Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Bobi Wine aachiwa, akamatwa tena na Jeshi la Polisi

$
0
0
Mbunge wa Kyadondo nchini Uganda Robert Kyagulanyi maarufu Bob Wine amekamatwa muda mfupi baada ya mahakama ya kijeshi kumuondolea mashtaka ya umiliki haramu wa silaha nchini humo.

Muda mfupi baada ya kuachiliwa huru, Wine alikamatwa tena na inaarifiwa kwamba anatarajiwa kushtakiwa katika mahakama ya hakimu mkuu kujibu mashtaka ya uhaini pamoja na wabunge wengine waliokamatwa.

Mbunge huyo ambaye pia ni mwanamuziki nchini kwa jina maarufu Bob Wine leo aliwasilishwa katika mahakama ya kijeshi mjini Gulu kaskazini mwa Uganda.

Mawakili wake awali walijuzwa kuwa kesi itasikilizwa katika kambi ya kijeshi ya Makindye anakozuiliwa mjini Kampala.

Mawakili wa jeshi wameeleza mahakama kuwa mashtaka dhidi ya Wine yameondolewa na kwamba mwanasiasa huyo akabidhiwe kwa polisi ili akabiliwe na mashtaka ya uhaini pamoja na wabunge wengine waliokamatwa .
 
Wakili wake Wine Medard Segona ameiambia mahakama kwamba licha ya kuwa wameridhishwa na hatua ya mahakama ya kijeshi , anapinga hatua ya sasa ya mteja wake kuhamishwa katika mahakama ya kiraia kukabiliwa na mashtaka mapya.

Alitaka mbunge huyo aachiwe huru ili aweze kupelekwa kupokea matibabu.

Mahakama iliamua kuwa Bobi Wine yu huru, iwapo hakuna mashtaka mengine yatakayowasilishwa dhidi yake.

Wakati huo Wine alionekana akilia na kupangusa machozi huku hukumu hiyo ikisomwa. Alitoka nje ya mahakama akiwa anatemba kwa magongo na kuonekana kuwa na maumivu makali. Hapo ndipo alipokamatwa upya.

Credit:BBC

Dr Kanengo: Bingwa Wa Tiba Asili Hutibu Matatizo Yafuatayo

$
0
0
NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo kupooza kupoteza fahamu 

MALABALA; hutibu kisukari , uti wa mgogo, Change, pumu, busha, kaswende, kifua kikuu, muwasho sehemu ya siri 

NKURUNGU,: Ni dawa kutibu  N, B, G, POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge 20 

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha , pia kuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe), maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu. 

NR SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Kuisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu 

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana. (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete) ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,.(4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wachafu ndani ya mji,.

Haya yote yanawezekana kwa DR KANENGO popote ulipo . Muone  DR KANENGO,anatibu nguvu za kiume anarefusha na kunenepesha uume kwa saizi uipendayo kwa muda mfupi sana, pamoja na kuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa mara 4 bila hamu kuisha Na utachelewa kufika kileleni kwa muda wa dakika 40 bila kuchoka .

Angalizo usitume meseji wala kubipu..
 
You can get it in all East African countries,,our service is fast and easy... contact Whatsapp 0784,47,59,46.Dar es salaam Tanzania. ,..Dr. KANENGO 0744,92,29,82...You are welcome. Yuko pia Khahama Mjini, Bunda kwa sasa

Wakili Kesi Ya Viongozi Chadema Ajitoa

$
0
0
Wakili Jeremiah Mtobesya, anayewatetea viongozi tisa wa Chadema akiwamo Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, amejitoa katika kesi hiyo baada ya mahakama kukubaliana na upande wa jamhuri kwamba washtakiwa wasomewe maelezo ya awali leo wakati leo kesi ilipangwa kwa ajili ya kutajwa.

Amedai akiendelea kuwatetea washtakiwa hao, haki haitatendeka.

Upande wa Jamhuri haukuwa na pingamizi kwa uamuzi wa Mtobesya ambapo baada ya kujitoa alibeba kila kilicho chake mezani na kutoka nje ya chumba cha mahakama.

Mbali na Mbowe, washtakiwa wengine ni Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Vincent Mashinji, Mbunge wa Iringa Mjini Peter Msigwa, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Salum Mwalimu na Naibu katibu Mkuu bara na Mbunge wa Kibamba, John Mnyika.

Wengine ni Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Mbunge wa Kawe Halima Mdee, Mbunge wa Bunda, Esther Bulaya na Mbunge wa Tarime mjini, Esther Matiko.

Washtakiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kuwa Februari 16, mwaka huu katika Barabara ya Kawawa Kinondoni Mkwajuni walikiuka tamko la kuwataka kutawanyika.

Mabasi ya Shule Yagongana Jijini Mwanza Na Kuua Mmoja

$
0
0




Basi la shule ya msingi Kivulini na la shule ya msingi Nyamuge yamegongana leo asubuhi na kusababisha kifo cha mtu mmoja.

Akizungumzia tukio hilo leo Agosti 23, Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza(anayehamia makao makuu ya Polisi Dar,) Ahmed Msangi amesema aliyefariki ni dereva wa gari la shule ya Nyamuge Albert Joram(58).
 
Amesema watu wengine wanane na dereva wa gari la Kivulini Kulwa Mayala 27, wamepata majeraha sehemu mbalimbali za miili yao zaidi hasa miguuni.
 
“Majeruhi hao walikimbizwa katika kituo cha afya cha Buzuruga na baadae mwanafunzi mmoja alilazimika kuhamishiwa hospitali ya rufaa, Bugando kwa matibabu zaidi huku wawili wakilazwa katika hospitali ya Sekou Toure jijini Mwanza,”amesema.
 
Amesema kwa sasa hali za majeruhi zinaendelea vizuri na tayari wale wa tano wameruhusiwa ingawa wanahitaji vipimo vya kina.

Diamond, Rich Mavoko Wakurana Uso kwa Uso BASATA

$
0
0
Msanii wa Bongo Fleva, Rich Mavoko na lebo ya WCB wamekutana tena Baraza la Sanaa Taifa (BASATA).

Team ya WCB ilikuwa ikiongozwa na Diamond Platnumz pamoja na Sallam SK.

Pande hizo mbili ziliitwa na BASATA kwa lengo la majadiliano mara ya baada ya upande wa Rich Mavoko kulalamikia kile walichodai ni mkataba wa unyonyaji kutokea WCB.

Hata hivyo hadi pande zote mbili zinaondoka eneo la BASATA hazijaweka wazi ni kipi hasa kinaeendelea, hivyo wenye kauli ya kueleza yalipofikia mazungumzo hayo ni Baraza hilo lenyewe.
 
Mavoko alijiunga na WCB mwaka 2016 akisaini chini ya lebo hiyo na kuanza kufanya kazi akiwa chini ya lebo hiyo ambayo boss wake ni Diamond Platinumz.

Baada ya kujiunga na lebo hiyo Mavoko alianza malalamiko mapema mwaka huu kuwa anataka kujitoa katika lebo hiyo ya WCB wasafi kwa madai kwamba ananyonywa kimaslahi.

Mbali na kunyonywa kimaslahi lakini pia ilidaiwa kuwa kuna vitu ndani ya makataba huo msanii huyo hakutimiziwa na boss wake kama mkataba ulikuwa unaelekeza.

Malalamiko ya Mavoko yalionekana kuwagusa wengi na ikachangia Mavoko kukaa kimya kwa muda ingawa siku za hivi karibuni aliachia ngama yake mpya inayokwenda kwa jina la Ndegele.

Katika moja ya mahojiano aliyofanya meneja wa Diamond Salam Sk katika moja ya Redio hapa nchini alipoulizwa kuhusiana na madai haya ya mavoko alisema “Mavoko bado ni msanii wa WCB na hayo malalamiko anayotoa sisi hatujui yanahusiana na nini kwani huduma zote wanazopatiwa wasanii wa WCB anazipata”

Meneja huyo aliongeza “Kabla ya mavokonkusaini mkataba alipewa akakae nao aupitie hadi ajirizishe na Mavoko alifanya hivyo na kukaa nao ndani ya wiki mbili ndio akaurizia mwisho wa siku akaja kusaini sasa anacholalamika ni nini? sisi hatujui kwani makataba huo una kurasa 10 kwahiyo hatujui ni kitu gani anataka haswa”

Baada ya Mavoko kupeleka malalamiko hayo Basata,Basata nao waliamua kuwaita Maboss wa WCB walipofika wakaongea nao na ndio wakakubaliana wakutane siku ya leo August 23 katika ofisi hizo hapa Jijini Dar Es Salaam. 




Mbowe: Waliomuua Akwilina Wanajulikana, Lakini Wanataka Sisi Ndo Tufungwe

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Freeman Mbowe amesema Tanzania inapitia kipindi kigumu cha viongozi wa kiserikali kutoheshimu sheria na katiba.

Akizungumza na wandishi Leo Makao Makuu ya Chama hicho, Mbowe amesema kumekuepo na uvunjifu wa sheria kwenye kesi inayomkabili yeye na viongozi wengine wandamizi wa Chama hicho huku wakiwa wananyimwa haki zao za msingi.

" Tunaheshimu mahakama zetu lakini kinachofanyika Hivi Sasa sio haki kwetu, hii ni kesi ambayo inawahusisha wabunge ambao wanapaswa kuwepo katika majimbo yao lakini kesi imekua ikipelekwa pelekwa tu muda mwingine hadi usiku.

" Mawakili wetu walipeleka maombi ya kutaka kesi yetu ipelekwe mahakama kuu kutoka kisutu lakini hakimu amekataa na kulazimisha tuingie kwenye shtaka jambo ambalo Wakili Mtobesya amekataa kukubaliana nalo na kuamua kujitoa mbaya zaidi Hakimu ametaka kesi iendelee kesho," Amesema Mbowe.

Mbowe amesema ubabe unaotumika na dola katika kuwakandamiza wapinzani katika kesi yao, uonevu wanaofanyiwa katika chaguzi zinazoendelea, utishwaji wa viongozi wao kutoka kwa viongozi ambao wanasaidiwa na Polisi utapelekea kutokea kile kinachoendelea nchini Uganda.

" Tunaheshimu mahakama lakini inawezekana mahakimu na majaji kutumika kwa kufanya kazi kwa maelekezo, na hii lazima tuzungumze ili Dunia na watanzania waelewe kwamba hatuoni haki ikitendeka kwa kesi yetu inayosikilizwa na hakimu Mashauri na ndio maana hata tulipoomba ajitoe ameendelea kukataa.

“Waliomuua Akwilina wapo, lakini tunatengenezewa kesi sisi ili tufungwe, tunasema hatuogopi kwenda jela, lakini tunataka tufungwe pale ambapo tuna haki ya kufungwa. Waue wengine, wapige risasi wengine, waumize wengine, walioonewa ndiyo wanakuwa washutumiwa?” amesema Mbowe

Taarifa MUHIMU Toka Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu

Irene Uwoya Awaonya Wanaopiga Picha za Nusu Uchi

$
0
0
Msanii wa filamu nchini Irene Uwoya na mke halali wa mwanamuziki Dogo Janja amefunguka na kuwataka ma-star wenzake kuacha kutumia 'skendo' za kupiga picha nusu utupu kwa madai vitendo hivyo vinamchukiza hadi Mungu na si TCRA pekee.

Uwoya ametoa kauli hiyo alipokuwa anazungumza kna  eNewz ya EATV, na kusema wanaofanya na vitendo hivyo wanajidhalilisha wao wenyewe bila ya kujijua.

"Mimi nadhani kuna kitu watu hawajui au hawakitambui, kuwa kuna tofauti ya kutaka kuwa 'star' na kufanya kitu ambacho unakipenda ambacho kitakupelekea kuwa 'star' moja kwa moja", amesema Uwoya.

Pamoja na hayo, Uwoya ameendelea kwa kusema "mimi nawashauri watanzania kama kuna mtu anataka kuwa muigizaji basi afuate misingi iliyowekwa nasio kupiga picha za nusu utupu kwa kuwa haitoweza kumfanya mtu kuwa star na badala yake inakushusha. Wanaopiga picha za nusu utupu wanajidhalilisha kiukweli maana hata Mungu hapendi".

Kauli hiyo ya Irene Uwoya imekuja baada ya kupita takribani siku 36 tokea alipopigwa onyo na Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA), kuhusiana na kuchapisha picha za nusu utupu kwenye mitandao ya kijamii na kusisitiziwa kuwa endapo atarudia kufanya hivyo adhabu kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Agosti 24

Picha ya Polisi Akinywa Bia Baa Yamponza Mwandishi wa Gazeti la Uhuru

$
0
0
Mwandishi wa habari wa gazeti la Uhuru, Constantine Mathias, amehojiwa na polisi kwa tuhuma za matumizi mabaya ya mitandao na kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Akizungumza jana Agosti 23 Kamanda wa polisi mkoa wa Simiyu, Deusdedit Nsimeki alisema Mathias alikamatwa, akahojiwa kisha akaachiwa.

Imeelezwa kuwa Mathias alisambaza picha kwenye mtandao wa kijamii wa facebook inayomuonyesha askari polisi akinywa bia akiwa na sare za kazi.

Picha anazodaiwa kusambaza ni za askari polisi PC Neto Mahenge wa kituo cha polisi Mwamapalala.

"Anahojiwa kwa tuhuma za matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii na madai ya kujihusisha na vitendo vya rushwa. Nimeagiza achukuliwe maelezo na kuachiwa kwa dhamana akikamilisha taratibu na mahitaji ya kisheria," alisema Kamanda Nsimeki.

Vigogo KCU Kizimbani Kwa Uhujumu Uchumi

$
0
0
Vigogo watatu wa zamani wa Chama Kikuu cha Ushirika, Mkoa wa Kagera KCU 1990 LTD wamesomewa mashitaka matano likiwamo la uhujumu uchumi na kusababisha hasara ya milioni 124.

Wakili Mwandamizi wa Serikali Athuman Matuma aliieleza mahakama ya Hakimu mkazi Mkoa wa Kagera jana kuwa watuhumiwa hao walitenda makosa hayo kwa nyakati tofauti mwaka 2011.

Washitakiwa hao ni Mwenyekiti wa zamani wa Bodi ya KCU, John Binunshu, aliyekuwa Meneja Mkuu KCU, Vedastus Ngaiza na aliyekuwa mhasibu, Bestina Rwebangira.

Aliyataja mashtaka hayo kuwa ni kula njama matumizi mabaya ya ofisi, kughushi, matumizi mabaya ya madaraka na kuhujumu uchumi kwa kuisababishia serikali hasara ya Sh124 milioni.

Watuhumiwa walisomewa mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi John Kapokolo  na wamenyimwa dhamana hadi Jumatatu kesi yao itakapotajwa tena.

Bunge Lanusa Harufu ya Ufisadi Serengeti.....Viongozi wa Halmashauri Watimuliwa Kikaoni

$
0
0
Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Abdallah Chikota.
 ****
 Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), imewatimua kwenye kikao viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti mkoani Mara kwa kushindwa kuwasilisha majibu ya hoja za jumla ya Sh. milioni 371 zilizoibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) za mwaka 2016/17.

Kufuatia hatua hiyo, viongozi hao wametakiwa kuandaa upya kitabu cha majibu ya hoja hizo kwa gharama zao na kukiwasilisha tena kwa kamati kwa muda utakaopangwa.

Hali hiyo ilijitokeza jana katika kikao cha kamati hiyo cha kufanya mahojiano na halmashauri hiyo kuhusu hoja za ukaguzi za mwaka huo kutokana na kamati kushindwa kuendelea na mahojiano hayo na kuitimua.

Akizungumzia hatua hiyo, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Abdallah Chikota alisema wameirudisha kuandaa upya majibu ya hoja hizo kutokana na upungufu ulioonekana kwenye kitabu kilichowasilishwa kwenye kamati hiyo.

Alisema kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge, kamati hizo za Hesabu za Umma ya LAAC na Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (PAC), zinafanya majadiliano kulingana na taarifa za CAG.

"Katika hesabu za mwaka 2016/17 kuna hoja kadhaa zimejitokeza kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo na tulitarajia leo (jana) watakuja na majibu, lakini kilichofanyika kwenye kitabu chao hawakuweka majibu wakaelekezwa na ofisi ya CAG kule Mara kwamba kitabu chao kina upungufu, hata hivyo hawakuweka,"alisema.

Aliongeza: "Wakaitwa na Ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa (RAS) kufanya kikao cha maandalizi wakaambiwa kitabu kina dosari, lakini bado hawajaweka hayo majibu na leo wametokea kwenye kamati yetu wakiwa na upungufu huo huo, sisi hatuwezi kuendelea na majadiliano kwa sababu hatujui matumizi ya fedha hizo zilizooneshwa kwenye hoja za CAG."

Chikota ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nanyamba (CCM), alisema miongoni mwa fedha ambazo hawajapata majibu ni Bakaa ya Sh. milioni 186 za Mfuko wa wahisani katika kuboresha huduma za afya (Basket Fund).

"Wangeleta majibu ya hizi fedha tungepima uzito wa majibu yao wametumia kwa matumizi gani, pia kuna matumizi yasiyotakiwa ya Shilingi milioni saba, tumeambiwa kwenye mradi wa maji kuna Bakaa ya Sh. milioni 26, tujue kama fedha zimetumika,"alisema.

Makamu Mwenyekiti huyo alisema kamati hiyo imefungwa mawanda ya kuhoji kilichojiri kutokana na kukosekana majibu.

"Kwenye akaunti ya maji kuna fedha Shilingi milioni nne zimetumika kwa shughuli ambazo hazikufanywa, yaani waliidhinisha malipo ya fedha hiyo kwa shughuli ambayo haijafanywa,"alisema.

Kadhalika, alisema katika Mfuko wa barabara kuna malipo yana dosari ya Sh. milioni 124, fedha za Tasaf Sh. milioni 24, zilitakiwa kurejeshwa makao makuu hazijarejeshwa na majibu hakuna.

"Kwa mazingira haya tumewafukuza wakaandae tena kitabu kwa gharama zao, maana hawawezi tena kutumia fedha za umma kwa ajili ya kuleta majibu ambayo walitakiwa kuleta kwa kipindi hichi na tutafuatilia kama mtalipana tena posho,"alisema.

Alimtaka RAS kuhakikisha anasimamia maandalizi ya kitabu kipya cha majibu ya hoja hizo na kupitia Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) watajulishwa siku ya kukutana na kamati.

Kwa upande wake, Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Josephat Kandege, alisema wamepokea maelekezo ya kamati na watahakikisha wanasimamia na majibu yatapatikana.

Trump awaonya wamarekani..... " Mkiniondoa Madarakani uchumi utaharibika na mtakuwa masikini"

$
0
0
Rais wa Marekani Donald Trump amejibu uvumi kuwa anaweza kuondolewa kwa kura ya kutokuwa na imani naye kwa kuonya kuwa uchumi utaharibika

Wakati wa mahojiano kwenye kipindi cha Fox & Friends alisema masoko yataporomoka na "kila mtu atakuwa maskini".

Alikuwa akizungumza baada ya Michael Cohen, wakili wake wa zamani kukiri kuvunja sheria za uchaguzi na kusema alishauriwa kufanya hivyo na Trump.

Si kawaida kwa Trump kuzungumzia suala la kutolewa mamlakani.

Waandishi wa habari wanasema haiwezekani kuwa wapinzani wa Trump watajaribu kumuondoa madarakani kwa kura ya kutokuwa na imani naye kabla ya uchaguzi wa kati ya muhula wa mwezi Novemba.

Sijui ni kwa njia gani mtamtoa madarakani mtu ambaye amefanya kazi nzuri," Trump alikiambia kipindi cha Fox and Friends.

"Ninawaambia hivi, ikiwa nitaondolewa nafikiri masoko yataporomoka, nafikiri kila mtu atakuwa maskini."

Trump alitetea malipo kwa wanawake wawili na kusema hakuwa anawajua wakati huo.

Matamshi yake yanaenda kinyume na taarifa zilizotolewa mapema na Cohen ambapo alisema kuwa Rais Trump aliimuagiza kufanya malipo hayo.

Mwezi Julai Cohen alitoa kanda ya sauti yake na Trump wakizungumzia moja ya malipo hayo kabla ya uchaguzi

Cohen anasem alifanya malipo hayo kwa wanawake wawili wakati wa kampeni ya urais ya mwaka 2016.

Wanawawe hao wawili wanatajwa kuwa manyota wa filamu za ngono Stormy Daniels na Karen McDougal, wote walidai walikuwa na uhusiano na Trump

Lakini Trump alisisitiza kuwa malipo hayo hayakukiuka sheria za uchaguzi.

Alisema malipo hayo yalitoka kwake mwenyewe na sio kutoka kwa kampeni lakini hakufahamua kuyahusu hadi baadaye. 

Credit:BBC

Diwani Mwingine CHADEMA Atimkia CCM.....Sababu ni Serikali Kununua Dreamliner, Kuhamia Dodoma

$
0
0
Uamuzi mgumu wa Rais John Magufuli wa kuboresha usafiri wa anga nchini kwa kununua ndege kubwa ya Boeing 787-8 Dreamliner, umemkimbiza Diwani wa Chadema katika Kata ya Ndumeti, Wilaya ya Siha, Jackson Rabo kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) leo mchana.

Kwa mujibu wa diwani huyo moja ya sababu iliyomvutia kujiunga na CCM baada ya uamuzi wa Rais John Magufuli kuhamishia ofisi zote za serikali mkoani Dodoma.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Valerian Juwal amethibitisha kuwa Diwani Jackson Rabo anakuwa Diwani wa tano katika wilaya hiyo kujiuzulu mwaka huu.


Askari Magereza Nchini Waonywa Kuhusu Matumizi Mabaya Ya Mitandao Ya Kijamii

$
0
0
Na Lucas Mboje, Singida;
MKUU wa Jeshi la Magereza nchini – CGP Phaustine Kasike ameonya vikali tabia ya maafisa na askari wa Jeshi la Magereza wanaojihusisha na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii kwani kufanya hivyo ni kinyume na kanuni za uendeshaji wa Jeshi hilo.

Kamishna Jenerali Kasike amesema hayo jana Alhamisi katika ziara yake ya kukagua utendaji kazi pamoja na kusikiliza changamoto mbalimbali za uendeshaji wa Jeshi hilo Magereza Mkoani Singida.

Alisema kuwa limezuka wimbi la askari wa Jeshi hilo kutumia vibaya mitandao ya kijamii kinyume na maadili ya Jeshi hilo kwa baadhi ya askari kuitumia vibaya kuchangia na kutoa maoni katika mitandao ya kijamii mambo yasiyofaa.

Jenerali Kasike  amewataka askari wote nchini kuepuka kulichafua jeshi hilo mbele ya jamii badala yake wanatakiwa kuwa kielelezo kwa Taifa.

“Niwasihi sana jiepusheni na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii bali itumieni kupashana habari za msingi na zenye manufaa kwenu kwani nafahamu mitandao ya kijamii inarahisisha kupashana habari kwa uharaka zaidi.” Alisisitiza Jenerali Kasike.

Aidha, Kamishna  Jenerali Kasike ameongeza kuwa Jeshi hilo halitasita kuwachukulia hatua kali za kinidhamu askari yeyote atakayebainika kutenda makosa hayo ya kimaadili kwani yanalifedhehesha Jeshi la Magereza mbele ya jamii.

Kuhusu upungufu wa nyumba za kuishi kwa watumishi wa Jeshi hilo, Jenerali Kasike amewataka wakuu wote wa magereza nchini kuwa wabunifu hususani katika kutumia fursa zilizopo katika maeneo yao ikiwemo fursa ya kufyatua tofali za kuchoma ili kupunguza tatizo hilo.

Kwa upande wake Mkuu wa Gereza la Kilimo na Mifugo Ushora, Mrakibu wa Magereza Kulwa Kabota ameushukru Uongozi wa Jeshi la Magereza kwa kuwawezesha kiasi cha Shilingi Milioni 9 ambazo zitasaidia kukamilisha ujenzi na upauaji wa nyumba ya askari katika gereza hilo.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike yupo katika ziara ya kikazi ya siku moja Mkoani Singida ambapo amekagua Gereza la Wilaya Singida na Gereza la Kilimo na Ufugaji Ushora kabla ya kuelekea jijini Dodoma kuendelea na majukumu mengine ya kitaifa.

Baba Kortini Kwa Kumbaka Mtoto wake wa Miaka 12

$
0
0
Mkazi wa Stendimpya, Mugumu, Nyamhura Werema (35)amepandishwa Mahakama ya Wilaya ya Serengeti kwa kosa la kumbaka mtoto wake wa miaka(12)

Akizungumza mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Ismael Ngaile, mwendesha mashtaka wa polisi, Paskael Nkenyenge amesema kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Julai mwaka huu.

“Mshitakiwa huyo alitenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 158(1) (a) cha kanuni ya adhabu sura 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002,” amesema

Amesema Upelelezi haujakamilika na mshitakiwa amekana shitaka. Mshtakiwa amenyimwa dhamana na kesi yake itatajwa tena Septemba mwaka huu.

Wabunge 19 CHADEMA Kulinda Kura Dodoma

$
0
0
Viongozi  wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wamesema watawatumia wabunge 19 wa chama hicho kulinda kura katika uchaguzi mdogo wa kata ya Kizota katika jiji la Dodoma.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Katibu wa Chadema Kanda ya Kati, Iddy Kizota alisema watawatumia wabunge wa Chadema kulinda kura za mgombea kutokana na kuwapo kwa hujuma za kuwapiga mawakala na kuwaondoa vituoni kwa lengo la kubadilisha matokeo.

Hata hivyo Kizota alisema kulikuwepo na njama kubwa ambazo zilikuwa zikifanywa na Ofisi Mtendaji wa Kata ya Kizota, Loyce Mrefu kwa kutaka kumkwamisha mgombea wa Chadema kwa kumwekea vikwazo visivyokuwa na sababu.

“Unaweza kujiuliza msimamizi wa uchaguzi anakuwa na visingizio kibao kwa kudai kuwa ofisi ya kata haina daftari ya orodha ya wapiga kura, mara hakuna risiti kwa kwa ajili ya kumpatia mgombea pamoja na mambo kadha wa kadha,” alisema Mrefu.

Amlisema kutokana na kuwapo dalili za hujuma ambazo zinafanywa na viongozi wa chama tawala kwa kushirikiana na watumishi wa serikali wamejipanga kuhakikisha wanalinda na kusimamia sheria, kanuni na misingi yote ya uchaguzi.

Hata hivyo Afisa Mtendaji wa Kata ya Kizota, Loyce Mrefu alipoulizwa juu malalamiko ya wanayoelezwa na wanachama wa Chadema alisema yeye siyo msemaji wa uchaguzi ingawa ni Ofasa Mtendaji kata.

Pamoja na kudai kuwa siyo msemaji alieleza kuwa vyama vilivyochukua fomu na kurejesha ni CCM, Chadema, NCCR-Mageuzi, CUF, UDPD na NLD.

Kwa upande wa mgombea udiwani kata ya Kizota kupitia Chadema, Omar Bangababo amesema amejitosa kuwania nafasi hiyo ili kupambana na changamoto ambazo mtangulizi wake ameshindwa kuzitatua kutokana na kukosa msimamo kwa wananchi walio mchagua.

Wananchi Waishi Nje Baada Ya Nyumba Zao Kchomwa Na Kubomolewa

$
0
0
Na John Walter-Manyara
Wakazi wa kijiji cha Manyara kata ya Magara  eneo la kambi ya fisi wilayani Babati mkoani Manyara wamejikuta wakilala katika mahema baada ya makazi yao kuchomwa moto na Kubomolewa na serikali kwa maelezo kuwa maeneo wanayoishi  ni ya hifadhi ya ziwa Manyara.

Kituo hiki kilifika katika kijiji hicho ambacho kipo pembezoni mwa ziwa Manyara na kukuta majivu ambapo nyumba 86 zimeteketezwa kwa moto na kubomolewa.

Wakizungumza na kituo hiki wanakijiji hao walieleza kuwa hawajui kwanini wamebolewa nyumba zao ili hali wameanza kuishi tangu miaka ya 1984,zaidi ya miaka 30 sasa.

Baadhi yao wamesema hawakuwepo wakati zoezi hilo la kuchoma na kubomoa nyumba likiendelea wamekuta vitu vyao vikiwa nje huku badhi vikiwa vimeteketea kabisa.

Akielezea Mgogoro huo kati ya kijiji na Halmashauri ya wilaya  Mwenyekiti wa kitongoji hicho Wiliam Muna amesema kuwa mgogoro huo umeanza tangu mwaka 2013.

‘’Alama za mpaka wa kijiji ziliwekwa mwaka 2003 baada ya hapo pakawa na marekebisho ambapo wananchi walipewa maeneo haya na kukabidhiwa risiti na Halmashauri ya kijiji’ alisema Muna.

Muna alisema ‘’Mimi kama kiongozi wa kitongoji jambo hii imeniumiza sana kwani wananchi wamekosa haki zao,na hata fidia hawakupatiwa.’’

Aliendelea kusema kuwa Maeneo hayo yamechukuliwa na mwekezaji kutoka  Jumuiya ya uhifadhi wanyamapori [Juibu].

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Babati Hamisi Iddy Malinga alifika katika eneo hilo na kueleza kuwa wameamua kuwaondoa kwa nguvu wananchi hao kwa kuwa wamefanya hivyo kuwaondoa ili kuendelea kulilinda ziwa Manyara.

Suala ambalo limejitokeza kwenye ekolojia wa Tarangire Manyara ni uharibifu wa Ziwa Manyara lakini pia  ushoroba unaounganisha Tarangire-Manyara.

Malinga amesema Katika eneo la kijiji cha  Manyara kumekuwa na vijiji kadhaa ambavyo siku ya nyuma  waliingia mpaka kwenye maeneo ya uhifadhi [eneo la kijani] lakini baada ya serikali kuwatangazaia waliondoka lakini imekuwa vigumu kijiji cha Mnayara kutii agizo hilo.

Mpaka sasa wanakijiji hao wamejikusanya kwa majirani wakiwa na watoto wao huku kukiwa na hofu ya kupata magonjwa ya milipuko kama vile kipindu pindu na kuhara kwani hakuna vyoo hali inayowalazimu kujisaidia vichakani.

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota, Mvuto wa Biashara na Mapenzi

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. 

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi 

+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara.?...... Tunazo dawa na PETE za bahati Zenye Uwezo wa Kubadili Maisha Yako

$
0
0
Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara,M saniiwa Maigizo, Mwanamziki, ama mwanafunzi tunazo Dawa na PETE za Bahati zenye uwezo mkubwawakuyabadilisha maisha yako nakukupatia mafanikio makubwa ndani ya mda mfupi tu. 
Kutana na Chief MAKATA.Yeye ni mtaalam na mtabibu wa nyota zab inadam na bingwa wa tiba za asili Afrikam ashariki. Wasiliana na mtaalam huyu kwani yeye ufaulu pale wote waliko shindwa na pia humaliza kazi zilizo shindikana ama zilizo achwa ndani ya siku1 tu. chief MAKATA  ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOASHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA-  Chief Sasa amezianza ziara zake za mikoani na atayatembelea maeneo mbali mbali ndani na inje ya nchi. 
Anatibu magonjwa sugu yanaojulikana nayasiojulikana kwakutumia QUR_AN MAJI , KIOO MAJINI NA MITISHAMBA.
Anazo dawa za mapenzi( Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu LIMBWATA) kumrudishaa alipote, kutoa Mikosi, Kutatuwa shida za chumaulete, mvuto wa biashara na sehem za kazi, kusafisha nyota, kurudisha mali zilizo ibiwa, zilizpotea, ama zilizodhulumiwa, kushika wezi na wachawi, kutoa ndagu, Kutoa kinga ya mwili, nyumba, Biashara, kufukuza majini wabaya, KUUZA kwa haraka (shamba, NYUMA, GARI..), Kesi mahakamani, Kuweka Zindiko ya mwili, nyumba, shamba, Gari, kupata Kazi na kupandishwa cheo, mali naU TAJIRI bila masharti na mengine mengi yaS iri. (Anazo Pia Pochi zisizo kwisha Hela MAGIC WALLET)

Kwa tiba na ushauri wasiliana na ofisi kwa
nambari ya simu
+255 676 014 385
+255 767 202 654 Chief MAKATA
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images