MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588 “KU** WEWEEE”
Nilimtukana baba Hawa, akaiweka ndoo chini kwa hasika. Akatembea hadi kwenye meza iliyomo ndani ya hichi chumba huku imejaa makorokocho, akachukua mkasi mrefu na wenye makali, akanisogelea, kisha akamshika jogoo wangu kwa mkono wake wa kushoto, akaupitisha mkasi katikati ya jogoo wangu na kuanza kumkata taratibu, jambo lililo nifanya niangue kilio kikali sana ambacho tangu kuzaliwa kwangu sikuwahi kulia kilo cha aina hiyo.
ENDELEA
Mlango ukafunguliwa hadi baba Hawa akasitisha zoezi la kumkata jogoo wangu japo alisha anza kumbana taratibu. Macho yetu yakamshuhudia Hawa akiingia kwa kasi ya ajabu, huku macho yake akiwa amemtumbulia baba yake.
“Umefwata nini humu?”
“Baba hii sio haki, huyu Dany unakumbuka kwamba unamchukulia kama mwanao wa kiume iweje leo unamtesa kwa kiasi hichi”
“Unatambua kwamba mtu mwenye dharau, tena ni mpelelezi kwangu huwa hana msamaha”
“Hata kama, unatambua ni jinsi gani Dany alivyo kuwa mtiifu kwake, hata wawo la kwenda kuiba chakula cha wakimbizi na kuwalisha wanajeshi wako, lililotoka kwako. Tazama hali halisi ya matatizo yake aliyo kueleza, tazama hali halisi ya shida yake alivyo izungumza kwako, so leo hii unaona hakuna umuhimu katika hilo si ndio.?”
Hawa alizungumza kwa sauti ya msisitizo huku akimtazama baba yake usoni mwake. Baba hawa akaka kimya pasipo kujibu kitu chochote kwa mwanye huyu.
“Hata kama ingekuwa ni mimni, wewe umeuliwa katika mazingira ya kutatanisha, na mtu mwengine ananijibu kama ulivyo kuwa unamjibu Dany, lazima ningebadilika na kuwa mkali kwako”
Maneno ya Hawa nikaanza kuhisi yanaweza kubadilisha msimamao wa huyu mzee, kwa maana akinikata jogoo wangu ndio basi tena, ujanja katika nyanja za vitumbua nduo nitausikia kwenye bomba, yaani ni bora hata unipige risasi kuliko kukata jogoo wangu ambaye kwa mara kadhaa ameniraisishia katika vitu vigumu kwenye maisha yangu.
Hawa akanitazama jinsi mwili wangu ulivyo chakaa kwa majeraha ya vidonda ambavyo nimevipata kwa kuchapwa kwa mjeledi.
“Mshusheni”
Hawa aliwaamrisha wanajeshi walio simama ila hakuna hata mmoja aliye weza kutii amri yake.
“NIMESEMA MSHUSHENI MWENZENUUU”
Hawa aliendelea kuzungumza kwa kufoka, ila wanajeshi wote wakabaki wakiwa wamesimama kikakamavu kama hawasikii kile anacho kizungumza.
“Toka humu ndani”
Baba Hawa alizungumza kwa ukali hadi mwili mzima ukanisisimka. Hawa akamtazama baba yake kwa mshangao mkubwa sana.
“Baba!!”
“Mkamateni na mumtoe humu ndani, hakikisheni munampeleka katika chumba cha uangalizi na anakaa humo hadi mimi mwenyewe nije”
Wanajeshi wakaifwata amri ya baba Hawa, wakataka kumkamata Hawa, ila kwa ishara ya mkono akawazuia wasimshike mavazi yake. Wakaongozana na Hawa wakiwa wamemuweka katika ulinzi mkali. Mlango ndani ya chumba hichi ukafungwa, nikabaki mimi na baba Hawa.
Baba Hawa hakunisemesha kitu chochote zaidi ya kuchukua pasi iliyopo mezani, akachomeka waya wa pasi hiyo kwenye soketi ya umeme. Akaiwasha, hayo yote yakiendelea, moyo wangu, unanienda kasi, kiasi kwamba naanza kumuona malaika mtoa roho akiranda randa katika eneo hili la chumba, akisubiria muda wake tu, kuja kuichukua roho yangu. Pasi ilipo kolea moto, baba Hawa akapiga hatua hadi katika sehemu nilipo, akazunguka nyuma yangu. Nikafumba macho taratibu kwa maana maumivu ninayo kwenda kupata hapa ni makali zaidi.
Katikati ya mgongo wangu, nikasikia uzito wa pasi hii, jinsi inavyo unguza kwenye mwili wangu. Machozi yaliyo anza kutulia kidogo, yakaanza kunibubujika kwa wingi sana, maumivu yakazidi kiwango ambacho binadamu hufikia, taratibu nikajikuta nikipoteza fahamu na nisijue kinacho endelea kuanzia hapo.
***
Mtetemeko mkali katika kifua changu, ukanifanya kuyafumbua macho yangu kwa haraka sana huku nikigema. Nikaona kundi la madaktari wakiwa wamanizunguka, huku daktari mmoja akiwa ameshika mashine ya umeme inayo tumia katika kustulia mapigo ya moyo.
“Ameamka”
Nesi mmoja alizungumza, wakaanza kunihudumia, huku mashine ya kuhesabu mapigo ya moyo ikiendelea kulia kijimlio kinacho ashiria mapigo yangu ya moyo kwamba yapo sahihi. Sindano za ganzia ambazo wamenichoma, zinanifanya nisijisikie chochote wanacho kifanya kwenye mwili wangu. Wakaendelea kufanya kila wanacho kifanya katika mwili wangu.
“Dokta chumba cha ICU kipo tayari”
“Haya sasa ni muda wa kumtoa”
Taratibu wakanishika vizuri na kuniweka katika kitanda kingine cha matairi, manesi wawili wanao kiongoza kitanda changu, mmoja akiwa mbele na mwingine akiwa nyuma anakisukuma. Wakanitoa katika chumba hichi na kunipeleka nisipo pajua. Nikaingizwa kwenye chumba ambacho kipo kimya sana na kina mitambo kadhaa ya kuhemea na kuhesabu mapigo ya moyo. Wakaanza kuniwekea kifaa maalumu cha kuhemea kwenye mdomo wangu, kisha wakaniweka vifaa maalumu kwenye kifia changu ambavyo vinasaidia mimi kuhema.
Nikatamani kuzungumza ila nikajikuta nikishindwa kabisa, menesi hawa baada ya kuniandaa, wakatoka katika chumba hichi na kuniacha mwenyewe. Nikajaribu kukumbuka kitu kilicho tokea hadi mimi kufika katika hospitali hii ambayo sifahamu ipo nchi gani, ila sikuweza kukumbuka chochote.
Muda na siku zikazidi kwenda, huku nikiendelea kuhudumiwa na manesi pamoja na madkatari katika hii hospitali. Kila siku nikatamani kufahamu imekuwaje kufika katika eneo hili, ila sikuweza kupata nafasi nzuri ya kumuuliza nesi wala daktari kwa maana kila wakija, wananihudumia na kuondoka zao.
“Habari yako bwana Dany?”
Daktari ambaye mara nyingi huwa anakuja kunihudumia alizungumza na mimi kwa mara ya kwanza tangu kuletwa katika hichi chumba.
“Salama”
Nilijibu kwa sauti ya unyonge huku nikimtazama usoni.
“Leo ni siku ya ishirini na mbili tangu kuletwa katika hospitali yetu. Kwa utaratibu wa kazi na huduma zetu pamoja na matatizo ambayo ulikuwa nayo. Ilitubidi tusikusemeshe ndani ya siku zote hizo ili tusiuvuruge mfomo wako wa ubongo ambao kidogo ulipata itilafu, ila tunashukuru Mungu kwa kupindi hicho chote mfumo wako wa ubongo umeweza kurudi katika hali ya kawaida”
Daktari alizungumza huku akinitazmaa usoni mwangu.
“Nilikuwa na tatizo gani?”
“Ubongo wako ulipata itilafu ya kupoteza uwezo fulani wa kukumbuka matukio ya nyuma, ila kwa siku zote hizi ishirini na moja tuliozo kaa kimya pasipo kuzungumza na wewe, ubongo umeweza kukaa sawa na hali yako kwa sasa inaendelea vizuri”
“Majeraha yote katika mwili wako yamesha funga kilicho baki hivi sasa ni kukupa dawa ambazo zinaweza kufuta majeraha hayo yote”
“Dokta ni nani aliye nileta katika hii hospitali?”
“Hakuhitaji kujulikana, ila aliweza kusema tukuhudumie hadi upone, kisha yeye atakuja. Ila garama zote za matibabu ameweza kuzilipa”
“Ni mwanamke au mwanaume?”
“Ni mwanaume”
Nikabaki nikiwa na maswali mengi kichwani mwangu kwa manaa sifahamu ni mwanaume gani ambaye anaweza kunisaidia mimi kutoka katika kifo nilicho kikosa kosa kwa baba Hawa.
‘Au ni baba Hawa? Hapana haiwezekani akawa yeye?’
Nilijiuliza maswali kadhaa kichwani mwangu, ila sikupata jibu sahihi ambalo lingeweza kunisaidia.
“Hapa nipo wapi?”
“Upo Nairobi Kenya, ulitetwa majira ya usiku, siku ishirini na mbili zilizo pita. Mwili wako wote ulijawa na majeraha mengi, tueyashuhulikia na sasa yanakwenda kuisha”
“Dokta je mbo** yangu?”
Niliuliza kwa shauku kubwa sana.
“Hahaa haina tatizo, japo kulikuwa na kijitatizo gidogo, ila sasa hivi ipo sawa sawa. Na tumeiweza kuifanyia kazi ambayo itakuwa bora zaidi ya ilivyo kuwa mara ya kwanza”
“Kweli dokta?”
Niliuliza huku nikiupeleka mkono wangu wa kushoto kwenye jogoo wangu, nikaanza kumpapasa, kweli nikahisi mabadiliko kidogo kwa maana, kitendo cha kumshika kidogo akaanza kusimama huku akiwa na uzito pamoja na urefu ambao ni tofauti na mwanzoni. Daktari akaachia tabasamu pana usoni mwake huku akitingisha tingisha kichwa. Nikashusha pumzi nyingi huku nikiwa nimejawa na furaha kubwa moyoni mwangu.
“Dawa ambazo tutakupatia zitakusafisha makovu yote mwilini mwako kwa siku sana. Kwa hiyo tungekuomba uwe mvumilivu kwa manaa umesha pona kabisa”
“Sawa sawa dokta, nashukuru kabisa”
“Unaweza kushuka kitandani na kutembea tembea eneo la hospitali, ili uweze kuuchamsha changamsha mwili”
“Sawa sawa dokta”
Nikajikuta nikishuka kitandani huku nikiwa na furaha siku zote nilizoea kushuka kitandani na kuingia chooni au bafuni ambavyo vyote vipo ndani ya hichi chumba changu. Nikavaa vijindala ambavyo siku zote ninavivaa. Nikaongozana na daktari huyu hadi nje ya hospitali hii yenye majengo makubwa sana na yakupendeza.
“Hii hospitali mara nyingi huwa tunahudumia wagojwa walio patwa na majeraha makubwa ambayo wanaamini kwamba hawawezi kupona, ila wakija hapa wanapona kabisa na wanarudi katika hali zao za kawaida. Hata mtu akija amekatika mkono, kuna mbinu za kidaktari ambazo tunazifanya hadi mtu huyo mkono wake tunaweza kuurudisha”
“Dokta ina maana hata mkono uwe umekatika katika munaweza kuurekebisha?”
“Ndio tunaweza, kila kitu kinawezekana, yaani kitu tunacho kihangaikia sasa hivi ni kuweza kutengeneza roho ya binadamu, tukifanikiwa katika hilo basi tutakuwa matajiri kabisa”
Tuakiwa katika moja ya bustani ambayo pembeni yake kuna barabara, likapita gari jeusi la kifahari, likafika maeneo ya maegesho, likasimama wakashuka walinzi wawili, mmoja akapiga hatua hadi mlango wa nyuma wa gari hilo, akafungua mlango wa gari hilo. Akashuka kijana mmoja aliye valia suti nyeupe pamoja na miwani ya macho.
“Ohoo tena mtu aliye kuleta yule pale”
Daktari alizungumza huku akiondoka, ikabidi kumfwata kwa nyuma huku nikijaribu kumtazama kijana huyu ambaye inasadikika kwamba amenileta katika hii hospitali. Kusema kweli sijawhai kumuona siku hata moja kwenye maisha yangu. Tukafika hasi sehemu alipo wakapeana mikono na daktari huku wakiwa katika furaha kubwa sana.
“Ohoo hali ya Dany ninaiona jinsi ilivyo kamili gado”
“Yaaa tumejitahidi katika uwezo wetu wote na tumefanikiwa kufanya leo hii kuwa vizuri”
“Dany naamini utakuwa unanishangaa, ila tukikaa tutazungumza mambo mengi na utanijua mimi vizuri”
“Sawa sawa hakuna tabu”
Nikaendelea kumtazama huyu jamaa ambaye kwa haraka haraka anaonekana kunipita kiumri, kwa miaka kadhaa.
“Daktari kilicho bakia kwa Dany ni kitu gani?”
“Ni kufuta haya majeraha, atakaa hapa hospitali hadi siku saba, baada ya hapo tutaweza kumruhusu kuondoka”
“Ohooo sawa sawa, mimi kwangu hilo halina tatizo kabisa. Ila Dany tunaweza kupata muda wa kuzungumza mimi na wewe”
“Sawa kaka”
“Twende tukakae pale kwenye bustani”
Nikatembe na jamaa huyu hadi kwenye bustani, huku walinzi wake wakiwa nyuma yake. Tukaka kwenye moja ya benchi zilizo tengenezwa kwenye hii bustani. Jamaa huyu akatoa simu yake mfukoni, akaanza kutazama tazama baadhi ya vitu kisha akanipatia simu yake. Nikaiona picha ya K2 ikiwa katika kioo cha simu yake.
“Naamini kwamba unamfahamu huyo vizuri?”
“Yaa ninamfahamu, ila kabla hatujasonga mbele ninahitaji kuweza kukufahamu wewe ni nani, na kwa nini uliamua kunisaidia?”
“Usiwe na haraka mdogo wangu, kunifahamu utanifahamu tuu. Ila kwanza tuzungumzie kuhusiana na swala la huyu K2. Nimeweza kufwatalia wewe tangu upo katika kisosi cha NSS. Hadi walivyo kubambikia kesi, na kukufunga gerezani. Kipindi chote hicho nilikuwa nikikufwatilia kwa ukaribu sana pasipo wewe kuweza kufahamu kama unafwatiliwa.”
Nikastuka sana kumsikia jamaa akizungumza maneno kama haya, kwa maana kila anacho kizungumza ni ukweli na kimesha nitokea kwenye maisha yangu miaka kadhaa ya nyuma.
“Sikukata tamaa ya kukudwatilia kwa kipindi cha miaka yote hii, kwa manaa hata mfumo wa utawala nchini Tanzania kwa sasa umebadilika”
“Umebadilika. Tangu lini?”
“Hahaa ni kajihistoria kimoja kirefu japo si sana, ila mfumo wake umebadilika. Raisi ailiyo sasa madarakani sio yule ambaye unamjua.”
“Kwa sasa Tanzania inatawaliwa na mwanamke, jambo ambalo hakuna anaye penda kuliona nchi kubwa kama Tanzania ikitawaliwa na mwanamke”
“Ngo….ngoja kwanza, unataka kuniambia kwamba Tanzania raisi sasa hivi ni K2?”
“Yaaa na ameingia madarakani hivi juzi juzi tu kwa hiyo kuna kazi kubwa mbayo ipo mbele yetu. Picha hiyo unayo iona kwa sasa ni jinsi K2 alivyo ingia madarakani kama raisi”
Nilijihisi kichwa kikinigonga kwa maumivu, mwanamke mshenzi aliye niharibia mfumo wa maisha yangu leo hii anakuwa raisi wan chi yangu kirahisi namna hii, kusema kweli haiwezekani.
“Naamini unatambua kwamba familia yako kwa sasa ipo mbinguni?”
“Yaaa”
“Na pia nina imani una hisi kuwa kuna mtu au watu wapo nyuma ya tukio la mauji ya familia yako?”
“Ndio”
“Basi sogeza picha ya mbele utamuona muhusika wa mauaji ya familia yako”
Nikasogeza picha ya mbele katika simu hii. Nikamuona mwanaume mmoja ambaye ndio mara yangu ya kwanza kuweza kumuona.
“Huyu ni nani?”
“Anaitwa EDDY GODWIN, huyu ndio mster plan wa maujia ya famili yako. Akiwa bega kwa bega na K2 ambaye kwa sasa ni mtu na mke wake?”
Maneno ya huyu jamaa yakanifanya nibaki nimemtumbulia macho, nisielewe ni kitu gani kinacho endelea.
“Naitwa JONH ni mkuu wa D.F.E”
Jamaa huyu alizungumza huku akinipa mkono wake wa kulia, huku sura yake ikiwa imejawa na tabasamu pana, nikabaki nikiwa ninautazama mkono wake pasipo kuupokea kwa maana bado sielewi ni kitu gani ambacho kinaendelea.
AISIIIII……….U KILL ME 94
Taratibu nikaunyoosha mkono wangu wa kulia na kuukutanisha na mkono wake. John akaonekana kuwa na furaha sana baada ya kuukutanisha mkono wangu na mkonno wake.
“Samahani nina swali moja”
“Uliza tu Dany”
“D.F.E ndio nini kwa maana sijaelewa?”
“Ohoo kirefu chake Destination of my enemies. Kundi hili muasisi wake anajulikana kwa jina mzee Godwin, mtoto wake ndio huyo Eddy Godwin”
“Sasa mimi hapa nitahusika kwa jambo gani?”
“Tutayazungumza, kikubwa ni hali yako kuweza kuwa sawa kwa kipindi hichi”
“Na ulikuwaje nikatoka katika mikono ya Al-Shabab, wakati nilikuwa katika hati hati ya kupoteza maisha?”
“Ni mengi sana yametokea katika wiki hizi mbili tatu ila usiwe na shaka kila jambo litakwenda kuwa sawa. Umenielewa Dany?”
Ikanibidi kutingisha kichwa tu kwa ajili ya kumridhisha John ila kusema kweli sijaelewa jambo hata moja.
“Utabaki chini ya uangalizi wa madaktari, baada ya wiki moja niakuja rasmi kukuchukua”
“Sawa”
Tukasimama kwenye benchi tulilo kalia. Taratibu tukarudi hadi sehemu tulipo muacha daktari.
“Dokta hakikisha mgonjwa hali yake inakuwa sawa”
“Usijali bosi, tutahakikisha kwamba anapona na kuwa fiti zaidi ya hapo mwazo”
“Shukrani dokta”
John na walinzi wake wakaingia kwenye gari na kuondoka, wakaniacha nikiwa nimesimama na daktari huku tukilisindikiza gari lao jinsi linavyo toka getini.
“Huyu John, miguu na mikono yake yote tuliipandikiza sisi, alikuwa amekatwa kabisa”
“Sijakuelewa?”
“Yaani hakuwa na miguu wala mikono, ila tulimfanyia Oparesheni, ambayo tulipandikiza miguu na mikono yake na kwa sasa kama unavyo weza kumuona anatembea yeye mwenyewe”
“Mmmm!!”
“Yaaa hii hospitali yetu ni mwisho wa matatizo”
“Sawa”
Tukaendelea kuzunguka katika maeneo haya ya hii hospitali huku akili yangu ikiwa na kazi ya kuhakikisha kwamba ninayahifadhi maeneo yote kwenye kumbukumbu ya kichwa changu, kwa maana hasira ya kulipiza kisasi kwa K2 bado ipo pale pale, na wala sihitaji mtu wa aina yoyote kuweza kunisaidia wala kuwa chini yake katika kulitekeleza azimio langu.
Siku zikazidi kusonga mbele nikiendelea kupatiwa matibabu ya kuweza kufuta makovu yaliyo jaa mwilini mwangu. Wazo la kutoroka katika hii hospitali taratibu likaanza kunijia kichwani mwangu. Zikiwa zimebaki siku tatu kabla ya kutimia siku saba, nikaanza kuchunguza mfumo mzima wa magari yanayo ingia na kutoka katika hii hospitali. Kuna gari moja la mataka taka ambali kila ifikapo saa ukumi na mbili asubihi linakuja kwenye hii hospitali na linaondoka hospitalini hapa saa moja asubuhi, na huwa getini halikaguliwi kabisa.
‘Hili ndio litanifanya mimi kuondoka hapa’
Nilisema huku nikilitazama gari hili linavyo tokomea nje ya geti. Nikarudi chumbani kwangu baada ya kumaliza kufanya mazoezi mepesi ya viongo. Nikaingia bafuni na kuanza kuoga taratibu, huku nikiwaza maneno ya John.
‘Haiwezekani K2 kuwa raisi wa Tanzania, kwanza ameanzia wapi?’
Nilijiuliza huku nikiyasikilizia maji ya bomba la mvua jinsi yanavyo mwagika mwalini mwangu, sikupata picha jinsi nchi yangu ya Tanzania hivi sasa jinsi inavyo ongozwa.
‘Nitajua mbele ya safari’
Nilizungumza huku nikifunga maji ya bomba hili, nikachukua taulo na kujifunga kiunoni mwangu, nikasimama mbele ya kioo kilichopo humu bafuni, nikajitazama kila kona ya mwili wangu, makovu ambayo yalikuwepo, sasa yananza kupotea, na mengine yamepotea kabisa. Misuli iliyo jijenga vizuri kwenye mwili wangu, bado ipo katika hali nzuri ya kuridhisha, na wala sijanenepa kwa siku hizi nilizo kaa kitandani nikiuguza majeraha yangu.
Nikatoka bafuni na kurudi chumbani, nikamkuta nesi ambaye kila asubuhi huwa ananiletea kifungua kinywa na baadhi ya dawa.
“Habari yako dada Linda”
“Salama tu, eheee nilijua upo nje?”
“Hapana, nilikuwa nina oga oga”
“Naona sasa makovu yako yanapotea?”
“Yaa kweli dawa zenu zinasaidia”
“Kweli kikubwa ni kuhakikisha kwamba unafwata masharti ya dawa jinsi yanavyo hitaji. Tena leo nimekueletea mafuta ambayo ukipaka yatasaidia sana ngozi yako kuondoa makovu haraka iwezekanavyo”
“Kweli?”
“Yaa haya hapa”
Nesi Linda akanipatia mafuta ambayo yamekaa kama losheni, nikaanza kuyasoma taratibu na kweli yameandikwa yanasaidia katika kufuta makovu ya mwili.
“Sasa haya ninapaka kwa siku mara ngapi?”
“Pale unapo maliza kuoga basi unapaka”
“Inabidi uwe unanipaka kwa maana kama huko mgongoni mimi sinto weza kujipaka”
“Usijali lala kifudi fudi nikupake”
Nikajilaza kitandani huku nikiwa nimelalia tumbo. Nesi Linda akachukua mafuta kiasi akayamimina kwenye kiganja chake cha mkono wa kulia kisha akaanza kunipakaza mwilini mwangu taratibu. Mikono ya nesi Linda yakaufanya mwili wangu kusisimka sana, hadi nikaanza kujitingisha.
“Dany vipi?”
“Mikono yako ina nisisimu”
“Weee acha utani”
“Kweli dada Linda”
“Mimi mke wa mtu bwana”
“Ahaa kwani mke wa mtu umefungwa na kufulia”
“Hahahaaa Dany kumbe mjinga sana eheee”
Nesi Linda alizungumza huku akicheka kwa maana siku zote amezoe kuniona nikiwa mpole na mkimya sana.
“Ndio ukweli, ungekuwa mke wa mtu alafu amekufunga kufuli hapo sawa, ila ni mke wa mtu alafu ipo kama ilivyo…….”
“Ipo nini?”
“Si nanilio”
“Nanilio nini?”
“K***”
“Yesu wangu, Dany kumbe wewe ni muongeaji ehee?”
Nikajigeuza na kulala chali huku nikimtazama nesi Linda usoni mwake. Nikayashusha taratibu macho yangu hadi kifuani mwake kwenye chch zilizo jazia kiasi, sikuishia hapo nikazidi kushuka chini hadi kwenye kiuno chake kilicho shikilia hispi mbili zilizo jazia japo zimefunikwa na koti refu jeupe alilo livaa ila zimetanuka vizuri.
“Dany unaniangalia nini jamani, hadi unanitisha”
Sikutaka kumjibu chochote, nikamshika mkono na kumvuta hadi kifuani mwangu, mkono wangu wa kushoto nikaupitisha kwa haraka kiunoni mwake. Tukabaki tumetazamana kwa macho yenye matamanio.
“Dany nimeolewa na ndoa yangu bado ni changa sana”
Nesi Linda alizungumza huku akinionyesha vidole vyake vya mkono wa kushoto, huku kidole kimoja kikiwa kimevishwa pete ya dhahabu ambayo ni ya ndoa.
“Kwa leo”
“Mmmm Dany”
“Noo, nani atakaye jua, utamuambia mume wako kwamba umenipa penzi?”
Nesi Linda akaka kimya akikosa cha kuzungumza, taratibu akayafumba macho yake, moyoni mwangu nikajawa na furaha kwa maana mpango wangu unaanza kuzaa matunda taratibu taratibu. Mkono wangu wa kushoto ukawa na kazi ya kucheza na kiuno chake huku nikikiminya taratibu. Nikazipeleka lipsi zangu hadi kwenye lipsi zake, nikaanza kumnyonya kwa fujo jambo lililo mfanya nesi Linda kulegea kisawa sawa. Nikamgeuza kwa haraka na kumlaza kitandani. Kwa haraka nikashuka kitandani na kuufunga mlango wangu kwa ndani, uzuri wa chumba changu kipo gorofani kwa hiyo hakuna haja ya kufunga pazia.
Nikarudi kitandani na kuendelea kumnyonya nesi Linda midomo yake ambayo ni milaini sana. Ndimi zetu zikawa na kazi ya kupigana pigana kwenye midomo, hapa ndipo nilipo amini kwamba ndoa ni bwebwe tu.
Nesi Linda yeye mwenyewe akaanza kuvua nguo zake haraka haraka huku akionekana kuhitaji kupata kile ambacho kipo mbele yetu sote wawili. Nesi Linda akanivuta taulo langu, nikabaki kama nilivyo zaliwa, taratibu akaanza kumshika jogoo wangu, aliye simama kidedea. Nikaanza kumuonyesha utundu wangu nesi Linda. Mikono yangu na ulimi wangu, vikawa na kazi ya kupita kila sehemu ya mwili wake. Nilipo muona amesha fikia hatu ya kumuhitaji jogoo wangu aweze kumla kitumbua chake, basi sikuwa na kipingamizi.
Taratibu jogoo wangu ambaye kidogo ameongezeka urefu na ujazo, akaanza kuzama kwenye kitumbua cha nesi Linda.
“Dany taratibu pleaseee”
“Ok”
“Usiingize yote, utanichana”
Nesi Linda alizungumza kwa sauti nyororo, nikafanya kama anavyo hitaji, kwa mana ninahitaji kumpa burudani kabambe. Kilia mudu unavyo zidi kwenda ndivyo jinsi nesi Linda alivyo zidi kumfurahia jogoo wangu na kutamani azidi kuingia ndani. Kwa mara zaidi ya nne, nesi Linda akawa analalamika kwamba anafika kileleni, ila kwa upande wangu, ndio kwanza ninazidisha kasi. Hadi ninawasikia waarabu weupe wakihitaji kutoka, nesi Linda amesha fika kileleni mara ambazo hata sikumbuki ni ngapi. Waarabu wangu nikawatolea kwenye kifua chake na kumfanya nesi Linda afurahi sana.
“Ahaa Dany mmmmmm”
“Nini?”
“Sijawahi kufika kileleni tangu nizaliwe”
“Heeee”
“Haki ya Mungu vile. Yaani leo ndio mara yangu ya kwanza kufikishwa kileleni na mwamaume”
“Mmmm mumeo ana kazi gani kwako?”
“Ahaa unajua hawa wanaume wetu wa hapa Kenya, wanaweka kusoma mbele na kazi ila kitandani ni sifuri sana”
“Poleni, hamieni Tanzania”
“Kwa staili hii hata leo ukiniambia twende nitakwenda”
“Hahaaa, upo kwenye ndoa lakini”
“Kwani ndoa, ni sheria ambayo itanifanya ninyongwee?”
“Si sheria ila mulifunga kanisani”
“Hata kama, huwezi amini ndoa yangu ina miezi sita, ila sijawahi kupata furaha y ambo** kama hii niliyo ipata leo. Kumbe Mungu naye anajua kuwakutanisha watu”
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Laiti ningekuwa sijakuleta mafuta haya na kifunga kinywa si ningekuwa sijapata hii raha”
“Kwani kila siku si huwa unaniletea?”
“Ndio, ila nilikuwa ninakuchukulia wa kawaida sana, na wala sikuwa ninahitaji mazoe na wewe”
“Imekuwaje leo?”
“Yaani imetoke tu wala sijui imekuwaje”
“Hahaa pole”
“Asante, yaani sijui kwa nini sikukuzoea mapema nikawa ninapata hizi raha”
“Kama inawezekana leo tunaweza tukatoka nje ya hospitali tukaenda kupeana raha huko mbele ya safari”
Nesi Linda akaka kimya kwa sekunde kadhaa kama mtu ambaye anafikiria jambo fulani.
“Alafu kweli, ngoja nifanye mpango wa kukutorosha”
“Mumeo itakuwaje?”
“Mumewangu tangu jana amekwenda Arusha kwenye kikoa atakaa wiki nzima huko, sasa wiki yote si utakuwa umesha nikamua nyege zangu zote zitaisha”
“Usijali katika hilo”
“Ngoja nioge fasta fasta, nikaanze kutengeneza mazingira”
“Poa”
Nesi Linda akaingia bafuni, akaoga haraka haraka, akatoka, kwa kutumia taulo langu akajifuta maji mwilini mwake, kisha akavaa nguo zake. Akajiweka vizuri nywele zake, alipo hakikisha yupo vizuri, akatoka chumbani kwangu na mimi nikaelekea bafuni.
“Yes, mimi ndio Dany”
Nilijikuta nikizungumza kwa furaha huku nikiwa nimesimama kwenye kioo. Nikaoga kwa haraka nikarudi chumbani, nikapata kifungu kinywa, kisha nikameza dawa zangu za adubihi. Siku nzima nimejawa na furaha hata daktari anaye nihudumia aliligundua hilo.
“Dany leo una raha sana kuna nini?”
“Ahaa yani hali yangu kuwa vizuri ninafurahi sana”
“Utazidi kufurahi makovu yakiondoka, zimebaki siku chache utakuwa vizuri”
“Nitazidi kufurahi sana”
“Sasa mimi nilipita kukuona mara moja, ninatoka sasa hivi, kidogo kuna sherehe ya mdogo wangu ana olewa leo, kwa hiyo ninahitaji kuwahi”
“Hakuna shaka kaka, ninaamini kesho utanijia na keki kubwa kubwa”
“Hahaa, usijali tutaangalia uwezekano katika hilo”
“Sawa ndugu kesho”
“Poa ushinde salama”
“Sawa”
Daktari akatoka na kuniacha chumbani kwangu nikiwa na furaha yangu ambayo kusema kweli haifichiki. Masaa yakazidi kusonga mbele, nikaletewa chakula cha mchana na nesi mwengine, nikataka kumuuliza kuhusiana na nesi Linda ila nikasita, nikaona niachane nae.
Nikapata chakula cha mchana na kuendelea kukaa ndani ya chumba changu, sikuhitaji kuubandua mguu wangu ndani ya chumba hichi, isije nesi Linda akaja akanikosa ikala kwangu. Hadi inafika saa moja usiku sikuona dalili yoyote ya nesi Linda kuweza kufika hapa hospitalini, furaha ikaanza kupungua taratibu, ikafika saa mbili usiku, sikumuona, hapo wasiwasi ukaanza kunijaa akilini mwangu. Macho yangu yakawa yanacheza na saa ya ukutani, nikatamani masaa yasimame na nesi Linda aweze kufika, ila mawazo yangu sio sheria ya kufanya masaa wala dakika kuweza kusimmaa.
Hadi inatimu saa nne usiku nesi Linda hajatokea, hata chakula ambacho huwa ninaletewa saa mbili na nusu usiku, sijaletewa. Nikajikuta nikinyanyuka kitandani kwangu, nikapiga hatua hadi mlangoni, taratibu nikaufungua mlango na kuchungulia nikaona askari wa ulinzi wakiranda randa kwenye kordo wakiimarisha ulinzi katika hii hospitali, jambo lililo nikatisha tamaa kabisaa ya kutoroka katika hii hospitali.
ITAENDELEA KESHO