Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mmoja Afariki dunia kwa kukosa hewa safi ndani ya mgodi

$
0
0
Mtu mmoja amefariki dunia na mwingine yuko mahututi katika Hospitali ya Wilaya ya Longido baada ya kuvuta hewa nzito ya baruti ndani ya mgodi wa madini ya rubi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng’anzi alisema kwamba tukio hilo lilitokea usiku wa Juni 30.

Alimtaja marehemu kuwa ni Baraka Lenguti (28) mkazi wa KIA wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro ambaye maiti yake ilichukuliwa na askari polisi wa Longido kwa ajili ya uchunguzi.

Alisema kwamba majeruhi aliyelazwa katika Hospitali ya Longido hajafahamika na bado yuko mahututi.

Kamanda Ng’anzi alisema mkasa huo umetokea baada ya wachimbaji hao kuingia ndani ya mgodi kabla ya muda wa saa 48 baada ya ulipuaji wa baruti kufanyika.

Alisema kwamba kwa mujibu wa kanuni za madini zilizowekwa na Serikali wachimbaji wakishalipua baruti katika miamba husubiri kwa muda wa saa 48 ndipo wanaruhusiwa kuendelea na shughuli.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

NEC yatangaza tarehe ya Uchaguzi mdogo Jimbo Moja na Kata 79

$
0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi  (NEC) itafanya uchaguzi mdogo kwenye Jimbo la Buyungu, Mkoani Kigoma na kwenye Kata 79 za Tanzania Bara, Mwenyekiti wa NEC, Jaji (R), Semistocles Kaijage amesema.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam, Jaji Kaijage amesema uchaguzi huo utafanyika tarehe 12 mwenzi Agosti na fomu za uteuzi wa wagombea zitatolewa kuanzia tarehe 8 hadi 14 Julai.

"Uteuzi wa Wagombea utafanyika tarehe 14 Julai, mwaka huu. Kampeni za Uchaguzi zitafanyika kati ya tarehe 15 Julai, hadi tarehe 11 Agosti, mwaka huu na siku ya uchaguzi itakuwa ni tarehe 12 Agosti mwaka huu,” amesema Jaji Kaijage.

Jaji Kaijage amebainisha kwamba Tume imetangaza uwepo wa nafasi wazi ya Ubunge kwenye Jimbo hilo la Buyungu baadaya kupokea taarifa kutoka kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Ndugu Job Ndugai baadaya ya kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo.

Kwa upande wa nafasi wazi za Udiwani, Jaji Kaijage amesema Tume ilipokea taarifa kutoka kwa Waziri wa Tamisemi akiitaarifu juu ya uwepo wa nafasi hizo na taratibu za uchaguzi mdogo zikaanza mara moja.

Jaji Kaijage amesema kuwa uchaguzi huo mdogo utafanyika ndani ya Halmashauri 43 zilizopo kwenye Mikoa 24 ya Tanzania Bara, na Mikoa hiyo ni pamoja na, Kigoma, Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Iringa, Kagera, Katavi, Kilimanjaro, Lindi, Manyara, Mara, Mbeya, Mtwara, Morogoro, Mwanza, Njombe, Rukwa, Ruvuma, Shinyanga, Simiyu, Singida, Songwe, Tabora naTanga.

Rais Magufuli Awataka Viongozi wa Dini Wasiruhusu Siasa Kuingilia Mambo ya Kidini

$
0
0
Viongozi wa dini mbalimbali hapa nchini wametwakiwa  kutoruhusu siasa kuingilia shuguli za dini ili kujenga ustawi wa kanisa na Taifa kwa ujumla pia kutowafanya watu wachche kujinufaisha kupitia taasisi za dini.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Jenista Mhagama  wakati alipomwakilisha Rais Dokta Jihn Pombe Magufuli kwenye misa ya kumweka wakfu Askofu wa sita wa Kanisa la Moraviani Tanzania jimbo la Magharibi.

Mhagama alisema  ni jambo la hatari kwa manufaa na ustawi wa imani pale siasa zitaruhusiwa kuingilia masuala ya dini kwani linaweza likasababisha migawanyiko ambayo sio vizuri kwa maendeleo ya nchi.

Aidha  Mhagama aliwataka  wanasiasa wenzake  kuacha dini zifanye kazi zake bila kuingiliwa na vivyo hivyo siasa zijiendeshe kwa mujibu wa Katiba za vyama kwa kuzingatia Katiba na sheria za nchi.

Alisema  kwamba siasa zikiingilia  dini  zitaleta  migogoro ndani ya dini ambayo  itasabaisha  mifarakano ndani ya taifa na kusababisha  kutoweka kwa amani na utulivu.

Mhagama alisisitiza Serikali itaendelea kushirikiana na na madhehebu ya dini zote kuhakikisha uhuru wa kuabudu unapatikana na kuheshimiwa na Watanzania wote.

Alisema Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dokta John Pombe Magufuli itaendelea kuhakikisha madhehebu mbalimbali ya dini hapa nchini yanaendelea kuendesha shughuli zake bila kubugudhiwa.

 Mhagama alisisitiza  kuwa Serikali haitakubali mtu yoyote anayetaka kusababisha dini zikorofishane ama zigombane na serikali kwani itamchukulia hatua kwa mujibu wa Sheria za Nchi.

 Katika salamu hizo Rais Magufuli alisema anatambua uwepo wa Kanisa la Moraviani katika jitiada zake za kujenga na kuimarisha udugu na kujenga imani na utulivu wa wananchi na ametoa shilingi milioni kumi zisaidie katika kulitegemeza Kanisa na Taasisi zake.

 Awali  askofu mteule wa sita wa kanisa hilo jimbo la Magharibi Ezekiel Yona ameipongeza serikali ya awamu ya tano kwa jinsi inavyoweka mazingira  mazuri ya kuliendeleza kiuchumi taifa la Tanzania.

 Alisema kazi yake ndani ya kanisa hilo itakuwa ni kusisitiza amani, kuhudumia watu kiroho na  kimwili kwa kutoa huduma za kijamiii kwa kushirikiana na serikali.

 Zoezi la kuwekwa wakfu kwa Askofu huyo wa sita limefanyika kwenye viwanja vya kanisa la Moraviani Milumbani mjini Tabora na kusimamiwa na Askofu Dokta Alinikise Cheyo, akisidiana na Maaskofu Conrad Nguvumali na Askofu Sam Gray  toka Amerika.

Viongozi wengine waliohudhuria sherehe hizo ni maaskofu wa kanisa hilo toka majimbo mbali mbalihapa nchini, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, wabunge na viongozi wa dini mbalimbali.

Full on: Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume

$
0
0
Full on: Ni dawa bora ya nguvu za kiume, hukufanya ufurahie tendo la ndoa kwa asilimia mia (100%) bila kuchoka 

Itakufanya urudie tendo la ndoa zaidi ya Mara 4  bila kuchoka, itakufanya pia uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30 kwa tendo la kwanza pia huchochea hormone za ashki,pia kuzalishwa kwa wingi kwenye mfumo wa uzazi

Gembe: huboresha maumbile madogo ya kiume na kuyafanya yawe kwenye umbo sahihi na litakalomtosheleza mke/mpenzi kwa asilimia 100% kwa kuwa matatizo haya huwa na vyanzo vyake kama vile kufanya punyeto,masturbation)diabetes) kisukari,matatizo ya neuron)yaani mishipa ya fahamu,mgoro,ngiri,tumbo kuunguruma,magonjwa ya mfumo wa mkojo mfano U.T.I.gono, miguu kuwaka moto na kufa ganzi.

Pia tunatibu kutokwa na nyama sehemu ya haja kubwa kwa siku3,pia kutibu busha bila kupasua,mvuto wa mapenzi
 
Kama huna muda wa kufika ofisini kwetu utaletewa popote. Mikoani unatumiwa bus 

Tupo Mbagala Rangi tatu

Simu;  0762606571 / 0787575969- Dr Mijingo

Kesi ya rushwa inayomkabili Mbunge wa Singida kuendelea July 4

$
0
0
Mahakama ya Wilaya ya Singida inatarajia kuendelea kusikiliza kesi ya rushwa ya Sh.Mil 2 inayomkabili Mbunge wa Singida Kaskazini, Haider Gulamali July 4,2018.

Awali mahakama hiyo ilisikiliza ushahidi wa mashahidi wanne wa upande wa mashtaka mbele ya Hakimu Mfawidhi,Flora Ndale.

Miongoni mwa mashahidi hao ni Ofisa Usalama mkoa wa Singida, Kiseo Nzowa anayedaiwa kupewa rushwa hiyo ambapo amedai anafanya kazi kwa mujibu wa sheria

Shahidi huyo amedai kuwa Gulamali alimpa Sh.Mil 2 ili amsaidie kupitisha jina lake kwenye kinyang’anyiro cha ubunge Singida Kaskazini na kwamba yeye hakuwa Mjumbe Kamati ya Siasa Wilaya.

Amedai kuwa Gulamali alimpa fedha hizo katika bahasha huku akisema hizo ni salamu zake naye alipokea na kumpatia Meneja wa Hotel ya Urafiki Resort.

Shahidi mwingine ni Jafari Uledi ambaye ni Afisa Upelelezi Takukuru aambapo aliomba kutoa bahasha yenye Sh. milioni 2 ndani yake kama kielelezo.

Hata hivyo, upande wa utetezi walipinga kwa sababu fedha hazikutaifishwa kwa mujibu wa kifungu cha 12 cha PCCB Act na Kanuni zake za 2009 yaani hakuna fomu iliyojazwa kutaifisha fedha.

Pia amedai kuwa aliyehusika kutaifisha fedha sio mtumishi wa PCCB bali ni meneja ama mlinzi wa Hotel.
 
Walidai hakuna karatasi iliyojazwa kwa mujibu wa Kifungu cha 38(3) CPA ili kuthibitisha kuchukua fedha na kwamba kifungu cha 169 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai kinakataza kupokea nyaraka ambazo zilichukuliwa kiharamu.

Kutokana na mvutano wa kisheria kuhusu kupingwa kupokelewa kwa bahasha, Mahakama iligoma kupokea bahasha yenye fedha hizo kwa kuwa haikufuata utaratibu, ambapo kesi imeahirishwa hadi July 4, 2018 ili kuendelea na usikilizwaji.

Magufuli Ampa Milioni 10 Binti Mlemavu Anayeandikia Ulimi....Ataka Watanzania Tuache Kukatishana Tamaa

$
0
0
Rais John Magufuli amemzawadia Sh10milioni  mwandishi wa miswada ya filamu, Wakonta Kapunda  ili kumuunga mkono katika uandishi wake, akieleza kuwa licha ya kuwa ni mlemavu hajakata tamaa.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Julai 2, 2018 katika uzinduzi wa kitabu cha Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk Reginald Mengi kinachoitwa, ‘I can, I must, I will’.

Wakonta alipewa fedha hizo baada ya kujinyakulia kitita cha Dola 20,000 za Marekani sawa na Sh45.6 milioni, ikiwa ni zawadi ya ushindi wa shindano la kuandika wazo la kibiashara lililotolewa na Dk Mengi.

Akizungumza katika hotuba yake, Rais Magufuli amesema alimfahamu Wakonta baada ya kusoma historia ya maisha yake kupitia vyombo vya habari.

 “Kitabu cha Mzee Mengi kiwe fundisho kwetu sote, nitoe wito kwa wafanyabiashara wote msisikilize maneno ya watu wanaowakatisha tamaa, fanyeni biashara kweli kweli”
 

“Hata mimi Nilijua ukishakuwa Rais huwezi kukatishwa tamaa na mtu yeyote kwa sababu wewe ni Rais lakini haikuwa hivyo, nilipoingia niliyaona.
 

“Nina matumaini makubwa kupitia kitabu chako hiki watanzania wengi watajenga matumaini, kujiamini na mafanikio makubwa na katika hili naomba kitabu hiki ukitafasiri kwa lugha ya kiswahili ili kupata fursa ya watanzania wengi kukisoma.
 

“Watanzania tuache kukatishana tamaa na ninafahamu katika historia ya Mzee Mengi yapo mengi amepambana nayo ya kukatishwa tamaa” – Rais Magufuli
 
“Nilisoma kwamba aligongwa na gari siku ya mahafari yake, lakini hajakata tamaa hana uwezo wa kuandika kupitia mikono yake, lakini anaweza kuandika anachokifikiria kwa kutumia ulimi wake, nitamchangia Sh10 milioni iweze kumsaidia katika mawazo yake anayoyapata kutoka kwa Mwenyezi Mungu,” amesema Rais Magufuli.

Binti huyo aliyepata ulemavu baada ya ajali, amekuwa akiandika kwa kutumia ulimi wake kwani viungo vyote vya mwili havifanyi kazi.

Hata hivyo shindano hilo lililowashirikisha vijana wa Afrika, liliibua washindi wawili akiwemo Brian Mwenda kutoka nchini Kenya.

Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Tatizo La Nguvu Za Kiume Kuboresha Uume Mdogo Tunatibu Busha Na Vidond Vya Tumbo

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME KUBORESHA UUME MDOGO TUNATIBU BUSHA NA VIDOND VYA TUMBO :acha kujiona mpweka pale ukutanapo na mke au mpenzi wako kwa sababu kutokuwa na uwezo wa kumridhisha na ni chazo kikubwa cha ndoa nyingi kuvunjika au kusababida mke au mpenzi kusalitiana

 NI NINI TIBA YA NGUVU ZA KIUME 
Mapro power no 2 ndio tiba tosha kwa sasa kwani hutibu matatizo yafutayo;
 1 kuwai kufika kileleni kabla mwenzi wako hajakojoa, dawa hii itakufanya uchelewa kwa mda wa dakika 15 -20 
2 dawa hii itakufanya urudie tendo La ndoa zaidi ya Mara tatu 3, dawa hii hutibu tatizo La uume kuwa legelege 

4 dawa hii huondoa uchovu, miungurumo ya tumbo pale umalizapo kufanya tendo La ndoa.

Unasubili nini sasa... OKOA NDOA YAKO NA MAISHA YAKO SASA 

Makakanua;hii ni dawa ya kuboresha uume mdogo na mwembamba na kurudi kwenye hali yake ya awali kwani dawa hii husaidia kuitanua misuli ya uume haswa kwa wanaume waliofanyiwa tohara wakiwa watu wazima, kumbuka hakuna dawa ya kuongeza maumbile endapo umezaliwa ukiwa na uume mdago

NI NINI KINACHOSABABISHA UUME KUWA MDOGO 1 kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima
 2 unene kupita kiasi 
3 kuvaa nguo za kubana sana
 4 kulala na nguo hasa zile za kubana kwa wale wanaoishi maeneo ya joto

TUNATOA DAWA YA KISUKALI,PRESHA, MIGUU KUUMA, KUPUNGUZA KITAMBI, MATITI MAKUBWA, PIA ZIPO DAWA ZA MVUTO WA MPENZI, MVUTO WA WATEJA KWENYE BIASHARA NK

Fika Mbagara Zakhemu barabara iendayo Kibonde maji utaona ofisi imeandikwa Mabura Crinic au piga simu no 0752348593 DR MABULA 

Kwa wateja wa Mwanza na mikoa ya jirani yupo wakala wetu hapo Mwanza. DAWA HIZI NI TOFAUTI NA ULIZOWAI KUTUMI WOTE MNAKALIBISHWA

Rais wa Urusi aipongeza timu ya taifa hilo kwa kupata ushindi

$
0
0
Rais wa Urusi, Vladimir Putin ameipongeza timu ya taifa hilo kwa kupata ushindi dhidi ya Hispania na kujihakikishia kusonga mbele mchezo wa michuano ya kombe la dunia inayoendelea kwenye nchi hiyo mwaka huu 2018.

Urusi ambayo ni mwenyeji wa michuano hiyo imeingia huku ikionekana kuwa timu dhaifu lakini imeweza kufanya maajabu makubwa mpaka sasa baada ya kutinga hatua ya robo fainali baada ya kuwafunga Saudi Arabia na Misri mpaka inatinga hatua ya robo fainali.

Timu hiyo ambayo imepata mafanikio makubwa mpaka sasa ya Urusi imehudhuriwa mara moja wakati wa ufunguzi na rais wa nchi hiyo wakati wa ufunguzi wa michuano hiyo ya FIFA.

Putin ameshindwa kuhudhuria kwenye mechi dhidi ya Hispania iliyopigwa kwenye dimba la Luzhniki jijini Moscow kwa sababu ya majukumu ya kiserikali yanayo mkabili.

Kwa mujibu wa msemaji wake, amesema kuwa Putin alimuita meneja wa kikosi cha Urusi, Stanislav Cherchesov kabla ya mechi na kumtakia kilalakheri na hata baada ya mchezo huo alimpa pongezi.

Mfalme Mswati atuma mswaada Bungeni kuhusu raia wa kigeni Kutozwa Kodi Kwa Kuwaoa Mabinti wa Nchi Hiyo

$
0
0
Mfalme Mswati wa swaziland ametuma mswaada bungeni kuhusu kutungwa kwa sheria mpya kwa raia kutoka nje ya nchi hiyo kulipa kodi watakapofunga ndoa na wanawake nchini Swaziland kwa kutozwa kiasi cha 30,000 lilangeni ( dola 2,200) .

Mfalme Mswati ametuma mswaada huo bungeni huku akidai kuwa sheria hiyo ni kwa ajili ya kuwalinda wanawake nchini humo.

“ Lengo la sheria hii ni kuwalinda wanawake na matendo ya unyanyasaji kutoka kwa wapenzi wao wa kigeni wanaotumia njia ya kuoa wanawake wetu kwa ajili ya kupata uraia” amesema Msemaji wa Serikali Percy Simelane.

Aidha mswada huo umepingwa vikali na mmoja wa wanaharakati wa kutetea haki za wanawake Dumsane Dlamini akidai kuwa sheria hiyo itawanyima haki wanawawake nchini Swaziland maana wanawake hao huwapenda wanaume wa kigeni kwa utanashati na wanajua thamani ya mapenzi.

Lakini 2016, Wizara ya mambo ya Kigeni ilianzisha mpango wa kutoa uraia kwa wageni nusu milioni hasa kutoka Asia ambao watakuwa sehemu ya idadi ya raia 1.3 milioni ya wananchi wote wa Swaziland .

Moto Wateketeza Gari Daraja La Kigamboni

$
0
0
Moto umewaka na kuteketeza gari dogo aina ya Toyota Ractics, leo Jumatatu, Julai 2, 2018 katika Daraja la Nyerere (Kigamboni) jijini Dar es Salaam huku mwenye gari akifanikiwa kutoka nje ya gari na kukimbilia sehem salama.

Chanzo cha ajali hiyo imedaiwa kuwa ni hitilafu ya umeme wa gari hiyo pindi limefika kwenye kukata ticket hitilafu hiyo imetoka na kuanza kuungua, juhudi za kuliokua gari hilo zilifanyika na kufanikiwa kuuzima moto huo hali likiwa limeshaungua mbele.

Inadaiwa ajali hiyo imetokea wakati dereva wa gari hilo akilipia fedha ili avuke ng’ambo, lakini pia huku kukiwa hakuna taarifa ya majeruhi wala vifo vilivyoripotiwa kutokana na ajali hiyo.

Hii ndio sababu ya Dkt. Mengi kuandika kitabu

$
0
0
Mwenyekiti wa makampuni ya IPP nchini Tanzania, Dkt Reginald Mengi amesema sababu kubwa ya yeye iliyomsukuma mpaka kufikia hatua ya kuandika kitabu kinachoelezea maisha yake kiujumla ni kutokana na mtoto wake Roodney ambaye ameshafariki kumsisitizia kuandika kitabu.

Dkt, Reginald Mengi amebainisha hayo leo Julai 02, 2018 wakati alipokuwa anazungumza mbele ya wageni viongozi wa nchi na wageni waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa kitabu chake kilichopewa jina la 'I Can, I Must, I Will- The Spirit of Success' iliyofanyikia katika ukumbi wa Serena Hotel Jijini Dar es Salaam.

"Nilikuwa na mtoto Roodney lakini kabla hajaondoka hapa duniani aliniomba sana niandike kitabu ambacho kitacho kuwa kinaelezea maisha yangu na mambo ambayo nimeyafanya kwa  hiyo nimefanya hivyo kama alivyotaka mwanangu na leo namshukuru Mungu nimeweza kutimiza ahadi yangu", amesema Dkt. Mengi.

Pamoja na hayo, Dkt. Mengi ameendelea kwa kusema "ahadi ya pili aliyonipa ni kunitaka niwe naenda kufanya mazoezi kila siku 'gym' lakini huwa nafanya hivyo mara tatu au nne nasio kila siku, ila kuanzia leo nitamiza hilo".

Mbali na hilo, Dkt. Mengi amesema jambo kubwa lililoweza kumsukuma mpaka leo hii kukizundua kitabu chake hicho ni kutokana na yeye kuzaliwa katika maisha ya kimasikini kitu ambalo ametaka wananchi wafahamu hilo ili nao waweze kujua namna ya kutoka huko na kuwa katika maisha mengine.

Kwa upande wake, Rais Dkt. John Magufuli ambaye ndio alikuwa mgeni rasmi wa hafla hiyo ya uzinduzi wa kitabu cha 'I Can, I Must, I Will- The Spirit of Success' amewataka watanzania na wafanyabiashara wote kiujumla kununua kitabu hicho ili kiweze kuwafundisha katika kutokana na hali ya umasikini huku akiwasisitizia zaidi kufanya kazi kwa bidii na kuacha kusikiliza maneno ya watu ambao wanawakatisha tamaa.

Kigwangalla Akabiliana na Majangili Msituni

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla amefanikiwa kutaifisha vifaa vilivyokuwa vikitumiwa na wahalifu katika pori la msitu wa Patamela baada ya kuhofia kukamatwa.

Hayo yamebainishwa na Waziri Kigwangalla ambaye yupo katika ziara ya pori kwa pori mkoani Songwe ambapo amebainisha kuwa baada ya wahalifu hao ambao walikuwa wakifanya ujangili katika machimbo ya madini walichoma moto na kutelekeza vifaa vyao kisha kutoroka.

Akisimulia tukio Waziri amesema " Kwenye ziara yetu wilayani Songwe, Mkoa wa Songwe, kwenye msitu wa Patamela, ambao ni msitu wa asili wa hifadhi wa kitaifa unaochukua sehemu kubwa ya wilaya za Songwe na Chunya, tulikuta kuna ujangili wa uchimbaji madini ulioshamiri, wahalifu walichoma moto ili kutuchelewesha tusifike eneo la tukio waweze kuondoka".
 
Ameongeza, "Bahati nzuri, tulipambana kwa ushirikiano wetu wote tuliokuwepo na tulifanikiwa kuudhibiti moto na kuendelea na safari mpaka eneo lililovamiwa na wachimbaji haramu wa madini. Tuliwawahi wakakimbia wakatelekeza vifaa na mashine (wheel loader) ambayo tumeitaifisha, sambamba na makinikia yote".

Hata hivyo Kigwangalla amesema kazi  bado inaendelea na ziara ya pori kwa pori inaendelea ambapo leo atakuwa Chunya mkoani Mbeya.

Watu 11 wa Familia Moja Wanyongwa

$
0
0
Watu 11 wa familia moja wamepatikana wakiwa wamekufa kwenye nyumba iliyo katika mji mkuu wa India Delhi, huku 10 kati yao wakiwa wananing'inia katika dari la nyumba hiyo, kwa mujibu wa polisi.

Mwanamke mmoja aliye na takribani miaka 70 alipatikana kwenye sakafu ya nyumba. Wengi wa wale waliokuwa wamekufa walikuwa wamefungwa macho na mikono nayo ilikuwa imefungwa kwa kamba mgongoni.

Familia hiyo imeishi wilaya ya Burari mjini Delhi kwa zaidi ya miaka 20 licha ya kwamba wametokea katika maeneo ya Rajathan huku familia hiyo ikiwa inamiliki maduka mawili katika ghorofa ya chini kwenye jengo la ghorofa tatu.

“Nilipokuwa naenda dukani niliona mlango ukiwa umefunguliwa na nilipoingia ndani niliona miili ya watu hao ikiwa imening’inia katika dari uku imefungwa mikono kwa nyuma” amesema Gurchan Sigh alipokuwa akiojiwa na moja ya chombo cha habari mjini Delhi.

Taarifa ya awali kutoka polisi inazungumzia karatasi zenye maandishi walizozipata kwenye nyumba hiyo ambazo zinaashiria kufanyika kwa matambiko yanayoonekana kuwa na uhusiano na vifo hivyo.

“Bado tunasubiri matokeo ya upasuaji, na kuwahoji majirani na kuchunguza video za CCTV eneo hilo” amesema afisa mmoja wa polisi alipokuwa akizungumza na chombo cha habari uko mjini Dehli..

Sababu za mauaji hayo pamoja na wahusika bado hazijawekwa wazi na polisi mjini Delhi imesema itatoa taarifa baada ya uchunguzi kufanyika.

Viwanja Vinauzwa Kwa Bei Nzuri Kabisa

$
0
0
VIWANJA VYENYE USALAMA:  Tunauza sqm 2600 Tsh 35 milioni na sqm 600 Tsh millioni 9 eneo Mingoi mita 300 kutoka Barabara ya lami yani Bagamoyo road pia km 1 kutoka Bunju sokoni 

Hapa umeme na maji vipo na majirani washajenga kulipa very standard pia sqm 1400 Tsh million 18, sqm 2400 Tsh million 24 .

Vipo ambayo tunakata vidogo vidogo yani mita 10kwa20 mil 2 pia awamu inaruhusiwa.Karibuni 0677705808


Mwenyekiti UVCCM apandishwa kizimbani, aachiwa kwa dhamana

$
0
0
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) Wilaya ya Tarime, Godfrey Francis leo Jumatatu Julai 2, 2018 amepandishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi wilaya ya Tarime, kushtakiwa kwa kosa la kusambaza taarifa za uwongo kwa njia ya mtandao wa kijamii.

Taarifa hizo ni kuhusu kukamatwa kwa mmiliki wa kampuni ya mabasi ya Zakaria, Peter Zakaria.

Kiongozi huyo ambaye jana alihojiwa na polisi kwa saa kadhaa amesomewa mashtaka na mwendesha mashtaka wa polisi, Kazeni Mrita.

Mbele ya hakimu mkazi Veronica Mugendi, Mrita amedai mshtakiwa amesambaza taarifa hizo mchana wa Julai Mosi, 2018 kwa kuandika kuwa Zakaria alitaka kutekwa na watu wasiojulikana ambao hata hivyo aliwazidi nguvu kwa kuwajeruhi wawili kati yao.

Francis anayetetewa na wakili Onyango Otieno ameachiwa kwa dhamana hadi Julai 30, 2018 shauri hilo litakapotajwa.

Ametimiza masharti ya kuwa na wadhamini wawili ambao kila mmoja amesaini hati ya dhamana ya Sh2 milioni.

Nassari Akana Kumshambulia Mwigulu Nchemba

$
0
0
Mbunge wa Arumeru Mashariki (CHADEMA), Joshua Nassari amekataa tuhuma za kumshambulia kwa maneno, katika mitandao ya kijamii aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba.

Nassari ametoa kauli hiyo leo na kudai kuwa hatumii akaunti hiyo twitter na amejaribu kufuatilia anayetumia jina lake kwenye mtandao huo kufanya vitu ambavyo hata yeye hapendezwi navyo lakini hajafanikiwa.

“Situmii hiyo akaunti twitter na siyo mara ya kwanza mwenye hiyo akaunti kuandika vitu vya ajabu ambavyo havinihusu na nimejaribu kumtafuta mara kadhaa lakini sijafanikiwa, bora angekuwa anaandika hata mambo ya kilimo ningemuona ana akili”, amesema Nassari.

Ikiwa imepita siku moja tangu kutangazwa kwa mabadiliko ya baraza la Mawaziri huku Mwigulu akiachwa, kupitia ukurasa wa ‘twitter’ wa mtu anayejiita Joshua Nassari ameandika ujumbe uliosomeka kuwa, “Kutumbuliwa kwa Mwigulu hakumsafishi kwa wananchi”.

Wizara Ya Afya Yatangaza Rasmi Kupokea Hospitali Za Rufa Za Mikoa

$
0
0
NA WAMJJW-DAR ES SALAAM
WIZARA ya afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto imetangaza rasmi kuanzia Juali 1 2018  imepokea Hospitali 28 za Rufaa za Mikoa ambazo zilikuwa chini ya usimamizi wa OR-TAMISEMI .

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati alipofanya ziara katika Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala.

“Hospitali ambazo tumezipokea zina jumla ya vitanda 7,474 na jumla ya watumishi 8,671 ambao, kati yao Wauguzi ni 3,960, Madaktari 536, Madaktari Bingwa wa fani mbalimbali ni 182, na waliobakia ni watumishi wa kada zingine mbalimbali za Afya” alisema Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema kuwa Hospitali ambazo Wizara imezipokea ni Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mount Meru (Arusha), Dodoma General (Dodoma), Kitete (Tabora), Shinyanga, Geita, Singida, Mpanda (Katavi), Mawenzi (Kilimanjaro), Bombo (Tanga), Morogoro, Ligula (Mtwara), Sokoine (Lindi), Maweni (Kigoma), Sekou Toure (Mwanza), Mwananyamala, Amana, Temeke (Dar es Salaam), Songwe, Kibena (Njombe), Iringa, Tumbi (Pwani), Sumbawanga (Rukwa), Bariadi (Simiyu), Musoma (Mara), Songea (Ruvuma), Mbeya, Babati (Manyara) na Bukoba (Kagera).

Waziri Ummy alisema kuwa katika mwaka wa fedha 2018/19, Wizara imetenga shilingi Bilioni 30 kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya kipaumbele katika Hospitali za Rufaa za Mikoa ambako tayari huduma zinatolewa ikiwemo Matibabu kwa wagonjwa wa dharura ,Huduma za upasuaji wa dharura hususan wakati wa ujauzito na uzazi pamoja na Huduma za tiba kwa wagonjwa mahututi zikiwemo za watoto wachanga .

Mbali na hayo Waziri  Ummy amesikitishwa na upungufu wa wodi pamoja na vitanda kwa ajili ya  wanawake wanaofika kujifungua katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala na kuahidi kulifanyia kazi mara moja iwezekanavo.

“Kama Mama,na nimeumia sana na lazima tulifanyie ufumbuzi mara moja kwahiyo namuagiza katibu mkuu alete mtaalamu wa majengo na tupandishe fedha za kujenga ghorofa mbili mara moja kwakweli halii hii haikubaliki” alisema Waziri Ummy.

Mnamo Novemba 25, 2017 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akizindua Hospitali ya Taaluma na Tiba (MAMC) ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) aliagiza kuwa Hospitali za Rufaa za Mikoa zihamishiwe kwenye usimamizi wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (WAMJW) kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI.

TRC Yaendelea Kuboresha Miundombinu Ya Reli Ya Kati Kutoka Dar Hadi Isaka

$
0
0
*Yasema ni marufuku kufanya biashara pembezoni mwa reli, yaiomba jamii kulinda miundombinu

SHIRIKA la Reli Tanzania(TRC)limesema linaendelea na mkakati wa uboreshaji wa reli ya kati kutoka Dar es Salaam hadi Isaka ambapo dola za Marekani milioni 300 zitatumika katika uboreshaji huo.

Limesema lengo la kuboresha reli hiyo ni muendelezo wa kuhakikisha usafiri wa treni nchini unakuwa wa uhakika zaidi na hiyo itafungua fursa za kiuchumi hasa katika kipindi hiki cha  mchakato wa ujenzi wa viwanda nchini.

Hayo yamesemwa leo na Mratibu wa Uboreshaji wa reli ya kati Mhandisi Mlemba Singo akiwa katika banda la TRC lililopo kwenye maonesho ya bishara yanayoendelea viwanja vya Sabasaba jijini Dar es salaam.

Amefafanua mradi huo umefadhiliwa na Benki ya Dunia na utatekelezwa na TRC katika kipindi cha muda wa miaka miwili kuanzia Juni mwaka huu hadi Juni mwaka 2020.

Amesema lengo la uboreshaji wa reli ya kati ni kutoa usafiri wa kuaminika na kukuza upatikanaji wa huduma bora nchini  na maboresho hayo yatasaidia kuinua uwezo wa kubeba mzigo toka tani 13.5 za uzito wa ekseli hadi tani 18.5.

Mhandisi Singo amesema maboresho hayo yataenda sambamba na kutandika upya njia za reli zenye uzani wa paundi 80 kwa urefu wa kilometa 312, kufanya ukarabati wa njia ya reli iliyosalia kwa urefu wa kilometa 658 na kufanya ukarabati wa makaravati na madaraja 442.

Pia kuboresha mfumo wa mawasiliano , kuboresha vituo vya kupakia na kupakua mizigo vya bandari ya Dar es Salaam ,Ilala na Bandari kavu ya Isaka.

Amesema kuwa katika maboresho hayo wamejipanga kuboresha na kuongeza kiwango cha ubebaji mizigo kwa miundombinu ya reli na madaraja na kuongeza mwendokasi wa treni kutoka kilometa 35 kwa saa hadi kufikia kilometa 70 kwa saa.

Ameongeza kupitia mradi huo TRC pia imetengeneza mpango endelevu wa matengenezo ya miundombinu ili kufanya njia ya huo kuwa wa uhakika na kuaminika.

“Kuimarika kwa usafiri wa reli kutapunguza gharama za matengenezo ya barabara na hivyo Serikali kuendeleza bajeti iliyookolewa kwenda kwenye huduma nyingine za kijamii.

Mhandisi Singo amesema lengo lao pia ni kupunguza gharama na muda wa usafiri wa mizigo kutoka bandari ya Dar es Salaam hadi bandari kavu ya Isaka hadi kufikia saa 24 kutoka zaidi ya saa 36 ya sasa.

Kwa upande wake Meneja Mawasiliano wa TRC Jamila Mbarouk amewataka Watanzania kuhakikisha wanakuwa walinzi wa miundombinu ya reli na kufafanua kuna baadhi ya wananchi wamekuwa wakiharibu miundombinu na kufanya hujuma ikiwamo ya kuiba kokoto.

Pia amesma ni marufuku kufanya biashara pembezoni mwa reli na kwamba anayateka kufanya biashara pembeni ya reli itawezekana pale tu atakapopata kibali maalumu.

Mbarouk amesema ni marufu kupitisha mifugo kwenye reli na kueleza dhamira ya TRC ni kuona wananchi wananufaka na mradi huo na hakuna madhara yanayoweza kutokea.

Ufunguzi Rasmi Wa Maonesho Ya Biashara Yanayoendelea Sabasaba Sasa Kufanyika Julai 4

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images