MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588“Kijana mbona unatushangaa?”
Raisi Donald Bush alizungumza huku akiupeleka mkono wake wa kulia kwenye tumbo la Hawa na kuanza kulipapasa taratibu taratibu. Nikafungua kifungo cha shati langu, taratibu nikaiinamisha sura yangu chini, nikaanza kuvua sura hii ya bandia hadi ninaimalizia na kuinyanyua sura yangu na kuwatazama raisi Donald na Hawa, wote wakabaki wamenitumbulia macho hata mkao wa kimahaba walio ukaa ukavurugika kila mtu akaka jinsi anavyo jua yeye mwenyewe huku mwili wake ukiwa unawatetemeka, kwani yule wanaye muogopa na waliye mkimbia huko walipo toka yupo mbele yao.
ENDELEA
“Da……..”
Hawa wala hakumalizia sentensi yake akapoteza fahamu, raisi Donald akataka kumshika mke wake ila alivyo yatupia macho yake kwenye mkono wangu ulio shika bastola akajikuta akishindwa hata kumsogelea. Kwa jabza kubwa ambayo ninayo nikajikuta nikishindwa kabisa kuzungumza, kifua changu kikaanza kutanuka kwa pumzi kali ninayo ivuta na kuitoa nje.
“Nilitee maji ya baridi”
Nilizungumza kwa sauti iliyo jaa mikwaruzo mingi inayo tokana na hasira, Winy akafungua friji na kunitolea chupa ya maji kisha akanikabidhi. Nikameza fumba moja la mate kisha nikafungua kifuniko cha chupa hii ya maji. Nikamtazama jinsi Hawa alivyo lalaa, maji yote ndani ya kichupa hichi nikamwagia usoni mwake jambao lililo mfanya akurupuke huku akijifuta futa uso wake. Hawa akanitumbulia macho huku akitetemeka sana, taratibu nikaanza kufunga kifuniko cha hii chupa ya maji kisha nikaitupia pembeni. Hata mlio wa chupa katika kuigusa hii meza ikamfanya raisi Donald Bush kushuka.
“Dany ninakuomba unisameheee”
Hawa alizungumza huku machozi yakianza kumwagika usoni mwake. Nikachomoa kiwambo cha sauti kwenye mfuko wangu na taratibu nikaanza kikifunga kwenye mdomo wa bastola yangu. Nilipo hakikisha nimekikaza vizuri nikamnyooshea bastola hii raisi Donald Bush.
“Da…da….ny u….un…a una jua….jua kwa….kwa….”
Sikuwahi kumuona raisi Donald Bush kuwa na kigugumizi ila muda huu amekipata na hata maneno anayo yazungumza hakuna hata moja linalo kamilika mdomoni mwake.
“Dany ninakuomba utusamehee, tazama hali yangu. Tumboni nimebeba malaika wa bwa……”
Nikamtandika raisi Donald Bush risasi ya paja na kumfanya kutoa ukelele mkali sana. Hawa akazidi kuangua kilio, akataka kunipigia magoti chini ila nikamkatalia kwa ishara.
“Hawa ulifikiria nini?”
Nilizidi kuzungumza kwa sauti nzito iliyo jaa mikwaruzo mingi, Hawa akashindwa kabisa kunijubu kwani kilio kimenamfanya hadi matamshi kuhindwa kumtoka na kubaki akichezesha chezesha mdomo wake.
“Nilidhani kwamba huyu mwanaharamu umekuwa naye kwa ajili ya kulipiza kisasi cha baba yako, ila umekwenda kumkumbatia hadi akakupatia mimba kwa nini?”
Nilizungumza kwa kufoka huku nikimtazama Hawa usoni mwake. Ujanja wote wa Hawa umemuishia, nikamtandika raisi Donald Bush risasi ya mguu wake wa pili na kumfanya kugaragara kwenye sofa hili kwa maumivi makali hadi akajikuta akianguka chini huku akiendelea kulia kwa uchungu sana.
“Mulihisi kwamba nitakufa. Hawa nilikuamini sana, nilikujali sana iweje unisaliti hadi umuue mtoto wa rafiki yako Yemi, mwanye amekufanyia nini. Je ni wivu wa mapenzi kisa nilikuwa naye eheeee”
Nilizungumza huku nikimvamia Hawa karibu yake na kumkaba koo lake kwa mkono wanug wa kulia nilio ukataza ila kwa hasira ambayo nipo nayo mkono unatetemeka. Nikamuachia Hawa koo lake na kumfanya akohoe huku akivuta pumzi kwa haraka sana kwani ningeendelea japo hata dakika mbili ningempotezea maisha yake.
“Niambie ni kitu gani ulikosa kwangu eheee”
Nilizungumza huku nikirudi kwenye kiti nilicho kuwa nimekaa, kabla ya kukaa nikamtazama raisi Donald Bush jinsi anavyo garagara hapa chini, nikamkanyaga kwenye jeraha la risasi mguu wake wa kulia huku nikigandamiza nguvu jambo lililo mfanya raisi huyu kuzidisha kilio.
“Ehee”
Nilisikia sauti ya Livna akishangaa anacho kiona. Nikaanza kumkanyaga haraka haraka raisi Donald kwenye jeraha lake huku nikiwa nimeyakaza meno yangu, hadi Livna akanizuida na kunisogeza pembeni.
“Dany hatupo chumba cha adhabu, hapa ni sebleni. Fikiria ni nini cha thamani unaweza kukipata kutoka kwako sawa”
“Kipi cha thamani hapo ambacho ninaweza kukipata kutoka kwao zaidi ya uhai wao”
“Kufa ni lazima uwaue, ila tazama kuna mali, mamlaka na mambo mengi sana ambayo unatakiwa kuyapata Dany”
“Sihitaji hivyo vyote zaidi ya maisha yao”
Nikaachana na Livna na kaunza kurudi sehemu walipo Hawa na mume wake, nikamnyanyua raisi Donald Bush na kumkalisha kwenye sofa.
“Wewe mseng** leo utalifahamu jina nililo zaliwa utotoni”
Nikamtandika ngumi nzito ya uso iliyo zidi kuzidisha maumivu makali kwa raisi huyu. Mlio wa simu wa Livna ukanifanya kusitisha zoezi zima la kumpiga raisi Donald na kumtazama Livna.
“K2”
Livna alizungumza huku akinigeuzia simu yake, nikaon jina la K2, nikataka kunyanyuka na kuipokea simu hiyo ila Livna kwa ishara akanizuia.
“Mzibe mdomo huyo anaye piga makelele”
Nikachukua kijimto kidogo na kumshindilia nacho raisi Donald cha mdomo na kukishikilia kuhakikisha kwamba hakichomoi mdomoni mwake na kupiga makelele yake.
“Muheshimiwa raisi?”
“Livna raisi wa Marekani haonekani”
Niliweza kuisikia sauti ya K2 kutokana na kuweka loud spoker, nikamtazama Hawa anaye endelea kulia kwa uchungu.
“Walinzi wake je?”
“Bado haijajulikana wapo wapi. Hembu wewe na timu yako fwatilieni”
“Sawa mkuu”
Livma akakata simu na kunitazama usoni mwangu, nikauchomoa mto mdogo kutoka mdomoni mwa raisi Donald Bush.
“Mpumbavu unahisi kwamba nchi yangu itakuacha salama katika hili?”
Raisi Donald Bush alizungumza kwa ukali huku akinitazama usoni mwangu. Sikumjibu kitu chochote zaidi ya kumpiga ngumi nyingine iliyo tua mdomoni mwake na kupelekea meno kadhaa kuanguka.
“Dany nakuomba unisamehee kama nitakufa nife ila ufahamu ukweli”
Hawa alizungumza huku akiendelea kulia.
“Ukweli gani ambao unaweza kuniambia?”
“HII MIMBA NI YAKO……”
“Ku**k** msen** wewe unahisi mimi boya wa kudanganyika kirahisi eheeee?”
Nilifoka huku nikinyanyuka kwa hasira nikaishika tena shingo ya Hawa na kuanza kuiminya kwa nguvu huku nikimkazia macho usoni mwake.
“Unahisi kwamba mimi ni fala wa kukubaliana na mimba zisizo na msingi wowote kwenye maisha yangu eheee”
“Kw…..ee….li…..”
Hawa alizungumza kwa sauti ya kukata kata kwani koo lake ninaliminya kisawa sawa.
“Dany ngoja kwanza”
Nikaisikia sauti ya Babyanka, nikamuachia Hawa koo lake huku nikisimama mikono yote ikinitetemeka kwa hasira.
“Dany kwa mke wa raisi nakuomba umpatie nafasi ya kuishi”
“Babyanka hivi unajua ni mangapi ambayo nimeyapitia eheee?”
“Natambua Dany, mimba iwe yayo au isiwe yako, ila ana kiumbe tumboni mwake kipe nafasi ya kuishi kipe nafasi ya kukaa”
“Siwezi kuishi maisha ambayo kiumbe chake kije kulipiza kisasi kwa kiumbe chochote ambacho kitabatizwa jina la baba kuwa ni Dany. Nitamuua yeye na kiumbe chake na ikiwezekana nitamfanyia oparesheni hapa watu wote mukishihudia”
“Dany tafadhalii sana”
Babyanka alizungumza huku machozi yakianza kumlenga lenga usoni mwake.
“Sipo kwa ajili ya kukuvurugia mipango yako, sipo kwa ajili ya kukuzuia kwa kile unacho kifanya. Dany damu ya kiumbe kilichopo tumboni mwake, hakina hatia yoyote, kiumbe hicho hakijafanya makoasa ya wazazi wazazi wake, kipe nafasi amini kile anacho kizungumza huyo dada tafadhali Dany, ninakuomba kama rafiki yako”
Babyanka alizungumza huku machozi yakimwagika, kwa hasira ambayo ninayo nikajikuta nikinyanyua kiti nilicho kikalia na kuanza kupiga nacho raisi Donald Bush hadi kikakatika vipande vipande.
“AKHAHAAAAAAAAA”
Nilipiga makelele ya hasira, uchungu ninao usikia kwenye moyo wangu hauna maelezo, kumbukumbu za wanajeshi zaidi ya laki mbili na nusu nilio kuwa ninawaongoza, pumzi zao zimetolewa na amri ya mjinga huyu. Nikamtazama raisi Donald Bush nikaona jinsi anavyo mwagikwa na damu usoni mwake.
Nikamshika mkono na kuanza kuburuta kuelekea nje.
“Mlindeni huyo malaya”
Nilimuambia Babyanka huku nikimtazama usoni mwake. Livna akaanza kunifwata nyuma. Marrtin na wezake wanao imarisha ulinzi huku nje walipo niona wakabaki wakiwa wamenikodolea macho ya kunishangaa.
“Mkuu”
“Pisha njia”
Nilimfokea Martin na akatii amri yangu, nikaendelea kumburuza raisi Donald hadi kwenye chumba ambacho Martin na Winy walimchinja mkuu wa polisi.
“Shiii ni nini hichi Dany?”
Livna aliniuliza huku akiziba pua yake kwani mwili wa mkuu wa polisi umesha anza kuoza.
“Huyo ni malaya wa K2”
Nilizungumza huku nikimsukumia raisi Donald Bush pembeni ya maiti ya mkuu wa polisi.
“Nani aliye ifanya hii kazi?”
“Martin”
“Ana roho mbaya kama hii?”
“Tuachane na hayo, ninahitaji Wamarekani wafahamu mimi ni nani na wajua wanadili na mtu wa aina gani sawa”
Nilizungumza kwa msisitizo huku nikimtazama Livna usoni mwake, japo kuna harufu mbaya ya uozo, ila kusema kweli siisikii kabisa wala kuihisi puani mwangu.
“Unataka mimi nifanye nini?”
“Simu yako si inachukua kamera vizuri?”
“Ndio”
“Nirekodi nikimchinja huyu malaya tena ninaanza kumkata **o yake”
“Dany are you serious?”
“Unahisi ninacheza au?”
Nilifoka huku nikichukua kisu kikubwa kilicho ganda damu, kilicho tupwa pembeni ya mwili wa mkuu huyu wa polisi. Nikaanza kufungua mkanda wa suruali wa raisi Donald Bush.
“Toa simu yako unirekodi unashangaa nini?”
“Sawa sawa”
Livna alizungumza huku akionekana kama haamini kama hichi ninacho taka kukifanya kitafanikiwa au laa. Nikaivua suruali ya raisi Donald Bush nikaimalizai nguo yake ya ndani, nikamtazama jinsi anavyo hema kwa tabu hapo chini.
“Nilimuamini sana huyu msen**”
Nilizungumza huku nikiipiga piga **o yake kwa kiatu changu cha mguu wa kulia.
“Shusha kamera huku chini watu waone ninavyo toa kikojoleo cha huyu malaya”
Nikachuchumaa huku nikimtazama raisi Donald Bush usoni mwake, nikaishika **o yake na kuanza kuitingisha tingisha.
“....., si unajua kuwapa mimba mademu za watu ehee”
“Dany kweli unawe…….”
Hata kabla Livna hajamalizia sentensi yake, nikaikata **o ya raisi Donald na kusababisha damu nyingi kunirukia usoni mwangu.
“Woooooooooooo”
Nilizungumza huku nikisimama na kuanza kuzunguka ndani ya chumba hichi huku nikishangilia kwa furaha sana. Kazi ya Livna ni kuhakikisha kwamba anarekodi kila kitu ninacho kifanya.
“America, muliwaua wanajeshi wangu. Muliwaangamiza pasipo huruma, muliwachukua mateka na kuwaua wengine pasipo huruma na hichi ndio ninacho kifanya kwa raisi wenu.
Nilizungumza huku nikiwa nimeisogelea simu ya Livna, nikaanza kuionyesha **o ya raisi huyu kwenye kamera hii.
“Na…..kufa….fa”
“Kufa k** k**”
Nilizungumza huku nikiwa nimejawa na furaha kubwa. Nikamnyanyua raisi Donald Bush na kumpigisha magoti. Nikakishika kichwa chake huku nikiwa nimesimama nyuma yake. Kumbukumbu ya familia yangu kuchinjwa ikanijia kichwani mwangu, woga wa kulifanya hili ninalo lifanya hivi sasa ukaniishia kabisa na kujikuta nikianza kukipitisha kisu hichi kwa nguvu kwenye shingo ya raisi Donald Bush, japo ni jambo gumu kulifanya ila nikazidi kujipa ujasiri wa kuendelea kukata kwa nguvu kichwa chake ili kuhakikisha kwamba ninakitenganisha na kiwili wili cha kichwa chake. Hadi ninamaliza kukitengenisha kichwa hichi nikamkuta Livna akiwa ameyafumba macho kwa woga.
“Hei”
Niliita huku nikijipangusa damu zilizo jaa usoni mwangu, nikakishika kichwa cha raisi huyu huku nikishisha pumzi nyingi.
“Jesus Christ Dany!!”
Livna alizungumza baada ya kuniona nimekinyanyua kichwa cha raisi Donald Bush juu.
“Kuanzia hivi sasa jina langu limeingia kwenye historia ya dunia kwa kumuua raisi wa taifa kubwa na kumchija kama kukua. Kizazi na vizazi vitanikumbuka jina langu kama munavyo mkumbuka Osama Bin Laden. Jina langu ninaitwa DANY, DANY LEONDARD”
Baada ya kuzungumza maneno hayo nikakishusha chini kichwa cha raisi Donald Bush ambaye kwa sasa ni marehemu tayari.
“Zima kamera yako kazi imeisha”
Livna akafanya kama nilivyo muagiza huku akinitazama usoni mwangu kwa wasiwasi mwingi.
“Usiogope mtoto wa kike”
“Dany sijawahi kushuhudia hichi ulicho kifanya leo, naogopa Dany”
“Usiogope mpenzi, njoo hapa”
“Ahahaa, sihitaji mijidamu hiyo”
Nikatabasamu, nikaokota **o ya raisi Donald kisha nikaanza kutoka humu ndani huku nikiwa nimeshika viongo vyake vyote viwili, watu wote walio niona wakabaki wakiwa wameshangaa, nikaingia sebleni na kumkuta Babyanka akiwa anazungumza na Hawa, walipo niona nimejawa damu wote wakabaki wameshtuka, ila hakuna aliye ona kwani vitu hivyo nimeficha kwa kuirudisha mikono yangu nyuma. Hawa akaanza kulia tena baada ya kuniona ninamsogelea, nikasimama mbele yake kisha nikamrushia kichwa cha mume wake pamoja na **o yake vikatua kwenye mapaja yake jambo lililo mfanya Hawa kupiga ukunga mkubwa hata Babyanka aliye kaa pembeni yake akakurupuka kwa kuogopa sana kuona viungo hivi.
AISIIIII……….U KILL ME 171
“Dany”
Babyanka alizungumza huku macho yakiwa yamemtoka, mwili mzima ukimtetemeka.
“Rudi hapa”
Nilizungumza kwa ukali huku nikimtazama Hawa usoni mwake. Hawa akaanza kutingisha kichwa huku naye mwili mzima ukimtetemeka.
“Nimesema njioo”
Niliendelea kuzungumza kwa hasira, nikamsogelea Hawa na kumshika mkono wake.
“Nahitaji chumba”
Nilizungumza huku nikimtazama Winy usoni mwake, akanielekeza gorofani, kwa haraka nikaanza kumvuta Hawa na kuwaacha watu wote wakiwa wanashangaa. Tukapandisha gorofani, nikafungua mlango wa chumba cha kwanza nilicho kikuta. Chumba hichi kina kitanda kikubwa pamoja na sofa moja na friji ndogo. Nikamsukuma Hawa kitandani huku nikimtazama kwa macho makali.
“Malaya wako nimesha muua, sasa niambie ukweli hii mimba ni ya nani?”
“Ya…..aa…..”
“SEMAAAA, Yaa…..yaa nini eheee?”
“Yako….ni yako Dany”
“Una uhakika?”
“Ndio Dany, siku ile tu…livyo fanya pale, kule kambini uliniacha na ujauzito”
Nikatabasamu kidogo kisha taratibu nikaanza kuvua nguo zangu, nikapanda kitandani. Hawa akaanza kurudi nyuma huku akiendelea kuniogopa.
“Wewe ndio ulianza kunisaliti Dany, ulitambua kabisa ni jinsi gani nilikuwa ninakupenda. Ukaona njia ya rahisi kuikamilisha kazi yako ni kunisaliti na kutembea na Yemi. Nililia sana zaidi ya siku mbili Dany, yaani nilotoka kwenye maisha ambayo nilipoteza kila kitu kwenye maisha yangu na wewe ndio mtu wa pekee ambaye nilikuwa nimebakiwa na ulikuwa na thamani kubwa sana ila ukaamua kunisaliti ni kwa nini na wewe ulifanya vile?”
Hawa alizungumza huku akianza kutokwa na machozi.
“Kitu kilicho kuja kunichanganya zaidi ni pale nilipo jigundua kwamba nina ujauzito wako, ili mwanangu aje kuishi maisha mazuri niliamua kuwa kimahusiana na raisi Donald Bush kwani wewe tayari ulisha ungana na Boko haramu”
Kitu alicho kizungumza Hawa nikajikuta kikiniingia akilini mwangu taratibu nikamsogelea na kusogeza karibu yangu, nikamkumbatia huku nikimbembeleza taartibu.
“Hawa”
“Beee”
“Sijui kama ninaweza kumuona mwanangu, sidhani kama dunia hususani Marekani itaniacha hai kwa hili nililo lifanya. Kama kweli ni damu yangu ninakuomba umtunze na asije kuwa kama mimi baba yake niliye ishia kwa kulipiza vissai kwenye maisha yangu yoye.”
“Utamlea mume wangu”
“Sina sifa ya kuitwa mume, Hawa kwa sasa sihitaji mahusiano na mwanamke wa aina yoyote. Ulipoteza familia yako kwa ajili yangu, sihitaji upoteze hichi kiumbe kwa ajili yangu”
Nikamuachia hawa taartibu na kurudi lilipo bomba, tukaanza kuoga kwa pamoja tulipo maliza tukatoka humu bafuni.
“Dany”
“Ndio”
“Tutavaa nini?”
Hawa alizungumza hukua akinionyesha nguo zetu, ngup zangu zimejaa damu huku gauni lake nikiwa nimelichana. Nikachukau nguo yangu ya ndani na kuvaa.
“Ngoja nikakutafutie nguo”
Nikatoka chumbani humu na kuanza kushusha ngazi za kueleka chini, nikawakuta Livna, Winy, Babyanka na Martin wakiwa wamekaa haa sebleni. Kila mmoja alipo niona akaonekana kushangaa uvaaji wangu.
“Kuna mpya?”
“Hakuna mpya zaidi ya K2 kunipigia simu kuniuliza kama nimefanikiwa kumpata raisi Donald”
“Winy wifi yako unaweza kumsaidia nguo”
“Wifi…..!!?”
“Unashangaa nini sasa”
“Kushangaa ni lazima kwa maana ni lisaa tu limepita ulikuwa unamzaba makofi huyo unaye muita wifi”
“Yamepita ninakuomba ukamsaidie nguo. Na kama inawezekana na mimi ninaombeni nguo”
“Sawa zipo huku juu”
Winy alizungumza huku akiondoka sebleni hapa.
“Mkuu ni niini kinacho fwata?”
“Kwa sasa nina imani kwamba K2 yupo kwenye hali ya wasiwasi mwingi, na huu ndio wakati wetu kuhakikisha kwamba tunampata”
“Kwa leo itakuwa ni ngumu?”
“Kwa nini?”
“Dany hivi kwa hili ambalo umelifanya unahisi kwamba Wamarekanai watakuwa wamelela. Yaani hivi sasa Dar nzima naihisi imejaa wapelelezi wa Kimarekani, NSS yenu yaani kila kikosi cha ulinzi kinaingia kwenye harakati za kumtafutua raisi Donald na mke wake”
“Ile ume ipost kwenye mitandao ya kijamii?”
“Bado”
“Unasubiria nini?”
“Hukuniruhusu, na hata ukiniruhusu siwezi kuipost hii kwa maana kuna sauti yangu imesikika humo, utanihatarishia maisha yangu ikiwa mimi sio muhusika sana kwa kifo chake”
“Ila tumeshirikiana kumteka si ndio?”
“Hata kama, acha kwanza tuangalie hali halisi tukiwa wajinga sote tutakufa pasipo kukamilisha lengo la huu umoja wetu”
“Ila alicho kizungumza Livna ni kweli mkuu inabidi kutulia kwanza hili tulilo lifanya ni kubwa sana kwa maana ni pigo kwa dunia na sin chi ya Marekani pekee”
Babyanka naye akashauri, nikamtazama Martin naye akatingisha kichwa kukubaliana na ushari nilio pewa.
“Sawa bila nyinyi mimi leo nisinge kamilisha hili nililo lifanya leo”
“Hayo ndio maneno. Ehee vipi huyo mke wa raisi?”
“Nimempa nafasi ya kujifungua mtoto wake kwa maana anadai kwamba ni mtoto wangu”
“Katika vitu ambayo Dany nimekupa asilimia mia ya mia ni katika hilo “
Babyanka alizungumza huku akiwa amejawa na furaha.
“Dany hembu angalia hizi nguo zitakutosha?”
Winy aizungumza hukua kinikabidhi suruali na tisheti, nikaanza kuvivaa taratibu na kwa bahati nzuri vikanienea mwilini mwangu.
“Shukrani”
“Inabidi mimi nitoke nikaangalie hali halisi inayo endelea huko nje”
Livna alizungumza huku akitutazama.
“Si inaweza kuwa hatari kama wakigundua kwamba wewe ndio ulihisika katika kumteka raisi Donald?”
Martin alizungumza huku akimtazama Livna usoni mwake.
“Hawawezi, kuna timu yangu nyingine ambayo inanilinda na si rahisi kwao kuacha ushaidi wa aina yoyoyte ambao unaonyesha mimi au sisi tumehusika katika hili”
“Sawa kama kuna salama”
“Pia kitu kingine nitatafuta sehemu nyingine ambayo itakuwa ni nzuri kwa sisi kuweza kujificha khadi hii hali itakapo tulia”
“Kichwa cha yule fala na **o yake vipo wapi?”
“Tumevihifadhi”
“Tumtumie K2 au munasemaje?”
“Dany acha papara, tumekulaliana kuangalia hali halisi ambayo inaendelea huko nje, sasa maswala ya kumtumia K2 hicho kichwa ya raisi mwenzake nakuhakikishia utakamatwa, wewe tulizana kwanza sawa”
Livna alizungumza kwa msisitizo sana huku akinitazama usoni mwangu.
“Sawa mkuu”
“Nitawaacha wasichana wangu wawili hapa ninaondoka na wengine, ninawaomba huduma zote muwapatie”
“Hilo halina shaka, tutegeeme utarudi muda gani?”
“Usiku kuanzia saa tano ila nitawapatia habari ya kila kitu kinacho endelea”
“Inabidi ni kupatie namba yangu”
Winy alizungumza huku akimtazama Livna usoni mwake
“Sawa”
Winya kamtajia Livna namba yake ya simu kisha Livna akampigia Winy.
“Ndio hii inayo ishia na nane nane”
“Ndio, ila usinipigie hadi mimi nikupigie”
“Sawa”
Livna akaondoka na vijana wake huku akiondoka na gari moja tulilo kuja nalo. Winy na wezake wakaanza kuandaa chakula.
“Mkuu”
Martin aliniita kwa sauti ya chini huku akinisogelea karibu yangu.
“Ndio”
“Ninataka kula Winy”
“Mmmmm”
“Yaaa nimesha rekebisha mambo yapo poa?”
“Sawa kama ni hivyo, mimi ngoja nikamtazame huyo bibie huko juu”
“Sawa”
Nikanyanyuka kwenye sofa nililo na kuanza kupndisha gorofani, nikaingia kwenye chumba nilicho muacha Hawa, nikamkuta akiwamalizia kuvaa nguo.
“Muda wote ulikuwa unavaa?”
Nilizungumza huku nikisimama nyuma ya Hawa na mikono yangu nikaipitisha kiunoni mwake na kushika tumboni mwake.
“Yaaa sina hata hamu ya kutoka huko nje”
“Kwa nini, au bado unaniogopa?”
“Hapana sikuogopi ila nina wasiwasi na wewe na hichi kiumbe”
“Wasi wasi wa nani kwa manaa hata leo nikikamatwa wewe wala huto guswa na utaokolewa kama mke wa raisi”
“Mmmmm ila kumbuka wewe ndio baba”
“Ya……”
Sikumalizia sentensi yangu nikaanza kusikia mlio wa helicopter kwa haraka nikamuachia Hawa na kukimbilia dirishani, nikafungua pazia taratibu nikaona helicopter ya jeshi la kimarekani ikishusha wanajeshi wanao tumia kwene nyumba ya tatu kutoka hapa tulipo jambo lililo niogopesha sana kwani kama wameshuka kwenye nyumba ya tatu kutoka tulipo basi kutufikia sisi hapa ni haraka sana jambo ambalo ni hatari sana kwangu na watu wanao nisaidia mimi.
ITAENDELEA
‘Haya sasa Wamarekani wamesha gundua ni wapi alipo jificha Dany na kikosi chake, Je ninani aliye itoa siri hiyo? Usikose sehemu inayo fwata ya hadi hii ya kusisimua kutoka kwa muandishi mahiri Eddazaria G.Msulwa”