Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Sababu Za Kiroho Kwanini Baadhi Ya Wanawake Wazuri Kupita Kiasi Huwa Hawaolewi.

$
0
0
Duniani  hakuna  mwanamke  mbaya. Wanawake  wote  ni  wazuri. Na  uzuri  wa  mwanamke  sio  sura  wa  umbo  uzuri  wa  mwanamke  ni  tabia  yake.

Kama  nilivyo  sema  hapo  juu  kwamba  wanawake  woote  duniani  ni  wanawake  wazuri, isipokuwa wamegawanyika  katika  makundi  makuu mawili.  Kundi  la  kwanza  ni  wanawake  wenye  uzuri  wa  kawaida  na  kundi  la  pili ni  wanawake  ambao  ni  wazuri  kupita  kawaida.

Katika  Makala  haya  nimewalenga  wanawake  walio  katika  kundi  la  pili, yani wanawake wazuri  kupita  kawaida.

Katika  jamii  inayo  tuzunguka  kuna  Imani  kubwa  imejengeka  kwamba  wanawake  wazuri  kupita  kiasi  hawafai  kuolewa  kwa  sababu inaaminika  kwamba  wanawake  wazuri  kupita  kiasi  ni  vigumu  sana  kutulia  na  mwanaume   mmoja  kwa  sababu  wana  tama asana na  kwamba  wengi  wao  hawana  mapenzi  ya  ukweli.  Bila  shaka  hii ndio  sababu  inayo  wafanya  wanaume  wengi  kuogopa  kuwaoa wanawake  wazuri  kupita  kiasi na  mwisho  wa  siku  wanawake wazuri  kupita  kiasi  kuishia tu kuwa  katika  mahusiano ya  kimapenzi  ya  muda  mfupi na  kuachwa.

Je  dhana  hiyo  ni  ukweli  au  ni  uzushi  tu  wa  walimwengu ?

 Katika  Makala  haya  utapata kuyajua  majibu  ya  kina  kwanini  baadhi au  kwanini  wengi  wa  wanawake  wazuri  kupita  kiasi  huwa  hawaolewi  na  hata  ikitokea  wakiolewa  basi  ndoa  zao  huwa  hazidumu ..  Nikiwa  kama  Tabibu  wa  Jadi, sababu  zangu  ni  sababu  za  kiroho.

Zipo  sababu  kadhaa  zinazo  fanya  wengi wa  wanawake  wazuri  kupita  kiasi  wasiolewe.

 Baadhi  ya  sababu  hizo  ni  kama  ifuatavyo :

1.       MAJINI  MAHABA.
Kuna  wanawake  ni  warembo  na  wazuri  kupita  kawaida  kiasi  kwamba  huwavutia  mpaka  majini  mahaba.

Kabla  sijaelezea  namna  majini  mahaba  wanavyo  sababisha  wanawake  wazuri  kupita  kiasi  wasiolewe ni  vyema  nikakujulisheni   kwa  ufupi  kuhusu  historia  ya  suala  la  majini  na  viumbe  wengineo  wa  kiroho  kua katika  mahusiano  ya  kimapenzi  na wanawake  wa  kibinadamu.

Suala  la  majini  na viumbe  wengine  wa  kiroho  kuvutiwa  kimapenzi  na  wanawake  wa  kibinadamu

( wenye  uzuri na urembo  ambao unapita  kawaida )na  kuanzisha  nao  mahusiano  ya  kimapenzi  halijaanza  jana  wala  juzi.

 Suala  hili  lipo duniani  toka  enzi  za  mitume  na  manabii.

Ukiisoma  vizuri  Taurati utagundua  kwamba  kuna  malaika  waliwapenda  wanawake  wa  kibinadamu  na  kuwaoa  kisha  kuzaliwa  viumbe  walio julikana  kama  wanefili. 

Kwa  hiyo  suala  la  viumbe  wa  kiroho  kuvutiwa  kimapenzi na  wanawake  wa  kibinadamu  ni  suala  la  kawaida  kabisa  katika  ulimwengu  wa  rohoni.

Nirudi  kwenye  mada yangu.  Majini  mahaba  huwa  wanavutiwa  sana  kimapenzi  na  wanawake  walio  jaliwa  uzuri  wa  sura  na  maumbo  ambao  si  wa  kawaida.

KITU   GANI  HUTOKEA  JINI  MAHABA  AKIMPENDA  MWANAMKE

Jini  mahaba  akimpenda  mwanamke  huwa anaingia   na  mwanamke  huyo  katika  agano  la  kichwa  na  mwili ( Jinni  mahaba  huwa  kichwa  na  mwanamke  huyo  huwa  mwili/ katika  ulimwengu  wa  kiroho  agano  la  kichwa  na  mwili  maana  ake  ni  agano  la  ndoa  kati ya  mwanamke  na  mwanaume )

 Kwa  lugha  ya  kawaida  jinni  mahaba  huyo  huingia  na mwanamke  huyo katika  agano  la  ndoa  ya  mke  na  mume .   Jinni  mahaba  huwa  mume  na  mwanamke  huyo  huwa  mke.

Agano  hili hufanyika  bila  ridhaa  ya  mwanamke huyo. Kwa  lugha  nyingine  mwanamke  huyo  anakuwa  amelazimishwa kuolewa  na  jinni  mahaba  huyo  bila  yeye  mwenyewe  kujua  au  kutaka.

KITU   GANI  HUTOKEA  JINNI MAHABA  AKIFUNGA  NDOA  NA  MWANAMKE

Jinni  mahaba  akifunga  ndoa  na  mwanamke, maana  yake  ni  kwamba  katika  ulimwengo  wa  rohoni  mwanamke  huyo  anakuwa  mke  halali  kabisa  wa  jinni  huyo.

Jinni  huyo  anakuwa  anammiliki  mwanamke  huyo  na  kumtumia  kama  mke  wake na  anakuwa  na  haki  za  kiroho  za  kufanya  jambo  lolote  juu  ya  mwanamke  huyo  kama  mke  wake ikiwa  ni  pamoja  na  kutoa  adhabu  kwa  wanaume  wanao mzengea  mwanamke  huyo.

KITU  GANI  HUTOKEA  PINDI  MWANAUME  ANAPOINGIA  KATIKA  MAHUSIANO  YA  KIMAPENZI  NA  MWANAMKE  AMBAE  AMEOLEWA  NA  JINNI  MAHABA.

Mwanaume unapoingia  katika  mahusiano  ya kimapenzi na  mwanamke  ambae  ameolewa  na  jinni  mahaba  maana  yake  katika  ulimwengu  wa  rohoni  ni  kwamba  umeingilia  ndoa  ya  “ mtu “ mwingine.

Umefanya  dhambi  ya  zinaa  kwa  kuzini  na  mwanamke  ambae  tayari  anamilikiwa  na  “ mtu “ mwingine.

Kitakacho  fuatia  hapo  ni  wewe  kulipa  deni  la  kiroho  kwa  ‘dhambi’ ya  kutembea  na  mke  wa  mtu.

Haijalishi  kwamba  ulikuwa  unajua   au  ulikuwa  haujui kama  mwanamke  huyo  anamilikiwa  na  jinni  mahaba, kwa  sababu  katika  ulimwengu  wa  rohoni  kutojua  kuhusu  jambo  sio  kinga  ya  kukuepusha  na  adhabu  ya  kufanya  jambo  ambalo  limekatazwa  ambalo  wewe  haulijui.

NI ADHABU  GANI  ZA  KIROHO  ANAZO  WEZA  KUZIPATA  MWANAUME  AMBAE  AMEINGIA  KATIKA  MAHUSIANO  YA  KIMAPENZI  NA  MWANAMKE  AMBAE  AMEOLEWA  NA  JINNI  MAHABA.

Zipo  adhabu  nyingi  sana  ila  leo  nitazitaja  chache  hususani  zile  ambazo  zinahusiana  moja  kwa  moja  na  suala  la  wanawake  wazuri  kupita  kiasi  kutokuolewa.

1.       KUHARIBIKIWA  MAMBO  YAKO  KIFEDHA  NA  KIMAISHA  KWA  UJUMLA :  Jinni mahaba  anae  mmiliki  mwanamke  ambae  umeingia  nae  katika  mahusiano  ya  kimapenzi akisha  gundua kwamba  wewe  ‘ umeingilia  ndoa  yake ‘  atakacho  kifanya  atatafuta  kujua  kitu  gani  ambacho  kimemvutia  ‘mke  wake’ huyo   kuja  kwako. Atataka  kujua  ni Kitu  gani  ambacho  kimemfanya  ‘mke  wake ‘ akupende  na  kuingia  katika  mahusiano  ya  kimapenzi  na  wewe.

Akigundua  kwamba  kitu  kilicho  mvutia  “ mke “ wake  kuwa  katika  mahusiano  ya  kimapenzi  au  kuolewa  na  wewe  ni  pesa  au  mali  zako, atakacho  kifanya  ni  kuharibu  ‘ chanzo  cha  tatizo’ (  Naposema  chanzo  cha tatizo  namaanisha  chanzo  cha  wewe  kuleta  matatizo  katika  ndoa  yake  kwa  kuingia  katika  mahusiano  ya  kimapenzi  na  mke  wake )

Kwa  hiyo  sasa  jinni  huyo  atakacho  kifanya  ni  kutia  giza , utupu  na  ukiwa  kwenye  nyota  yako.

Kwa  lugha  rahisi  ni  kwamba  jinni  huyo  ataharibu  na  kuua  nyota  yako.  Na  kama  nilivyo  wahi  kufundisha  kwenye  masomo  yangu  yaliyo  pita,   nyota  ya  mtu  ndio  chanzo  cha  kila  kitu  katika  maisha  ya  mwanadamu.

Jinni  huyu  akiharibu  nyota  yako  basi  mambo  yako  yataanza  kuharibika  taratibu, kama  ni  kazini  basi  itaanza  kutokea  misuko suko, utashushwa  cheo  au  kufukuzwa  kazi  kabisa, na  maisha  yako  yataanza  kuyumba  taratibu  na  mwisho  wa  siku  utafilisika  kabisa.

Kama  ni  mfanyabiashara  basi  ataua  biashara  zako  zote  na  kuziba  vyanzo  vyote  vya  pesa  katika  maisha  yako  na  kukufanya  uwe  na  maisha  magumu  na  hatimaye  kufilisika  kabisa.

Kwa sababu  huyu  mdada  mzuri  alikupenda  kwa  sababu  ya  pesa  zako  na  wewe  sasa  hivi  hizo  pesa  huna  tena  wala  maisha  yako  hayaonyeshi  dalili  zozote kwamba  utaanza  kupata  pesa  kama  hizo tena  hivi  karibuni, mwanamke  huyo  ima  atakuacha na  kuchukuliwa  na  mwanaume  mwingine  mwenye  pesa  na  uwezo  wa  kumtunza  au  wewe  mwenyewe  utamkimbia  kwa  kushindwa  kumudu  kumuhudumia  au  kwa  kukimbia  aibu  ya  kuadharauliwa  na  mwanamke  huyo  kwa  sababu  utakapo  anza  kuishiwa  pesa  za  kumuhudumia  na  atakapo  kuwa  akikuomba  pesa  za  matumizi  na  mahitaji  ambazo  wewe  huna  atakuwa  akipokea  pesa  za  matunzo  kutoka  kwa  wanaume  wengine  ambao  watakuwa  wanamtaka.

Mwanaume  atakae  kupokea  kijiti  nae  mambo  yake  yatakuwa  hivyo  hivyo  kama  ilivyo  kuwa  kwako. Hali  hii  itajirudia  na  kujirudia  kwa  mwanamke  huyo. Na  anaweza  kwenda  nayo  hivyo  hivyo katika maisha  yake  yote.

Watu  wa  nje  wataanza  kumuogopa  na  kumnyanyapaa  mwanamke  huyo  kwa  kusema  ana  nukushi ( nuksi )  na  mwanaume  yoyote  mwenye  pesa  atakae  ingia  katika  mahusiano  nae  ya  kimapenzi  basi atafilisika.

Mwisho wa  siku  sasa  wanaume  waoaji  wataanza  kumkwepa  mwanamke  huyo  na kumbuka  kuwa  muda  hausimami.

Mwisho  wa  siku  mwanamke  huyo  atafikisha  miaka  35  bado  yupo  nyumbani  kwa  wazazi  wake  akiwa  na  mtoto  Zaidi  ya  mmoja  na  kila  mmoja  akiwa  na  baba  yake  wakati  huo  uzuri  wake  unakuwa  umeisha  chuja  na  kunakuwa  hakuna  mwanaume  mwingine  wa  maana  ambae  ana  fikiria  kumuoa.

Wakati  watu  wa  nje  wakimuona  mwanamke  huyo  kama  mwanamke  mwenye  nuksi  ambae  kila  mwanaume  anaeingia  nae  katika  mahusiano  huishia  kufilisika,  hali huwa tofauti  kabisa  ndani  ya  nafsi  ya  mwanamke  huyo.

Ndani  ya  nafsi yake mwanamke  huyu  hubaki  kujilaumu  mwenyewe  kwa  kudhani kuwa  suala  la  yeye  kutopata  mume  wa  kumuoa   limesababishwa  na   tabia  zake  za kutowavumilia  wanaume  zake  pindi  wanapo kuwa  wamefulia.

Na  mara  nyingi  huanza  kujitafakari pindi umri  unapokuwa  umeanza  kusogea.

Katika  kipindi  hiki  mwanamke  huyu  anakuwa  tayari  ana  miaka  thelathini  au  na  Zaidi na  anakuwa  na  mtoto  Zaidi  ya  mmoja  huku  kila  mtoto  akiwa  na  baba  yake.

Mara  nyingi  wanaume  ambao  aliwaacha  baada  ya  kufilisika  wanakuwa   tayari  wanaendelea  na  maisha  yao  na  wengi  wao  wanakuwa  wameoa  na  kutulia  na  wanawake  wengine  ambao  uzuri  wao  ni  kawaida.

 Wanawake  hawa  hujilaumu  sana na  hatimae  huanza  kubadili  tabia  na  mtazamo  wao  kuhusu  wanaume  wa  kufunga  nao  ndoa .

Kinapokuwa  kimefikia  kipindi  hiki  mwanamke  huyu  anakuwa  yupo  tayari  kujishusha  na  kuishi  na  mwanaume  wa  aina  yoyote  ile hata  kama  hana  kitu.

Cha  kushangaza  ni  kwamba  hata  inapo  tokea  wakaingia  katika  mahusiano  na  mwanaume  asie  na  kitu  nayo  huishia  hewani  bila  sababu  yoyote  ya  msingi.

Dada   huyu  anasema “  Kuna  mwanaume  mmoja  alinifuata  tukaanzisha  nae  mahusiano. Baada  ya   kuzoeana  nikaanza  kumshawishi  nataka  tufunge  ndoa  akasema  mambo  yake  ya  kifedha  bado  hayajakaa  sawa  nikamwambia  nitamkopesha  hela  afungue  biashara.  Mipango  ya  kwenda  kujitambulisha  nyumbani  kwetu  ikaanza kufanyika  na  huwezi  kuamini  pesa  aliyo  nitolea  mahali  mimi  ndio  nilimpa  kwa  sababu  hakuwa  na  uwezo. Lakini  kitu  cha  ajabu  mipango  ile  iligeuka  ghafla na  mimi  na  yule  mwanaume  tukabaki  kuwa  maadui  wakubwa “.

Mwisho  wa  siku  wanawake   hawa  huamua  kukubaliana  na  matokeo  na  kuishi  maisha  ya  kusononeka  kutokuwa na  mume  katika  maisha  yao  yote.  Hubaki  kujilaumu  kwa  usaliti  walio  wafanyia  wapenzi  wao  wa  awali  bila  kujua  kwamba  ilisababishwa  na  jinni  mahaba.

2.       KUSABABISHIWA  MARADHI  YA  UKHANITHI : Jinni  mahaba  akigundua  kwamba  kinacho  mfanya mke  wake  akupende  wewe  ni  uwezo  wako  mzuri  kitandani  basi  atakacho  kifanya  ni  kukutia  ukhanithi  jambo  litakalo  kufanya  kutokuwa  na  uwezo  tena  wa  kumridhisha  mwanamke  huyo  na  hali  hiyo ikiendelea  kwa  muda  mrefu  basi  mwanamke  huyo  atakuacha  na  kwenda  kwa  mwanaume  mwingine  ambae  nae  atafanyiwa  hivyo  hivyo.

Mzunguko huo  utaendelea  na  kuendelea  na  mwisho  wa  siku  mwanamke  huyo  atawachukia   kabisa  wanaume  na  kudharau  uwezo  wao  wa  kufanya  tendo  la  ndoa  pamoja  na  kulichukia  tendo  la  ndoa  kabisa.

Na  hii ndio  sababu  kwanini  baadhi  ya  wanaume  hulalamika   kwa  kusema “ Nikiwa  na  mwanamke  Fulani  nakuwa  sina  uwezo  kabisa  wa  kufanya  tendo  la  ndoa  au  nafanya  mara  moja  halafu  nachoka  sana  kiasi  ambacho  nakuwa  siwezi  kurudia  tena  tendon na  kama  ni usiku  basi  nitalala  fofofo  hadi  asubuhi  na  kumuacha  mwenzangu  akiwa  bado  ananihitaji  lakini  nikienda  kwa  mwanamke  mwingine  ninakuwa  na uwezo  mkubwa  sana.   Mbaya  Zaidi  mwanamke  huyo  anaweza  kuwa  mke  wako  wa  ndoa  kabisa ( UNAWEZA  KUMUOA  KABISA  MWANAMKE  AMBAE  AMEOLEWA  NA  JINNI  MAHABA  LAKINI NDOA  YENU  HAITADUMU  NA  ITAVUNJIKA  KWA  SABABU  YA  MUME  KUTOKUWA  NA  UWEZO  WA  KUMTIMIZIA  UNYUMBA  MKE  WAKE    AU  KINYUME  CHAKE  YANI  MUME  KUTOKUWA  NA  HAMU  KABISA  YA  KUFANYA  TENDO  LA  NDOA  NA  MUME  WAKE )

3.        KUKUSABABISHIA  MARADHI  NA  MAGONJWA  MBALIMBALI : Jinni  mahaba  anaweza  kuamua  kukusababishia  maradhi  mbalimbali ya  kisheitwani  ili  ya  kufanye  uwe  bize  kutafuta  tiba  yake  na  kuachana  na  ‘mke wake’

4.       KIFO :  Baadhi  ya  majini  mahaba  hutoa  adhabu  ya  kifo  kwa  wanaume  wanao  tembea  na  wanawake  ambao majini  hao  wamewaoa.  Majini  hawa  wanakuwa  hawataki  kushea  ‘mke’ na  wanaadamu  na  hutoa  adhabu  ya  kifo  ili  kuwatisha  wanaume  wengine  wasijaribu  kumfuata  mwanamke  huyo.

Hali  hii  inapotokea  wanaume  huogopa kumfuata  mwanamke  huyo  na  mwanamke  huyo  husalia  kuishi  maisha  hayo  ya  upweke  ya  bila  kuwa  na  mume  wala  mpenzi  katika  siku zote  za  maisha  yake.  Wapo  wanawake  wengi  tu  ambao  wamefungwa  kwenye  kifungo  hiki.

 Miaka  ya  tisini  alikuwepo  dada  mmoja  huko  Chalinze  ambae  uzuri  na urembo  wake  ulikuwa  sio  wa  kawaida. Dada  huyo  alitoka  katika  familia  ya  kawaida  na  alifanya  biashara  ya  kuuza  chakula.   Binti  huyu ‘aliua’ madereva  wengi sana  wa  malori  yaliyo  kuwa  yakitoka  Dar  kwenda  mikoani  na  nchi  jirani.  Kila  mwanaume  aliyejaribu  kufanya  mapenzi  na  dada  huyo  alifariki  dunia  baada  ya   wiki kadhaa. Hali  hii  ilizua  taharuki  sana  miongoni  mwa  madereva  hao  na  mwisho wa siku wote  walimuepuka  wakidhani amewekewa  tego.

MWISHO  WA  SEHEMU  YA  KWANZA. KATIKA  MAKALA  YANGU  YA  KESHO  NITAENDELEA  NA  SEHEMU  YA  PILI AMBAPO  NITAELEZEA  SABABU  NYINGINE  ZINAZO  WAFANYA   BAADHI YA  WANAWAKE  WAZURI  KUPITA  KIASI  WASIOLEWE.

MAKALA  HAYA  YAMESIMULIWA    NA  DOKTA. MUNGWA  KABILI. ANAPATIKANA  KWA  SIMU NAMBA  0744  - 000  473.

Waziri Mkuu kuwa mgeni rasmi kwenye mchezo wa tamasha la 'Simba Day'

$
0
0
Klabu ya soka ya Simba leo imemtangaza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa kuwa mgeni rasmi kwenye mchezo wa tamasha la 'Simba Day' dhidi ya Asante Kotoko ya Ghana Agosti 8, 2018.

Akiongea leo na wanahabari, msemaji wa timu hiyo Haji Manara, amethibitisha kuwa tayari Waziri mkuu ameshakubali ombi lao na kuahidi atakuwepo uwanjani kuwaongoza mashabiki wa Simba katika tamasha lao lenye shughuli mbalimbali ikiwemo kutambulishwa kwa wachezaji wapya.

''Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekubali ombi letu, na ninaomba nitangaze rasmi kuwa yeye ndio atakuwa mgeni rasmi kwenye tamasha letu la 'Simba Day' akiongoza shughuli zote ambazo zitafanyika siku hiyo'', - amesema.

Mbali na kumtangaza mgeni rasmi, Manara amewataka mashabiki wa timu hiyo kutojihusisha na masuala ya kugushi tiketi kwani wao kama klabu wamejidhatiti kuhakikisha watu wa aina hiyo hawapati mwanya ndio maana suala la usimamizi wa tiketi uwanjani wamelikabidhi kwa Suma JKT.

Aidha Manara amesema kikosi cha Simba kitatua nchini Jumatatu ya Agosti 6 kikitokea Uturuki ambako kimeweka kambi ya maandalizi ya msimu wa 2018/19. Pia siku hiyo Simba watatambulisha jezi zao mpya za nyumbani na ugenini msimu huu.

Bwege ataka akamatwe yeye badala ya Zitto

$
0
0
Mbunge wa Kilwa kusini –CUF Suleiman Bungara maarufu Bwege ameingilia ugomvi wa Zitto Kabwe na Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola kwa kumtaka Waziri huyo amkamate yeye kwanza kwa kuwa yeye ndiye alimuita Zitto kwenye mkutano wake.

Kauli hiyo ya Bwege imekuja baada ya waziri wa mambo ya ndani Kangi Lugola kumtaka mbunge wa Kigoma mjini Zitto Kabwe kujisalimisha polisi mwenyewe kwa  kosa la kutoa  kauli za kichochezi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika jimbo la Kilwa kusini mkoani Lindi.

" Mh Zitto mimi ndiye niliyemwandikia barua aje kwenye mkutano wangu, naona ni kukandamiza haki na uhuru wa wabunge siyo sahihi kumkamata Zitto Kabwe kwa sababu mimi ndiye niliyemuita kama kunikamata wanikamate mimi".

Amemtaka waziri wa mambo ya ndani ya nchi Kangi Lugola kujali na kufuata sheria za nchi katika utendaji kazi wake kwa kuwa Tanzania ni nchi ya demokrasia inaendeshwa kwa mujibu wa sheria na siyo kwa amri.

Bwege amesema Waziri Lugola ni mbunge aliyepata uwaziri, hivyo anamshauri kabla hajasema jambo lolote hadharani ni vema akawatumia wanasheria waliopo kwenye wizara yake kwa ajili ya kumshauri mambo muhimu ya kuongea hadharani badala ya  kuongea mambo ambayo kisheria hayapo.

Mbunge huyu ameongeza kuwa kwa upande wake amepigiwa simu na polisi mkoani Lindi wakimtaka kuripoti kituoni hapo na baada ya kufanya hivyo kutoka na maelezo yake amefunguliwa jalada la uchunguzi katika kesi ya uchochezi.

Aidha baada ya agizo la Waziri Kangi Lugola la kutaka Zitto Kabwe aripoti kituo cha polisi mkoani Lindi ndani ya siku mbili vinginevyo akamatwe popote alipo, jeshi la polisi kupitia kwa msemaji wake Barnabas Mwakalukwa lilitoa taarifa kuwa polisi wamefungua jalada la  uchunguzi dhidi ya kauli zilizotolewa na Mbunge Zitto Kabwe ambaye pia ni kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo.

Hata hivyo kupitia kwa  Katibu Kamati ya Uenezi na Mawasiliano  Ado Shaibu chama cha ACT Wazalendo kilitoa tamko rasmi kwamba baada ya kushauriana na wanasheria wa chama wamekubaliana kwamba kiongozi wao Zitto Kabwe hatakwenda kuripoti polisi kama waziri Lugola alivyoagiza kwa kuwa waziri huyo hana mamlaka kisheria ya kutoa agizo hilo na kwamba wenye mamlaka ni polisi.

Hata hivyo , hadi sasa Zitto hajaripoti kituo chochote cha polisi kama alivyotakiwa na waziri Lugola, kwa sasa anaendelea na mikutano yake ya kampeni za uchaguzi mdogo jimbo la Buyungu kama kawaida.

Jokate Mwegelo Aapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya....Tazama Picha

$
0
0
Mkuu mpya wa wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo ameapishwa leo huku akipewa onyo kuepuka wapotoshaji. Pamoja na Jokate, Zainab Kawawa naye ameapishwa kuwa mkuu wa wilaya ya Bagamoyo.

Jokate, ambaye aliwahi kuwa mlimbwende wa mashindano ya Miss Tanzania mwaka 2006, aliteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Kisarawe, Julai 28 mwaka huu.

Jokate ameapishwa leo Agosti 3 huku ndugu, jamaa, marafiki na viongozi wa CCM wakihudhuria hafla za uapisho huo.

Akizungumza mara baada ya wakuu hao wawili wa wilaya kuapishwa, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Pwani, Ramadhani Maneno amewataka wateule hao waepuke wanaofika ofisini kutaka kuwapotosha katika utendaji wao.

Amewataka wakakae na makatibu tawala ili wakusanye mapato kwani mkoa wa Pwani una  viwanda.

“Kwa nafasi mlizopata hakikisheni mnakua karibu na viongozi wa chama hilo ni jambo kubwa. Wakati sasa mnaenda kuripoti kwenye wilaya mkaanzie kwenye ofisi za chama,”amesema.

Ameongeza: "Huko mnapoenda mtafute desturi na mila za maeneo yenu msizipuuzie, lakini mtafute yale yanayoendana na nyaraka zilizopo.”

Amesema anawakabidhi vitu vitatu, macho, masikio na mdomo ambavyo vitawasaidia kwenye utendaji wao wa kazi.

Pamoja na kuwepo kwa idadi ndogo ya waliohudhuria sherehe hizo za uapisho, hakuna msanii hata mmoja aliyeonekana.

Wengi walitarajia kuona wasanii wakijitokeza kwa wingi katika sherehe hizo kwa kuwa Jokate ni msanii wa filamu, muziki na ni mwanamitindo.

Mzee Majuto Azidiwa Tena na Kulazwa ICU Muhimbili

$
0
0
Msanii maarufu wa maigizo Amri Athuman maarufu ‘King Majuto’ amelazwa chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum (ICU) katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa MNH Aminiel Aligaesha amesema Majuto aliletwa hospitalini hapo Jumanne wiki hii saa 12 jioni.

“Ni kweli yupo chumba cha wagonjwa mahututi, tunaye hapa,” amesema.

Ofisa Habari wa Chama cha Waigizaji Kinondoni Masoud Kaftany naye amethibitisha taarifa hizo.

“Tayari madaktari wameanza kufanya vipimo ili kubaini ugonjwa unaomsumbua,” amesema.

Hii ni mara ya pili kwa Mzee Majuto kulazwa MNH, mara ya kwanza alilazwa kabla ya kwenda India kwa upasuaji wa tezi dume.

Kauli ya Rais Magufuli Yamuumiza Kichwa Makonda

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam,  Paul Makonda ameitisha kikao na wakurugenzi wa manispaa zote za mkoa kwalengo la kupitia takwimu za mapato na matumizi ya mkoa huo ili kujiridhisha kwanini wameshuka kimapato na kuzidiwa na jiji la Dodoma ambalo limepandishwa hadhi hivi karibuni.

Makonda ametoa kauli hiyo leo Agosti 3, 2018 katika hafla ya kuwakaribisha wakuu wa wilaya wapya na kuwaaga waliohamishwa vituo vya kazi, ambapo amemtaka katibu tawala wa mkoa kuipanga upya Idara ya Ardhi kwani ni maeneo yenye uongo mwingi na imekuwa na viongozi ambao wanachukuwa nyaraka za wananchi na kisha kuwapelekea matajiri na kuwanyima haki wanyonge.

“Haiingii akilini Mkoa wa Dar es Salaam kushuka kimapato pamoja na kuzidiwa ukusanyaji kodi wakati ni mkoa wa kiuchumi, kuna nyumba na viwanja vya serikali ambavyo vimechukuliwa na watu binafsi, mikataba ya unyonyaji ambayo imesainiwa na inaiminya serikali”, amesema

Makonda ameongeza kuwa viongozi wengi wa Dar es Salaam wanatoa taarifa nyingi za uongozi juu ya utendaji na utekekezaji wa miradi na mfumo wa biashara pia uangaliwe ili kuiwezesha kuwepo kwa mfumo rahisi ambao unarahisisha huduma za kitengo cha biashara kwani kumekuwa na urasimu uliopitiliza.

“Katika suala la ulinzi na usalama, wanaendelea na kuweka Camera katika maeneo mbalimbali ya jiji na baada ya hapo tutaruhusu ufanyaji wa biashara kwa masaa24”, ameongeza Makonda.

Agosti 1, 2018 wakati akizungumza na wakuu wa mikoa baada ya kuwaapisha viongozi mbalimbali aliowateua, Rais Magufuli alisema kati ya majiji yote, Dodoma inaongoza kwa makusanyo ya mapato ya Shilingi bilioni 24.2 ikiwa ni asilimia 123 ya makisio yao ya Shilingi bilioni 19.

Amesema Jiji la Dar es Salaam ambalo ni kongwe kuliko yote lilikusanya pesa kidogo tofauti na ukubwa wake ambapo lilikusanya kiasi cha Sh15.3 bilioni, Arusha (Sh10.3 bilioni), Mwanza (Sh9.3bilioni), Tanga (Sh9.1bilioni) na Mbeya (Sh4.2bilioni).

Mizizi 29 Power ,ndio Dawa Bora Na Imara Kwa Sasa Kwa Kutibu Na Kuponesha Tataizo La Nguvu Za Kiume Kwa Dakika 30 Tu

$
0
0
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume limekuwa ni janga kubwa sana kwa sasa sio vijana au wazee wanalalamiki kukimbiwa na wa wapenzi wao au ndoa kuvunjika kutokana na mwanaume kulala na mwanamke kitanda kimoja hata wiki mbili bila kushiriki tendo la ndoa na hii ndio inachangia wanawake wengi kutoka nje ya ndoa kwa nini huteseke na wakati dawa zipo ambazo zitarudisha heshima yako ya ndoa 

MIZIZI 29 POWER; ni ambayo hutibu na kurudisha virutubisho mwilini ambavyo humfanya mwanaume awe na matatizo yafatayo 1 kuwahi kukojoa kabla mke au mpenzi wake

 2. kushindwa kurudia tendo dawa, hii itakufanya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 

3... dawa hii inatibu uume uliolegea na kusinyaa 

4. dawa hii inatoa miungurumo ya tumbo na uchovu wakati wa kumaliza tendo 

NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupiga punyeto kwa mda mrefu 
2 upungufu wa vichochoe mwilini 
3 magonjwa ya moyo, kisukari, presha, vidonda vya tumbo kiuno na mgongo 
4 utumiaji ovyo wa madawa ya kizungu 
4 usongo wa mawazo, hasira, tumbo kujaa gesi na kutopata choo.

 PATA TIBA YANGU NA NI TOFAUTI NA ULIZO WAHI KUTUMIA: 

Je una uume mfupi na mwembamba? MASHESHA MIX ni dawa ya kuboresha uume saiz upendayo asa kwa wale waliofanyiwa tohara wakiwa wadogo.. chagua saizi upendayo inch 5,6,7, adi 8 iyo ni kwa urefu na unene sentimita 2,3,4, adi 5 .dawa hizi zipo za kupaka na kunywa na hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ,

Tunatibu kisukari,vidonda vya tumbo,ngiri, korodani iliyovimba, kupnguza kitambi, maziwa makubwa NK 

KWA TIBA NA USHAULI FIKA OFISINI KWANGU DARE S SALAAMU MBAGALA ZAKHEMU NA MIKOA YA KANDA YA ZIWA YUPO WAKALA WETU HAPO MWANZA NA KWA AMBAO HAWANA NAFASI YA KUJA OFISINI HUDUMA YETU UTALETEWA POPOTE ULIPO PIGA SIMU 0783185060 DR MAKOYE

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,

Wolper: Siwezi kudanga na siku nikikamata mmoja ni mimba tu

$
0
0
Msanii wa Filamu Bongo, Jackline Wolper amesema kitu ambacho hawezi kufanya ni kudanga. Wolper amefunguka hayo wakati akimjibu shabiki yake katika mtandao wa Instagram kufuatia mrembo huyo kuposti picha ya Rais wa Kenya na kuandika; My second home.
 
Sasa shabiki huyo alitupia comment yake kwenye post hiyo ambayo ilisomeka; "Siku Wakenya Watakukata ki******m ndo utajua ni second home au ni neighbor country we endeleaa tu kudangaaaa kwa waikikuyu"

Naye Jackline Wolper akajibu; "Siwezi kudanga na siku nikikamata mmoja ni mimba tu usijali, halafu kasome ujue maana ya kudanga.. na me kudanga siwezi, wanadanga watoto, am sorry".

Jackiline Wolper amekuwa nafari za mara kwa mara nchini Kenya kutokana na biashara zake hasa ile ya ushonaji kupitia duka lake la House of Stylish.

Dr Kanengo: Bingwa Wa Tiba Asili Hutibu Matatizo Yafuatayo

$
0
0
NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo kupooza kupoteza fahamu 

MALABALA; hutibu kisukari , uti wa mgogo, Change, pumu, busha, kaswende, kifua kikuu, muwasho sehemu ya siri 

NKURUNGU,: Ni dawa kutibu  N, B, G, POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge 20 

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha , pia kuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe), maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu. 

NR SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Kuisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu 

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana. (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete) ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,.(4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wachafu ndani ya mji,.

Haya yote yanawezekana kwa DR KANENGO popote ulipo . Muone  DR KANENGO,anatibu nguvu za kiume anarefusha na kunenepesha uume kwa saizi uipendayo kwa muda mfupi sana, pamoja na kuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa mara 4 bila hamu kuisha Na utachelewa kufika kileleni kwa muda wa dakika 40 bila kuchoka .

Angalizo usitume meseji wala kubipu..
 
You can get it in all East African countries,,our service is fast and easy... contact Whatsapp 0784,47,59,46.Dar es salaam Tanzania. ,..Dr. KANENGO 0744,92,29,82...You are welcome.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya TWAWEZA Adai Kunyang'anywa Paspoti

$
0
0
Idara ya Uhamiaji inadaiwa kuishikilia pasipoti ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Twaweza, Aidan Eyakuze.

Pamoja na hatua hiyo, Eyakuze amewaambia waandishi wa habari leo Agosti 3 kwamba suala hilo halitawayumbisha, bali taasisi hiyo itaendelea na kazi zake kama kawaida.

"Niliombwa nifike Uhamiaji na kupeleka pasi, nikatekeleza, lakini mpaka leo sijapata maelezo wala barua ya kwa nini washikilie pasi yangu," amesema Eyakuze.

Amesema baada ya pasi ya kusafiria kushikiliwa, aliomba pasi ya muda kwa ajili ya safari ya kwenda Nairobi kikazi lakini pia alinyimwa, "Hatujapata taarifa ya kuwepo kwa kesi mahakamani," ameongeza.

Amesema walipokea barua mbili zikihoji kwa nini wasichukuliwe hatua na wakazijibu.

Ingawa hakutaka kuingia undani wa baru hizo, Julai 5, Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech), iliiandikia barua Twaweza ikiitaka itoe maelezo ndani ya siku saba kuhusu utafiti iliofanya wa Sauti za Wananchi bila ya kibali. Utafiti huo pamoja na mambo mengine umeonesha kushuka kwa uungaji mkono wa wananchi kwa wawakilishi na viongozi waliowachagua.

"Hatutishiki kwa kuitwa na kuhojiwa na Serikali lakini tunadhani ni haki yao kuhoji na sisi kama wajibu wetu kuwajibu. Kwa sababu sheria inaeleza wazi ni tafiti tunazofanya,” amesema.

Msemaji wa Idara ya Uhamiaji, Ally Mtanda amesema hana taarifa ya kushikiliwa kwa pasi ya kusafiria ya Eyakuze.

"Bado sijapata hizo taarifa, niko nje ya Dar es salaam, nikirudi nitaifanyia kazi," amesema.

Waziri Mkuu: Tanzania Kuendeleza Ushirikiano Na Kuwait

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Tanzania itaendeleza ushirikiano na Serikali ya Kuwait katika sekta mbalimbali ikiwemo ya usafiri wa anga.

Ameyasema hayo leo (Ijumaa, Agosti 3, 2018) wakati alipokutana na Balozi wa Kuwait nchini, Balozi Jasem Al Najemkatikamakazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Balozi Al Najem ambaye anamaliza muda wake, amekutana na Waziri Mkuu kwa lengo la kumuaga na kwamba leo anatarajia kuondoka nchini na kurejea Kuwait.

Waziri Mkuu amemshukuru balozi huyo kwa ushirikiano alioutoa Tanzania katika kipindi chote cha uwakilishi wake na kwamba nchi hizo zinatarajia kuanza ushirikiano katika usafiri wa anga.

Amesema Kuwait ni moja kati ya nchi rafiki, ambayo imeshirikiana na Tanzania katika uboreshaji wa shughuli za maendeleo kupitia Balozi Najem, hivyo wataendelea kumkumbuka.

“Balozi Najem amejitoa sana katika kuwasaidia Watanzania hususan kwenye miradi ya huduma za jamii kwa kupeleka maji mashuleni, vituo vya afya, zahanati na hospitalini,”.

“Pia Ubalozi wa Kuwait umesaidia kuleta vifaa tiba katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete na madaktari katika baadhi ya hospitali nchini. Ushirikiano huu umeleta tija sana,” amesema.

Waziri Mkuu amesema mbali na miradi hiyo ya huduma za jamii, pia balozi huyo ameshiriki kuendeleza Sekta ya utalii nchini kwa kuleta watalii wengi kutoka nchini Kuwait kuja Tanzania.

Waziri Mkuu meongeza kuwa Balozi Al Najem ameshiriki kikamilifu katika kuratibu shugughuli zote za maendeleo kati ya nchi hizo mbili ikiwa ni pamoja na kuunganisha sekta binafsi.

Kadhalika, Waziri Mkuu amemuhakikisha balozi huyo kwamba Tanzania itaendelea kuimarisha ushirikiano wake na Kuwait na kwamba ipo tayari kumpokea mwakilishi mwingine.

Kwa upande wake, Balozi Al Najem ametumia fursa hiyo kuishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano iliyompa katika kipindi chote alichokuwa akiiwakisha Serikali ya Kuwait nchini.

Amesema tangu alipowasili nchini amekuwa akipewa ushirikiano mkubwa na viongozi wote wa Serikali jambo lililomrahisishia utekelezaji wa majukumu yake nchini.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya Agosti 4

Rais Magufuli ampongeza Mnangagwa kwa Kuchaguliwa kuwa Rais wa Zimbabwe

$
0
0
 Rais John Magufuli amempongeza rais mteule wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa kwa kuchaguliwa kuliongoza Taifa hilo katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika takribani siku nne zilizopita.

Mnangagwa ameshinda uchaguzi huo baada ya kujikusanyia asilimia 50.8 ya kura huku Nelson Chamisa wa Muungano wa chama kikuu cha upinzani (MDC) akipata asilimia 44.3.

Katika ujumbe alioutuma kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter, Rais Magufuli amesema ushindi huo ni dalili ya imani ya watu wa Zimbabwe kwake.

“Kwa niaba ya Serikali na Tanzania nakutumia salamu za pongezi kwa ushindi wako katika nafasi ya urais. Ushindi wako unaonyesha imani iliyopo kwa watu wa Zimbabwe katika kuwaongoza kwenye mafanikio,” amesema Rais Magufuli.

Hata hivyo, MDC  umeyakataa matokeo ya uchaguzi huo yaliyompa ushindi Mnangagwa wa chama tawala cha Zanu PF.

Hata kabla ya Tume ya Uchaguzi Zimbabwe kuthibitisha matokeo, maofisa waandamizi wa MDC Morgan Komichi na Nkululeko Sibanda ambaye ni msemaji wa Chamisa waliingia kwenye ukumbi wa kutangazia matokeo na kuyakataa.

Komichi amesema matokeo yanayotangazwa ni ulaghai mkubwa akiongeza hawakutia saini kabla ya kukamatwa na polisi na kutolewa nje.

Watekaji wawili wakamatwa na Polisi Dar

$
0
0
Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam inawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kuteka watu na kudai fedha kiasi cha Sh60 milioni kwa ndugu wa waliotekwa.

Watuhumiwa ni Mkazi wa Kimara Mwisho Hussein Shilingi (30) na mkazi wa Tabata Martine Pumba(35).

Watuhumiwa wote walikamatwa Julai 26 mwaka huu maeneo ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wakitumia gari aina ya Toyota Land Cruiser yenye namba ya Umoja wa Mataifa (UN) huku wakiwa na watu watano waliowateka.

Kamanda wa Polisi kanda hiyo Lazaro Mambosasa akizungumza jana Agosti 3 amesema baada ya kufanya upekuzi ndani ya gari hilo walifanikiwa kukamata vifaa mbalimbali vilivyokuwa vikitumiwa na wahalifu hao ikiwamo namba za magari za mashirika ya serikali, Umoja wa Mataifa na namba za binafsi.

Mambosasa amesema baada ya kuhojiwa, waliotekwa walisema walitekwa kuanzia 23 Julai hadi 25 mwaka huu.

Amesema walitakiwa kutoa Sh60milioni ambapo watekaji hao walikuwa wanatumia mbinu ya kupiga simu kwa ndugu waliotekwa na kudai fedha hizo ili wawaachie huru.

“Hawa watekaji walikuwa wanatumia gari moja lakini walikuwa wanabadilisha namba tofauti za magari kama za serikali, ubalozi na za umoja wa kimataifa ili mtu usiweze kuwagundua na pia walikuwa wanatembea na matunguli wakiamini hawakamatwi lakini wajue Serikali hailogwi hata siku moja na tunaendelea kumtafuta mganga wao wa kienyeji,”amesema Mambosasa.

Mambosasa amesema vitu vingine walivyokamata ni kitambulisho cha kugushi chenye nembo ya polisi chenye jina la Martin Pumba simu za mkononi, silaha ikiwamo panga, nondo sime na maganda matatu ya risasi yanayodhaniwa kuwa ni ya bunduki aina ya SMG.

Amesema jeshi la polisi kanda hiyo linaendelea na mahojiano na watuhumiwa ili kubaini wanaoshirikiana nao na watafikishwa mahakamani ili kujibu tuhuma zinazowakabili.

Wakati huo huo aliwaagiza makamanda wa polisi mikoa mitatu ya jiji la Dar es Salaam waimarishe doria ili kuhakikisha wananchi wake wanakuwa salama.

Hayo yamekuja baada ya wananchi wa eneo la Mabibo na Mtongani wakiwalalamika askari polisi wa eneo husika kutochukua hatua ya kuwakamata vibaka wanaoiba maeneo hayo.

Mambosasa amesema atafuatilia maeneo yaliyolalamikiwa na wananchi hao na atakapobaini kuna uzembe atawachukulia hatua za kisheria askari polisi wa eneo husika.

Waziri Wa Kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba Azindua Maadhimisho Ya Sikukuu Ya Wakulima Nanenane Kitaifa Mkoani Simiyu

$
0
0
Na Mathias Canal, WK-Simiyu
Waziri wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba, jana 3 Agosti 2018 amezindua maadhimisho ya 25 ya Nanenane kwa mwaka 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi, Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu huku akitoa wito kwa wananchi wote wa mikoa  inayounda kanda ya Ziwa Mashariki ambayo inayojumuisha mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga kutumia fursa ya kutembelea katika maonesho hayo ili kujifunza mbinu mbalimbali za kitaalamu katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi.

Akizungumza na mamia ya wananchi waliojitokeza kwenye uzinduzi wa maonesho hayo Dkt Tizeba aliwasihi wananchi wote kutumia fursa ya maonesho hayo kwa kuwatumia ipasavyo wataalamu ambao watakuwepo katika viwanja hivyo kwa siku zote za maonesho hayo ili kupata ushauri na maelekezo ya kuboresha shughuli zao za kiuchumi kupitia Kilimo, Ufugaji, Uvuvi na Ushirika.

Alisema kuwa wananchi wanapaswa kutembelea katika maonesho hayo kwa lengo la kujifunza ili kuwa tayari kuanza kutumia teknolojia na maarifa watakayopata kwa lengo la kujiletea mapinduzi halisi katika kilimo, mifugo na uvuvi.

Mhe waziri Tizeba alisema kuwa sekta ya kilimo nchini itaendelea kuwa sekta muhimu katika maendeleo ya uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla hususani katika wakati huu ambapo serikali imejidhatiti kufikia uchumi wa viwanda. Alisema sekta ya kilimo imeendelea kuimarika kwa kuchangia Pato la Taifa hadi asilimia 30.1 kwa mwaka 2017 ikilinganishwa na asilimia 29.2 mwaka 2016.

Sambamba na hayo Mhe Tizeba alisema kuwa ushirika ni sekta mtambuka inayohusisha sekta mbalimbali zikiwemo Kilimo, Ufugaji, Uvuvi, Madini, Viwand, Nyumba na Fedha (Ushirika wa Akiba, Mikopo na Benki) ambazo zinagusa wananchi wengi zaidi.

Alisema kutokana na umuhimu wa sekta hiyo, Wizara kupitia Tume ya maendeleo ya ushirika imeendelea kuwezesha na kuimarisha ushirika ili wananchi waweze kunufaika na fursa zinazopatikana katika ushirika kwa lengo la kuchangia katika kuongeza kipato kwa wananchi wengi hususani waliopo vijijini.

Alisema katika mwaka 2017/2018, Tume imefanya uhamasishaji wa wananchi kujiunga au kuanzisha vyama vya ushirika ambapo hadi kufikia Disemba 2017 vyama vipya 394 vilisajiliwa na kufanya idadi ya vyama vya ushirika kufikia 10,990 kutoka 10,596 vilivyokuwepo Machi 2017.

Alisema vyama hivyo vinakadiriwa kutoa ajira mpya kwa wananchi takribani 1,182 huku katika kipindi cha mwaka 2017/2018 wanachama wapya 385,295 walijiunga au kuanzisha vyama vya ushirika na kufanya idadi ya wanachama kuongezeka kutoka 2,234,016 hadi kufikia 2,619,311

Kilele cha maadhimisho ya 25 ya Nanenane kwa mwaka 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi, Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu ni Tarehe 8 Agosti 2018 ambapo Rais Mstaafu wa awamu ya tatu nchini Tanzania Mhe Benjamin Willium Mkapa atakuwa mgeni rasmi akimuwakilisha Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.

Mgodi Wa Bulyanhulu Hatarini Kufungwa Endapo Watashindwa Kutekeleza Hukumu Ya Mahakama Kuu Shinyanga ya Kulipa Bilioni 3.1

$
0
0
Mahakama  Kuu Kanda ya Shinyanga, imetoa siku saba kwa uongozi wa kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu mgodi wa Bulyanhulu Gold Mine, ulioko Msalala wilayani Kahama, kulipa Sh. bilioni 3.1 inazodaiwa na wafanyakazi 17 ambao waliofukuzwa  kazi.

Naibu Msajili wa Mahakama hiyo, Eugenia Rujwahuka, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa Mahakama imetoa muda huo kuanzia Julai 31 hadi keshokutwa  fedha hizo ziwe zimeshalipwa. Alisema iweapo kampuni hiyo itashindwa kutekeleza amri hiyo, mahakama itaishikilia akaunti ya mgodi huo.

Alisema kesi hiyo ilifunguliwa na wafanyakazi wa mgodi huo tangu mwaka (2007) kupitia Mahakama Kuu Kanda ya Tabora  na kisha kuhamishiwa Mahakama Kuu Kanda ya Shinyanga miaka 10 iliyopita.

Rujwahuka alisema wametoa muda huo kabla hawajaishikilia akaunti ya mgodi au kusitisha shughuli za uchimbaji wa madini mpaka fedha hizo zitakapolipwa.

"Fedha hizi tumeelekeza zilipwe kwenye akaunti ya Mahakama inayosimamiwa na Benki Kuu ya Tanzania na  sisi tutawapatia wahusika. 

"Mgodi usipofanya hivyo ndani ya siku hizo saba, itatulazimu kuishikilia akaunti yao na kama hakutakuwa na fedha hizo Sh. bilioni 3.1 itabidi tusitishe shughuli zote za mgodi," alisema Rujwahuka.

Aliongeza kuwa: "Nashauri waajiri pale wanapowaachisha kazi wafanyakazi wawe wanawapatia stahiki zao kwa sababu ni haki yao na waachane na tabia ya kuanza kupelekana mahakamani na kuongeza utitiri wa kesi ambazo zingine wangeweza kumalizana wenyewe."

Kesi hiyo ya madai ilifunguliwa na wafanyakazi 1,511 waliokuwa wanafanya kazi ndani ya mgodi huo, lakini baada ya kuchukua muda mrefu kwa kampuni hiyo pale inaposhindwa kukata rufani, ndipo wengine 1,494 wakakata tamaa na kubaki 17 ambao waliifufua na kuendelea nayo.

Mrema Adai Kuna Wabunge Hatari CCM, Wanamchonganisha Rais Kwa Wananchi

$
0
0
Mwenyekiti wa TLP, Augustino Mrema amemtaka waziri wa mambo ndani, Kangi Lugola kuwachukulia hatua wabunge wanaomchafua Rais John Magufuli.

Amesema kuna vikundi vya wabunge ambao wanatengeneza chokochoko dhidi ya Rais na kwamba hatua zichukuliwe kabla hawajatimiza azma yao mbaya dhidi yake.

Akizungumza na waandishi wa habari jana  Agosti 3 katika ofisi za chama hicho zilizopo Magomeni, Dar es Salaam, Mrema amesema wabunge hao ambao baadhi ni wanachama wa CCM wanahatarisha usalama wa Rais kwa kumchonganisha na wananchi.

Mrema ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani katika serikali ya awamu ya pili amesema anawafahamu wabunge hao licha ya kutowataja majina yao.

Ameahidi kumpa ushirikiano Waziri Lugola endapo atahitaji kwa kuwa anafahamu mambo hayo kiundani.

"Mimi nimewasikiliza wabunge tena wa CCM kwa mfano waliosema Rais amechukua Trilioni 1.5 ni kweli au ni kumchafua? Kwa hiyo kuna hiyo tabia imezuka ya kumzulia Rais maneno ya uongo na ya kumdhoofisha,"alisema.

Alisema vikundi hivyo nimekuwa vikitengeneza "chokochoko" ambazo zinalenga kumchonganisha Rais na wananchi.

"Wabunge hao nawafahamu na niko tayari kuwataja kabla hawajatimiza uovu kama ilivyokuwa kwangu,"amesema.

Alieleza kuwa atakuwa mstari wa mbele kuhakikisha Rais anaheshimiwa na kuungwa mkono kwa sababu kazi aliyonayo ni kubwa.

Pia amemshauri Rais Magufuli kuwa makini na viongozi wake kwa kuwa wengi wanafanya mambo kwa kutafuta ‘kiki’ na huenda wakawa si rafiki katika kazi zake.

Waziri Kairuki: Leseni Za Madini Sasa Kutolewa Kwa Masharti Magumu

$
0
0
Na Asteria Muhozya, Simanjiro
Waziri wa Madini Angellah Kairuki amesema kuanzia sasa Serikali itaanza kutoa Leseni za madini biashara ya madini kwa masharti magumu huku ikimtaka kila mwombaji  kutoa taarifa za mauzo ya uzalishaji, usafirishaji pamoja na mnyororo mzima wa biashara ya madini ikiwemo fedha zinazoingia nchini kutokana na biashara hiyo.

Pia, ameiagiza Tume ya Madini kuchukua hatua stahiki kwa kuhakikisha kila jambo katika mnyororo huo linasimamiwa kikamilifu na kuongeza kuwa, yeye kama waziri mwenye dhamana atahakikisha anafuatilia kila hatua itakayochukuliwa  na tume hiyo.

“Tume ichukue hatua. Nitakuwa na ninyi. Msiache hata mmoja atakayekwenda kinyume na haya. Nilifanya hivyo katika Sekta ya Utumishi wa Umma hata huku kwenye sekta ya madini, sitashindwa kufanya hivyo,” alisisitiza Waziri Kairuki.

Waziri kairuki aliyasema hayo jana tarehe 3 Agosti, Wilayani Simanjiro Mkoa wa Manyara wakati akipokea taarifa ya Kamati Maalum iliyoundwa kuchunguza mnyororo wa madini ya vito nchini.

Kamati hiyo ilifanya kazi yake kwa muda wa siku 30  kuanzia tarehe 26 Aprili, 2018 kwa jukumu la kuchunguza  mnyororo wa madini ya vito kuanzia kuzalisha hadi usafirishaji nje ya nchi pamoja na kubaini sababu za utoroshaji wa madini na kupendekeza hatua za kuchukuliwa ili kuzuia utoroshaji.

Pia, aliiagiza tume ya madini kuanzia tarehe 4 Agosti, kuhakikisha inapata taarifa za uzalishaji za migodi yote inayozalisha huku akitaka migodi husika ieleze mahali inakouzia madini yao, anayeuziwa madini hayo na kuongeza kuwa, zoezi husika linawajumuisha pia dealers.

Waziri Kairuki alisema, wizara yake imeamua kusimamia suala husika ikiwa ni jitihada za kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli za kuhakikisha kuwa rasilimali madini zinawanufaisha watanzania wote.

“ Lazima watanzania tutambue kuwa madini haya yanamilikiwa na watanzania wote. Tunatakiwa kuyalinda kwa ajii ya maendeleo yetu na kwa manufaa ya vizazi vijavyo,” alisema Kairuki.

Akizungumzia biashara ya madini ya tanzanite katika ukuta unaozunguka migodi ya tanzanite mirerani, alisema hakuna serikali inayotaka watu wake wasifanye biashara, hivyo, lengo la ukuta huo ni kuhakikisha kwamba inadhibiti utoroshaji wa madini na kuweka mfumo mzuri ambao utawezesha madini hayo kuzinufaisha  pande zote.

Alisema tayari wizara imeandaa Kanuni za Mirerani (Mirerani Contolled Area) ambazo hivi sasa zinafanyiwa maboresho  baada ya kuwepo changamoto kadhaa katika utekelezaji wake.

Katika hatua nyingine, Waziri Kairuki alisema serikali imebaini  baadhi ya wenye leseni za ‘broker’ kukaribisha wageni kutoka nje kufanya biashara hiyo kinyume na taratibu na  hatimaye kusafirisha madini hayo, hivyo, aliwataka wote wanaofanya hivyo kuacha mara moja na kuwataka watanzania wote wenye taarifa kuhusu suala hilo kutoa taarifa  katika mamlaka zinazohusika.

“Kamati hii imefanya uzalendo na imefanya kazi kubwa sana. Nimeipokea taarifa ya kamati lakini natamani wangenitajia majina ya watoroshaji. Nilitamani sana kuona majina lakini naamini itaniuma sikio,” alisisitiza Waziri Kairuki.

Pia, aliongeza kuwa serikali itazifuta leseni za  uchimbaji madini kwa wale wote ambao wameshindwa kuyaendeleza maeneo yao na kupewa wengine wenye nia ya dhati ya kuendeleza shughuli za uchimbaji madini nchini.

Akizungumzia mkakati wa serikali katika kuhamasisha shughuli za uongezaji thamani nchini, alisema kuwa serikali inaendelea kukiimarisha kituo cha TGC kilichopo jijini Arusha, kwa kuongeza wataalam katika masuala ya ukataji na unga’rishaji wa madini ya vito.

“Tayari tumepata walimu  7 kutoka nchini India, lakini bado tunafuatilia wengine kutoka nchini Thailand,”alisema Kairuki.

Akiwasilisha  taarifa ya Kamati kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo,  Mratibu wa Kituo cha Jimolojia Tanzania (TGC), Eric Mpesa alisema Kamati husika ilipata fursa ya kutembelea mgodi wa Mundarara mpaka wa Namanga, Uwanja wa ndege wa KIA, Machimbo ya Tanzanite Mirerani, TGC, Ofisi ya Afisa Madini Mkazi Morogoro na Machimbo ya Epanko, Morogoro

Akiwasilisha mapendekezo ya kamati husika Mpesa alisema kuwa, kamati inapendekeza Serikali kutengeneza mpango wa makazi katika eneo lililozungushiwa ukuta wa Mirerani ikizingatia uwepo wa eneo la uchimbaji, biashara, uanzishwaji wa kituo cha One Stop Centre, huduma za kijamii, maegesho ya vyombo vya usafiri, maeneo ya starehe na maeneo ya utalii.

Pia, alisema serikali ihakikishe kuweka mfumo wa ulinzi katika eneo lililozungushiwa ukuta na pia ilishauri serikali kuongeza wataalam wa Wizara katika maeneo ya migodi ili kurahisisha ufanyaji biashara na kuwezesha kuzuia utoroshaji wa madini ya vito.

Pendekezo lingine ni serikali kuwawezesha wachimbaji wadogo kupata teknolojia za kisasa pamoja na tafiti za kijiolojia kufanywa na watalaam  kutoka Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kwa malipo ya gharama nafuu yatakayolipwa baada ya uzalishaji kupatikana.

Pia, Kamati ilipendekeza seriakali kuishawishi mifuko ya jamii isaidie wadau  kuanzisha benki ya Madini itakayowapa wachimbaji na wafanyabiashara mikopo yenye masharti nafuu.

Akizungumzia mcchango wa sekta ya madini, alisema sekta hiyo inachangia fedha za kigeni cha kiasi cha wastani wa dola za Marekani milioni 27.8 kwa mwaka isipokuwa almasi na kati ya hizo, asilimia 27.8 ni madini yaliyosanifiwa na kunga’rishwa na asilimia 71.3 ni madini ghafi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Manyara  Alexander Mnyeti alisema kwa muda mrefu serikali imekuwa ikichazewa kwa wadau katika migodi kutokulipa kodi stahiki za serikali.

Aliishauri wizara kufuta leseni za wale wote walioohodhi maeneo yao bila kuyafanyia kazi ili kuwezesha leseni husika kutumiwa na wengine wenye nia ya kuendeleza sekta ya madini.

Kuhusu suala la mikataba  ya ajira katika migodi hiyo aliishauri serikali na wadau kukaa pamoja na kujadili suala husika na kulitafutia ufumbuzi.

Kamati iliyoandaa taarifa husika ilikuwa na wajumbe 13 ikiongozwa na Mwenyekiti Sammy Mollel, Makamu Mwenyekiti Hamis Kim, Katibu Adam Rashid pamoja na wajumbe 10 na Sekretarieti.

Wajumbe wa Kamati hiyo walitoka TAMIDA, MAREMA, AREMA, RUVREMA, TAWOMA, BROKER pamoja na wajumbe kutoka Wizara ya Madini na TGC.

Breking News: Msafara Wa Waziri Kigwangala Wapata Ajali,mwandishi Afariki.

$
0
0
Na John Walter –Babati
Taarifa ambazo zimepatikana muda huu kutoka Magugu Babati mkoani Manyara  zinaeleza kuwa gari la Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla wakitokea Arusha kwenda Dodoma wamepata ajali mbaya na inaelezwa kuwa mwandishi wake amepoteza maisha pale pale.

Kamanda wa polisi mkoa wa  Manyara Agustino Senga amesema kuwa Dr.Kigwangala aliejeruhiwa  vibaya maeneo ya kifuani  na dereva wake wamelezwa katika kituo cha Afya Magugu kwa matibabu.

Taarifa za awali kutoka kwa kamanda wa polisi Agustino Senga  zinaeleza kuwa ajali hiyo imesababishwa na mnyama aliekuwa akivuka bara bara eneo la Magugu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images