Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Upungufu Wa Nguvu Za Kiume, Maumbile Mdogo, Busha Bila Kupasua

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO : Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliohangaika sehemu mbalimbali bila mafanikio.

Mabula Clinic ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya jeshini. Je unaupungufu wa nguvu za kiume au uume wako mdogo na mwembamba? 

Mapro pawer no 2 ndio tiba, kwa sasa hutibu matatizo matatu kwa pamoja 1. itakufanya uchelewe kufika kileleni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2. Huimalisha misuli iliyolegea na kusinyaa hasa kwa wale walio athirika na upigaji punyeto 3. itakufanya upate hamu ya kurudia tendo zaidi ya mara tatu :Kwa nini ujione mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo 

Makakanua mix ni dawa iliyochanganywa na miti shamba 9 na kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 kwa urefu na unene sentimita 1-5, dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona

 Zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke kwa masaa matatu tu ,mvuto wa biashara, kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu.

Tunatibu ngiri, miguu, mgongo na kiuno kuumwa, kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa 

Tiba na ushauli muone Dr Mabula au piga simu no 0743362017.Huduma zangu utazipata popote ulipo kama uwezi kufika ofisini

Sister Fey :-Sijui Umri Wake Mimi Ninachojali Ananifurahisha na Yuko Vizuri

$
0
0
Msanii wa bongo music Sister Fey amefunguka na kuelezea mambo  anayokumbana nayo katika penzi lake jipya na msanii Holystar ambae ameanza kumuweka katika mitandao hivi karibuni.

Fey anasema kuwa video na picha ambazo zimekuwa zikisambaa katika mitandao alikuwa amezipost yeye mwenyewe ingawa mpenzi wake huyo alikuwa hataki kupost video na picha hizo  lakini yeye ndie aliamua kufanya hivyo baada ya kutukanwa na dada wa mpezi wake huyo.
 
Fey anasema kuwa watu  na ndugu wa mwanaume huyo wamekuwa wakimtukana kuwa  anatembea na ndugu yao mwenye umri mdogo lakini cha ajabu yeye hata umri wa mwanaume wake haujui anachojali ni raha anazopata tu.

"wanza kuhusu ile video mimi ndio nilikuwa nimemwambia kuwa dada ake amenitukana lakini akaniambai niache nisiseme kitu,niliipost mwenyewe maana yeye hata alikuwa hajapenda mimi nipost.Dada ake alinitukana kutokana na mambo ya watu ya kiswaili swahili.

"Dadaake anasema kuwa mdogo wake mdogo lakini mimi hata miaka yake sitaki kuijua na sioni udogo wake.... ana udogo gani sasa wakati mimi ananifurahsiha na yuko vizuri, hata sijui nimepishana nae miaka mingapi wala sijui ana umri gani."

Mke wa Ephraim Kibonde afariki dunia

$
0
0
Mke wa Mtangazaji wa Clouds FM katika kipindi cha Jahazi, Ephraim Kibonde anayejulikana kwa jina la Sara Kibonde amefariki dunia.

Kwa mujibu wa mtangazaji mwenzake, Gadner G. Habash amesema kuwa mke wa Kibonde aitwaye Sara amefariki usiku wa Jana akiwa anapatiwa matibabu katika hospitali ya Hindu Mandal.

Msanii maarufu nchini Kenya Alilia Penzi la Wema Sepetu

$
0
0
Msanii wa muziki maarufu nchini Kenya, Brown Mauzo ametangaza wazi kuwa kwa namna na hali yoyote ile yupo tayari kumuoa mrembo Wema Sepetu.

Brown amesema kuwa amekuwa akivutiwa sana na Wema Sepetu na yupo tayari muda wowote kumuoa mrembo huyo hata kama ikibidi awe spea tairi.

Akifunguka kupitia kipindi cha eNEWS cha EATV Brown amesema; “Mimi namzimia sana Wema Sepetu kwa bahati mbaya sijawahi kuonana naye namzimiaga sana.

"Kila mtu anasema ukweli kutoka moyoni kila shetani na mbuyu wake. Licha ya kwamba alikuwa na nani sijui na nani ila mimi nipo tayari kumuoa, na popote atakapokuwa namwambia mimi nampenda na nataka kumuoa.. hata kama akiwa na mtu mwingine mimi nipo tayari hata niwe spea tairi,”.

Kwa upande mwingine Brown amesema kuwa Wema Sepetu ni mwanamke mwenye sifa zote anazozitaka na ikiwezekana hata kesho yeye yupo tayari kufunga naye ndoa.

Brown Mauzo alishawahi kufanya ngoma na Alikiba iliyokwenda kwa jina la Nitulize na kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ya Zagada.

Gigy Money afunguka kuwa ndoto yake kwa sasa ni kuzaa na Diamond pamoja na Idriss

$
0
0
Mwanadada Gigy Money ambae kila siku huwa huwa haishiwi vituko  amefunguka na kusema kuwa katika maisha yake ya sasa anatamani sana kuzaa na msanii Diamond Platnumz au Idriss Sultan kwa kuwa ni wanaume warefu na yeye anependa wanaume warefu, hivyo anaamini akizaa nao atapata watoto wazuri zaidi.

Gigy amefunguka hayo katika interview  ya kipindi cha The Play List kinachorushwa na TimesFM

"Natamnai kupata mtoto na Idris na Diamond kwa sababu naamini mtoto atakuwa mzuri kweli kweli , mimi ninapenda sana wanaume warefu kwakweli .Lakini pia siwezi kuwa kwenye mahusiano na Nay wa mitego."

Shamsa Ford: Vijana Wengi wa Dar ni Chawa, Wambeya, Wapambe, Vibenten

$
0
0
Msanii wa filamu Shamsa Ford ambaye ni mama wa mtoto mmoja, amedai vijana wengi wa Dar es salaam ni chawa, wambea na vibenten kwa kuwa walikosa elimu ambazo zingewawezesha kwenda kushindana kwenye soko la ajira.

Muigizaji huyo amedai mwanaume anatakiwa kuwa na misimamo na muonekano wa kiheshima katika jamii na sio kuonekana wakifanya mambo ya ajabu. 

“Wanawake wenzangu tujitahidi sana kuwapa elimu ya kutosha watoto wetu wote haswa watoto wa kiume. 

"Nimejikuta kuwa na huruma zaidi na watoto wa kiume kwasababu wa kwangu ni wa kiume. Huwa naumia sana nikiona mtoto wa kiume anavyohangaika kupata riziki,” aliandika Shamsa Ford kupitia Instagram yake.

Aliongeza, “Mtoto wa kiume asipokuwa na elimu ya kutosha au ujuzi wowote mwisho wao huwa ni mbaya kuliko watoto wa kike. 

"Sasa hivi vijana wengi ambao hawana kazi au hawakubahatika kusoma ndo WAMBEA,WAPAMBE,VIBENTEN MARA CHAWAAA” 

Muigizaji huyo ameongeza kwa kusema atahakikisha kwa upande wake anatimiza majuku yake ipasavyo ili mtoto wake asiingie kwenye makundi hayo. 

"“Kuwa mwanaume ni heshima kubwa sana kama ukisimama kwenye misingi ya kiume..Nitauza vitumbua, madira hata kufagia barabara ilimradi mwanangu apate elimu,” alisema Shamsa.

Kelechi: Brown Hana Hadhi Ya Kutembea na Wema Sepetu

$
0
0
Msanii wa muziki anayefanya kazi zake  Mombasa Kenya, Kelechi amefunguka na kudai msanii mwenzake Brown Mauzo hawezi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Wema Sepetu.

Brown Mauzo ameibuka  na kufunguka juu ya mapenzi yake kwa msanii wa filamu Tanzania Wema Sepetu na kudai anataka kumuoa jumla jumla.
 
Kwenye mahojiano na Enews ya East Africa Tv, Kelechi amefunguka na kudai Brown hawezi kumuoa Wema Sepetu wala hata kumuhudumia hawezi:

"Huyu Brown ni mtoto mdogo sana hawezi kumpata Wema Sepetu alafu isitoshe ni Dogo sana kwa Wema na pia hana hata hadhi ya kuwa  naye kimapenzi”.

Lakini pia Kelechi amedai Brown amekimbia Mombasa na kurudi Tanzania baada ya kutembea na mke wa Meneja wake.

TWAWEZA Walimwa Barua Kwa Kutoa Utafiti Bila Kibali cha Costech

$
0
0
Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech) imeitaka Taasisi ya Twaweza kujieleza ndani ya siku saba kwa nini isichukuliwe hatua za kisheria kwa kosa la kutoa matokeo ya utafiti bila ruhusa.

Barua hiyo ya Costech imesema, Twaweza waliomba kibali cha tafiti nne ambazo mmoja umekamilika na nyingine tatu bado zinaendelea.

Kwa mujibu wa barua hiyo iliyosambaa mitandaoni ikionyesha imesainiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Costech, Dk Amos Nungu, tume hiyo ndiyo yenye mamlaka ya kusajili na kutoa kibali cha tafiti zote za muda mfupi na mrefu zinazofanywa nchini.

Barua hiyo imedai kuwa mwishoni mwa wiki, kulikuwa na taarifa za Twaweza kutoa utafiti uliopewa jina la ‘Sauti za Wananchi’  ambao, tume haina rekodi zilizoruhusu kuchapishwa kinyume cha sheria.

“Kwa mujibu wa kifungu cha sheria namba 7 cha mwaka 1986, tume hiyo ndiyo yenye mamlaka kusajili na kutoa kibali cha kufanyika tafiti nchini,” imesema barua hiyo.

Taarifa kutoka Twaweza zinathibitisha taasisi hiyo kupokea barua kutoka Costech na kwamba wanaifanyia kazi.

Hivi karibuni Twaweza walitoa ripoti ya utafiti wa ‘Sauti za Wananchi’ ukielezea maoni ya wananchi kuhusu siasa nchini.

Utafiti huo umeonyesha kuporomoka kwa ukaribu wa wananchi na vyama vya siasa, utekelezaji wa majukumu kwa viongozi walioko madarakani, Rais anavyotekeleza majukumu yake tangu alipoingia madarakani na uhuru wa kujieleza katika baadhi ya maeneo.

Ambulance ya Serikali Yakamatwa na Shehena ya Mirungi

$
0
0
Gari la kubeba wagonjwa (ambulance) la Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Mara, limekamatwa likiwa na shehena ya dawa za kulevya aina ya mirungi.

Akizungumzia tukio hilo leo, Julai 11, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima amesema gari hilo lilikamatwa jana Julai 10, wilayani Bunda.

"Dereva wa gari hilo aliitwa kwa ajili ya kufanya kazi ya kubeba mgonjwa usiku wa jana lakini alisema yupo mbali na gari halina mafuta,” amesema Malima.

Malima amesema dereva huyo alitakiwa kumsafirisha mgonjwa kutoka Hospitali ya Wilaya ya Tarime kwenda Hospitali ya Rufaa ya Bugando.

Akifafanua zaidi Malima amesema baada ya dereva kutoa udhuru, mgonjwa aliyehitaji huduma ya rufaa alisafirishwa kwa kutumia gari la polisi.

“Lakini gari la polisi likiwa njiani kuelekea jijini Mwanza, waliokuwamo ndani ya gari hilo waliiona ‘ambulance’ inayodaiwa kutokuwa na mafuta ikiwa eneo la Bunda.”

"Askari polisi na maofisa wengine waliokuwamo kwenye gari la polisi walilazimika kulisimamisha lile gari la wagonjwa kujua lilikotoka na linakoelekea ndipo wakamkuta dereva ambaye awali alidai gari halina mafuta ndipo walipokuta limesheheni shehena la mirungi,” amesema

Amesema dereva yule hakuwa na la kujitetea ndipo alipotiwa mbaroni na anaendelea kushikiliwa kwa mahojiano,"

Mkuu huyo wa mkoa amesema taarifa zaidi kuhusu tukio hilo la aina yake kuwahi kutokea mkoani Mara zitatolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Tarime/Rorya, Henry Mwaibambe.

Rais Magufuli Akutana Na Kuagana Na Mabalozi Watatu Waliomaliza Muda Wao Hapa Nchini

$
0
0
Rais Dkt. John Magufuli amewasihi Mabalozi watatu waliomaliza muda wao wa kuziwakilisha nchi zao hapa nchini Tanzania wawaeleze watakaokuja kuchukua nafasi hizo kuendeleza ushirikiano mzuri uliopo baina ya nchi hizo na Tanzania.

Dkt. Magufuli ametoa kauli hiyo leo Julai 11, 2018 wakati akiagana na Balozi Hawa Olga Ndilowe – Balozi wa Malawi nchini Tanzania, Mhe. Katarina Rangnitt – Balozi wa Sweden nchini Tanzania pamoja na Mhe. Hanne-Marie Kaarstad – Balozi wa Norway nchini Tanzania, Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuwashukuru kwa kazi nzuri walizozifanya katika kipindi walichoziwakilisha nchi zao hapa nchini.

"Natambua mchango mkubwa ambao nchi hizo zinautoa kwa maendeleo ya Tanzania, na niwasihi muwaeleze Mabalozi watakaokuja kuchukua nafasi zenu kuendeleza ushirikiano  mzuri uliopo kati ya nchi hizo na Tanzania na dhamira ya serikali ya awamu ya tano ya kuhakikisha uhusiano huo unakuzwa kwa kujikita zaidi katika diplomasia ya uchumi", amesema Dkt. Magufuli.

Kwa upande wao Mabalozi hao kwa pamoja wamempongeza Rais Magufuli kwa juhudi kubwa alizozifanya katika kuimarisha mapambano dhidi ya rushwa, kusimamia rasilimali za Taifa, kutekeleza miradi mikubwa ya kukuza uchumi na kuvutia uwekezaji kupitia kupitia mwongozo wa uwekezaji 'blue print' ambao umelenga kuondoa kero zinazowakabili wawekezaji.

Kwa upande mwingine, Mabalozi hao wamemuahidi Rais Magufuli kuwa watakuwa mabalozi wazuri wa kuinadi Tanzania katika nchi zao ili kukuza uwekezaji, biashara, utalii na ushirikiano utakaokuwa chachu ya manufaa kwa Tanzania na nchi hizo.

Dk. Kigwangalla Aagiza Kukamatwa Mkuu Wa Kanda Pori La Akiba Rukwa, Amsimamisha Kazi Meneja Wa TFS

$
0
0
Na Mwandishi Maalum, Mlele Katavi
....................................................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla ameliagiza Jeshi la Polisi mkoani Katavi kumkamata na kumfungulia mashtaka Mkuu wa Kanda - Pori la Akiba Rukwa, Emannuel Barabara kufuatia tuhuma za uhujumu uchumi zinazomkabili.

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni miezi mitatu tangu alipomsimamisha kazi kupisha uchunguzi wa tuhuma hizo ambazo amesema tayari zimethibitishwa kupitia taarifa mbalimbali za kiuchunguzi.

Waziri Kigwangalla ametoa agizo hilo jana muda mfupi baada ya kupokea taarifa ya Wilaya ya Mlele iliyowasilishwa kwake na Mkuu wa Wilaya hiyo, Rachel Kasanda  wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja wilayani humo.

Amesema Barabara anatuhumiwa kwa vitendo vya uhujumu uchumi kwa kushindwa kutimiza majukumu yake ipasavyo pamoja na kushirikiana na majangili kuruhusu uvunaji holela wa raslilimali za misitu ndani ya pori hilo kwa maslahi yao binafsi.

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Mlele, Rachel Kasanda alisema katika kipindi cha mwezi Desemba 2017 hadi Februari 2018 kamati yake ya ulinzi na usalama ilipata taarifa za uvamizi mkubwa katika Pori la Akiba Rukwa ambapo iliamua kufanya operesheni maalum iliyosaidia kukamata watu 22 waliokuwa wakichana mbao na kukamata mbao 5,122, slipa 924 na magogo 188.

Alisema kwa kiasi kikubwa uhalifu huo ulichangiwa na ndugu Barabara ambaye hakutaka kuweka wazi uhalifu uliokuwa ukifanyika ndani ya pori hilo kwa kamati yake ya ulinzi na usalama na badala yake aliiaminisha kuwa mambo ni shwari ndani ya pori hilo.

Halikadhalika, Dk. Kigwangalla ameagiza maofisa na askari wote 34 wa Pori la Akiba Rukwa kurudishwa makao makuu ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) ili kupangiwa kazi nyingine, ambapo kabla ya zoezi hilo ameagiza wahojiwe na TAKUKURU kuhusu mwenendo wa vitendo vya Mkuu wa Kanda hiyo, Emmanuel barabara na endapo nao watathibitika kuhusika wafunguliwe mashtaka ya kushirikiana nae katika tuhuma zinazomkabili.

Wakati huohuo Waziri Kigwangalla amemsimamisha kazi, Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu wa wilaya ya Mlele, Ezeckiel Mbilinyi na  watumishi wengine watatu kwa kile alichokieleza kuwa ni uzembe wa kushindwa kusimamia vizuri rasilimali za misitu wilayani humo sambamba na tuhuma za kushirikiana na ndugu Emmanuel Barabara kuhujumu rasilimali za misitu kwa kutoa vibali na kugonga nyundo (mihuri) rasilimali hizo zilizokuwa zikivunwa kinyume cha sheria kwenye maeneo ya hifadhi.

Kufuatia uamuzi huo, Dk. Kigwangalla ametangaza kusimamisha zoezi la utoaji wa vibali vipya vya uvunaji na usafirishaji wa mbao na magogo kwa mikoa ya kanda ya magharibi ikiwemo Katavi na Tabora kwa kipindi cha miezi mitatu mpaka hapo utaratibu mzuri utakapowekwa wa kudhibiti uvunaji wa rasilimali hiyo kwenye maeneo ambayo hayaruhusiwi kisheria.

Aidha ameiagiza Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya Mlele kufanya uhakiki wa vibali vya uvunaji wa mbao na magogo ambavyo vimeshatolewa ili kujiridhisha juu ya uhalali wake kabla ya kutoa vibali vya usafirishaji.

ACT-Wazalendo Waitaka Serikali Isitumie Mabavu Kudhibiti Tafiti Zinazofanywa Nchini

$
0
0
 Chama cha ACT Wazalendo kimeitaka Serikali kutotumia mabavu kudhibiti tafiti zinazofanyika nchini badala yake itoke hadharani na kujibu hoja zinazoibuliwa.

Chama hicho kimetoa tamko hilo leo Julai 11 baada ya kuiona barua mitandaoni iliyoandikwa na Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech) ikiitaka Taasisi ya Utafiti ya Twaweza kujieleza kwa nini wasiadhibiwe kwa kufanya utafiti bila kupata kibali chao.

Akizungumza na vyombo vya habari leo Julai 11 jijini Dar es Salaam, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano, Ado Shaibu amesema ni aibu kwa serikali kudhibiti mpaka shughuli za utafiti.

"Kama barua hiyo ni ya kweli, basi ni aibu kubwa kwa Serikali kudhibiti utafiti. Tutasimama imara kulinda na kutetea hadhi ya utafiti ili mradi utafiti huo uwe unakidhi vigezo," amesema Shaibu.

Amesema Serikali isiogope mapambano ya hoja kwa sababu ina watu wengi wanaoweza kuzungumza na kutetea hoja badala ya kutumia mabavu na kutaka kuiadhibu Twaweza kwa kufanya utafiti wa Sauti za Wananchi.

Amefafanua kwamba kwa miaka mingi Twaweza wamekuwa wakifanya tafiti na Costech walikuwepo, lakini kwa sababu utafiti wao wa hivi karibuni umeigusa Serikali, wamejitokeza wakisema hawajafuata taratibu.

"Ninavyofahamu mimi, taasisi yoyote ikitaka kufanya utafiti lazima iwasiliane kwanza na NBS (Ofisi ya Taifa ya Takwimu). Ni jambo la kushangaza kama utafiti hauwezi kufanyika kama haujapata approval ya Costech, suala hili linaibua mjadala," amesema katibu huyo.

Kuhusu uchaguzi mdogo wa Agosti mwaka huu, Shaibu amesema kamati kuu ya ACT Wazalendo imeamua kushiriki kwenye uchaguzi huo kwenye nafasi mbalimbali.

Hata hivyo, amesema wameunda kamati maalumu ya mashauriano itakayoongozwa na Omary Shaibu Shaaban ili kushauriana na vyama vingine juu ya kusimamisha mgombea mmoja kwenye maeneo ya kimkakati.

Wadau Waipongeza Serikali Kuondoa Vat Kwenye Taulo Za Kike

$
0
0
Wadau mbalimbali wa bidhaa za taulo za kike, (pedi), wameipongeza hatua ya serikali kupunguza Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT),  kwa bidhaa hiyo kwa asilimia 18.

Wakizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Jumatano Julai 11, wadau hao wamesema kitendo cha kushuka kwa kodi hiyo kimewafanya wapunguze bei ya taulo hizo.

“Baada ya kusikia serikali imepunguza kodi ya VAT kwa asilimia 18, tumeamua kupunguza bei ya bidhaa za taulo ya kike kwa gharama ya Sh 59,000 kutoka Sh 65000 Kwa bei ya jumla,” amesema Meneja Mkuu wa Kampuni ya NN General Supplies Vumilia Tomito inayosambaza pedi aina ya HQ.

Aidha, amesema kutokana na hali hiyo, bei ya reja reja ya bidhaa hiyo itakua Sh 2,800 kutoka Sh 3,500 kwenye maduka mbalimbali nchini.

“Kwa sasa kampuni yetu iko kwenye mchakato wa ujenzi wa kiwanda cha pedi mara baada ya kukamilika kwa mazungunzo na serikali,” amesema.

Serikali Yafanya Marekebisho Ya Ramani Ya Ardhi Lindi

$
0
0
Serikali imesema imefanya marekebisho ya ramani ya mwaka 2007 ya Wilaya ya Liwale ili kumaliza mgogoro wa ardhi uliopo katika Kijiji cha Mirui na Nanjilinji A kilichopo wilaya ya Kilwa mkoani Lindi.

Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amesema hayo jana kwenye mkutano wa hadhara aliyoifanya katika vijiji hivyo ambapo pamoja na mambo mengine amesema ramani itakayotumika katika kuonyesha mipaka ya vijiji hivyo ni ya mwaka 1947.

“Ramani hiyo ni ile inayoonyesha mpaka unaanzia Mlima wa Nandanga kuelekea Mlima wa Nakman na kwenda kukutana na Mto Mbwenkuru na Mto Kipelele inapoanzia Wilaya za Kilwa na Liwale.

“Hii inatokana na timu ya wataalam kubaini kuwapo na muingiliano wa mipaka baina ya vijiji hivyo viwili,” amesema Lukuvi.

Aidha, amemsema nyaraka zilizotumika katika uanzishwaji wa wilaya hizo kwa kutumia GN91 ya tarehe 16/05/1947 inaonyesha Wilaya ya Liwale inapakana na Wilaya ya Nachingwea kabla ya Novemba 13, mwaka 1980 kuigawa Wilaya hiyo ya Nachingwea na kupata Wilaya ya Liwale ambapo ugawaji wa Wilaya hiyo haukuathiri mipaka ya awali ya Nachingwea na Kilwa.

TRA Yatangaza Msamaha Wa Madeni Ya Riba Na Adhabu Kodi Za Nyuma

$
0
0
Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA imetangaza msamaha wa riba na adhabu za madeni ya nyuma ya Kodi hadi asilimia mia moja ili kutoa unafuu kwa walipakodi wenye malimbikizo kulipa kodi ya msingi tu yaani “Principal Tax”

Akitangaza msamaha huo, Kamishna Mkuu wa TRA Charles Kichere amewaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuwa msamaha huo ni matokea ya utekelezaji  Maelekezo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli katika Mkutano wa Baraza la Wafanyabiashara (TNBC) uliofanyika Ikulu tarehe 20/03/2018 ambapo wafanyabiashara walilalamikia kuwepo kwa malimbikizo makubwa ya madeni ya kodi za nyuma yakijumuisha riba na adhabu,

Kichere amesema kuwa, ili kukamilisha hilo, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limefanya marekebisho kupitia Sheria ya Fedha ya mwaka 2018 na sehemu ya Sheria ya Usimamizi wa Kodi ya Mwaka 2015.

“Katika marekebisho hayo Waziri mwenye dhamana ya Fedha na Mipango amepewa mamlaka ya kutoa utaratibu maalum wa kuwezesha Kamishna Mkuu kutoa msamaha riba na adhabu wa hadi asmilia mia moja riba na adhabu kwenye malimbikizo ya madeni ya kodi kwa asilimia mia moja tofauti na asilimia 50 ya hapo awali”, amesema.

Aidha, amebainisha kuwa lengo kuu la msamaha huu ni kutoa unafuu kwa walipakodi wenye malimbikizo ya madeni ya riba na adhabu kwa kuwapa fursa ya kulipa malimbikizo ya madeni ya msingi ya kodi “Principal Tax” kwa awamu ndani ya mwaka wa fedha 2018/19 ili kuwapa motisha ya kulipa kodi kwa hiyari na kwa Wakati.

Amesema kuwa msamaha wa riba na adhabu utahusu kodi zotezinazotozwa kwa mujibu wa Sheria zinazosimamiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania, isipokuwa: Ushuru wa Forodha unaosimamiwa chini ya Sheria ya Ushuru wa Forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya mwaka 2004; na malipo  mengine yasiyo ya kodi ambayo TRA imepewa jukumu la kisheria la kuyakusanya. Mapato hayo ni kama vile: Kodi za Majengo na Ada za Matangazo.

Hata hivyo, Kamishna Mkuu wa TRA amesema kuwa watakaonufaika na utaratibu huu watatakiwa kuwa na sifa zifuatazo: Wawe wamewasilisha ritani za kodi lakini bado wanadaiwa kodi yote au sehemu ya kodi zitokanazo na ritani hizo; Hawajawasilisha ritani za kodi na wana madeni ya kodi; Ambao walikuwa wanafanyabiashara bila kusjiliwa na kupatiwa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN), namba ya usajili wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VRN) au usajili mwingine wa kodi kwa mujibu wa sheria zinazosimamiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania;

Sifa nyingine ni wawe wamewasilisha pingamizi za kodi kwa Kamishna Mkuu na ambao pingamizi zao bado zinashughulikiwa katika ofisi za Mamlaka ya Mapato na sio kwenye mahakama za kikodi;  Ambao wamewasilisha pingamizi katika mahakama za kikodi na mashauri yao bado hayajatolewa maamuzi na wale ambao  wana madeni ya nyuma ya kodi ambayo hayatokani na kesi za jinai za kodi, utakatishaji Fedha, Usafirishaji wa binadamu au shughuli nyingine haramu.

Aidha, Mlipakodi atastahili kupata msamaha wa riba na adhabu endapo yeye binafsi au mwakilishi wake aliyeidhinishwa kisheria atawasilisha maombi ya msamaha kwa kujaza Fomu maalumu Na.ITX207.01.E  inayopatikana katika tovuti ya TRA ikiambatana na; Maelezo ya kuonyesha kiasi anachodaiwa pamoja nakukubali kwa hiyari kulipa deni lake la msingi “Principal Tax”  

Kukubali kwa maandishi kulipa kiasi chote cha kodi bila riba na adhabu ndani ya mwaka wa fedha 2018/2019 ikiwa na maana kabla au ifikapo tarehe 30 Juni 2019; na Kwa madeni yaliyo katika pingamizi; kukubali deni la kodi alilokadiriwa na kuwa tayari kutoendelea na pingamizi au shauri husika la kodi lililowasilishwa kwa Kamishna Mkuu, Bodi ya Rufani za Kodi au Mahakama ya Rufaa.

Hata hivyo, msamaha utatolewa kwa maombi yatakayokidhi masharti na kukubaliwa na Mamlaka ya Mapato ambapo Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania na Mlipakodi husika watasaini mkataba wa makubaliano utakaoanisha deni lote la kodi; riba na adhabu inayosamehewa, pamoja na kodi isiyo na riba wala adhabu itakayopaswa kulipwa kabla ya tarehe 30 Juni, 2019.

TRA inawahimiza walipakodi wote nchini kutumia fursa hii adhimu kwa kushiriki kikamilifu katika zoezi hili maalum la utoaji wa msamaha wa riba na adhabu na kwamba utoaji  wa taarifa sizizo sahihi ni kosa kisheria, endapo itabainika hivyo itapelekea muombajikupoteza sifa ya kufaidika na msamaha huu

Kangi Lugola aagiza askari wenye sifa kupandishwa vyeo

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amemwagiza Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu kuandaa mapendekezo ya kuwapandisha vyeo askari wote wenye sifa.

Ameagiza mapendekezo hayo yakamilike  ndani ya Julai ili kuwasaidia  askari wenye sifa na ambao wamekaa muda mrefu bila kupandishwa vyeo.

Lugola  ametoa agizo hilo leo Julai 11 alipotembelea Gereza la Ukonga  na kuzungumza na maofisa na askari wa magereza kutoka vituo mbalimbali vya Mkoa wa Dar es Salaam.

Amesema tayari ameshakula kiapo cha kuwa mwenyekiti wa tume ya magereza na polisi ambayo ina kazi mbalimbali ikiwamo kuwapandisha vyeo askari.

Amesema viongozi wenye chuki binafsi na askari watakaokataa kutoa mapendekezo kwa askari wenye sifa za kupanda vyeo wakati wana sifa hatawavumilia.

“Sitokubaliana na hali hii.  Nataka nidhamu na hali itendeke kwa askari wote wenye sifa za kupanda vyeo. Naomba kwenye mchakato wa mapendekezo kwa askari wenye sifa hali itendeke, atakeyefanya kinyume atakiona cha mtema kuni," amesema Lugola.

Lugola ambaye pia mbunge wa Mwibara amewataka askari magereza kufanya kazi kwa bidii na weledi na kukaa mkao wa kula wa kupanda vyeo siku zijazo

Mbali na hilo, Lugola amemuagiza pia katibu mkuu huyo kuhakikisha ifikapo mwishoni mwa Agosti askari wote wanalipwa mishahara stahiki kulingana na utendaji wao.

"Sitaki kuona askari analipwa mshahara tofauti, wakati anastahili kulipwa kulingana na utendaji kazi wake. Askari ambao mishahara yao haijarekebishwa naomba orodha yao pia," amesema.

Pia, amemtaka Kamishna Jenerali wa Magereza, Dk Juma Malewa kuandaa orodha hiyo na sababu za askari hao kutorekebishiwa mishahara yao ili aweze kulitatua.

Ushahidi wa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Ilala (RCO) Katika Kesi ya Halima Mdee Dhidi ya Rais Magufuli

$
0
0
Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Ilala (RCO), Davis Msangi ameileleza mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu  kuwa hajawahi kumuhoji Rais John Magufuli jinsi anavyojisikia kuhusu maneno yaliyotamkwa na mbunge wa Kawe Halima Mdee dhidi yake.

RCO Msangi ameyaeleza hayo wakati akitoa ushahidi wake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wakati alipohojiwa na Wakili wa Mdee, Peter Kibatala.

Akimuhoji shahidi huyo Wakili Kibatala alimuuliza Msangi kuwa anamfahamu John Magufuli na anaishi wapi….? alijibu kuwa anaishi Ikulu.

Pia wakili Kibatala alimuuliza shahidi huyo kuwa uliwahi kwenda kumuhoji jinsi anavyojisikia kuhusu maneno yanayodaiwa kutamkwa na Mdee kwa sababu yeye ndiyo muhanga.

RCO Msangi alijibu kuwa hajawahi kwenda kumuhoji wala hakutumia taratibu zozote za kumuhoji.

Pia RCO Msangi amedai kuwa hafahamu msimamo wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusiana na kauli ya Rais Magufuli kuhusu watoto wa kike waliopata mimba shule wasirudishwe shule.

Pia RCO Msangi alipoulizwa kwamba Mdee alikaa muda gani chini ya ulinzi, amedai kuwa sio kwa zaidi ya Saa 48, ambapo alifikishwa Polisi July 4,2018 ila tarehe kuondoka haijui.

Baada ya shahidi huyo kumaliza kuhojiwa na Wakili Kibatala, Hakimu Simba amesema kesi hiyo imeshatimiza mwaka mmoja na ilipaswa iwe ishatolewa hukumu, ambapo ameahirisha kesi hiyo hadi August 7 na 8, 2018 ili kuendelea na ushahidi.

Katika kesi hiyo Mdee anadaiwa July1 3,2017 katika Makao Makuu ya Ofisi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) iliyopo mtaa wa Ufipa wilaya ya Kinondoni ni kuwa Rais John Magufuli “anaongea hovyohovyo , anatakiwa afungwe breki” na kwamba kitendo ambacho kingeweza kusababisha uvunjifu wa Amani.

Kangi Lugola Kapiga Biti Zito Gereza Lolote Litakaloruhusu Simu na Madawa Kuingizwa Kwa Wafungwa

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amesema gereza litakalobainika kuingiza vitu visivyoruhusiwa ikiwamo simu, mkuu wa gereza hilo atakamatwa na kuwekwa ndani.

Lugola ametoa kauli hiyo leo, Jumatano Julai 11, 2018 wakati alipotembelea gereza la Ukonga na kuzungumza na maofisa na askari wa jeshi hilo.

Amesema matukio ya uingizaji wa simu na dawa yamekithiri katika magereza mbalimbali likiwamo la Ukonga na kwamba hatakubali kuona suala hilo likiendelea.

"Tutamweka ndani mkuu wa gereza husika na wale askari walioko zamu wakati vitu hivyo vinaingia watakuwa katika wakati mgumu sana.Watapata misukosuko,"amesema Lugola.

Lugola ambaye pia ni askari polisi mstaafu amesema haingii akilini wafungwa kufanya mawasiliano wakiwa gerezani.

Amesema wafungwa hao wamekuwa wakishirikiana na askari wasiowaaminifu katika mchakato huo wa mawasiliano.

“Sitakubali hali hii iendelee nitakuwa mkali sana.Kabla sijatumbuliwa na rais nitahakikisha wewe wa chini yangu utumbo uko nje ili nipate cha kujitetea, nataka kila abiria abebe mzigo wake,"amesema Lugola.

Ameongeza kuwa Rais John Magufuli amechoshwa kusikia taarifa za uingizaji wa vitu visivyoruhusiwa hasa simu kwenye magereza.

Awali akimkaribisha Lugola Kamishna Jenerali wa Magereza Dk Juma Malewa alimpongeza waziri huyo kwa uteuzi na kuahidi kuwa jeshi hilo lipo litampa ushirikiano wa kutosha katika utekelezaji wa majukumu yake.

Mhasibu Mkuu Bodi ya Pamba Afikishwa Mahakamani Kwa Makosa ya Uhujumu Uchumi

$
0
0
Mhasibu Mkuu wa Bodi ya Pamba Tanzania, Simon Maganga amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na makosa 6 ikiwemo uhujumu uchumi wa kuisababishia Serikali hasara ya Sh.Milioni 55.6

Katika makosa hayo, mashtaka 4 ni matumizi mabaya ya nyaraka kwa lengo la kumdanganya mwajiri, shtaka la ufujaji, ubadhilifu na uhujumu uchumi kusababisha hasara.

Akimsomea hati ya mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, wakili wa TAKUKURU, Maxi Ali amedai mshtakiwa ametenda makosa hayo kwa nyakati tofauti.

Miongoni mwa mashtaka hayo anadaiwa kati ya January Mosi, 2009 na December 31, 2010 katika ofisi ya Bodi ya Pamba Tanzania iliyopo Wilaya ya Ilala kwa cheo Mhasibu Mkuu, alimdanganya mwajiri wake kuwa alitumia vocha za kuwasilisha mbegu za Pamba msimu wa 2009/2010 akijaribu kuonesha kampuni ya Afrisian Ginning Ltd ilinunua mbegu za Pamba kilo  25,129,258k wakati akijua kuwa si kweli.

Pia alimdanganya tena mawajili wake kwamba alitumia vocha za kuwasilisha mbegu za Pamba msimu wa mwaka 2009/2010 akijaribu kuonesha kampuni ya Nyanza Cooperative Ltd ilinunua Kilo 3,708,998 za mbegu za Pamba wakati akijua si kweli.

Katika kosa jingine anadaiwa kutumia vocha za kuwasilisha mbegu za Pamba msimu wa mwaka 2009/2010 akijaribu kuonesha kampuni ya kampuni ya S&C Ginning Ltd  ilinunua kilo 17,152,590 za mbegu za Pamba wakati akijua si kweli.

Pia anadaiwa kutumia vocha za kuwasilisha mbegu za Pamba msimu wa mwaka 2009/2010 akijaribu kuonesha kampuni ya kampuni ya Kahama Oil Mill Ltd ilinunua 16,326,038  za mbegu za Pamba wakati akijua si kweli.

Katika shtaka la tano anadaiwa, akiwa katika ofisi ya bodi ya Pamba Tanzania, alifanya ufujaji na ubadhilifu wa Shilingi Milioni 55,637,680.

Mshtakiwa Maganga anadaiwa kuwa kati ya January Mosi, 2009 na December 31,2010 kwa makusudi aliisababishia mamlaka hiyo hasara ya Sh.Mil 55,637,680.

Mshtakiwa amekana kujibu mashtaka hayo baada ya kuruhusiwa kujibu mashtaka hayo kwa sababu Mkurugenzi wa Mashtaka DPP aliwasilisha kibali cha kuipa ridhaa mahakama hiyo kuisikiliza kesi hiyo.

Kufuatia kibali hicho, mahakama imemsomea mshtakiwa masharti ya dhamana ambapo imemtaka kuwa na wadhamini wakili kila mmoja akitakiwa kuwa na barua na nakala ya vitambulisho ambapo kila mmoja atatakiwa kusaini bondi ya Sh, Milioni 28.

Aidha mdhamini mmojawapo ametakiwa kuwasilisha fedha Sh. Milioni 28 ama hati ya Mali isiyohamishika yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha pamoja na hati yake ya kusafilia. Kesi imeahirishwa hadi July 24,2018.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya July 12

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images