Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara.?...... Tunazo dawa na PETE za bahati Zenye Uwezo wa Kubadili Maisha Yako

$
0
0
Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara, Msanii wa Maigizo, Mwanamziki, ama mwanafunzi tunazo dawa na PETE za bahati zenye uwezo mkubwa wakuyabadilisha maisha yako nakukupatia mafanikio makubwa ndani ya mda mfupi tu.
 
Kutana na Sharif Al_noor. Yeye ni mtaalam na mtabibu wa nyota za binadam na bingwa wa tiba za asili Afrika mashariki. Wasiliana na mtaalam huyu kwani yeye ufaulu pale wote waliko shindwa na pia humaliza kazi zilizo shindikana ama zilizo achwa ndani ya siku1 tu. -SHARIF ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOASHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA- Sasa amezianza ziara zake za mikoani na atayatembelea maeneo mbali mbali ndani na inje ya nchi.
 
Anatibu magonjwa sugu yanaojulikana nasiojulikana kwakutumia QUR_AN MAJI , KIOO MAJINI NA MITISHAMBA.
 
Anazo dawa za mapenzi( Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu LIMBWATA) kumrudisha  alipotea(MSUKULE), kutoa Mikosi, Kutatuwa shida za chumaulete, mvuto wa biashara na sehem za kazi, kusafisha nyota, kurudisha mali zilizo ibiwa, zilizpotea, ama zilizodhulumiwa, kushika wezi na wachawi, kutoa ndagu, Kutoa kinga ya mwili, nyumba, Biashara, kufukuza majini wabaya, KUUZA kwa haraka (shamba, NYUMA, GARI..), Kesi mahakamani, Kuweka Zindiko ya mwili, nyumba, shamba, Gari, kupata Kazi na kupandishwa cheo, mali na UTAJIRI bila masharti na mengine mengi ya Siri. (Anazo Pia Pochi zisizo kwisha Hela MAGIC WALLET) Kwa tiba na ushauri wasiliana na ofisi kwa nambari ya simu
 
+255 746 426 604

Croatia Yaitandika England 2-1 Na Kufanikiwa Kuingia Fainali Kombe la Dunia

$
0
0
Timu ya Taifa ya England imeaga michuano ya Kombe la Dunia kwa kupoteza mchezo wa nusu fainali dhidi ya Croatia kwa idadi ya mabao 2-1.

Katika mchezo huo, dakika 90 zilimalizika kwa timu hizo kwenda sare ya bao 1-1 na kuamuliwa kuongezwa dakika30 za ziada ili kupata mshindi wa mechi.

England walikuwa wa kwanza kuandika bao mnamo dakika ya 5 ya mchezo kwa njia ya mpira wa adhabu uliopigwa na kuwekwa kimiani na Kieran Trippier na baadaye kipindi cha pili Croatia walisawazisha kupitia kwa Ivan Perisic dakika ya 68.

Baada ya dakika 90 kumalizika kwa sare hiyo, 30 zingine ziliongezwa na Croatia walizitumia vema kwa straika wake, Mario Mandzukic kuandika bao la pili kwenye dakika ya 106.

Mpaka Mwamuzi anamaliza mchezo, matokeo yalibaki kuwa 2 kwa Croatia na 1 kwa England.

Kutokana na England kuondoshwa , sasa itacheza dhidi ya Ubelgiji kusaka mshindi wa tatu Jumamosi huku Croatia ikiungana na Ufaransa kucheza fainali Jumapili ya wiki hii.

Jeshi la Polisi Dar Lawatia Mbaroni Wahalifu Mbalimbali Wakiwemo 12 wa Mtandao wa Wizi wa Magari

$
0
0
Jeshi la polisi Kanda Maalum limewakamata watuhumiwa mbalimbali wa uhalifu wakiwamo 12 wa mtandao wa wizi wa magari na walioiba viatu vyenye thamani ya Sh 600 milioni.

Akizungumza na wanahabari jana Julai 11, Kaimu Kamanda wa polisi, kanda maalum ya Dar es Salaam, Liberatus Sabas alisema  Mei 23 polisi walikamata watuhumiwa hao wakiwa na katoni 500 za viatu zenye thamani ya Sh600 milioni zilizoibwa kwenye ghala la kampuni ya Bata Mei, 21.

“Watuhumiwa hao pia walikamatwa na gari aina ya mistubishi canter T 686 BWY ambalo lilikuwa limebeba mizigo hiyo pamoja na katoni 71 za bia mifuko 18 ya sabuni ya unga,injini 4 za pikipiki,na maboksi 61 ya nguo za mitumba”amesema

Kadhalika alisema Jeshi hilo linawashikilia watuhumiwa 12 wa mtandao wa wizi wa magari na pikipiki katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya mkoa wa Dar es salaam.

Kamanda Sabas amesema watuhumiwa wote wanaendelea kuhojiwa upelelezi utakapokamilika watafikishwa Mahakama

Pia jeshi hilo la polisi limemkamata Omwalimu Binyakusha mmiliki wa Kampuni ya Arise Special Sunrise Safaris kwa kuwatapeli raia wawili wa kigeni.

“Mtuhumiwa huyu alichukua fedha kwa raia hao wa kigeni kwa makubaliano ya kuwapeleka safari lakini mwishoni aliwatelekeza hadi Serikali ilipoamua kuwahudumia,”amesema Sabas.

Tiba Bora ya Tatizo Sugu la Nguvu za Kiume

$
0
0
OFA! Je umepungukiwa nguvu za kiume na umetumia dawa bila mafanikio? Sasa utapona kwa sh 15000 tu .Ofa ni kwa watu kumi wakwanza kila siku .Ofa hii itadumu ndani ya wiki 2 baada ya hapo bei itakuwa nyingine na kama hujapona tunakurudishia hela yako !

Dawa hii ni dawa ya maajabu, huwezi kuamini Ila wengi wameiamini,inatibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na utapewa garantee ya mwezi mmoja 

Dawa hii inapatikana hapo hapo ulipo nyumbani kwako na tutakupatia maelezo ya namna ya kuiandaa wewe mwenyewe na baada ya kuiandaa utakunywa Mara moja tu,na hautatumia dawa yoyote ya nguvu za kiume 

Dawa hii inawafaaa watu kuanzia miaka 18 mpaka miaka 70 zaidi ya miaka hyo haitakusaidia 

Ni dawa ya asilia, haina madhara yoyote,watafiti na waganga wameikubali pia hii dawa inawafaa hata wanawake wasiopata hisia za mapenzi

Pia tunaweza kukutumia dawa popote ulipo lakini s kwa bei ya ofa, ukiitumia dawa hii unakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 3 bila hamu kuisha na itakufanya uwe na uwezo wa kufanya tendo la ndoa muda wowote 

Imesaidia watu zaidi ya 148 ndani ya mwaka mmoja tangu igunduliwe  na Dr kiboko mganga wa tiba za jadi toka kisiwani mafia 

Pia tunatibu magonjwa mbalimbali, kurudisha mpenzi aliye kuacha,biashara iliyoyumba, nk 

Maelezo zaidi ; Dr kiboko-  0679923297

Naibu Waziri wa Madini, Dotto Biteko Akamata Tani Saba Za Madini Ya Vito Yaliyofichwa Ndani

$
0
0
Na Greyson Mwase, Morogoro
Naibu Waziri wa Madini, Dotto Biteko amekamata madini  ya vito aina ya Rhodilite yenye uzito wa takribani tani saba yaliyokuwa yamefichwa nyumbani kwa mchimbaji wa madini hayo, Juvenal Mnene ambaye ni mmiliki wa kampuni ya J. J. Mnene & Partners na kuamuru kukabidhiwa Serikalini pamoja na mmiliki huyo kufikishwa mahakamani.

Naibu Waziri Biteko amekamata madini hayo katika ziara yake aliyoifanya katika wilaya ya Gairo mkoani Morogoro lengo likiwa ni kukagua shughuli za wachimbaji wadogo  wa madini ya vito na ujenzi na kutatua changamoto mbalimbali.

Katika ziara hiyo, Biteko aliambatana na watendaji kutoka Wizara ya Madini, Tume ya Madini, Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Siriel Mchembe, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Gairo, Madiwani na Mwakilishi wa Mbunge wa Gairo.

Mara baada ya kuwasili katika mgodi wa mchimbaji huyo uliopo eneo la Rubeho, Bitteko alibaini kuwa  mchimbaji huyo alikuwa amelipa mrabaha wa shilingi 400,000 tu tangu mwaka 2013 ndipo akataka kupewa taarifa ya uzalishaji  na kiasi cha malipo yaliyolipwa serikalini ikiwa ni pamoja na kodi mbalimbali ambapo alielezwa na mmiliki wa mgodi huo Juvenal Mnene kuwa  taarifa ya uzalishaji wa madini hayo na vielelezo vya malipo yaliyofanyika serikalini ipo nyumbani.

Naibu Waziri Biteko pamoja na msafara wake alielekea nyumbani kwa mmiliki wa mgodi huo, ambapo alishuhudia madini ya vito aina ya Rhodilite yakiwa yamerundikwa kwenye chumba kimoja na kufungwa kwa kufuli bila kuwekwa lakiri (seal) ya serikali kinyume na sheria ya madini inavyotaka.

“Huu ni utoroshwaji wa madini kwasababu haiwezekani madini yahifadhiwe ndani ya chumba bila serikali kufahamu na kuweka lakiri, na kama serikali hatuwezi kukubali kuona madini yakitoroshwa nje ya nchi na wachimbaji wa madini wasio waaminifu,” alisema Biteko

Katika hatua nyingine, Biteko alibaini mchimbaji huyo alikuwa na mtambo wa kuchenjua madini hayo  nyumbani kwake kwa nyuma bila kuwa na leseni ya uchenjuaji madini kama sheria ya madini inavyotaka.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya tukio hilo, Naibu Waziri Biteko alimwagiza Mkuu wa Polisi Wilaya ya Gairo, Musa Mwakasula kwa kushirikiana na Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Morogoro kukamata madini hayo kuyapima ili kujua kiasi chake halisi na kisha kumfikisha mtuhumiwa katika vyombo vya sheria.

Aliongeza kuwa Wizara ya Madini itawachukulia hatua kali za kisheria watu wote waliohusika na mchakato mzima wa kuficha madini hayo.

“ Haiwezekani kabisa juzi juzi  tumekamata madini yenye uzito wa tani 75 jijini Dar es Salaam, ni lazima tuhakikishe tunalinda rasilimali za madini kwa nguvu zote ili ziwe na mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa nchi,” alisisitiza Biteko.

Wakati huo huo, akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kichangani kilichopo wilayani Gairo mkoani Morogoro, Naibu Waziri Biteko alisema Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dk. John Magufuli kupitia Wizara ya Madini imeweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha kuwa sekta ya madini inakuwa na mchango mkubwa wa uchumi wa nchi kwa kuboresha sheria za madini.

Alifafanua kuwa, Wizara ya Madini ipo katika mchakato wa kurasimisha  wachimbaji wadogo kwa kuwapatia leseni  mara baada ya taratibu kukamilika ili kuondokana na umaskini kutokana na kujiajiri

Alisema kuwa, awali rasilimali za madini zilichukuliwa kama umiliki wa wawekezaji wa nje ya nchi lakini mara baada ya maboresho ya Sheria ya Madini wananchi sasa wana haki zote za umiliki wa rasilimali za madini.

Akizungumzia suala la bei elekezi kwenye madini ya ujenzi, Biteko alisema Serikali ipo katika mpango wa kukaa na wanunuzi wa madini hayo hasa wenye viwanda vya kutengeneza marumaru( tiles) na kukubaliana bei ambayo itafanywa kuwa bei elekezi ya madini hayo ili wananchi wanufaike.

Katika hatua nyingine, Biteko aliwataka wachimbaji hao kulipa kodi mbalimbali na kufuata kanuni na sheria za uchimbaji madini.

Wakati huo huo akizungumza katika mkutano huo, Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Siriel Mchembe alieleza changamoto mbalimbali katika uchimbaji madini katika wilaya yake kuwa ni pamoja na wachimbaji wadogo wa madini kutokuwa na leseni kwa kisingizio wameshawasilisha maombi yao kwenye ofisi za madini, kutokuwepo kwa utaratibu mzuri wa uchimbaji madini na kutokuwepo kwa sehemu za kuhifadhia madini.

Aliendelea kusema  changamoto nyingine kuwa ni pamoja na ukosefu wa mitaji hususan kwa wachimbaji wadogo wa madini na upatikanaji wa soko la uhakika la madini hayo.

Waziri Tizeba: "Hakuna Bei Nzuri Ya Kahawa Uganda Inayozidi ya Tanzania"

$
0
0
Na Mathias Canal-WK, Mtukula-Kagera
Imebainika kuwa bei ya uuzaji wa Kahawa nchini Uganda haina tofauti kubwa na bei ambayo ingepatikana nchini Tanzania endapo wakulima wangeuza Kahawa zao kwenye soko la awali jambo ambalo linawatoa wasiwasi wakulima wa Kahawa nchini waliokuwa wakidanganywa kuwa bei ya Uganda ni kubwa na yenye tija kwa wakulima kuliko hapa nchini.

Kilogramu moja ya Kahawa ya maganda nchini Uganda inanunuliwa kwa shilingi 2000 ya Uganda sawa na Shilingi 1400 za Kitanzania (exchange rate 1.7) ilihali hapa nchini Tanzania bei ya Kahawa kwa kilo moja ya maganda ni Shilingi 1460 ya bei elekezi hivyo kuwa na tofauti ya Shilingi 60.

Hata hivyo, wakulima wa Tanzania watapata zaidi kwa kuuza mnadani moja kwa moja na kuachana na bei ya shambani kwa kutumia ushirika wao ambapo bei ya chini inayopatikana ni wastani wa Shilingi 1950 kabla ya gharama za uendeshaji. 

Kwa kuuza mnadani mkulima anapata bei kutokana na Ubora wa Kahawa yake na ikiwa kwenye madaraja na hivyo kutoa motisha kwa wakulima kuzalisha Kahawa bora kuliko kuuza ikiwa ghafi.

Hayo yamebainishwa jana 11 Julai 2018 na Waziri wa Kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba wakati akizungumza na wadau wa biashara ya Kahawa katika ukumbi wa Happiness Hoteli uliopo katika eneo la Mtukula Wilayani Misenyi.

Dkt Tizeba amezungumza hayo ikiwa ni muda mchache tangu alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Biashara na Ushirika nchini Uganda Mhe Fredrick Ngobi Gume katika mkutano uliohudhuriwa pia na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe Charles Mwijage.

Mkutano huo ni muendelezo wa utekelezaji wa maagizo ya Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli aliyoyatoa wakati akiwaapisha viongozi mbalimbali Ikulu Jijini Dar es salaam tarehe 2 Julai 2018 na kuitaka Wizara ya Kilimo kufuatilia kwanini wakulima wa zao la Kahawa wanacheleweshewa malipo yao sambamba na kujua kwanini wakulima wanauza Kahawa yao nchini Uganda.

"Ndugu zangu kuna jambo hamlifahamu wale wanaosema Uganda bei ya Kahawa ni nzuri kuliko Tanzania wanawadanganya hakuna bei nzuri Kule kinachofanya watu kupeleka Kahawa Uganda ni kutokana na mikopo wanayokopeshana isiyo rasmi (Butura) hivyo makubaliano ya kurejesha mkopo yanakuwa na masharti magumu yanayowataka wakulima wa Kahawa nchini kulipa madeni kwa kupeleka Kahawa sio fedha" Alisisitiza Dkt Tizeba wakati akizungumza na wadau wa Kahawa eneo la Mtukula Wilayani Misenyi

Waziri wa biashara na ushirika nchini Uganda Mhe Fredric Ngobi Gume amemuhakikishia mwenyeji wake kuwa biashara ya Kahawa nchini humo ina changamoto sawa katika nchi zote mbili kwa kuwa swala la mikopo isiyo rasmi inayowanyonya wakulima (Butura) nchini Uganda ipo kwa kiwango cha juu kiasi kwamba ameomba kuja kuja nchini kwa miadi maalumu kwa minajili ya kujifunza kuhusu namna bora kuendesha ushirika na kuanzisha mfumo wa stakabadhi ghalani.

Aidha, Gume alisema kuwa serikali ya Uganda inayoongozwa na Rais wa nchi hiyo Mhe Yoweri Kaguta Museveni itaendeleza ushirikiano na serikali ya Tanzania inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli hivyo panapohitajika ushirikishwaji katika biashara hususani kwenye sekta ya Kilimo watakuwa na msimamo wa pamoja.

Katika hatua nyingine pande zote mbili kutoka Tanzania na Uganda wameeleza changamoto mbalimbali zinazoikabili mipaka ya nchi hizo ikiwemo biashara ya magendo inayofanyika huku wakiahidi kutokomeza kadhia hiyo.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

IGP Sirro Awataka Viongozi wa Dini Waendelee Kuhubiri Amani kwa Kufanya Doria za Kiroho Huku Jeshi lake Likifanya Doria za Kimwili

$
0
0
Na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro amewaomba Viongozi wa dini nchini kuendelea kufanya doria za kiroho huku Jeshi hilo likiendeleza doria za kimwili kwa pamoja ili kuukabili uhalifu ikiwemo mauaji yanayosababishwa na wivu wa mapenzi ambayo yameanza kuongezeka katika siku za hivi karibuni.

IGP Sirro ameyasema hayo  kwa nyakati tofauti katika Wilaya za Ukerewe na Sengerema mkoani Mwanza wakati wa Ziara yake inayoendelea katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa yenye lengo la kubaini changamoto za kiuhalifu na kuzipatia ufumbuzi wa haraka ili wananchi waendelee kufanya kazi zao kwa Amani na utulivu.

Amesema Polisi wanafanya doria za kimwili ambazo wakati mwingine hutumia nguvu kushurutisha watu kutii sheria lakini Viongozi wa dini nao wana nafasi yao katika jamii kwa kufanya doria za kiroho na kukemea maovu.

IGP Sirro amesema makosa ya mauaji yanayosababishwa na wivu wa mapenzi yameanza kujitokeza kwa kasi katika siku za karibuni hivyo viongozi wa dini wana nafasi kubwa zaidi kuwaelimisha waumini wao kabla vifo havijatokea kwa kuwa wengi wao wanakuwa nao kila siku za ibada.

Katika hatua nyingine IGP Sirro ameahidi kuchangia Shilingi milioni kumi na tano ili kusaidia ujenzi wa kituo cha Polisi katika  Kisiwa cha Kome, Wilayani Sengerema baada ya Wananchi kuomba kujengewa kituo hicho ili kukabiliana na uhalifu.

Wakizungumza katika mkutano wa hadhara Kisiwani Kome Wananchi hao walisema kujengwa kwa kituo hicho kutasaidia kuimarisha usalam katika maeneo hayo huku wakiomba kufufuliwa kwa Vikundi vya Ulinzi Shirikishi.

IGP anaendelea na ziara yake huku akitumia usafiri wa Helkopta ili kujionea kwa uhalisia maeneo hayo ili kuweza kuzipatia ufumbuzi changamoto za uhalifu.

Kiwanda Cha Sukari Kagera Chaagizwa Kuacha Urasimu Katika Kuuza Sukari Wanayozalisha

$
0
0
Na Mathias Canal-WK, Misenyi-Kagera
Uongozi wa kiwanda cha Sukari Kagera umeagizwa kuacha urasimu katika mfumo wa uuzaji wa Sukari wanayozalisha badala yake kuingiza mtaani kwa wingi Sukari kwa wananchi ili kuepuka kadhia ya upungufu wa huduma hiyo muhimu katika jamii.

Agizo hilo limetolewa na Mawaziri wa sekta ya Kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba na waziri wa sekta ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe Charles Mwijage wakati wakizungumza na uongozi wa kiwanda hicho Jana 11 Julai 2018 walipotembela kiwanda cha Sukari wakiwa kwenye ziara ya siku tatu ya kikazi Mkoani humo iliyoanza Juzi 10 Julai 2018.

Mawaziri hao kwa kauli moja wametoa siku 14 kwa kiwanda hicho kuongeza kasi ya uzalishaji kutoka uzalishaji wa Sukari kwa Tani 350-360 kwa siku ili kufikia walau Tani 450 mpaka 500 kwa siku kwani kufanya hivyo wataimalisha uwezo wa Sukari kupatikana kwa wingi kwa wananchi hivyo kuondoa usumbufu wa gharama katika ununuzi wa bidhaa hiyo.

Aidha, Mawaziri hao wametoa kalipio Kali kwa uongozi wa kiwanda hicho kwa kuwa na mawakala wachache wa usambazaji wa sukari jambo ambalo linapelekea ushindani wa kibiashara kuwa mchache mbinu inayopelekea Sukari kuuzwa kwa gharama isiyokuwa rafiki kwa watumiaji.

Walisema kuwa ndani ya muda mfupi uongozi wa kiwanda hicho unapaswa kutathmini upya namna ya kuongeza Uwekezaji ili kurahisisha huduma za wananchi ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015-2020 hatimaye kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ifikapo mwaka 2025.

Dkt Tizeba alisema kuwa kumekuwa na uingizaji wa Sukari kwa magendo kutoka nje ya nchi kwa sababu Viwanda vya Sukari ndani ya nchi vimefungia sukari kwenye magodaoni bila kuingiza sokoni kwa wingi kuwafikia watumiaji.

Pia, alisema kuwa wataalamu wa kiwanda cha Sukari wanapaswa kutoa elimu ya muwa kwa umma ili kuona umuhimu wa uzalishaji wa zao hilo sambamba na kushirikiana na wakulima wadogo zaidi ya 490 katika vijiji vya jirani na kiwanda hicho.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe Charles Mwijage alisema kuwa serikali inatazama namna bora zaidi ya kukuza takwimu za uzalishaji wa Sukari nchini hivyo Viwanda vya Sukari vinapaswa kuunga mkono juhudi hizo kwa kuchochea Uwekezaji ili kuongeza tija katika uzalishaji.

Pia alisisitiza kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli haitasita kuvifungia Viwanda vyote vitakavyobainika kukiuka taratibu, sheria na kanuni za nchi katika utekelezaji wa majukumu yake.

Mwalimu Aliyembaka na Kumpa Mimba Mwanafunzi Atiwa Mbaroni

$
0
0
Jeshi la Polisi limefanikiwa kumkamata mwalimu wa shule ya sekondari Loliondo, Erick Kalaliche mkoani Lindi ambaye anatuhumiwa kwa kosa la kumbaka mwanafunzi wake wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari Loliondo kabla ya mwalimu huyo kuhamishwa.

Hayo yamebainishwa jana na Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng'anzi  baada ya Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha kutoa agizo la kutafutwa na kukamatwa kwa mwalimu huyo ambaye ametenda kosa la jinai na kuhamia katika shule nyingine.

"Agizo la Naibu Waziri wa Elimu tumelipokea na kama inavyofahamika kuwa kumpa ujauzito mwanafunzi ni kosa la jinai na jarada limeshafunguliwa la kupeleleza tukio hilo kwasababu baada ya kuwasiliana na Mkurugenzi wake yule
mwalimu alipewa uhamisho tangu mwaka 2017 lakini tumewasiliana na wenzetu katika kituo chake kipya kule Lindi na wametuambia kwamba wamefanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo leo hivyo tunafanya mpango wa kurudishwa huku kwenye kesi yake", alisema Kamanda Ng'anzi.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Elimu William Ole-Nasha amesisitiza kuwa, Wizara yake haiwezi kuvumilia walimu wanaofundisha watoto ambao pia ni kama wazazi wanaofumbia macho vitendo vichafu ambavyo vinarudisha nyuma sekta ya elimu na juhudi za serikali za kuhakikisha watoto wa kike  wanapata haki yao ya elimu.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Yaahirisha Uchaguzi Kata 4

$
0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza uchaguzi kwenye kata mbili mpya na kuahirisha uchaguzi wa kata nyingine nne. Mabadiliko hayo yanafanya jumla ya kata zenye uchaguzi kuwa 77 badala ya 79 zilizotangazwa awali.

Akizungumza  jana Julai 10, Jijini Dar es Salaam  Mwenyekiti wa NEC, Jaji  Semistocles Kaijage amezitaja kata hizo mpya kuwa ni Kelamfua  ya Halmashauri ya Wilaya ya Rombo na Kata ya Kitaya,  Halmashauri ya Wilaya ya Nanyamba.

“Kwa mujibu wa Kifungu cha 13 (1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa aliitaarifu Tume uwepo wa nafasi wazi za Madiwani katika Kata ya Kelamfua iliyoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Rombo na Kata ya Kitaya iliyoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Nanyamba,” alisema Jaji Kaijage.

Jaji Kaijage alisema kwamba nafasi zote mbili za Udiwani zimetokana na kujiuzulu kwa madiwani waliokuwa wamechaguliwa awali.

Alisema uteuzi wa wagombea udiwani utafanyika Julai 16 na  kampeni zitaanza  Julai 17 mpaka 11 Agosti na siku ya kupiga kura ni  Agosti 12.

Jaji Kaijage amevialika vyama vya siasa, wadau wote wa uchaguzi na wananchi kwa ujumla kushiriki uchaguzi huo.

Katika hatua nyingine Jaji Kaijage ametangaza kuahirishwa kwa uteuzi wa wagombea kwenye kata tatu za Tindabuligi, Kisesa, Katumba na Mlimba.

Tume itatangaza hapo baadae tarehe nyingine za uteuzi na uchaguzi katika kata hizo.

Uteuzi Mwingine Uliofanywa na Rais Magufuli

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Casmir Sumba Kyuki kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja (UTT AMIS) iliyo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango. Uteuzi wa Kyuki unaanza  July 11, 2018.

Kyuki ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria.

Viwanja Vimeshuka Bei: Mapinga (Baobab Sec).....Changamkia Fursa Hii

$
0
0

Viwanja viko Kimele, ni kilometa 3 kutoka main road (Bagamoyo Road). Viwanja viko planned (kwa mpangilio mzuri) na ukinunua unapimiwa ili upate hati kwa gharama ya sh 300,000 tu.
 
Bei ya viwanja inabadilika kuendana na size ya kiwanja ulichochagua.
 
Bei ni: milion 2 for 10/20, mil 3 for 15/20, mil 4 for 20/20, mil 5 for 25/20, mil 6 for 20/30, mil 8 for 20/40, mil 11 for 25/45, mil 12 for 30/40 na mil 16 for 40/40, mil 20 for 0.5acre, mil 38 for 1 acre. 

Ruksa kulipa kwa awamu ndani ya miezi 3-4. Hakuna dalali, mpigie mhusika; 0757489709

Polisi Ajiua kwa Kujipiga Risasi Kisa Wivu wa Mapenzi

$
0
0
Askari mwenye nambari G 3777 PC Nelson William, amejiua kwa kujipiga risasi katika eneo la kambi za jeshi la Polisi alipokuwa anaishi mkoani Mara kwa kile kilichosemekana kuwa ni wivu wa mapenzi.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoani ya Mara Juma Ndaki  amesema kuwa askari huyo amejipiga risasi jana saa 8:30 mchana akiwa eneo la kambi za Polisi alikokuwa anaishi, kutokana na kuwa na mgogoro na aliyekuwa mpenzi wake.

“Kabla ya kujipiga risasi ameacha ujumbe kuwa ameamua kujiua kutokana na wivu wa mapenzi kwa madai amekuwa hana mahusiano mazuri na mwanamke wake ambaye alikuwa ni mpenzi wake, ambaye hakuwa anaishi naye”, amesema Kamanda.

Kamanda Ndaki ameongeza kuwa  askari huyo kabla ya kuchukua uamuzi huo yaliibuka malumbano na mpenzi wake baada ya kwenda kwenye chumba cha mpenzi wake na kisha kuamua kuharibu mali alizomnunulia, baada ya kuharibiwa mali mwanamke aliamua kwenda kutoa taarifa Polisi, kitendo ambacho askari William hakikumfurahisha kwani aliona kama amedhalilishwa.

Kamanda amesema kuwa akaona njia pekee ni kuchukua uamuzi wa kujiua na ilipofika muda huo akaamua kujiua kwa kujipiga risasi, mwili wa askari huyo umehifadiwa chumba cha kuhifadhia maiti wakati taratibu za mazishi zikiendelea

Serikali Kufuta Tozo Ya Usajili,kuhuwisha Na Kushikilia Usajili Kwa Wawekezaji Wa Ndani

$
0
0
NA WAMJW-MWANZA
SERIKALI kupitia wizara ya afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto imefuta tozo ya usajili , kuhuwisha pamoja na kushikilia usajili wa bidhaa zao kwa wawekezaji wa ndani kupitia Mamlaka ya chakula na Dawa TFDA .

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati alipotembelea kuangalia ujenzi wa jengo la TFDA ambalo linajengwsa Jijini Mwanza ili kusogeza huduma kwa wananchi wa mkoa huo.

“Ili kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. John Pombe Magufuli za kukuza nchi kupitia uchumi wa viwanda hivyo TFDA msiwe kikwazo kwa wawekezaji hao hivyo kuanzia leo nafuta tozo za kusajili bidhaa,kuhuwisha bidhaa na tozo ya kushikilia usajili wa bidhaa”, alisema Waziri Ummy.

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa kuendana na juhudi hizo pia Serikali  imefuta tozo ya udhibiti ya thamani ya 0.25 za dawa,vifaa na vifaa tiba zinazoingizwa kwenye hospitali za Umma kutoka kwa wafadhili.

Mbali na hayo Waziri Ummy amesema kuwa TFDA ina wajibu wa kusimamia Tanzania isiwe jalala la bidhaa zisizo na ubora kwa watanzania hivyo wanatakiwa kuweka afya ya wananchi mbele kuliko manufaa binafsi.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Bi. Agness Kijo amesema kuwa ujenzi wa jengo hilo ukikamilika utasaidia kuhudumia huduma za kimaabara kwa bidhaa zinazoingia nchini kwani itakuwa sio lazima tena kwenda kupima bidhaa hizo jijini Dar es salaam.

“Maabara hizi zikikamilika zitasaidia kufanya vipimo na udhibiti wa bidhaa katika mipaka mingi ya kanda ya ziwa ikiwemo Silali,Lusumo na Mtukula ili kuweka usalama wa bidhaa zinazoingia na kutoka nje ya nchi kwa usalama wa wananchi.

Sambamba na hilo Waziri Ummy alipata nafasi ya kutembelea kukagua ujenzi wa jengo la wodi ya mama na mtoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou toure na kuhakikisha ujenzi unakamilisha ili kuokoa vifo vya mama na mtoto vinavyotokana na uzazi.

“Kama watu wa mwanza wanaridhishwa na huduma zinazotolewa katika hospitali hii basi ni lazima huduma za afya ziboreshwe ikiwemo afya ya mama na mtoto hivyo ninaleta mashine ya CT Scan kwa ajili ya kuboresha matibabu hapa” alisema Waziri Ummy.

Aidha Waziri Ummy aliwataka watendaji wa Hospitali  kutoa taarifa za utendaji kwa Waziri wa Afya na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo pamoja na kusimamiwa na Wakuu wa Mikoa yao ili kuimarisha huduma za afya nchini.

Machangudoa Watiwa Mbaroni Kwa Kuwauzia Ngono Wanafunzi

$
0
0
Jeshi  la Polisi mkoani Katavi limewakamata wanawake 14 wanaodaiwa kufanya biashara ya kuuza miili yao maarufu ‘madadapoa’ au  'Machangudoa', ambao inadaiwa wateja wao wakubwa wakiwa wanafunzi wa kiume wa sekondari.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Damas Nyanda, alisema watuhumiwa hao walikamatwa juzi usiku kufuatia msako uliofanyika katika Mtaa wa Majengo maarufu ‘Mtaa wa Fisi’ katika Mji wa Mpanda Manispaa ya Mpanda, huku akisisitiza msako huo ni endelevu.

Alibainisha kuwa msako huo ulifanyika katika madanguro matano na nyumba ya kulala wageni jirani na kituo cha mafuta cha Allyen katika Mji wa Mpanda.

Kamanda Nyanda alieleza kuwa madada hao kabla ya kupelekwa mahakamani, watachukuliwa alama za vidole vyao na kupigwa picha.

Alisema msako huo umefanywa kufuatia malalamiko ya wazazi kuwa wanafunzi wa kiume wa sekondari ni miongoni mwa wateja wa uhakika wa ‘madadapoa’ hao, huku wakionyesha wasiwasi wao wa uwezekano wa kupata maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU).

Taarifa za uhakika zinaeleza wengi wa ‘madadapoa’ hao wanatoka mikoa ya Tabora, Kigoma, Mbeya, Rukwa, Singida, Manyara, Arusha, Dodoma na mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Inadaiwa kuwa ‘dadapoa’ hao awali walikuwa wakifanya biashara hiyo ya kuuza miili yao katika machimbo ya madini ya dhahabu ya Isumamilolo mkoani Katavi, lakini baada ya dhahabu kupungua na biashara yao kudorora, waliamua kuvamia Mtaa wa Fisi na kuendelea na biashara ya kuuza miili yao.

Baadhi yao ambao wamenusurika kukamatwa wakati wa msako huo, walikiri kuwa wamepanga nyumba yote ambapo wanamlipa mmiliki nyumba Shilingi 6,000 kila siku kwa kila chumba, hivyo kwa mwezi kila chumba kinalipiwa Shilingi 180,000.

“Biashara ni nzuri inalipa sana kwani katika siku nzuri napata na kuwahudumia kingono wateja kati ya kumi hadi kumi na watano … wateja wetu wa kubwa ni wanafunzi wa sekondari na vijana wa kiume ambao wanachangamsha sana biashara,” alibainisha mmoja wao.

Peter Amtuhumu Muna Kwa Kusambaza Picha Zake Chafu Mtandaoni

$
0
0
Mzazi mwenza wa Muna anayejulikana kama Peter Zachariah amemjia juu mzazi mwenzake na kudai yeye ndiye mtu  aliyehusika kwa usambazaji wa picha zake Chafu Kwenye mitandao ya kijamii.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Peter alidai kuwa anajua wazi anayezisambaza picha hizo mitandaoni ni Muna kwa nia ya kumchafua kwa sababu Aprili, mwaka huu alirudi nyumbani kwake Mwananyamala-Kisiwani na kujifanya kuwa anapanga vitu vyake ndani ya nyumba hiyo kumbe nia ni kunasa picha hizo.
 
"Unajua chochote kinachoendelea hivi sasa najua wazi ni mpango wa Muna, anajitahidi kuufanya ili mimi nionekane wa ajabu baada ya kuona watu walivyonichukulia tofauti kwenye kipindi chote cha msiba wa mtoto wetu hivyo anataka kunichafua lakini mimi kwa hilo sitetereki“.

Peter amekiri alikuwa Kwenye Mahusiano na mwanamke huyo baada ya kuachana na Muna na kumtaja kwa jina la Rehema na kudai kuwa Muna anamfahamu mwanamke huyo.

"Kinachonishangaza mimi Muna anataka kujifanya huyo mwanamke ni mpya kwake lakini sio kabisa, anajua kila kitu na jinsi alivyokuwa akitangatanga kwa wanaume tofautitofauti, mimi ningeishi vipi kama mwanaume? Nafikiri anajua fika kwa kufanya hivyo atanichafua mimi kumbe anajichafua yeye”.

Mgogoro wa Muna na mumewe ulijulikana hadharani hivi karibuni mara baada ya mtoto wao kipenzi Patrick kufariki nchini Kenya alipokuwa amekwenda kutibiwa.

Mara baada ya Patrick kufariki, mjadala mzito uliibuka mitandaoni ambapo kuna baadhi walisema baba yake ni Mtangazaji wa Clouds TV, Casto Dickson aliyewahi kuwa mpenzi wa Muna lakini wengine wakasema ni wa Peter.

Muna alipotafutwa atoe neno kuhusu tuhuma hizo hakupatikana haraka. Siku chache zilizopita Muna alitangaza atafanya mkutano na waandishi wa habari na kujibu tuhuma zote.

Gigy Money: Mastaa Tuliobaki ni Mimi na Zari Tu....Wengine Hamna Kitu

$
0
0
Video vixen na Msanii wa muziki wa Bongo fleva Gift Stanford maarufu kama Gigy Money ameibuka na kudai staa pekee ambaye yupo kwenye level zake ni Baby mama wa Diamond Platnumz, Zari.

Gigy Money amefunguka hayo alipokuwa anaongelea trend yake ya kubadilisha Mawigi na mawiving siku za hivi karibuni.

Kwenye mahojiano na Kipindi cha The Playlist cha Times Fm, Gigy amedai yeye na Zari ndio mastaa pekee ambao wanabadilisha nywele kichwani na wengine wote wanakuwa na tabia ya kurudia rudia nywele kichwani.

"Yaani hao wanaojiita mastaa wengi Hawako katika level zangu maana sitaki kufanana nao ndio maana natumia pesa nyingi.

"Hata wewe ukifatilia utajua mademu wanaobadilisha nywele kuna Zari na Gigy na labda nimuweke Irene Uwoya lakini kwa kuwa na yeye ni mtu wa siku nyingi namtoa lakini kwa sasa hivi ni mimi na Zari tu na tunavaa human hair hatuvai plastiki kabisa”.

Lakini pia Gigy Money amedai yeye ni kivutio cha taifa hasa mwili wake umekuwa kivutio kwa wengi ndio maaana anapenda kuchezesha mwili wake na ku twerk Kwenye shoo zake.

Hamissa Mobetto na Ray C Ndani ya Bifu Zito

$
0
0
Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo fleva Rehema Chalamila maarufu kama Ray C amejikuta katikati ya bifu zito na mzazi mwenza wa Diamond Platnumz, Hamisa Mobetto.

Sintofahamu hiyo Ilianza siku mbili nyuma baada ya Ray C kuzisema nguo aina ya‘Fendi’ ni feki ambazo zimekuwa zikiuzwa sana na Hamisa ambaye ni mfanyabiashara ambapo Ray C alitoa kama maneno ya kejeli kuhusu nguo hizo ingawa hakutaja jina.
Basi Hamisa baada ya kuona kama Dongo lile katupiwa yeye basi moja kwa moja akaandika ujumbe ambao uliwakosoa watu ambao hawaonyeshi sapoti kwa biashara za wengine badala yake wanakuwa na wivu.
Baada ya sakata hilo na mashabiki wa Hamisa kumvamia Ray C basi aliweka wazi kuwa hakumtaja Hamisa jina kwa lile Dongo lakini baada ya kuona wanazidi ikabidi amvae Hamisa na kumsema kuhusu Zari na kudai yeye mwenyewe alimuumiza Zari kwa kitendo cha kuzaa na Diamond.

Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Upungufu Wa Nguvu Za Kiume, Maumbile Mdogo, Busha Bila Kupasua

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO : Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliohangaika sehemu mbalimbali bila mafanikio.

Mabula Clinic ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya jeshini. Je unaupungufu wa nguvu za kiume au uume wako mdogo na mwembamba? 

Mapro pawer no 2 ndio tiba, kwa sasa hutibu matatizo matatu kwa pamoja 1. itakufanya uchelewe kufika kileleni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2. Huimalisha misuli iliyolegea na kusinyaa hasa kwa wale walio athirika na upigaji punyeto 3. itakufanya upate hamu ya kurudia tendo zaidi ya mara tatu :Kwa nini ujione mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo 

Makakanua mix ni dawa iliyochanganywa na miti shamba 9 na kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 kwa urefu na unene sentimita 1-5, dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona

 Zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke kwa masaa matatu tu ,mvuto wa biashara, kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu.

Tunatibu ngiri, miguu, mgongo na kiuno kuumwa, kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa 

Tiba na ushauli muone Dr Mabula au piga simu no 0743362017.Huduma zangu utazipata popote ulipo kama uwezi kufika ofisini
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images