Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

RC Makonda Ammwagia Sifa Diamond....Amruhusu Kukata Mauno, Amshauri asioe kwanza

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Saalam,  Paul Makonda amesema amempa ridhaa ya kutokuoa msanii Diamond na kumtaka aendelee kuwa ‘sukari ya mioyo ya watu’ sambamba na kuweka video za kukata mauno mtandaoni kutokana na alichokifanya kwa wakazi wa Tandale.

Makonda ambaye ni mlezi wa Kampuni ya WCB inayomilikiwa na Diamond amesema kwa kazi anayofanya huenda akioa mapema itamletea shida na kwamba anahitaji muda zaidi wa kufikiria kuwasaidia Watanzania wenzake.
 
 “Haya mambo mkiyajua vizuri bana kwanza ukiwa msanii halafu mashabiki wako wengi wakiwa wanawake ukioa wanaweza kukimbia, utafikiri ungewaoa wote,” Amesema

Makonda amewataka wasanii wote kuiga mfano wa Diamond wa kurudi na kusaidia jamii iliyowalea.

“Kwa alichokifanya Diamond hata nikiona video yake anakata mauno wala simfanyi, kitu Ila msanii hujafanya chochote halafu unasherehekea siku yako kwa kujirekodi video unakata mauno nakuweka ndani,” amesema.

Birthday ya DIAMOND: Nasaha Nzito ya Jacqueline Mengi Tandale

0
0
Aliyewahi kuwa Miss Tanzania Jacqueline Mengi ametoa somo kwa kinamama wanaohitaji mitaji kibiashara  kuthamini mitaji midogo ili kufikia mafanikio kibiashara.

Akizungumza leo Oktoba 5,2018 katika viwanja vya Maguniani Tandale jijini Dar es Salaam katika sherehe ya kuzaliwa Diamond, Jacqueline amesema wanawake wanapaswa kuwa na malengo ili kufanikisha ndoto zao kibiashara.

“Hakuna kitu muhimu kama kuwa na malengo, mkipewa mtaji msije kufika nyumbani na kwenda kupika uji, hizo fedha za mtaji hamtakiwi kuzila msisahau kina baba watawaambia zileteni msitoe.”

“Nawategemea mtakaopata mitaji leo mwakani tukirudi mtakuwa watu wakubwa, vijana cha kwanza ni kujiamini kwamba mnaweza kama Diamond japokuwa anawazidi lakini kijana ukijitambua unaweza kufanya jambo jiamini kwani ndiyo njia ya mafanikio,” amesema Jacqueline ambaye ni mke wa Mwenyekiti wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi

Manara Aibuka Sherehe ya Kuzaliwa Diamond na Kuahidi Kusomesha Walemavu Tandale, Kuanzisha Ligi ya Diamond

0
0
Msemaji wa klabu ya Simba, Haji Manara leo aliamua kuingiza siasa baada ya kuibuka  kwenye sherehe ya kuzaliwa kwa mwanamuziki Diamond.

Haji Manara aliufananisha umati uliofika kumuona nyota huyo na wapiga kura kwa kusema Diamond angepita bila kupingwa iwapo angegombea nafasi yoyote ya ubunge.

“Kama Diamond angetaka kufanya siasa hizi zote kura zake nawaambia, nimejaribu kumuuliza kuhusu hilo lakini mwenyewe amesema hataki kufanya siasa hivyo wanasiasa mtulize roho zenu,” amesema Manara.

Mara baada ya kusema hayo shangwe ziliibuka uwanjani hapo na baadaye Manara alizungumza tena na baadaye alitoa mipira kwa shule za Tandale.

Amesema ili watoto wakue vizuri ni muhimu wapate muda wa kucheza hivyo anatoa mipira hiyo ili kuhakikisha wanashiriki michezo.

Amesema katika kumuunga mkono Diamond amezungumza na wadau ambao wamekubali kuweka ligi Tandale itakayofahamika kwa jina la ‘Diamond Tandale Super Cup.’

Manara ametangaza kugharamia ada za wanafunzi wote walemavu watakaoanza shule Januari mwakani.

“Wanafunzi walemavu wote watakaoanza mwakani nitalipa ada kuanzia msingi hadi sekondari ili mradi iwe shule za serikali,” amesema Manara huku akishangiliwa.

Basata yampongeza Diamond Kwa Kutoa Msaada Tandale

0
0
Baraza la Taifa la Sanaa (Basata) limempongeza msanii Diamond kwa kuwasaidia watu wa eneo lake la Tandale jijini Dar es Salaam.

Hayo yamesemwa leo Oktoba 5, 2018 na Katibu Mtendaji wa Basata, Godfrey Mngereza katika sherehe za kuzaliwa msanii huyo zinazofanyika viwanja vya Maguniani Tandale.

Amesema ni nadra kwa watu waliofanikiwa kukumbuka walikotoka kitendo cha kuwasaidia wana Tandale kimeonyesha utofauti wake.

Katibu Mtendaji huyo ametoa pongezi hizo za aina yake kwani alipopanda jukwaani alianza kwa kuchana mistari ya kumpongeza Diamond.

BREAKING: Rais Magufuli Kateua Mwenyekiti wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA).

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli leo ametangaza kumteua Habbi Gunze kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA).

Uteuzi wa Gunze umeanza rasmi October 1 2018, hivyo kwa sasa Baraza la Sanaa la Taifa, limeongezewa nguvu ambapo mwenyekiti mpya ataenda kushirikiana na Katibu mtendaji wa Baraza hilo Geofrey Mungereza kuleta maendeleo katika sanaa.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi Ya October 6

Mambo 6 ya kuzingatia unapofanya kazi na bosi uliyemzidi umri

0
0
Katika kizazi cha wafanyakazi mchanganyiko katika ajira, makampuni huamua kuajiri au kupandisha vyeo wafanyakazi wenye ujuzi na uwezo mzuri kikazi kuwa wasimamizi wakuu. 

Hii hupelekea kuwe na uwezekano wa wewe kuwa na Bosi uliyemzidi umri na huenda usifurahie kwa sababu ya umri wa bosi wako. 

Tafiti unaonyesha kwamba wafanyakazi katika makampuni yenye mabosi wenye umri mdogo kuliko wao huwa na hisia hasi ikilinganishwa na wale walio na mabosi waliowazidi umri.

Ikiwa wewe na meneja wako mnaheshimiana, kufanya kazi pamoja haipaswi kuwa tatizo. Hata ikiwa umemzidi umri. Ni muhimu zaidi kuzingatia ukuaji wa kazi yako kuliko kuhangaika juu ya umri mdogo wa bosi wako. 

Hivi ni vidokezo unavyopaswa kufikiria ili kufurahia kufanya kazi na meneja uliyemzidi umri.

    Waheshimu Inavyostahili
Bosi wako anaweza kuwa na umri mdogo kuliko wewe, lakini si kwamba hana uwezo unaotakiwa. Ni muhimu kusikiliza na kuheshimu maamuzi yake. 

Hata hivyo, mambo ambayo utafanya ili kuonyesha heshima kwa bosi aliyekuzidi umri hayana tofauti na kwa bosi mwenye umri mdogo kwako. Kubali kuwa yeye ni mtu sahihi kufanya kazi hioyo na daima kuwa muwazi kwa mawazo anayoleta na kukubali kwa mtazamo chanya. Ikiwa unaonyesha heshima kwa bosi wako, ni wazi kabisa kuwa utaipata ya kwake kwa urahisi pia.

2. Uzoefu Wako ni wa Muhimu
Uzoefu wako wa kazi ndani ya kampuni ni moja ya zana muhimu sana ambazo unaweza kutumia katika kuimarisha uzalishaji na ufanisi wa shirika. 

Unaweza kutumia hii kumsaidia bosi wako mdogo kukuza ujuzi wake katika kuongoza timu na kusaidia kampuni kukua. Bosi wako anaweza kuwa na ujuzi katika eneo fulani kama vile teknolojia lakini hajui mengi kuhusu mawasiliano. Unapaswa kuwa tayari kumfundisha ujuzi uliyopata kwa miaka mingi na atatambua mchango wako kwa kampuni kirahisi zaidi kwa ukuaji bora wa kazi yako baadaye.

    Kubali Kubadilika na Kujifunza Mambo Mapya

    Usifikirie sana Kuhusu Hilo
Maamuzi uliyofanya katika kazi zako ndio yamekusaidia uwe katika nafasi yako ya sasa. Uko katika nafasi hii kwa sababu ya kazi yako na kwamba unapaswa kujivunia. Hutakiwi kufikiri kwamba timu ya uongozi inakuona kuwa duni zaidi kwa sababu walitoa jukumu la ubosi kwa mtu mwingine aliye mdogo kuliko wewe. 

Kuwa na ujasiri kukubaliana na ukweli kwamba walikuajiri ili kuleta thamani maalum kwa timu. Hakikisha unajaribu kufanya kazi na bosi wako mdogo na kujitoa kwa kila ulicho nacho kufanikisha kazi hiyo.

    Wasiliana Vyema na Mapema
Mawasiliano ya wazi kati ya wewe na bosi wako yatawafanya muweze kuelewana na kujenga mazingira mazuri ya kazi. Tafuta njia yake nzuri ya mawasiliano ili kuunda mazungumzo sahihi, kujenga imani na kuboresha tija ya kampuni.

    Ukuaji wako wa Kazi na Kampuni Ndio Kipaumbele
Mwisho, unapaswa kukumbuka kuwa upo katika nafasi uliyopo kama ulivyokusudia waukianza kazi yako. 

Daima amini kwamba kazi yako itaendelea kukua bila kujali tofauti ya umri kati yako na bosi wako. Kwa kuongeza, kumbuka kwamba wewe na bosi wako mpo kwenye timu moja na lengo lenu ni moja, kukuza kampuni.

Daktari FEKI Anaswa Bugando

0
0
Daktari feki anayefahamika kwa jina la Joseph Samwel (26), amekamatwa katika Hospitali ya Rufani ya Bugando mkoani Mwanza, baada ya kutafutwa takriban mwezi mmoja kutokana na malalamiko ya wagonjwa.

Wagonjwa na watu mbalimbali wanaofika hospitalini hapo wamekuwa wakilalamika kutapeliwa fedha na watu wanaojitambulisha kwao kuwa ni watumishi wa hospitali hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Bugando, Abel Makubi, Ofisa Uhusiano wa Hospitali hiyo, Lucy Mogele, alisema uongozi ulifanya jitihada za kufuatilia malalamiko hayo kwa kuweka mitego kadhaa, ambayo ilifanikisha kumkamata mtuhumiwa huyo ambaye ni mkazi wa wilaya ya Magu mkoani Mwanza.

"Joseph amekuwa akijitambulisha kwa nafasi mbalimbali kama daktari, muuguzi na mwanafunzi wa udaktari na baada ya jitihada kufanyika, daktari huyo feki alikamatwa Oktoba 3, mwaka huu, majira ya saa moja jioni ndani ya eneo la hospitali kwa msaada wa wauguzi na madaktari, "alisema Mogele.

Kwa mujibu wa Mogele, katika maelezo yake, Joseph alidai kuwa ni mwanafunzi wa mwaka wa pili wa shahada ya uuguzi katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino kilichoko jijini Dodoma.

"Kimsingi kozi hiyo haipo katika mitaala ya kitabibu na chuo kilichotajwa hakiko jijini Dodoma," alisema.

Katika mahojiano ya uongozi wa hospitali hiyo, mtuhumiwa huyo alikiri kuhusika na matukio mengi ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kutoka kwa wagonjwa huku akiwaahidi kuwapatia huduma.

"Kijana huyu amekuwa akizungukia sana maeneo ya wodini na hata wagonjwa wenyewe wamekiri kuwa alikuwa akiwatapeli. Watu kama hawa wamekuwa wakisumbua wagonjwa, ikiwamo upotevu wa vitu na fedha zao na kuwapatia huduma ambazo si sahihi," alisema Mogele.

Naye Mwanasheria wa hospitali hiyo, Anacket Kamara, alitoa wito kwa wananchi wote wanaofika katika hospitali hiyo kwa ajili ya kutibiwa, kufuata taratibu za matibabu zilizowekwa na uongozi.

Alisema kama kuna mahitaji ya kupata ufafanuzi au maelekezo na ushauri, watumie dawati la maulizo au kuonana na watumishi wenye sare za ‘niulize nikusidie’ au wapige simu zilizoko katika mbao za matangazo.

"Ni haki ya kila mwananchi kuomba kuona kitambulisho cha mtoa huduma katika eneo husika ili kuepukana na madaktari feki ambao wanachukua fedha na kushindwa kuwahudumia na kusababisha malalamiko na mtuhumia Joseph yuko chini ya ulinzi akisubiri sheria ichukue mkondo wake," alisema Kamara.


Askari JWTZ afa Kwa kujitosa baharini

0
0
Askari  wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), amefariki dunia baada ya kujirusha baharini akisafiri na boti ya Azam.

Kifo cha askari huyo ni moja ya matukio matatu ya watu waliojitupa baharini wakiwa safarini kwa kutumia usafiri huo, akiwamo mtoto aliyeokolewa akiwa hai.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Azam Marine, Abubakar Aziz, alisema jana kuwa askari huyo alifariki dunia hivi karibuni na kwamba hayo ni miongoni mwa matukio ambayo yamewahi kujitokeza katika boti zao.

Aziz alisema katika matukio hayo, watu wawili akiwemo mwanajeshi huyo walijitosa baharini wakati meli ikiendelea na safari na askari huyo alijitosa eneo lenye kina kirefu kiasi kwamba asingeweza kuokolewa.

"Matukio haya yalitokea kwa nyakati tofauti ambapo baada ya kujitupa baharini licha ya juhudi kufanyika za kuwatafuta, hatukuwapata. Walipatikana siku nne baadaye akiwa tayari wameshafariki dunia," alisema.

Credit: Nipashe

Ufugaji wa nguruwe : Gharama na Faida Zake

0
0

Utangulizi

Nguruwe ni mnyama amabaye hutumika kama chakula / mboga na pia ni zao la biashara kwa mfugaji, mjasirimali na mfanyabiashara.

NGURUWE HUTEGEMEA SANA MAMBO YAFATAYO

1 . Banda imara na rafiki kwake
2. Usafi ni muhimu sana katika banda la Nguruwe
3 Mchaganyo bora wa chakula
4. Tiba bora na kinga
5. Maji na Lishe ( access ya vyakula Muhimu kwake )

CHANGAMOTO

KATIKA UFUGAJI WA NGURUWE KUNACHAGAMOTO ZAKE LAKINI ZAWEZA KUTATULIWA KWA KUFATA MAMBO KADHAA.
Katika ufugaji wa nguruwe kunachagamoto ya vifo vya nguruwe wachanga ambao hupunguza faida ya biashara ya nguruwe kwa kupunguza idadi ya nguruwe wazima wa kuuzwa lakini utunzaji mzuri wa nguruwe wachanga huepusha vifo vinavyotokana na shida kama:

Matatizo ya kupumua

Ni kifo kinachosababishwa na mama anapomlalia nguruwe mchanga.chagamoto hii inaweza kutatuliwa kwa kuwatenga au kuwa na mabanda makubwa ya kulelea watoto.

Baridi

Nguruwe wachanga huathiriwa na baridi haswa katika majuma mawili au matatu ya mwanzo. Hii ni kwa kuwa wana kiwango kidogo cha utando wa mafuta wa kuwakinga.
Unashuriwa kuwaweka katika hali ya joto, wape matandiko na utumie vipasha joto kama vile kuwasha globu za joto kama utakuwa umewaweka kwenye mabanda ya kuta au nyumba yenye sakafu baridi.

Namna bora utunzaji wa nguruwe wachanga

Nguruwe moja wa kike ana uwezo wa kuzaa watoto 12. Namna ifuatayo itasaidia kupunguza idadi ya vifo vya nguruwe wachanga:
1.Pale nguruwe awapo na kidonda nyunyizia dawa ya ayodini 5% kwenye kovu ili kuzuia kuambukizwa kwa magonjwa.
2.Wawekee matandiko (nyasi kavu au maganda ya miti) mahali pa mapumziko ili wapate joto au utumie globu za joto.
3Wadunge sindano ya madini ya chuma (iron) siku ya tatu baada ya kuzaliwa ili kuzuia upungufu wa damu.
3. Yalainishe meno ya vichaga kabla ya masaa 24 ili kuzuia uharibifu wa matiti wakati wanaponyonya.
4. Watie vibandiko au utoboe masikio ili uwatambue na uhifadhi rekodi zao kama kuna umuhimu kama vile wafanyavyo wafugaji wa ng’ombe.
5. Wapime uzani wanapozaliwa na uhifadhi rekodi hiyo itakusaidia kujua ukuaji wao na maendeleo yao
6. Wahasi wale wa kiume juma la tatu, wale ambao hawafai katika kuendeleza kizazi kwa kutumia mtindo wazi (open method) kama unaona inafaa.
7. Wapatie dawa ya kuzuia minyoo pia zipo dawa za asili kama unga wa mkaa na majivu pia zipo za kitaalamu, wasiliana na wataalamu wa mifugo
8.Waachishe kunyonya katika juma la nane au wafikapo kilo 14 hadi 20 hii itasaidia kujitegemea na kukua kwa haraka.

Nguruwe Walioachishwa Kunyonya

1.Walioachishwa kunyonya wawekwe makundi ya 10 hadi 12 kulingana na uzito au ukubwa wao kwenye eneo ambalo watajitosheleza.
2.Watenganishe wakubwa kwa wadogo ili kuzuia kupigana.
3.Wakati wa kuwaachisha kunyonya mwondoe mama yao kutoka kwa watoto ili kupunguza usumbufu.
4Watoto wa nguruwe wa mama tofauti wasiwekwe pamoja maana hii husababisha mapigano kati yao na
5.Unapowachanganya watoto wa mama tofauti wapake mafuta ya gari yaliyotumika kwenye ngozi yao au mafuta ya kula ili kuiondoa harufu ya kutambulika ili wasipigane

FAIDA YA UFUGAJI WA NGURUWE

Faida kuu ya nguruwe ni zao la chakula lakini pia ni zao la kukuongezea kipato ukiwa kama mjasirimali / mfanyabiashara.
Lengo langu nikueleza namna unavyoweza kufuga na kutupa faida, Steps zifatazo ni muhimu kuzigatia.
JIPE MTAJI WA MILLION 4 / 3.5 KWA NGURUWE 50
UANDAAJI WA BADA WEKA MAKADILIO YA LAKI TANO (800,000/=) .
Hapo nazugumzia banda lenye heru U yenye mstatili ikiwa na kitako kirefu
Eneo lenye ukubwa wa mita 50 kwa 50 litafaa zaidi ili kuhakikisha usalama wa nguruwe wako na ukuaji bora.
1. Tafuta mabati used kwa bei ya 5000 mfano mabati 20 ya futi 10 /10 = 100,000/=
2. Tafuta mabazi ya futi 10 kwa 2000 kila moja utapata mabazi pic 100 = 200,000/=
3. Tafuta miti ya nguzo na kechi ya 1000 na 2000 miti ya 1000*70 na 2000*3 = 120,000/=
4. Tafuta chagalawe / moramu trip 10*3000 =30000/=
5. Cement mifuko kwa ajiri ya sakafu na mashimo ya kulishia 5 *18000 = 90,000/=
6. Misumari ya aina 4, nch 6 kg5,nch 3 kg5 nch 5 kg10 na nch4 kg10, Bawaba na komeo =100,000/=
7. Malipo ya fundi 75000 fundi uashi na 75000 fundi seremala =150,000
JUMLA HAPO INAKUWA 790,000/= MAKADILIO INAKUWA 800,000/=

UNUNUZI WA NGURUWE WA KUANZIA .

Nguruwe wadogo wadogo ni vinzuri zaidi kuanza nao kwa sababu watakuzalia watoto wengi na kwa muda mrefu . Chukua mfano MILLION 2.5 . Nguruwe wadogo wa dogo wanauzwa 50000 au 40000 inategemeana na mahala na maelewano . Milioni 2.5 inakupa vitoto 50 au 55 . Hivyo unawexa kuwa na vitoto jike 50 na vidume 5. baadaye ukaongeza madume matano ya kuazima au kukondi kwa ajiri ya kupandishia

MAANDALIZI YA CHAKULA

Mchaganyiko wa chakula cha nguruwe na gharama zake tunaweza ukadilia kujitosheleza kwa laki tatu kwa mwenzi mmoja kwa nguruwe hao 50, kwa 300,000/= , ambapo itajumuisha tiba / kinga, lishe, vyakula vya nguruwe vinaweza kuwa pumba ya mpunga ile laini,pumba ya mahindi, mashundu, mabaki ya magada ya vianzi amba mabaki ya chakula yaliyosalama

MALIPO YA MSIMAMIZI NA ENEO LA KUWEKEZA

Katika kipengele hiki makadilio ya juu ama ya chini kwa msimamizi wa kazi yako waweza mlipa 100,000/= ama chini yake pia kwa mwenye eneo huwa nimaelewano tu aunaweza pata kwa fair au kukakodi kwa laki tatu, 300,000/= kwa mika miwili.
HIVYO JUMLA YOTE YA GHARAMA ZA UAZISHAJI UWEKEZAJI WA NGURUWE 50 ZITAKUGHARIMU MILLION 4 AMA MILLION 3.5 KWA MAANA KUWA HAPO JUU NIMETUMIA MAKADILIO YA JUU NA UKIINGIA KWENYE UHALISIA KAMA MJASIRIMALI LAZIMA IPUNGUE NA KUFIKIA 3.5

KIPATO AU FAIDA YA UFUGAJI NGURUWE

Nguruwe wanafaida ya haraka na nimradi wa uhakika kabisa, ukipitiia mchanganuo hapo juu wa nguruwe 50 utatupa faida kama ifatavyo
Nguruwe huzaa Mara mbili kwa mwaka na huzaa watoto zaidi ya watanoyaani huzaa watoto 12 ama nane .
Basi chukua nguruwe 50 * vitoto 5 yaani ufanye kuwa nguruwe wako 50 wakupatie vitoto vitano vya uhakika
Nguruwe 50*5 = 250 ukijumlisha na wale 50 wa mtaji umakuwa nao 300 . Chukua zao la nguruwe la 250 na uza kwa 200000 kwa kila nguruwe yaan bei ya kawaida kabisa. Utapata Million 50. 

Hivyo zao la kwanza ndani ya robo tatu ya mwaka inakutegenezea million 50 pia na mienzi sita ijayo inakupa tena 50 na zaidi ili kukamilisha uzao wa pili hii inkupa uhakika wa kutegeneza million 100 za uakakika ndani ya mwaka mmoja na nusu ama miaka miwili ukijipa timeframe work lakini kumbuka hapo tumefanya kwa hesabu ya uzao wa chini kabisa ambapo tumeangalia na hasara ya vifo kama vifo visipotokea na uzao ukawa mkubwa utakuwa na uhakika wa kutegeneza million 150 kwa miaka miwili.
 
Kwenye hesabu ya kuwale unaweza kuwaza sana kuwa itaongezeka na kukughalimu sana jibu ni hapana mpka kufikia kuuza hawatokugharimu zaidi ya million 7 je million 7 kwenye million 150 ni kitu kisicho nafaida ?
NB . jambo lolote linahitaji umakini naa dhamira ya dhati pia kushirikisha wataalamu na wenye uzoefu ili kufikia leng Ewe ndugu kila kitu kinawezekana UTAYARI WAKO / UTHUBUTU WAKO, UAMINIFU .NA MAAMZI YAKO.
 

Dkt Tizeba Atengua Uteuzi Wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu Wa Bodi Ya Sukari

0
0
Waziri  wa Kilimo, Dk. Charles Tizeba, ametengua uteuzi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Sukari Tanzania, Miraji Kipande.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Mawasiliano ya serikali cha Wizara hiyo, Dk. Tizeba ametengua uteuzi wa Kipande kuanzia juzi.

Aidha, Dk. Tizeba amemrejesha Kipande katika nafasi ya awali aliyokuwepo kabla ya kuteuliwa kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa bodi ya Sukari Tanzania.

Chid Benz Aibukia kwa Diamond....Azungumza Maneno Mazito Kuhusu Madawa Ya Kulevya

0
0
Mwanamuziki wa kizazi kipya Chid benz ambaye alihusishwa na matumizi ya madawa ya kulevya,jana aliweza kupewa nafasi ya kuongea katika sherehe za siku ya kuzaliwa ya msanii Diamond Platnumz na kuongea maneno ya kuumiza sana. 

Sherehe hizo zilizofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Tandale  zilihudhuria na watu mbali mbali wakiwemo viongozi wa serikali pia wadau mbali mbali wa sanaa ya muziki Tanzania. 

Chid benz alipata nafasi hiyo ya kuongea huku akipafomu nyimbo yake ya “Dar es salaam stand up” na kupokelewa kwa shangwe sana na wakazi wa kata hiyo ya Tandale waliohudhuria mahala hapo. 

Baada ya kumaliza kupafomu aliweza kumshukuru Diamond pamoja na wageni wote lakini pia shukrani nyingi alizirudisha kwa mashabiki wake na kuongea maneno yaliyomuumiza kila mmoja aliyefika mahala hapo kuhusiana na matumizi ya madawa ya kulevya. 


“Madawa ya kulevya si mazuri lakini watu wanatumia na wanauza hii yote ni katika kutafuta hela, ila si kitu kizuri kama kinaweza kukusumbua ni vizuri kuachana nacho.

“Nashukuru kwa msaada wa Tale na Diamond kwangu, nashukuru sana kila kitu kiko sawa sasa cha msingi ni kufuatilia ili kupata maisha bora.

 

“Nashukuru kwa uongozi wa Wasafi kunipa nafasi, nafurahi kwa kila kitu kinachotokea hapa leo, kama wote tunakanyaga chini ya ardhi hakuna mtu anayeweza kupaa.” Alisema Chid Benz

Rais Magufuli Apokea Taarifa Ya Udhibiti Mapato Ya Serikali

0
0
Rais  John Magufuli amepokea taarifa ya maendeleo ya kazi ya udhibiti wa mapato ya serikali kutoka kwa timu ya wataalamu wanaotengeneza na kusimamia mifumo ya mapato ya serikali, wakaguzi na wataalamu wa bajeti. 

Alipokea taarifa hiyo jana ikulu kutoka timu inayoongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Doto James iliwasilisha taarifa ya uanzishwaji wa mifumo katika taasisi za umma 304 nchini, ongezeko la mapato baada ya kuwekwa kwa mifumo hiyo, ukaguzi wa ndani na masuala ya bajeti.

Katibu Mkuu Doto James alimueleza Rais Magufuli kuwa katika kipindi cha mwaka 2016/2017 hadi 2017/2018 timu hiyo imefanikisha kuokoa zaidi ya Sh trilioni 3.2 zikiwamo Sh trilioni 2.2 zilizookolewa kutoka kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii baada ya kufanya uhakiki wa madeni ya serikali, kuondoa watumishi hewa na wenye vyeti feki. 

Doto alibainisha kuwa timu hiyo pia imefanikiwa kudhibiti mianya ya upotevu wa fedha za serikali baada ya kuziunganisha taasisi 304 katika mfumo unaodhibitiwa moja kwa moja na Wizara ya Fedha na Mipango.

Taasisi hizo ni pamoja na zinazokusanya maduhuli ya serikali kama vile Shirika la Umeme nchini (Tanesco), Idara ya Ardhi, Wakala wa Vipimo, Hifadhi za Taifa (Tanapa), Wakala wa Misitu, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), Hifadhi ya Ngorongoro na Wizara ya Ardhi, na kuondoa mawakala wa kulipa mishahara ya watumishi. 

Rais Magufuli aliwapongeza wataalamu hao kwa kazi nzuri waliyoifanya na wanayoendelea kuifanya na alimuagiza Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi kuhakikisha taasisi zote za serikali zinazopaswa kuunganishwa na mifumo hiyo ya udhibiti zinaunganishwa haraka iwezekanavyo, vinginevyo awachukulie hatua viongozi ambao hawatatekeleza agizo hilo.

“Nimefurahi sana kwamba sasa vijana wetu mmeweza kutengeneza mifumo yetu sisi wenyewe kwa ajili ya kudhibiti mapato ya serikali, nawapongeza sana, mnafanya kazi kubwa ya kujenga nchi yetu, mmeonesha uzalendo wa hali ya juu, nawahakikisha nipo na nyinyi na endeleeni kuchapa kazi.

 “Mmeaniambia kuwa mpaka sasa mmeunganisha mifumo ya kudhibiti mapato kwa taasisi 304 na bado kuna taasisi nyingi bado hazijaunganishwa, naagiza taasisi zote za serikali zitumie mifumo mnayoitengeneza na ambayo inadhibitiwa na sisi wenyewe.

“Nafahamu mmeokoa fedha nyingi sana ambazo zilikuwa zinapotea, hatuwezi kuendelea kuachia fedha ziendelee kupotea,” alisisitiza Rais Magufuli. 

Aliongeza kuwa fedha ambazo zimepatikana baada ya udhibiti wa mifumo ya ukusanyaji wa mapato ndizo zimesaidia kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo kwa ajili ya wananchi ikiwemo ujenzi wa vituo vya afya 208 katika nchi nzima. 

Mingine ni ujenzi wa hospitali mpya 67, ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (SGR), madaraja makubwa na madogo, barabara, kusambaza umeme, maji na mingine mingi iliyotekelezwa katika kipindi kifupi cha tangu serikali iingie madarakani.

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asili

SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,

Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Dawa za Asili ya Kuzuia Mimba kutoka, Mtu Aliyepata Ajali, Degedege, Busha, Kuota Nyama Sehemu za Siri

0
0
Mbepe; ni dawa ya nguvu za kiume,kurefusha na kunenepesha maumbile madogo kwa muda mfupi.

MHOLA; ni dawa inayotibu kisukari,presha,degedege,kifafa,mwili kupooza, Kipanda uso,kiuno,mgongo,kuzuia mimba isotoke, Kuuma tumbo chini ya kitovu.

NDAGULA; ni dawa ya kuunga mifupa kwa mda mfupi kwa aliye pata ajali na kuvunjika,ataanza kupata nafuu ndani ya siku 14 na kufanya mazoezi

Inhondi; ni kwa wale wenye busha,kuota nyama sehemu ya Siri, Miguu kuwaka moto.

Lukomolo;  Ni dawa ya mvuto wa mapenzi Kumvuta mme, Mke, Mchumba hawala atakutafuta mwenyewe

Tupo mbagala rangi 3, kwa dar huduma utaletewa popote ulipo kwa tiba na ushauli piga no. 0742215230/0787131395/0712757594 dr MASELE

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 91 na 92 )

0
0
ILIPOISHIA           
Nikatazama picha ya pili, nikaona askari mmoja akiwa amepigwa risasi ya kichwa, picha ya tatu ikanifanya ninyanyuke kwa haraka huku macho nimeyatoa.
Ili kuhakikisha ninacho kiona ni chenyewe na si utani, nikaikuza picha ya mama yangu anaye onekana kuchinjwa kikatilia sana jambo lililo nifanya nianze kutetemeka mwili mzima, huku nguvu za mwili nikihisi zinaanza kunishia. 

Nikajikaza hivyo hivyo kusogeza picha ya mbeleni, hapo napo nikamuona Diana mdogo wangu akiwa amachinjwa huku maziwa yake yakiwa yamekatwa jambo lililo nifanya nijikute nikiiachia simu ya mama Mariam ikaanguka chini, hata mimi mwenyewe siku sikumaliza hata sekunde tatu, nikajikuta nikianguka chini na kutulia tuli.

ENDELEA           
Kwa mbali nikamuona Mariam akimuachia mama yake na kuniwahi mimi hapa chini nilipo anguka.
“Mama umefanya nini, kumuonyesha Dany hizi picha lakini?”
Niliisikia sauti ya Mariam ikilalama kwa mbali sana.
“Mshike huko tumuweka hapa kwenye sofa amezimia”
Nikahisi nikinyanyuliwa, nikawekwa kwenye sofa.
“Mama kalete maji ya baridi”    
 
Vitendo vyote wanavyo vifanya Mariam na mama yake ninavisikia kwa mbali sana, japo mwili na viungo vyangu havina nguvu ya kuweza kukabiliana na hii hali. Maji ya baridi niliyo mwagiwa kichwani mwangu, yakanifanya nikurupuke katika hali ya kusizi. Nikasimama wima huku macho nikiwa nimeyatoa, mimi mwenyewe nikakiona kifua changu jinsi kinavyo panda na kushuka kutokana na mapigo yangu ya moyo kunienda kasi sana.
“Dany”
Mariam aliniita huku akiwa ameninyooshea mkono wa kulia, nikamtazama kwa umakini sana, akausogeza mkono wake na kunishika bega la upande wangu wa kulia.
“Dany tulia, tulia”
Mariam alizungumza huku akizidi kunisogelea. Nikajaribu kuzungumza kitu, ila kinywa changu hakikuweza kunyanyuka kabisa, taratibu Mariam akanirudisha na kunikalisha kwenye sofa walilo kuwa wamenilaza muda mchache ulio pita. Nikaendelea kufikiria nilicho kiona ni sahihi au nilikuwa ninaota. Nikamnyooshea mama Mariam mkono, jambo lililo mfanya kubaki amenitumbulia macho.
 
“Simu”
Nilizungumza kwa ufupi, mama Mariam akageuka nyuma na kuitazama simu  yake iliyo anguka katika sehemu ambayo nilianguka. Akapiga hatua taratibu na kuifwata hadi sehemu  nilipo aungukia, akaichukua na kurudi nayo, akanikabidhi pasipo Mariam kuzungumza chochote. Kwa bahati mbaya kioo cha simu hii kimepasuka na hakifanyi kazi ya aina yoyote.
 
Nakaanza kuikagua simu hii, nikaifungua nyuma na kutoa chipu ya kuhifadhia kumbukumbu(memory card). Nakaito chipu iliyopo kwenye simu yangu na kuiweka chipu hii ya mama Mariam, haikuchukua sekunde nyingi, ikawa imekubali kufanya kazi kwenye simu yangu, kwa haraka nikaingia kwenye upande wa picha, nikaanza kuziona picha za mwanzo nilizo ziona. Nikaiona picha ya mama yangu, machozi ya hasira taratibu yakaanza kunimwagika usoni mwangu, nikatazama picha ya Diana, nikapeleka mbele, hapo nikaona picha ya Asma, pamoja na mwanagu nao wakiwa wamechinjwa kikatili sana.
 
Nilihisi kama moyo unakwenda kupasuka kwa hasira na maumivu ninayo isikia, mwili mzima ukaanza kusisimka huku meno yakikaza, jasho jingi likaendelea kunimwagika.
“Dany”    
 
Mariam aliniita kwa sauti ya upole sana, ila jicho nililo mtazama nalo, hakuweza kuendelea kuzungumza tena akaka kimya, ukimya ukatawala ndani ya seble hii. Mlio wa simu yangu, ukanistua na kunifanya nitazame anaye nipigia. Jina la hawa lililo jitokeza juu ya simu yangu, likanifanya nibaki nikiwa nimelikodolea macho tuu, kwa hasira niliyo kuwa nayo sikuweza kuzungumza kitu cha ina yoyote.
Taratibu nikanyanyuka, kwenye sofa nililo kalia, nikaanza kutembea kueleka nje. Mariam kwa haraka akwahi mlangoni na kunizuia kwa kuichanua mikono yake, ili nisipite.
“Dany nakuomba unisikilize tafadhali”
“PISHA NJIA”
Hata sauti yangu imebadilika, inatoka ikiwa imekusanya besi kubwa, na mikwaruzo ambayo tangu kuzaliwa kwangu sikuwahi kuisikia.
 
“Dany siwezi kukupisha pasipo wewe kunisikiliza katika hili ninalo kwenda kulizungumza”
Mariam alizungumza kwa msisitizo sana, nikaendelea kumtazama kwa hasira, kwani anacho kifanya ninaona kama nikipingamizi kwangu.
“Dany natambua kwamba kifo cha familia yako ni lazima kinakuuma sana, ila tukae chini tuzungumze tufahamu kwamba tunaanzia wapi katika hili”
Nikaupeleka kwa nguvu mkono wangu wa kulia, ukaushika mkono wa Mariam, nikamvuta pembeni na akaanguka chini. Nikapiga hatua mbili mbele, Mariam akaniwahi kunidaka mguu  wa kulia akiendelea kunizuia kuondoka. 

Nikageuka nyuma na kumtazama kwa hasira sana, Mama Mariam aliye simama pembeni akishuhudia kinacho endelea, usoni mwake anamwagikwa na machozi mengi asijue anafanya kitu gani.
“Dany unajua ni jinsi gani ninayo kupenda, unajua ni jinsi gani ninavyo umia kukuona katika hiyo hali, tafadhali Dany, nakuomba usiondoke”
Mariam alizungumza huku machozi yakimwagika sana. Sikuhitaji kusikiliza porojo zake, nikauvuta mguu wangu kwa nguvu na ukaponyoka kwenye miguu yake. Kwa haraka nikatoka ndani kwao. 

Moja kwa moja nikaelekea nilipo lisimamisha gari langu, nikafungua na kuingia ndani, bastola yangu niloyo kuwa nimeiacha chini ya siti ta hili gari nikaiweka magazine na kuikoki vizuri, simu yangu nikaiweka kwenye siti ya pembeni, nikawasha gari kwa haraka na kuanza kulirudisha nyuma ili kuliweka sawa kueleka getini. Mariam akatoka ndani na kusimama mbele ya gari langu huku akinitazama machozi yakiendelea kumwagika usoni mwake. 
 
Mama yake naye akatoka akiwa analia, akasimama barazani, akitazama kinacho endelea. Nikamtazama Mariam machoni mwake, huruma ya kibinadamu tayari imesha niondoka moyoni mwangu, nikaichukua bastola yangu na kushuka kwenye gari, nikamnyooshea Marima, ambaye bado amesimama mbele ya gari langu.
“Dany niue tuu, naomba nafasi unisikilize”
Mariam alizungumza huku akinitazama, nikaendelea kumsogelea huku nikiwa nimemnyooshea bastola, moyoni mwangu nikaanza kusikia sauti mbili zikishindana, moja ikiniomba nimsikilize Mariam anacho hitaji kuzungumza huku nyingine ikiniomba nimpige risasi na nitaenda kujua mbele ya safari nani ni muhusika wa kifo cha familia yangu.
 
“Sihitaji kukuua Mariam, kwa mana sina chuki na wewe, japo nilishatumwa kukuua wewe na bosi wangu, ila sijafanya hivyo, tafadhali ninakuomba unipishe kabla sijafanya hivyo”
Niliendelea kuzungumza kwa sauti ya kukoroma, walinzi wa Mariam kwa haraka wakafika katika eneo tulilo simama huku wakiwa wameninyooshea bunduki.
“Dany ni vyema ukaniua, ni vyema nikafaa mimi. Kwa nini unashindwa kunisikiliza, kwa nini unashindwa kuheshimu ombi langu. Unajua nani ni muuaji wa familia yako”
Mariam alizungumza kwa sauti ya juu iliyo jaa ukali na uchungu ndani yake. 
 
“Nani ni muuaji? Livna, K2 au?”
Nilizidi kumuuliza Mariam kwa ukali zaidi, akaka kimya, baada ya kuona anaendelea kunipotezea muda, nikarudi kwenye gari langu, nikaingia ndani na kufunga. Nikakanyaga mafuta na breki, jambo lililofanya tairi za gari langu kuanza kuserereka kwa kasi sana. Mlizi mmoja alipo ona gari linaaza kusogea akamuwahi kumrukia bosi wake na kumsogeza pembeni nikapita kwa spidi sehemu alipo kuwa amesimama Mariam. 

Kasi yangu ikaishia getini baada ya kuoga geti limefungwa, kwa haraka nikashuka kwenye gari, nikalifungua geti nikarudi kwenye gari na kuondoka kwa mwendo wa kasi.
Kutokana si mwenyeji katika nchi hii ya Somalia, akili yangu kwa haraka ikanituma kutafuta ramani kupitia hii simu, ambayo itanipa maelekezo ya kuweza kufika Tanzania kwa kutumia gari. 

Nikasimamisha gari pembeni ya barabara umbali mrefu sana kutoka sehemu ilipo nyuma ya Maria. Haikuchukua muda sana kuweza kuiunganisha huduma ya GPRS, iliyo anza kunielekeza kwa mshale maalumu, kuanzia sehemu nilipo na sehemu ninayo hitaji kuelekea. Masaa niliyo yayo hadi kufika Tanzania ni masaa thelathini na tano sawa na siku mbili na masaa kumi na moja kwa mwendo  wa gari. Kwani kuanzia hapa nilipo hadi kufika Tanzania, nikipitia nchi ya Kenya itachukua kilomita elfu mbili mianne na nane.
 
Cha kumshukuru Mungu pesa zote alizo nipa Hawa ninazo, na kiasi nilicho nacho kinaweza kunifikisha Tanzania, katika siku hizi mbili. Mafuta niliyo nayo ni nusu tenki, katika kuendesha kwangu muda mwingi nikawa nitazama tazama kama ninaweza kupata sheli ya kujaza mafuta. Kwa bahati nzuri nikafanikiwa kupata sheli, taratibu nikasimama kwenye moja ya mashine ya kujazia mafuta. Nikashuka, huku nikiwa na kiasi cha kutosha cha pesa kwa maana katika jengo la hii sheli kuna Supermakert ya kununulia vitu mbali mbali.
“Lita ngapi muheshimiwa?”  
  
Kijana wa kiume wa kisomali aliniuliza huku akiwa ameshika bomba la kujazia mafuta.
“Hadi tanki ijae”
“Sawa”
Akaanza kujaza mafuta, nikaelekea ndani ya suoer makert. Nikaanza kuchukua vitu vya kula njiani pamoja na maji mengi ya kutosha. Nilipo hakikisha kwamba vitu nilivyo vichukua vinanitosheleza, nikalipia, wakaniwekea vitu vyangu kwenye mifuko mkubwa na kurudi navyo kwenye gari. Nikamkuta kijana huyu ambaye ni miongoni wa wahudumu kwenye hii sheli, akiendelea kujaza mafuta kwenye gari langu.
“Dogo bado?”
“Bado kidogo mkuu”
“Muna uaza madungu”
“Yaliyo na mafuta au matupu?”
“Yaliyo na mafuta”
“Hayo yametuishia, kama vipi nikuuzie dumu tupu, kisha nikujazie mafuta”
 
“Sawa hakuna shida katika hilo”
Dogo akamaliza kuweka mafuta katika gari langu, akafungu vizuri mfuniko wa tanki la mafuta yangu, nikahakikisha amekkaza vizuri mfuniko huo, nilipo jiridhisha, nikasimama pembei ya gari langu nikimsubiria kijana huyu kurudi. Nikaisikia simu yangu ikiita ndani ya gari langu, jambo lililo nifanya nifungue mlango na kuichukua simu. Nikakuta ni Hawa anapiga, nikaipokea na  kuiweka simu sikioni.
“Dany ni kitu gani ambacho unakifanya?”
“Kivipi?”
“Umepoteza mawasiliano, huku sikuoni. Tafahadhali rudisha hiyo chipu kwenye simu”
Hawa alizungumza kwa ukali sana, nikakitazama kioo cha simu kisha nikairudisha sikioni mwangu.
“Nina kazi muhimu ambayo ninahitaji kuifanya ukiachilia mbali na kazi yako ambayo ulinipatia”
“WHAT………..!! Wewe ndio wa kunijibu mimi hivyo kumbuka mimi ni mkuu wako”
“Sijakuvunjia heshima, nawala sihitaji nikivunjie heshima, ila hutambui ni kitu gani kinacho endelea katika maisha yangu, hujui maisha yangu ya nyuma Hawa. Hii ni nafasi ya mimi kufanya kile ambacho kilikuwa nyuma ya maisha yangu”
“Bosi huruhusiwi kuzungumza na simu katika eneo hili la sheli”
 
Kijana anaye nihudumia aliniambia, jambo lililo nifanya nikate simu na kuitupia ndani ya gari, huku nikiwa nimejawa na hasira mara dufu.
“Bosi wewe ni Mtanzania nini?”
“Kwa nini unaniuliza hivyo?”
“Watanzani wanajulikana, hushangani kwa nini nilikuongelesha Kiswahili?”
“Ok kwa hiyo?”
“Ahaa hapana, ila mimi mwenyewe ninapafahamu Tanzania, kuna kaka zangu, wapo maeneo ya Dar es Salaam maeneo ya Kariakoo wana maduka yao huko”
“Dogo niwekee mafuta, sipendi blaaa blaaaa nyingi”
Nilizungumza kwa ukali, hadi kijana wa watu akapoteza tabasamu usoni mwake. Akanijazia dungu langu mafuta ya kutosha, kisha nikafungua buti ya gari, akaliweka dungu la mafuta na kulifunga buti la gari langu.
 
“Sina pesa ya kisomali, kama vipi ninakupatia Dola. Niambie itagarimu dola ngapi?”
“Ahaahaa…..ahaa dola kama mia nne”
Nikampatia noti za dola mia mia zikiwa nne, kisha nikaingia kwenye gari na kuufunga mlango kwa nguvu.
“Kaka uendeshe gari kwa umakini, hasira sio nzuri”
“Nenda kamuambie baba yako”
Nilimjibu kijana wa watu vibaya huku nikisindikiza na msunyo  mkali, kisha nikapandisha kioo cha gari langu na kuondoka katika eneo la sheli. Nikajifunga mkanda wa siti na kuendelea kuendesha gari langu kwa kasi huku nikifwatisha ramani ya simu inayo niongoza. Simu yangu ikaita tena, nikaichukua, sehemu nilipo iweka, nikaitazama kwa muda kisha nikapokea.
 
“Ndio”
“Dany hujui unajiingiza kwenye matatizo ya aina gani, hujui majibu yako ni jinsi gani yanavyo mkasirisha baba, tena anakusikia hapa ninavyo zungumza na wewe, kwa nini Dany unafanya hivyo lakini”
“Hawa, nimeishi katika mikono ya baba yako na wewe kwa kipindi kirefu sasa, ila hakuna hata mmoja wenu aliye weza kuniuliza maisha yangu ya kiundani sana, si wewe wala si baba. Nina wapenda tena sana, kazi ambayo baba na wewe mumenipatia imezalisha kazi nyingine. Kazi ambayo hata kama ungekuwa ni wewe usinge weza kuiacha kuifanya. Ni kazi ambayo imegarimu maisha yangu, ni kazi ambayo imeupasua moyo wangu, hakuna siku hata moja ambayo Hawa umenisikia mimi nikizungumza katika hali na sauti kama hii.”
 
Nikanyamaza kidogo huku nikijipangusa machozi, kwa maana maneno niliyo yazungumza yananitoa machozi ya uchungu.
“Sikuwahi kukuvunjia heshima, nimekuwa mtiifu  kwa kila mtu ndani ya hiyo ngome, nimekuwa nikijitahidi kwa kila jambo ambalo ninalifanya ninalifanya kwa juhudi na moyo  mmoja, kwa nini leo hii nimekuwa hivi. Kwa nini Hawa unashindwa kuniuliza kwa umakini zaidi eheee?”
Niliendelea kuzungumza huku nikilia, kasi ninayo liendesha gari langu, huku nimeshika mskani kwa mkono mmoja, inaweza kunihatarishia maisha yangu muda na wakati wowote, ila silijali hili.
 
“Dany mwanangu kuna kitu gani kimetokea”
Nilisikia sauti ya baba Hawa, hapa ndipo nikaamini kwamba kila ninacho kizungumza mzee ananisikia.
“Baba, mimi nilikuwa na familia. Ilikuwa nchinia Tanzania, mama, dada yangu, mke wangu pamoja na mwanagu mdogo wa kike. Ila hadi muda huu ninavyo zungumza, sipo nao tena. Wameuliwa kikatili, wamechijwa kikatili, sababu sijui ni nini. Ni vyema wangeniua mimi, ila si familia yangu, nimepoteza watu ambao ni muhimu sana kwenye maisha yangu”
Nikamsikia mzee akishusha pumzi, ukimya wa sekunde kadhaa ukatawala kati yetu.
“Wewe umejuaje Dany?”
“Ngoja nikutumie picha, nilifahamu hilo swala kutoka kwa mtu ambaye muliniagiza mimi kuweza kumuu.”
“Tutumie kwenye hii simu ya Hawa”
“Sawa mzee”
 
Nikakata simu, huku nikiwa ninaendesha gari, nikaanza kumtumia picha moja baada ya nyingine kupitia mtandao wa Whatsapp. Picha zote zikafunguliwa katika muda huo huo ambao nimezituma.
Nikaendelea kuendesha gari kwa mwendo wa kasi huku nikijitahidi kwenda na muda kwa mana ninahitaji usiku unikute nikiwa nipo kwenye mpaka kati ya Kenya na Somalia, naamini hapo nikifika usiku ninaweza kuhonga ma askari wa mipakani na itakuwa ni rahisi kwa mimi kuweza kupita hilo eneo kiurahisi sana. Simu ikaita tena, nikaipokea na kuiweka sikioni.
“Dany rudi kambini, kama ni kazi hii itafanywa na vijana maalumu”
Mzee alizungumza jambo lililo nishangaza sana akilini mwangu.
 
“Unasema?”
“Umenisikia, ninatoa amri kama mkuu wako wa kambi, na si baba tena. Rudi kambini kazi hii nitawakabdhi vijana”
“Kwa nini uwakabidhi vijana na si mimi, ninaiweza kuifanya kazi hii peke yangu. Na hakuna ambaye atanizuia, si wewe wala si mwanao. Ninakwenda kuifanya hii kazi mwenyewe”
“NITAHAKIKISHA HUTOKI NJE YA SOMALIA, NA NITAHAKIKISHA UNALETWA MBELE YANGU UKIWA HAI AU UMEKUFA, MWANA HARAMU MKUBWA WEWEEEE”
“Hahahaaa, mimi ni mwana haramu tena mkubwa sana, endapo nitajua umehusika na wewe katika hili. KICHWA CHAKO, nitakikata kwa mikono yangu mimi mwenyewe, na mbaya zaidi. Mimi ni mpelelezi niliye fuzu mafunzo mbali mbali tofauti na hayo unayo wapatia NGEDERE wako. Na ninakuhakikishia kwamba hiyo NGOME yako nitakuja kuifumua chini juu, juu chini. PUMBAVUUU”
Nikampiga mkwara mmoja ambao ninaamini ni mtakatifu kwa baba Hawa, kisha nikakata simu na kuongeza mwendo kasi wa gari langu, nilio kuwa nimeupunguza kidogo ili kuzungumza na huyu mzee mjinga.
                                                                           
AISIIIII……….U KILL ME 92                                                                                                 


Naamini kila ninapo katiza watu watakuwa wananishangaa kwa mwendo kasi wa gari langu ninalo liendesha. Nikaendelea kujitahidi kuhakikisha kwamba ninatoka ndani ya nchi hii ya Somalia haraka iwezekanavyo kwa maana hai ya hatari baba Hawa amesha itangaza kwangu mimi. Simu yangu ikaita, nikaitazama na kuona ni namba ngeni inaingia, kwa mara ya kwanza nikasita kuipokea, ikaita hadi ikakata. Simu ikaita tena, ikanibidi kuipokea ili kufahamu ni nani anaye nipigia.
 
“Dany, Dany please msikilize baba, usiende kinyume na sheria yake”
Niliisikia  sauti ya Hawa akizungumza kwa majonzi sana.
“Hawa naamini unafahamu uchungu wa familia, kwa mfano angeuwawa baba yako kipenzi wewe ungechukua maamuzi gani?”
Swali langu likamfanya Hawa kukaa kimya kwa takribani dakika moja.
“Dany upo  wapi?”   
“Sio jibu la swali nililo kuuliza?”
“Nimekuuliza kwa maana nahitaji kukusaidia, natambua ukiwa katika hali hiyo ya asira huto weza kufanya jambo lolote mwisho wa siku utaishia pabaya”
“Sijalishi hilo, nipo tayari kufa, na wala sihitaji msaafa wako Hawa. Umeyaokoa maisha yangu, asante sana kwa hilo”
“Dany tafadhali niambie ni wapi ulipo niweze kukusaidia?”
“Wewe na baba yako ni kitu kimoja, kama kweli unahitaji kunisaidia mimi subiri nikifika nchini Tanzania, ndio nitahitaji msaada wako”
 
“Sawa, ila kila mpango ambao  baba yangu ataupanga juu yako nitakueleza”
“Nitashukuru kama ni kweli”
“Nafanya haya yote kwa ajili ya upendo wangu kwako, tafadhali Dany sihitaji kukuona unapoteza maisha yako”
Nikashusha pumzi nzito huku nikiyafikiria maneno ya Hawa kichwani mwangu.
“Dany”
“Naam, ninakusikia”
“Fikiria hilo, nipo tayari kupoteza uaminifu wangu kwa baba yangu, kwa ajili yako. Tafadhali usife Dany wangu ninakupenda”
Niliendelea kumsikia Hawa anaye zungumza huku akilia kwa uchungu.
“Sawa nitaishi”
“Safari njema”
“Ok”
“Alafu Dany, unitafute kwenye hii namba, ile nyingine anayo baba. Pia usiiweke hiyo memory card uliyo itoa kwenye simu”
“Sawa
 
Nikakata simu, nikairudisha katika sehemu ambayo nimeitoa. Safari ikazidi kusonga mbele huku baadhi ya maeneo ambayo ninahisi kuna askari wa usalama wa barabarani, ninapunguza mwendo. Hadi inafika majira ya saa sita kasoro usiku nikawa nimefika eneo la Afmadow, mpakani mwa Kenya na Somalia. Bastola pamoja na magazine nikazivisha katika sehemu ambayo si rahisi kwa askri wakaguzi kuweza kuziona. Nikaandaa noti zangu mbili za dola mia mia. Taratibu nikaendesha gari langu hadi kwenye geti la kuingilia nchini Kenya.
 
“Habari yako mkuu”
Nilianza kujipendekeza kwa askari ambaye amefika karibu yangu, akiwa na bunduki mkononi mwake.
“Salama, washa taa ya gari lako”
Nikatii amri ya kuwasha taa ya ndani ya gari huku nikiwa na tabasamu pana usoni mwangu.
“Unaelekea wapi usiku huu?”
“Ahaa ninarudi nyumbani hapo Ijara, nimetoka Somalia mara moja”
Ilinibidi kudanganya kwani mji unao fwata kutoka nikisema ninakwenda mbali na hapo, wataanza kuniletea longolongo jambo ambalo sihitaji linitokee kwa muda huu.
“Naomba kipande chako”
 
“Ehee!!”
Niliuliza kwa mshangao kwa maana kingereza cha kikenya na kitanzania vina toafauti kubwa sana.
“Unashangaa ina maana hutambui kipande ni nini?”
“Ok ok muheshimiwa, kidogo nilipitiwa”
Nilizungumza huku nikianza kujipapasa mfukoni mwangu. Galfa askari huyu akaanguka chini, huku milio ya bunduki ikisikika ikitokea nyuma ya gari langu. Kwa kupitia kioo cha pembeni nikaona gari mbili zikija kwa mwendo  kasi sana. Kwa haraka sana nikafungu kioo cha  gari langu, huku nikianza kuliondoa eneo hili kwa kasi ya ajambu nilikilifwata geti lililopo barabarani. Askari waliopo kwenye hui mpaka wakaanza kushambulia watu ambao ninatambua fika wamegizwa na baba Hawa. 
 
Nikaligonnga getu na kuliangusha chini, nikaendelea kuongeza mwendo kasi wa gari langu, sikujali kama limebonyea seheu ya mbele.
Watu wa baba Hawa wakazidi kuniandama, kadri ninavyo watazama kupitia kioo changu cha pembeni, ndivyo jinsi ninavyo waona wanavyo zidi kuongezeka. Si magari mawili kama nilivyo yaona mwanzo, ila hadi sasa ninaona gari zisizo pungua saba, na zote zinakuja kwa mwendo wa kasi sana. Nikaichomoa bastola yangu, sehemu nilipo ificha, nikaweka magazine moja na kuanza kujibu mashabulizi ya wanajeshi wa Al-Shabab.
 
Hali haikuwa nzuri kabisa kwa upande wangu, kwani kadri ninavyo zidi kuongeza mwendo kasi wa gari langu, ndiovyo jinsi wana jeshi hawa wananikaribia, hadi ikafikia hatua nikaanza kukata tama. Nikaitazama simu yangu pembeni, mtando haupo kabisa jambo lililo ifanya hadi ramani ambayo nilikuwa ninaitegemea, kupotea kabisa. Gari sasa za wanajeshi wezangu, zikanisogelea pembeni hadi zikaanza kuwa karibu na mimi. Wakaanza kuligonga gari langu kwa kutumia ubavu wa gari zao. Sikuhitaji kuwa mnyonge, na mimi nikaanza kuendesha kwa kuyagonga magari yao kwa kutumia ubavu wa gari langu, japo yanabonyea ila dawa ya ubishi ni ubishi.

Kitu kilicho zidi kunishangaza kwa hawa wezangu, kitendo cha wao kunikaribia hakuna hata mmoja aliye thubutu kufyatua risasi kwangu, hapo ndipo nikagundua kwamba wameagizwa wanipeleke nikiwa hai. Nikatumia nafasi hii kwa kuwa jeuri zaidi, nilicho kifanya ni kuanza kupunguza mwendo kasi wa gari langu huku nikitazama gari hizi mbili zilizopo pembeni yangu kwa maana wameniweka kati kati na nyuma kuna magari mengie.
 
Nilipo waona nao wamepunguza mwendo kasi, nikaongeza mwendo kasi, nikawafanya nao kuongeza mwendo kasi, nilipo fika mbele kidogo nikafunga breki za gafla huku nikiwa nimekaza meno, mzinga ulio lia nyuma ya gari langu, ninaujua mimi na Mungu wangu, kwani gari mbili zilijikuta zikinivaa kwa nyuma na kulifanya gari langu kuhama kabisa kutoka barabarani, japo niinajitahidi kufunga mbreki, ila likaendelea kuserereka kwa maana limepoteza muelekeo katika barabara. Gari langu likaserereka hadi kwenye mti mkubwa ulipo karibu na barabara, likabamiza kwa nguvu na kutulia. Nikaanza kujitoa kwenye ftuza kubwa lililo tokeza kwenye mskani, kipindi nilipo funga breki za gafla. Japo nina maumivu sehemu mbali mbali katika mwili wangu, nikajitahidi kutola hivyo hivyo kwenye gari huku nikimwahikwa na damu za pua.
 
Nikajaribu kusimama, ila nikajikuta nikiyumba yumba kwa kizungu zungu kikali ambacho kimenitawala. Nikaanguka chini, huku nikiwaona wanajeshi  wengine wakinisogelea kwa haraka huku wakiwa na bunduki mikononi mwao. Nikajaribu kuinyanyua bastola yangu hata mikono haikuwa na nguvu kabisa. Kitu kizito kikatua kichwani kwangu, na kusababisha giza kali kutawala kwenye macho yangu.
                                                                                                                    ***
“Mfungeni vizuri”   
Niliisikia sauti ya baba Hawa kwa mbali sana, taratibu nikajitahidi kuyafumbua macho yangu, ila sikuona vizuri. Nikaanza kusikia maumivu ya mikono pamoja na miguu yangu katika sehemu ya viungio.
“Kaza na huko”
Niliendelea kuisikia sauti ya baba Hawa. Nikamwagiwa maji ya baridi usoni mwangu. Kidogo nikaanza kumuona baba Hawa pamoja na wanajeshi wengine wanne walio valia mabushori meusi yaliyo ficha sura zao. Nikaanza kujitazama, nikajikuta nikiwa sina nguo hata moja, huku mwili wangu unameremeta sana kwa mafuta ya kupikia niliyo mwagiwa mwilini mwangu.
 
“Mwanaharamu mkubwa wewe, uliye nipumbaza kutokana na meneno ya mwangu, nikakuamini. Nikakupenda na nikakujali kumbe ni mpelelezi, na siku zote huwa nachukia wapelekezi”
Baba Hawa alizungumza kwa hasira kali hadi mate kwenye mdogo wake yakawa yanamwagika mdomoni mwake. Woga wote ambao siku zote ninamuogopa huyu mzee, nikashangaa ukiwa unanitoweka moyoni mwangu. Nikajikuta nikicheka kwa dharau, baba Hawa akanitandika ngumi nzito ya tumoni iliyo nifanya nigugumie maumivu ya ndani kwa ndani.
 
“Ahaaaa haaaaa!!”
Niliendelea kucheka, huku nikijikaza tumbo langu.
“Nilikuambia huto toka ndani ya hii nchi, ukaniletea dharau si ndio?”
“Hivi wewe ni binadamu wa aina gani, wewe ni mtu wa aina gani usiye tambua uchungu wa familia. Eheheee……??”
“Ohooo siku zote ninapo agiza kazi yangu, sihitaji mtu kwenda kinyume na kile ninacho kipanga, ila wewe ukakiuka sheria zangu. Katika hilo sihitaji kukusamehe”
“Niueeeeeee, siogopi kufa, kwa maana mimi nimesha kufaa”
“Ohooo safi?”
Baba hawa akachukua fimbo aina ya mjeledi. Akasimama mita chache kutoka sehemu waliyo nifunga, pasipo kuwa na huruma ya aina yoyote akaanza kunichapa kwa nguvu. Nikaendelea kugugumia kwa maumivu makali sana, ila baba Hawa akaendelea kupitandika kwa mjeledi huu ambao akivuta basi anaondoka na nyama za mwili wangu.
“Wewe ulikuja nikupeleleza au?”
Sikumjibu chochote baba Hawa zaidi ya kumtemea mate yaliyo tua kwenye sura yake. Akaendelea kunitandika mijeledi, hadi mwenyewe akachoka kabisa.
“Hakikisheni munaimarisha ulinzi hapa na asiingie mtu yoyote”
“Sawa mkuu”
“Na musimfungue na wala asipate chakula cha aina yoyote wala maji”
“Sawa mkuu”
Baba Hawa akatoka katika chumba hichi. Nikatamani malaika mtoa roho, ashuke na kuichukua roho yangu, kwa maana hadi hapa nilipo fikia nimepabaya sana, sidhani kama ninaweza kurudi katika mapambano dhihi ya maadui zangu. Mwili wangu umejaa majeraha ambayo, yatachukua muda mwingi sana kupona. Nikaendelea kukaa huku miguu na mikono ikiwa imechanuliwa na kamba zake zimefungwa kwenye engo tofuati tofauti katika hichi chumba.
Hapakuwa na mwajeshi hata mmoja ambaye alinigeuzia sura yake kwa kunitazama, kila mmoja alibaki akiwa amesimama upande wake.
 
“Heii”
Nilizungumza kwa sauti ya kukoroma, nikiwa na lengo la kuwaita wanajeshi hawa walio jikausha huku wakiwa wamesimama kama milingoti.
“Hei mimi si mwenzenu, mutaishi kwa kufwata amri hadi lini?”
Niliendelea kuzungumza kwa kujikaza sana, huku damu zikiwa zinanimwagika mdomoni mwangu.
“Ni umasikini au nini, kukubali kuona kijama mwenze….nu nikifa kwa mateso kisa amri ya huyu mzee. NI kipi anacho tupa zaidi ya chukula, maladhi na nguo. Tumekuwa watu wakujitolea muhanga kwa ajili ya huyu mseng** mmoja. Ni moja wa kubadilisha mifuno ya akili zetu”
Nilizungumza maneno ya kuwahamasisha hawa wezangu wanao nilinda, ila sikuona dalili yoyote ya hata mmoja wao kunielewa kwa kile ninacho kizungumza.
Mlango ukafunguliwa akaingia baba hawa akiwa amebadilisha mavazi yake. 
 
“Za asubuhi wewe bweha”
Baba hawa alizungumza huku akinisogelea sehemu nilipo. Nikamtazama kwa macho ya dharau huku nikimpandisha na kumshusha.
“Kanileteeni maji, pilipili ya unga na chumvi”
“Sawa mkuu”
Mwanajeshi mmoja akatoka, hakuchukua muda mwingi sana akarejea akiwa na ndoo pamoja na mfuko mweusi. Akakabidhi baba Hawa mfuko mweusi huku ndoo ya maji akiiweka mbele ya baba Hawa.
Mzee huyu akaanza kuchanganya pilipili pamoja na chumvi kisha akaviweka kwenye ndoo hii yenye maji yaliyo jaa. Alipo rishika akaanza kunimwagia maji hayo mwili mwangu.
Hata kama mtu ni jasiri kiasi gani ila kwa  maumivu ninayo yapata kwenye majeraha yangu, nikatamani ardhi ipasuke niingine na inimeze.
 
“Kidume huwa hapigi kelele iweje leo unapiga kelele”
“KU** WEWEEE”
Nilimtukana baba Hawa, akaiweka ndoo chini kwa hasika. Akatembea hadi kwenye meza iliyomo ndani ya hichi chumba huku imejaa makorokocho, akachukua mkasi mrefu na wenye makali, akanisogelea, kisha akamshika jogoo wangu kwa mkono wake wa kushoto, akaupitisha mkasi katikati ya jogoo wangu na kuanza kumkata taratibu, jambo lililo nifanya niangue kilio kikali sana ambacho tangu kuzaliwa kwangu sikuwahi kulia kilo cha aina hiyo.

ITAENDELEA KESHO

Jeshi La Polisi Mwanza Lanasa Mtandao Wa Majambazi Sugu

0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza  limemkamata Jambazi mmoja sugu aitwaye Peter Thomas  Nyanchiwa  kwa kosa la wizi wa gari lenye namba T.122 DLY aina ya Toyota Costa mali ya Ismail Abdallah na kukamata silaha bastola aina ya Berete  yenye namba H44780Y, ikiwa na risasi kumi na mbili ndani ya magazini huko maeneo ya Runzewe Mkoani Geita.


Tukio hilo limetokea wiki moja iliyopita, hii ni baada ya mtuhumiwa tajwa hapo juu akiwa na wenzake wawili kukodisha gari hilo toka kwa mmiliki wa gari aliyop hapa jiji Mwanza kwa ajili ya kwenda kuwachukua watalii waliokuwa wameharibikiwa gari awapeleke mbugani kuendelea na utalii katika mbuga ya wanyama ya Serengeti.

Lakini walipofika Serengeti eneo la Nata  mtuhumiwa akishirikiana na wenzake wawili walimshusha dereva kwenye gari na kumpiga risasi kwenye maeneo ya taya kisha waliondoka na gari wakiamini kuwa  tayari amefariki dunia. Wananchi waishio jirani  na eneo hilo baada ya kusikia mlio wa risasi walikwenda eneo la tukio kutoa msaada  na kumkimbiza dereva huyo hospitali ya Wilaya ya Serengeti kisha walitoa taarifa Polisi.

Majambazi hao baada ya kutenda uhalifu huo waliondoka  na gari hilo kurudi walipotoka wakipitia barabara ya bariadi, Shinyanga, Kahama ambapo wamedai kuwa walikuwa wakielekea Nchini Uganda kwenda kuliuza. Wakati wakiendelea na harakati hizo Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza tulipata taarifa hizo na kwa kutumia kikosi chetu kabambe  na chenye uweledi wa hali ya juu na kushirikiana na wenzetu wa Mkoa wa Mara na Geita tulianza ufuatiliaji wa kina ambapo vijana wetu walifanikiwa kufukuza gari hilo maeneo ya Runzewe

Mkoani Geita waliliamuru kusimama lakini majambazi hao walianza kuwarushia risasi askari wetu .Lakini kutokana na umahiri wa askari  waliendelea kukabiliana na majambazi hao na baada ya majambazi hao kuzidiwa watuhumiwa wawili walifanikiwa kutoka kwenye gari na kutokomea porini na momja wao alikamatwa akiwa na silaha aina ya bastola (pistol) na risasi kumi na mbili. Pia upekuzi wa kina ulifanyika ndani ya gari hiyo yenye usajili namba T.122 DLY aina ya Toyota Costa ambapo tulikuta vitu vifuatavyo;
  1.     Gari iliyoibiwa namba  T.122 DLY aina ya Toyota Costa.
  2.     Magazini mbili za silaha aina ya AK 47, moja ikiwa na risasi 30 na nyingine ikiwa haina risasi.
  3.     Bastola aina ya Berete namba H44780Y
  4.     Leseni/kitabu cha bastola chenye namba 00097399
  5.     Passport namba AB362201 ya Peter Thomas Nyanchiwa.
  6.     Hati ya dharura ya kusafiria ya namba AB10528412 ya Rashidi Rashidi
  7.     Cheti cha Veta namba 35912 cha Abdallah Omary Shabani
  8.     Plate namba mbili nyeupe ya gari namba T.876 DMB aina ya Toyota Costa.
  9.     Kivuli cha kadi ya gari namba 6032015 ya gari namba T.876 DMB Toyota costa
  10.     Simu tecno mbili, simu fero moja na simu Samsung moja
  11.     Line za simu nane.
  12.     ATM Card tatu, moja ya CRDB na mbili za NMB
  13.     Vifaa vya kuvunjia -plaizi 1, pipe range 1, nyundo 1 na spanner 1.
  14.     Driving licence ya Peter Thomas.
  15.     Fedha kiasi cha TSH 1,330,000/=, za kusafishia njia
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza tunaendelea na upelelezi pamoja na mahojiano na mtuhumiwa, pindi uchunguzi ukikamilika Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani. Aidha msako mkali wa kuwatafuta wenzake waliotoroka bado unaendelea. Dereva aliyejeruhiwa kwa risasi anaendelea na matibabu na hali yake inaendelea vizuri.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza, tunatoa onyo kwa baadhi ya vijana wanaojihusisha kwa namna moja au nyingine na uhalifu tukiwataka waache kwani ni kosa la jinai, lakini pia wanaweza kujihatarishia maisha yao hivyo wafanye kazi zilizo halali za kujipatia kipato. Sambamba na hilo tunawasisitiza wananchi waendelee kutupa ushirikiano Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza ili tuendelee kuimarisha amani katika Mkoa wetu.

Katika tukio la Pili; Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza tumemkamata Mtu mmoja tapeli anayefahamika kwa jina la Nkwabi Samweli @ Kabinza, miaka 26, Mkazi wa Mtaa wa Pasiansi kwa kosa la kijifanya tabibu (daktari) wakati si daktari katika hospitali ya rufaa ya Bugando, kitendo ambacho ni kosa kisheria.

Tukio hilo limetokea tarehe 3/10/2018 majira ya saa 01:00hrs mchana, mara baada ya uongozi wa hospitali hiyo kupokea malalamiko toka kwa wagonjwa ya kuibiwa mara kwa mara wodini. Ndipo Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza kwa kushirikiana  na uongozi wa hospitali ya rufaa ya Bugando tuliweka mtego na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa akiwa chumba cha upasuaji na akiwa amevalia sare kama ambazo huvaliwa na madaktari  wakiwa chumba cha upasuaji (thieta).

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza tunaendelea na mahojiano na mtuhumiwa ili kujua alipopata sare hizo na jinsi alivyoingia katika chumba hicho cha upasuaji pindi uchunguzi ukikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza, tunatoa onyo kwa baadhi ya wananchi wenye tabia ya kujifanya watumishi wa serikali wakati sio waache kwani ni kosa kisheria na endapo mtu atabainika hatua stahiki za kisheria zitachukuliwa dhidi yake. Aidha na wale wote ambao waliwahi kuchukuliwa fedha wafike kituoni ili kumtambua kwani tapeli huyu anachafua jina la hospitali yetu ya rufaa ya Bugando.

Katika tukio la Tatu; mtoto wa kike aliyefahamika kwa jina la Solile Emmanuel, miaka 5, amefariki dunia katika  ajali ya moto iliyounguza nyumba yao ya chumba kimoja na sebule iliyojengwa kwa tofali za tope na kuezekwa kwa bati na kuteketeza mali na vitu vyote vilivyomo ndani ya nyumba hiyo huko mtaa wa Nh’obola Wilayani Nyamagana.

Tukio hilo limetokea tarehe 03/10/2018 majira ya saa 17:00 jioni, wakati marehemu alipoachwa peke yake chumbani akila chakula huku wazazi wake wakiwa bustanini wakilima. Inadaiwa marehemu alikuwa akichezea njiti ya kiberiti na kupelekea kuwasha moto ulioanza kuunguza godoro, nguo na hatimaye kushika nyumba nzima hali iliyopelekea marehemu kukosa hewa  na baadae kufariki dunia.

Polisi tulifika kwa haraka eneo la tukio na kushirkiana na wananchi kutoa msaada lakini moto ulikuwa tayari umepoteza uhai wa mtoto na kutekeza mali na vitu vyote katika nyumba hiiyo. Thamani ya mali na vitu vilivyoteketea katika ajali hiyo bado haijafahamika. Mwili wa marehemu tayari umefanyiwa uchunguzi na kukabidhiwa kwa ndugu wa marehemu kwa ajili ya mazishi.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza, tunawataka na kuwasisitiza wazazi na walezi kuwa waangalifu na watoto wakati wote, waache tabia ya kuwaacha watoto kwenye nyumba peke yao kwani kunaweza kuhatarisha usalama wao na baadae kupata majeruhi au kufariki dunia.

Katika tukio la nne; Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza linamshikilia kijana mmoja mwizi/Jambazi  anayefahamika kwa jina la Jackson Elias @ Longoko, miaka 20, mkazi wa mtaa wa Shamaliwa Igoma, kwa kosa la kuvunja nyumba yenye mashine ya kusaga usiku na kuiba mota tatu katika kijiji cha Lugeye Wilayani Magu, kitendo ambacho ni kosa kisheria.

Tukio hilo limetokea tarehe 28/09/2018 majira ya saa 23:00hrs usiku, ambapo mtuhumiwa tajwa hapo juu akishirkiana na wenzake watatu walivunja nyumba hiyo usiku na kuiba moto tatu. Wananchi walitoa taarifa polisi ambapo tulifanya ufuatiliaji wa haraka na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa watatu na tayari wamefikishwa mahakamani wakiwa na mota tatu walizoziiba, huku mtuhumiwa tajwa hapo juu akifanikiwa kutoroka.

Polisi tuliendelea na msako mkali wa kumtafuta mtuhumiwa aliyetoroka, ndipo tarehe 03/10/2018 majira ya saa 11:00hrs asubuhi katika mtaa wa Shamaliwa Igoma tulifanikiwa kumkata mtuhumiwa akiwa nyumbani kwake. Polisi tulifanya upekuzi hapo nyumbani kwake na kufanikiwa kukamata vitu vifuatavyo;
  1.     Bendera moja ya Taifa.
  2.     Mkasi mmoja mkubwa wa kukata vyuma na mabati.
  3.     Bisibisi moja
  4.     Nondo moja iliyochongwa
  5.     Plaizi moja
  6.     Tindo moja ya kufungulia kufuli.
Polisi tunaendelea na mahojiano na mtuhumiwa, pindi uchunguzi ukikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza, tunatoa onyo na kuendelea kusisitiza wananchi wenye tabia ya kiuhalifu kuacha mara moja kwani Mkoa wa Mwanza si mahali pake hivyo waache  na wajihusishe na shughuli halali za kuwaingizia kipato. Pia tunawataka wananchi waache kumiliki nyara za serikali kwani ni kosa  kisheria na atakae bainika atashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Katika tukio la tano; watu wawili  wanashikiwa na Jeshi la Polisi kwa kosa la kujifanya watumishi wa serikali kisha kuwatapeli wananchi wawili feedha kiasi cha laki moja na elfu sitini (TSH 160,000) huku wakiendelea kudai kiasi cha milioni moja ( TSH 1,000,000) ili wawapatie nafasi watoto wao ya kwenda kwenye mafunzo ya Uaskari katika chuo cha taaluma ya Polisi Moshi (CCP) na mwingine mtoto wake aweze kwenda kwenye chuo cha udaktari  cha Haidom kilichopo Mkoani Manyara , kitendo ambacho ni kosa kisheria.

Tukio hilo limetokea tarehe 03/10/2018 majira ya saa 13:30hrs mchana, katika mtaa wa Nyegezi stand, hii ni baada ya polisi kupata taarifa toka kwa raia wema kwamba katika mtaa tajwa hapo juu wapo watu wanaowatapeli wananchi kwa kujifanya watumishi wa serikali. Polisi tulifanya ufuatiliaji katika eneo hilo  na kuweka mtego na baadae tulifanikiwa kuwakamata watuhumiwa wawili.

Watuhumiwa waliokamatwa ni 1.Elias Malelemba @ Mayombya, miaka 47, fundi ujenzi, Mkazi wa Dar es Salaam na 2.. Sharifu Hamis @ Mgene, miaka 58, Mkazi wa Mkarama Mkoani  Singida. Polisi tunaendelea na upelelezi pamoja na mahojiano na watumiwa wote, pindi uchunguzi ukikamilika watuhumiwa wote wawili watafikishwa mahakamani.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza, tunatoa onyo kwa watu wanaodhani kuwa Mwanza ni sehemu ya kufanya uhalifu kuwa waache kwani tutawakamata na kuwashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Imetolewa na;
Jonathan Shanna – ACP.
Kamanda wa Polisi (M) Mwannza.
06 October, 2018.

Waziri Ndalichako Amtumbua mkuu wa chuo cha Ualimu Shinyanga

0
0
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amemuagiza katibu mkuu wa wizara hiyo kumuondoa mara moja katika nafasi yake Mkuu wa Chuo cha Ualimu Shinyanga (SHYCOM), Paschal Highmagway kutokana na kutoa taarifa ya uongo ya kumsifia mkandarasi ambaye ameshindwa kukamilisha ujenzi.
 
Agizo hilo alilitoa jana Oktoba 5, 2018 alipotembelea chuo hicho na kukagua ujenzi wa majengo mbalimbali pamoja na ukarabati unaofanywa na wakandarasi wawili tofauti ambao ni Kampuni ya Masasi iliyokwisha kamilisha kazi na mkandarasi Afriq Engeneering yenye makao yake jijini Dar es salaam ambayo haijakamilisha.

Profesa Ndalichako alisikitishwa na taarifa aliyoitoa mkuu wa chuo hicho akionyesha wazi kumsifia mkandarasi Afriq Engeneering kwa kazi nzuri, ambaye tangu apewe mkataba  Agosti 22 mwaka 2016 hakuna hata jengo alilokamilisha huku mkataba wake ulikuwa unamalizika Aprili 5, 2018 huku Serikali ilimuongezea muda hadi Septemba 15, 2018.

Kutokana na hali hiyo, Profesa Ndalichako amemuomba Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Diwani Athuman kutuma wataalamu wake kwenda kuchunguza ujenzi wa mradi huo unaofanywa na Afriq Engeneering unaoonyesha dalili za wazi za kutawaliwa na vitendo vya rushwa.
 
“Nitamuomba mkurugenzi mkuu wa Takukuru nchini (Diwani) kuanza kuchunguza mradi huu wa Shinyanga pia maofisa wa wizara yangu waliohusika kusimamia mradi huu nao wachunguzwe,” alisema

 “Haiwezekani huyu mkandarasi ameshapewa onyo halafu wamesikia na kuja huku Oktoba 2, 2018 wakamlipa Sh244.8 milioni kitendo hicho kimenisikitisha sana,” aliongeza

Alisema wale wote waliotumia fedha hizo kinyume na maelekezo watazitapika huku akionyesha kushangaa na kusikitishwa kitendo cha mkuu wa chuo kumsifia mkandarasi ambaye ameharibu kazi.

 “Mradi huu ninakuagiza mkandarasi AFRIQ  Engeneering kukamilisha majengo yote ndani ya mwezi mmoja kuanzia sasa ufanye kazi usiku na mchana maana Serikali imetumia Sh9.4 bilioni kwenye ujenzi huo na mkandarasi ambaye hajakamilisha kazi tayari ameshalipwa Sh2.7 bilioni,” amesema.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images