Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,

Hatimaye Mbunge wa Tunduma (Chadema), Frank Mwakajoka Kaachiwa Kwa Dhamana

$
0
0
Mbunge wa Tunduma (Chadema), Frank Mwakajoka na katibu wa Baraza la Vijana la chama hicho (Bavicha) Mkoa wa Songwe, Ayub Sikagonamo wameachiwa kwa dhamana  jana  jioni Jumapili Julai 15, 2018.

Viongozi hao walikamatwa na polisi juzi  baada ya kwenda kituo cha polisi kuonana na mkuu wa kituo hicho (OCD) ili awape ulinzi wa askari.

Walichukua uamuzi huo ili kwenda na askari hao katika ofisi za Halmashauri ya Tunduma kuchukua fomu za wagombea udiwani wa chama hicho. Awali walikwenda katika ofisi hizo na kukuta zimezingirwa na polisi.

Akizungumza baada ya kuachiwa huru, Mwakajoka amesema wakiongozwa na wakili wao Boniphace Mwabukusi, wameelezwa kuwa wanatuhumiwa kwa kosa la kuchoma moto nyumba ya mgombea wa udiwani kata ya Mwaka Kati, Ayub Mlimba (CCM).

“Ni mambo ya ajabu sana. Sisi  tulikwenda Polisi kuomba ulinzi ili tusindikizwe katika ofisi za halmashauri kuchukia fomu za wagombea wetu. Eneo lile kulikuwa na ulinzi na tulijua tukienda tunaweza kuambiwa  tumekwenda kufanya vurugu,” amesema Mwakajoka.

“Tulikataliwa na wakati tukijiuliza sababu tukaelezwa kuwa tupo chini ya ulinzi, kutuhumiwa kuwa tumechoma moto nyumba ya mgombea wa CCM.”

Wakati Mwakajoka na Sikagonamo wakiachiwa wa dhamana, wanachama 15 wa Chadema wameendelea kusota mahabusu baada ya kukosa dhamana.

Kwa mujibu wa Mwabukusi, wanachama hao wanatuhumiwa kufanya shambulio kali licha ya shambulio husika kutowekwa wazi.

Waziri Mpina Aruhusu Uingizaji Wa Nyavu Za Kuvulia Samaki Na Dagaa Kutoka Nje Ya Nchi.

$
0
0
NA MWANDISHI MAALUM, DODOMA
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina ameruhusu uingizaji wa vyavu za kuvulia samaki na dagaa kutoka nje ya nchi baada ya kubaini kuwa viwanda vya kuzalisha nyavu hizo vilivyopo nchini kushindwa kuhimili mahitaji ya soko la ndani na kusababisha usumbufu mkubwa kwa wavuvi.

Akizungumza katika kikao cha tathmini ya operesheni Sangara 2018 jijini Dodoma, Waziri Mpina amemuagiza Katibu Mkuu- Uvuvi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Rashid Tamatama kuhakikisha kuwa katika kipindi cha siku 14 awe amekamilisha kupitia maombi na kuruhusu uingizaji wa nyavu hizo kutoka nje ya nchi. Pia kuweka utaratibu ambao hautaathiri soko la viwanda vya ndani.

Mbali na hilo Waziri Mpina ameigiza wizara yake kuandaa mkakati wa kudhibiti upotevu wa mapato, usimamizi na udhibiti wa rasilimali za uvuvi nchini ili kuondoa mianya yote  ya upotevu wa mapato ya Serikali na kuweka ulinzi thabiti wa rasilimali za uvuvi.

Pia ametaka Wizara hiyo kufanya mapitio ya mkakati wa ufugaji wa samaki kwenye maji, kufufua  vituo vya kuzalisha vifaranga na kufanya tathmini ya uwekezaji wa sekta binafsi na kuainisha mahitaji ya sasa ili kuongeza uzalishaji utakaochangia kupunguza nguvu ya uvuvi kwenye maziwa na  hivyo kutokomeza uvuvi haramu, kuongeza ajira na upatikanaji wa malighafi za viwanda nchini.

Akizungumzia matokeo ya operesheni Sangara 2018, Waziri Mpina alisema jumla ya watuhumiwa 3,998 walikamatwa kwa makosa mbalimbali na kutozwa faini na wengine kufikishwa Mahakamani, nyavu haramu 575,152, makokoro 11,144 na kamba za kokoro zenye urefu wa mita 859,304 zilikamatwa na kuteketezwa kwa moto.Pia ndoano 1,910, 135 zisizoruhusiwa kisheria ziliharibiwa.

Pia kilo 359,869 za samaki wasioruhusiwa zilikamatwa na kutaifishwa na Serikali ambapo kilo 176,780 za samaki wachanga na wazazi ziligawiwa bure kwenye taasisi mbalimbali zikiwemo shule,magereza,hospitali na watu wenye mahitaji maalum huku kilo 183,059 za samaki wakavu (kayabo) pamoja na kilo 5,889 za mabondoziliuzwa kwa njia ya mnada.

Alizungumzia mafanikio ya operesheni hiyo, Waziri Mpina alisema miezi 6 (Julai-Disemba 2017) kabla ya operesheni Sangara 2018 jumla ya sh. Bilioni 8.5 zilikusanywa ikilinganisha na jumla ya sh. Bilioni 17.7zilizokusanywa miezi 6 (Januari- Juni 2018) kipindi cha operesheni.

Akitolea mfano Soko la Samaki la Kirumba jijini Mwanza, Waziri Mpina alisema mapato yake yameongezeka kutoka sh milioni 206.3 katika kipindi cha Julai-Dis 2017 kabla ya kuanza operesheni na kufikia sh milioni 848.3 katika kipindi cha Januari hadi Juni 2018 baada ya kuanza operesheni hii inaonesha kuwa kwa kipindi cha miezi sita mapato katika soko hilo yameongezeka mara nne.

Alisema jumla ya makusanyo ya sh.bilioni 26.3 yalikusanywa katika mwaka wa fedha 2017/2018 ukilinganisha na makusanyo ya jumla ya shilingi bilioni 18.5 yaliyokusanywa katika mwaka wa fedha 2016/2017. 

Aidha katika kutekeleza operesheni hiyo jumla ya sh. Bilioni 9.3 zilikusanywa na Serikali kutokana na tozo,faini na mauzo ya mazao ya uvuvi yaliyotaifishwa na Serikali.

Pia mauzo ya sangara nje ya nchi yameongezeka kutoka tani 26,000 mwaka 2016/2017 na kufikia tani 26,700 katika mwaka 2017/2018,urahisi wa upatikanaji wa samaki wenye ukubwa unaokubalika kisheria, kuongezeka kwa ukubwa wa samaki wanaochakatwa viwandani huku mahitaji ya vyavu halali yameongezeka  na wananchi kujitokeza kwa wingi kuunga mkono vita ya uvuvi haramu kwa kuwafichua watu wanaojihusisha na vitendo vya uvuvi haramu.

Aidha Waziri Mpina alisema katika operesheni hiyo walibainika baadhi ya watendaji wa Serikali,Madiwani,Wenyeviti wa Halmshauri,Wabunge wakihusika kufadhili uvuvi haramu na kwamba tayari majina ya viongozi hao yameshawasilishwa kwenye vyombo vya dola kwa hatua zaidi huku kwa upande wa watumishi wa wizara hiyo 12 wakisimamishwa kazi.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais(TAMISEMI), Suleiman Jafo aliwaagiza Wakuu wa Mikoa kuwabainisha kwa majina watumishi wote wa Serikali ngazi ya Serikali za Mitaa waliohusika kushiriki ama kufadhili uvuvi haramu na kuyafikisha ofisini kwake ili aweze kuwachukulia hatua kwa mujibu wa sheria.

Waziri Jafo alisema suala la ulinzi wa rasilimali za Taifa ni watanzania wote hivyo kama kuna baadhi ya watumishi wanashiriki hujuma katika kipindi hiki cha Serikali ya awamu ya tano hawatapata nafasi kwani uvuvi ni miongoni mwa sekta inayotegemewa hasa katika ujenzi wa uchumi wa viwanda.

‘Kama Taifa tuna kila sababu ya kuungana katika mapambano ya uvuvi haramu hasa katika kipindi hiki cha uchumi wa viwanda,ofisi yangu haitasita kuwachukulia hatua kali za kinidhamu kwa watumishi wote watakaobainika kutajwa kushiriki uvuvi haramu”alisema Jafo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge,Kilimo, Mifugo na Maji, Mahmoud Mgimwa alimtaka Waziri Jafo kusimamia kikamilifu agizo lake kwani baadhi ya watendaji walioko chini ya wizara yake ndio wafadhili wakubwa wa mtandao wa uvuvi haramu na kukwamisha juhudi za Serikali za kumaliza tatizo hilo.

Mgimwa alisema mapato mengi ya uvuvi yalikuwa yanaishia mifukoni mwa watu wachache lakini kwa juhudi na ubunifu mpya uliofanywa na Waziri Mpina na wizara yake umewezesha kukusanya sh.  bilioni 9.3 katika kipindi cha miezi sita na fedha hizo zimeingia mfuko mkuu wa Taifa na kwenda kusaidia kwenye ununuzi wa ndege,ujenzi wa reli, umeme,maji,elimu bure na uboreshaji wa sekta ya afya.

 Kamanda Mkuu wa Operesheni Sangara 2018, Emanuel Bulai alisema operesheni hiyo imebaini kuwepo uvunjifu mkubwa wa sheria ikiwemo matumizi ya zana haramu za uvuvi, utoroshaji mkubwa wa mazao ya uvuvi na raia wa kigeni kuingia nchini na kufanya biashara ya samaki na mazao na yake bila kufuata Sheria za nchi.

Barack Obama Aisifia Hifadhi ya Serengeti....Aahdi Kusaidia Sekta ya Utalii Nchini

$
0
0
Rais mstaafu wa Marekani, Barack Obama ameeleza kufurahishwa na vivutio vya utalii vilivyopo katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Hayo yameelezwa jana Jumapili Julai 15, 2018 na Waziri wa Mambo ya Nje, Dk Augustine Mahiga katika mkutano wake wa naandishi wa habari.

Dk mahiga alikuwa akieleza kwa ufupi mazungumzo yake ya Obama ambaye alitembelea hifadhi hiyo alipokuwa nchini.

“Obama amevutiwa na hifadhi ya Serengeti, ameahidi kuisaidia Tanzania kuvutia wawekezaji zaidi katika hifadhi hii. Amesema ameona mambo mengi ambayo hajawahi kuona akiwa na familia yake,” alisema Dk Mahiga.

Kuhusu usiri wa ujio wa Obama nchini, Balozi Mahiga amesema kiongozi huyo mstaafu alikuwa na ziara binafsi.

“Alikuja kutembelea hifadhi ya Serengeti ikiwa ni safari yake binafsi hivyo ni lazima tuheshimu,” alisema.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira alisema ujio wa Obama na familia yake umeitangaza Tanzania na kuungwa mkono na meneja uhusiano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa), Pascal Shelutete ambaye  alisema ujio wa rais huyo mstaafu unatokana na jitihada za nchi kutangaza vivutio vya utalii.

Mfanyakazi wa Ndani Atiwa Mbaroni Kwa Wizi wa Mtoto wa Bosi Wake

$
0
0

Na, magdalena kashindye
Jeshi la polisi Mkoa wa shinyanga linamshikilia binti wa miaka 20 Habiba Abubakari kwa wizi wa mtoto.
 
Katika taarifa ya Jeshi hilo kwa vyombo vya habari iliyotolewa na kamanda wa polisi wa Mkoa huo Simon Haule inasema walipata taarifa za kupotea kwa mtoto William Emmanuel kutoka kwa Jeshi la polisi singida.

Taarifa hiyo inaeleza binti huyo aliyekuwa msichana wa kazi za ndani 'House Girl'  wa Hawa Rojas miaka 20 alimuacha mtoto na binti wa kazi na kwenda kwenye shughuli zake na aliporudi nyumbani alimkosa binti huyo na alitoa taarifa kituo cha polisi na juhudi za kumtafuta ziliendelea.

Julai 13, 2018 binti huyo alikamatwa kata ya Nyasubi wilayani Kahama mkoani Shinyanga na baada ya kuhojiwa alikiri kutenda kosa hilo na kueleza sababu ya kufanya hivyo ni ugumba uliopelekea kuachana na mumewe Yohana Cyprian (24)

Haule amesema binti huyo atasafirishwa hadi mkoani singida lilipotokea tukio hilo na kuwataka wazazi kuwa makini na watoto wao.

Waziri Mkuu Atoa Siku 14 Wajasiriamali Wahame......Ni baada ya kukagua eneo la viwanda vidogo na kupewa malalamiko

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kahama Mji, Bw. Anderson Msumba ahakikishe ndani ya siku 14 anawahamisha wajasiriamali wote waliogoma kuhamia eneo la viwanda la Bukondamoyo.

“Wauza mbao, wachomeaji grili, wenye gereji wote, hakuna ruhusa kuendelea kubakia mjini wakati tumewapa eneo la bure la ekari 500. Lile eneo ni zuri kwa biashara lakini kuna watu wamegoma kuhamia kule. Mkurugenzi hakikisha wote hawa wanahamia kule mara moja na atakayekiuka, akamatwe,” alisema.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana (Jumapili, Julai 15, 2018) wakati akizungumza na wajasiriamali wachache waliohamia kwenye eneo la viwanda la Bukondamoyo katika kata ya Zongomela, wilayani Kahama mkoani Shinyanga mara baada ya kulikagua.

“Ninawaagiza wajasiriamali wote walioko mjini wawe wamehamia huku ifikapo tarehe 30 Julai, 2018. Mkuu wa Mkoa ikifika tarehe moja Agosti, wewe njoo na Kamati yako ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na mkiwakuta huko mjini, wakamateni na kuwaweka ndani,” alisema.

Alimwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kahama Mji aimarishe barabara za eneo hilo kwa sababu kuna magari yanatakiwa kupeleka mizigo lakini pia kuna magari ya wateja yatapaswa kwenda huko kwa hiyo ni lazima pafikike kwa urahisi.

“Tengeneza barabara, weka taa za barabarani za solar, lakini pia uangalie uwezekano wa kuweka kituo kidogo cha polisi kwa sababu kuna kundi kubwa la wafanyabiashara na wateja. Pia wekeni zahanati ili hawa wakipata majeraha, wahudumiwe kwa haraka,” alisema.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wajasiriamali wawili, Bw. Haji Selemani na Bw. Sudi ambao walisema wajasiriamali wote walipewa agizo la kuhamia eneo la viwanda lakini kuna wenzao wamegoma, na wanaendelea kufanya biashara mjini ambako kuna wateja wengi.

Akizungumza na maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa Taifa wa Kahama, Waziri Mkuu alirudia kutoa agizo hilo na kuwaahidi kwamba watapatiwa mafunzo ya uwezeshaji na taasisi iliyoko kwenye ofisi yake ifikapo Julai 30, mwaka huu.

“Ifikapo Julai 30, atakuja Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) hapa Kahama na kutoa mafunzo ya namna ya kupata mikopo na kufanya biashara. Haya mafunzo yatatolewa kulekule, kwa hiyo wahini kuhamia mpate kushiriki fursa hiyo,” alisema.

Wakati huohuo, Mkurugenzi wa Mji wa Kahama, Bw. Anderson Msumba alisema eneo hilo la viwanda lina ukubwa wa ekari 500 na lilipimwa na kugawanywa kisha vikapatikana viwanja 678 vyenye ukubwa wa kati, wa chini na wa juu (high, medium and low density).

“Viwanja hivyo wamepewa bure isipokuwa wanapaswa kulipia gharama za kupata hati ambazo zinaanzia sh. 150,000 hadi 300,000 kutegemeana na ukubwa wa kiwanja. Maji yapo ila yataongezwa mradi wa Zongomelo ukikamilika.”

Kuhusu barabara za eneo hilo, Bw. Msumba alisema TARURA walishatoa makadirio yao ambayo ni sh. bilioni 1.3 na wameshapeleka maombi hayo TAMISEMI. Alisema maeneo kwa ajili ya ujenzi wa kituo kidogo cha polisi pamoja na mabenki, yameshatengwa, ni suala la wahusika kwenda kuomba.

Waziri Mkuu Apiga Marufuku Michango Ya Shule......Yadaiwa Wazazi Kahama wanatozwa sh. 20,000 kwa kaya

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema hakuna michango yoyote itakayokusanywa kutoka kwa wazazi kwa ajili ya shule kama haina kibali cha Mkurugenzi wa Halmashuri.

“Mheshimiwa Rais wetu, Dkt. John Pombe Magufuli alishapiga marufuku michango ya aina hii na akatangaza mpango wa elimumsingi bila malipo. Sasa hivi zinaletwa zaidi ya sh. bilioni 20 kila mwezi kwa ajii ya kuboresha elimu ya msingi katika kila wilaya.”

Waziri Mkuu ametoa katazo hilo jana (Jumapili, Julai 15, 2018) wakati akizungumza na maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa Taifa wa Kahama, wilayani Kahama mkoani Shinyanga.

Alikuwa akijibu hoja ya Mbunge wa Kahama, Bw. Jumanne Kishimba ambaye alisema kuna michango inatozwa bila kibali chochote na kwamba kila kaya inatakiwa ilipe sh. 20,000. “Michango hii itolewe kwa kibali ina iangalie uwezo wa familia kiuchumi,” alisema.

Akitoa mfano, Mbunge hiyo alisema kuna familia ina madebe matatu tu ya mahindi ukiitoza hiyo hela, manake wauze mahindi yao yote ndiyo walete  michango  hiyo wabaki na njaa kwa mwaka mzima. Ni vema michango hiyo izingatie kipato halisi cha kaya,” alisema,

Katika hatua nyingine,Waziri Mkuu aliwaeleza wananchi hao juhudi mbalimbali ambazo Serikali imezichukua ili kuboresha maisha ya Watanzania kupitia huduma za maji, umeme, elimu na afya.

Alisema ameridhishwa na ujenzi wa viwanda unaoendelea kwenye mkoa wa Shinyanga na kukiri kuwa ameguswa kuona kuna uzalishaji mkubwa wa mafuta ya kula yanayotokana na mazao ya mbegu kama pamba na alizeti wakati kuna watu wanaagiza mafuta ya kula kutoka nje ya nchi.

“Nimetembelea kiwanda cha kukamua mafuta ya pamba cha Kahama Oil Mills, na mwenye kiwanda ameniambia kuwa miaka yote huwa anafanya kazi kwa miezi mitatu tu lakini mwaka huu ana uhakika wa kufanya kazi kwa miezi tisa, kutokana na jinsi ambavyo wakulima wameitikia wito wa kufufua zao la pamba,” alisema.

“Jana pia nilitembelea kiwanda cha JIELONG ambacho kiko kwenye Manispaa ya Shinyanga. Na kwenyewe nimeona uzalishaji mkubwa wa mafuta ya kula ambao sijapata kuona,” alisema Waziri Mkuu.

Mapema,Waziri Mkuu alizindua kituo cha afya cha Mwendakulima ambacho kilianza kujengwa mwaka 2010 na kukamilika mwaka 2016 kwa ufadhili wa kampuni ya kuchimba madini ya ACACIA kupitia mpango wake wa Corporate Social Responsibility.

Kampuni hiyo imejenga chumba cha wagonjwa wa nje (OPD), nyumba mbili za watumishi (2 in 1) ambazo zinakaliwa na watumishi wanne, wameweka vitanda na solar panel kwa gharama za dola za Marekani 710,000/- (kwa exchange rate ya kipindi hicho).

Mwanajeshi wa JWTZ Akutwa Amefariki Kisimani

$
0
0
Polisi Mkoa wa Kusini Unguja imesema inaendelea na uchunguzi kubaini sababu za kifo cha askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), ambaye mwili wake ulikutwa kisimani.

Kamanda wa polisi mkoani hapa, Suleiman Hassan Suleiman alisema jana kuwa wanaendelea na uchunguzi, huku akimtaja mwanajeshi huyo kuwa ni Othman Khatib Othman (36), mzaliwa wa kisiwani Pemba.

Suleiman alisema Alhamisi jioni wiki iliyopita, walipata taarifa kutoka kwa wasamaria wema kuwa kuna mwili umeonekana kisimani.

Alisema kisima hicho kipo eneo la Ubago jirani na kambi ya JWTZ alikokuwa akifanya kazi na kwamba, mwili uliopolewa Ijumaa saa 11:45 asubuhi.

Kamanda Suleiman alisema baada ya uchunguzi mwili ulizikwa eneo jirani kutokana na kuharibika, hivyo kushindikana kusafirishwa kupelekwa nyumbani kwao.

LIVE: Tazama Hapa Rais Magufuli Akizinduzi chuo cha CCM Kibaha

$
0
0
Rais John Magufuli leo Jumatatu Julai 16, 2018 anazindua ujenzi wa Chuo cha Uongozi cha Julius Nyerere kilichopo Kibaha mkoani Pwani.

Viongozi mbalimbali wa chama tawala na Serikali wameshiriki uzinduzi huo, wakiwemo viongozi mbalimbali wa vyama vya ANC (Afrika Kusini),  Swapo (Namibia),  MPLA ( Zimbabwe), Frelimo (Msumbiji) na ZANU-PF.

Uzinduzi huo pia unashuhudiwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Chama cha Kikomunisti cha Watu wa China (CPC),  Song Tao.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM,  Humphrey Polepole amesema chuo hicho kitakuwa kikiwaandaa viongozi na kuwapika makada wa chama hicho na vyama vingine vilivyoshiriki harakati za ukombozi kusini mwa bara la Afrika.

==>>Tazama tukio zima hapo chini

Lugola Ampa Siku 10 Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya vitambulisho- NIDA

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Kangi Lugola ametoa siku zisizozidi kumi kwa Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya vitambulisho NIDA, akiwa na kampuni ya Iris Dilham kufika ofisini kwake mjini Dodoma ili kueleza sababu ya kutofika kwa mtambo wa kuchapisha vitambulisho mpaka sasa.

Agizo la Mh. Lugola linakuwa ni utekelezaji wa miongozo aliyopatiwa na Rais Magufuli siku alipomuapisha kuwa Waziri wa Mambo ya ndani baada ya kutengua uteuzi wa Dkt. Mwigulu Nchemba.

Wakati akitoa muongozo wa maeneo sugu ndani ya Wizara ya Mambo ya Ndani, Julai 2 Rais Magufuli alisema "Kuna suala la NIDA, mambo ni hovyo. Kuna pesa zilichezewa, kuna vifaa viliagizwa na havikufika. Tumewachukulia hatua lakini waliofanya mambo hayo mpaka leo hatua gani wamechukuliwa? Je, pesa hizo zimerudishwa? Kasimamie hayo mambo," Rais Magufuli.

Mhe. Lugola amesema hayo baada ya kutembelea Ofisi ya Uzalishaji vitambulisho hivyo kilichopo Kibaha, mkoani Pwani na kutoridhishwa na kazi ya utoaji wa vitambulisho kwa wananchi, zoezi ambalo linaendelea kufanywa na NIDA katika maeneo mbalimbali nchini.

Waziri huyo amesema kuwa mpaka sasa kuna dalili za kuwa kampuni hiyo iliyopewa tenda imeshindwa kuleta mtambo huo hivyo atahitaji maelezo ya kina kuhusiana na hilo kabla hajachukua maamuzi mengine.

"Dalili zinaonyesha kwamba kampuni ya Iris Dilham haina mpango wa kutuletea huo mtambo. Sasa kama hawana mpango ni vyema wakatueleza fedha zetu ziko wapi. 

"Nakuagiza Mkurugenzi Mkuu nataka nikiwa Dodoma Julai 25 mwaka huu majira ya saa nne mfike ofisini kwangu ukiwa na hao wenye kampuni ya Iris, na kwa kuwa wameonyesha kushindwa waje na hizo pesa in 'advance' kabisa ili kusudi tukazihifadhi benki tena tutapeleka na 'escort' ya juu. Ztafanyiwa shughuli nyingine. Hatuwezi kucheza na pesa za watanzania " amesema Waziri Lugola.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Hukumu ya Wema Sepetu yasogezwa mbele

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeahirisha kesi ya dawa za kulevya inayomkabili muigizaji wa filamu nchini, Wema Sepetu hadi Julai 20, 2018 siku ya Ijumaa kwa ajili ya kutoa  hukumu juu ya kesi hiyo.

Hukumu hiyo ilipaswa kusomwa leo lakini imesogezwa mbele hadi Julai 20 kutokana na hakimu anayesikiliza shauri hilo kutokamilisha kuandika hukumu.

Uamuzi huo umetolewa leo Jumatatu Julai 16, 2018 na  Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba.

“Naomba mniwie radhi kuna vitu vichache bado sijaviweka katika hukumu yangu, hivyo naomba kuiahirisha hadi Julai 20, ili niweze kuvikamilisha,” amesema hakimu Simba.

Hukumu hiyo inatarajia kutolewa Julai 20 baada ya mawakili wa upande wa utetezi, Albert Msando na wa mashtaka, Costantine Kakula kuwasilisha hoja za majumuisho katika kesi hiyo.

Tayari mashahidi watano wa upande wa mashtaka wameshatoa ushahidi, mahakama hiyo kuwaona  washtakiwa kuwa na kesi ya kujibu na walianza kujitetea.

Mbali na Wema, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni  wafanyakazi wake Angelina Msigwa (23) na Matrida Abas (19) ambao wote kwa pamoja  wanakabiliwa na kesi ya kutumia dawa za kulevya aina ya bhangi.

Nape Asema Hana Mpango wa Kuhama CCM.....Mtazame Hapa Alivyojumuika na Wapiga Kura Wake Kutazama Kombe la Dunia

$
0
0
Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amesema hawezi kukihama chama hicho tawala kwa kuwa ana hisa nyingi.

Nape ametoa kauli hiyo jana jioni Jumapili Julai 15, 2018 mbele ya  wananchi wa Mtama ambao jioni hiyo alijumuika nao kutazama fainali za kombe la Dunia..

Amewataka wananchi hao kuondoa hofu juu yake akiwataka kupuuza maneno yanayosemwa kuhusu hatima yake CCM ambapo alisisitiza kuwa hataondoka katika chama hicho.
Kuhusu asilimia 65 ya ushuru wa zao la korosho kwenda Serikali Kuu, Nape amesema ataendelea kufuatilia jambo hilo na kusisitiza kuwa kuteleza si kuanguka.

Mizizi 29 Power ,ndio Dawa Bora Na Imara Kwa Sasa Kwa Kutibu Na Kuponesha Tataizo La Nguvu Za Kiume Kwa Dakika 30 Tu

$
0
0
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume limekuwa ni janga kubwa sana kwa sasa sio vijana au wazee wanalalamiki kukimbiwa na wa wapenzi wao au ndoa kuvunjika kutokana na mwanaume kulala na mwanamke kitanda kimoja hata wiki mbili bila kushiriki tendo la ndoa na hii ndio inachangia wanawake wengi kutoka nje ya ndoa kwa nini huteseke na wakati dawa zipo ambazo zitarudisha heshima yako ya ndoa 

MIZIZI 29 POWER; ni ambayo hutibu na kurudisha virutubisho mwilini ambavyo humfanya mwanaume awe na matatizo yafatayo 1 kuwahi kukojoa kabla mke au mpenzi wake

 2. kushindwa kurudia tendo dawa, hii itakufanya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 

3... dawa hii inatibu uume uliolegea na kusinyaa 

4. dawa hii inatoa miungurumo ya tumbo na uchovu wakati wa kumaliza tendo 

NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupiga punyeto kwa mda mrefu 
2 upungufu wa vichochoe mwilini 
3 magonjwa ya moyo, kisukari, presha, vidonda vya tumbo kiuno na mgongo 
4 utumiaji ovyo wa madawa ya kizungu 
4 usongo wa mawazo, hasira, tumbo kujaa gesi na kutopata choo.

 PATA TIBA YANGU NA NI TOFAUTI NA ULIZO WAHI KUTUMIA: 

Je una uume mfupi na mwembamba? MASHESHA MIX ni dawa ya kuboresha uume saiz upendayo asa kwa wale waliofanyiwa tohara wakiwa wadogo.. chagua saizi upendayo inch 5,6,7, adi 8 iyo ni kwa urefu na unene sentimita 2,3,4, adi 5 .dawa hizi zipo za kupaka na kunywa na hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ,

Tunatibu kisukari,vidonda vya tumbo,ngiri, korodani iliyovimba, kupnguza kitambi, maziwa makubwa NK 

KWA TIBA NA USHAULI FIKA OFISINI KWANGU DARE S SALAAMU MBAGALA ZAKHEMU NA MIKOA YA KANDA YA ZIWA YUPO WAKALA WETU HAPO MWANZA NA KWA AMBAO HAWANA NAFASI YA KUJA OFISINI HUDUMA YETU UTALETEWA POPOTE ULIPO PIGA SIMU 0783185060 DR MAKOYE

Rais Magufuli: CCM itatawala milele, wanaoshindana Nayo watapata tabu sana

$
0
0
Rais na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Magufuli amefunguka na kudai chama hicho kitaendelea kutawala milele na milele huku akiwapiga vijembe upinzani kuwa watapata tabu sana siku zote kushindana na chama hicho.

Dkt. Magufuli ametoa kauli hiyo leo Julai 16, 2018 wakati alipokuwa anahutubia mamia ya wakazi wa Mkoa wa Pwani, Kibaha waliojitokeza kushuhudia zoezi la kuweka jiwe la msingi la Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Nyerere ambacho kitakuwa kina kazi kubwa ya kuwapika wanasiasa nchini Tanzania na Afrika kiujumla.

"CCM ni chama tawala na kitaendelea kutawala milele na milele, wanaohangaika watapata tabu sana siku zote. Chama hiki kipo na kitaendelea kuwepo na kitaendelea kuleta maendeleo kwaajili ya watanzania. hakuna mbadala wa CCM", amesema Dkt. Magufuli na kuongeza;

"Kwa wananchi na wanachama wa CCM tembeeni kifua mbele. Tumeamua kuleta Tanzania ya kisasa zaidi na yenye maendeleo, viwanda, muelekeo Tanzania inayoshirikiana na vyama vingine katika Afrika. 

"Tanzania inayowapigania wananchi hasa wanyonge ili waweze kushiriki maendeleo yao. Tanzania inayopiga vita rushwa, unyonyaji pamoja na uonevu".

Kwa upande mwingine, Dkt. Magufuli amesema chuo hiko hakitakuwa na ubaguzi wa aina yoyote ile huku akielekeza kuwa chuo hicho kiwe na dira ya waafrika wote na kuleta ukumbozi wa maendeleo ya kiuchumi ndani ya Tanzania.


Waziri Mbarawa Amsimamisha Kazi Mkurugenzi Mamlaka Ya Maji Kigoma

$
0
0
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Mkoa wa Kigoma (KUWASA), Simon Lupuga baada ya kutoridhishwa na utendaji kazi wake.

Mbarawa amefikia hatua hiyo baada ya malalamiko ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga kuwa mamlaka hiyo, Bonde la Mto Tanganyika na wahandisi wa maji hawatimizi majukumu katika nafasi zao kutokana na kufanya kazi kwa mazoea.

Vile vile, Waziri Mbarawa amesema atamuagiza Katibu Mkuu kuandika barua ya uhamisho wa  Mkurugenzi huyo kurejeshwa Dar es Salaam kuanzia leo.

Kamishna Jenerali Mpya Wa Magereza Akabidhiwa Ofisi....Aahidi Kutekeleza Maagizo Yote ya Rais Magufuli

$
0
0
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Phaustine Kasike ameahidi kutekeleza kikamilifu agizo la Rais John Magufuli aliyetaka wafungwa kuzalisha chakula kwa ajili ya kujilisha wakiwa gerezani.

Akizungumza leo Jumatatu Julai 16, 2018 wakati akikabidhiwa ofisi na Kamisha Jenerali mstaafu wa jeshi hilo, Juma Malewa amesema ataanzia pale alipoishia mtangulizi wake.

Katika hafla fupi ya kumuapisha Kasike iliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam, kiongozi mkuu huyo wa nchi alimtaka kutekeleza mambo mbalimbali, huku akimpongeza kidogo na kumpa pole.

Rais Magufuli alisema ni aibu Magereza kutegemea Bajeti ya Serikali wakati ina wafungwa wanaoweza kutumika kuzalisha chakula.

Kasike amesema tayari mtangulizi wake alishaanza kulifanyia kazi jambo hilo, yeye atakachokifanya ni kuendeleza alipoishia.

“Nitaendelea kuukamilisha mpango mkakati huu ili wafungwa kuanza uzalishaji na kujitegemea katika upande wa chakula,” amesema.

Amesema watawatengea kiasi cha fedha wafungwa watakaojishughulisha na uzalishaji ili wafanye shughuli hizo kwa ufanisi.

Kwa upande wake Malewa amesema,  “changamoto bado zipo nyingi, zingine zimeshafanyiwa kazi lakini kubwa  ni kwa hawa ambao tunawalinda ili wawe raia wema. Hivi sasa mbinu na matukio ya uhalifu yamebadilika, kwa uwezo wa Mungu utaweza kukabiliana nayo.”

Waziri Mkuu Amwagiza RPC Shinyanga Awakamate Viongozi Tisa Wa AMCOS Ya Ushetu.....Ni kwa upotevu wa dola za Marekani 21,000

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemwagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Simon Haule awakamate viongozi wa Chama cha Msingi cha Mkombozi kwa upotevu wa dola za marekani 21,000 za chama hicho.

“Wabebe hawa watu, wahoji waseme hiyo fedha iko wapi na jambo la kwanza wailete hiyo fedha ya wakulima. Wakishindwa kurejesha fedha, wawekwe ndani,” amesema.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumatatu, Julai 16, 2018) wakati akizungumza na mamia ya wananchi wa kijiji cha Kangeme, kata ya Ulowa katika Halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama ambao alienda kuzindua mpango wa Ushirika Afya na NHIF.

Waziri Mkuu amefikia uamuzi huo baada ya kuwaita viongozi wa chama cha Mkombozi watoke hadharani na kubaini kuwa hakuwepo hata mmoja. Inadaiwa kwamba walitoroka baada ya wananchi kuanza kuzomea.

Kamanda Haule amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Mwenyekiti, Bw. Shilinde Abdallah na mhasibu wa AMCOS hiyo, Bw. Kulwa Shinzi pamoja na wajumbe saba wa bodi ya chama hicho.

Akiwa katika tukio hilo, Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Kahama (KACU), Bw. Emmanuel Cherehani alisoma taarifa ya Chama na alipotaja bei ya tumbaku kuwa ni nzuri, wananchi walimzomea kupinga kile alichokisema. Bw. Cherehani alikuwa akitoa mafanikio ya chama hicho, na kusema kuwa bei ya tumbaku ni nzuri.

Akitoa ufafanuzi kuhusu kadhia hiyo, Waziri wa Kilimo, Dk. Charles Tizeba alisema kuna tatizo katika uteuzi (grading) wa tumbaku kwani wakulima wanalima tumbaku nzuri lakini katika upangaji bei, wanalipwa bei ndogo. “Kuna wakulima wanakidai chama cha Mkombozi kiasi cha dola za Marekani ambayo ni madai ya tumbaku waliyoiuza tangu mwaka 2014.”

Akizungumza na wananchi hao, Waziri Mkuu alisema Serikali imeamua kufufua ushirika kwa sababu ndiyo mkombozi wa wakulima. “Tumeamua kurudisha ushirika aminifu kwa wakulima, na nirudie kutoa onyo kwa viongozi waliopata dhamana ya kuongoza ushirika wasidhani kule wameenda kupata ulaji.”

“Tunataka ushirika unaosimamiwa na viongozi waaminifu. Kwenye ushirika kuna fedha na kuna mali za chama, kwa hiyo ni lazima tupate viongozi ambao ni waaminifu,” amesema.

“Kwa mfano, hapa Ulowa wakulima wamekuwa wakilalamikia kupewa bei ya chini wakati wakati wao viongozi wanabeba kile cha juu na kuwaumiza wakulima. Kiongozi wa KACU kasoma taarifa hapa mkaanza kuzomea, hiyo ni dalili tosha kwamba kuna tatizo la msingi,” amesema.

Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuwaasa wakulima waachane na tabia ya kukopa pembejeo na kufunga mikataba na makampuni ya ununuzi wa tumbaku na badala yake wajiwekee akiba ili msimu wa kilimo ukianza wasirudie tena kukopa.

“Gharama za kulima ekari moja, kuweka dawa, palizi na kuchoma haizidi sh. 150,000. Wewe amua unataka kulima ekari ngapi, weka fedha zako kwenye akaunti usubiri msimu ujao. Kwenye hii biashara ya tumbaku, ukitafuta mikopo utabakia kuwa maskini kwa sababu huna nguvu ya kubishania bei. Wenzenu wanaolima korosho, wameacha kukopa na bei mnazisikia kila mwaka zinapanda,” amesema.

“Ukiwa na mazao yako utaweza kubishana na mnunuzi. Tanzania bei ya tumbaku iko chini sababu wakulima mmetufikisha hapo kwa kupitia mikopo na mikataba na makampuni ya ununuzi. Kuanzia sasa badilikeni, ili muweze kuinua bei ya zao hili muhimu, alisema.

TRA Yakusanya Trilioni 15.5 Kwa Mwaka Wa Fedha 2017/18

$
0
0
Na Veronica Kazimoto
Makusanyo ya kodi kwa Mwaka wa Fedha wa 2017/18 yameongezeka hadi kufikia shilingi trilioni 15.5 kutoka shilingi trilioni 14.4 kwa Mwaka wa Fedha 2016/17 sawa na ongezekeo la asilimia 7.5.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati akitoa taarifa ya makusanyo ya kodi ya mwaka wa fedha 2017/18, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Richard Kayombo amesema kuwa katika mwezi Juni, 2018 pekee, TRA imekusanya jumla ya shilingi trilioni 1.5 ikilinganishwa na shilingi trilioni 1.4 kwa mwezi Juni, 2017 ambayo ni sawa na ukuaji wa asilimia 8.0.

“TRA inapenda kuwapongeza na kuwashukuru walipakodi wote ambao mchango wao umeiwezesha Serikali kupata mapato haya tunayotangaza leo kwa ajili ya kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo na za jamii zikiwemo ujenzi wa miundombinu ya reli na barabara, ununuzi wa ndege, upatikanaji wa elimu, afya na mambo mengine kwa manufaa ya watanzania wote,” alisema Kayombo.

Kayombo amezitaja sababu zilizosababisha kuongezeka kwa makusanyo hayo kuwa ni pamoja na elimu ya kodi kuzidi kueleweka kwa walipakodi na wananchi kwa ujumla, kuongeza ukaribu na walipakodi kwa kuwasikiliza na kutatua changamoto zao za kikodi, kuongezeka kwa walipakodi wapya kupitia kampeni ya kuwasajili kwa kuwafuata waliko na kurahisisha ulipaji wa kodi kwa njia ya kielektroniki.

Aidha, Mkurugenzi huyo alisema kuwa, katika Mwaka huu wa Fedha 2018/19, TRA imedhamiria kutekeleza kwa vitendo kampeni kabambe ya msamaha wa riba na adhabu kwa malimbikizo ya madeni ya nyuma na inategemea kuongeza urahisi wa kulipa madeni ambayo yalikuwa kikwazo kwa wafanya biashara wengi kulipa na hata kuendelea na biashara.

“Vilevile, mamlaka imedhamiria kuongeza kasi ya usajili wa walipakodi wapya. Hivyo, tunaendelea na kasi ya utambuzi na usajili wa wafanyabiashara wadogo ili kila mtu anayestahili kulipa kodi asajiliwe na kuchangia kikamilifu maendeleo ya Taifa,” alieleza Kayombo.

Mkurugenzi Kayombo ametoa wito kwa walipakodi na wananchi wote kuendelea kulipa kodi kwa hiari na kujenga utamaduni wa kudai Risiti za Kielektroniki za Kutolea Risiti (EFDs) kila mfanyabiashara anapofanya mauzo na mnunuzi anatakiwa kudai risiti kila anaponunua bidhaa na huduma mbalimbali.

Mahakama yatengua hukumu kesi ya ufukwe wa Oysterbay

$
0
0
Mahakama ya Rufani imetengua hukumu na mwenendo wa kesi ya mkataba wa uendelezaji wa ufukwe wa Oysterbay kwa kuwa Jaji Aghaton Nchimbi aliyetoa hukumu hiyo hakueleza sababu za kuisikiliza yeye, badala ya jaji wa awali.

Kutokana na hali hiyo, Mahakama hiyo imeirudisha kesi hiyo Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi ili ianze kusikilizwa upya na jaji mwingine tofauti na aliyetoa hukumu hiyo.

Uamuzi huo umetolewa na jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani, lililoongozwa na Kipenka Mussa akishirikiana na Jaji Richard Mziray na Jaji Gerald Ndika.

Jopo hilo la majaji lilisikiliza rufaa ya kesi ya Manispaa ya Kinondoni dhidi ya Kampuni ya Q Consult Limited.

Mahakama Kuu katika hukumu yake iliyotolewa na Jaji Nchimbi Julai 23, 2015, ilikubaliana na madai ya mlalamikaji, Q Consult Limited kuwa Manispaa ya Kinondoni ilivunja makubaliano ya uendelezaji wa ufukwe huo kwa kutotekeleza majukumu yake.

Hivyo, Jaji Nchimbi aliiamuru manispaa kutekeleza wajibu wake kulingana na makubaliano ya mkataba huo na pia akaiamuru imlipe mdai fidia ya Sh500 milioni.

Manispaa ya Kinondoni ilikata rufaa kupinga hukumu hiyo, ikidai kuwa Jaji Nchimbi aliyetoa hukumu hiyo hakuwa na mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo.

Hata hivyo, Mahakama ya Rufani katika hukumu yake iliyoandikwa na Jaji Ndika kwa niaba ya jopo hilo, ilieleza kuwa Jaji Nchimbi kutokueleza sababu za kuisikiliza kesi hiyo kunamfanya akose mamlaka ya kushughulika nayo.

Katika hukumu hiyo ambayo Gazeti la Mwananchi imeiona nakala yake, Mahakama ya Rufani imeeleza msimamo wa kisheria kwamba jaji au hakimu anapolazimika kuendesha kesi ambayo tayari ilishaanza kusikilizwa na jaji/hakimu mwingine ni lazima aeleze sababu za yeye kuisikiliza.

Huku ikirejea hukumu za kesi mbalimbali pamoja na kifungu cha 214 (1) cha Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai (CPA), Mahakama ya Rufani imesema kutokuwepo kwa sababu yoyote kwenye kumbukumbu za shauri husika kunamfanya jaji/hakimu huyo asiwe na mamlaka kuiendesha.

Imesisitiza kuwa matokeo yake mwenendo wote wa shauri hilo ambao umeshaendeshwa na jaji/hakimu mwingine unakuwa ni batili.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images