Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Polisi Ruvuma watishia Kupiga Marufuku biashara ya bodaboda mkoani humo

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limesema litaomba vyombo vya kutunga sheria kuondoa biashara ya bodaboda, kufuatia madereva wa vyombo hivyo kutotii magizo mbalimbali ya serikali ikiwemo la kuwataka kila mwendesha bodaboda kuwa na kofia ngumu mbili.

Kauli hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Gemini Mushy  kufuatia agizo la Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Christina  Mndeme alilolitoa mwezi mmoja na nusu uliopita wa kuwataka  madereva wa bodaboda kuhakikisha ndani ya mwezi mmoja wanakuwa na kofia ngumu mbili, jambo ambalo bodaboda wanaonekana wameshindwa kulitekeleza huku  wakitoa sababu mbalimbali.

Mbali na Kamanda huyo kusema hivyo nao baadhi ya abiria wa bodaboda mkoani humo  wamesema, hata wao wangependa kuvaa kofia hizo lakini linapofika suala la kudai kofia, madereva bodaboda hao hutoa sababu zisizo na msingi.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma amesema wamechukua hatua mbalimbali za kuwakamata baadhi ya madereva bodaboda kuwaweka ndani na kuwafikisha mahakamani lakini bado wamekuwa wagumu kutii bila shuruti.

Viongozi wa zamani wa KCU 1990 Ltd wakosa dhamana

$
0
0
Viongozi wa zamani wa Chama Cha Ushirika Kagera (KCU 1990 Limited) wataendelea kusota rumande baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba mkoa wa Kagera   kuwanyima dhamana kutokana na kukabiliwa na mashtaka ya kuhujumu uchumi kwa ubadhilifu wa shilingi Milioni 218 wanaodaiwa kuufanya.

Akisoma uamuzi kuhusu ombi la washitakiwa kutaka wapatiwe dhamana jana Agosti 27, 2018 hakimu mkazi mfawidhi, John Kapokolo alisema mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi za uhujumu uchumi na kutaka maombi yao yapelekwe kwenye mahakama sahihi.

Akizungumza  mara baada Hakimu Kapokoro kutoa uamuzi huo, mwendesha mashaka wa serikali alisema mahakama hiyo haina mamlaka ya kutoa dhamana kwa watuhumiwa hao kwa kuwa baadhi ya tuhuma zinazowakabili zinahusiana masuala ya kuhujumu uchumi.

Kufuatia uamuzi huo wakili anayewatetea watuhumiwa hao, Aron Kabunga alisema mahakama hiyo haikuwatendea haki wateja wake  kwani mahakama hiyo haikuwa na sababu zozote za kuwanyima dhamana hadi kesi hiyo itapotajwa tena Septemba 10, mwaka huu.

Washitakiwa hao John Binunshu aliyekuwa mwenyekiti wa bodi, Vedastus Ngaiza aliyekuwa meneja mkuu na Bestina Rwebangira walifikishwa katika mahakama hiyo wiki iliyopita na kusomewa mashitaka matano.

Mashtaka yaliyosomwa na wakili mwandamizi wa Serikali, Athumani Matuma ni kula njama, matumizi mabaya ya ofisi, matumizi mabaya ya madaraka, kughushi nyaraka na kuhujumu uchumi na kusababisha hasara ya Sh124 milioni.

Wakili wa washitakiwa Aaron Kabunga alipinga hati ya mashitaka kuwa iliunganisha makosa ya uhujumu uchumi na mengine bila kuwa na kibali cha mkurugenzi wa mashitaka na hivyo alitaka hati hiyo itupiliwe mbali na wateja wake wapewe dhamana.

Tayari Serikali Ilishavunja Uongozi huu uliofikishwa mahakamani na kuchagua uongozi mpya unaokiendesha chama hicho cha Ushirika KCU 1990 Ltd.

Serikali Yaweka Mikakati Thabiti Ili Kudhibiti Ugonjwa Wa EBOLA Usiingie Nchini

$
0
0
Na WAMJW – KAGERA, NGARA
Serikali kupitia Wizara ya Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inaendelea kuweka mikakati thabiti katika maeneo yote hatarishi ikiwemo mipakan na njia za panya ili kudhibiti ugonjwa wa Ebola kuingia nchini.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu jana wakati alipofanya ziara katika Mpaka wa Rusumo kati ya nchi ya Tanzania na Rwanda ili kuangalia ni jinsi gani Mkoa wa Kagera umejipanga katika kudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Ebola kuingia nchini.

Waziri Ummy amesema kuwa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola ambao umetokea eneo la Kivu katika Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo unaiweka Tanzania katika hatari zaidi ya kuweza kupata wagonjwa wa Ebola kutokana na muingiliano wa wananchi baina ya nchi hizo.

“Mlipuko huo wa Ugonjwa wa Ebola ambao umetokea katika Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo sasa hivi inatuweka Tanzania katika hatari kubwa zaidi kupata wagonjwa kutokana na mlipuko huo kutokea eneo la Kivu Kaskazini ambalo ni karibu na Tanzania na muingiliano wa wananchi baina ya nchi hizi mbili ni mkubwa ” Alisema Waziri Ummy Mwalimu.

Aidha, Waziri Ummy alisema kuwa Serikali inaendelea kutoa mafunzo kwa wahudumu wa Sekta ya Áfya ili kufahamu jinsi ya kuwahudumia wanaohisiwa kuwa na Virusi vya ugonjwa wa Ebola sambamba na hilo Serikali imeleta vifaa kinga watakavyovaa wakati wakitoa huduma kwa mgonjwa au mhisiwa wa ugonjwa wa Ebola.

“Kama Serikali, kubwa ambalo tumelifanya ni kuhakikisha tunatoa mafunzo kwa watoa hudumu wa sekta ya Áfya nchini.kwa mujibu wa taarifa ya WHO nchini Kongo watoa huduma wa Áfya 9 wamepata ugonjwa wa Ebola huku mmoja amefariki” Alisema Waziri Ummy.

Pia Waziri Ummy alimwagiza Mkuu wa mkoa wa Kagera kuhakikisha wanatenga Zahanati moja katika maeneo ya mipaka ambayo itakuwa inapokea wahisiwa au wagonjwa wa Ebola, vivyo hivyo kwa ngazi ya Wilaya kutenga hospitali kwa ajili ya wahisiwa pindi utapoingia nchini.

Hata hivyo h Waziri Ummy amewataka wananchi wanaokaa katika vijiji vya mipakani ambavyo vinapokea watu kutoka Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo na Burundi wamuonapo mtu mwenye dalili za ugonjwa wa Ebola wamwelekeze kufika kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya vilivyo jirani.

” Wananchi ambao wanakaa mipakani hasa katika vijiji ambavyo vinapokea watu kutoka Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo na Burundi mnaowajibu wa kuhakikisha mnafuata taratibu za uhamiaji, lakini pale ambapo mtu ameingia na ana dalili za ugonjwa wa Ebola muelekezeni aende kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya” alisema Waziri Ummy

Kwa upande mwingine Waziri Ummy alisema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Áfya imeajiri Watumishi wapya wa Sekta ya Áfya 33 ambao wamesambazwa kwenye maeneo ya mipakani ili kusaidia kudhibiti ugonjwa wa Ebola usiingie nchini.

“Zuli ambalo tumelifanya, tumeajiri watumishi wapya wa Áfya 33 kwa ajili ya kuwasambaza katika maeneo haya ya mipakani ili kudhibiti ugonjwa huu wa Ebola usiingie nchini kwetu” alisema Waziri Ummy.

Mbali na hayo Waziri Ummy amekiagiza kitengo cha Elimu ya Áfya kwa umma kutoka Wizara ya Áfya kutoa Elimu juu ya ugonjwa wa Ebola kwenye Serikali za vijijini kupitia Redio, vipeperushi, video jambo litalosaidia kuweka msukumo kwa wananchi ili kujua athari za ugonjwa huo kwa maendeleo ya Taifa.

Mwisho Waziri Ummy aliendelea kuwatoa hofu wananchi wa Tanzania kuwa ugonjwa wa Ebola bado haujaingia nchini.

Kampuni Za Bima Zatakiwa kuwageukia Wakulima

$
0
0
Na Ahmed Mahmoud Arusha
Kampuni za Bima nchini zimesisitizwa kuepuka kutoa huduma kimazoea badala yake kutoa huduma ya bima kwa makundi yaliyo sahaulika yakiwemo ya wakulima kwa kutoa mikopo ili kufikia uchumi wa kati .

Kauli  hiyo imetolewa jana Agost 27, jijini Arusha  na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk, Ashatu Kijaji wakati  alipofungua mkutano wa 41 wa Umoja wa Kikanda wa Makampuni ya Bima ya Nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika (OESAI) unaoshirikisha nchi 39.

Dk, Kijaji alisema asilimia 75 ya Watanzania ni wakulima ambao bado hawana elimu juu ya bima ikiwemo kupata mikopo ya bei nafuu kwaajili ya kutatua changamoto za kilimo na kufikia katika uchumi wa kati.

Alitoa rai kwa makampuni ya bima nchini kuangalia kundi hilo la wakulima ili nao waweze kunufaika na bidhaa wanazozalisha kwakuwa kundi hilo ni kubwa na ni fursa kwa makampuni ya bima nchini kuongeza idadi ya watumiaji wa bima.

Alisisitiza kuwa watanzania wanatumia bima ni chini ya asilimia moja idadi ambayo hairidhishi kabisa kwakuwa watanzania wapo zaidi ya milioni 45 kwa mujibu wa Takwimu za Taifa.

Naye Kamishna wa Bima wa Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima Nchini (TIRA) Dk, Baghayo Saqware alisema mkutano huo ni wa 41 kufanyika hapa nchini ambapo mkutano wa mwisho ulifanyika mwaka 1995 na kusisitiza kuwa mkutano huo unatoa fursa kwa kampuni za bima zilizopo hapa nchini kujifunza jinsi kampuni za nje the bima zinavyofanya kazi kwa ufanisi.

Pia kampuni hizo zitapata fursa ya kujifunza uboreshaji wa huduma kwa kutumia mfumo wa Tehama unaoleta mageuzi katika utoaji wa huduma bora zako bima,  rasilimali watu, kuongeza wigo wa kutafuta watu mbalimbali kwaajili ya kulipia bima ya maisha.

Naye  Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya mkutano huo,Khamis Suleiman alisema lengo la mkutano huo ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2020 asilimia 50 ya watanzania wawe na aina yoyote  ya bima kwani kwa sasa Tanzania ipo kwenye nafasi ya pili  kwa nchi za Afrika Mashariki kwa kutoa huduma za bima.

Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Yatekeleza Miradi Ya Sh. Trlioni 4.4 Nchini Tanzania

$
0
0
Na Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam
Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zinapewa fedha nyingi  kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) katika kutekeleza miradi ya maendeleo katika Sekta ya Nishati, Maji, Kilimo na Barabara ili kuchochea uchumi na kutimiza malengo ya kuwa nchi yenye uchumi wa kati unaotegemea viwanda ifikapo  mwaka 2025 ambapo mpaka sasa Benki hiyo imewekeza nchini zaidi ya  shilingi trilioni 4.4.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, alipokutana na kufanya mazungumzo na  Mkurugenzi wa  wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) anayeiwakilisha Marekani Bw. J. Steven Dowd katika Ofisi za Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Isdor Mpango, alieleza kuwa Tanzania inapata fedha nyingi za kutekeleza miradi kutoka Benki ya AfDB kutokana na vipaumbele vya Benki hiyo kuendana na vipaumbele vya Serikali ya Tanzania katika Awamu ya Tano ya Uongozi wa Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

“Miradi inayotekelezwa kwa fedha za AfDB ni pamoja na mradi wa kusafirisha umeme kutoka Mbeya, Sumbawanga hadi Nyakanazi utakao gharimu shilingi dola za Marekani milioni 123, miradi mingine ni ile ya ushirikiano na Sekta Binafsi (Dola Milioni 57.6m), ujenzi wa barabara ya Nyakanazi mpaka Burundi kupitia Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma na pia mradi wa ujenzi wa uwanja wa ndege wa Msalato Jijini Dodoma ambao AfDB imeahidi kutoa shilingi bilioni 200 kwa kuanzia”, alieleza Dkt. Mpango.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa  wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) anayeiwakilisha Marekani Bw. J. Steven Dowd, alisema kuwa ameona dhamira ya dhati ya Tanzania katika kufikia malengo tarajiwa hivyo anaangalia uwezekano wa kukaa na bodi ya Benki ya AfDB ili kuendelea kuisaidia Tanzania katika miradi mikubwa ya Nishati ya Umeme na Ujenzi wa Reli ya Kisasa.

Pia ameahidi kuwashawishi wawekezaji kutoka Marekani kuja kuwekeza Tanzania kwa kuwa kuna mazingira mazuri ya uwekezaji na kuishauri Serikali kuweka mazingira mazuri zaidi ya kimikataba kati yake na wawekezaji ili waweze kuwa na uhakikak wa usalama wa uwekezaji wao.

Aliahidi kutumia ushawishi wake katika masuala ya biashara na uwekezaji ili wafanyabiashara wengi kutoka nchji hiyo waweze kuwekeza mitaji na teknolojia hapa nchini na kuisaidia Tanzania kufikia malengo yake ya kukuza uchumi wan chi na watu wake.

Alisema kuwa Rais wa Marekani Donald Trump ni mtu wa vitendo kuliko maneno na kuihakikishia Tanzania kwamba itapata ushirikiano mkubwa kutoka Serikali ya nchi hiyo ili kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais FDkt. John Pombe Magufuli za kujenga uchumi wan chi.

Akieleza kuhusu maombi ya Serikali ya kutaka Benki yake isaidie ujenzi wa MIradi mikubwa ya Maendeleo ikiwemo ujenzi wa Reli ya kiwango cha Kimataifa-SGR, Mradi mkubwa wa kufua umeme kutoka Mto Rufiji, na miundombinu mbalimbali, Bw. J. Steven Dowd alisema kuwa wataijadili miradi hiyo ili kuangalia namna ya kuifadhili.

Akizungumza na vyombo vya habari baada ya Mkutano kati ya Waziri wa Fedha na Mipango na mgeni wake kumalizika, Mkurugenzi wa AfDB Kanda ya Afrika, Dkt. Nyamajeje Weggoro, alisema kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi za Afrika Mashariki yenye hisa nyingi katika Benki hiyo hivyo kunufaika katika fedha zinazotolewa kwa ajili ya miradi ya Maendeleo.

“Tanzania  inahisa takribani asilimia moja kati ya asilimia tano zinazomilikiwa na nchi nane ikiwemo Uganda, Rwanda, Ethiopia, Kenya na Sudani Kusini na pia inatekeleza miradi mbalimbali inayofadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika yenye thamani ya Sh.Trilioni 4.4”, a;lieleza Dkt. Weggoro.

Waziri Mpango amemshukuru Bw. Dowd kwa kuitembelea Tanzania na kuonesha dhamira ya kusaidia miradi ya maendeleo na akaahidi kuendeleza ushirikiano na Benki ya AfDB na pia Marekani.

Mwisho.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne ya Agosti 28

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara.?...... Tunazo dawa na PETE za bahati Zenye Uwezo wa Kubadili Maisha Yako

$
0
0
Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara,M saniiwa Maigizo, Mwanamziki, ama mwanafunzi tunazo Dawa na PETE za Bahati zenye uwezo mkubwawakuyabadilisha maisha yako nakukupatia mafanikio makubwa ndani ya mda mfupi tu. 
Kutana na Chief MAKATA.Yeye ni mtaalam na mtabibu wa nyota zab inadam na bingwa wa tiba za asili Afrikam ashariki. Wasiliana na mtaalam huyu kwani yeye ufaulu pale wote waliko shindwa na pia humaliza kazi zilizo shindikana ama zilizo achwa ndani ya siku1 tu. chief MAKATA  ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOASHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA-  Chief Sasa amezianza ziara zake za mikoani na atayatembelea maeneo mbali mbali ndani na inje ya nchi. 
Anatibu magonjwa sugu yanaojulikana nayasiojulikana kwakutumia QUR_AN MAJI , KIOO MAJINI NA MITISHAMBA.
Anazo dawa za mapenzi( Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu LIMBWATA) kumrudishaa alipote, kutoa Mikosi, Kutatuwa shida za chumaulete, mvuto wa biashara na sehem za kazi, kusafisha nyota, kurudisha mali zilizo ibiwa, zilizpotea, ama zilizodhulumiwa, kushika wezi na wachawi, kutoa ndagu, Kutoa kinga ya mwili, nyumba, Biashara, kufukuza majini wabaya, KUUZA kwa haraka (shamba, NYUMA, GARI..), Kesi mahakamani, Kuweka Zindiko ya mwili, nyumba, shamba, Gari, kupata Kazi na kupandishwa cheo, mali naU TAJIRI bila masharti na mengine mengi yaS iri. (Anazo Pia Pochi zisizo kwisha Hela MAGIC WALLET)

Kwa tiba na ushauri wasiliana na ofisi kwa
nambari ya simu
+255 676 014 385
+255 767 202 654 Chief MAKATA

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE;LUKUBA 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO   0658920640/ 0754372325 / 0620806813
 
HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.

Dr Kanengo: Bingwa Wa Tiba Asili Hutibu Matatizo Yafuatayo

$
0
0
NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo kupooza kupoteza fahamu 

MALABALA; hutibu kisukari , uti wa mgogo, Change, pumu, busha, kaswende, kifua kikuu, muwasho sehemu ya siri 

NKURUNGU,: Ni dawa kutibu  N, B, G, POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge 20 

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha , pia kuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe), maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu. 

NR SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Kuisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu 

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana. (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete) ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,.(4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wachafu ndani ya mji,.

Haya yote yanawezekana kwa DR KANENGO popote ulipo . Muone  DR KANENGO,anatibu nguvu za kiume anarefusha na kunenepesha uume kwa saizi uipendayo kwa muda mfupi sana, pamoja na kuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa mara 4 bila hamu kuisha Na utachelewa kufika kileleni kwa muda wa dakika 40 bila kuchoka .

Angalizo usitume meseji wala kubipu..
 
You can get it in all East African countries,,our service is fast and easy... contact Whatsapp 0784,47,59,46.Dar es salaam Tanzania. ,..Dr. KANENGO 0744,92,29,82...You are welcome. Yuko pia Khahama Mjini, Bunda kwa sasa

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

PICHA: Rais Uhuru Kenyatta Alivyokutana na Trump Ikulu ya Marekani

$
0
0
Rais Donald Trump wa Marekani amekutana na mwezake wa Kenya Uhuru Kenyatta mjini Washington na kuzungumzia masuala mbalimbali, zaidi wakiangazia biashara na usalama.

Kwa mujibu wa taarifa ya ikulu ya Marekani, wakati wa ziara hiyo mataifa hayo mawili yalikubaliana na kutangaza mikataba ya jumla ya $900 milioni.

Rais Kenyatta ni kiongozi wa tatu kutoka kusini mwa Jangwa la Sahara kukaribishwa Ikulu ya White House na kufanya mazungumzo na Rais Trump.

"Tumekuwa na ushirikiano mzuri na wa kipekee na Marekani katika masuala ya usalama na ulinzi, hasa katika harakati za kukabiliana na ugaidi. Muhimu zaidi tuko hapa kuboresha ufungamano wetu katika biashara na uekezaji, " kasema Rais Kenyatta.

Rais Trump alisema Kenya na Marekani zitaendelea kushirikiana kuimarisha ufungamano wao katika biashara, uekezaji na usalama.

"Tunafanya shughuli nyingi za utalii, biashara na ulinzi. Na kwa wakati huu tunajibidiisha kuboresha usalama," alisema Rais Trump. " Tunafurahia sana kuwa nawe hapa."

Miongoni mwa mengine, Bw Trump alifurahia pendekezo lililowasilishwa na kampuni ya ujenzi kutoka Marekani Bechtel Corporation kutaka kupewa kandarasi ya ujenzi wa barabara ya kisasa ya kutoka Nairobi kwenda Mombasa.

Mataifa yote mawili yalikubaliana na kuendelea na mashauriano zaidi ili kuafikiana kuhusu ufadhili wa ujenzi huo.

Viongozi hao wawili walijadiliana pia kuhusu safari za ndege za moja kwa moja kutoka Nairobi hadi New York zitakazoanza mwezi Oktoba mwaka huu na kukubaliana kwamba safari hizo za ndege zitaimarisha zaidi utalii na biashara kwa manufaa ya nchi hizi mbili.

Marekani ndiyo chanzo kikuu cha watalii wanaozuru Kenya na taifa hilo la Afrika Mashariki linatarajia kutumia fursa ya safari za moja kwa moja za ndege za Kenya Airways kati ya mataifa hayo mawili ambazo zitaanza Oktoba 28 kuimarisha idadi ya watalii wanaofika kenya.

Viongozi hao wawili kwa pamoja wamejadili njia za pamoja za kupambana na ugaidi na ushirikiano wa kibiashara. Mpango wa upanuzi wa barabara inayohusisha miji mikubwa ya Kenya, Mombasa na Nairobi pia ilijadiliwa.

VIDEO: Waziri wa Fedha Dr. Mpango Alivyopangua Laana za Makonda

$
0
0
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango ameagiza makontena 20 ya samani yaliyoingizwa nchini na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda yapigwe mnada ikiwa ni sehemu ya kusimamia sheria na kanuni za kodi zilizopo nchini.

Ametoa maagizo hayo jana  jijini Dar es salaam mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza kwenye Ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA na kukagua makontena hayo katika Bandari Kavu ya (DICD).

Aidha, Waziri Mpango ameweka wazi kwamba hajali vitisho vya mkuu huyo wa mkoa wa Dar es Salaam na ameapa kuendelea kusimamia sheria na kanuni za kodi nchini na hilo halichagui mtu wala nafasi yake.

Akiwa kwenye ibada jana huko Wilayani Ngara mkoani Kagera, Paul Makonda alitoa onyo kwa mtu atakayenunua makontena hayo  yenye samani za ndani kama vile meza, viti na mbao za kufundishia  kuwa atapata laana yeye pamoja na kizazi chake chote.

==>>Msikilize hapo chini Dr Mpango akizipangua hizo laana

Tanesco yaamriwa kuilipa mabilioni Benki ya Standard Chartered

$
0
0
Mahakama ya kimataifa ya usuluhishi wa migogoro ya uwekezaji (ICSID) imeikataa rufaa ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kupinga hukumu ya kuilipa Benki ya Standard Chartered Dola 148.4 milioni za Marekani (Sh336 bilioni).

Hata hivyo, si Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Dk Tito Mwinuka wala msemaji wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Maura Mwingira walioeleza kufahamu kuhusu hukumu hiyo.

Akiongoza jopo la wajumbe waliosikiliza rufaa hiyo, Rais wa ICSID, Claus von Wobeser ametupilia mbali hoja za Tanesco za kuitaka mahakama hiyo kutengua uamuzi wa awali ulioipa ushindi benki hiyo ya Hong Kong.

Uamuzi huo umetolewa baada ya Tanesco kukata rufaa kupinga hukumu iliyotolewa mwaka 2016 ikilitaka shirika hilo kulipa kiasi hicho cha fedha.

Fedha hizo ni madai ya malipo ya umeme baina ya Tanesco na kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) iliyopewa zabuni ya kufua umeme wa dharura kuanzia Mei 26, 1995 huku ikidaiwa na benki hiyo.

IPTL ilikuwa ikidaiwa na benki hiyo ya Hong Kong kutokana na mkopo iliyochukua kutekeleza mkataba kati yake na Tanesco.

Mahakama hiyo imetupilia mbali madai yote ya Tanesco kupinga hukumu hiyo na kuitaka ilipe fedha kama ilivyoamriwa katika hukumu ilitolewa mwaka 2016.

Tanesco katika nakala ya hukumu hiyo ya Agosti 2  imeagizwa kulipa gharama zote za uendeshaji wa shauri hilo ikiwamo ada ya kesi na malipo ya wajumbe wa kamati waliolisikiliza.

Tanesco katika shauri hilo iliwakilishwa na mawakili Richard Rweyongeza wa kampuni ya R.K. Rweyongeza & Co Advocate; Beredy Maregesi (Crax Law Partners); David Hesse, Devika Khanna, Thomas Roberts na Nefeli Lamrou wa kampuni ya Clyde & Co ya Uingereza. Usikilizaji wa shauri hilo ulifanyika Novemba 27 na 28 mwaka jana.

Crtedit: Mwananchi

Hawa Ghasia ajiuzulu uenyekiti kamati ya Bunge ya Bajeti

$
0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, Hawa Ghasia na makamu mwenyekiti wa kamati hiyo, Jitu Soni wamejiuzulu nafasi hizo. Katibu wa Bunge Stephen Kagaigai amethibitisha taarifa hizi.

Ghasia ambaye ni mbunge wa Mtwara Vijijini (CCM) na Soni (Babati Vijijini), wametangaza uamuzi wao huo leo asubuhi mjini Dodoma mbele ya wajumbe wa kamati hiyo.

Mtawa afariki dunia baada ya kujirusha kutoka Ghorofani

$
0
0
Mkurugenzi wa fedha na mipango wa hospitali ya Rufaa Bugando, Mtawa Suzan Bathlomeo amefariki dunia baada ya kujirusha kutoka ghorofani muda mfupi baada ya kutoka kusali misa ya saa 12:00 asubuhi, leo Jumanne Agosti 28, 2018.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jonathan Shana amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa taarifa kamili atazungumza na waandishi wa habari baadaye.

Kwa mujibu wa ofisa uhusiano wa Bugando, Lucy Mogele amesema kuwa Mtawa huyo amefariki dunia leo alfajiri, huku akibainisha kuwa hospitali hiyo haina mamlaka ya kuzungumzia suala hilo na kutaka litafutwe shirika la Watawa la Kagera, ambalo makao makuu yake yapo mjini Bukoba mkoani Kagera.

“Ni kweli Sister Suzan amefariki dunia baada ya kujirusha kutoka ghorofani lakini Bugando hatuna mamlaka ya kuzungumzia suala hilo,” amesema Lucy

Naibu Jaji Mkuu Kenya Akamatwa Kwa Rushwa

$
0
0
Naibu Jaji Mkuu nchini Kenya, Philomena Mwilu, amekamatwa katika mahakama ya juu jijini Nairobi kutokana na tuhuma za rushwa na ufisadi.

Jaji Mwilu, amechukuliwa katika Mahakama Kuu na Kurugenzi ya Mashtaka ya Jinai na wapelelezi kutoka kwenye Uongozi wa Upelelezi wa Jinai (DCI) kwa madai ya kuhusishwa na kufilisika kwa Benki ya Imperial.

Mwilu amepelekwa katika Makao Makuu ya Idara ya Uchunguzi wa Uhalifu, kwa mahojiano.

Muda mfupi baada ya kukamatwa, mwendesha mashtaka mkuu nchini humo Noordin Haji, ameitisha mkutano wa dharura na waandishi wa habari kuzungumzia suala hilo.

Lugola awachimba mkwara Wakuu wa Wilaya na Mikoa wanao waweka ndani wananchi

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola amewaonya wakuu wa mikoa na wilaya kutotumia vibaya sheria na kuwaweka ndani wananchi. Amesema Serikali ya Awamu ya Tano haitakubali wananchi wanyanyaswe.

Agosti 14, 2018 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo alikemea tabia ya baadhi ya wakuu wa wilaya kutumia vibaya mamlaka waliyonayo kuwaweka watu ndani.

Aliwataka wakuu hao wa wilaya kuhakikisha wanasoma na kuzielewa sheria zinazowaongoza ili kufanya kazi kwa weledi.

Katika siku za karibuni, wakuu wa wilaya wamekuwa wakitumia ‘sheria ya saa 48’ kutoa adhabu kwa kuwaweka baadhi ya watu mahabusu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Agosti 28, 2018 Lugola mbali na kuwaonya wakuu hao wa mikoa na wilaya, pia aliwashukia askari polisi wanaolichafua jeshi hilo kwa kuwabambikia kesi wananchi.

“Hayo mambo yako kisheria na hiyo sheria ina vigezo vyake na kama vimetimia, watakuweka ndani. Kama DC ameona huyu tusipomweka ndani usalama wake utakuwa hatarini, lazima atakuweka,” amesema.

“Lakini siyo mtu yuko kwenye mkutano ameuliza swali ambalo DC anaona linaleta challenge (changamoto), anasema huyo weka ndani saa 48. Hilo halitawezekana, katika Serikali hii hatutaki wananchi wapate shida.”

Polisi Wawili Jijini Mwanza Wafukuzwa Kazi

$
0
0
Askari wawili mkoani Mwanza wamefukuzwa kazi baada ya kupatikana na nyara za Serikali ambazo ni meno mawili ya tembo yenye kilo 20.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Agosti 28, 2018, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jonathan Shanna amesema askari hao, H.5461 Enock wa kikosi cha kutuliza ghasia  mkoa wa Mwanza na H.4165 Robeth wa kikosi maalum walifukuzwa kazi Agosti 27, 2018 kutokana na kosa hilo.

Amesema askari hao walikamatwa Agosti 23, 2018 mtaa wa Nyamhongolo wilayani Ilemela wakiwa na nyara hizo.

Amesema taarifa za awali zilionyesha kuwepo kwa watu wanaojihusisha na biashara ya meno ya tembo, kwa kushirikiana na kikosi kazi cha Taifa cha kupambana na ujangili Kanda ya Ziwa walifanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao.

Amewataka wote waliokuwa wakishirikiana na askari hao kujisalimisha katika kituo chochote cha polisi, kwa kuwa wakianza kuwasaka ni lazima watawapata kwa kuwa walifanikiwa kuwamakamata askari hao.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya Agosti 29

Utawala bora chachu ya maendeleo nchini,Waziri Mkuchika

$
0
0
Na; Daudi Manongi -MAELEZO
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mhe. Kapt. Mstaafu George Mkuchika amesema kuwa maendeleo yaliyopatikana nchini  yametokana na  Utawala bora unaosimamiwa vyema na Serikali ya awamu ya tano.

Akizungumza katika kipindi cha TUNATEKELEZA kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na kuratibiwa na Idara ya Habari-MAELEZO Waziri Mkuchika amesema kuwa Serikali imefanikiwa kutekeleza miradi ya maendeleo kutokana na kuwepo kwa utawala bora.

“Katika miaka mitatu  ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe.John Pombe Magufuli  ameonyesha  mfano bora katika kusimamia utawala bora ambapo Tanzania imeshika nafasi ya 17 kati ya nchi 54 za Afrika katika kusimamia  na kutekeleza dhana ya utawala Bora kwa mujibu wa ripoti ya Mo Ibrahim”alisema Mkuchika.

Amesema tathmini ya utawala bora katika miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Tano imeleta sura nzuri nchini ambayo imechangiwa na utashi wa kisiasa ambapo katika awamu zote tano zimesimamia suala hilo.

 Mhe. Mkuchika amesema kuwa nidhamu ya watumishi wa umma imeimarika nchini hali inayoongeza tija katika huduma zinazotolewa kwa wananchi.

Aliongeza kuwa  Taasisi za nje na ndani ya nchi zimeonesha kuwa suala la rushwa nchini limepungua  kufuatia hatua za makusudi zinazochukuliwa na Serikali katika kuimarisha utawala Bora.

“Shilingi bilioni 127 zimeokolewa na serikali  kwa kuzuia vitendo vya rushwa ambapo mali zenye thamani ya shilingi bilioni 4.5 zimezuiliwa na Serikali” aliongeza Mkuchika.

Aidha, ameongeza kuwa Taasisi za kimataifa zimeonesha kuwa Tanzania inafanya vizuri katika kusimamia na kutekeleza  dhana ya utawala bora. Utawala Bora umeisaidia nchi yetu kuongeza makusanyo ya kodi,kununua ndege ,kuondoa watumishi hewa,kuanzishwa kwa mahakama ya mafisadi na kufutwa  kwa matumizi yasiyo ya lazima.

Kipindi cha TUNATEKELEZA kinarushwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na kuratibiwa na Idara ya Habari MAELEZO ambapo awamu hii inawahusisha Waheshimiwa Mawaziri.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images