Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Wanafunzi Wawili wa familia moja Wafariki Dunia Wakiogelea

$
0
0
Wanafunzi wawili wa tumbo moja, Dotto Juma (10), aliyekuwa anasoma darasa la nne katika shule ya msingi Serengeti wilayani Bunda na Maduhu Juma (7) aliyekuwa anasoma darasa la awali shuleni hapo, wamekufa maji mtoni.

Kwa mujibu wa Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Serengeti, Marwa Samu, watoto hao walikufa maji baada ya kuogelea katika mto mkubwa ulioko katika eneo hilo na ndipo walipozidiwa na maji na kupoteza maisha.

Samo alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 10:00 jioni wakati watoto hao wakiwa wanachunga ng’ombe katika eneo hilo.

Kaka mkubwa wa marehemu hao, Kija James, alisema taarifa ya vifo hivyo ilitolewa na mtoto mwenzao, Kulwa Juma (10) waliyekuwa naye wakichunga mifugo hiyo.

James alisema baada ya kufika katika eneo hilo, walikuta nguo za watoto hao pembezoni mwa mto na walipomuuliza Kulwa, alisema walikuwa katika eneo hilo.

“Tulifika katika eneo hilo, ambako ni lile lile ulikokutwa mwili wa tajiri wa mabasi, Super Sammy. Tulipomuuliza Kulwa kwamba wenzake walikuwa wapi, alitujibu kuwa walikuwa katika eneo hilo,” alisema.

“Tulimuuliza kwamba huenda wamekwenda kuchungia ng’ombe sehemu nyingine akatujibu kwamba walikuwa hapo hapo tu,” aliongeza James.

Alisema juhudi za kuopoa miili yao zilifanyika na ndipo wazamiaji walipoingia ndani ya mto huo na kufanikiwa kuiopoa na kutoa taarifa polisi.

Ofisa mmoja wa polisi wilayani hapa, ambaye hakutaka kutaja jina lake kwa madai kuwa si msemaji wa polisi, alisema miili ya marehemu hao ilihifadhiwa katika Hospitali Teule ya Wilaya ya Bunda na kwamba tayari imefanyiwa uchunguzi na daktari na kukabidhiwa kwa ndugu zao kwa ajili ya mazishi.


Nyumba 36 zamponza RPC.....Naibu Waziri Atoa Maagizo kwa IGP Sirro

$
0
0
Mkuu  wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali (IGP) Simon Sirro, ameagizwa kumpangia kazi nyingine Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kusini Pemba, Mohamed Shekhan Mohamed, kutokana na kusuasua kwa ujenzi wa nyumba 36 za polisi.

Agizo hilo lilitolewa jana na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yussuf Masauni, alipofanya ukaguzi wa ujenzi wa nyumba hizo mpya za askari.

“Hatua ya kwanza namwelekeza IGP ambadilishe Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba na ampangie kazi nyingine. Pili, kwa muda mfupi aje mwenyewe aangalie kinachofanyika asisubiri ripoti,” alisema.

Nyumba hizo ni zile zinazojengwa eneo la Mfikiwa, wilaya ya Chake Chake, Kusini Pemba ambazo jiwe la msingi liliwekwa Machi 20, mwaka huu, na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza katika eneo hilo jana, Masauni alimtaka IGP Sirro kufika Pemba ndani ya wiki mbili akajionee yanayoendelea badala ya kusubiri ripoti.

“Akija amchukue na Kamishna wasimamie ujenzi wa nyumba hizi kama nilivyotoa ahadi wakati wa kuweka jiwe la msingi mbele ya  Makamu wa Rais na wakati wa uzinduzi wa nyumba Arusha uliofanywa na Rais John Magufuli,” alisema.

Wakati wa uzinduzi huo, Makamu wa Rais alimtaka IGP Sirro kuwachukulia hatua mara moja askari polisi ambao wamekiuka maadili na taratibu za jeshi katika mkoa wa Kusini Pemba.

Aidha, alilipongeza Jeshi la Polisi nchini kuhakikisha nchi inakuwa tulivu na yenye amani.

Baada ya Shule ya Jangwani Kuwa ya Mwisho, Mwalimu Mkuu na Walimu wengine 47 Waondolewa

$
0
0
Matokeo mabaya ya kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Jangwani, jijini Dar es Salaam, yamesababisha walimu 48, akiwamo Mkuu wa Shule hiyo, Geraldine Mwaisenga, kuondolewa.

Mbali na walimu hao, serikali pia imetangaza kuwaondoa walinzi wote waliokuwapo pamoja na watumishi ambao hawakuwa walimu ikiwa ni jitihada za kuinusuru shule hiyo inayozidi kuporomoka kielimu.

Katika matokeo ya kidato cha sita yaliyotangazwa hivi karibuni na Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania (Necta) na kuwa gumzo miongoni mwa wadau wa elimu, shule hiyo kongwe ilishika moja kati ya nafasi 10 za mwisho. Kwa mujibu wa matokeo hayo, Shule hiyo ilikuwa ya 451 kati ya 453 zilizofanya mtihani huo.

Hatua ya shule hiyo kuwa mkiani kwenye matokeo hayo, ilisababisha Waziri wa elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Ndalichako, na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo, kufika shuleni hapo na kutoa ya moyoni.

Jafo katika ziara yake shuleni hapo, bila kuuma maneno, alisema sababu zilizofanya kupatikana kwa matokeo hayo mabaya ni udhaifu katika uongozi wa shule, uasherati miongoni mwa wanafunzi na walimu kufika na kutia saini kisha kuondoka na kwenda kufanya shughuli zao binafsi.

Akitangaza uamuzi huo jana wakati akizungumza na kituo kimoja cha televisheni , Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando, alisema hatua hizo zimechukuliwa kuinusuru shule hiyo kongwe nchini.

Alisema shule hiyo ilikuwa na walimu 87, hivyo baada ya kuwaondoa 48 ambao ni zaidi ya nusu ya waliokuwapo serikali itahakikisha inaiongezea shule hiyo walimu angalau wengine 20.

“Tumewaondoa pia watumishi wasio walimu wakiwamo walinzi ambao walibainika kuwa ni kikwazo na walichangia kwa namna mbalimbali wanafunzi kufeli,” alisema.

“Tunahakikisha tunabadilisha utawala mzima na baadhi ya watumishi ili kuimarisha uongozi na usimamizi. Lengo ni kuhakikisha shule hiyo inafanya vizuri kwenye matokeo ya kidato cha nne na cha sita,” alisema.

Pia alisema serikali imeweka mkakati kuhakikisha wanafunzi wa shule hiyo wanakuwa na nidhamu inayotakiwa ili kufanya vyema kwenye mitihani.

Breaking News: Pigo Kubwa CHADEMA....Mbunge Wake Jimbo la Ukonga Mwita Waitara Atangaza Kuhamia CCM

$
0
0
Mbunge wa Ukonga (Chadema), Mwita Waitara amejiuzulu uanachama wa chama hicho na kujiunga na CCM leo Jumamosi Julai 28, 2018.

Waitara ametangaza uamuzi wake huo leo katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika ofisi ndogo za CCM Lumumba mjini hapa, akiwa sambamba na katibu wa itikadi na uenezi wa chama hicho, Humphrey Polepole.

Kwa uamuzi huo wa Waitara ambaye alikuwa CCM kabla ya kujiunga Chadema, jimbo la Ukonga linabaki wazi.

Waitara amekuwa mbunge wa pili wa Chadema na wa tatu wa upinzani kuhama chama na kujiunga na CCM. Wengine wa Dk Godwin Mollel (Siha) na Maulid Mtulia (Kinondoni).

Waitara Asema Kilichomuondoa CHADEMA ni Ugomvi Kati yake Na Mbowe Baada ya Kumtaka Asigombee Tena Uenyekiti wa Chama Hicho

$
0
0
Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara amesema kilichosababisha kujivua uanachama wa Chadema na kujiunga na CCM ni Uenyekiti.

Waitara ametangaza uamuzi  wa kujiunga na CCM leo Julai 28 katika mkutano na wanahabari uliofanyika Ofisi za CCM, Lumumba.

“Shida ni uenyekiti wa Chadema, ukianzia kwa akina Chacha Wangwe, Zitto Kabwe, hata mimi ni uenyekiti hapo kuna shida,” amesema.

Amesema suala la uenyekiti sio lake peke yake bali wapo wabunge wengi wanaoguswa nalo lakini hataki kuwataja kwa majina.

“Kuna kikao tulikaa na wabunge wengi wa majimbo na viti maalumu tukawa tunazungumza kwamba Tundu Lissu agombee uenyekiti baadaye hoja hiyo wakaicha mimi nikaendelea nayo. Wakaniambia ninataka Tundu Lissu agombee au ni mimi mwenyewe?” amesema na kuongeza:

“Mbowe amewahi kuniambia kamanda unanipinga na mimi ntakushughulikia na kwenye Chadema bado hakuna mtu kama yupo ntamng'oa hikii chama ni mali yangu.”

Waitara amesema kwamba ugomvi huo uliibuka kwa sababu mchakato wa Uchaguzi ndani ya chama hicho unakaribia na kosa lake ni pale alipotaka kujua ni kwa nini kiongozi huyo mpaka sasa anaendelea kushikilia Uenyekiti kwa takribani miaka 20 sasa.

"Sisi watu wa Tarime tulishaathiriwa naCHADEMA, Marehemu Chacha Wangwe alisema kwamba anataka kugombea nafasi y Uenyekit na Mbowe alimuambia kwamba atamshughulikia na sasa hatunaye. Sasa mimi nimeona bora nikimbie kabla sijashughulikiwa" Waitara.

Mbali na hayo Waitara amesema kwa kuwa anatamani kuwatumikia wananchi wa Ukonga amelazimika kuhamia CCM illi aweze kufanya kazi kwa kushirikiana na serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi wake.

"Mimi nimeona kabla hawajanipiga chini nijiondoe mwenyewe. Sasa ndani ya CHADEMA, ukionekana na mtu wa CCM unaulizwa kwa nini unaonekana na watu hao. Mimi shida yangu siyo CCM shida yangu ni kuona wananchi wangu wa Ukonga wanatatuliwa shida zao. Wananchi wa Ukonga wavumilie natafuta namna bora ya kuweza kuwana viongozi wa serikali bila kuhojiwa kama nimefumaniwa na mke wa mtu. Nimetaka kuwa huru" ameongeza.

Waitara amesema amejivua uanachama kwa kutumia Katiba ya CHADEMA, Ibara ya 5.41 ambapo ameweka wazi atakuwa siyo Mbunge wa Ukonga na hakihitaji tena chama hicho "Nimetupa jongoo na mti wake".

Waitara amesema uamuazi wake wa kuhamia CCM tayari ameungwa mkono na wazee wa jadi wa Musoma, na watu wake wa karibu.

Jeshi la Polisi Jijini Mwanza Lakamata Sila 4 na Jambazi Moja

$
0
0
Mnamo tarehe 26/07/2018 majira ya saa 21:00hrs usiku katika mtaa wa bugarika wilaya ya nyamagana jiji na mkoa wa mwanza. Mussa faustine, miaka 19, mkazi wa mtaa wa bugarika, alikamatwa na wananchi na kupigwa sana, hii ni baada ya kuwatishia kuwapiga kwa bastola iliyotengenezwa kienyeji wananchi wale, ndipo wakati wakiendelea kumpiga taarifa zilifikishwa polisi ambapo askari waliokuwa doria walikwenda haraka  kutoa msaada na kumuokoa kijana huyo huku akiwa na silaha hiyo na risasi saba za silaha aina ya short gun. 

Pamoja ya kwamba alikuwa katika hali ya kipigo ilibidi askari waondoke nae na kwenda kumhoji vizuri wapi alilopata hiyo silaha, anafanya shughuli gani na anashirikiana na nani.

Kijana huyo alitoa ushirikiano vizuri kwa askari japo alikuwa katika hali ya kujeruhiwa sana, alitoa ushirikiano na kueleza kikundi chake ambacho wanashirikiana katika kufanya na kupanga matukio ambayo walikuwa wamepanga kufunya katika siku za hivi karibuni kisha alimtaja kiongozi wake aitwaye hamza @ mjomba. 

Katika maelezo yake tuliweza gundua kwamba hamza huyu ni  mmojawapo mwa wale majambazi waliokuwa wametoroka katika tukio la tarehe 08.7.2017 , ambapo katika tukio lile waliweza kuuawa majambazi wapatao saba huko maeneo ya fumagila.

Pia kijana huyu alitueleza kuwa hamza amerudi tena mwanza na sasa ivi wameanza kujipanga tena ili waweze kufanya matukio mengine zaidi, lakini pia aliwataja watu wengine wanao wawezesha kifedha ili waweze kufanikisha mambo yao wanayoyapanga, majina yao tunayo tutayashughulikia kwa kuwatafuta mmoja baada ya mwingine ili tuweze kuwahoji na hatua stahiki ziweze kuchukuliwa dhidi yao.

Sambamba na hilo kijana huyo tuliweza kumhoji kama anazo silaha nyingine na yeye alitoa ushirikiano vizuri na alieleza zilipokuwepo tulikwenda nyumbani kwake na kuweza kupekua na kukuta silaha nyingine mbili zilizo tengenezwa kienyeji. 

Vilevile alitupeleka kwenye nyumba nyingine iliyopo eneo la kisesa ambapo ndipo alipokuwa anakaa hamza napo ilipatikana silaha nyingine moja, jumla zilipatikana silaha nne na risasi saba za silaha aina ya short gun. 

Lakini kwa taarifa alizotupa alisema wanazo silaha nyingine, ndio maana sasa tunafanya juhudi kubwa za kumtafuta kiongozi wao hamza pamoja na kundi lake  ili tuweze kusambaratisha kikundi hicho.

Pia tulikuta makaratasi yaliyochorwa namna ya kutengeneza silaha, tumepata habari kuwa kundi hili ndilo linalochukua watoto na kuwapeleka huko wanapokujua wao wenyewe na kuwafundisha namna ya kutumia silaha ili kuja kufanya uhalifu hapa mwanza na maeneo mengine katika nchi yetu. 

Aidha wakati tulipoona kijana huyo hali yake inazidi kuwa mbaya tulimpeleka hospitali kupatiwa matibabu lakini baadae alifariki dunia wakati akiendelea kupatiwa matibabu. Mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitali ya rufaa ya bugando kwa ajili ya uchunguzi, pindi uchunguzi ukikamilika utakabidhiwa kwa ndugu wa marehemu kwa ajili ya mazishi.

Kamanda wa polisi mkoa wa mwanza naibu kamishina wa polisi ahmed msangi anatoa wito kwa wakazi wa jiji na mkoa wa mwanza hususani vijana akiwataka kuacha kujihusisha na uhalifu tena uhalifu wa kutumia silaha kwani matokeo yake yanaweza yaweza kuwa kifo, kilema cha maisha au kufungwa, hivyo vijana wafanye kazi zilizo halali za kujiongezea kipato na sio vinginevyo. Vilevile anawaomba wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi kama walivyofanya wananchi wa mtaa wa bugarika.

 IMETOLEWA NA:
DCP: AHMED MSANGI
KAMANDA WA POLISI (M) MWANZA

CCM Watangaza Kumpokea Rasmi Mwita Waitara....Tazama Hapa Alichokisema Polepole

$
0
0
Chama cha Mapinduzi CCM Kimetangaza kupokea rasmi Maombi ya Mbunge wa jimbo la ukonga kupitia CHADEMA kujiunga na chama hicho muda mfupi baada ya mbunge huyo kutangaza kujivua uanachama na nafasi zake zote kisha kujiunga CCM .

Akizungumza mbele ya vyombo vya habari katika ofisi za makao makuu CCM Limumba jijini Dar- es Salaam , Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM Humphrey Polepole ameeleza kuwa Chama cha mapinduzi kinathamini sana mchango wa mbunge huyu kwani amekuwa ni mbunge anayeamini katika kusimamia ukweli.

Polepole  amesema pamoja na ndugu Mwita Waitara kuacha dhamana ya ubunge, mshahara,  na marupurupu yake, CCM kinatangaza rasmi moja kwa moja kuazia leo hii kitampeleka kwa watanzania kwa ajili ya kusema ukweli wote kwa kuwa ameonesha ujasiri mkubwa kisiasa.

"Wapo wengine ambao wangalikubali wauache ukweli wayaishi maslahi lakini wapo viongozi wachache ambao wapo radhi kupoteza yao ila umma upate kwa hiyo mimi nikupongeze sana ndugu Waitara" amesema Polepole.

Amesema baada ya kupata taarifa za mbunge huyo amezungumza na viongozi wa CCM akiwemo Katibu Mkuu Bashiru Ally, ambaye amempongeza sana Waitara kwa kujiamini kwake na kusimamia ukweli, hivyo CCM itaanza kwenda naye maeneo tofauti kwa hatua ya awali hasa kwenye maeneo ambayo kampeni za uchaguzi mdogo unafanyika ikiwemo jimbo la Buyungu mkoani Kigoma.

Polepole ameongeza kuwa wana-CCM wanayofuraha kushirikiri na Waitara katika kampeni zinazoendelea, na baada ya hapo atapata utambulisho na makaribisho rasmi ya wana-CCM wenzake katika eneo analoishi.

Awali akizungumza mbele ya Waandishi wa habari ndugu Waitara alisema moja kati ya vitu vilivyomuondoa ndani ya chama CHADEMA ni ugomvi wake na Mbowe ndani ya chama.

"Mimi nimeona kabla hawajanipiga chini nijiondoe mwenyewe. Sasa ndani ya CHADEMA, ukionekana na mtu wa CCM unaulizwa kwa nini unaonekana na watu hao. Mimi shida yangu siyo CCM shida yangu ni kuona wananchi wangu wa Ukonga wanatatuliwa shida zao. Wananchi wa Ukonga wavumilie natafuta namna bora ya kuweza kuwa na viongozi wa serikali bila kuhojiwa kama nimefumaniwa na mke wa mtu. Nimetaka kuwa huru" aliongeza. Waitara.

Ikumbukwe kuwa mwaka 1998 Mwita Waitara aliwahi kuwa mwanachama wa CCM  kisha kuhamia CHADEMA lakini leo hii amerejea tena CCM kwa mara nyingine akiwa miongoni mwa wabunge machache machachari wa upinzani waliotikisa kwa hoja nzito katika bunge 11.

Makamu wa Rais aagiza wataalamu wa ughani kupelekwa kwa wakulima wa ndizi Rungwe na Kyela

$
0
0
Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan ameuagiza uongozi wa Mkoa wa Mbeya kupeleka wataalamu wa ughani kwa wakulima wa ndizi katika wilaya za Rungwe na Kyela ili kuboresha kilimo cha zao.

Amesema lengo la kupeleka wataalamu hao ni kufungua soko la Kimataifa la ndizi wilayani Kyela.

Samia amebainisha hayo leo Julai 28 wakati akizungumza na viongozi wa Serikali ya wilaya ya Kyela na mkoa wa Mbeya pamoja na wananchi wa Kiwira Wilayani Kyela baada ya kukagua meli moja ya abiria inayoendelea na uundwaji katika bandari ya Itungi na mbili za mizigo ambazo zimeanza kufanya kazi katika Ziwa Nyasa.

“Maofisa ugani hawa sasa washuke kwa wakulima, washughulikie wazalishaji wa ndizi ili zitokote ndizi zenye viwango vinavyotakiwa katika soko la kimataifa kwa sababu najua ndizi yetu Kyela inakwenda hadi Afrika Kusini,” amesema.

Mbali na hilo, Samia amesema utekelezwaji wa mradi wa meli mbili za mizigo na moja ya abiria katika Ziwa Nyasa umelenga uwepo wa viwanda na shughuli za kilimo na biashara zilizopo Mkoa wa Mbeya na mikoa jirani ya Nyanda za Juu Kusini.

Basata Yasisitizwa Kuwatambua Wasanii Na Kuwaweka Katika Mfumo Rasmi

$
0
0
Na Anitha Jonas – WHUSM
Baraza la Sanaa la Taifa limeagizwa  kufanya kazi kwa bidii  na kuhakikisha linawafikia  wasanii wengi zaidi nchini na ili kuweza kuwatambua na kuwatambulisha kwenye mfumo rasmi.

Agizo hilo limetolewa leo katika kijiji cha Chwamwino Jijini Dodoma na Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi alipokuwa akifungua tamasha la kumi la muziki wa Cigogo liliandaliwa na Kituo cha Sanaa Chamwino.

“Tusipotunza Ngoma na Nyimbo zetu siyo tu maarifa yetu yanapotea bali hata utu wetu na historia yetu itapotea kwani jamii nyingi duniani zimepoteza utamaduni wao hivyo ni vyema tulinde na tuenzi utamaduni wetu”Katibu Mkuu Suzan Mlawi.

Akiendelea kuzungumza katika ufunguzi wa Tamasha hilo Katibu Mkuu huyo alisisitiza suala la wasanii kujiuliza maswali kama wanajitambu na kutambua thamani ya kazi zao na je wanatambua kazi zao za Sanaa ni mtaji mzuri wa kujiletea maendeleo.A

Pamoja na hayo nae Katibu Mtendaji Bw.Godfrey Mngereza alieleza kuwa Tamasha hilo la Chamwino ni chachu katika sekta ya Sanaa kwani linasaidia kujenga kizazi cha sasa na kizazi kijacho kutambua thamani ya utamaduni wao.

“Muziki na Sanaa ndiyo vitu vinavyotumika kututofautisha sisi watu weusi na kupitia tamasha hili linasaidia kutoa elimu kwa watoto namna ya kuthamini muziki wetu na namna Sanaa inaweza kusadia ukuaji wa uchumi”Katibu Mtendaji BASATA Godfrey Mngereza.

Kwa upande wa Mwanadaaji wa Tamasha hilo Dkt.Kedmon Mapana amesema tamasha hilo limeonyesha kukuwa na katika msimu huu idadi ya washiriki imeongezeka na kufika vikundi Zaidi ya sitini kutoka maeneo mbalimbali nchini na kumekuwa na wageni kutoka nje ya nchi kama Marekani na nchi za jirani.

Wachimbaji Wadogo Watakiwa Kulipa Maduhuli Ya Serikali

$
0
0
Na Jonas Kamaleki-MAELEZO, Dodoma
Serikali imewataka wachimbaji wadogo wadogo Mkoani Dodoma kulipa maduhuli yake ili kuiwezesha kutekeleza mipango yake ya maendeleo ikiwemo kutatua changamoto zinazowakabili wachimbaji hao.

Rai hiyo imetolewa leo na Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Prof. Idris Kikula wakati wa ziara ya kukagua shughuli za uchimbaji madini Mkoani Dodoma.

“Utakuta leseni moja inatumiwa na watu kama kumi ambao hawalipi kodi ya Serikali, hii haivumiliki, ulipaji wa maduhuli hayo uanze mara moja”, alisema Prof. Kikula.

Akiongea kuhusu uchenjuaji wa dhahabu baada ya kutembela kiwanda hicho, Prof. Kikula amesema kuwa kuna changamoto katika uchenjuaji, hivyo imeundwa timu ndogo ya kufuzifuatilia ili utatuzi wake uweze kupatikana.

Changamoto zilizobainishwa na wachenjuaji ni pamoja na kutokuwa na umeme wa uhakika katika viwanda vyao, hivyo kuiomba Serikali kuingilia kati.

Naye Meneja wa Mgodi wa Nholi, Raphael Simba ameishukuru Serikali kwa kufanya ziara mgodini hapo kwani itawasaidia kutatua changamoto wanazokumbana nazo.

Simba amebainisha changamoto wanazokutana nazo kuwa ni uchimbaji wa kizamani unaotumia zana zisizoridhisha.

Ameiomba Serikali kuwasaidia katika upatikanaji wa zana za kisasa ikiwemo na umeme, kuwapatia wataalaam wa miamba kwa ajili ya kuainisha maeneo yenye dhahabu, jambo ambalo litawapunguzia kutumia nguvu nyingi katika kuchimba sehemu zisizo na madini hayo.

Aidha, Simba ameiomba Serikali kuwapatia mafunzo ya uchimbaji bora na wenye tija ikiwemo kuwafundisha kuhusu Sheria ya Madini ya Mwaka 2017. Akijibu kuhusu mafunzo, Mwenyekiti wa Tume ya Madini amemwagiza Afisa Madini Mkazi wa Mkoa kwa kushirikiana na Kamishina wa Tume, Haroun Kinega kutoa mafunzo hayo kuanzia wiki ijayo.

Kwa upande wake, Kamishina wa Tume ya Madini ambaye pia ni Mtendaji Mkuu wa Shirikisho la Wachimbaji Madini nchini, Haroun Kinega amesema katika ziara hiyo, amebaini changamoto zinazowakabili wachimbaji wadogo wadogo na kwamba zitafanyiwa kazi ili uchimbaji uwe na tija kwa wachimbaji na Serikali iweze kupata mapato yake.

Amesisitiza kuwa Tume itaendelea kukagua shughuli za uchimbaji na kuwapa elimu hasa wachimbaji wadogo wadogo kwa ajili ya kuboresha uchimbaji huo hivyo kuwaongezea kipato.

Ziara hiyo inayolenga kuainisha changamoto za uchimbaji madini na kuzitafutia suluhisho itaendelea wiki ijayo katika Mkoa wa Dodoma.

Breaking News: Rais Magufuli Kafanya Mabadiliko ya Wakuu wa Wilaya na Makatibu Wakuu....Jokate Mwegelo, Jerry Murro, Kafulila Wameteuliwa

$
0
0
Rais Magufuli  amefanya mabadiliko madogo katika nafasi mbalimbali za kiungozi kama ifuatavyo;

Rais John Magufuli amemteua Jokate Mwegelo kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe mkoa wa Pwani

Rais pia amemteua Jerry Muro kuwa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru mkoa wa Arusha.

Patrobas Katambi ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma.

Wakati huo huo, David Kafulila ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe.

Moses Machali ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu mkoa wa Mtwara

Lengay Ole Sabaya ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoa wa Kilimanjaro

Daniel Godfrey Chongolo ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mkoa wa Dar Es Salaam.

Rais Magufuli amemteua Ally Hapi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa , kabla ya uteuzi huo Hapi alikuwa mkuu wa wilaya ya Kinondoni.

Dr Jim Yonaz ameteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya July 29

Kalulumila:Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
 BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO KALULUMILA.
----------------------------------------
Ni dawa pekee iliyojipatia umaarufu nchini na nje ya nchi kwa kufanya kazi mara 3, kwa wakati mmoja 1, kurefusha uume na kunenepesha saizi uipendayo kuongeza nguvu za kiume na inatibu matatizo na gerentii miaka 30. Na kuendelea haina madhara, inaimarisha mishipa ya uume iliyoregea na udhalishaji wa mbegu za kiume. 


---------NINI HUCHANGIA MATATIZO HAYA--Ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya ili kujua kwamba una ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya, ili kujua kama unangiri dalili zake ni kufika haraka kileleni wakati wa tendo la ndoa, 2)kushindwa kurudia tendo la ndoa. 3)kutoa choo kama cha mbuzi. 4)tumbo kujaa gesi na kuunguruma. 5)kukosa choo kabisa. 6)maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi. 7) korodani moja kuvimba 8)kutosikia hamu ya tendo la ndoa na maumivu ya kiuno wakati wa tendo la ndoa. 9)maumivu ya kiuno na mgongo pia tunatibu kisukari kwa siku7, presha, busha, bila kupasuliwa na magonjwa mbalimbali. 

---------------------------------------
TUPO TEGETA KWA NDEVU KARIBU NA MACHINJIO YA NGOMBE UTAONA OFSI IMEANDIKWA KALULUMILA HERBALIST CLINIC HOSPITAL SIMU .
----------------------------------------
-0655-557-182.
-0755-557182.
-0784-557-182.
PIA UTAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
---------------------------------------
KARIBUNI SANA.
----------------------------------------

RC Mnyeti Awapa Onyo Wanaofungia Viwanda Ovyo

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti amesema hatakubali kuona maamuzi mabovu yanatolewa kwenye mkoa wake ikiwemo kufungia kiwanda bila sababu ya msingi.

Mnyeti ameyasema hayo mjini Babati kwenye kiwanda cha pombe cha Mati Super Brands Ltd ambacho kilifungiwa hivi karibuni na mkemia wa serikali na yeye akaagiza kifunguliwe.

Alisema viongozi wa serikali wanapaswa kuwa wasaidizi kwa kuwaelewesha kitaalamu wawekezaji ili warekebishe mapungufu pindi yakiwepo na siyo kufungia viwanda.

Alisema hivi sasa serikali ipo kwenye mchakato wa ujenzi wa viwanda vipya hivyo wataalamu wanatakiwa kutumia elimu yao kuwaelimisha wawekezaji na siyo kuwakandamiza.

“Hizo mbwembwe kafanyie sehemu nyingine siyo Manyara, haiwezekani mtu eti anajiita mtaalamu wa serikali anafungia kiwanda sababu ya ukosefu wa komeo la mlango au kuwa na eneo dogo la kuhifadhi bidhaa,” alisema Mnyeti.

Alisema kabla ya kukifungulia kiwanda hicho kilichofungiwa na mkemia alifuatilia na kupeleleza ili kujiridhisha sababu ya kukifungulia akabaini hazina mantiki.

Mkurugenzi wa kiwanda cha Mati Super Brands Ltd, David Mlokozi alisema ili kuunga mkono kauli ya Tanzania ya viwanda wapo mbioni kuanzisha viwanda vingine mkoani Manyara.

Mlokozi alisema hivi karibuni watamuomba mkuu huyo wa mkoa afungue kiwanda kingine cha vinjwaji vikali ili kukuza uchumi wa nchi na kutoa ajira kwa wananchi wa eneo hilo.

Alisema kwenye kiwanda hicho wakati huu wa uzalishaji hulipa sh60 milioni kama kodi ya mapato serikalini kupitia mamlaka ya mapato nchini (TRA).

Jaji Mkuu Awataka Mahakimu Kutochelewesha Mashauri

$
0
0
Na Magreth Kinabo
Jaji Mkuu wa Tanzania,Mhe .Profesa Ibrahim Juma amewataka mahakimu wapya wasiwe chanzo cha ucheleweshaji  wa mashauri.

Aidha   kuacha kulalamika bali pale linapotokea matatizo, bali wawe chachu ya kuyatafutia   ufumbuzi katika utendaji wao wa kazi wa kutoa  huduma  za haki kwa wananchi.

Kauli hiyo imetolewa jana na Jaji Mkuu huyo wakati akiwaapisha Mahakimu  wapya  kwenye hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam.

“ Kiapo mlichoapa ni uzito muda wote mtakaofanya kazi  ya kuwatumikia  wananchi,  wananchi wanataka kutatuliwa kwa malalamiko yao kwa haraka,”

Aliongeza kwamba  mfumo wa sasa sio  wa kukaa na kulalamika, kama kuna tatizo litafutiwe ufumbuzi na kuepuka kuwa   chanzo cha ulalamishi.

Alisema  mahakimu hao  wanapaswa kuwa weledi  wanapotoa huduma za utoaji haki ili waweze kutoa hukumu zinazoeleweka kwa kujibu wa sheria na kanuni.  Hivyo wanapaswa kushirikiana na wadau wengine wa mahakama  ili kuahakikisha hukumu zinatoka kwa haraka.

Alisisitiza  mahakimu  hao kwamba kufanya kazi kwa kuepuka rushwa na kwa nidhamu.

Jaji Mkuu huyo  alifafanua kuwa changamoto za majengo chakavu na umbali , visikwamishe  utendaji kazi  wao, hivyo   mahakama iko katika Mpango Mkakati wa Miaka Mitano   ambao unalenga kutoa huduma  za haki kwa wote   na   wakati, ikiwemo  kuboresha miundombinu.

Aliwataka mahakimu hao kuielewa taasisi inayofanyakazi na mpango mkakati huo.  

Je Umepungukiwa Nguvu Za Kiume Na Umetumia Dawa Nyingi Bila Mafanikio?

$
0
0
Hakika nawashukuru wote mliotumia hii dawa na kunipa pongezi nyingi Sana sasa offa imeisha maana nilitoa ya wiki 2 tu     na watu wengi walioitumia wamepona kabisa 

Dawa hii ni dawa ya maajabu kabisa na huwezi kuamini ila wengi walioitumia wameiamini maana kati ya watu 89 walioitumia ndani ya wiki 2 watu76 wamepona kabisa na watu 9 hawajapona na watu 4 hawajatoa majibu! 

Dawa hii ni dawa inayotibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na unapona kabisa, dawa hii ni dawa ya asili,(mitishamba) utaitumia mara moja tu na hautatumia dawa ya nguvu za kiume tena 

Dawa hii inawafaa watu kuanzia miaka 18 mpaka miaka 70, zaidi ya miaka hyo haitakusaidia ....watafiti wa dawa asilia pamoja na waganga  wameikubali pia dawa hii inawafaa hata wanawake wasiopata hisia za mapenzi 

Ukitumia hii dawa unakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3 bila hamu kuisha, inauwezo wa ajabu na tiba bora kabisa

 SOMA DALILI HIZI;  kutokuwa na hamu ya tendo la ndoa 2 .kushindwa kurudia tendo la ndoa 3. kuwahi kufika kileleni 

Dawa hii imesaidia watu wengi sana dawa hii imegunduliwa na dr kiboko mganga wa tiba za jadi kutoka mafia pia tunatibu matatizo mbalimbali kama mambo ya biashara, nyota, kesi, mapenzi, nk, pia tunahitaji WAKALA wa kupokea dawa zetu katka nchi ya KENYA, ZAMBIA, UGANDA, mikoani tunatuma kwanjia ya mabasi au fika ofisini kwangu  Mafia kisiwani  

maelezo zaidi wasiliana na DR KIBOKO 0679923297

TFS Kukusanya Bil. 100 Kuchangia Serikali

$
0
0
Wakala wa Huduma za Misitu nchini (TFS), imejiwekea malengo zaidi ya kukusanya kiasi cha Sh bilioni 122 kutoka katika vyanzo vyake mbalimbali ili waweze kuchangia mfuko mkuu wa fedha za serikali.

Akifunga mafunzo ya siku nne ya kuhusu taratibu za kukusanya maduhuli ya serikali iliyofanyika ukumbi wa VETA mjini hapa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFS Profesa Donsantos Silayo, amesema lengo hilo litatilia mkazo uibuaji vyanzo vipya vya mapato.

“TFS inajivunia na inayo furaha baada ya kuchangia katika mfuko mkuu wa serikali kiasi cha Sh milioni 22.4 baada ya kuvuka lengo lake la kutoa gawio hilo ambalo awali tulipanga kutoa serikali Sh milioni 18.5 kama mchango wao lakini tumetoa zaidi.

“Kwa kweli ni fahari kwetu kama taasisi zilizoweza kuwasilisha fedha hizo katika mfuko huo wa serikali kiasi kwamba tumeshika nafasi ya tano katika utoaji wa gawiwo hilo,” amesema Profesa Silayo.

Akizungumzia mikakati waliyoiweka katika mwaka huu wa fedha, Profesa Silayo amewataka wahasibu kuhakikisha wanabuni vyanzo vipya vya mapato vya taasisi hiyo ili kuondoa dhana iliyojengeka kwamba TFS kazi yao ni kuuza mbao na mkaa.

Awali akizungumza katika mafunzo hayo Mhasibu Mkuu wa TFS Peter Mwakosya alisema miongoni mwa changamoto walizonazo ni migongano baina ya wahasibu na maofisa misitu inayosababisha migogoro inayohitaji ufumbuzi wa haraka ili taasisi hiyo iweze kuwndelea kukua katika kipindi cha miaka minane tangu kuanzishwa kuwa wakala wa serikali.

“Migongano hiyo isipotafutiwa ufumbuzi mapema kwa luleta mashirikano baina ya idara zilizomo ndani ya taasisi hiyo, inaweza kuzorotesha ufanisi na kasi iliyojiwekea taasisi katika inapiga hatua na kuwa bora katika kuhudumia wananchi katika shughuli mbalimbali za TFS,” amesema.

Muleba Kuunganishwa Umeme Gridi Ya Taifa

$
0
0
SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco), lipo mbioni kuiunganisha Wilaya ya Muleba mkoani Kagera na umeme wa gridi ya Taifa ili kuvutia wawekezaji hasa katika sekta ya viwanda nchini.

Akizungumza jana wakati wa shughuli ya kuunganishaji wa laini ya umeme wa gridi ya Taifa inayofanyika katika vijiji ya Kitete Wilayani Chato Mkoani Geita, Meneja wa Tanesco Wilaya ya Muleba, Julius Bagasheki, amesema kazi ya uunganishaji wa umeme wa gridi ni utekezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya chama tawala CCM kwa kuhakikisha wanatekeleza sera ya Tanzania ya Viwanda.

Alisema umeme huo wa gridi kwa Wilaya ya Muleba tayari wameanza na mradi wa uunganishaji 33KV ambao sasa unakwenda kuifanya Muleba kuwa na umeme wa uhakika.

“Umeme wetu tunachukulia kutoka Uganda ila ila kwa mradi huu sasa unakwenda kuifanya Wilaya ya Muleba kuwa na umeme wa uhakika wa gridi wa Taifa ambao haukatiki ovyo.

“Sisi Tanesco Muleba na Mkoa wa Kagera kwa ujumla tumejipanga vema kuitekeleza kwa vitendo sera ya Tanzania ya viwanda. Hivyo tunawaalika wawekezaji mbalimbali hasa wa sekta ya viwanda sasa waje Muleba kujenga viwanda kwani muda si mrefu tunakwenda kuwa na umeme  wa uhakika wa gridi ya Taifa ambao ni mkombozi wa uhakika,” alisema Bagasheki

Baadhi ya wananchi ambao wameshafikiwa wa umeme wa REA III, katika Kijiji cha Kitete, wamesema kuwa hatua ya kupata huduma hiyo sasa wanakwenda kupata maendeleo ya kasi ya kuweza kujiletea maendeleo kwa kuwa na uhakika wa umeme.

Mmoja wa wananchi hao Veronica John, ambaye ni mmiliki wa Duka la Dawa Muhimu (DLDM) ameishukuru serikali kwa kuwafikishia huduma ya umeme kwenye kijiji chato.

“Zamani tulikuwa tunanunua mafuta ya taa kwa gharama kubwa lakini baada ya serikali tuletea umeme nasi sasa tutapata maendeleo.  Hivi karibuni nitatununua jokofu kwa ajili ya kuhifadhi dawa ili zisiweze kuharibika baada ya kupata umeme. Kwa kweli tuna furaha ya hali ya juu,” amesema Monica

Naye Kinyozi Makoye Mwango, amesema kuwa hatua ya kupata umeme imemsadia kutoa huduma ya uhakika kwa wateja wao ambao hufika kunyoa nywele kwa uhakika.

“Awali tulikuwa tunachaji betri kwa gharama kubwa na unanyoawateja wawili hadi watatu… kwa sasa baada ya umeme kuja kwa kweli ninaweza kunyoa watu wengi za zaidi na kipato changu kimeongezeka mara dufu, hongera serikali pamoja na Tanesco,” amesema Mwango.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Serikali Yatoa Siku 30 Kwa Madiwani Wa Kigoma Ujiji.......Yasema wasipojirekebisha italivunja baraza lao

$
0
0
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa siku 30 kwa Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kujirekebisha na kumaliza tofauti zao ndani ya siku 30 na iwapo wataendelea na vurugu Serikali haitosita kuvunja baraza la Madiwani.

Amesema hatua hiyo inatokana na Madiwani hao kutumia muda mwingi wakigombana badala ya kuwahudumia wananchi, Serikali inataka kuona wananchi wakihudumiwa kwa kuboreshewa maendeleo katika maeneo yao na si kushuhudia viongozi wakigombana kwa maslahi binafsi.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana (Jumamosi, Julai 28, 2018) wakati akizungumza na wananchi wa mkoa wa Kigoma katika mkutano wa hadhara uliofanyika Manispaa ya Kigoma Ujiji kwenye uwanja wa Kawawa, akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake mkoani Kigoma.

“Serikali hairidhishwi na utendaji wenu na nimewapa muda wa mwezi mmoja kumaliza tofauti zenu. Nataka muendelee kufanya kazi za kuwatumikia wananchi wa Manispaa hii ambao wamewachagua ili muwatatulie kero zao na si kuendeleza migogoro,” amesisiza.

Amesema Madiwani hao wanatakiwa kufuatilia changamoto zinazowakabili wananchi wao ikiwemo ya upatikanaji wa dawa katika hospitali, zahanati na vituo vya afya, ambapo licha ya Serikali kutoa fedha nyingi kwa ajili ya ununuzi wa dawa lakini bado wananchi wanaendelea kukosa huduma hiyo.

Waziri Mkuu amesema matatizo ya madiwani wa Manispaa hiyo anayafahamu na iwapo watashindwa kujirekebisha Serikali haitosita kulivunja baraza hilo kwa sababu Madiwani wake wanatumia muda mwingi kugombana badala ya kuwahudumia wananchi.

Katika hatua nyingine,Waziri Mkuu amewahakikishia wananchi wa mkoa wa Kigoma kwamba Serikali itaboresha miundombinu ya mkoa huo ikiwemo ya reli, barabara, ujenzi wa bandari na uwanja wa ndege utakaokuwa na uwezo wa kutua ndege kubwa.

Amesema lengo la maboresho hayo ni kuufanya mkoa huo kuwa kitovu cha biashara utakaounganisha nchi za Rwanda, Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) na Burundi kwa kuimarisha vivutio vya uwekezaji.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images