Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

COSTECH yasikitishwa na uamuzi wa TWAWEZA Kuisambaza Barua Mitandaoni

$
0
0
Wakati taasisi ya TWAWEZA ikipewa siku saba kujieleza ni kwanini isichukuliwe hatua za kisheria kwa kutoa matokeo ya utafiti bila ruhusa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), imesema kuwa imesikitishwa na kusambaa kwa barua hiyo mtandaoni.

Mara baada ya kusambaa kwa barua ya TWAWEZA iliyoandikwa kutokea COSTECH, Kaimu Mkurugenzi wa tume hiyo Dkt. Amos Nungu amesema kuwa baada ya kufuatilia barua hiyo waligundua kuwa ni yao.

“Baadaya kufanya uchunguzi tuligundua kuwa barua inayosambaa mitandaoni ni yetu tulioiandika kwenda TWAWEZA, tunasikitika kuona mawasiliano halali ya kiofisi yanapelekwa mitandaoni hata kabla ya kujibiwa”, amesema Dkt. Nungu.

Dkt. Nungu amesema kuwa COSTECH pekee ndio chombo cha kutoa ushauri katika masuala yote yanayohusu sayansi, teknolojia na uvumbuzi na moja ya majukumu yake ni kusajili na kutoa vibali vya tafiti zote za muda mfupi na mrefu zinazofanywa nchini.

Mwishoni mwa wiki iliyopita TWAWEZA ilitoa ripoti ya utafiti wa sauti za wananchi ukieleza hali ya siasa nchini, ambapo utafiti ulionesha kuporomoka kwa ukaribu wa wananchi na viongozi wa vyama vya siasa.

Kesi ya Tido Mhando yaendelea kupigwa kalenda

$
0
0
Kesi inayomkabili Mkurugenzi mkuu wa zamani wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Tido Mhando imepigwa tena kalenda na itasikilizwa Julai 18 mwaka huu.

Kesi hiyo ilipaswa kusikilizwa leo Julai 12, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, lakini Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru) Leonard Swai alimueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa shahidi waliyemtarajia atoe ushahidi leo ana udhuru hivyo akaomba kesi hiyo ipangiwe tarehe nyingine.

Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, Hakimu Shaidi aliipanga kesi hiyo hadi Julai 18,2018 ambapo mashahidi wa upande wa mashtaka wataendelea kutoa ushahidi katika kesi hiyo.

Katika kesi hiyo tayari mashahidi watatu wa upande wa mashtaka wamekwishatoa ushahidi  katika kesi hiyo,  ambao ni Ofisa uchunguzi wa Takukuru, Victor Lesuya, Mwanasheria wa TBC, Gwakisa Mlawa na Mkurugenzi Mkuu mstaafu wa TBC, Clement Mshana.

Tido anakabiliwa na mashtaka manne ya kutumia madaraka vibaya na moja la kuisababishia Serikali hasara ya Sh887.1 milioni.

Katika kesi hiyo inadaiwa kuwa Juni 16, 2008,   akiwa Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Tido ambaye alikuwa mkurugenzi wa TBC, kwa makusudi alitumia madaraka yake vibaya kwa kusaini mkataba wa kuendesha na utangazaji wa vipindi vya televisheni kati ya TBC na Channel 2 Group Corporation (BV1) bila ya kupitisha zabuni, jambo  ambalo ni kinyume na Sheria ya Manunuzi na kuinufaisha BVl.

Tido  anatetewa na Wakili Ramadhani Maleta na yupo nje kwa dhamana.

Twaweza Yakanusha Kuisambaza barua ya Costech mitandaoni

$
0
0
Muda mfupi baada ya Tume ya Sayansi na Teknolojia, (Costech) kusema wamesikitishwa na kitendo cha kusambaa mitandaoni kwa barua waliyowaandikia taasisi ya Twaweza, Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Aidan Eyakuze amesema hawajahusika kuisambaza.

Eyakuze ameyasema hayo leo Julai 12, kwenye ukurasa wa twitter wa taasisi hiyo.

“Kama tulivyosema awali, tumepokea barua kutoka Costech na tunaifanyia kazi. Twaweza haijasambaza barua hiyo wala kuhusika kuisambaza kwenye mitandao ya kijamii,” imesema taarifa hiyo

Eyakuze amesema, barua zote zinazopelekwa Twaweza huwekwa muhuri mbele ya aliyetumwa kuipeleka pamoja na risiti.

“Barua inayosambaa mitandaoni haina muhuri wetu, tunaheshimu mawasiliano yote yanayofanywa na wadau wetu,” amesema

Leo Kaimu Mkurugenzi wa Costech  Dk Amos Nungu alizungumza na wanahabari na kusema wamesikitishwa na kusambaa mitandaoni  kwa barua hiyo waliyopelekewa Twaweza

Ada mbalimbali ambazo wote wanaojihusisha na sanaa watapaswa kulipa kwa mujibu wa BASATA ili kuendesha kazi zao za sanaa

$
0
0
Baraza la Sanaa la Taifa  (BASATA) limefanya mabadiliko kwa baadhi ya huduma zitolewazo na baraza hilo kuanzia Julai 1, 2018 kama yalivyoainishwa kwenye kanuni mpya za baraza hilo zilizotoka mwezi wa pili mwaka huu. (February, 2018).

Waziri Ummy Mwalimu Amtumbua Dereva wa Gari la Wagonjwa Lililokamatwa na Kilo 800 za Mirungi

$
0
0
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Tarime, Elias Ntiruhungwa kumsimamisha kazi dereva wa gari la kubeba wagonjwa la halmashauri hiyo aliyekamatwa akiwa amepakia kilo 800 za mirungi.

Kauli hiyo imetolewa leo Alhamisi Julai 12, 2018 katika uzinduzi wa mradi wa Tuwatumikie katika viwanja vya Halmashauri ya Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu.

Amesema mbali na dereva huyo, maofisa waliokuwa wamepanda gari hilo nao wasimamishwe kazi.

“Nimesikitishwa na taarifa za kukamatwa kwa gari la kubeba wagonjwa likiwa na mirungi, inasikitisha maana magari yanabadilishwa matumizi huku wagonjwa wakipata shida na wengine hata kufariki dunia,” amesema.

Amewataka waganga wakuu wa wilaya na mikoa kusimamia matumizi ya magari hayo ili wagonjwa wawe wanafika kwa haraka katika vituo vya afya kwa ajili ya matibabu.

Amesisitiza kuwa hataki kuona magari ya wagonjwa yanafanya shughuli nyingine na kuagiza kuwa yanapaswa kuwa katika vituo vya afya yalivyopangiwa.
 
“Ni marufuku gari la kubeba wagonjwa kubeba mkaa wala bidhaa nyingine, nalipongeza jeshi la polisi mkoani Mara kwa kuchukua hatua na mkurugenzi wa mkoa wa Mara nakuagiza kuchukua hatua mara moja usisubiri kusikiliza popote”, amesema ummy.

Waziri wa Elimu Amtumbua Ofisa manunuzi wa wizara Hiyo

$
0
0
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Joyce Ndalichako, amemtaka katibu Mkuu wa wizara hiyo, Leonard Akwilapo kumsimamisha kazi Ofisa manunuzi wa wizara Audifasy Myonga kwa kufanya manunuzi ya vifaa vya maabara visivyo hitajika na kuvisambaza katika vyuo vya ualimu.

Ndalichako ametoa maamuzi hayo leo Julai 12, alipotembelea chuo cha ualimu Kasulu, mkoani Kigoma na kufanya kikao na watumishi kwa lengo la kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Alisema chuo hicho kilipokea vifaa hivyo ambavyo viko chini ya kiwango huku vingine kutohitajika kwa matumizi ya maabara.

“Serikali inaanza na ofisa manunuzi na baadaye itawachukulia hatua stahiki baada ya kukamilika kwa uchunguzi watu watakaokuwa wamehusika kupokea vifaa hivyo chuoni hapo kwani kama walijua vifaa hivyo havihitajiki kwanini walivipokea,” amesema Profesa Ndalichako

Amesema serikali kupitia wizara yake walinunua vifaa vya maabara kwa awamu mbili, awamu ya kwanza vifaa vya zaidi ya Sh298 milioni na awamu ya pili zaidi ya Sh759 milioni ambavyo vifaa hivyo vilisambazwa katika vyuo mbalimbali vya ualimu nchini.

"Nimeona shehena ya vifaa chuoni hapa ambavyo vimekaa tu tangu mwaka 2016 walipopokea ambavyo ukiwauliza wanasema havina kazi kwanini wapokee vitu ambavyo havina kazi na kukaa navyo?" amehoji waziri huyo.

"Niwaombe mniandalie taarifa ya kuomba vifaa hivyo na taarifa ya upokeaji wa hivyo vifaa baada ya hapo nitajua cha kufanya kwani hapa kila mtu anamtupia mpira mwenzie, na ikibainika kama kuna kitu kinaendelea serikali itaondoka na vichwa vya watu waliohusika, "amesema waziri Ndalichako.

Boharia chuoni hapo Meckisedeck Waziri, amesema wao walipokea vifaa hivyo vya maabara kutoka wizarani Desemba 13, 2016 na awamu ya pili walipokea Juni 23, 2017.

Gari la Serkali Lililokamatwa na Mirungi LAMTUMBUA Mganga Mkuu Hospitali ya Mji wa Tarime na Wenzake Wawili

$
0
0
Mkurugenzi wa Halamshauri ya Mji wa Tarime Elias Ntiruhungwa
**
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Tarime Elias Ntiruhungwa amewasimamisha kazi watumishi watatu akiwimo kaimu mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Tarime baada ya gari la wagonjwa la Hospitali hiyo kukamatwa likisafirisha  dawa za kulevya aina ya mirungi Wilayani Bunda Mkoani Mara Julai 11 Mwaka huu.

Waliosimamishwa kazi ni Kaimu Mganga Mkuu (DM) Dkt Innocent Kweka, Kaimu Mganga Mfawidhi Dkt Amir Kombo na katibu wa Hospitali Rwegasira Karugwa kutokana na uzembe waliofanya mpaka kitendo hicho kinafanyika.

“ Namsimamisha kazi DMO, Mganga Mfawidhi na Katibu wa hospitali kuanzia leo hadi tuakapomaliza uchunguzi wetu ambao umeanza kubaini kwa nini gari la wagojnwa lilitumika kusafirisha madawa ya kulevya .Kama hawana hatia watarudi kazini”alisema Mkurugenzi.

Ntiruhungwa amesema hawezi kuvumilia kitendo hicho ambacho kimechafua jina la Hamashauri yake na nchi kwa ujumla na kwamba yeyote ambaye atabainika kuhusika katika tukio hilo atachukuliwa hatua kali.

Ameongeza kuwa tayari suala hilo linafanyiwa uchunguzi wa kina ili kubaini dereva huyo George Matai alipataje fursa ya kusafirisha madawa ya kulevya kwa kutumia gari la wagonjwa na kusema kuwa tayari amemsimamisha kazi kuanzia leo.

Mkurugenzi huyo aliwataka wakuu wa idara katika Halmashauri yake kutimiza wajibu wao kikamilifu ili kuepuka vitendo vya aibu kama hivyo kutokea tena.

Taarifa MUHIMU Kwa Wanafunzi Wote Toka Bodi ya Mikopo HESLB

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inapenda kuwataarifu waombaji wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2018/2019 kuwa imeongeza muda wa kutuma maombi kwa njia ya mtandao kwa wiki mbili kuanzia Julai 15, 2018.

Hivyo basi, tarehe ya mwisho ya kuwasilisha maombi kupitia mtandao wa HESLB (https://olas.heslb.go.tz ) itakuwa Jumanne, Julai 31, 2018.

Aidha, tarehe ya mwisho ya kutuma nakala ngumu kwa ‘EMS’ kupitia Shirika la Posta Tanzania (TPC) ni Jumanne, Agosti 14, 2018 ili kutoa nafasi kwa HESLB kuchambua, kuhakiki na kupanga mikopo kwa waombaji wenye sifa.

Hatua hii inalenga kutoa fursa kwa waombaji wa mikopo ambao hawajakamilisha nyaraka mbalimbali zinazohitajika kufikia Julai 15, 2018 kukamilisha na kuwasilisha HESLB ndani ya muda ulioongezwa.

Uhakika wa upatikanaji wa bahasha maalum za kutuma maombi
HESLB pia inapenda kuwafahamisha waombaji wote wa mkopo kwa mwaka 2018/2019 kuwa tunafanya kazi kwa karibu na Shirika la Posta Tanzania (TPC) na tumehakikishiwa kuwa limesambaza bahasha za kutosha nchini kote ili kuwawezesha waombaji wa mikopo kutuma maombi yao kwa njia ya ‘EMS’ bila usumbufu.

Kwa upande wa uhakiki wa vyeti vya kuzaliwa vya waombaji wa mikopo na vile vya vifo vya wazazi wao, tumehakikishiwa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) kuwa maombi yote ya uhakiki wa vyeti yatakamilishwa ndani ya muda ulioongezwa.

HESLB inawahakikishia waombaji wote wa mikopo kuwa maombi yao yatakayowasilishwa ndani ya muda uliotolewa yatapokelewa na kufanyiwa kazi.

Hitimisho
Tunapenda kuwakumbusha waombaji wa mikopo kuusoma na kuuzingatia ‘Mwongozo wa Utoaji Mikopo kwa mwaka 2018/2019’. Mwongozo huu unapatikana katika tovuti ya HESLB (www.heslb.go.tz). Iwapo wana maswali, wawasiliane nasi kupitia:

Simu:         0736665533 au 022 5507910
Barua pepe:    adcp@heslb.go.tz au info@heslb.go.tz
Taarifa hii pia inapatikana kwenye tovuti ya HESLB www.heslb.go.tz

Imetolewa na:
Abdul-Razaq Badru
Mkurugenzi Mtendaji
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
DAR ES SALAAM

Mbunge Afikishwa Mahakamani Kwa Utapeli

$
0
0
Mbunge wa zamani wa Dimani – Zanzibar (CCM), Abdallah Sharia Ameir (54) na mwenzake wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu shtaka la kujipatia Sh55 milioni kwa njia ya udangan yifu.

Mbali na Ameir ambaye ni mkazi wa Mnazi mmoja, mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ya jinai namba 229 ya mwaka 2018 ni Dk Athuman Rajabu (32).

Wakili wa Serikali, Janeth Magohe leo Alhamisi Julai 12, 2018 amedai mbele ya Hakimu Mkazi, Hamisi Ally kuwa washtakiwa walitenda kosa hilo kati ya Julai 17 na Septemba 26, 2017 jijini Dar es Salaam.

Wakili Magohe amedai washtakiwa walijipatia kiasi hicho cha fedha kutoka kwa Abdi Hirsi Warsame wakiahidi kuwa wangemsambazia vifaa tiba katika hospitali, wakati wakijua kuwa ni uongo.

Washtakiwa wamekana shtaka na upande wa mashtaka umedai kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.

"Upelelezi wa shauri hili bado haujakamilika hivyo tunaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kukamilisha upelelezi,” amesema wakili huyo.

Baada ya upande wa mashtaka kueleza hayo wakili wa utetezi, Thimotheo Wandiba ameiomba mahakama kuwapatia dhamana wateja wake kwa sababu shtaka lao linadhaminika.

"Naomba mahakama yako iwapatie dhamana wateja wangu kwani shtaka lao linadhaminika,” amedai wakili Wandiba.

Hakimu Ally ametaja masharti ya dhamana kwa washtakiwa hao ni kuwa na wadhamini wawili watakaosaini bondi ya Sh27.5 milioni kila mmoja.

Pia, wadhamini wao wanatakiwa kuwasilisha fedha taslimu Sh27.5 milioni au hati ya mali isiyohamishika yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha.

Hata hivyo, washtakiwa hao wameshindwa kutimiza masharti ya dhamana na kurudishwa rumande. Kesi hiyo imeahirishwa hadi kesho, Julai 13 itakapotajwa kwa ajili ya dhamana.

Waziri Mkuu azitaka taasisi za dini kuwekeza kwenye viwanda

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka viongozi wa dini wasibaki nyuma katika suala zima la kuwekeza kwenye viwanda ili waweze kuendana na azma ya Serikali ya awamu ya tano ya kuifikisha Tanzania kwenye uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

“Serikali ya awamu ya tano imeazimia kukuza uchumi wa viwanda. Nawaomba msiwe nyuma katika suala hili, tumieni fursa ya ardhi tuliyonayo hasa katika ujenzi wa viwanda vya usindikaji ili kuongeza thamani ya mazao,” amesema.

Waziri Mkuu ametoa rai hiyo leo (Alhamisi, Julai 12, 2018) wakati akifungua Mkutano wa Halmashauri Kuu ya 52 ya Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT). Mkutano huo wa siku mbili, umehudhuriwa na maaskofu zaidi ya 80, wenyeviti wa makanisa na wawakilishi wa vyama vishiriki.

Amesema uwepo wa viwanda hivyo utachangia ukuaji wa sekta ya kilimo na kuongeza ukuaji wa mnyonyoro wa thamani ya mazao. Akitoa mfano fursa zilizopo hivi sasa, Waziri Mkuu aliwaeleza Maaskofu hao kwamba bei ya ufuta kwa mwaka huu imepanda na kufikia sh. 3,100/- ikilinganishwa na sh. 1,400/- ambayo ilikuwa ni bei ya mwaka jana.

Ametumia fursa hiyo kuwapongeza viongozi wa dini kwa kwa kubwa wanayofanya ya kukemea maovu kama vile ujangili, ukatili wa kijinsia na matumizi ya dawa za kulevya.

“Serikali inaheshimu mahubiri yenu sababu tunajua yana nguvu sana. Kupitia mahubiri yenu, watu wakimjua Mungu, watakuwa na hofu ya Mungu, kwa hiyo watu watakuwa waadilifu na maovu mengine yatapungua,” amesema.

“Nitumie fursa hii kuwajulisha kwamba Tanzania imekuwa mfano wa kuigwa wa nchi zilizosimamia vizuri mapambano dhidi ya dawa za kulevya barani Afrika. Kwa hiyo tumepewa heshima ya kuandaa mkutano mkubwa wa kimataifa utakaofanyika hapa nchini Septemba, mwaka huu.”

Amesema mshikamano uliopo baina ya viongozi wa Serikali na viongozi wa dini hauna budi kuendelea. “Natoa wito kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya wajenge mshikamano wa pamoja na viongozi wa dini katika maeneo yao husika. Viongozi wa Kitaifa nasi, tutaunga mkono katika ngazi ya kitaifa,” amesema.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na maaskofu hao, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania, Askofu Dkt. Anilikisa Cheyo alisema Jumuiya hiyo inaendelea kusisitiza suala la umoja na mshikamano wa Kitaifa.

“Suala la umoja wa kitaifa na amani ya nchi yetu ni masuala mtambuka; tena ni nguzo ya utaifa wetu. Tunashukuru jinsi Serikali inavyosimamia masuala haya kwa hekima na uthabiti. Tunaahidi kuwa tutaendelea kuliombea Taifa letu pamoja na viongozi wake ili mzidi kuilinda amani ya Taifa letu pamoja na watu wake.”

“Hata wakati inapotokea masuala haya yanapoguswa au kuumizwa, Kanisa limeendelea kuhimiza mara zote kutafuta ufumbuzi wake kwa njia ya mazungumzo,” amesema.

Waziri Mkuu Ataka Maafisa Ugani Wawezeshwe......Awataka wasimamie mifumo rasmi ya ununuzi wa mazao

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema ofisi za maafisa ugani zinapaswa kuwepo walipo wakulima, wafugaji na wavuvi na kwamba maafisa ugani katika ngazi zote lazima wawezeshwe na wasimamiwe kikamilifu.

Waziri Mkuu ametoa wito huo leo (Alhamisi, Julai 12, 2018) wakati akifungua mkutano wa siku mbili wa maafisa kilimo, mifugo na uvuvi kutoka Tanzania Bara ulioanza leo kwenye ukumbi wa Chuo cha Mipango, jijini Dodoma. Mkutano huo unahudhuriwa na washiriki 570.

“Maafisa ugani katika ngazi zote lazima wawezeshwe na wasimamiwe kikamilifu kutekeleza majukumu yao. Wataalam wa Wizara washuke hadi ngazi ya mikoa na Halmashauri kusaidiana na waliopo kwenye ngazi hizo.

“Walioko ngazi ya mkoa washuke mara kwa mara hadi ngazi ya Halmashauri na ngazi ya Halmashauri ishuke na kushirikiana na maafisa ugani wa kata na vijiji kuelekeza wakulima, wafugaji na wavuvi kuhusu utaalam na maarifa yanayohitajika katika kuendeleza sekta hizi kibiashara,” amesema.

Amesema wakulima, wafugaji, na wavuvi hawana budi kupatiwa mbinu bora kuanzia hatua ya uzalishaji hadi kupata masoko ikiwa ni pamoja na matumizi ya teknolojia sahihi zenye tija katika uzalishaji wa mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi.

Amesisitiza kwamba maafisa ugani ni lazima wawe na orodha sahihi ya wakulima, wafugaji na wavuvi wote kuanzia ngazi ya kitongoji na aina ya mazao wanayoshughulikia, malengo ya uzalishaji na utekelezaji.

“Maafisa ugani wawe na takwimu sahihi za aina na kiasi cha mahitaji ya teknolojia na  pembejeo za uzalishaji wa mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi katika maeneo yao lakini pia wasaidie kuunganisha vikundi vya wakulima, wafugaji, wavuvi na kuunda ushirika imara ili kuendeleza juhudi za kufufua ushirika kama mkombozi kwa wakulima, wafugaji na wavuvi.”

“Ukiwa na ushirika imara hata kama unataka kuwapatia taarifa ya haraka kuhusu ongezeko la bei, au tarehe ya mnada inakuwa rahisi kwa sababu wana Mwenyekiti wao au Katibu wao na kupitia kwake, wote wanaweza wakaitishwa na kupewa taarifa kwa haraka,” amesema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka maafisa ugani waende wakasimamie mifumo rasmi ya ununuzi wa mazao ili kuwasaidia wakulima kupata bei nzuri za mazao yao.

“Hatutaki kusikia watu wanatumia mifumo isiyo rasmi kama chomachoma (kwenye ufuta), butura (kahawa huko Karagwe), katakichwa (kahawa Moshi), kangomba (korosho) na vishada (tumbaku). Nenda kapambane nao, wewe ni afisa wa Serikali na hupaswi kuacha wananchi wanateseka,” alisema.

“Nenda kahimize mfumo wa kuuza mazo kwa ushirika badala kuruhusu wanunuzi kwenda kwa mkulima mmojammoja. Pia mtusaidie kufafanua dhana ya Stakabadhi za mazao Ghalani kwamba siyo malipo ya papo kwa papo. Muwaeleze wakulima kwamba wanapeleka mazao pake wakati wakisubiria bei iwe nzuri, siyo kwamba wanakopwa,” amesisitiza.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na watumishi hao, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Bw. Selemani Jafo alisema Aprili mwaka huu, Serikali ilifanya tathmini ya utekelezaji wa agizo la kuwa na viwanda 100 kwa kila mkoa na kubaini kuwa umefikia 49.4 ndani ya miezi mitatu tu.

“Tarehe 20 Aprili, 2018, tulifanya kikao cha kwanza cha utekelezaji wa wa agizo la kila mkoa uhakikishe unajenga viwanda 100 vidogo na vya kati. Kwenye agizo hilo, tulilenga malighafi za viwanda hivyo zitokane na mazao ya kilimo, uvuvi na mifugo. Agizo hilo lilitaka wakuu wa mikoa wawe wamelitekeleza kati ya Desemba 2017 na Desemba 2018; na kufikia Aprili 2018, viwanda 1,280 vilikuwa vimeshajengwa sawa na asilimia 49.4 ya lengo tulilojiwekea,” alisema.

CHADEMA yaipigia goti Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kupitia Katibu Mkuu wake Dkt. Vicent Mashinji wameitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kusimamia haki katika uchaguzi mdogo wa Ubunge na udiwani ambao umepangwa kufanyika Agosti 12 mwaka huu kwa kata 77 za Tanzania Bara.

Dkt. Mashinji ametoa Kauli hiyo leo Julai 12, 2018 wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam na kuitaka Tume hiyo kuendesha uchaguzi uliokuwa huru ili mradi amani na utulivu iendelee kuwepo nchini.

"Katika uchaguzi huu wa marudio kumeanza kujitokeza vitendo vya ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi, ikiwemo kughushi saini za viongozi ili kuhalalisha wagombea katika Halmashauri ya Tunduma mkoani Songwe kupitishwa kinyume na sheria. Tunaviomba vyombo vya dola kuwachukulia hatua wote waliohusika. Kutokuwa na uchaguzi huru kunaweza kusababisha machafuko katika nchi", amesema Dkt. Mashinji.

Pamoja na hayo, Dkt. Mashinji ameendelea kwa kusema "tunahitaji kuwepo na Tume huru ya uchaguzi na katika uchaguzi huu, Tume isimamie haki na hizi figisu figisu zilizoanza kujitokeza izimalize mapema pamoja na matukio ya wagombea kukamatwa na kunyang'anywa fomu zao za ushiriki".

Uchaguzi huo mdogo wa marudio umekuja baada ya kuwepo wazi Jimbo la Buyungu Mkoani Kigoma kufuatia Mbunge Kasuku Bilago kufariki dunia mwanzoni mwa mwezi Mei mwaka huu pamoja na madiwani wa maeneo mbalimbali kuyaacha majimbo yao na kujiunga CCM kwa lengo la kumuunga mkono Rais Magufuli.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya July 13

Wahasibu watatu wa TTCL wafikishwa Mahakamani kwa Ubadhirifu wa Milioni 57

$
0
0
Wahasibu watatu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa tuhuma za uhujumu uchumi.

Washtakiwa katika kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba 50 ya mwaka 2018  ni Mercy Semwenda (49) maarufu Mercy  Frank Lema  mkazi wa Mwananyamala, Frola Bwahawa (54) mkazi wa Mbagala na Hawa Tabuyanjaa (54) mkazi  wa Mwenge.

Jana Alhamisi Julai 12, 2018 wakili wa Serikali mwandamizi, Patrick Mwita alidai mbele ya hakimu mkazi, Augustine Rwizile  kuwa washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka mawili ya wizi na  kuisababishia hasara Serikali ya Sh 57.7milioni.

Katika shtaka la kwanza la wizi linalomkabili Mercy  pekee anadaiwa katika tarehe tofauti  kati ya Januari  Mosi,  Septemba 21, 2017 jijini Dar es Salaam, mshtakiwa aliiba vocha za muda wa maongozi zenye thamani ya Sh44milioni.

Pia, anadaiwa kuiba fedha za mauzo kiasi cha Sh5.9milioni na fedha taslimu Sh 8.5milioni, vyote vikiwa na thamani ya Sh 57.7milioni mali ya TTCL, wakati akijua kuwa ni mtumishi wa shirika hilo.

Katika shtaka pili la kuisababishia Serikali hasara linalowakabili washtakiwa wote, inadaiwa katika kipindi hicho jijini Dar es Salaam, washtakiwa kwa makusudi waliisababishia TTCL hasara ya Sh57.7milioni.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, hakimu Rwezile alisema  washtakiwa hawatakiwi kusema chochote mahakamani hapo, kutokana na mashtaka yanayowakabili kuwa ni ya uhujumu uchumi.

Hata hivyo, Mwita alidai upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika na kuomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

Wakili anayemtetea mshtakiwa wa pili na wa tatu, Thimotheo Wandiba alidai kuwa wanafanya utaratibu wa kuwasilisha maombi ya dhamana Mahakama Kuu.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Julai 24, 2018 itakapotajwa tena huku washtakiwa wakirejeshwa rumande.

Rais Magufuli Kateua Kamishina Mpya wa Magereza Kuchukuwa Nafasi ya Juma Malewa

$
0
0
Aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Magereza, Juma Malewa ambaye Amestaafu.



Nahodha wa timu ya Taifa ya Croatia Adai MATUSI na DHARAU Ziliwaponza England Wakajikuta Wanapigwa 2-1

$
0
0
Nahodha wa timu ya Taifa ya Croatia, Luka Modric, amesema kilichowasaidia wao kuing’oa England katika nusu fainali ya Kombe la Dunia ni dharau.

Modric anayeichezea Real Madrid ya Hispania, alisema kuanzia wanahabari, mashabiki na wachezaji wa England ‘Three Lions’, waliidharau Croatia jambo lililowapa mwanya wa kuifunza adabu kwa kuichapa 2-1.

Licha ya England kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa bao 1-0 lakini iliruhusu bao la kusawazisha kwa Croatia na baadaye wakajikuta wakiishiwa nguvu katika dakika 30 za nyongeza ndipo mkongwe Mario Mandzukic alipowafunza adabu kwa kupachika bao la ushindi.

“Naweza kusema vyombo vya habari na wachambuzi wote wa soka wa Uingereza waliiponda na kuidharau Croatia, waliwapamba wachezaji wao mpaka wakatuona kama wanasesere, hili ndilo lililotufanya tushinde mchezo huu,” alisema Modric.

Alibainisha kuwa matusi na dharau hizo ndizo zilizowasukuma wao kucheza kwa bidii hadi kufanikiwa kuing’oa England katika mchezo huo.

Kwa upande wake Kocha wa Croatia, Zlatko Dalic, amewapongeza wachezaji wake chini ya uongozi wa Luka Modric, kupambana na kuweza kuitoa England kwa kichapo cha mabao 2-1.

Rais Magufuli Kuongoza Mkutano Mkubwa wa Kisiasa Duniani Unaoratibiwa na Chama cha kikomunisti cha China (CPC)

$
0
0
Rais  John Magufuli anatarajiwa kuongoza mkutano wa vyama vya siasa vyenye mlengo wa kijamaa utakaofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Julai 17, mwaka huu.

Mkutano huo pia utashirikisha viongozi wa mataifa mbalimbali akiwamo Waziri wa Mambo ya Nje wa China, Wang Yi ambaye atawakilisha Chama cha kikomunisti cha nchi hiyo (CPC).

Wengine watakaoshiriki katika mkutano huo ni viongozi wa vyama vilivyopigania uhuru na ukombozi wa Bara la Afrika na Kusini mwa bara hilo, vikiwamo vyama vya Frelimo, ANC ,ZANU PF na vinginevyo.

Mkutano huo ni wa pili kufanyika Duniani, ambapo wa kwanza ulifanyika Beijing, China Desemba mwaka jana, ambapo Rais wa nchi hiyo, Xi Jinping alihudhuria na kuziasa nchi za Afrika kuleta maendeleo.

China ni miongoni mwa nchi zilizo mstari wa mbele kusaidia nchi za Afrika ikiwamo Tanzania katika kuhakikisha kuwa nchi hizo zinapiga hatua za kimaendeleo katika nyanja mbalimbali za kisiasa, kiuchumi na kijamii, hali ambayo inaweza kuwasaidia kuondoka kwenye utegemezi.

Miongoni mwa miradi iliyotekelezwa na China kwa upande wa Tanzania ni pamoja na ujenzi wa reli, barabara na kwenye miradi mingine ya kimaendeleo na kimkakati.

Hivyo basi katika mkutano huo, wadau wataweza kubadilisha mawazo na uzoefu na kujenga taswira mpya ya kimaendeleo kupitia vyama vya siasa na kuandaa mikakati mipya katika utekelezaji wa majukumu yao.

Hata hivyo katika mkutano huo, pamoja na mambo mengine, Rais Magufuli ataongozana na Waziri Wang Yi kwa ajili ya kuweka jiwe la jiwe la Msingi la ujenzi wa Chuo Cha Uongozi Cha Chama Cha Mapinduzi(CCM) kitakachojengwa Kibaha mkoani Pwani.

Chuo hicho kitaanza kutoa mafunzo mwaka 2020 ambapo, wanafunzi kutoka nchi zilizopigania uhuru na ukombozi wa Bara la Afrika watapata mafunzo.

Waziri Wa Biashara Na Ushirika-Uganda Avutiwa Na Uendeshaji Ushirika Nchini Tanzania ....Aomba Ridhaa Kuja Kujifunza Nchini Tanzania

$
0
0
Mathias Canal-WK, Mtukula-Kagera
Serikali ya Uganda imeeleza kuvutiwa na uendeshaji wa ushirika nchini Tanzania hivyo imeomba kupata ridhaa ya kuzuru nchini Tanzania ili kujifunza namna bora ya uendeshaji wa ushirika.

Ombi hilo limetolewa  Julai 11, 2018 na Waziri wa Biashara na Ushirika nchini Uganda Mhe Fredrick Ngobi Gume wakati akizungumza kwenye mkutano uliohudhuriwa pia na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe Charles Mwijage uliofanyika katika eneo la Mtukula Wilayani Misenyi.

Katika mkutano huo Waziri huyo  anayeshughulikia Ushirika nchini Uganda alimpongeza Waziri wa Kilimo nchini Mhe Dkt Charles Tizeba kwa Nazi kubwa aliyoifanya katika kipindi cha muda mfupi kurejesha imani kubwa na ushirika kwa wakulima ambapo alimpongeza pia kwa tuzo ya heshima aliyokabidhiwa na Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe Kassim M. Majaliwa kwa niaba ya wana ushirika wakati wa sherehe za kilele cha siku ya ushirika Duniani kwenye viwanja vya Furahisha Jijini Mwanza.

Waziri wa biashara na ushirika nchini Uganda Mhe Gume alimuhakikishia mwenyeji wake kuwa biashara ya Kahawa nchini humo ina changamoto sawa katika nchi zote mbili kwa kuwa swala la mikopo isiyo rasmi inayowanyonya wakulima (Butura) nchini Uganda ipo kwa kiwango cha juu.

Alisema kuwa serikali ya Uganda inayoongozwa na Rais wa nchi hiyo Mhe Yoweri Kaguta Museveni itaendeleza ushirikiano na serikali ya Tanzania inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli hivyo panapohitajika ushirikishwaji katika biashara hususani kwenye sekta ya Kilimo watakuwa na msimamo wa pamoja.

Alisema miongoni kwa mambo mengine ya kujifunza nchini Tanzania itakuwa ni pamoja na kujifunza kuhusu namna bora  ya kuendesha ushirika na kuanzisha mfumo wa stakabadhi ghalani.

Kwa upande wake, Waziri wa Kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba alimueleza Waziri Gume kuwa njia mojawapo ya kusimamia ushirika ni pamoja na mkakati wa usimamizi madhubuti ikiwa ni pamoja na kuwaweka kizuizini wabadhilifu wote katika ushirika.

Mkutano huo ni muendelezo wa utekelezaji wa maagizo ya Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli aliyoyatoa wakati akiwaapisha viongozi mbalimbali Ikulu Jijini Dar es salaam tarehe 2 Julai 2018 na kuitaka Wizara ya Kilimo kufuatilia kwanini wakulima wa zao la Kahawa wanacheleweshewa malipo yao sambamba na kujua kwanini wakulima wanauza Kahawa yao nchini Uganda.

Naye Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe Charles Mwijage aliongeza kuwa wakulima wa Tanzania na Uganda wanapaswa kuweka msisitizo katika Kilimo kwani kufanya hivyo kutaongeza uimara na uanzishwaji wa viwanda vitakavyoongeza chachu ya ajira kwa wananchi.

MWISHO

Waziri wa Kilimo: “Gharama Za Uendeshaji Wa Vyama Vikuu Vya Ushirika Kudhibitiwa”

$
0
0
Na Mathias Canal-WK, Bukoba-Kagera
Malalamiko ya muda mrefu ya wakulima yaliyokuwepo kwamba ushirika unatoa bei ndogo, sasa yamepatiwa muarobaini baada ya serikali kupitia kwa kina gharama za uendeshaji na uongezaji thamani kwa zao la kahawa kwa Vyama vikuu vya ushirika Mkoani Kagera.

Serikali imepiga marufuku kwa vyama hivyo vya ushirika kutoza zaidi ya shilingi 490 kwa kilo moja ya Kahawa ya maganda kama gharama za uendeshaji na uongezaji thamani, Awali maainisho ya gharama hizo yalikuwa ni makubwa ambapo kiasi cha shilingi 1350 kwa kilo moja ya Kahawa ya maganda ilianishwa kama gharama za uendeshaji.

Waziri wa Kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba ameeleza agizo hilo jana 12 Julai 2018 wakati akizungumza na wajumbe wa Halmshauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera kwenye Hoteli ya Bukoba Coop ambapo miongoni mwa ajenda ya kikao hicho ilikuwa ni kujadili kuhusu soko la Kahawa na uendeshaji wa ushirika.

Dkt Tizeba amewaeleza wajumbe hao kuwa amepiga marufuku hiyo kufuatia malalamiko ya wadau wa Kahawa Mkoani Kagera ambapo gharama hizo zilionekana kuwa kubwa ukilinganisha na gharama halisi.

"Ndugu zangu wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM inawezekanaje shilingi mia mbili inatozwa kama ushuru wa chama kikuu, na shilingi mia mbili tena inatozwa kama ushuru wa chama cha msingi, ni nani anaweza kukupa faida namna hii sasa rasmi ushuru huu tumeupunguza kama nilivyoeleza" Alikaririwa Mhe Tizeba

Aliongeza kuwa swala la ushirika ni utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi ambayo ni mkataba kati ya wananchi na serikali katika kipindi cha miaka mitano kuanzia 2015-2020 kwa imani kubwa kwamba ndicho chombo pekee kitakacho mkwamua mkulima na changamoto anazo kabiliana nazo kwenye Kilimo na masoko ikiwa ni pamoja na kujiondoa katika umasikini.

Aidha, Dkt Tizeba aliwaeleza wajumbe hao kuwa vyama vya ushirika havipaswi kuendeleza mazoea ya kujiwekea gharama bila kwanza kutazama kipato cha mkulima huku akieleza kuwa amewaelekeza wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi ambapo Wilaya zao zinalima Kahawa kote nchini kufuatilia kwa karibu mwenendo wa masoko ya Kahawa kuanzia inavyokusanywa mpaka wakati inapouzwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera Bi Costansia Buhiye amempongeza Waziri huyo wa kilimo kwa kujibu kero namba 10 ya kikao cha Halmshauri kuu ya CCM kuhusu wasiwasi wa bei ya kahawa na namna na uendeshaji wa ushirika.

Buhiye alimpongeza Waziri huyo kwa kutatua kadhia mbalimbali za wakulima wa Kahawa katika ziara yake ya siku tatu Mkoani humo huku akieleza kuwa ana imani kubwa sasa kuwa wajumbe hao watatembea kifua mbele endapo wakulima wao watapatiwa bei nzuri.

MWISHO.

Clement Sanga Wa Yanga Avuliwa Uenyekiti Bodi ya Ligi (TPLB) Baada ya Yanga Kudai Bado Wanamtambua Yusuf Manji

$
0
0
Kikao cha Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kilichofanyika jana Julai 12,2018,  makao makuu ya shirikisho hilo, kimemuondoa  aliyekuwa mwenyekiti wa Bodi ya Ligi (TPLB), Clement Sanga,  kwenye nafasi hiyo kwa kukosa sifa baada ya klabu ya Young Africans kuthibitisha Yusuph Manji kuwa ndiye mwenyekiti wa klabu hiyo.

Wakati huohuo, Kamati ya Uchaguzi  ya TFF imeelekezwa kuandaa uchaguzi wa kuziba nafasi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa mikutano wa TFF uliopo Uwanja wa Karume mjini Dar es Salaam, Rais wa shirikisho hilo, Wallace Karia,  alisema  hatua hiyo imefuatia mkutano wa Juni 10 wa wanachama wa Yanga ambao ulitamka kuwa bado unamtambua Yussuf Manji kama Mwenyekiti wao.

Kamati imepitisha kanuni za kuruhusu usajili wa idadi ya wachezaji 10 wa kigeni katika Ligi Kuu kuanzia msimu ujao.  Wachezaji hao wanaweza kutumika wote kwa wakati mmoja,

Pia, Kamati ya Utendaji ya TFF imemthibitisha Wilfred Kidao kuwa Katibu Mkuu wa shirikisho hilo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images