Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Septemba 25


Waziri Lugola Aibukia Kituo Cha Polisi Katoro, Awahoji Watuhumiwa Makosa Yao Wakiwa Wamepanga Foleni Mahabusu

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, Geita
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amefanya ziara ya kushtukiza katika Kituo cha Polisi Katoro mkoani Geita  na kuwahoji watuhumiwa wa makosa mbalimbali waliokuwepo katika mahabusu kituoni hapo.

Lugola ambaye alikua safarini kuelekea Mkoani Kigoma kwa ziara yake ya kikazi, ghafla aliibukia katika kituo hicho akitaka kujua utendaji kazi wa polisi pamoja na makosa mbalimbali wanayowakabili watuhumiwa waliopo katika mahabusu hiyo na pia kujua changamoto mbalimbali zinazowakabili askari wa kituo hicho.

Lugola aliowasili kituoni hapo jana mchana na akaelekea moja kwa moja mahabusu na akaomba kitabu cha taarifa ya makosa mbalimbali yaliyoripotiwa kituoni hapo, na akamuelekeza askari wa zamu awapange foleni watuhumiwa hao ili aweze kuwahoji makosa yao na pia Mkuu wa Kituo cha polisi hicho, aweze kufafanua makosa yao.

Baada ya watuhumiwa hao, Lugola licha ya kuwapongeza polisi wa kituo hicho kwa kufanya kazi vizuri, pia alimtaka Mkuu wa Kituo hicho, Steven Kimaro kua makini na utendaji wake na kuwafuatilia kwa umakini utendaji kazi wa askari wake kwasababu yeye ndio kiongozi wa kituo hicho.

“Sipendi wananchi waonewe, haki itendeke na si kila kosa lazima mtuhumiwa awekwe mahabusu, tumieni busara umakini ili tuweze kutenda haki na pia nataka jeshi hili liwe na picha nzuri zaidi kwa jamii,” alisema Lugola.

Pia alifafanua kua, hataki kusikia askari polisi anatuhumiwa kwa rushwa au kunyanyasa wananchi, na endapo taarifa hizo zitamfikia basi atahakikisha askari huyo anachukulia hatua za kisheria.

Aidha, Waziri Lugola alitaka polisi wa usalama barabarani kufuata sheria na pia si kila kosa lazima mwenye gari kuandikiwa risiti ya malipo, makosa mengine watoe elimu zaidi kwa madereva hao ili taifa liweze kusonga mbele.

Lugola Septemba 25 anatarajia kuanza ziara yake ya kutembelea mikoa yote nchini, ambapo ataanza ziara katika Wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma ambapo atazungumza na askari na maafisa polisi, watumishi wa taasisi zilizopo katika wizara yake na baadaye atafanya mkutano wa hadhara kwa kuzungumza na wananchi pamoja na kusikiliza kero zao mjini humo.

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Salamu Za Rambirambi Kutoka Mataifa Mbalimbali Na Balozi Za Tanzania Nje Ya Nchi

$
0
0
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeendelea kupokea salamu za rambirambi kutoka kwa marais, mawaziri wakuu wa mataifa mbalimbali duniani kwenda kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, kufuatia ajali ya kuzama kwa kivuko cha MV Nyerere iliyotokea kwenye Ziwa Victoria, Mkoani Mwanza tarehe 20 Septemba, 2018 na  kusababisha vifo, majeruhi na upotevu wa mali.

Baadhi ya salamu zilizopokelewa ni pamoja na kutoka kwa Rais wa Kenya, Mheshimiwa Uhuru Kenyatta, Rais wa Urusi, Mheshimiwa Vladmir Putin, Rais wa China, Mheshimiwa Xi Jinping, Rais wa Ujerumani, Mheshimiwa Frank-Walter Steinmeier, Rais wa Saharawi, Mheshimiwa Brahim Ghali, Mtawala wa Kuwait, Mtukufu Sheikh Sabah Al-Ahmad al Jaber Al-Sabah, Baba Mtakatifu, Papa Francis, Rais wa Italia, Mheshimiwa Sergio Mattarella, Rais wa Uturuki, Mheshimiwa Recep Tayyip Erdogan, Rais wa Finland, Mheshimiwa Sauli Niinistö, Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Mheshimiwa Joseph Kabila Kabange na Rais wa Jamhuri ya Sudan, Mheshimiwa Omar Hassan Ahmed Al-Bashir. 

Viongozi wengine ni Waziri Mkuu wa Israel, Mheshimiwa Benjamin Netanyahu, na Waziri Mkuu wa Sweden, Mheshimiwa Stefan Löfven.

Viongozi hao wameeleza kusikitishwa kwao na taarifa za vifo vilivyosababishwa na  ajali hiyo na kuwatakia majeruhi kupona haraka.

Sehemu ya nukuu za salamu hizo zinasema “Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, nilipokea kwa huzuni na masikitiko makubwa taarifa za ajali ya kivuko cha MV Nyerere iliyosababisha vifo vya watu wengi, majeruhi na wengine kutojulikana walipo. Kwa niaba ya Serikali na wananchi wa Kenya naomba upokee na kufikisha salamu zetu za rambirambi kwa wafiwa na wananchi wote wa Tanzania kufuatia ajali hiyo na tunawaombea majeruhi wote wapone haraka” ni sehemu ya nukuu ya salamu kutoka kwa Mheshimiwa Rais Kenyatta

“Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, nilishtushwa na taarifa za ajali hiyo mbaya iliyotokea Mkoani Mwanza. Kwa niaba ya Serikali ya China, wananchi na mimi binafsi natoa pole kwa wafiwa wote na majeruhi” inasema sehemu ya salamu kutoka kwa Rais wa China, Mheshimiwa Xi Jinping.

Naye Rais wa Urusi, Mheshimiwa Putin amesema “Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, tafadhali naomba upokee salamu zangu za rambirambi kufuatia ajali iliyotokea. Naomba salamu hizi ziwafikie wafiwa wote na ninawaombea majeruhi wapone haraka”

Aidha, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imepokea salamu za rambirambi kutoka kwa balozi mbalimbali zinazowakilisha nchi zao hapa nchini pamoja na mashirika ya kimataifa yaliyopo nchini, ikiwemo ubalozi wa Marekani, ubalozi wa Ufaransa, ubalozi wa Sudan Kusini, Ubalozi wa Falme za Kiarabu (UAE), Serikali ya Brazil, Ubalozi wa Cuba, ubalozi wa Nigeria na salamu kutoka kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Kimataifa nchini.

Wakati huohuo, Wizara imepokea salamu za rambirambi kutoka kwa mabalozi wanaowakilisha Tanzania kwenye nchi mbalimbali. Salamu zilizopokelewa zinatoka kwa mabalozi wote wa Tanzania  katika nchi za Qatar, Ufaransa, Uingereza, Uholanzi, Afrika Kusini, Sweden, Nigeria, Burundi, Uganda, Kenya, Ubelgiji, Zambia, Msumbiji, China, Japan, Brazil, Comoro, Algeria, Sudan,  Canada,

Kadhalika tumepokea salamu kutoka kwenye balozi zetu zilizoko Marekani, Uturuki, Rwanda, Umoja wa Falme za Kiarabu, Misri, Kuwait, Saudi Arabia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Zimbabwe, Malawi, Uswisi, India, Italia, Jamhuri ya Korea, Urusi, Israel, Ethiopia, Ujerumani, Oman na Malaysia.

Baadhi ya nukuu ya salamu za rambirambi za mabalozi hao zinasomeka kama ifuatavyo “Inna Lillah Wainna Illah Rajiuon.  Kwa  niaba  ya  Ubalozi  Abuja  na  Watanzania  waliopo  katika  eneo  letu  la  uwakilishi,  tunatoa  pole  kwa  Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  familia  na  Watanzania  kwa  ujumla  kwa  msiba  mkubwa  uliotufika.  Mwenyezi  Mungu  atupe  subira  na  faraja  katika  kipindi  hiki  cha  majonzi  na  aziweke  roho  za  marehemu  mahali  pema  na  majeruhi  wapone  haraka, Amin  Amin,”  ni kauli yake Mheshimiwa Muhidin Ally Mboweto, Balozi wa Tanzania nchini Nigeria.

Naye Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mheshimiwa Dkt. Wilbroad Slaa anasema “kwa niaba ya wenzangu katika kituo cha Stockholm tunatoa pole za dhati kwa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ndugu na familia zote zilizoguswa na msiba huu mkubwa. Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi na kuwatia nguvu na ujasiri ndugu wote walioguswa na msiba huu”.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Mheshimiwa Balozi Modest Mero alisema haya; “Ubalozi wa New York tunatoa pole kwa ajali mbaya ya Meli ya MV Nyerere iliyopelekea wengi kupoteza maisha na wengi kuumia.  Tunawaombea marehemu pumziko la milele na wote waliojeruhiwa wapone haraka.”

Balozi wa Tanzania nchini China, Mheshimiwa Mbelwa Kairuki alieleza masikitiko yake kwa kusema kuwa “nasi huku Beijing tunaungana na wenzetu kutoa pole kwa Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Watanzania na wanafamilia walioguswa msiba huu mzito. Mwenyezi Mungu awape nguvu na awajalie moyo wa subira wakati wote mnaposhughulika na msiba huo.

“Japan na diaspora yetu tunatoa pole kwa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Watanzania wote kwa msiba huu uliotokana na kuzama kwa kivuko. Mungu atupe nguvu wote tuliobaki na awape pumziko la amani wenzetu waliotutangulia. Kwa majeruhi tunawaombea wapone haraka na wavumilie mstuko huu mkubwa katika maisha yao. Marehemu wapumzike kwa amani”. Hizi ni salamu kutoka kwa Mheshimiwa Mathias Chikawe, balozi wa Tanzania nchini Japan.

Kwa upande wake, Balozi wa Tanzania nchini Abu Dhabi alisema haya; “Ubalozi wa Tanzania Abu Dhabi, tumepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za ajali ya MV Nyerere.Kwa niaba ya watumishi wote wa Ubalozi, tunatoa mkono wa pole kwa Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Watanzania wenzetu wote kwa msiba huu mkubwa. Mwenyezi Mungu awajaalie marehemu wapumzike mahali pema na awajaalie majeruhi kupona mapema. Amin”.

Naye Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mheshimiwa Dkt. Asha-Rose Migiro akieleza kuguswa na ajali hiyo alitoa kauli hii “Ubalozi wa Tanzania London unajumuika na Watanzania wenzetu kutoa pole kwa Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, familia na ndugu wa wale wote waliopatwa na msiba kutokana na ajali hii. Tunawaombea majeruhi wapone haraka na warejee katika shughuli zao za kujikimu na kulijenga taifa letu”.

Kwa upande mwingine, Wizara imepokea salamu za rambirambi kutoka Baraza la Diaspora wa Tanzania ulimwenguni kote (TDC Global) ambao wameeleza masikitiko makubwa kufuatia ajali hiyo mbaya. Sehemu ya ujumbe wao unasomeka kama ifuatavyo; “TDC Global, kwa masikitiko makubwa, inatoa salamu za rambirambi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Watanzania wote, ndugu, jamaa na marafiki kwa vifo vilivyotokana na ajali ya kuzama kwa kivuko cha MV. Nyerere kinachofanya safari zake kati ya visiwa vya Bugorora na Ukara katika Ziwa Victoria. Kama TDC Global, tunaungana na Watanzania wote katika kuomboleza msiba huu mzito kwa taifa letu. Pia tunatoa pole kwa majeruhi wote na kuwaombea wapone haraka”.

Hassan Hassan Alivyojishindia Laki 5 FASTA.....Ni Rahis Mno, Jaribu Bahati Yako

$
0
0

Hassan Hassan (23), Mkazi wa Pugu, Dar es Salaam ni mshindi wa Shilingi Laki 5 kupitia MojaSpesho, ambaye amebainisha kuwa alianza kucheza siku nne zilizopita, na siku zote hizo alidaka ushindi.

“Siku ya kwanza nilishinda Elfu tano, Siku ya pili Elfu mbili, siku ya tatu Elfu moja na siku ya nne nkashinda laki tano.” amefafanua Hassan.

Hassan ameeleza kuwa, pesa aliyoshinda itamsaidia kusogeza mbele ujenzi wa nyumba yake aliouanza kabla ya kushinda.

Nawe pia unaweza kuwa mshindi kila siku na jackpot ya kila wiki. Jinsi ya kucheza Mojaspesho ni rahisi
 
1. Nenda kwenye menu yako ya #Mpesa, #TigoPesa, #AirtelMoney au #Halopesa;
2. Chagua lipia bili
3. Ingiza kampuni namba 123255
4. Ingiza kumbukumbu namba zako 3 za bahati zikifuatiwa na neno SEE mf. 123SEE
5. Weka kiasi kuanzia sh 1000 na utakua umecheza #Mojaspesho.

TCU Yasitisha Udahili wa Wanafunzi Kwa Vyuo 7.....Viwili Vyafungiwa

$
0
0
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), imesitisha masomo na udahili wa wanafunzi wapya kwa ngazi zote za masomo na katika programu kwenye baadhi ya vyuo vikuu kutokana na kukosa vigezo.

Pia imefuta vituo viwili vya vyuo vikuu na kuamuru wanafunzi wanaoendelea na masomo wahamishwe.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Jumanne Septemba 25, Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa amevitaja vyuo hivyo kuwa ni pamoja na Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala nchini (KIUT), Chuo cha Teofilo Kisanji (TEKU), Chuo Kikuu kishiriki cha Marian (MARUco) na Chuo Kikuu Kishiriki cha Kumbukumbu ya Kardinali Rugambwa  (CARUMUCo).

Vyuo vingine ni Chuo cha kumbukumbu ya Sebastian Kolowa (SEKOMU), Chuo kikuu cha Mt. Yohana cha Tanzania (SJUT-St. Marks Centers na Chuo kikuu cha Umoja wa Afrika Tanzania (UAUT).

Vyuo hivyo ni pamoja na Chuo kikuu Teofilo Kisanji, Kituo cha Tabora  na Chuo kikuu Mt. Yohana cha Tanzania, Msalato (SJUT -Msalato Center).

Aidha, amevitaja vyuo vilivyositishiwa utoaji mafunzo na kuamuru wanafunzi wote wanaoendelea na masomo wahamishwe kuwa ni Mlima Meru (MMU), Chuo Kikuu cha Bagamoyo (UoB), Chuo cha Eckernforde Tanga (ETU) cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta Kituo cha Arusha na Chuo Kikuu Kishiriki cha Josiah kibira (JOKUCo).

“Asitokee mwanafunzi yeyote akasajiliwa katika vyuo hivyo na wanaotakiwa kuhama wawasiliane na vyuo vyao haraka,” amesema Profesa Kihampa.

Kwa upande wake mwakilishi kutoka Bodi ya Mikopo (HELSB), Deus Changala amesema waliokuwa na mikopo wasiwe na wasiwasi itapelekwa watakapokuwa.

Kila Mfiwa Ajali ya MV Nyerere Kulipwa Milioni 1 Badala ya Laki 5

$
0
0
Rais John Magufuli ameagiza wafiwa wote waliopoteza ndugu zao kwenye ajali ya kivuko cha Mv Nyerere kupata Sh 1 milioni baada ya awali kupewa Sh 500,000 kila mmoja.

Hata hivyo watu 41 walionusurika kwenye ajali hiyo nao watapewa Sh1 milioni kila mmoja.

Fedha hizo zinatokana na michango ya kampuni, watu na taasisi mbalimbali wanaoendelea kujitokeza kuchangia waathirika hao.

Awali, familia za waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo iliyotokea Alhamisi iliyopita walipewa Sh500,000 kwa kila mtu aliyefariki, fedha ambazo zimepatikana kutokana na michango ya Watanzania, kampuni na taasisi mbalimbali.

Akizungumza na vyombo vya habari jana kisiwani Ukara wilayani Ukerewe, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isaac Kamwelwe alisema leo wataanza kutoa fedha hizo kama walivyoagizwa na Rais Magufuli kwa familia za marehemu na wote walionusurika.

“Rais ameniagiza niwaambie kwamba fedha kwa waliopoteza ndugu zao na wale 41 walionusurika, sasa watapata Sh1 milioni kila mmoja. Kuanzia kesho (leo) tutaanza kutoa fedha hizo, wapeni taarifa,” alisema Kamwelwe.

Alisema kiwango cha fedha kilichokusanywa mpaka jana jioni ni Sh397 milioni ambazo zimetolewa na watu na taasisi mbalimbali. Alisema Rais Magufuli amesema fedha hizo ni za wananchi walioathirika na ajali hiyo.

Waziri huyo alisema mpaka kufikia jana jioni, miili miwili ya watoto ilipatikana wakati kazi ya kukiinua kivuko hicho ikiendelea na kufanya idadi ya waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo kufikia 226.

Kuhusu kurudisha hali ya usafiri katika kisiwa hicho, Kamwelwe alisema leo au kesho kitapelekwa kivuko kingine kinachoitwa Mv Temesa ambacho kiko Mwanza kwa ajili ya kutoa huduma wakati shughuli ya kukiinua kivuko cha Mv Nyerere ikiendelea.

Mkebe Spesho Wa Dawa Ya Mitishamba Yenye Uwezo Mkubwa Wa Kumsaidia Mtu Aliyeathirika Na Upungufu Wa Nguvu Za Kiume

$
0
0
Je, Unamatatizo haya na yamekusumbua kwa muda mrefu bila kupata tiba?

Wanaume wengi wanaupungufu wa nguvu za kiume. na kuwa na maumbile madogo ya kiume. 

Magonjwa kama. kisukari. presha, ngiri, kolodani kuvimba busha tumbo kuunguruma kujaa ngesi na kutopata choo vizuri , punyeto nk huchangia kwa kiasi kikubwa upotevu wa nguvu za kiume 

Tumia dawa nzuri ya mitishamba ambayo haina madhara kwa mtumiaji ata uwe na miaka 80 ,    inatibu na kuponyesha matatizo haya yote         

 SUPER SHAFT;  ni dawa yenye uwezo mkubwa wa kuogeza nguvu za kiume mara dufu na maumbile madogo ya uume                                    
 (1) itakufanya uwe na nguvu za ajabu ukiwa unafanya tendo la ndoa                                        
 (2) inaongeza hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka.                           
 (3) itakufanya uchelewe kufika kileleni ndani ya dk 30 na kuimalika uume zaidi                                  
(4) pia itakupa nguvu za kusimamisha uume wako barabara kama msumari wakati wa tendo la ndoa 
    
NYATI POWER; inarefusha na kunenepesha uume saizi utakavyo kuazia 1_8 unene  sm 2_4 
(1) inaimalisha mirija ya uume iliyo legea ama kusinyaa                                                                       
(2) inasaidia kusafisha mirija ya kwenye uume na hivyo kusaidia kuongeza kasi ya msukumo wa damu kwenye mishipa ya uume                        
(3) Husaidi kuurudisha nje uume uliyoigia ndani      
(4) inasaidia kuongeza manii nyingi ambazo zina viini vya uzazi                                                              
(5) Husaidia kutibu madhara ya punyeto matumizi makari ya madawa ya kizungu mirungi bangi na sigara

Tunatibu Magonjwa Yote Sugu Ngiri Kolodani Kuvimba Busha Bila Kufanyiwa Opresheni Tezi Dume Kisukari Presha Aina Zote Ugonjwa Wa Moyo Kwikwi Kichomi Miguu Kufa Ngazi Nk

Tunapatikana Magomeni Mikumi Karibu Na Kanisa Katoriki La Roma

Tumaini Tradition Clinc Ndiyo Sululisho La Matatizo Tote 

PIGA SIMU 0745_495181 AU  0682_ 644040                               
WOTE MNAKARIBISHWA TUMAINI TRADITION CLINC 
 

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE;LUKUBA 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO   0658920640/ 0754372325 / 0620806813
 
HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.

Makontena ya Makonda kugaiwa bure

$
0
0
Baada ya minada mitatu iliyofanyika kushindwa kupata mnunuzi wa makontena 20 ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) sasa inafanya taratibu za kuyatoa bandarini ili kuyagawa bure katika taasisi za kiserikali na pamoja hospitali..

Kamishana Mkuu wa TRA, Charles Kichere amesema kuwa watayagawa bure hivi karibuni kwani sheria inaruhusu kugawa katika taasisi za kiserikali na sio binafsi pamoja na maeneo yoyote yenye huduma za kijamii, endapo mali inapokosa mteja.

“Sheria inaturuhusu kugawa popote kwenye huduma za kijamii ikiwemo hospitali, kwakuwa minada yote hakuna mnunuzi aliyepatikana, kuna utaratibu ulioelekezwa kisheria wa kuziondoa mali hizo sehemu ya mnada na moja ya utaratibu huo ni kugawa bure”, amesema Kamishna Kichere.

Mara ya kwanza makontena hayo yalipigwa mnada Agosti 25, lakini yalikosa wanunuzi, watu wengi walishindwa kufikia bei iliyotakiwa, baadhi wakitaja Shilingi milioni 10 kwa kontena badala ya Shilingi milioni 60 inayotakiwa, baaada ya makontena hayo kutouzika ambapo Agosti 26, Makonda alitoa onyo akiwa mkoani Kagera kuwa atakayeyanunua atalaaniwa yeye na uzao wake.

Agosti 27, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Phillip Mpango alikwenda bandarini kuyakagua na kuwataka viongozi wenzake serikalini kutathmini kauli zao na akawaomba wanaotaka kuyanunua wasiogope.

Akizungumza na madiwani, viongozi na watumishi wa Halmshauri ya Wilaya ya Chato mkoani Geita, Agosti 30, Rais John Magufuli alizungumzia sakata hilo akiwataka viongozi kuwatumikia wananchi bila kujali wapo kwenye nafasi gani.

“Umesikia hili sakata la Dar es salaam, eti Mkuu wa Mkoa ameleta makontena, ameambiwa alipe kodi, kwa nini asilipe kodi?” Alihoji Rais Magufuli. Sheria za nchi zinasema ni mtu mmoja katika nchi mwenye dhamana ya kutolipa kodi kwa mujibu wa sheria ya fedha, sheria ya madeni, sheria ya dhamana na ya misaada.

“Sasa ukichukua makontena kule umezungumza na watu wengine labda na wafanyabiashara, unasema ni makontena yako halafu ukasema tena labda ni ya walimu, wala hata shule hazitajwi maana yake nini”.

Chanzo:Eatv

Serikali Yakanusha Uwepo Wa Vidonge Vyenye Dawa Kwenye Chupa Za Chai

$
0
0
Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na Shirika la Viwango nchini (TBS), zimetoa ufafanuzi kuhusu vidonge vinavyodaiwa kuwapo kwenye chupa ya chai ambavyo vinadaiwa kuwa na madhara kwamba si sumu na havina madhara kama inavyodaiwa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na taasisi hizo, vidonge hivyo si sumu bali ni vitu vilivyotengenezwa kwa kutumia karatasi ambavyo ni teknolojia ya kisasa inayotumika kutenganisha kuta mbili za chupa ili kutunza joto la kimiminika kilichowekwa kwenye chupa husika.

“Hivi karibuni kumekuwepo na video inayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu vidonge vilivyomo kwenye baadhi ya chupa za chai kuwa vidonge vyenye dawa yenye madhara kwa watumiaji na video nyingine ya lugha ya kiarabu ikieleza vidonge hivyo vina madini ya asbestos.

“Tunawahakikishia wananchi kuwa bidhaa hizo ni salama kwa matumizi ya kutunza joto la kimiminika kama vile chai,” imesema taarifa hiyo.

Pamoja na mambo mengine, taasisi hizo zimeonya wananchi kuepuka kusambaza taarifa kupitia mitandao ya kijamii zisizohakikiwa na taasisi hizo ili kuondoa taharuki zisizo za lazima.

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Michango ya Mv. Nyerere yafikia milioni 557....Mwili Mwingine Waopolewa Leo

$
0
0
Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Injinia Isaac Kamwelwe amesema michango ya kusaidia waathirika wa ajali ya Mv Nyerere ambayo ilipelekea vifo vya mamia ya watu  katika kisiwa cha Ukara imeshafikia milioni 557 huku zoezi la ugawaji wa fidia kwa familia hizo likiwa limekwisha anza.

Akizungumza wakati akipokea misaada kutoka kwa taasisi mbalimbali leo ikiwemo Kanisa katoliki jimbo kuu la Dar es salaam Waziri Kamwele amesema kwa leo kamati hiyo imepokea shilingi milioni 160.

“Kwa leo kuanzia asubuhi mpaka sasa hivi akaunti yetu ya maafa imepokea milioni 160 na jumla ina  shilingi milioni 557, tumeshanza kulipa wafiwa kila aliyepoteza maisha ndugu yake atapatiwa shilingi milioni 1 kuanzia leo, na fedha tunayotumia ni hii ambayo watanzania wamewachangia wenzao ndo tunayoigawa..” Amesema Waziri Kamwelwe.

Akizungumzia zoezi la utoaji wa kivuko cha Mv Nyerere kilichozama Mkuu wa Majeshi nchini Jenerali Venance Mabeyo amesema wamefikia hatua za mwisho za kuhakikisha kivuko hicho kinasimama kama kawaida.

“Tumejitahidi kukinyanyua lakini kililala ubavu, Mafundi wanaendelea kufunga vifaa vya kusaidia kukiokoa, vilevile tunaendelea na uokozi wa miili na asubuhi hii tumepata maiti moja, tutahakikisha tunaimaliza shughuli hii mapema.” Amesema Jenerali Mabeyo.

Serikali Kuendelea Kushirikiana Na Wadau Kuboresha Elimu Nchini.

$
0
0
Na Lilian Lundo – MAELEZO, Dodoma.
Serikali imesema itaendelea kushirikiana na wadau wa maendeleo nchini ili kuhakikisha kila mtoto wa kitanzania anapata elimu bora.

Hayo yameelezwa leo Jijini Dodoma na Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Joyce Ndalichako alipokuwa akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Wadau wa Elimu wa kujadili mafanikio na changamoto za elimu nchini.

“Mkutano huu ni muhimu sababu unapitia na kujadili mafanikio na changamoto katika sekta ya elimu na kutoa mapendekezo ya changamoto hizo ili kuboresha sekta hii,” amesema Prof. Ndalichako.

Aidha, amesema Serikali itaendelea kutumia mapendekezo yanayotolewa na wadau wa maendeleo ya elimu nchini ili kuhakikisha hakuna mtoto wa Kitanzania anaachwa nyuma katika kupata elimu bora mijini na vijijini.

Amesema, Serikali ya Awamu ya Tano imekuwa na mafanikio makubwa katika sekta ya elimu ambapo imefanikiwa kutoa elimu bila malipo kwa shule za msingi na sekondari, mafunzo kwa mbalimbali kwa walimu, walimu wamepangiwa kazi kulingana na uhitaji pamoja na kuendelea kuwaajiri.

Vile vile Wadhibiti Ubora wa Elimu wamewezeshwa kwa kununuliwa magari na pikipiki ili kuzifikia shule kwa urahisi.

Prof. Ndalichako amewataka wadau hao kuutumia mkutano huo kujadili na kutoa mapendekezo ya namna ya kuimarisha ufundishaji wa masomo ya sayansi, kuunganisha elimu ya nadharia na vitendo, mafunzo ya walimu, elimu yenye usawa mijini na vijijini pamoja na mahudhurio shuleni.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Dkt. Leonard Akwilapo amesema mkutano huo umehusisha wadau mbalimbali wa elimu hapa nchini zikiwemo taasisi za utafiti, wadau wa maendeleo ya elimu, maafisa elimu pamoja na wanafunzi ambapo kwa pamoja watajadili mafanikio na changamoto katika sekta ya elimu na kutoa mapendekezo ya namna ya kukabiliana na changamoto hizo.

CHADEMA Wazindua SERA Mpya ya Chama Chao

$
0
0
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimezindua kitabu cha sera za chama hicho toleo la mwaka 2018 ikiwa na sera 12 ambazo zimezungumzia namna ambavyo chama hicho kimejipanga kuinua maisha ya mtanzania na taifa kwa ujumla.

Akizungumza leo Septemba 25, 2018 wakati wa uzinduzi huo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema sera hizo zitakuwa zinafanyiwa marekebisho kulingana na wakati.

Amesema eneo la kwanza lililoko kwenye sera hiyo ni ile inayolinda uhuru wa wananchi.

Mbowe amesema Mwalimu Julius Nyerere aliwahi kuzungumzia suala la maendeleo ya watu na uhuru, jambo ambalo wamelijadili kwa kina kwenye sera hiyo.

“Mwalimu Nyerere alisema sera za Chadema zilikua sera za kuinua maisha ya watanzania, kwa hiyo chama chetu sio chama cha kutafuta uhuru, bali sera zetu zimejikita zaidi kuhakikisha kila mtanzania anakua na maisha bora, sera hizi zimelenga maeneo 12 na tutaweza kuzifanyia marekebisho mara kwa mara pindi zitakapohitajika pia ni ruhusa kunakiliwa na vyama vingine.”

Amelitaja eneo lingine ni nafasi kuwa na sera zinazolenga misingi ya uchumi.

Amesema katika eneo hilo wameainisha ni kwa namna gani wananchi watapata huduma za kijamii.

Amefafanua eneo hilo limeainisha namna uchumi utakavyokuwa endelevu badala ya kuwa uliohodhiwa na Serikali.

Mbowe ameitaja sera nyingine ni zinazoilinda na kuihuisha jamii kupata huduma ya maji, barabara yasiwe mambo yanayofanywa na sekta binafsi bali yafanywe na Serikali.

"Sasa hivi kumejengeka dhana kuwa Serikali uliyojenga shule, zahanati inakuwa ni kama msaada, hii si sawa hayo ni majukumu ya Serikali," amesema Mbowe.

Mbowe amesema kabla ya kutayarisha sera hiyo wametumia mwaka mzima kufanya tafiti na kukusanya maoni kutoka kwa watu mbalimbali.

KCB Bank wachangia Mil 125 maafa ya ajali ya Mv Nyerere

$
0
0
Bodi ya Wakurugenzi, Menejimenti na Wafanyakazi wa KCB Bank Group, wameungana na waombolezaji wa msiba uliotokana na kuzama kwa kivuko cha MV Nyerere kwa kuchangia kiasi cha fedha taslim shilingi 125,000,000/=

Akikabidhi msaada huo wa fedha Mkurugenzi wa Bodi ya KCB, Zuhura Muro, alieleza kuwa wameguswa na maafa hayo na hivyo wanaahidi kuungana na serikali kadri wanavyoweza.

"Tunajua hatuwezi kumaliza shida au mahitaji ya waathirika hawa, hivyo tunapenda kuhamasisha taasisi nyingine zinazoguswa  kama sisi kutoa misaada yao ya hali na mali, huku tukiwaombea marehemu wapumzike  kwa amani na majeruhi majeruhi wapate kupona haraka," amesema.

Kutokana na kiasi hicho kilichotolewa na Bank KCB pamoja na michango ambayo  wananchi na tasisisi mbalimbali zilizoguswa na kuchangia rambirambi katika maafa hayo imefikia jumla ya shilingi milioni 557

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi astaafu utumishi wa umma

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi amewataka watumishi wa wizara hiyo kufanyakazi kwa weledi ili kuogeza tija kwa Taifa.

Katibu mkuu huyo ametoa rai hiyo leo, Septemba 25, 2018 alipokuwa akiwaaga watumishi wa wizara baada ya kustaafu jeshini na kwa mujibu wa sheria tangu Septemba 16.

Milanzi amesema kwa muda wote aliitumikia wizara hiyo alipata ushirikiano wa kutosha uliomuwezesha kuiongoza vyema wizara hiyo na kuchangia mafanikio yaliyojidhihirisha kwenye sekta za wanyamapori, utalii, misitu na nyuki na malikale.

Katika kipindi cha uongozi wake wizarani hapo, amesema wizara imepata mafanikio katika  vita dhidi ya ujangili.

“Tumekamilisha mambo mengi. Kila mmoja wenu alikuwa akinisaidia ili wizara isonge mbele. Hakuna aliyetaka kunikwamisha. Ninawashukuru sana,” amesema Milanzi.

Akizungumza kwenye hafla fupi ya kumuaga Milanzi iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu cha Dodoma, kaimu katibu mkuu wa wizara hiyo, Dk Aloyce Nzuki amempongeza kwa utumishi wake.

“Umeweka mifumo mizuri na kubuni mikakati na mbinu za kutatua changamoto zilizokuwa zinaikabili wizara na kuhakikisha watumishi wanapata utulivu wa akili kwa kujali maslahi yao. Uliwawezesha kufanya kazi wakiwa watulivu wa akili jambo liliongeza ufanisi kazini,” ameeleza Dk Nzuki.

Milanzi aliteuliwa kuwa katibu mkuu wa wizara hiyo Disemba 2015. 

“Nashukuru nimestaafu salama. Wizara hii ni muhimu sana kwa maendeleo ya nchi na inagusa masilahi ya wengi. Jukumu nililopewa lilikuwa kusimamia maslahi ya nchi, naamini kuna masilahi ya watu yalivurugwa hivyo mimi kuwa mwiba kwao,” amesema akiaga kamanda huyo wa Jeshi la Wananchi (JWTZ).

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya Septemba

Kiswahili Kuwa Lugha Kuu Ya Mawasiliano Barani Afrika

$
0
0
Na Fatma Salum-MAELEZO
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe amebainisha kuwa lugha ya Kiswahili inatarajiwa kuwa lugha kuu ya mawasiliano katika bara la Afrika ifikapo mwaka 2063.

Waziri Mwakyembe ameyasema hayo jana Jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya Kampeni Ya Uzalendo na Utaifa kwa mwaka 2018 yanayotarajiwa kufanyika Desemba 8 Jijini Dodoma ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais John Pombe Magufuli.

Alisema kuwa kampeni hiyo kwa mwaka huu imejikita katika kuhamasisha matumizi ya lugha ya Kiswahili ambayo ni kielelezo kikubwa cha utashi na uhai wa taifa la Tanzania na inakua kwa kasi sana barani Afrika na duniani kote kwa ujumla.

“Sasa hivi Kiswahili ni lugha ya kumi kati ya lugha elfu 6 zinazoongelewa na watu wengi duniani na kwa mujibu wa Tafiti za Umoja wa Afrika zinaonesha kuwa ifikapo mwaka 2063 Kiswahili kitakuwa lugha kuu ya mawasiliano katika bara la Afrika na utambulisho wa mtu mweusi duniani,” alisema Mwakyembe.

Alieleza kuwa dunia yote inatambua kwamba Tanzania ndio chimbuko la lugha adhimu ya Kiswahili hivyo watanzania wanapaswa kujivunia lugha hiyo na kuitangaza kwa kuwa ni sehemu ya utamaduni wa taifa na msingi wa uzalendo na utaifa.

Waziri Mwakyembe alibainisha kuwa kampeni hiyo mwaka huu imejikita katika kuhamasisha matumizi ya lugha ya Kiswahili ili kuwasisitiza watanzania kuthamini lugha yao na utamaduni wao na kurejea kwenye misingi ya maadili ya taifa lao.

Alisema kuwa sasahivi kuna changamoto kubwa ya mmomonyoko wa maadili inayosababishwa na baadhi ya watu hasa vijana kuiga tamaduni za nje kutokana na utandawazi hivyo kupelekea kudharau utamaduni wao ikiwemo lugha ya Kiswahili jambo ambalo lisipochukuliwa hatua madhubuti litaleta athari kwa jamii.

Pia Waziri Mwakyembe alitoa pongezi kwa Rais John Pombe Magufuli kwa mchango wake mkubwa anaoonesha katika kutumia, kukuza na kuitangaza lugha ya Kiswahili ndani na nje ya nchi hivyo amekuwa ni mfano wa kuigwa.

Aidha alitoa rai kwa watanzania wote na wadau mbalimbali kuunga mkono kampeni hiyo kwa hali na mali ili Tanzania iweze kufanikiwa kulinda misingi ya utamaduni na utaifa hususan lugha ya Kiswahili.

Kampeni ya Uzalendo na Utaifa ilianza rasmi mwaka jana 2017 na itakuwa ikiadhimishwa kila mwaka ambapo kwa mwaka huu kauli mbiu yake ni ‘Kiswahili Uhai Wetu, Utashi Wetu’. 

Waziri: “Sehemu Pekee Ya Vijana Kuimarisha Kipato Ni Kupitia Sekta Ya Kilimo”

$
0
0
Na Mathias Canal-WK
Imeelezwa kuwa sehemu pekee ya kuimarisha kilimo cha mwananchi mmoja mmoja, wananchi katika makundi ya kijamii hususani vijana ni kupitia sekta ya kilimo kwani ndio sehemu pekee ya ukombozi wa mkulima katika jamii.

Imeelezwa kuwa kuna uwezekano wa kufanya biashara mbalimbali nchini ambazo zinaweza kuongeza kipato lakini sahemu sahihi isiyokuwa na jazba na dhoruba katika utendaji ni kufanya kilimo biashara ambacho kamwe hakiwezi kumtupa mkulima.

Dkt Charles Tizeba Waziri wa kilimo, ameyasema hayo leo tarehe 25 Septemba 2018 wakati akizungumza na vijana wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Tanga ambao wapo katika kambi maalumu ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.

Vijana hao ambao wameamua kutumia nguvu zao pasina malipo wameamua kwa umoja wao kuunga mkono juhudi za Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli kwa kauli yake inayohamasisha chachu na juhudi za kiutendaji kwa wananchi ya “Hapa Kazi Tu”.

Aidha, katika kuhamasisha juhudi za kiutendaji Waziri huyo mwenye dhamana ya kilimo ameunga mkono juhudi za vijana hao kwa kuchangia fedha ya chakula shilingi 1,100,000 sambamba na kushiriki ujenzi wa jengo maalumu la upasuaji.

Waziri wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba alitembelea ujenzi huo wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza akiwa safarini kutembelea mashamba ya mkonge ikiwa ni siku ya pili ya ziara ya kikazi Mkoani Tanga aliyoianza jana tarehe 25 Septemba 2018 ya kukutana na makundi mbalimbali ya wakulima wa zao la Mkonge ili kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazowakabili wakulima wa zao hilo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>