Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Baba aondoka na mtoto wa Masogange siku moja ya mazishi

$
0
0
Ikiwa ni siku moja tangu msanii Agnes Gerald ‘Masogange’ azikwe, mtoto wake wa pekee Sania Sabri ameondoka na baba yake kurudi jijini Dar es Salaam.

Marehemu Masogange alizikwa jana Aprili 23 mwaka huu pembeni mwa nyumba ya baba yake, Gerald Waya katika kijiji cha Utengule, Mbalizi II mkoani Mbeya.

Baba wa marehemu, Waya amesema mjukuu wake, Sania ameondoka leo Aprili 24 na baba yake Sabri Athman kuelekea jijini Dar es Salaam, ili kuwahi masomo  kwa kuwa sasa hakuna shughuli yoyote ya familia.

Amesema licha ya kumfahamu mjukuu wake Sania, hakuwahi kumfahamu baba yake hivyo msiba huo ndiyo uliowakutanisha na kufahamiana kwa mara ya kwanza. 

 “Mjukuu wangu Sania ameondoka leo alfajiri na baba yake. Sababu ni kuwahi masomo shuleni kwani tumeona shughuli zote ziliisha jana hakuna sababu ya kuendelea kuwa naye hapa, atakuja wakati wa kumaliza matanga,” amesema.

Waya amesema shughuli za kuondoa matanga zitafanyika baada ya siku 40 kupita na  jana walifanya shughuli ya kuwaaga waombolezaji waliolala msibani hapo na kubakia familia tu.

“Hivi sasa kama unavyoona hakuna kinachoendelea, tumebaki familia tu ambayo tutaendelea kuomboleza hadi baada ya siku 40 ya matanga. Haitafanyikia hapa nyumbani badala yake tutarudi kule nyumbani asili ambako ndiko kuna makaburi ya ukoo na nyumba ya baba yangu ipo kule,” amesema  Waya.

Amesema familia zao zote huzikwa kwenye makaburi hayo, lakini mtoto wake ameamua azikwe pembezoni mwa nyumba yake ili asikae mbali naye. Pia, kwenye makaburi ya pamoja kwa sasa hapapitiki kwa urahisi kutokana na mvua zinazoendelea.

John Heche: Waliniambia Watanipoteza

$
0
0
Mbunge wa Tarime Vijijini (Chadema), John Heche amesema anatishiwa maisha kutokana na kauli zake za kuikosoa Serikali, likiwemo sakata la ufisadi wa mradi wa hati za kielektroniki ya kusafiria.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Aprili 24, bungeni mjini Dodoma, Heche amesema licha ya kutotishika na vitisho hivyo amebainisha kuwa kuna kesi inaandaliwa dhidi yake na muda wowote anaweza kukamatwa.

“Kuna njama za kutishia watu wanaohoji masuala mbalimbali ambayo tunayazungumza na kuonekana wazi kuigusa Serikali,” amesema.

Sakata la mradi huo lilitikisa katika mkutano wa Bunge uliofanyika Februari mwaka huu, ambapo mbunge wa Momba (Chadema), David Silinde pia aliligusia na kubainisha kuwa mradi huo umekuwa ikitekelezwa kwa gharama za Dola 40milioni za Marekani, wakati taarifa zilizopo ni kuwa mradi huo ulikuwa na thamani ya dola 16 milioni za Marekani, sawa na Paundi 11 milioni.

Mradi huo wa hati za kusafiria ulizinduliwa Januari 30, 2018 na Rais John Magufuli.

Makamu Wa Rais Amuwkilisha Rais Magufuli Kwenye Mkutano Wa SADC Double Troika

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo amemuwakilisha Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ni Mwenyekiti wa Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC aliyemaliza muda wake kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Troika Mbili wa SADC kuhusu hali ya Usalama katika Kanda umefanyika hapa Luanda, leo tarehe 24 Aprili, 2018.

Mkutano huu umeitishwa baada ya mashauriano kati ya Mheshimiwa Dkt. Cyril Ramaphosa, Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini na Mwenyekiti wa SADC na Mhe. João  Lourenço, Rais wa Angola na Mwenyekiti wa Asasi ya Ushirikino ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC

Mkutano huu umetanguliwa na kikao cha Mawaziri ambacho kilifanyika jana tarehe 23 April 2018.

Mkutano huu ulihusisha nchi wanachama sita tu wa SADC Double Troika na Viongozi wafuatao walihudhuria,

Mhe. Dkt. Cyril Ramaphosa, Rais wa Afrika Kusini na Mwenyekiti wa Summit, Mhe. João Lourenço  , Rais wa Angola na Mwenyekiti wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama – (SADC Organ on Politics, Defence and Security Cooperation),Mhe. Hage Geingob, Rais wa Namibia na Makamu Mwenyekiti wa Summit, Mhe. Edgar Lungu, Rais wa Zambia na Makamu Mwenyekiti wa SADC Organ, Mfalme Mswati III, Mfalme wa Swaziland na Mwenyekiti wa Summit anayetoka;

Mheshimiwa Joseph Kabila Kabange, Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Mheshimiwa Thomas Thabane, Waziri Mkuu wa Lesotho walialikwa na walihudhuria.

Mkutano huu utapitia na kujadili ajenda zifuatazo:-
  1.  Hali ya siasa na usalama katika Falme ya Lesotho;
  2.  Hali ya siasa ulinzi na usalama katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo;
  3. Hali ya siasa, ulinzi na usalama nchini Madagascar; na
  4. Masuala ya demokrasia katika kanda ( Consolidation of Democracy in the region)
KUHUSU HALI YA SIASA, ULINZI NA USALAMA NCHINI LESOHO:-
  1. Mkutano huu umevitaka  Vyama vyote vya Siasa kulipa uzito suala la Mjadala wa Kisiasa na Mchakato wa Mageuzi ya Kisekta na kushiriki kikamilifu kwenye michakato yote ili kupata suluhisho la kudumu katika changamoto za kiusalama na kisiasa;
  2. Pia Mkutano huu umeitaka Serikali ya Lesotho na wadau wengine kukamilisha mjadala wa kitaifa ifikapo mwezi Juni, 2018 na kutoa taarifa kwenye kikao kijacho cha kawaida cha Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC ambacho kimepangwa kufanyika Augosti, 2018;
  3. Pia Misheni ya Ulinzi nchini Lesotho (SADC Preventive Mission in the Kingdom of Lesotho – SAPMIL ) imeongezewa muda kwa kipindi kingine cha miezi sita kuanzia Mei 20, 2018.
KUHUSU  HALI YA SIASA, ULINZI  NA USALAMA JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA    KONGO (DRC)

Nchi wanachama zitaombwa kuisaidia Jamhuri  ya Kidemokrasia ya   Kongo (DRC)  kwenye kipindi hiki wanachoelekea kwenye Uchaguzi Mkuu kwa lengo la kuhakikisha kuwa uchaguzi huu unafanyika katika mazingira ya amani.

Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano huu ulitumia fursa hiyo kuomba nchi wanachama wa SADC kumuunga mkono Mheshimiwa Stephen Maselle ( Mb), ambaye anawania  nafasi ya Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika ( Deputy President of the Pan African Parliament).

TLS Ni Chama Cha Umma Kifanye Kazi Kwa Mujibu Wa Sheria

$
0
0
Na Lydia Churi, Magreth Kinabo-Mahakama
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amesema Chama cha Wanasheria cha Tanganyika (TLS) ni taasisi ya Umma na siyo binafsi hivyo amekitaka kutekeleza majukumu yake ya msingi ya kisheria kwa kushirikiana na Mahakama na kuacha kujiingiza kwenye masuala ya uanaharakati na siasa.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo jijini Dar es salaam Jaji Mkuu amesema TLS ni chama huru cha kitaaluma kwa kuwa kilianzishwa kwa mujibu wa sheria kufanya kazi kwa manufaa mapana ya Umma.

“Hatuwezi kukubali chama hiki kikajisemea kuwa wao ni chama binafsi na tukakubali, dhana ya ubinafsi haipo”, alisisitiza Jaji Mkuu.

Alisema jukumu la TLS ni Kuisaidia Serikali na Mahakama kuhusu mambo yoyote yanayogusa sheria, utawala wa sheria na kazi za kisheria na akaongeza kuwa dhana hii ndiyo inayoiunganisha Taasisi hiyo na Mahakama ya Tanzania.

Aidha, Jaji Mkuu amewataka viongozi wa TLS kushirikiana na Mahakama pamoja na Mihimili mingine ya dola  na kuacha malumbano kwenye vyombo vya habari kwa kuwa hayawasaidii kuendeleza chama hiki muhimu kwa wanasheria nchini.

Jaji Mkuu pia amewashauri viongozi wa chama hicho kumuheshimu Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuwa Sheria na Kanuni zote ni lazima zipitie kwake.

Alisema Mamlaka ya Baraza la Uongozi la TLS katika Kutekeleza Majukumu ya Umma ni kusaidia kuboresha elimu ya sheria na taaluma ya Sheria Tanzania na kuwawezesha wanataaluma wa sheria kupata elimu ya ziada ya sheria kwa kadri mabadiliko yanayotokea nchini na duniani.

Majukumu mengine ya TLS ni pamoja na kuwawakilisha, kuwatetea na kuwasaidia wanasheria Tanzania kuhusu mazingira ya kufanya kazi za kisheria na kuwasaidia wananchi wa Tanzania katika masuala ya kisheria yanayogusa Sheria.

TLS ni Taasisi iliyoanzishwa kwa mujibu wa Sheria za nchi kabla ya Uhuru na kukubalika kuendelea kuwepo kama Taasisi ya Kisheria kwa malengo ya kuanzishwa kwake kuelekezwa kwenye manufaa ya umma kwa kushirikiana na Mahakama, Bunge, pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Chama hiki kilianzishwa kwa Sheria ya Baraza la Kutunga Sheria (Legislative Council) Namba 30 ya 1954 na ni moja ya Sheria nyingi za iliyokuwa Tanganyika kabla ya Uhuru, ambazo kwa mujibu wa Kifungu cha 4 cha Katiba ya Tanganyika  ziliruhusiwa kuendelea kutumika Tanganyika ilipopata Uhuru Disemba 9 mwaka 1961 kama Sheria za Tanganyika huru.

Rais Magufuli; EAC Tunaweza Kujitegemea

$
0
0
Na Lilian Lundo – MAELEZO,Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewataka Wanaafrika Mashariki kujiamini kuwa wanaweza kutekeleza miradi ya maendeleo bila kutegemea mataifa mengine.

Rais Dkt. Magufuli ameyasema hayo leo Mjini Dodoma alipokuwa  akihutubia Bunge la Nne la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalofanyika mkoani humo kwa mara kwanza  tangu kuanza kwa Bunge hilo.

“Ninazungumza hili si kwamba hatuhitaji msaada au hatuhitaji ushirikiano, lakini ni lazima tuliweke hili wazi, kwamba tukiamua tunaweza na mifano ipo mingi ikiwemo Tanzania”. Alisisitiza Mhe. Rais Dkt. Magufuli.

“Tanzania tunajenga reli ya kisasa yenye urefu wa kilometa 700.26 kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma kwa thamani ya shilingi Trilioni 7.6, tumeweza kununua ndege sita na pia tumejenga meli kubwa katika Ziwa Victoria bila kuomba mkopo popote,” amesema Rais Magufuli.

Aidha, Rais Magufuli ameongeza kuwa wabunge wa Afrika Mashariki wanaowajibu wa kuhakikisha wanalinda na kuendeleza mafanikio yaliyopatikana ndani ya Jumuiya hiyo.

Akitaja baadhi ya mafanikio yaliyopatikana na Jumuiya hiyo Rais Magufuli amesema kuwa kabla ya kuanza kwa umoja wa forodha mwaka 2005 biashara kati ya nchi wanachama ilikuwa na thamani ya dola za kimarekani bilioni 1.8 lakini baada ya kuanzishwa kwa umoja wa forodha imeongezeka hadi kufikia zaidi ya dola za kimarekani bilioni 5.

Mbali na hayo Rais,  Magufuli ameshukuru uamuzi wa bunge hilo kufanyika mjini Dodoma ambapo kwa sasa Serikali imehamishia shughuli zake zote katika mkoa huo, na tayari watumishi wa serikali zaidi ya 3000 wameshahamia huku Rais Magufuli akitarajiwa kuhamia muda wowote mwaka huu.

Kwa upande wake Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Dkt. Martin Ngoga amesema Bunge hilo linasubiri marekebisho ya mkataba wa kuanzishwa kwa jumuiya hiyo ili  lugha ya Kiswahili ianze kutumika kama lugha rasmi katika vikao vya bunge hilo na katika jumuiya hiyo kwa kuzingatia azimio lililokwishapitishwa.

“Hatuoni sababu ya kutumia lugha za wageni wakati kuna lugha yetu ambayo tunazungumza ambayo ni kiswahili,” alisema Dkt. Ngoga.

Bunge la Afrika Mashariki linaendelea na vikao vyake mkoani Dodoma katika ukumbi mdogo wa Bunge wa Pius Msekwa. Bunge hilo limefanyika kwa mara ya kwanza mkoani humo.

Msanii Diamond Kutoa Burudani Kombe La Dunia 2018 Nchini Urusi

$
0
0
Msanii nguli wa Bongo Fleva nchini Tanzania, Diamond Platnumz, kwa kushirikiana na kampuni ya Coca-Cola ametangaza kuwa ameshiriki kuimba wimbo utakaosherehesha Kombe la Dunia 2018 uitwao Colours.

Wimbo huo uliotungwa na mwanamuziki Jason Derulo wa Florida, Marekani, Diamond ameshiriki kuweka maudhui ya lugha ya Kiswahili na umetayarishwa na prodyuza Nahreel kwa kushirikiana na maprodyuza kutoka nchi nyingine chini ya udhamini wa kampuni ya Coca-Cola.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, amesema anayo furaha kupata fursa ya kushiriki kuimba kuimba wimbo wa mashindano haya makubwa ya kidunia na kuitangaza Tanzania na lugha ya Afrika bila kusahau tasnia ya muziki kwa ujumla.

“Kwangu hii ni nafasi nyingine ambayo najivunia kuipata ya kutangaza muziki wa kitanzania sambamba na lugha ya Kiswahili kwa kuwa sehemu niliyoshiriki kuimba nimetumia lugha ya taifa la Tanzania ambayo inazidi kupata umaarufu mkubwa duniani”alisema Diamond

Kwa upande wake Meneja wa Chapa ya Coca-Cola nchini, Sialouise Shayo, alisema kampuni ya Coca-Cola ambayo ni moja ya mdhamini wa mashindano haya makubwa ya soka duniani inayo furaha kwa msanii kutoka nchini Tanzania kushiriki kuimba wimbo maalum wa mashindano haya. “Tuna imani watanzania watapata mzuka wa soka dimbani na kujisikia sehemu ya mashindano haya”alisisitiza.

Prodyuza nguli wa muziki nchini na kanda ya Afrika Mashariki, Nahreel ,ambaye ameshiriki kutengeneza wimbo huu aliishukuru kampuni ya Coca-Cola kwa jitihada mbalimali ambazo imekuwa ikifanya kuwanyanyua wasanii wa hapa nchini ambapo mbali na Diamond naye ameshiriki kwenye tukio hili kubwa. “Ninayo furaha ya kufanya kazi na Diamond kwa mara nyingine katika tukio hili kubwa la mashindano ya Kombe la Dunia na najivunia heshima kubwa tuliyopewa”

Mzee Majuto Bado ni Mgonjwa...Mkewe Awaomba Watanzania Wamuombee

$
0
0
Mke wa mwigizaji na mchekeshaji maarufu nchini, Amri Athumani ‘Mzee Majuto’, Aisha Yusufu (39), amewaomba Watanzania wamuombee mume wake apone na aendelee na shughuli zake.

Mzee Majuto ambaye alifanyiwa upasuaji katika Hospitali ya Tumaini jijini Dar es Salaam, Januari mwaka huu na kuruhusiwa, alirudishwa tena hapo jana baada ya hali yake kuwa mbaya kutokana na kidonda kushindwa kufunga.

Aisha amesema mume wake alifikishwa hapo akiwa katika hali mbaya lakini anashukuru kwa sasa anaendelea vizuri.

“Ninachoomba Watanzania waendelee kumuombea tu mume wangu apone na kuruhusiwa kutoka hospitali kwa kuwa akilala kitandani na mambo yake yanalala,” amesema.

Amesema huo ni upasuaji wa pili kwa Majuto kufanyiwa baada ya ule wa kwanza wa henia aliofanyiwa jijini Tanga  Julai mwaka jana.

“Wakati tunahangaika kuangalia namna ya kupata tiba ya nyonga ndipo alipogundulika kuwa ana tezi dume na hivyo kufanyiwa upasuaji,” amesema.

Mzee Majuto amewahi kucheza filamu mbalimbali ikiwemo Welcome Back, Mshamba, Pedeshee, Si Sawa, Mama Ntilie, Nahama, Gumzo, Mrithi Wangu, Rent House, Ndoa ya Utata, Daladala na Nimekuchoka.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya April 25


Rais Magufuli awafunda Wabunge wa Afrika Mashariki

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewataka Wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kutilia mkazo ajenda zitakazoimarisha zaidi umoja, upendo, ushirikiano na mshikamano baina ya nchi wanachama ili kufanikisha jukumu muhimu la kupambana na umasikini wa wananchi na kukuza uchumi.

Mhe. Rais Magufuli amesema hayo tarehe 24 Aprili, 2018 wakati akihutubia Bunge la Afrika Mashariki kwa mara ya kwanza tangu aingie madarakani, katika ukumbi wa Pius Msekwa uliopo ndani ya viwanja vya Bunge Mjini Dodoma ambako Bunge hilo linafanyia vikao vyake kwa mara ya kwanza katika mji huo.

Mhe. Rais Magufuli amesema Wabunge hao wanao wajibu wa kushughulikia migogoro ambayo imekuwa ikigharimu maisha ya wananchi, vikwazo vya biashara na uwekezaji, na kutilia mkazo ujenzi wa viwanda vitakavyochakata na kuzalisha bidhaa zitokanazo na rasilimali lukuki zilizopo ndani ya Afrika Mashariki ili manufaa ya rasilimali hizo yawanufaishe wananchi.

Ametaja miongoni mwa mambo yanayopaswa kutiliwa mkazo na nchi zote kuwa ni kuimarisha miundombinu ya usafirishaji na uzalishaji wa umeme wakutosha na wenye gharama nafuu, ambavyo ni muhimu katika ujenzi wa viwanda.

“Tafiti zinaonesha gharama za usafiri kwenye ukanda wetu ni mara 4 hadi 5 ukilinganisha na gharama za Asia Mashariki, Marekani na Ulaya na zinachangia kuongezeka kwa gharama za bidhaa kwa asilimia 40.

“Umeme pia umeonekana kuwa sio mwingi, utafiti uliofanywa na taasisi ya Power Africa mwaka 2015 umeonesha kuwa nchi zote 6 za Jumuiya ya Afrika Mashariki zina takribani megawati 6,500 tu za umeme, hiki ni kiwango kidogo mno kuweza kuhimili mahitaji ya uchumi wa kisasa” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Katika kutekeleza azma hiyo Mhe. Rais Magufuli ametoa wito kwa nchi wanachama kubadilishana uzoefu wa namna ya kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza na kutekeleza miradi muhimu ya maendeleo, na pia ameshauri nchi wanachama zisitegemee misaada pekee na badala yake zifikirie kutekeleza miradi kwa fedha zake zenyewe ili kuokoa muda na kupunguza gharama za miradi husika.

Mhe. Rais Magufuli amezungumzia juhudi zinazofanywa na Tanzania katika kufikia dhamira hiyo kuwa ni pamoja na kuanza ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge) kuanzia Dar es Salaam hadi Dodoma ambayo itaunganisha hadi nchi za Burundi, Rwanda na Uganda, kujenga meli katika ziwa Victoria, kutekeleza mradi wa uzalishaji wa umeme katika mto Rufiji (Stieglers’ Gorge), kununua ndege 6, kujenga barabara, kupanua bandari ya Dar es Salaam, ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga nchini Tanzania, kuboresha viwanja vya ndege 11 na amepongeza juhudi mbalimbali zinazofanywa na nchi nyingine wanachama wa Afrika Mashariki.

“Nataka kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge wa Afrika Mashariki kuwa Serikali ninayoiongoza itaendelea kushirikiana na Bunge hili katika masuala mbalimbali ya kuiunganisha jumuiya yetu, na ninawaomba nanyi mtekeleze wajibu wenu wa kuwaunganisha na kuwaelimisha wananchi ili waone umuhimu wa jumuiya hii” amebainisha Mhe. Rais Magufuli.

Kwa upande wake Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Martin Ngoga amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kulihutubia Bunge hilo na amempongeza kwa jitihada zake za kujenga nidhamu ya utumishi wa umma, kuzidisha mapambano dhidi ya rushwa, kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo, kukuza uwekezaji na biashara ikiwemo ujenzi wa viwanda na kuonesha uongozi mahiri, na ametoa wito kwa Watanzania kuunga mkono juhudi hizo.

Pamoja na Wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, viongozi wengine waliohudhuria wakati Mhe. Rais Magufuli akihutubia bunge hilo ni Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Naibu wa Pili wa Waziri Mkuu wa Uganda Mhe. Kirunda Kivejinja, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Yustino Ndugai, Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi John Kijazi, Mawaziri, Mabalozi wanaowakilisha nchi mbalimbali hapa nchini, viongozi wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dodoma
24 Aprili, 2018

Polisi Dar Yatoa ONYO Kwa Waliopanga Kuandamana

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewataka wananchi wote kuendelea na shughuli zao kama kawaida kwa kuwa maandamano yanayozungumzwa hayapo na ni batili.

Akizungumza leo Jumatano Aprili 25 na shirikisho la waendesha bodaboda Mkoa wa Dar es Salaam, Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum, ACP Sweethbert Njwele amesema jeshi la polisi limejipanga kuhakikisha kila mtu anafanya shughuli zake kama kawaida bila uvunjifu wowote wa amani.

"Niwahakikishie jeshi la polisi tumejipanga na mkoa wetu utaendelea kubaki salama hakuna maandamano yatakayofanyika hivyo kila mtu aendelee na shughuli zake kama kawaida," amesema Njwele.

Amesema waendesha bodaboda ni kundi kubwa ila kuna baadhi yao si waaminifu na kutaka wajiepushe na watu watakaowashawishi kuvunja sheria za nchi.

Kwa upande wake, Msemaji wa Shirikisho hilo Adamu Kyando amesema uvumi unaosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Aprili 26 bodaboda watashiriki si kweli kwani hakuna bodaboda yeyote atakayeshiriki maandamano hayo.

"Kuna taarifa zinazosambaa kwenye mitandao yakijamii ikihamasisha bodaboda kushiriki maandamano taarifa hizi si za kweli na ni batili," amesema Kyando.

Amesema kwa yeyote atakayeshiriki maandamano hayo uongozi hautahusika kwani taarifa zinazosambazwa hazitoki kwenye shirikisho hilo.

Uingereza Yatoa Tahadhari kwa Raia Wake Nchini Kuhusu Maandamano

$
0
0
Serikali ya Uingereza imewataka wananchi wake wanaoishi hapa nchini kuchukua tahadhari na maandamano ya kisiasa yanayotarajiwa kufanyika Aprili 26.

Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari  jana Aprili 24 imesema kwamba kuna raia zaidi ya 75,000 wanaoingia nchini hapa kila mwaka.

Hivyo imewatahadharisha kujihusisha na maandamano hayo kwa madai kwamba wanaweza kupata madhara kutoka kwa jeshi la polisi.

Katika taarifa hiyo ilitolewa tahadhari kwamba kwa sababu maandamano hayo yalishapigwa marufuku hivyo polisi ni lazima watatumia mabomu ya machozi au silaha za moto.

“Hivyo muwe makini sana mnapokuwa kwenye mizunguko yenu muepuke mikusanyiko ya watu au watu wanaoandamana, muda wote muwe mnasikiliza vyombo vya habari, mjue nini kinachoendelea,’’ ilisema taarifa hiyo na kuongeza:

“Ikiwa mnahitaji mawasiliano na namba ya dharura ya kupiga haraka ni 112 uliza huduma ya dharura unayohitaji.’’

Pia taarifa hiyo iliwataka raia hao wa Uingereza kuwa makini wawapo barabarani kwa sababu watu wanaweza kutumia mwanya huo kufanya jambo lolote nchini hapa.

Hivyo raia hao wamepewa ushauri wa kuwasiliana na ofisi za ubalozi wa Uingereza ikiwa watahitaji msaada wowote.

Marekani Nayo Yawaonya Raia Wake Kuhusu Maandamano Nchini

$
0
0

Ubalozi wa Marekani nchini umetoa tahadhari kwa wananchi wao wanaoishi Tanzania kuhusu maandamano ya kisiasa yanayotarajiwa kufanyika Aprili 26.

Maandamano hayo yanatarajiwa kufanyika siku ya Muungano huku baadhi ya wanasiasa wakiwa tayari wameshafunguliwa kesi mahakamani kutokana na tuhuma mbalimbali.

Ubalozi umetoa tahadhari kwa raia wake wote kwamba siku ya Aprili 26 wanatakiwa kuwa makini kwa sababu inawezekana kabisa maandamano yakatokea.

Kwenye taarifa hiyo ambayo imetolewa kwa vyombo vya habari imesema kwamba polisi wamejiandaa kukabiliana na maandamano hayo.

“Polisi wanaweza wakatumia mabomu ya machozi na risasi za moto ili kudhibiti maandamano hayo hivyo ni muhimu kukaa mbali na waandamanaji hao.

Serikali ya Marekani inawatakia kila la kheri raia wa Marekani kwa kuwataka kukaa mbali na makundi ya watu siku hiyo ya Aprili 26 na kufuatilia taarifa kwenye vyombo vya habari ili kujua kinachoendelea.

Bunge Laibua Tuhuma Nzito Kwa Wamiliki wa Sober House

$
0
0
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia baadhi ya wabunge wake, wameibua tuhuma nzito juu ya tabia chafu inayofanywa na wamiliki wa majumba yanayotumika kutibu waathirika wa madawa ya kulevya (sober house), kitendo kinachozidi kuwaathiri vijana wakiwa humo.

Akizungumza Bungeni kutaka maelezeo kutoka kwa serikali inachukua hatua gani juu ya hilo, Mbunge Kijana Halima Bulembo amesema kwamba wamili wa majumba hayo wana tabia ya kuwachoma tena sindano za madawa ya kulevya vijana ambao wanakaribia kupone ili wasitoke, na lengo kubwa likiwa ni kuendelea kuingiza pesa kupitria wao.

“Kumekuwa na malalamiko mengi ya waathirika wa madawa ya kulevya wanapokuwa rehab, wanapokaribia kupona wahusika wanawachoma dawa tena za madawa ya kulevya ili wasiweze kutoka lengo likiwa waendelee kijipatia fedha”, amesema Halima Bulembo.

Taarifa hiyo iligongewa msumari na Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Jenista Mhagama, kwa kusema kwamba malalamiko hayo sio mara ya kwanza Bungeni, na kutoa onyo kali kwa wamiliki.

“Tumepokea hii taarifa sasa kwa mara kadhaa, waheshimiwa wabunge wametuarifu kwamba upo mchezo mchafu unaoendelea kwenye sober house, badala ya kuwasaidia vijana wetu wapone, na waondoke sober house, lakini wamiliki wanataka kuendelea kuwaweka pale kwa faida yao binafsi. Nitoe agizo kwa wamiliki wa sober house ambao wana mchezo huo kuacha haraka, na naagiza mamlaka husika kufanya uchunguzi wa kina na yeyote atakayebainika kufanya jambo hilo tutamchukulia hatua kali”, amesema Waziri Jenista Mhagama.

Kwa upande wa serikali wamesema hawajapokea taarifa hizo rasmi kwa sababu asilimia kubwa ya sober house zinamilikiwa na watu binafsi, lakini imeweka miongozo kusaidia soiber house, na kuhakikisha kuwa mpango wa serikali kuwa na sober house nyingi inazomiliki unafanikiwa ili kuondokana nalo.

Bunge Lawaagiza Heche, Zitto Kabwe Kuripoti Polisi

$
0
0
Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson amemtaka Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche (Chadema) na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT- Wazalendo) kwenda kuripoti polisi taarifa zao za kutishiwa uhai.

Pia amemuagiza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba kufuatilia kwa karibu taarifa hizo za wabunge kutishiwa uhai.

Agizo hilo la Naibu Spika limetolewa leo bungeni mjini Dodoma wakati akitolea ufafanuzi mwongozo wa Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema) aliyeiomba serikali itoe maelezo kuhusu taarifa za wabunge hao kutishiwa uhai.

Waitara amesema licha ya Spika wa Bunge, Job Ndugai kusema wabunge wako salama, taarifa zilizopo kwenye vyombo vya habari ni kwamba wabunge hao wamesema wanafuatiliwa na watu wanaowatishia uhai hivyo wakapewa nafasi ndani ya bungeni kuelezea taarifa hizo.

Bashe Ahoji Ahadi Ya Rais Magufuli Kufufua Skimu Ya Umwagiliaji

$
0
0
Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM), ameibana Serikali akiitaka itoe majibu kuhusiana na ahadi ya Rais John Magufuli mwaka 2015 ya kufufua Skimu ya Umwagiliaji katika kijiji cha Idudumo Wilayani Nzega.

Akiuliza swali bungeni leo Aprili 25, Bashe amedai kwamba mwaka 2015 wakati wa kampeni, Rais Magufuli aliahidi kuifufua Skimu ya Umwagiliaji katika Kijiji cha Idudumo Wilayani Nzega.

Akijibu swali hilo Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso amesema miradi ya utekelezaji inategemea na upatikaji wa fedha na ikipatikana itatekelezwa.

Mgogoro Udart, Maxmalipo Watua Bunge

$
0
0
Mgogoro kati ya Kampuni ya Usafiri wa Mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam (Udart) na Kampuni ya Maxicom Tanzania (Maxmalipo) umetua bungeni leo baada ya Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson kumuagiza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa kuutolea maelezo wakati akihitimisha hoja ya bajeti ya wizara yake.

Hatua hiyo imekuja baada ya Mbunge wa Kinondoni, Maulid Mtulia (CCM), kuomba mwongozo kwa Naibu Spika kuwa serikali itoe maelezo kuhusu mgogoro huo uliozua usumbufu kwa wananchi wa Jiji la Dar es Salaam kwa muda wa siku tatu sasa.

“Mgogoro huo umesababisha abiria wanaotumia usafiri huo Dar es Salaam kutoka sehemu mbalimbali za jiji kupata usumbufu kwa kukosekana kwa mashine za eletroniki za kutolea tiketi ambayo imesababisha usumbufu lakini pia kuna upotevu wa fedha kwenye upatikanaji wa tiketi hizo jambo lililosababishwa na mgogoro huo wenye harufu ya ufisadi,” amesema.

Hoja hiyo ya Mtulia iliungwa mkono na Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea (Chadema) ambaye aliomba mwongozo kwa Naibu Spika kuwa bunge litumie kanuni ya 47 kusitisha shughuli za bunge na kujadili mgogoro huo kwa dharura.

Akijibu miongozo hiyo Dk. Tulia amesema kwa kuwa miongozo hiyo inahusiana na hoja ya bajeti ya Wizara ya Ujenzi inayohitimishwa leo, waziri husika alitolee maelezo.

“Waziri wakati unahitimisha hoja yako bunge linakuagiza ulitolee maelezo suala hili. Lakini pia haliwezi kusitisha shughuli zake na kulijadili kwa dharura kwa sababu waziri utalitolea maelezo leo baadaye,” amesema Naibu Spika.

Rais wa zamani Malawi Apanga Kurejea Tena Nchini humo baada ya Kukaa Uhamishoni Miaka 4

$
0
0
Rais wa zamani wa Malawi, Dkt. Joyce Banda anatarajia kuingia nchini humo wiki hii baada ya kuishi miaka minne uhamishoni.

Dkt. Banda aliondoka nchini humo baada ya jeshi la polisi kutoa amri ya kumkamata akidaiwa kujihusisha na rushwa.

Msemaji wa Banda, Nowa Chimpeni amesema kuwa chama chake cha People’s Party (PP) kinampokea akiwa na lengo la kukijenga upya katika kuelekea kwenye uchaguzi wa mwaka 2019.

“Naweza kuthibitisha kwa wafuasi na wananchi wa Malawi kwamba rais wa zamani wa nchi hii, Dkt. Joyce Banda atawasili Jumamosi ya wiki hii,” alisema Chimpeni na kuongeza kuwa Banda atakiunga upya chama chake baada ya viongozi wengi kuondoka wakitimkia kwenye chama cha Democratic Progressive Party (DPP).

Dkt. Banda amekuwa akitembelea nchi za Uingereza, Afrika Kusini pamoja na Marekani katika kipindi cha miaka minne, akiwa uhamishoni.

Msemaji wa Jeshi la polisi, James Kadadzera amesema kuwa hati ya kumkamata bado inaendelea kuwepo lakini alikataa kueleza kama Dkt Banda anaweza kukamatwa punde atakapoingia nchini humo.

Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. 

Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.

Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.

Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa

SILYA: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
 
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni

Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto

Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0785 234 837  au 0656 551 093  au 0746473974

Okoa Ndoa Yako Sasa : Je Umepungukiwa Na Nguvu Za Kiume Au maumbile Au Mpenzi Wako Hakutimizii Utakacho?

$
0
0
Acha kujiona mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kwa sabubu ya kutokuwa na nguvu za kiume au uume wako mdogo dawa YA MAPRO POWERA ndio dawa sahihi na tiba tosha kwa sasa kutibu tatizo na kuponesha kabisa tatizo LA;
 1 KUWAI KUFIKA KILELENI KABLA YA MWENZI WAKO
2 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA NA MWILI KUCHOKA 
3 UUME KUSINYAA NA KUWA LEGELEGE 
4 KUUMWA NA TUMBO WAKATI UNAPOMALIZA KUFANYA TENDO

MAKAKANUA; HII NI dawa ya maumbili madogo...hufusha na kunenepesha saizi upendayo saiz 5-6-7-8 na unene sm 3-4-5

Tunarudisha mke au mpenzi ndani ya masaa matatu tu zipo dawa za presha kisukali vidonda vya tumbo korodani iliyovimba, dawa za uzaz,Mi tunapunguza matiti makubwa kitambi na mwili mkubwa dawa zipo 

FIKA OFISINI KWANGU MBAGALA ZAKHEMU. KWA WATEJA AMBAO AMTAKUWA NA NAFASI YA KUJA OFISINI AU MLIO MKOANI MTALETEWA. piga simu 0743362017. 0789234653 DR AGU

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0753471612, 0623386305, 0655283534 -DR KUZENZA
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images