April
16 2014 saa saba kasoro mchana makamu mwenyekiti wa bunge la katiba
hapa Dodoma aliwasha kipaza sauti na kuzungumza kuhusu matangazo mawili
yaliyomfikia, moja la wageni na la pili ni la hati ya muungano ambayo
hatimae imepelekwa bungeni baada ya kuzungumziwa sana na Wajumbe
mbalimbali hasa wanaotaka uwepo wa serikali tatu waliosema hati hiyo
haipo.
Makamu Mwenyekiti alisema ‘
Alichosema bungeni Mh. Wassira kuhusu Tundu Lissu
↧
↧
Hati ya Makubaliano ya Muungano yawasilishwa Bungeni.
Makamu mwenyekiti wa bunge maalum la katiba, Samia Suluhu Hassan
amesema amepokea hati ya makubaliano ya muungano wa Tanganyika na
Zanzibar iliyothibitishwa kisheria.
Hati hiyo imefikishwa bungeni hapo baada ya mjumbe wa bunge hilo,
Tundu Lissu kuomba hati hiyo ioneshwe hadharani siku mbili zilizopita.
Waziri wa nchi ofisi ya rais, Stephen Wasirra alieleza kuwa ametimiza
↧
Muasisi wa CHADEMA, mzee Edwin Mtei alaani kitendo cha Tundu Lissu kumtukana Baba wa Taifa, Mwl. Julius Kambarage Nyerere
Nilimsikiliza Mheshimiwa Tundu Lissu na nasikitika kwamba
sikubaliani naye jinsi alivyoeleza shutma juu na dhidi ya Mwalimu
Julius Nyerere, Baba na Muasisi wa Taifa letu.
Inajulikana na umma wa Watanzania, kwamba mimi binafsi, kama Waziri wa
Fedha, nilitofautiana na Mwalimu, nikajiuzulu Uwaziri Decemba,1979,
nikimwomba ateuwe Mtanzania mwingine atakayeshauri mambo ya Uchumi na
↧
VIDEO: Sikiliza mchango wa Profesa Lipumba uliopelekea wajumbe wa UKAWA kususa na kutoka nje ya bunge la Katiba leo jioni
Audio na Video za mchango wa
Prof. Ibarahim Lipumba alioutoa Bungeni siku ya Jumatano, Aprili 16,
2014 na kutamatia kwa baadhi ya wajumbe kutoka nje ya Bunge Maalum la
Katiba ipo hapo chini baada ya mchango huo kwa maandishi ifuatavyo:-
Mhe. Mwenyekiti gazeti la Mwananchi la tarehe 14 Aprili 2014 limeandika
kuwa “Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Uratibu na Bunge),
William
↧
Wajumbe wa Bunge la Katiba toka vyama vya upinzani leo jioni waligoma na kutoka nje ya Ukumbi wa Bunge.....Hizi ni picha za tukio hilo
Wajumbe wa Bunge Maalum la
Katiba ambao wanaunga mkono mfumo wa Serikali za tatu wakitoa katika
Ukumbi wa Bunge leo mjini Dodoma baada ya kususia kikao
Wajumbe wa Bunge Maalum la
Katiba ambao wanaunga mkono mfumo wa Serikali za tatu wakitoa katika
Ukumbi wa Bunge leo mjini Dodoma baada ya kususia kikao
***********
Wajumbe karibu wote wa vyama vya upinzani wanaoshiriki
↧
↧
Taarifa ya TAHADHARI ya mvua kubwa katika Visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na mikoa ya Tanga, Pwani na Dar es Salaam.
Taarifa kwa Umma: Vipindi vya mvua kubwa vinatarajiwa.
Taarifa Na.
201404-02
Muda wa Kutolewa
Saa 10:00 Alasiri
Saa za Afrika Mashariki
Daraja la Taarifa:
Tahadhari
Kuanzia:
17
Aprili, 2014
Tarehe
Mpaka:
18
Aprili, 2014
Tarehe
Aina ya Tukio Linalotarajiwa
Vipindi vya mvua kubwa inayozidi milimita 50 ndani ya saa 24,
ukanda wa pwani.
↧
Bunge maalumu la Katiba kuendelea leo licha ya baadhi ya wajumbe ( UKAWA ) kususia kikao hicho jana jioni
Vikao vya Bunge Maalum la Katiba vitaendelea tena leo kwa kujadili sura
ya 1 na ya ile ya 6 ya Rasimu ya Katiba licha ya baadhi ya wajumbe
kususia kikao hicho jana jioni na kutoka nje ya ukumbi kwa kile
walichodai ni kuchoshwa na matusi, dharau na ubaguzi .
Kauli
ya kuendelea kwa kikao leo ilitolewa usiku wa jana na Mwanasheria Mkuu
wa Serikali, Jaji Federick Werema kabla ya
↧
Magazeti ya leo Alhamisi ya tarehe 17 April 2014
↧
Mwanafunzi wa chuo cha IFM akamatwa na Bangi kilo 50
Jeshi
la Polisi Mkoa wa Dodoma linawashikilia abiria wa tatu waliokuwa
wakisafiri na Basi la New Force kutoka Kahama kuelekea Jijini Dar es
Salaam.Wanaoshikiliwa ni Kevin Prospar(aliyekaa pichani kulia),Joseph
Charles (aliyekaa kulia) na John Joseph(aliye kaa katikati) Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma David Misime kushoto akikagua bangi iliyo kamatwa.Basi
la New Force lililokamatwa
↧
↧
UKAWA wamegoma kabisa kuhudhuria mkutano wa bunge maalum la katiba
Umoja wa katiba ya wananchi bungeni -UKAWA- umegoma kabisa kuhudhuria
mkutano wa bunge maalum baada ya kutoka katika mkutano uliofanyika
Aprili 16 kwa madai ya mkutano huo kugubikwa na matusi, kashfa na
vitisho vinavyofanywa na baadhi ya viongozi kwa wananchi.
Akizungumzia masikitiko yake mwenyekiti wa kamati
ya bunge maalum, Mhe. Samweli Sita amesema licha ya bunge hilo kumwita
↧
Rais Kikwete akerwa na kitendo cha wanasiasa kumtukana Mwalimu Nyerere....Asema ni utovu wa nidhamu kuwatukana waasisi wa Tanzania
Rais Jakaya Kikwete amesema ni utovu wa nidhamu na ukosefu wa
adabu unaoonyeshwa na baadhi ya Watanzania kuwatukana, kuwadhihaki na
kuwakejeli waanzilishi wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere na
Sheikh Abeid Amani Karume.
Rais Kikwete alitoa kauli hiyo juzi alipokuwa
kwenye mahojiano maalumu na wahariri wa baadhi ya vyombo vya habari (wa
Mwananchi hawakuwapo) ya kuadhimisha
↧
Magazeti ya leo Ijumaa ya tarehe 18 April 2014
↧
Martin Kadinda amwita Lulu Michael Nyau
Mwanamitindo maarufu Bongo, Martin Kadinda amempongeza Elizabeth Michael ‘Lulu’ kwa kumuita nyau.
Martin alifanya ishu hiyo wakati akimtakia Lulu Happy Birthday Aprili
16 ambapo mwanadada huyo alikuwa akitimiza umri wa miaka 19. Mwandishi
wetu alipomhoji kuhusiana na kumuita nyau, Martin alifunguka:
“Yule kwangu ni mdogo, nimemlea tangu akiwa anasoma sekondari pale
Perfect Vision
↧
↧
Mwigulu Mchemba asimamisha malipo ya posho ya wabunge wote waliosusia vikao vya bunge juzi
Naibu Waziri wa
Fedha, Mwigulu Mchemba amesema serikali imesimamisha malipo ya posho ya
wabunge wote waliosusia vikao vya bunge juzi.
Pia, amesema wajumbe ambao ni watumishi wa umma, wataripotiwa kwa Katibu Mkuu Kiongozi kwa ajili ya hatua za kinidhamu.
Alisema licha
ya kuwa wajumbe hao wameshalipwa posho hizo hadi Aprili 26, mwaka huu,
tayari amesitisha malipo hayo ambayo yalikuwa
↧
Stephen Wasira afunguka....Asema hashangazwi na kitendo cha kutoka nje ya bunge wajumbe wa UKAWA kwani, ni matukio yaliyopangwa muda.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Stephen
Wasira, amesema hakushangazwa na kitendo cha kutoka nje ya bunge wajumbe
wa UKAWA kwani, ni matukio yaliyopangwa muda.
Wasira alisema
UKAWA walikuwa na mpango huo muda mrefu baada ya kuona hoja yao kuhusu
kutokuwepo kwa hati ya muungano kukosa ukweli.
Akizungumza na
waandishi wa habari jana, Wasira alisema sababu
↧
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2014 kuahirishwa....“Nikiri nafasi ni finyu sana ila tutalizungumza serikalini,” asema Rais Kikwete
UCHAGUZI wa serikali za mitaa, ambao hufanyika mwaka mmoja kabla ya uchaguzi mkuu, huenda usifanyike mwaka huu, imeelezwa.
Hatua hiyo inatokana na uchaguzi huo kuingiliana na masuala ya kupata Katiba mpya, ambayo mchakato wake bado unaendelea.
“Nikiri nafasi
ni finyu sana ila tutalizungumza serikalini,” alisema Rais Jakaya
Kikwete, alipozungumza na baadhi ya wahariri Ikulu mjini Dar
↧
Taarifa ya mabadiliko ya uelekeo wa barabara jijini Dar.....
MABADILIKO YA UELEKEO WA BARABARA KATIKATI YA JIJI LA DAR ES SALAAM
KUANZIA SIKU YA TAREHE 28/04/2014. (TRAFFIC CIRCULATION AT CBD)
Ufunguo wa ramani iliyopachikwa hapo juu:-
RANGI YA NJANO - Njia ya uelekeo mmoja (One Way)
RANGI YA BLUE MPAUKO - Njia ya mielekeo miwili (Two Way)
RANGI YA KIJANI - Mitaa ya kutembea kwa miguu, magari marufuku (Walking streets)
RANGI NYEKUNDU - Barabara
↧
↧
Taarifa ya jeshi la Polisi kuelekea sikukuu ya pasaka.....
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Tunapoelekea kipindi hiki cha sikukuu ya Pasaka, Jeshi la Polisi nchini,
linatoa tahadhari kwa wananchi kuwa makini katika suala la usalama wa
maisha na mali zao. Uzoefu unaonyesha kwamba, katika kipindi kama hiki
cha sikukuu kuna baadhi ya watu hupenda kutumia fursa hiyo kufanya
vitendo vya uhalifu.
Hata hivyo, Jeshi la Polisi katika mikoa yote
↧
Taarifa ya Jeshi la Polisi kuhusu kusitishwa Mkutano wa hadhara wa UKAWA uliopangwa kufanyika kesho Jumamosi 19/04/14
YAH: TAARIFA YA KUSITISHWA MKUTANO WA HADHARA
Naomba urejee barua yangu Kumbu. Nam. W/MGH/SO/7/2/A/4 ya tarehe 17 Aprili, 2014 inahusika.
Ninakujulisha rasmi kuwa mkutano huo uliokuwa ufanyika kesho tarehe 19
Aprili, 2014 hapo Viwanja ya Demokrasia Kibanda Maiti umesitishwa kwa
sababu za
KIUSALAMA WA NCHI.
Kwa barua hii unatakiwa kuwajulisha Wanachama na wapenzi wote wa
↧
Magazeti ya leo Jumamosi ya tarehe 19 April 2014
↧
More Pages to Explore .....