawa na bumbuwazi  kwani kwenye maisha yangu sijawahi kukutana na msichana mzuri kama huyu, japo nilio wahi kukutana nao ni waziru ila huyu amewazidi wezake kwa asilimi zote mia moja.
“Salama”
Nikashindwa hata kuijibu salamu yake kwani msisimko ninao upata hapa ukaanza kumuamsha jogoo wangu taratibu. Nikameza funda zito la mate kisha nikauachia mkono wa huyu msichana.
“Bado Osama yupo Tanzania?”
Niliuliza ili kuipoteza hali ya uchu wa mapenzi nilio nao juu ya huyu msichana ambaye kusema kweli ni kibarua kikubwa cha kupambana na hisia zangu.
 
“Bado hajaondoka Tanzania na leo usiku kutakuwa na sherea ya mtoto wa shemeji yake anaoa. Na harusi hiyo ndio iliyo mfanya kubaki nchini Tanania”
“Amejiingiza machinjioni”
”Hatari moja ni kwamba katika hiyo ulinzi ni mkali sana, ukiachilia mbali tu watu wake basi kuna NSS ya Taania na wana FBI kutoka Marekani”
“Wote wanafanya nini?”
Niliuliza huku nikiwa nimejawa na mshangao mkubwa sana.
“Wanamlinda Osama, sasa itakuwa ni ngumu sana kuweza kumteka katika hiyo harusi”
 
Ester aliendelea kunipatia maelekezo huku akinitazama usoni mwangu.
“Na hapo Dany humuwezi kutumia bunduki ni lazima itakuwa ni hatari kwenu”
Livna naye alisisitizia katika hilo.
“Ila kuna njia ambayo munaweza kuitumia”
Logate alizungumza huku akinikabidhi simu aina ya iphone 7.
“Kupitia hiyo simu tutakusaidia kukutumia video za kamera zote ambazo zipo ndani ya huo ukumbi. Mbili kuna hivi viji layer vya macho ya bandia, unatakiwa kuyavaa, ili hata kukitoke kukafanyika ukaguzi  wa macho basi hakuna anaye weza kukugundua kwamba wewe ndio Dany”
Logate alizungumza huku akitoa viji leyer vya macho na kunivisha katika macho yangu. Akanikabidhi kioo, macho yangu yangu yamebadilika mboni yake na kuwa mboni ya kijani kwa mbali jambo lililo zidi kunipendezesha.
“Ingia upande wa wa picha katika hiyo simu”
Logate alinipatia maelekezo na nikafanya hivyo.
“Jicho lako la upande wa kushoto utaweza kuona jinsi muonekano wa watu kwa ndani, it’s mean unaweza kutuona sote hapa nguo zetu za ndani”
“Kweli bwana”
Nikata kumgeuzia Logate simu hii ila Livna akaniwahi.
“Hembu acha utoto Dady, sikiliza maelekezo”
“Unataka nikuone wewe tu ehee?”
“Ndio”
“Sawa mama, mwalimu wangu ehee endelea”
“Lengo la kuweza kuitumia program hiyo ni nini haswa, ni kuhakikisha kwamba unaweza kumuona kila mlinzi mwenye silaha ndani ya ukumbi mzima, pili utaweza kuiona sura ya Osama vizuri kwani kuna watu watakuwa wamejifunga vilemba usoni mwao na kubakisha macho ilimradi kutoweza kumtambua Osama ni yupi”
 
“Sawa sawa”
“Magreti si unanielewa vizuri?”
“Ninakuelewa Logate”
“Na wewe Magreti simu yako hiyo hapo, na ina uwezo kama huu wa Dany hapo. Na wewe itakulazimu kuvaa hivi viji leyers vya macho kwa maana kupitia macho yako nawe rekodi zako wakizidaka basi utatiliwa mashaka. Hapa tumewatengenezea vitambulisho vya uraiAi nchini , ambavyo kwa Dady utatumia jina la Mpoki Samweli na Magreti utatumia jina la Nagenjwa Petro”
“Wewe Logate majina ya wapi haya jamani?”
Niliuliza huku nikitazama kitambulisho changu.
“Wewe ni Muhaya na Magreti weweni Mpare sawa?”
“Sawa ila hili jina la Mpoki ahaaa sio haki jamani”
“Dany be serious”
 
Livna alizungumza huku akinikazia macho.
“Tuendelee, nina imani kwamba kila mmoja ana silaha zake, ila katika ukumbi ambao mutaingia nilazima gari zetu zitakaguliwa, sio kukaguliwa kwa kutazamwa kwa macho. Ila computer ndio itakuwa na kazi ya kukagua gari lenu. Sasa kuna gari aina Aud A7, ambayo ipo huko  chini ya meli, mutaondoka nayo sasa hivi”
“Usiniambie kwamba ina uwezo wa kutembea juu ya maji?”
“Hapana, munaondoka na boti kubwa, mutapelekwa hadi katika fukwe za Kigamboni, kisha mutapita katika daraja na kuitokea katikati ya jiji. Sasa maana yangu ni kwamba mutaacha silaha zenu ndani ya gari, mukiwa munaingia ukumbini, na hakuna program yoyote ya kukagulia magari itakayo weza kuona silaha zenu, japo itawaonyesha nyinyi katika mfumo wa mafuvu ya watu pale munapo kaguliwa”
“Kwa hiyo watauona nguo za ndani?”
“Hapana, watawaona nyinyi katika mfumo wa mafumfu tu kwa ndani”
 
“Sisi nasi tutajiona?”
“Hapana, mtaalamu atakaye kaa kwenye computer hiyo ndii atakaye weza kuona kila kitu, si nyinyi tu bali wageni wote watakao ingia kwa miguu, magari wataonekana hivyo”
“Hapo nimekupata”
“Kuna hii kadi, hapa. Ukiitazama unaweza kusema kwamba ni kadi ya benki, ila hii ndio kadi ya harusi sasa. Ukifika mlangoni utawakabidhi hii kadi wakaguzi nao wataweza kuipitisha kwenye mashine ya ukaguzi na majina yenu yataokea. Kumbuka kwamba Dany unaitwa Mpoki Samweli na Mage”
“Nagwenjwa”
Magreti alimuwahi kumjibu Logate na kunifanya nimtazame kisha nikatabasamu.
“Picha zenu zitatokea katika kadi hiyo”
“Picha mulinipiga saa ngapi?”
“Sasa hivi ulivyo simama hapo”
Nikamtazama Ester nikamuona akininyooshea dole gumba ikionyesha kwamba yeye ndio aliye nipiga picha anayo izungumzia Logate.
“Kuna hivi vinasa sauti kila mmoja avae kwenye sikio lake, mutaweza kuwasiliana nasi moja kwa moja”
“Nimevimisije hivi vidumwana, nakumbuka nilivivaa kipindi nilipokuwa nina oparesheni ya kuliangamizi kundi la Al-Shabab”
“Dany mbona unaongea sana leo, unafuraha. Hembu tilia maanani kwa kazi unayokwenda kuifanya basi”
Livna alizungumza kwa kulalamika kidogo, nikamkonyeza huku nikitabasamu na kumfanya akenue midomo yake akionyesha kupuuzia mkonyezo wangu.
“Kuna hii sindano ndogo, Magreti unaweza kuficha kwenye nywele zako, hiyo sindano utamchoma nayo Osama na italewesha, na atakusikiliza kila utakacho muambia. Hakikisha kwamba unautumia uzuri wako kumteka mzee huyo”
 
“Sawa”
Magreti akapokea kisindano kidoho na kichomeka katika nywele zake na si rahisi kwa mtu kuweza kufahamu kwamba ana sindano ndogo.
“Baada ya hapo nina imani kwamba kila kitu kitakuwa kimekamilika kwa upande wenu. Sisi kazi yetu itakuwa ni kuwapa maelekezo kuhakikisha kwamba munakwenda salama na kurudi salama kama tulivyo kubaliana”
“Tunashukuru”
“Ninawatakia kazi njema”
“Asante Ester”
“Twende tukawaonyeshe gari mutakayo tumia”
Ester alizungumza, tukatoka katika chumba hichi huku Livna akitufwata.
“Dany mpenzi wangu ninakuomba uwe serious katika hii kazi, kumbuka tayari umesha pandikiza kitu kwangu, sinto kubali kukuona unaingia kwenye matatizo”
 
“Mungu nisaidie, nitakuwa serious nitahakikisha kwamba ninarudi salama sawa”
“Sawa mpenzi wangu mimi ninakuombea kwa Mungu. Magreti hakikisha kwamba unamlinda huyu”
“Sawa mkuu”
Tukafika katika sehemu maalumu ambayo boti maalumu huwa ndipi zinapo tokea, tukakuta boti moja ikiwa tayari imesha andaliwa huku kukiwa na gari nzuri yenye rangi nyekundu.
“Dany hembu shika kioo cha upande wa dereva”
Nikauweka mkono wangu. Logate akaanza kuminya minya tablate yake kubwa, mlango ukafunguka.
“Utaweza kuifungua hiyo gari kwa mkono wako wa kulia. Mage na wewe weka mkono wako kwenye mlango upande wa dereva. Dady wewe funga mlango”
 
Nikaufunga mlango, kusema kweli dunia inazidi kukua na tecknologia inazidi kuchukua nafasi kwenye maisha ya watu.
“Tayari, sasa nyinyi kupitia mikono yetu ya kulia munaweza kufungua mlango wa hilo gari, hakuna mtu mwengine atakaye weza kufungua. Gari unawasha kwa hiyo batani iliyo andikwa start engine. Itawaka na utaweza kuendesha”
“Halina funguo?”
“Hakuna funguo. Ingieni ndani ya gari”
Tukaingia ndani ya gari huku nikikaa upande wa dereva.
“Angalizo, ambaye hatofunga mkanda wa siti aliyo kalia awe dereva ama abiria wa siti ya mbele wala nyuma, gari haliwaki sasa muwe waangalifu katika hilo”
“Mmmmmm kazi kweli kweli”
“Yaa ndio magari ya kisasa. Kitu kingine, hii gari haiingii sirasi, pia ina uwezo wa kubadilisha mfumo wa rangi yake ya nje, hapo kuna rangi tatu. Hii nyekundu, nyeupe na  nyeusi. Kila rangi ina namba zake za usajili sasa inaweza kuwa rahisi kwenu kubadilisha muonekano wa gari lenu pale endapo kutakuwa na hatari itakayo wafanya mufanye hivyo.”
“Tunabadilishia wapi hiyo rangi?”
 
“Mimi ninafahamu”
“Magreti anafahamu, so vitu vya ndani ya gari atakuelekeza kama wewe ndio utakuwa dereva?”
“Mfuno wake ni manuel au automatics?”
“Ina mifumo yote miwili chaguo ni lako wewe mwenyewe”
“Ohoooo sawa sawa”
“Kwa mimi nimemaliza, nami nitawakie safari njema”
“Tunashukuru”
Livna akainama kwenye dirisha langu, akanitazama kwa muda huku akitabasamu kinyonge.
“Dany fanya hii kazi ila kumbuka kwamba huku nyuma umeacha watu wawili wenye viumbe vyako, watatu ni Yemi ambaye amekwenda kuchukuliwa, hakikisha kwamab hii kazi unaifanya kiumakini mpenzi wangu sawa”
 
“Usijali mama”
“Mungu awatangulie”
Livna bila kujali wasichana wake hawa wawili waliopo katika hili eneo, akaninyonya midomo yangu taratibu huku akinitazama usoni mwangu kwa macho malagevu.
“Mage, mlinde huyu”
“Sawa mkuu, atarudi salama”
“Jamani kushuka je, kuna haja ya kuweka mkono kwenye kioo?”
“Hapana, unafungua mlango kama kawaida”
“Ahaaaa hapo sawa”
Livna na Logate wakatoka katika boti hii ambayo ni kubwa kiasi yenye uwezo wa kubeba gari hili la kifahari ikaanza safari huku ikiendeshwa na msichana mmoja.
“Tutachukua masaa mangapi kufika Tanzania?”
“Masaa kama manne au matano”
“Duu kumbe kuna umbali ehee?”
“Ndio”
Nikabaki kumtazama Magreti kwa macho ya matamanio. Hakulijali hilo, kwani anatambua kwamba mimi ni mume wa bosi wake. Ili hali ya matamanio isiendelee humu ndani, nikafungua mlango na kutoka, nikaanza kutazama mandhari ya hii bahari kwani tangu siku nifike hapa sijawahi kutoka kabisa. Magreti naye baada ya muda kidogo akashuka kwenye gari na kunifwata sehemu nilipo simama.
“Kwa mavazi yako utaweza kupambana kweli?”
“Yaa tena yananipa uhuru mzuri sana wa kufanya chochote ninacho jisikia”
“Upo vizuri”
“Kwenye nini?”
Nikatamani kumsifia ila ninashindwa kwani mazungumzo yetu yote Livna na watu wake wanayasikia.
“Kupambana na nguo hizo”
“Kawaida, ukiwa unaifanya hii kazi inabidi uwe unaweza kupamba kwa kila vazi, liwe ni shele, suruali, baibui. Chochote unatakiwa kuweza kupambana”
“Kweli, nina imani kwamba mke wangu amenichagulia mtu sahihi”
“Hajakosea kabisa.”
Meli ikazidi kusonga mbele, huku tukipata kifungua kinywa. Baada ya masaa kadhaa tukafanikiwa kufika katika fukwe za mji wa Kigamboni. Tukaagana na msichana alite tulete kisha tukaingia kwenye gari hili, nikafwata maelekezo kama jinsi  alivyo nieleza Logate, nikawasha gari hili. Taratibu nikaanza kulitoa ndani ya boti hii, nikaanza kuondoka taratibu kwenye eneo hili, japo kuna mchanga mwigi wa bahari ila gari hii haititii chini wala kuyumbishwa na mchanga huu. Tukafanikwia kuingia barabarani na kuianza safari ya kuelekea katikati ya jiji.
Tukafanikiwa kufika darajani na kukuta mlolongo mrefu wa magari yanayo elekea Dar es Salaam. Ikatulazimu na sisi kupanga foleni. Tataratibu gari ikaanza kusogea mbele hadi tukafika katika sehemu ya ukaguzi, mwanajeshi mmoja akaniomba nishushe kioo cha gari langu, nikafanya hivi, akachungulia ndani na kututazama.
 
“Habari yako kiongozi”
Nilimsalimia mara baada ya kutuona anatutazama sana, hakunijibu kitu chochote zaidi ya kuendelea kunikazia macho mimi na Magreti jambo lililo anza kunipa mashaka, akaiwasha simu yake ya upepo iliyo anza kukoroma kwa sauti ya juu. Kwa kupitia kioo changu cha pembeni nikaanza kuona wanajeshi wengine wawili wakilisogela gari letu huku wakiwa wamezishika bunduki  kwa  umakini wakionekana wakiwa na mashaka nasi jambo lililo nifanya nianze kuupeleka mkono wangu katika sehemu nilipo ichomeka bastola yangu kujiandaa na lolote litakalo jitokeza mbele yetu.
 
AISIIIII……….U KILL ME 189
   
Magret taratibu akanishika mkono wangu na kwa ishara ya macho akaniomba nisifanye kitu chochote.
“Tunaomba vitambulisho vyenu”
Mwanajeshi huyu alizungumza, taratibu nikachia tabasamu. Nikaingiza mkono wangu mfukoni na kutoa kitambulisbo changu. Magreti naye akanipatia kitambulisho chake na kwapamoja nikamkabidhi huyu mwanajeshi. Wanajeshi wawili waliokuwa wanakuja nyuma yetu wakachungulia chungulia ndani ya gari.
“Habari zenu”
“Salama tu, munaelekea wapi?”
“Posta hapo”
“Ohooo, aisee dada Mungu amekujalia. Kama ni manzi wako kusema kweli umepata mwanamke”
“Shukrani kiongozi”
“Munaweza kwenda”
Askari tuliye mpatia vitambulisho vyetu alizungumza huku akinirudishia. Taratibu nikafunga kioo cha upande wangu na kuondoka eneo hili.
 
“Huwa una maamuzi ya haraka eheehee”
“Yaa nilidhani wanahitaji kutuzingua”
“Siku  nyingine usijaribu kufanya hivyo. Inaweza kuharibi mipango yote tuliyo nayo”
“Sawa bosi, au uliwapagawisha kwa uzuri wako”
“Shauri yao ila kikubwa ni kufanya kazi iliyo tuleta huku”
“Poa, sasa harusi si inafanyika usiku na muda huu, tutafanyaje?”
“Tutafute hoteli ambayo tunaweza kupumzika”
“Mimi sina pesa yoyote”
“Usijali”
“Unazo wewe?”
“Wewe twende”
“Sawa.”
Tukafika katika hoteli moja ya kitalii, iliyopo maeneo ya hapa Posta.
“Silaha zetu tunatakiwa kuziacha ndani ya gari tukifika kwenye hiyo hoteli unayo kwenda”
Magreti alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.
“Poa poa”
Nikasimamisha gari sehemu ya maegesho na kushuka. Nikajiweka vizuri koti langu la suti na kuanza kutembea kuelekea ndani, Magreti taratibu akaingiza mkono wake wa kulia katikati ya nafasi iliyo achwa na mkono wangu wa kushoto, nikamtazama kwa macho ya mshangao.
“Tunatakiwa kutembea kama mume na mke”
“Una uhakika?”
“Ndio upo huru kwangu kwa muda huu”
“Weeeee”
Nilizungumza huku nikiwa nimejawa na tabasamu. Kila tunapo pita watu hawakusita kututazama hususani Magret kwani anavutia kwa kila macho ya kila mwanaume. Tukachagua sehemu iliyo tulia na iliyo jificha kidogo, tukakaa huku sote macho yetu yakiwa na kazi ya kutazama tazama eneo hili kwa umakini.
 
“Habari zenu”
Dada mmoja muhudumu alizungumza huku amesimama pembeni yetu kwa heshima kubwa sana.
“Salama tu dada, tunaomba menu ya chakula”
“Sawa”
Dada huyu akaondoka, baada ya dakika mbili akarudi akiwa ameshika vitabu viliwi. Akatukabidhi kila mtu cha kwake, nikaanza kutazama orodha ya vyakula hivi, vilivyo orodheshwa na bei zake.
“Niletee chipsi na miskaki na juisi ya embe”
“Na mimi niletee hicho alicho kiagiza mume wangu”
“Sawa karibuni”
Dada huyu akaondoka.
“Unapenda sana nionekane kama kama mume wako”
“Ni kama, na hii nikazi na ninacho kizungumza sikimaanishi”
“Sawa mwaya”
“Ila umependeza na wewe, ninaona wadada wakikushangaa shangaa”
Tukaendelea kuzungumza mambo mengi hadi chakula kikaletwa pamoja na vinywaji. Tukaanza kula tartaibu huku kkwa mara kadhaa nikiwa na kazi ya kumtazama Magret usoni mwake.
 
“Hivi tunakula tutalipa na nini?”
“Mbona una wasiwasi, tukishindwa kulipa si tutaosha vyombo vya hii hoteli”
“Hahahaaa wewe acha masihara”
“Eheee tunaosha, tunasogeza sogeza muda mbele”
“Oya kama huna pesa seme nianze kufikiria njia ya kuondoka hapa”
“Usiwe na wasiwasi”
Magreti alizungumza huku akifungua kipochi yake kidogo, akanionyesha jinsi noti za dola mia mia zikiwa zimejipanga vizuri kwenye hii pochi.
“Tuna uwezo wa kula chochote na kunywa chochote”
“Daaa hapo nina amani, inabidi tule kwa maana kazi tunayo kwenda kuifanya ni kubwa sana”
“Ukila ukishiba utashindwa kufanya kazi, kula wastani”
Kusema kweli Magreti ni mchangamfu sana na endapo anatokea mtu ambeye hatufahamu katika huu moango anaweza kusema kwamba sisi ni wapenzi wa muda mrefu sana.
“Unajua katika haya mahusiano yetu feki kilicho kosekana ni pete. Hapa hata tukimuambia mtu sisi ni mke na mume inaweza kula kwetu, atakapo hiji kuhusiana na pete”
Magreti alizungumza alizungumza huku akinitazama kwa macho malegevu kiasi, japo tupo kazini ila kuna kitu ambacho tayari nimesha kihisi kwa Magreti, ninaimani kwamba kuna chembechembe za hisia za penzi langu vimeingia moyoni mwake. Nikaitazama saa yangu ya mkononi mwa sekunde kadhaa.
“Hivi sasa ni saa kumi kasoro, tunaweza kutafuta pete za kofoji”
“Sawa”
Magreti akamuita muhudumu aliye tuhudumia.
“Dada naomba bili”
“Sawa”
Dada huyu akaondoka na kurudi akiwa na kijitabu kidogo akamuwekea Magreti pembeni yake. Akakifunua na kutoa kararasi ndogo.
“Elfu thelathini na mbili eheee?”
“Ndio”
Magreti akafungua pochi yake na kutoa noti ya dola mia.
“Si ninaweza kulipa hata kwa dola?”
“Ndio dada unaweza kulipia”
Magreti akaiweka noti hiyo kwenye kijitabu hichi tulicho letewa.
“Chechi itakayo baki chukua mdogo wangu”
“Asante sana dada yangu”
Binti huyu  aliondoka huku akiwa amejawa na tabasamu pana. Tukasimama na kutoka nje huku tukiwa tumeshikana mikono.
 
“Unajua umemuachia pesa nyingi sana”
“Ahahaa hembu acha ubaili kama mpare bwana”
“Ohoo pesa ni nyingi ile”
“Muache bwana”
“Hembu nipe kiasi kidogo cha pesa, maswala ya wewe kutoa pesa ninaonekana mimi ni boya bwana”
Magreti akaanza kucheka hadi tunaingia ndani ya gari bado anacheka.
“Wewe mwanaume sijui mwanamke utakaye muoa atapataje tabu”
Magreti alizungumza huku akifungua kipichi chake akachomoa noti kumi za dola mia mia na kunikabidhi, nikazikunja vizuri na kuziweka kwenye mfuko wa suti.
“Hapo sawa, ngoja tumtafute sonara kwanza”
“Hakia ya Mungu, Dany unanipa raha una vituko hadi basi”
Tukafika katika duka moja kubwa la sonara, tukashuka kwenye gari na kuingia ndani. Tukachagua ni pete gani ambazo tunahitaji kuchongeshewa kisha nikafanya malipo na kila pete moja ina thamani ya milioni moja na nusu na ikamlazimu Magreti kuongeza kiasi cha pesa kwani alichonipatia kimekwisha.
 
“Ndugu zitachukua muda gani?”
“Nusu saa muheshimiwa”
“Sawa, fanyeni fanyeni kwa maana tuna haraka”
Simu yangu ikata nikaitoa mfukoni na kukuta namba isiyo na jina, nikamuonyesha Magreti kwa sauti ya chini akaniambia kwamba ni Livna. Nikaipokea na kuiweka sikioni
“Mume wangu?”
“Niambie”
“Munaendeleaje?”
“Tunaendelea vizuri tu, vipi”
“Nimekumiss tu ndio maana nikakupigia”
“Kwani husikii tunacho kizungumza?”
“Mimi sipo chumba cha mawasiliano, kidogo ninajisikia sikia joto mwilini. Nipo chumbani nimepumzila”
“Umepata sawa?”
“Yaa dokta ndio amenitazama muda huu, ameniambia ni mabadiliko ya hali ya hewa”
 
“Pole mama”
“Nashukuru. Ninakuomba uwe makini”
“Usijaki nitakuwa makini sana”
“Ninakupenda Dany wangu”
Nikawatazama waty walipo karibu nasi ambao nao wamekaa kwenye viti wakisubiri huduma zao.
“Na mimi pia”
Nikakata simu na kuirudisha hewani.
“Mr na Mrs Mpoki ninawaomba munifwate”
Dada mmoja wa kiarabu alizungumza, tukaingia kwenye moja ya chumba na kukutana na muarabu mmoja menene akiwa amekaa kwenye kiti kikubwa cha kuzunguka.
“Habari zenu”
“Salama tu”
“Pete zenu zipo tayari, nina imani kwamba zitawapendeza”
Muhindi huyu alizungumza huku akitukabidhi pete zetu za dhahabu na zimechonga vile tulivyo hitaji. Nikaichukua pete ya Magreti, nikamtazama muhindi huyu, kisha nikauchukua mkono wa kushoto wa Magretu na nikamvisha  pete hii kwenye kidole husika cha pete ya ndoa.
“Mulikuwa bado hamjavishana pete?”
“Hapana, pete zetu za ndoa, kuna sehemu kidogo tuliziacha”
“Ahaaaa, ila mumependezana. Dada na wewe mvishe mwenzio”
Magreti kwa tabasamu pana, akaichukau pete yangu ambayo nilipanga kujivisha mimi mwenyewe, akanivisha kidole changu cha pete. Taratibu nikamsogelea na kumbusu mdomoni jambo lililo nifanya nipate msisimko mkali sana. Magreti hakuonekana kuchukizwa na lolote zaidi ya kufurahi kwa kile nilicho kifanya kwake.
“Tunashukuru ndugu”
“Karibuni sana”
Tukatoka katika ofisi hii na kuridi ndani ya gari letu. Magreti akanitazama kwa macho ya matamanio, taratibu nikamshika mkono wake wa kulia, nikamsogeza kichwa chake karibu yangu, tukatazama kwa sekunde kadhaa huku nikizilamba lamba lipsi zangu tararibu. Nikausogeza mdomo wangu hadi sehemu ulipo mdomo wake.
“Mmmmmm”
Magreti alizungumza huku  akikaa sawa kwenye siti yake akafunga mkanda wa siti.
“Tuondoke, tuna kazi ya kufanya”
Safari ya kuelekea ukumbini ikaanza huku  nikihakikisha kwamba ninafuta mawazo yote ya kijinga ninayo muwazia Magreti na ninahitaji kukakikisha kwamba ninawaza kazi iliyopo nbele yetu. Kutokana na foleni kubwa ya barabarani. Tukafika ukumbi muda husika,, gari letu likakaguliwa mlangoni kisha tukaruhusiwa kuingia ndani.
 
“Tupo kazini sasa, tuwe makini, kila kilicho tokea muda ulio pita tupotezee, hakikisha kwamba unajilengesha kwa Osama Bin Laden ninahitaji akiwa hai”
“Nimekuelewa”
“Sawa”
Sote tukashuka kwenye gari huku kadi ya mualiko nikiwa nayo mimi. Nikamshika kiuono Magrerti hadi mlangoni. Walinzi kusema kweli wapo wengi sana katika huu ukumbi huu, nikatoa kadi hii na kumkabidbi jamaa ambaye ndio mkabidi, akaipitisha katika mashine ya ugaguzi na macho yake akayatupia kwenye computer iliyopo pembeni yake. Akanirudishia kadi yangu huku akiwa ametabasamu.
“Karibuni sana”
“Shukrani ndugu”
Tukaingia ndani humu ambapo kumejaa watu wengi sana wakiwa na wamependeza sana.
“Hakikisha kwamba hugusi sikio lako sawa”
Magreti alizungumza kwa sauti ya kunining’oneza.
“Usijali katika hilo ninaelewa kila kitu”
Tukatafuta viti ambavyo tunaweza kuliona jukwaa vizuri na tukaa.
“Mungu wangu tunamuonaje hapa”
Nilizungumza kwa sauti ya chini huku nikiwa nimesogelea karibu sana Magreti.
“Tutamuona, Logate unatusikia?”
“Ndio ninawaiskia tangu mulipo ondoka hapa”
“Basi tunakuomba utusaidie katika hili”
“Nipo kwa ajili yenu”
Sherehe ikaanza huku tukiendelea kuwatazama watu waliomo humu ndani. Wakaingia watu wapatao nane wakiwa wamevalia kanzu na wamejifunika nyuso zao na kubakisha macho tu
‘Osama ameingia ukumbini’
Tuliisikia  sauti ya Logate akitupatia maelekezo.
“Ni yupi sasa kati ya hawa watu tisa?”
‘Tumieni simu zenu kifanyeni kama munapiga picha’
Tulaemdelea kutazama walinzi walipo katika eneo hili. Bibi harusi na bwana harusi walipo anza kuingia ukumbini hapa, watu wote wakanyanyuka huku  wenye simu zao wakijitahidi kuchukua video kwa kile kinacho endelea katika eneo hili. Na sisi tukatoa simu zetu mifukoni na kuanza kuchupiga picha maharusi hawa wanao ingia kwa mbembe kubwa za kucheza.
Nikaweka upande wa video na kuigeuza simu yangu sehemu alipo Osam Bin Laden na kundi lake, nikajikuta macho yakiwa yamenitoka kwani watu wote walio zifunika sura zao kwa vitambaa ni sura ya Osama Bin Laden.
“Mage umeona hichi kinacho tokea hapa?”
“Mbona wamefanana jamani?”
“Logate hii inakuwaje?”
“Hata sisi tunashangaa huku hatujui Osama ni nani kati yao kwa maana wote wanafanana”
Hatukujua ni nini cha kufanya hadi watu wote tulipo ruhusiwa na muongoza sherehe(MC) tukae kwenye viti vyetu.
 
 ITAENDELEA
‘Haya sasa DANY na MAGRETI hadi sasa wameshindwa kumtambua Osaman ni nani kati ya watu walio ingia kwenye ukumbi huo. Ni nini watakacho kifanya? Usikose sehemu inayo fwata ya hadi hii ya kusisimua kutoka kwa muandishi mahiri Eddazaria G.Msulwa”

Katibu Mkuu Wizara Ya Mifugo Na Uvuvi Awashtukiza Suma Jkt Usiku

0
0
Na. Edward Kondela
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amefanya ziara ya kushtukiza usiku majira ya saa 5:30 13.01.2019, kujionea maendeleo ya ujenzi wa jengo la wizara katika mji wa serikali jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Prof. Gabriel mara baada ya kufika katika eneo hilo alikuta ujenzi wa jengo unaendelea kama ambavyo mkandarasi SUMA JKT alivyokubaliana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kujenga jengo hilo kwa saa 24 na kuridhishwa na ujenzi unavyoendelea na kushukuru ushirikiano unaotolewa na wafanyakazi wa wizara.

“Tunaridhika kwa kweli kama uongozi wa wizara ikiwa ni pamoja na viongozi wetu wa kisiasa Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Joelson Mpina amekuwa akitutaka kuwa tusilale tufuatilie kama kazi zinafanyika ndio maana leo hii nimeamua kuja usiku, maana unaweza kuambiwa watu wanafanya kazi usiku na mchana kumbe nikilala na kazi huku zinalala.” Alisema Prof. Gabriel.

Aidha Prof. Gabriel amemtaka mkandarasi SUMA JKT kutobweteka kwa kile alichoelezwa kuwa hadi sasa anafanya kazi nzuri katika ujenzi wa jengo la Wizara ya Mifugo na Uvuvi na kumkumbusha aendelee kufanya kazi kwa kufuata makubaliano yaliyopo katika mkataba waliosaini kwa kujenga jengo hilo kwa ubora na kulikabidhi kwa wakati.

Katibu mkuu huyo pia amesema hatua ya Shirika la Umeme nchini (TANESCO) kufikisha huduma ya umeme katika eneo hilo, imesaidia kufanya kazi ya ujenzi kuwa na kasi zaidi na kupunguza gharama ya mafuta ya dizeli ambayo yalikuwa yakitumika kwenye jenereta hususan nyakati za usiku kwa ajili ya kuwashia taa na kusukumia mitambo ya ujenzi.

Prof. Gabriel ameitaja pia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuwa ni moja ya wizara ambayo imechimba kisima chake katika eneo hilo na kutumia maji ya kisima kwa ajili ya ujenzi.

Kwa mujibu wa mkandarasi SUMA JKT jengo la Wizara ya Mifugo na Uvuvi linatarajiwa kukamilika mwezi februari mwaka huu na kuanza kutumiwa na baadhi ya watendaji wa juu wa wizara kabla ya kujengwa jengo lingine kubwa katika eneo hilo, ambalo litatumiwa na wafanyakazi wote wa wizara waliopo mkoani Dodoma katika mwaka ujao wa fedha wa 2019/2020.

MWISHO.
Imetolewa: Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
                    Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Super Mkongo: Kiboko ya Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
********************************
SUPER MKONGO MPYA,
_______________________________
********************************
Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile,

- kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa
- maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo
- kukosa hamu ya tendo la ndoa
- kushindwa kurudia tendo la ndoa
- uume kusimama kwa kulegea
- uume kulegea katikati ya tendo
- kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu
- kuishiwa nguvu kutokana na punyeto.

Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MCONGO MPYA, kiboko ya matatizo haya.
_______________________________
Pia kuna MCONGO POWER Kiboko ya uume mdogo inaboresha maumbile ya uume kwa kurefusha na kunenepesha kwa saizi uipendayo haijalishi umri hata kwa walioathirika na upigaji punyeto.
_______________________________
Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume na uume mdogo.
_______________________________
(1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea.
(2) ngiri
(3) kuugua chango la uzazi kwa muda mrefu.
(4) kupungukiwa hormone za testosterone.
(5) ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na visivyo na virutubisho  vya kutosha.
(6) kutokufanya mazoezi na mwenendo wa maisha.
(7) kisukari.
(8) tumbo kuunguruma na kujaa gesi.
(9) maumivu ya kiuno nk.
_______________________________
Kwanini uhangaike? Kwanini uhuzunike?
Hii ni spesho kwa waliotumia madawa mengi bila kufanikiwa hakika hautajuta kuitumia. _______________________________
WASILIANA NA:
DR. MCONGOMANI
SIMU NO:
📞0658816558
📞0682323682
Popote ulipo huduma hii inakufikia
_______________________________
********************************

Rudisha heshima yako Kwa Mpenzi Wako, Mke Wako...Tumia Tiba Hii ya Asili

0
0
Rudisha heshima yako sasa kwa kutumia Dawa hii iitwayo SUPER GAFINA, kwa ajili ya nguvu za kiume na NKOLOMIJE ni kwaajili ya kuongeza maumbile.

Kwa mwanaume aliye kamilika anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara mbili ,ila ukiwa unapiga moja tena kwa shida wewe ujue  unamatatizo ya upungufu wa nguvu za kiume.

TIBA YA TATIZO LAKO NI; Dawa iitwayo SUPER GAFINA, dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge na unga wa asili ambavyo havina madhara kwa mtumiaji ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja;-

1).itakufanya urudie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuchoka.

2).ltakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15 hadi 20 kwa tendo la kwanza.

3).lnaimarisha uume uliolegea na uliosinyaa na kuupa nguvu maradufu.

Je unamaumbile madogo pamoja na uume mfupi? NKOLOMIJE ni suluisho la tatizo lako. Na ni dawa inayoboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi kuanzia inch. 5 hadi 8 kwa muda mfupi sana .Dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk.30 ukisha tumia guarantee miaka 50  ikishakutibu.

Pia ninatibu;- KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU, MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE ,BP, NK.

IGULYATI, ni dawa ya mvuto wa biashara, kazi,kupandishwa cheo na humfanya mfanyakazi kupendwa na mwajiri wake. Pia humvuta mke,Mme,hawara ,mchumba unae muitaji utampata kwa dk.30 tu na atatulia na kumfunga asitoke nje ya ndoa, Pia natoa Pete za bahati ambazo zimetajirisha wengi.

Pia ipo dawa ya kupunguza matiti,unene ,tumbo,na kitambi ,hupunguza mafuta ,kuondoa makovu,chunusi,michilizi mwilini na kuongeza hipsi, makalio na mguu wa bia nk. 

Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR,HOSUTWA .Anapatikana Mbagara

Simu no, 0756241666 na 0672186977.

       Huduma hii utaipata popote ulipo

Kesi Ya Zitto Kabwe Yapigwa Kalenda Hadi January 29

0
0
Kesi ya 'uchochezi' inayomkabiili Mbunge wa Kigoma Mjini, Zito Zuberi Kabwe imeahirishwa mpaka Januari 29, itakapoitwa kwa ajili ya kwenda kusikilizwa

Kesi hiyo  ya Jinai namba 327 ya Mwaka 2018 inayomkabili Kiongozi huyo leo tarehe 14 Januari 2019 katika Mahakama ya Kisutu, Jijini Dar es salaam ilifika kwa ajili ya kutajwa na kutolewa maamuzi ambayo yalitolewa na Hakimu Mkazi, Janeth Mtega baaada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili (Mashtaka na utetezi).

Upande wa Mashtaka ukiwakilishwa na Wakili wa Serikali, Adolf Kissima  ulidai kwamba kesi hiyo leo ilikwenda kwa ajili ya kutajwa lakini upande wa mashtaka hawakuwa na jalada halisi la kesi hiyo.

Upande wa utetezi ukiongozwa na Wakili wa Zitto, Steven Mwakibolwa uliikumbusha mahakama kuwa shauri hilo lilikuja kwa ajili ya kutajwa na mahakama hiyo kupitia Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama, Huruma Shaidi na ilishapanga tarehe ya kuanza kusikilizwa, ambayo ni Januari 29, 2019.

Inadaiwa kuwa Oktoba 28,2018 katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika ofisi za makao makuu ya chama cha ACT Wazalendo, kiongozi huyo alitumia maneno yenye kuleta kuleta chuki miongoni mwa wananchi wa Tanzania dhidi ya Jeshi la Polisi.

Mbunge huyo alifikishwa Mahakama ya Kisutu kwa mara ya  kwanza, Novemba 2, 2018, bado anaendelea na dhamana.

Mahakama Kuu Yaitupilia Mbali Kesi ya Zitto Kabwe na Wenzake Kupinga Muswada Wa Vyama vya Siasa

0
0
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imeifuta kesi iliyofunguliwa na Kiongozi wa ACT Wazalendo na wenzake wa vyama vya upinzani  waliyokuwa wakiitaka mahakama hiyo kuzuia kusomwa kwa Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ya Vyama vya Siasa wakidai kuwa uko kinyume na katiba ya nchi.

Mahakama imetoa uamuzi huo leo Jumatatu, Januari 14, 2018 ambapo walalamikaji, Zitto na wenzake wamekubali maamuzi hayo na kusema sasa nguvu yao ni kwenda kuupinga muswada huo kwenye kamati za bunge.

Jaji Benhajo Masoud amesema Mahakama imeliondoa shauri hilo baada ya waombaji kuchanganya mashataka mawili kwa pamoja.

“Mahakama imeondoa shauri letu dhidi ya serikali kupinga muswada wa sheria ya vyama vya siasa na kifungu cha 8(3) cha sheria ya Haki na Wajibu ( BRADEA ) kwa sababu ya maombi hayo mawili kuunganishwa. Kufuatia uamuzi huo wa mahakama tumeagiza mawakili leo wafungue kesi mpya ya BRADEA.

“Tunaheshimu maamuzi ya mahakama na tunaamini mahakama imetenda haki. Hivyo tumeamua kurudi mahakamani kwa ombi moja la kupinga kifungu cha 8(3) cha sheria ya Haki na Wajibu. Kifungu hiki kinakiuka katiba kwa kuzuia mashauri ya kupinga miswada ya sheria. Mahakama ni chombo cha haki.

“Tutaendelea kuupinga muswada wa sheria ya kurekebisha sheria ya vyama vya siasa mbele ya kamati za bunge na ndani ya bunge. Muswada ukipita kuwa sheria kama ulivyo au kuwa mbaya zaidi, tutaupinga mahakamani tena. Hatutakata tamaa katika kudai haki,” amesema Zitto.


Mbunge CHADEMA Ampigia Promo ya Urais Tundu Lissu

0
0
Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Jesca Kishoa amesema zawadi pekee ambayo Watanzania wanaweza kumpa mbunge wa chama hicho jimbo la Singida Mashariki, Tundu Lissu ni kumuunga mkono katika ndoto zake za kugombea urais mwaka 2020.

Kishoa ametoa kauli hiyo leo Januari 14, 2019 katika mkutano wake na waandishi wa habari mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali kuhusu afya na maendeleo ya Lissu.

“Lissu ni kaka yangu, ni mbunge mwenzangu na kiongozi wangu, mambo ya kuangalia ni kupata baraka za chama lakini anafaa,” amesema Kishoa.

Amesema wakati ukifika atatamani kuona jina la Lissu likipitishwa kuwania urais, kwa kuwa Watanzania wanajua msimamo wa kiongozi huyo na ndio anayefaa kuwaongoza.

Lissu kwa sasa anaendelea na ziara yake kwenye nchi za Ulaya na marekani kwa ajili ya kuelezea mkasa wa kupigwa risasi uliompata Septemba 2017 Jijini Dodoma.

Waziri Mhagama Akerwa Na Sekta Binafsi Ya Ulinzi Kuongoza Kwa Migogoro Mahala Pa Kazi

0
0
Waziri wa  Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama ameiagiza Tume ya Usuluhishi na Uamuzi, kuweka mpango Maalum wa kuhakikisha migogoro   katika sekta  binafsi ya Ulinzi haizalishwi tena kwa wingi kwani inasababisha kutumika vibaya kwa rasilimali muda kati ya mwajiri na Mfanyakazi hali inayopelekea kuchelewesha Maendeleo.    
         
Waziri Mhagama amebainisha sekta  nyingine zinazoongoza kuwa na migogoro mahala pa kazi   kuwa ni  Sekta  ya Ujenzi na Sekta  ya Elimu. Aidha, ameitaka Tume hiyo kufanya utafiti kwa sekta   zote zinazoongoza kwa migogoro ya kikazi ili kubaini chanzo cha migogoro hiyo na kuandaa Mkakati Maalum wa kuishughulikia. 

Mhagama ameyasema hayo leo mjini Morogoro  tarehe 14 Januari,  2019, wakati wa kikao cha Baraza la  wafanyakazi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi kilichowakutanisha Wasuluhishi na  waamuzi wa migogoro ya kikazi nchi nzima.        

"Hii sekta  Binafsi ya Ulinzi kwa nini huko migogoro  haiishi? Nataka mpango wa kumaliza migogoro hiyo, shirikianane na Taasisi nyingine muweke mpango maalum utakao weza kutatua na kuhakikisha haizalishwi mogogoro  mingine" Alisisitiza Mhagama.  

Mhagama alifafanua kuwa Serikali ya Awam  ya Tano  inayoogozwa na Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli imedhamiriakwa vitendo vya kupiga vita uzembe, ubadhirifu na vitendo vyote  Vya rushwa mahala  pa kazi.    

  "Nisisitize kazi ya Usuluhishi na Uamuzi ni  kazi ya heshima na pia ni  kazi ya wito. Hivyo wekeni mkazo kwenye suala la Usuluhishi ili kupunguza muda  na mlundikano wa  mashauri, pia bainisheni sekta  nyingine zenye migogoro  mikubwa. Elimu ni  vyema iendelee kutolewa kwa Wadau kuhusu Sheria za Ajira na mahusiano kazini." alieleza Mhagama. 
   
Awali akiongea katika Mkutano huo, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi, Shanes Nungu alibainisha kuwa Tume hiyo itatekeleza maagizo hayo kwa kuboresha Mkakati Wa Mpango kazi Wa Tume ili kuwa na mpango mkakati kwenye mtazamo Wa kupunguza migogoro  na unaolenga kumaliza migogoro kwa nataka katika sekta  zinazoongoza kuwa na migogoro mahala  pa kazi. 

 "Tumekuwa tunajitahidi kumaliza na kuipunguza migogoro ya kikazi, kwani tumefanikiwa kumaliza migogoro hiyo kwa asilimia 80 kwenye hatua ya Uamuzi na asilimia 77, kwenye hatua ya Usuluhishi" alieleza Nungu.        
              
Tume ya Usuluhishi na Uamuzi  ipo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, ambapo  Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Tume hiyo kimefanyika kwa mujibu wa Agizo la Rais Na.1 la mwaka 1970. Baraza hilo   huiwezesha Tume kuboresha Huduma na masuala ya utatuzi Wa migogoro ya kikazi kwa njia ya Usuluhishi na Uamuzi.

IMETOLEWA NA:
KITENGO CHA MAWASILINO SERIKALINI
OFISI YA WAZIRI MKUU
 

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) Chalaani tukio la trafiki watatu kumshambulia dereva

0
0
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimelaani tukio la askari wa Jeshi la Polisi kutumia nguvu kupita kiasi kupambana na raia.

Taarifa iliyotolewa leo Jumatatu Januari 14, 2019 na kituo hicho na kusainiwa na mkurugenzi mtendaji wake, Anna Henga imeeleza kuwa kufanya hivyo ni kinyume na  sheria ya kanuni ya adhabu sura 16, sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sura ya 20 na sheria ya jeshi la polisi na huduma saidizi sura ya 322.

Tamko hilo limekuja kufuatia kusambaa kwa video inayowaonyesha askari watatu wakitumia nguvu kupita kiasi wakati wa kumkata mtuhumiwa katika mji wa Tunduma, mkoani Songwe.

Katika taarifa hiyo LHRC imelitaka jeshi la polisi kuzingatia haki katika utekelezaji wa majukumu yake huku likilinda uhai wa raia na mali zake.

Sanjari na hilo kituo hicho kimewaasa wananchi kutoa ushirikiano kwa polisi pale wanapotimiza wajibu wao ikiwemo kukamata, kuhoji, kupekua ili kuepusha ulazima wa matumizi ya nguvu kubwa dhidi ya raia.

Mstaafu Auawa Kikatili na Mfanyakazi Wake wa Ndani Kisa Mafao

0
0
Tunsume Sakajinga (60), mkazi wa wilayani Temeke jijini Dar es Salaam ameuawa baada kupigwa na kitu kizito kichwani kisha kuchomwa na mkasi shingoni na mtu anayedaiwa kuwa kijana wake wa kazi za nyumbani.

Tukio hilo lilitokea Jumamosi Januari 12, mwaka huu nyumbani hapo ambapo marehemu alikuwa akiishi na huyo kijana huyo akimsaidia kazi mbalimbali zikiwamo za nyumbani na shambani.

Akisimulia mkasa huo, mkwe wa dada wa marehemu ambaye hakutaka kutaja jina lake, leo Jumatatu Januari 14, amesema marehemu alikuwa akiishi peke yake nyumbani kwake hapo na kijana huyo ambaye aliishi nae mwaka 2017 kabla ya kuondoka na kurudi tena Septemba mwaka jana.

“Siku ya tukio marehemu alitoka kwenda dukani akarudishia milango, lakini alivyorudi akakuta milango imefungwa hali iliyomshtua kwani yeye hakuacha mtu ndani.

“Alivyokuta mlango umefungwa akampigia simu fundi anayemjengea na anayemsaidia akiwa na shida mbalimbali, kumuelezea kuna mtu ndani wakati yeye alipotoka hakuacha mtu, hivyo akabaki nje akimsubiri fundi.

“Baada ya muda mfupi, fundi alipofika akakuta geti limefungwa akagonga bila mafanikio na akipiga simu hazipatikani akachukua jukumu la kuwaita mafundi wenzie wakashirikiana kugonga lakini ikashindikana ikabidi waende kwa Mwenyekiti wa Mtaa na kisha polisi walipofika eneo la tukio waliruka ukuta na walipoingia ndani wakakuta milango yote imefungwa lakini kupitia dirisha la jikoni waliona kitu kimefunikwa kwa mkeka.

“Kwa sababu milango ilikuwa imefungwa walitumia bomba refu kufunulia mkeka huo ambapo walikuta mwili wa marehemu ukiwa na mchi na mkasi uliotumika kumchomea, wakabomoa milango na kuingia ndani.

“Walipoingia ndani walikuta mikeka mingine imefunikwa na walipoifunua walimkuta kijana huyo ambaye alianza kupiga kelele na kusema msiniue siyo mimi niliyefanya hivyo bali tulivamiwa na majambazi,” ameeleza.

Hata hivyo, mkwe huyo amesema inahisiwa kijana huyo alifanya hivyo ili achukue mafao ya marehemu ambaye mwanzoni alikuwa mfanyakazi wa Mamlaka ya Bandari (TPA), na alistaafu Desemba 30 mwaka jana.

Aidha, amesema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Temeke ukisubiri taratibu za kipolisi kabla ya kusafirishwa kwenda kuzikwa Tukuyu jijini Mbeya.

Kamanda wa Polisi mkoa wa kipolisi Temeke,  Emmanuel Lukula amethibitisha kuwapo kwa tukio hilo lakini amesema bado wanafanya uchunguzi kubaini nani alihusika na kwamba hakuna mwenye uhakika kama aliuawa na mvulana wake wa kazi.

“Hilo bado tunachunguza na hakuna mwenye uhakika kama ‘houseboy’ wake ndiye alimuua. Siwezi kuthibitisha ila bado tunachunguza,” amesema.

Freeman Mbowe Anyang'anywa Ofisi yake ya Ubunge Hai

0
0
Mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya amemnyang'anya ofisi ya Ubunge, Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe baada ya kueleza hajaitumia tangu mwaka 2010.

Mbowe ambaye ni mwenyekiti wa Chadema amekuwa mbunge wa Hai kwa awamu ya tatu na ofisi hiyo imekuwa ya mbunge na kuwekewa kibao cha ofisi ya mbunge kwa zaidi ya miaka 20.

Ofisi hiyo ipo katika jengo la mkuu wa wilaya hiyo, ambapo pia zipo ofisi za halmashauri ya wilaya ya Hai na sasa itakuwa inatumiwa na idara ya uhamiaji.

Sabaya amesema lengo la Serikali kutoa ofisi kwa mbunge huyo ilikuwa ni kusaidia wananchi lakini ofisi hiyo imekuwa haifunguliwi.

"Tangu mimi nimeteuliwa kuwa Mkuu wa wilaya hapa mwezi wa nane (mwaka jana) ofisi haijafunguliwa sasa kwa kuwa kuna uhitaji wa ofisi muhimu ya uhamiaji nimeamua kuwapa," amesema.

Amesema amepata taarifa pia tangu Mbowe achaguliwe mwaka 2010 hajawahi kuingia tena katika ofisi hiyo kusikiliza kero za wananchi.

"Sijui yupo wapi ila namsikia huko maeneo mengine akifanya vurugu sasa ofisi hii itatumika kusaidia wananchi," amesema.

Jeshi la Polisi Latoa Ufafanuzi Tukio la Dereva Kushambuliwa na Trafiki Watatu

0
0
Jeshi la Polisi mkoani Songwe limeeleza sababu ya askari wa usalama barabarani kumshambulia dereva kwa kumpiga kuwa alitumia lugha ya matusi na kutotii amri ya kumtaka atoe ushirikiano kwa wanausalama hao ambao walikuwa wakifanya kazi kwa kushirikiana na maofisatoka Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchikavu (Sumatra).

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa Yusuph Sarungi amewaambia waandishi wa habari leo Jumatatu Januari 14, 2019 kuwa tukio hilo lilitokea juzi Jumamosi Januari 12, 2019 saa 2:30 asubuhi katika eneo la Transforma, halmashauri ya mji wa Tunduma wilayani Momba wakati askari hao wakishirikiana na maofisa toka Sumatra wakiwa kwenye ukaguzi wa magari mbalimbali.

Amesema dereva huyo Mawazo Jairos (29) mkazi wa Mbeya aliyekuwa akiendesha gari aina ya Mistubishi Fuso lenye namba za usajili T842 AAC, baada ya kusimamishwa alianza kutoa lugha za kashifa na matusi kwa askari na maofisa wa Sumatra.

Kamanda huyo amesema Jairos aliliondoa gari bila ya kuruhusiwa kwa kupitia barabara ya vumbi hali iliyolazimu askari hao kumfuatilia na kumkamata tena katika eneo la Makambini ambapo walimzuia tena.

Sarungi amesema dereva huyo aliteremka kwenye gari kwa jazba huku akiendelea kutoa matusi na kumshambulia askari ambapo hata hivyo askari hao walifanikiwa kumdhibiti hali iliyofanya apige kelele kuomba msaada.

Amesema wananchi walifika lakini wakati wananchi wanamsaidia dereva huyo alifanikiwa kuwatoka na kwenda kwenye gari kisha kuchukua panga kuwatishia askari hao na kufanikiwa kuondoa gari eneo la tukio hadi alipokamatwa tena katika mji wa Vwawa.

Kamanda Sarungi aliongeza kuwa askari polisi hao walikuwa wanatimiza wajibu wao wa kazi kwa kumdhibiti dereva huyo kwa vile sheria inawaruhusu kutumia nguvu za kadri ili kumdhibiti mhalifu.

Serikali yafuta umiliki wa mashamba sita ya Mo Dewji

0
0
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angeline Mabula leo Jumatatu ametangaza uamuzi wa Serikali wa kuyafuta mashamba sita yenye ukubwa wa ekari 12, 915. 126 ya kampuni ya Mohammed Enterprises Limited (MeTL) yaliyopo Korogwe jijini Tanga.

Taarifa ilitolewa kwa umma na kitengo cha mawasiliano cha wizara hiyo imesema uamuzi wa kufuta mashamba hayo umefikiwa baada ya mapendekezo yaliyotolewa na halmashauri ya wilaya ya Korogwe kufutwa mashamba hayo kutokana na kutoendelezwa kwa muda mrefu.

Imesema mapendekezo hayo yaliwasilishwa kwa Rais John Magufuli na wizara kwa nia ya kufutwa mashamba hayo ya MeTL  ambayo ofisa mtendaji mkuu wake ni bilionea namba moja kijana barani Afrika, Mohammed Dewji ‘Mo.’

Mashamba yaliyofutwa ni yale yaliyopo eneo la Mombo, Mabogo pamoja na Kwalukonge wilayani Korogwe.

Akizungumza mara baada ya kutembelea mashamba hayo, Mabula amesema mashamba yaliyobatilishwa ni kati ya mashamba 14 yanayomilikiwa na kampuni ya Mohammed Enterprises, Mazinde wilayani Korogwe.

Amesema uamuzi huo unalenga kujenga nidhamu kwa waliopewa rasilimali za Serikali kuzingatia masharti ya uwekezaji.

Amesema mara baada ya halmashauri ya wilaya ya Korogwe kupeleka mapendekezo ya kufutwa mashamba ya Mohammed Enterprises, wizara ya ardhi ilifanya ufuatiliaji katika halmashauri husika kuhusu kutoendelezwa mashamba na baada ya kujiridhisha ikawasilisha maombi hayo kwa Rais na kuridhiwa.

Mabula amesema uamuzi huo wa Rais kuridhia ubatilishaji mashamba sita kati ya 14 yanayomilikiwa na Mohammed Enterprises unalenga kuhakikisha wote waliopewa maeneo kwa ajili ya uwekezaji wanazingatia masharti na taratibu za uwekezaji.

Naibu waziri huyo amesema mashamba ambayo hayajabatilishwa yamewekewa utaratibu kwa nia ya kuyaboresha kwa kuwa baadhi yake yanahitaji maboresho kwa nia ya kufanya vizuri.

Ameitaka halmashauri ya Korogwe kupanga mpango wa matumizi bora ya ardhi katika eneo la mashamba yaliyofutwa na kipaumbele kwa watakaopewa maeneo katika mashamba hayo ni wananchi waliokuwa wakiishi katika mashamba hayo na sehemu itakayobaki atafutwe mwekezaji mwingine kwa kuwa lengo la Serikali ni kuwa na uwekezaji wa viwanda.

Mabula amempongeza mkuu wa mkoa wa Tanga, Martin Shigella kwa kufanya kazi nzuri ya kufuatilia na kusimamia maagizo mbalimbali tangu Rais Magufuli alipoanza kubatilisha mashamba ambayo hayajaendelezwa katika mkoa wa Tanga.

Kwa upande wake, Shigella amewataka wananchi wa Korogwe kutovamia maeneo ya mashamba yaliyobatilishwa hadi hapo halmashauri ya wilaya ya Korogwe itakapopanga matumizi bora ya ardhi katika mashamba hayo.

Amesema ndani ya wiki hii ataitisha mkutano na wataalamu wa sekta ya ardhi katika mkoa huo pamoja na wale wa bodi ya Mkonge kuangalia matumizi ya ardhi iliyobatilishwa kwa wananchi.

Ujenzi Wa Ofisi Za Wizara Ya Fedha Na Mipango Mji Wa Serikali Ihumwa Dodoma Waendelea Kwa Kasi

0
0
Na Peter Haule, WFM, Dodoma
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Isdor Mpango amelitaka Shirika la Nyumba lililopewa kandarasi ya kujenga Jengo la Ofisi za Wizara hiyo katika Mji wa Serikali-Ihumwa, Jijini Dodoma, kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha ujenzi huo unakamilika kwa wakati na ofisi hizo zinaanza kutumika mapema mwezi Februali Mwaka huu.

Dkt. Mpango ametoa rai hiyo alipofaya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Ofisi hizo zitakazogharimu zaidi ya shilingi bilioni moja.

Amesema kuwa licha ya kuwa ujenzi unakwenda vizuri lakini ni lazima Mkandarasi aongeze bidii ya ujenzi kwa kuwa vifaa vyote vinavyohitajika vipo ikiwemo pia raslimali watu ambayo ipo tayari kufanya kazi na kujiongezea kipato.

"Nataka kutumia Ofisi hii ifikapo Februari na nitakuja na kiti changu hapa tayari kuchapa kazi" alisema Dkt. Mpango

“Kwangu mimi ujenzi unaoendelea una umuhimu mkubwa kwa kuwa watu wanapata ajira, hivyo ni vema kuendelea kuhakikisha kunakuwa na raslimali hiyo kwa idadi inayotakiwa itakayosaidia kuhakikisha ifikapo Januari, 31, mwaka huu ujenzi uwe umekamilika” alisema Dkt. Mpango.

Aidha amepongeza jitihada zinazofanywa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa hatua waliyofikia, kwa kuwa tayari hatua ya ujenzi wa kuta ipo katika hatua za mwishoni na kilichobakia ni kupiga plasta na baadae kupaua.

Kwa upande wake Mbunifu Majengo wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Msafiri Msaki, ameahidi kuhakikisha kazi hiyo inamalizika kwa muda uliopangwa kwa kuwa kwa sasa hatua ya ujenzi ipo ndani ya muda.

Hata hivyo ameitaja changamoto iliyojitokeza kuwa ni pamoja na maji kutopatikana kwa wakati kwa baadhi ya siku kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni kupasuka kwa mabomba.

Dkt. Mpango aliagiza wasimamizi wa ujenzi huo kuhakikisha tatizo hilo linatafutiwa ufumbuzi haraka iwezekanavyo ili kutokua kikwazo katika ukamilishaji wa ujenzi wa ofisi hizo.

Baadhi ya vijana wa kike na wa kiume wameelezea kufurahishwa na ajira zinazopatikana kwenye eneo la ujenzi wa majengo ya ofisi za Serikali katika eneo hilo la Mji wa Serikali Ihumwa, na kuwataka vijana wenzao kuchangamkia fursa mbalimbali za ajira katika eneo hilo.

Mwisho

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya January 14

Serikali Haitabomoa Nyumba Za Watu Waliojenga Katika Makazi Holela

0
0
Na Hassan Mabuye, Wizara ya Ardhi
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi amesema kwamba Serikali ya awamu ya tano kuanzia sasa haitabomoa tena nyumba za wananchi waliojenga maeneo ya makazi yasiyo rasmi badala yake itarasimisha makazi holela.

Waziri Lukuvi amesema Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli ametoa fursa kwa wananchi wote masikini waishio mijini waliojenga bila ya kufuata mipango miji na hawana hatimiliki za ardhi kufanyiwa urasimishaji wa makazi yao na wasibomolewe nyumba zao tena kwakuwa haikuwa ni makosa yao kujenga maeneo hayo.

Lukuvi ameyasema hayo alipokuwa wilayani Simanjiro mkoa wa Manyara alipofanya ziara yake ya kusikiliza na kutatua migogoro ya ardhi kwa wakazi wa mji huo, ambapo amesema wananchi wote wachangamkie fursa hii iliyotolewa na Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ya kuwapa fursa ya kumiliki hati katika maeneo ambayo siyo rasmi kwa kurasimishiwa.

“Serikali ya awamu ya tano inajali sana wananchi wake kwakuwa zamani wananchi ambao hawakujenga kwa kufuata mipango miji wangebomolewa nyumba zao, lakini kwa sasa Serikali ya awamu ya tano imeanzisha mpango kurasimisha makazi holela na kuwapatia hati wananchi wote waishio mijini ili waishi katika makazi rasmi” Amesema Lukuvi.

Aidha, Lukuvi amewataka wananchi wote waishio mijini kuwa wazalendo kwa kurasimisha maeneo yao waweze kujipatia hati na ili walipe kodi ya pango la ardhi jambo ambalo litaiongezea Serikali mapato.

Lukuvi alipokuwa ziarani Simanjiro mwishoni mwa wiki aligundua kuwa wakazi wa mji wa Simanjiro walio na hatimiliki za ardhi hawazidi 1,000 wakati nyumba zilizopo ni nyingi zaidi ya idadi hiyo. Hivyo Waziri Lukuvi akawataka wachangamkie fursa hii ya kujipatia hati ili kuzipa hadhi nyumba zao.

“Nyumba isiyokuwa na hati haina thamani kwakuwa hata ukienda Benki kukopa pesa hawatakuuliza umejenga nyumba ya uzuri gani, lakini watakachotaka ni hati yako ya kumiliki ardhi ambacho ndio kitu kilicho na thamani zaidi kwako kuwa nacho” aliongeza Lukuvi.

Naye Mbunge wa Simanjiro Mheshimiwa James Ole Millya ambaye amehamia CCM akitokea Chadema amemshukuru Mhe. Lukuvi pamoja na Serikali ya Awamu ya Tano katika kuwajali wananchi wake kwa kuwaletea maendeleo makubwa na kusimamia suala la wananchi wa kawaida kupata fursa ya kumiliki ardhi kutoka kwa wawekezaji wakubwa ambao walikuwa hawayaendelezi mashamba yao kwa muda mrefu.

Simanjiro ndio wilaya inayoongoza kwa wamiliki wa mashamba makubwa walio na hati na hata wengine wasio na hati rasmi. Kwa sasa wamiliki wa mashamba walio na hati rasmi wanafika 158 yaliyo na hekari zaidi ya 120,000 ambapo wasio na hati ni zaidi ya hao, hivyo Waziri amenza utaratibu wa kufuta mashamba makubwa 55 yanayomilikiwa kwa kuwa wamiliki wake wamekiuka masharti ya umiliki.

Kangi Lugola awasimamisha kazi maofisa watano Kisa Sare za Jeshi Za Burundi Zilizoingizwa Nchini

0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola  amewasimamisha kazi vigogo watano wa idara ya wakimbizi kwa madai ya kushindwa kutoa taarifa mapema za uwepo wa marobota  1,947 ya nguo zinazodaiwa kuwa ni za jeshi katika kambi za wakimbizi za Nduta na Mtendeli zilizopo mkoani Kigoma.

Waliosimamishwa ni mkurugenzi wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi,  Harrison Mseke; mkurugenzi msaidizi wa huduma kwa wakimbizi,  Deudsdedit Masusu; mkurugenzi msaidizi huduma kwa wakimbizi usalama na operesheni, Seleman Mziray.

Mkuu wa kambi ya Nduta,  Peter Bulugu na John Mwita ambaye ni mkuu wa kambi ya Mtendeli.

Lugola ametangaza uamuzi wake huo jana Jumapili Januari 13, 2019 katika mkutano wake na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam.

Alisema nguo hizo za msaada zilitolewa na shirika la Uniqlo la Japan kwa ajili ya wakimbizi wa kambi hizo lakini viongozi wa idara hiyo hawakutoa taarifa mapema kwa viongozi wa wizara.

“Mizigo yote ya wakimbizi inayotolewa lazima ikaguliwe lakini hawa walikaa kimya. Uwepo wa nguo hizo hauleti picha nzuri hasa katika kipindi hiki ambacho Serikali ipo katika mchakato wa kuwarudisha wakimbizi Burundi," alisema Lugola.

“Kwa vyovyote nchi ya Burundi itakuwa na mtazamo hasi dhidi ya Tanzania baada ya wananchi wake kupewa nguo za kijeshi. Lazima tuwe makini maana tusipofanya hivi tunaweza tukakuta hadi silaha katika misaada.”

Lugola alisema baada ya kuwasimamisha kazi amemwagiza katibu mkuu wa Wizara hiyo kuunda kamati kwa ajili ya kuchunguza tukio hilo, kuipa siku 10 za kuchunguza.

Lugola ameagiza mamlaka zinazohusika kumchukulia  hatua mratibu  wa wakimbizi kanda ya Kigoma,  Tony Laizer kuhusiana na mchakato huo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya January 15

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images