Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ziara Ya Ujumbe Wa Idara Ya Maadili Na Nidhamu Ya Chama Tawala Cha Frelimo Kutoka Msumbiji Ilipotembelea CCM Arusha.

$
0
0
Jana tar. 13 Juni, 2018  Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Arusha imekutana na Ujumbe wa Idara ya Maadili & Nidhamu ya Chama Tawala cha FRELIMO Kutoka Nchini Msumbiji. 

Ujumbe huo uliongozwa na  Katibu wa Sekretarieti ya Kamati Kuu na Gavana wa Jimbo la Mkoa wa  Maputo Nchini Msumbiji Mh. Raimundo Maico Diomba Umekutana na Uongozi wa CCM Mkoa wa Arusha mapema jana Ofisi za CCM Mkoa wa Arusha ili kujifunza mambo kadha wa kadha ikiwemo ni jinsi gani CCM inaweza kusimamia na kuongoza Vikao vya ngazi mbalimbali kwa nyakati mbalimbali pindi kiongozi ama mwanachama anapokwenda kinyume na maadili ya Chama.

“Ama kwa hakika tumejifunza mengi na kubadirishana mawazo  jinsi ya kuboresha Vyama vyetu viendelee kufanya vizuri kwa Wananchi wake ikiwemo kusimamia vyema Maadili kwa wanachama na  Viongozi wake

"Nimependa sana Katiba ya chama cha FRELIMO inayomtambua Mkuu wa Mkoa kama  Katibu Msaidizi wa FRELIMO Mkoa husika lakini pia Katiba ya nchi yao inasema baada ya Uchaguzi Mkuu ilani inayotekelezwa ni ya Chama kilichoshinda nafasi ya Urais," Alisema Robert  Kaseko ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Arusha  na kuongeza kuwa;" Urafiki wetu  na ndugu zetu  FRELIMO daima  utaendelea Kulindwa  kwa  nguvu zote."


Polisi yatoa onyo magari ya Serikali yanayovunja sheria

$
0
0
Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam limesema linaanzisha operesheni maalum kuanzia leo Juni 14,2018 ya kukamata magari yote yatakayopita katika barabara za mwendokasi yakiwemo magari ya serikali kwa madai wao ndio wamekuwa watu wakubwa wa kuvunja sheria.

Hayo yameelezwa na Kamanda Lazaro Mambosasa leo Jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari na kusema kumekuwa na tabia ya vyombo vya moto kutumia barabara zisizo kuwa rasmi kwa wao kutumia bila ya kuwa na dharula yoyote huku akitolea mfano wa gari la wagonjwa lililosababisha ajali hivi karibuni na kuua wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kipindi linawakimbiza kuwapeleka hospitalini eneo la River Side, Ubungo Jijini Dar es Salaam.

"Kumekuwa na tabia sasa ambayo inataka kuota mizizi watu wanahama kwenye barabara husika wanaingia kwenye barabara ya mwendokasi. Barabara hiyo imetengwa kwaajili ya mabasi ya kwenda haraka lakini sasa hivi vyombo vya ulinzi na usalama, madereva wote wanataka kupita katika njia hiyo", amesema Kamanda Mambosasa.

Pamoja na hayo, Kamanda Mambosasa ameendelea kwa kusema "nitoe wito na onyo ni vema barabara zikatumika kwa mujibu wa sheria, maeneo ambayo yana makatazo tusilazimishe kufanya hivyo, nitaendesha opereshe kali na kuhakikisha hili linafanyika na mtu yoyote akikamatwa asipige makelele ninaeleza kila mtu aelewe, magari ya serikali ndio yanaongoza katika hili na hakuna sababu yoyote ya msingi kufanya hivyo".

Kwa upande mwingine, Kamanda wa Kanda maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa amewataka wazazi na walezi kuwa makini na watoto wao wakati wa kuvuka barabara kipindi hiki cha kuelekea Sikukuu ili ajali zisizokuwa za lazima zisitokee.

Mikopo Sekta binafsi Imeongezeka kwa Bilioni 75

$
0
0
Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amesema mikopo iliyotolewa kwa sekta binafsi katika kipindi cha mwaka 2017 imeongezeka kwa  Bilioni 75

Mikopo hiyo imeongezeka kutoka Sh16.808 trilioni zilizotolewa 2016 hadi Sh16.883 trilioni 2017.

Akizungumza bungeni  leo Juni 14, 2018 mjini Dodoma wakati akiwasilisha hali ya mwenendo wa uchumi kwa  mwaka 2017, Waziri Mpango amesema kiasi hicho ni sawa na ukuaji wa asilimia 1.7 ikilinganishwa na asilimia 7.2 kwa 2016.

Amesema hatua hiyo ilichagizwa na tahadhari zilizochukuliwa na benki za biashara baada ya kuongezeka kwa mikopo  iliyoshindikana kulipwa pamoja na benki hizo kupendelea zaidi kuwekeza katika dhamana za serikali.

“Katika kukabiliana na hilo, serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania, imeendelea kuchukua hata mbalimbali ili kuongeza mzunguko wa fedha na kuimarisha ukuaji wa mikopo katika sekta binafsi, hatua hizo ni pamoja na kupunguza kiwango cha kisheria cha sehemu ya amana kinachotakiwa kuwekwa BoT na benki za biashara,”amesema Waziri

Hatua nyingine ni kupunguza riba za BoT, kupunguza riba za dhamana ya serikali , serikali kuendelea kulipa malimbikizo ya madeni kwa wakandarasi na watoa huduma wa hapa nchini. 

Waziri Mpango: Shilingi ilishuka kwa Shilingi 57 mwaka jana

$
0
0
Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amesema licha ya uchumi kuwa imara lakini thamani ya Shilingi dhidi ya Dola ya Marekani ilishuka kidogo.

Akizungumza leo Juni 13, wakati akiwasilisha mwenendo wa uchumi kwa mwaka 2017, Dk Mpango amesema thamani ya Shilingi dhidi ya Dola ilikuwa ya kuridhisha ikibadilishwa kwa Sh2, 228 kwa dola moja.

"Hadi Desemba mwaka 2016 Dola moja ilikuwa inabadilishwa kwa Sh2, 177 na mpaka Desemba 2017 kulikuwa na tofauti ya wastani wa Sh57.79," amesema Mpango.

Mwenendo huo, amesema umetokana na kuboresha kwa usimamizi, utekelezaji wa Sera thabiti za bajeti na fedha na mwenendo mzuri wa urari wa mapato ya fedha za kigeni.

Chenge aitaka serikali kuangalia upya katazo la kusafirisha madini ghafi

$
0
0
Mwenyekiti wa Bunge Andrew Chenge ameiagiza Serikali kuangalia upya katazo la kusafirisha madini ghafi (cabon) kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine kwa sababu halikuzingatia athari watakazozipata wawekezaji wa mitambo ya uchenjuaji.

Chenge amesema hayo bungeni leo Juni 14 baada ya kuombwa mwongozo na wabunge wawili Stanislaus Mabula(Nyamagana_CCM) na John Heche ( Tarime Vijini-Chadema).

Miongozo hiyo imekuja baada ya taarifa iliyotolewa na Waziri wa Madini Angela Kairuki  kuhusu utekelezaji wa agizo la Spika la kuzuia usafirishaji wa kaboni,  baada ya hivi karibuni kuombwa mwongozo na Heche kuhusu suala hilo.

Katika majibu yake Kairuki amesema katazo hilo linalenga kuzuia utoroshwaji wa madini, ukwepaji wa kodi, ada za ukaguzi na ushuru wa huduma.

Akifafanua hayo, Kairuki amesema siku tisa baada ya katazo hilo hilo Serikali mkoani Geita imetoa vibali vya uchenjuaji 40 tofauti na vibali saba walivyokuwa wakitoa kabla ya katazo hilo.

Hata hivyo baada ya maelezo hayo Heche aliomba mwongozo  na kusema katazo hilo limewaathiri kiuchumi wafanyabiashara wanaomiliki mitambo ya uchenjuaji.

"Wengine mheshimiwa mwenyekiti walikuwa na mikopo katika taasisi za fedha wamesitishiwa ghafla. Watawezaje kujenga mitambo haraka haraka? “Amesema.

Naye Mabula amesema watu wanataabika kutokana na katazo hilo na kushauri kuwa Serikali inaweza kuongeza udhibiti na ikapata mapato yake bila kuweka zuio.

"Mwaka  2014 Serikali iliruhusu gesi kusafirishwa kwasababu  ni raslimali ya Taifa... Hawa watu wanataabika. Tatizo ni uchenjuaji ama usimamizi? Usimamizi unaweza kuimarishwa na Serikali ikapata mapato yake," amesema Mabula

Baada ya miongozo hiyo Chenge amesema miongozo hiyo imetokana na wabunge kutoridhika na majibu ya Serikali.

“Unapopiga marufuku na kuanza ( utekelezaji) leo leo, unapaswa kuzingatia upande wa pili pawe na nafasi. Mwongozo wangu Serikali muangalie tena lengo ni mpate mapato halali lakini tusitoe mkanganyiko."amesema.

Serikali Yafuta VAT kwenye taulo za kike (Pedi)

$
0
0
 Serikali imefuta Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT),  kwa taulo za kike (pedi) zinazoagizwa kutoka nje ya nchi.

Msamaha huo umetangazwa leo Alhamisi Juni 14 na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alipokuwa akiwasilisha bajeti  kuu ya serikali kwa mwaka 2018/19.    
                                                                                     “Napendekeza kusamehe VAT kwenye taulo za kike kwa lengo la kuwezesha upatikanaji wa bidhaa hizo kwa bei nafuu kulinda afya ya mama na mtoto wa kike hasa walio vijijini na shuleni,” amesema waziri.

Baada ya kutangaza msamaha huo, Bunge lililipuka kwa shangwe na vigelegele ikizingatiwa ni suala lililokuwa na mchango mkubwa wakati wa mijadala ya hoja za wizara mbalimbali zilizwasilishwa kwenye vikao vinavyoendelea.

Pikipiki na Magari ya mashindano nazo kuondolewa kodi

$
0
0
Waziri wa Fedha, Philip Mpango amesema serikali inatarajia kufanya mabadiliko kwenye sheria ya forodha la jumuiya ya Afrika Mashariki inayotoa msamaha wa kodi kwa magari yanayotumika kwenye mashindano ya mbio za magari na kujumuisha pikipiki kwenye msamaha huo.

Waziri Mpango ameyasema hayo leo Juni 14 wakati akiwasilisha bajeti kuu kwa mwaka wa fedha, 2018/19, bungeni.

 “Hatua hiyo inatarajiwa kuhamasisha mashindano hayo na kukuza sekta ya utalii nchini,” amesema

Dk Mpango pia amesema serikali imepanga kuondoa tozo kwa vifaa vya zima moto, tozo ya ushauri kuhusu usalama wa afya.

Amesema hatua za upunguzaji wa kodi na tozo, zitaanza kutekelezwa Julai mosi, mwaka huu.

Waziri Mpango: Ukusanyaji wa mapato Ulikuwa Trilioni 21 Mwaka 2017/2018

$
0
0
Waziri wa Fedha, Dk Philip Mpango amesema ukusanyaji wa mapato katika vyanzo vyote kwa mwaka 2017/18 yalifikia Sh21.89trilioni sawa na asilimia 69 kwa mwaka.

Ameyasema hayo leo Juni 14, wakati akisoma bajeti kuu  ya serikali kwa mwaka wa fedha, 2018/19.

Amesema kutofikiwa kwa malengo ya ukusanyaji kumetokana na ukwepaji wa kodi, ugumu wa kukusanya kodi kutoka kwa wafanyabiashara wasio rasmi na hawarunzi kumbukumbu, mazingira yasiyo rafiki ya kukusanya kodi, ugumu na gharama kubwa za kulipa kodi.

Ametaja sababu nyingine kuwa ni pamoja na udhaifu wa kutumia mashine za EFD, mpango mdogo na utegemezi wa sekta ya umma kwa sekta binafsi.

Kuhusu mikopo ya ndani, Dk Mpango amesema Serikali ilikopa jumla ya Sh4.9 trilioni sawa na asilimia 80 ya zilizotarajiwa kukopwa na Serikali ilikopa kutoka soko la nje Sh414 bilioni.

"Fedha hizi zimeelekezwa kwenye miradi ya mkakati," alisema Dk Mpango.

Kuhusu deni la Serikali, alisema limekuwa likiongezeka lakini bado ni himilivu.

"Uwiano kwa pato la Taifa ni asilimia 34 ukilinganisha na asilimia 56 ya ukomo," amesema.

Amesema Serikali imeandaa mkakati wa kulipa madeni na kuzuia ulimbikizaji wa madeni kama wakandarasi na wazabuni.

Ajali ya Basi Yaua Wanajeshi 10 wa JKT

$
0
0
Basi lenye namba za usajili T 755 BAB lililokuwa likisafiri kutoka mkoani Tabora kuelekea mkoani Mbeya, limepata ajali leo Alhamisi, Juni 14, 2018 katika eneo la Igodima jijini Mbeya na kusababisha vifo vya askari 10 wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) waliokuwa wakitoka mafunzoni na kujeruhi wengine kadhaa.

Taarifa za awali kutoka eneo la tukio zinadai kuwa, basi lililokuwa limewabeba wanajeshi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania lililokuwa likitokea Tabora kuelekea Mbeya limepinduka katika mteremko wa Igodima, Mbeya.

Chanzo cha ajali hiyo kimesekana kuwa ni mwendokasi uliopelekea  kukatika kwa ‘break’ kutokana na mteremko mkali katika eneo la Igodima na kuangukia korongoni.

Serikali yaongeza ushuru wa Chokoleti, Pipi

$
0
0
Ili kuhamasisha uzalishaji wa ndani, Serikali imetangaza kupandisha ushuru wa forodha kwenye peremende, chokoleti, bazoka (chewing corn) na nyanya zilizosindikwa kutoka nje.

Akizungumza bungeni leo Juni 14, wakati akiwasilisha bajeti kuu ya serikali kwa mwaka wa fedha 2018/19, Dk Mpango amesema ushuru huo umeongezeka kwa asilimia 10 kutoka asilimia 25 iliyokuwa inatozwa mwaka huu wa fedha mpaka asilimia 35 kuanzia Julai Mosi.

“Lengo la hatua hii ni kulinda uzalishaji wa bidhaa hizo katika viwanda vya ndani, ajira,” amesema Dk Mpango.

Waziri Mpango amesema nchi za Afrika Mashariki zina uwezo wa kuzalisha  chokoleti na kutosheleza mahitaji ya soko.

Salah Ufufua Matumaini Ya Waafrikakombe La Dunia

$
0
0
Na magdalena kashindye.
Nyota wa Liverpool na timu ya taifa ya Misiri, Mohamed Salah amepona majeraha yake.

Mchezaji huyo anapewa nafasi kubwa ya kukiongoza kikosi cha Misri Ijumaa ya wiki ijayo dhidi ya Uruguay ukiwa ni mchezo wa kwanza kwa taifa hilo katika michuano ya Kombe la Dunia inayoanza leo.

Salah aliumia katika mchezo wa fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya kwa kuchezewa faulo mbaya na nahodha wa Real Madrid, Sergio Ramos na kuondolewa nje wa uwanja hali iliyozua hofu kwa mashabiki wa misiri kuwa angekosa mchezo ya fainali la kombe la dunia inayofanyika nchini Urusi.

Kupona kwa Salah kumefufua  matumaini ya Waafrika  kwenye safu ya ushambuliaji wa timu hiyo kutokana na uwezo  mkubwa aliouonesha uwanjani mwaka huu.

Mtoto Afanyiwa Ukatili Kwa Kuchomwa Moto Makalio

$
0
0
Na magdalena kashindye kahama
Mtoto mwenye umri wa miaka {11}amechomwa moto makalioni na kufungiwa ndani kwa muda wa siku mbili kwa kosa la kuiba pesa kiasi cha shilingi elf tano kitendo ambacho ni cha kikatili katika maisha yake .

Mtoto huyo   anayesoma darasa la tatu  katika shule ya msingi Mwinyi iliyopo mkoani Tabora jina limehifadhiwa  amefanyiwa ukatili huo siku ya jumatatu ya tarehe 11  /06 /2018 akiwa kwa baba yake mdogo wilayani kahama.

 Akizungumza na kituo hiki Mtendaji wa mtaa wa nyihogo Bwn.Antony Costa  amesema kuwa amepata taarifa kutoka kwa mwenyekiti pamoja na majirani wa familia hiyo na kuwa mtuhumiwa wa kosa hilo bado hajakamatwa

'Nilipata taarifa za tukio hilo kutoka kwa mwenyekiti wa mtaa na majirani na ndiponilipofika eneo la tukio na mtuhumiwa hajakamatwa "alisema Costa. .….

Pia msemaji wa Dawati La Jinsia wilayani Kahama mkoani shinyanga Bi . Jenny Joakim Eras  amekili kupokea  tukio la mtoto huyo ofisi kwake na kuwa mtoto anaendelea na matibabu katika hospitali ya halmashauri ya mji wa kahama .

Eras  ametoa ushauri kwa wanajamii  kuwa na malezi bora kwa watoto woa kwa kuzingatia sheria ya mtoto ya mwaka 2009. .

Urusi Yaanza Vyema Kombe La Dunia....Yaitandika Saudi Arabia Bao 5-0

$
0
0
Dakika 90 zimemalizika katika Uwanja wa Luzhniki kwa wenyeji Urusi kuibuka na ushindi wa kishindo wa mabao 5-0 dhidi ya Saudi Arabia katika mechi ya ufunguzi wa michuano ya Kombe la Dunia.

Mechi hiyo ya aina yake imeshuhudiwa bao la kwanza likiwekwa kimiani mnamo dakika ya 12 na Ganzizky ambalo limeandika rekodi ya kuwa bao la kwanza katika mashindano ya Kombe la Dunia kwa mwaka huu.

Mabao mengine yametiwa kimiani na Cheryshev (43' minutes, 90'+1), Dzyuba (71' ) na Golovin (90'+4).

Baada ya wenyeji kuanza vizuri, mechi zingine za kesho zitakuwa ni Iran itakayowakaribisha Morocco na vilevile Ureno itakuwa inacheza dhidi ya Spain.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya June 15

Miti Na Mimea Inayo Kaliwa Na Majini Mseto

$
0
0
Katika  uganga  na  uchawi  miti  na  mimea imegawanyika  katika  makundi  makuu  matatu.

Kundi  la  kwanza  linahusisha  miti na  mimea  inayo kaliwa  na majini  na  malaika  watukufu  pekee.

Kundi  la  pili  ni  miti  na mimea  inayo  kaliwa  na  majini  wa  kisheitwani  pekee.

Na   kundi  la  tatu  ni  miti  ambayo   ina kaliwa  na  majini  wa  kisheitwani  pamoja  na  majini  watukufu  kwa  wakati mmoja.

Katika  lugha  yakitabibu  miti  na  mimea  inayo  kaliwa  na  majini  wa  kisheitwani  na  majini  watukufu  kwa  pamoja, hujulikana  kama  miti  au  mimea  mseto.

Hii ni  miti   ambayo  ndani  yake  wanaishi  majini  wa  kisheitwani  na  majini  watukufu  kwa  pamoja.

Miti  hii  ina  sifa  moja  kubwa  na  ya  kipekee  nayo  ni  kutumika  katika uganga  na  uchawi  .

Uchawi  kwa  maana  ya  ufisadi  na  uharibifu   na  uganga  kwa  maana  ya  kujenga, kutengeneza  pamoja  na kupambana  na  uharibifu  unao  sababishwa  na  wachawi.

Miti   inayo  kaliwa  na  majini mseto  (  Yaani  majini  wa  kisheitwani  na  majini  watukufu )  ipo mingi  sana.

Miongoni  mwa  miti  hiyo   ni  pamoja  na  mti  wa  Tumbaku au  Mtumbaku.

MAJINI  WA  KISHEITWANI  NA  MAJINI  WATUKUFU  WANAWEZA  VIPI  KUKAA  NDANI  YA  MTI  MMOJA  KWA  WAKATI  MMOJA.

Majini  wa  kisheitwani  na  majini  watukufu  wanaweza  kukaa  ndani ya  mti  au  mmea  mmoja  katika  namna  inayo  fanana  kwa  kiasi  kikubwa  sana  na namna  ambavyo  matangazo  ya  vituo  mbalimbali  vya  redio yanavyo  weza  kupatikana  ndani  ya  redio  moja.

Mfano  wewe  una  redio  yako  aina  ya   Panasonic.  Ukiweka  masafa  ya  100  utanasa  matangazo  ya  kituo  kimoja  cha  redio, lakini  katika  redio  yako  hiyo  hiyo  ukihamisha  masafa  na  kwenda  masafa  ya  200  utanasa  matangazo  ya  kituo  kingine  cha  redio.  Ukihamisha  masafa  na  kupeleka  masafa  ya  300, utapata  matangazo  ya  kituo  kingine  cha  redio.

Redio  ni  moja  lakini  ndani  ya  redio  hiyo  hiyo  moja  unaweza  kupata  matangazo  ya  vituo  tofauti  vya  redio  lakini  katika  masafa  tofauti.

Vivyo  hivyo  kwa  majini  mseto. Majini  hawa  wanaishi  ndani  ya  mti  au  mmea  mmoja  lakini  wanapatikana   katika  masafa  tofauti. Unacho  takiwa  kufahamu  ni  kujua  jinni yupi  anapatikana  kwenye  masafa  yepi.

Kuhusu  masafa  hapo  namaanisha  muda , saa  na  siku  wanazo  tawala  majini  hao.  Kwa  hiyo  unatakiwa  kuwa  makini  sana  unapoenda  kuchuma  dawa  kwenye  mti  Fulani  kwa  ajili  ya  matumizi  yako.  Unatakiwa  uwe  uujue  mti  huo  ndani nje.  Unatakiwa  kujua  mti  huo  je  unakaliwa  na  majini  watukufu  pekee  au  majini  wa  kisheitwani  pekee  au  majini  mseto  yaani  majini  wa  kisheitwani  na  watukufu  kwa  wakati  mmoja.

Kwa  bahati  nzuri sana  taratibu  za  kuwatumia  majini  wanao  kaa  kwenye  miti  inayokaliwa  na  majina  wa  aina  moja  yaani  majini  watukufu  pekee  au  majini  wa  kisheitwani  pekee  zinajulikana  vizuri.

Tatizo  linakuja  kwenye  miti  inayo  kaliwa  na  majini  mseto.  Watu wengi  sana  hawana  ufahamu  kuhusu  jambo  hili . Ndio  maana  wengi  wao  huishia  kupata  matatizo  au  kupata  matokeo  tofauti  na  kile  wanacho  kitaka.

Kabla  ya  kwenda kuchuma  dawa  kwa  ajili  ya  matumizi  yako  unatakiwa  kuujua  mti  husika  juu  chini.  Unatakiwa  kuitambua  miti  yote  inayo  kaliwa  na  majini  mseto.  Na  ukisha  ijua  unatakiwa  ujue  masafa  ya  majini  wanao  kaa  ndani  ya  miti  hiyo.

Katika  masafa  hapa  namaanisha  siku, saa  na  wakati . ( Wakati   namaanisha  usiku  na  mchana )

Kwa  mfano  mti  wa  tumbaku.  Mti  huu  unakaliwa  na  majini  Zaidi  ya  thelathini  wazuri  kwa  wabaya.

Majini  hawa  wameganyika  katika  makundi  makuu  mawili, kundi  la  kwanza  ni  majini  wa  kisheitwani  na  kundi  la  pili  ni  majini  watukufu.  Kundi  moja  lina  utawala  mchana  na  kundi  jingine  linautawala  usiku.

Hivyo  basi  unatakiwa  kuwa  makini  sana  unapoenda  kuchuma  mmea  wa  tumbaku  kwa  ajili  ya  tiba.   Nimesema  hivyo  kwa  sababu  najua  watu  wengi   wanaujua  mmea  wa  tumbaku  kama  mmea  unao  tumika  katika  kusafisha  na  kupandisha  nyota  lakini  ukienda  kuuchuma  mmea  huu  katika  muda  ambao  mmea  huu  unakuwa  chini  ya  utawala  wa  kisheitwani  basi  utaambulia  kupata  nuksi, mabalaa  na  mikosi.

Unatakiwa  ujue  saa, siku na  wakati  ambao  mmea  wa  tumbaku  unakuwa  chini  ya  utawala  wa  majini  watukufu, bila  kusahau maneno  ya  kuzungumza  unapoenda  kuchuma  tumbaku  kwa  ajili ya  kusafisha  na  kupandisha  nyota.

Na  hii  ndio  sababu  kwanini  mmea  wa  tumbaku  ni  moja  kati  ya  mimea  yenye  matumizi  mengi  sana  katika uganga  na  uchawi  yakiwemo  mazuri  kwa  mabaya.

Majini  ( wabaya  kwa  wazuri  )  wanaoishi  ndani  ya  mmea  wa  tumbaku  wana  tumika  kufanya  mambo  mengi  sana  mazuri  kwa  mabaya.  Baadhi  ya  mambo  hayo  ni  kama  ifuatavyo :

1.    Kutengeneza  na  kusababisha  maradhi  ya  kichawi  yasiyo weza  kutibiwa  kwa  dawa  za  hospitalini

2.    Kuua  nyota  ya  mtu

3.    Kuua  biashara  ya  mtu

4.    Kuua  nguvu  za  kiume

5.    Kusababisha  maradhi  ya  upofu  na  uziwi  feki  ( Upofu na  uziwi  wa  kichawi )

6.    Kuua  mtu  kichawi

7.    Kuzika  vitu  mbalimbali

8.    Kumtia  mtu  nuksi, balaa  na  mikosi

9.    Kumletea  mtu  uchimvi  au  uchuro

10.  Kuleta  uhasama  na  uadui  mkubwa  kati  ya  wanandugu

11. Kusababisha  ndugu  wa  tumbo  moja  kuchukiana  na  hata  kuuana

12.  Kumtia  mtu  mikosi  ya  kukamatwa  na  polisi  na  kwenda  jela  mara  kwa  mara

13.  Kulinda  mali, mke, familia, uhusiano, ndoa  nakadhalika

14. Kulinda  pesa  na  utajiri  ( Ulinzi  kwa  ujumla ) Kwa  mfano, mti  huu  wa  tumbaku  hutumiwa  sana  na  watu  wanao  fanya  kazi  ya  ulinzi  wa  mali  za  watu

15.Mafanikio  katika  elimu  hususani  kwa  watu  wenye ndoto  za  kuwa watalaamu  katika  fani tatu  ambazo  utazijua  ni  fani  zipi  na  kivipi  mmea  wa  tumbaku  unawasaidia  watu  wenye  ndoto  za  kuwa wana  fani  hizo  kupitia  kitabu  changu  MAMBO TISA  MUHIMU  YANAYO  UNDA  NYOTA  YA  MWANADAMU  : UHUSIANO  KATI  YA  NYOTA  YA  MTU  NA  MAFANIKIO  YAKE  KATIKA  MAISHA  ambacho  kitakuwa  mitaani  kuanzia  kati kati  ya  mwezi wa  Julai

16.Kazi  na  ajira  hususani  kwa  watu  wenye  ndoto  za  kufanya  kazi aina  tano  ambazo  utazijua  ni  zipi  ndani  ya  kitabu  changu :    MAMBO TISA  MUHIMU  YANAYO  UNDA  NYOTA  YA  MWANADAMU  : UHUSIANO  KATI  YA  NYOTA  YA  MTU  NA  MAFANIKIO  YAKE  KATIKA  MAISHA  ambacho  kitakuwa  mitaani  kuanzia  kati kati  ya  mwezi wa  Julai.

17. Humsaidia  mtu  aliedhulumiwa  mali au  pesa  au  anae  taka  kulipwa  fidia

18.  Kumtia  mtu  umasikini

19. Ni  dawa  nzuri  sana  ya  biashara  hususani  kwa  wanao  fanya  biashara  ya  kuuza  vikorokocho  vya  kula  wanafunzi  mashuleni  kama  vile  visheti, ice  cream  nakadhalika. Kama unafanya  biashara  ya  kuuza  vikorokocho  vya  kula  wanafunzi  mashuleni  basi  nakushauri  utumie  mvuto  wa  tumbaku..Inshalaah  utapata  matokeo  mazuri  san.

20.Kuleta  na  kulinda  mali, pesa  na  utajiri

21. Kumloga  mtu  ukichaa  wa  kumtembeza

22.  Kuleta  heshima  na  kukubalika  mbele  za  watu

23.  Kuleta  na  kuharakisha  ndoa

24. Kuleta  watoto  na  furaha  katika  maisha

25. Pamoja  na mambo  mengine  mengi  sana.  Kuyajua  yote  haya  kwa  kina  pamoja  na  jinsi  unavyo  weza  kutumia  mmea  wa  tumbaku  katika  mambo  yako pamoja  na miti  mingine  muhimu  inayo kaliwa  na  majini  mseto  pamoja  na masharti  na  taratibu  zake, jiandae  kusoma  kitabu  changu MAMBO TISA  MUHIMU  YANAYO  UNDA  NYOTA  YA  MWANADAMU  : UHUSIANO  KATI  YA  NYOTA  YA  MTU  NA  MAFANIKIO  YAKE  KATIKA  MAISHA  ambacho  kitakuwa  mitaani  kuanzia  kati kati  ya  mwezi wa  Julai.

Pamoja  na  mambo  mengine  mengi, ndani  ya  kitabu  hiki  utafahamu  kwa  kina  kuhusu  mti  wa  tumbaku  na  jinsi  ya  kuutumia  katika  mambo  yako, majini  wanao  utawala  mmea  wa tumbaku  na  jinsi  ya  kuwaita na  kuwatumia. Utapata  kufahamu  kuhusu  maneno  yanayo tumika  kutamka  wakati  unakwenda  kuchuma  mti  wa  tumbaku.  Na  habari  njema  ni  kwamba, maneno  hayo  yameandikwa  kwa  maandishi  ya  kawaida  kwa  hiyo  hata  wewe  ambae  haujui  kiarabu  unaweza  kusoma  na  kuelewa.

Mbali  na  mmea  wa  tumbaku, utapata  kufahamu  kwa  kina  kuhusu  mimea  mingine  inayo  kaliwa  na  majini  mseto , bila  kusahau  kuhusu  miti  na  mimea  inayo  kaliwa  na  majini  wa  kisheitwani  pamoja  na  ile  inayo  kaliwa  na  majini  watukufu  pekee.

Kufahamu  kuhusu  mambo  mengine  yaliyomo  ndani  ya  kitabu  hiki, tembelea :


MAKALA  HAYA  YAMEANDALIWA  NA  DOKTA  MUNGWA  KABILI.  ANAPATIKANA  KUPITIA  NAMBA

0744  000  473.


CCM Yamkana Lembeli

$
0
0
Na magdalena Kashindye -KAHAMA
Chama cha mapinduzi (CCM) wilayani Kahama mkoani Shinyanga kimesema hakina taarifa ya urejeo wa James Daud Lembeli katika chama hicho kutokana na kushindwa kufuata taratibu na katiba ya chama.

Akizungumza na Mpekuziblog ofisini kwake katibu mwenezi wa CCM wilayani ya  Kahama Joachim Simbila amesema chama kimesikia urejeo wa Lembeli  lakini hakuna taarifa rasmi iliyothibitishwa, hivyo alichokifanya ni kuutangazia umma kuwa amehama kutoka Chadema kujiunga na CCM.

Simbila amesema katiba ya chama inasema mwanachama aliyehama chama na kurudi kwa mara ya pili anatakiwa kujaza fomu ambayo itaidhinishwa na tawi la eneo analoishi ambapo wao kama viongozi baada ya kusikia taarifa hizo waliwasiliana na uongozi wa eneo husika lakini hakuna taarifa za James Daud Lembeli kujaza fomu

Pia Simbila amesema mkutano aliouandaa James Lembeli haukuwa na viongozi wa chama wilaya sambamba na viongozi wa tawi ambapo katika mkutano huo alikuwepo kiongozi wa serikali ya kijiji kitu ambacho kiongozi huyo hana mamlaka ya kumpokea mwanachama mpya kuingia ndani ya chama.

Daud James Lembeli (mwanamaria) June 13, 2018 alitangaza kuachana na Chadema na kurejea chama cha mapinduzi CCM ambapo alisema ameachana na siasa za majukwaani kwani wazazi wake wote ni waasisi wa TANU ambacho kiliunda CCM hivyo yeye kuwa chama cha upinzani ni kuwakataa wazazi wake

Rais Magufuli Atoa Zawadi Za Idd kwa Watu Wenye Mahitaji Maalum

$
0
0
Habari na Wizara ya Afya.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametoa zawadi ya Idd El Fitri zenye thamani ya shilingi 11,370, 000 kwa vituo 5 vya Mkoa wa Dar es Salaam, vituo 2 vya Zanzibar na vituo 17 kutoka mikoa ya Tanzania Bara.

Zawadi hizo zimekabidhiwa leo katika Mahabusu ya Watoto iliyoko Upanga Jijini Dar es Salaam na Kamishina Msaidizi wa Ustawi wa Jamii, Idara ya Ustawi wa Jamii, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee, na Watoto, Bw. Rabikila Mushi kwa niaba ya Mhe. Rais, Dkt. John Pombe Magufuli.

Bw. Mushi amezitaja zawadi zilizotolewa kuwa ni mchele, mbuzi na mafuta ya kupikia ambazo zitawezesha makundi hayo kufurahi na kusherehekea sikukuu kama ilivyo kwa watu wengi.

“Mhe. Rais kwa upendo wake wa dhati kabisa ameona umuhimu wa kushiriki pamoja na watu walio katika makundi maalum wakiwemo watoto walio katika mazingira hatarishi na wazee  wenye ulemavu wasiojiweza, wanaohudumiwa  katika makazi, katika kusherehekea sikukuu ya Idd El Fitri mwaka 2018,” amesema Bw. Mushi.

Aidha, amevitaja vituo vilivyonufaika na zawadi za Mhe. Rais kwa Mkoa wa Dar es Salaam ni Dar Al Arquam, Makao ya Taifa ya watoto Kurasini, Makao ya Watoto yatima kurasini,Makao ya watoto yatima  Mburahati, Makao ya wazee wasiojiweza Nunge Temeke na Mahabusu ya watoto ya Taifa Upanga.

Vile vile, amevitaja vituo vilivyonufaika kwa upande wa mikoa ya Tanzania Bara kuwa ni Vituo vya Watoto yatima vya Renato Granti na Bulongwa vyote vya Njombe, Makazi ya Wazee wasiojiweza Magugu mkani Manyara, Makazi ya Wazee ya Taifa  wasiojiweza Fungafunga Morogoro, na baadhi ya vituo vingine vya binafsi na Taifa Nchini.

Kwa upande wa Zanzibar, vituo vilivyonufaika ni Kituo cha Watoto Mazizini cha Mjini Unguja na Makao ya Wazee Limbani Pemba.

Utoaji zawadi hizi umekuwa wa kawaida kwa Wahe. Marais wa Tanzania kwa awamu zote nne kutoa zawadi  za vyakula kama vile mafuta, mchele na mbuzi ili kuwawezesha kufurahi na kusherekea Siku kuu kama ilivyo kwa watu wengine.

Rais Magufuli Awalilia Wanajeshi 12 Waliofariki Ajalini

CECAFA Yakubali Kujitoa Kwa Yanga Kombe La Kagame Cup Msimu Wa 2018

$
0
0
 Shirikisho la Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), limekubali maombi ya Yanga kujiondoa katika mashindano ya KAGAME baada ya kutuma barua iliyoeleza kuomba kujitoa

Yanga ilituma barua kupitia TFF ikiomba kujiondoa ili kuwapa nafasi wachezaji wake mapumziko kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Gor Mahia FC ya Kenya.

Barua hiyo ilieleza kuwa ratiba ya michuano imekuwa si rafiki kwao na itakuwa inawabana sababu wanapaswa kuwajibika kwenye mashindano ya shirikisho pia wachezaji wake wengi hawana mikataba.

Kutokana na maombi hayo, CECAFA wamemua kuuwaalika Vipers SC ya Uganda kuchukua nafasi ya Yanga ambapo katika kundi C wataungana na Simba, Dakadaha ya Somalia na St. George ya Ethiopia.

Michuano hiyo inatarajia kuanza kurindima June 28 mwaka huu na kumalizika Julai 13 2018.

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images