Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

BREAKING: Diamond Platnumz Aanguka Stejini Sumbawanga

$
0
0
Msanii Bongo Fleva, Naseeb Abdul maarufu kama Diamond Platnumz ameanguka stejini wakati akifanya shoo jioni ya leo katika Uwanja wa Nelson Mandela Sumbawanga .

Kabla ya kuangua Diamond alikuwa akiiimba wimbo wa Zilipendwa akiwa na Mbosso na Rayvan huku wakirukaruka na baadae gafla steji ilifunuka na kupeleka Diamond na Rayvan kuanguka chini ya steji.

Tazama kipande cha video hapa chini

Naibu Katibu Mkuu wa Chadema-:Muswada wa marekebisho wa vyama vya siasa Utaliweka Taifa Katika Hatari Kubwa Ya Machafuko

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu wa Chadema- Zanzibar, Salum Mwalimu amesema muswada wa marekebisho wa vyama vya siasa uliosomwa bungeni Novemba 16 utaliliweka Taifa katika hatari kubwa kwa sababu utavuruga vyama vya siasa pamoja na maisha ya wananchi.
 
Amesema hayo leo Desemba 9  katika mkutano uliovikutanishwa vyama 15 vya siasa vya upinzani wakati vikitoa tamko  lao linalopinga muswada wa marekebisho ya sheria ya vyama vya siasa uliosomwa bungeni Novemba 16 mwaka huu.
 
Akizungumza katika mkutano huo Mwalimu amesema muswada hupo umelenga kuviua vyama vya upinzani baada ya kushindwa kupitia kuwarubuni madiwani na hivi sasa wanataka kutumia sheria.
 
“Yaani leo hii tukitaka kuwajengea uwezo viongozi wa vyama vyetu tukaombe kibali kwa msajili wa vyama vya siasa tena tuwaambie tunawafundisha nini, nani kadhamini na kwa muda gani huu ni wendawazimu,”
 
Amesema suala hilo linalenga kudhoofisha ushiriki wa wabunge wa upinzani wawapo bungeni washindwe kufanya jambo lolote.
 
Amesema pia suala la kumtaka msajili kutaka taarifa yoyote ya chama kutoka kwa mtu yoyote unalenga kuvigombanisha vyama.
 
 “Kama wanayoyafanya ni mema kwa nini wawekewe kinga ya kutoshitakiwa na kwa sababu kapewa nguvu ya kuviagiza vyama vya siasa kufanya marekebisho ndani ya miezi sita juu ya jambo lolote wanaweza siku kutuambia hawataki tuwe na makatibu wakuu.
 
“Na huyu anaweza kutuamuru tuondoe vifungu vya msingi katika katiba zetu ili waweze kutudhofisha, sisi tutasema hapana.
 
“Sheria ya kusema chama kitakachopata ripoti isiyoridhisha kizuiliwa ruzuku kwa miezi sita ni jambo gumu kwa sababu tangu awali tulikuwa tukimpinga  na hivi sasa ameamua kujipa kinga ili afanye mambo kwa mujibu wa sheria,” amesema Mwalimu.
 
Amesema pia mamlaka ya kumvua uanachama mtu yoyote haujalenga wananchi bali watu walio na ushawishi ndani ya vyama pamoja na viongozi wakubwa.

Habari Njema: JWTZ Yatangaza Nafasi Za Kuandikishwa Jeshini Madaktari Wa Binadamu Na Fani Nyingine Za Tiba

$
0
0
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) linatangaza nafasi za kuandikishwa Jeshini Madaktari wa Binadamu na fani nyingine za Tiba.

Nafasi hizo zinatolewa ili kuongeza idadi ya wataalamu wa tiba watakaotoa huduma za afya katika Hospitali zetu, vituo vya afya na Zahanati kulingana na mahitaji  ya sasa na siku zijazo.

Watakao andikishwa Jeshini ni wale wenye taaluma zifatazo:-

a. Daktari Bingwa wa Meno    -  Dental Surgeon

b. Daktari Bingwa     -       Specialist Neurasurgeon

c. Mkemia   (Chemisist)

d.Mteknolojia Msaidizi (Maabara) - Assistant Laboratory Technician.

e. Tabibu msaidizi     -  Assistant Clinical officer.

f. Katibu wa Hospitali  -

g.Msaidizi wa kumbukumbu.  – Medical Records (Certificate)

h. Daktari  - Medical Doctors.

j. Afisa Muuguzi  -  Registered Nursing Officer.

k. Fundi sanifu vifaa tiba  -  Bio Medical Engineer.

l.  Tabibu   - Clinical Assistant  (Certificate).

m. Mteknolojia msaidizi -  Laboratory Assistant (Certificate)

n. Mfamasia -  Pharmacist  (Degree)

o. Mtoa tiba kwa vitendo  - Physiotherapist  (Diploma)

p.  Afisa Muuguzi msaidizi  - Assistant Nursing officer

Sifa za kuandikishwa Jeshini ni zifuatazo:-

a.  Awe raia wa Tanzania kwa kuzaliwa.

b. Awe na umri kati ya miaka 18 hadi 28 isipokuwa specialist

c. Awe na afya njema ya mwili na akili timamu.

d.  Awe mwenye tabia njema na nidhamu nzuri

e. Awe hajawahi kupatikana na hatia ya makosa ya jinai Mahakamani na kufungwa jela.

f. Awe na cheti halisi cha kuzaliwa (Original Birth Certificate), vyeti vya shule (Academic & School Leaving Certificates) na vyeti vya Chuo (Transcript & Academic Certificates).

g. Kama ni Daktari awe amemaliza mafunzo kwa vitendo (Internship) na kutunukiwa vyeti pamoja na kusajiliwa na Bodi.

h.Awe hajatumikia Jeshi la Polisi, Magereza, Chuo cha Mafunzo au Kikosi Maalumu cha Kuzuia Magendo.

Wenye sifa tajwa na kuhitaji kujiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania waripoti katika Kambi yaJenerali Abdallah Twalipo, Mgulani    Dar es Salaam tarehe              17, Desemba, 2018 kuanzia saa 1.00 Asubuhi kwa usaili.

Waombaji wafike na vyeti halisi (Original Certificates) vya kuzaliwa na masomo pia wajitegemee kwa usafiri, chakula na malazi.

Aidha, watakaochaguliwa na kuandikishwa Jeshini watapatiwa mafunzo mbalimbali ya Jeshi na yatakayo waendeleza katika taaluma zao. Wakiwa Jeshini majukumu watakayopatiwa ni yale yatakayowapa changamoto na fursa nzuri za kutumia taaluma zao.

JIUNGE NA JWTZ UJIFUNZE MENGI, UONE MENGI NA UFAIDI MENGI

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya Disemba 10

Waziri Lugola Amsweka Selo Afisa Mtendaji

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amemsweka ndani Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Namalebe, Kata ya Chitengule, Jimbo la Mwibara, wilayani Bunda, kwa kosa la kutafuna fedha za wanakijiji wilayani humo.


Waziri Lugola ambaye ni Mbunge wa jimbo hilo alitoa maamuzi hayo katika mkutano wa hadhara na wananchi hao uliofanyika kijijini hapo jana, baada ya kuwataka wananchi wenye malalamiko, maswali pamoja na ushauri watoke mbele ili aweze kuwasikiliza wananchi hao.

Baada ya agizo hilo, zaidi ya wananchi kumi walijitokeza na kuuliza maswali pamoja na kutoa kero zao, ndipo watu saba kati ya waliotoka mbele wakiwa wamepanga foleni walitoa tuhuma mbalimbali kuhusiana na Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho, Wilbard Malea kutafuna fedha zikiwemo fedha za maendeleo ya kijiji pamoja na za faini kutokana na mashtaka yanayowasilishwa na wananchi kwake kwa ajili ya usuluhishi pamoja na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Mkazi wa Kijiji hicho, Simon Joseph alimtuhumu katika mkutano huo, Mtendaji huyo alimfuata katika kikundi chao cha Muungano cha kuweka na kukopeshana alisema anaomba kukopa fedha shilingi 91,000 na kijiji kitarudisha fedha hizo, lakini mpaka leo hajazilipa na hakutumwa na Serikali ya Kijiji bali alisema uongo ili ajipatie kwa njia ya udanganyifu.

Pia Happyness Tabonwa mkazi wa kijiji hicho, alimlalamikia mtendaji huyo amechukua mbuzi wake watatu baada ya kushindwa kulipa shilingi 50,000, akaamua kuwakamata mbuzi hao na baada ya kumpeleka elfu 50 anayoidai Mtendaji huyo akashindwa kuwarudisha mbuzi hao kwa kuwa alishawauza na pesa kazitafuna.

Wananchi hao pia walimlalamikia Waziri Lugola, kuwa Mtendaji huyo wanapopeleka mashtaka  yao, watuhumiwa hupigwa faini lakini fedha ikitolewa haiendi mfuko wa maendeleo ya kijiji bali fedha hizo uzitumia mtendaji huyo.

Pia mtendaji huyo analalamikiwa kuchukua simu ya mkononi ya Joseph Japhet ambaye alipohamia kijijini hapo aliambiwa alipe shilingi 50,000 ikiwa ni malipo kwa ajili ya maendeleo kijijini hapo, hata hivyo fedha hiyo hakuwa nazo ndipo Mtendaji huyo akamnyang’anya simu yake.

Wakati wananchi hao wanatoa malalamiko hayo, mtendaji huyo alikuwa mbele katika mkutano huo baada ya kuitwa na Waziri Lugola ili aweze kujibu tuhuma hizo zikiwemo za kujipatia fedha kwa njia ya udanganyi pamoja na kuwadhulumu wananchi mbalimbali wa kijiji hicho.

Akijibu tuhuma hizo Mtendaji huyo, Malea alizikana tuhuma hizo na baada ya kubanwa huku wananchi hao wakielezea kwa mifano, ndipo akakiri kutafuta fedha za wananchi hao na akaahidi katika mkutano huo atawalipa wananchi wote wanaomdai.

Baada ya kukiri ndipo Waziri Lugola akamwita Mkuu wa Kituo cha Polisi Kibara Wilayani Bunda, Mkaguzi Boniface Mwalupale, ili Polisi walipo katika mkutanon huo wamkamate Mtendaji huyo na akafunguliwe mashtaka endapo atashindwa kuwalipa wananchi mbalimbali wanao mdai kama alivyokiri.

“Ndugu wananchi, kwanini hawa viongozi mnaowachagua wanakua sio waadilifu?, nimefanya mikutano katika vijiji mbalimbali nimekutana na changamoto kama hii, na pia katika kijiji ambacho tumetoka, Mtendaji wa Kijiji pamoja na Mwenyekiti wa Kijiji hicho wametafuna fedha za mchanga zilizotolewa na kampuni inayojenga barabara ya Bunda hadi Kisorya, tunaenda wapi ndugu zangu, viongozi wadokozi kama hawa lazima tuwakamate, najua polisi mnahamu ya kukamata  mhalifu, mkamateni ili akaeleze hizo fedha alizipeleka wapi na kwanini alizitafuna fedha za wanakijiji,” alisema Lugola.

Akizungumza saa mbili baada ya kumkamata mtuhumiwa huyo, Mkuu wa Kituo cha Polisi Kibara (OCS), Mwalupale alisema Mtendaji huyo anadaiwa zaidi ya shilingi 300,000 lakini mpaka sasa ameshatoa 206,000, hata hivyo hawajamuachia bado yupo polisi mpaka atakapomaliza kulipa madeni yote.

“Bado hatujamtoa mtuhumiwa huyo ambaye amejipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na utapeli, mpaka sasa tayari ametoa 206,000, bado mbuzi watatu hajalipa,” alisema OCS Mwalupale.

Lugola anaendelea na ziara yake kwa kutembelea vijiji vyote jimboni kwake Mwibara akisikiliza kero za wananchi pamoja na kuhamasisha kilimo cha mazao ya pamba, mahindi, mpunga, viazi na mengineyo ambayo wakazi wa jimbo lake wanalima mazao hayo kwa wingi.

Serikali: Mradi wa Bomba la Mafuta Uganda-Tanga haujasimama

$
0
0
Serikali imesema utekelezaji wa Mradi wa Bomba la Mafuta kutoka (Hoima) Uganda hadi Mkoani Tanga haujasimama na kwamba hatua za utekelezaji wa mradi huo zinaendelea na

Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam na Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani baada ya kumalizika Mkutano wa majadiliano ya utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa bomba hilo uliomkutanisha na Waziri wa Nishati na Madini wa Uganda, Irene Muloni.

Amesema kuwa utekelezaji wa mradi huo uko katika hatua nzuri na kwamba pande zote mbili wamejadiliana na kukubaliana kuhakikisha unakamilika kwa wakati uliopangwa pamoja na hatua za utkelezaji za mradi.

“Mradi haujasimama tunaendelea na utekelezaji tumekubaliana tukamilishe ndani ya waakati tuliokubaliana pande zote mbili,” amesema Dkt. Kalemani.

Amebainisha kuwa katika upande wa Tanzania tayari wamekamilisha tafiti ya tathmini ya mazingira, ustawi wa jamii pamoja ulipaji fidia mkoani Tanga.

Dkt. Kalemani amesema malengo ya majadiliano ya mkuano huo ni hatua za utekelezaji wake ikiwemo usafirishaji wa mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga na kuyauza nje za nje.

Ameongeza kuwa mradi huo utakuwa manufaa kwa jamii na makampuni ya ndani na kusisitiza bomba lina urefu kilometa 1435 huku kilometa 1115 zikiwa sehemu ya Tanzania.

Kwa upande Waziri Muloni amesema watahakikisha watafikia makubaliano na makampuni ili yaweze kusaini utekekezaji wa mradi ukamilike mwaka 2020 ilivyopangwa.

Amefafanua kuwa ifikapo Januari 14 mwakani mkutano mwingine utafanyika nchini Uganda lengo likiwa kujadiliana mambo yaliyobaki makampuni yaanze utekelezaji

Serikali Yasema Tayari Imekwishalipa Billion 83 Kwa Wakulima 82,835 Wa Korosho.

$
0
0
Na Bakari Chijumba, Mtwara.
Hadi kufikia  tarehe 8 Disemba 2018 serikali imefanikiwa kuwalipa jumla ya wakulima 82,835 katika Mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma.

Jumla ya fedha iliyolipwa kwa wakulima hao ambao tayari wamefanyiwa uhakiki ni Bilioni 83 ambapo katika mkoa wa Mtwara wakulima 50,835 wamelipwa mkoa wa Lindi wakulima 22,131 na Mkoa wa Ruvuma ni wakulima 9,445

Hayo yamesemwa na Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga jana tarehe 9 Disemba 2018 wakati akizungumza kwenye mkutano wa wabanguaji wadogo wa korosho kutoka katika mikoa mitano ya Mtwara, Lindi, Ruvuma, Pwani na Morogoro uliofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Mtwara.

 Mhe Hasunga amesema, jumla ya vyama 328 vimefanyiwa uhakiki kati ya vyama 504 vilivyopo katika mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma ambapo jumla ya vyama 319 vimekwishalipwa.

Aidha, Hasunga amewatoa hofu wananchi wanaopotoshwa kuwa bado wakulima hawajalipwa kiasi chochote cha fedha huku akisisitiza kuwa wakulima wanalipwa kupitia njia ya benki hivyo wanapaswa kuwa na utamaduni wa kwenda benki.

Mhe Hasunga amesisitiza kuwa serikali imedhamiria kuwanufaisha wakulima wa korosho ambapo tayari amewaelekeza watendaji wa Bodi ya Korosho Tanzania kuwasajili wakulima wote wa korosho ili watambulike.

Waziri Hasunga amesema kuwa kikao hicho kina lengo la Kujadiliana na kukubaliana utaratibu uliopangwa na serikali katika ubanguaji wa korosho mwaka 2018/2019 kwa kuelekeza ubanguaji kufanyika nchini ili kuwanufaisha wananchi katika ajira hiyo.

“Tumeiona changamoto ya mitaji kwa wabanguaji wadogo nchini sambamba na wabanguaji wakubwa hivyo ili serikali iwarahisishie upatikanaji wa mitaji tumeamua kuwapa kazi ninyi wenyewe” Amesema Hasunga.

Waziri Hasunga amesema swala la uhakiki limejikita zaidi kubaini udanganyifu unaofanywa na baadhi ya wahujumu wa biashara ya korosho .

“Kuna watu walikuwa wametoa akaunti za benki lakini zinatofautiana na majina ya watu waliwasilisha korosho zao kwenye maghala ya kuhifadhia korosho” amesema  Hasunga 
 
Hasunga, amesema lengo la serikali ni kutaka kuona wakulima wananufaika hivyo korosho zote zitabanguliwa hapa nchini.

“Tulipoona soko la korosho linayumba huku lengo la serikali likiwa ni kutaka kuonana wakulima wananufaika tuliamua kuingilia kati na kuanza kununua korosho zote na kwa kwenda mbele Zaidi tumeamua kubangua korosho zote hapa hapa nchini”

MWISHO.

LIVE | Rais Magufuli Kakutana na Uongozi wa Juu TRA Katika Kikao Maalumu....Tazama Kila Kitu hapa

$
0
0
Rais Dkt John Magufuli, leo Desemba 10, anazungumza na watendaji wa juu wa Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) katika kikao maalum kitakachodumu kwa muda wa saa tatu.Tazama hapo chini. Video kwa hisani ya Globaltv

Darasa Aibuka Upya Baada ya Ukimya wa Muda Mrefu

$
0
0
Msanii  nyota wa muziki wa bongo fleva, Darasa amekuja na ujio mpya kwa nyimbo mbili Kali ambazo ataziachia rasmi Jumatano.

Darasa ambaye anatamba na nyimbo zake moto ukiwamo 'Muziki' ambao umefanya vizuri, amesema ukimya wake ulikuwa na maana kubwa licha ya kuzushiwa mambo mengi mabaya.

"Wasanii hatupendani, unapofanya vizuri badala ya mtu kukuchalenji kwa kutoa nyimbo nzuri wenyewe wanazusha vitu tofauti, muziki umekuwa na siasa sana, nilikuwa kimya na 'projekiti' zangu na nimekamilisha sasa naziachia," amesema Darasa.

Amesema Jumatano ataachia wimbo mpya wa 'Pisha Njia" ambayo tayari ameufanyia video.

"Huu wimbo video yake nimeifanyia Afrika Kusini..., nimetumia mtindo wangu ninaoutumia katika kuimba, naamini utakuwa aibu kwa wote ambao hawanitakii mema na kunizushia uongo," amesema Darasa

IKULU Yampongeza Msanii Diamond...Mwenyewe Afunguka Maneno Mazito

$
0
0
Baada ya ukurasa wa kijamii wa instagram wa Ikulu kumpongeza msanii Diamond Platnumz kwa mchango wake wa maendeleo ya jamii ikiwemo kuchangia shule ya msingi ya Sumbawanga katika ujenzi wake hatimaye mwanamuziki huyo ameandika ujumbe wa shukrani kwa Serikali  kwa kutambua mchango wake na sanaa kwa ujumla.

Diamond ambaye kwa sasa yupo Sumbawanga kwaajili ya tamasha lake la Wasafi Festival, amekubali kubeba jukumu la kujitolea kuimalizia shule ya Msingi ya Sumbawanga ambayo ilihitaji milioni 68 ili kuhakikisha imemalizika na kuanza kupokea wanafunzi mwezi Januari ambapo aliridhia kubeba jukumu hilo huku akiongezea kuwa yupo tayari kujitolea na mabati 150.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH....Anatoa Pete za Bahati, Anasafisha Nyota, Anazuia Chuma Ulete na Mengine

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam Shariff,  Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
 
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Adam Shariff Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. 

Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Mawasiliaono: +255715971688  au +255756914036
 
Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power

$
0
0
Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power Kwaajili Ya Nguvu Za Kiuume Na Promix Kwaajili Ya Kuongeza Maumbile;
Kwa mwanaume aliyekamilika na mwenye Afya njema ili kumridhisha mke au mpenzi anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara mbili hapo utamridhisha mpenzi wako ila ukiwa unapiga moja au mbili hapo ujue umejilidhisha wewe 

Tiba Ya Tatizo Lako Ni Dawa Hiitwayo Simpo Power No, 1; dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge vya miti shamba na unga ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja :-1 itakufanya urudie tendo zaidi ya mara tatu 
2 itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika 15-20 kwa tendo la Kwanza 
3 huimarisha uume uliolegea na kusinyaa 

Je Una Mke Au Mpenzi Aliyebalikiwa Kuwa Na Kario Kubwa Au Mwili Mnene Na Wewe Mume Wake Una   Maumbile Mafupu?; tumia sasa dawa ya PROMIX dawa itakufanya umfikishe shemu nyeti maana inaboresha maumbile saizi upendayo.

Dawa zangu haziina madhara yoyote kwa mtumiaji 

MARKSU; ni dawa ya kisukari dozi siku 21 
MWARU; ni dawa ya uzazi,hufungua milija ya uzazi ata kwa Wale waliofungiwa uzazi  
MTUNDUU; ni dawa ya busha bila kupasua 
MAZANZA; ni dawa ya kisukar zipo dawa za miguu Kuuma,tumbo,kupunguza Matiti,kutoa minyama uzembe ngiri,vidondo vya tumbo  

FIKA OFISINI KWANGU BUGURUNI MALAPA KARIBU NA KOTA ZA POLISI AU PIGA  SIMU ULETEWE MAHALI ULIPO SIMU NO 0783185060,  0752348593  -DR AGU

Wimbo Mpya: Paschal philibert- Bwana Kimbilio

$
0
0
Wimbo Mpya: Paschal philibert-  Bwana Kimbilio. utazame hapo chini

Serikali Yazitaka Taasisi za Dini Ziendelee Kuhubiri Amani

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), Seleman  Jafo amesema taasisi za dini na viongozi wake wana kila sababu ya kuhimiza upendo na mshikamano wa kuliombea Taifa ili Watanzania waendelee kuishi kwa amani  na utulivu.

Jafo ambaye ni Mbunge wa Kisarawe ametoa kauli hiyo, jana Jumapili Desemba 9,2018 wakati ufunguzi wa mkutano wa 34 wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Mashariki ya Pwani (DMP).

Ufunguzi wa mkutano huo wa siku tatu ulitanguliwa na ibada iliyoendeshwa na Askofu kwa kanisa hilo, Dk Alex Malasusa iliyofanyika katika kanisa la Kilutheri la Mbezi Beach.

Jafo alisema baadhi ya mataifa hayana amani wala utulivu lakini Tanzania kuna  hali hiyo na vyema viongozi wa dini na taasisi hizo zikaendeleza maombi kwa Taifa ili Watanzania kuishi kwa usalama.

"Taifa bado linahitaji maombi, nawashukuru viongozi wa dini kwa kuliombea Serikali ipo bega kwa bega na ninyi kwa sababu mnaisadia kuwajenga  wananchi kwenye msingi wa kiroho," alisema Jafo.

Dk Malasusa alisema mkutano huo una malengo mbalimbali ikiwamo kujadili masuala kadhaa yanayohusu dayosisi katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.

"Ndani ya miaka miwili tumefanikiwa masuala kadhaa ndani ya dayosisi hii. Miongoni mwa mambo hayo ni kuunda mfuko wa elimu wa dayosisi hii kwa ajili kutoa huduma," alisema Dk Malasusa.

Reli mpya kujengwa Dar es salaam Ili Kupunguza Msongamano wa Magari

$
0
0
Shirika la Reli Tanzania (TRC), linatarajia kujenga reli mpya katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ili kupunguza msongamano wa magari.

Mradi huo ambao uko katika hatua za usanifu utaenda sambamba na ule wa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) na uboreshaji reli ya kati.

Akizungumza jana, Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa, alisema kutokana na ongezeko la idadi ya watu katika jiji hilo usafiri wa reli ndio njia pekee inayoweza kuchukua watu wengi na kuondoa msongamano.

“Kwa Jiji la Dar es Salaam lilivyo mwaka 2030 idadi ya watu inaweza kuwa mara mbili ya ilivyo sasa, huwezi kuwahudumia kwa kutumia mabasi tu usafiri pekee unaofaa na kwa wakati ni reli,” alisema Kadogosa.

Alisema reli hizo mpya zitahusisha usafiri wa kutoka Dar es Salaam – Bagamoyo, Dar es Dalaam – Mbagala na Dar es Salaam – Uwanja wa Ndege.

Alisema hivi sasa wanafanya upembuzi yakinifu na kwamba kutakuwa na timu ya wataalam itakayohusisha vyombo vyote kuhakikisha suala hilo linasimamiwa kwa umakini.

“Kuna watu wamevamia maeneo ya reli, walijaribu kitafuta hati hawajapewa lakini kwa sababu ya ukaidi wamejenga, sasa ambaye amejenga maeneo ya reli aondoke na chochote kitakachofanyika kitakuwa ndani ya sheria,” alisema.

Katika hatua nyingine alisema wameanza kupanga matumizi bora ya ardhi katika maeneo yote inakopita reli ya kisasa (SGR) ili kuzuia uvamizi.

“Tumeanza ‘ku – design’ njia yote kuanzia Dar es Salaam na kandokando ya reli kutakuwa na maeneo yatakayojulikana shughuli zake,” alisema.

Mkurugenzi huyo alisema kuelekea katika uchumi wa kati reli hiyo ni fursa kubwa katika uchumi wa viwanda na biashara ya bandari na kuwataka wadau mbalimbali kuchangamkia fursa hiyo.

Alisema pia reli ya kisasa itawekwa uzio ili kuepusha mdhara kwa sababu itakuwa na mwendo mkali.

Kuhusu ukarabati unaoendelea katika reli ya zamani, alisema umefikia katika hatua nzuri na kwa ile ya Tanga – Arusha walishapita Mombo na hivi sasa wamefikia katika eneo la Same.

“Reli ya zamani bado ni muhimu kwa sababu hata sasa ndiyo inayotumika kusafirisha vifaa vya ujenzi wa SGR na wananchi wanaitegemea. Na reli zote zitaendelea kufanya kazi kwa pamoja kama ilivyo katika nchi zingine,” alisema Kadogosa.

LIVE: Rais Magufuli akihutubia kwenye kikao maalumu na Vigogo wa TRA

$
0
0
LIVE: Rais Magufuli  akihutubia kwenye kikao maalumu na Vigogo wa TRA

Gavana BOT: Mikopo mingi chechefu inatokana na wafanyakazi wa benki wasio waaminifu

$
0
0
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Florens Luoga, amebainisha sababu za benki kutokopesha linatokana na benki zenyewe kutokuwa na wafanyakazi waaminifu kwa kuruhusu wakopaji wasiokidhi vigezo na kusababisha mikopo chechefu.

Kutokana na hali hiyo, amesema BoT imechukua jukumu la kufuatilia kuajiriwa kwa watumishi hao pamoja na mambo mengine.

Profesa Luoga amesema hayo leo Jumatatu Desemba 10, katika mkutano wa Rais John Magufuli na uongozi wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA).

“Ni kweli benki zinapaswa kuwa huru lakini BoT inapaswa kuangalia mwenendo wao, kwa mfano kuna wakati mikopo ilikuwa haitolewi, BoT imechukua jukumu na imekuwa ikikaa chini na benki nchini kutathmini kwanini mikopo haitolewi na mara nyingi majibu na kwamba benki inaogopa hasara kwa sababu watu hawajulikani lakini BoT imechukua jukumu kuhakikisha watu wanajulikana.

“Pia kumekuwa na tatizo la rushwa, wakopaji wengine wabovu wamekuwa wakihonga ili wakopeshwe sasa tunajiuliza inakuwaje benki inamkopesha mkopaji mbovu,” amesema.

Pamoja na mambo mengine, Profesa Luoga amesema kumekuwa na tatizo la wafanyakazi wasio na uwezo au ujuzi usiotakiwa kwani si rahisi kuwa benki inakopesha kwa mradi ambao mkopo wake haurudishiki.

“Pale inapoonekana benki haina watu wenye weledi katika uongozi BoT itaendelea kutoa masharti kuwa watu wote lazima wawe na watumishi stahiki,” amesema.

Je Unapata Pesa Lakini Hujui Iendako Au umetupiwa Jini Chuma Ulete....Bofya Hapa Kupata Suluhu

$
0
0
Je Unapata Pesa Lakini Hujui Iendako Au umetupiwa Jini Chuma Ulete Na Tambua Jinsi Nyota Yako Inavyoweza Kutembelewa Na Watu Bila Wewe Kujijua:Kutana mganga wa tiba asili ambaye anatumia kipaji chake alichajaliwa na muumba wake... anatumia kioo cha asili kutibu magonjwa sugu yaliyoshindikana ata kama upo mbali 

Je Unauza Mali Zako Kama Vile Gari,nyumba,shamba,au Kiwanja lakini havihuziki? wasiliana na Mimi Leo uweze kuona nguvu ya maajabu ili mpaka vitu Mali iyo iwe ni yako halali isiwe na malalamiko hakika mungu atatia mkono wake. 

Je Umepotelewa Na Pesa Au Mali Yako Au Ndugu Yako Aliyepotea Kimiujiza Na Hujui Alipo? Acha kukata tamaa kipo kioo cha asili kitakulejea kile kilichopokea bila masharti magumu 

Je Unahitaji Kupata Mafanikio Bila Kutoa Kafara Au Unahitaji Pesa Za Majini?  acha kuogopa sasa wapo wengi waliokuwa hawaamini kama wewe ila kwa sasa wanamiliki pesa,majumba ya kifahar,maduka ya jumla,pamoja na viwanda kumbuka kuwa uwoga wako ndio umasikini wako na hakuna anayefanikiwa bila kuwa jasiri 

Je Umeachwa Na Mke Au Mme Au Unampenda Lakini Yeye Hakutaki ? onana Leo na chifu Ruyamba ili aweze kukupatanisha na mpenzi wako ndani ya Massa sita 6 tu atakuelewa 

Je Umegombana Na Bosi Wako Au Unataka Kupandishwa Cheo Au Wewe Ni Mpenzi Wa Kucheza Bahati Nasibu? acha kujiona mpweke utapatiwa Pete au saa itakayoendana na shughuli yako unamdai mtu ataki kukulipa au unakesi mahakamani ujui cha kufanya CHIFU RUYAMBA NDIO SURUHISHO WA YOTE .Hata kama ujawai pata mtoto uzazi wako utafunguliwa pia natibu kisukari,presha,busha bila kupasua,nguvu za kiume,na kuongeza maumbile ya kiume  saizi upendayo 

OFISI INAFUNGULIWA SAA MBILI ASubui adi saa mbili usiku na kwa sasa CHIFU RUYAMBA KAANZA  ZIARA MIKOANI PIGA SIMU 0764638796

Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Kuendelea Kuyafunga Maduka ya Kubadilishia Fedha

$
0
0
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Florens Luoga amesema wataendelea kudhibiti biashara ya ubadilishaji fedha ili kuhakikisha sekta ya fedha haiyumbi nchini.

Amesema BoT ina akiba ya kutosha ya fedha za kigeni zinazoweza kutumika kwa kipindi cha miezi mitano.

Novemba mwaka huu, BoT ilifunga zaidi ya maduka 100 ya kubadilishia fedha mkoani Arusha yaliyoshindwa kukidhi masharti ikiwamo kutokuwa na leseni halali.

Akizungumzia suala hilo leo wakati wa kikao cha kazi kati ya Rais John Magufuli na Mamlaka ya Mapato (TRA) na wakuu wa mikoa, Profesa Luoga amesema BoT inachukua jitihada mbalimbali kuhakikisha sekta ya fedha inazidi kuimarika.

“Udhibiti utaendelea kuwa mkali. Hii ni moja ya hatua zitakazoendelea, kanuni ambazo zilikuwepo ziliongeza udanganyifu na maduka yakazidi kuongezeka kiholela,” amesema.

Amesema hakuna haja ya kuwa na maduka mengi ya kubadilishia fedha badala yake yatapatikana katika sehemu maalumu pekee ikiwamo hoteli za kitalii na benki.

“Hatuhitaji maduka 100 ya kubadilisha fedha Dar es Salaam, kwani kuna benki za kutosha. Tunahitaji maduka ya fedha kwenye sehemu muhimu kama kwenye mahoteli ya kitalii na mipakani,” amesema.

 Aidha, amewaonya wafanyabiashara wanaobeba fedha kwenye mabegi wanapoenda kulipia bidhaa nje ya nchi akisema kufanya hivyo ni kuvunja sheria.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala- Dar
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images