Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli ataka uchunguzi mkataba wa Lugumi

$
0
0
Rais John Magufuli amemuagiza waziri mpya wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola kufanya uchunguzi wa mradi wa Sh37 billioni wa ujenzi wa vituo 108 vya polisi ulioingiwa kati ya wizara hiyo na kampuni ya Lugumi Enterprises Limited.

Amesema Serikali ilipewa maagizo na Bunge kuchukua hatua kwa baadhi wa watu waliobainika kufanya makosa katika utekelezaji wa mradi huo lakini anashangaa mpaka sasa haoni hatua zinazoonekana zikichukuliwa.

Kiongozi Mkuu huyo wa ncuhi ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Julai 2, 2018 Ikulu Dar es Salaam muda mfupi baada ya kuwaapisha viongozi aliowateua jana, wakiwemo mawaziri watatu na naibu mawaziri wawili.

“Kuna baadhi ya vitu katika mradi huo havijakamilika, vitu vingine wame-exaggerate (wameongeza makadirio) lakini hakuna hatua zilizochukuliwa,” amesema Rais Magufuli.

Amemwagiza pia kuchukua hatua kwa waliohusika na mradi wa kuagiza magari 777 ya polisi aliyodai yaliagizwa kupitia mkataba wa ovyo.

Amesema baadhi ya magari hayo yaliagizwa kama mapya lakini tayari yametembea zaidi ya kilomita 4, 000 na yapo ambayo hayajaandikwa hata tarehe ya kutengenezwa.

“Mkataba wenyewe ni wa ajabu, nimempeleke katibu mkuu (Wizara ya Mambo ya Ndani) Meja Jenerali sikufanya makosa, nimefanya kwa makusudi. Ninaposema mkataba ni wa ovyo najua ni wa ovyo. Niliowapeleka pale hawakuyaona haya,” amesema Rais Magufuli.

Wizara Ya Mambo Ya Ndani Yamkera Rais Magufuli.....Kasema Kachoka Kutuma Salamu za Rambirambi

$
0
0
Rais John Magufuli amesema amechoka kutuma rambirambi kufuatia wingi wa ajali za barabarani zinazopoteza maisha ya wananchi wengi.

Akizungumza leo Julai 2 baada ya kuwaapisha viongozi aliowateua Julai 1, Rais Magufuli amesema kuwa anashangazwa na kuwa yeye tu ndiye hutoa salamu hizo wakati Waziri wa Mambo ya Ndani yupo na anaenda kwenye mambo yake.

“Kinachonisikitisha waziri na katibu mkuu wao hawatumi hata rambirambi. Mfano mzuri ni ajali ya Mbeya watu 40 wamekufa hakuna hatua hata ya kuwaambia RPC na RTO wajiuzulu ili wajue uchungu wa damu zilizomwagika. Hiyo kazi si ya Rais ni ya waziri na hata katibu mkuu,” alisema Rais Magufuli.

Ameonesha pia kusikitishwa na Wizara ya Mambo ya Ndani kushindwa kuchukua hatua kwa watu waliotajwa kuhusika na ufisadi kupitia mradi wa vitambulisho vya taifa na mingineyo.

“Kuna pesa za Nida zilichezewa ovyo ovyo tukachukua hatua kuwasimamisha wahusika lakini waliofanya hivyo sijaona hatua zilizochukuliwa kwa waliofanya ovyo. Je, pesa wamerudisha? Alihoji Rais Magufuli na kuongeza kuwa kuna ucheleweshaji wa kutoa maamuzi katika suala hilo.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amemtaka waziri mpya wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Kangi Lugola kusimamia vitengo vyote vya wizara yake na akieleza wazi wazi kusikitishwa na kutojaliwa kwa idara ya Zimamoto.

“Wizara ina mambo mengi na vitengo vyake, Zimamoto wana magari 53 tu lakini sikumbuki kuletewa maombi ya Zimamoto. Haya tumeyajua kwa kuuliza uliza tu lakini wenye wizara hawasemi,” aliongeza.

Profesa Mbarawa amshukuru Rais Magufuli kwa kumteua tena

$
0
0
Profesa Makame Mbarawa amemshukuru Rais John Magufuli kwa kumteua tena kuwa waziri, safari hii akipewa Wizara ya Maji na Umwagiliaji.

Katika mabadiliko ya baraza la mawaziri yaliyofanywa na kiongozi mkuu huyo wa nchi jana Jumapili Julai Mosi, 2018, Profesa Mbarawa amehamishwa kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, kwenda wizara yake hiyo mpya.

Mwigulu aenguliwa akiwa mgeni rasmi

Katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter, msomi huyo amemshukuru Rais Magufuli kwa kuendelea kumuamini.

“Namshukuru Rais kwa kuendelea kuniamini na kuniteua tena kwa nafasi ya waziri kuongoza wizara ya maji,” amesema.

“Nawashukuru pia wote ambao tumeendelea kushirikiana katika utumishi kwenye wizara Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Tuendelee kushirikiana kwa maendeleo ya Watanzania wote.”

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya July 3

Mbowe na Viongozi 8 wa CHADEMA wamemkataa Hakimu

$
0
0
Vigogo tisa wa Chadema akiwemo mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe wamewasilisha ombi la kutaka Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Wilbard Mashauri kujitoa kusikiliza shauri lao.

Kufuatia ombi hilo, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imepanga Julai 5, 2018 kutoa uamuzi katika kesi inayowakabili viongozi hao.

Uamuzi huo wa mahakama umetolewa jana Jumatatu Julai 2, 2018 na Mashauri baada ya  washtakiwa hao  kueleza sababu ya kutokuwa na imani nae.

“Baada ya kusikiliza sababu za washtakiwa walizotoa hapa mahakamani za kumtaka hakimu anayeendesha shauri hili kujitoa, Julai 5 mahakama hii itatoa uamuzi kama hakimu huyo ajiondoe kuendesha shauri hilo au asijiondoe” alisema hakimu Mashauri.

Wakili wa utetezi, Peter Kibatala alisema wateja wake wamemueleza kuwa hawana imani na hakimu Mashauri anayeendesha kesi hiyo na wanaomba ujitoe kusikiliza shauri hilo, hivyo wanaomba nafasi ili waweze kueleza sababu za kutokuwa na imani nae.

Aliyeanza kueleza sababu za kutokuwa na imani na hakimu huyo ni Mbowe ambaye alidai kuwa ana sababu kumi.

Baada ya kupitia hoja za pande zote ambazo pia zilitolewa na washtakiwa wengine, Hakimu Mashauri aliahirisha kesi hiyo hadi Julai 5, 2018  atakapotoa uamuzi.

Washtakiwa katika Kesi hiyo  ni Mbowe, naibu makatibu wakuu, Salum Mwalimu (Zanzibar) na John Mnyika (Bara); mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche; mbunge wa Kawe, Halima Mdee; mbunge wa Bunda, Esther Bulaya.

Wengine ni Katibu Mkuu wa Chama hicho, Dk Vicent Mashinji;  mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa na mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko.

Washtakiwa kwa pamoja  wanakabiiwa na mashtaka 13.

Mbunge Majimarefu afariki dunia

$
0
0
Mbunge wa Korogwe Vijijini (CCM),  Steven Ngonyani maarufu Profesa Majimarefu amefariki dunia  usiku wa Julai 2,  2018 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
 
Taarifa ya kifo cha mbunge huyo imethibitishwa na ofisa uhusiano wa Muhimbili,  Aminiel Eligaeshi.
 
Juni 20,  2018 Majimarefu alihamishiwa kwa ndege kutoka mkoani Dodoma kwenda MNH kwa matibabu. Hata hivyo kilichokuwa kikimsumbua mbunge huyo hakikuwekwa wazi.
 
Juni 6,  2018 mbunge huyo alifiwa na mkewe,  Mariam aliyekuwa akipatiwa matibabu MNH

Familia ya Tundu Lissu kudai matibabu mahakamani

$
0
0
Wakati mbunge Tundu Lissu akiendelea na matibabu nchini Ubelgiji, kaka yake, Alute Mughwai amesema wanatarajia kwenda mahakamani kudai haki ya kisheria ya matibabu ya mbunge huyo.

Akizungumza jana Jumatatu Julai 2, 2018 na waandishi wa habari, Mughwai alisema wanachukua hatua hiyo baada ya Bunge kuiandikia barua familia hiyo, ikieeleza kuwa kuanzia sasa haitajishughulisha na matibabu ya mbunge huyo.

Mughwai alisema Juni 18, 2018  walipokea barua kutoka uongozi wa Bunge kuwa haitajishughulisha na matibabu ya mbunge huyo kwa kuwa yuko nje ya nchi kwa utaratibu binafsi.

“Limesema kwa kuwa anapatiwa  matibabu uko nje ya nchi kwa  utaratibu binafsi na hakufuata utaratibu wa matibabu,”alisema

Alisema kutokana na hali hiyo wanaangalia utaratibu wa kwenda mahakamani  kuangalia kama mwakilishi huyo anahaki kisheria ya  kupatiwa  matibabu.

Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Yanayosumbua Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume, Kisukari,

$
0
0
BABU MADUHU NI BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU YANAYOSUMBUA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME, KISUKARI, MIVUTO YOTE, KUSAFISHA NYOTA, KURUDISHA MALI, NK.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:

KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni NYASOSE MIX, Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1. MKEBE NO.1 Hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo la kwanza bila kuchoka naitakufanya uwe na hamu ya kuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

MHESHA POWER
MKEBE NO 2 ni dawa ya kuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,

KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ITINYA,
Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake, humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa pia ana pete za bahati ambazo zimetajilisha wengi.

SUPER POWER,
Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO HOTEL/KANISANI

SIMU NO 0652 102 152/0755 684 297/0788 330 105.

HUDUMA HII UNAWEZA KUIPATA/KULETEWA MAHALI POPOTE NCHINI

Rais Magufuli: Mikoa Ya Kusini Mngefanya Vurugu Kisa Koroshoi Ningetoa Kipigo Kizito

$
0
0
Rais John Pombe Magufuli amesema alikuwa akisubiri wakulima wa mikoa ya Lindi na Mtwara wafanye fujo kama jinsi ambavyo Wabunge wa mikoa hiyo walivyokuwa wakidai na kueleza kwamba angewashughulikia kwa kipigo na angeanza na jimbo linaloongozwa na Waziri Mkuu.

Rais Magufuli ameyasema hayo jana wakati alipokuwa akitoa hotuba yake baada ya kuwaapisha Mawaziri na viongozi wengine ambao aliwateua siku ya jana alipofanya mabadiliko madogo katika wizara yake.

"Watu wanataka popularity, wengine nilisikia wanasema watachomewa nyumba, nilimwambia Waziri Mkuu nataka nione wakifanya fujo.  Ningewapa kipigo. Tena ningeanza kwenye jimbo lake kama kuna shangazi zake ningeanza kupiga hao. Nasema ukweli wala sifichi"

Rais aliongeza "Lazima tufike mahali tuambizane ukweli, ndiyo maana nilimwambia Katibu Mkuu CCM, aende Dodoma siku ya kupiga kura. Wabunge wa CCM ambao hawakuwepo wachukuliwe hatua".

Katika kuonyesha kukasirishwa na kitendo ambacho kilifanya na Wabunge wa Mikoa hiyo ambo pia ni wa CCM, Rais Magufuli alisema anashangaa wanafanya nini mpaka saizi kwenye Chama Cha Mapinduzi  badala ya kuondoka.

"Watu wanashangilia uongo, tumechoka, nilimuuliza Waziri Mkuu kuna wabunge wangapi wa CCM, Mtwara na Lindi akasema wapo 17, nikasema bora waondoke wote, hata Waziri Mkuu ni wa huko naye angeondoka, bado tungeweza kuongoza nchi. Nilimpigia simu Katibu wa CCM tukae kwenye mpango huo. Wangeondoka,"

Pamoja na hayo, Rais Magufuli alisema "Siku ya kupitisha bajeti nikamwambia Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru nenda Bungeni ukaangalie wabunge wangapi wa CCM hawapo bungeni uwalime barua, na kweli amewaandikia barua wote. Japo wapo Wabunge waliokuwa na sababu za Msingi lakini kuna wale ambao wamelimwa barua. Prof. Kabudi alikuwa amelazwa lakini kapokea barua yake na ataambatanisha na vyeti vya hospitali"

Mbali na hayo Rais amempongeza Naibu Waziri Mpya wa Kilimo na Umwagiliaji kwa kuweza kupambana kuitetea serikali wakati wa hoja ya Korosho ilipokuwa imepamba moto.

“Nakupongeza Naibu Waziri wa Kilimo (Omary Mgumba) kwa kazi uliofanya Bungeni, huwa nafuatilia michango ya CCM, mwingine anasema tukienda hivi tutashindwa, kwa nini bado uko CCM, si utoke huko? Ulinyimwa nafasi ya kutetea hoja yako, mmoja akapewa nafasi ya kukupiga na mwingine tena akakupiga, hiki ulichokipata ndicho ulistahili, nakuomba ukashirikiane na wenzako Wizara ya Kilimo." Alisema

Silya: Dawa Bora ya Nguvu za Kiume

$
0
0
SILYA:  Ni dawa ya nguvu za kiume inayoponesha na kuongeza ndani ya dakika 10 tu. Dawa hii inaimarisha misuli ya uume iliyolegea au kusinyaa, ni dakika 3 tu.

Dawa hii inarefusha maumbile mafupi kufikia Inch 6-7, inanenepesha uume mfupi cm 4. Dawa hii inakufanya uchelewe kufika kileleni wakati wa tendo la ndoa dk 20-30.

Inaongeza uzalishaji wa mbegu za kiume, inakufanya uweze kurudia tendo hata mara 5 bila kujali umri kama nikijana au mzee.

Pia ipo dawa ya kumrudisha mume, mke aliyekuacha au kumpata yeyote umpendaye.. Je umedhulumiwa,au umeibiwa Pesa zako ? Utarudishiwa ndani ya masaa  3.

Tunatibu Presha, Mgongo,Kisukari, Kiuno, Vidonda vya tumbo, kujaa gesi nk. Pata dawa ya mvuto, toa makovu, chunusi mabaka, punguza unene wa mwili, tumbo.

Tupo Dar es Salaam.

Simu: 0784 066 543 /  0653 715 642- Dr Hussein

Rais Magufuli Kafanya Uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Ngenya Athuman Yusuf kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Dkt. Ngenya Athuman Yusuf umeanza tarehe 30 Juni, 2018.

Kabla ya uteuzi huo Dkt. Ngenya Athuman Yusuf alikuwa Mhadhiri Mwandamizi katika Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro (MUM).

Dkt. Ngenya Athuman Yusuf amechukua nafasi ya Prof. Egid Beatus Mubofu ambaye ameteuliwa kuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Ndege kubwa ATCL kufika mwezi huu

$
0
0
Shirika  la Ndege Tanzania (ATCL) limebainisha kuwa ndege yake mpya yenye uwezo wa kubeba abiria 262, itawasili mwezi huu. Ndege hiyo itafanya safari nchini kwa mwezi mmoja kabla ya kuanza safari zake rasmi kwenda Mumbai, India.

Limesema ikiwa nchini itafanya safari katika viwanja vya Kilimanjaro na Mwanza kwa gharama nafuu, kwa lengo la kuwezesha Watanzania kutumia ndege yao kwa bei ya punguzo.

Mkuu wa Idara ya Biashara, Lily Fungamtama amebainisha hayo katika Maonesho ya 42 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam na kueleza kuwa ndege hiyo ina uwezo wa kwenda safari ya moja kwa moja kwa saa 18 na ya kwanza kwa ajili ya safari za nje ya nchi kwa kuanzia na Mumbai.

Fungamtama amesema, kabla ya mwisho wa mwaka huu, wanatarajia kupokea ndege nyingine mbili hivyo kuongezeka kwa safari za masafa ya mbali.

Amesema, kwa sasa shirika hilo linafanya safari ndani ya nchi katika mikoa ya Kilimanjaro, Mwanza, Mbeya, Tabora, Kigoma, Bukoba na visiwa vya Zanzibar huku wakifanya safari za Songea lakini kwa sasa wamesitisha kwa ajili ya kiwanja kinafanyiwa marekebisho.

Fungamtama amesema kwa nje ya nchi wanafanya safari za Comoro huku wakiwa na mipango ya kuanza safari Bujumbura Burundi na Entebbe Uganda huku wakiwa tayari kukabiliana na ushindani wa kibiashara katika sekta hiyo.

'Hatuogopi ushindani kwani tuko imara katika kuongeza ubora wa huduma zetu, uhakika wa safari, kupunguza kuchelewa, muda, kusitisha safari, pamoja na usalama wa abiria na mali zao, uaminifu, maadili pamoja na kusimamia miongozo ipasavyo,`alisema.

Alisema shirika hilo lina wataalamu waliobobea katika kila sekta kuanzia uongozi hadi huduma ndani ya ndege, kwani wamepikwa na chuo chao na wengine kutoka nje ya nchi huku wakialika watu kusoma katika chuo chao chenye wataalamu waliopitishwa na Mamlaka ya Anga..

“Watanzania wameitikia huduma zetu hasa kwa kuwa na bei shindani, kwa kweli wananchi wanatupa support kubwa pamoja na Rais amekuwa akitusaidia katika kila nyanja hivyo ni vema wananchi kutumia ndege yetu ili kutunza chetu kidumu,`alisema.

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Bunge laomboleza Kifo cha Mbunge Profesa Maji Marefu

$
0
0
Spika wa Bunge Job Ndugai ameeleza kusikitishwa na kifo cha Mbunge wa Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani aliyefariki usiku wa kuamkia leo wakati akiendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, jijini Dar es Salaam.

“Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai anasikitika kutangaza kifo cha Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini mkoani Tanga, Mheshimiwa Stephen Ngonyani, maarufu kwa jina la Profesa Maji Marefu, kilichotokea usiku wa leo (jana usiku) 2 Julai, 2018 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili,” Bunge limeeleza.

Taarifa ya Bunge iliyosambazwa na Kitengo chake cha Habari, Elimu na Mawasiliano imebainisha kuwa chombo hicho kinaendelea kuratibu mazishi kwa kushirikiana na familia ya marehemu na kuongeza, “taarifa zitaendelea kutolewa.”

Profesa Maji Marefu ambaye alizaliwa 25 Mei, 1952, amekuwa Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini tangu mwaka 2010.

Mwaka 2015 alichaguliwa tena kuingia kwenye chombo hicho cha kutunga Sheria lakini katika awamu hii, ameshindwa kushiriki mikutano kadhaa ya Bunge kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa ambao umesababisha kifo chake.

Brazil Yazidi Kuwa Tishio, Yawapiga Mexico 2-0 Na Kutinga Robo Fainali Kombe La Dunia

$
0
0
Mshambuliaji  wa Brazil, Neymar Jr, ameivusha timu ya Taifa ya nchi hiyo hatua ya robo fainali baada ya jana kufunga bao moja kwenye ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mexico, mchezo wa hatua ya 16 ya michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea nchini Urusi.

Mabao ya Brazil yalifungwa na Neymar  dakika ya 51 na Roberto Firmino dakika ya 88.

Dakika ya saba, Neymar, alishindwa kuipatia Brazil bao la kuongoza akiwa katika nafasi nzuri baada ya  kipa wa  Mexico, Guillermo Ochoa, kupangua mchomo wake.

Mexico ilijibu kwa kufanya shambulizi dakika ya 10, lakini beki wa Brazil, Fagner Lemos, alikuwa imara kuokoa  mpira wa hatari usilete madhara langoni mwao.

Mexico ilionekana kuimudu vema Brazil dakika 15 za awali kutokana na kuokoa mipira mingi ya hatari ambayo ingeweza kuleta madhara.

Pia ilifanya mashambulizi kadhaa ya kushtukiza kupitia kwa Chicharito na  Hirving Lozano, lakini kikwazo kilikuwa kwa ukuta wa Brazil uliokuwa chini ya Thiago Silva na Filipe Luis.

Kwa upande mwingine, Neymar na Willian da Silva, mara kwa mara walilitia kashkashi lango la Mexico ambayo wa kiasi kikubwa ilibebwa na uhodari wa kipa wao Ochoa.

Pamoja na jitihada za kila upande kutaka kuandika bao la kuongoza, dakika 45 za kipute hicho zilimalizika kwa nyavu kubaki salama bila kutikiswa.

Kipindi cha pili, kasi ya mchezo huo iliongezeka kutokana na kila upande kusaka bao la kuongoza.

Hata hivyo, Mexico iliendelea na mbinu yake ya kufanya mashambulizi ya kushtukiza na kuiacha Brazil ikimiliki mpira.

Mbinu hii ndiyo iliyoisaidia Mexico kuichapa Ujerumani, ikimuacha mshambuliaji wao, Jesus Gallardo, karibu na eneo la wapinzani.

Dakika 51, Willian aliwahadaa mabeki wa Mexico kabla ya kumdondoshea pasi makini, Neymar ambaye hakujiuliza nini cha kufanya zaidi ya kuukwamisha mpira wavuni.

Bao hilo liliilazimisha Mexico kufanya mabadiliko dakika ya 55, alitoka Edison Alvarez na nafasi yake kuchukuliwa na Jonathan Dos Santos.

Brazil nayo ilifanya mabadiliko dakika ya 86 kwa kumpuzisha Philippe Coutinho na nafasi yake kuchukuliwa na Roberto Firmino.

Mabadiliko hayo yalikuwa na manufaa kwa Brazil kwani dakika ya 88 ilifanikiwa kuandika bao la pili na la ushindi kupitia kwa Firmino.

Kiungo huyo wa Liverpool ya England alifunga bao hilo baada ya kumalizia wavuni mpira uliotemwa na Ochoa aliyepangua kiki ya Neymar.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Ubelgiji Yatinga Robo Fainali Kombe La Dunia..... Ilipigwa 2-0 na Japan, Ikaamka Na Kushinda 3-2

$
0
0
Ulihitajika moyo wa chuma kuamini Ubelgiji wangetoboa. Ilikuwa ni zaidi ya mechi ya hatua ya 16. Ilikuwa ni kufa na kupona. Ulikuwa ni ubabe. Baada ya kushuhudia wakipigwa 2-0 ndani ya dakika nne, ubelgiji waliishangaza dunia.
 
Katika mchezo mkali pengine kuliko yote yaliyoshuhudiwa kwenye fainali za mwaka huu, Ubelgiji walijikuta wakipigwa bao la kwanza katika dakika ya 48 Genki Haguchi kupiga shuti kali lililomzidi ujanja kipa wa Ubelgiji, Thibaut Coutouis kabla Takashi Inui hajaiweka Japan mguu mmoja ndani ya robo fainali, katika dakika ya 52.
 
Japan wakiamini wamemaliza biashara iliyowapeleka katika uwanja wa Rostov Don, Kocha wa Ubelgiji, Roberto Martinez alifanya maamuzi ya kijasiri ambayo mwisho wa siku yaliiokoa Ubelgiji. Mhispania huyo baada ya kuona kikosi chake kimezidiwa, aliamua kuwatoa Ferreira Carrasco na Dries Martens kwa mpigo.
 
Akawaingiza Nacer Chadli na Maroune Fellaini. Wote hawa ni warefu.

Kuanzia hapo Ubelgiji ni kama walizaliwa upya kabisa. Wakapiga mpira mwingi na kuwapoteza Samurai Blue kabisa. Katika dakika ya 69, Jan Vertonghen alipiga krosi iliyotinga nyavuni moja kwa moja.
 
Dakika tano baadaye, Fellaini akasawazisha kwa kichwa safi akiunganisha krosi ya Eden Hazard, huku la tatu na ushindi likiwekwa kambani na Nacer Chadli, kufuatia shambulizi la kushtukiza, kunako dakika ya 90. Mwisho wa siku ndio kama mlivyosikia, Ubelgiji wakashinda 3-2.
 
Licha ya kuwapa tiketi ya kuwafuata Brazil kibabe, Ubelgiji waliweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza kufufuka na kushinda mechi ndani ya dakika 90, baada ya kutanguliwa kwa mabao mawili au zaidi, tangu Ureno wafanye hivyo miaka 52 iliyopita. Mwaka 1966, Ureno walitoka nyuma na kuinyuka DPR Korea 5-3, baada ya Korea kutangulia kupata mabao matatu ya haraka.
 
Aidha ushindi huo, unamaanisha kuwa, Ubelgiji wamefuzu hatua ya robo fainali ya Kombe la Dunia mara mbili mfululizo kwa mara ya kwanza. Hata hivyo, mabao mawili waliyofungwa na Japan yalimaanisha kuwa, Ubelgiji hawajawahi kumaliza mechi bila kufungwa katika mechi 12 za Kombe la Dunia, walizocheza kwenye hatua ya mtoano.

Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Upungufu Wa Nguvu Za Kiume, Maumbile Mdogo, Busha Bila Kupasua

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO : Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliohangaika sehemu mbalimbali bila mafanikio.

Mabula Clinic ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya jeshini. Je unaupungufu wa nguvu za kiume au uume wako mdogo na mwembamba? 

Mapro pawer no 2 ndio tiba, kwa sasa hutibu matatizo matatu kwa pamoja 1. itakufanya uchelewe kufika kileleni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2. Huimalisha misuli iliyolegea na kusinyaa hasa kwa wale walio athirika na upigaji punyeto 3. itakufanya upate hamu ya kurudia tendo zaidi ya mara tatu :Kwa nini ujione mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo 

Makakanua mix ni dawa iliyochanganywa na miti shamba 9 na kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 kwa urefu na unene sentimita 1-5, dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona

 Zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke kwa masaa matatu tu ,mvuto wa biashara, kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu.

Tunatibu ngiri, miguu, mgongo na kiuno kuumwa, kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa 

Tiba na ushauli muone Dr Mabula au piga simu no 0743362017.Huduma zangu utazipata popote ulipo kama uwezi kufika ofisini

Apandishwa kizimbani kwa kumkashifu Rais Magufuli kwa Maneno “Rais kitu gani bwana”.

$
0
0
Mkazi wa Wilaya ya Ngara, Kagera Justin Emmanuel (31)   amefikishwa Mahakama ya Wilaya Misungwi mkoani Mwanza, kwa tuhuma ya kutoa lugha chafu dhidi ya Rais John Magufuli.

Mwendesha mashtaka wa polisi Ramsoney Sarehe alisoma hati ya mashtaka mbele ya ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Erick Marley leo Julai 3.

Sarehe amesema mshtakiwa alitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha sheria namba 89 (1) ya mwaka 2002.

Amesema mshtakiwa alitoa lugha ya kumdhihaki Rais Juni 25 katika Kivuko cha Kigongo saa 10:00 jioni kwa kutamka maneno ya “Rais kitu gani bwana”.

Hata hivyo mshtakiwa alikana kosa hilo na hakimu aliahirisha shauri hilo hadi Julai 26 itakapotajwa tena mahakamani.

Mshtakiwa yupo nje kwa dhamana baada ya kukamilisha masharti ya kuwa na mdhamini mmoja aliyewasilisha bondi ya mali isiyohamishika yenye thamani ya Sh500, 000.

Mwigulu Nchemba Amlilia Profesa Majimarefu

$
0
0
 Mwigulu Nchemba, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ametuma rambirambi kwa msiba wa mbunge wa Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani maarufu Profesa Majimarefu.

Kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter, Dk Nchemba ambaye ni mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), amesema:

“Maandiko matakatifu yanasema, mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake za kuishi si nyingi. Tumempoteza kaka, ndugu na rafiki Comrade Stephen Hilary Ngonyani (Prof. Majimarefu), tumempoteza kiongozi na kada kwelikweli wa Chama cha Mapinduzi. Mungu akupumzishe kwa amani.

Dk Nchemba ametuma rambirambi leo Julai 3, 2018 ikiwa ni twiti yake ya kwanza tangu alipoondolewa kwenye baraza la mawaziri Julai Mosi, 2018.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images