Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

BREAKING: Rais Magufuli Katengua Uteuzi wa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Susan Kolimba


Waziri Lugola Afuta Utaratibu Wa Utoaji Vibali Kwa Wananchi Wanaolima Jirani Na Kambi Za Wakimbizi Nchini

$
0
0
Na Felix Mwagara, MOHA-Kakonko
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewataka wananchi wa Kakonko wanaolima jirani na Kambi ya Wakimbizi ya Mtendeli, pamoja na kambi zingine zote zilizopo mkoani Kigoma waendelee kulima bila kuomba kibali chochote kama ilivyoagizwa awali.

Waziri Lugola amefuta utaratibu huo wa utoaji wa vibali kwa ajili ya kuruhusiwa kwenda kulima katika maeneo hayo, baada ya wananchi wilayani humo kuulalamikia utaratibu huo ambao walisema unawafanya wasiwe huru na unawachelewesha kuendeleza shughuli zao za kilimo kama ilivyokua awali.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na mamia ya wananchi mjini Kakonko, Mkoani Kigoma, jana, Lugola alisema Serikali ya Awamu ya Tano haitaki wananchi wake wanyanyaswe, wananchi wanapaswa kua huru katika nchi yao.

 “Naagizia huu utaratibu ufutwe na wananchi wawe huru kwenda kulima katika maeneo ambayo yapo jirani na hiyo kambi pamoja na kambi zinginezo, na pia wasisumbuliwe na mtu yeyote, ” alisema Lugola.

Pia Waziri Lugola alielekeza baadhi ya wananchi ambao hawajalipwa fidia wakati mashamba yao yalipochukuliwa kwa ajili ya kuanzisha kambi hiyo wafanyiwe uhakiki ili waweze kulipwa haki zao.

Hata hivyo, Mratibu wa Idara ya Wakimbizi Kanda ya Kigoma, Tony Laiser ambaye alikuwepo katika mkutano huo alipokea maagizo hiyo na kuahidi kuyatekeleza.

Aidha, kabla ya mkutano huo wa hadhara, Waziri Lugola alizungumza na  watendaji waliopo katika wizara yake mkoani humo na alisema Serikali imepeleka mafunzoni vijana 1,500 kwaajili ya kujiunga na Jeshi la polisi pamoja na kuagiza magari kwa ajili doria.

Pia aliwataka watendaji hao kufanya kazi kwa bidii kwani serikali yao ipo na inawajali na pia itahakikisha inatatua kero zao ambazo zinawakabili ikiwemo ukosefu wa majengo, upungufu wa vitendea kazi na uhaba wa askari katika sehemu mbalimbali nchini.

Meli mbili za Mv Nyakibare na Orion II, zawasili kukinasua kivuko Mv Nyerere kisiwani Ukara

$
0
0
Mitambo na vifaa maalum vya kunyanyua, kubeba na kuvuta vitu vizito imewasili katika gati ya Bwisya kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe tayari kufanya kazi ya kunyanyua na kugeuza kivuko cha Mv Nyerere kilichopinduka katika ziwa Victoria.

Mpaka kufikia jana wataalam wa uokoaji na masuala ya majini walifanikiwa kukilaza ubavu kivuko hicho ambacho awali kililala kifudifudi tangu kilipopinduka Septemba 20.

Mitambo na vifaa hivyo vimewasili asubuhi ya leo vikiwa ndani ya meli mbili kubwa binafsi za Mv Nyakibaria ya kampuni ya Mkombozi and Fisheries na Mv Orion II inayomilikiwa na kampuni ya Kamanga Ferry, zote za jijini Mwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jioni, Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa ya Mv Nyerere, Isaac Kamwelwe alisema mitambo na vifaa hivyo vitarahisisha kazi ya kunyanyua, kugeuza na kukivutia ufukweni kivuko hicho.

Uteuzi Wa Wagombea Ubunge Katika Jimbo La Liwale Na Udiwani Katika Kata 37

$
0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi  ilitangaza tarehe 13 Septemba 2018 kuwa siku ya uteuzi wa wagombea Ubunge  katika jimbo la Liwale Mkoani Lindi  na tarehe 21 Septemba 2018  kuwa siku ya uteuzi kwa wagombea Udiwani katika  kata 37 zilizopo katika Hamashauri ishirini na saba na mikoa kumi na tatu ya Tanzania Bara.  

Hata hivyo, baada ya uteuzi huo Tume imepokea malalamiko kupita vyanzo mbalimbali  juu ya kutotendewa haki kwa baadhi ya wagombea Udiwani katika baadhi ya maeneo yenye chaguzi hizo.

Tume, imefanya ufuatiliaji na kupokea taarifa za awali kutoka kwa baadhi ya  wasimamizi wa uchaguzi kwenye maeneo  yanayolalamikiwa.

Kwa mujibu wa maelezo ya wasimamizi hao wagombea ambao hawakuteuliwa ni kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo kuwekewa pingamizi, kutorejesha fomu siku ya uteuzi, kujitoa baada ya kuteuliwa na baadhi kutotimiza masharti ya  uteuzi ambayo ni ujazaji wa fomu za uteuzi kikamilifu na kutotimiza idadi ya wadhamini inayokubaliwa kisheria.

Maeneo ambayo wagombea wake wamewekewe Pingamizi na wagombea wenzao ni pamoja na kata ya Kibutuka  Halmshauri ya wilaya ya Liwale, Kata ya Ruvu Halmashauri ya Wilaya Kibaha, Kata ya Njianne Halmasahuri ya wilaya Mkuranga, Kata ya Jibondo na Kilindoni Mafia na  Kata ya Ikwiriri  Halmashauri ya Rufiji, ambapo ni Wagombea wa CUF waliowekewa Pingamizi.

Aidha, katika Halmashauri zote ambazo wagombea wa CHADEMA walichukua fomu kuomba kuteuliwa kugombea nafasi ya udiwani hawakurejesha fomu hizo kwa ajili ya uteuzi.

Vile vile, Baadhi ya  wagombea mfano Mgombea wa CUF kata ya Ruaruke, Wagombea ACT WAZALENDO na CUF katika  kata ya Mailimoja  na Mgombea wa ACT WAZALENDO katika kata ya Mbwawa zote kutoka Halmashauri ya Mji wa Kibaha hawakuteuliwa kwa sababu hawakurejesha fomu za uteuzi.

Wengine ambao hawakurejesha fomu ni mgombea wa CUF kata ya Kisiju Halmshauri ya Mkuranga, mgombea wa CUF na mgombea TLP  kata ya Mjimwema Halmashauri ya Kigamboni.

 Aidha, katika kata  ya  Kagando wagombea wa CUF,TLP NCCR-MAGEUZI  na ACT WAZALENDO na  Kata ya Hamugembe Mgombea wa CUF wote wa  Halmashauri ya  Manispaa ya Bukoba hawakurejesha fomu ili wateuliwe.

Vile vile, katika Halmashauri ya Kakonko kata ya Rugenge mgombea wa CUF hakurejesha fomu na mgombea wa NCCR-MAGEUZI Katika Halmashauri ya Sumbawanga kata ya Ikozi hakurejesha fomu pia.

Katika Halmashauri ya wilaya ya Geita wagombea wa Vyama CCK na ADC hawakurejesha Fomu kwa Msimamizi wa Uchaguzi kata ya Nyankumbu, wakati huo huo wagombea wa CUF na NCCR-MAGEUZI kata ya QURUS hawakurejesha fomu za uteuzi. Wakati katika Halmashauri ya Monduli Mji mgombea wa ACT WAZALENDO hakurejesha Fomu.

Baadhi ya wagombea  hawakuteuliwa kwa kuwa hawakujaza fomu za uteuzi kikamilifu ikiwemo kutotimiza idadi ya wadhamini  na wengine kutodhaminiwa na Vyama vyao vya Siasa. Mfano; Wagombea wa CUF katika kata za Jibondo na Kilindoni Halmashauri ya wilaya Mafia, wagombea wa CUF na ACT WAZALENDO Kata ya Mabatini Halmashauri ya Nyamagana hawakuteuliwa kutoka na mapungufu haya.

Vile vile, kuna baadhi ya wagombea waliojitoa baada ya uteuzi, hili limejitokeza katika Halmashauri ya Babati mji ambapo mgombea wa CUF kata ya Sigino alijitoa baada ya kurejesha fomu kabla ya muda wa uteuzi kumalizika, na pia Halmashauri ya Geita Mji kata ya Nyankumbu ambapo wagombea wa ACT WAZALENDO na CUF walijitoa pia baada ya kuteuliwa.

Kwa ujumla hiyo ni taarifa ya awali katika zoezi la uteuzi wa wagombea Ubunge na Udiwani katika kata 37 uliofanyika katika  maeneo mbalimbali yenye uchaguzi. Katika Uchaguzi huu vyama vya ACT WAZALENDO, CCM, CUF, DP, NCCR –MAGEUZI, NRA na SAU vitashiriki kwa kuwa vimesimamisha wagombea.

Taarifa kamili kuhusu  zoezi la uteuzi ikiwemo matokeo ya rufaa  itatolewa hapo baada  mchakato wote kukmilika.

Imetolewa na,
Mkurugenzi wa Habari na Elimu kwa Umma Tume ya Taifa ya uchaguzi
23 Septemba 2018

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Septemba 25

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga

Viwanja (Vimepimwa), Vinauzwa: Bunju na Mapinga (Baobab Sec)

$
0
0
Viwanja (Vimepimwa), Vinauzwa: Bunju na Mapinga (Baobab Sec)

Kwa Mapinga Kimele, vipo viwanja vya sqm 400 (20/20) kwa tsh 4 mil, sqm 600 (20/30) kwa tsh 6 mil, sqm 800 (20/40) kwa tsh 8 mil, sqm 400 (35/40) kwa tsh 18 mil. Viko umbali wa km 3 kutoka main road (Bagamoyo road).

Process ya upimaji wa viwanja hivi haijakamilika, bado inaendelea na hati zake ni za kusubiri. Pia maji katika viwanja hivi yako umbali wa km 1, umeme upo umbali wa mita 600 (nguzo 8 zinatakiwa).

Kwa Mapinga, Baobab sec, viko viwanja vya sqm 700 kwa tsh 9 mil, sqm 1500 kwa tsh 20 mil, sqm 2000 kwa tsh 30 mil, sqm 3000 kwa tsh 39 mil. Viko umbali wa km 2.5 kutoka main road (Bagamoyo road).

Process ya upimaji wa viwanja hivi imekamilika kwa 100% na hati zake ziko tayari. Maji na umeme viko site tayari.

Luksa kulipa kwa awamu 2 ndani ya miezi 3.

Kwa Bunju, viko viwanja 2 vya pamoja na vimegusa main road (Bagamoyo road) na kila kiwanja kina ukubwa wa sqm 1700 kwa bei ya tsh 45 milion, ukiviunganisha unapata sqm 3400 kwa tsh 90 milion.

Biashara hii haina dalali.
call 0758603077, whatsap 0757489709, email: menejadar@yahoo.com

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE;LUKUBA 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO   0658920640/ 0754372325 / 0620806813
 
HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Umoja wa Ulaya,China na Urusi Waitosa Marekani

$
0
0
Ulaya,Urusi na China zimejiweka katika nafasi ya kuvutana na rais wa Marekani Donald Trump baada ya hapo jana usiku kutangaza mipango ya kuunda njia maalum za kurahisisha shughuli za kibiashara na Iran,hatua ambayo inakiuka vikwazo vya Marekani.

Baada ya mkuu wa sera za nje wa Umoja wa Ulaya Federica Mogherini kukutana na wajumbe kutoka Uingereza,Ufanasa,Ujerumani ,Urusi China na Iran hapo jana alitangaza kwamba nchi hizo ambazo zote zimesaini makubaliano ya Nuklia ya Iran zimefikia uamuzi wa kuendelea na shughuli za kibiashara na Iran.Akafafanua zaidi kwa kusema:

''Washiriki wamesisitiza haja ya kulinda uhuru wa uendeshaji wa kiuchumi ili kuwa na fursa ya kufanya biashara kwa njia halali na Iran kwa kuzingatia kwa ukamilifu azimio la baraza la usalama la Umoja wa mataifa nambari 2231''

Maamuzi yaliyofikiwa na nchi hiyo yanamaanisha kwamba sasa Umoja wa Ulaya utaunda taasisi huru ya kisehria ambayo itaratibu shughuli kutowa na kupokea malipo ya fedha katika shughuli za kibiashara na Iran.

Mogherini aliendelea kusema kwamba kundi hilo la nchi Umoja wa Ulaya,China na Urusi  zimeidhinisha kwa kauli moja mapendekezo ya kiutendaji ya kuendelea kuzibakisha na kuziimarisha njia za kurahisisha mchakato wa malipo  yanayohusiana na biashara na Iran ikiwemo biashara ya mafuta.

Nchi zote zilizoshiriki katika mkutano uliofikia maamuzi hayo jana ziliafiki kwamba Iran inatekeleza majukumu yake kama sehemu ya mkataba wa Nyuklia uliosainiwa 2015 na hilo limethibitishwa katika ripoti 12 mfululizo zilizowahi kutolewa na shirika la kimataifa la Atomiki IAEA

Lakini hatua iliyochukuliwa na nchi hizo ni dhahiri inaweka mazingira ya kuzuka mvutano mkubwa na Marekani ambayo iliiwekea tena vikwazo Iran mnamo mwezi Agosti ambavyo pia vinataja kwamba nchi yoyote au makampuni yatakayoshirikiana kibiashara  na Iran yataadhibiwa. Duru nyingine ya vikwazo vya Marekani kuelekea Iran inatarajiwa kutangazwa mwezi Novemba na hasa vikilenga kukwamisha kabisa usafirishaji wa mafuta wa jamhuri hiyo ya kiislamu.

 Vikwazo hivyo vitamaanisha kwamba makampuni zaidi makubwa yatalazimika kuamua ama kuondowa vitega uchumi vyao Iran au kupoteza fursa zao za kibiashara na Marekani.
 
 Jana waziri wa mambo ya nje wa Marekani Mike Pompeo alifanya mkutano na waandishi habari akasema kwamba rais Trump atatumia nafasi yake kama mwenyekiti wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kuzitolea mwito nchi zote kuunga mkono kampeini ya kuishinikiza Iran katika mpango wake wa Nyuklia.
 
 Uamuzi huo wa Marekani  lakini huenda ukasabababisha cheche za moto na wanachama wengine wa baraza la usalama la Umoja huo wa Mataifa,Uingereza,Ufaransa China na Urusi.

Walimu Hazina mbaroni kwa kuwapa wanafunzi darasa la saba mitihani

$
0
0
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Kimataifa ya Hazina, Patrick Cheche na walimu wenzake wanne wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kuwapa maudhui ya mtihani wa taifa wa darasa la saba watahiniwa wa shule hiyo.

Washtakiwa hao walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi leo Jumatano Septemba 26 na kusomewa  mashtaka Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi kwa kushirikiana na Wakili wa Serikali Mwanaamina Kombakono.

Wakili Kombakono aliwaja washtakiwa hao kuwa ni,  Mwalimu Cheche, Laurence Ochieng, Justus James, Nasri Mohammed na Mambo Iddi.

Washtakiwa hao wanadaiwa Septemba 5, mwaka huu waliingilia mitihani ya taifa isivyo halali, walipata kwa makusudi wakawaonyesha watahiniwa maudhui ya mitihani hiyo ambapo walikana mashtaka hayo, kesi hiyo itatajwa Oktoba 10 mwaka huu.

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kusimamia wananchi kudai Katiba Mpya

$
0
0
Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Anna Henga, amesema kituo hicho kipo katika mpango wa kuwajengea uelewa wananchi ili wadai Katiba mpya wao wenyewe baada ya mchakato wake kusimama tangu mwaka 2014.

Henga ametoa kauli hiyo leo Jumatano Septemba 26, wakati wakisherehekea miaka 23 tangu kuanzishwa  kwa kituo hicho ambacho amedai kimekuwa kimbilio la wananchi wengi.

Amesema hawataacha kupaza sauti kudai Katiba hiyo kwa sababu imeligharimu taifa fedha nyingi pamoja na kukusanya maoni ya wanachi ambayo hawataki yapotee.

“Hatutaacha kudai Katiba Mpya ila kwa sasa tunachokifanya ni kuelimisha wananchi ili wao wenyewe waweze kuidai katiba hiyo, kama mnavyojua mchakato huu umechukua  fedha nyingi na wananchi tulitoa maoni ambayo hatutapenda yapotee.

“Sisi tulianzisha mchakato wa Katiba mpya nchini uliyosababisha vuguvugu kubwa la watu kushiriki katika mchakato wa mabadiliko ya Katiba mwaka 2014, hata kabla ya Serikali kuanzisha mchakato huo,” amesema.

Aidha, amesema kumekuwa na hali mbaya ya haki za binadamu katika kipindi cha miaka mitatu ikilinganishwa na wakati walipokuwa wakisherehekea miaka 20 ya kuanzishwa kwa kituo hicho.

Utekelezaji wa Agizo la Waziri Lugola Kufunga Tela Bodaboda

$
0
0
Ikiwa imepita miezi miwili tangu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola kuagiza pikipiki zote zinazotumika kusafirisha abiria zifungwe tela katika kile kinachoaminika kudhibiti wimbi la ajali za bodaboda,Taasisi mbalimbali za Serikali zimekutana jijini Dodoma ikiwa ni mazungumzo ya awali kuelekea mkakati huo wa kupunguza ajali.

Akizungumza jijini Dodoma  baada ya mkutano  na ukaguzi wa pikipiki ya mfano iliyofungwa tela  iliyotengenezwa na Shirika la Mzinga,lililoko chini ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu, amesema Serikali imedhamiria kuondoa na kukomesha ajali za bodaboda pamoja na kulinda usalama wa watumiaji wa usafiri huo.

Akielzezea juu ya mazungumzo hayo yaliyokutanisha taasisi hizo, Katibu Mkuu Meja Jenerali Jacob Kingu, amesema Wizara yake kwa kushirikiana na wadau wengine kutoka taasisi za serikali; Shirika la Mzinga, Mamlaka ya Elimu na Ufundi Stadi (VETA), Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), Kiwanda cha Kutengeneza Magari (NYUMBU) na Jeshi la Polisi watahakikisha wanakuwa na mpango wa pamoja wa kuratibu na kuhakikisha mkakati huo utakaosaidia kupunguza ajali unakamilika.

“Leo tumekutana hapa kujadili jinsi ya kuliendea jambo hili la kufunga tela na kamati ya  wataalamu hawa ndio itakutana na kuratibu andiko ambalo litapelekwa  kwa viongozi wa wizara mbalimbali zinazohusika na suala la kudhibiti ajali za barabarani na kumlinda mtumiaji wa huduma ya usafiri huo,” alisema Meja Jenerali Kingu.

Aliwaomba wananchi wawe na subira katika kipindi hiki ambacho kamati hiyo ya wataalamu inaenda kuandaa mpango huo, na mapema mwishoni mwa mwaka huu mpango huo utatangazwa .

Akizungumzia pikipiki hiyo ya mfano yenye tela, Mtaalamu kutoka Shirika la Mzinga, Mhandisi Salum Kipande alisema pikipiki hiyo wameitengeneza vizuri na itakua na uwezo wa kubeba abiria wanne na dereva mmoja huku akiahidi kuunga mkono adhma hiyo ya serikali kupunguza ajali za bodaboda nchini kwa kutengeneza pikipiki hizo kwa ustadi.

Naye Kaimu Mkurugenzi Elimu na Mafunzo wa Mamlaka ya Elimu na Ufundi Stadi (VETA), Stella Ndimubenya  alisema  wao kama VETA watahakikisha wanatumia teknolojia waliyonayo kuweka kifaa maalumu ambacho kitadhibiti upakiaji wa abiria kupita kiwango kilichopitishwa na mamlaka husika huku akiahidi kutoa mafunzo kwa madereva pindi pikipiki hizo zitakapopitishwa na kuanza kutumika.

Rais Magufuli Kuzindua Flyover ya Tazara Kesho

$
0
0
Rais Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa Daraja la Juu ‘flyover’ mpya iliyojengwa hivi karibuni katika makutano ya Barabara za Mandela na Nyerere katika eneo la TAZARA jijini Dar es Salaam.

Tukio hilo litafanyika kesho Alhamisi, kesho Septemba 27, 2018 ambapo Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda amesema Flyover hiyo itapunguza changamoto ya msongamano barabarani iliyokuwa inaleta hasara ya Tsh. Bilioni 400 kwa mwezi.

Makonda amewaalika viongozi wa upinzani kwenda kushuhudia tukio hilo na kuwa atawawekea sehemu maalumu ya kukaa akiamini wao ndio wanaongoza kuponda maendeleo hayo na kwamba Flyover hiyo ilianza kutumika kwa majaribio mnamo Septemba 15 mwaka huu.

Soudy Brown, Maua Sama Waachiwa Kwa Dhamana Wimbo Wake Ukifikisha Views Milioni 1

$
0
0
Hapo jana msanii wa Bongo Fleva, Maua Sama aliachiwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam baada kushikiliwa kwa takribani wiki nzima.

Habari nzuri kwa sasa ni kwamba wimbo wa Maua Sama uitwao Iokote umeweza kufikisha views zaidi Milioni 1 kwenye mtandao wa YouTube. 

Maua Sama anakuwa msanii wa kwanza wa kike Tanzania wimbo wake (audio pekee) kufikisha views milioni 1 YouTube ndani ya wiki tatu, wimbo huo ulitoka September 03, 2018.

Wimbo huo ambao amemshirikisha Hanstone ndio ulipelekea yeye kukamatwa na Polisi kutokana na kuweka video ya watu wakiucheza huku wakichezea fedha za Kitanzania kitu ambacho ni kinyume na sheria.

Mbatia Agoma Kuhudhuria Uzinduzi Flyover Tazara.....Adai Mwaliko wa Makonda Haujafuata Taratibu

$
0
0

Wakati Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kesho akitarajiwa kuzindua matumizi ya barabara ya juu (Flyover) Tazara viongozi mbalimbali walipewa mualiko na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akiwemo Freeman Mbowe, Halima Mdee, pamoja na James Mbatia kushiriki tukio hilo.

Mbatia alipotafutwa ili kufahamu kama angeitikia wito wa mkuu huyo wa mkoa Mbatia amesema anapenda maendeleo lakini kiongozi huyo alipaswa kufata taratibu kutoa mwaliko kwa viongozi hao.

“Yaani kweli mimi Mbatia nialikwe na Mkuu wa Mkoa (Makonda) kupitia vyombo vya habari sio sawa kabisa, hatukatai maendeleo lakini alipaswa kufata taratibu kabla za kunialika kwa kunitumia barua sio kutumia vyombo vya habari. ”, amesema Mbatia

Mapema jana katika mkutano wake za kifedha Makonda aliwaalika baadhi ya wabunge wa Upinzani ili kuhudhuria tukio hilo ambalo linatajwa kupunguza adha ya foleni kwa watumiaji wa barabara ya Mandela a Nyerere na kusaidia kuokoa zaidi ya shilingi bilioni 400.

“Ningependa kuona viongozi wa vyama vyote waje, akiwemo Mbatia, Mbowe, Zitto Kabwe na Halima Mdee wasisusie kama ilivyo mambo ya uchaguzi, nawaalika vyama vyote vya siasa mimi nitakuwa mwenyeji wao na tutawawekea viti ” alisema Makonda

Rufaa ya Vigogo CHADEMA Yaibua Mvutano Mahakamani

$
0
0
Rufaa ya viongozi wa Chadema iko njia panda baada ya Mahakama ya Rufani kuhoji uhalali wa taarifa ya kusudio la kukata rufaa hiyo ambayo ndiyo msingi wa rufaa yenyewe.

Mahakama hiyo imehoji uhalali wa taarifa hiyo ya kusudio la kukata rufaa leo wakati rufaa hiyo ilipoitwa kwa ajili ya usikilizwaji baada ya kubaini upungufu kwa kutokueleza asili ya amri au uamuzi ambao wanaukatia rufaa.

Katika rufaa hiyo viongozi hao wa Chadema akiwamo Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe wanapinga uamuzi wa Mahakama Kuu.

Rufaa hiyo ni mwendelezo kutokana na kesi ya msingi ya jinai inayowakabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ambapo wanapinga uamuzi na amri mbalimbali ambazo mahakama hiyo imekuwa ikizitoa.

Awali, walifungua maombi ya mapitio Mahakama Kuu wakiiomba Mahakama hiyo iitishe jalada la mwenendo wa kesi ya msingi na kuuchunguza pamoja na amri zake ili kujiridhisha na usahihi na uhalali wa mwenendo na amri hizo.

Hata hivyo, mjibu maombi (upande wa mashtaka) kupitia kwa jopo la mawakili wa Serikali likiongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Paul Kadushi uliweka pingamizi ukiomba Mahakama hiyo iyatupilie mbali kwa madai ni batili kutokana na kukiuka sheria ya Mahakama za hakimu mkazi.

Mahakama Kuu katika uamuzi wake uliotolewa na Jaji Rehema Sameji aliyesikiliza maombi hayo ilikubaliana na hoja za pingamizi za Jamhuri na ikaitupilia mbali maombi hayo ndipo wakakata rufaa wakaenda Mahakama ya Rufani kupinga uamuzi huo.

Kabla ya kuanza usikilizwaji huo, Jaji Mbarouk aliwataka mawakili wa pande zote kutoa maoni yao iwapo taarifa ya kusudio la kukata rufaa imekidhi matakwa ya kanuni za Mahakama hiyo.

Jaji Mbarouk alisema kanuni za Mahakama hiyo za uendeshaji wa mashauri ya jinai kanuni ya 68 (2) zinaelekeza taarifa ya kusudio la kukata rufaa lazima iainishe asili ya uamuzi au amri ambayo inakatiwa rufaa.

Wakili Peter Kibatala wa wakata rufaa licha ya kukiri kanuni hiyo inaelekeza taarifa ya kusudio la kukata rufaa kuonyesha asili ya uamuzi unaokatiwa rufaa, lakini alisema hata hivyo kutokuonesha hivyo hakuna athari.

Alisema lengo la taarifa hiyo ni kutoa ujumbe tu kuwa kuna jambo linalolalamikiwa na kwamba zipo kesi nyingi za rejea, huku akisema jambo hilo lingekuwa na athari kama wangekuwa wanapinga sehemu tu ya uamuzi lakini wao wanapinga uamuzi wote wa Mahakama Kuu.

Wakili Mtobesya kwa upande wake alisema taarifa hiyo ya kusudio la kukata rufaa iko sahihi na kwamba hapakuwa na haja ya kubainisha wanachokikatia rufaa kwani wanakata rufaa dhidi ya uamuzi wote na si sehemu tu ya uamuzi.

Wakili wa Serikali Kadushi akisaidiana na mawakili wenzake, Dk Zainabu Mango, Wankyo Simon na Jacquiline Nyantori walidai kwa mujibu wa kanuni hiyo ni sharti la msingi kuainisha asili ya uamuzi au amri inayokatiwa rufaa.

Alidai kutokufanya hivyo taarifa hiyo inakuwa batili na inapaswa kutupiliwa mbali na kwa kuwa rufaa inatokana na  taarifa ya kusudio la kukata rufaa basi nayo inakufa moja kwa moja.

Naye Wakili Kadushi alisisitiza kuwa kwa kua taarifa ya kusudio la rufaa haijakidhi matakwa hayo inakosa uhalali wa kisheria kuanzisha rufaa hiyo na akaiomba Mahakama iitupilie mbali, huku akiongeza kuwa rufaa hiyo haiwezi kusimama.

Mahakama baada ya kusikiliza hoja za pande zote iliahirisha shauri hilo hadi tarehe itakayopangwa ambayo watajulishwa kwa ajili ya uamuzi.

Mbali na Mbowe, washtakiwa wengine ni Katibu Mkuu, Dk Vicent Mashinji, manaibu katibu wakuu, John Mnyika (Bara) na Salum Mwalimu (Zanzibar) na Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa.

Pia wamo Mweka Hazina wa Baraza la Wanawake la chama hicho (Bawacha), Esther Matiko, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche na Mbunge wa Bunda, Ester Bulaya.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka 12 ambayo ni kufanya mikusanyiko na maandamano yasiyo halali yanayowakabili wote, huku Mbowe, Msigwa Mdee na Heche kila mmoja peke yake akikabiliwa na mashataka zaidi.

Wanadaiwa kutenda makosa hayo Februari 16 katika barabara ya Kawawa, Mkwajuni, Kinondoni, siku wakihitimisha kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Kinondoni na kusababisha vurugu zilizosababisha kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwiline.

Mwanafunzi Chuo cha Mipango Dodoma Atiwa Mbaroni Kwa Wizi

$
0
0
Polisi mkoani Dodoma inamshikilia mwanafunzi wa Chuo cha Mipango kilichopo jijini hapa, James Senya (21) kwa tuhuma za kujihusisha na makosa ya uvunjaji na wizi katika maeneo mbalimbali ya jiji hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo ofisini kwake, Kamanda wa polisi wa mkoa huo, Gilles Muroto amesema mwanafunzi huyo amekamatwa baada ya kufanyika doria na kugundua kuwa anashirikiana na wahalifu kuvunja na kuiba katika nyumba za watu.

Amesema mwanafunzi huyo wa mwaka wa kwanza katika chuo hicho, amekuwa akiwachorea wahalifu ramani ya kuvunja ambapo wahalifu hao hufika na kuvunja na kupora mali zote kwa kushirikiana na mwanafunzi huyo.

“Hii inaonyesha kuwa hata wanafunzi wanajihusisha na uhalifu badala ya kufuata masomo yeye anajihusisha na uhalifu,” amesema Kamanda Muroto.

Mwanafunzi huyo amekamatwa na watu wengine watano anaodaiwa kushirikiana nao katika uhalifu ambao ni Ayubu Hosea (23), Saudi Mosse (23), Semen Njaid (24), Salum Abdallah (16) na Godfrey Mashauri (26) wote wakazi wa Jiji la Dodoma.

Mjukuu wa Malkia wa Uingereza Prince William Awasili Nchini Leo

$
0
0
NA ANDREW CHALE, DAR
MJUKUU wa Malkia wa Uingereza, Prnce William ametua Nchini Tanzania jioni ya leo Septemba 26, 2018 kwa ziara maalum ya siku tatu ambapo kesho Septemba 27, anatarajiwa kukutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano Ikulu ya Magogoni Jijini Dar es Salaam.

Prince William katika kukutana na Rais Magufuli atafanya mashauriano kuhusu juhudi zinazochukuliwa na Tanzania katika kukabiliana na ujangili na ulanguzi wa wanyama pori.

Prince William ametua mchana wa leo na ujumbe wake ambapo amepokelewa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla, Waziri wa Katiba Sheria Profes Kabudi  pamoja na viongozi wengine akiwemo Balozi wa Uingereza hapa Nchini na Mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha Nchi zao Nchini.

Akiwa uwanjani hapo wa Mwalimu Julius Nyerere eneo la wageni mashuhuri, Prince William amepata wasaha wa kuteta na viongozi hao kwa muda mfupi.

Kwa mujibu wa ratiba ya Mwanamfalme huyo, kesho hiyohiyo ya Septemba 27, anatarajiwa kutembelea bandari ya Dar es salaam katika kitengo cha Polisi Marine (Marine Polisi Unit) na ambapo pia atatembelea maeneo mbalimbali ikiwemo yale ya kupokelea mizigo, upekuzi na ukaguzi wa vinavyoingia na kutoka katika eneo hilo la bandari.

Pia Prince William anatarajiwa kukutana na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dkt. Hamisi Kigwangalla katika ofisi ndogo ya Wizara hiyo Mpingo Jijini Dar es Salaam.

Aidha, Prince William na ugeni wake huo unatarajiwa kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi na baadae Chuo cha Wanyamapori cha Mwika (College of African Wildlife Management, Mwika (CAWM), kilichopo Moshi, mkoani Kilimanjaro na kisha kuendelea na ziara yake Nchini Kenya.

Hata hivyo, imeelezwa kuwa lengo kuu ya ziara hiyo ya Prince William ni pamoja na kufuatilia juhudi za kukabiliana na ujangili na uhifadhi wa wanyama.

Prince William atafanya ziara hiyo katika wadhifa wake kama rais wa mashirika yanayotetea uhifadhi wa wanyama ya United for Wildlife na Tusk Trust. Amekuwa pia mlezi wa shirika la Royal African Society linalolenga kukuza uhusiano kati ya Afrika na Uingereza na hushiriki sana juhudi za kukabiliana na ujangili.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Azindua Taasisi ya Walemavu

$
0
0
SERIKALIi imeipatia Taasisi ya Dr Reginald Mengi Foundation ( DRMF) kiasi cha Tsh Milioni 10 ikiwa ni sehemu ya kuunga juhudi za taasisi hiyo mpya itayojihusisha katika kulinda na kutetea haki za watu wenye ulemavu nchini.

Akikabidhi Msaada huo leo (Jumatano Septemba 26, 2018)  kwa niaba ya Serikali wakati wa uzinduzi wa taasisi hiyo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema jamii ya walemavu ni kundi mtambuka hivyo ni jukumu la wadau wa maendeleo kujitokeza katika kusaidia juhudi za Serikali katika ulinzi na haki yao.

Waziri Mkuu Majaliwa alisema Serikali imendelea kutekeleza sera, sharia, miongoni na mikataba mbalimbali inayohusu haki za walemavu nchini ili kuliwezesha kundi hilo kupata huduma zote za msingi ikiwemo afya, elimu, kazi, ajira n.k

Alisema Serikali tayari imetoa maelekezo kwa Wakuu wa Mikoa na Wakurugenzi wa Halmashauri mbalimbali nchini kwa ajili ya kukusanya taarifa rasmi za watu wenye ulemavu waliopo katika vijiji, kata na vitongoji mbalimbali na kutambua umri, jinsia na shughuli wanazofanya.

Aidha Majaliwa alisema Serikali pia imetoa maelekezo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri mbalimbali nchini kutenga asilimia 2 ya mapato ya makusanyo ya ndani kwa ajili ya kusaidia ili kuliwezesha kundi hilo kuondokana na utegemezi wa kiuchumi pamoja na kupata mitaji ya biashara.

“Serikali itachukua hatua kali kwa Mkurugenzi wa Halmashauri yoyote nchini ambaye atakikua matakwa haya ya kisheria na sasa tumeagiza pesa hizi zikusanywe na mapato yake yatangazwe hadharani kwa njia mbalimbali za matangazo ili kila mmoja ajitokeza na kupata” alisema Majaliwa.

Akifafanua zaidi Waziri Mkuu Majaliwa alisema katika kutekeleza haki za kisheria na mikataba mbalimbali ya kimataifa kwa watu wenye ulemavu, Serikali imefanya mageuzi makubwa katika sekta za ajira na kazi, ambapo idadi kubwa ya watu wenye ulemavu wameweza kuajiriwa nchini kupitia Sekretarieti ya Ajira na kupangiwa kazi katika taasisi mbalimbali za umma.

Kwa mujibu wa Majaliwa alisema Serikali pia imetoa miongozo kwa mamlaka mbalimbali za udhibiti wa  masuala ya majengo ikiwemo Bodi ya Wabunifu Majengo na Bodi ya Usajili wa Makandarasi kujenga miundombinu rafiki kwa kwa watu wenye ulemavu ikiwemo kuwa vipando, viti, maliwato, lifti.

Aliongeza kuwa Serikali pia imekuwa ikitenga kiasi cha Milioni 6.5 na kuzipeleka katika Halmashauri mbalimbali kwa ajili ya ununuzi wa vifaa mbalimbali kwa watu wenye ulemavu ikiwemo mafuta pamoja na vyombo vya usikivu.

Nitoe wito kwa mashirika, makampuni, taasisi pamoja na wadau wa ndani na nje ya nchi kujitokeza ili kuunga mkono juhudi za Taasisi ya Reginald Mengi Foundation, kwa kuwa suala hili linagusa kila mtu katika jamii yetu” alisema Majaliwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Taasisi hiyo, Dkt. Reginald Mengi alisema Ofisi yake imepanga kutenga kiasi cha Tsh. Bilioni 5 kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda kitachojengwa Jijini Dar es Salaam na kitakachotoa ajira kwa watu wenye ulemavu nchini.

Aidha Dkt. Mengi aliitaka jamii ya watu wenye ulemavu nchini kutokata tama kwa kuwa ulemavu haimfanyi mtu kupoteza uwezo wa kufanya kazi, na badala yake aliwataka kufanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo waliyofikia.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Chama cha Watu wenye Ualbino Tanzania Mussa Kabimba alisema kuanzishwa kwa Taasisi hiyo kutatoa fursa kwa watu wenye ulemavu kuwa na umoja wao utaowawezesha kuwa na sauti moja ya kushiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii kiuchumi na kujiletea maendeleo yao.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images