Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Zao La Mchikichi Kumaliza Uhaba Wa Mafuta Nchini

0
0
SEKTA ya kilimo ni mhimili wa uchumi wa Taifa na inategemewa katika kuifikisha Tanzania kwenye uchumi wa kati ifikapo 2025, kupitia viwanda kwa sababu kilimo ndicho kitawezesha viwanda kwa kuvipatia malighafi.

Kutokana na umuhimu wa sekta hiyo katika kukuza uchumi wa nchini, serikali imekuwa ikifanya juhudi kubwa kuhakikisha inaiboresha ili iweze kuwa na tija na kufikia malengo iliyojiwekea.

Sekta hiyo mbali na kuwa mhimili wa uchumi wa Taifa, pia imekuwa ikichangia pato la mkulima mmoja mmoja, kaya na pia ni tegemeo la mapato ya fedha za ndani na za kigeni.

Kufuatia hali hiyo, Serikali imeweka msisitizo katika kusimamia mazao makuu matato ya biashara ambayo ni pamba, chai, kahawa, korosho na tumbaku ambayo uzalishaji wake umeonyesha tija.

Baada ya kupata mafanikio katika mazao hayo Serikali kwa sasa inaboresha kilimo cha mazao ya alizeti, ufuta, michikichi ili kuzalisha mafuta ya kula ya kutosha kwa kutumia mazao hayo na mbegu za pamba.

Itakumbukwa kwamba kila mwaka, Serikali inatumia sh. bilioni 600 kwa ajili ya kuagiza mafuta ghafi ya kula kutoka nje ili kukidhi mahitaji kwa kuwa kiwango kinachozalishwa nchini hakitoshi.

Katika kuhakikisha kuwa jambo hilo linafanikiwa Serikali ya awamu tano inayoongozwa na Rais Dk. John Magufuli imeamua kuanzisha kampeni ya kufufua zao la michikichi ili kuweza kuzalisha mafuta ya kutosha.

Akizindua kampeni hiyo mkoani Kigoma hivi karibuni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, amesema Serikali imedhamiria kumaliza tatizo la upatikanaji wa mafuta ya kula nchini kwa kufanya mageuzi makubwa katika zao la michikichi.

Uamuzi huo sasa umelifanya zao hilo kuwa la sita la biashara ambalo katika miaka ya l960 hadi 1970, mkoa wa Kigoma ulijipatia umaarufu kwa uzalishaji wa zao hilo.

Waziri Mkuu anasema kampeni ya kufufua zao la michikichi mkoani Kigoma inaenda sambamba na kuanzishwa kwa kituo cha utafiti wa zao hilo katika chuo cha Maendeleo ya Jamii cha Kihinga kilichopo wilayani Kigoma kwa kuwa ndiko zao la Michikichi linalimwa kwa wingi.

Anasema zao la mchikichiki ni muhimu katika ukuzaji wa uchumi wa nchini, hivyo ufufuaji wa zao hilo ni kichocheo cha viwanda kwa kuwa kutakuwa na uhakika wa upatikanaji wa malighafi na kuvutia wawekezaji.

Waziri Mkuu anabainisha kuwa licha ya kuwepo kwa michikichi mingi nchini lakini uzalishaji wake unafanyika kwa njia za kienyeji, hivyo Serikali imedhamiria kuboresha kilimo hicho kwa kutumia teknolojia ya kisasa ili liweze kuleta manufaa makubwa kwa Taifa na wakulima.

Anasema kuwa Serikali haiwezi ikaendelea kutumia fedha nyingi za kigeni kuagiza mafuta ya kula kutoka nje wakati uwezo wa kulima michikichi na kuzalisha mafuta ya mawese kwa wingi tunao.

Anasisitiza kwamba inawezekana kujitosheleza kwa mafuta ya kula kwa sababu Tanzania ina ardhi ya nzuri yenye rutuba na watu ambao kilimo ndiyo shughuli kubwa wanayoitegemea kujipatia kipato.

Waziri Mkuu anasema ili kufanikisha kampeni hiyo ni lazima  viongozi wa Serikali wabadilike na wawafuate wakulima kwenye maeneo ya vijijini wakawaelimishe na kuwashauri namna bora ya kulima zao hilo.

“Tunataka kufanya mageuzi makubwa ya zao la michikichi, tunataka tuzalishe mafuta ya kutosha kutokana na zao hili, hivyo tuanze kupanda michikichi mipya na kuiondoa ile ya zamani kwa awamu,”.

Kadhalika, Waziri Mkuu anasema Serikali inataka kuona mabadiliko ya zao hilo, hivyo amewaagiza Maafisa Ugani katika maeneo yote wanayolima michikichi wafualitie maendeleo ya zao hilo kwa ukaribu zaidi.

Waziri Mkuu amewataka wananchi wote wa mkoa wa  Kigoma pamoja na mikoa mingine inayolima michikichi, wahakikishe wanapanda michikichi kwa wingi kuanzia kwenye makazi yao na kwenye mashamba yote wanayolima mazao mengine ili kuongeza uzalishaji.

“Serikali imefanya maamuzi ya kumaliza tatizo la upatikanaji wa mafuta ya kula nchini, kila mmoja lazima awajibike katika kuinua zao la michikichi ili tuweze kuzalisha mafuta ya kutosha,” amesema.

Waziri Mkuu amesema Serikali itafuatilia kwa umakini kuhakikisha zao la michikichi linalimwa kwa wingi na kuleta tija kwa wananchi na Taifa kwa ujumla. “Tutumie zao hili kama fursa ya kujikwamua na umasikini pamoja na kumaliza changamoto ya upatikanaji wa mafuta nchini,”.

Pia amewaagiza Wakurugenzi wa halmashauri zote nchi kuhakikisha mashamba ya wananchi yanapimwa na wahusika kupewa hati ili ziwawezeshe kupata dhamana ya mikopo kwenye taasisi mbalimbali za kifedha na kuwekeza kwenye kilimo.

Waziri Mkuu anabainisha kuwa halmashauri zinazolima michikichi viongozi wake wanatakiwa kuanzisha vitalu vya miche ya zao hilo na watakaoshindwa kuanzisha vitalu hivyo pamoja na kuhamasisha kilimo cha michikichi kwenye maeneo yao wajitathimini mwenyewe.

Anaongeza kuwa kuanzia sasa mkoa huo uhakikishe miche ya michikichi inapandwa katika maeneo yote yakiwemo ya pembezoni mwa barabara, katika mashamba ya shule za msingi na sekondari, kambi ya JKT na kwenye magereza na kwenye makazi ya wananchi.

Hata hivyo Waziri Mkuu alitoa angalizo kwa wawekezaji watakaowekeza katika kilimo cha michikichi kutoanzisha migogoro na wananchi watakaowakuta katika maeneo yao na badala yake washirikiane nao vizuri kwa sababu migogoro haina tija kwao na kwa wananchi.

Waziri Mkuu anasema Serikali imeliteua Gereza la Kwitanga lililopo wilayani Kigoma kuwa kituo kikuu cha uzalishaji wa zao la michikichi nchini kwa kuwa tayari lilishaanza kujishughuliza na kilimo cha zao hilo.

Ameuagiza uongozi wa gereza hilo kuongeza nguvu katika uzalishaji wa michikichi kwa kupanua mashamba na kuongeza askari wenye ujuzi wa kilimo cha michikichi.

Kwa upande wake,Mkurugenzi Mtendaji wa Trade Mark East Africa, Bw. John Ulanga alisema walifanya utafiti kuhusu zao la michikichi na walibaini kuwa kuna soko kubwa la mafuta ya mawese ndani ya nchi yetu, pamoja na nchi za jirani ila uzalishaji wa mafuta hayo ndani ya nchi bado ni mdogo sana.

Alisema hali hiyo inachangiwa na kuwepo kwavikwazo vichache vinavyokwamisha ongezeko la uzalishaji wa ndani, ambavyo ni matumizi ya teknologia hafifu katika kilimo cha mchikichi, na ukamuaji  wa mafuta ya mawese.

Pia ukosefu wa miundombinu na usafiri, ukosefu wa maghala ya kukusanyia matunda ngazi ya wilaya, na badala yake mkulima mmoja mmoja anahangaika kupeleka kwa mteja hivyo kumuongezea gharama, ukubwa wa gharama za usafiri kutoka shambani mpaka sokoni.

Naye, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Bw. Josephat Faustine alisema kilimo cha zao la michikichi kina faida kubwa na kinawekezeka, hivyo wao wataanisha maeneo yote yanayofaa kuwekeza.

Pia Mkurugenzi huyo wa TADB alisema benki yao inauwezo wa kutoa mikopo ya mitaji kwa vituo vya uzalishaji mbegu za zao la michikichi na kumaliza changamoto ya upatikanaji wa mbegu, hivyo ni muhimu kwa wakala wa mbegu kuchangamkia fursa hiyo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
ALHAMISI, AGOSTI 2, 2018.

Mizizi 29 Power ,ndio Dawa Bora Na Imara Kwa Sasa Kwa Kutibu Na Kuponesha Tataizo La Nguvu Za Kiume Kwa Dakika 30 Tu

0
0
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume limekuwa ni janga kubwa sana kwa sasa sio vijana au wazee wanalalamiki kukimbiwa na wa wapenzi wao au ndoa kuvunjika kutokana na mwanaume kulala na mwanamke kitanda kimoja hata wiki mbili bila kushiriki tendo la ndoa na hii ndio inachangia wanawake wengi kutoka nje ya ndoa kwa nini huteseke na wakati dawa zipo ambazo zitarudisha heshima yako ya ndoa 

MIZIZI 29 POWER; ni ambayo hutibu na kurudisha virutubisho mwilini ambavyo humfanya mwanaume awe na matatizo yafatayo 1 kuwahi kukojoa kabla mke au mpenzi wake

 2. kushindwa kurudia tendo dawa, hii itakufanya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 

3... dawa hii inatibu uume uliolegea na kusinyaa 

4. dawa hii inatoa miungurumo ya tumbo na uchovu wakati wa kumaliza tendo 

NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupiga punyeto kwa mda mrefu 
2 upungufu wa vichochoe mwilini 
3 magonjwa ya moyo, kisukari, presha, vidonda vya tumbo kiuno na mgongo 
4 utumiaji ovyo wa madawa ya kizungu 
4 usongo wa mawazo, hasira, tumbo kujaa gesi na kutopata choo.

 PATA TIBA YANGU NA NI TOFAUTI NA ULIZO WAHI KUTUMIA: 

Je una uume mfupi na mwembamba? MASHESHA MIX ni dawa ya kuboresha uume saiz upendayo asa kwa wale waliofanyiwa tohara wakiwa wadogo.. chagua saizi upendayo inch 5,6,7, adi 8 iyo ni kwa urefu na unene sentimita 2,3,4, adi 5 .dawa hizi zipo za kupaka na kunywa na hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ,

Tunatibu kisukari,vidonda vya tumbo,ngiri, korodani iliyovimba, kupnguza kitambi, maziwa makubwa NK 

KWA TIBA NA USHAULI FIKA OFISINI KWANGU DARE S SALAAMU MBAGALA ZAKHEMU NA MIKOA YA KANDA YA ZIWA YUPO WAKALA WETU HAPO MWANZA NA KWA AMBAO HAWANA NAFASI YA KUJA OFISINI HUDUMA YETU UTALETEWA POPOTE ULIPO PIGA SIMU 0783185060 DR MAKOYE

Aliyetaka Kumhonga Waziri Lukuvi Milioni 90 Afikishwa Mahakamani

0
0
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)  imempandisha kizimbani Mkurugenzi wa Kampuni ya Kiluwa Steal Group. Co.ltd na Kiluwa Free Processing Zone, Mohamed Kiluwa (50) kwa tuhuma za kutoa rushwa ya Shilingi Milioni 90 kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi.

Mshtakiwa huyo amepandishwa kizimbani mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shaidi na kusomewa shtaka moja la kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Akisomewa shtaka hilo mbele ya Hakimu Shaidi, Wakili wa Serikali Mkuu kutoka TAKUKURU, Maghela Ndimbo amedai July 16,2018 kati ya saa 6 na 8 mchana mshtakiwa huyo akiwa Mkurugenzi wa kampuni hizo mbili alitoa rushwa ya Dola za kimarekani 40,000 sawa na Sh. Milioni 90 kwa Waziri Lukuvi.

Wakili Ndimbo amedai mshtakiwa huyo alitoa fedha hizo kwa lengo la kutowasilisha hati ya umiliki wa kiwanja namba 57 ‘Block B’ Kikongo na ‘Block D’ Disunyura kilichopo eneo la viwanda Kibaha mkoani Pwani.

Baada ya kusoma shtaka hilo, Wakili Ndimbo ameiomba mahakama kuwapangia tarehe ya kutajwa kwa shauri hiyo na kuongeza kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado unaendelea na hawana pingamizi kuhusiana na mshtakiwa huyo kupewa dhamana.

Naye Wakili Upande wa Utetezi Imani Madega amedai kuwa kwa kuwa upande wa mashtaka hauna pingamizi na dhamana dhidi ya mshtakiwa wanaiomba mahakama itoe dhamana kwa kuzingatia masharti.

Hakimu Shaidi amesema ili mshtakiwa huyo apate dhamana anatakiwa kuwa na wadhamini 2 na mmoja atoe fedha taslimu mahakamani hapo kiasi cha Sh. Milioni 45 na kama hana awasilishe hati ya mali isiyo hamishika yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha, Masharti ambayo upande wa utetezi uliyatekeleza na mshtakiwa akaachiwa kwa dhamana. Kesi hiyo imeahirishwa hadi August 15,2018.

Jokate Mwegelo Kuapishwa Kesho

0
0
Na Mwamvua Mwinyi,pwani
MKUU wa mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo August 3(ijumaa) mwaka huu ,anatarajia kuwaapisha viongozi wateule Jokate Mwegelo na Zainab Kawawa .
 
Akizungumzia juu ya hafla hiyo fupi ,Ndikilo alisema inatarajiwa kufanyika asubuhi katika viwanja vya ofisi ya mkuu wa mkoa huyo .

Alisema viongozi hao bado ni vijana ambao anaamini kwa kasi ya maendeleo ya kiuchumi ya awamu ya tano wilaya ya Kisarawe na Bagamoyo zitapiga hatua zaidi .
 
Alisema kikubwa ni kwenda pamoja na kuinua sekta ya viwanda na kuhimiza kilimo cha biashara cha korosho kwenye maeneo yao .
 
“Katika miaka ya 1995 zao la korosho lilikuwa juu wilaya ya Kisarawe ,hivyo endapo tutaendelea kulipa msukumo kwa kulifufua, itasaidia kuinua zao hilo tegemezi la kibiashara katika mkoa wa Pwani”alisema Ndikilo.
 
Hata hivyo Ndikilo alisema, mkoa huo unatekeleza vyema ujenzi wa viwanda na wawekezaji hivyo kutokana na uteuzi wa Rais Dk. John Magufuli anashukuru kuongezewa nguvu ya viongozi wengine ambao ni vijana katika wilaya hizo.
 
Mkuu huyo wa mkoa alieleza ,kwa upande wa Kisarawe pia lipo tatizo la maji ambapo juhudi kubwa zitatakiwa katika kusimamia mradi wa bilioni kumi ambao utatoa maji Mloganzila hadi Kisarawe.
 
” Jokate ni kijana mwenye kipaji ,alishapitia chipukizi ,umoja wa vijana na masuala mengine ya kimaendeleo ,naamini ataweza kukimbiza gurudumu la maendeleo kwa kusimamia kutatua changamoto zilizopo Kisarawe ikiwemo mkandarasi huyo wa mradi wa maji Mloganzila-Kisarawe”
 
Pamoja na hayo ,Ndikilo aliwataka wakuu wa wilaya mkoani hapo ,kuwatumikia wananchi ,kusimamia miradi ya maendeleo na mapato katika maeneo yao .
 
Alieleza kwa umoja wa wakuu wa wilaya ,watendaji ,chama cha Mapinduzi na kamati za ulinzi na usalama kwenye maeneo yao hakuna litakaloshindikana.
 
Wateule hao ni miongoni mwa waliteuliwa walioteuliwa na Rais Dk.John Magufuli Julai 28 mwaka huu .

Joseph Kasheku Msukuma Afunga Bara Bara Kwa Muda Babati.

0
0
Na John Walter- Babati
Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Kasheku ‘King Msukuma’ amemwakikishia mgombea udiwani wa chama cha Mapinduzi Nikodemus Bonifasi kuwa atashinda kwa kishindo katika uchaguzi wa Marudio utakaofanyika Agosti 12 mwaka huu.

Msukuma amemtabiria ushindi huo Mgombea huyo akiwa katika mkutano wa kampeni  kata ya Bagara mjini Babati uliofanyika mtaa wa Osterbay na kuhudhuriwa na Mamia ya wakazi wa Babati.

Huku msukuma akitumia zaidi ya dakika 45 kumnadi mgombea huyo maarufu kwa jina la Nyeusi aliongoza maandamano ya amani hadi ofisi za Ccm mtaa wa Osterbay kwa miguu na kuziba bara bara kwa muda huku wakiimba na kucheza nyimbo maarufu ya chama hicho ‘Ccm mbele kwa mbele.

Uchaguzi huu katika kata ya Bagara unakuja baada ya diwani wa Chadema Bwana Nyeusi ambaye ndiye mgombea wa Ccm kukihama cha hicho.

Kwa upande wa Chadema wamemsimamisha mwenyekiti wa mtaa wa Miomboni  Mathayo Zebedayo kugombea nafasi hiyo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Agosti 3

Jaji Kiongozi Apewa Ufafanuzi Jinsi Mfumo Wa ‘Video Conference’ Utakavyofungwa Na Utakavyofanya Kazi Mahakamani

0
0
Na Mary Gwera, Mahakama
Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi amewasihi Watumishi wa Mahakama kuwa na utayari katika matumizi ya mifumo mbalimbali ya Teknolojia inayoanzishwa Mahakamani ili kuendelea kuboresha  huduma ya utoaji haki nchini.

Aliyasema hayo Agosti 02, alipokuwa akiwasilishiwa mada juu ya mfumo wa ‘Video Conferencing’ utakavyofungwa na utakavyofanya kazi katika Mahakama husika iliyowasilishwa na Mkandarasi atakayefanya kazi  ya ufungaji wa mfumo wa ‘Video Conferencing’, Kampuni ya ‘Invention Technologies.’

“Mahakama yenyewe inatakiwa kuwa tayari kutumia mifumo mbalimbali inayowekwa ili hata Wadau wengine kama Magereza, Polisi waweze kwenda sambasamba na Mahakama katika kuboresha huduma ya utoaji haki,” alisisitiza Mhe. Feleshi.

Aidha Wajumbe wengine waliohudhuria katika kikao hicho, ambao ni Majaji wawili wa Mahakama Kuu, Msajili Mkuu-Mahakama ya Tanzania, Msajili Mahakama ya Rufani, Mkurugenzi wa TEHAMA-Mahakama, na Maafisa wengineo waliunga mkono juu ya Mahakama kuwa na mfumo huo na kumtaka Mkandarasi kutekeleza kazi hiyo kwa wakati kama alivyoahidi.

Kwa kuanzia mfumo wa ‘Video Conferencing’ utafungwa maeneo yafuatayo; Mahakama ya Rufani, Mahakama Kuu, Kanda ya Bukoba, Chuo cha Uongozi wa Mahakama (IJA) Lushoto na Gereza la Keko.

Aidha; Mkandarasi anayefanya kazi hii ameahidi kukamilisha kazi hii mwishoni mwa mwezi Oktoba, 2018.

Kwa sasa mfumo wa ‘Video conferencing’ Mahakamani umefungwa katika Kituo cha Mafunzo-Kisutu pamoja na Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya.

Mfumo wa ‘Video conference’ Mahakamani utasaidia na utakuwa ni chachu kubwa ya kuharakisha uendeshaji wa mashauri, kupunguza gharama za mashahidi watokao mbalina Mahakama husika na vilevile utasaidia hata katika kuendesha mafunzo mbalimbali ya Watumishi wa Mahakama katika vituo vyao vya kazi.

Mahakama ya Tanzania kupitia Mradi wa Maboresho ya huduma za Mahakama chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia inaendelea na miradi mbalimbali ya maboresho yote yakiwa na lengo la kuwapa wananchi huduma bora ya upatikanaji wa haki zao.

Jeshi La Polisi La Kamata Wahalifu 96 Na Silaha Mbili Katika Operesheni.

0
0
Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna Liberates Sabas amesema Jeshi la Polisi kwa sasa linaendesha Operesheni mkoani Mtwara kwa kushirikiana na Nchi ya Msumbiji ili kuwakabili wahalifu wanaokimbili nchini humu

Aidha  Jeshi la Polisi kupitia Operesheni Maalum inayoendelea mkoani Mtwara limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 96 kati yao 10 wamefikishwa mahakamani kwa kesi mbalimbali na  wengine 16 wamefikishwa katika idara ya Uhamiaji kwa makosa yanayohusu maswala ya uhamiaji, katika operesheni hiyo kumepatikana silaha mbili zilizokuwa zikitumiwa na wahalifu katika maeneo mbalimbali.

Aidha Afande Sabas amewashukuru wananchi wa Mkoa wa Mtwara kwa kuendelea kutoa ushirikiano mzuri ndani ya Jeshi la Polisi na kuwataka wananchi wote nchini kuendelea kutoa ushirikiano ili kutokomeza uhalifu nchini.

Mnangagwa ashinda urais nchini Zimbabwe

0
0
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa ameshinda uchaguzi wa urais nchini Zimbabwe kwa mujibu wa tume ya uchaguzi wa nchi hiyo.

Kwamujibu wa BBC katika majimbo yote 10 yalioyotangazwa, Mnangagwa ameshinda kwa asilimia 50.8 ya kura kwa asilimia 44.3 alizopata mgombea wa chama cha upinzani Nelson Chamise.

Polisi waliwaondoa upinzani wakati wa kutangazwa matokeo baada ya kukataa kuyakubali matokeo hayo.

Mwenyekiti wa chama cha MDC Alliance, Nelson Chamisa amesema kuhesabiwa kwa kura hakukufanyiwa uhakiki.

Kwa ushindi wa asilimia 50 wa Mnangagwa umesababisha aepuke kwenda duru ya pili ya uchaguzi dhidi ya Chamisa.

Rais Mnangagwa amesema katika ukurasa wake wa Twitter kuwa huu ni mwamzo mpya.

Bwana Chamisa amesisitiza kuwa ZANU-PF haikushinda uchaguzi huu, wanajaribu tuu kupitisha suala lisilo na ukweli, amesema pia watapambana na suala hilo.

Uchaguzi huu ulikuwa wa kwanza tangu kiongozi wa muda mrefu Robert Mugabe kung’atuliwa madarakani.

Muungano wa Ulaya umekosoa kuchelewa kutangazwa kwa matokeo ya urais .

Umesema kuwa ilibaini baadhi ya matatizo, ukiwemo upendeleo wa vyombo vya habari, vitisho kwa wapiga kura na kutokuwa na imani na tume ya uchaguzi , ukiongeza kuwa ”mazingira ya uchaguzi hayakuboreshwa na hivyo kusababisha kuwepo kwa hali ya kiwango kikubwa cha ukosefu wa uaminifu “.

Hii ni mara ya baada ya miaka 16 kwa serikali kuwaruhusu waangalizi wa uchaguzi kutoka Muungano wa Ulaya na Marekani kuchunguza uchaguzi

Kwa upande wa Muungano wa Afrika, mapema wiki hii umesema kuwa uchagauzi huo ulikuwa huru na wa haki , akiongezea kuwa unaadhimisha wakati muhimu wa mabadiliko ya kisiasa.

Ripoti ya awali kutoka waangalizi wa SADC inasema kuwa uchaguzi huo ulikuwa wa amani na ulifanyika kulingana na sheria.

Wawakilishi wake, waziri wa maswala ya kigeni nchini Angola Manuel Domingos Augusto ameutaja uchaguzi huo kuwa wa  kidemokrasia.

Hakimu Kesi ya Akina Mbowe Awaonya Kumpigia Simu Akiwa Nyumbani

0
0
Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu , Wilbard Mashauri ameonya tabia ya washtakiwa kumpigia simu kuhusu masuala ya kesi akiwa nyumbani.

Hakimu Mashauri ameyasema hayo  jana katika kesi ya kufanya maandamano yasiyo halali inayowakabili Viongozi 9 wa CHADEMA akiwemo Freeman Mbowe.

Hatua ya Hakimu Mashauri kutoa onyo hilo ni baada ya kumuhoji mdhamini wa mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko ambaye hakufika mahakamani kwa madai amepigiwa simu ya dharura kwenda shuleni kwa mwanaye nchini Kenya.

Hakimu Mashauri amesema kuna mshtakiwa alimpigia simu akiwa nyumbani, hivyo mdhamini anatakiwa kujua sababu ya mshtakiwa kutokuwa mahakamani.

“Ninapokuwa nyumbani mimi ni Mashauri, suala la kunipigia simu kuhusiana na mambo ya kesi siyo sahihi.” Hakimu Mashauri

“Mambo yanayohusu mahakamani yaishie mahakamani  na siyo nikiwa nyumbani kwenye masuala ya kifamilia,” alisema Mashauri.

Baada ya kueleza hayo aliahirisha kesi hiyo hadi August 6,2018.

Awali upande wa mashtaka kupitia Wakili Serikali Mkuu, Faraja Nchimbi ulidai kuwa shauri hilo limeitishwa kwa ajili ya usikilizwaji wa awali kutokana na Matiko kutokuwepo mahakamani wanaomba ahirisho.

Kwa upande wa Wakili Kibatala alidai mshtakiwa Matiko hayupo alipigiwa simu ya dharura kwenda Kenya shuleni kwa mwanae.

Mbali na Mbowe, washtakiwa wengine kwenye kesi hiyo ni Katibu mkuu wa CHADEMA, Dk. Vincent Mashinji, Mbunge wa Iringa Mjini Msigwa, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu na Naibu katibu Mkuu bara na Mbunge wa Kibamba, John Mnyika, Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Mbunge wa Kawe Halima Mdee na Mbunge wa Bunda, Esther Bulaya.

Miongoni mwa mashtaka  yanayomkabili washitakiwa hao ni kula njama kwa nia ya kutenda kosa, kufanya mkusanyiko usio halali, kufanya mkusanyiko wenye ghasia na kukiuka tamko la kutawanyika na kuendeleza mkusanyiko wenye ghasia.

Washtakiwa hao wanadaiwa kati ya Februari mosi na 16, mwaka huu, Dar es Salaam kwa pamoja na ujumla wao walikula njama ya kutenda makosa ya kufanya mkusanyiko usiohalali, mkusanyiko wenye ghasia na kukiuka tamko la kutawanyika.

Mbowe na wenzake pia wanadaiwa Februari 16, mwaka huu, katika viwanja vya Buibui na barabara ya Mwananyamala na Kawawa, Kinondoni, wakiwa wamekusanyika kwa nia ya kutekeleza azma ya pamoja ya kuandamana hivyo kuwatia hofu wananchi kwamba kutakuwa na uvunjifu wa amani.

Pia wanadaiwa wakiwa na wenzao 12 ambao hawapo mahakamani siku hiyo waliandamana isivyo halali wakiwa na lengo la kuvamia ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni na kutokana na mkusanyiko huo wa ghasia walisababisha kifo cha Akwilina Akwiline na majeraha kwa  askari H. 7856PC Fikiri na E6976 CPL Rahim Msangi.

Aua mke kwa shoka, ajinyongakwa kamba kisa wivu wa mapenzi

0
0
Mwanamke  mkazi Njage wilayani Kilombero Mkoa wa Morogoro, ameuawa kwa kukatwa kwa shoka kichwani na mumewe kwa kilichoelezwa kuwa ni wivu wa mapenzi.

Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Willibrod Mutafungwa, alisema hayo jana na kufafanua kuwa tukio hilo lilitokea Julai 28 majira ya asubuhi ambapo mwanamke huyo, Rose Mngwe (43), aliuawa na mumewe, Jacob Kambo (45), mkazi wa Kijiji cha Njage.

Kwa mujibu wa Kamanda Mutafungwa, mwanaume huyo baada ya kumuua mkewe kwa kumkata kwa shoka kichwani, alikimbilia porini na kujinyonga kwenye mti kwa kutumia kamba.

Kamanda Mutafungwa alisema inadaiwa kuwa mwanaume huyo aliamua kufanya kitendo hicho baada ya kuona mkewe amempuuza alipomwambia kuwaondoa watoto wake wa kike aliowazaa nje ya ndoa.

Kamanda alifafanua kuwa alitaka waende kwa waliomzalisha watoto hao kwa madai kuwa wanawanyima nafasi wakiwa hapo.

Alisema miili ya marehemu hao imeshakabidhiwa kwa ndugu zao kwa ajili ya kuendelea na shughuli za mazishi.

Katika tukio lingine, Leo Charles Mashaka (61), mkazi wa Kitongoji cha Igagafu wilayani Kilosa, ameuawa kwa kupigwa na kitu chenye butu kichwani na usoni na mtoto wake wa kumzaa, Emmanuel Leo Charles, sababu ikitajwa ni kudai urithi.

Kamanda Mutafungwa alisema tukio hilo lilitokea Julai 30, alfajiri katika Kata ya Lumuma Tarafa ya Idete ambapo Mashaka alimpigwa na kitu chenye butu kichwani na usoni upande wa kulia na kumsababishia jeraha na michubuko mgongoni.

Alisema tukio hilo lilisababishwa na mgogoro katika familia kuhusu urithi.

Kamanda huyo alisema mtuhumiwa alikamatwa na atafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika.

Katibu Mkuu Hazina Awafunda Mameja Wa TRA Nchini

0
0
Serikali  imeiagiza Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), kuhakikisha inakuwa na uhusiano mwema na walipakodi ili kuondoka dhana iliyojengeka kuwa mamlaka hiyo inatumia nguvu na vitisho katika kudai kodi.

Agizo hilo lilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James, wakati wa mkutano wa maofisa wa TRA wa nchini.

"Mchukue hatua za makusudi kuboresha uhusiano kati yenu na walipa kodi ili kuondoa dhana iliyojengeka kuwa Mamlaka ya Mapato TRA inatumia nguvu na vitisho katika kudai kodi, " alisema James.

James alisema majadiliano ni jambo muhimu katika kujenga uhusiano bora wa kufanya biashara na kuimarisha ulipaji kodi kwa hiyari.

Akifafanua alisema Sh. trilioni 20.15 ni mapato ya ndani kutoka Serikali Kuu na Sh. trilioni 18 yanayotokana na kodi ambayo inatakiwa ikusanywe na TRA.

Alisema wizara, idara, taasisi na mashirika ya Umma, yanatarajia kukusanya Sh. trilioni 2.15.

Alisema katika mwaka huu wa fedha 2018/2019 sera ya mapato inalenga kuongeza wigo wa kodi, kuimarisha usimamizi wa vyanzo vilivyopo hususani katika matumizi ya mfumo wa kieletroniki na hatua nyingine za kiutawala.

Alisema kuwa serikali inaendelea na uunganishaji wa wizara, Idara, wakala, taasisi na mashirika ya umma kwenye mfumo wa serikali wa kieletroniki wa ukusanyaji mapato ili kuboresha ukusanyaji na udhibiti wa upotevu wa mapato ya serikali.

Aidha, alisema madhumuni ya mkutano huo ni kujadili namna ya utekelezaji wa bajeti ya serikali ya mwaka 2018/2019 pamoja na kuweka mipango madhubuti ya namna ya kufikia malengo hayo.

Alisema mkutano huo pia unatoa fursa kwa washiriki wote wanaohusika katika ukusanyaji wa kodi kujadili changamoto mbalimbali zilizopo na kuzitafutia ufumbuzi kwa lengo la kuimarisha ukusanyaji wa mapato na kufikia lengo la mwaka huu la Sh. trilioni 18 ifikapo Juni mwaka 2019.

"Matumaini yangu ni kwamba tutafikia malengo na kuvuka kwa kuwa masuala mengi ya kisera na utendaji yatajitokeza kwenye majadiliano yetu," alisema James.

Wajumbe wa Menejimenti wa Wizara ya Fedha na Mipango, wakiwa pamoja na Viongozi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, kujadili namna ya kuhakikisha kuwa zaidi ya shilingi trilioni 18 kati ya shilingi trilioni 32.47 zilizopitishwa na Bunge kwa ajili ya Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2018/2019 zinazotakiwa kukusanywa na Mamlaka hiyo zinapatikana kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo.

Bodi ya Mikopo Yasema Wanafunzi 17,000 Kati ya Wote Waliotuma Maombi Hawajakidhi Vigezo vya Kupatiwa Mikopo

0
0
Imeelezwa kuwa zaidi ya wanafunzi 17,303 hawajakidhi vigezo vya kupatiwa mikopo ya elimu ya juu na Bodi ya Mikopo nchini kutokana na kutokamilisha viambata muhimu vinavyohitajika hali iliyopelekea kuongezwa siku nyingine 15.

Afisa Mawasiliano mwandamizi kutoka Bodi ya Mikopo, Veneranda Malima amesema kuwa mpaka kufikia Julai 31, 2018 ambapo ndiyo ilikuwa tarehe ya mwisho kwa wanafunzi kutuma maombi kwa ajili ya kupatiwa mkopo, wanafunzi 88,502 walituma maombi na 78,290 pekee ndio waliokidhi vigezo mpaka sasa.

Kufuatia takwimu hizo zaidi ya wanafunzi 17,303 hawajakamilisha vitu muhimu vya kuambatanisha katika fomu za kuomba mikopo ikiwemo vyeti vya kuzaliwa na vitambulisho vya wadhamini hivyo kupelekea bodi kuongeza muda wa siku kumi na tano.

“Kwasasa hatupokei maombi mapya, lakini muda tulioongeza ni kwa wale waombaji ambao hawakukamilisha viambatanisho muhimu kutokana na wengi kutokuweka vyeti vya kuzaliwa na vitambulisho vya wadhamini”, amesema Malima.

Mei 10, 2018 Bodi ya mikopo ilianza rasmi kupokea maombi kutoka kwa wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na elimu ya juu na tarehe 31 Julai, 2018 Bodi ilifunga zoezi la udahili wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu nchini.

Kiasi cha shilingi Bilioni 427.5  kimetengwa kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu kwa mwaka 2018/2019 ambazo ni kwa wanafunzi wenye mikopo hivi sasa , na waombaji wapya ambao wana sifa za kujiunga na kozi za shahada katika vyuo vikuu nchini.

Ajali Yaua Watu Wanne Dodoma huku Watatu Wakiwa ni wa Familia Moja

0
0
Watu wanne wamefariki dunia watatu wakiwa ni wa familia katika ajali iliyohusisha gari na pikipiki.

Akizunguma na wanahabari jana Agosti 2, Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma Gilles Muroto, alisema ajali hiyo imetokea usiku wa kuamkia jana wilayani Bahi, Dodoma kwenye barabara kuu ya Singida-Dodoma.

Waliofariki ni watoto Yusra Salum (5), Karialino Hamis (2), Hussein Hamisi (miezi miwili) na Mfaume Hamis (30) ambaye alikuwa dereva wa bodaboda.

Kamanda Muroto amesema mwendesha pikipiki huyo alikuwa amewapakia watoto watatu na mama yao na aliingia barabarani ghafla na pikipiki hiyo iligongwa na basi la kampuni ya Satco.

Muroto ameeleza kuwa basi hilo lilikuwa likitokea Mwanza kuelekea jijini Dar es salaam.

“Kwenye hiyo pikipiki walikuwa wamepanda jumla ya watu watano, watoto watatu na mama yao dereva amefariki dunia papo hapo na watoto watatu mama huyo na mama mwenyewe naye ni majeruhi hospitali,”alisema.

Bill Nass amshauri Steve Nyerere kufungua kampuni ya kusimamia misiba

0
0
Msanii wa Bongo Flava, Bill Nass amemshauri muigizaji Steve Nyerere kufungua kampuni ya kusimamia misiba kwa sababu ni kazi anayoiweza zaidi.

Bill Nass akipiga stori na Wasafi TV amesema kuliko Steve Nyerere kutumia fedha zake kuandaa event za comedy ni bora akafanya hivyo na anaweza kupata fedha nyingi zaidi.

"Kuliko kuwekeza fedha zake sijui kuandaa comedy kubwa anaweza akafungua kampuni za kushughulika na misiba na akatengeneza fedha," amesema Bill Nass.

"Anaweza akatumia mtaji huo huo mdongo akanunua gari za kubebea maiti, akawa na vitu ambavyo vina-deal na hiyo fild kwa sababu anaiweza sana," ameongeza.

Bill Nass kwa sasa anatamba na wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Labda.

Lulu Diva Adai Anamiliki Gari La Thamani Kuliko Wasanii Wote Tanzania

0
0
 Aliyewahi kuwa video vixen na sasa ni msanii wa muziki wa bongo fleva, Lulu Diva anae hit na ngoma yake ya 'Ona' amefunguka kuwa yeye ni msanii pekee anaemiliki gari ya thamani Tanzania nzima.

Akipiga story Ayo tv, Lulu Diva, amefunguka na kusema kuwa hana mpango wa kubadilisha gari kwa sababu gari lake ni zuri na lina thamani kuliko magari ya wasanii wote Tanzania. 

“Hapana sina mpango wa kubadilisha gari lakini nitabadiisha rangi kwa sababu sijaona gari ambayo ninaweza nikabadilisha tofauti na Jeep naipenda sana, halafu pia katika wasanii wote mimi peke yangu ndio nina gari nzuri halafu la thamani nyie wenyewe mkiangalia mnaona na sio kitu ambacho naongea ili kujisifia ila am proud of myself” alisema Lulu Diva huku akiongeza kwa kusema kuwa gari hilo hajanunuliwa na mwanaume bali kanunua mwenyewe kutokana na juhudizake binafsi za kimziki, biashara na ukulima wa kahawa.

Mfanyabiashara Davis Mosha akamatwa na Askari wa Uhamiaji

0
0
Mfanyabiashara Davis Mosha alikamatwa Agosti Mosi, 2018 kwa madai ya kuwazuia askari wa Idara ya Uhamiaji kutekeleza majukumu yao na bado anaendelea kushikiliwa kwa hatua zaidi.

Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Ali Mtanda amesema Mosha aliwashambulia askari hao na kumnyang’anya mmoja wao simu ya mkononi baada ya kufika katika jengo la Delina lililopo Sinza Mori.

“Askari walifika kwenye majengo hayo na kujitambulisha kwa mlinzi na moja kwa moja walionyeshwa ofisi za meneja. 

"Wakati wakifanya mazungumzo ya kikazi na meneja huyo, ghafla akatokea Mosha na kuanza kuwafokea, kisha kuwashambulia na kumnyang’anya askari mmoja simu yake.” –Mtanda

Amesema alichofanya Mosha ni kinyume cha sheria ya uhamiaji namba 54 kifungu cha 45 kipengele 1 F, kinachozungumzia kumzuia ofisa wa uhamiaji kufanya kazi yake ya ukaguzi.

Mtanda amesema bado wanamshikilia Mosha kwa uchunguzi zaidi na kama kuna hatua nyingine zitafuata watatoa taarifa.

Je Umepungukiwa Nguvu Za Kiume Na Umetumia Dawa Nyingi Bila Mafanikio?

0
0
Hakika nawashukuru wote mliotumia hii dawa na kunipa pongezi nyingi Sana sasa offa imeisha maana nilitoa ya wiki 2 tu     na watu wengi walioitumia wamepona kabisa 

Dawa hii ni dawa ya maajabu kabisa na huwezi kuamini ila wengi walioitumia wameiamini maana kati ya watu 89 walioitumia ndani ya wiki 2 watu76 wamepona kabisa na watu 9 hawajapona na watu 4 hawajatoa majibu! 

Dawa hii ni dawa inayotibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na unapona kabisa, dawa hii ni dawa ya asili,(mitishamba) utaitumia mara moja tu na hautatumia dawa ya nguvu za kiume tena 

Dawa hii inawafaa watu kuanzia miaka 18 mpaka miaka 70, zaidi ya miaka hyo haitakusaidia ....watafiti wa dawa asilia pamoja na waganga  wameikubali pia dawa hii inawafaa hata wanawake wasiopata hisia za mapenzi 

Ukitumia hii dawa unakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3 bila hamu kuisha, inauwezo wa ajabu na tiba bora kabisa

 SOMA DALILI HIZI;  kutokuwa na hamu ya tendo la ndoa 2 .kushindwa kurudia tendo la ndoa 3. kuwahi kufika kileleni 

Dawa hii imesaidia watu wengi sana dawa hii imegunduliwa na dr kiboko mganga wa tiba za jadi kutoka mafia pia tunatibu matatizo mbalimbali kama mambo ya biashara, nyota, kesi, mapenzi, nk, pia tunahitaji WAKALA wa kupokea dawa zetu katka nchi ya KENYA, ZAMBIA, UGANDA, mikoani tunatuma kwanjia ya mabasi au fika ofisini kwangu  Mafia kisiwani  

maelezo zaidi wasiliana na DR KIBOKO 0679923297

Kalulumila:Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

0
0
 BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO KALULUMILA.
----------------------------------------
Ni dawa pekee iliyojipatia umaarufu nchini na nje ya nchi kwa kufanya kazi mara 3, kwa wakati mmoja 1, kurefusha uume na kunenepesha saizi uipendayo kuongeza nguvu za kiume na inatibu matatizo na gerentii miaka 30. Na kuendelea haina madhara, inaimarisha mishipa ya uume iliyoregea na udhalishaji wa mbegu za kiume. 


---------NINI HUCHANGIA MATATIZO HAYA--Ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya ili kujua kwamba una ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya, ili kujua kama unangiri dalili zake ni kufika haraka kileleni wakati wa tendo la ndoa, 2)kushindwa kurudia tendo la ndoa. 3)kutoa choo kama cha mbuzi. 4)tumbo kujaa gesi na kuunguruma. 5)kukosa choo kabisa. 6)maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi. 7) korodani moja kuvimba 8)kutosikia hamu ya tendo la ndoa na maumivu ya kiuno wakati wa tendo la ndoa. 9)maumivu ya kiuno na mgongo pia tunatibu kisukari kwa siku7, presha, busha, bila kupasuliwa na magonjwa mbalimbali. 

---------------------------------------
TUPO TEGETA KWA NDEVU KARIBU NA MACHINJIO YA NGOMBE UTAONA OFSI IMEANDIKWA KALULUMILA HERBALIST CLINIC HOSPITAL SIMU .
----------------------------------------
-0655-557-182.
-0755-557182.
-0784-557-182.
PIA UTAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
---------------------------------------
KARIBUNI SANA.
----------------------------------------

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images