Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Uzinduz FlyOver: Rais Magufuli Ammwagia Sifa Mfugale

$
0
0
Rais John Magufuli, amewataka wataalamu nchini kuiga uchapakazi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (Tanroads) Patrick Mfugale, kwa kuwa waaminifu na kutanguliza Utanzania kwanza.

Ameyasema hayo leo Septemba 27 katika sherehe ya uzinduzi wa daraja la juu la Mfugale lililopo katika makutano ya Barabara ya Mandela na Nyerere eneo la Tazara jijini Dar es salaam ambapo amesema kwa uaminifu wa Mfugale hauwezi ukasahaulika kamwe.

“Wataalamu wa Tanzania wasiwe chanzo cha kurudisha nyuma maendeleo ya nchi yetu kwani badala yake waige uchapakazi wa Mfugale yeye hakupendelewa bali alitanguliza Utanzania mbele badala ya ubinafsi,” amesema.

Amesema kutokana na changamoto na hatua mbambalimbali alizozifanya Mfugale tangu mwaka 1977 akiwa mhandisi Wizara ya Ujenzi, ana imani Watanzania watakubaliana naye kuwa daraja hilo lilistahili kupewa jina lake.

“Ninampongeza Waitara (Mbunge mteule Jimbo la Ukonga, Mwita Waitara) kwa kurudi kwani maendeleo hayana chama sijasema wote waje siwahitaji ila wale ambao wanaosumbuka na mizigo waje tutawakaribisha kwa mikono miwili tujenge maendeleo ya nchi yetu.

Daraja hilo lililopewa jina la ‘Mfugale Flyover’ limegharimu Sh bilioni sita iliyohusisha usimamizi wa ujenzi wenyewe, limejengwa kwa nguzo kubwa 26 na uwezo wa kubeba tani 180 kwa wakati mmoja pia lnatarajiwa kudumu zaidi ya miaka 100.

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Kivuko cha MV Nyerere kilichokuwa kimepinduka na kuzama chainuliwa

$
0
0
Kivuko cha MV Nyerere kilichokuwa kimepinduka na kuzama kichwa chini, kimeinuliwa nakuwa wima kama kilivyokuwa hapo awali kabla ya ajali.

Zoezi hilo la kukinasua kivuko hicho  kilichonasa katika Ziwa Victoria Septemba 20,2018 limekuwa na mafanikio makubwa

Kivuko hicho kimenyanyuliwa baada ya jitihada za siku tano tangu Jumapili Septemba 23, 2018 zilizofanywa na wataalam wa uokoaji kutoka vyombo vya ulinzi na usalama wakiongozwa na maofisa wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).

Wataalam hao walikuwa wakifanya kazi ya kukinyanyua kivuko hicho usiku na mchana huku wakitumia njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupitisha maboya chini ya maji, kuyajaza upepo sambamba na kukifunga kamba kivuko hicho na kukivuta.

Waziri Muu: Serikali Kwa Sasa Inaboresha Maeneo Ya Utawala....Asema Lengo Ni Kuziwezesha Halmashauri Kujiendesha Zenyewe

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kipaumbele cha Serikali ya Awamu ya Tano kwa sasa ni kuboresha maeneo ya utawala kwa lengo la kutekeleza miradi ya maendeleo na kuongeza uwezo wa halmashauri kujiendesha zenyewe.

Ameyasema hayo leo (Alhamisi, Septemba 27, 2018) wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 34 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT), kwa niaba ya Rais Dkt. John Magufuli. Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Jakaya Mrisho Kikwete, jijini Dodoma.

Ametoa kauli hiyo baada ya kuwepo kwa maombi mengi ya kuanzisha maeneo mapya ya utawala nchini. “Kama mnakumbuka nimekuwa nikieleza mara kadhaa kwamba tunazishukuru Serikali za Awamu zilizotangulia kwa kuainisha maeneo ya utawala.”

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema viongozi hao wanapaswa wajitathmini sambamba na kuainisha mikakati mizuri ili kuhakikisha lengo la kusogeza huduma kwa wananchi linatimia.

Waziri Mkuu amesema katika kipindi cha mwaka 2014/15 jumla ya halmashauri 66 na mkoa mmoja wa Songwe vilianzishwa pamoja na vijiji 1,949, mitaa 1,379 na vitongoji 8,777. Hadi sasa, maeneo hayo hayajaweza kuwa na miundombinu, vifaa na watumishi wa kutosha ili kuwezesha wananchi kupata huduma iliyokusudiwa.

“Mathalani, mkoa wa Songwe halmashauri zake zote, hata halmashauri ya wilaya ya Mbozi ambapo ndiyo makao makuu ya mkoa bado haujafikia vigezo vya kuwa Manispaa. Baadhi ya halmashauri zinaendelea na ujenzi wa ofisi wakati nyingine kama Mafia, Rufiji, Handeni na Ludewa zipo kwenye magofu na huwezi kuamini kama ni Ofisi za Halmashauri.”

“Taarifa nilizonazo hadi sasa ni kwamba tayari sh. bilioni 120.7 zimepokelewa kwenye halmashauri mbalimbali kati ya sh. bilioni 238.8 zinazohitajika kukamilisha ujenzi wa majengo ya halmashauri sawa na asilimia 50.54 ya fedha zote.

Amesema kiasi kilichobaki kitaendelea kutolewa kupitia bajeti ya Serikali na mapato ya ndani ya halmashauri, ambapo baadhi yake zitapewa fedha za kukamilisha ujenzi baada ya uhakiki kwa sababu zimekuwa zikipokea fedha kwa muda mrefu.

Kadhalika, Waziri Mkuu amewaagiza viongozi wa halmashauri hizo wahakikishe wanajenga Ofisi za Serikali za Vijiji, Mitaa na Vitongoji badala ya kuendelea kuanzisha Serikali hizo huku zikiwa hazina hata ofisi.

Kuhusu uhaba wa watumishi wa kada mbalimbali katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea na zoezi la kuajiri watumishi hususan wa kada za afya na elimu, ambapo kati ya mwaka 2015/2016 hadi 2017/2018 Serikali imeajiri watumishi wa kada ya elimu 13,472 na afya 8,238 kwa lengo la kuziba mapengo yaliyopo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Rais Magufuli Aridhia Ombi La RC Makonda Kufanya Ziara Dar Es Salaam.

$
0
0
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amepokea kwa mikono miwili ombi Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda la kufanya ziara ya kikazi Mkoani humo ili kujionea miradi mikubwa ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ya awamu ya tano pamoja na kusalimiana na wananchi ambao wameonyesha kuwa na shauku kubwa ya kuonana na Rais.

Uamuzi huo umekuja baada ya RC Makonda kumuomba Rais Maguguli afanye ziara ya kikazi na kuzungumza na wananchi.

Hayo yote yamejiri leo wakati wa uzinduzi wa Flyover ya Mfugale iliyopo makutano ya TAZARA ambapo RC Makonda amempongeza Rais Magufuli kwa kufanikisha ujenzi wa Daraja hilo la aina yake linaloenda kumaliza kero ya Msongamano jijini Dar es salaam.

Aidha RC Makonda amemshukuru Rais Magufuli kwa kukamilisha miradi mingi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa barabara za kisasa, Madaraja, mifereji, vituo vya afya, miradi ya maji na miradi mingine lukuki ambayo imekuwa faraja kwa wananchi.

Rais Magufuli Akutana Na Kufanya Mazungumzo Na Mjukuu Wa Malkia Elizabeth Ii Wa Uingereza, Prince William Ikulu

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mjukuu wa Malkia wa Uingereza Prince William mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mazungumzo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Mjukuu wa Malkia wa Uingereza Prince William picha ya wanyama wanaopatikana katika mbuga mbalimbali nchini mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu: Jumla Ya Viwanda 1,596 Vimejengwa Nchini....Asema ni utekelezaji wa agizo la ujenzi wa viwanda 100 katika kila mkoa

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema hadi kufikia Juni, 2018 jumla ya viwanda 1,596 vimejengwa ambapo ni sawa na asilimia 61.4 ya lengo la kujenga viwanda 2,600 hadi Desemba 31, 2018 ikiwa ni utekelezaji wa agizo la ujenzi wa viwanda 100 katika kila mkoa.

Ameyasema hayo leo (Alhamisi, Septemba 27, 2018) wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 34 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT), kwa niaba ya Rais Dkt. John Magufuli. Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Jakaya Mrisho Kikwete, jijini Dodoma.

Waziri Mkuu amesema kuwa viwanda hivyo vimejengwa kupitia agizo la Waziri wa Nchi OR- TAMISEMI kwamba kila Mkoa ujenge viwanda 100.

Amesema tathmini ya utekelezaji wa mkakati wa Serikali kuelekea uchumi wa viwanda, inaonesha kwamba mpaka sasa jumla ya hekta 367,077 zimetengwa katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa ajili ya viwanda vikubwa, viwanda vya kati na viwanda vidogo. 

“Nitoe wito kwenu kwamba mwendelee kupiga hatua nyingine mbele zaidi katika hili, tujue katika hekta hizo zilizotajwa ni kiasi gani kimerasimishwa kwa viwanda vipi, bidhaa zipi zinazalishwa, hali ya miundombinu ikoje na kuna mikakati gani ya kuiendeleza. Pia tufahamu ni ajira ngapi zilizozalishwa kutokana na uanzishwaji wa viwanda hivyo.” 

Kadhalika, Waziri Mkuu amewaagiza viongozi na wasimamizi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kutekeleza majukumu yao kikamilifu ili kuwawezesha wananchi kushiriki katika kubuni na kusimamia miradi ya maendeleo na kuibua fursa za uwekezaji.

Pia kuanzisha na kuendeleza viwanda vidogo na vikubwa ili Tanzania iweze kufikia lengo la kuwa nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. “Tumieni asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri kuwawezesha wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kupitia vikundi vyao ili wawekeze katika viwanda vidogo vidogo vyenye kuleta tija na kuongeza pato la kaya ili kuutokomeza umaskini.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema lengo la Serikali katika Dira ya Maendeleo ya 2025 ni kuhakikisha Halmashauri zinakuwa na uwezo wa kujitegemea kimapato kwa zaidi ya asilimia 80 ifikapo 2025. 

Amesema Serikali ya Awamu ya Tano imekuwa ikichukua hatua mbalimbali ili kuhakikisha lengo hilo linatimia. Serikali imeanzisha utaratibu wa kugharamia miradi ya kimkakati yenye lengo la kuziongezea halmashauri mapato ya uhakika na kupunguza utegemezi wa ruzuku.

“Hadi sasa, sh. bilioni 131.5 zimeidhinishwa kutekeleza miradi ipatayo 22 katika halmashauri 17 zilizokidhi vigezo kwenye mikoa 10. Hivi ninavyozungumza, tayari kiasi cha sh. bilioni 16.4 zimekwishapelekwa kwenye halmashauri hizo kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa miradi iliyokusudiwa.”

Waziri Mkuu amesema kuwa uchambuzi wa miradi mingine zaidi unaendelea na halmashauri zitakazokidhi vigezo zitapata fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo.

Amesisitiza kwamba fedha hizo zikatumike kwa ajili ya malengo yaliyokusudiwa na si vinginevyo. Amesema kwa sasa, hatutakuwa na utaratibu wa kutoa fedha bila kufahamu kwa kina fedha hizo zinakwenda kufanya nini na zitaleta mabadiliko gani.

“Nimesikia kwamba katika baadhi ya halmashauri fedha zilizokwishatolewa bado hazijaanza kutumika kikamilifu watu wanaendelea kujadili namna ya kuzitumia, niwakumbushe tu kwamba Mheshimiwa Rais hakutoa fedha hizo ili zikakae benki. Wakurugenzi wa Halmashauri mlisaini makubaliano ya matumizi ya fedha hizo, hivyo, zingatieni hilo.”

Waziri Mkuu amewataka Madiwani wasimamie matumizi ya fedha hizo ili halmashauri zipate miradi yenye ubora unaotakiwa, inayolingana na kiasi cha fedha kilichotolewa pamoja na inayokamilika kwa wakati. 

Kauli mbiu ya Mkutano huo wa 34 inasema “Umuhimu wa Mamlaka za Serikali za Mitaa katika Kutoa Huduma na Ushiriki wa Wananchi Kupitia Fursa na Vikwazo Kuelekea Uchumi wa Viwanda”.

Amesema kauli mbiu hiyo, inatilia mkazo maneno ya awali ya Rais Dkt. Magufuli, kwamba Mamlaka za Serikali za Mitaa zipo karibu zaidi na wananchi na zinapaswa kutoa huduma na kuwashirikisha wananchi katika kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Rais Magufuli: Wataalamu Tusikwamishe Miradi Ya Maendeleo

$
0
0
Na. Immaculate Makilika- MAELEZO
RAIS Dkt. John Pombe Magufuli amewataka wataalamu wa kitanzania kutokuwa chanzo cha kukwamisha miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa nchini yenye lengo la kuleta maendeleo kwa taifa.

Akizungumza leo Alhamisi (Septemba 27, 2018) Jijini Dar es salaam, wakati akifungua rasmi barabara ya juu ya Patrick Mfugale iliyopo katika makutano ya barabara ya Mandela na Nyerere, Rais Magufuli alitoa wito kwa wataalamu wa kitanzania wasiwe chanzo cha kukwamisha miradi mbalimbali kwa kuwa miradi hiyo ina lengo la kuwasaidia Watanzania.

“Wataalamu wasiwe chanzo cha kukwamisha miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa, ni lazima  tuweke maslahi yetu kwanza, tusitumike  kukwamisha kutekeleza miradi itakayoasaidia Watanzania” alisisitiza Rais Magufuli

Aidha, Rais Magufuli alimpongeza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS)  Mhandisi  Patrick Mfugale na kusema kuwa anamfahamu mhandisi huyo kama mtu  mzalendo, mwaminifu, mwadilifu na mchapakazi.

“Nampongeza Mtendaji Mkuu Mfugale kwa kubuni, kuandaa mchoro wa barabara hii, ambapo pia amebuni michoro ya daraja la Mkapa lenye urefu wa km 10, ambalo ni daraja refu kuliko yote katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na kati” alisema Rais Magufuli.

Vilevile, Rais Magufuli aliishukuru Serikali ya Japan kwa kutoa msaada ulioasaidia katika ujenzi wa barabara hiyo, na kusema kuwa  ni misaada inayolenga kutatua changamoto yenye kuleta mabadiliko ya kweli.

Aidha, Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Mhandisi Patrick Mfugale alisema kuwa  barabara hiyo inayojulikana kama barabara ya juu ya Mfugale yenye urefu wa takribani kilomita moja, imefanikiwa kupunguza msongamano wa magari kwa asilimia 100 kutoka Airport kuelekea mjini na asilimia 50 kutoka Bandarini kuelekea Ubungo.

Naye, Mwakilishi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA),Toshio Nagase aliipongeza kampuni za Japan na Tanzania ambazo zimeshirikiana katika ujenzi wa barabara hiyo kwa kuwa mradi huo umekamilika kwa asilimia kwa wakati na kutopata ajali yoyote wakati wa utekelezaji wake.

“Najivunia uwepo wenu katika mradi huu, hii imeonesha ushirikiano na urafiki mkubwa uliopo kati ya nchi za Tanzania na Japan, pia mmefanikiwa kukamilisha mradi huu kwa kutumia masaa 2, 100,000 ya ujenzi bila kupata ajali yoyote na umekabidhiwa kwa Watanzania kama ilivyopangwa” alisema Nagase

Kwa upande wake, Balozi wa Japan nchini Tanzania, Balozi Masaharu Yoshida alisema kuwa barabara hiyo imepunguza msongamano wa magari kwa kiasi kikubwa, itasaidia ukuaji wa uchumi kwa vile inarahisisha usafirishaji wa watu na mizigo.

Aidha, aliongeza kuwa mradi huo ni alama muhimu ya urafiki na uhusiano wa kudumu kati ya nchi za Tanzania na Japan.

Mradi wa ujenzi wa barabara ya juu ya Mfugale ulianza  kujengwa mwaka 2016, kwa kutumia fedha za  mkopo wa nchi ya Japan na kiasi kingine kikiwa ni fedha kilitolewa na Serikali ya Tanzania.

Barabara hiyo yenye mita 425, imejengwa kwa kutumia nguzo kubwa sita, ina urefu wa kilomita moja, yenye uwezo wa kubeba uzito wa tani 180 kwa wakati mmoja.

Vigogo Kiwanda cha chai Mponde mahakamani kwa uhujumu uchumi

$
0
0
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru) imewafikisha mahakamani vigogo sita wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kiwanda cha wakulima wa chai cha Mponde kwa tuhuma za uhujumu uchumi.

Watuhumiwa hao wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Mkoa wa Tanga, mbele ya Hakimu Desidery Kamugisha na kusomewa mashitaka mawili ya uhujumu  uchumi.

Vigogo hao waliofikishwa mahakamani ni pamoja na  Nawabu Mulla, Shahdadi Mulla, Wiliam Shelukindo, Richard Mbuguni, Richard Madandi na Rajabu Msagati.

Akiwasomea mashitaka mwanasheria wa serikali, Seth Mkemwa akisaidiana na Magulo Waziri, alidai kati ya mwaka 2000 na 2013 watuhumiwa hao wote kwa pamoja walikula njama na kuisababishia serikali hasara ya shilingi bilioni 30.

Katika kosa la pili kwa watuhumiwa wanadaiwa kuidanganya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kutaka msamaha wa kodi katika vifaa mbalimbali walivyodai kuviingiza kwa ajili ya wakulima wadogo wa chai jambo ambalo si kweli.

Aidha watuhumiwa hao hawakutakiwa kujibu lolote mahakamani hapo kwa kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza shauri hilo.

Maamuzi Ya Mahakama Baada Ya Mchungaji Msigwa Kusema Hajapata Wakili

$
0
0
Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa anayekabiliwa na kesi ya jinai namba 112 ya 2018 na wenzake wanane, ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa bado hajapata wakili wa kumtetea mahakamani hapo.

Mchungaji Msigwa leo Septemba 27, mbele ya Hakimu Mkazi, Maira Kasonde amedai hadi sasa bado hajapata wakili hivyo ameiomba Mahakama muda ili aweze kupata wakili wa kumtetea katika kesi hiyo.

Washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo, wanatetewa na wakili Peter Kibatala ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman  Mbowe, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu na Naibu katibu Mkuu bara ambaye pia ni Mbunge wa kibamba John Mnyika.

Wengine ni mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, mbunge wa Kawe, Halima Mdee, mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya, mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Vincent Mashinji.

Msigwa ameeleza hayo mara baada ya Wakili wa Serikali, Simon Wankyo kueleza kesi ilipangwa kwa ajili ya washtakiwa hao kusomewa maelezo ya awali (PH) na kwamba Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri anayeisikiliza kesi hiyo yupo likizo.

Wankyo ameendelea kueleza kuna rufaa namba 215 ya mwaka huu Mahakama ya Rufaa iliyofunguliwa na washtakiwa na inatarajiwa kutolewa uamuzi wiki ijayo katika tarehe ambayo watajulishwa hivyo ameiomba mahakama kuipanga kesi hiyo Oktoba 8, 2018.

Amedai anapendekeza tarehe hiyo kwa kuwa Hakimu Mashauri atakuwa amesharejea na Mahakama ya Rufaa watakuwa wameshatoa uamuzi.

Wakili Kibatala baada ya kusikiliza hoja hizo ameiomba mahakama iwapatie muda wa kutosha Oktoba 25, 2018 ili pia na mshtakiwa Msigwa aweze kutafuta wakili wa kumtetea. Pia siku hiyo washtakiwa hao watasomewa maelezo ya awali kwa Hakimu Mashauri.

Hakimu Kasonde amekubaliana na ombi la kuahirisha kesi hiyo na aliiahirisha hadi Oktoba 25, 2018 ili kumpa muda wa kutosha Msigwa kutafuta wakili wa kumtetea.

Washtakiwa hao kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 13, ikiwemo kula njama, kufanya mkusanyiko wenye ghasia, kuhamasisha hisia za chuki, kushawishi hali ya kutoridhika, uchochezi na kushawishi utendaji wa kosa la jinai kati ya Februari 1 na 16, 2018, Dar es Salaam.

BodaBoda Kortini Kwa Kumbaka Mwanafunzi

$
0
0
Dereva wa bodaboda, Aman Mika (22) amepandishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni kwa kosa la kumbaka mwanafunzi wa  darasa la saba(14).

Akisoma shtaka hilo jana mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Frank Moshi, Wakili wa Serikali, Ramadhani Mkimbu alidai tarehe tofauti mwaka 2017 hadi Agosti maeneo ya Mbweni mshtakiwa alimbaka mwanafunzi huyo.

Mkimbu alidai mshtakiwa huyo alifanya kosa hilo huku akijua kubaka ni kinyume cha  sheria.

Hata hivyo alisema upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika hivyo alimuomba hakimu apange tarehe ya kutajwa.

Hakimu Moshi alimweleza mshtakiwa kuwa dhamana yake iko wazi kwa kuwa shtaka linalomkabili linadhaminika.

Moshi alimtaka mshtakiwa kuwa na wadhamini wawili kila mmoja awe na barua inayotambulika na asaini bondi ya Sh500,000.

"Kwa kuwa umeshindwa masharti ya dhamana unaenda mahabusu hadi Oktoba 11 mwaka huu kesi yako itakapotajwa tena,"alisema Hakimu Moshi

Mahakama yataka upelelezi kesi ya Seth, Rugemarila ukamilike

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeutaka upande wa mashtaka katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili mshtakiwa Harbinder Singh Sethi na James Burchard Rugemarila ijitahidi kukamilisha upelelezi ili hatma ya kesi hiyo iweze kujulikana.

Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi amesema hayo leo Septemba 27, 2018 mara baada ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa kudai kesi hiyo ilipangwa kwa ajili ya kutajwa na upelelezi wake bado haujakamilika.

Baada ya wakili Kishenyi kueleza hayo, wakili anayemtetea Rugemarila, Didas Respicius ameeleza mahakamani hapo kuwa sera ya mahakama ni mashauri yasikilizwe na kutolewa maamuzi kwa wakati.

"Tunashangaa kila kesi inapokuja upande wa mashtaka unaomba tarehe ya kuitaja kesi kwa zaidi ya mwaka sasa, washtakiwa wanateseka mahabusu," amesema Didas mahakamani hapo.

Wakili Kishenyi amedai wataendelea na upelelezi ili pande zote mbili zipate haki sawa.

Baada ya kusikiliza hoja hizo, Hakimu Shaidi ameutaka upande wa mashtaka ujitahidi kukamilisha upelelezi ili hatma ya kesi ijulikane kabla ya kutangaza kuiahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 11,2018 kwa ajili ya kutajwa.

Washtakiwa hao, wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi  kwa kula njama, kujihusisha na mtandao wa uhalifu, kighushi, kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, kutakatisha fedha na kuisababisha hasara ya Dola 22.1 milioni na Sh 309 bilioni.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 28

BREAKING: CHADEMA Wapata Pigo, Mbunge wa Serengeti Ajiuzulu na Kuhamia CCM

$
0
0
Usiku wa  kuamkia Leo, Septemba 28 Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimepata pigo baada ya kuondokewa na Mbunge wa Serengeti mkoa wa Mara Marwa Chacha ambaye amejiuzulu nafasi yake ya Ubunge na kuhama CHADEMA kisha kujiunga na CCM kwa madai ya kuamua kuunga jitihada za Rais Dr John Pombe Magufuli.

Amesema wakati akigombea ubunge  aliahidi kuwaletea maendeleo wananchi wake lakini dhamira yake haijafanikiwa kutoka na vikwazo anavyokumbana navyo ndani ya Chadema.

Chacha amewataka wakazi wa Serengeti kumchagua mtu atakayeweza kushirikiana nao pamoja ili kuleta maendeleo kupitia CCM

Diwani Mwingine CHADEMA Ajiuzulu na Kutimkia CCM

$
0
0
Diwani wa kata ya Nkoanekoli katika Halmashauri ya Meru wilayani Arumeru kupitia (Chadema), Ndg. Wilson Nanyaro  ameandika barua ya kujiuzulu udiwani na kujiunga na chama a Mapinduzi CCM kwa maelezo kwamba anamuunga mkono Rais John Magufuli.

Nanyaro ni diwani wa kumi na moja katika Halmashauri ya Meru kujiuzulu kwa kwa kipindi hiki  kwa kumuunga mkono Rais Magufuli.



Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Ndg. Emanuel Mkongo amethibitisha kupata taarifa za kujiuzulu kwa Nanyaro.

Msikilize hapo chini akifunguka

Soko La Mlango Mmoja Jijini Mwanza Linateketea kwa Moto

$
0
0
Soko la Mlango Mmoja jijini Mwanza linateketea kwa moto muda huu na jitihada za kuudhibiti zinaendelea chini ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji. Chanzo cha moto huo bado hakujajulikana 

Mkebe Spesho Wa Dawa Ya Mitishamba Yenye Uwezo Mkubwa Wa Kumsaidia Mtu Aliyeathirika Na Upungufu Wa Nguvu Za Kiume

$
0
0
Je, Unamatatizo haya na yamekusumbua kwa muda mrefu bila kupata tiba?

Wanaume wengi wanaupungufu wa nguvu za kiume. na kuwa na maumbile madogo ya kiume. 

Magonjwa kama. kisukari. presha, ngiri, kolodani kuvimba busha tumbo kuunguruma kujaa ngesi na kutopata choo vizuri , punyeto nk huchangia kwa kiasi kikubwa upotevu wa nguvu za kiume 

Tumia dawa nzuri ya mitishamba ambayo haina madhara kwa mtumiaji ata uwe na miaka 80 ,    inatibu na kuponyesha matatizo haya yote         

 SUPER SHAFT;  ni dawa yenye uwezo mkubwa wa kuogeza nguvu za kiume mara dufu na maumbile madogo ya uume                                    
 (1) itakufanya uwe na nguvu za ajabu ukiwa unafanya tendo la ndoa                                        
 (2) inaongeza hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka.                           
 (3) itakufanya uchelewe kufika kileleni ndani ya dk 30 na kuimalika uume zaidi                                  
(4) pia itakupa nguvu za kusimamisha uume wako barabara kama msumari wakati wa tendo la ndoa 
    
NYATI POWER; inarefusha na kunenepesha uume saizi utakavyo kuazia 1_8 unene  sm 2_4 
(1) inaimalisha mirija ya uume iliyo legea ama kusinyaa                                                                       
(2) inasaidia kusafisha mirija ya kwenye uume na hivyo kusaidia kuongeza kasi ya msukumo wa damu kwenye mishipa ya uume                        
(3) Husaidi kuurudisha nje uume uliyoigia ndani      
(4) inasaidia kuongeza manii nyingi ambazo zina viini vya uzazi                                                              
(5) Husaidia kutibu madhara ya punyeto matumizi makari ya madawa ya kizungu mirungi bangi na sigara

Tunatibu Magonjwa Yote Sugu Ngiri Kolodani Kuvimba Busha Bila Kufanyiwa Opresheni Tezi Dume Kisukari Presha Aina Zote Ugonjwa Wa Moyo Kwikwi Kichomi Miguu Kufa Ngazi Nk

Tunapatikana Magomeni Mikumi Karibu Na Kanisa Katoriki La Roma

Tumaini Tradition Clinc Ndiyo Sululisho La Matatizo Tote 

PIGA SIMU 0745_495181 AU  0682_ 644040                               
WOTE MNAKARIBISHWA TUMAINI TRADITION CLINC 
 

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga

Video Mpya Ya Rich Mavoko - Naogopa

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Rich Mavoko ameachia video ya wimbo wake mpya uitwao Naogopa. Itazame hapa

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE;LUKUBA 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO   0658920640/ 0754372325 / 0620806813
 
HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>