Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Dr Kanengo: Bingwa Wa Tiba Asili Hutibu Matatizo Yafuatayo

$
0
0
NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo kupooza kupoteza fahamu 

MALABALA; hutibu kisukari , uti wa mgogo, Change, pumu, busha, kaswende, kifua kikuu, muwasho sehemu ya siri 

NKURUNGU,: Ni dawa kutibu  N, B, G, POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge 20 

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha , pia kuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe), maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu. 

NR SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Kuisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu 

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana. (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete) ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,.(4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wachafu ndani ya mji,.

Haya yote yanawezekana kwa DR KANENGO popote ulipo . Muone  DR KANENGO,anatibu nguvu za kiume anarefusha na kunenepesha uume kwa saizi uipendayo kwa muda mfupi sana, pamoja na kuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa mara 4 bila hamu kuisha Na utachelewa kufika kileleni kwa muda wa dakika 40 bila kuchoka .

Angalizo usitume meseji wala kubipu..
 
You can get it in all East African countries,,our service is fast and easy... contact Whatsapp 0784,47,59,46.Dar es salaam Tanzania. ,..Dr. KANENGO 0744,92,29,82...You are welcome. Yuko pia Khahama Mjini, Bunda kwa sasa

Bei Imepungua 10%off Pata Saa Kali Na Lipa Mzigo Ukifika 😍😍

$
0
0
  • Tunauza saa ambazo zote ni waterproof 5atm pia saa zetu ni original ukiagiza saa zetu utapata ndani ya saa 24 tu ..utalipia mzigo ukifika mikoa hii tu  dar,mwanza ,arusha,mbeya ,moshi ,tanga,zanzbar  dodoma na morogoro ...tu ...kama hauko maeneo haya usiagize ...ukisha agiza tutakutumia na utalipia mzigo ukifka NDANI ya saa 24 TU saa ziko tunazo dar ,,chini ya mtandao wa daresalaamshop.com
  • AGIZA NA LIPA MZIGO UKIFIKA NDANI YA 24...kwa wateja serious kumbuka ni ndani ya 24 tu unapata saa yako daresalaamshop.com






Video Mpya ya Goodluck Gozbert – NIPE

$
0
0
Muimbaji wa nyimbo za Injili, Goodluck Gozbert ameachia video ya wimbo wake mpya wa NIPE. 

Audio ya wimbo huu imeongozwa na Crucial Sounds/Johntez na video imeongozwa na TrueDpictures/SammyD.

==>>Utazame hapo chini

Msanii Shilole Kapata Dili Jingine Kubwa Kutoka TTCL

$
0
0
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Shilole ameendelea kuneemeka kwa kupata madili makubwa kwa mwaka huu ambapo amepata dili lingine na shirika la kizawa la simu za mkononi la TTCL.

Shilole amethibitisha dili hilo kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuandika; "Asanteni sana TTCL Tanzania kwa kuniamini na kunipa Nafasi hii! Mkataba umeshasainiwa. Asante Kaka yangu Waziri kwa kuniamini pia. Sasa turudi Nyumbani mashabiki zangu. #RudiNyumbaniKumenoga .Wakati ndio huu! @ttcl_corporation".

Hili ni dili la pili kwa mwaka huu kwa msanii Shilole kusaini, mwezi uliopita alisaini dili la ubalozi na British Council ambalo mwenyewe alidai kuwa ni dili nono.


Jeshi La Polisi Linamshikilia Dereva wa Treni Aliyekutwa Amelewa

$
0
0
NA TIGANYA VINCENT
JESHI la Polisi Mkoa wa Tabora limewakata watu watatu kwa matukio tofauti akiwemo dereva aliyekuwa akiendesha Treni ya abiria huku akiwa amelewa na wengine wawili walikutwa wakisafirisha madawa ya kulevya aina ya Bhangi.

Taarifa ya Polisi iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo  imemtaja Dereva aliyekamatwa akiendesha treni ya abiria akiwa amelewa kuwa ni Elirehema Macha mkazi wa Dodoma.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora Kamishna Msaidizi Emanuel Nley alisema kuwa dereva huyo alikamatwa wiki iliyopita baada ya kuendesha treni ya abiria namba B 12 iliyokuwa ikitoka Dar es salaam kuelekea Kigoma akiwa amelewa na kutosimama kusimama katika kituo cha Malongwe.

Aliongeza kuwa kitendo cha dereva kutosimamisha treni kwenye kituo hicho kulileta taharuki kwa abiria waliokuwa wakitelemka na wale waliokuwa wakitaka kupanda ndipo taarifa ikatolewa polisi ambao waliweza kumkamata.

Katika tukio jingine Kamanda Nley alisema Polisi imekamata na madawa ya kulevya Amos Maziku ambaye ni Ajenti wa mabasi na Hassan Selemani dereva ambao walikutwa kwenye Kituo cha mabasi Sagara cha mjini Nzega wakiwa na Bhangi kilogram 51.45 wakiisafirisha.

Kamanda Nley alisema kuwa watuhumiwa hao walikuwa wakisafirisha bhangi hiyo kwenye basi la Shabco lenye namba za usahili T 501 BRZ lililokuwa likielekea jijini Mwanza huku wameweka ndani ya Ndoo kubwa ya maji na wamefunga ndani ya mifuko ya  Sandarusi wakiwa wamechanganya na sufuria na sahani ili wasijulikane.

Aidha Kamanda huyo alisema katika misako inayoendelea wamefanikiwa kukamata Silaha mbili zilizotengeneza kienyeji

NACTE Nacte Yatoa Ufafaunzi Kuhusu Maombi Ya Namba Ya Uhakiki Wa Tuzo (Avn) Kwa Wahitimu Wanaotaka Kujiunga Na Elimu Ya Juu

$
0
0
Baraza la Elimu ya Ufundi (Nacte) limebainisha kuwa hakuna mwombaji atakayefanyiwa udahili wa kujiunga a na chuo kama hana namba ya uhakiki wa tuzo (AVN).

Utoaji wa  AVN ulianza mwaka jana baada ya kutoka katika mfumo wa udahili wa pamoja kupitia Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU)  ambapo sasa waombaji wanawasilisha maombi katika vyuo husika.

Akizungumza leo Ijumaa Agosti 24, 2018 juu ya umuhimu wa kuwa na AVN, mkuu wa kitengo cha udahili wa Nacte, Twaha Twaha amesema  kabla ya kuwapo kwa mfumo huo, vyuo vilikuwa vinapata tabu kufanya uchaguzi wa wanafunzi wenye sifa za kozi husika.

Amebainisha kuwa walikuwa wanashindwa kujua kama vyeti vya mwombaji husika vya stashahada kama vinatambuliwa na Nacte.

Amefafanua kuwa kabla ya kuwapo kwa AVN hatua ya udahili wa wanafunzi kwenye vyuo ilikuwa ngumu na kusababisha usumbufu mkubwa.

“AVN itaondoa urasimu, ucheleweshaji wa taarifa za mwanafunzi na udanganyifu wa vyeti uliokuwa ukifanyika, ”amesema.

“Kwa kupata AVN chuo kikiingiza katika mifumo yake kinaweza kuona kama ni matokeo, kozi ya mwombaji na taarifa zake nyingine kwa sababu imeunganishwa na vyuo,  TCU, Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu na mifumo mingine ya elimu.”

Amesema kuwa tofauti na hapo wangekuwa wanapata barua nyingi za kuomba uhakiki wa vyeti vya wanafunzi wanaotaka kujiunga na elimu ya juu.

“Kwa mfano mwaka huu 2018 tumeshatoa AVN zaidi ya 9,000 na Nacte inavitambua vyuo 535 ambavyo vimesajiliwa, hivyo unaweza kuona wote hawa wangeleta barua za kuomba uhakiki,” amesema.

Ameeleza kuwa Nacte inaufahamisha umma na wananchi kwa ujumla kuwa huduma ya kuomba na kupewa AVN inafanyika mwaka mzima, hivyo kila anayetaka kujiunga na elimu ya juu lazima awe nayo.

Ameitaja changamoto kubwa wanayokutana nayo kwa waombaji wa AVN ni waombaji kutokamilisha taarifa zao.

Amesema maombi ya AVN hufanyika kwa njia ya mtandao kupitia kwenye tovuti ya baraza.

“Mwombaji hulazimika kuweka taarifa za msingi kadri zinavyotakiwa na mfumo ikiwamo namba ya usajili ya mtihani wa kidato cha nne, mwaka aliohitimu na chuo alichosoma stashahada,” amesema.

Uhakiki Mwingine Mali za CCM

$
0
0
JUMUIYA ya Wanawake ya Chama Cha Mapinduzi (UWT), inatarajia kuunda kamati maalumu ya kufanya uhakiki wa mali za jumuiya hiyo kuanzia ngazi ya mtaa hadi taifa.

UWT imechukua hatua hiyo ikiwa ni miezi michache tangu Mwenyekiti wa     CCM, Dk. John Magufuli, kuunda tume iliyochunguza mali za chama hicho nchi nzima.

Tume hiyo ya Rais ambayo iliongozwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Bashiru Ali, ilibaini upotevu mkubwa wa mali za chama hicho na jumuiya zake, ikiwamo Umoja wa Vijana (UVCCM), Jumuiya ya Wazee na UWT yenyewe.

Jana, Katibu Mkuu wa UWT, Mwalimu Queen Mlozi, alisema kamati hiyo itasaidia kubaini mali za jumuiya hiyo ambazo   zilifichwa au hazikutajwa wakati wa kamati ya Dk Bashiru.

“Tunaamini kuna mali nyingi za chama ambazo hazijaorodheshwa kwenye kamati ya Dk. Bashiru kutokana na sababu mbalimbali, hivyo basi kama jumuiya tuna kila sababu ya kuhakiki mali zetu tuweze kuzitambua,”alisema Mlozi.

Alisema mpaka sasa jumuiya hiyo ina mali nyingi ambazo nyingine hazijulikani zilipo na hata waliouziwa hawakufuata taratibu.

Alisema wakati umefika kwa jumuiya hiyo kupita kwa wananchi kuanzia ngazi ya mtaa hadi taifa   kubaini mali hizo na kuziorodhesha.

Aliwataka makatibu wa jumuiya katika ngazi za mikoa na wilaya kushirikiana na watu watakaopita kwenye maeneo yao.

“Hatuna haraka katika hili, kama kuna mali imefichwa tutajua  kwa sababu tutafuatilia hatua moja hadi nyingine  i tuweze kujua.

“Ninachowaomba makatibu wa jumuiya wa mikoa na wilaya kutoa ushirikiano kwa watu ambao watapita kwenye maeneo yao na kufuatilia suala hilo,”alisema.

Alisema baada ya kumalizika  uhakiki huo, kamati hiyo itawasilisha ripoti kwa viongozi wa juu wa jumuiya ambao nao   wataiwasilisha kwa Mwenyekiti wa CCM Rais Magufuli na Katibu Mkuu waweze kuipitia na kutoa uamuzi.

Alisema kwa wale ambao wamechukua mali hizo bila  kufuata utaratibu, uamuzi wao utatolewa  baada ya viongozi hao kupitia ripoti hiyo.

Alisema tayari imeundwa bodi ya wadhamini ambayo pamoja na mambo mengine, itaweza kusimamia mali hizo kwa utaratibu maalumu   baada ya kuhakikiwa.

Mlozi alisema  mkakati wa jumuiya hiyo ni kufanya uwekezaji kwenye mali hizo ikiwamo viwanja, maduka na mashamba hali ambayo inaweza kuwasaidia kupata mapato.

Wakati umefika wa mali hizo kusimamiwa kwa umakini na jumuiya zake  ziweze kuwanufaisha wanachama wa CCM kuanzia ngazi mbalimbali nchini, alisema.

Alisema jumuiya hiyo imekuwa mstari wa mbele kutetea maslahi ya wanawake   na kuikumbusha serikali kuteua nafasi za uongozi wa jinsia hizo   waweze kufikia malengo ya asilimia 50 kwa 50.

Alisema mpaka sasa nafasi za uongozi za wanawake ni asilimia 36, hivyo basi bado wanahitaji nafasi zaidi za uteuzi  kufikia malengo waliyokusudia.

Mlozi alisema jumuiya hiyo itaendelea kuwajengea uwezo wanawake   waweze kujikwamua katika uchumi na kujiondoa kwenye utegemezi jambo ambalo linaweza kupunguza umaskini.

Alisema wanawake popote walipo bila ya kuangalia tofauti zao za rangi, chama au kabila, wanapaswa kupaza sauti  wanapoona wenzao wanaonewa na kukemea uovu unaojitokeza kwenye maeneo yao.

Kwa mujibu wa Mlozi  jumuiya hiyo imekwisha kuanzisha dawati la jinsia ambalo pamoja na mambo mengine, litajitika kusikiliza kero za wanawake na kutoa elimu ya jinsi ya kujikomboa.

Aliwataka wanawake kujitokeza kwenye uchaguzi mbalimbali ukiwamo wa siasa na jamii ili kuwania nafasi mbalimbali za uongozi.

Diamond Ampa Makavu Shabiki Kisa Wema Sepetu

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya na C.E.O wa lebo ya WCB Naseeb Abdul a.k.a Diamond Platnumz ameamua kubishana na shabiki wake mtandaoni kisa Wema Sepetu (Madame).

Povu hilo limemtoka Diamond kutokana na shabiki huyo ku-coment katika video iliyokuwa ikimuonyesha Diamond akiwa na wema kabla ya kuelekea Samaki samaki katika birthday party ya Dj wake Rom Jones.

Video hiyo Diamond aliiweka kwenye Insta stori yake lakini pia ilionekana kwenye Snap ya Madame,licha kuonekana wakiwa wote kabla ya party kuanza lakini baada ya party kuanza Diamond alionekana peke yake lakini Wema hakufika katika party hiyo.


Katika ujumbe ambao Diamond alimwandikia shabiki wake huyo alionekana kabisa kuwa na ukaribu na Wema sepetu.

Soma ujumbe wa Diamond kwa Shabiki wake pia angalia picha zote hapa chini


DC Jokate Mwegelo apokea vifaa vya usafi na vitanda vya wagonjwa

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani, Jokate Mwegelo amepokea msaada wa vifaa vya usafi na vitanda vyenye thamani ya Sh5milioni vitakavyotumika katika hospitali ya wilaya hiyo.

Vifaa hivyo vimetolewa na uongozi wa Kampuni ya  Builder’s Center ya jijini Dar es Salaam.

Akipokea msaada huo leo Ijumaa Agosti 24, 2018, Jokate amesema uamuzi wa kampuni hiyo ni wa kuigwa kwa maelezo kuwa utapunguza changamoto zilizopo hospitali sambamba na kuboresha huduma za afya.

“Ninawashuruku kwa hiki mlichokifanya nawaomba mwakani mkifikiria kufanya jambo hilo, basi msiisahau Kisarawe,” amesema.

Amebainisha kuwa awali kampuni hiyo iliahidi kutoa vifaa vya usafi pekee lakini aliwaomba kuongeza na vitanda jambo ambalo walilikubali.

Ofisa masoko wa kampuni hiyo, Mussa Mondosha amesema wamechukua uamuzi huo kuunga mkono juhudi za Serikali kukabiliana na changamoto ya afya.

“Tumeguswa na kuamua kutoa msaada ili kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kuboresha huduma za afya. Kubwa zaidi ni kupunguza vifo vya mama na mtoto,” amesema Mandosha.

Mganga mkuu wa wilaya ya Kisarawe, Dk Jonathan Budenu ametoa wito kwa jamii na kampuni mbalimbali kutoa misaada katika hospitali za Serikali.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya Agosti 25

Viwanja Vikubwa, Vinauzwa: Bunju na Mapinga (Baobab sec)

$
0
0
Kwa upande wa Mapinga Vipo viwanja kuanzia ukubwa wa sqm 400 kwa milion 4, sqm 800 kwa milion 8, sqm 1000 kwa milion 18, sqm 1400 kwa milion 18.2, sqm 1578 kwa milion 20.5, sqm 1986 kwa milion 25.8, sqm 2386 kwa milion 31, sqm 3018 kwa milion 39.2

Viwanja hivi vyote viko umbali wa km 2.5 kutoka main road. Miundombinu ya barabara, maji na umeme yote ipo. na viko na view nzuri sana.

Kwa upande wa Bunju vipo viwanja vya ukubwa wa sqm 1700 kwa milion 50 na sqm 3400 kwa milion 95

Viwanja hivi vimegusa main road (Bagamoyo Road).
Pia ipo Nursary school space yaenye ukubwa wa sqm 4600 na inauzwa kwa milion 46 tu.

Ruksa kulipa kwa awamu 2 ndani ya miezi 3.

Hakuna dalali. contact mhusika:
call 0758603077, whatsap 0757489709

Nuh Mziwanda: Siwez Kumpongeza Shilole Kwa Kujenga Nyumba

$
0
0
Msanii wa muziki wa bongo fleva, Nuh Mziwanda amefunguka na kudai hawezi kumpongeza aliyekuwa mpenzi wake wa zamani Shilole, kwa kuweza kujenga nyumba ya kuishi licha ya kwamba alikuwa anafahamu juu ya jambo hilo.

Nuh ametoa kauli hiyo jana alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha eNewz kinachorushwa nakituo cha  EATV, na kusema kwamba anayepaswa kutoa pongezi au kumtia moyo wa faraja ni mumewe Uchebe nasio yeye.

"Siwezi kuzungumzia chochote kuhusiana na suala la Shilole kujenga nyumba. Mimi sitaki kuongea mambo ya Shishi halafu siwezi kumpa moyo kuhusu nyumba moyo atapewa na Uchebe sio mimi japo nilikuwa najua kuwa Shishi anajenga", amesema Nuh.

Kauli hizo za Nuh zimekuja ikiwa zimepita takribani siku nne tokea mwanadada Shilole, kuweka picha mtandaoni ikiwa inamuonyesha yupo katika harakati za kumaliza ujenzi  wa nyumba hiyo.

Mbali na hilo, Nuh Mziwanda amefafanua kuwa sio kweli nyimbo yake aliyoitoa hivi karibuni amemshirikisha Ben Pol, bali kazi hiyo wamefanya wote pamoja kwa maana ni kazi yao wote.

Ruto ajibu utafiti unaoonesha anatajwa kuongoza kwa rushwa

$
0
0
Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto amejibu matokeo ya utafiti uliofanywa unaoonesha kuwa anatajwa na asilimia 33 ya Wakenya kuwa anaongoza kwa vitendo vya rushwa.

Utafiti huo uliofanywa na taasisi ya Ipsos Synovate, iliyopitia Kaunti 45 na kuwahoji jumla ya watu 2,000 unamuweka Ruto kwenye nafasi ya kwanza akiwa na silimia 33, akifuatiwa na Gavana wa Kirinyaga ambaye amepata asilimia 31.

Kadhalika, utafiti huo umeonesha kuwa asimilia 51 ya Wakenya wana imani na jinsi ambavyo Rais Uhuru Kenyatta anapambana na vitendo vya rushwa.

Ruto ameeleza kuwa utafiti huo umefanywa kama propaganda ya kumchafua kwakuwa wapinzani wake hawawezi kushindana naye kwenye rekodi ya kuwaletea maendeleo Wakenya.

“Wakimalizana na propaganda zao za vichwa vya habari, tukutane kwenye kilinge cha kuwaletea maendeleo Wakenya kwa sababu hapo ndipo ushindani wa kweli  ulipo,” alisema Ruto.

“Wapinzani wangu wakimalizana na utafiti walioufadhili, habari za uongo, tukutane kwenye hiki kilinge cha kuleta maendeleo kinachomlenga mwananchi wa chini, reli ya kisasa, pato la mwananchi, barabara, kuwaunganishia wananchi umeme, kuboresha huduma za afya na mani. Nawangojea huko,” aliongeza.

Utafiti huo unachukuliwa na wafuasi wa Ruto kama njia ya kutaka kukwamisha mbio zake za kuelekea Ikulu, kwani imewekwa wazi kuwa atawania nafasi ya urais katika uchaguzi ujao wa mwaka 2022.

Hata hivyo, utafiti wa Ipsos haukuwaacha salama wanasiasa wengine, Daniel Arap Moi (Rais Mstaafu), Mwai Kibaki (Rais mstaafu), Raila Odinga (Kiongozi wa upinzani) na Rais Kenyatta wametajwa kwenye nafasi sita za juu japo wana asilimia chache.

Kigwangalla atembea kilomita nne....Hali Yake Inazidi Kuimarika kwa sasa

$
0
0
Hali  ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla, aliyelazwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI), inazidi kuimarika na juzi alifanya mazoezi ya kutembea umbali wa kilometa nne kwa kutumia saa moja na dakika 23.

Dk. Kigwangalla alifanya mazoezi hayo juzi jioni kwa kutembea umbali huo kisha kupanda jengo la MOI kwa kutumia ngazi kutoka chini mpaka ghorofa ya Sita.

"Kwa sasa naendelea vizuri tofauti na awali nilipokuwa natembea umbali mdogo kutoka Wodi ya Mwaisela nilipokuwa nimelazwa na kutembea mpaka geti la kuingilia hospitali hii ya Muhimbili.

“Kwa sasa natembea umbali mrefu Zaidi. Nilianza na kilomita moja, nikaongeza kilometa moja na nusu na baadae mbili, lakini nikaona leo (juzi) niongeze zaidi na  kumaliza kilomita hizi nne,’ alisema.

Aliongeza kuwa: “Mazoezi haya ya kutembea yananisaidia kuimarisha zaidi mapafu. Lakini kwa sasa bado nashughulikia mkono pekee."

Dk. Kigwangalla huanza kufanya mazoezi hayo kila siku jioni kwa lengo la kujiimarisha kiafya pamoja na tiba kwa hali yake hiyo ambayo kwa sasa anaendelea na matibabu.

Kwa upande wao madaktari bingwa wanaomtibu waziri huyo, walibainisha kuwa licha ya kuendelea vizuri, bado wanafuatilia kwa karibu hali ya afya yake hadi watakapojiridhisha ndipo watamruhusu kurejea nyumbani kuendelea na majukumu yake.

Dk. Kigwangalla alipelekwa MOI Agosti 12, mwaka huu, na kufanyiwa upasuaji wa mkono ambao ulivunjika kutokana na ajali aliyoipata Agosti 4, akiwa kwenye ziara ya kikazi mkoani Manyara.

Dkt. Jakaya Kikwete kumwakilisha Rais Magufuli nchini Zimbabwe


Uchaguzi Mdogo Jimbo la Liwale ni October 13

$
0
0
Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Liwale Mkoa wa Lindi, utafanyika Oktoba 13 baada ya aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo, Zuberi Kuchauka (CUF) kujiuzulu na kujiunga na CCM.

Akitangaza uchaguzi huo Jijini Dar es Salaam leo Agosti 25, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC) Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Semistocles Kaijage amesema tangazo la uchaguzi linakuja baada ya Tume kupokea barua kutoka kwa Spika wa Bunge la Tanzania.

“Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilipokea barua kutoka kwa Spika wa Bunge, ambaye kwa kuzingatia kifungu cha 37(3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, ameitaarifu Tume kuwepo kwa nafasi wazi ya Ubunge katika Jimbo la Liwale Mkoa wa Lindi, kuanzia tarehe 13 Agosti, 2018,” amesema Jaji Kaijage

Akizungumzia  ratiba ya uchaguzi huo mdogo, Jaji Kaijage amesema, fomu za uteuzi zitatolewa Septemba 7 hadi 13  mwaka huu na uteuzi wa wagombea utafanyika Septemba 13 mwaka huu.

Taarifa hiyo imesema kampeni za uchaguzi zitaanza Septemba 14 na kumalizika Oktoba 12 mwaka huu na siku ya uchaguzi itakuwa  ni Oktoba 13 mwaka huu.

“Tume inavikumbusha vyama vya siasa na wadau wote wa uchaguzi kuzingatia sheria, kanuni, maadili ya uchaguzi, miongozo, na maelekezo yote wakati wa kipindi cha uchaguzi huo mdogo,” Jaji Kaijage amesema.

Aliyemuua Mkewe kwa Risasi Akutwa Porini Amejinyonga

$
0
0
NA TIGANYA VINCENT
Mkazi wa Kijiji cha Ikongoro wilayani Uyui Said Ramadhan ambaye alimuua mkewe Mwajuma Hussein kwa kumpiga risasi

kutokana na kile kilichodiwa  wivu wa mapenzi na kisha kukimbia amekutwa amejiua kwa kujinyonga  juu ya mti.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana  na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora Emmanuel Nley kwa vyombo vya habari imesema kuwa matukio hayo yametokea Agosti 21 mwaka huu.

Alisema kuwa Ramadhani ambaye alikimbilia porini baada ya kutenda tukio la mauaji ya mkewe akiwa na bunduki aina ya gobore alikutwa amekufa kwa kujinyonga huku silaha hiyo ikiwa pembeni.

Kamanda Nley alisema kuwa uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa chanzo cha mauaji hayo ni wivu wa mapenzi kwani kabla Ramadahi ambaye sasa ni marehemu hajamuoa Mwajuma naye Marehemu alikuwa ameolewa na Jumanne Malawiro ambaye walizaa naye watoto wawili.

Alisema  kuwa marehemu Ramadhan alihisi kuwa uenda mkewe bado ana mahusiano ya kimapenzi na mzazi mwenzie huyo ndipo akaamua kumuua na kisha yeye kujiua.

Katika tukio jingine Polisi wanamshikilia mkazi wa kijiji cha kombe wilayani Kaliua Chiga Lutumbiga kwa tuhuma ya kumpiga na kumuua mkewe Mwanza Kushema na kisha kutelekeza mwili wake katika msitu wa hifadhi ya Usawima.

Alisema kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 21 mwaka huu kwenye msitu wa Isawima kitongoji cha Kombe kata ya Igagala mwili wa mwanamke huyo uliokotwa ukiwa na majeraha kichwani na sehemu mbali mbali za mwili.

Kamanda Nley alisema kuwa katika ufuatiliaji imegundulika kuwa kabla ya kifo hicho marehemu alitumwa kufuata mahitaji kijiji cha Ugasa na alipochelewa kurudi nyumbani mumewe alimfuatilia  na kumkuta njiani akirudi ndipo akampiga nakumwacha porini akiwa uchi.

Aliongeza kuwa mtuhumiwa baada ya kufika nyumbani alipiga kelele za kuomba msaada kwa wananchi  wamsaidie kumtafuta mkewe ambaye walimkuta amekufa hapo msituni akiwa uchi huku akiwa na majeraha.

Hali ya Ommy Dimpoz ni mbaya, arudishwa hospitalini Afrika Kusini

$
0
0

Msanii wa Bongo Fleva, Omar Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ amerudishwa nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’ kwa ajili ya matibabu baada ya hali yake kuendelea kutokuwa vizuri licha kutolewa hospitalini huko siku chache zilizopita.

Dimpoz ambaye miezi miwili iliyopita alifanyiwa upasuaji mkubwa wa koo nchini Afrika Kusini, hali yake imekua haiimariki ipasavyo jambo lililosababisha kupandishwa ndege na kurudishwa tena huko kendelea na matibabu zaidi.

Tokea June 15,2018 Ommy Dimpoz hajaongea chochote wala kupost chochote kupitia ukurasa wake wa instagram zaidi ya vyombo vya habari kupata taarifa kutoka kwa Manager wa Ali Kiba ambaye ni Seven Mosha na kusema kuwa Ommy alikuwa akiendelea vizuri

Kupitia ukurasa wa instagram wa Madee Ali amempost Ommy Dimpoz na kuandika caption inayoonyesha kuwa hali ya Ommy Dimpoz sio nzuri hivyo anahitaji maombi kutoka kwa mashabiki.

“Kwenye maombi yetu ya kila siku tusimsahau Omary tumuombee apone haraka aendelee na majukumu yake Omary anaumwa tuseme Ameeeen🙏🙏”

Tanzanite Kuwa Na Hati Ya Utambulisho Kimataifa

$
0
0
Na Asteria Muhozya, Dodoma
Serikali imesema inafanya utaratibu wa kuwa na Hati ya Utambulisho wa Kimataifa wa Madini ya Tanzanite, ambayo yanapatikana katika nchi ya Tanzania pekee katika vilima vya Mirerani, Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara.

Hayo yamebainishwa leo tarehe 25 Agosti na Waziri wa Madini Angellah Kairuki wakati wa Semina ya mafunzo kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ambayo imefanyika Makao Makuu ya Wizara, jijini Dodoma.

Waziri Kairuki amesema kuwa, serikali inataka kuona kuwa dunia inafahamu kuwa, madini hayo yanapatikana Tanzania pekee na kuhakikisha kwamba yanajulikana zaidi.

Semina ya wabunge imefanyika kufuatia maelekezo ya Kamati hiyo ambayo ilitaka kufahamu kuhusu mwenendo mzima wa Madini ya tanzanite, biashara na udhibiti wa madini hayo baada ya kujengwa kwa Ukuta wa Mirerani unaozunguka migodi ya madini ya tanzanite, Muundo wa Wizara ya Madini, Tume ya Madini na majukumu yao.

Waziri Kairuki amesema kuwa, Wizara imepata fursa ya kuwasilisha kwa Kamati hiyo taarifa za utekelezaji wa majukumu mbalimbali ikiwemo mikakati ya serikali katika kudhibiti utoroshaji wa madini hayo na mipango madhubuti ambayo serikali inakusudia kuifanya ili kuhakikisha kwamba rasilimali madini inalinufaisha taifa na hatimaye sekta ya madini iweze kufikia asilimia 10 ya machango wake katika pato la taifa ifikapo mwaka 2025.

Ameongeza ni  kikao ambacho kimekuwa na manufaa kwa upande wa Serikali kwa kuwa imetoa elimu kwa Kamati hiyo kuhusu yale ambayo serikali imefanya na inayokusudia kufanya kuhusuiana na madini  ya tanzanite lakini pia serikali imepata wasaa wa kupokea maoni, mapendekezo na maelekezo kutoka kwa wabunge ambayo yatawezesha kupeleka mbele sekta ya Madini.

Mbali ya tanzanite, Waziri Kairuki amewaeleza wabunge hao kuhusu mkakati wa serikali kuanzisha Mineral Exchange ambapo amesema tayari wizara imeshaandaa timu ya wataalam ili kwenda kujifunza na kufanya utafiti katika nchi nyingine ili suala hilo liweze kufanyika kwa ubora .

Pia, ameeleza kuwa, Wabunge wa Kamati hiyo, wamepata fursa ya kufahamu majukumu ya Wizara baada ya kuundwa kwa Tume ya Madini, majukumu ya tume ya madini na mahusiano ya kiutendaji kati ya Tume na Wizara.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mariam Ditopile, amesema kuwa, kamati imebaini kuwa, Serikali imechukua hatua nyingi za kulinda na kudhibiti madini ya tanzanite ikiwemo  kudhibiti utoroshaji wa madini hayo. “Kama kamati tumeona mnyororo mzima wa thamani ya madini ya tanzanite, awali tulikuwa hatunufaiki kama taifa,” amesema Ditopile.

Awali, akiwasilisha mada kuhusu hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kudhibiti utoroshaji wa madini ya tanzanite na usimamizi wa shughuli za uchimbaji na biashara ya madini ndani ya ukuta, Afisa Madini Mkazi wa Mirerani Mhandisi David Ntalimwa, amezungumzia sababu za kushuka kwa mapato na kueleza kuwa, kunategemea kiwango cha ubora na sifa za madini husika.

Ameongeza kuwa, kutokana na mazingira hayo, kiwango cha thamani ya madini na tozo ya mrabaha kitakuwa tofauti kutegemea na mwezi na uzalishaji uliopo.

Akizungumzia sababu za utoroshaji wa madini ya tanzanite, Mhandisi Ntalimwa amesema kuwa, zinatokana na uwezo mdogo wa kusanifu na kuongeza thamani na kunga’risha madini ya vito na hivyo watu kutamani kuuza tanzanite ghafi.

Pia, amesema utoroshaji wa madini unatokana na kukwepa kulipa kodi na tozo mbalimbali zinazotozwa na serikali ili kujipatia faida kubwa, kuwepo kwa raia wa kigeni nchini wanaofanya biashara ya madini kinyume na sheria kwa kushirikiana na wazawa na kukosekana kwa masoko ya uhakika ya kuuzia madini yanayozalishwa.

Akizungumzia hatua zilizochukuliwa na serikali katika kudhibiti utoroshaji wa madini baada ya kujengwa ukuta amesema kuwa, serikali imeimarisha ulinzi na ukaguzi getini kwa kutumia vikosi vya ulinzi na usalama, kuzuia magari kuingia na kutoka ndani ya ukuta, watu kuingia ndani ya ukuta kwa vitambulisho maalum.

“ Sasa watu wanaingia kwa utaratibu maalum tofauti na walivyozoea awali. Ukuta umeleta utaratibu mzuri na si kero, kama baadhi ya watu wanavyodhani,” amesisitiza Ntalimwa.

Amezitaja hatua nyingine kuwa ni pamoja na kuzuia Mabroker kwenda migodini na badala yake kutakiwa kusubiria madini getini, uthaminishaji madini kufanyika ndani ya ukuta na serikali kujenga jengo lenye ofisi ya ukaguzi, uthaminishaji na ukumbi wa mabroker ndani ya ukuta.

Aidha, pamoja na kushiriki semina hiyo, pia wabunge hao wamepata fursa ya kutembelea Makumbusho ya Taifa ya Jiolojia na Madini katika Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania, (GST).

Ugonjwa wa Dimpoz wamaliza tofauti yake na Diamond

$
0
0
Msanii Diamond Platnumz amezitupilia mbali tofauti zake zilizokuwepo kati yake yeye na msanii mwenzake Ommy Dimpoz katika wakati huu mgumu kwa Ommy Dimpoz na kumuombea apone mapema ili aweze kurudi katika hali yake ya mwanzo.

Diamond ameweka picha ya msanii mwenzake huyo katika mtandao wake wa kijamii wa Instagram, akimwombea apone haraka na kurejea katika muziki.

“Inshaallah! Mwenyezi Mungu akufanyie wepesi uweze kupona haraka na kurudi kuendelea na sanaa ili pamoja tuzidi kupeleka muziki wetu mbali zaidi,” ameandika Diamond.

Hii ni mara ya kwanza kwa mwanamuziki huyu kuweka ujumbe katika mtandao wake kuhusu  Ommy Dimpoz tangu walipojibizana katika vyombo vya habari Agosti, 2017 huku kila mmoja akimtuhumu mwenzake mambo mbalimbali.

Dimpoz akiwa msanii chini ya lebo ya Rock Star 4000 pamoja na Alikiba, wamekuwa na uhasama wa kimuziki na Diamond Platnumz kwa muda mrefu.

Mashabiki wa Diamond wamempongeza kwa kuweka pembeni tofauti zao za kibiashara na kumpa pole mwenzake kupitia mtandao huo wa kijamii.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images