Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Okoa Ndoa Yako Mke,Mume Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Za Asili

$
0
0
Asilimia kubwa ya binadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wengi wamejaribu kutumia tiba sehemu tofauti bila mafanikio na  kukata tamaa hasa kina baba ambao ndoa zao au mahusiano yao na wapenzi wao yapo hatarini kuvunjika kwa sababu Mume hana uwezo wa kumridhisha mpenzi wake 

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MKE AU MPENZI WAKO SABABU ETI UNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME MDOGO: tumia dawa ya NSENWA POWER ;dawa hii hutibu na kuponesha tatizo la  nguvu za kiume .

1 itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 
2 itakupa uwezo kuchelewa kukojoa mda wa dakika 15-20 na kumfanya mpenzi wako naye aridhike 
3 huimalisha misuri iliyo legea na kusinyaa 

JE UNA UUME MFUPI NA MWEMBAMBA : tumia dawa ya MASHESHE NO 2; hii huboresha uume saizi upendayo kuazia urefu wa inch 5,6,7,8 na unene  wa sentumita 2,3,4,5, dawa hizi hazina madhara yeyote kwa mtumiaji hata wazee hutumia na kupona 

MASANZA ni dawa ya vidonda vya tumbo zipo dawa za mvuto wa biashara ,mpenzi,uzazi ngiri,korodani kuvimba miguu. mgongo,kiuno kuuma nk 

MAHALI ILIPO OFISI UNAWEZA UKASHUKIA BUGURUNI MALAPA AU BUGURUNI ROZANA na MWANZA YUPO WAKALA pia unaweza ukaletewa popote ulipo wasiliana nami 0783185060  0752348593 DR AGU

Ikulu yakanusha Rais Magufuli kutaka wanaume waoe wake wawili

$
0
0
Ikulu kupitia kwa Mkurugenzi wake wa Mawasiliano ya Rais, Gerson Msigwa, imekanusha na kuwataka wananchi kupuuza taarifa zinazosambaa katika mitandao ya kijamii zinazodai kuwa Rais Dk. John Magufuli amewataka wanaume nchini kuoa wanawake zaidi ya mmoja kutokana na wingi wao ili kupunguza vitendo vya ukahaba.

Kauli hiyo ya Ikulu imekuja baada ya taarifa zilizowekwa kwenye tovuti ya nipasheonline.com inayodaiwa kusajiliwa nchini Kenya na zaidi ikiwa haina uhusiano wowote na gazeti la Nipashe kusambaa kwa kasi na hivyo kuzua mjadala ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.

Taarifa hizo tayari zimeonekana kuishtua Ikulu ambapo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter, Msemaji huyo wa Rais Magufuli, Msigwa aliandika huku akiwa ameambatanisha na picha ya habari hiyo kuwa; “Ni uzushi  na uhalifu wa mtandao ,Mhe. Rais hajawahi kuzungumzia jambo hili mahali popote, puuzeni.”
Mtandao huo ulidai kuwa Rais Magufuli alitoa kauli hiyo katika mkutano wa wanaume 14,000 ambao walipokea mafunzo katika nyanja tofauti jijini Dar es Salaam.

Mtandao huo umeandika kuwa kuna idadi kubwa ya wanawake nchini na kulingana naye kuna wanawake milioni 40 na wanaume milioni 30.

“Siwalazimishi, lakini ninawashauri kuoa wake wawili au zaidi ili kupunguza idadi ya wanawake wasio na waume,” uliandika mtandao huo  na kudai kuwa ni kauli ya Dk. Magufuli.

Taarifa za mtandao huo ambazo zimesambaa maeneo mbalimbali ndani ya na nje ya bara la Afrika  zimeonekana kuibua mjadala mzito.

Mbunge wa Muleba Kusini, Profesa Anna Tibaijuka ni miongoni mwa walioibuka na kujadili suala hilo.

Mama Tibaijuka kupitia andiko lake alilolituma katika mitandao ya kijamii, licha ya kuonyesha wasiwasi kuhusu ukweli wa taarifa hiyo, alichambua kwa kutumia namba ambazo zilionyesha kuwa ni jambo lisilowezekana kwa wanaume wote wa Watanzania kuoa wake wawili kila mmoja.

“Nijuavyo mimi Mhe Rais wetu Magufuli ni mcheshi sana, huwa anapenda kutania, lakini wengine labda tunamiss  huo utani, sasa hizi habari eti kasema kuna uwezekano wa kila mwanaume Mtanzania kuoa wanawake wawili wawili eti kwa kuwa ni wengi kwa nini magazeti yetu kama (analitaja gazeti lililonukuliwa kudaiwa kuandika kauli hiyo) yanauchukulia literally kama ni kweli kasema hivyo?

“Niko Marekani, sijaona hiyo audio clip ya Rais, ila naona anakuwa quoted out of context, kiuhalisia  haiwezekani kuwa na wanawake wawili wawili, hakuna wanawake wengi namna hiyo kwa kuzaliwa ni hamsini kwa hamsini.

Tofauti ni ndogo, tunasema “it is not statistical significant”. Mungu anabalansi jinsia zote,” aliandika Profesa Tibaijuka.

Alisema katika sensa ya mwisho ni ya 2012 ilibaini kwamba  Tanzania ilikuwa na watu 44,928,923 ambapo kati ya hao wanaume walikuwa 21,869,990 na wanawake 23,058,933.

Alisema takwimu hizo zinaonyesha kuwa, ongezeko la watu kwa kila mwaka ni asilimia 2.7%. Kwa hiyo mwaka 2018 Tanzania inakadiriwa kuwa na wanaume 23,066,912 na wanawake 27,786,401. Jumla 50,853,314.

“Je, kuna wanawake wangapi kwa kila mwanaume kwa sasa? Unachukua milioni 27 unagawa kwa milioni 23 unapata 1.204…. kwa hiyo hakuna uwezekano wa kila mwanamume kuoa wake wawili wakatosha,” alisema Profesa Tibaijuka.

Alisisitiza kuwa, kwa maana hiyo, sera ya wake wawili wawili haitekelezeki, kwani hakuna wanawake wa kutosha na namba hazikubali.

Alisema taarifa  inayosambaa kwamba  wanawake wanaonekana ni wengi kuliko wanaume zinatokana na sababu za kijamii na kiuchumi.

Alisema wanaume wana hali ngumu zaidi kuliko wanawake kutokana na wengi wao wamefungwa, wamelowea wanatumia madawa ya kulevya, hawana kazi, wakati jamii ikiwataka wanawake kuolewa na mtu mwenye uwezo.

“Kwa hiyo ni wanaume wanasakamwa zaidi na tatizo la umaskini, wanaume wengi wanashindwa kumudu familia na kuzitunza, kwa hiyo ama hawaoi au wanatelekeza familia zao, kwa hiyo ukiangalia unakuta wanaume wapo, lakini wengi hawana uwezo wa kuoa, wazungu wanasema “eligible bachelors”, aliandika Profesa Tibaijuka.

Profesa Tibaijuka aliwataka watu wanaopenda kufahamu kuhusu utafiti huo wasome machapisho yake kwenye jarida maarufu la ‘Journal of World Development Vol 25 No 6’ lililochapishwa na Pergamon Press of the American University Juni 1997.

Alisema ndoa ya wake wengi haifai, kwakuwa itawatesa wanaume, wengine watakosa wake, pia itachochea umalaya badala ya kuupunguza.

Profesa Tibaijuka aliendelea kuhoji suala hilo kwakutolea mfano wa nchi ya China walipokuwa na sera ya mtoto mmoja mmoja.

“Kwa kuwa wanaume ndio wanapendwa wazazi wengine waliwaua watoto wa kike kusudi wapate wa kiume wanaopendelewa, kwa hiyo China kuna uhaba mkubwa wa wanawake hadi wanatekwa nyara hata wale walioolewa na kupelekwa vijijini,” aliandika Profesa Tibaijuka.

Alimaliza kwakushauri sera ya hamsini kwa hamsini  na mume mmoja.

Serikali Yatangaza ajira mpya 171

$
0
0
Watumishi wapya 513 wa kada mbalimbali za afya wameajiriwa na Serikali ili kujaza nafasi zilizoachwa na wenzao waliochaguliwa awali na kushindwa kuripoti kwenye vituo vya kazi walivyopangiwa.

Watumishi hao 513 ni kati ya watumishi 6,180 walioajiriwa na kupangiwa vituo vya kufanyia kazi ikiwa ni zahanati na vituo vya afya katika maeneo mbalimbali nchini.

Waziri wa Nchi, Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo amesema Oktoba 5, 2018 kuwa licha Serikali kutoa ajira hizo bado kuna kada ambazo zimekosa watu wenye sifa wa kuajiriwa na Serikali.

Amezitaja kada ambazo hazijapata watu wenye sifa wakati wa shughuli ya kuajiri ni pamoja na ile ya ofisa uuguzi msaidizi daraja la pili, ofisa muuguzi daraja la pili, daktari daraja la pili, tabibu daraja la pili, na tabibu msaidizi.

Waziri Jafo amezitaja kada nyingine zilizokosa watu wenye sifa ni pamoja na nafasi ya mteknolojia mionzi, mfamasia daraja la pili na mtoa tiba kwa vitendo.

Aidha, Serikali  imetangaza ajira mpya 171 za kada mbalimbali za sekta ya afya ambapo nafasi hizo zinapaswa kuombwa kuanzia Oktoba 5 2018 hadi  Oktoba 12 2018.

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Meya Boniface Jacob: Napenda Ukuu wa Mkoa, Lakini Siwezi Kuwasaliti Wananchi Wangu

$
0
0
Meya wa Manispaa ya Ubungo kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Boniface Jacob amesema anapenda nafasi ya Ukuu wa Mkoa na Ukuu wa wilaya ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) lakini hawezi kuhamia chama hicho kwa kile alichokidai atakuwa amewasaliti wananchi wake, wanaoishi mazingira magumu hasa kwenye halmashauri yake.

Meya Boniface Jacob amesema katika vitu ambavyo hatamani kuvisikia kwa mtu yeyote ni kwamba yeye binafsi ana  mipango ya kuhamia CCM na kusema kauli hiyo ni inalenga kumdhalilisha.

“Kwa mfano mimi nina maisha magumu napenda Ukuu wa Mkoa, Ukuu wa Wilaya shida ni kwamba nitafata vitu vizuri lakini sitakuwa na amani ya roho sababu nitawasiliti watanzania wenye maisha magumu, hicho ndio kinanifanya nisiwe upande wa CCM,” Amesema Meya wa Ubungo Boniface Jacob.

Kuhusiana na mapigano ya hivi karibuni yaliyotokea kwenye Uchaguzi wa Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala amesema tukio hilo limemkumbusha uchaguzi wa Naibu Meya wa Jiji ambapo Meya huyo wa Ubungo alishikana mashati na Meya wa Temeke Abdallah Chaulembo.

“Unajua wananchi wanapaswa kujua kuwa vyama vya upinzani huwa vinapata tabu sana kwenye uchaguzi hapa nchini lakini niwaambie hatutakata tama, tutaendelea kutetea haki zetu.” Ameongeza Meya wa Ubungo Boniface Jacob.

Mwigulu Nchemba Awazuia Wananchi Wake Kuuliza Milioni 50 Za Kila Kijiji

$
0
0
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi na Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka wananchi wa Jimbo lake kutoulizia Milioni 50 za kila kijiji ambazo ziliahidiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa Mbunge huyo Serikali imetoa milioni 800 kwa ajili ya kujenga hospitali za Tarafa katika baadhi ya kata kwenye jimbo hilo pamoja kupatiwa bilioni 2 kwa ajili utekelezaji miradi ambayo itawanufaisha wananchi wote.

Katika mkutano wake wa hadhara jimboni kwake, Mwigulu amesema; “nisikilizeni wana Iramba, Serikali imetupatia milioni 800 za kujenga hospitali za Tarafa Kinampanda na Ndago, tumepata zaidi ya bilioni 2 kujenga daraja tarafa ya Shelui, tumeshapata zaidi ya bilioni 2 kwa ajili ya maji.

"Hizi ni huduma za watu wote na hazikuwepo kwenye ilani, ni upendo na maono ya Rais. Tumshukuru mhe Rais wetu mpendwa badala ya kuulizauliza milioni 50. Na kwa Vikundi tutaendelea kuwapa asilimia kumi ya mapato ya ndani."

Wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kupitia ilani ya Chama Cha Mapinduzi aliahidi kutoa milioni 50 kwa kila kijiji kwa nchini kwa ajili ya maendeleo.

Waziri Mkuu Majaliwa Mgeni Rasmi Maonesho Ya SIDO Kitaifa Simiyu

$
0
0
Na Stella Kalinga, Simiyu
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Maonesho ya Kwanza ya Viwanda vidogo (SIDO)  ambayo Kitaifa yatafanyika mkoani SIMYU katika Viwanja vya nane nane Nyakabindi, kuanzia tarehe 23-28 Oktoba, 2018.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka  katika kikao cha maandalizi ya maonesho  hayo kilichowashirikisha baadhi ya viongozi wa mkoa wa Simiyu na mameneja wa Shirika la Viwanda vidogo (SIDO) kutoka mikoa ya Simiyu, Dodoma ,Mwanza, Kagera ,Mara, Shinyanga na Arusha.

Mtaka amewakaribisha wananchi wa mkoa mwenyeji Simiyu Watanzania wote kwa ujumla kuja kushiriki maonesho ya SIDO yatakayobebwa  na Kauli Mbiu “Pamoja Tujenge Viwanda Kufikia Uchumi wa Kati” na kubainisha kuwa mkoa wa Simiyu unaamini kuwa maonesho hayo yatakuwa ni maonesho darasa, mahali ambapo watu watajifunza na kufanya biashara.

Ameongeza kuwa maonesho ya SIDO yanabeba ajenda ya Serikali ya awamu ya tano na matamanio ya Mhe. Rais ya kuwa na Tanzania ya Viwanda na kuifikisha  nchi katika Uchumi wa Kati, hivyo akaawaalika wadau wote wenye teknolojia mbalimbali kushiriki maonesho haya.

“Ninawaalika wadau wote wenye teknolojia mbalimbali waweze kushiriki maonesho haya , nayaalika makampuni, taasisi na mashirika yenye vitu vinavyoweza kuwafaa wajasiriamali na Watanzania ambao wangehitaji kuwekeza kwenye viwanda, waweze kuleta teknolojia zao”

“Ninawaaalika Wajasiriamali wote kushiriki maonesho haya maana yatatoa nafasi kila mjasiriamali kujifunza kwa mwenzake, kupata elimu na kubadilisha ujuzi ili waweze kuzalisha bidhaa bora zaidi” alisema Mtaka

Aidha, ametumia mkutano huo kuzialika taasisi za fedha ili ziweze kujitangaza kwa wajasiriamali nao wakaona ni namna gani wanaweza kupata mitaji, huku akisisitiza na kuzialika taasisi za kitaaluma na vitivo vya uhandisivya Vyuo vikuu  pamoja na mashirika mbalimbali ya Kimatifa yanayofanya kazi hapa nchini.

Akizungumzia ada ya ushiriki Mtaka amesema wajasiriamali wenye mahitaji maalum watashiriki bure, wajasiriamali wadogo watashiriki bila kulipia gharama yoyote isipokuwa watalipa shilingi elfu kumi (10,000/=)  kwa ajili ya sare, wajasiriamali wa kati watachangia shilingi laki mbili (200,000/=) taasisi, makampuni na mashirika ambayo hayapo katika makundi la wajasiriamali wadogo , wa kati na wadhamni watatakiwa kuchangia shilingi milioni mbili (2000,000/=) kama ada ya ushiriki.

Kwa upande wa udhamini Mtaka amesema kuwa kwa taasisi, mashirika au kampuni zitakazo dhamini maonesho hayo,  kiwango cha juu kitakuwa shilingi milioni thelethini (30,000,000/=), kiwango cha kati shilingi milioni kumi  (10,000,000/= ) na kiwango cha chini kitakuwa milioni tano (5,000,000/=)  huku akisisitiza kuwa  wadhamini hawa watambuliwa kwa vyeti na watapewa kipaumbele cha mgeni rasmi kutembelea mabanda yao.

Jumla ya  wajasiriamali wadogo, wa kati na wakubwa 1000 wanatarajia kushiriki Maonesho haya ya Viwanda Vidogo SIDO Kitaifa pamoja na taasisi, mashirika na makampuni ya Umma na binafsi yatashiriki pia.

MWISHO

Waziri Mkuu: Serikali Haitalipa Madeni Yaliyokopwa Na Ushirika

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka  viongozi wa vyama vya ushirika nchini kutumia vizuri rasimali za vyama hivyo na kwamba Serikali haitalipa deni lolote lililokopwa na vyama hivyo. 

“Biashara ya kununua madeni yaliyokopwa na vyama vya ushirika haipo kwenye Serikali hii ya awamu ya tano, badala yake itawachukulia hatua wote waliohusika na ubadhilifu huo.”

Pia Waziri Mkuu amepiga marufuku wafanyabiashara kuwaibia wakulima kwa kununua kahawa mbichi ikiwa shambani maarufu kama butura.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Oktoba 6, 2018) wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na wafanyabiashara pamoja na wadau wa zao la kahawa baada ya kuwasili mjini Bukoba kwa ajili ya ziara ya kikazi mkoani Kagera.

Waziri Mkuu amesema Serikali itachukua hatua kali kwa viongozi wa vyama vya ushirika ambao si waaminifu na wabadhilifu wa mali za ushirika.”Tunahitaji wakulima wapate fedha.”

Amesema Serikali itahakikisha wafanyabiashara wote, hususani wa mazao ya kilimo wanakuwa na mfumo sahihi wa ununuzi wa mazao utakao ongeza tija kwao na kwa wakulima.

Amesema kwa sasa Serikali inataka kuondoa mfumo uliopo wa vyama vya ushirika kufanya biashara na badala yake jukumu hilo libakie kwa wafanyabiashara.

Kadhalika, Waziri Mkuu amewataka wafanyabiashara hao waihakikishie Serikali kwamba watanunua kahawa yote iliyopo kwa wakulima pamoja na kwenye vyama vya ushirika. Wafanyabiashara wameridhia kununua kahawa yote.

Awali, Waziri wa Kilimo Dkt. Charles Tizeba alisema katika msimu wa mwaka huu jumla ya kilo 3,000,464 za kahawa isiyokobolewa  na kilo 8,191,86 za kahawa safi bado hazijanunuliwa.

Dkt. Tizeba alisema kahawa iliyobakia katika maghala ya vyama vya ushirika ni kama ifuatavyo, chama cha KCU (1990) kina kilo 1,1513 za kahawa isiyokoborewa na kilo 1,936, 367 za kahawa safi.

Pia chama cha KDCU kina kilo 6,012,840 za kahawa safi, Ngara Farmers C.S Ltd kina kilo 592,354 za kahawa isiyokobolewa na kilo 192,660 za kahawa safi.

“Nkwenda AMCOS ina kilo 175,553 za kahawa maganda na kilo 50,000 za kahawa safi na Magata AMCOS kina kilo 433,634 za kahawa safi.”

Alisema vyama vya ushirika vinakabiliwa na changamoto ya kiwango kidogo cha kahawa kinachonunuliwa mnadani na wakati mwingine kutonunuliwa kabisa. Hali hii inatokana na kushuka kwa bei katika soko la dunia.

Alisema changamoto nyingine ni kuwepo kwa taarifa za upotoshaji kwa wakulima kutoka kwa walanguzi za kuzuia wakulima kukusanya kahawa yao kupitia Vyama vya Ushirika vya Msingi kwa wao  watanunua na kuwapatia bei nzuri.

IGP Sirro Kasema Hali ya Ulinzi na Usalama Nchini Imeimarika.....Kaongelea Pia Dhamana kwa Watuhumiwa

$
0
0
Na Ahmed Mahmoud Arusha
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Simon Sirro  amewashuru wananchi kwa ushirikiano uliopelekea matukio ya uhalifu nchini kupungua kwa kiasi kikubwa ikiwemo matukio ya matumizi ya silaha.

Akizungumza na vyombo vya habari Jijini hapa Siro amesema kuwa matukio mengi ya uhalifu hapa nchini yamepungua ambapo amewataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano utakaosaidia kuondoa uhalifu nchini.

Amesema kuwa Dhamana ipo kisheria na kila mmoja na haki ya kuipata hivyo inategemea na kosa ulilofanya ndio linepelekea kupewa dhamana tena kwa siku yoyote na muda wowote.

“Swala la dhamana lipo kwa mujibu wa sheria na dhamana inatolewa wakati wowote ila inategemea na makosa ya mtuhumiwa”alisema siro

Amesema Hali ya ulinzi na usalama hapa nchi kwa sasa ni shwari kuanzia hapa Arusha na mikoa mengine isipokuwa kwa kigoma wameongeza askari kuendelea kudhibiti matukio kwa kuwa mkoa huo ni miongoni mwa mikoa ya mipakani ina muingiliano.

Aidha amesema kuwa matukio ya mauaji ya mapenzi yamekuwachangamoto kubwa na yanalisumbua jeshi hilo hususani masuala ya ubakaji lazima tuwe wastaarabu kuepuka matukio yatakayopelekea mauaji na familia kuteseka.

“Suala la mauaji ya wapenzi kwa wapenzi ikiwemo kufumaniana limekuwa changamoto kwetu tumejipanga kuyashughulikia na kuwataka viongozi wa madhehebu ya dini kulishughulikia hilo lipo kwenye uwezo wao”alitanabisha Sirro

Amesema kuwa ushamba ndio unaopelekea mtu kumuua mpenzi wake hivyo kuifanya familia kuteseka na kuwasihi watanzania kuweza kuepuka matukio hayo kwa kuwa wastaarabu na kuvumiliana.

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 01

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
Mama kwa haraka akaniziba mdomo wangu huku tukiwa tumejibanza kwenye migomba mingi sana, iliyopo karibu kwenye kijumba chetu cha udongo huku tukimshuhudia baba akipigwa kipigo na watu walio valia mavazi meusi huku wakiwa wamezificha sura zao kwa vitambaa. Baridi kali na  mvua kubwa inayo endelea kunyesha katika eneo hili la kijiji chetu cha Umbwe hapa Moshi, ikamfanya mama azidi kunikumbatia huku akilia kwa sauti ya chini chini sana. Machozi na hasira zikazidi kunitawala, ila sina uwezo wa kufanya kitu chochote nikiwa bado ni mtoto mdogo mwenye umri wa miaka sita.
 
“Wewe si unajifanya mjanja kuwashawishi wakulima wezako kukataa mimi kuwekeza kwenye hichi kijiji si ndio?”
Sauti ya mwanaume aliye zungukwa na watu hawa wanao endelea kumtesa baba ilisikika vizuri, japo mama alijitahidi kuniziba macho yangu nisishuhudie kitendo hicho anacho fanyiwa baba yangu, ila nikazidi kujitahidi kuangalia ila mama aliigeuza sura yangu pembeni na nikaendelea kunikumbatia. Niliendelea kusikia miguno ya baba yangu na kilio chake cha maumivu. 
 
“Sasa utakufa kama shujaa mpuuzi, mpigeni hadi afe na mwili wake mkautupe shambani kwake”
Sauti ya mwaunaume huyo ilitoa maagizo hayo na kuwafanya watu hao kuendelea kumpiga baba kwa magongo mazito. Kwa bahati mbaya ikapiga radi mwanga wake ukaangaza kila eneo hili.
“Kuna watu kule kwenye migomba”
Kijana mmoja alizungumza huku akinyoosha mkono wake kwenye eneo hili  tulilo jificha na mama. Kwa haraka mama akanishika mkono wangu wa kulia na hapakuwa na budi tena zaidi ya kuanza kukimbia.
 
“Lole kimbia”
Mama alizungumza huku akiniachia mkono na kuanza kuchechemea.
“Ndefo mama”(Mama twende)
Nilizungumza kwa lugha ya kichaga huku nikijaribu kumshika mkono mama ila mama kwa ishara akaniomba nikimbie kwani watu hao wanazidi kutukaribia. Machozi ya yakazidi kunimwagika usoni mwangu, kwani sina uwezo wa kupambana na wanaume hawa na wala sina uwezo wa kumtetea mama yangu. Mama kwa ishara ya mkono akazidi kunisisitizia niweze kukimbia ili kuyaokoa maisha yangu.
 
    Nikakimbia kwenye hii migomba mingi, huku nyuma nikaanza kusikia sauti ya mama yangu akipiga mayowe ya kuomba msaada. Ila mvua na mingurumo hii ya radi na umbali  tulipo  kutoka jirani mmoja hadi mwengine ni swala ambalo ni gumu sana kusikika. Kila nilipo jaribu kusonga mbele, nikajikuta nikisita kabisa kuendelea na safari hii. Nikaangaza angaza chini na kuona fimbo, nikaichukua na kuanza kurudi eneo nilipo muacha mama yangu huku machozi yakinimwagika usoni mwangu na hasira ikiwa imejaa kifuani mwangu.
Nikafika katika eneo ambalo yupo mama yangu, nikawakuta vijana hawa sita wakimbaka kwa nguvu, jambo lillo nifanya nianza kumchapa mmoja wao.
“Ametokea wapi huyo mtoto”
Kijana mmoja ambaye ndio yupo katikati ya mapaja ya mama alizungumza huku akiwa amevua kitambaa kilicho kuwa kimeiziba sura yake.
 
“Mpigeni”
“Mkuu ila huyu ni mtoto”
“Mtoto mpigeni na mumuue”
“Ja….ma…..ni….musi….mp……”
Mama alizungumza kwa shida sana kwani amepigwa kipigo kizito sana na kubwa juu.
“Muondoeni hapa”
Kijana huyo anaye endelea kumuingilia mama kinguvu alizungumza na vijana wake wawili wakanishika na kunibebe juu juu. Nikajitahidi kwa nguvu zangu zote ili mradi niweze kujitoa mikononi mwao na kwenda kumsaidia mama ila utoto wangu na kuto kuwa na nguvu, ukawafanya vijana hawa kunihimili. Vijana hawa wakaendelea kunibeba huku wakinitandika magofi mazito pamoja na ngumi katika kila sehemu ya mwili wangu. 
 
“Tumuue”
Kijana mmoja  alizungumza  kwa ukali huku wakinibwaga chini kama mzigo wa kuni.
“Hapana huyu ni mtoto mdogo sana, hatuna haja ya kumuua”
“Tumepewa agizo na mkuu?”
“Ni bora tumtupe huko kwenye korongo, akafie mtoni”
Niliweza kuyasikia mazungumzo ya vijana hawa vizuri sana, ila uwezo wa kusimama sina kwa maana wamenipiga sana ngumi na makofi kana kwamba wana mpiga mtu mzima mwenzao. Wakanisukumia bondeni kwenye korongo kubwa na nikaanza kumbingirika huku nikipia kelele za kuomba msaada, ila galfa nikahisi kishindo kikubwa kichwani mwangu na taratibu macho yangu yakapoteza uwezo wa kuona na sikujua ni nini kinacho endelea.
                                                                                                                         ***
    Nikaanza kusikia sauti ya watu wawili wakizungumza huku mmoja akiwa ni mwanamke. Sauti ninazisikia ila kile wanacho kizungumza kwangu ndio mtihani kabisa kwani ni lugha ambayo siifahamu. Nikafumbua macho yangua, taratibu ila ukungu mwingi ulio yatawala macho yangu ukanifanya nisiweze kuona watu hao.
 
“Heii boy”
Niliisikia sauti ya kike ikizungumza pembeni yangu.
“Ameamka”
“Unajisikiaje kijana?”
Watu hawa waliendelea kuniuliza maswali ambayo sikuweza kuyajibu kwa maana siwaoni vizuri.
“Unaweza kuzungumza?”
Mwanamke aliniuliza kwa sauti ya upole.
“Tumuache apumzike kwa muda ndio tumulize maswali”
“Ila ni kijana mzuri sana”
“Yaa sijui ni kwa nini waswahili wanawanyanyasa watoto hivi”
Nikajaribu kumtazama mwanaume huyu, taratibu nikaanza kuiona sura yake, ni mzee wa kizungu mwenye mvi nyingi sana kichwani mwake. Nikamtazama mwanamke aliye simama pembeni ya mzee huyu, naye ni bibi wa kizungu, ila hajazeeka sana kama huyu mzee.
 
“Mtengenezee supu nzuri ya kuku”
Mzee huyu alizungumza, bibi huyo akambusu mumewe shavuni kisha wakatoka ndani hapa. Mzee huyu akavuta stuli na kukaa pembeni ya hichi kitanda. Akaanza kunishika shika mguu wangu wa kushoto, taratibu nikautazama mguu wangu na kujiona nikiwa nimefungwa bandeji kwenye mguu mzima. Nikaanza kulia, kwa maumivu niliyo anza kuyahisi mara tu ya kuuona mguu wangu.
“Hapana kijana usilie”
“Nipo wapi…...?”
Niliendelea kulia huku nikijitahidi kukaa kitandanii. Mzee huyu akajitahidi na kunirudisha na kulala. Maumivu ya kichwa nayo yakazidi kunichanganya. Mzee huyu akachukua moja ya bomba la sindano lenye dawa na kunichoma mkononi mwangu. Taratibu  nikaanza kuhisi usingizi ulio nifanya nilale fofofo ndani ya muda mchache tu.
                                                                                                                       ***
    Baada ya siku mbili nikapata nafuu kidogo hata ya kuka mwenyewe kitandani, mzee Klopp na mke wake Bi Jane Klopp, kama walivyo jitambuisha jana, wakaniomba waweze kuzungumza na mimi. Kwa haraka haraka katika kipindi hichi cha siku hizi mbili nilizo kaa nao wamekuwa ni watu wa kunijali kwa kila jambo. Muda wao mwingi wanautumia katika kunitazama na kujua hali yangu inaendeleaje.
“Unaitwa nani?”   
Bi Jane Klopp aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.
“Eheee?”
“Unaitwa nani?”
Nikajaribu kukumbuka jina langu, ila nikajikuta nikishindwa kulikumbuka kabisa.
“Je unajua ni nini kimekukuta?”
Bi Jane Klopp aliendelea kuniuliza kwa upole, ila nikashindwa kabisa kufahamu ni kitu gania mbacho kimenipata.
“Hapana, kwani nipo wapi?”
Niliuliza kwa suati ya upole na unyonge.
“Upo Arusha mjini”
“Nimefikaje fikaje?”
Bibi Jane Klop wakatazamana na mume wake huku wakionekana kujawa na mshangao sana.
 
“Okay, siku chache zilizo pita tulikuwa Moshi, kwenye matembezi yetu ya kufanya uchunguzi ulio tuleta huku nchini Tanzania, kwa bahati nzuri tuliweza kukuta kwenye moja ya mto ukiwa umepoteza fahamu, ilikuwa ni alfajiri sana.”
 Mzee Klop alizungumza kwa upole huku akinitazama usoni mwangu.
“Tulipo kuchunguza vizuri tukagundua kwamba upo hai, tukaona sio mbaya tukakusaidia kwa maana bado ni mtoto mdogo sana”
“Asanteni”
“Usijali, ni jukumu letu. Je unakumbuka kama una ndugu, au marafiki ambao tunaweza kuwasiliana nao wakaja kukuchukua hapa?”
 
Nikatingisha kichwa huku nikijitahidi kuvuta japo taswira ya mtu yoyote ninaye mfahamu kwenye maisha yangu ila sikuweza kukumbuka. Kitu kilichopo hapa kichwani mwangu ni hawa wazee wawili mbele yangu.
“Kutokana hapa Tanzania tumebakisha muda mchache wa kukaa, basi tutafanya mpango wa kuondoka na wewe na kurudi nchini Ujerumani yalipo makazi yetu sawa”
“Sawa”
“Na kuanzia leo utaitwa Ethan Klopp, hilo ndio litakuwa ni jina lako”
“Ethan Klopp?”
“Ndio hilo ndio jina lako kuanzi hii leo”
Nikatabasamu kidogo kwani ni jina zuri kwa upande wangu na wala sioni sababu ya kukataa kulikataa kwa maana jina langu halisi silifahamu.
“Na sisi tutakuwa ni wazazi wako, kwa maana tuna binti yetu mmoja tu yupo nchini Ujerumani, na wewe utakuwa ni mtoto wetu wa pili sasa”
“Ninashukuru sana”
Nikajikuta furaha ikinitawala moyoni mwangu. Taratibu bibi Jane Klopp akanikumbatia kwa nguvu, huku akitawaliwa na furaha. 
 
     Siku zikazidi kusonga mbele huku hali yangu ikizidi kuimarika, matibabu anayo nipatia bibi Jane Klopp na mume wake yananifanya nizidi kuwa imara. Wakaanza kunifundisha vitu vingi, na wakazidi kushangazwa na uwezo wangu wa akili kwani katika kipindi cha muda mchache kila wanacho nifundisha basi ninakielewa kwa haraka na ni vigumu sana kuweza kukisahau. Wakaanza kunifundisha Kijerumani, japo ni lugha ngumu kidogo ila nikajitahidi hivyo hivyo ndani ya mwezi mzima nikawa tayari nipo vizuri kwenye lugha hiyo na hawa wakiniongelesha ninaweza kuwaelewa na kuwajibu kiufasaha.
“Ethan unajua wewe ni genius?”
Bibi Jane Ethan aliniambia tukiwa jikoni nikimsaidia kuandaa chakula cha usiku.
 
“Genius ndio nini?”
“Ni mtu mwenye upeo mkubwa wa kiakili, tofauti na watu wengine”
“Mtu akiwa hivyo ndio anaitwa Genius?”
“Ndio, ninakuahidi, nitahakikisha kwamba tunakupatia elimu bora unakuwa mtu bora kabisa hapa duniani”
“Nashukuru sana mama”
Bibi Ethan kama kawaida yake akainama kidogo na kunibusu kwenye paji langu la uso ikiwa ni ishara ya upendo ambao amenizoesha kuanzia siku ya kwanza kuanza kuishi nao.
“Ukiwa mkubwa Ethan unapenda kuwa nani?”
“Mmmmmm……nahitaji kuwa na nguvu?”
“Hahaaa…..hata hapo mbona una nguvu. Au unataka kuwa na nguvu ya kisiasa, kiuchumi au ushawishi katika jamii?”
“Yoyote tu ila nahitaji kuwa na nguvu tu”
“Hupendi kuwa dokta, au rubani?”
“Mmmmmmhhhh”
 
“Kweli?”
“Ndio mama”
“Basi kama nitaendelea kupewa maisha marefu basi nitahakikisha kwamba unakuwa na nguvu mwanangu”
“Nashukuru sana mama”
Tukaendelea kuandaa chakula hichi cha usiku, hatukuchukua muda mrefu sana tukafanikiwa kumaliza kupika, nikasaidana na bibi Klopp kutenga chakula mezani, baada ya maandalizi hayo yote kunalizika nikaelekea chumbani kumuita baba ambaye ni mzee Klopp.
“Ohooo nina kuja sasa hivi?”
“Sawa baba”
Nikaanza kuelekea mlangoni, ila kabla sijafika mlangoni akaniita, nikageuka na kumtazama, kwa ishara ya mkono akaniita na nikafika hadi kwenye kiti alicho kaa huku akiwa ana andika andika vitu kwenye kipakato chake(laptop)
“Kuna shule za primary, nilikuwa ninazitafuta hapa, nahitaji tukirudi Ujerumani uende ukasome, je ni ipi kati ya hizi mbili ni ipi hapa unaipenda?”
 
Mzee Klop alinonyesha majengo makubwa mawili ya shule zilizopo kwenye nchi ya Ujerumani ambapo kila siku nina tamani siku zao za kuishi hapa nchini Tanzania ziishe ili nirudi nao Ujerumani.
“Hii hapa”
Nilizungumza huku nikimuonyesha jengo moja zuri.
“Umeipenda hii?”
“Ndio baba”
“Sawa, tena hizi ni shule za watoto wenye uelewa maalumu. Tumeweza kugundua kwamba una uwezo huo”
“Nashukuru baba”
Unyenyekevu na utii ndio ngao yangu kubwa sana ya kuendelea kuishi na wazee hawa, malengo yangu na nia yangu ni kuhakisha kwamba nina pata nguvu kubwa kwenye maisha yangu, na nilazima yatime pale tu nitakapo kuwa mtu mzima. Tukatoka kwa pamoja humu chumbani na kurudi sebleni, tukapata chakula cha usiku kwa pamoja kisha tukasali ibada ya usiku kama ilivyo kuwa desturi waliyo jiwekea.  Baada ya sala wao wakaelekea chumbani kwao na mimi nikaelekea chumbani kwangu na kulala.
 
    Baada ya siku wiki  tatu, kuisha, siku ya kuondoka nchi Tanzania ikawadia, kila hatua zote za kiserikali za kuondoka na mimi nchini humu walizikamilisha, japo sifahamu sana kuhusiana na mambo hayo. Tukapanda ndege ya shirika la Fast Jet hadi jijini Dar es Saalam ikiwa ndio mara yangu ya kwanza kufika katika jiji hili ambalo nilikuwa nikilisikia sikia tu kipindi cha nyuma kwamba ndio jiji zuri sana hapa nchini Tanzania.
 
‘Lazima nitawale hili jiji siku’
Nilijikuta nikila kiapo moyoni mwangu huku nikitazama magorofa marefu, tukiwa njiani tunaelekea katika hoteli ya karibu ili kupumzika kwa muda ili kesho asubuhi na mapema tuweze kuondoka na ndege kuelekea nchini Ujerumani. Tukafika hotelini, mzee Klopp na mkewe wakachukua chumba kimoja, huku na mimi wakinipangishia chumba changu. Baada ya kupata chakula cha usiku, tukaelelea katika vyumba vyetu ili kupumzika ili kesho alfajiri na mapema tuwe tumewasili katika uwanja wa ndege.  Shauku na hamu ya kwanza ya kupanda ndege, nimesha imaliza kwa kupanda ndege kutoka Moshi hadi jijini hapa Dar es Salaam. Shauku  yangu ya pili ni kwenda nchini Ujerumani kuishi kabisa. Uzuri wa mataa katika magorofa mengi ninayo yaona kwa mbali, ukanifanya muda wangu mwingi sana niutumie nikiwa nimesimama dirishani hapa nikishangaa taa hizi.
 
‘Nilazima uwe na nguvu ya kuawala hili jiji’
Niliisikia  sauti nzito akilini mwangu iliyo nistua kidogo na kunipa wasiwasi. Damu mwili mzima ikaanza kunisisimka na vinyweleo vyangu vikaanza kusimama. Mapazia yaliyopo pembeni yangu hapa dirishani yakaanza kupepea, jambo lililo zidi  kunifanya niwe na wasiwasi kwa maana madirisha ni ya vioo na yote yamefungwa vizuri sana na hakuna nafasi ya upepo kuweza kuingia na kuyafanya mapazia haya kutikisika.
 
‘Ethan…..Ethan…….Ethan……’
Niliisikia sauti ya kiume ikiniita kwa mbali, nikajaribu kuangaza macho yangu ndani ya chumba hichi ili niweze kuona ni nani anaye niita ndani ya hichi chumba ila sikuweza kuona zaidi ya mapazia kuendelea kutingishika sana. Woga ukanijaa, mwili mzima ukazidi kunitetemeka.
 
“ETHAN……..”
Sauti hii nzito nikaisikia vizuri kwenye masikio yangu, taa zote ndani ya chumba hichi zikazima na nikaona kivuli cha mtu chenye mwanga hafifu sana kikiwa kimesimama kwenye moja ya ukuta wa humu chumbani huku kivuli hicho kikionesha mtu huyo akiwa amevaa joho kubwa sana, ila haonekani kichwa ni kipi wala miguu ni ipi jambo lilo nifanya niaguke chini mzima mzima huku nikitamani kupiga kelele ila sauti yangu haikuweza kutoka.
                                                                                                       ITAENDELEA  KESHO

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya October 7

Video Mpya: Maua Sama X Hanstone - Iokote

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Maua Sama anakukaribisha kutazama video ya wimbo wake mpya uitwao Iokote ambao amemshirikisha Hanstone. Itazame hapa.

VideoMPYA: Vanessa Mdee akiimbia Kihindi ( Vaishnav Jan To for Ghandi Jayanati )

$
0
0
VideoMPYA: Vanessa Mdee akiimbia Kihindi ( Vaishnav Jan To for Ghandi Jayanati )

Video Mpya: Lava Lava - GO Gaga

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Lava Lava ameachia video ya wimbo wake mpya uitwao GO Gaga. Itazame hapa.

Nandy afunguka kuhusu kolabo na Ruby

$
0
0
Muimbaji Nandy amejibu iwapo itatokea kolabo kati yake na Ruby. Nandy ambaye anatamba na ngoma inayokwenda kwa jina la Aibu amesema bado wao kama wasanii na menejimenti zao hazijawahi kukaa kujadili hilo.

"No hatujawahi, labda time itafika, unajua yupo bize na shughuli zake za muziki unajua hata kama ni ngoma lazima zianze kufikiria menejimenti ili waweze kutukutanisha tupange naamini ipo siku tutakuja kufanya," Nandy ameiambia The Playlist ya Times FM.

Ni mara kadhaa imekuwa ikidai kuwa wawili hao hawapatani lakini kile kinachoonekana hakuna kitu kama hicho kwani Ruby amekuwa akiimba nyimbo za Nandy mara kadhaa.

Alichojibu Nyandu Tozzy kuhusu kolabo na Harmonize

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Nyandu Tozzy amefunguka kuhusu mipango ya kufanya kolabo na Harmonize.

Nyandu Tozzy ambaye anafanya vizuri na wimbo mpya 'I don't care' amesema kuwa kutokana na ukaribu wao lolote linaweza kutokea lakini bado hawajakaa na kuzungumzia hilo.

"Unajua kwanza naweze kusema mimi na Harmonize ni wana ambao hatuwezi kukaa wiki mbili hatujawasiliana, so naweza kusema ni mdogo wangu kwenye huu muziki. Hivyo usishangae chochote kikatoka baina yangu mimi na yeye," Nyandu ameiambia The Playlist ya Times FM.

Nyandu Tozzy amekuwa akitumbuiza kwenye show kadhaa ambazo Harmonize amekuwa akiziandaa ikiwemo ile aliyofanya Dar Live mwaka huu.

Hamissa Mobetto: Diamond Anapendwa na Wanawake Wengi, Kuwa Naye Ni Kama Vita Vile!

$
0
0
Mwanamitindo Hamisa Mobetto amesema kuwa kwenye mahusiano na Diamond Platnumz ni moja ya vitu vigumu sana.

Mrembo huyo ameeleza kuwa hilo linatokana na muimbaji huyo kupendwa na wanawanake wengi, hivyo muda mwimgine inakuwa kama vita.

"Yaani ukiwa na yule mtu inakuwa kama vita, anapendwa na watu wengi, ana ma-EX wengi kwa hiyo unajikuta inaingia katika ugomvi, migogoro ambayo haukupaswa uingie," Hamisa ameiambia The Playlist ya Times FM.

Utakumbuka kuwa Hamisa Mobetto na Diamond Platnumz waliwahi kuwa kwenye mahusiano ambayo waliyafanya kuwa siri zaidi na kujaliwa kupata mtoto mmoja.

Video Mpya: Nay wa Mitego: Alisema ( Mwalimu Nyerere Alisema, Vijana Wote Tuamke)

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Nay wa Mitego ameachia video ya wimbo wake mpya uitwao Alisema. Itazame hapa.

Waziri Mkuu: Viwanda Vimepunguza Tatizo La Ajira Kwa Vijana

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema changamoto ya upatikanaji wa ajira hususani kwa vijana imeanza kupungua nchini baada ya viwanda vingi kuanza kufanya kazi.

Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imedhamiria kukuza uchumi kutoka wa chini hadi wa kati kupitia sekta ya viwanda ifikapo mwaka 2025.

Aliyasema hayo jana jioni (Jumamosi, Oktoba 6, 2018) alipotembelea kiwanda cha kukoboa kahawa cha BUKOP na cha kusindika kahawa cha Tanica, mjini Bukoba.

Alisema kwa sasa tabia ya vijana wengi kukaa vijiweni imepungua kwenye maeneo mengi nchini baada ya wengi kuajiriwa katika viwanda mbalimbali vilivyoanzishwa na kufufuliwa.

Waziri Mkuu alisema viwanda vimekuwa vikitoa ajira nyingi kwa wananchi, ambapo alitolea mfano kiwanda kimoja cha Tanika kilichoajiri watumishi 800.

“Nyie mlioajiriwa kiwandani hapa hakikishe mnafanya kazi kwa bidii, weledi, uaminifu na uadilifu wa hali ya juu ili kukiwezesha kiwanda kuendelea na uzalishaji,” alisisitiza.

Waziri Mkuu ambaye yuko mkoani Kagera kwa ziara ya siku nne, inayolenga kufuatilia maendeleo ya viwanda na zao la kahawa, ambalo ni kati ya mazao makuu sita ya biashara.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alimuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba  Bw. Bernad Limbe kuhakikisha anatafuta eneo kwa ajili ya wafanyabiashara ndogondogo.

Aliyasema hayo baada ya kupata malalamiko kutoka kwa wananchi waliokuwa wakifanya biashara katika eneo bandari na kuondolewa bila ya kupewa eneo lingine.

Waziri Mkuu alisema ni marufuku kuwaondoa wananchi katika maeneo yao ya kufanyia biashara bila ya kuwaonesha eneo lingine  ambalo watalitumia kwa aliji ya kufanyia biashara zao.

Awali, Meneja Mkuu wa kiwanda hicho, Bw. Linus Leopord alisema kwa mwaka wanazalisha tani 600 za kahawa iliyokaangwa na kusagwa, ambayo inatosheleza kwa mahitaji ya soko.

Pia kiwanda cha kahawa cha Tanica kinauwezo wa kuzalisha kahawa ya unga tani 500 kwa mwaka ila kutokana na uchakavu wa miungombinu kinazalisha tani 300 kwa mwaka.

Kuhusu masoko Bw. Leopord alisema kwa sasa mauzo yameongezeka, wanauza tani 50 ya kahawa iliyokaangwa na kusagwa kwa mwezi, ambapo awali walikuwa wanauza tani 32.

Kadhalika, Meneja huyo alisema wameimarisha na kuongeza soko la nje ambapo kwa sasa wanauza tani 35 za kahawa ya unga kwa mwezi, awali walikuwa wanauza tani 20.

Alisema kiwanda cha Tanika kinamilikiwa na chama cha ushirika cha KCU (53.37 %), KDCU (31.8%), Hazina (7.67), TFC (6.22%) na wafanyakazi wa Tanica (0.92%).

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images